NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT) 1 BUNGE LA TANZANIA ____________ MAJADILIANO YA BUNGE ___________ MKUTANO WAKUMI Kikao cha Pili – Tarehe 31 Januari, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae. Karibuni kwenye kikao chetu cha pili. Katibu! NDG. THEONEST RUHULABAKE – KATIBU MEZANI HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:- WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMMAVU: Maelezo ya Waziri Mkuu kuhusu Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma wa Mwaka 2018 (The Public Service Social Security Fund Bill, 2018). NDG. PETER J. SERUKAMBA – MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII: Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Muswada wa Sheria ya Mfuko
309
Embed
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO …parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1518416897... · kuuliza swali moja la nyongeza. Bagamoyo imepata hadhi ya Mamlaka ya Mji
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
1
BUNGE LA TANZANIA____________
MAJADILIANO YA BUNGE___________
MKUTANO WAKUMI
Kikao cha Pili – Tarehe 31 Januari, 2018
(Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)
D U A
Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alisoma Dua
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae.
Karibuni kwenye kikao chetu cha pili.
Katibu!
NDG. THEONEST RUHULABAKE – KATIBU MEZANI
HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI
Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:-
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE,KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMMAVU:
Maelezo ya Waziri Mkuu kuhusu Muswada wa Sheriaya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma waMwaka 2018 (The Public Service Social Security Fund Bill, 2018).
NDG. PETER J. SERUKAMBA – MWENYEKITI WA KAMATIYA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII:
Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hudumana Maendeleo ya Jamii kuhusu Muswada wa Sheria ya Mfuko
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
2
wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma wa Mwaka2018 (The Public Service Social Security Fund Bill, 2018).
NDG. NAGHENJWA L. KABOYOKA – MWENYEKITI WAKAMATI YA HESABU ZA SERIKALI:-
Maoni ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzanikuhusu Ofisi ya Waziri Mkuu juu ya Muswada wa Sheria yaMfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma waMwaka 2018 (The Public Service Social Security Fund Bill, 2018)
MWENYEKITI: Ahsante. Katibu.
NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI:
MASWALI NA MAJIBU
MWENYEKITI: Ahsante. Swali letu la kwanzalinaelekezwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na linaulizwa naMheshimiwa Silvestry Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini.
Na. 16
Mji wa Kibaha kuwa Manispaa
MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:-
Mji wa Kibaha ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwanina yapo maombi yaliyokwishapelekwa Serikalini kuomba Mjihuo upewe hadhi ya kuwa Manispaa lakini hakuna majibukwa ombi hilo hadi sasa:-
Je, ni kwa nini mpaka sasa Serikali haijaupa hadhi Mjihuo kuwa Manispaa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri waNchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
3
Mheshimiwa Silvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjinikama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maombi yakuupandisha hadhi Mji wa Kibaha kuwa Manispaakupokelewa mwezi Agosti, 2016; Ofisi ya Rais , TAMISEMI ilifanyauhakiki uliobaini kuwa Mji wa Kibaha ulikuwa na wakazi128,488 (sensa ya Mwaka 2012), Kata 14, Mitaa 73 ambapo niasilimia 56 tu ya wakazi ndio walikuwa wakipata hudumaza maji safi na pia haukuwa na mpango kabambe wauendelezaji wa Mji (Master plan).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa mwongozowa Serikali wa mwaka 2014, vigezo vya kupandisha hadhimiji kuwa manispaa unatakiwa kuwa na wakazi si chini ya300,000, Kata si chini ya 15, Mitaa si chini ya 75, wakaziwanaopata huduma za maji wawe si chini ya asilimia 75 yawakazi wote wa mji na uwepo mpango kabambe wauendelezaji wa Mji (Master plan). Kutokana na vigezo hivyokutofikiwa, ilidhihirika kuwa Mji wa kibaha haukuwa umefuzukupandishwa hadhi kuwa Manispaa. Katibu Tawala wa Mkoawa Pwani alijulishwa matokeo hayo kwa barua yenye kumb.Na. CCB.132/394/01/16 ya tarehe 12 Juni, 2017.
MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti,pamoja na majibu ya Serikali lakini nina maswali mawilimadogo ya nyongeza. Ikumbukwe kuwa Mji huo wa Kibahandio Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani wenye Wilaya sita nayenye idadi ya watu zaidi ya 1,100,000, Mji huu wa Kibahaumekuwa unaongoza katika ujenzi wa viwanda ukiwa naviwanda vikubwa sita, vya kati 16, vidogo 78,vinavyoendelezwa kujengwa vitatu na ambavyo vipo katikataratibu za ujenzi kwenye makaratasi 20.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukipata kikwazokikubwa hasa kwa wawekezaji hasa wanapotaka
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
4
kuendeleza viwanda wanapobaini kwamba huu ni mji tuna wala hauna hadhi ya Manispaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hiyo basi natukizingatia kwamba Sera Kuu ya Serikali yetu ya Awamu yaTano kwenda katika uchumi wa kati ni viwanda nainatekelezwa vizuri na kipekee na kwa kuongoza kwa mjiwa kibaha, ni kwa nini sasa Serikali isitoe upendeleo wa pekeena kuupatia mji huu hadhi ya manispaa ili tuweze kwendakwa kasi kulingana na sera ya Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi waKibaha kwa utiifu na unyenyekevu kabisa wanaomba ombilao hili lipewe uzito wa kipekee. Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napendakwanza nimsifu Mheshimiwa Silvestry Koka, Mbunge waKibaha Mjini kwa jinsi anavyopangilia hoja zake kwa niabaya wananchi wa Kibaha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa vigezovilivyowekwa na mwongozo wa Serikali wa mwaka 2014bado tunahimiza kwamba Halmashauri ya Mji wa Kibahaifanye kila linalowezekana ili kuweza kutimiza vigezo hivinilivyovitaja mwanzoni kwenye jibu la msingi ili wawezekufikia hadhi ya kupandishwa kuwa Manispaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi kwa kwelitunaungana nao wakazi wa Kibaha. Ni mji wa muda mrefuna sisi tunashangaa kwa nini hawajaweza kuwavutia watuwengi waongezeke kwenye Mji. Hii idadi ya watu wotewaliotaja inafanana na idadi ya wakazi wa Mkoa mzimawa Pwani. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka 2012,Mji wenyewe wa kibaha ambao ndio uko kwenyeHalmashauri ya Mji wa Kibaha ulikuwa na wakazi 128,488,hizo ndizo taarifa tulizonazo. Kwa hiyo pamoja na kutilia uzito
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
5
ombi lake bado tunahimiza kwamba Mji wa Kibahawajitahidi kutimiza vigezo vilivyowekwa. Ahsante sana.
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: MheshimiwaMwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Naombakuuliza swali moja la nyongeza. Bagamoyo imepata hadhiya Mamlaka ya Mji Mdogo mwaka 2005 na miaka 10 baadayemwaka 2015 baada ya kujitathimini na kuona tumetimizavigezo tumeomba kupandishwa hadhi kuwa Halmashauriya Mji. Je, Serikali inatupa jibu gani kuhusu Bagamoyokupandishwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwambatulipokea maombi ya Mji wa Bagamoyo kupandishwa hadhikuwa Halmashauri ya Mji sawa sawa na ambavyo tumepokeamaombi mengi ya aina hiyo. Kwa sababu kupandisha hadhiMji kuwa Halmashauri ya Mji kunaweza kusababisha ongezekola mahitaji mengi ya kiutawala, bado maombi hayo yakokwenye mchakato na tutayafikiria muda utakapofika nakuzingatia na uwezo wa Serikali.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Hussein.
MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja. Ningependakujua Wilaya ya Nyangh’wale Makao yake Makuu niKarumwa, lakini nikiuliza kila mara hapa kuhusu GN ya MakaoMakuu ya Wilaya Nyangh’wale ambayo ni Karumwa, leo hiliswali ni mara ya tano, kila nikiuliza naambiwa GN iko tayarilakini cha ajabu mpaka leo hatujakabidhiwa katikaHalmashauri yetu ya Nyangh’wale. Je, GN hiyotutakabidhiwa lini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.Naomba uniruhusu nitoke na Mheshimiwa Amar mara baadaya kipindi hiki twende kwenye Idara yetu ya Sheria ili tuwezekumpatia majibu sahihi.
NWENYEKITI: Ahsante. Tunaendelea na swalilinalofuata, linaelekezwa Ofisi hiyohiyo ya Rais, TAMISEMI nalinaulizwa na Mheshimiwa Shally Joseph Raymond, Mbungewa viti Maalum.
Na. 17
Ugatuaji wa Madaraka
MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:-
Halmashauri zina wataalam wa kusimamia nakutekeleza mipango yao na zina uwezo kisheria kupangana kutekeleza mipango ya maendeleo, elimu, afya, majikilimo na ardhi pasipo kuingiliwa. Viongozi na Watendaji waSerikali ngazi za Mkoa na Wilaya huambiwa watawajibishwakufikia malengo mathalani, katika ujenzi wa maabara,madarasa na kutengeneza madawati:-
Je, mipaka ipi ni ya kinadharia (theoretical) na ipiinatekeleza (practical) kiutendaji na uwajibikaji kati yaviongozi wa Serikali Kuu na Halmashauri za Majiji, Miji naWilaya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri waNchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali laMheshimiwa Shally Joseph Raymond, Mbunge wa Viti Maalum,kama ifuatavyo:-
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
7
Mheshimiwa Mwenyekiti, ugatuzi wa madaraka yakisiasa, fedha na utawala kutoka Serikali Kuu kwenda kwawananchi kupitia Serikali za Mitaa umetokana na mahitajiya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya145 na 146. Madhumuni ya ugatuzi ni kuwapa wananchikupitia Mabaraza yao ya Madiwani, uwezo wa kufanyamaamuzi kulingana na mahitaji yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali za Mitaa zimeundwakwa mujibu wa Sheria Na.7 (Mamlaka za Wilaya) na SheriaNa.8 (Mamlaka za Miji)kwa malengo ya kuboresha nakuimarisha utoaji wa huduma mbalimbali za jamii kwawananchi pamoja na kusimamia ulinzi na usalama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na sheria kuwekautaratibu wa Serikali za Mitaa kujiamulia mambo yake kupitiavikao rasmi, hazijapewa uwezo wa kukataa maelekezo yaSerikali Kuu. Kwa mujibu wa Sera ya Maboresho ya Serikali zaMitaa ya Mwaka 1998, Serikali Kuu ina majukumu ya kutungasera, kutoa miongozo ya namna bora ya kutekeleza sera,kuandaa mikakati ya kitaifa, kuweka mazingira bora yautekelezaji wa sera kwa kuzipatia Serikali za Mitaa rasilimaliwatu, rasilimali fedha na baadhi ya vitendea kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuweka viwango vyautekelezaji, kufuatilia utekelezaji i l i kujiridhisha kuwamiongozo na viwango vinazingatiwa na kuchukua hatuadhidi ya utekelezaji usioridhisha inapobidi hasa inapobainikamatumizi yasiyo sahihi ya fedha ikiwemo viwango duni vyamiradi visivyolingana na thamani ya fedha iliyotumika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali Kuuhuwakilishwa na viongozi wa Mikoa na Wilaya katikakusimamia utekelezaji wa sera na miongozo, Viongozi Wakuuwa Serikali ngazi ya Mikoa na Wilaya hutekeleza majukumuyao ya kisheria ya kuziwezesha Serikali za Mitaa kutimizamajukumu yao kikamilifu ikiwemo kutekeleza maagizo halalina ushauri wa viongozi hao.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
8
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikibainika kiongozi wa Mkoaau Wilaya ameshindwa kutimiza wajibu wake na hivyokusababisha Mamlaka ya Serikali za Mtaa zisitimize vizurimajukumu yao, Mamlaka ya uteuzi huchukua hatua zakiutawala. Napenda kusisitiza kwamba Katiba, Sheria,Kanuni, Taratibu na Miongozo ya Utumishi zikirejewa vizurihakuna mgogoro wowote wa kimipaka wala kiutendajiutakaodhihiri.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Shally Raymond.
MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri,lakini nina swali la nyongeza. Serikali iko moja nayo ni SerikaliKuu na hao wote waliotamkwa wanatekeleza kutokana namaagizo ya Serikali Kuu. Je, inakuwaje pale ambapo helahazipelekwi za kutosha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikaliinafuatilia vipi kuepusha migongano hiyo kati ya Serikali Kuuna Serikali za Mitaa?
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri.
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pale ambapofedha za kutekeleza mradi fulani hazijapelekwa zotemawasil iano yanafahamika kati ya waliopokea nawaliopeleka. Kwa hiyo hayo yanakuwa ni maelezo sahihiwakati wa tathmini kwamba hatukuweza kutekeleza vizurimradi huu au hatukukamilisha kwa sababu fedha imekujanusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hiyo ni mawasilianoya ndani ya Serikali na mara nyingi imefanyika; lakini kitukimoja kizuri kwa upande wa Serikali za Mitaa ni kwambawanapopewa wakati mwingine fedha imezidi auimechelewa kuja imekuja mwishoni mwa mwaka wa fedhawenzetu wanaruhusiwa kubaki na fedha ile halafu mwezi
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
9
wa Saba wanakaa kwenye vikao vyao rasmi wanazipitishakwa ajili ya matumizi yaliyovuka mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hil i la pil i kwambatunafuatiliaje mgogoro; Serikali ina macho usiku na mchana.Kule kule ziliko Serikali za Mitaa wapo waangalizi wa Serikaliambao wanakusanya taarifa kila siku asubuhi na mchanakwa masaa yote. Kwa hiyo kama kuna harufu yoyote yamgogoro Serikali Kuu huwa inapata taarifa hizo mara moja.Ahsante sana.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Maida.
