Top Banner
www.inclusion-international.org Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa akili kushiriki katika masuala ya kijamii na harakati za kisiasa. Warsha kwa ajili ya Watetezi Binafsi (Watu Wenye Ulemavu wa Akili) na Familia zao Tarehe 31 Julai 2015, Zanzibar
40

Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Sep 25, 2020

Download

Documents

dariahiddleston
Welcome message from author
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
Page 1: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

www.inclusion-international.org

Sauti Yangu Isikilizwe!

Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa akili

kushiriki katika masuala ya kijamii na harakati

za kisiasa.

Warsha kwa ajili ya Watetezi Binafsi (Watu

Wenye Ulemavu wa Akili) na Familia zao

Tarehe 31 Julai 2015, Zanzibar

Page 2: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Utaratibu wa Uwasilishaji

• Utangulizi

• Madhumuni, Malengo na Matarajia ya Mradi

• Ukweli juu ya WWUA duniani

• Ushirikishwaji wa WWUA katika Siasa

• Wajibu wa Serikali

• Uchaguzi Jumuishi

• Mambo yanayopelekea Ujumuishi

• Vikwazo na Vihunzi – Tulichojifunzo

• Tathmini ya Warsha

Page 3: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

“Piga kura na mimi nipige

Kama mimi sistahiki kupiga kura na wewe

pia hustahiki, Amua!!!”

Page 4: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Kwa nini tupo hapa? Kuhamasisha ushiriki wa watu wenye ulemavu wa akilikatika harakati za kisiasa.

Warsha hii inalenga :

Kutoa elimu kuhusu namna ya kushiriki katika harakati zakijamii kwa familia, watetezi binafsi na jumuiya za familia zawatetezi binafsi

Kuweka mikakati ya kuongeza ushiriki wa watu wenye ulemavuwa akili katika harakati za kisiasa

We gratefully acknowledge the UN Democracy Fund for its support of this project, Accessing the Ballot Box.

Page 5: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Makaribisho na Utangulizi

– Je! Wewe ni NANI?

– Utanufaika vipi nawarsha hii?

Page 6: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Mradi II: Nje ya kisandukucha kupigia kura

• Warsha hii ni sehemu ya mradi wa kuhamasisha ushiriki katikaharakati za kisiasa kwa watu wenye ulemavu wa akili: Kukifikiakisanduku cha kupigia kura

• Madhumuni ya mradi huu ni: – Kujenga msingi wa ushriki wa watu wenye ulemavu wa akili kwenye

harakati za siasa katika nchi za Kenya, Lebanon na Zanzibar.

– Kuongeza uelewa wa watu wenye ulemavu wa akili, familia na jumuiyazao pamoja na taasisi za serikali juu ya haki ya watu wenye ulemavu waakili kushiriki katika harakati za siasa

– kupeana nyenzo (mbinu) ili kuleta mabadiliko chanya

Page 7: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Mradi II: Matarajio

• Kuongeza uelewa juu ya ushiriki wa watu wenye ulemavu waakili katika harakati za siasa katika nchi 3 teule.

• Watu wenye ulemavu wa akili, familia na Jumuiya zao katikanchi hizo wana uwezo wa kutatua baadhi ya vikwazovinavyowakabili watu wenye ulemavu wa akili kuhusiana naushiriki wao katika harakati za kisiasa.

• Kuongeza uelewa miongoni mwa Maafisa wa Tume ya Uchaguzina wanajamii juu ya jinsi ya kuwasaidia watu wenye ulemavuwa akili kutekeleza haki yao ya kushiriki katika harakati zakisiasa

Page 8: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu
Page 9: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Pamoja:

• Tutajifunza kuhusu ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu waakili katika harakati za kisiasa

– Nini maana ya ushirikishwaji wa kisiasa na una umuhimu gani

• Tutafahamu kwa nini sauti zetu hazisikilizwi– Vikwazo vinavyotuzuia kushirikishwa

• Tutajifunza jinsi ya kuishawishi jamii itushirikishe

– Namna ya kupaza sauti zetu na kusikilizwa

• Tutasaidiana fikra za jinsi ya kuchukua HATUA

Page 10: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu
Page 11: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Tunamaanisha Nini Tunaposema “Ushirikishwaji wa Harakati za Kisiasa”

Unamaanisha pia:

• Kupiga kura na kushirikishwa katika utungaji waSera na Sheria zinazotuhusu.

– Pia unajulikana kama ushirikishwaji katikamasuala ya kiraia .

