anamed team DAWA ZA ASILI KATIKA NCHI ZA TROPIKI II MATIBABU Matibabu ya magonjwa ya kawaida na matumizi ya baadhi ya mimea muhimu katika nchi ya tropiki. Kitabu cha Semina Ki-suahili Numba: 119
anamed team
DAWA ZA ASILI KATIKA NCHI ZA
TROPIKI
II MATIBABU
Matibabu ya magonjwa ya kawaida na matumizi ya
baadhi ya mimea muhimu katika nchi ya tropiki.
Kitabu cha Semina Ki-suahili Numba: 119
Kitabu hiki kimeandikwa na anamed team: Dr. Hans-Martin Hirt, Dr.Peter Feleshi, Philip
Mateja, Dr. Lindsey na washiriki wengine wengi wa anamed.
Anamed Angola: Baptista Nsenda, Margarethe Roth
Anamed Congo – Kinshasa: Konda Ku Mbuta, Bindanda M´Pia
Anamed Congo South Kivu: Innocent Balagizi
Anamed Congo Prov. Equator: Dieudonne, Akuma Tande
Anamed Eritrea: Nighisti Alazar, Micele Paliaro
Anamed Ethiopia: Ralph Wiegand, Belay Bekele, Temesgen Choleyea
Anamed India: Sr. Rosita Kandathil, Kambala Subramanyam
Anamed Kenya: Roger Sharland, Rebecca Nzuki
Anamed Mozambique : Pascoal Cumbane, Myriam Wahr
Anamed Nigeria: YMCA Jos
Anamed Afrika Kusini: Margrit Hirt
Anamed Sudan: Dr. Elijah
Anamed Tanzania: Philip Mateja, Peter Feleshi, Maike Ettling
Anamed Uganda Christopher Nyakumi
na msaada wa uchunguzi wa Prof. Dr. Christoph Schäfer
Kwa toleo hili la ki-swahili tunamshukuru Emmanuel Biligeya kwa kazi yake ya utafsiri na
Mchg Hezron Shimba na Maike Ettling kwa kuhariri. Pia tunaishukuru HUYAMU (Idara ya
Afya ya AICT – Dayosisi ya Mara & Ukerewe) kwa ushirikiano wao wa karibu.
Toleo la tatu September 2015
© 2008 Hakimiliki na anamed
Anamed ingependa taarifa zilizo katika kijitabu hiki zisambazwe mahali popote zinapowezekana
kufika. Tunawahamasisha watumiaji wa kitabu hiki kukitafsiri katika lugha zao. Hata hivyo kwa
kuwa mambo yaliyomo yanaboreshwa mara kwa mara, tafadhali wasiliana na anamed kwanza.
Haki miliki ya tafsiri zote inabaki na anamed. Hakuna sehemu ya kitabu hiki inayoruhusiwa
kuchapwa na kuuzwa tena.
Mabango ya rangi (anamed No. 403) vinaonyesha mimea iliyoelezwa katika kitabu hiki.
Toleo la pili la kitabu hiki linapatikana katika lugha ya kifaransa, kireno, kijaluo, kiamharic,
kiateso na kichichewa. Baadhi ya vitabu vya anamed vinapatikana katika baadhi ya nchi za
Afrika.
Wafuatao wanaunganisha anamed na ndio wauzaji na wasambazaji wa vitabu na vifaa vya
anamed:
anamed, Schafweide 77, D – 71364 Winnenden, Germany
Email: [email protected]
Website: www.anamed.net
mailto:[email protected]://www.anamed.net/
YALIYOMO
Sehemu I: Kuzuia magonjwa ya kawaida Sura 1: Kuzuia magonjwa ya kawaida....................…………………………..3
Sehemu II: Tiba ya magonjwa ya kawaida Sura 2: Vidonda, kuungua, majipu na uvimbe………………………………...5
Sura 3: Magonjwa ya ngozi……………………………………………………8
Sura 4: Kuharisha…………………………………………………………….11
Sura 5: Malaria ………………………………………………………………16
Sura 6: UKIMWI: Imarisha mfumo wa kinga mwilini………………………19
Sehemu III: Matumizi ya baadhi ya mimea
muhimu ya nchi za Tropiki Sura 7: Allium Sativum (kitungu saumu)……………………………………21
Sura 8: Artemisia annua anamed (A – 3)…………………………………….23
Sura 9: Azadirachta Indica (Mwarobaini)…………………………………….38
Sura 10: Carica papaya (Mpapai)…………………………………………….42
Sura 11: Moringa oleifera (Mlonge)
Sehemu IV: Utengenezaji wa baadhi ya madawa Sura 12: Mafuta na dawa za mafuta …………………………………………47
Sura 13: Jiwe jeusi……………………………………………………………49
Sehemu V: Msingi wa matumizi ya dawa za asili Sura 14: Kazi ya kikundi – Maendeleo ni nini?...................................
Sura 15: Anzisha bustani ya mimea ya madawa……………………………...50
Sura 16: Mawazo ya ki-biblia ………………………………………54
Sura 17: Mwongozo na maadili kwa “Waganga wa asili”.……………………55
anamed
Madawa ya asili katika nchi za Tropiki: Matibabu II
Matibabu, mimea, madawa, kazi ya vikundi na maadili.
Kitabu cha maelezo kwa semina ya madawa ya asili
kwa muda wa juma moja.
Na anamed team na
Washiriki wengi wa anamed duniani kote.
anamed (Action for Natural Medicine) ni shirika la Kikristo na Muungano wa huduma
unaolenga kusaidia watu katika nchi za Tropiki kujitegemea kadri iwezekanavyo, hasa kwa
masuala ya kiafya. anamed inafanya kazi na watu wa imani zote waliojitoa kuinua hali ya afya
ya majirani zao, mkoa na taifa.
anamed inafanikisha lengo hili kwa kuwasikiliza waganga wa jadi, kufanya uchunguzi wake
binafsi, na kuboresha mchanganyiko wa madawa kwa matibabu. Tunatoa matokeo katika kitabu
kiitwacho “Dawa za asili katika nchi za tropiki.” Kwa hiyo tangu 1985, tumeweka wazi kwa
watu wote ujuzi wetu wote juu ya afya na uponyaji kwa kutumia mimea inayopatikana bure kwa
jamii nzima. Hatuna siri, na hakika hatuna sheria inayozuia kuigwa!
anamed inatoa ujuzi na uzoefu huu, hasa katika Afrika, kwa kuendesha semina za “Dawa za
asili” kwa muda wa juma moja kwa wafanya kazi wa afya, madaktari, waganga wa jadi, viongozi
wa dini, wahudumu wa jamii na kadhalika. Semina inapitia utambuzi na uchunguzi zaidi wa
baadhi ya mimea ya dawa, utayarishaji wa madawa kutokana na mimea hiyo, matumizi yake
katika tiba na matatizo ya kawaida ya kiafya na magonjwa.
Kwa kusema “dawa za asili,” anamed ina maana ya muungano wa faida za madawa ya jadi na
zile za huduma za tiba za kisasa zenye msingi wa kisayansi.
Kitabu kiki, kitabu cha pili katika mfululizo wa “Dawa za asili katika nchi za Tropiki,” ina
karibu masomo yote yanayohitajika kwa mafunzo ya semina kwa juma zima la kwanza katika
dawa za asili. Nafasi hairuhusu maelezo zaidi juu ya falsafa ya kazi yetu, ingawa jambo hili ni la
muhimu sana. Jambo hili limeelezwa katika kitabu cha kwanza, ambacho pia kinaeleza mimea
mengi zaidi na kina maelezo zaidi juu ya kujitengenezea dawa nyumbani. Kitabu cha tatu ni
msaada wenye taarifa nyingi kwa viongozi wa semina. Kitabu cha nne kimetolewa kwa ajili ya
huduma kwa wanaoishi na VVU/UKIMWI.
Sehemu I ya kitabu hiki inaelezea jinsi ya kuzuia baadhi ya matatizo ya kitabibu yaliyo ya
kawaida katika nchi za tropiki, na sehemu ya II ni juu ya kutibu. Sehemu III inaelezea mimea na
miti mitano maalumu, ambayo yote inaweza kustawi katika nchi za tropiki. Kwa miti hii mitano
tu matatizo mengi ya kiafya yanaweza kutibiwa. Kwa nyongeza, unaweza kupata chakula chenye
virutubisho, kusafisha maji, kurutubisha ardhi na kutengeneza kiuatilifu kizuri. Sehemu ya IV
inaeleza jinsi ya kutengeneza baadhi ya madawa. Na sehemu ya V inatoa baadhi ya msaada kwa
ajili ya semina, pamoja na mtiririko muhimu wa rejea kwa ajili ya waganga wa dawa za asili.
Ukishahudhuria semina ya anamed juu ya dawa za asili, tafadhali endelea kuwasiliana na
wengine katika mkoa wako na nchi yako ambao wanatibu kwa madawa ya asili. Panga
kutembeleana, endesha mafundisho, na julisha anamed International huku Ujerumani juu ya
mafanikio yako! Asante!
Sehemu I
Sura 1:
Kuzuia magonjwa ya kawaida. Kama tukijali mtindo wetu wa maisha, lishe, afya na mazingira tunayoishi tunaweza kutoa
mchango mkubwa sana katika afya bora ya familia zetu, mimea yetu na wanyama.
1.1.Kula vizuri!
Mara nyingi ni tatizo kwamba, watu wakitajirika kidogo, ubora wa lishe yao unashuka.
Vyakula bora (angalia jedwali hapo chini) vinatujengea nguvu na mfumo wetu wa kinga
mwilini – yaani uwezo wetu kushambulia maambukizi na magonjwa. Vyakula visivyo
bora kama vile sukari nyingi, unga uliokobolewa, mkate mweupe, soda mbalimbali,
vyakula vya kwenye makopo, hupelekea ukosefu wa vitamini na protini. Kwa hiyo
tunakuwa na uwezekano mkubwa kupata maambukizi yoyote na magonjwa.
Jedwali I: Vyakula vya ki-msingi
Kwa kupata nguvu kwa
urahisi
Mizizi ya wanga: Mihogo, viazi vitamu, “Taro”
Matunda ya wanga: Ndizi, “breadfruit”
Kwa kupata nguvu na
protini
Nafaka na mbegu: Ngano, mahindi, mchele, mawele,
mtama, mkate. Kula mkate wa unga usiokobolewa na
unga wa mahindi yasiyokobolewa.
Epuka mkate uliotengenezwa kwa unga mweupe na
mahindi yaliyokobolewa!
Kwa chakula chenye protini
kwa wingi
Mbegu za mafuta: boga, tikitimaji, ufuta na alizeti.
Jamii ya kunde: maharage, njugu, dengu, soya zenye
kokwa, karanga, korosho, “almonds”
Mazao ya wanayama: maziwa, mayai, jibini, samaki,
kuku, na nyama yoyote.
Kwa vitamini na madini Mboga: majani ya kijani – nyeusi, majani ya mihogo,
viazi vitamu na majani ya viazi vitamu, nyanya, karoti,
maboga, majani ya mlongelonge, mbegu za amaranth na
mengine zaidi.
Matunda: maembe, machungwa, limao, mapapai, mapera,
passion fruit n.k.
Jusi ya matunda.
Kwa kinga imara ya mwili Kula vitunguu swaumu vibichi, unga wa majani ya
mlonge, mbegu za amaranth, nyama laini ya jamii la
msubili.
Lima matunda, mbogamboga na mimea ya madawa wewe mwenyewe! Siyo jambo lililopitwa na
wakati wala rahisi! Vyakula vya kujitengenezea kutokana na bustani ya nyumbani ndivyo
vyenye virutubisho bora zaidi.
Lisha watoto mara kadhaa kwa siku. Wanahitaji vyakula kidogo kidogo mara kwa mara.
Kunywa jusi ya matunda halisi – nchi za Tropiki zina wingi wa matunda !
Hatari za lishe mbaya
a) Watu wa Afrika kwa sasa wanakula sukari zaidi kuliko ilivyowahi kutokea. Soda zina sukari
nyingi, hata wanga katika mkate mweupe unabadilishwa na vimengenya kuwa sukari mdomoni.
Matokeo yake watu wengi sasa wameoza meno na kupata kisukari au matatizo mengine ya afya.
Wengi hawawezi kugharimia matibabu yake. Kwa hiyo punguza utumiajii wa sukari ya
kiwandani. Na jaribu kunywa chai na kahawa bila sukari!
b) Watoto wanaokula mkate mweupe, ugali wa mahindi na mihogo wanaweza kuingia katika hali
ya utapiamlo kwa sababu ya upungufu wa protini, vitamin na madini.
c) Kama kwa vyovyote ikiwezekana, nyonyesha mtoto kwa maziwa ya titi – usishawishiwe na
matangazo ya biashara juu ya maziwa ya chupa kwa mtoto. Uchafu na maambukizi mengine
yananywewa na mtoto kwa urahisi kupitia hizi chupa, ambapo hupelekea kuharisha na
magonjwa mengine. Vyakula vya madukani vya watoto hudhoofisha mtoto wako na uchumi wa
familia yako!
d) Matukio ya saratani na madhara ya ki-afya yanaongezeka kwa sababu ya kuongezeka kwa
idadi ya madawa ya viwandani kutengenezwa. Soda na vinywaji vitamu vingine pamoja na
bidhaa zingine za kibiashara zinakuwa na madawa na sukari ya kiwandani ambazo zinaweza
kuharibu afya yako. Vyakula vya makopo pia vinakuwa na madawa hatarishi ya kuhifadhi
chakula. Hata Blue Band ya mikate ina hayo madawa ya kuhifadhi chakula. Ni vizuri zaidi
kupaka embe mafuta kwenye mkate wako!
