Top Banner
TAASISI YA ELIMU YA WATU WAZIMA DAR ES SALAAM KOZI: SHAHADA YA ELIMU YA WATU WAZIMA NA MAFUNZO ENDELEVU MWAKA WA MASOMO: 2013/2014 MWAKA WA PILI MODULI: KUCHAMBUA NADHARIA ZA UHAKIKI MSIMBO WA MODULI: KIU 07431 MWEZESHAJI: MWALIMU KILEO AINA YA KAZI: KAZI YA KIKUNDI NAMBA TATU WASHIRIKI KATIKA KAZI:- 1. SADI ISSA 2. TESHA ANTUSA 3. MLINGWA AGNESS 4. MASIMBA SHABANI R.A. 5. HABIBU ABASSI
22

FANI KILIO CHA HAKI

Feb 21, 2023

Download

Documents

Welcome message from author
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
Page 1: FANI KILIO CHA HAKI

TAASISI YA ELIMU YA WATU

WAZIMA

DAR ES SALAAMKOZI: SHAHADA YA ELIMU YA WATU WAZIMA NA

MAFUNZO

ENDELEVU

MWAKA WA MASOMO: 2013/2014 MWAKA WA PILI

MODULI: KUCHAMBUA NADHARIA ZA UHAKIKI

MSIMBO WA MODULI: KIU 07431

MWEZESHAJI: MWALIMU KILEO

AINA YA KAZI: KAZI YA KIKUNDI NAMBA TATU

WASHIRIKI KATIKA KAZI:-

1. SADI ISSA

2. TESHA ANTUSA

3. MLINGWA AGNESS

4. MASIMBA SHABANI R.A.

5. HABIBU ABASSI

Page 2: FANI KILIO CHA HAKI

6. MSHANA EMELINE

7. KISHIMBWE HALIMA

8. GODFREY RENATUSI

9. HAMISI SHABANI

SWALI:

Uhakika wa Fani katika Kitabu CHA KILIO CHA HAKI.

UTANGULIZI

“KILIO CHA HAKI” ni Tamthilia iliyoandikwa na Alamin Mazrui(1981). Tamthilia hii inaelezea mapambano baina ya wafanyakazi naudhalimu wa makaburu. Tamthilia hii ina sawiri mapambano ya nchinyingi za kiafrika kutaka kujikomba kutoka kwa watawala wakikoloni.

Katika tamthilia hii mwandishi amemchora mwanamke jasiri

aliyejikomboa kimawazo na ndiye aliyekua kiongozi wa mapambano na

anadhihirisha udhalimu wa jamii yake unaowapata wafanyakazi kwa

Mwanamke huyu.Alifaulu katika kuwazindua wafanyakazi wenzake ili

wapambane na udhalimu na watetee haki zao. Mapambano haya

yanaleta mwamko wa kisiasa ambao ndio mwanzo wa matayarisho ya

vita vilivyoikomboa nchi nzima kutoka na ukoloni.

UHAKIKI WA TAMTHILIA KILIO CHA HAKI

FANI

Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001).Introduction to the study

of literature.

Page 3: FANI KILIO CHA HAKI

“Fani ni ufundi wa mwanafasihi anaoutumia katika uandishi wa kazi

yake, ili aweze kufikisha ujumbe wake kwa wasomaji wake. Katika

uchambuzi wa tamlithiliya hii vipengele vilivyo chambuliwa ni

muundo, mtindo, lugha, wahusika, mandhari, maleba, vifaa,

matumizi ya jukwaa, jina la kitabu, kufaulu na kutofaulu kwa

mwandishi.

MUUNDO

Muundo uliotumika ni wa rejea kwani kuna mwingiliano wa matukio

na mchanganyiko wamatukio,matini au mchanganyiko msimbo (code

mixing).