MHE. MAIDA H. ABDALLAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali moja lanyongeza. Kwa kuwa miradi mingi ya maendeleo ngazi yaHalmashauri imekuwa ikisuasua na ikikwama kutokana naucheleweshwaji wa fedha kutoka Hazina. Je, Serikali inatoakauli gani katika ukamilishwaji wa miradi ya maendeleoiliyopitishwa na bajeti ya Serikali mwaka 2015/2016 na 2016/2017?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kusuasuakwa miradi; huku kunategemea na eneo na mradi naHalmashauri husika. Ziko Halmashauri ambazo tumekuwatukizifuatilia na kuwashauri kuhusu matumizi ya fedha kwawakati. Wakati mwingine wanakuwa na fedha kwenyeakaunti lakini wakati mwingine watekelezaji kule kwenyemradi wanakuwa hawajui kama fedha zimekuja. Kwa hiyomatatizo mengine ni ya kimawasiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kusisitiza,Halmashauri mara zinapopata fedha kutoka Serikali Kuu,zijipange kwa haraka na kwa wakati kutumia fedha hizokwa ajili ya wananchi, wasiziache kwenye akaunti. Paleambapo kuna ucheleweshaji wa aina yoyote wafanyemawasiliano haraka na Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kusudi tuwezekufuatilia kwa wenzetu tuweze kusuluhisha suala hilo maramoja.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
10
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Cecilia Paresso.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo lanyongeza. Baadhi ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa hapa nchiniwamekuwa wakiwasimamisha hovyo watumishi wa Serikaliza Mitaa bila kufuata taratibu na sheria zilizopo. Je, nini kaulina msimamo wa Serikali katika suala hili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naombakukanusha, hakuna sehemu yoyote ambayo Mkuu wa Wilayaau Mkuu wa Mkoa amesimamisha watu kazi hovyo, hakuna!Nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwambausimamishaji wowote wa kazi unafuata masharti ya taratibuza kazi na sheria zinazomwongoza anayetoa amri hiyo.Ahsante sana. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante. Waheshimiwa Wabungetunaendelea, bado tupo Ofisi ya Rais, TAMISEMI, linaulizwana Mheshimiwa Kasuku Samson Bilago, Mbunge wa Buyungu.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,kabla sijaruhusu swali langu lijibiwe naomba kusema tukwamba madhara ya mikanda kuvuliwa sasa tumeyaonaleo. (Kicheko)
MWENYEKITI: Mheshimiwa, uliza swali!
MHE. KASUKU S. BILAGO: Naomba swali langu namba18 sasa lijibiwe.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
11
Na. 18
Wahitimu wa Elimu Maalum Kutopangiwa Vitengo Husika
MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:-
Walimu wa Elimu Maalum wanapohitimu kwenyeVyuo vya Patandi na SEKOMU hawapelekwi kwenye shule zavitengo vya elimu maalum:-
(a) Je, Serikali haioni kama inapoteza rasilimalifedha na watu kwa kutoa elimu isiyo na tija kwa Walimuhao?
(b) Je, ni lini Serikali itawapanga walimu wenyeelimu maalum kwenye shule na vitengo vyenye mahitajihayo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ali losemaMheshimiwa Bilago halihusiani kabisa na swali lake. Hatahivyo, nataka kumwambia kwamba kukatika kwa mkandasi kuvuliwa kwa mkanda. Ahsante sana. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri waNchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali laMheshimiwa Kasuku Samson Bilago, Mbunge wa Buyungulenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoa mafunzo kwa Walimuni miongoni mwa mikakati ya kuongeza tija ya kazi na uborawa elimu inayotolewa, si kupoteza rasilimali fedha narasilimaliwatu. Kwa muktadha huo, Chuo wa Walimu waElimu Maalum Patandi hudahili Walimu kutoka kazini ambaohuhitimu kwa viwango vya astashahada na stashahada.Chuo Kikuu cha Elimu Maalum SEKOMU hudahili walimukutoka kazini na pia Walimu wapya kwa kiwango chashahada.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
12
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vyuo vyote viwili,wahitimu waliodahiliwa kutoka kazini hurudi kwenye vituovyao vya kazi wakisubiri uhamisho kwenda kwenye shule zavitengo vya elimu maalum; na wahitimu ambao hudahiliwakabla ya ajira huajiriwa na Serikali na kupangiwa shule zenyevitengo vya elimu maalum na wengine huajiriwa na SektaBinafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya mwaka 2012 na 2015Serikali iliajiri Walimu wapya 614 wa elimu maalum ambaowalipangiwa kufundisha kwenye shule zenye vitengo vyaelimu maalum. Hadi Desemba 2016 wapo Walimu 3,957 waelimu maalum nchini sawa na asilimia 74.3 ya Walimu 5,324wanaohitajika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha Walimu wotewenye taaluma za elimu maalum wanatumika vizuri,nazielekeza Halmashauri zote ziwahamishie Walimu wa elimumaalum kwenye shule zenye vitengo vya elimu maalumifikapo Desemba 31, 2018. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Bilago.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,pamoja na majibu ya Serikali, nina maswali mawili yanyongeza. Maagizo yaliyotolewa na Serikali ya kuhamishiawatoto wenye uhitaji wa elimu maalum ifikapo Desemba 31mwaka huu hayatekelezeki; kwa sababu hata kwanguWilaya ya Kakonko hakuna shule hiyo. Swali la kwanza,Serikali iko tayari kujenga shule ya watoto wenye uhitaji waelimu maalum katika Wilaya ya Kakonko ikizingatiwakwamba kuna watoto zaidi ya 200, Walimu wako watanotu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa maelezohayo hayo ambayo nchi nzima itaathiriwa na agizo hili laSerikali, je, Serikali inaweza ikajiridhisha kwamba kila wilayainapata shule ya watoto wenye vipaji maalum yenyemabweni ili kuwaokoa katika usumbufu wanaoupata?Ahsante.
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanzanamshukuru Mheshimiwa Kasuku Samson Bilago, hajasahautaaluma yake licha ya kuwa Mbunge. Sasa naomba kujibumaswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasuku kamaifuatavyo:-
Serikali imeshatoa maagizo tangu mwaka janakwamba kila halmashauri iteue shule angalau moja ili watotowenye mahitaji maalum waweze kusomeshwa vizuri kwamujibu wa mazingira ya mahitaji yao. Sasa kama kwenyewilaya yake hakuna hata shule moja, natoa agizo kwaMkurugenzi wa Halmashauri hiyo ili aweze kutekeleza agizola Serikali lililotolewa tangu mwaka jana mara moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, amezungumzakwamba kwenye eneo lake la Ubunge wapo Walimu watanotu ambao wana taaluma ya elimu maalum. Namhakikishiakwa agizo ambalo limetolewa na Serikali leo; miminimesisitiza tu lilishatolewa siku nyingi, nasisitiza na kuwapamuda kwamba ifikapo Desemba 31, 2018 agizo hil ilinatekelezeka. Ndiyo maana tumewapa muda mrefuvinginevyo tungeweza kuwapa mwisho tarehe 30 mwezi waJuni, lakini tumewapa muda mrefu hadi Desemba ya 2018 iliHalmashauri ziweze kujipanga vizuri kuhakikisha agizolinatekelezeka. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Selasini.
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru sana. Ni kweli baadhi ya halmashaurizimetekeleza agizo la Serikali la kutenga shule moja kwa ajiliya watoto wenye mahitaji maalum, lakini ni kweli piakwamba shule hizi hazina vitendea kazi pamoja na Walimuwa kutosha na matokeo yake hata ufaulu wa watotoumekuwa ukitia shaka.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
14
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatoa mfano Shule yaSekondari ya Viziwi Njombe ambayo matokeo ya Form Fourya mwaka uliopita shule nzima wamepata division zero. Sasaje, Serikali iko tayari pamoja na agizo hili kuhakikisha kwambashule hizi zimepata Walimu wa kutosha na vitendea kazi ilihawa watoto waweze kuangaliwa kwa uzito ule ule wawatoto wengine ambao hawana mahitaji kama hayo?(Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante. Majibu Mheshimiwa NaibuWaziri, Ofisi ya Rais, TAMISEMI.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuruamerejea kauli yangu kwamba agizo hili la kila Halmashaurikuwa na angalau shule moja ambayo watasoma watotowenye mahitaji maalum. Napenda kumhakikishia kwambaagizo lile lililotolewa tangu mwaka jana lilienda sambambana maagizo kwamba wahakikishe shule hizo zinakuwa navifaa na vitendea kazi pamoja na Walimu ambaowatawafundisha watoto hawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano wake wa Njombealioutoa, namwagiza Mkurugenzi wa Elimu pale ofisinikwangu afuatilie hiyo shule ya Njombe kuona je, ni ukosefuwa vifaa au ukosefu wa Walimu au ni tatizo la wanafunziwenyewe lililosababisha wote wapate division zero? Hatahivyo, tunafuatilia na naagiza kwamba kila Halmashauriinapoteua shule ya watoto wenye mahitaji maalumwahakikishe kwamba kunakuwa na vifaa vya kutosha vyakuwafundishia. Ndiyo maana tunaita ni mahitaji maalumkwa sababu mtu ambaye ana ulemavu wa macho anahitajivifaa maalum vya kusomea. Mtu ambaye ana ulemavu waakil i anahitaji vifaa malum vya kusomea. Kwa hiyowahakikishe vifaa vyote vinapatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu ni wakati wa kupangabajeti, kwa hiyo wahakikishe kwamba ikifika mwezi wa Sabatarehe moja, utekelezaji uanze kufanyika kwa mujibu wamaelezo ya Serikali. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
15
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, UTUMISHI NAUTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inayotaarifa kwamba wako Walimu wa kufundisha shule zawalemavu wamehitimu hawajaajiriwa bado. Tumefanyamazungumzo na Ofisi ya Waziri Mkuu, nimezungumza naNaibu Waziri anayeshughulika na walemavu, tuleteweorodha ya mahitaji ya Walimu kwa ajili shule za walemavu,tutapata kutoka Wizarani orodha ya wale ambao tayariwamehitimu. Tutawaajiri mara moja ili wanafunzi hao naowapate elimu kama wanafunzi wengine. (Makofi)
MWENYEKITI: Tunakushukuru sana Mheshimiwa Waziriwa Nchi, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora kwa majibuyako.
Tunaendelea, Mheshimiwa Desderius Mipata, Mbungewa Nkasi Kusini, anauliza swali lake kwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI.
Na. 19
Kuanzishwa kwa shule ya Sekondari ya Mlundikwa
MHE. DESDERIUS J. MIPATA aliuliza:-
Wananchi wa Kata ya Nkandasi wamejitahidi kujengashule ya Sekondari ya Kata ya Milundikwa hadi kufikia kidatocha sita lakini Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi laKujenga Taifa imeamuru shule hiyo kuhamishwa mara mojakuanzia tarehe 1 Januari, 2017 kuachia Jeshi:-
(a) Wananchi walitumia muda na rasilimali zaokukamilisha ujenzi huo na sasa wanakwenda kuanza upya:je, ni upi mchango wa Wizara kwa ujenzi mpya wa shule?
(b) Wizara ya Elimu imeafiki kuhamishwa shulehiyo ya Kata; Je, ni upi mchango wa Wizara katika uhamishajiwa shule hiyo?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
16
(c) Je, Serikali iko tayari kufanya uthamini wamiundombinu yote ya shule na majengo, yaliyojengwa nawananchi na thamani hiyo kuitoa katika fedha taslimu kwaujenzo wa shule mpya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba yaWaziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swalila Mheshimiwa Deusderius John Mipata, Mbunge wa NkasiKusini, lenye sehemu (a), (b) na (c) kwa pamoja, kamaifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na Jeshi la KujengaTaifa kuhitaji eneo lao ilipokuwa imejengwa shule ya sekondariya Milundikwa kuanzia Januari 2017, Serikali ilihamishia shulehiyo kwenye eneo jipya la Kijiji cha Kasu A. Ushirikiano mzuribaina ya Serikali Kuu, Halmashauri, JKT, Mbunge na wananchiumewezesha ujenzi wa madarasa 13, vyoo matundu 26 nabweni moja kukamilika. Ujenzi wa maabara moja ya sayansina bweni la pili uko katika hatua za mwisho ambapowanafunzi 461 wakiwepo 92 wa kidato cha tano wanasoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza MheshimiwaMbunge kwa kuchangia shilingi milioni mbili na wananchiwa Kata ya Nkandasi hususan Vijiji vya Katani, Kisula,Malongwe, Milundikwa, Kasu A na Kasu B kwa kujitoleakuchimba msingi, kukusanya mawe na mchanga, kuteka majikwa ajili ya ujenzi kwa utaratibu wa 50 kwa 50 yaaniwanaume 50, wanawake 50 kila siku ya ujenzi na kufyatuatofali za kuchoma laki mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya yaNkasi nayo ilitoa milioni arobaini na tisa kwa ajili ya ujenzihuo na Serikali Kuu kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi naTeknolojia ilitoa shilingi milioni mia mbili hamsini na tisazilizotumika kujenga vyumba vya madarasa manne, vyoomatundu 22 na mabweni mawili ambapo ujenzi wa bwenila pili unaendelea.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
17
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangiaukamilishaji wa bweni la pili, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoana Serikali za Mitaa mwezi Desemba, 2017 imepeleka shilingimilioni mia moja na Jeshi la Kujenga Taifa nalo lilichangiamabati 204, miche 300 ya miti kwa ajili ya mazingira na piaimetoa Walimu 10 wanajeshi ambao wanafundisha shulenihapo. Katika Mwaka wa Fedha 2018/2019, Serikaliimependekeza shule hiyo itengewe shilingi milioni 230 ilikujenga maabara za sayansi mbili, jengo la utawala, bwalona nyumba za Walimu endapo Bunge litaridhia.