Madawa hatarishi ya viwandani yanakuwepo sio tu kwenye vyakula vya madukani, lakini pia
kwenye kilimo (kama mbolea ya madawa ya kuulia wadudu), katika moshi ya magari na hata
kwenye nguo na vifaa vya ujenzi.
1.2. Angalia maji yako! Hakikisha maji unayokunywa ni salama. Kutokana na ubora wa maji yako, unaweza kutengeneza
chujio la maji kwa mchanga, unaweza kutumia mbegu za mlongelonge zilizosagwa kama
ilivyoelezwa katika sura ya 11, au unaweza kuchemsha maji katika jiko la jua.
Shirikiana na wengine kuhakikisha mto wako unabaki msafi. Toeni matakataka yote! Kama
watu wakifulia nguo zao, au hata baiskeli na magari, katika maji ambayo wengine wanakwenda
kutumia kwa kunywa, basi wanasababisha matatizo ya afya!
1.3. Rutubisha ardhi yako – kiasili.
a) Panda mimea jamii ya kunde (ambayo huongeza naitrojeni kwenye udongo). Mimea jamii ya kunde ni pamoja na mboga kama vile maharage na karanga, miti kama vile
Lusina. Lusina inaweza kupandwa kufuata kontua kuzuia mmonyoko wa ardhi, na zikatwe
ncha zake mara kwa mara ili kutengeneza uzio. Matawi yanayokatwa yanasaidia
kurutubisha udongo.
b) Ozesha takataka za mimea, maganda yote ya matunda, majani ya mboga, takataka za shambani (lakini epuka mbegu za magugu), samadi ya kuku na wanyama wengine
virundikwe (siyo karibu sana na nyumbani lakini). Kama vikidumishwa katika hali ya
unyevu na uvuguvugu, udongo mzuri mweusi utapatikana ndani ya miezi 3, ambao,
ukichanganywa katika shamba lako, utaweka virutubisho (naitrojeni na madini) taratibu
kwenye shamba lako.
c) Tandazia nyasi – angalia sura ya 14. d) Epuka matumizi ya madawa hatarishi ya kilimo. Usitumie au tumia kiasi kidogo sana
cha mbolea za viwandani au dawa za kuua wadudu. Zinachafua maji, zinaua viumbe,
wanyama na mimea visivyo na madhara (na zaidi vyenye umuhimu) na zinadhuru rutuba
ya asili katika udongo.
1.4. Vyoo vya kienyeji ni visafi na ni rahisi kutumia!
Kinyesi na mkojo vinaweza kuwa vyanzo vya maambukizi mengi. Chimba shimo, jenga kijumba
juu yake. Tundu la shimo lazima lifunikwe wakati wote. Kama ukiweka dohani ambayo
huchukua hewa kutoka kwenye shimo hadi juu ya paa, choo hakitatoa harufu. Shimo likijaa,
lifunike kwa udongo na upande mwembe juu yake! Kisha tengeneza choo kingine cha kienyeji
mahali pengine. Vyoo vya kienyeji vinatunza rutuba ndani ya ardhi, wakati ambapo vyoo vya
maji vinachafua vijito na mito. Na vinatumia maji kidogo, ambayo katika sehemu nyingi
yamezidi kuwa adimu.
1.5. Tupa takataka kwa uangalifu !
Katika miji mingi unaweza kuona “moto wa milele”, ambao mara chache unazima na ambamo
takataka - ikiwa ni pamoja na plastiki na metali – vinatupwa. Moto huu una moshi mweusi mzito
wenye sumu kali zinazoitwa dioxins.
Takataka zinazozagaa hazipendezi. Vitu vyenye ncha kali vinaweza kukata watu, betari na
baadhi ya vifaa vya umeme vina sumu, ni pamoja na maji ya mvua yaliyotuama katika mifuko ya
plastik, magurudumu yaliyochakaa ambamo pia hutengeneza sehemu za mbu wa malaria
kuzaliana.
Kwa hiyo tupa takataka zako kama ifuatavyo:
Mara utakapozoea kutenganisha takataka zako namna hii nyumbani kwako, wafundishe mfumo
huu kijijini kwako au hata mjini unapoishi.
a) NDOO YA KIJANI: Tupa kila siku: Kwa ajili ya takataka za ki-mimea kutoka bustani yako au jikoni (“0rganic waste”). Uziozeshe kupata mbolea. Au afadhali zaidi: uwalishe
kuku zako na takataka za ki-mimea ili panya na nyoka wasikaribishwe karibu na nyumba
yako
b) NDOO YA BLUE: Tupa kila wiki: Kwa ajili ya karatasi. Ukusanye kwenye ndoo na mara moja kwa wiki choma karatasi pamoja na plastiki inayoweza kuchomwa ndani ya dakika 5.
Majivu yatupwe pamoja na metali.
c) NDOO NYEKUNDU: Tupa kila mwezi. Kwa ajili ya metali, vioo, plastiki, betari. Kama kuna uwezekano wowote wa kuvitumia tena au kuvibadilisha kuwa vitu vingine, fanya
hivyo. Sisitiza serikali yako idai fedha za kuwekesha kwa kila mfuko wa plastiki na chupa za
vioo inayouzwa, ili kwamba ziweze kutumika tena au kurudishwa viwandani. Vikusanye
kwa uangalifu, na kama hakuna mfumo wa kuweza kuvitumia tena kila mwezi uvizike chini
sana kwenye udongo. Betari hasa zina sumu! Usipande mboga zako juu ya shimo hilo!
d) Mbao: Uchome na uweke majivu yake shambani, yana madini yenye thamani.
1.6. Mifuko ya Plastiki
Baadhi ya nchi za kiafrica sasa zinazuia matumizi ya mifuko ya plastiki. Katika miji mifuko ya
plastiki pamoja na chupa zimekuwa zikichafua mazingira na yanapochomwa yanatoa hewa za sumu.
Imekuwa ikiziba mifereji ya maji na kusababisha mafuriko mvua kubwa zinaponyesha.
Mashambani, mifuko ikiliwa na ng´ombe na mbuzi inaziba matumbo yao na wanyama wanakufa.
Hata watoto wanaweza kufa baada ya kuchezea mifuko ya plastiki au chupa zilizoathiriwa na mate
au kinyesi.
1.7.Usafi na Afya
Wakati wote osha mikono yako kwa sabuni na maji kabla ya kula au kutayarisha chakula, na baada
ya kutoka chooni. Kama huna sabuni jitengenezee, au sugua mikono yako kwa maji ya majani ya
mpapai.
Kuoga mwili mzima kila jioni hufanya mwili na kitanda kuwa safi.
1.8. Kwa upishi wa ndani, weka dohari!
Kama wakati mwingi chumba chako kimejaa moshi basi uko katika hatari kubwa ya kupata matatizo
makubwa ya macho na magonjwa ya mapafu. Ufumbuzi bora zaidi wa tatizo hili ni kutengeneza jiko
linalotumia nishati kidogo (maana yake matumizi ya kuni kidogo ) pamoja na dohani.
1.9. Mazoezi na uimara wa mwili
Watu wengi wana mazoezi mengi, mfano wanawake wanaotembea kilometa nyingi kila siku
kutafuta kuni na maji. Wengine wana mazoezi kidogo sana. Je familia yako “ina maendeleo“au
“haijaendelea”? Katika familia “zilizoendelea” mwanaume na mwanamke wanafanya kazi kwa
pamoja, hivyo wana mazoezi yanayofanana. Kwa njia hii mke hawi dhaifu sana, wala mme hanenepi
sana. Kama ukiuweka mwili katika hali inayofaa, utakuwa na kinga bora zaidi kwa magonjwa.
1.10. Zuia ajali za barbarani
Kuongezeka kwa kasi kwa idadi ya magari inaongeza matukio ya ajali zinazosababisha majeraha
makubwa na vifo katika nchi za joto. Himiza kampeni za kuangalia usalama wa magari, vidhibiti
mwendo, vipunguza moshi wa magari na njia za ziada kwa wote watembea kwa miguu na
waendesha pikipiki
SEHEMU II MATIBABU YA MAGONJWA YA KAWAIDA
SURA 2 Vidonda, kuungua, majipu na uvimbe
Tumia kitambaa kilicho safi. Wakati wa dharula, kama unahitaji huduma lakini ukawa huna
kitambaa, chukua vipande vya nguo hasa za pamba. Ili kuzifanya salama zichemshwe katika
maji kwa dakika 20 na zikaushe kwa kutumia kaushio la jua (sola) lililo safi au kama huna
kaushio la jua zikaushe kwa kuanika kwenye kamba ya nguo juani.
Muhtasari ya tiba ya vidonda, kuungua na uvimbe:
Aina ya Ugonjwa Chaguo la kwanza Chaguo la pili Chaguo la tatu
Vidonda
Vidonda
vipya
Tibu kwa sukari Tibu kwa asali Tibu kwa papai
lililoiva
Vidonda
vyenye
uambukizo
Papai na sukari Tibu kwa papai
bichi ukibadilisha
na tiba ya sukari
Embwe la majani
ya mpera
Kuungua
Kuungua
kupya
Ute wa Aloe
(msubili)
Maji ya chumvi Osha kwa chai ya
mpera
Kuungua
kuliko na
uambukizo
Utomvu mweupe
wa mpapai, maji
yenye chumvi
Ute wa Aloe
(msubili)
Dawa ya mafuta ya
vitunguu
Jipu
Jipu
lililofungwa
Vitunguu saumu
vilivyopondwa
pondwa
Dawa ya pilipili ya
mafuta
Dawa ya mafuta ya
vitunguu
Jipi lililo wazi Papai na sukari Tibu kwa papai
bichi ukibadilisha
na tiba ya sukari
Embwe la jani la
mpera
A. Vidonda
Lengo kuu la tiba hii ni kuzuia kidonda kupata maambukizi, hivyo kuruhusu mchakato wa mwili
kujiponya wenyewe vizuri iwezekanavyo.
a) Kwanza osha kidonda.
Kwa Vidonda vilivyo wazi, visafi, vipya, visivyo na usaha
Tumia ama i) Maji baridi yaliyochemshwa na kuwekewa chumvi kidogo,
au ii) Chai ya mpera:
Chemsha kiganja 1 cha majani ya mpera kwenye lita 1 ya maji kwa muda wa
dakika 15. Yapoe na baadaye yachuchwe. Osha kidonda kwa kutumia maji haya.
Tengeneza upya kila unapoosha kidonda.
Kwa kidonda kinachoonesha dalili za maambukizo,
tumia maji yenye utomvu wa mapapai
Maji yenye utomvu wa mapapai: Kama kidonda ni kichafu ukioshe mara kadhaa kila siku kwa
kutumia maji yenye utomvu wa mapapai. Osha papai bichi lililopo mtini kwa kutumia kitambaa
safi na maji safi ya moto. Weka lita 1 ya maji yaliyochemshwa na kupoa kwenye chupa safi.
Ongeza kijiko 1 cha mezani cha chumvi na koroga vizuri. Kata papai na kukusanya matone 3 – 5
ya utomvu wake kwenye chupa ile (kama ilivyooneshwa kwenye picha ya kitabu hiki). Usitoe
tunda kwenye mti, kwa sababu utomvu unakauka kwa haraka papai linapovunwa. Lakini
ukiliacha kwenye mti unaweza kuendelea kulitumia mara kwa mara.
A. 1. Vidonda safi, vilivyowazi na visivyo na usaha
A.1.a. Sukari pekee
Rundika sukari kwenye kidonda. Funga kidonda kwa kitambaa ili kuzuia sukari isitoke. Sukari
huondoa unyevu kwenye vimelea vya magonjwa kwa mchakato uitwao mfyonzo (osmosi) na
vimelea hivyo hufa.
Kihudumie kidonda mara 3 kwa siku kwa kuongeza sukari, usikioshe.
A.1.b. Mchanganyiko wa asali na sukari
Hakikisha una asali halisi. Njia bora ni kununua sega la nyuki, na ukamue asali mwenyewe. Hii
inafanyika kwa namna hii: Pondaponda sega hilo. Unaweza kufanya hivyo kwa kutumia kinu
kipya au chombo cha kusagia nyama ikiwa kimeondolewa kitufe cha kusagia. Ni vizuri kufanya
hivyo usiku ili kuepuka kusumbuliwa na nyuki. Sambaza mchanganyiko huu kwenye kitambaa
safi cha pamba kilichofungiwa juu ya bakuli safi la metali. Viweke kwenye jiko la jua (solar
oven) mchana kutwa hadi asali na nta vyote vivujie kwenye bakuli. Vitaunda matabaka tofauti.
Jioni funua jiko la jua na ondoa nta, ambayo inaweza kutumika baadaye kwa kutengeneza dawa
za mafuta (angalia sura ya 12).
Sasa asali ni tayari kwa matumizi. Weka kiwango sawa cha asali na sukari. Sukari huzuia asali
kusambaa kwa urahisi. Asali huua bakteria na kuacha kidonda kikiwa safi. Kidonda kitibiwe kwa
mchanganyiko wa asali na sukari mara kadhaa kwa siku pasipo kukiosha tena.
A.1.c. Papai lililoiva (Carica papai)
Weka kipande chembamba na laini cha papai lililoanza kuiva juu ya kidonda.
A.2. Vidonda vyenye maambukizo, majipu yaliyopasuka ya siku nyingi, vidonda vya wazi
Papai (Carica Papai)
Kwa matayarisho ya papai yafuatayo, vidonda vya wazi vilivyokuwa sugu kwa miaka mingi
vimeweza kupona, kwa kawaida hata ndani ya wiki 1. Hii ni moja kati ya mifano kadhaa ambapo
dawa za asili zimekuwa bora kuliko madawa ya hospitalini.