Msanii AlaminMazrui aliandika tamthiliya hii katika maonyesho

kumi, kama ifuatavyo:-

Onyesho la kwanza ukurasa wa kwanza hadi kumi na nne. Mussa na

Dewe wanasoma taarifa toka gazetini zinazo eleza kuwa Kamishina

Hunderson amemkamata Lanina wa Muyaka kwa tuhuma za mauaji ya

watu watatu kwenye shamba la Bwana Delamon. Onyesho la pili

ukurasa wa kumi na tano hadi ishirini. Lamina kwa mara ya pili

tena anahojiwa na makechero kwenye kituo cha polisi kuhusina na

mauaji ya watu watatu kwenye shamba la Bwana Delamon. Onyesho la

tatu ukurasa wa ishirini na moja hadi ishirini na nane. Lanina

anawajibu makachero kuwa Delamon na wenzake hawakuja kutunufaisha

bali kuja kunyonya nchi yetu ukurasa wa 24.

Onyesho la Nne (uk 29-36)

Page 4: FANI KILIO CHA HAKI

Lanina alirudi nyumbani lakini alikutana na lawama za mume wake

Bwana Mwengo kwa kumuachia familia kwa muda mrefu. Hata hivyo

walisamehana na kutaka waendelee kushirikiana.

Onyesho la Tano (uk 37-42)

Lanina anakutana na wazazi wake kijijini,baba yake anamlaani na

hata kuwapiga yeye na mama yake kwa sababu Lanina hafuati mila na

desturi za kwao na mama yake ndiye aliyepewa kumfunza.

Onyesho la Sita (uk 43-48)

Hapa wasaliti Matovu, Tereki naPelekha wanajifariji na kuwaona

akina Musa na Dewe na Lanina kuwa ni wajinga, kwa kukataa msamaha

wa Bw. Delamon.

Onyesho la Saba (uk 49-55)

Wasaliti hawa wana washawishi Lanina arudi kazini kwa vile

wameruhusiwa kuendesha shughuli za siasa na mshahara unapanda juu

kidogo. Lanina anakataa na kuwafukuza nyumbani kwake.

Onyesho la Nane (uk 56-65)

Lanina yupo kwenye kioski cha mzee Ingeli. Musa, Dewe na Lanina

wanakutana kupeana taarifa kuwa eti Delamoni ameruhusu kuanzisha

chama na kumruhusu kurudi kazini.

Onyesho la Tisa (uk 66-72)

Katika ofisi ya Bwana Delamoni wamesikia Sauti za wafanyakazi za

waliokuwawanaimba nyimbo za siasa.

Page 5: FANI KILIO CHA HAKI

Onyesho la Kumi (uk 73-77)

Hapa Lanina akiwa gerezani anakutana na Askari Malaya aliyekuwa

anamtongoza Lanina, lakini Lanina anamkatalia na kumpiga teke

sehemu zake za siri, pia Lanina anaitwa na jaji na kumsikiliza

maelezo yake, uk 77.

MTINDO

Katika tamthilia hii mwandishi ametumia mtindo wa mwingiliano

matini ambapo ameonyesha mambo mabalimbali yaliyounda kazi hii ya

fasihi. Mfanonidialojia, hapa mwandishi aneonyesha mazungumzo

mbalimbali ya wahusika wakijibizana.

Matumizi ya gazeti, pia mwandishi ametumia gazeti lengo lake ni

kusambaza habari kwa watu, hata wale waliogerezani, pia kuonyesha

kuwa baadhi ya wahusika ni wasomi, na matumizi ya gazeti

yameonyeshwa katika uk 1 na 2.

LANINA KUPELEKWA MAHAKAMANI

Lanina waMuyuka, mwanamke aliyekuwa mfanya kazi katika shamba

maarufu la Bwana Delamon, ametiwa tena kizuizini.

Pia alitumia lugh ya ushairi. Pia mwandishi ametuamia lugha ya

ushairi katika uk 62.