MHE. DESUDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru sana na nichukue nafasi hii kutambua juhudikubwa sana na kuipongeza Serikali kwa kazi nzuriwaliyoifanya kwenye shule hii, lakini pia usimamizi mzuriuliotolewa na Mkuu wetu wa Wilaya na kwa hakikanimeridhika sana na majibu ya Serikali, lakini hata hivyo ninamaswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; shule hii niya bweni kwa kidato cha tano na cha sita. Haina nyumbaya matron wala haina uzio wa ulinzi wa wanafunzi. NaombaSerikali itoe hela zaidi kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na hudumaya vijana hawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Halmashauriilijitahidi kuchimba kisima cha maji lakini kiko mbali kidogona shule. Naomba Serikali itoe pesa zaidi kwa ajili ya kusogezamaji kwa ajili ya huduma ya wanafunzi hawa. Ahsante sana.(Makofi)
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisanampongeza Mheshimiwa Mipata na Mheshimiwa Keissy,
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
18
wilaya yao ni miongoni mwa wilaya zinazoongoza katikaujenzi wa madarasa. Mwaka jana peke yake wamejengamadarasa 550 ambayo yanatakiwa kuezekwa sasa hivi. Kwahiyo nawapongeza sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili hitaji la kwanza alilosemala nyumba ya matron, uzio; nilifika pale Milundikwa, nimeonakweli ni mahitaji halisi nayo tutayafikiri kadri ambavyotunapata uwezo wa kifedha lakini kwa kushirikiana nahalmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusukisima, shule ya sekondari ya Milundikwa tumeiingiza kwenyeorodha ya shule 100 ambazo zitapata ufadhili wa fedhakutoka kwa Sultan Qaboos wa Oman. (Makofi)
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: MheshimiwaMwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swalila nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Tunduma ni mjiunaokuwa sana na una msongamano mkubwa sana wawatoto; na mwaka wa jana Waheshimiwa Madiwani kwakushirikiana na wananchi waliweza kuanzisha shule mpyanane ambazo zingine zina madarasa matatu, zingine zinamadarasa nane lakini shule hizi mpaka sasa hivi hazijaanzakutumika kwa sababu DC amewasimamisha Madiwani.Kwa, hiyo kuna baadhi ya shughuli ambazo zilitakiwa zifanyikekama vioo na mambo mengine hayajafanyika kwa sababuwananchi pia walikuwa wanategemea Madiwani. Je, ni liniSerikali itatia mkazo kuhakikisha kwamba Madiwani wanarudikazini ili shule hizi zianze kutumika haraka iwezekanavyo?Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NASERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwambaHalmashauri ilijitahidi ikajenga shule nane na hizi shulehazijaanza kutumika, ni kweli; lakini ni matokeo ya migogoroambayo haina sababu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana wenzetu waHalmasahuri ya Mji wa Tunduma walipokaa kwenye kikaocha rasmi walikataa ushirikiano wa aina yoyote naMheshimiwa Mkuu wa Wilaya. Sasa hilo likawa ni chanzo chamatatizo ambayo yamesababisha Waheshimiwa Madiwaniwasiweze kutimiza majukumu yao. Suala lao tunalishughulikiakitaifa na namwahidi Mheshimiwa Mbunge kwambatutalitatua hivi karibuni, ili kusudi waweze kuendeleakutekeleza majukumu yao kama kawaida. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante. Waheshimiwa Wabunge,tunaendelea kwa sababu ya muda. Swali linalofuatalinaulizwa na Mheshimiwa Magdalena Hamis Sakaya, Mbungewa Kaliua na linaelekezwa Ofisi ya Rais, Utumishi na UtawalaBora.
Na. 20
Mradi wa TASAF III – Jimbo la Kaliua
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka mradi wa TASAF awamuya III katika vijiji ambavyo havijapata mradi katika Jimbo laKaliua?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, UTUMISHI NAUTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa kunusuru kayamaskini ambao umo ndani ya TASAF awamu ya III unaendeleana utekelezaji wake katika halmashauri 159 pamoja naUnguja na Pemba. Mpango wa kunusuru kaya masikini unasehemu tatu ambazo ni uhaulishaji fedha kwa kutimizamasharti ya elimu na afya kwa watoto walioko shuleni nawale wanaotakiwa kuhudhuria kliniki pamoja na walengwakufanya kazi za ajira ya muda. Sehemu nyingine ni kukuzauchumi wa kaya kwa kuweka akiba na kuanzisha miradi yakuongeza kipato na uboreshaji wa miundombinu ya elimuna afya ili kuwawezesha walengwa kutimiza masharti yaelimu na afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa kunusuru kayamaskini unatekelezwa katika halmashauri 159 za TanzaniaBara na Tanzania Zanzibar kwa maana ya Unguja na Pembalakini si katika vijiji, mitaa na shehia zote. Mpango ulipoanzautekelezaji mwaka 2013, rasilimali zilizokuwepo zilitoshelezakufikia asilimi 70 tu ya maeneo yote, ambayo ni sawa navijiji, mitaa, shehia 9,989 na maeneo yaliyobaki yana vijiji,mitaa, shehia zaidi ya 5000. Kila halmashauri nchini imegusakwa wastani wa asilimia 30 ya maeneo yake ambayohayajafikiwa na mpango wa kunusuru kaya maskini na hili sikwa Jimbo la Kaliua pekee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba yapomaeneo yenye kaya zenye vigezo vya umaskini na uhitajiambavyo bado havijafikiwa. Serikali ipo katika hatua zamwanzo za kuanza kuandaa sehemu ya pili ya TASAF awamuya tatu ambayo itaendelea kwa miaka mingine mitano.Lengo la sehemu hii ya pili ni kuzifikia kaya zote maskini nchinina kuimarisha utekelezaji wa mpango na kuwasaidiawananchi kuwa na shughuli za kiuchumi na uzalishaji zaidi iliwaweze kuondokana na umaskini.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Sakaya.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: MheshimiwaMwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Wazirinaomba kumuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
21
Kwanza Halmashauri ya Kaliua hatujafikiwa kuwa asilimia70 tumefikiwa kwa asilimia 50 tu; kati ya vijiji 102 ni vijiji 54 tu.Katika vijiji ambavyo vilipata miradi kuna baadhi ya makosaambayo yalifanyika katika kuanisha wale ambao walikuwani walengwa na baada ya kulalamika wakaambiwawaandike rufaa kwa sababu kuna wazee ambao wanastahilikupata mradi hawakupewa mradi wakaenda kupewa watuambao wana uwezo. Leo ni mwaka wa pili waliambiwawaandike rufaa na mpaka leo rufaa haijarudi wala majinayao hayajaingizwa kwenye mradi, jambo ambalo limeletamanunguniko makubwa na masikitiko kwa sababuwanashindwa kuishi lakini wenzao ambao wana hali nzuriwanaendela kupata mradi.
MWENYEKITI: Mheshimiwa uliza swali.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: MheshimiwaMwenyekiti, je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwambazile rufaa ambazo ziliandikwa na walengwa zinarudi iliwaingizwe kwenye mradi waendelee kunufaika na mradi huuwa kunusuru kaya maskini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili mradi huuumeanza mwaka 2013, lakini kwa baadhi ya wilaya ikiwemoKaliua tumeanza mwaka 2015, Januari. Naomba kuulizaSerikali kwa zile wilaya ambazo zilichelewa kupata mradikwa miaka miwili, je, wataendeleza mradi kwa miaka 10kama ilivyo kawaida au wataenda kufanya evaluation kamawanavyokwenda nchi nzima na kusahau kwamba sasa hivimradi ni mwaka wa tatu wakati wengine ni mwaka watano? (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Waziri, Ofisi yaRais, Utumishi na Utawala Bora, Mheshimiwa GeorgeMkuchika.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALABORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kumpongezaMheshimiwa Sakaya kwa jinsi anavyofuatilia kunusuru kayamaskini katika jimbo lake.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
22
Mheshimiwa Mwenyekiti, ameeleza kwamba kwaketumefikia asilimia 50 sio 70 kama katika maeneo menginemimi kama Waziri ninayesimamia masuala ya TASAFnitafuatilia nione nini kimesababisha wao wawe chinikulingana na wilaya nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, anasema makosayalifanyika katika kuwabaini walengwa na naomba nichukuenafasi kulieleza Bunge lako Tukufu, Watendaji wa TASAFhawana kauli juu ya nani asaidiwe. Wenye kauli juu ya naniasaidiwe ni watu katika mtaa, shehia, wao ndio wanaokaawanasema hapa kijijini fulani bin fulani hali yake si nzuri. Kwahiyo kwa yale maeneo ambayo makosa haya yamefanyikani makosa ya wanavijiji na hasa viongozi wa vijiji kule Kaliua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale ambapo mmetuleteawatu ambao hawakuhusika wamelipishwa fedha. Juzinilikuwa Singida vijijini, watu walilipishwa milioni tatu laki tisaambao hawahusiki, wamesharudisha milioni tatu bado lakitisa; na kila mahali wanarudisha. Katika maeneo menginetumewawajibisha watendaji wa TASAF ambao walishirikikatika udanganyifu huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nataka nimhakikishieMheshimiwa Mbunge kwamba zile wilaya ambazozilichelewa nalo siwezi kuwa na jibu la moja kwa moja hapa,nitalifanyia utafiti nijue walichelewa kwa sababu gani nanitachukua hatua stahiki.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Zitto Kabweatafuatiwa na Mheshimiwa Flatei.
MHE. ZITO Z. KABWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, wakatimchakato wa bajeti mpya ya Serikali ya Mwaka 2018/2019unaendelea, kumekuwa na taarifa kwamba Serikali sasainajiondoa katika mfumo wa conditional cash transfer, yaanikwenda kuwapa fedha wananchi na inaanzisha mfumotofauti. Baadhi ya mikataba ambayo Wizara ya Fedha ilikuwaiingie na baadhi ya nchi wafadhili ikiwemo Benki ya Dunia,Wizara ya Fedha imesitisha kusaini kwa sababu Serikali haitaki
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
23
tena kuendelea kutoa hizi conditional cash transfer.Tunaomba taarifa rasmi ya Serikali ndani ya Bunge kuhusianana jambo hili.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Waziri, Ofisi yaRais, majibu.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALABORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kama Waziri mwenyedhamana ya TASAF sina taarifa ya Serikali sasa hivi kujiondoakatika kuwapelekea hizi fedha. Taarifa nilizonazo ni kwambasasa hivi tunafanya utafiti wa hizi fedha. Badala ya watukwenda kupanga foleni pale wilayani kila siku tunaangaliauwezekano wa kupekea fedha zao kwa njia ya simu ilikuwaondolea usumbufu wa kwenda wilayani. Hilo ambaloanasema Mheshimiwa Zitto Kabwe kama analisema likonjiani, lakini halijafika mezani kwa Waziri mwenye dhamanaya TASAF. (Makofi)
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogola nyongeza. Kwanza naipongeza Serikali kwa kuandaampango huu wa kunusuru kaya maskini. Katika jimbo languMheshimiwa Waziri alishawahi kuwa Mkuu wa Wilaya. Je,Mheshimiwa Waziri, kwa sababu anajua Bonde la YaedaChini kwa Hadzabe kule wana tatizo hili la umaskini. Je,ataweza kutuongezea angalau Vijiji vile Mungwamono,Eshkeshi na Endagechani tukapata zaidi msaada huu waTASAF?
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Waziri, Ofisi yaRais, Utumishi na Utawala Bora, majibu.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS UTUMISHI NA UTAWALABORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nakubali kwambanilikuwa DC wa Mbulu 1983 mpaka 1988 na maeneoanayoyataja ya Yaeda Chini nimefika, wanakaa Wahadzabe,wanaishi kwa kuwinda tu badala ya kulima. Natakanimwahidi kwamba kwa kushirikiana na MheshimiwaMbunge, wanachotakiwa wao ni kuzitambua zile kaya
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
24
maskini, wakituletea sisi tutachukua hatua. Nilipita siku nyingikule Yaeda Chini, Mheshimiwa Mbunge akinialika kwendakuwahamasisha, nitashirikiana naye.
MWENYEKITI: Ahsante. Waheshimiwa Wabunge,tunaendelea, swali linalofuata linaulizwa na MheshimiwaDokta Shukuru Jumanne Kawambwa, Mbunge wa Bagamoyona linaelekezwa kwa Waziri wa Viwanda, Biashara naUwekezaji.
Na. 21
Fidia kwa Wananchi Waliopisha Mradi wa EPZA-Bagamoyo
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA aliuliza:-
Wananchi wapatao 1,025 wa Vijiji vya Kiromo, Zinga,Pande, Mlingotini na Kondo walifanyiwa uthamini wa malizao tangu mwaka 2008 ili kupisha mradi wa EPZA Bagamoyolakini hadi sasa hawajalipwa fidia:-
Je, ni lini Serikali itawalipa wananchi hao fidia stahiki?
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJIalijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la ukanda maalum lakiuchumi la Bagamoyo (Bagamoyo Special Economic Zone)ni moja ya miradi ya kimkakati ya kitaifa. Awamu ya kwanzaya mradi huu inahusisha ujenzi wa bandari kubwa ya kisasa,eneo la viwanda kando ya bahari ambapo kwa kuanziaviwanda 190 vitajengwa na ujenzi wa miundombinu wezeshina saidizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2008 mpaka mwaka2010 Serikali ilifanya uthamini wa eneo lengwa lililokuwa nawananchi 2,273 na kubaini mahitaji ya fidia ya shilingi bilioni
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
25
58.771. Katika kipindi cha kati ya Agosti, 2012 na Februari,2015 Serikali iliwalipa wananchi 1,155 jumla ya shilingi 26.66kama fidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kasi ndogo yaupatikanaji wa fedha ya fidia kutoka Bajeti Kuu ya Serikalimwaka 2017, Septemba, Serikali iliamua kubadilisha chanzocha fedha za fidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chini ya utaratibu mpyawabia katika mradi wa Bagamoyo (China Merchant na StateReserve Fund SGRF) ya Oman watatoa fedha za fidia kwamakubaliano maalum na mbia mwenzao (Serikali ya Jamhuriya Muungano wa Tanzania)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwahakikishiawananchi wa vijiji vya Pande, Zinga, Kiromo, Mlingotini naKondo kupitia kwa Mheshimiwa Mbunge wao, kuwa pindimajadiliano ya hawa wabia watatu yanayoendelea sasayatakapokamilika watalipwa pesa zao mara moja.
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: MheshimiwaMwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibumazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. MweziSeptemba, 2015 Serikali iliwalipa fidia wananchi wanaopishamradi wa bandari katika Vijiji vya Pande na Mlingotini.Miongoni mwao wananchi 687 walibainika kwambawalipunjwa fidia zao; kwa hivyo Serikali iliwafanyia uhakikimwezi wa kwanza mwaka jana ili kubaini fidia stahiki zawananchi hao. Je, ni lini wananchi hawa watalipwa fidiazao stahiki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tarehe 22 Mweziwa sita mwaka jana wakati anazindua kiwanda cha Elvinkatika Kata ya Mapinga, Mheshimiwa Rais aliwatangaziawananchi wanaopisha mradi wa EPZ Bagamoyo kwambawale wote ambao hawajalipwa fidia zao wanaweza
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
26
wakarudi sasa katika maeneo yao wayaendeleze maeneoyao. Je, ni lini EPZA na Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyoitawaruhusu wananchi hao kumiliki maeneo yao kamailivyoelekezwa na Mheshimiwa Rais?
