Top Banner
MIUJIZA KATIKA MIILI YETU HARUN YAHYA Mfasiri: IBRAHIMU H. KABUGA © Islamic Centre for Research P.O.BOX 76644 Dar es Salaam Tanzania Phone: +255 712 566595 / 0763348213 E-mail: [email protected]
35

Miujiza Katika Miili Yetu

Sep 30, 2014

Download

Documents

X-PASTER

Wanangu wapendwa, jiandaeni kuingia ndani ya ulimwengu mpana na wenye miujiza kwa muda mfupi. Kwa hakika ulimwengu huu utawashangaza sana. Japokuwa mpaka sasa mnaweza mkawa hamuelewi, lakini matrilioni ya wafanyakazi wa ulimwengu huu wamekuwa wakikutumikieni bila kukoma. Mnashangaa, sio?

Ulimwengu huu wa ajabu ni mwili wako na wafanyakazi hao wanaokutumkia ni seli za mwili wako. Kila eneo la mwili wako linaundwa na seli. Wakati huu, kuna matrilioni ya seli katika mwili wako zinazokutumikia. Zinafanya kazi hata wakati unaposoma kitabu hiki. Kwa mfano, seli za macho yako zinatekeleza michakato kadhaa bila kusimama ili kukuwezesha kusoma. Unapopumua, seli katika koo yako na kisha seli katika mapafu huingia kazini. Wakati huohuo, seli katika tumbo lako zinayeyusha chakula ulichokula saa chache zilizopita.

Tuliyoyataja hapa ni machache tu katika kazi zinazofanywa na mwili wako bila kusimama. kazi hizi zote hutokea bila hata wewe kuwa na taarifa yoyote wala kuhisi kama zinatokea. Matrilioni hayo ya seli yanaungana vipi, kujua la kufanya na kushirikiana katika kazi? Aidha, hakuna matatizo yoyote yanayotokea wakati wa michakato hii. Hakuna seli inayojaribu kufanya kazi tofauti au kukataa kutekeleza kazi yake. Mbali na hilo, kazi zote hizi hufanyika kwa kasi isiyokuwa ya kawaida.

Katika kurasa zijazo, tutachunguza jinsi kazi za kila siku, kama vile uyeyushaji wa chakula, kupumua, kuona na kusikia, zilivyokuwa za ajabu sana. Tutashuhudia kwamba wakati fulani seli zetu hufanya kazi kama mkemia kuzalisha vitu vya kikemikali, wakati mwingine hufanya kazi kama mhandisi kufanya mahesabu na wakati mwingine hufanya kazi kukidhi mahitaji ya seli nyingine...
Welcome message from author
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
Page 1: Miujiza Katika Miili Yetu

MIUJIZA KATIKA MIILI YETU

HARUN YAHYA

Mfasiri:

IBRAHIMU H. KABUGA

© Islamic Centre for Research

P.O.BOX 76644 Dar es Salaam – Tanzania

Phone: +255 712 566595 / 0763348213

E-mail: [email protected]

Page 2: Miujiza Katika Miili Yetu

Ewe mwanaadamu! Nini kilichokughuri ukamwacha Mola wako Mlezi

Mtukufu?

Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha, katika sura yoyote

aliyoipenda akakujenga. (Surat al-Infitar: 6-8)

Page 3: Miujiza Katika Miili Yetu

YALIYOMO

Utangulizi

Kiwanda kikubwa kisichoonekana kwa macho: seli

Mtandao mkubwa unaoizunguka miili yetu

Ubongo unafanya kazi namna gani?

Safari ya chakula mwilini

Safari ya damu katika mishipa

Kiunzi cha mifupa

Mota ndogo sana zilizopo katika mwili: misuli

Kiboresha hewa kinachofanya kazi katika miili yetu bila kusimama

Hitimisho

Page 4: Miujiza Katika Miili Yetu

KUHUSU MWANDISHI

Akitumia jina la uandishi la HARUN YAHYA, alizaliwa mjini Ankara mwaka

1956. Baada ya kumaliza elimu yake ya msingi na sekondari mjini Ankara, alisoma

masomo ya sanaa (arts) katika Chuo Kikuu cha Mimar Sinan cha Istanbul na masomo

ya Falsafa katika chuo kikuu cha Istanbul. Tangu miaka ya 1980, amechapisha vitabu

vingi kuhusu masuala ya kisiasa, kisayansi na kiimani. Harun Yahya ni maarufu sana

kwa kuandika vitabu muhimu vinavyofichua ulaghai wa waenezaji wa nadharia ya

mageuko (evolutionists), madai yao batili, na mahusiano ya giza kati ya u- Darwinist na

aidolojia nyingine za kikatili kama vile ufashisti na ukommunisti.

Jina lake la uandishi linaundwa na majina ya Harun na Yahaya, katika

kuwakumbuka Mitume wawili watukufu waliopambana na ukosefu wa imani wa watu

wao. Muhiri wa Mtume (s.a.w) katika majalada ya vitabu vya mwandishi huyu ni ishara

maalumu na ina uhusiano na kile kilichomo. Ishara hiyo inawakilisha Qur’an

(Maandiko matakatifu ya mwisho) na Muhammad (s.a.w), Mtume wa mwisho. Kwa

muongozo wa Qur’an na Sunnah (mafundisho ya Mtume), mwandishi anafanya lengo

lake kuwa ni kubatilisha kanuni ya msingi wa itikadi za kikafiri na kutoa “neno la

mwisho”, ili kunyamazisha kabisa pingamizi zinazotolewa dhidi ya dini. Anatumia

mhuri wa Mtume wa mwisho, ambaye alikuwa na hekma ya hali ya juu na ukamilifu wa

kimaadili, kama alama ya kusudio lake la kutoa neno la mwisho.

Vitabu vyote vya Harun Yahya vina lengo moja: kufikisha ujumbe wa Qur’an,

kuwahamsisha wasomaji kuyatamaali mambo ya msingi yanayohusu imani kama vile

kuwepo kwa Mwenyezi Mungu, Umoja na maisha ya Akhera, na kufichua misingi

dhaifu ya mifumo ya kikafiri na itikadi potovu.

Vitabu vya Harun Yahya vinasomwa sana katika nchi nyingi, kuanzia India mpaka

Marekani, Poland mpaka Bosnia, na Hispania mpaka Brazil. Baadhi ya vitabu vyake

vinapatikana katika lugha za Kiingereza, Kifaransa, Kiswahili, Kijerumani, Kihispania,

Kitaliano, Kireno, Kiurdu, Kiarabu, Kialbania, Kirusi, Kiserbo-Croat (Kibosnia), ki -

Polish, ki – Malay, ki – Uygur, Kituruki, na ki- Indonesia.

Kutokana na kukubalika ulimwenguni kote, vitabu hivi vimekuwa chombo

muhimu cha watu wengi kuimarisha imani yao kwa Mwenyezi Mungu na kupata

maarifa ya kina kuhusu dini yao. Hekima na ukweli wa vitabu vyake, pamoja na mtindo

wa kipekee unaoeleweka kiurahisi, kwa pamoja humuathiri yeyote anayevisoma. Wale

wanaovizingatia kwa dhati vitabu hivi, hawawezi kupendelea tena ukanaji Mungu

(atheism) au itikadi yoyote potofu au falsafa za kidunia, kwa sababu vitabu hivi vina

sifa ya kipekee ya kumuathiri mtu kwa haraka mno, kupata matokeo ya moja kwa moja,

na kutopingika. Hata kama wataendelea kufanya hivyo, itakuwa ni msisitizo wa kihisia

tu, kwa sababu vitabu hivi vinabatilisha itikadi hizo kuanzia chini kabisa kwenye

Page 5: Miujiza Katika Miili Yetu

mizizi. Harakati zote za sasa za wakanaji zinashindwa kiitikadi, kutokana na vitabu

vilivyoandikwa na Harun Yahya.

Bila shaka haya ni matokeo ya hekma, udhahiri na uwazi wa Qur’an Tukufu. Kwa

unyenyekevu kabisa, mwandishi anakusudia kutumika kama njia ya binadamu kuitafuta

njia ya kweli ya Mwenyezi Mungu. Hakusudii kupata faida ya kidunia katika

uchapishaji wa vitabu hivi.

Wale wanaowahamasisha wengine kusoma vitabu hivi, kufungua akili na nyoyo

zao na kuwaongoza ili wawe waja wa kweli wa Mwenyezi Mungu, hupendelea kutoa

huduma yenye thamani kubwa mno (kuliko faida ya kidunia).

Wakati huohuo, itakuwa ni kupoteza muda na nguvu za bure kueneza vitabu

vingnine vinavyotengeneza hali ya mkanganyiko katika akili za watu, kuwaongoza

kwenye vurugu za kiitikadi, na hivyo kutokuwa na athari madhubuti na imara katika

kuondosha shaka katika nyoyo za watu, kama ambavyo pia ilithibitishwa katika uzoefu

wa huko nyuma. Vitabu vilivyotungwa kwa ajili ya kuonyesha nguvu ya kiuandishi ya

mtunzi husika badala ya lengo lake tukufu la kuwaokoa watu dhidi ya kupoteza imani,

haviwezi kuwa na athari kubwa kama hiyo. Wale wenye shaka na hili wanaweza kuona

wazi kuwa lengo pekee la vitabu vya Harun Yahya ni kuushinda ukafiri na kueneza

tunu za kimaadili za Qur’an. Mafanikio na athari ya huduma hii yanaonekana kwa

kusadikishwa na wasomaji.

Nukta moja yapaswa kuzingatiwa: sababu kuu ya kuendelea kwa ukatili,

migogoro, na misukosuko mingine inayowakumba watu wengi inatokana na kuenea

ukafiri kiitikadi. Hili linaweza tu kukomeshwa kwa kuushinda ukafiri kiitikadi na kwa

kutangaza maajabu ya uumbaji na maadili ya Qur’an ili kwamba watu waishi kwa

kuifuata. Kutokana na hali ya ulimwengu hivi sasa, inayoongoza kwenye shimo la

mzunguko wa vurugu, uovu na migogoro, ni wazi kwamba huduma hii inatakiwa

kutolewa kwa kasi na kwa umadhubuti, la sivyo tunaweza kuwa tumechelewa mno.

Katika juhudi hii, vitabu vya Harun Yahaya vimeshika hatamu. Inshallah, vitabu

hivi vitakuwa njia ambayo watu katika karne ya ishirini na moja watapata amani,

uadilifu, na furaha iliyoahidiwa ndani ya Qur’an.

Page 6: Miujiza Katika Miili Yetu

KWA MSOMAJI

Katika vitabu vyote vya mwandishi huyu, masuala yanayohusu imani

yamefafanuliwa kwa muongozo wa Aya za Qur’an na watu wanapewa wito kujifunza

maneno ya Mwenyezi Mungu na kuishi kwa mujibu wake. Mada zote zinazohusu Aya

za Mwenyezi Mungu zimefafanuliwa katika namna ambayo haiachi shaka au alama za

viulizo katika akili ya msomaji. Mtindo wa ukweli, uwazi na ufasaha uliotumika

unamhakikishia kila mtu wa rika lolote na wa kundi lolote la kijamii kuwa anaweza

kuvielewa vitabu hivi kwa urahisi. Simulizi hii halisi na yenye kueleweka kwa urahisi

itakuwezesha kuvisoma kwa mkupuo mmoja. Hata wale wanaokana vikali mambo ya

kiroho huvutiwa na mambo ya hakika yaliyoelezwa katika vitabu hivi na hawawezi

kuyakana maelezo yake yenye ukweli.

Kitabu hiki na vitabu vyote vya mwandishi huyu vinaweza kusomwa na mtu

mmojammoja au katika vikundi wakati wa mazungumzo. Wasomaji wanaotaka

kufaidika na vitabu hivi watakuta kuwa mfumo wa majadiliano unafaa sana kwa maana

kwamba wataweza kuwaeleza wenzao juu ya hisia na uzoefu wao.

Aidha, itakuwa ni mchango mkubwa kwa dini kugawa vitabu hivi wakati wa

kuwasilisha na usomaji wa vitabu hivi ambavyo vimeandikwa kwa kutaka radhi ya

Mwenyezi Mungu pekee. Vitabu vyote vya mwandishi ni vyenye ushawishi na mvuto

mkubwa. Kwa sababu hii, mojawapo ya mbinu zenye athari kubwa kwa wale

wanaowahubiria dini watu wengine ni kuwahamasisha vitabu hivi.

Inatarajiwa kuwa msomaji atatumia muda wake kupitia vitabu vingine vilivyo

kwenye ukurasa wa mwisho wa kitabu hiki, na atautambua utajiri mkubwa wa

machapisho juu ya masuala yanayohusu imani, machapisho ambayo ni yenye kufaa

sana na yenye kufurahisha kuyasoma.

Katika vitabu hivi, tofauti na baadhi ya bitabu vingine, hutokuta mawazo binafsi

ya mwandishi, maelezo yatokanayo na vyanzo vyenye kutia shaka, mtindo usiochunga

heshima na hadhi ya mada adhimu, na wala hutokuta maelezo dhaifu, yenye kuibua

shaka, na yasiyokuwa na matarajio mema ambayo hutengeneza mikengeuko ndani ya

moyo.

Page 7: Miujiza Katika Miili Yetu

UUTTAANNGGUULLIIZZII

Wanangu wapendwa, jiandaeni kuingia ndani ya ulimwengu mpana na wenye miujiza

kwa muda mfupi. Kwa hakika ulimwengu huu utawashangaza sana. Japokuwa mpaka

sasa mnaweza mkawa hamuelewi, lakini matrilioni ya wafanyakazi wa ulimwengu huu

wamekuwa wakikutumikieni bila kukoma. Mnashangaa, sio?

