www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 1 KITABU: NGUZO MAMA MWANDISHI: PENINA MUHANDO WACHAPISHAJI: DUP MWAKA: 1982 UTANGULIZI Tamthiliya ya Nguzo Mama iliyoandikwa na Penina Muhando inayasawiri na kuyaelezea matatizo mbalimbali yanayowakabili na kuwaelemea wanawake wengi wa Tanzania na Afrika kwa ujumla. Wanawake wengi wamekuwa wakinyanyasika kwa kunyanyaswa na kuteswa na waume zao. Penina Muhando anathibitisha hayo kwa kutueleza maisha waliyokuwa wakiishi wanawake wa Patata. MAUDHUI DHAMIRA KUU: UKOMBOZI WA MWANAMKE Penina Muhando ndani ya kitabu hiki cha Nguzo Mama anaelezea na kuonesha juhudi mbali mbali zifanywazo na wanawake katika kujikomboa kutoka minyororo ya utumwa wa mwanaume na manyanyaso mazito anayoyapata kutoka kwa mwanaume na jamii nzima inayomzunguka. Mwandishi, baada ya kusawiri maisha halisi ya mwanamke wa Kiafrika na manyanyaso anayoyapata kama vile kupigwa, kufanyishwa kazi kuliko uwezo wake, mfano :- kulima peke yake, kufua, kuosha vyombo, kukusanya kuni n.k., anaamua kutumia kipaji chake kuelezea jinsi gani mwanamke anaweza kujikomboa. Katika kitabu cha Nguzo Mama, mwandishi anawaonesha wanawake wa Patata wahangaikavyo katika kujikomboa. Ukombozi huo umegusa nyanja zote za maisha yaani kisiasa,
30
Embed
KITABU: NGUZO MAMA MWANDISHI: PENINA MUHANDO …€¦Bi Nne naye hakuwa nyuma katika kazi yake ya ualimu. Akaanzisha Umoja wa Walimu, nia ikiwa kuwasaidia kutatua matatizo yao mbalimbali
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 1
KITABU: NGUZO MAMA
MWANDISHI: PENINA MUHANDO
WACHAPISHAJI: DUP
MWAKA: 1982
UTANGULIZI
Tamthiliya ya Nguzo
Mama iliyoandikwa na Penina Muhando inayasawiri na kuyaelezea matatizo
mbalimbali yanayowakabili na kuwaelemea wanawake wengi wa Tanzania na
Afrika
kwa ujumla. Wanawake wengi wamekuwa wakinyanyasika kwa kunyanyaswa na
kuteswa
na waume zao. Penina Muhando anathibitisha hayo kwa kutueleza maisha
waliyokuwa
wakiishi wanawake wa Patata.
MAUDHUI
DHAMIRA KUU: UKOMBOZI WA
MWANAMKE
Penina Muhando ndani ya kitabu hiki cha Nguzo Mama anaelezea na kuonesha
juhudi
mbali mbali zifanywazo na wanawake katika kujikomboa kutoka minyororo ya
utumwa
wa mwanaume na manyanyaso mazito anayoyapata kutoka kwa mwanaume na
jamii nzima
inayomzunguka. Mwandishi, baada ya kusawiri maisha halisi ya mwanamke wa
Kiafrika na manyanyaso anayoyapata kama vile kupigwa, kufanyishwa kazi kuliko
uwezo wake, mfano :- kulima peke yake, kufua, kuosha vyombo, kukusanya kuni
n.k., anaamua kutumia
kipaji chake kuelezea jinsi gani mwanamke anaweza kujikomboa. Katika kitabu
cha
Nguzo
Mama, mwandishi anawaonesha wanawake wa Patata wahangaikavyo katika
kujikomboa. Ukombozi huo umegusa nyanja zote za maisha yaani kisiasa,
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 2
kiuchumi
na kijamii.
Kiuchumi katika kujikomboa, wanawake wa Patata wanaamua
kuanzisha miradi mbalimbali ambayo itawawezesha kujipatia fedha kwa ajili ya
maendeleo. Miradi ikashamiri sehemu zote za Patata.
‘’……….Miradi tutatilia
mikazo, miradi ya kila aina vilabu vya pombe, maduka ya khanga, ushirika wa
kushona, kupika, hoteli na mengi……..’’(uk 52).