Tumia matayarisho yafutayo ya mapapai hadi kidonda kisiwe na usaha tena. Kisha tibu kidonda
kwa sukari au mchanganyiko wa asali na sukari.
A.2.a. Sukari ya papai
Changanya gramu 10 za sukari (nusu ya kikopo cha mikanda ya picha) na matone 10 ya utomvu
wa papai bichi. Tengeneza upya kila siku. Tusemapo sukari „halisi“ tuna maana ya sukari
ambayo imechukuliwa moja kwa moja kutoka kwenye mfuko mpya kwenye kiwanda. Weka hii
sukari ya papai kwa wingi kwenye kidonda, na mara tu inapoanza kuwa na majimaji ongeza
nyingine. Kidonda kinaweza kuhitaji huduma hii mara kadhaa kwa siku.
A.2.b. Papai bichi
(i) Kipande chembamba: Weka kitambaa kwenye maji yanayochemka, wakati kikiwa bado cha
moto sana osha papai bichi vizuri ambalo bado liko mtini. Osha kisu, kiweke ndani ya maji
yanayochemka kwa dakika kadhaa, kisha kata kipande chembamba cha papai chenye unene wa
kidole kidogo cha mtoto. Kiwekwe juu ya kidonda na ukishikize kwa kukifunga kwa kitambaa.
Usikiondoe kwa masaa 8. Kama kikisababisha maumivu sana kiondoe mapema! Fanya huduma
hii mara 3 kwa siku kwa siku kadhaa hadi kusiwe na usaha tena. Endeleza tiba hii na pia tumia
tiba ya sukari kama tiba mbadala kwa hii. Baada ya kila huduma ya sukari rudi kwenye mti,
ondoa sehemu ile nyembamba ya lile papai ambayo kwa sasa itakuwa chafu, kisha kata na weka
kipande chembamba kinachofuata kwenye kidonda.
(ii) Vijiti: Vidonda vyembamba vyenye kina mara nyingine hutokea, kwa mfano, kwenye
migongo ya wagonjwa waliolazwa muda mrefu. Katika mazingira yasiyo na maambukizo,
waganga katika hospitali wanaweza kukata vipande vyembamba vya papai bichi na kuviingiza
kwenye kidonda.
A.2.c. Embwe la majani ya mpera (Psidium Guajava)
Tiba hii haina gharama yoyote. Kwa hiyo inapatikana kwa wale wasioweza hata
kununua dawa za gharama ya chini kabisa. Twanga kiganja kizima cha majani ya mpera
yaliyooshwa. Yachemche taratibu pamoja na kikombe cha maji kwenye chungu kilichofunikwa
kwa dakika 15. Iache ipoe. Weka embwe kwenye kidonda na vifunge. Rudia tiba hii asubuhi na
jioni.
A.2.d. Papai lililoiva
Weka kijiko na bakuli katika maji yanayochemka kwa muda wa dakika 10 na kisha uvitumie
kusaga nyama za papai lililoanza kuiva na kusambazia embwe lake kwenye kidonda. Fanya
hivyo kwa kufuata kila hatua, asubuhi, mchana na jioni. Jinsi kidonda kinavyoonesha kuwa na
maambukizo zaidi ndivyo unavyotakiwa kutumia papai bichi zaidi.
A.2.e. „Gel“ ya Aloe (Msubili)
Kwa vidonda vya siku nyingi vilivyo wazi na vilivyokataa kupona, kifunike kidonda kwa gel ya
Aloe iliyochukuliwa moja kwa moja kutoka kwenye jani lililo kwenye mmea mara 3 kwa siku.
A.2.f. Mafuta ya Kitunguu saumu
Tumia mafuta ya kitunguu saumu (Allium Sativum), angalia sura ya 7.5. Weka mara kadhaa kwa
siku. Kwa kutengeneza kiasi kidogo cha mafuta ya kitunguu saumu changanya kijiko 1 cha
mezani kitunguu kilichokatwakatwa vipande vidogovidogo sana na vijiko 2 vya mezani vya
mafuta ya mimea. Weka kwenye chombo cha kioo, tikisa vizuri. Yatumike ndani ya masaa 24.
A.2.g. Mafuta au dawa ya mafuta ya vitunguu maji (Allium cepa):
Angalia sura ya 12
A.2.h. Kwa vidonda na majipu yanayotoa usaha tumia jiwe jeusi (angalia sura ya 13)
B. Kuungua
B.1. Kidonda kipya cha kuungua
Kwanza poza kidonda kwa maji safi ya baridi. Kumbuka, lengo kuu la huduma hii ni kuzuia
maambukizo. Mweke mgonjwa kwenye chandarua ili kuzuia inzi kwenye kidonda.
B.1.a. Aina za Msubili (Aloe barbadensis, Aloe ferox au Aloe arborescens)
Osha jani vizuri bila kuliondoa kwenye shina. Kisha likate toka kwenye shina. Osha kisu kikali
na ukiweke kwenye maji yanayochemka. Kwa kutumia kisu hiki, kata ile sehemu iliyo wazi tena
ili kuifanya iwe safi kabisa, na pia kata na kuondoa ncha zenye miiba. Kisha ukate katikati kwa
kufuata urefu ili kuweka wazi sehemu kubwa ya „gel“ iliyokatikati, ndani ya jani. Paka sehemu
ya majimaji ya jani la msubili kwenye sehemu yote iliyoungua. Rudia mara kadhaa kwa siku.
Mweke mgonjwa ndani ya chandarua kuzuia inzi. Msubili hufanya kazi ya kuzuia maambukizo
na kuzuia kuvimba.
B.1.b. Chumvi ya mezani
Yeyusha gramu 9 (kijiko 1 cha mezani kilichojaa kabisa) za chumvi ya mezani katika lita 1 ya
maji, chemsha kwa dakika 20 na iache ipoe. Mwagie mchanganyiko huu kwenye sehemu
iliyoungua mara kadhaa kwa siku. Kama kidonda kina kina kirefu, kifunge kwa „bandaji“ au
kitambaa kisafi (kilichoondolewa maambukizo). Mwaga haya maji ya chumvi mara kadhaa kwa
siku juu ya kitambaa hicho. Matone kadhaa ya utomvu kutoka kwenye papai bichi yanaweza
kuongezwa kama kuungua kunaonekana ni hatari sana. Kwa dharula, kama huna chumvi,
chemsha mkojo wa mgonjwa na utumie! Mkojo una chumvi!
B.1.c. Chai ya mpera (Psidium guajava)
Chemsha taratibu kiganja 1 cha majani mabichi yaliyooshwa ya mpera kwenye lita 1 ya maji
katika chungu kilichofunikwa kwa dakika 15. Acha ipoe na uichuje. Baada tu ya kuchuja osha
kidonda kwa chai hii. Rudia mara 3 kwa siku. Itakayobaki uimwage – tengeneza chai mpya kila
inapohitajika.
B.1.d. Mafuta na dawa ya mafuta ya kitunguu maji: Angalia sura ya 12.
B.2. Kuungua kuliko na maambukizo
B.2.a. Maji yenye utomvu wa papai na chumvi
Kama sehemu iliyoungua ni chafu, isafishe mara kadhaa kwa siku kwa kutumia maji ya utomvu
wa papai kama iliyoelekezwa hapo juu (A). Tumia pia “Gel” ya Aloe (angalia B.1.a.) au mafuta
ya vitunguu maji (angalia B.1.d.)
C. Majipu Jipu ni maambukizo yanayosababisha kifurushi kidogo cha usaha chini ya ngozi.
C.1. Jipu lililofungwa usaha chini ya ngozi, ni pamoja na majipu yaliyo na mdomo,
vidonda vilivyofungwa, maambukizo ya ngozi kuzunguka makucha ya vidole vya mkono
au miguu n.k.
C.1.a. Vitunguu saumu (Allium sativum)
(i) Kata vipande vyembamba vya vitunguu saumu na uvifungie kwenye sehemu iliyoathirika
(fanya hivi kwa usiku mzima kwa siku kadhaa) au
(ii) Pondaponda kitunguu saumu na upake sehemu iliyoathirika au
(iii) Tumia mafuta ya kitunguu saumu (angalia sura 7)
Vitunguu saumu vina nguvu sana kuliko vitunguu maji. Uwe mwangalifu: Mgonjwa mwenye
udhaifu wa ngozi anaweza kupata mabaka. Kufungia kitunguu saumu kwenye ngozi ndiyo njia
bora zaidi, lakini pia iletayo maumivu zaidi. Kupaka ngozi kwa mafuta ya vitunguu saumu ni
tiba dhaifu kidogo lakini pia isiyosababisha maumivu sana.
C.1.b. Dawa ya mafuta ya pilipili: Angalia sura ya 12
C.1.c. Kitunguu maji (Allium cepa)
Fuata matumizi ya vitunguu saumu hapo juu (C.1.a.). Badala ya mafuta ya vitunguu saumu tumia
dawa ya mafuta ya vitunguu maji (angalia sura ya 12). Dawa ya vitunguu maji siyo kali kama
dawa ya vitunguu saumu.
C.2. Jipu lililo wazi
Utibu kama vidonda vyenye maambukizo, angalia A.2.hapo juu.
Sura 3: MATATIZO YA NGOZI
A. Utangulizi: Matunzo ya ngozi na usafi Tengeneza na tumia sabuni inayolinda ngozi. Kwa kufua, tumia sabuni ya kujitengenezea
iliyotengenezwa kama ifuatavyo: Chukua vipimo 4 vya sabuni ya kawaida, na kipimo 1 cha
mafuta ya mboga na kipimo 1 cha maji. Pondaponda sabuni, ichanganye na mafuta na maji.
Chemsha mchanganyiko polepole hadi sabuni itakapoyeyuka. Koroga mchanganyiko huo mpaka
utakapopoa, kisha uumwage kwenye vyombo vya chapa. Acha kwa majuma 2 kabla ya
kuutumia. Sabuni hii inaweza kuwekewa dawa kwa kudondoshea matone kadhaa ya mafuta ya
mwarobaini, au majani makavu yaliyopondwa yanayotokana na mwarobaini au mlongelonge
kabla ya kuimwaga kwenye vyombo vya chapa.
B. Matatizo mbalimbali ya ngozi
Kwa matatizo ya ngozi yasiyojulikana chanzo chake, kunywa mchanganyiko wa aina mbalimbali
za chai za dawa, hasa Rozela na Artemisia, ili kuondoa sumu mwilini. Zinasaidia kusafisha
damu, kulainisha takataka kwenye utumbo mkubwa, na kuzisaidia kutolewa nje hadi chooni.
Uchafu na takataka mwilini zinaweza kusababisha matatizo ya ngozi.
Kwa matibabu ya ngozi, tunapendekeza uanze na matibabu rahisi zaidi yanayonawirisha ngozi
(yaliyotajwa mwanzoni), na endelea kwa utaratibu hadi kwenye zile zenye nguvu - lakini pia
madhara - zaidi.
Persea americana (avocado/ embe-mafuta) Upakaji wa nyama ya embe-mafuta lililoiva hufanya kazi kama huduma ya msingi ya kuanzia
au dawa nzito ambayo hunawirisha ngozi yenye maambukizo au ngozi kavu. Dawa hii
inaweza kutayarishwa jioni kwa kutumiwa kwa urembo; lakini lazima itumike haraka baada
ya kutengenezwa. Changanya nyama ya embe-mafuta lililoiva na matone kadhaa ya limau na
upake kwenye sehemu iliyoathirika kwa muda wa masaa 12 kwa siku; kwa mfano usiku
mzima. Nyama ya embe-mafuta inaweza pia kutumika kama kiungo cha msingi kwa madawa
au vipodozi, mfano: kwa kuchanganya na maji ya limau, mafuta ya mbegu za mwarobaini,
nyama ya msubili n.k.
Mafuta ya mbegu, kama vile mafuta ya mbegu za mchikichi, mafuta ya alizeti, mafuta ya karanga. Changanya kijiko 1 cha chai cha mafuta kwa kipimo kilekile cha maji kwenye
kiganja cha mkono wako na usugue kwenye sehemu iliyoathirika.
Nyama ya msubili: angalia sura ya 2.
Brassica oleracea (kabeji): Tengeneza uzingo kutokana na jani la kabeji liliooshwa, na ulizungushe sehemu iliyoathirika. Huko Nigeria, mtoto mmoja aliamka mara 4 kila usiku
akitoka damu, mwenye ngozi kavu. Kumzinga kwa jani la kabeji kulileta nafuu haraka.
Mafuta au dawa ya mafuta iliyotengenezwa kutokana na mafuta ya mbegu na mimea kama vile mpera, chamomila au artemisia. Kwa mchanganyiko huu angalia sura ya 12.
Mafuta ya mbono (kutokana na Ricinus Commonis), ama iliyotengenezwa kiwandani, iliyotengenezwa kienyeji kijijini au iliyotengenezwa kwa kutumia mchanganyiko kutoka
“Madawa ya Asili katika Nchi za Tropiki I”.
Cassia alata (ringworm bush): Tengeneza embwe kwa kutumia majani yaliyopondwa na mafuta.
Azadirachta Indica (Mwarobaini): Tumia kama embwe la majani na mafuta au maji, au dawa ya mafuta kutokana na majani, au mafuta ya mbegu za mwarobaini.
Allium Cepa (Kitunguu maji): Tumia mafuta yake au dawa ya mafuta. Angalia sura ya 12.