Ulimwengu huu wa ajabu ni mwili wako na wafanyakazi hao wanaokutumkia ni seli za

mwili wako. Kila eneo la mwili wako linaundwa na seli. Wakati huu, kuna matrilioni ya

seli katika mwili wako zinazokutumikia. Zinafanya kazi hata wakati unaposoma kitabu

hiki. Kwa mfano, seli za macho yako zinatekeleza michakato kadhaa bila kusimama ili

kukuwezesha kusoma. Unapopumua, seli katika koo yako na kisha seli katika mapafu

huingia kazini. Wakati huohuo, seli katika tumbo lako zinayeyusha chakula ulichokula

saa chache zilizopita.

Tuliyoyataja hapa ni machache tu katika kazi zinazofanywa na mwili wako bila

kusimama. kazi hizi zote hutokea bila hata wewe kuwa na taarifa yoyote wala kuhisi

kama zinatokea. Matrilioni hayo ya seli yanaungana vipi, kujua la kufanya na

kushirikiana katika kazi? Aidha, hakuna matatizo yoyote yanayotokea wakati wa

michakato hii. Hakuna seli inayojaribu kufanya kazi tofauti au kukataa kutekeleza kazi

yake. Mbali na hilo, kazi zote hizi hufanyika kwa kasi isiyokuwa ya kawaida.

Katika kurasa zijazo, tutachunguza jinsi kazi za kila siku, kama vile uyeyushaji wa

chakula, kupumua, kuona na kusikia, zilivyokuwa za ajabu sana. Tutashuhudia kwamba

wakati fulani seli zetu hufanya kazi kama mkemia kuzalisha vitu vya kikemikali, wakati

mwingine hufanya kazi kama mhandisi kufanya mahesabu na wakati mwingine hufanya

kazi kukidhi mahitaji ya seli nyingine.

Inashangaza sana kuwa yote haya hufanywa na seli ambazo ni ndogo sana zisizoweza

kuonekana kwa macho. Zaidi ya hivyo ni kwamba, seli zilizo katika miili yetu hufanya

kazi hizi kubwa bila kusaidiwa hata kidogo. Kumbuka kuwa seli hizi sio binadamu kama

sisi. Haziwezi kuonana, kusikia wala kuamua kufanya kazi ya busara. Hazina masikio

wala ubongo. Hazijasoma kemia, lakini, kama tutakavyoona katika hatua za baadaye,

zinajua formula mbalimbali za kemikali na zinaweza kuzalisha mada (substances)

mbalimbali kulingana na formula hizi. Zinawezaje kufanya yote haya?

Utajawa na mshangao utakaposoma na kugundua kuwa seli hazitendi kazi hizi zote kwa

akili zake zenyewe. Lazima utakuwa unajua kwamba haiwezekani ziwe zinajua

kutekeleza kazi hizi ndani ya wakati kwa bahati bahati.

Bado tuna deni kubwa la uhai wetu kuyafahamu matendo ya viumbe hivi vidogo sana

ambavyo hatuwezi kuviona hata kwa macho. Kwa hakika katika seli hizi kuna jambo

muhimu sana kwetu kulitambua. Kuna yule mwenye kumiliki hekima na busara za juu

zaidi ambaye anazifanya seli zetu zitekeleze kazi zote hizi na kuzielekeza kipi cha

kufanya. Mmiliki wa hekima hii ya milele ni Mwenyezi Mungu, aliyeumba kila kitu,

anatupenda na anaujua udhaifu na mahitaji yetu yote.

Kila seli moja miongoni mwa matrilioni ya seli zilizo katika miili yetu hutekeleza kazi

Page 8: Miujiza Katika Miili Yetu

zake kikamilifu kutokana na mpangilio kamili wa Mwenyezi Mungu, ili kwamba tuweze

kuendesha maisha yetu bila shida yoyote. Unapoamka kila siku asubuhi na kwenda shule,

unapoonja ladha tamu ya asali, unapopumua na kuvuta hewa bila tabu,

unapokimbiakimbia katika bustani la shule yako na kucheza na marafiki zako,

unapoandika, unaposoma na mambo mengine unayofanya ni kwa huruma na rehma ya

Mwenyezi Mungu.

Kama ilivyo kwa vitu vingine vyote ardhini, Mwenyezi Mungu amekuumba katika

namna ya ukamilifu na kukupatia kila kitu unachokihitaji. Unachotakiwa kufanya kwa

hisani hii ni kumshukuru Mola wetu aliyekupatia neema zote hizi zenye thamani sana

kuliko zawadi nyingine yoyote ile unayoweza kuwa nayo katika huu ulimwengu.

Kwa sababu hii, tunahitaji kuyatafakari kwa kina yale tuliyojaaliwa na Mwenyezi

Mungu. Katika aya mbalimbali za Qur’an Tukufu, Mwenyezi Mungu ametoa mifano

mingi ili watu waitaamali na kuitafakari. Ifuatayo ni mojawapo ya aya hizo:

Hakika katika kuumbwa kwa mbingu na ardhi, na kukhitalifiana usiku na

mchana, na marikebu ambazo hupita baharini kwa viwafaavyo watu, na maji

anayo yateremsha Mwenyezi Mungu kutoka mbinguni, na kwa hayo akaihuisha

ardhi baada ya kufa kwake, na akaeneza humo kila aina ya wanyama; na katika

mabadiliko ya pepo, na mawingu yanayoamrishwa kupita baina ya mbingu na

ardhi, bila shaka zimo Ishara kwa watu wanaozingatia. (Surat al-Baqara: 164)

Katika kitabu hiki, tutatafakari juu ya miili yetu. Tutaangalia jinsi Mwenyezi

Mungu alivyouumba mwili wa mwanadamu kwa ukamilifu na kwa uangalifu.

Utakaposoma kitabu hiki, utazidi kumpenda Mwenyezi Mungu na kumshukuru.

Utashangazwa na mghafala wa watu wanaokuzunguka, ambao hawatafakari, na

utakuwa na hamasa ya kuwaambia kile unachokijua ili nao pia wawe wasikivu.

Page 9: Miujiza Katika Miili Yetu

KIWANDA KIKUBWA KISICHOONEKANA KWA MACHO: SELI

Kama tulivyoeleza mwanzoni mwa kitabu hiki, miili yetu inaundwa na matrilioni ya seli.

Idadi hii haitakiwi kupuuzwa. Kwa kweli trilioni ni namba kubwa sana na isiyokuwa ya

kawaida. Kila mwili wa mtu mzima una seli zipatazo trilioni 100. Lakini kutokana na

ukweli kwamba seli hizi ni ndogo sana, miili yetu haina ukubwa wa kutisha. Mfano

tutakaoutoa utakusaidia kuelewa namna seli zilivyokuwa ndogo. Mamilioni ya seli za

mwili yanapokusanyika pamoja, hutwaa nafasi isiyozidi ukubwa wa ncha ya sindano.

Lakini licha ya udogo wake, muundo wa seli bado haujaeleweka kikamilifu.

Wanasayansi bado wanaendelea kufanya tafiti juu ya mifumo ya seli.

Seli ya kwanza iliyokutengeneza ilitoka katika tumbo la mama yako kwa muunganiko wa

seli mbili, moja ikifyatuliwa na mwili wa mama yako na nyingine ikitokana na mwili wa

baba yako. Muda mfupi baadaye seli hii iliendelea kugawanyika na kuwa kipande cha

nyama. Kisha, huku seli zilizotengeneza nyama hii zikiendelea kugawanyika ili

kutengeneza seli mpya, mwili wako ulikuwa ukitengenezwa kidogokidogo.

Kila seli mpya ilichukua umbo tofauti. Huku baadhi zikiwa seli za damu, baadhi zikawa

seli za mifupa na nyingine zikawa seli za neva. Katika miili yetu kuna aina 200

tofautitofauti za seli. Kwa kweli, hizi seli zote zina vijenzi vyenye kufanana sana

(identical components), lakini kila seli inafanya kazi tofauti. Kwa mfano, seli za misuli

katika miguu yako ni kama kamba iliyosukwa ili kwamba uweze kutembea na kukimbia.

Kutokana na muundo wa seli hizo, misuli ya mikono na miguu haichanikichaniki

kutokana na kunyooka kulikozidi wakati unapocheza mpira. Kwa umbo, seli zako za

damu ni mviringo (blobular), kazi yake ni kusafirisha oksijeni inayohitajika katika mwili

wako, kwa kutumia mirija (vessel) ya damu. Kutokana na muundo wake, zinaweza

kutiririka kiurahisi kupitia ndani ya mirija ya damu zikiwa pamoja na oksijeni

ziliyoibeba. Kwa upande mwingine, seli za ngozi zimebanwa pamoja na kupangiliwa

katika msitari mmoja kwa ukaribu. hivyo ngozi yako haipitishi vijidudu (microbes) na

maji.

Kadhalika, seli zote nyingine pia zina maumbo kamili yanayofaa kwa majukumu yake.

Hata hivyo, seli hizi hazikupata maumbo haya kwa bahati tu. Angalia kompyuta, magari

au ndege. Kuna mtu aliyebuni maumbo na mifumo muhimu kwa ajili ya ufanyajikazi wa

vifaa hivi. Mambo yote yamezingatiwa na kupangwa na wanateknolijia wa makampuni

husika. Magari yametengenezwa ili kuhakikisha safari ya raha na salama; televisheni

imekusudiwa kusafirisha picha na sauti nzuri na zenye ubora wa hali ya juu kwenda kwa

watazamaji. Jambo hili halihusu vifaa vya kiteknolojia pekee, bali linahusu pia vitu vyote

tunavyovitumia. Meza, viti, nyumba unayoishi, penseli unayotumia, vyombo vya ndani

kama vile vijiko au uma jikoni kwako ... kila kimoja ni matokeo ya ubunifu maalumu.

Kila kimoja kimepangiliwa kwa undani kabisa na hakuna kilichotokea kwa bahati nasibu.

Kama ujuavyo, ili usanifu na bidhaa fulani iwepo, panahitajika chanzo cha ujuzi.

sasa tuzitafakari seli za miili yetu. Seli zetu zina mpangilio na kazi za hali ya juu kuliko

televisheni au chombo kingine chochote cha kiteknolojia. Aidha, vikosi hivi vya

kimuundo vyenye sifa zisizokuwa za kawaida, ni vikosi hai. Kama tulivyoeleza hapo

Page 10: Miujiza Katika Miili Yetu

mwanzo, wanasayansi hawajaugundua kikamilifu mfumo wenye kushangaza uliopo

katika vikosi hivi vidogo vidogo.

Unastaajabu jinsi usanifu huo, ambao akili ya binadamu hijaweza kuugundua kikamilifu,

ulivyotokea katika uwanda huu mdogo?

Hii yatuonyesha kuwa seli zetu zilipangiliwa na ziliumbwa na mwenye ujuzi wa hali ya

juu. Mmiliki wa ujuzi huu ni Mwenyezi Mungu aliyetuumba kwa ukamilifu na kwa

undani wa hali ya juu.

MTANDAO MKUBWA UNAOIZUNGUKA MIILI YETU

Je umewahi kujiuliza maswali yafuatayo?

Je nipumue sasa hivi?

Je kiwango cha damu kinachosukumwa na moyo wangu kinatosha?

Ni seli na kiungo kipi katika viungo vyangu inayohitaji kiwango gani cha

nishati?

Ni wakati gani tumbo langu linatakiwa kusaga chakula nilichokula?

Je nguvu ya mwanga inayoingia katika macho yangu ina uwiano?

Ni misuli gani ninayotakiwa kuiangalia ili nihamishe mkono wangu?

Maswali haya yanaonekana kuwa ya ajabu, au siyo? Ni kwa sababu huwa

hatujiulizi maswali kama hayo. Zaidi ya hilo, wengi wetu hawajui hata utendaji kazi

wenye kuendelea wa michakato hii. Miili yetu hufanya kazi zote hizi kwa kujiendesha

yenyewe (automatically). Na inatumia mtandao wa neva kufanya hivyo. Mtandao huu

unaundwa na muungano wa matrilioni ya seli za neva, ambayo waweza kuyaona katika

kurasa hizi. Mtandao huu wa neva unaofika kila kona ya mwili wetu, tunaweza

kuulinganisha na barabara ya magari (motorway). Kutokana na mtandao huu, seli katika

ubongo wetu huunganishwa na seli zilizopo miguuni, na seli zote zinawasiliana

zenyewe kwa zenyewe. Lakini, mfumo wetu wa neva una mfumo mkubwa sana kuliko

kilomita za barabara za magari zenye njia panda nyingi na sehemu nyingi

zinazotenganisha barabara za magari yanayopita upande wa pili. Kama ambavyo magari

hutembea kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine juu ya barabara, misukumo ya

kiumeme ya neva husafirishwa katika mtandao wa neva katika miili yetu. Misukumo hii

hupeleka ujumbe kutoka eneo moja kwenda jingine.