Bila Pili yeye akaamua kuanzisha kilabu cha pombe ili
aweze kujikomboa kwenye maisha magumu yanayomkabili.
„’Kaamua Bi
Pili, Pombe kujipikia, na kilabuni kuiuza
Pesa akipata, Pesa msema
kweli
Na nguzo mama itasimama’’ (uk 14).
Mwandishi anaonesha umuhimu wa pesa katika kujikomboa
kwa wanawake, kwani pesa ndio hasa iletayo maendeleo stahiki. Hali kadhalika Bi
Moja na wenzake nao wakajiunga na kuanzisha viwanda vyao vya kufuma
mapambo ya
nyumbani.
„‟Kutokea Bi
Moja, Na lake jipya kiwa nda kuanzisha
Mapambo ya nyumbani kufuma
Mapambo akiyauza na pesa
kujipatia
Itakuwaje nguzo mama
isisimame’’ (uk 17).
Kijamii, wanawake wa Patata wamehamasika kwa kuanzisha
vikundi vya akina mama, ambavyo vitasimama imara kutetea maslahi yao na
kusaidiana wao kwa wao katika kujikomboa. Mfano mzuri ni kikundi lcha kina Bi
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 3
Nne, yeye alikuwa kiongozi wa umoja huo akiwahamasisha wanawake wenzake ili
waweze kuinua „‟nguzo Mama‟‟
„’Bi Nne anapiga
makofi nao
Anasimama na kutoa hotuba
Nguzo mama hoyee’’ (uk 11).
Bi Nne naye hakuwa nyuma katika kazi yake ya ualimu.
Akaanzisha Umoja wa Walimu, nia ikiwa kuwasaidia kutatua matatizo yao
mbalimbali yanayowakabili katika ufundishaji, Bi Nne anawashauri walimu
wenzake
kuanzisha umoja huo ili kwanza waanze na matatizo yao yanayowakabili katika
hatua ya kujikomboa kama wanawake.
„’Kutokea Bi
Nne, wenzake wengi
Makubwa hawakujitakia,
vizuri walishauri
Tuanze na yetu matatizo,
Ndani yah ii yetu kazi
Kazi yetu ya kufunza vyema
kuichapa
Vigingi vikitokomea, vyema vijana watafunzika
Wakifunzika wote Patata
‘’Nguzo Mama itasimama’’ (uk 20).
Hapa Penina Muhando anaonesha elimu kama njia moja
wapo itakayoweza kuwakomboa wanawake pale aliposema;
„’Vigingi
vikitokomea, vyema vijana watafunzika, wakifunzika wote Patata nguzo mama
itasimama’’
Mwandishi pia anaonesha ushirikianao wa jamii nzima,
wanawake kwa wanaume kutasaidia sana katika kuleta ukombozi wa mwanamke
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 4
na
mwanamke peke yake, abadani hatoweza kusimamisha „’Nguzo Mama’’
‘’Bi Nane ‘’Tushirikishe
wanaume pia. Nguzo mama ina faida kwa wote
Tuite na watoto wote faida
kwa wote – wao taifa la kesho’’
Kwa hiyo, mwandishi licha ya kuonesha utakiwaji wa
jamii nzima katika ukombozi wa mwanamke, pia anaonesha faida za ukombozi
huo
hazitamlenga mwanamke tu bali na jamii nzima inayomzunguka mwanamke.
Pia umoja nao unachorwa na kuoneshwa kama njia
itakayowezesha wanawake waweze kujikomboa.
„’Bora tufanye
mikutano
Labda na maandamano
Maazimio tuyatangaze
Tukupambeje maua’’ (uk 7).
Mikutano kama ilivyo kawaida yake ingewezesha
kuwapasha watu wengi zaidi juu ya ukombozi wa mwanamke na manyanyaso
wapatayo.
Hivyo watu wengi wangehabalishwa katika uwanja wa siasa. Nafasi za uongozi
kwa
wanawake ni moja kati ya njia ambazo zingemwezesha mwanamke kujikomboa.
Katika tamthiliya hii, mwandishi anaonesha juhudi
mbalimbali zifanywazo na wanawake wa Patata katika kuchukua uongozi wa
Serikali.
„‟………Akina
mama watapewa vyeo, orodha tumeshapanga. Tutapata mawaziri, mameneja,
mabalozi
na kadhalika. Wengine tayari wameshapata kama mnavyofahamu’’ (uk 52).