Capsicum frutescens (pilipili): Paka mafuta ya pilipili au dawa ya mafuta yake kwenye sehemu iliyoathirika. Pilipili ina viasili vinavyoua maambukizo na mara nyingine huondoa
maumivu. Angalia sura ya 12.
Allium Sativum (vitunguu saumu – kama mafuta ya vitunguu saumu). Angalia sura ya 7.
“Mafuta ya upele”: Kipimo cha 50:50 cha mchanganyiko wa mafuta ya taa na mafuta ya mbegu hautumiki kwa upele pekee, bali pia kwa matatizo mengine, k.mf. maumivu
yanayosababishwa na filaria. Angalia D.1.
Allium Sativum (kitunguu saumu): Sugua kipande chembamba, au kifungie, kwenye sehemu iliyoathirika.
C. Maambukizi ya mba Maambukizi ya mba yanaweza kutokea kwenye sehemu yoyote ya mwili, lakini mara nyingi
yanapatikana katikati ya vidole vya miguu (athlete’s foot), au vidole vya mikono na katikati ya
paja. Baka (alama nyeupe ya mviringo kichwani) pia ni maambukizi ya mba. Sehemu
zilizoathirika zioshwe kila siku kwa maji na sabuni. Baadaye ziwekwe katika hali ya ukavu na
zihudumiwe kama ilivyoelekezwa hapo chini. Ikiwezekana, ukae kwenye hewa nzuri na mwanga
wa jua. Vaa nguo zilizotengenezwa kutokana na malighafi asilia, yaani pamba. Endelea na
matibabu hayo mpaka majuma 2 baada ya dalili kupotea.
C.1. Vigunguu saumu (Allium sativum)
Sugua mafuta ya vitunguu saumu (angalia sura ya 7.5) kwenye sehemu iliyoathirika. Kwa mba
wa kwenye vidole vya miguu unaweza kuweka kikonyo cha kitunguu saumu katikati ya vidole
vya miguu.
C.2. Ringworm bush (Cassia alata) na mbono au mafuta ya mawese.
Twanga majani mabichi ya Cassia alata, na uchanganye vijiko vyake 10 na kijiko 1 cha mafuta
ya mbono. Kama mafuta ya mbono hayapatikani, tumia mafuta ya mawese au mafuta mengine
ya mimea. Weka mara 3 kila siku. Tengeneza upya kila siku. Kama huna mafuta kabisa, twanga
haya majani mabichi na uyasugue kwenye sehemu iliyoathirika mara 3 kwa siku.
C.3. Ringworm bush (Cassia alata), papai na mafuta
Twanga kiganja kizima cha majani mabichi na machanga ya ringworm bush, ongeza matone 10
ya utomvu wa papai bichi na kijiko kizima cha mezani cha mafuta ya mbono au ya mawese.
Changanya na usugue kwenye sehemu iliyoathirika mara 3 kwa siku. Tengeneza dawa mpya kila
siku.
C.4. Dawa ya mafuta ya kuzuia mba. Tumia mwarobaini, melia au ringwormbush (Angalia
sura ya 12).
D. Upele (Scabies)
Upele hutambulishwa na uvimbe mdogomdogo unaowasha, ambao unaweza kutokea mwili mzima.
Katikati ya uvimbe huu kuna vipele vyeusi vidogovidogo zaidi vyenye vichwa vyenye ukubwa wa
vichwa vya sindano. Upele ni kawaida kwa watoto. Unapatikana zaidi katikati ya vidole vya
mikono, kwenye kiungo cha mkono na kitanga, kiuno, na sehemu za siri. Husababishwa na vijidudu
vidogo vinavyotengeneza njia chini ya ngozi. Unaambukiza kwa urahisi sana. Kama mtu mmoja
katika familia akiwa na upele, lazima familia nzima itibiwe. Usafi ni muhimu. Oga mwili mzima na
badilisha nguo zako kila siku. Nguo zote na matandiko lazima yafuliwe na kuanikwa juani. Njia
rahisi ni kuziweka kwenye jiko la jua. Safisha sehemu za chuma au za mbao za kitanda chako kwa
mafuta ya taa.
D.1. Mafuta ya taa na mafuta ya mboga (“Mafuta ya upele”)
Tayarisha mafuta ya upele kwa kuchanganya kikombe 1 cha mafuta ya taa na kikombe 1 cha mafuta
ya mboga. Mara 2 kwa siku na kwa siku 2 hadi 3, oga mwili mzima na upake mafuta ya upele
kwenye sehemu iliyoathirika. Mchanganyiko huu wa anamed kwa sasa unatumiwa na hospitali
nyingi. Matibabu haya ni mazuri pia kwa mwasho unaosababishwa na filariasis (minyoo
midogomidogo kwenye damu) kuzunguka kiuno. Filaria husafiri hadi sehemu nyingine za mwili.
Weka mafuta ya taa na haya mafuta ya upele mbali na moto na watoto pia.
D.2. Mafuta ya Vitunguu saumu (Allium sativum) Angalia C.1. hapo juu
D.3. Mwarobaini (Azadirachta indica). Angalia sura ya 9.
D.4. Mimea mingine
Kwa watu wazima wenye upele, na kwa upele kwenye sehemu ndogo, bila kuwa na fedha ya
kununua mafuta ya taa, na kama vitungu saumu na mwarobaini havipatikani, kuna njia tatu: Iliyo na
sumu ndogo zaidi ni Tephrosia vogelii (kibaazi). Chaguo la pili ni Rauwolfia vomitoria
(kimusukulu) na la tatu ni Nicotiana tabacum (tumbaku). Matumizi ya kila mmea ni kusugua majani
safi yaliyokomaa kwenye sehemu zilizodhurika. Mbadala ni bora zaidi kwa ngozi kuponda majani
haya na kuyachanganya na kiasi fulani cha mafuta ya mboga. Sugua mchanganyiko huu kwenye
sehemu iliyoathirika mara 3 kwa siku. Tengeneza mpya kila siku. Uwe mwangalifu, karibu mimea
hii yote ina sumu!
SURA 4: KUHARISHA
Mtu anaharisha wakati haja kubwa inapokuwa ya majimaji. Kama haja kubwa pia itakuwa na
kamasi na damu, tatizo linaitwa “kuharisha damu” (Dysentry).
Kuharisha ni ugonjwa hatari sana. Inahusika na vifo vya zaidi ya watoto millioni 3 katika nchi
zinazoendelea kwa mwaka. Karibu mara zote watoto wasingekufa – kama tu wazazi wao au hata
klinki zingejua matibabu yaliyoelezwa katika sura hii. Kuharisha ni hatari hasa kwa watoto
waliopungukiwa lishe.
Kuharisha kunaweza kuwa dalili za magonjwa mengine, ambayo pia yanahitaji matibabu,
angalia jedwali hapo chini 4.1. Kama ukienda chooni mara moja, lakini ukakaa huko siku nzima,
una kipindupindu!
Watoto wanapoharisha, wakati wote wapewe maji ya chumvi (Oral)! Watu wazima wangependa
kwanza kujaribu dawa rahisi zaidi kama vile dawa ya mkaa, matunda ya mpera mabichi n.k.,
lakini kama kuharisha kukiendelea, au kwa matatizo makubwa zaidi, maji ya chumvi ni ya
lazima kwa watu wazima pia! Mgonjwa lazima aendelee kula vyakula vinavyoongeza vitamini
na madini ya kutosha.
Mara nyingi kuharisha kunaweza kuzuiwa, hasa kwa kujali suala la usafi.
4.1. Jinsi ya kuzuia uharishaji.
a) Osha mikono yako kwa sabuni (au majani ya mpapai) na maji yanayotiririka kabla ya kula na baada ya kutoka chooni.
b) Usitumie chupa za watoto za kunyonyeshea kwa watoto - zina uwezekano mkubwa wa kusababisha maambukizo. Maziwa ya mama ni bora zaidi!
c) Wakati wote tupa chooni kinyesi cha watoto wachanga na wakubwa. d) Oga kila jioni na ulale sehemu iliyo safi. e) Watu wazima na watoto lazima watumie vyoo kwa haja kubwa na ndogo. Tundu la choo lazima
lifunikwe na kifuniko ili kuzuia inzi kusambaza maambukizo kutoka kwenye kinyesi kwenda
kwenye chakula. Pambana na mila na desturi zinazozuia matumizi ya vyoo.
f) Kula chakula kizuri, chenye lishe kamili na hamirojo (mfano: mahindi na mawele), protini (mfano: nyama na mayai) na vitamini (mfano: mboga na matunda). Angalia sura ya 4.
g) Kula vitunguu saumu mbichi na/au kipande cha jani la mpapai chenye urefu wa sm 5 za mraba kila siku ili kuzuia minyoo na maambukizo ya amiba. Njia hii ni msaada hasa kwa wale wenye
matatizo ya kuharisha mara kwa mara.
4.2. Jinsi ya kutibu kuharisha
A. Rudishia maji yaliyopotea, nguvu na madini kwa maji ya chumvi (Oral).
Kwa kuharisha, jambo la muhimu zaidi ni kufidia maji yaliyopotea. Kwa watu wazima na watoto,
wakati wote tumia maji ya chumvi na wakati wote jitengenezee maji ya chumvi mwenyewe.
Usitumie ya madukani (ORS) - ni gharama kubwa. Hatufurahishwi pia na viroba vya chumvi za
haya maji vinavyotolewa bure na umoja wa mataifa, maana jambo hilo linachochea hali ya
utegemezi! Kila mzazi lazima ajue jinsi ya kutengeneza maji-chumvi
A.1. Yaliyomo katika maji-chumvi.
Maji chumvi yana vitu 3: Maji, sukari, na chumvi. Maji ni muhimu kwa shughuli zote za mwili,
sukari kwa ajili ya nguvu, na chumvi kufidia chumvi iliyopotea wakati wa kuharisha.
Jedwali 4:1: Jinsi ya kutambua na kutibu kuharisha.
Dalili Sababu zinazoweza
kusababisha.
Tiba
Hakuna damu
kwenye kinyesi,
hakuna homa.
Sumu kwenye chakula. Watoto: maji-chumvi;
Wazima: maji-chumvi/ mkaa.
Kuharisha
kunakosababishwa na
virusi
Watoto: maji-chumvi,
Wazima: maji-chumvi/ mkaa
Kipindupindu (kuharisha Tumia maji-chumvi kwanza kisha
kwa nguvu ambako mharo
wake ni kama maji ya
mchele).
mpeleke hospitali.
Hakuna hospitali? Tumia antibiotic (ni
dawa za kuua bacteria).
Hakuna anti-biotic? Jaribu chai ya
anamed ya kuharisha (angalia B.3. chini)
au chai ya Artemisia.
Hakuna damu
kwenye kinyesi,
homa
Malaria Wakati wote tumia maji-chumvi; chai ya
mchachai wakati wote na dawa za kutibu
malaria (angalia sura ya 5).
Homa ya matumbo Maji-chumvi na antibiotic. Hakuna
antioitic? Jaribu maji-chumvi na chai ya
majani ya Azadirachta indica, au
Artemsia annua, au Vernonia amygdalina
au Melia azedarach.
Damu kwenye
kinyesi – hakuna
homa
Kuharisha damu sababu ya
amiba.
Maji-chumvi na chai ya mziwaziwa
(euphorbia hirta). Kuharisha kukiendelea:
Maji chumvi na chai ya kuharisha ya
anamed (angalia B.3 chini).
Damu kwenye
kinyesi au mkojo.
Hakuna homa.
Kichocho. Maji-chumvi. Jaribu chai ya artemisia
annua. Nenda kwenye Zahanati au
hospitali kwa matibabu.
Damu kwenye choo
na homa.
Kuharisha kwa sababu ya
bacteria (“Bacterial
Disentery”)
Maji-chumvi na chai ya kuharisha ya
anamed (angalia B.3. chini). Kama
hakuna maendeleo yoyote, nenda
Hospitali.
Hakuna Hospitali? Tumia antibiotic, maji-
chumvi na chai ya kuharisha ya anamed.
Hakuna antibiotic? Tumia maji-chumvi,
na ongeza Vinca rosea kwenye chai ya
kuharisha ya anamed hadi kuharisha
kukome. Angalia B.6. chini.
MAJI: Tumia maji mazuri, kama hakuna maji safi ya chemchemi, tumia maji yaliyochemshwa au tengeneza chai ya majani ya mpera na uitumie badala ya maji.
SUKARI: Hasa tumia asali, isipokuwa kwa watoto walio chini ya mwaka mmoja, ambao kwao haishauriwi kutumia asali. Kama hakuna asali, tumia sukari ya nyumbani (baadhi
ya hospitali zinatumia glucose). Kama huna sukari au mgonjwa ana kisukari, badala ya
gramu 30 za sukari kwenye mchanganyiko ulioelezwa hapo chini (A 2), unaweza
kutumia na kuchanganya vizuri moja kati ya vifuatavyo katika lita 1 ya maji:
a) Gramu 100 za ndizi tamu zilizosagwa (kama nusu kiganja, usichemshe). b) Gramu 100 za viazi vitamu (kama nusu kiganja, chemsha kwa dakika 10). c) Gramu 30 (vijiko 3 vya chai vilivyojaa sana) vya unga wa ngano, mchele
uliotwangwa au mtama. Chemsha kwa dakika 5.
CHUMVI: Hasa, tumia ile inayoitwa “chumvi ya kienyeji.” Hii inatengenezwa kwa kienyeji kwa kuchukua majivu ya miti iliyochomwa, ongeza maji, chemsha hadi maji
yakauke kwenye chungu cha udongo (kwa sababu vyombo vya metali vinaweza
kuharibika) na kukusanya chembechembe zinazojitokeza. Hii ni nzuri, kwa sababu ina
potassium. Ama sivyo tumia chumvi ya mezani (sodium chloride).