Misukumo hii hutembea mwilini mwako kwa kasi kubwa sana zaidi ya unavyoweza

kufikiria. Kwa mfano, kiamshi/kichocheo cha kiumeme huondoka na kuanza safari

kutoka katika ubongo wako pindi unapotaka kukunja mkono wako. Wakati wa safari hii

ngumu, kichochea husimama kwanza kwenye neva kuu (spinal cord). Kisha huendelea

kwenye kiungo husika ambacho ujumbe unatakiwa kufika. Misuli ya mkono wako

Page 11: Miujiza Katika Miili Yetu

hunywea kwa ujumla na unaukunja mkono wako kwenye kiwiko (elbow). Mtiririko huu

wa kazi hutokea kufumba na kufumbua (a mere thousandth of a second). Ukizingatia

kuwa inachukua takriban sekunde kuyafunga na kuyafungua macho yako, unaweza

kuelewa vema jinsi muda wa kufumba na kufumbua (thousandth of a second) ulivyo

mfupi. Vivyo hivyo, vichocheo (stimuli) hutumwa kutoka katika mwili wote kwenda

kwenye ubongo kwa kutumia neva. Kutoka kila eneo moja la mwili wako ujumbe

huendelea kutumwa kwenda kwenye ubongo wako na kwa kasi ya ajabu. Ni kwa sababu

hiyo kwamba waweza kuongea, kucheka, kukimbia, kuonja ladha ya ice cream, kucheza

… michakato na kazi zote hizo hutokea bila kuwepo na uingiliaji kati wa aina yoyote;

unafanya jambo papo hapo unapolifikiria. Unakiona kitu wakati unapokitazama, unasikia

maneno wakati huo huo unapoyatamka, unatambua kitu kama ni cha moto au cha baridi

mara unapokishika. Yote haya yanatokana na uelewano uliopo baina ya ubongo wako na

mfumo wa neva.

Kwa yakini, wakati huu huu pia misukumo ya neva inafanya kazi mwilini mwako. Neva

katika ncha za vidole vyako zinatuma ujumbe kwenye ubongo wako kuhusu uzito wa

kitabu ulichokibeba mkononi mwako, ili kwamba ukiinue kitabu hiki kwa nguvu

inayolingana na uzito wake. Vile vile wakati huohuo, vichocheo vinatumwa kutoka

machoni, puani, masikioni, miguuni na maeneo mengine mengi ya mwili wako kwenda

kwenye ubongo.

Ubongo wako huvitathimini vichocheo/viamshi (stimuli) hivi na kutuma majibu

muafaka (relevant responses) kwenye maeneo husika ya mwili wako, ambayo hufanya

kazi kulingana na majibu haya. Sasa jaribu kukumbuka kazi zote hizi. Michakato mingi

hutokea ndani ya mwili wako kwa pamoja. Unasoma kitabu wakati huo huo ukisikia sauti

kutoka ulimwengu wa nje, unahisi manyoya laini ya paka wako anapopita katikati ya

miguu yako, unaonja ladha ya juisi ya matunda unayokunywa, moyo wako unaendelea

kudunda na kazi nyingine nyingi zinatokea mwilini mwako.

Kitu gani kingetokea iwapo ungetakiwa kuyadhibiti mambo yote haya kwa sekunde

kadhaa? Bila shaka usingeweza kuyadhibiti yote haya kwa wakati mmoja. Lakini, kutokana

na ukamilifu wa uumbaji wa Mwenyezi Mungu, ubongo wako na maeneo mengine ya

mwili wako hufanya kazi kwa pamoja na kutekeleza kazi zote hizi bila haja yoyote ya wewe

kuingilia kati. Aina zote za taarifa zinasafirishwa kutoka mwilini kwenda kwenye ubongo

katika namna ya vichocheo viamshi (stimuli) ambavyo vinahitaji kutafsiriwa. Ni hapo tu

ndipo unapoweza kutambua ulaini wa manyoya ya paka wako, ubaridi wa upepo, ladha ya

juisi ya pichi, harufu ya viazi vilivyokaangwa. Sasa basi, je unadhani kuwa ubongo wako,

ambao ni kipande cha nyama chenye uzito usiozidi kilo 1.5, kuwa unaweza kufanya yote

hayo wenyewe? Bila shaka hapana? Kutokana na uumbaji adhimu wa Mwenyezi Mungu,

ubongo wako unaweza kutekeleza kazi zote hizi kwa wakati mmoja.

Utapepesa macho yako iwapo rafiki yako atakukaribia kimyakimya na kupiga makofi

ghafula wakati ukiwa huna taarifa ya ujio wako. Hakuna njia nyingine, kwa sababu hiki

ni kitendo kisohiari (reflex). Kitendo kisohiari ni itikio la papo kwa hapo litokealo bila

hiari ya mtu. Sababu ya kuwa ya papo kwa hapo ni kwamba katika hali hiyo

Page 12: Miujiza Katika Miili Yetu

vichocheo/viamshi (stimuli) havisafirishwi kwenda kwenye ubongo na itikio (response)

litakiwalo hupokelewa moja kwa moja kutoka kwenye neva kuu. Hii ni tunu muhimu

ambayo Mwenyezi Mungu aliiumba kwa ajili yetu kwa sababu, kutokana na vitendo

hivyo visohiari (reflex), tunalindwa dhidi ya hatari nyingi. Kwa mfano, unaweza

kuondosha mkono wako haraka unapogusa bilauri ya moto. Kitendo kisohiari (reflex) ni

chombo cha ulinzi ambacho Mwenyezi Mungu amekiumba kwa ajili ya ulinzi wa miili

yetu. Kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu, vichocheo vya neva husonga mbele mwilini

mwako kwa kasi ya takriban kilometa 9 (maili 6) kwa sekunde na kwa hiyo unalindwa

dhidi ya hatari nyingi.

Page 13: Miujiza Katika Miili Yetu

UBONGO UNAFANYA KAZI NAMNA GANI?

Tawanya vipande mbalimbali juu ya sakafu kwa namna isiyokuwa ya utaratibu na kisha

chukulia kuwa (vipande hivyo) ndio maarifa yote kuhusu ulimwengu. Kwa mfano,

baadhi ya vipande viwakilishe mwanga, vingine viwakilishe rangi na vingine pia

viwakilishe sauti. Sasa vichukue vipande hivyo kimoja baada ya kingine na kisha anza

kuvikusanya ili kutengeneza picha. Kitu unachoweza kukifanya kwa kukifikiria kwa

kina, kwa muda mrefu na kwa undani hufanywa na ubongo ndani ya sekunde moja kwa

mamia ya mara. Ubongo huo hufanya kazi kwa nguvu na amri (inspiration) ya Mwenyezi

Mungu. Je washangazwa na jinsi kazi hiyo inavyofanyika?

Ubongo hukusanya taarifa zinazotoka kwenye macho, pua, masikio, ngozi, mdomo, n.k

na kuzitafsiri. Kinachofanya tafsiri hii ni mkusanyiko wa seli za neva bilioni 100 zilizopo

ndani ya ubongo wako. Seli hizi hufanya kazi bila kuchoka na kukuwezesha kuona rangi

ya tunda unalokula, kutambua sauti ya rafiki yako na kuitambua harufu ya chocolate.

Picha iliyopo katika ukurasa ujao inaonyesha baadhi ya watoto wanaoongea, kusikia,

kuvuta harufu, kutembea na kulala ndani ya ubongo. Lakini picha hii ni ya kufikirika tu,

ambayo imekusudiwa kuonyesha sehemu fulani katika ubongo pamoja na kazi zake. Kwa

uhalisia, ubongo unaundwa na seli za neva, ambazo zinaweza kuonekana tu kwa kutumia

hadubini (microscope). Unadhani seli za neva zinaweza kuuona mwanasesere wako

unaoupenda au kuonja ladha ya ice cream ya chocolate? Bila shaka hapana. Hiyo ni kwa

sababu seli za neva zinaundwa na vipande vyembamba vya nyama (fine pieces of flesh).

Hivyo lazima awepo Mwenye nguvu aliyeuumba ulimwengu huu wa ajabu (wa seli).

Muumbaji huyu ni Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu, Mmiliki wa kila kitu,

ameumba kila kitu kwa ukamilifu na kumpa kila mmoja wetu maisha mazuri.

Tunachotakiwa kukifanya (kwa zawadi hii ya uhai) ni kumshukuru Mola wetu.

Mwenyezi Mungu ameyafanya macho na masikio yetu kuwa mfano na akatwambia

tumshukuru kwa kutupatia neema hiyo:

Na Yeye ndiye aliyekuumbieni kusikia na kuona na nyoyo za kufahamu. Ni

kuchache mno kushukuru kwenu! (Surat al-Muminun: 78)

Page 14: Miujiza Katika Miili Yetu

SSAAFFAARRII YYAA CCHHAAKKUULLAA NNDDAANNII YYAA MMIIIILLII YYEETTUU

Tunapata nishati inayohitajika kwa ajili ya miili yetu kufanya kazi kutoka kwenye

vyakula na vinywaji mbalimbali. Hata hivyo, kila chakula tunachokula, kama vile pasta,

nyama au ndizi, kinahitaji kusagwa kwanza ili kiwe tayari kutumika katika mwili.

Vyakula hivi hutumiwa na seli za mwili baada ya kusagwa. Sukari inayopatikana ndani

ya ndizi au tofaa hutoa fueli/kichocheo kwa ajili ya seli zako na kuongeza nguvu/nishati

(energy) yako; protini zinazopatikana ndani ya nyama ni muhimu kwa ukuaji wa seli

zako, na hivyo mwili wako hupata kukua. Jaribu sasa hivi kurudi nyuma kwenye utoto

wako.

Ulipozaliwa ulikuwa na takriban kilo 2 – 3. Ukifikisha miaka 10 uzito wako utaongezeka

na kufikia kilo 30 – 35, ukifikisha miaka 15 utakuwa na uzito wa kilo 40 – 50, na

ukifikisha miaka 20 – 25 utakuwa na kilo 50 – 60.

Sababu ya hii tofauti kubwa ni kwamba mada (substances) zinazopatikana katika

chakula unachokula huongezwa mara dufu katika mwili wako. Miongoni mwa vyakula

hivi hukupatia nguvu unayoihitaji kwa ajili ya kuendesha baskeli yako, kukimbia na

kucheza, huku vyakula vingine hurudufiwa katika mwili wako na kutengeneza nyama na

mifupa. Vile visivyotumika / vilivyoharibika huondolewa mwilini. Mchakato wote huu

hufanywa katika mfumo wako wa usagaji (digestive system). Viungo na tezi (glands)

mbalimbali ikiwa ni pamoja na tumbo lako, matumbo (intestines) na kongosho (pancreas)

vina majukumu katika usagaji chakula.

Utendaji kazi wa mfumo wa usgaji ni sawa na utendaji kazi wa kiwanda cha kusafisha

mafuta ghafi. Mafuta yasiyosafishwa (ghafi) yanapofika kama mali ghafi kwenye

kiwanda cha kusafishia hufanyiwa mchakato na kusafishwa na mashine ili yaweze

kutumika. Chakula tunachokula huwa ni mali ghafi katika hatua yake ya awali na kisha

husafishwa na tumbo ili kitumiwe na mwili. Baada ya kuvunjwa vunjwa ndani ya tumbo

na matumbo (intestines), chakula huwa tayari kutumiwa kama kirutubisho (nourishment)

cha seli na kupelekwa kwenye maeneo husika ya mwili kupitia mirija/mishipa ya damu.

Kitu chenye asili moja (single parent substance) husafishwa katika kiwanda cha

kusafishia mafuta na kutoa aina mbalimbali za bidhaa kama vile petroli ambayo ni

kichocheo (fuel) cha motokaa, au mpira unaotumika kama soli ya viatu vyako. Vivyo

hivyo, virutubisho ndani ya chakula huvunjwa vunjwa na kuwa mafuta (fats), sukari na

kabohaidreti/chakula cha wanga ndani ya tumbo lako. Lakini kumbuka kuwa

kinachotokea ndani ya tumbo lako baada ya kula sandwichi tamu ni kazi ngumu zaidi

kuliko kazi inayofanyika katika kiwanda cha kusafishia mafuta. Aidha, mlolongo wa kazi

tutakaoujadili hivi karibuni haufanyiki katika kiwanda kikubwa mno, bali hufanyika

katika eneo dogo la mwili wako wewe mwenyewe.

Urefu wa njia yote ambayo ndani yake chakula hupata kusagwa ni mita 10 (futi 30). Hii

ni mara 6 -7 ya urefu wa wastani wa mwanadamu na inashangaza sana jinsi urefu huo

ulivyowekwa na kuenea katika miili yetu. Mfereji huo mrefu umewekwaje ndani ya

mwili wa binadamu? Jibu la swali hili linaonyesha kwa mara nyingine kuwa kuna usanifu

maalumu katika kuumbwa kwa miili yetu.

Kwa kuwa njia ya chakula, kama unavyoweza kuona katika picha kwenye ukurasa

Page 15: Miujiza Katika Miili Yetu

wa kushoto, imeviringiswa, imeweza kuwekwa katika eneo dogo licha ya urefu wake.

Umbo hili maalumu ni usanifu uliokamilika wa Mola wetu, aliyeumba kila kitu. Tabia hii

ya mfumo wa usagaji chakula ni moja tu katika maajabu mengi ambayo Mwenyezi

Mungu ameyaumba ndani ya miili yetu.

Je wajua kwanini meno yako yana maumbo tofauti tofauti?

Sababu ya kwanini meno yana umbo tofauti ni kwamba kila jino lina kazi yake

tofauti. Kwa mfano, meno yako ya mbele ni makali, ili kwamba uweze kung’ata tunda

kwa urahisi. Ingekuwaje kama meno yenye umbo la bapa (molars) yangekuwa mbele?

Usingeweza kung’ata kipande cha tunda kwa meno yako ya bapa. Vivyo hivyo, kama

meno yako ya mbele yengekuwa nyuma, usingeweza kusaga chakula unachokula.

Kama ilivyo kwa kila eneo moja la mwili wako, meno nayo yamepangwa na Mwenyezi

Mungu kwa mpangilio unaofaa na wenye faida na manufaa kwa ajili yako.