• Uwezo wa kusema kile ninachokiona muhimukwangu na kuamua mustakabali wa nchi yangu

– Hii inajumuisha haki yangu ya kupiga kura nakutoa maoni juu ya Sera na Sheria ambazozinanigusa.

Ushirikishwaji katika harakati za kisiasa unamaanisha kuishawishi Serikali yakoikusikilize.

Page 12: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Tunachokijua kuhusu Ushirikishwaji katika harakati za kisiasa duniani ?

• Familia nyingi za watu wenye ulemavu wa akili na Jumuiya zao hazilipi umuhimu suala la ushiriki wao katika harakati za siasa.

• Kuna unyanyapaa wa kimfumo dhidi ya watu wenye ulemavuwa akili hususan wanawake ambao hawashirikishwi katikamasuala ya siasa.

• Watu wenye ulemavu wa akili wananyimwa haki ya kupiga kurana kushiriki katika mchakato wa kisiasa.

Page 13: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

LAKINIWatu wenye ulemavu wa akili wana hamu ya kupatiwa fursa ya kushirikikatika harakati za ujenzi wa jamii zao ili na wao watambuliwe nakuthaminiwa kama sehemu ya jamii.

Kufanikisha hilo:

• Watu wenye ulemavu wa akili na familia zao hapana budi wapewe fursasawa ya kushiriki katika harakati za siasa kikamilifu kama raia wengine.

• Watu wenye ulemavu wa akili, familia na Jumuiya zao lazima wapewefursa za kutoa maoni yao kuhusu programu zinazogusa maisha yao, sanjarina maamuzi yanayoathiri ustawi wao na jamii zao.

• Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa CRPD ni fursa muhimu kwa sababuunatambua haki ya watu wenye ulemavu wa akili kushiriki katika harakatiza siasa (Ibara 29).

Page 14: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Ibara ya 29 ya CRPD

Serikali zitabeba dhamana ya kuhakikisha kwamba watu wenye ulemavuwanapata haki zao za kisiasa na fursa za kufurahia haki hizo katika hali yausawa kama raia wengine, na kwamba:

a) Zitahakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanashiriki vilivyo katikaharakati za kisiasa na kijamii katika hali ya usawa kama raia wengine, waowenyewe au kupitia wawakilishi waliowachagua pasi na shinikizo,zikiwemo haki na fursa za kushiriki katika kuchagua na kuchaguliwa,ikiwemo:

i. Kuhakikisha utaratibu wa kupiga kura, vifaa na nyenzo zilizopo nimuafaka, zinapatikana na ni rahisi kufahamika na kutumiwa;

ii. Kulinda haki za watu wenye ulemavu kwa kupiga kura ya siri, nakushiriki katika kura za maoni bila vitisho, na kugombea nyadhifambali mbali, kushika nyadhifa za uongozi na kutekeleza majukumuyote katika ngazi zote za serikali, na kurahisisha matumizi ya vifaa nateknolojia saidizi kila inapowezekana;

Page 15: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Ibara 29 ya CRPD

iii. Kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wanakuwa huru katika kutoa maoni yao na kueleza dhamira zao kama wapiga kura, na pale itapolazimu, kwa utashi wao wenyewe, kuruhusu usaidizi kutoka kwa mtu waliomteuwa wenyewe;

a) Kujenga kwa makusudi mazingira ambayo yataruhusu watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika harakati za maendeleo ya nchi yao, ikiwemo:

i. Kushiriki katika jumuiya zisizo za kiserikali na vyama vinavyojihusisha na masuala ya umma na siasa katika nchi, na katika harakati na uongozi wa vyama vya siasa;

ii. Kuunda na kujiunga na jumuiya za watu wenye ulemavu ili kuwawakilisha katika medani za kimataifa, kitaifa, kimkoa na hata mtaa.

Page 16: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

CRPD katika lugha rahisiIbara ya 29: Jinsi ya kushirikishwa katika harakati za siasa

Watu wenye ulemavu wana haki ya kushiriki kama

katika harakati za siasa kama watu wengine

Watu wenye ulemavu wana haki ya kupiga

kura kwa kuwahakikishia kuwa:

• Mchakato wa upigaji kura ni rahisi na

wenye kufahamika

• Upigaji kura ni siri

Page 17: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

CRPD katika lugha rahisi Ibara ya 29: Jinsi ya kushirikishwa katika harakati za siasa

• Kuruhusu usaidizi ili kuwawezesha watu wenye

ulemavu kupiga kura katika namna wanayoitaka, na

inapohitajika.

• Kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu

wanashirikishwa katika jumuiya zisizo za kiserikali

na vyama vya siasa.

• Kuhakikisha kuwa watu wenye ulemavu wana fursa

ya kujiunga na jumuiya za watu wenye ulemavu.

Page 18: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Hii inamaanisha nini?

• Fomu za kupigia kura zinapatikana, vituo na taratibu za upigaji kura zimerahisishwa kwa ajili yangu

• Naweza kupiga kura katika hali ya faragha siku ya uchaguzi

• Nasaidiwa kupata kitambulisho na cheti cha kuzaliwa ili nisajiliwe katika daftari la mpiga kura

• Taarifa za upigaji kura kama vile maeneo ya vituo vya kupigia kura na wagombea zinapatikana katika namna iliyorahisishwa – hii ni pamoja na matumizi ya lugha iliyo rahisi kufahamika na picha pia

• Nina uhuru wa kumteua mtu wa kunisaidia kupiga kura. Hii inajulikana pia kama usaidizi wa kupiga kura

• Naweza kuchaguliwa kuiongoza taasisi ya serikali

• Naweza kushiriki katika jumuiya za kiraia zinazojihusisha na masuala ya kijamii na kisiasa na uongozi katika vyama vya kisiasa

• Naweza kuunda au kujiunga na jumuiya zinazowakilisha watu wenye ulemavu wa akili kuanzia ngazi ya mtaa, mkoa, taifa na kimataifa

Page 19: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu
Page 20: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Kwa nini hatusikilizwi?

• Sheria inatamka kuwa haturuhusiwi kupiga kura au kushiriki katika shughuli za kiserikali.

• Jamii haiamini kuwa tunaweza kuwa na mchango wa maana

• Hatujui Sera na Sheria zinazungumzia nini na jamii haioni umuhimu wa sisi kujua

• Sijui jinsi ya kuifanya jamii inisikilize au jinsi ya kuleta mabadiliko

• Sijawahi kupewa fursa ya kushirikishwa katika jamii yangu. Na mimi nahitaji kupata elimu na nahitaji kufanya kazi.

• Familia zetu hazioni umuhimu wa sisi kupiga kura au kutoa maoni yetu kuhusu Sera na Sheria.

• Jamii haituthamini.

Page 21: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Vikwazo Vikuu

1. Kunyimwa uwezo wa kisheria

2. Sera na Sheria zinazotubagua

3. Changamoto za kufikiwa

4. Desturi za kijamii na kiutamaduni

5. Ukosefu wa elimu juu ya Haki za Watu Wenye Ulemavu wa Akili

6. Ukosefu wa miundo mbinu au nyenzo sahihi za kushughulikia Haki za kushirikikatika harakati za kisiasa na kiraia

7. Harakati za kisiasa na kiraia hazipewi kipa umbele kinachostahiki na familia zetu

8. Kutengwa na kunyanyapaliwa.

Page 22: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu
Page 23: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Kwa nini nisikilizwe?

• Maamuzi yanayofanywa na serikali yananigusa kwahivyo lazima inisikilize.

– Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali najinsi jamii zetu zinavyoendeshwa.

• Nina maoni kuhusu yale mambo ninayohisi ni muhimukwangu.

• Jamii yangu inapaswa kujua kilicho muhimu kwangu namsaada ninaouhitaji ili nikubalike na kushirikishwakatika jamii yangu.

– Ushiriki wangu unaweza kusaidia kujenga jamiishirikishi ambayo inajali mahitaji ya watu wenyeulemavu wa akili.

Page 24: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Kwa nini nisikilizwe?

• Kusikilizwa ndiko kunakonifanya niwe raia sawa na wengine. Sitaki kutengwa!

• Nikisikilizwa najua kuwa makundi YOTE yanasikilizwa. Hii inaifanya jamii yetu iwe rafiki kwa KILA MTU.

• Serikali yangu itakapotambua mahitaji yangu itatunga sera na sheria ambazo zinatilia maanani mahitaji ya kila mmoja wetu.