Ari yetu ndio mwokozi wetu

Ari yetu lazima tuisujudie,

Ari hii ya mwaka tuliyoivumbika,

Iliyojaa joto lisiloburudika

Page 6: FANI KILIO CHA HAKI

Ije ituongoze mpaka mwisho kufika,

Na kutuzimia kiza cha mwaka

Pia matumizi ya simu.Pia yamejitokeza katika tamthiliya hii ya

Kilio cha Haki, pale ambapo Shindo alipompigia simu kamishna

Hunderson. Lengo ni kuonesha uhalisia wa kimazungumzo.

Shindo:- “Eee….halo ka….ka…..kamishina Henderson yup…….yupo?

wap…. “uk 67.

Uchanganyaji msimbo (code mixing); pia mwandishi wa KILIO CHA

HAKI ametumia lugha ya kuchanganya, kama vile Kingereza na

Kiswahili, lengo lilikuwa kuonyesha katika matini palikuwepo na

watu tofauti kama vile wazungu na waswahili. Mfano katika uk 10.

Delamon:- (kwa hasira)

Coming Sir! Coming Sir!

Kwanini hamtafuti maboi wenye akili zaidi,

Foolish baboons!

Kimbo: Yes…Sa……

Delamon: nenda kamwite……..aaa…….aaa……

Matumizi ya lugha ya matusi, wa mfano Lanina aliyekuwa akitukanwa

na baba yake

Page 7: FANI KILIO CHA HAKI

MATUMIZI YA LUGHA

Lugha ni ufundi anaotumia mwandishi katika kuandika kazi yake. Ni

sifa za kipekee mfano. Misemo, methali tamathali za semi kama

takriri na tashibiha.

NAHAU/MISEMO

Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema Nahau ni misemo

iliyojegwa kwa kutumia maneno ya kawaida lakini huwa imesitiri

maana tofauti iliyobeba maneno katika hali ya kawaida.

Katika tamthiliya hii mwandishi ameipamba kazi yake kwa kutumia

misemo na nahau kama ifuavyo:-“Mhitaji ni mtumwa” uk 24. Msemo

huu ulijitokeza pale ambapo kachero wa pili alipomwambia Lanina

anyenyekee kwa sababu inaonyesha kuwa unapokuwa na shida lazima

unyenyekee.

Msemo mwingine ulijitokeza pale mama yake Lanina alipokuwa

anamwambia mwanawe. “Mkosa chema haachi kuguna” uk 37. Pia

aliendelea kusena “Jicho la hasidi lisimkumbe” uk 37 hapa mama

Lanina alikuwa anamwombea mwanawe dua.

“Huyu ni punda tu asiyekuwa na fadhila!” uk 38 msemo huu

ulitumiwa na Baba yake Lanina akimtaka asimsalimie na wala

asimwite Baba kwani si Baba yake kutokana na tabia yake.

METHALI

Page 8: FANI KILIO CHA HAKI

Ni misemo inayotumiwa kuelezea kitu kwa njia ya picha, na kwa

ufupi ili itoe maadili au maonyofulani, methali huwa na sehemu

mbili saehemu ya kwana husemwa na mshauri na ya pili hukamilishwa

na mshauriwa. Humfanya msikilizajiawe katika hali ya kufikiri,

kuchambua na kupatanisha ukweli, na hali ili ajue maana ya ndani

iliyokusudiwa.

Katika tamthiliya hii ya “KILIO CHA HAKI” mwandishi ameipamba na

kuipendezeasha kazi yake kwa kutumia methali mbalimbali. Mfano

katika ukurasa wa 27” ametumia methali “Hasira hasara” mwandishi

ametumia methali hii pale Matovu na Tereki walipokuwa wakimshauri

Lanina akubali kurejea kazini. Hivyo methali hii katika jamii

yetu, inatufundisha kuwa tufikiri kuona ndipo tujue maamuzi.

Methali nyingine ni “Dalili ya mvua ni mawingu” uk 36 pale baba

Lanina alipokuwa anaongea na mama yake Lamina kuhusu mabadiliko

ya Lanina na minong’ono ambayo inasemwa kijijini kuhusu Lanina.