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Waziri waViwanda, Biashara na Uwekezaji, majibu.
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipende kumshukuruMheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyofuatilia suala hili; lakinina yeye amekiri kwamba uhakiki ulifanyika kufuatilia walewaliopunjwa. Hapa tatizo kama nilivyosema kwenye sualala msingi ni ukosefu wa pesa za kutosha kutoka kwenye Bajetiya Serikali kufidia maeneo ya kiuwekezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa sababu Serikaliimeshapata njia hii ya pili ya wabia watatu kutafuta pesa,nimshauri Mheshimiwa Mbunge tuendelee kushirikiana kusuditupate fedha za kuweza kuwafidia kila mtu aridhike kusudimradi wetu uweze kufanikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili kuhusu tamkola Mheshimiwa Rais. Tamko la Mheshimiwa Rais ni maelekezo,watu wa EPZA, watu wa halmashauri na hapa kunapashwakuingia wananchi, watakaa kusudi watekeleze tamko laMheshimiwa Rais. Jambo ambalo ningependa Watanzaniawalielewe li le eneo limeamuliwa kwamba ni ExportProcessing Zone. Sasa kuna mchakato unapaswa ufanyikekusudi wewe ukawekeze vinginevyo; lakini kwa mamlakaniliyonayo EPZ na halmashauri na wananchi na wewe Mbungetutakaa chini tuangalie namna ya kuwekeza kwa manufaaya watu wote.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Khadija Nassir.
MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru kwa kuniona. Ripoti ya CAG inaonesha kwambamdaiwa mkubwa wa viwanda vyetu vya ndani ni Serikalihususan halmashauri zetu. Je, Serikali ina mkakati gani
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
27
madhubuti ya kuanza kulipa madeni hayo ili kunusuru angukola viwanda vyetu ambavyo tunavianzisha kwa nia njema?Ahsante. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa. MheshimiwaWaziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, majibu kwakifupi.
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo, Serikali inadaiwa na Serikalisasa tunaongeza jitihada za kuhakikisha kwamba kila stahiliya Serikali inakusanywa na kile kitakachokusanywa ndichokitawalipa wale. Hatujawalipa wale kwa sababu na sisihatujalipwa kuna watu hawapendi kulipa kodi, hata ukisomaeasy of doing business Tanzania tunafanya vibaya kwa sababuwatu hawataki kulipa kodi, lakini katika nchi nyingine huwezikupewa haki nyingine hata kwenda kuchumbia kama huwezikuonesha tax clearance.
MWENYEKITI: Ahsante. Waheshimiwa Wabunge,tunaendelea na swali linalofuata ambalo linaulizwa naMheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini nalinaelekezwa kwa Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Na. 22
Utaratibu Unaotumika kwa AliyepotezaCheti cha Taaluma
MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-
Kumekuwepo na matangazo mengi ya watuwaliopoteza vyeti vya kitaaluma hasa vinavyotolewa naBaraza la Mitihani:-
(a) Je, ni utaratibu gani unaotumika pale mtuanapopoteza cheti ili aweze kupata cheti kingine?
(b) Je, anapata cheti halisi au nakala ya cheti?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
28
(c) Baadhi ya wananchi wanalalamika kuwakumekuwa na ucheleweshaji mkubwa kwa Baraza la Mitihaniwanapoombwa kuwasilisha cheti katika mamlaka fulaniambayo mtu ameomba kazi au nafasi ya masomo na hivyokusababisha waombaji wengi kukosa nafasi kutokana naucheleweshaji huo; je, ni taratibu gani mtu anatakiwakuzifuata ili ombi lake lifanyiwe kazi ipasavyo na kwa wakati?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIAalijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri waElimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali laMheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini,lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mhitimu aliyepoteza chetihupatiwa cheti mbadala au uthibitisho wa matokeo kwakufuata utaratibu ufuatao:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kutoa taarifa kwaJeshi la Polisi kuhusu upotevu wa cheti na kupata hati yaupotevu wa cheti na kupata hati ya upotevu. Lengo lakuripoti polisi ni kupata msaada wa kiuchunguzi ili kusaidiakukipata cheti kilichopotea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mbili, kutangaza gazetinikuhusu upotevu wa cheti kwa lengo la kuutarifu umma ilikusaidia kukipata cheti kilichopotea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, endapohakikupatikana hata baada ya kutangazwa katika vyombovya habari, mhitimu atajaza fomu ya ombi la cheti mbadalaau uthibitisho wa matokeo na kuwasilisha Baraza la Mitihanila Tanzania. Fomu hiyo inapatikana kwenye Ofisi za Barazala Mitihani Tanzania na pia kwenye tovuti ya Baraza ambayoni www.necta.go.tz.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nne Baraza la MitihaniTanzania hufanya uchunguzi wa uhalali wa umiliki wa cheti
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
29
husika na kutoa huduma stahiki. Wahitimu waliofanyamtihani kuanzia mwaka 2008 ambao vyeti vyao vina picha,hupatiwa vyeti mbadala (Duplicate Certificate) nawaliofanya mtihani kabla ya mwaka 2008 hupatiwauthibitisho wa matokeo ambao hutumwa kwa waajiri waoau mahali pengine kwa mahitaji yaliyotolewa na mwombaji.Hivyo, kundi hili la pili hawapewi cheti mbadala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, cheti mbadalakinachotolewa ni cheti halisi. Hata hivyo, kinaongezewamaandishi yanayosomeka Duplicate kuonesha kuwa chetihicho kimetolewa kwa mara ya pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwombaji wa chetimbadala au uthibitisho wa matokeo hupatiwa hudumabaada ya kukamilisha taratibu zinazohitajika na zilizowekwa.
MWENYEKITI: Ahsante sana. Mheshimiwa Chumi.
MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya serikali, nina maswalimawili ya nyongeza. La kwanza litalenga wale waliofanyamitihani kabla ya mwaka 2008 ambao hawapewi chetimbadala. Kwa mujibu wa majibu ya Serikali badala yakupewa cheti wanapewa uthibitisho na mara nyingiuthibitisho huu mtu anakuwa ameomba ili uelekezwe amasehemu anayoomba kazi anayoomba kujiunga na masomozaidi.
Sasa Serikali haioni umuhimu wa hata hawa ambaowalipoteza Cheti ambao walihitimu kabla ya mwaka 2008,kuwafanyia utaratibu wa kuwapa hiyo duplicate?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa maranyingi watu wanaoomba Baraza la Mitihani liwasilishe hizotaarifa kama vyeti kule walikoomba kazi au masomo, vyetihivyo mara nyingi uthibitisho upo kwamba, vimekuwavinachelewa na hivyo kuwasababishia watu hao ama kukosahizo nafasi za kazi walizoomba au nafasi za masomo.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
30
Je, Serikali haioni haja ya kuwa na mifumo kama yavyuo vya elimu ya juu ambapo mtu ambaye amepoteza chetianaweza akapewa nakala hata mbili tatu akazitunzamwenyewe, midhali Serikali na Baraza la Mitihani limejiridhishakwamba, huyo mtu kweli alihitimu masomo hayo? (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri waElimu, Sayansi na Teknolojia, majibu.
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NAUFUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wahitimuwaliomaliza shule kabla ya mwaka 2008, kwa sasa imekuwani vigumu kuwapatia vyeti mbadala kwa sababu wakati huovyeti havikuwa vinabeba picha za wahitimu. Kwa hiyotukitaka kubadilisha maana yake ni lazima tutafute pichaza wale wote ambao wamemaliza shule kabla ya 2008. Kwavyovyote vile ni kazi kubwa, hata hivyo, sio jambo ambalohaliwezekani kufanyika kwa hiyo, nalibeba tukajadilianendani ya Serikali kama linatekelezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kuhusukuchelewa kupatiwa nakala au cheti mbadala au uthibitishokwa wale ambao wanakuwa wamepoteza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto iliyopo nikwamba, mara nyingi watu wanaenda kuomba vyetimbadala au uthibitisho pale wanapokuwa na uhitaji. Ushauriwangu kwa Watanzania wote ni kwamba, kila maraunapopoteza cheti usisubiri mpaka uhitaji kutumia chetihicho ndio ukaanze kutafuta mbadala au uthibitisho.Ukishapoteza anza taratibu za kuanza kutafuta, ili ikitokeakwamba, unahitaji iwe ni rahisi kwa sababu, tayariunakuwanacho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, kwa sasa kwamwombaji yeyote yule, ukiomba inachukua angalau siku 30,lakini hizo ndiyo siku nyingi ambazo kinaweza kuchukua, nimaximum. Inaweza ikawa chini ya hapo na kwa sasa hivi
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
31
kwa kweli, Baraza la Mitihani la Taifa ni moja kati ya Taasisiza Serikali zinazofanya kazi kwa ufanisi mkubwa sana kwahiyo, mara nyingi hazifiki hata hizo siku ukikamilisha taratibuzote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu pendekezo lake lakutumia utaratibu unaotumiwa na vyuo vikuu la kutoanakala, naomba nilibebe, ni wazo zuri, tukaangalie namnaya kutekeleza, ili ikiwezekana tunapotoa cheti tutoe nakalakadhaa ili mtu aweze kutumia pale atakapopoteza. Ahsante.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Anatropia.
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: MheshimiwaMwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa taarifa zinaelezakwamba, vyeti vimekuwa vikizalishwa nje ya nchi. Je, Serikaliina mkakati gani wa kuzalisha vyeti hapa nchini ili zoezi lakuvitoa liwe rahisi zaidi?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NAUFUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa nilizonazo mimivyeti vinatengenezwa hapa hapa nchini, tuna vifaa vyakisasa, Baraza la Mitihani lina vifaa vya kisasa sana na ni taasisiambayo kwa ufanisi wake nchi nyingi sasa hivi zimeanza kujakujifunza namna tunavyofanya. Kama Mbunge ana taarifatofauti na hizi naomba tuonane baada ya Bunge hili ili nijuekwa nini yeye ana taarifa ambazo si sahihi.
MWENYEKITI: Ahsante. Tunaendelea, swali linalofuatalinaulizwa na Mheshimiwa Profesa Jumanne AbdallahMaghembe, Mbunge wa Mwanga na linaelekezwa Wizaraya Nishati. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
32
Na. 23
Utekelezaji wa REA Awamu ya I na II Wilaya ya Mwanga
MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:-
Miradi ya REA I na II katika Wilaya ya Mwangahaikukamilika na fedha zil izokuwa zimepangwahazikutumika:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatiaumeme wananchi waliopitiwa na umeme huo bilakufungiwa?
(b) Je, Awamu ya III ya REA iliyozinduliwa Mwanga,mwezi Septemba, 2017 itaanza kutekelezwa lini?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya MheshimiwaWaziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa ProfesaJumanne Abdallah Maghembe, Mbunge wa Mwanga, lenyeSehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya vijiji 38 kati ya vijiji44 vya Wilaya ya Mwanga vilipata umeme kupitia Awamuya II ya Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini ambapo watejazaidi ya 2,241 waliunganishiwa umeme. Aidha, vijiji sitavilivyosalia havikuweza kupatiwa umeme kutokana naMkandarasi, Kampuni ya SPENCON, aliyekuwa anafanya kazihiyo kushindwa kukamilisha kazi hiyo na mkataba wakekusitishwa mwezi Disemba, 2016.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Nishati Vijijini(REA) imempata Mkandarasi Kampuni ya M/S OctopusEngineering Limited atakayeikamilisha kazi ya kupelekaumeme katika vijiji vilivyosalia kwa awamu ya pili. Kazi hizozimeanza rasmi mwezi Januari, 2018 na zitakamilika ndaniya miezi sita.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
33
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa Mradi wa REAAwamu ya Tatu katika Wilaya ya Mwanga ulianza mweziOktoba, 2017 chini ya Mkandarasi Kampuni ya Urban andRural Engineering Services Limited. Kazi za mradi zinahusishaujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefuwa kilometa 10.98; njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4urefu wa kilometa 24; ufungaji wa transformer 12 za kVA 50;pamoja na kuunganisha wateja wa awali 347. Gharama zamradi ni Dola za Marekani milioni 1.7 na shilingi bilioni 12.3;mradi huu utakamilika mwezi Juni, 2021.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa ProfesaMaghembe.
MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: MheshimiwaMwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Wazirikwa majibu yake. Wizara ya Nishati imesema mara nyingindani na nje ya Bunge kwamba katika vijiji ambavyovinahusika na mradi wa REA watu wote walioko kwenye vijijihivyo, hata wale ambao nyumba zao ni za majaniwatapewa umeme. Hata hivyo, katika utekelezaji wa miradihii Awamu ya Kwanza na Pili katika Wilaya ya Mwanga nifamilia chache sana zilizokuwa zimejitayarisha kupewaumeme ambazo zimefungiwa umeme huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeambiwa kwamba niayake ni kuipa TANESCO biashara ya kuzifungia kaya hizoumeme kwa Sh.177,000/= baada ya mradi kukamilika. Je,sera hii tuliyotangaziwa hapa imefutwa lini ikaja hii yaTANESCO kuchagua watu wachache kuwapa umeme nawengine kuwaacha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, tuliambiwakwamba, mkandarasi huyu ambaye ameshindwa kazi yakusambaza umeme pale awali hawezi tena kupewa kazikatika Wizara ya Nishati na Madini, hasa kazi ileile ambayoyeye alifukuzwa kwa kushindwa kutekeleza. Sasa katikaWilaya ya Mwanga aliyekuwa anatekeleza mradi huu kwaniaba ya SPENCON alikuwa bwana mmoja anaitwa Mrs.Njarita & Company Limited. Sasa Njarita huyo huyo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
34
amepewa kazi ya kutekeleza mradi huo kwa jina lingine laOctopus. Je, inatuambia nini au inawezaje kututhibitishiakwamba, huyu aliyeshindwa kutekeleza huu mradi hukonyuma, sasa ataweza kutekeleza round hii? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti,kwanza namshukuru Mheshimiwa Profesa Jumanne AbdallahMaghembe kwa maswali yake mawili ya nyongeza, lakinina kwa kazi nzuri anayofanya katika kufuatilia mahitaji yanishati katika Jimbo lake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa kwenye ziara wikiiliyopita katika Jimbo la Mheshimiwa Maghembe, kukaguamaeneo mbalimbali ambako mradi huu wa REA Awamu yaPili haukufanyika vizuri, lakini utakubaliana na mimi kwamba,ni kweli kuna mahitaji makubwa na kwa kuwa, hizi kazizinatekelezwa kwa mujibu wa scope na kwamba, scope ileinakuwa haikidhi mahitaji, lakini Serikali ya Awamu ya Tanokwa kutambua hilo imekuja na Mradi Mpya wa Ujazilizi(densification).
Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu unatekelezwakatika mikoa sita ya awali ya mfano. Ilipofika Mkoa waKilimanjaro na wao Mkandarasi Mshauri Elekezi yupo ndaniya mkoa ule kujaribu kufanya feasibility study kwa ajili ya mradihuu, densification kwa maeneo ambayo au kwa kayaambazo hazijaguswa au taasisi za kijamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie Mbungehakuna ukweli wowote kwamba, zile kaya ambazohazijaunganishwa nia ya kwamba, iipe kazi TANESCO.
Mheshimiwa Mwenyekiti, TANESCO ni Serikali ambayonayo ina kazi ya kusambaza umeme, lakini kwa utaratibumwingine, lakini si kweli kwamba, kaya hazifikiwi kwa sababuya kuipa kazi TANESCO. TANESCO itaendelea na kazi yakusambaza umeme, lakini kama umeme vijijini na ndio
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
35
maana Serikali imetambua uwepo wa ukubwa wa mahitajiimekuja na huo Mradi wa densification. Kwa hiyo,nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge zile kaya ambazohazijaunganishwa, zi le taasisi za umma ambazohazijaunganishwa, zitaunganishwa kupitia mradi huu wadensification ambao umefanya vizuri katika Mikoa ya Songwe,Mbeya, Pwani, Arusha, Tanga, Iringa na Mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ameelezakwamba mbona mkandarasi yuleyule ndio amepewa kazina kwamba, Wizara itathibitishaje kwamba kazi zitafanyika.Ni kweli kazi ilifanywa na Kampuni ya SPENCON ambayo ndioilikuwa main contractor. Huyu Kampuni ya Njarita Octopuswalikuwa Sub Contractor. Uchunguzi uliofanyika na Serikalina Wakala wa Umeme Vijijini ulithibitisha kwamba, tatizolilikuwa kwa main Contractor mwenyewe ambaye ni Spenconsi hawa Sub Contractor.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sambamba na hilonilipokuwa katika ziara tulikuwa na Mkandarasi huyu Njaritana sisi tumempa maelekezo na masharti, ndani ya miezi sitakazi zile zilizoshindwa kufanywa zimalizike na zikamilike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati nzuri nilipokuwaeneo la tukio mkandarasi alikuwa ameshaanza kazi naniliwaomba viongozi wa maeneo hayo, WaheshimiwaWakuu wa Wilaya, Waheshimiwa Wenyeviti wa Halmashauri,pia nilizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mamayangu Anna Mghwira kwamba Ofisi yetu au Wizara yetuitasubiria taarifa za mara kwa mara za Mkandarasi huyu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimthibitishie MheshimiwaMbunge kwamba Wakandarasi hawa waliopewa kazi hiitutawafuatilia kwa kila hatua kuona kwamba, makosayaliyojitokeza awamu zilizopita hayajitokezi tena. Ahsantesana. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante, nakushukuru sana kwa majibuyako mazuri Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini angaliawaliosimama humu kwa swali hili, wengi na muda sio rafiki
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
36
kwa hiyo, nitachukua wawili tu Waheshimiwa Wabunge.Najua ni tatizo na Serikali inaona, REA III, REA II, tufanye lamaana.
MHE. SULEIMAN S. MURAD: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru kwa kunipa nafasi. Nina swali moja dogo lanyongeza. Pamoja na majibu mazuri sana ya MheshimiwaNaibu Waziri katika masuala ambayo yanahusu umeme,Mwanga. Tatizo la Mwanga linafanana sana na tatizo laMvomero. REA Awamu ya Pili ambayo Mkandarasi wakealikuwa MDH Power ameishia kwenye maeneo ya makaomakuu ya vijiji, mradi ule haujafika kwenye kaya wala kwenyevitongoji vya ndani. Kwa namna hii maana halisi ya kupelekaumeme vijijini inapotea na nia na madhumuni ya Serikali niwananchi wafaidike na wananchi ambao wana uwezomdogo ni wale ambao wako ndani ya kwenye vitongoji. Je,Naibu Waziri yuko tayari sasa kutoa maelekezo kwacontractor huyu wa REA Awamu ya Pili aje amalizie mradiwake? Pia, yule wa Awamu ya Tatu ambaye ni State…(Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante, swali moja.
MHE. SULEIMAN S. MURAD: Mheshimiwa Mwenyekiti,na yeye apewe maelekezo afike kwenye kaya zote. NaMheshimiwa Naibu Waziri nakukaribisha Mvomero karibusana. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri,majibu kwa kifupi tu.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti,kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Murad kwa swali lakela nyongeza na kazi anazoendelea kufanya za kufuatiliamiradi ya umeme. Nakubaliana na yeye kwamba, huyu
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
37
Mkandarasi MDH kwa kweli hakufanya vizuri na hakuwamkandarasi katika mkoa wake tu, lakini alikuwa mkandarasipia katika Mkoa wa Pwani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi tumetoamaelekezo kwa REA kwa sababu, wakandarasi wote waMiradi ya REA Awamu ya Pili ni Mikoa miwili tu Tanga na Arushaambao wametimiza vigezo na wamemaliza kipindi chauangalizi. Kwa hiyo mikoa mingi ina changamoto, Singida,Mbeya, Mikoa ya Kanda ya Ziwa. Kwa hiyo, tumetoamaelekezo na tumewataka REA wafanye tathmini natutachukua hatua na kwamba, maelekezo ni kwamba,awamu ya tatu isiruke kitongoji chochote wala taasisi yaumma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niliahidi Bungelako Tukufu kwamba, nimesema tangu awali kwamba,upungufu wa awamu ya pili tumeubaini, tathmini imefanyika,awamu ya tatu tumejipanga vizuri kuhakikisha kwamba,umeme huu au miradi hii inatimiza lengo lililotarajiwa namaelekezo ya Serikali kwamba, kila kitongoji kisirukwe.Ahsante sana.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Nnauye na wamwisho Mheshimiwa Gekul.
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.Kwanza niipongeze Serikali chini ya Wizara ya Nishati kwakazi nzuri wanayofanya ya usambazaji wa umeme vijijini, hasahii REA Awamu ya Tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwamba, kwakuwa gharama za kuunganisha umeme wakati mradiunaendelea katika eneo ni Sh.27,000 na mradi ukishapita niSh.177,000; na kwa kuwa idadi nzuri na kubwa ya watumiajiwa umeme ni biashara nzuri kwa TANESCO, kwa nini sasabei hii isiwe moja hiyohiyo ya 27,000 badala ya bei kupandabaada ya mradi kwisha? Kama haiwezekani, basi REA hawawaendelee na kazi ya usambazaji wa nguzo na
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
38
miundombinu na TANESCO wafanye kazi moja tu yakupeleka umeme na kukusanya kodi yao baada ya kupelekaumeme?
MWENYEKITI: Ahsante. Majibu Mheshimiwa NaibuWaziri wa Wizara ya Nishati.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru sana kwa kunipa fursa na namshukuru sanaMheshimiwa Mbunge, Kaka yangu Nape Nnauye. Ni kwelibei ya kusambaza umeme ya vijijini ni Sh.27,000 kipindi chamradi na hii ni hatua ya Serikali yetu ya Awamu ya Tanokwamba, imegharamia gharama zote za uunganishwaji kwaumeme huu na kwamba mwananchi yeye gharama yake nianalipia VAT.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wazo alilolisemakwamba, mara baada ya mradi kukamilika na miundombinukukabidhiwa TANESCO ni kweli wananchi wanaunganishwakwa bei ya Sh.177,000, lakini hata hivyo niseme hata hii beipia, Sh.177,000 nayo ina mchango wa Serikali kwa sababu,mijini kwa bei hii wanaunganishwa kwa Sh.321,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, wazo alilosemalinapokelewa na litafanyiwa kazi na ni la msingi kwa sababu,Wizara yetu na Shirika letu la TANESCO na wadau wenginewa nishati kwamba, tunauza bidhaa ya umeme. Kwa hiyo,ni vema zaidi kwamba, tunapoiuza tupate wateja wengi, ilitupate mapato na kuendesha shughuli mbalimbali nauwekezaji mpya wa maeneo ya nishati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimthibitishieMheshimiwa Mbunge, nimelipokea na Serikali itaona utaratibugani wa kufanya ili iweze kurahisisha. Ahsante sana.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Gekul.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti,nikushukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
39
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikiahidimara nyingi sana kulipa fidia wananchi ambao maeneo yaoyanapitiwa na umeme wa KV400. Miongoni mwa maeneohayo ni Mkoa wa Manyara na katika Jimbo langu la BabatiMjini, wameahidi zaidi ya mara tatu na ahadi ya mwisho nitarehe 17 Disemba, kwamba, mngewalipa. Hata hivyo,mpaka sasa Mheshimiwa Naibu Waziri mmekuwa mkisemakwamba, Wizara ya Fedha haiwapi pesa na Waziri wa Fedhayuko hapa. Naomba awatangazie wananchi wa Jimbolangu la Babati Mjini kwamba, ni lini wanawalipa fidia hiyokwa sababu, wamechoka kusubiri?
MWENYEKITI: Lini mnawalipa?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti,namshukuru sana Mheshimiwa Pauline Gekul kwa swali lakezuri, lakini naomba niseme haijapata kutokea Wizara yetuya Nishati ikasema Wizara ya Fedha haijatupa pesa, kwasababu Serikali inafanya kazi kwa pamoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ambayoilijitokeza ni kwamba tulipata jedwali la thamani ya fidia.Wizara yetu ya Fedha kazi yake yeye hata inapoleta pesa nikuangalia malipo yanafanyika kwa walengwa na kwaviwango sahihi. Kwa hiyo kulikuwa na changamoto ndogondogo tu za kumalizia kwa ajili ya kuthibitisha uhalali,kiwango na walipwaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimwambieMheshimiwa Mbunge mradi huu wa KV400 msongo huu nimuhimu ambao unaunganisha na nchi ya jirani ya Kenya kwakusafirisha umeme kwa maeneo mbalimbali. Kwa hiyonimthibitishie kwamba fidia ya wananchi wa maeneo hayoitalipwa muda si mrefu, ndani ya mwaka huu wa fedha namaandalizi yanaendelea vizuri. Ahsante sana.
MWENYEKITI: Ahsante. Swali linalofuata linaulizwana Mheshimiwa Sussane Peter Masele, Mbunge wa VitiMaalum na linaelekezwa kwa Wizara ya Madini.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
40
Na. 24
Kuwapatia leseni na vibali wachimbaji wadogowadogo - Misungwi
MHE. SUSANNE P. MASELE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatekeleza kauli ya Mheshimiwa Raiskuhusu kuwapatia wachimbaji wadogo wadogokipaumbele cha leseni na vibali vya kuchimba madini kwakuonesha mfano kwa wachimbaji wadogo wa machimboya Dhahabu ya Ishokelahela, Misungwi?
NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO)alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajibu swali laMheshimiwa Susanne Masele naomba nichukue nafasi hiinimshukuru sana Mungu kwa kunipa kibali cha kusimamahapa, lakini vile vile nimshukuru sana Mheshimiwa Rais waJamhuri ya Muungano Tanzania Dkt. John Pombe JosephMagufuli kwa Imani kubwa aliyonipatia na akaona nawezakumsaidia kwenye Sekta hii ya Madini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo hayonaomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa Susanne Peter MaseleMbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, wachimbaji wa Madiniwadogo wa Ishokelahela Wilayani Misungwi walivamia nakuanza shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu katikaeneo la Leseni kubwa ya utafutaji wa madini inayomilikiwana Kampuni ya Carlton KitongoTanzania Limited yenyeukubwa wa kilomita za mraba 12.4 tokea mwezi Julai, 2017.Kabla ya hapa wachimbaji hao walikuwepo lakini kwa kiasikidogo. Mpaka kufikia sasa leseni hiyo imevamiwa nawachimbaji wadogo zaidi ya 1000 ambao wanachimbamadini hayo ya dhahabu.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
41
Mheshimiwa Mwenyekiti, leseni ya CarltonKitongoTanzania Limited ilitolewa tarehe 5 Agosti, 2014 naitamaliza muda wake wa awali tarehe 4 Agosti 2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkuu wa Wilaya ya Misungwikwa kushirikiana na kampuni ya Carlton Kitongo TanzaniaLimited ambaye ni mmiliki wa leseni hiyo waliamua kutengaeneo kwa ajili ya kuwaachia wachimbaji wadogo ambalolikuwa linamilikiwa na kampuni hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, makubaliano hayoyalihitimishwa rasmi mwezi Desemba mwaka 2017 kati yammiliki wa leseni na vikundi ambayo viliungana kuundakikundi kimoja kwa jina la Basimbi and Buhunda MiningGroup. Nakala ya makubaliano hayo ipo Ofisi ya MadiniMwanza na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Misungwi. Vikundi hivyovilipatikana baada ya Wizara kupitia Ofisi yetu ya MadiniMkoani Mwanza kutoa elimu ya umuhimu ya kujiunga katikavikundi na kuendesha shughuli za uchimbaji madini ili ziwezekuwa na tija zinazozingatia matakwa ya Sheria ya Madini naKanuni zake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza kauli yaMheshimiwa Rais kuhusu kuwapatia wachimbaji wadogokipaumbele cha leseni na vibali vya kuchimba madini, leseniza wachimbaji madini katika eneo hilo zitatolewa kwavikundi hivyo mara tu baada ya taratibu za kisheria zakushughulikia maombi hayo kukamilika.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Sussane Masele.