Page 25: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu
Page 26: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Ushirikishwaji katika harakati za kisiasa

KABLA YA UPIGAJI KURA

Kupitia na kushinikiza mikutano ya vyama; mipango yaserikali/vipaumbele

WAKATI WA UPIGAJI KURA

Kupiga kura; ufikiwaji wa mchakato mzima wa uchaguzi

BAADA YA UPIGAJI KURA

Kushiriki katika utungaji wa sera za umma na kusimamiataasisi za serikali kwa kufanya ukaguzi na mbinunyengine

Page 27: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

KABLA ya uchaguzi

Mtu mmoja mmoja

• JIANDIKISHE

– Unaweza kuhitajikitambulisho cha uraia ilikujiandikisha

• Kutana na kiongozi wako mteule

– Serikali na viongozi wanahitajikujua masuala ya watu wenyeulemavu ili kuyaingiza katikavipa umbele vyao

– Waelezee hali yako ya maisha, matumaini yako na yaleambayo ungependawakufanyie.

Makundi

• Waite wagombea na waelezematatizo ya watu wenye ulemavukwa ufasaha

• Kutana na wawakilishi wa serikali

• Shinikiza mabadiliko

– Je! Kuna sheria zinazowazuiawatu wenye ulemavu kupigakura?

• Uchambuzi wa Sera jumuishi

– Utekelezaji wa mkataba waCRPD

– Sera, bajeti, mchanganuo waprogramu

Page 28: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Wakati wa uchaguzi

Mtu mmoja mmoja

• Elezea kile unachokiona muhimukwako na kile ambachoungependa serikali ikufanyie ilikufikia lengo la ujumuishi

• Piga simu katika vipindi vya rediona runinga na uulize maswalikuhusu watu wenye ulemavu

• Fuatilia midahalo na jinsi ganiwananchi wanaweza kushiriki

• Wagombea wanaweza kuhitajimaoni yako

– Waite na uzungumze nao, waulize watawafanyia niniwatu wenye ulemavu

Jumuiya

• Wapeni wanachama wenu taarifaza kiuchambuzi kuhusiana namikutano yote ya kisiasa

• Andikeni “waraka” mtaowapawagombea ambao unaainishamasuala ya msingi na“waombeni” wayatekeleze

• Andaeni au shirikini katikamidahalo yote inayozungumziamasuala ya watu wenye ulemavu

• Fanyeni kampeni za kuhamasishawatu juu ya haki ya kupiga kura

• Kwa kutumia mfano wafundisheniwatu wenye ulemavu jinsi yakupiga kura

Page 29: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Siku ya UchaguziMtu mmoja mmoja

• Jua kilipo kituo chako cha kupigiakura

– Hwenda ukahitaji kituomaalum cha kupigia kura

• Piga kura

Jumuiya• Ziwasaidie watu wenye ulemavu

kuvifikia vituo vya kupigia kura

• Ziwasaidie watu wenye ulemavukupiga kura

Page 30: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Baada ya UchaguziMtu mmoja mmoja• Fuatilia kwa viongozi wako

wateule

– Mahusiano yanapaswa kuwaendelevu na sio wakati wauchaguzi pekee

• Shiriki katika midahalo

• Hadithia maisha yako/uzoefuwako kwa ajili ya ripoti n.k

• Jihusishe!

Jumuiya• Fuatilia utekelezaji wa ahadi za

vyama/viongozi wa serikali

• Shinikiza mabadiliko

– Kuna sheria zinazowazuiawatu kupiga kura?

• Tathmini ya sera jumuishi

– Hii inapaswa kuwa endelevukabla na baada ya uchaguzi

– Utekelezaji wa mkataba wa CRPD

– Sera, bajeti, uchanganuzi watathmini ya programu

• Fuatilia na tathmini athari/matokeoya juhudi za serikali

– Ripoti serikalini, ripoti kwamashirika ya kimataifa

Page 31: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Mfano: PANAMA

Juhudi zinazofanywa kabla ya uchaguzi ilikuongeza ushiriki wa raia, ni pamoja na kuandaamikutano ya kutoa elimu kwa umma na kuandaamidahalo na wagombea wa kiti cha urais.

Kuchukua ahadi ya utekelezaji wa sera ambazozitaboresha ushiriki wa watu wenye ulemavu nafamilia zao katika nyanja zote za maisha

Kuanzisha Sekretarieti ya kitaifa kwa ajili yaushirikishwaji wa watu wenye ulemavu katikajamii (SENADIS).

Page 32: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu
Page 33: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Pata taarifa

• Ziombe familia zetu, marafiki na watu wa kuaminika/jumuiya ili wakupatietaarifa hizo

• Fanya utafiti iwapo sheria kwenye nchi zetu zinatuzuia tusipige kura

– Shirikiana na jumuiya zetu kwa kutumia vigezo maalum tathmini iwaponchi zetu zinatekeleza mkataba wa CRPD. Vigezo hivyo vinapatikanakatika ripoti kuu.