Pia mwandishi ametumia tamathali za semi mbalimbali. Tamathali za

semi ni maneno au sentensi ambazo hutumiwa na wasanii wa fasihi

ili kutia nguvu katika maana, mtindo na hata sauti katika

maandishi ama usemi, Tamathali hutumiwa kuipamba na kuongezea

utamu katika lugha ya fasihi. Kuna aina nyingi za tamathali za

usemi baadhi yake ambazo zimejitokeza katika tamthilia ya KILIO

CHA HAKI ni:-

TASHIBIHA

Page 9: FANI KILIO CHA HAKI

Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema tashibiha

hutumika kulinganisha kitu kimoja au Zaidi kwa kutumia

viunganishi kwa mfano. (kama, mithili ya).

Mfano:- Nyinyi ni kama punda msiyojua fadhila. Uk 22 alisema

kachero wa kwanza kwa Lanina pale walipomtia kizuizini.

Anajikunyata kama anayesikia baridi uk 28 hii ni sauti ya

msimuliaji ilisikika kutoka nje

Nchi zetu ni kama jaa la bidhaa zinazowazidia uk 24,

aliongea Lanina akiwambia kachero wa kwanza na wa pili.

Kimya kama hayawani uk 76, Lanina alikuwa akijisemea

mwenyewe. Hii ina maana kuwa kunyamaza kama kayawani ni kama

kuwa mwendawazimu au mtu aliyechanganyikiwa na mambo.

TAKRIRI

Ni kujirudia kwa maneno au sauti.

Katika tamthilia hii Takriri zilizotumika ni kama ifuatayo

“Ndiyo ndiyo uk 16. Hii ina maana kuwa mwandishi alikuwa

anakubaliana na jambo hilo lakini kwa mashaka.

………….. na …………… nauk 16 na uk 17

Kufikiria! Kufikiria! Uk 19

Halafu! Halafu uk 29

La! La! La! Uk 22

Lamina! Lamina! Uk 29

Tafadhari Tafadhari uk 42

Page 10: FANI KILIO CHA HAKI

Twende! Twende! Nikakupeleke kwa shangazi yako akakufundishe

kumtii bwana wako uk. 42.

Alisema baba Lanina akimueleza mkewe.

Haya sema ulilonalo! Sema basi, sema na mimi nisikilize

sema! Uk 30

Mwengo aliongea akimwambia mkwewe Lanina.

“Yawache yachache Dewe yawache yachache”

yawache yachache”

Alizungumza musa uk 4

Lamina! Lamina!

Wakili alimuita Lanina uk 76

MDOKEZO

Ni kauli ambazo hazimalizii jambo au ni tamathali ambazo hudokeza

kitu Fulani na kukiacha bila kukimalizia au kukikamilisha kwa

maana kwamba kinaweza kukamilishwa na mtu mwingine kisanaa.

Mfano

Usijali tutapata tu karibu………….. uk 1. Hapa mwandishi

anajaribu kuonyesha matumaini kuwa Dewe na mwenzake Mussa

wangeruhusiwa kurudi nyumbani kwao.

(Alisema Dewe)

“………… maharamia hawa wasio heshimu sharia……..”

Alisema Dewe uk 4

“Nenda kamwite ……aaa…aaa…. Uk 10

Alisema Delamon.

“Sasa tunaweza kuzungumza kama” uk 11 (alisema Delamon)

Page 11: FANI KILIO CHA HAKI

“Afrika…. Tamaa ya mtu mweusi” Uk 5

Alisema Dewe

Sisi wenyewe lakini…………

(Aliongea Delamon) uk 9

Maneno usemayo ni mazuri bwana Delamon na tunayaelewa vyema.

Lakini…..lakini…...tukiwa tunataka……..