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 5
Baadhi ya wanawake ambao walipata uongozi ni Bi Nne
ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya vyeo.
„‟He! Kweli nimekumbuka looo!
Nimechelewa mkutano wa kamati ya vyeo
Na mimi ndiye mwenyekiti, si
mnajua tunavyokazana kuwaombea mabibi vyeo maana wanasahauliwa. Lazima
tufanye
huo mkutano’’ (uk 42).
Bi Tatu yeye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya malezi
bora
„’My God !
Mmeona! Tena Shangazi mwenyewe ndiye mwenyekiti wa malezi bora’’ (uk 50).
Ukombozi wa fikra pia umeoneshwa kama tatizo linalowasumbua
wanawake wa Patata. Mfano anamuonesha Bi Nane dhidi ya madai aliyoambiwa.
Bi
Nane hasa alipokubaliana na kila kitu alichoelezwa na Bi Nne.
DHAMIRA NDOGONDOGO
1.
UONGOZI MBAYA
Uongozi mbaya ni kati ya dhamira zilizooneshwa kwenye
tamthiliya ya Nguzo Mama. Mwandishi wa tamthiliya hii, Penina Muhando
anaanza
kwa kuonesha umuhimu wa kiongozi katika jamii yoyote ile. Pia anaonesha
kiongozi kama mtu aliyeshikilia jamii anayeweza kuipeleka jamii anayeweza
kuipeleka jamii yake kwenye neema au mdomo wa samba kutegemeana na
uongozi wake
atakavyokuwa anaupeleka.
„‟……..Tena
kwetu sie kiongozi huongoza njia
Aweza kuwapeleka kwenye
neema
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 6
Au mdomoni kwa samba……..‟‟ (uk 22).
Lakini viongozi hao, wengi wao wamekuwa wakizipeleka
jamii zao kwenye mdomo wa samba, kwani viongozi hao hutumia uongozi kama
dhama
ya kuonesha wao ni watu watukufu na walio kwenye daraja la juu katika jamii.
Wakiamuawatakavyo bila kufuata miongozo iliyopo katika uongozi huo.
„‟ Bi Nane
akawaza
Kumbe kazi hii ya uongozi au
uwenyekiti
Inampa mtu uwezo wa kufanya
Mambo kinyume cha
kawaida……‟‟ (uk 24).
Penina Muhando anaonesha uongozi mbovu kama ndio
chanzo cha matatizo yanayoikabili jamii ya Wanapatata. Viongozi kama akina Bi
Nne na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashauri, wanaoneshwa kama viongozi
wabovu
wanaosababisha kuwa na matatizo katika jamii ya Patata.
„‟ Lahaula!
Kumbe ndio maanawatu wengi wanaulilia uwenyekiti, kwani ni rahisi kazi yake,
kiholela mambo kujifanyia masikini Patata si ajabu kumbe vurugu kutapakaa’’
(uk 25).
Mwandishi anaonesha vurugu zinazoisonga Patata kuwa
zimechangiwa na uongozi mbovu. Udikteta pia unaoneshwa kuwa ni zao la
uongozi
mbovu uliopo kwenye jamii ya wana Patata. Viongozi kama mwenyekiti wa
kamati ya
mashauri wamechorwa kama madikteta, wanaotumia uongozi wao watakavyo,
wajisikiavyo kutoka mioyoni mwao au vile waambiwavyo na watu wao wa karibu
bila
kufuata misingi na miongozo waliyowekewa
na katiba ya jamii zao. Mwenyekiti wa kamati ya mashauri anatumia vitisho
kumlazimisha Bi Nane kusemaasichokijua ili mradi tu yeye ni kiongozi. Pia
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 7
mwenyekiti anaonesha udikteta wake pale alipotaka kuamua kesi aliyosikiliza
upande mmoja tu wa mashtaka, tena maelezo hayo kapewa wakati mshtakiwa
hayupo.
„‟……..Vipi
mtu atakubali kutoa ushauri kutumia vitisho!
Kufuatilia maelezo ya
mshtaki peke yake
Tena yaliyoelezwa wakati
mshtakiwa hakuwepo
Vipi mtu atamshauri
mshtakiwa
Bila kujua mawazo yake’’ (uk 24).