BB aa kk tt ee rr ii aa ww ee nn yy ee mm aa nn uu ff aa aa nn aa mm ss aa aa dd aa hh uu ii ss hh ii nn yy uu mm aa yy aa uu ll ii mm ii

ww aa kk oo

Kwa ujumla Bakteria hujulikana kuwa wanazalisha maradhi na ili watu wajikinge

na madhara yake, wanatakiwa kuwa waangalifu kuhusu usafi wa mavazi na mazingira

wanamoishi. Lakini hivi karibuni, wanasayansi wamegundua uwepo wa baadhi ya

bakteria wenye faida ndani ya mwili wa binadamu, hususan nyuma ya ulimi. Ndiyo,

hujakosea kusoma; kuna bakteria wenye faida katika mwili wako. Kazi ya bakteria

wanopatikana nyuma ya ulimi wako ni kuua vijidudu hatari (harmful microbes) katika

tumbo lako. Lakini kwa hakika hii sio kazi rahisi na inahitaji mlolongo wa kazi.

Kwanza kabisa, bakteria huibadilisha nitrati/chumvi (esta) ya asidi nitriki inayopatikana

katika mboga za majani (green – leafed vegetables) kama vile letusi/saladi na kuwa

asidi/nitriti (nitrite). Hata hivyo, kazi bado haijamalizika. Asidi/nitrite kwa kuunganisha

na mate ya mdomoni, huwa na athari dhidi ya vijidudu. Kwa maneno mengine bakteria

walioko nyuma ya ulimi wako husaidia kuzalisha mada inayoua vijidudu (microbe –

killing substance). Kama ujuavyo, vijidudu husababisha maradhi. Kutokana na bakteria

hawa wenye faida ambao huzalisha kitu kinachoua vijidudu unapata kukingwa dhidi ya

maradhi mengi. Bakteria hawa ni moja tu katika ishara za huruma ya Mola wetu

aliyeiumba miili yetu katika namna bora yenye ukamilifu mkubwa. Mwenyezi Mungu

ametupatia neema na tunu nyingi. Kwamba neema na tunu hizi ambazo hazihesabiki

zimeelezwa ndani ya aya ya Qur’an kama ifuatavyo:

Na mkizihisabu neema za Mwenyezi Mungu, hamwezi kuzidhibiti. Hakika

Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira, Mwenye kurehemu. (Surat an-Nahl: 18)

Page 16: Miujiza Katika Miili Yetu

TUMBO LINASAGA VIPI CHAKULA?

Sasa tuchunguze zaidi kazi ya usagaji chakula. Tafakari juu ya upumuaji,

kuogelea, kuendesha baskeli, kula … Yote haya ni ni sehemu ya maisha yetu ya kila

siku, lakini mara nyingi hatutafakari hata kidogo namna yanavyotokea. Miili yetu

inahitaji nishati. Tumekwishaeleza kuwa nishati hii tunaipata kutoka katika vyakula

tunavyokula. Lakini virutubisho vinavyotakiwa na mwili vinatakiwa viwe vyepesi na

vipande vidogovidogo ili kwamba viweze kupita katika mirija/mishipa ya damu.

Tofauti na hivyo haviwezi kupenya/kuenea katika seli. Lakini vyakula tunavyovitumia

ni vipande vikubwa vikubwa. Hivyo, tunahitaji mashine maalumu ili kuuwezesha mwili

kukitumia chakula hicho. Kwa kweli, kwa ufupi hii tunaweza kuiita mashine ya kusaga,

ambayo kimsingi hukipunguza chakula tunachokula na kuwa vipande vidogo zaidi.

Mashine hii ya kusaga iliyopo katika mwili wako inaitwa “mfumo wa usagaji”

(digestive system).

Mfumo huu, kama mifumo yote ya mashine, huundwa na viungo/vijenzi (components)

mbalimbali na kutokana na utendaji kazi kamili wa kila kimoja katika viungo hivyo,

ndipo tunapoweza kusaga chakula. Ni muhimu kwamba viungo/vijenzi vya mfumo wa

usagaji viwe vyenye kuchukuana/kuafikiana na viwe kamili kwa sababu mfumo mzima

hauwezi kufanya kazi mpaka viungo hivyo viwe hivyo.

Hapa tunatoa mfano ili kubainisha kwa nini vijenzi vyote vya mfumo wowote lazima

viwe kamili kwa ajili ya utendaji kamili wa mfumo husika:

Gari inayoendeshwa kwa mtambo maalumu (remote – controlled car) inaundwa na vifaa

mbalimbali kama vile magurudumu, kifaa kinachotawala (controlling device), mota,

betri, gia, koili, antenna, n.k. Vivyo hivyo, mfumo wa usgaji chakula unaundwa na

vijenzi mbalimbali. Vijenzi hivyo vinajumuisha meno, ulimi, umio wa chakula

(oesophagus), tumbo na matumbo (intestines).

Sasa tafakari. Je gari inayoendeshwa kwa mtambo maalumu yaweza kufanya kazi

kama haina antenna au magurudumu? Bila shaka hapana. Gari hiyo inaweza tu kutembea

iwapo itakuwa na vifaa vyake vyote. Hali ni hiyo hiyo kwa mfumo wa usagaji chakula.

Uwepo wa tumbo hautokuwa na maana yoyote mpaka upatikane pia umio wa chakula

(oesophagus), kwa sababu kinachobeba chakula na kukipeleka tumboni ni umio wa

chakula. Katika namna kama hiyo hiyo, Matumbo (intestines) hayawezi kuwa na faida

yoyote mpaka liwepo tumbo, kwa sababu chakula kinachosagwa hupitshwa katika

matumbo, ambapo hupewa muundo kamili ili kupelekwa kwenye seli za mwili.

Hii inaonyesha wazi kuwa Mola wetu, Muumba wa kila kitu, aliumba kwa ajili yetu

mfumo ambao ni kamili katika kila nyanja. Hii inaonyesha tena kuwa hakuna mungu

zaidi ya Mola wetu:

Hakika Mungu wenu ni Allah, Mwenyezi Mungu, tu. Hapana Mungu isipo

kuwa Yeye. Ujuzi wake umeenea kila kitu. (Surah Ta Ha: 98)

Page 17: Miujiza Katika Miili Yetu

MASHINE YA USAGAJI CHAKULA YAANZA KAZI…

Usagaji chakula huanza mdomoni. Kabohaidreti zipatikanazo katika chakula

unachokula huvunjwa vunjwa kwanza na kuwa vipande vidogo zaidi kwa mate

yaliyopo mdomoni mwako. Kwa mfano, mkate uliokula wakati wa kifungua kinywa

ulianza kumeng’enywa kwanza. Lakini itachukua muda kwa jibini uliyokula na mkate

huo kumeng’enywa.

Virutubisho vinavyomeng’enywa mdomoni hupitia katika umio wa chakula na

kufika tumboni. Tumboni kuna hali nyingine ya ajabu ya utulivu na mlingano. Usagaji

wa chakula tumboni hufanywa na kimiminika / kioevu (fluid) chenye nguvu sana.

Kimiminika hiki ni asidi ya haidrokloriki (hydrochloric acid). Kama ujuavyo, asidi ni vitu

vinavyoharibu. (Asidi hizo) zinaweza kuyeyusha kile kinachogusana nazo. Kwa mfano,

mama yako hutumia kitu chenye asidi ili kusafisha tundu iliyoziba. Kumeng’enya vile

vichafu na vilivyoharibika ambavyo vimeziba bomba, asidi hizi huziondosha. Ni

kutokana na asidi yenye nguvu inayopatikana tumboni kwamba chakula kinachokuwa

katika vipnde vikubwa vinapofika kwanza tumboni humeng’enywa na kuwa vipande

vidogo zaidi vinavyoweza kutumiwa na mwili. Lakini kuna nukta moja zaidi inayohitaji

kueleweka.

Tumeeleza kwamba chakula kinacholiwa humeng’enywa katika vipande

vidogovidogo kwa tumbo au asidi ya tumbo. Sasa inakuwaje hii asidi isiliharibu tumbo

lenyewe, ambalo nalo limetengenezwa kwa nyama? Sasa tafakari kuhusu jambo hilo.

Asidi ya tumboni inaisaga nyama, mathalan, uliyokula wakati wa chakula cha mchana,

lakini inaliacha tumbo ambalo nalo ni kipande cha nyama. Kwa nini inakuwa hivyo?

Katika nukta hii, ubora katika uumbaji wa Mola wetu unadhihirika kwa mara nyingine.

Mwenyezi Mungu aliyeumba kila kitu kwa ukamilifu aliweka ulinzi maalumu ili kwamba

tumbo lenyewe lisimeng’enywe.

Ulinzi huu unaweza kuelezwa kwa mukhtasari kama ifuatavyo; kimiminika

kingine kiitwacho “mucous”, huwekwa ndani wakati wa umeng’enyaji ili kuizuia asidi

ya haidrokloriki (hydrochloric acid) isilimeng’enye tumbo. Utando maalumu wa

kimiminika cha mucous huufunika mzunguko wa ndani wa tumbo na kulizuia tumbo

lisiharibiwe na asidi hii yenye nguvu. Hivyo tumbo halijimeng’enyi lenyewe.

Sehemu inayofuata ya safari ya umeng’enyaji wa chakula ni matumbo (intestines).

Virutubisho humeng’enywa na kuwa vidogo zaidi na kufanywa kuwa vyenye kutumiwa

na mwili pindi vinapopita kwenye matumbo (intestines) mawili, utumbo mpana na ule

mdogo. Kile chenye manufaa katika hivi virutubisho huingizwa kwenye mkondo wa

damu na mabaki yasiyofaa hutolewa nje ya mwili kwa mfumo wa utoaji taka za mwilini.

Hatua/awamu ambazo chakula hupitia ndani ya matumbo nazo pia ni muhimu sana.

Umeng’enyaji huendelea ndani ya matumbo kama ilivyokuwa kwa hatua ya tumboni.

Virutubisho huendelea kumeng’enywa na kuwa vidogo zaidi. Na sasa vinakuwa vidogo

mno kiasi kwamba hufyonzwa na mirija ya damu inayoyazunguka matumbo na

kuingizwa katika mkondo wa damu kwa ajili ya kusafirishwa kila eneo la mwili wako.

Hakika mmetambua kuwa mfumo wa usagaji chakula umepangiliwa moja kwa

Page 18: Miujiza Katika Miili Yetu

moja na kwa ukamilifu. Wakati wa safari hii inayoanzia mdomoni na kuendelea ndani

ya umio la chakula, tumboni na hata kwenye matumbo/utumbo, chakula husika hupitia

hatua/awamu kadhaa wa kadhaa. Na hatimaye virutubisho vinavyohitajiwa na seli za

miili yetu hupatikana. Virutubisho hivyo hufyonzwa ndani ya matumbo/utumbo na

kupelekwa mwilini kupitia mkondo wa damu. Usagaji wa chakula ungekuwa mgumu

sana kama mfumo huu usingefanya kazi kikamilifu. Kwanza kabisa, kama tungekuwa

hatuna meno tusingeweza kutafuna chakula chetu vya kutosha na kisingeweza kupita

kooni. Hata kama kingepita kingeumiza sana umio wa chakula. Kama tumbo letu

lisingekuwa na uwezo wa kusaga chakula, kila kitu tulichokula kingebaki kuwa

kikubwa ndani ya tumbo, jambo ambalo lingeleta usumbufu sana. Aidha, kutokana na

kushindwa kusaga chakula, miili yetu isingepata virutubisho inavyovihitaji. Mwili

usiokuwa na virutubisho hukosa nguvu baada ya muda mfupi na seli za mwili huanza

kufa. Mfumo huu bora na wa kushangaza hufanya kazi bila hitilafu na bila ya sisi

wenyenyewe kuwa na taarifa juu ya ufanyaji kazi huu. Ubora huu katika uumbaji

umeelezwa ndani ya aya ifauatyo:

Yeye ndiye Mwenyezi Mungu, Muumbaji, Mtengenezaji, Mtia sura, Mwenye

majina mazuri kabisa. Kila kilioko katika mbingu na ardhi kinamtakasa, naye ni

Mwenye kushinda, Mwenye hikima. (Surat al-Hashr: 24)

Page 19: Miujiza Katika Miili Yetu

SAFARI YA DAMU NDANI YA MISHIPA /VENA (VEINS)

Katika sura zilizotangulia tuliuangalia mtandao mkubwa wa neva unavyofanya kazi

ndani ya miili yetu. Kuna mtandao mwingine wa ajabu kama huo. Mtandao huu unaundwa

na mishipa ya damu. Kama ilivyo kwa mtandao wa neva, mishipa ya damu nayo

inazunguka ndani ya mwili. Mishipa hii ni mirefu sana kiasi kwamba urefu wake unaweza

kuwa takriban kilometa 100,000 (maili 62,000) kama zikitandazwa kwenye eneo la

tambarare. Kwa kweli, sio jambo gumu hata kidogo kuelewa kuwa kuna mishipa ya damu

kuuzunguka mwili wako wote. Hata mkwaruzo mdogo tu kwenye kiungo chochote cha

mwili wako huweza kutiririsha damu haraka. Hii inathibitisha kwamba damu huzunguka

sehemu zote za mwili wako. Kuna umuhimu mkubwa wa sisi kuwa na mishipa ya damu

katika kila eneo kwa sababu, kama ilivyoelezwa katika sura iliyotangulia, kirutubisho

kinachohitajiwa na seli za mwili husafirishwa kupitia mishipa ya damu. Oksijeni ambayo

seli zinaihitaji ili kuziwezesha kufanya kazi kikamilifu nayo pia hupelekwa kwenye seli kwa

kutumia damu inayotiririka ndani ya vena (vein).

Usafirishaji wa kirutubisho katika mishipa ya damu yaweza kulinganishwa na

usafirishaji wa shehena kwa kutumia meli. Kabla ya usafirishaji wa bidhaa, kwanza mizigo

yote hupakiwa bandarini. Mizigo inatakiwa ipakiwe na kupangwa vizuri. Baada ya mizigo

yote kupakiwa, meli huanza safari kuelekea kwenye bandari inayopelekewa mzigo huo.