Naam…..Basi labda mnayaweza (alisema Delamon)UK 12

Ninyi ndio washenzi mnao…..mnao….Uk 12 (alisema Zari)

Aaaa….rafiki zangu…..kusena kweli...kwa hakika….sifahamu kwa

nini(Delamon Uk 13)

SITIARI

Sitiari hulinganisha vitu au watu bila kutumia viunganishi.Hulinganisha vitu kama vinafanana kabisa.

Katika riwaya hii mwandishi ameweza kuipamba kazi yake kwakutumia sitiari mbalimbali.

Mfano:“Mimi ndiye simba” Uk 32 hapa baba yake lanina alikuwa namaana ya kuwa yeye ndiye mkuu wa familia akiomgea kitu hakuna wakumpinga.

Mfano “Huyu ni punda tu asiyejua fadhila Uk 38 hapa tumemuonababa Lanina alikuwa akimwambia mwanawe Lanina. Akimaanishamwanawe hana shukrani maana shukrani ya punda ni mateke.

Mfano “Siasa ni mchezo mchafu”Uk 76.Hapa mwandishi amelinganishasiasa na mchezo mchafu, kama vile kufungwa gerezani na kuaibishwambele za watu.

TASHIHISI

Page 12: FANI KILIO CHA HAKI

Ni kuvipa vitu uwezo wa kufanya jambo anbalo halina uwezo au sifa

ya kufanya jambo tofauti na uwezo wa kibinadamu.

Mfano: mzee alisema:

“Kwa nini ewe bara la Afrika

Ewe nchi uliyepambwa kwa weusi

Ewe roho wa kizazi chetu

Tukutilieje mbolea siku baada ya siku

Kwa kutaraji utatuzalia

RIDAA.

Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema ridaa ni misemo

ambayo kuonyeshwa kushangazwa kwa jambo fulani. Misemo hii

huambatana na matumizi ya alama za mshangao katika kukubali

jambo, kuchukia au kuonyesha heshima maalumu.

Mfano:

Na malalamiko yatapungua!” Uk 15 alisema shindo

“Tafadhali usinifanyie uhuni huo!” alisema Lanina Uk 25

“Mimi si Malaya” alisema Lanina Uk 25

“Aaa! Ni hilo tu Lanina” Uk 25 (alisema kachero)

“Lanina! Tereki!” (alisema kachero) Uk 26

“Ewe twende tukalale mama eh!” alisema Lanina Uk 30

WAHUSIKA

Page 13: FANI KILIO CHA HAKI

Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema mwandishi Alamin

Mazrui wa tamthilia ya KILIO CHA HAKI amewatumia wahusika kwa

kuwagawa katika makundi mbalimbali ambayo ni wahusika wakuu,

wahusika wasaidizi na wahusika mviringo.

MHUSIKA MKUU

Mhusika nkuu katika tamthilia yaKILIO CHA HAKIni Lanina. Alamini

Mazrui alimtumia Lanina kwa kutumia nadharia ya ufeministi.

Lanina amekuwa mwanamke aliyepigania haki na ukombozi wa mwanamke

pamoja na kutetea maslahi ya wafanyakazi wenzake. Hivyo alisimama

kidete bila kukata tamaa katika kupigania haki pamoja na kuwa

alipata mateso na manyanyaso mbalimbali hadi kufikia hatua ya

kuwekwa kizuizini.

Mfano

Katika ukurasa wa 14 anasema

“Lakini sisi tunajaribu kutetea haki zetu……”

Askari anampiga kofi na kusema wacha upuuzi wako huo. Haki! Haki

unapigania kitu hata hujui ukipewa utafanyia nini?

Pia Lanina ni mama wa watoto wawili yaani Dida na Badi.

Hii inadhihirika pale ambapo Lanina alipokuwa akimpapasa mwanawe

Dida

“Pole Dida mwanangu.

Nimesharudi sasa hivi.uk 30

Page 14: FANI KILIO CHA HAKI

Wasifu mwingine wa Lanina ni mke wa Mwengo. Hii inadhihirika pale

ampapo Mwengo alipokuwa akiongea na Lanina.