POTASSIUM: Ni kitu kinachopaswa kuongezwa kama chumvi ya mezani ikitumika na kama kuharisha kutaendelea kwa siku kadhaa. Potassium inasaidia misuli ya utumbo na
matumbo kufanya kazi vizuri. Vyanzo vizuri vya potassium ni pamoja na mchicha, embe-
mafuta, ndizi, boga, maji ya nazi, karoti, soya iliyopikwa, njugu, moringa na majani ya
mboga za kijani-nyeusi yaliyochemshwa.
Kwa watoto wadogo ambao hawawezi kula chakula kingi, ongeza kijiko 1 cha chai cha
majivu safi (kutokana na miti au nyasi zisizo na sumu, au kutokana na magugu maji
yaliyokaushwa, ambayo yana potassium nyingi) kwenye lita 1 ya maji inayotumika
kutengenezea maji-chumvi (angalia chini). Baada ya dakika kadhaa, chuja maji.
Angalizo: Chumvi za potassium ziongezwe tu kama mgonjwa anaweza kukojoa.
Kama chochote kati ya vifaa vyako (maji, sukari au chumvi) siyo safi kikamilifu,
chemsha mchanganyiko huo kwa dakika chache ili kuua bacteria. Nyongeza ya rangi na
harufu havisaidii kwa lolote.
A.2. Kutengeneza maji-chumvi
Nyumbani: Ama, ongeza vijiko 4 vya mezani vya asali au vijiko 2 vya mezani vilivyojaa sana
vya sukari (gramu 30) na nusu kijiko cha chai kilichosawazishwa cha chumvi, kwenye lita 1 ya
maji. Au, kwenye kikombe kikubwa cha maji (ml 500), ongeza vijiko 2 vya mezani vya asali au
kijiko 1 cha mezani cha sukari kilichojaa sana, na mbinyo 1 wa chumvi kiasi cha chumvi laini
unachoweza kubeba kati ya kidole gumba na shahada.
Hospitalini: Kwenye lita 1 ya maji ongeza gramu 20 za glucose au gram 30 za sukari ya
nyumbani, gramu 2.9 za trisodium citrate dihydrate, gramu 3.5. za chumvi ya mezani (NaCl) na
gram 1.5 za potassium chloride.
A.3. Maji-chumvi: Kipimo cha kunywa.
Kwa siku: ml 200 (glass moja) kwa kila kilo 1 ya uzito wa mtoto wako. Kama hujui uzito wa
mtoto wako, na huwezi kupima ml, jedwali lifuatalo litakusaidia: Vikombe ni vipimo vizuri zaidi
kuliko chupa, kwa sababu ni vigumu kuosha chupa vizuri.
Jedwali 4:2: Matumizi ya kila siku ya maji-chumvi.
UMRI ML IDADI YA VIKOMBE AU CHUPA ZENYE
UKUBWA WA ………….
LITA 0.33 LITA 0.5 LITA 0.7 LITA 1
Chini ya miezi 6 700 2 1.5 1 ¾
Miezi 6 – miaka 2 1,400 4 3 2 1½
Miaka 2 – 6 2,100 6 4 3 2
Miaka 7 na zaidi 2,800 8 6 4 3
Watu wazima 3,500 10 7 5 3½
Kunywa taratibu kwa uaminifu kutwa nzima. Kwa watoto wachanga lazima uendelee
kunyonyesha maziwa ya mama.
B. Kutibu kwa chai ya mimea ya dawa au mkaa wa dawa.
B.1. Mpera (Psidium guajava)
Mpera huzuia maambukizo, huzuia mshituko wa mwili, na ina kemikali ya hudhurungi
inayosaidia usukumaji wa damu kwenye misuli. Sifa zote hizo ni nzuri kwa kutibu kuharisha.
Kutengeneza chai ya mpera, chukua kiganja (maana yake: kiasi cha majani ambayo mgonjwa
mwenyewe anaweza kuzinga katika kiganja chake) cha majani ya mpera, yachemshe katika lita 1
ya maji kwa dakika 2. Baadaye uache ikolee kwa dakika nyingine 30, chuja na tumia ndani ya
masaa 24.
a) Kuharisha kwa kawaida kwa watu wazima: Kunywa lita 1 ya chai ya majani ya mpera ya kawaida. Hii husaidia katika 90% ya matukio yote ya kuharisha.
b) Kwa kuhara kunakodumu kwa watu wazima na watoto tumia “maji-chumvi ya mpera” kwa kiasi kilichotolewa kwenye jedwali 4.2. Tayarisha chai ya mpera kama ilivyoelezwa
hapo juu, na ongeza sukari na chumvi kama ilivyoelezwa kwenye A.2. hapo juu.
c) Chai ya mpera inasaidia pia kwa vidonda vya tumbo: Kunywa kidogokidogo kila baada ya saa 1.
B.2. Mziwaziwa (Euphorbia hirta)
Kama chai ya mpera haisaidii: Chemsha kiganja 1 cha
majani mabichi (kata kwa mkasi, ukiacha mizizi ili mmea
uweze kustawi tena) kwenye lita 1 ya maji kwa dakika 2
(Kama una mzani: tumia gramu 10 za majani mabichi au
gramu 2 za majani yaliyokauka) na uache ikolee kwa dakika
nyingine 30. Chuja na unywe kwa awamu kutwa nzima.
Endelea na tiba hii kwa siku 8.
Hii inafaa sana, hasa kwa maambukizi ya amiba. Ni muhimu
kuutambua mmea huu kama ulivyo. Umeenea katika nchi za
tropiki. Unakua kati ya sm 30 na sm 40 kwa urefu, na una
majani (yenye menomeno mafupi) kwenye vikonyo vifupi. Mashina yamefunikwa na
nywelenywele ngumu zilizotapakaa zenye rangi ya njano.
Unafanana na magugu mengine mengi, lakini una tofauti tatu zinazoonekana:
a) Utomvu mweupe unaovuja kutoka katika shina linapokatwa. b) Kitita cha maua madogo madogo sana ya kijani yanakuwa kwenye shina fupi ambao
linatokeza mahali ambapo jani linaungana na shina.
c) Matunda yana mbegu zenye rangi nyekundu, ambazo zina urefu usiofikia milimeta 1 na zenye kingo 3.
B. 3. Kuhara sana na kuhara damu. “Chai ya kuhara ya anamed”
Chai ya kuhara ya anamed inafaa sana, na imeokoa maisha ya watu wengi. Hata hivyo,
inatakiwa kutumika pale tu unapokuwa umetumia chai ya mpera na ukaona haitibu. Osha na
changanya kiganja 1 (maana yake: kiasi ambacho mgonjwa mwenyewe anaweza kushika
katika kiganja chake) cha kila vifuatavyo:
Mziwaziwa (Euphorbia hirta – mmea mzima lakini siyo mizizi)
Majani ya mpera
Majani ya mwembe machanga ya kijani.
Jedwali 4:3 - Kipimo cha anamed cha dawa ya kuhara.
Umri Kipimo cha kila siku
Mwaka 1 – 3 ¼ lita kila siku
Miaka 4 – 6 ½ lita kila siku
Miaka 7 – 12 ¾ lita kila siku
Miaka 13 – watu wazima lita moja
Chemsha kwa dakika 2 katika lita 1 ya maji, na uache ikolee kwa dakika nyingine 30. Kama mwembe au mpera haupatikani tumia majani ya mpapai. Lakini chai hiyo itakuwa
chungu na mtoto anaweza kuikataa.
Kunywa kiasi hiki cha chai kwa masaa 24. Endelea kwa siku 8 hata kama dalili zimetoweka. Tiba inayoendelezwa huondoa mayai yaani amiba kutoka kwenye matumbo.
Mara nyingi inaondoa minyoo ya kwenye matumbo pia.
Bakavu, huko Kongo, mahali ambako kumbukumbu zimetunzwa kwa uangalifu, walikuwa na mafaniko ya 99% katika kutibu zaidi ya wagonjwa 200 wanaosumbuliwa na amiba na
kuharisha damu kwa kutumia chai ya majani ya Euphorbia Hirta, mpera na mwembe.
Dokezo kwa Mahospitali: Unaweza kupendelea kutayarisha chai hii ya kuharisha ya anamed
kutokana na majani makavu. Vuna mimea hii kwa kiwango kilicho sawa kuelekea mwisho wa kipindi
cha mvua, ikaushe vizuri na uisage. Kipimo sasa kitakuwa kuchemsha kijiko 1 kilichojaa katika lita 1
ya maji kwa dakika 2 na baadaye uache ikolee kwa dakika nyingine 30. Kama unga wa majani makavu
ukitunzwa kwenye chombo kisichoruhusu hewa kuingia, itadumu salama kwa mwaka mmoja.
B.4. Mimea mingine
Mimea iliyotajwa juu isipopatikana, chai inaweza kutengenezwa kwa kutumia majani ya
mwarobaini (angalia sura ya 9), kutokana na Artemisia annua (angalia sura ya 8) au kutokana
na majani mabichi ya kijani ya mwembe (Mangifera indica).
Majani ya mpapai (Carica papai) pia yanatibu: Chemsha kiganja 1 kilichojaa cha majani
katika lita 1 ya maji kwa dakika 1, kisha acha ikolee kwa dakika 20. Chuja na unywe kwa
sehemu sehemu kutwa nzima. Watoto hupendelea chai ya majani ya mpera kwa sababu chai
ya majani ya mpapai ni chungu. Kama hakuna kingine kinachopatikana, kunywa maji
uliyotumia kupika mchele.
B.5. Mkaa wa dawa
Mkaa unatumika kwenye matukio ya chakula chenye sumu au kwa kuhara polepole. Uwe
mwangalifu kwa watoto, hata mkaa lazima wakati wote unywewe ukiambatana na maji-
chumvi. Tengeneza mkaa kutokana na mti ambao hauna sumu. Kwa mfano, tumia matawi
yanayoota kuelekea katikati ya mwembe ambao kamwe hayazai matunda, au tumia maganda
ya karanga yaliyopondwapondwa. Yachemshe katika chombo cha chuma kilichofunikwa
hadi mti au maganda yawe mkaa. Uwe mwangalifu wakati unafunua, unga unaweza kushika
moto kwa ghafla! Ponda mkaa, uchekeche, uchemshe tena ili kuhakikisha hauna
maambukizo. Kunywa kijiko 1 cha chakula, mara 3 kwa siku katika maji. Endelea kunywa
maji mengi au maji-chumvi wakati wote (angalia A.2. juu).
B.6. Vinca rosea
Katika hali zinazotishia maisha, ambapo hata chai ya kuzuia kuhara ya anamed haisaidii,
tayarisha chai ya anamed ya kuzuia kuhara kama ilivyoelekezwa hapo juu. Kisha, mara moja
baada ya kushusha chai kutoka kwenye moto, ongeza kiganja kizima cha majani mabichi ya
Vinca rosea kwenye chai na uiache ikolee kwa dakika 30. Chuja na kunywa kwa awamu kwa
muda wa siku nzima.
Angalizo: Vinca rosea ina sumu!
SURA 5: MALARIA
5.1. Utangulizi
Katika dunia nzima karibu watu milioni 500 hupata malaria kila mwaka. Kati ya hao, millioni 1
hadi 2 hufa. Wengi kati yao ni watoto chini ya miaka 5.
Malaria huambukizwa kutoka mtu mmoja hadi mwingine na mbu wa jamii ya Anopheles.
Wanapochukua damu kutoka kwa mtu aliyeambukizwa wanachukua vimelea vya malaria
(vijidudu viitwavyo plasmodium). Kisha wanapochukua damu kutoka kwa mtu mwingine,
wanaingiza plasmodium pamoja na mate yao. Plasmodium husafiri hadi kwenye ini, na kutokea
hapo huingia hadi kwenye chembe nyekundu za damu. Mtu huugua baada ya siku 7 hadi 10
baada ya kuumwa na mbu.
Kwa kawaida mgonjwa wa malaria huhisi baridi na mara nyingine hutoka jasho. Inawezekana
lakini kwamba dalili mojawapo ikawa na nguvu zaidi, kiasi kwamba haidhihiriki haraka kwamba
mgonjwa ana malaria. Kwa njia hii malaria inaweza kujificha nyuma ya safu ya dalili za
magonjwa, mfano: kuharisha na kutapika, matatizo ya kiakili, kupoteza fahamu, upungufu wa
damu au homa.
Mimea inayotibu inaweza kuokoa maisha ya wengi. Mfano wa kushangaza unatokea Kongo
D.R.C.: Mwaka 1997 Askofu wa Dayosisi ya Bolungu–Ikela ilimbidi kuwakimbia waasi na
kujificha porini kwa majuma 4, akiwa na watu wengine 20. Hawakuwa na nyumba wala
chandarua, wala madawa. Waliishi chini ya miti! Walipopata homa walikunywa chai za dawa
zilizoorodheswa hapa chini. Askofu alisema, “Pamoja na hofu yetu, hakuna mmoja wetu
aliyekuwa mgonjwa sana kwa malaria.”
5.2. Jinsi ya kuzuia malaria
1. Punguza idadi ya mbu nyumbani kwako na katika mazingira yaliyo karibu.
Usiwe na maji yaliyo wazi katika mapipa au matenki yote; yanahitaji vifuniko au nyavu za kuzuia mbu.
Kusiwe na maji yaliyosimama ya aina yoyote.
Kusiwe na taka zinazozagaa – mfano mbu huzaliana katika taili zilizochakaa na makopo.