• Tafuta jumuiya katika nchi zetu ambazo zinajihusisha na mahitaji yetu.

Page 34: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Tufanye tusikilizwe

• Zungumza na viongozi wetu wateule au wawakilishi. Wawakilishi wetu wapo kwa ajili ya maslahi yetu. Wanawajibu wa kusikiliza maoni yetu kuhusu mambo yenyemaslahi kwetu.

“Sisi (familia zilizoathiriwa na ulemavu) hatuonekani kama makundi yawatu wengine…….sababu hakuna watu wengi wenye ulemavu katika maeneno yetu

tunayoishi kama walivyo wakulima na wafanya biashara. Kuna mengi tuwezayokuyafanya lakini uwezo duni wa kifedha unatukwaza. Lakini siku tulipotembelewa

[na kiongozi wetu tuliomchagua] tulibaini kuwa iwapo kila mwanasiasa angejipangiautaratibu wa kututembelea kama hivi ingesaidia kuongeza uelewa,”

• Wasilisha ripoti mbadala kwa mashirika ya Umoja waMataifa kuhusu juhudi ambazo nchi yako inachukua kutatuachangamoto za watu wenye ulemavu.

Page 35: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

ShirikianaHatuwezi kufanya haya peke yetu

• Shirikiana na wataalamu mbali mbali ili tuweze kuongeza uelewa wao juu ya masuala ya watu wenye ulemavu

• Anzisha jumuiya zinazohamasisha haki za watu wenye ulemavu na ushiriki wao kisiasa.

Page 36: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Jifunze kupitia wengine

• MENCAP – Makundi yote ya Wanachama; Kampeni ya Pata kura yangu

• Holland – midahalo ya siasa

– Andaa midahalo ili kujadili mambo ambayo ni muhimu kwako/kundi lako

• Lebanon – Shirikisho la Watu wenye Ulemavu

– Kufanya kazi pamoja na kushirikiana na wadau wengine

• Canada – candidate pledge cards; inaandaa midahalo yote na wagombea

• Germany/Japan/Peru – strategic litigation – inapigania kufuta sheria inayowazuia watu walio chini ya uangalizi (kulelewa) kupiga kura

• Kenya/Zanzibar – viti maalum vya uwakilishi bungeni na Baraza la Wawakilishi

Page 37: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Kuwa MTETEZI

• Orodhesha malengo maalum tunayokusudia kuyafikia.

• Orodhesha matatizo tunayokabiliana nayo.

• Orodhesha njia za kuyatatua

• Weka bayana (kadiri inavyowezekana) ni msaada gani tunaweza kuupata kwako, hasa ikiwa hatuwezi kufikia malengo uliyoyakusudia wewe

• Orodhesha wadau ambao unahisi wanaweza kutusaidia

• Orodhesha wadau ambao unahisi tukishirikiana nao tutafikia malengo

Page 38: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Chukua HATUA

Tunaweza:

• Tunaweza kushiriki katika mikutano ya kujadili masuala ya kiraiana harakati za kisiasa

• Kupashana taarifa kuhusu mambo ambayo ni muhimu kwetu

• Kujenga uelewa kuhusu haki za watu wenye ulemavu

• Kuzungumzia vikwazo tunavyokabiliana navyo

• Kupendekeza njia za kupambana na vikwazo hivyo

Page 39: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Sababisha MABADILIKO yatokee

• Jamii hutunga sheria na sera mbali mbali na sisi tunaweza kushirikishwa katika kuzifanyia mabadiliko.

• Unaweza kudhani kwamba tunapaswa kubadilisha mambo mengi kabla ya athari ya mabadiliko hayo kuonekana.

• Mabadiliko huchukua muda athari yake kuonekana. Anza kuchukua hatua kwa kuangazia changamoto moja au mbili za msingi.

• Inawezekana hujui hilo lakini tayari tumeshaanza kuchukua hatua!

• Kupambana ili kuhakikisha kuwa tunapata elimu na ajira au hata kukubalika katika jamii zetu ni namna mojawapo ya ushiriki wa kisiasa.

Page 40: Sauti Yangu Isikilizwe! Kuwasaidia watu wenye ulemavu wa ... · –Tuna haki ya kutoa maoni juu ya shughuli za serikali na jinsi jamii zetu zinavyoendeshwa. • Nina maoni kuhusu

Rahisisha upigaji kura: Ushirikishwaji katika masuala ya kiraia