Mimi ni mume wako ala!Umesahau? Kwa nini hunijibu? Kwa nini

umenipuuza namna hii?

DELAMON

Huyu ni mhusika mkuu pia kwani ameonekana tangu mwanzo wa matukio

katika tamthiliya hii hadi mwisho. Hapa mwandishi ametumia

nadharia ya ubada (ukoloni) akiwakilisha jinsi wakoloni walivyo

wagandamiza wafanyakazi wa kiafrika kiuchimi.

Hii imejitokeza katika ukurasa wa 13 pale ambapo Lanina anamjibu

Delamon kwa hasira “….. nyingi hamkuja hapa kwa manufaa/faida

yetu…… mmekuja kwa maslahi yenu wenyewe………… uk 13.

Pia Delamon ni mmiliki wa shamba kwa maana nyingine ni mnyonyaji,

Hii inajidhihirisha katika onyesho la 6

“Katika shamba la Delamon wakati wa mapunziko. Tereki, matuvu,

Dewe, Mussa na mfanyakazi mwingine wanatokeza wamevaa nguo za

kazi. Uk 43.

WAHUSIKA WASAIDIZI

Mwandishi amewagawa wahusika wasidizi katika makundi mawili,

ambayo ni wale wenye msimamo wa nadharia ya Ki-Marx na wale

wasaliti. Nadharia hii ya kimary huonyesha wahusika wa

kimaendeleo, pia huonyesha matumaini ya juu ya kizazi cha

Page 15: FANI KILIO CHA HAKI

binadamu (tabaka fulani lina kandamizwa lakini linaonyesha

matumaini)

Wahusika aliowatumia kwa nadharia ya Ki-Marx ni Mussa na Dewe

ambao walishirikiana na Lanina katika harakati za kuwakomboa

wafanyakazi ili kupata maslai yao ya kazi. (katika ukurasa wa

2).

“Mussa (kwa hasira) “wasikilize wapumbavu hawa! Ati Lanina

amechochea mgomo

Lanina hata hakuwepo siku ya mgomo.

Lanina, Dewe na Mussa walikuwa watu wenye msimamo, hawakukata

tamaana waliendelea na mapambo hadi mwisho katika uk 62 pale

Lanina alivyokuwa anaonge na Mussa na Dewe.

“Ndugu zangu, ari yetu ndiyo mwokozi wetu, ari yetu lazima

tuisujudie

Isitoshe walipenda maendeleo kwa sababu walikuwa wanapinga

kunyanyaswa na kuonana na makaburu uk 14.

“Lakini sis tunajaribu kutetea haki zetu tu kama….”

Mhusika mwingine ni baba Lanina, amechorwa na mwandishi kama

mfuasi wa mfumo dume na kuona kuwa mwanamke hawezi kutetea haki

wala kufanya mapinduzi, ukurasa wa 38.

Baba akionyesha yenye ndiye msemaji wa mwisho.

Page 16: FANI KILIO CHA HAKI

“Mimi ndiye simba wa nyumba hii ningurumapo sitaki kuzisikia

sauti zenu za kijinga hapa (Akimgeukia Lanina)

Na wewe binti ya shetani?

Mimi si wale wanaume wengine unaochezeachezea. Mimi si kina

Mwengo mimi ni dume kweli kweli umesikia hivyo!

Mtu katili

Hafai kuigwa katika jamii

JUKWAA

Onyesho la Kwanza (uk 1-14)

Mussa na Dewe wanasoma taarifa tokea gazetini zinaeleza kuwa

kamishina Hunderson amemkamata Lanina wa Muyake kwa tuhuma ya

mauaji ya watu watatu wenye shamba la bwana Delamon.

Onyesho la Pili (uk 15-20)

Lanina anawajibu makachero kuwa Delamon na wenzake hawakuja

kutunufaisha bali kunyonya nchi zetu.

Onyesho la Nne (uk 29-36)

Lanina karudi nyumbani lakini amekutana na lawama za mume wake

Bwana Mwengo kwa kumuachia familia kwa muda mrefu. Hata hivyo

walisamehana na kutaka waendelee kushirikiana.