Inapofika bandarini, mizigo hupakuliwa na kusambazwa kwenye maeneo husika. Katika

mishipa ya damu, kirutubisho nacho husafirishwa hivyo hivyo kwenda kwenye seli, kama

meli zinavyosafirisha mzigo baharini. Oksijeni, mafuta/shahamu na asidi amino hutiririka

katika mkondo wa damu katika vifurushi na kuvipakua kwenye seli zinazolengwa

kupelekewa shehena hiyo. Kamwe utaratibu huu wa usafirishaji haushindwi hata kidogo.

Kiwango cha shehena kinachotakiwa hufikishwa kwenye seli husika kwa wakati

unaotakiwa. Tofauti na hivyo, mathalani, kama seli fulani inayohitaji oksijeni badala yake

ikapelekewa mafuta, seli hiyo itakufa. Ifahamike kuwa hata kosa dogo katika mfumo huu

linaweza kusababisha madhara makubwa. Lakini, makosa kama hayo huwa hayatokei

isipokuwa katika hali zisizokuwa za kawaida kwa sababu mambo haya hayakutokea kwa

bahati nasibu. Mwenyezi Mungu, Muumba, aliumba mfumo huu katika namna ya ukamilifu

ili ututumikie.

Damu inapokuwa inazunguka katika mwili wote, ndivyo inavyotekeleza kazi zake. Na

sasa tuangalie kwa mukhtasari kazi hizi.

USAFIRISHAJI WA SHEHENA

Tumekwishaeleza kuwa aina zote za shehena zinazohitajiwa na miili yetu hufikishwa

kwenye viungo husika kwa njia ya damu. Wakati huohuo, seli za damu hukusanya vile

Page 20: Miujiza Katika Miili Yetu

vilivyoharibika, kama vile kaboni dayoksaidi na kuhakikisha kuwa vinatolewa mwilini.

Katika namna fulani, damu hufanya kazi kama mashine ya kusaga uchafu/taka (garbage

grinder). Kwa kuipitia mara kwa mara kila seli katika seli trilioni 100 kwa siku nzima,

damu huziachia seli kile zinazokihitaji na wakati huohuo hukusanya kile kisichohitajika.

Damu ambayo ni kimiminika tu, inaweza kufanya kazi inayohitaji umakini na

uwajibikaji kama huo bila kukosea. Inajua kila kitu ilichokibeba, kitatumika kwa ajili gani

na mahali kinapotakiwa kufikishwa. Kwa mfano, damu haikosei kuipelekea seli kaboni

dayoksaidi iliyoichukua kwenye seli nyingine kama uchafu. Mara zote inazipatia seli

oksijeni na kuondosha kaboni dayoksaidi. Damu hufanya kazi hii bila kukosea au kuchoka,

kwa sababu ni sehemu ya mpango kamili ambao Mwenyezi Mungu ameuumba ndani ya

mwili wa binadamu. Wakati zikisalimu amri moja kwa moja kwenye mfumo ulioumbwa na

Mola wetu, seli za damu hutekeleza kazi zake bila kufanya makosa yoyote.

ASKARI NDANI YA DAMU

Kila siku miili yetu hupambana dhidi ya bakteria, virusi na vijidudu vingi. Baadhi

huzuiliwa visiingie mwilini, huku vingine vikiweza kuingia. Lakini kuna seli maalumu

za ulinzi ndani ya miili yetu zinazopambana navyo ambazo hujulikana kama “seli za

kinga” (immune cells). Seli hizi, ambazo ni kama askari wanaopambana dhidi ya adui

na kuilinda miili yetu dhidi ya hatari mbalimbali, hupita katika mkondo wa damu.

Panapokuwa na shambulio la adui, huweza kufika kwenye eneo husika la mwili kupitia

mishipa ya damu na kupambana kwa urahisi zaidi dhidi ya adui. Seli za kinga

hazikujifunza majukumu yake zenyewe. Ziliyajua majukumu hayo tangu zilipoumbwa.

Huanza kutekeleza jukumu lake na kuulinda mwili tangu pale mtoto anapozaliwa. Haya

yanaelezea ubora katika uumbaji wa Mwenyezi Mungu. Mola wetu amezifundisha seli

ambazo haziwezi kuonekana kwa macho ujuzi muhimu sana na akazifanya zitutumikie.

MAWASILIANO

Damu pia hufanya kazi kama nyezo ya mawasiliano katika mwili. Kuna wajumbe

mbalimbali wanaochukua ujumbe kutoka sehemu moja ya mwili kwenda sehemu

nyingine. Wajumbe hawa wanaojulikana kama homoni, husafirisha ujumbe kwenda

kwenye viungo husika kama mfanyakazi wa posta apelekavyo barua. Kazi nyingi za

muhimu, ikiwa ni pamoja na ukuaji wa mwili, kiu, jasho na udhibiti wa kiwango cha

sukari ya damu hutokana na ujumbe huo mbalimbali unaofikishwa kwa wakati.

DAMU INAYOPONYA MAJERAHA

Bila shaka utakuwa umeshaona kuwa jeraha dogo la ngozi hukoma mara moja

Page 21: Miujiza Katika Miili Yetu

kuvuja damu baada ya muda mfupi. Kwa hakika jambo hili ni lenye kukanganya kwa

sababu, kwa hali ya kawaida, kimiminika kinachotiririka kwenye tundu hakiwezi

kuacha kuvuja kwa matakwa yake. Ili kulielewa zaidi jambo hili, fikiria mfano kwamba

una puto lililojazwa maji. Ukitoboa tundu dogo kwenye hilo puto kwa kutumia sindano,

maji yataanza kuvuja. Je yataacha kuvuja baada ya muda bila wewe kuyaziba? Bila

shaka hapana. Maji yataendelea kuvuja mpaka maji yote yaishe katika puto. Jambo hili

linavihusu vimiminika vyote vilivyowekwa katika maeneo yaliyofungwa.

Damu hupita katika mzunguko uliofungwa wa vena na huvuja pindi inapotokea

jeraha hata dogo sana. Lakini, ni muhimu sana damu hiyo ikome kutiririka kwa

manufaa ya afya yetu. Utakuwa umewahi kusikia kuhusu watu wanaokufa kutokana na

kupoteza damu nyingi katika ajali au oparesheni/upasuaji. Sasa basi, kitu gani

kinachosababisha damu kuacha kuvuja muda mfupi baada ya jeraha kuanza kutoa

damu?

Jambo hili hujulikana kama ugandaji wa damu (blood clotting), ambalo ni

mojawapo ya mifumo ya kiulinzi inayojiendesha yenyewe ndani ya miili yetu. Baadhi

ya mada zinazopatikana ndani ya damu huikatisha na kulifunga jeraha. Kutokana na

uwezo wa damu kuganda, uvujaji mkubwa wa damu hupata kuzuiliwa. Baadhi ya seli

hutaarifiwa juu ya vena iliyoharibika na huelekea mara moja kwenye eneo hilo.

Kwanza hujikusanya kwenye jeraha na kuzuia mtiririko wa damu kwa kutengeneza

utando. Utando huu hukauka ndani ya muda mfupi na kutengeneza kitu tunachokiitwa

“scar” (kovu).

Sasa tutafakari kwa pamoja. Je mlolongo huu wa kazi zilizopangiliwa unaweza

kutokea kwa bahati nasibu? Inakuwaje baadhi ya seli za damu zipate taarifa juu ya

jeraha mahali fulani katika mishipa ya damu, ambayo ni kama ulimwengu mkubwa

mno kwa kulinganishwa na ukubwa wake? Kwa nini zinapambana kuzuia utiririkaji wa

damu? Zinajuaje kwamba zinatakiwa kulifunga jeraha ili kuzuia upotevu wa damu?

Nani aliyezifundisha seli hizi kwamba zinatakiwa kufunga jeraha?

Seli zisingeweza kuyajua yote haya kwa bahati nasibu na wala zisingeweza

kuyakamilisha zenyewe binafsi. Hata binadamu wenye akili hawawezi kutengeneza

mfumo mpana kama huo na kuzifundisha seli kipi cha kufanya. Kwa hakika, uelewa

mkubwa unaoonyeshwa na seli hizi sio milki yao. Mwenyezi Mungu huzifunulia na

hufanya kazi kulingana na mpangilio uliokamilika.

Mwenyezi Mungu anatueleza kuhusu ubora wa uumbaji Wake kama ifauatavyo:

Aliyeumba mbingu saba kwa matabaka. Huoni tafauti yoyote katika uumbaji

wa Mwingi wa Rehema. Hebu rudisha nadhari! Unaona kosa lolote? Tena

rudisha nadhari mara mbili, nadhari yako itakurejea mwenyewe hali ya kuwa

imehizika nayo imechoka. (Surat al-Mulk: 3-4)

Page 22: Miujiza Katika Miili Yetu

KIMIMINIKA CHA AJABU KISICHOKUWA NA MFANO WA

KUTENGENEZWA UPYA: DAMU

Wanasayansi wamefanya tafiti nyingi ili kutengeneza kimiminika sawa na damu.

Lakini, wakiwa wameshindwa kufanya hivyo, walikata tamaa na wakaacha kabisa kujaribu

(utengenezaji wa) kuiga na wakajikita katika kufanya utafiti wa nyanja nyingine.

Wanasayansi hawana uwezo wa kutengeneza mfano wa damu kwa sababu sampuli

za damu zinazochukuliwa kutoka kwenye mrija/mshipa wa damu huganda mara moja na

muundo wa damu unakuwa haufai tena kwa uchunguzi/kipimo. Aidha, ni kazi bure

kutunza sampuli za damu katika glasi za mirija ya vipimo (glass test tubes), kwa sababu

seli za damu haziishi hata kidogo katika mirija (tubes). Hivyo, wanasayansi walilazimika

kuzitenganisha seli na damu na kuzipima pekee yake. Bila shaka, hii ni miongoni mwa

maelezo yasiyoingia akilini kabisa duniani kudai kwamba mada (substance) hiyo

iliyoumbwa kwa ukamilifu, ambayo haiwezekani hata kuiga mfano wake pamoja na

taarifa zote ambazo binaamu wamezikusanya kwa miaka mingi, kwamba iwe ilitokea

mara moja na kwa bahati nasibu. Mwenyezi Mungu aliumba damu kama kitu

kisichokuwa na mfano. Seli ya damu yenye vipawa vingi vya kustaajabisha ni moja tu

katika ishara za hekima isiyo na kikomo ya Mwenyezi Mungu ndani ya mwili wa

binadamu.

MM OO TT AA YY AA MM WW II LL II :: MM OO YY OO

Je umewahi kufikiria namna lita za damu zinavyozunguka bila kusimama ndani ya

miili yetu juu na chini? Kila kifaa kinahitaji mota ili kiendelee kutembea. Magari,

ndege, motaboti na hata mwanasesere wako wa gari unaoendeshwa kwa rimoti

hutembea kwa kutumia mota. Vivyo hivyo, mzunguko wa damu ndani ya miili yetu nao

pia unahitaji mota. Mota inayosukuma damu yetu usiku na mchana, kwa muda wa

miezi na hata miaka ni moyo.

Weka vidole vyako kwenye kifundo chako (cha mkono) na subiri kwa muda.

Utahisi mapigo ya moyo wako. Moyo wako hupiga mara 70 kwa dakika, na husukuma

kiasi cha lita milioni 152 (galoni milioni 40) za damu katika kipindi chote cha uhai wako.

Kiwango hicho cha damu kinakadiriwa kuwa sawa na kiasi kinachoweza kubebwa na

meli 10,000 za mafuta. Takwimu hizi zinashanga, au sio? Sasa fikiria kwamba unatakiwa

kuchota kikombe cha maji kutoka kwenye ndoo moja kwenda kwenye ndoo nyingine,

mara 70 kwa dakika. Mwishoni mkono na misuli yako itauma na utahitaji kupumzika.

Lakini moyo wako hufanya kazi hii kwa kipindi chote cha uhai wako bila kupumzika

hata kidogo.

Page 23: Miujiza Katika Miili Yetu

PPAAMMPPUU BBOORRAA ZZAAIIDDII IILLIIYYOOKKAAMMIILLIIKKAA

Pampu iliyotengenezwa kwa ubora zaidi kushinda yote duniani sasa hivi inapiga

kwenye upande wa kushoto wa moyo wako. Kutokana na muundo wake wenye

kushangaza na utendaji kazi wake wa bila kusimama, moyo wako huifanya damu yote

katika mwili wako ikamilishe mizunguko kamili 1,000 kwa siku.

Moyo ni pampu iliyotengenezwa kwa nyama yenye ukubwa wa takriban sawa na

ngumi ya mtu. Lakini ndio injini yenye nguvu zaidi, yenye kudumu zaidi na madhubuti

zaidi kuliko injini zote ulimwenguni kulingana na uwezo wake. Tunazo sababu nyingi za

kuielezea nguvu ya moyo katika namna hii. Sababu kubwa kabisa, moyo hutumia

kiwango kikubwa sana cha nishati/nguvu wakati unapopiga. Kutokana na nishati/nguvu

inayotumiwa na moyo, damu inaweza kuruka kwa kiwango cha mita 3 juu. Itafaa zaidi

kama tukitoa mfano ili iwe rahisi kuelewa uwezo wa moyo. Kwa saa moja moyo

unaweza kuzalisha kiwango cha nishati/nguvu inayotosha kunyanyua gari ya wastani kwa

umbali wa mita moja juu kutoka kwenye uso wa ardhi.