Tunza msitu wako kwa sababu huko wanaishi maadui wa asili wa mbu.
Usiwe na mimea mirefu (mfano nyasi) karibu na nyumba, isipokuwa mimea yenye harufu nzuri kama vile Cymbopogon citrates (mchaichai), jamii za tururu, (Tagetes
erecta, Tagetes minuta) au Artemisia annua. Inashauriwa hata kuwa na mimea hiyo
ndani ya nyumba (ikiwa imeoteshwa kwenye vyombo).
2. Punguza mgusano kati ya mbu na watu.
Tumia chandarua, hasa wakati wa kulala na nyavu za kuzuia mbu kwenye madirisha. Weka kiasi kidogo cha mafuta ya mwarobaini katika mafuta ya kuwashia taa.
Weka maua ya pyrethrum yaliyokaushwa na kupondwapondwa kwenye kona ya chumba chako.
3. Punguza idadi ya vimelea.
Tibu wagonjwa Zuia vimelea kuwa sugu – tumia tiba za aina mbalimbali (angalia jedwali Na. 5).
4. Jenga kinga nzuri ya mwili
Unapokuwa na malaria – itibu inavyopaswa. Kula matunda na mboga kwa wingi – ambavyo vina vitamini C. Weka vitunguu saumu vingi kwenye chakula chako hasa vibichi. Angalia sura ya 6. Epuka uvutaji sigara na pombe
Jedwali 5 Madawa ya asili kwa ajili ya kutibu Malaria
Jina la mmea Utumike hadi
joto la mwili
(°C)
Sehemu
ya mmea
Jinsi ya kutumia Nguvu ya
mmea
Madhara
Cymbopogon
citratus
(mchaichai)
wakati wote Majani chai (angalia point 3) + Hakuna
Allium Sativum
Vitunguu
saumu
(angalia sura
ya 7)
Wakati wote Vitunguu vijiko 3 vya vitunguu
saumu
vilivyokatwakatwa
++ Maumivu ya
tumbo
Zingiber
officinale
(tangawizi)
37.5 Mizizi kula tangawizi bichi
kiganja 1 au chemsha
kwa dakika 10.
Usichuje, kula na
kunywa kila kitu
+ Hakuna
Psidium
guajava
(mpera)
37.5 Majani chai (decoction) + Hakuna
Carica Papaya
(mpapai)
angalia sura ya
10
38.0 Majani chai (infusion) ++ Kuna
uwezekano wa
kutapika au
kupata allergic
readtion
Vernonia
amygdalina
38.5 Majani au
mizizi
majani: infusion
mizizi: decoction
++ Haijajulikana;
ina aina ya
(bitter leaf) (angalia
maelezo
No 4 na 8)
sumu lakini
Azadirachta
indica
(mwarobaini) –
angalia sura ya
9
38.5 Majani
(angalia
maelezo
No 4 na 8)
majani: infusion
++ Inaathiri ini
Cinchona
officinalis
39.0 Gome
(angalia
maelezo
No
5 na 8)
chai (decoction) +++ Mlio masikioni
Wakati
mwingine
kichefuchefu na
kutapika. Dawa
ikizidishwa
kiziwi kinaweza
kujitokeza au
kutoka kwa
damu masikioni
Artemisia
Annua (angalia
sura ya 8)
39.0 Majani
(angalia
maelezo
No 8)
chai (infusion) +++ Hakuna
5.3.Kutibu kwa mimea
Tumia mimea ya dawa ya aina nyingi ili kuzuia vimelea vya malaria kuwa sugu kwa
tiba.Tunapokwua na maambukizi, vijidudu vinasababisha homa, hasa vinapokufa na kuanza kuoza.
Vitu vyovyote vinavyosababisha homa vinaitwa “pyrogens.” Unywaji husaidia mwili kuondoa
pyrogens. Pyrogens pia hutolewa nje kupitia kwenye ngozi kwa njia ya jasho. Chai ya moto ya
mchaichai hasa husababisha mwili kutoa jasho na kukojoa sana, kwa jinsi hiyo husafisha damu na
mwili. Kutokwa jasho hasa kunaondoa sumu mwilini. Tunapendekeza kwamba mtu mzima mgonjwa
wa malaria anywe lita 2 za chai ya mchaichai kwa nyongeza kwenye lita 1 ya chai ya dawa ya
mimea iliyotajwa kwenye jedwali Na. 5. Hata hivyo, tunapendekeza kwamba mtu mzima ye yote
mwenye joto kali anywe lita 2 za mchaichai kila siku - kwa tatizo lolote.
Kila tiba ya hii mimea iendelezwe kwa siku 7. Sukari au asali inaweza kuongezwa kwenye aina zote
za chai. Malaria huharibu sukari mwilini, na kwa hiyo kufidia sukari katika damu ni jambo
linalosaidia. Pia wagonjwa wa malaria ni vyema wapewe chakula kwa kuwa mara nyingi hupoteza
hamu ya chakula na hivyo kupungukiwa lishe.
Muhtasari wa matibabu
1. Watu wazima wanatakiwa kunywa jumla ya lita 3 kwa siku. Watoto nao ni lazima pia wanywe sana kiwango kikitegemea uzito wa miili yao.
2. Chai ya dawa inaweza kutengenezwa kwa kuchemsha dawa katika maji au kumwagia maji ya moto.
Kumwagia maji ya moto (Infusion): Mwaga lita 1 ya maji yanayochemka kwa kiganja
kizima cha majani mabichi ya dawa, au gramu 15 ya majani makavu (kama ni Artemisa
annua au Azadirachta indica iwe gramu 5). Iache kwa dakika 10 hivi, kisha ichuje.
Kuchemsha (Decoction): Kipimo ni kama katika kumwagia maji ya moto. Chemsha
maji na mimea kwa pamoja kwa dakika kama 20 hivi. Poza na uchuje.
3. Kwa mchaichai, chemsha majani yake kwa dakika 2. Acha itulie kwa angalau dakika 10, kisha ichuje.
4. Vernonia amygdalina. Majani yake ni machungu sana. Magamba ya mizizi yake lina nguvu zaidi. Tumia mizizi yenye unene wa kidole, mizizi ya pembeni, siyo mzizi mkuu, ili mti
usife. Tumia kiganja 1 cha magamba ya mizizi na uchemshe kwenye lita 1 ya maji kwa
dakika 20. Chuja na unywe kwa awamu 4 kwa siku 1. Endeleza tiba hii kwa siku 7.
5. Cinchona officinalis: Chemsha gram 10 au vijiko 3 vya chai vya magamba yaliyopondwapondwa katika lita 1 ya maji kwa dakika 10, chuja na unywe kwa awamu ndani
ya masaa 24. Watoto wanywe kiasi kidogo zaidi kufuatana na uzito wao.
6. Katika hali ambayo mimea yote hii haisaidii, endelea kutumia lita 2 za mchaichai kila siku, na pia tumia dawa za hospitalini (k.mf. Amodiaquine au Fansidar). Hakikisha pia kwamba ni
malaria kweli inayomsumbua mgonjwa na si ugonjwa mwingine.
7. Kumbuka kuwa hakuna wagonjwa wawili wanaoweza kuwa na hali zilizo sawasawa kamwe. Ingawa watu wawili wanaweza kuwa na dalili zile zile, wanaweza wasitibiwe na dawa ile ile
ya mmea.
8. Akina mama wajawazito wasitumie Azadirachta indica (mwarobaini) au Vernonia amygdalina (mtukutu). Katika miezi 3 ya mwanzo ya ujauzito tumia Cinchona officinalis
(mkwinini) au Artemisia annua chini ya uangalizi wa Daktari tu.
SURA 6: UKIMWI: Imarisha mfumo wa kinga mwilini
Ili kudumu katika afya njema, kila mtu anatakiwa kuhakikisha mfumo wake wa kinga mwilini
uko imara kadri iwezekanavyo. Jambo hili ni la muhimu hasa kwa watoto wadogo, wajawazito
na watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU).
Jali haya yote yafuatayo:
a) Ishi kwa matumaini, uwe na uhusiano mzuri na majirani zako na uwe karibu na Mungu. b) Hakikisha kuwa chakula chako ni kizuri na kina lishe kamili. Kunywa maji ya matunda
na maji salama kwa wingi. Jiepushe na aina mbalimbali za soda. (angalia sura ya 1)
c) Usivute sigara, na kama unakunywa pombe, kunywa kiasi kidogo sana. d) Fanya mazoezi ya viungo. Tembea kwa miguu, endesha baiskeli au fanya shughuli
kwenye bustani kila siku.
Mimea na mazao ya asili yafuatayo yanasaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini. Vinafaa
kwetu sote. Kama unaishi na VVU, tumia mimea miwili au mitatu kati ya ifuatayo. Washiriki
wa anamed katika nchi nyingi wametoa taarifa za mafanikio mazuri katika matumizi ya kila siku
ya unga wa majani ya mlonge na chai ya artemisia – bila kujali kama wanatumia madawa ya
kupunguza makali ya VVU (ARV´s) au la.
1. Allium Sativum (kitunguu saumu) Tia vitunguu saumu kisichopikwa (kibichi) kingi kiasi uwezacho katika chakula chako cha kila
siku. Unaweza kuvikata vipande vidogovidogo na kuvichanganya katika chakula chako
unapotaka kula.
Vitunguu saumu vina kiasili cha kuua bacteria (antiseptic, antibiotic, antiviral, antifungal na
antidiabetic). Umuhimu wake kwa UKIMWI ni kwamba vitunguu saumu vimeonekana kuzuia
jamii za ugonjwa wa mkanda wa jeshi (herpes simplex) ambao ni kirusi kinachochochea
kuzaliana kwa VVU. Watu wanaopata maumivu ya tumbo wanapokula kiasi kikubwa cha
vitunguu saumu wanashauriwa kula kiasi kidogo cha mafuta ya maji kama vile mafuta ya alizeti
au samuli ambayo hufunika ukuta wa tumbo na kusambaza viini vinavyoleta maumivu. Huko
China vitunguu saumu vinatumika kutibu vidonda vya tumbo.
2. Aloe Vera (Msubili) Aloe ina acemannon, kiini kinachoharibu VVU kwa kubadilisha ngozi yake ya protini kiasi
kwamba hakiwezi kujishikiza kwenye T-lymphocytes, ambayo ni sehemu muhimu kwenye
mfumo wa kinga ya mwili. Kata jani kubwa lililokomaa sana la aloe kama ilivyoelezwa katika
sura ya 2, kisha parua ute wake mzito kwa kijiko. Chukua kijiko 1 hadi 2 vya mezani vya ute
mzito wa msubili. Kula kijiko 1 hadi 2 vya mezani vya ute mzito wa msubili kila siku,
ikiwezekana kabla hujala chochote.
3. Artemisia annua Washiriki wa anamed wanaoishi na VVU walitumia chai ya artemisia kama ifuatavyo:
a) Wakati wa hali mbaya ya ayfa (acute phase): Mwaga maji ya moto kwenye gramu 5 (yaani
vijiko 4 vya chai vilivyojaa sana) za majani makavu ya artemisia, acha itulie kwa dakika 15,
chuja na unywe chai hii kwa awamu 4 ndani ya siku moja. Kutegemea hali ya mgonjwa njia hii
inaweza kuendelea kwa muda wa wiki kadhaa au hata miezi.
b) Baada ya hapo (chronic phase): Mwaga robo lita ya maji ya moto kwenye gramu 1,25 (yaani
kijiko 1 cha chai) ya majani makavu ya Artemisia, acha itulie kwa angalau dakika 15, chuja na
unywe chai hii wakati wa asubuhi. Unaweza kuendelea hivyo kwa wiki au hata miaka.
Kama una mimea ya Artemisia kwenye bustani yako unaweza kutumia gramu 25 (acute phase)
au gramu 6,25 (chronic phase) ya majani mabichi kila siku.
4. Azadirachta indica (mwarobaini) Mradi wa permaculture huko Malawi na Kuluva Hospital huko Uganda vyote hutengeneza unga
wa majani ya mwarobaini yaliyokaushwa na huwapa wagonjwa wa UKIMWI kijiko 1 hadi 2 vya
chai kila juma.
5. Citrus limon (Limau) Limau lina vitamin C nyingi. Kunywa maji ya limau 1 kila siku, ama katika maji vuguvugu (siyo
ya moto ili usiharibu vitamin C) au lililokamuliwa katika chakula chako.
6. Cymbopogon Citratus (mchaichai) Chai ya mchaichai: Chemsha kiganja 1 cha majani ya mchaichai mabichi katika lita 1 ya maji
kwa dakika 2, acha ikolee kwa dakika 15 na kisha uichuje kwa chujio. Kunywa lita 2 kwa
awamu kwa siku nzima. Huko Afrika kusini kwenye Moretele Sunrise Hospice, Mpho
Sebanyoni na wenzake wamegundua kwamba wagonjwa wa UKIMWI ambao wanakunywa
mchaichai kila siku wanapata tena hamu ya chakula, wanaongeza uzito na wanakuwa na nguvu
tena.
7. Lishe: Moringa Oleifera na/ au mbegu za Amaranth
Majani ya Moringa Oleifera (mlongelonge) na Moringa Stenopetala yanajulikana sana kwa
kuwa yana kiasi kikubwa cha vitamin, protini na madini pamoja na amino acids. Kwa sababu hii
kula mlongelonge kila siku, ama mbichi iliyotayarishwa kama mboga au kama unga wa majani
(angalia sura ya 11) unaochanganywa katika chakula cha kila siku. Mlongelonge unaonesha
mafanikio makubwa kurudisha afya ya watoto walioathirika kwa kukosa lishe. Unasaidia sana
pia kwa wajawazito na kina mama wanaonyonyesha. Kutumia unga wa majani ya mlongelonge
siyo tu kwamba kunajenga upya mwili, bali mara nyingi huondoa matatizo nyemelezi kama
kuharisha na matatizo ya ngozi.