MHE. SUSANNE P. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili yanyongeza. Swali la kwanza, baada ya taratibu kukamilika,je, Serikali itachukua muda gani kuwapatia leseniwachimbaji hao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, yamejitokezamadai kuwa zuio la mchanga pale bandarini makinikiahalikuwagusa wachimbaji wakubwa tu hata wadogo pia.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
42
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwambawachimbaji hao wadogo wanasafisha mchanga wao hapanchini ili kuendeleza uwekezaji na kutengeneza ajira zaidikwa wachimbaji hawa wadogo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri waMadini, kwa kifupi.
NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itachukua muda gani,naomba nimjibu Mheshimiwa Mbunge kwamba, taratibu zakuunda Tume ambayo ndiyo imepewa mamlaka ya leseniya uchimbaji madini, iko katika hatua za mwisho zakuundwa. Mara itakapokamilika kazi hiyo itaanza mara moja,kwa hiyo, haitachukua muda mrefu sana baada ya Tumehiyo kuwa imeshakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili la zuio lamchanga, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbungepamoja na Watanzania, kwamba Sheria ya Madini haijazuiausafirishaji wa michanga nje ya nchi isipokuwa zipo taratibuna sheria ambazo yule mtu anayetaka kusafirisha mchangakama madini lazima azifuate kwa mujibu wa sheria. Kwahiyo, naomba nimhakikishie kwamba tumezuia yalemakontena kwa sababu yalikuwa na mgogoro ambaoSerikali tuliona kuna haja ya kujiridhisha kabla ya kuruhusu.
Mheshimiwa Mwenyekti, kama kuna wananchiambao wana madini ya mchanga ambao wanatakakuyasafirisha kwenda nje ya nchi kama wengine ambavyowanapata vibali na wao wafuate taratibu watapewa vibali.(Makofi)
MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru. Serikali iliahidi kutenga maeneo ya Ibindi, Dirifu,
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
43
Society na Kapanda kwa wachimbaji wadogo wa hukoMpanda, je, ni lini wachimbaji hawa watapatiwa leseni?
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri waMadini, lini watapewa leseni kwenye maeneo husika.
NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimpongeze sanaMheshimiwa Kapufi kwa ufuatiliaji wake kwenye jambo hili.Kwa muda mfupi ambao nimeingia ofisini amekuwa maranyingi akiniambia jambo hili juu ya wachimbaji wakewadogo wadogo. Naomba nitumie fursa hii kuwaambiaWatanzania wote wakiwepo na wananchi wa Kibindikwamba wale wote ambao wamejiunga kwenye vikundiwakaomba maeneo mbalimbali kwa ajili ya uchimbajimadini Wizara ya Madini iko tayari kuwasaidia mara tu, Tumeya Madini itakapoanza kazi baada ya kuwaimekwishakuundwa.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa RidhiwaniKikwete, Mbunge wa Chalinze.
MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti,kwanza nami nimpongeze Mheshimiwa Dotto kwakuchaguliwa kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Madini.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hilo naombaniombe kuuliza au kupata kauli ya Serikali juu ya lini Serikaliitaruhusu mwekezaji wetu Gulf Concrete awalipe fidiawananchi wapatao 80 wanaoishi katika maeneo mbalimbaliya Kata ya Lugoba ili waweze kuendeleza eneo lile na waowaweze kuondoka na kulinda afya zao?
NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTTO M. BITEKO):Mheshimiwa Mwenyekiti, mwekezaji wa Gulf Concrete andCement Product ambaye yuko Chalinze kwenye Kijjiji cha
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
44
Nguza amekuwa akichimba kwa muda mrefu kwenye eneohilo; na kwa kweli anachimba kwenye eneo hiloametengeneza ajira zaidi ya 170 kwa watu wa Chalinzeambako Mheshimiwa Mbunge anafuatilia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumetoa mgogoro mdogoambao sisi kama Wizara ya Madini tunaushughulikia.Mwekezaji huyu amechimba na akaingia kwenye eneo lamwekezaji mwingine ambaye ana leseni anaitwa GlobalMining; ameingia kwenye eneo ambalo lina ukubwa kamahekta 1.5.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulichofanya kwa sasa,tunataka tuumalize kwanza mgogoro huu ambao yeye GulfConcrete ameingia kwenye eneo la mtu mwingine.Tukishamaliza twende kwenye hatua ya pili sasa ya kumsaidiaMwekezaji huyo ambaye kwa kweli ana tija kwa watu waChalinze na watu wa Mkoa wa Pwani aweze kulipa fidia iliaendeleze mradi wake.
MWENYEKITI: Nashukuru. Waheshimiwa Wabunge,tunaendelea tuko nyuma sana ya muda. Swali lililofuatalinaulizwa na Mheshimiwa Emmanuel Mwakasaka, Mbungewa Tabora Mjini na linaelekezwa kwa Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, majibu.
Na. 25
Migogoro ya Ardhi Nchini
MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA,aliuliza:-
Kumekuwa na migogoro mingi ya ardhi nchiniinayosababisha uvunjifu wa amani miongoni mwa wananchina hata katika baadhi ya maeneo migogoro hiyoimesababisha vifo;
(a) Je, Serikali imechukua hatua gani kutatuamigogoro hiyo?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
45
(b) Kwa kuwa Maafisa Ardhi wengi ndiyo chanzocha migogoro hiyo, je, ni Maafisa Ardhi wangapiwamechukuliwa hatua kwa kusababisha migogoro hiyo?
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEOYA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba uniruhusu kwanzakwa sababu ni mara ya kwanza mwaka huu niwatake heriya mwaka mpya wote na tumshukuru Mungu kwambatunaendelea kulijenga Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo,naomba nijibu swali la Mheshimiwa Emanuel AdamsonMwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uwepowa migogoro ya ardhi nchini na tayari imeweka mikakatimbalimbali ya kuitatua na kuzuia uwezekano wa kuibukamigogoro mipya. Baadhi ya mikakati hiyo ni pamoja na:-
(i) Kutoa elimu kwa watendaji wanaohusika nautatuzi wa migogoro ya ardhi kuanzia ngazi za Serikali zaMitaa hadi Serikali Kuu na kuzifanyia marekebisho sera nasheria mbalimbali zinazosimamia sekta ya ardhi;
(ii) Kuboresha Mabaraza ya Ardhi nakuyaongezea watumishi pamoja na vitendea kazi;
(iii) Kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhiya wilaya na vijiji; na
(iv) Kutekeleza mkakati wa kupima kila kipandecha ardhi nchini na kuboresha mifumo ya kutunzakumbukumbu za ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Wizara imeanzishautaratibu wa kushughulikia migogoro ya ardhi ambapoMheshimiwa Waziri akiambatana na wataalam wa sekta yaardhi amekuwa akikutana na wananchi papo kwa papo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
46
na kutatua migogoro na changamoto zinazowakabili kwamfumo ambao tunaita Funguka na Waziri wa Ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya ardhi kwanamna moja ama nyingine husababisha pia na watendajiwa sekta ya ardhi wasio waaminifu; lakini Serikali imeendeleakuwachukulia hatua maofisa hao kwa mujibu wa sheria,kanuni na taratibu zilizopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya mwaka 2014/2015 na2016/2017, watumishi wanne wamesimamishwa kazi baadaya kufikishwa Mahakamani kutokana na ukiukwaji wa maadiliya Utumishi wa Umma; watumishi 16 walifukuzwa kazi kwamakosa mbalimbali ya kiutendaji; na watumishi 19waliandikiwa barua za onyo na kutakiwa kutekelezamajukumu yao kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibuzinazoongoza utumishi wa umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa watendaji wa sekta yaardhi walio chini ya usimamizi wa Mamlaka za Serikali zaMitaa Wizara imekuwa ikishirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMIkatika kuhakikisha kuwa hatua stahiki zinachukuliwa dhidiya watendaji hao ambao wamekuwa wakisababishamigogoro kutokana na kutowajibika au kukiuka masharti yaajira zao.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Mwakasaka.
MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: MheshimiwaMwenyekiti nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswalimawili ya nyongeza. Tabora Manispaa imeathirika sana namigogoro ya ardhi. Kuna kata ambazo zinapakana namaeneo ya jeshi, ambazo ni Kata za Cheyo, Mbugani,Tambuka Reli, Uyui na Micha. Maeneo yale yamekuwa namigogoro ya mipaka ya muda mrefu. Je, Wizara ya Ardhiimejipangaje kwa kushirikiana na Wizara ya Ulinzi ili wawezekuoanisha sasa mipaka halisi ili kuweza kutatua migogorohii ya mipaka katika kata hizo?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
47
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Tabora kamanilivyosema manispaa imekuwa na migogoro mikubwa yaardhi na hasa bomoa bomoa. Tabora imeathiriwa sana nazoezi la bomoa bomoa; si maeneo ya reli tu lakini hatamaeneo mengine yanayopaka na mashule kama TaboraGirls…
MWENYEKITI: Mheshimiwa uliza swali.
MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Wananchi wale namaafisa kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri wenginesi waaminifu. Je, Serikali kwa kuwa hawa wananchi wengiwaliobomolewa hayakuwa makosa yao, inawachukuliahatua gani hawa ambao wamesababisha wananchiwamepata hasara kubwa na sasa hawana hata amani nawamekuwa katika hali isiyoeleweka?
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri waArdhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, majibu kwa kifupi.
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEOYA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanzaamezungumza habari ya mipaka kuathiri maeneoyaliyopakana na Jeshi na ametaja kata ya Cheyo, TambukaReli na nyingine. Naomba tu nimthibitishie MheshimiwaMwakasaka kwamba Wizara ya Ulinzi ilishachukua hatua yakuunda Kamati ambayo imepitia katika maeneo yoteambayo yana migogoro ya Jeshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo hayowalikuwa wakifika wanaongea na watu wa eneo lile nakuweza kubainisha mipaka; kwa sababu kuna mengineambayo wananchi lakini maeneo mengine Jeshi liliingiandani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kabla ya kuanzakuweka mipaka upya au kuipitia kwanza wanachambua yalemaeneo. Wakishamaliza shughuli hiyo ndiyo Wizara itaingilia
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
48
kati katika suala la kupanga. Hata hivyo, kwanza tuitambuetuibaini ili kuondoa ile migogoro. Zoezi limeshaanza katikabaadhi ya wilaya na Kamati ile inafanya kazi vizuri kwasababu inashirikisha uongozi wa maeneo husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala labomoa bomoa katika maeneo ambayo yamevamiwa auwatu wamebomolewa pengine hawakuwa na tahadhari;kwanza naomba nitoe tahadhari kwa wananchi wengi,kwamba maeneo mengi ya taasisi za umma yamevamiwasana na wananchi na wengine wamejenga nyumba zakudumu kwa muda mrefu. Hata hivyo, unapoangalia kisheriana taratibu na ukubwa wa shule yanayotakiwa kuwaunakuta sehemu nyingi yamevamiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kwa makosa yawatendaji wetu kuna wengine pia walithubutu kutoa hatikatika maeneo ambayo ni ya shule. Kwa hiyo zoezi hililinafanyika ili kuhakikisha kwamba maeneo yote yanapimwana yanatambulika na wale wote walioingia ndani basi sheriainachukua mkondo, wake kwa maana ikiwa ni pamoja nakuvunjiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wale ambaowatakuwa wamevunjiwa kimakosa ni lazima uhakikiufanyike tuweze kujua pengine hata ile hati aliyonayo si sahihi.Kwa hiyo kama tukikuta mtu amevunjiwa katika utaratibuambao ni wa kimakosa basi tutaona namna ya kuwezakumpatia kiwanja mbadala. Nitoe rai tu kwamba wale wotewalioko kwenye maeneo ya umma ni vizuri wakayaachia.
MWENYEKITI: Ahsante. Waheshimiwa Wabunge,tunaendelea. Swali linalofuata linaulizwa na MheshimiwaMachano Othman Said toka Baraza la Wawakilishi. Zanzibarlinaulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Saada Mkuya nalinaelekezwa kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianowa Afrika Mashariki.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
49
Na. 26
Kufungua Ubalozi Nchini Cuba
MHE. SAADA MKUYA SALUM (K.n.y MHE. MACHANOOTHMAN SAID) aliuliza:-
Kwa muda mrefu Tanzania imekuwa na uhusiano mzurikiuchumi, kiafya na kisiasa na Jamhuriya Muungano wa Watuwa Cuba, lakini Tanzania haina Ubalozi katika nchi hiyo:-
(a) Je, ni lini Tanzania itafungua ubalozi wakenchini Cuba hasa ikizingatiwa kuwa Cuba tayari wanaUbalozi nchini muda mrefu?
(b) Je, Serikali inajua kwamba kutokana naTanzania kutofunga Ubalozi nchini Cuba, imesababishasanamu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyeree kutowekwakatika uwanja wa Viongozi muhimu wa Afrika katika Jiji laHavana?