Pia mwandishi anaonesha udikteta uliokithiri
unavyoitawala jamii ya Patata, yaani mtu mmoja anaweza kuamua maamuzi
yanayotakiwa
kufanywa na kamati nzima. Tena ajifanyiaye mambo bila kushirikisha kamati hiyo.
Mfano ni pale mwenyekiti wa kamati ya mashauri walipokaa na kuunda kamati ya
watu wawiliili wamshitaki Bi Nane.
„‟ ….Vipi watu hawa, wawili, moja, mbili kujifanya wao
kikao.
Katiba gani inasema
mwenyekiti peke yake
Awe na kikaocha kuamua
mashauri
Au asaidiane na mtu si
mwanakamati
Mwenyekiti na mshtaki kuwa kikao?!
Sijapata kusikia, hiki ni
kikao cha hila.
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 8
Kusema sitajisumbua, kimya
akijikalia’’ (uk 24).
Mwandishi anaendelea kutuonesha maajabu ya uongozi
mbaya ya wana Patata ulivyokithiri, kwani wale viongozi walikuwa
wanategemewa
ndio haohao wanaofanya mambo ya ajabu.
„’Na ajabu
kupita yote
Vipi mwenyekiti bila kamati
Akatoa ushauri katika
mashtaka?’’ (uk 25).
Hapa msimulizi alikuwa anaendelea kutuonesha jinsi
mambo yalivyo mabaya hapo Patata.
Kwa wema na huruma
‘’Mwanangu mie sijui labda
kamuulize Bi Nne’’
(uk 54).
Chizi anamshangaa Bi Saba, kwani licha ya kuwa
kiongozi hajui hata ninimaana ya Nguzo Mama. Chizi anaendelea kusema;
‘’Lakini juzi kachaguliwa
katibu
Sijui wa kamati gani ile.
Nimesahau’’ (uk 55).
2.
DHULUMA
Penina Muhando anaitumia vyema kazi yake ya usanii
kueleza tatizo la dhuluma lilivyoigubika jamii yetu ya leo. Katika tamthiliya
yake ya Nguzo Mama anajaribu kutuonesha jinsi jamii ya Patata, kama zilivyo
jamii nyingine, ilivyooza kwa dhuluma, hasa kwa wanawake wajane pindi tu
wanapofiwa na waume zao.
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 9
Katika tamthiliya ya Nguzo Mama, mwandishi anatumia
mhusika wake Bi Saba kuonesha jinsi ganiwanawake wengi wa Kiafrika
wanavyodhulumiwa mali na ndugu za waume zao pindi tu wanapofariki. Bi Saba
baada ya tu ya kufiwa, shemeji walikuja na kugawana vitu vya Bi Saba pasipo
kumuachia hata kitu. Watoto nao walichukuliwa, wakimwacha Bi Saba masikini
akihangaika huku na kule bila mafanikio.
‘’ Haa! Shemeji mmerudi
kuchukua hata kitanda!
Hata sufuria! Nitalala wapi
na nitapika wapi jamani?’’
(uk 43).
Mwandishi anaendelea kueleza uozo wa dhuluma ndani ya
Patata ilivyoletamatatizo na huzuni kwa wanaodhulumiwa huku wakikosekana
watu
wa kuwasaidia, hakuna mtu wa kumsaidia mwenzak, dhuluma imetapakaa kila
mahali
Patata.
„’Akalia Bi Saba
tena akalia, hana wa kumsaidia
Mumewe kafa nduguze wamekuja
juu,
Pesa wamechukua senti tano
haikubaki
Vyombo na nguo zote wakagawana
Roho ikampasuka Bi Saba
kuwaona hao ndugu
Walivyogombania mali wasiyochuma
„’Kiti hiki
changu’’ Mie lile jembe’’
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 10
‘’Mie suruali hizi’’ ili
mradi ilikuwa zogo’’
(uk 43-44).
Mwandishi pia anaelezea juu ya dhuluma, kwa kitu au
mali uliyoichuma kwa jasho lako mwenyewe, ukahangaika huku na kule kutafuta
mali hiyo lakini mwisho wanakuja wachache kukudhuluma mali hiyo. Mfano Bi
Saba.