Ongeza kijiko 1 cha chai kilichojaa cha unga wa mlongelonge kwenye chakula mara 3 kwa siku.
Wagonwja wa UKIMWI wafanye hivi kila siku katika maisha yao.
Amaranth ni mboga inayozalisha mbegu na majani yenye virutubisho inayofanana kabisa na
mlonge. Mbegu zinaweza kusagwa kutengeneza unga na kuliwa kama uji pamoja na unga wa
ulezi au mahindi, au unaweza kutumika katika kuumua mikate, keki na biskuiti.
8. Mazao ya asili ya nyuki Asali: anamed Bukavu huko D. R. Kongo hutibu kwa chai ya artemisia na mchanganyiko wa
asali na aloe pamoja na kitunguu saumu kwa siku 20 kila mwezi. Kila siku, changanya kijiko 1
cha chakula cha ute mzito wa msubili na vijiko 2 vya mezani vya asali na unywe katika siku
moja. Mara 3 kwa siku, kata kata vikonyo 3 vya kitunguu saumu na unywe kwa maji kiasi. Chai
ya artemisia inanywewa kama kwa malaria.
Propolis: Gundi hii ni fukizo la kiasili linalotengenezwa na nyuki katika mizinga yao, na
imeonekana kuwa ni antibiotic, anti-fungal, antiseptic na antiviral. Changanya gramu 10 za
propolis na ml 100 za kileo halisi cha kutengenezea dawa (98%) kwa matumizi ya ndani
(kunywa). Tikisa mara moja kwa siku kwa muda wa siku 30. Chuja. Kipimo: kunywa matone 20
mara 1 hadi mara 3 kwa siku.
Kwa maelezo zaidi angalia katika kitabu cha anamed “Ukimwi na madawa ya asili”
Jani, mbegu na vitumba vya Moringa oleifera, unga wa majani ya mlongelonge unaweza pia kunywewa kama chai.
SEHEMU III: MATUMIZI YA BAADHI YA MIMEA MUHIMU
KATIKA ENEO LA TROPIKI
SURA 7: Allium Sativum (Kitunguu saumu)
7.1. Maelezo ya kibotania (asili ya mimea) Familia: Liliaceae
Vitunguu saumu ni zao linalostawi mwaka hadi mwaka. Hurefuka hadi kati ya sm
30 na 90, na shina lake huwa na vikonyo kati ya 5 na 15. Asili yake ni Ulaya na
Afrika kaskazini, lakini jamii mpya kwa sasa zinaweza kustawi katika maeneo ya
tropiki.
7.2. Ulimaji
Vitunguu saumu hupendelea udongo wenye rutuba unaopitisha maji vizuri. Pogoa kikonyo kwa
uangalifu kutoka kwenye shina la saumu, na ukipande kwenye eneo yenye kivuli kwa kina cha
sm 5, na umbali wa sm 15 mche hadi mche kwenye mstari wa sm 30 mstari hadi mstari. Kama
mmea ukianza kutoa maua likate ua kusudi nguvu ya mmea iende kustawisha shina. Vuna wakati
majani yakianza kuwa na rangi ya hudhurungi na kuanza kunyauka. Kausha vitunguu kivulini
mahali ambapo kuna hewa nzuri inayopita, na kwa uangalifu vifute udongo na majani ya juu
(ukifanya hivi wakati vitunguu vina unyevu, vikonyo vitaharibika). Vitunze katika chombo cha
udongo.
7.3. Nguvu ya uponyaji ya vitunguu saumu
Imekuwa ikisemwa kwamba kitunguu saumu ndio mfano mzuri zaidi wa falisafa inayosema
kwamba dawa yako ndiyo iwe chakula chako, na chakula chako kiwe dawa yako.
Kuna hadithi juu ya nguvu za dawa za vitunguu saumu tangu mapema miaka ya 1700. Wezi
wanne walikuwa wamegundua njia ya kujilinda dhidi ya ugonjwa wa tauni na walikuwa
wanaishi maisha mazuri kwa kuiba maiti za wahanga wa tauni. Mara alipokamatwa, wale wezi
waliokoa maisha yao kwa kufichua siri yao – walikunywa siki kingi kilichochanganywa na
vitunguu saumu. Wachunguzi wanaamini kwamba allicin ndicho chanzo kikubwa sana (lakini
siyo yote) cha nguvu ya uponyaji – ikiwa pia ndio chanzo cha harufu yake. Inatengenezwa
kutokana na muungano wa alliin na mmeng’enyo wa alliinase, ambao hutokea mara kitunguu
saumu kinaposagwa, kinapokatwa vipande vyembamba au vidogovidogo.
Kuna madai kwamba kitunguu saumu kinaweza kutumika kutibu matatizo mengi, pamoja na
kifaduro, maambukizi ya njia ya hewa na njia ya mkojo, matatizo ya uyeyushaji wa chakula na
kutapakaa kwa vidudu vibaya mwilini, matatizo ya ngozi, magonjwa yanayoshika watu wengi
kwa mara moja (epidemic) na homa. Katika vita vya kwanza vya dunia vilitumika kuzuia kuoza
kwa vidonda na damu kupata sumu sababu ya maambukizo ya kidonda. Huko China imekuwa
ikitumika kutibu kuharisha, kuharisha damu, kifua kikuu, diptheria, ugonjwa wa ini, ringworm,
homa ya matumbo na trachoma. Katika nchi za magharibi vimekuwa vikitumika kutibu
magonjwa sugu ya njia ya hewa.
7.4. Vilivyomo:
Allicin: Vitunguu saumu vinaposagwa, enzaimu alliinase inaibadilisha alliin na kuwa allicin.
Allicin ni dawa ya bakteria na fangasi yenye nguvu. Alisini pia inatibu kukaza kwa mishipa ya
moyo (Arteriosclerosis).
Ajoene: Pamoja na kuwa na asili ya kuua vidudu na fangasi (anti-bacterial na antifungal) pia
inazuia kuganda kwa damu na kupunguza uwezekano wa kutokea magonjwa ya moyo
Flavonoids: Ni vizuizi vya kupotea kwa oksijeni na inapunguza hatari za saratani, magonjwa ya
moyo na baadhi ya magonjwa ya mishipa ya fahamu.
7.5. Kujenga mfumo wa kinga
Ulaji wa vitunguu saumu wa kila siku umeonyesha kupunguza uwezekano wa kutokea
kwa:
o Magonjwa ya moyo o Stroke (kupooza upande mmoja wa mwili) o Saratani o Shinikizo la damu o Mafua
Vinafanya hivyo kwa:
o Kupunguza kiasi cha “cholesterol” katika damu o Kuvunja fibrin ambayo ni moja kati ya vilivyomo katika vigandisha damu. o Kupambana na vijidudu, mba na jamii za virusi. Kwa baadhi ya magonjwa
‘antiobitic’ zinaweza kuwa na nguvu zaidi, lakini mara nyingi vitunguu saumu
vina nafasi kubwa ya kutibu na vinapenya kwa urahisi zaidi katika sehemu
iliyoambukizwa. Vitunguu saumu pia vina madhara kidogo zaidi.
Wakati wa maambukizo ya watu wengi ya ugonjwa wa uti wa mgongo katika eneo fulani huko
Ethiopia, wenyeji wa eneo hilo walihamasishwa kula vitunguu saumu vibichi. Kati ya wale
waliokula hakuna aliyekufa, lakini wale wengine wengi wao walikufa. Harufu ya vitunguu
saumu katika pumzi ya mtu inaweza kupunguzwa kwa kula tangawizi kwa njia yoyote.
7.6. Kutayarisha tiba ya vitunguu saumu
Kula vitunguu saumu vibichi. Hii ndiyo njia bora zaidi.
Vipike katika chakula.
Asali ya vitunguu saumu. Jaza chupa kubwa ya kioo kwa vikonyo vya vitunguu saumu vilivyomenywa na kukatwa katwa. Taratibu mimina asali ili ijaze nafasi zote kati ya
vikonyo. Weka chupa hiyo kwenye joto la wastani na nyuzi 20ºC. Kati ya majuma 2 na
4 asali itafyonza maji ya vitunguu saumu hivyo vitakuwa tepetepe na visivyo vyeupe
tena. Vichuje. Tumia ndani ya miezi 3.
Mchanganyiko wa kitunguu saumu na sukari. Pondaponda kijiko 1 cha chai cha vikonyo vya kitunguu saumu. Changanya na kiwango
kile kile cha sukari au asali. Tumia haraka.
Mafuta ya vitunguu saumu Chukua sehemu 1 ya vitunguu saumu vlivyokatwakatwa na changanya na sehemu 2 za
mafuta ya mimea. Koroga vizuri. Kama huna fridge, tumia ndani ya wiki 1. Hatushauri
tena kuyatunza kwa muda wa mwezi 1 kutokana na hatari ya kuingilia kwa vijidudu
vinavyoweza kusababisha sumu ya botulism. Botulism inaweza kusababisha kupooza
kwa mwili.
Saumu ya kileo (Tincture): Tumbukiza gramu 200 za vikonyo vilivyomenywa na kukatwa katwa katika lita 1 ya mvinyo au 40% ya kileo kingine kwa siku 14 katika eneo
lililo na joto kama nyuzi 20ºC katika chupa yenye kifuniko kisichopitisha hewa. Tikisa
chupa mara kadhaa kwa siku. Chuja vipande vya vitunguu. Dawa ya aina hii inaweza
kutumika mwaka mzima.
7.7. Magonjwa ambayo vitunguu saumu vinaweza kutibu:
A. Kikohozi, mafua na koo linalouma 1. Kula kikonyo cha kitunguu saumu kutwa mara 3. 2. Kunywa kijiko 1 cha chai kilichojaa cha dawa ya asali ya vitunguu saumu kila
baada ya masaa chache.
3. Tumia kijiko kizima cha chai cha mchanganyiko wa sukari na vitunguu saumu kila baada ya masaa machache.
4. Kunywa kijiko cha chai cha mafuta ya vitunguu saumu mara 6 kwa siku.
B. Maambukizi sugu ya ‘sinus’, maumivu ya kichwa, maumivu ya kichwa ya upande mmoja yaumayo kwa vipindi.
Mara kwa mara dondosha tone la mafuta ya vitunguu saumu katika kila tundu la pua, au
kata ncha za vikonyo 2 vya vitunguu na uweke kikonyo 1 katika kila tundu la pua.
(Angalizo: ni muhimu kuacha ganda la kitunguu saumu, vinginevyo kitunguu saumu
kitaunguza ngozi nyepesi (mucose membrane) ndani ya pua).
C. Sprains, maumivu, maambukizo ya mba, matatizo madogo madogo ya ngozi Sugua mafuta ya vitunguu saumu moja kwa moja kwenye eneo lililoathirika. Angalia
sura ya 3
D. Kisukari: Kula kitunguu saumu kila siku. Vitunguu saumu na vitunguu maji hupunguza sukari kwenye damu na shinikizo la damu.
E. Shinikizo la damu: Kula vitunguu saumu vibichi, au tumia matone kati ya 5 na 25 ya vitunguu saumu ya kileo (tincture) mara kwa mara kwa siku, kiasi kinachohitajika.
F. Malaria: Katakata kitunguu saumu vizuri. Meza kijiko 1 cha mezani cha vitunguu hivi mara 3 kwa siku, na unywe lita 2 za chai ya mchaichai kwa siku. Endeleza tiba hii kwa
siku 5. Ikibidi ongeza tiba nyingine ya malaria.
G. UKIMWI: Changanya vitunguu saumu vingi kiasi iwezekanavyo katika chakula chako cha kila siku ili kuimarisha mfuno wa kinga mwilini. Vitunguu saumu kwa sasa vinazidi
kutumika kama tiba ya msaada kwa malaria na UKIMWI.
H. Kuumwa na wadudu: Wadudu wana vidudu vya maambukizo. Maambukizo au mzio vinaweza kufuata baada
ya kuumwa na mdudu. Sugua sehemu iliyoumwa kwa kitunguu saumu kibichi, au fungia
kipande bapa chembamba cha kitunguu saumu kwenye sehemu iliyoumwa kwa kutumia
plaster.
I. Maumivu ya jino Kwa dalili ya kwanza ya maumivu ya jino (kutokana na usaha chini ya jino) weka
kipande bapa chembamba cha kitunguu saumu kwenye sehemu iliyoathirika. Kiweke kati
ya shavu na jino. Upande uliokatwa uwe upande wa jino, upande mwingine uwe upande
wa shavu. Badilisha kila siku na ukiacha kwa muda wa siku kadhaa wakati wa mchana au
usiku. Athari ya kuungua kwenye taya au ulimi itatoweka baada ya dakika chache.
Kitunguu saumu huua bacteria wanaosababisha meno kuoza kwa sababu kinaweza
kupenya katika nyama na katika tabaka gumu la juu la jino.
Pia kula vitunguu saumu vibichi mara kwa mara.
J. Majipu yasiyo na mdomo; usaha chini ya ngozi (pamoja na maumivu na usaha kwenye vidole au kucha)
Tumia kitunguu saumu kilichosagwa au mafuta ya kitunguu saumu (angalia sura a 2).
Kitunguu saumu kina tabia ya kupambana na bacteria kupitia ngozi. Hata hivyo,
unatakiwa kuwa makini, kwa sababu kitunguu saumu kina nguvu sana na kinaweza
kuunguza ngozi na kuacha makovu ya kudumu.