Onyesho la Tano (uk 37-42)

Page 17: FANI KILIO CHA HAKI

Lanina anakutana na wazazi wake kijijini, baba yake anamlaani na

hata kupigwa yeye na mama yake kwa sababu Lanina hafuati mila na

desturi za kwao na mama yake ndiye aliyepewa kumfunza.

Onyesho la Sita (uk 43-48)

Hapa wasaliti Matovu, Tereki naPelekha wanajifariji na kuwaona

akina Mussa na Dewe na Lanina kuwa ni wajinga, kwa kukataa ofay a

Bw. Delamon.

Onyesho la Saba (uk 49-55)

Wasaliti hawa wana wanamshawishi Lanina arudi kazini kwa vile

wamemhusiwa kuendesha shughuli za siasa na mshahara unapanda juu

kidogo. Lanina anakataa na kuwa fukuza nyumbani kwake.

Onyesho la Nane (uk 56-65)

Lanina yupo kwenye kioski cha mzee Engeli. Mussa, Dewe na Lanina

wanakutana kupeana taarifa kuwa eti Delamon ameruhusu kuendesha

shughuli za kisiasa na kuendeleza mapambano ya kudai haki zao

kazini.

Onyesho la Tisa (uk 66-72)

Katika ofisi ya Bwana Delamon wamesikia Sauti za wafanyakazi

walipoamua kuimba nyimbo za kimapinduzi.

Onyesho la Kumi (uk 73-77)

Hapa Lanina akiawa gerezani anakutana na Askari malaya,ambaye

alimtongoza Lanina lakini Lanina anamkatalia na kumpiga teke

Page 18: FANI KILIO CHA HAKI

sehemu zake za siri, pia Lanina anaitwa na jaji ili kutoa utetezi

wake katika(uk 77).

MANDHARI

Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema mandhari ni

sehemu au mahali ambapo kazi ya fasihi hutendeka. Katika

tamthiliya ya KILIO CHA HAKI mwandishi ametumia mandhari tofauti

tofauti kama vile shambani (kwa bwana Delamon) uk 43 mahamamani,

kijijini (kwa baba na mama wa Lanina) mtunzi ametumia mandhari

hayo ili kuonyesha matendo mbalimbali ambayo yalitumika kuibua

dhamira mbalimbali.

MALEBA NA VIFAA

Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasemamaleba ni mavazi

anayotumia msanii katika Sanaa yake. Kalika kumpamba mhusika.

Mavazi yaliyotumika katika tamthiliya hii ni pamoja na:-

Matambara uk 5 na uk 77. Matambara ni nguo zilizochanika

zinazoonyesha suala la umaskini, hapa alivaa mzee ambaye hali

yake ya maisha ilikuwa duni.

Khanga uk 39, mama alipojifuta machozi kwa kutumia khanga. Khanga

katika tamthiliya hii ya kilio chetu inawakilisha utamaduni

wamavazi ya mwanamke wa Kitanzania.

VIFAA

Page 19: FANI KILIO CHA HAKI

Vifaa ni zana zinazotumiwa na wahusika wa kazi ya fasihi ili

kuweka uhalisia.

Mfano wa kiko kilichotumiwa na bwana Delamon inaashiria tabia za

wakoloni kuvuta kwa kutumia kiko, (ukurasa wa 10).

Sigara ni kifaa kilichotumiwa na Lanina kuonyesha tabia ya

mwanamke huyu jasiri kuwa ni mvutaji sigara. Pingu nabundiki ni

silahazilizotumiwa na wakoloni ili kuwatisha na kuwagandamiza

waafrika ili wawanyonye kwa urahisi (ukurasa wa 14).

TASWIRA NA ISHARA

I. ISHARA

Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). AnasemaTaswira na

Isharani maelezo yanayoeleza jambo kwa njia ya kufichika ili

msomaji afikiri na kugundua mwenyewe.