NAIBU WAZIRI MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WAAFRIKA MASHARIKI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ruhusa yako na kwaniaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianowa Afrika Mashaki, kabla ya kujibu swali la MheshimiwaMachano Othman Said, Mbunge wa Baraza la Wawakilishinaomba kutoa maelezo mafupi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Tanzania na Cubaimekuwa na mahusiano mazuri ya Kidiplomasia, Kisiasa,Kiuchumi, Kielimu, Kiafya na Kiutamaduni kwa muda mrefuyalioanzishwa na waasisi wa Mataifa haya mawili, HayatiBaba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere waTanzania na Hayati Fidel Alejandro Castro Ruz wa Cuba. Kwaujumla mahusiano haya mazuri yamedumu kwa miaka mingikutokana na kuwa na maslahi mapana na nchiyanayozingatia usawa.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
50
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo hayamafupi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa MachanoOthman Said, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, lenyevipengele (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu yaTano kwa kutambua mahusiano mazuri na ya muda mrefuyaliyopo baina ya nchi hizi mbili ina mpango wa kufunguaubalozi katika Mji wa Havana Cuba. Hivi sasa taratibu zakufungua Balozi hizi zinaendelea, mara zitakapokuwazimekamilika ubalozi huo utafunguliwa kama ulivyopangwa.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Cuba kwakutambua na kuthamini mchango mkubwa uliotolewa namashujaa katika vita vya ukombozi wa bara la Afrika iliamuakujenga mnara wa kumbukumbu kuenzi juhudi na harakatihizo pamoja uzalendo wa viongozi hao akiwemo HayatiBaba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Mheshimiwa Mwenyekiti, si kweli kwamba Tanzaniakutokufungua Ubalozi nchini Cuba kumesababisha sanamuya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyererekutokuwekwa katika Uwanja wa Viongozi Muhimu Afrikakatika Jiji la Havana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sanamu hiyo haikuwekwakatika uwanja huo kutokana na muonekano wake kutokuwana uhalisia wa sura ya Hayati Baba wa Taifa, hivyoutengenezaji wake kuanza upya. Matengenezo ya sanamuhiyo yanaendelea na Serikali inafanya juhudi ili sanamu hiyoikamilike na kuwekwa sehemu iliyopangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kulithibitishia Bungelako Tukufu kuwa mahusiano ya Tanzania na Cubayataendelea kuwa mazuri katika nyanja mbalimbali hapanchini kama vile diplomasia, afya, elimu, michezo, utalii nabiashara.
MHE. SAADA MKUYA SALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa NaibuWaziri, nina maswali mawili ya nyongeza. KwanzaMheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba mipangoinaendelea kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kufunguaUbalozi. Hata hivyo, tunaomba tu awaambie Watanzaniahii mipango imefikia hatua gani i l i na wao wapateconfidence kwamba Ubalozi huu utafunguliwa karibuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili, kwa upande wamashirikiano, Zanzibar inashirikiana kwa karibu sana na Cubahasa katika nyanja ya afya na imekuwa ikipeleka wanafunzimbalimbali kwa ajili ya masomo ya muda mfupi na mrefu.Je, Mheshimiwa Waziri haoni kwamba kuchelewa kufunguaBalozi hii katika Mji wa Havana kunawapa maisha magumuwanafunzi wale kwa maana wanakuwa hawajuiwanapopata matatizo wakimbilie wapi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANOWA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukurukwa maswali mawili ya nyongeza ambayo yameulizwa naMheshimiwa Saada Mkuya akitaka kujua hatua iliyofikiwakwa sasa hivi. Naweza kumwambia tu utaratibu wa mwanzohuwa tunafanya kutafiti kutengeneza gharama za kuanzishaBalozi, uanzishwe wapi, watu wangapi wapelekwe, lakinimwisho kabisa ni lazima tuwe tumejiandaa kwamba tunapesa ya kutosha na imewekwa kwenye bajeti ndipo hapoUbalozi unaweza ukafunguliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa pia anajuakwamba tuna Balozi nyingine sita ambazo zimefunguliwakwa mwaka wa fedha 2016/2017 ambazo bado tunatakatuhakikishe kwamba tumekamilisha mambo yote
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
52
yanayohusiana na staffing, gharama za nyumba nauendeshaji. Hatuwezi tu tukafungua kwa sababu tumesema,tukishakuwa tumejiandaa tutaweza kusema ni lini. Hatahivyo, utaratibu wa kuangalia aina ya watuwatakaopelekwa na gharama za uendeshajizimekwishakamilika, tunasubiria kwanza zile ambazozimepangwa zikamilike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini suala la pil itunatambua kwamba mahusiano baina ya Tanzania naCuba ni mazuri na Zanzibar kama yeye anavyojua kwambani sehemu pia ya Tanzania. Nataka kumhakikishia kwambawale wanafunzi ambao wanasoma kule Cuba kwa kozi zamuda mrefu na mfupi watakuwa wanaendelea kusimamiwana Balozi yetu ya Canada maana ndiyo wanaosimamiawanafunzi au wafanyakazi wote wa Tanzania walioko Cuba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimwambiemahusiano hayo hayako mazuri tu kwa upande wa Zanzibarni mazuri kwa Tanzania nzima. Kwa kumpa tu taarifa mwakajana Manesi 16 pamoja na Madaktari kwa mkataba wamiaka miwili wa kutoka Cuba watakuwa wanafanya kazikatika Hospitali yetu ya Muhimbili na Waziri wa Afya yukohapa anaweza kukiri hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuna mahusiano mazurikwenye suala la elimu, kuna Madaktari na Wataalam waafya ambao wanatoa mihadhara katika vyuo vyetu vikuu.Kwa hiyo, nataka kumhakikishia kwamba wale wanafunziambao wamepelekwa kutoka Zanzibar wataendeleakuhudumiwa na Balozi yetu ya Canada.
MWENYEKITI: Ahsante. Waheshimiwa Wabunge,tunaendelea na swali l inalofuata na linaulizwa naMheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge waSame Mashariki na linaelekezwa kwa Waziri wa Mambo yaNdani ya Nchi.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
53
Na. 27
Hitaji la Vituo vya Polisi Tarafa ya Mamba na Gonja-Same
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:-
Jimbo la Same Mashariki lina Kata 14 lakini lina Kituokimoja cha Polisi kilichopo Kata ya Maore na vituo vidogovilivyopo Kata ya Ndungu na Kihurio; vituo vyote hivyo vipokatika tarafa moja yenye kata tano, kata nyingine tisaambazo zipo katika tarafa mbili zilizoko mlimani na zipo mbalisana na vituo hivyo vya Polisi zinapata shida sana kutoa ripotiza uhalifu. Kwa kuwa wananchi wa tarafa hizo mbili zamlimani tayari wametenga maeneo ya kuweka vituo vyaPolisi:-
(a) Je, Serikali ipo tayari kuanzisha Vituo vya Polisikatika Tarafa ya Mamba/Vunta na Tarafa ya Gonja?
(b) Kama Serikali ipo tayari kuanzisha Vituo hivyovya Polisi, je, ni lini Polisi hao wataanza kazi?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri waMambo ya Ndani, najibu swali la Mheshimiwa NaghenjwaLivingstone Kaboyoka, Mbunge wa Same Mashariki, lenyesehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimuwa kuwa na Vituo vya Polisi katika ngazi ya Kata na Tarafanchi nzima, Mamba/Vunta na Gonja zikiwemo. Katika Tarafaya Gonja kuna Kituo cha Polisi, Daraja B kinachotoa hudumaza kipolisi katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Tarafa ya Mambawananchi wamejitolea eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa Kituocha Polisi ambapo kwa sasa majadiliano kati ya Jeshi la Polisina wananchi kuhusu ujenzi wa Kituo cha Polisi, Daraja la Byanaendelea. Hata hivyo, kwa sasa Tarafa ya Mamba ina
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
54
Kituo kidogo Daraja la C ambacho kinatoa huduma kwawananchi katika Tarafa hiyo. Aidha, Jeshi la Polisi hufanyadoria mara kwa mara katika maeneo hayo ya milimaniambayo hafikiwi kirahisi na vyombo vya usafiri kutokana najiografia yake.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naghenjwa.
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: MheshimiwaMwenyekiti, nashukuru sana. Naomba Naibu Waziri aliombeBunge lako Tukufu radhi kwa kulidanganya. Amesema Tarafaya Gonja ina Kituo cha Polisi cha Daraja B, naomba afanyehome work, tarafa hii mimi ndiyo natoka na hakuna hataKituo cha Daraja C, sasa hicho cha Daraja B amekitoa wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, hata huko anakosemakipo Kituo cha Daraja C, iko nyumba haijawahi kuwekwapolisi hata siku moja. Naomba sana Mheshimiwa NaibuWaziri aeleze Bunge lako Tukufu kwa nini anatoa taarifa zauongo ambapo hata wananchi katika Jimbo languwatashangaa kwamba hicho kituo Daraja B, kiko wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili yanyongeza. La kwanza, Waziri atakumbuka kwambanimeshawaandikia Wizara yao barua mara mbili kuombakituo hiki kilichopo Maore, Tarafa ya Ndungu ambachokimejengwa mwaka 1959, kimechakaa ceiling boardzimedondoka, vigae vilivyowekwa hata kabla ya Uhuruvimebomoka hata OCS hana mahali pa kukaa kufanyia kazi,aseme lini Serikali itaweza kukarabati kituo hiki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pil i amesema Polisiwanafanya doria kwenye Jimbo hili, atajua kwamba Polisiwa Kituo cha Maore chenye Daraja B kama anavyosemakipo Tarafa ya Ndungu hawana hata matairi kwenye magariyao, usafiri wao ni wa shida, sasa hiyo doria wanaifanyaje?Ahsante.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri waMambo ya Ndani ya Nchi, majibu.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
55
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nilichokieleza katika majibuyangu ya msingi, nilieleza kwamba kulingana na maeneoambayo walileta maombi ya ujenzi wa vituo katika Tarafaya Gonja kwamba kuna Kituo cha Daraja B sio C. KatikaTarafa ya Mamba nilichokisema ni kwamba wananchiwametoa eneo, kwa hiyo tupo katika mchakato wa ujenziwa kituo hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kituo cha Maore nikweli Mheshimiwa Mbunge aliwahi kuwasilisha barua yakekwa Mheshimiwa Waziri kuhusiana na ukarabati wa kituo hikina barua yake tunaifanyia kazi na pale uwezo utaruhusu basitutafanya marekebisho ya kituo hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusiana na ubovuwa magari kwa ajili ya doria, nimhakikishie MheshimiwaMbunge kwamba natarajia muda siyo mrefu kufanya ziarakatika Jimbo lake nitamwomba na yeye kama atakuwa nanafasi tuambatane ili tukaone changamoto hizo. Tatizo lausafiri katika nchi yetu ni kubwa sana, kwa hiyo itategemeauzito tutakavyoona katika eneo hilo kulinganisha na maeneomengine katika nchi nzima tuone uwezekano wa kusaidiausafiri ili waweze kufanya kazi zao vizuri hasa maeneo yamilimani ambapo hakuna mawasiliano mazuri ya usafiri.
MWENYEKITI: Ahsante. Tunaendelea Waheshimiwa naswali linalofuata ambalo linaulizwa na Mheshimiwa FakhariaShomar Khamis, linaelekezwa Wizara hiyo hiyo ya Mambo yaNdani ya nchi.
Na. 28
Tatizo la Kupotea kwa Watoto-Dar es Salaam
MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-
Tatizo la kupotea kwa watoto katika Jiji la Dar esSalaam limekuwa kubwa. Aidha, taarifa za kupotea kwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
56
watoto hao zimekuwa zikitolewa kwenye vyombo vyahabari:-
(a) Je, ni sababu zipi zinazochangia kuongezekakwa tatizo hilo siku hadi siku?
(b) Je, kwa nini taarifa za upatikanaji wa watotohao hazitolewi kwenye vyombo vya habari?
(c) Je, Serikali ina mkakati gani kuondoa tatizohilo?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri yaMambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali laMheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa VitiMaalum lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya hivi karibunikumekuwepo na wimbi la upoteaji wa watoto katikamaeneo mbalimbali nchini ikiwemo Jiji la Dar es Salaam.Aidha, sababu za upotevu wa watoto hawa ni pamoja nauangalifu hafifu wa watoto kutoka kwa wazazi au walezina jamii kwa ujumla, mazingira magumu wanayoishi baadhiya watoto, imani za kishirikina, visasi kati ya familia nakupotea kwa bahati mbaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na hali hiyo, Serikalikupitia Jeshi la Polisi imekuwa ikifanya jitihada mbalimbaliza kudhibiti matukio hayo kwa kutoa elimu kupitia programuya Polisi Jamii kwa watoto mashuleni na wazazi kupitiamihadhara ya kijamii na vyombo vya habari. Jitihada hizozimekuwa zikizaa matunda kwa kuongeza elimu ya usalamawetu kwanza miongoni mwa jamii na hivyo kuongezaumakini wa kulinda watoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kipindi cha kuanziaJanuari hadi Disemba, 2017 kwa Mkoa wa Dar es Salaamwalipotea watoto 184, ambapo watoto waliopatikana ni
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
57
176 na watoto ambao wanaendelea kutafutwa ni nane.Jeshi la Polisi linaendelea kutoa rai kwa taasisi na idarambalimbali kama Ustawi wa Jamii kushirikiana na kuwa naprogramu za pamoja ili kutoa elimu ya kumlinda mtoto waTanzania.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Fakharia.
MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: MheshimiwaMwenyekiti, ahsante. Kwanza sina budi kumshukuruMheshimiwa Naibu Waziri kwa kulitamka vizuri jina langu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuuliza maswalimawili ya nyongeza ambapo maswali ya msingi amenijibuvizuri na yameeleweka lakini kuna kifungu cha mwisho hapaambacho kimenifanya niweze kupata maswali ya nyongeza.Amekiri kwamba watoto 184 walipotea na 176wamepatikana na nane hawajapatikana lakini badowanaendelea kutafutwa. Sasa napenda kumuuliza hiviMheshimiwa Waziri kwa hao waliopatikana na haowaliokutwa nao, Serikali imechukua hatua gani yakuwawajibisha kisheria? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wale watotobaada ya kupatikana ambapo alikuwa hayuko kwenyemazingira ya wazazi lazima afya itakuwa ni mgogoro. Je,Serikali au vyombo vimechukua hatua gani baada ya watotohao kupatikana kupelekwa kwenye vyombo vya utibabu ilikuangaliwa hali yao na wazee kuweza kujiridhisha? (Makofi)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili yanyongeza ya Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbungewa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katikamajibu yangu ya msingi kwamba, kupotea kwa watotohawa 184 kulitokana na sababu mbalimbali ambapo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
58
miongoni mwa sababu hizo ilikuwa ni mazingira magumuambayo wanaishi baadhi watoto, imani na kishirikina, visasi,kukosekana uangalifu wazazi/walezi na sababu nyingine nikupotea kwa bahati mbaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sababu hizi nitofauti na hatua ambazo zinachukuliwa zinategemea nasababu husika. Kwa zile sababu ambazo zimesababishwana njia ya uhalifu basi hatua mbalimbali zimeshachukuliwakwa mujibu wa sheria kwa watu ambao wamehusika naupotevu huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utakumbukuka juzi tukulikuwa na tukio la kijana mmoja ambaye amejihusisha nautekaji wa watoto na kuomba fedha, kijana yulealikamatwa na kwa bahati mbaya alipata majeraha naakafariki. Nikuhakikishie kwamba Serikali kupitia Jeshi la Polisiiko makini sana kuhakikisha kwamba inalinda watoto wanchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, ni kuhusu hatuaambazo watoto hawa wanachukuliwa. Kama ambavyonimesema kwamba kwa kuwa sababu ni tofauti kwa walewatoto ambao wamepatikana na madhara mbalimbali basinao vilevile hufikishwa katika mamlaka husika kwa ajili yakuweza kupata huduma mbalimbali ili kuwaweka katika halinzuri ya kimaisha na kiafya.