Pampu halisi katika moyo

Moyo, ambao ni kiungo chenye nguvu na ukubwa wa sawa na takriban ngumi ya mtu,

unaundwa na nusu mbili. Kuna pampu mbili katika sehemu hizi. Pampu ya upande wa

kushoto, ambayo ndiyo yenye nguvu zaidi, husukuma damu yenye oksijeni kwenda kwenye

maeneo yote ya mwili. Pampu ya upande wa kulia ni dhaifu kuliko ile ya kwanza na

husukuma damu isiyokuwa na oksjeni kidogo (oxygen-poor blood) kwenda kwenye

mapafu. Safari hii ya kutoka kwenye moyo kwenda kwenye mapafu ni ya umbali mfupi na

kwa hivyo hujulikana kama “mzunguko mdogo” (small circulation). Ule wa awali

unajulikana kama “mzunguko mkubwa” (large circulation).

Kila moja katika hizi nusu mbili za moyo imegawanyika katika sehemu mbili zaidi.

Damu iliyopo baina yake hupita kwenda kwenye eneo lingine kupitia kwenye vali za moyo

(heart valve). Pampu hizi hufanya kazi bila kukoma kwa kiwango kikubwa cha nishati,

kutokana na mizunguko ya damu inayofanywa katika miili yetu mara 1,000 kwa siku.

MOYO HUJITUNZA WENYEWE

Mashine huhitaji matengenezo ya mara kwa mara. Wakati mwingine ni muhimu

kuyafanyia matengenezo baadhi ya maeneo ya mashine au kubadilisha vifaa ambavyo

vimechakaa. Mashine inahitaji kutibiwa kwa mafuta baada ya kufanya kazi kwa kipindi

fulani cha muda, ili kupunguza uchakavu unaotokana na msuguano.

Page 24: Miujiza Katika Miili Yetu

Kama mashine, moyo ambao huendelea kufanya kazi muda wote nao pia unahitaji

matengenezo. Lakini, moyo hujifanyia matengenezo wenyewe; hujilainisha wenyewe.

Unadhani moyo unajilainishaje wenyewe? Jibu la swali hili linapatikana ndani ya

mfumo wa uumbwaji wake. Eneo la nje la moyo limefunikwa na kifuko chenye

utando/viwambo viwili. Baina ya tando hizi kuna majimaji/kimiminika chenye

kuteleza. Majimaji haya (yenye utelezi) hufanya kazi kama mafuta ya mota huwezesha

moyo kufanya kazi kwa urahisi. Muundo huu wa kujilinda unaopatikana katika moyo

unaonyesha kwa mara nyingine namna usanifu wa Mwenyezi Mungu ulivyo mkamilifu

katika uumbaji wake.

KIUNZI CHA MIFUPA

Kuna mifupa 206 katika mwili wako. Unaweza kudhani kuwa kiwango hiki ni

kikubwa mno, lakini kwa mfano tutakaoutoa, utaelewa jinsi ilivyo muhimu kuwa na

mifupa mingi kiasi hicho. Hebu tuviangalie vidole. Iwapo kila kidole kimoja kingekuwa

na mfupa mmoja tu usingeweza kubeba hiki kitabu kama ufanyavyo sasa. Hii ni kwa

sababu mfupa usio kunjufu hauwezi kupinda na bila shaka ukiulazimisha utavunjika.

Kwa kuwa huwezi kuvikunja vidole vyako, hutoweza kushika au kukamata vitu. Wala

hutoweza kuandika au kula. Kinachokufanya uweze kubeba kitabu hiki kwa urahisi na

wakati huohuo kunywa juisi yako ya matunda ni uwepo wa mifupa 27 iliyoingiliana

ndani ya mkono wako ikiwemo ile ya vidole vyako.

Kama ilivyoelezwa hapo awali, kuna mifupa 206 katika miili yetu, ambayo

imeungana kama ile iliyopo katika mikono yetu. Kila mfupa miongoni mwa mifupa hii

umekaa mahali pake kulingana na mpangilio wa hali ya juu. Kutokana na mpangilio

huu kamilifu unaweza kuupinda mwili wako mbele, unaweza kupiga magoti na

unaweza kukizungusha kichwa chako. Lakini usikosee: huwezi kufanya yote haya kwa

kutumia tu mifupa yako, kwa sababu mifupa haiwezi kukunjika. Kuna maungio kwenye

eneo la makutano ya mifupa yako. kutokana na maungio haya, unaweza kuukunja

mkono wako kwa urahisi, unaweza kunyanyua mguu wako na unaweza kutumia vidole

vyako.

Ngoja tukupe mfano ili uweza kuelewa jinsi maungio yalivyo na umuhimu katika

usogevu wa mifupa yetu:

Chukulia mfano umetengeneza karagosi wa mbao. Utafanyaje ili mikono yake

isogee? Mikono yake haitosogea mpaka uweke maungio sehemu ambayo mikono

hikutana na mabega. Utafanyaje ili miguu yake iwe ni yenye kusogea? Lazima utumie

kiungio tena mahali ambapo miguu inakutana na pingiti. Hapo ndipo unapoweza

kuisogeza mikono na miguu ya karagosi wako wa mbao. Vivyo hivyo, kama

ukitenganisha ubao ulioutumia kutengeneza mikono na miguu na kuwa vipande vipande

na ukaweka viungio, au maungio, baina ya vipande hivi, hapo mikono na miguu ya

Page 25: Miujiza Katika Miili Yetu

karagosi wako nayo pia itaweza kukunjika kwenye viwiko na magoti kwa pamoja.

Kama ulivyoelewa wazi kwenye huu mfano, kuwa na mifupa mingi na maungio

yaliyowekwa baina yake inatuwezesha sisi ktembea na kusogea kwa urahisi.

RASILIMALI ZA MIFUPA ZISIZOWEZA KUIGWA

Kuna aina mbalimbali za maungio katika mifupa yetu. Huku baadhi ya maungio

yakiiwezesha mifupa kwenda mbele na nyuma, maungio mengine huiwezesha mifupa

kusogea upande upande. Sasa tuyaangalie maungio na mifupa kwa undani zaidi.

Mifupa yetu ina majukumu mbalimbali ya kutekeleza na kuilinda miili yetu. Kwa

yakini, imeumbwa ikiwa na uwezo na uimara wa kutekeleza majukumu hayo.

Mifupa yetu ni myepesi na imewekewa matundu madogo madogo katikati kama sega

la nyuki. Lakini ingawa ni myepesi kutokana na muundo huu nywelevu, pia ni imara sana.

Hata hivyo hii haimaanishi kuwa ni rahisi kuvunjika. Kinyume chake, ni imara sana kiasi

kwamba ukichukua kiwango hichocho cha mfupa na chuma, utakuta kwamba mfupa ni

imara mara 5 zaidi ya chuma. Kwa mfano mifupa ya paja katika miguu yetu, ina uwezo

mkubwa wa kuinua juu tani moja ya mzigo ikiwa imesimama kuelekea juu. Unaporuka au

kuchupa kutoka upande mmoja kwenda mwingine, mfupa huu huwekwa kwenye uzito ulio

sawa na mara 3-4 ya uzito wa mwili wako. Lakini hupati madhara yoyote kutokana na

uimara wa mifupa yako.

Kitu gani kinachoifanya mifupa iwe imara kiasi hicho? Kwa kweli, jibu la swali hili

linapatikana katika mfumo wa uumbaji usiomithilika wa mifupa, ambao tumeuelezea kwa

ufupi hapo juu. Mifupa imetengenezwa kwa tishu nywelevu iliyo kama sega la nyuki. Ni

kutokana na muundo huu kwamba ni imara sana na myepesi kwa matumizi rahisi. Kama

ingekuwa kinyume, yaani kama sehemu za ndani ya mifupa zingekuwa ngumu na zikawa

hazina uwazi (spaces) wowote kama sehemu ya nje, mifupa ingekuwa mizito sana. Aidha,

kwa kuwa isingekuwa nyumbulifu hata kidogo ungeona mifupa ikivunjika au kupata ufa

kwa kupigwa na kitu kidogo tu, mathalani ukiupiga kidogo mkono wako kwenye ukingo wa

kabati. Lakini, Mwenyezi Mungu ni Mwenye huruma na aliiumba mifupa yetu katika

namna hiyo ili kwamba iweze kukabiliana na tatizo la kimwili na kuwa na ulinzi.

Kile ambacho mifupa imetengenezwa nacho kimewashangaza na kuwavutia sana

wanasayansi na wamejaribu kuiga kwa kutengeneza tishu ya mfupa kwa miaka mingi.

Tishu hii, ambayo ni imara sana, licha ya kuwa nyepesi, na ambayo inaweza kujikarabati

yenyewe, inaweza kukua yenyewe binafsi. Sababu ya urefu wa mwili wako wa sasa

kutokuwa sawa na urefu wako ulipokuwa na miaka 4-5 na sababu ya kuwa tofauti

utakapokuwa na umri wa miaka 19-20 ni ukuaji mifupa yako. Kwa ajabu kabisa, ukuaji huu

umepangiliwa kwa uwiano na urari mzuri sana. Mikono yako hukua wakati miguu yako

ikikua; vidole vyako vya mkono na vidole vya mguu hukua kwa pamoja na ukuaji wa kila

mfupa hukoma katika kipindi fulani cha muda. Aidha, hili halitokei tu katika mwili wako

Page 26: Miujiza Katika Miili Yetu

bali hutokea pia kila mwili wa mtu mwenye siha. Kila mtu ana mifupa yenye kubeba sifa na

tabia hizi.

Wanasayansi wanafanya utafiti ili kutengeneza malighafi (substance) kama ile

inayounda mifupa ya mwili wa binadamu. Lakini, hakuna ambaye ameweza kutengeneza

malighafi (substance) yenye sifa na tabia za hali ya juu kama za mifupa.

Ni kutokana na huruma ya Mola wetu kwamba mifupa yetu inatuwezesha kuishi

maisha yetu kwa urahisi na kutembea sana bila kupata shida na bila kupatwa na maumivu

yoyote.

MIFUPA INAYOJITUNZA

Tulieleza kuwa kuna maungio mahali ambapo mifupa hukutana. Kwa mfano,

tunaweza kuikunja na kuinyoosha mikono na miguu yetu kutokana na maungio

yaliyopo kwenye viwiko na magoti yetu. Japokuwa hutembea katika kipindi chote cha

maisha yetu, maungio haya kamwe hayahitaji kuwekewa kilainisho. Lakini, mashine

zinahitaji matengenezo ya mara kwa mara. Kwa mfano, unatakiwa kuweka kilainisho

kwenye pedali au mnyororo wa baskeli yako mara kwa mara kwa sababu kiwango cha

mafuta hupungua kadiri yanavyotumika, jambo ambalo hatima yake ni kuizuia baskeli

isitembee. Vivyo hivyo, maungio ya mifupa yako hutumika wakati wote, lakini huna

haja ya kuyawekea kilainisho. Kwa nini?

Jawabu la swali hili limetafutwa na wanasayansi, ambao hatimaye waligundua

ukweli ufuatao: katika maungio, kuna tishu imara, ya mpira ainayoitwa “gegedu”

(cartilage) ambayo huyakinga/huyalinda maishilio ya mifupa katika sehemu

inapokutana. Kuna utando/kiwambo kinachoyazunguka maungio yote ambacho ndani

yake kuna majimaji maalumu. Pindi mfupa unapotumia shinikizo kwenye maungio,

majimaji haya hulazimishwa kutoka kwenye kiwambo hicho na maungio hupata

“kulainishwa”.

Mambo haya yote yanatuonyesha kuwa mwili wa binadamu ni matokeo ya usanifu

wa ajabu na uumbaji bora. Ni kutokana na usanifu huu wa ajabu kwamba tunaweza

kufanya harakati nyingi kwa urahisi na kwa haraka. Tabia hizi za mifupa zimeumbwa

na Mola wetu. Mwenyezi Mungu anawaita watu kwenye kutafakari juu ya uumbaji wa

mifupa:

... Iangalie hii mifupa yake jinsi tunavyoinyanyua kisha tunaivisha nyama ...

(Surat al-Baqara: 259)

MIFUPA ILIYOVUNJIKA INAPONAJE?

Tumeeleza kuwa mifupa ni migumu na imara. Lakini inaweza kuvunjika pindi

inapopatwa na pigo kali. Sasa kitu gani hutokea? Mfupa hujikarabati wenyewe.

Madktari huuandaa mfupa na kuuwekea bandeji ya piopi ili kwamba mfupa uweze

Page 27: Miujiza Katika Miili Yetu

kujiunga sawa sawa. Hakuna kazi inayobaki kwa madaktari kwa sababu mfupa

wenyewe una utaratibu wa kujirekebisha wenyewe. Ni ajabu na muujiza kwamba

mfupa uliovunjika hujiponyesha na kuwa imara zaidi kuliko hata mwanzo. Muujiza

huu hufanya kazi kama ifuatavyo:

Damu inayouzunguka mfupa uliovunjika huganda na kutengeneza "haematoma",

ambayo ni kiwango kikubwa cha damu iliyoganda. Ugandaji huu ni utandu ambao ni

sawa na kigaga kitokeacho kwenye ngozi yako baada ya jeraha. Madini yapatikanayo

ndani ya seli zinazotengeneza mifupa huubadilisha mgando huu na kuwa mfupa imara.

Awamu hii inapokamilika, seli za ufifishaji wa mifupa huingia kazini. Zikifanya kazi

kama mtaalamu wa metali (sculptor), seli hizi huupunguza mfupa huo mpya kwa asidi

ya haidrokloriki, ambayo ni asidi kali sana, na kuupa mfupa huo umbo maalum.

Mchakato huu huendelea mpaka mfupa huo unaporudi katika umbo lake la asili. Hata

baada ya mwaka mmoja, seli hizi za ufifishaji wa mifupa huendelea kuupunguza mfupa

kama wataalamu wachapakazi wa metali ili kuupa umbo.