Uongozi mbaya pia umesababisha kuondoka kwa demokrasia
kwa watu wa Patata, kwani wachache wenye
madaraka ndio wanaoonekana kupewa kipaumbele kuzidi wenzao,
wanaowaongoza.
Mfano ni pale Chizi alipokuwa anamuuliza Bi Nne akimwonesha kuwa yeye ni
mtu
mkubwa na anapewa kipaumbele zaidi. Ansema;
‘’…….Lakini bibi yangu
aliniambia
Binadamu wote sawa, lakini
wengine ni sawa zaidi.
Na huyu ni mmoja wa hao’’ (uk 58).
Pia mwenyekiti wa kamati ya mashauri hafuati demokrasia inayotakiwa kwa
kumlazimisha na
kumpa masharti yaliyo kinyume kabisa na katiba,yenye kuonesha udikteta
uliokithiri usiofuata na unaoepuka kibisa demokrasia .
„’ Jambo la pili
nakueleza kuwa hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kufanya mkutano bila kibali
cha
ofisi hii. Na ofisi hii lazima iletwe kumbukumbu za mikutano yote iliyofanyika
hapa Patata. Sheria hii ipo na inajulikana kwa hiyo urudi ufuate mashauri
yangu’’ (uk 25).
Viongozi wa Patata wanaoneshwa pia viongozi wasiopenda kuwajibika katika
kufanya kazi za
kuliletea taifa lao maendeleo yao, wawapo tu! Kazi kuongea maneno
yasiyotekelezwa. Mfano ni Bi Tatu, yeye ni kiongozi wa malezi bora lakini
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 11
ameshindwa hata kulea watoto wa kaka yake anayehangaika mtaani (chizi). Pia
anashindwa hata kujishughulisha kufanya vijibiashara.
„’My God!
Mmeona! Tena Shangazi mwenyewe ndiye mwenyekiti wa kamati ya malezi bora
yeye
mwenyewe hafanyikazi…..‟‟(uk 50).
Licha ya kuwa kiongozi wa Patata hawapendi kuwajibika,
lakini pia wanaoneshwa kama wasiokuwa na elimu, na wasiojua nini kinaendelea
hata kwenye uongozi wao. Viongozi kama hawawezi kubadilisha kama jamii
yoyote ile kama ilivyo kwa jamii
ya Patata. Chizi anasema;
„‟…..Siku moja nikamwendea, labda niwe kweli chizi
‘’Shikamoo’’ ‘’Marhaba’’ Bi
Saba nieleze.
Nini kitu Nguzo Mama, naona hapa Patata mambo
yamevurugika, kila ninakogeuka nasikia nguzo mama, Nguzo Mama kitu gani?
Vizuri, alijibu.
Yeye alihangaika huku na kule ili ajiletee maendeleo
yake nay a watoto wake, lakini bado mumewe alipofariki nduguze wakaja na
kumdhulumu jasho halali.
„’Atawaambiaje
watu hawa,
Kuwa vyote walivyochukua
Zaidi ni jasho lake
Watoto wake wapenzi mwenyewe
aliwalea
Wakati wao baba mnatindi
akiyachapa
Na pesa kwa pombe kuangamiza
Pesa ya ndugu yao iliishia
chooni’’ (Uk 44).
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 12
3.
ELIMU
Katika tamthiliya hii ya „‟Nguzo Mama‟‟, dhamira ya
elimu inaoneshwa kama jambo la muhimu sana kwenye maendeleo ya jamii yoyote
ile. Mwandishiameonesha kuwa kila nyumba ya mafanikio au maendeleo yoyote
yale
kuna elimu. Bi Nne anakubaliana na ukweli huu pale alipokuwa anasisitiza somo
la ushonaji liingizwe kwenye mitaala ya wanafunzi mashuleni ili waweze
kujifunza kushona vitu mbalimbali kama mapambo na nguo. Kisha wauze wapate
maendeleo.
„’……….Pia somo
la ushonaji litatiliwa mkazo mashuleni. Kila shule italifundisha ili watoto
wetu wajue kushona, wavae vizuri na kupamba nyumba zao vizuri’’ (uk 18).
Bi Nane naye anaonesha na kuthibitisha ukweli juu ya
umuhimu wa elimu kwa maendeleo ya jamii ya Patata. Yeye anaonesha kuwa
kama
watu hawatopata elimu, basi hata maendeleo hawatayasimamisha yakasimama.