SURA 8: Artemisia annua anamed “A-3” (Sweet annie)
8.1. Maelezo ya kibotania: Familia Asteraceae.
Artemisia annua anamed (A-3) ni zao la mwaka 1 linaloweza kurefuka hadi meta 3. A – 3 ni
zao la mchanganyiko wa aina za Artemisia annua, ambalo linapolinganishwa na aina zake za
porini, yenyewe ina faida nyingi zaidi:
Inarefuka zaidi Ina majani mengi zaidi Inastawi kwa muda mrefu zaidi kabla ya kutoa maua na kufa Ina kiwango kikubwa cha viasili vya dawa. Muhimu zaidi ni kwamba inastawi katika eneo la tropiki
8.2. Ulimaji
Hifadhi mbegu zikiwa kavu na zidumu kuwa kavu. Tumia kiasi chake kidogo sasa, na kilichobaki kwa kila mwezi. Kama zikitunzwa katika hali ya
ukavu kabisa, hazitaharibika. Kiwango cha kuota kinapungua kwa 10% kwa mwaka. Mbegu na
miche inayozaliwa ni midogo sana na dhaifu. Vinahitaji uangalizi mkubwa! Usijaribu kulima A
– 3 mpaka wewe au mtunza bustani yako awe amejitayarisha kutoa muda wake mwingi kwa
jambo hili, ni pamoja na Jumamosi na Jumapili.
Tayarisha kitalu cha mbegu.
Ni vyema kutayarisha kitalu kinachobebeka. Mfano: Ubao bapa mpana wenye ukingo wenye
urefu wa sm 6, au tumia kingo za plastiki za ndoo. Kwa mbegu 500 unahitaji kitalu cha mbegu
cha sm 50 × sm 50. Au trei chache ndogo ndogo. Kamwe usisahau kutoboa matundu ya kutosha
kwenye kitako ili maji ya ziada yaweze kutoka na ili maji yaweze kunyonywa kupitia kitako.
Weka tabaka la udongo mzuri lenye unene wa sm 3 kwenye kitako cha trei, na ufunike kwa
tabaka nyingine la mchanga la sm 3. Mchanga huu uchemshwe kwa dakika lisizopungua 5 ili
kuua mbegu za magugu ambazo zinaweza kuwemo. Mbegu zenyewe zina virutubisho vya
kutosha vinavyohitajika wakati wa hatua za mwanzo za kukua.
Hakikisha kwamba kitalu kina unyevu sana lakini hakina maji yaliyotua. Mbegu zisambazwe
kwa usawa kwenye uso wa udongo – chujio la jikoni linaweza kusaidia mchakato huu. Usifunike
mbegu.
Mbegu za Artemisia huhitaji mwanga na unyevu ili kuota na kustawi.
Weka kitalu chini ya paa ili kuzuia mvua. Kiwe mahali ambapo kitapata mwanga wa jua moja
kwa moja. Joto la kadri kwa uotaji ni kati ya nyuzi 20 na 30ºC lakini uotaji pia umefanikiwa
katika joto la chini kiasi cha nyuzi 10ºC na joto kali kiasi cha nyuzi 40ºC. Kama kuna hatari
yoyote kutoka kwa ndege, panya au kuku, funika kitalu kwa waya wa mbu.
Kuhakikisha kwamba udongo una unyevu wakati wote, mara kwa mara weka kitalu chako katika
trei kubwa lenye maji kidogo kwa dakika 10, ili maji yaingie kupitia kwenye kitako.
Majani ya kwanza ya kijani hutokeza baada ya siku 3 na 7. Artemisia annua ni “dicotyledon”,
maana yake ni kwamba inapoota majani mawili hutokea. Kwa hiyo inaweza kutofautishwa na
miche ya majani ambayo huchipua jani moja tu. Siku 8 baada ya kupanda miche iotayo karibu
karibu sana inatakiwa ing’olewe kwa kutumia kikoleo na ipandwe sehemu nyingine kwenye
kitalu cha mbegu tena.
Kuweka miche katika viroba
Kati ya wiki 1 hadi 4 baada ya kupanda, ihamishe kwenye viroba. Unaweza kutumia vyungu vya
kupandia, vifijo vya plastiki au vyungu vilivyotengenezwa kwa majani ya migomba. Udongo
huu uwe na rutuba nyingi; mchanganyiko wa sehemu zilizo sawa za mboji iliyooza vizuri ( au
udongo mweusi) na mchanga ndio bora zaidi.
Kuhamishia shambani
Mimea ikifikia urefu wa sm 15, kama majuma 8 baada ya kupanda, tayarisha
shamba lako.
Artemisia hustawi vizuri katika aina mbalimbali za udongo na hali ya hewa.
Inastawi vizuri zaidi katika udongo wa hali ya kati au wa hali ya “alkaline” kidogo,
lakini inavumilia udongo wenye hali ya acid kidogo.
Zao zuri kulima kabla ya artemisia ni viazi vitamu au viazi mviringo, kwa sababu
viazi huufanya udongo uingize hewa nzuri . Artemisia ni mmea wa jalalani, maana
yake ni kwamba inastawi vizuri kwenye udongo unaopitisha hewa vizuri ambao una
nitrojeni nyingi kama vile udongo kutoka kwenye rundo la mboji. Kwa hiyo lainisha udongo.
Kama ardhi ni ngumu sana na ina udongo wa mfinyanzi, chimba kwanza shimo ambalo ni kubwa
zaidi sana ya kipimo ulichotaka, tuseme sm 70 × sm 70 × sm 70 na ndani yake tupia vijiti na
majani mengi (lakini siyo yatakayo katika mimea yenye “acid” kama vile conifers au mkaratusi)
na kwenye udongo changanya mbolea iliyooza ambayo ina kinyesi cha ng’ombe au kuku. Kama
ukipanda miche ya artemisia kwa umbali wa sm 60 toka mche hadi mche, utapata miche 30,000
katika hekta. Kama nafasi itaruhusu panda kwa umbali wa meta 1. Kati ya miche ya artemisia
unaweza kupanda maharage au karanga, ambavyo hurutubisha udongo, au panda mpapai,
mahindi au mtama katika mistari kwa kubadilishana na mstari wa artemisia. Katika udongo
wenye rutuba artemisia itakua na kufikia upande wa meta 1 na urefu wa meta 3!
Badala ya kupanda artemisia katika shamba moja kubwa, ipande katika maeneo mbalimbali,
kwenye jua, kwenye kivuli, karibu na mlima, kwenye ardhi tambarare, ili ugundue mwenyewe ni
sehemu ipi inayofaa zaidi. Kwenye eneo lenye joto ni bora zaidi ardhi ikikaa na unyevu. Kama
joto litakuwa zaidi ya nyuzi 30º wakati wote na hakuna uwezekano wa kumwagilia wakati wote,
tengeneza kivuli. Hili linawezekana kwa kutengeneza kiunzi cha mianzi ambacho kwacho
unaweza kustawisha mimea yenye virutubisho kama maharage yanayotambaa, Passion fruit na
maboga, au kwa kubadilishana katika mistari kati ya mistari ya A – 3, na mistari ya mapapai au
mahindi.
Kama unaishi katika eneo kame sana, pandikiza miche kwenye mistari kama sm 5 chini ya uso
wa ardhi. Kama unaishi katika eneo ambalo mara nyingine maji hutua kwa siku kadhaa
mfululizo, panda miche kwenye mistari juu kidogo ya usawa wa kawaida wa ardhi.
Tumia jembe na umwagilie mara kwa mara. Ardhi lazima ikae na unyevu, hasa majuma 2 ya
kwanza baada ya kupanda. Mmea huitikia matatizo, hasa ya ukame mkali, kwa kutoa maua kabla
ya kukomaa. Mimea ikifikia sm 50 kwa urefu, unaweza kuiwekea mbolea ya asili, kama vile
kinyesi cha wanyama kilichoozeshwa vizuri. Tumia mbolea za viwandani pale tu unapokuwa
huna njia nyingine. Kwa hali hii, jaribu kutumia mbolea ya N-P-K.
Kuzalisha artemisia annua
Kama ilivyoelezwa hapo juu, A-3 ni chotara, kwa hiyo mbegu zake haziwezi kutumika. Zingine
zitaota lakini mimea yake itakuwa dhaifu, ikiwa na sura mchanganyiko na upungufu wa 30% wa
viasili vya dawa. Hii inaweza kuwa ndogo sana kiasi cha kutoweza kutibu malaria.
Kwa hiyo artemisia lazima izalishwe kwa vipandikizi! Miezi 2 au zaidi baada ya kupanda,
chagua mimea 3 yenye nguvu na afya zaidi. Kata matawi katika vipande vyenye urefu wa sm 2
hadi 3 kwa kutumia wembe. Kwa njia hii, katika mmea moja unaweza kupata vipandikizi 1,000
vyenye uwezo wa kutibu wagonjwa 5,000 na zaidi! Tengeneza vipandikizi kila mwezi. Kamwe
usitumie mimea yenye maua, au chipukizi. Ukitumia hivyo, mimea yako itaanza kutoa maua
mapema!
Ondoa majani yote makubwa katika vipandikizi hivi. Tayarisha udongo na uvipande sm 1
udongoni kwenye kitalu cha kile kilichotayarishwa kama ilivyoelezwa hapo juu lakini kikibeba
udongo ambayo ni mchanganyiko wa mchanga na mboji iliyoozeshwa vizuri.
Kila kipandikizi lazima kiwe na vifundo visivyopungua 2. Mkato wa chini lazima uwe chini
kidogo tu ya kifundo ama sehemu ya kipandikizi iliyo
udongoni itaoza. Ondoa majani yote kwenye kifundo cha chini, na kwenye kifundo cha juu.
Ondoa jani kubwa tu, na uache kichipukizi cha pembeni salama. Vichomeke vipandikizi hivi
udongoni ili mizizi iote kuanzia kwenye kifundo cha chini, na ili kipandikizi hicho kiwe kwenye
ulalo wa nyuzi 30º kutoka kwenye wima. Kama hewa ni kavu sana, funika vipandikizi kwa
plastiki ambayo umeitoboa vitundu. Lakini kama hali ya hewa ina unyevu sana, acha wazi.
Vipandikizi lazima viwe kwenye mwanga, lakini visiwekwe kwenye jua moja kwa moja. Jambo
zuri ni kuwa na vitalu 2 ambavyo unavihudumia kwa namna tofauti kidogo, ili kujifunza namna
nzuri katika mazingira yako.
Wakati watu wengine hawana tatizo kabisa katika kuzalisha kwa kutumia vipandikizi, wengine
wanaona ni vigumu sana. Kama ni hivyo, weka vipandikizi vyako, kama ilivyoelekezwa hapo
juu – katika maji ambayo yana matone kidogo ya mbolea ya viwandani au mbolea ya asili.
Mbolea ya maji ya asili inaweza kutengenezwa kwa kuchanganya maji na kinyesi cha mbuzi na
kuachwa kitulie kwa majuma 6.
Kutoka katika mimea inayokua unaweza kuchukua vipandikizi zaidi, na katika mimea mipya vile
vile, unaweza kuchukua vipandikizi kwa njia hii mwaka hadi mwaka bila kupoteza kiasi
chochote cha “artemisinin” katika mmea.
Njia mbadala (stone-method), wakati mmea ukifikia urefu wa sm 50, ni kupinda matawi ya chini
na kuzika sehemu zake za kati kwa udongo. Jiwe linaweza kuhitajika kuzuia lisifyatuke. Mara tu
tawi lililozikwa likianza kuota mizizi, likate kutoka kwenye shina mama na ulipande shambani.
Kama kawaida tumia mmea wenye afya zaidi, na mimea isiyo na maua pekee au hata vitumba.
1. Changanya vikombe kumi kumi kila kimoja cha udongo, mchanga na maji. 2. Chemsha mchanganyiko huu kuua mbegu za magugu. 3. Tengenza kitalu kinachochukulika kutokana na miti na uweke vitundu vidogovidogo kwenye kitako. 4. Weka udongo kwenye kitalu. 5. Fungua mfuko wenye mbegu – ambazo ni ndogo sana!! 6. Sambaza mbegu kwa usawa. Usizifunike, na uweke kitalu kwenye sehemu yenye mwanga. Udongo
ukianza kukauka, weka kitalu ndani ya maji.
7. Mbegu huota kati ya siku 3 hadi 7. Zinahitaji jua la kutosha. 8. Punguza mimea.
9. Juma 1 baada ya kupanda, weka kila mche kwenye kifuko chake. 10. Mara mmea ukifikisha urefu wa sm 10, ukaupande bustanini au shambani.
11. Achanisha mimea kwa umbali wa mita 1.
12. Kutoka katika mimea bora, chukua vipandikizi. 13. Au zalisha mmea kwa njia ya “stone – method.” 14. Mmea unahitaji kiasi cha kutosha cha mwanga wa jua, maji mengi, na mboji nyingi. 15. Mara tu unapochanua maua, vuna mmea mzima. Kata majani kuanzia kwenye ncha za matawi hadi kwenye
kitako.
16. Ondoa matawi yote, katakata majani katika vipande vidogovidogo, na yakaushe kwa siku 3 tu. 17. Sugua majani makavu kupitia kwenye chekecheo na mabaki uipe mifugo wako. 18. Majani ya artemisia, katika kifuko chenye maelezo, kilichozibwa, tayari kwa matumizi. Tunza sehemu
kavu.
Picha: Bindanda Tsobi, Kinshasa. Taarifa na hakimiliki: www.anamed