Kama ulivyoona, kazi zote hizi zinazofanywa na seli za mifupa ambazo ni ndogo

mno kiasi cha kutoonekana kwa macho, ni dalili na alama za utaalamu na ajuzi wa hali

ya juu. Hiyo ni kwa sababu seli hazina macho, lakini zinaweza kujenga mifupa. Aidha,

zinaweza kuelewa ni wakati gani nafasi baina ya vipande hivyo viwili inatakiwa kujaza

na hivyo zinaweza kuamua wakati wa kuacha. Kisha seli zinazofifisha mfupa

zinafahamu kuwa mfupa uliojengwa upya unahitaji kusawazishwa, na huanza

kuupunguza. Ili seli ziweze kufanya hivyo, zinatumia asidi kali kuusawazisha mfupa na

kuupa umbile kwa kutumia asidi hii kwa kiwango kidogo au kikubwa kadiri

inavyotakiwa.

Kama unavyoweza kuona, seli zote za mifupa zinaelewa vizuri jambo la kufanya

na jinsi ya kulifanya. Mfumo uliotengenezwa kwa ajili ya kuiponya mifupa yetu

hufanya kazi kikamilifu na kuiwezesha mifupa kujikarabati. Kwa miaka mingi,

wanasayansi wamestaajabishwa na uwezo huu wa mifupa wenye kushangaza.

Seli za mifupa zilipata vipi uwezo huo wa ajabu unaofanya kazi moja kwa moja

bila mhusika kujua? Seli zinajua vipi kinachohotajika kukarabati mfupa uliovunjika na

hatua gani za kufanya ili kuuponya? Wakati baadhi ya seli zina uwezo wa kujenga

mifupa, nyingine zina jukumu la kuisawazisha na kuipa umbo. Nani aliyezipa kazi na

majukumu hayo? Inakuwaje kwamba hakuna vurugu na vipi kila moja inatekeleza kazi

zake kwa wakati muafaka unaotakiwa? Je seli za mifupa zilijua mambo yote haya

zenyewe?

Kwa hakika kazi hizi za ajabu haziwezi kutekelezwa kwa hiari ya seli

zisizoonekana kwa macho. Wala hazikuweza kuzijua kazi hizo. Ikifanya kazi kwa

muongozo wa Mwenyezi Mungu Mwenye hekma, seli za mifupa yetu zinaweza kuipa

umbo mifupa yetu kama afanyavyo mtaalam wa metali.

Page 28: Miujiza Katika Miili Yetu

Je umeshangazwa namna seli za zinavyotengeneza mifupa?

Maumbile ya zaidi ya mifupa 206 iliyo katika miili yetu yanatofautiana. Tofauti

hii ilianza pindi mifupa hiyo ilipotokea kwa mara ya kwanza, yaani, ulipokuwa katika

tumbo la mama yako. Seli, ambazo zilikuwa zikiongezeka kidogo kidogo kwa idadi,

zilichukua maumbo mbalimbali kutokana na eneo husika la mwili ambalo kila seli

ilitakiwa kukaa.

Baadhi ya seli ziligawanyika ili kuunda mifupa yako, nyingine kuunda ini,

nyingine kuunda mafigo na nyingine kuunda macho yako. Lakini seli zitakazounda ini,

mifupa au macho hazijikusanyi tu pamoja. Zinahitaji kugawanyika zaidi na zaidi. Kwa

mfano, seli za mifupa zinatakiwa kujua eneo la mfupa zitakazouunda ndani ya mwili.

Zinatakiwa kwenda kwenye eneo sahihi kikamilifu na kuchukua umbo sahihi.

Seli za mifupa ndani ya miguu yako hufanya kazi kama mtaalamu wa metali na

kuunda kikamilifu mifupa ya mguu iliopinda pamoja mibonyeo na uchomozaji wa

vidole vya miguu. Kana kwamba zainajua ukubwa wa ubongo, seli za mifupa

zinazotengeneza fuvu lako hujenga kiunzi laini cha mifupa ambacho huuhifadhi

kikamilifu ubongo wako. Sio dogo sana na wala sio kubwa sana, hivyo haliubani

ubongo na wala halifanyi upate shida kukiinua juu kichwa chako.

Nini chanzo cha utambuzi huu wa seli zinazoipa mifupa umbile kamili zikijua

muundo zinaotakiwa kuuchukua na tishu gani zinayotakiwa kuiunda?

Mola wetu ameuweka mpangilio huu tata ndani mwao. Ujuzi Mkuu wa Mwenyezi

Mungu umeashiriwa katika aya zifuatazo:

Na vyake Yeye vilivyo mbinguni na katika ardhi. Vyote vinamt'ii Yeye.

Na Yeye ndiye anaye anzisha uumbaji, kisha ataurudisha mara nyengine. Na

jambo hili ni jepesi zaidi kwake. Naye ndiye mwenye mfano bora katika mbingu

na ardhi. Na Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima. (Surat ar-Rum: 26-27)

Page 29: Miujiza Katika Miili Yetu

MOTA NDOGO SANA ZILIZOPO KATIKA MWILI: MISULI

Misuli ni vituo vya umeme (power stations) vya miili yetu. Kazi ya misuli ni

kubadilisha nishati kuwa umeme, kazi ambayo huifanya kikamilifu katika kipindi chote

cha uhai. Wakati fulani jambo hili huliona, lakini muda mwingi hatuitambui. Kwa

mfano, baadhi ya misuli hunywea (contract) ingawa hatufanyi juhudi yoyote kwa

uangalifu. Misuli ya moyo na ya tumbo ni ya aina hii. Kazi zake ziko juu ya uwezo na

udhibiti wetu. Misuli ambayo hunywea (contract) kwa utashi wetu imeshikamana na

kiunzi chetu cha mifupa (skeleton). Kuna misuli 650 inayofanya kazi (voluntary) katika

mwili wa binadamu. Tunapotembea, misuli hii hunywea (contract) na kulegea pamoja

na mifupa iliyoshikamana nayo.

Misuli huendeshwa na mirija ya damu na neva. Mirija ya damu hubeba oksijeni na

virutubisho kwenda kwenye miuli, huku neva zikiongoza mwendo wa misuli.

Ingekuwaje kama ungeachiwa wewe udhibiti wa misuli moja kwa moja? Fikiria,

kwa mfano, kwamba misuli ya moyo wako kuanzia leo na kuendelea inashikamana na

udhibiti wa utambuzi pekee. Hutoweza kufanya chochote zaidi ya kumakinika kwenye

unyweaji na ulegezaji wa misuli ya moyo wako. Hii ni kwa sababu kama misuli ya

moyo wako isingenywea hata kwa muda, ungekufa. Na usingeepuka kifu unapokuwa

usingizini, kwa sababu usingeweza kuudhibiti ufanyaji kazi wa moyo wako. Lakini hilo

halitokei kwa sababu huhitaji kufikiri kuhusu mambo hayo kutokana na mfumo kamili

wa udhibiti katika mwili wako.

Tunachotakiwa kufanya kuliko mambo yote ni kumshukuru Mola wetu Mwenye

huruma, aliyekifanya kila kitu kuwa rahisi kwa ajili yetu, na tufanye mambo katika

namna inayomridhisha. Mwenyezi Mungu anatupa amri ya kumuabudu Yeye pekee

yake katika aya ifuatayo:

Huyo ndiye Allah, Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu, hapana mungu ila

Yeye, Muumba wa kila kitu. Basi muabuduni Yeye tu. Naye ni Mtegemewa wa

kila kitu. (Surat al-An‘am: 102)

Misuli hufanya kazi kwa uelewano

Je wajua kuwa kuna misuli 17 usoni mwako inayonywea (contract) kwa pamoja

pindi unapotabasamu? Kama isingenywea au kufanya kazi nyingi, usingeweza

kutabasamu. Aidha, usingekuwa na muonekano wowote usoni mwako.

Kuna misuli 28 inayodhibiti muonekano wa uso wako. Kwa mnyweo wa pamoja

wa misuli hii, unaweza kutengeneza mamia ya mionekano mbalimbali. Kutokana na

misuli hii, unaweza ukaelezea na kuonyesha ghdhabu, mkanganyiko, furaha na

burudani na mionekano mingine mingi. Mbali na misuli ya usoni, pia misuli mingine

katika mwili wako hufanya kazi kwa uelewano. Kwa mfano, ili kupiga hatua moja,

misuli 54 hufanya kazi wakati mmoja. Kwa namna hiyo tunaweza kupiga mamia ya

Page 30: Miujiza Katika Miili Yetu

hatua kwa urahisi, jambo linaloonekana kuwa la kawaida kwetu. Lakini baada ya

kuyasoma yote haya, mtu anatakiwa kusimama na kutafakari, kwa sababu watu

hawachangii chochote katika utendaji kazi wa misuli hii. Kama misuli isingefanya kazi

kikamilifu, isingewezekana kupiga hata hatua moja, achilia mbali kukimbia, kuogelea

au kuendesha baskeli. Kwa hiyo, tunatakiwa kuweka akilini mwetu jambo moja la

muhimu sana: Mwenyezi Mungu aliumba mfumo kamili katika mwili wa binadamu. Hii

ni zawadi kutoka kwa Mola wetu. Tunachotakiwa kufanya ni kutafakari juu ya rehma

ya Mwenyezi Mungu isiyokuwa na kikomo, kukumbua ukuu Wake na kumshukuru.

Mikono hubeba kila kitu kwa ustadi

Kugeuza kurasa za kitabu, kufungua mlango wa gari, kuosha mikono ... Haya ni

mambo machache sana tunayoyafanya kila mara kwa kutumia mikono yetu, bila kupata

tabu yoyote. Tunatumia mikono yetu katika kufanya mamia ya matendo.

Mkono wa mwanadamu ni imara sana kiasi kwamba unaweza kutumia shinikizo

kwenye kitu chenye uzito wa kilogramu 45 (paundi 100) bila hata kukunja sana ngumi.

Mbali na nguvu hizo, tunaweza pia kuitumia mikono yetu katika matendo mzuri na

yenye kupendeza sana kama vile kutunga uzi kwenye sindano kila tunapotaka kufanya

hivyo. Wakati kundi moja la matendo likihitaji kiwango kikubwa cha nguvu, mengine

yanahitaji usahihi wa hali ya juu (strict accuracy). Hata, hatutambui hata kidogo kazi

kubwa inayofanywa na mikono yetu katika uhalisia wake. Kamwe hatuamui kutumia

nguvu ya gramu 500 (paundi 1.1) kwa ajili ya kunyanyua juu karatasi kutoka kwenye

meza au kutumia nguvu ya kilogramu 5 (paundi 11) ili ktupa mpira. Tunafanya yote

hayo moja kwa moja (automatically) bila kuwaza, kwa sababu Mwenyezi Mungu

alituumba katika namna ya ukamilifu. Ufanisi huu mkubwa wa mikono yetu ni matokeo

ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu usiokuwa na kifani.

Je wajua kuwa mojawapo ya majaribio makubwa ya wanasayansi imekuwa ni

kutengeneza mkono bandia ulio sawa na mkono wa binadamu? Mikono ya roboti

iliyotengenezwa imekuwa sawa na mkono wa binadamu katika upande wa nguvu, lakini

imekosa hisia ya kushika (kugusa) na uwezo wa kufanya kazi nyingi wa wakati mmoja.

Kwa hakika, wanasayansi wengi wana maoni kwamba haiwezekani kutengeneza

mkono wa roboti wenye uwezo wa kufanya kazi zote za binadamu. Mhandisi Hans J.

Schneebeli, aliyebuni mkono wa roboti unaojulikana kama "The Karlsruhe Hand",

alieleza kwamba kadiri alivyozidi kufanya kazi ya kutengeneza mikono ya roboti,

ndivyo alivyozidi kuustaajabia mkono wa binadamu. Aliongezea kusema kwamba

watahitaji muda mwingi kuweza kushughulia hata kazi ndogo zinazofanywa na mkono

wa binadamu.

Mikono yetu, ambayo haiwezi kuigwa hata na teknolojia ya kisasa,

imetengenezwa kwa ufanisi na Mwenyezi Mungu. Mikono hii ni ishara ya ukamilifu wa

ustadi wa uumbaji wa Mwenyezi Mungu.

Hakuna muumba mwingine tofauti na Mwenyezi Mungu. Katika aya ifuatayo,

Page 31: Miujiza Katika Miili Yetu

Mwenyezi Mungu anatuhabarisha kwamba hakuna mungu mwingine isipokuwa Yeye

tu na anawaambia wale wasiouona ukweli huu:

Sema: Ni nani Mola Mlezi wa mbingu na ardhi? Sema: Mwenyezi Mungu.

Sema: Basi je, mnawafanya wenginewe badala yake kuwa ni walinzi, nao

hawajifai wenyewe kwa jema wala baya? Sema: Hebu kipofu na mwenye kuona

huwa sawa? Au hebu huwa sawa giza na mwangaza? Au wamemfanyia Mwenyezi

Mungu washirika walio umba kama alivyo umba Yeye, na viumbe hivyo

vikawadanganyikia? Sema: Mwenyezi Mungu ndiye Muumba wa kila kitu. Na

Yeye ni Mmoja Mwenye kushinda!.’ (Surat ar-Ra‘d: 16)

Page 32: Miujiza Katika Miili Yetu

KIBORESHA HEWA KINACHOFANYA KAZI NDANI YA MIILI YETU BILA

KUSIMAMA

Kupumua ni mojawapo ya matendo unayoyafanya kwa siku nzima bila kutambua.

Michakato mingi hutokea katika hatua hii, ambayo pua, koo na mapafu yanahusika.