Kutikisa kichwa, katika ishara hii tunaona Lanina akimkatalia

Mwengo juu ya mawazo yake potofu juu ya mkewake Lanina hii

inapatikana uk 34. Pia mama yake Lanina alitikisa kichwa

kuonyesha kukubaliana na mumewe. Ishara hizi zinaonyesha matumizi

mbalimbali ya viungo vya mwili vya wahusika wake.

II. TASWIRA

Page 20: FANI KILIO CHA HAKI

Paneli la Kiswahili (2009-2014) wanasema taswira ni matumizi ya

lugha inayotumia maneno yanayojenga picha au fumbo fulani kwa

msomaji.

KILIO CHA HAKI, inaonyesha mifadhaiko na manung’uniko

yawafanyakazi wakidai haki zao kama vile, mshara ndogo, mazingira

mabovu ya kazi, na vifaa duni vya utendaji kazi.

Makaburu; hii ni taswira iliyotumika kuonyesha wanyonyaji ambao

walikuwa wakiwanyonya na kuwanyanyasa wafanyakazi wao kwa

kuwalipa ujira mdogo na hata kufanya kazi kwa muda mrefu.

Lanina; alikuwa akiwakilisha kundi la wapenda maendeleo, pia

anawakilisha wanawake wanaojitambua na wanaoelewa matatizo

yanayowakumba wananchi wa maeneo wanayoishi.

Shamba la bwana Delamon. Hii ni taswira inayowakilisha mandhari

yaliyokuwa yakitumika kunyonya na kudhurumu haki ya wanyonge

mfano; Lanina na wenzake.

Wanfanyakazi hii ni taswira iliyokuwa ikiwakilisha umma ulio kuwa

ukionewa na kunyanyaswa na bwana Delamon.

Picha ya jalada la KILIO CHA HAKIni ishara ya mwanamke

anayedondosha machozi kwa kulia kutokana na dhuluma na

unyanyasaji anaofanyiwa na jamii yake.

KUFAULU KWA MWANDISHI WA RIWAYA YA KILIO CHA HAKI

Page 21: FANI KILIO CHA HAKI

Mwandishi ametumia lugha rahisi inayoeleweka yenye lugha ya

kishairi, nyimbo na matumizi mazuri ya wahusika waliobeba dhamira

mbalimbali, hivyo kufanya kazi imvutie msomaji na kuchangamsha

hadhira. Kuna mfano wa shairi (uk 62).

Ari yetu ndio mwokozi wetu

Ari yetu lazima tuisujudie, Ari hii ya mwaka tuliyoivumbika, Iliyojaa joto lisiloburudika

Ije ituongoze mpaka mwisho kufika,

Na kutuzimia kiza cha mwaka

JINA LA KITABU

Jina la kitabu linasadifu yaliyomo. KILIO CHA HAKI, kitaswira

linaangalia matatizo na manung’uniko yaliyokuwa yakiwakumba

wafanyakazi katika shamba la bwana Delamon.

Matatizo hayo ni kama vile, ujira mdogo, kufanya kazi kwa muda

mrefu, mazingira mabovu ya kazi pamoja na vifaa hafifu vya

utendaji kazi, pia ukosefu wa demokrasia.

Matatizo na manung’uniko hayo ni vilio vya haki ambayo

viliwapelekea wawe na vilio kutafuta ufumbuzi wa matatizo hayo au

waweze kujikomboa kutoka kwenye mikono ya makaburu.

“uk 9. Wafanyakazi walivyokuwa wakitoa sauti”. “Nirudishe jasho

langu, nirudishe damu yangu, nirudishe haki yangu, nirudishe utu

wangu” (uk 36-42 na uk 8).

Page 22: FANI KILIO CHA HAKI

REJEA

Gereld Njagi Matti. (2001).Introduction to the Study of

Literature.

Senkoro. (1982). Kitabu cha Fasihi.

Roninson Kruso. (1790). Vita na Amani.