Kwa kweli, kuvuta pumzi ina maana ya kuzalisha seli za mwili wako kwa oksijeni. Seli

haziwezi kuishi mpaka zipate oksijeni. Ndiyo maana unaweza kuizuia pumzi yako kwa

muda mfupi pekee. Iwapo muda huo utakuwa mrefu, seli zako zitakufa na hatimaye

mwili wako utakufa.

Hewa unayovuta husafishwa kwanza ndani ya pua yako. Pua yako, ambayo

hutekeleza kazi ya kuboresha hewa, imewekewa nywele zinazofanya kazi kama chujio.

Nywele hizi huifanyia mchakato hewa iliyochafuliwa au hewa baridi ili kuifanya

ikubaliane na mapafu. Ni kutokana na nywele hizi kwamba hewa tunayoingiza ndani

huwa imechujwa, imesafishwa, imewekewa unyevunyevu (humidified), imewekewa

uvuguvugu na kutakaswa dhidi ya bakteria. Kwa hakika, nywele hizi nyembamba

huilinda miili yetu dhidi ya chembechembe zipatazo bilioni 20 za vitu vinavyotoka nje

kila siku.

Bilioni ishirini ni karibu mara 3 ya idadi ya watu wote ulimwenguni. Ni mchakato

mkubwa sana ambao pua inautambua na ni kwa jinsi gani inavyochambua

chembechembe nyingi kiasi hicho zitokanazo na mada (matter) za nje. Chembechembe

bilioni ishirini za mada za nje haiyumkini zitambuliwe na zizuiwe kuingia puani kwa

bahati nasibu/sadfa. Hii inaonyesha wazi ukuu wa uwezo wa uumbaji wa Mwenyezi

Mungu. Hata hivyo, baadhi ya watu hudai kuwa mambo haya hutokea kwa bahati

nasibu, hata kama wanaujua vyema ukweli. Watu hao wanaoiamini nadharia ya

mageuzi yenye kuendelea (evolution theory), wanadai kuwa viumbe hai vyote, ikiwemo

kila kitu tulichokizungumzia hapo nyuma katika hiki kitabu, vilitokea mara moja/papo

kwa papo na kutokana na matukio yasiokuwa na utaratibu maalumu yaliyotokea hapo

zamani. Je, wajua kwa nini wanadai hivyo? Wanadai hivyo ili kukanusha uwepo wa

Mwenyezi Mungu. Na ili kufanya hivyo wanadhani kuwa kuna njia moja tu, nayo ni

kudai kuwa kila kitu hutokea kwa bahati nasibu. Lakini, ni rahisi sana kuelewa jinsi

madai hayo yasivyokuwa na maana. Sasa tuufanye mfumo uliopo ndani ya pua kama

mfano ili kukanusha madai haya.

Mfumo wa kuboresha hewa (air conditioning system) unaopatikana ndani ya pua

ni eneo lingine lenye kushangaza la mwili wa binadamu. Kwa hakika mfumo huo

unaofanya kazi kwa ukamilifu usingetokea kutokana na bahati nasibu/sadfa. Kufanya

ulinganisho kutatusaidia kuelewa vyema namna jambo hilo lisivyowezekana. Fikiria

kiyoyozi/kiboresha hewa (air conditioner), kinachodhibiti hali ya joto ili kukulinda

dhidi ya joto kali wakati wa majira ya joto / kiangazi na kukupatia joto wakati wa

majira ya baridi, na mabacho kinaendeshwa na kifaa maalumu. Je mfumo huo unaweza

kuwa umetokea kwa bahati nasibu? Kitu gani kitatokea iwapo vifaa vyake

Page 33: Miujiza Katika Miili Yetu

vitatenganishwa na kuachwa katika hali hiyo? Je vitaweza kujileta pamoja na

kubadilika kuwa kiyoyozi kamili?

Kwa hakika hapana. Kwani ili mashine yoyote iwepo, lazima mtu fulani mwenye

utaalamu aitengeneze. Hili ni jambo lisilopingika hata kidogo. Achilia mbali mashine,

hata katika fumbo la mlinganisho (jigsaw puzzle) lazima mtu avikusanye vizuri vipande

husika ili kupata picha. Pua yako, ambayo hufanya kazi kama kiyoyozi, nayo pia

inaundwa na vijenzi (components) na ina mfumo uliokamilika zaidi kuliko kiboresha

hewa /kiyoyozi chochote ulimwenguni. Kama ambavyo kiyoyozi hakiwezi kutokea kwa

bahati nasibu, hata pua ambayo ni ya hali ya juu zaidi haiwezi kuwa hivyo. Ukweli huu

unatuonyesha kuwa kiungo hiki kijulikanacho kama "mfumo bora wa uboreshaji hewa

kuliko mifumo yote ulimwenguni", kimeumbwa na Mola wetu. Mwenyezi Mungu

anasisitiza juu ya sifa yake ya kuwa Muumba katika aya ifuatayo:

Yeye ndiye Mwenyezi Mungu, Muumbaji, Mtengenezaji, Mtia sura, Mwenye

majina mazuri kabisa. Kila kilioko katika mbingu na ardhi kinamtakasa, naye ni

Mwenye kushinda, Mwenye hikima (Surat al-Hashr: 24)

NN yy ww ee ll ee kk oo oo nn ii zz ii nn aa zz oo ww ee zz aa kk uu tt oo aa mm aa ee ll ee kk ee zz oo bb ii ll aa

kk uu kk oo ss ee aa

Hewa inayosafishwa puani husonga mbele kupitia kwenye mashine ya kupumlia

(respiratory tract). Eneo la pili kwa hewa iliyovutwa baada ya puani ni kooni. Katika

hewa hii bado kunakuwa na mada kutoka nje - kama vile vumbi - ambazo zina madhara

kwa afya ya mtu. Kwa hiyo, ni muhimu hewa iliyovutwa ipite katika ukaguzi mwingine

wa kiuslama kabla haijafika kwenye mapafu. Usalama huu hutekelezwa na tabaka lenye

utelezi lililopo juu ya mashine ya kupumlia (respiratory tract). Utando huu hujulikana

kama mucous layer.

Utelezi (mucous), unaounda utando huu, huzitambua chembechembe ndogo kama

vumbi ambazo tumezivuta pamoja na hewa na huzizuia zisiweze kuingia kwenye

mapafu. Lakini, mbali na hayo, mada hizo zilizoingizwa kutoka nje lazima pia

ziondolewe mwilini. Katika hatua hii, mtambo mwingine wa usalama huingia kazini.

Mtambo huu unaundwa na vitu vidogovidogo vinavyofanana na nywele vijulikananvyo

kama cilia, ambayo iko chini ya mucous layer. Nywele hizi ndogo ndogo hupiga juu

kwa mpangilio kuelekea mdomoni. Hii inaweza kufananishwa na mashuke ya ngano

zinazopeperuka angani kwa uelekeo mmoja. Kutokana na harakati hii ya cilia

(vinyweleo), mucous, ambayo huzishikilia mada kutoka nje, hupandishwa juu kooni.

Pindi mada hizi ngeni zinapopelekwa juu kooni, moja kwa moja unahisi kuwa

unataka kuzimeza. Hivyo mada zote ngeni ambazo zingeweza kuidhuru afya yako

hupelekwa tumboni ambapo huko humomonyolewa na kuharibiwa na majitumbo

(gastric juice).

Vinyweleo (cilia) vilivyopo kooni havina macho ya kuona wala havina ubongo wa

Page 34: Miujiza Katika Miili Yetu

kuvipa uwezo wa kiakili. Lakini vinaweza kutambua eneo la koromeo ambalo liko

mbali sana kwa kulinganisha ukubwa wa vinyweleo hivyo. Aidha, vikiwa vinajua

uwezekano wa madhara ya mada ngeni, haviziruhusu kuingia mwilini. Licha ya miaka

mingi ya utafiti wa kisayansi, utaratibu wa ufanyaji kazi wa nywele hizi

haujagunduliwa kikamilifu. Lakini kumbuka kuwa hizi nywele, ambazo mfumo wake

bado haujagunduliwa kikamilifu, zimekuwa zikifanya kazi kwa ukamilifu kama ilivyo

kwa vijenzi vingine vya mwili tangu mwanadamu wa kwanza alipoumbwa kwenye uso

wa ardhi.

HEWA ILIYOVUTWA SASA IKO MAPAFUNI ...

Hewa inayokuja mapafuni iko tayari kwa matumizi baada ya kusafishwa na

unyevunyevu wake umedhibitiwa ndani ya koo. Kwa njia ya mzunguko wa damu

kutoka kwenye mapafu, hufikishwa kwenye seli zote za mwili ili izirutubishe. Wakati

huohuo hupokea kaboni dayoksaidi, ambayo ni mali ghafi isiyotumika (iliyoharibika).

Tunapotoa pumzi, tunatoa nje hii kaboni dayoksaidi inayokusanywa kutoka kwenye seli

zetu.

Waweza kudhani kuwa kupumua ni mchakato rahisi, lakini mabadilishano

muhimu ya oksijeni na kaboni dayoksaidi hufanyika katika kina cha ndani ya mwili

wako. Yote haya ni zawadi za Mwenyezi Mungu kwetu sisi; aliviumba vyote na

kuvifanya vitutumikie. Fikiria ingekuwaje lau kama hata upumuaji mdogo ungewekwa

chini ya udhibiti wetu. Tusingeweza kufanya kazi hii bila kukosea. Tungechoka na

hatimaye baada ya muda mfupi tungeacha. Mola wetu anajua kwamba hatuwezi

kufanya kazi hii sisi wenyewe. Hivyo akaumba mfumo wa upumuaji unaofanya kazi

kikamilifu kama ilivyo kwa mifumo mingine tuliyoielezea ndani ya kitabu hiki. Hii ni

mojawapo ya tunu ambazo Mwenyezi Mungu ametujaalia katika hii dunia. Kama

anavyoeleza katika aya hii:

Na akakupeni kila mlicho muomba. Na mkihisabu neema za Mwenyezi

Mungu hamwezi kuzidhibiti. Hakika mwanaadamu ni dhaalimu mkubwa,

mwenye kuzikufuru neema. (Surah Ibrahim: 34)

Page 35: Miujiza Katika Miili Yetu

HITIMISHO

Ndani ya kitabu hiki tumetoa baadhi ya mifano na kueleza kuwa kuna kazi nyingi

zinazofanyika ndani ya miili yetu bila ya sisi kuwa na taarifa hata kidogo. Kila kiungo

na kila seli ya miili yetu hukimbia kwa kasi ya ajabu na wakati huo huo ikifanya kazi

kwa ukamilifu. Vyote hufanya kazi vilivyopangiwa kwa uelewano. Damu huendelea

kuzipelekea seli kirutubisho kinachohitajika ili ziendelea kuishi. Tumbo na matumbo

hukivunjavunja kirutubisho hiki katika vipande mbalimbali na kukifanya kiwe ni

chenye kufaa kwa matumizi ya seli. Seli za neva huendelea kutuma viamshi (stimuli)

kwenye maeneo yote ya mwili; ubongo huvitathmini viamshi hivi, na matokeo yake

tunaweza kuona, kusikia, kuonja na kutambua hisia nyingine zote.

Mojawapo katika kazi hizi inapocheleweshwa au kutofanywa, nidhamu ya

kawaida ya utendaji kazi wa mwili huharibika. Kama seli za neva zikiathirika/

kupungua nguvu midomo yetu haitafanya kazi; kama seli za tumbo zikiathirika,

hatuwezi kusaga chakula tunachokula; kama seli zilizopo katika ulimi zikiathirika,

hatuwezi kuonja keki za chocolate, machungwa au ndizi tunazokula. Lakini hakuna

hata kimoja kinachotokea, isipokuwa katika hali fulani ya maradhi. Kila kiungo cha

mwili wako kinaendelea kufanya kazi zake za kawaida bila kusimama huku wewe

ukiendelea kufurahia maisha yako ya kila siku. Ukamilifu ambao umejaaliwa katika

kila hatua ya maisha yako bila shaka ina chanzo na sababu. Hakuna kinachoweza

kujianzishia chenyewe na kuwa na mfumo kamili na usiokuwa na kasoro kama huo.

Runinga, friji, kompyuta, kalamu unazotumia kuandika, kwa ufupi kila kitu kina

aliyekibuni na kukitengeneza. Gari au ndege haiwezi ktokea yenyewe. Utendaji kazi

wake umewezeshwa na wahandisi na mafundi waliovibuni na kuzitengeneza. Hali

ikiwa hivyo, haiwezekani kabisa kwa mfumo kamili kama wa mwili wa binadamu

utokee kwa bahati nasibu.

Lazima utakuwa unashangaa kwamba inakuwaje baadhi ya watu wanadhani kuwa

miili yao inafanya kazi kwa ukamilifu wa namna hiyo kutokana na bahati nasibu. Kwa

hakika madai haya ndiyo madai yasiyoingia akilini hata kidogo kuliko madai yote

yanayoweza kutolewa. Nidhamu bora katika mwili wa binadamu isingeweza kutokea

kwa bahati nasibu. Nidhamu hii bora inathibitisha kwamba imewekwa na Mwenye

uelewa na hekma ya hali ya juu. Ni uumbaji wa Muumba mkuu, Mola wetu.

Mwenyezi Mungu anatuhabarisha ndani ya Qur'an kuwa Yeye ni Mwingi wa

rehma na huruma kwa waja wake. Tunachopaswa kufanya ni kuwa wenye kujisalimisha

kwake, kumtii moja kwa moja na kumshukuru kwa neema zote ambazo ametujaalia.

Katika aya ya Qur'an, Mwenyezi Mungu anatueleza yafuatayo:

Huyo ndiye Allah, Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu, hapana mungu ila

Yeye, Muumba wa kila kitu. Basi muabuduni Yeye tu. Naye ni Mtegemewa wa

kila kitu. (Surat al-An‘am: 102)