MWENYEKITI: Ahsante. Tunaendelea na swali letu lamwisho kwa leo. Swali Na.29 linaulizwa na Mheshimiwa JakuHashim Ayoub kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar nalinaelekezwa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti,kabla ya kuuliza swali, napenda nichukue fursa hii kwa dhatikabisa kumpongeza Kaimu Waziri Mkuu, Mheshimiwa Dkt.Mwakyembe, kwa juhudi na umakini wake katika shughulihizi. Nimwambie tu dalili ya mvua ni mawingu na nyota njemahuonekana asubuhi. (Makofi/Kicheko)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
59
Na. 29
Malipo Kuhusu Utaratibu wa Kuingiza Mafuta nchini
MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:-
Utaratibu wa kuingiza mafuta nchini unaosimamiwana Petroleum Bulk Procurement Agent (PBPA) kwa mfumowa Bulk Procurement System, wakala hukusanya mahitajikutoka kwa makampuni ya ndani na nje ya nchi lakinikampuni zote zikiweko zile zinazopeleka mafuta nje ya nchizinalipa Dola za Marekani tatu hadi nne kwa tani kwa mafutayanayopitia transit ya Dar es Salaam isipokuwa mafutayanayopelekwa Zanzibar ambayo hutozwa Dola za Marekani10 kwa tani.
(a) Je, ni utaratibu gani unaotumika kutoa nafuuya malipo ya Wharfage kwa kampuni za nje zinazopitishamafuta Dar es Salaam na kuitoza Zanzibar malipo makubwa?
(b) Mafuta yanayopitishwa transit ya Dar esSalaam kwenda Zanzibar yanalipiwa aina zote za ushuru, je,Serikali haioni kuwa inawabebesha wananchi gharamakubwa ya ununuzi wa mafuta kuliko nchi nyingine?
(c) Je, ni hatua gani Serikali inachukua katikakuhakikisha mafuta yanayopita transit ya Dar es Salaamyanalipwa kama mafuta mengine yanayopita transit yabandari hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NAMAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niabaya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, napenda kujibuswali la Mheshimiwa Jaku Hashimu Ayoub, lenye sehemu (a),(b) na (c), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu unaotumikakupanga tozo za bandari hautoi upendeleo kwa upande
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
60
wowote. Tozo hizo zimewekwa kwa kuzingatia gharamaza kutoa huduma, hali ya soko na umuhimu wa kuvutiashehena ya nchi jirani ili kutekeleza sera ya uchumi wakijiografia na kufanya bandari ya Dar es Salaam kuwa kitovuyaani hub ya usafirishaji. Ushindani wa shehena ya mafuta nimkali sana (cut throat competition) kwa bandari za TPAhususani Dar es Salaam na bandari za nchi jirani za Kenya,Msumbiji, Afrika Kusini, Namibia na Angola.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kutokana na haliya soko (market place exigencies), tozo za bandari kwashehena ya nchi ya jirani hutofautishwa na shehena ya ndaniya nchi ili kuvutia shehena nyingi kuhudumiwa na bandari yaDar es Salaam. Kwa hivi sasa gharama ya Wharfage kwashehena ya Tanzania ya kupakuliwa (imports) ni asilimia 1.6ya thamani ya mzigo ulioidhinishwa na TRA na kwa kiwangocha chini kilichowekwa cha Dola za Marekani 10 kwa tanimoja.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania Bara na Zanzibarni nchi moja na kwa hiyo shehena yoyote iendayo Zanzibarikiwa ni pamoja na shehena ya mafuta hutambuliwa kamani shehena ya nchini (local cargo) na sio shehena ya nchijirani yaani transit. Kwa mantiki hii, tozo zinazotumika ni tozoza shehena ya ndani (local cargo) ambayo ni sawa kwa Barana Zanzibar.
(c) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia majibuya (a) na (b) hapo juu ni dhahiri kwamba matumizi ya tozoni miongoni mwa mikakati maalum ya kibiashara na masokokwa ajili ya kuvutia shehena za nchi jirani ambazo huletafaida ya uchumi na kijamii hapa nchini (multiplier effect) siyotu kwa bandari bali kwa wadau wote wa bandari nawananchi kwa ujumla.
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Ayoub Jaku.
MHE. JAKU HASHIM AYUBU: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante sana. Kwanza mnyonge mnyongeni, nimpongezeMheshimiwa Naibu Waziri, kwa kitendo alichoonyesha
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
61
asubuhi hii leo cha uungwana na ungwana ni vitendo.Nikupongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa masikitikomakubwa, tena makubwa, tena makubwa kwa mara yatatu. Wizara yake anayoiongoza Mheshimiwa Waziri imekuwaikiwaonea wananchi wa Zanzibar, Unguja na Pemba. Nipotayari kumthibitishia hilo kwani mafuta yanayouzwa Zanzibarsasa hivi ni ghali kuliko hapa Dar es Salaam. Nimwombe tukwa unyenyekevu, ni lini atakaa na watu wa upande waZanzibar kutatua tatizo hili? Kama anavyojua mafuta ni nguzomuhimu. Mafuta Zanzibar yanauzwa ghali, kodi zimekuwanyingi na amekiri, nimpongeze kuwa Zanzibar wamechajiDola 10, wakaiacha Rwanda Dola tatu, Zambia Dola tatuBurundi Dola tatu, kwa nini wanaionea Zanzibar kwa Dola10? Mawaziri wengi husema Muungano huu wetu …
MWENYEKITI: Mheshimiwa uliza swali.
MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti,lazima ujenge hoja kwanza. Bila kujenga hoja hawezi kujakufahamu Mheshimiwa Naibu Waziri. Mheshimiwa NaibuWaziri, nimwombe ni lini atakaa na upande wa Zanzibarmaana kuna barua mpaka leo Katibu wake Mkuu hajawajibuWazanzibari, je, kalamu ya kuandikia hana au anaandikaspelling moja moja? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni uonevu, mafuta Zanzibaryanauzwa ghali, sisi tunaumia. Mafuta ni nguzo muhimu …
MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu ni liniutaketi na wafanyabiashara wa Zanzibar kuzungumzia sualahili?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NAMAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ahsante sana.Kwanza nikiri kweli kwamba kuna changamoto katika hizitozo ambazo zinatozwa na bandari, lakini nimhakikishieMheshimiwa Jaku kwamba tupo tayari kama Wizara kwakushirikiana na Wizara ya Uchukuzi ya Zanzibar lakini vilevile
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
62
na Mamlaka ya Mapato kukaa na kuangalia hizi tozoambazo ni kero sana kwa wananchi wetu wa Tanzania,tuweze kuzitatua kwa pamoja. Katika hilo, nitamkaribishaMheshimiwa Jaku tukae pamoja tulijadili kwa kina tuliondoetatizo hilo ambalo linasumbua wananchi kwa njia moja aunyingine. Hili linatatulika kwa mustakabali wa nchi yetu yaTanzania. Ahsante.
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, hapa ndiyotumefika mwisho wa kipindi cha maswali, mliona nimeminyasana lakini mnaelewa mimi siwezi kuwafundisha utaratibuwa kulinda muda. Tunarembaremba mno maswali,tunarembaremba mno majibu. Nenda straight swali lako najibu straight, Watanzania hawa wanataka wayasikie kwakifupi tu. Tumechukua muda zaidi ya nusu saa, tunaendelea.
Waheshimiwa Wabunge, wageni wetu waliopo leohapa Bungeni, naanza na wagei waliopo Jukwaa la Spika.Tunao wageni 46 wa Mheshimiwa Jenista Mhagama, Waziriwa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajirana Wenye Ulemavu) ambao ni viongozi kutoka Ofisi ya WaziriMkuu wakiongozwa na Katibu Mkuu Ndugu Eric Shitindi.Karibuni sana Katibu Mkuu na timu yako. Nafahamu tunaMuswada muhimu sana leo. (Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, tunao pia Wajumbe nawadau kutoka Shirika la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA)wakiongozwa na Rais wa Shirikisho hilo Ndugu PeterNyamhokya. Karibu sana Mheshimiwa na timu yako. (Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, tunao pia Wakuu wa Mifukoya Hifadhi ya Jamii, kwa umoja wenu simameni tuwaone.Karibuni sana. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
63
Waheshimiwa Wabunge, tunaye pia MwakilishiMkaazi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO). Karibuni sana. (Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, kundi la pili ni wageni waWaheshimiwa Wabunge. Kuna wageni watano waMheshimiwa Lathifah Chande kutoka Liwale Mkoa wa Lindi.(Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, tunao wageni watatu waMheshimiwa Venance Mwamoto ambao ni marafiki zakekutoka Kilolo, Mkoa wa Iringa pamoja na wageni wenginekutoka nchi ya Uholanzi - Netherlands. Karibuni sana. (Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, wageni wengine ni walewaliotembelea Bunge letu kwa ajili ya mafunzo. Tunaowanafunzi 16 kutoka Chuo cha Habari Maalum kilichokoMkoa wa Arusha. Karibuni sana kwenye mafunzo yetu.(Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, tunao pia Walimu wannena wanafunzi 49 wa Mafunzo ya Usanifu wa Majengo kutokaChuo Kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Uhandisi wa Miundona Ujenzi, Kitivo cha Uhandisi na Teknolojia. Ahsanteni sana,karibuni sana, muone shughuli zetu za Bunge. (Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, nina tangazo lingine, kwaniaba ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Mtakatifu Thomas Moore,Mheshimiwa Shally Raymond, anawatangazia WaheshimiwaWabunge Wakristo Wakatoliki, leo tarehe 31 Januari, 2018kutakuwa na Ibada ya Misa mara baada ya kuahirishwa kwaBunge saa 7.00 mchana katika Kanisa dogo lililopo ghorofaya pili, ukumbi wa Msekwa. Waheshimiwa Wabunge wenginewote mnakaribishwa kushiriki Ibada hii Takatifu.
Hayo ndiyo matangazo niliyonayo hapa mezani.Baada ya hapo…
MWONGOZO WA SPIKA
WABUNGE FULANI: Mwongozo.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
64
MWENYEKITI: Mniruhusu nikae basi.
WABUNGE FULANI: Kaa tu Mheshimiwa.
MWENYEKITI: Kwa sababu ya muda nitachukuawachache, Mheshimiwa Masoud, Mheshimiwa Waitara naMheshimiwa Paresso.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Nina hoja ya msingisana.
MWENYEKITI: Tuanze na Mheshimiwa Masoud.
MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: MheshimiwaMwenyekiti, nakushukuru. Naomba mwongozo wako kwakutumia Kanuni ya 68(7) juu ya jambo lililotokea Bungenimapema sambamba na Kanuni ya 46(1) maswali kutojibiwakikamilifu sambamba na Kanuni ya 64(1) kuhusu mamboyasiyoruhusiwa Bungeni na (a) inasema hakuna kutoa taarifaza uongo Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeanza na taarifa hizikutaka mwongozo wako juu ya swali la nyongeza laMheshimiwa Paresso wakati Mheshimiwa Naibu Waziri,TAMISEMI, Mheshimiwa Joseph Kakunda akijibu kwambahakuna hata Mkuu wa Mkoa mmoja aliyemsimamishaMwenyekiti wa Mtaa au na ngazi nyingine katika maeneombalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mwongozo wakokwa kuwa watu hawa wapo wengi sana hata hapaDodoma, tarehe 1 Aprili, 2017, Mwenyekiti wa Mtaa waMlimwa Kusini alisimamishwa na aliyekuwa Mkuu wa Wilayawakati huo. Hii orodha ya watu wa aina hii ni kubwa ambapoMheshimiwa Joseph Kakunda ama amelidanganya Bungeau amedanganywa na wataalam wake. Naombamwongozo wako juu ya jambo hili ambalo limetokea leomapema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
65
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Waitara.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru. Naomba Mwongozo wako kwa mujibu waKanuni ya 68(7).
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati swali Na.19 linajibiwana Mheshimiwa Mwakajoka anapata majibu ya swali lakela nyongeza alionesha kwamba katika Wilaya yake kunashule ambazo hazijafunguliwa kwa sababu shughuli zaMadiwani zimesitishwa na Naibu Waziri akasema kwambahicho kitu siyo kweli na akarudia mara tatu anakataa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba niwekemambo sawa kwamba Naibu Waziri jibu lake halikuwa sahihikwa sababu hilo jambo limetokea Tunduma lakini jambo hilohilo nimemwona kwenye Televisheni Mkuu wa Mkoa waManyara, Bwana Mnyeti akimsimamisha Mwenyekiti wa Mtaaambaye pia ni Mheshimiwa Diwani, anamlazimisha ajiudhurunafasi moja hapa hapa lakini vilevile imefanyika Shinyanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mkuu waManyara, Bwana Mnyeti, ambaye kumbukumbu zinaoneshaamewahi kuitwa na Bunge hili kuja kwenye Kamati ya Maadilikwa kudharau Bunge, lakini juzi tulimwona kwenye clipmbalimbali akitoa maelekezo kwa Mheshimiwa Mbunge waKiteto, akimweleza kwamba wewe ukija kwenye Kijiji Busizungumze mambo ya Kijiji B. Anasema Mkuu wa Wilayaana masikio makubwa kuliko mtu mwingine katika Wilayaile na Mbunge akisema jambo lolote anatakiwa awajibishwemara moja na kama atashindwa yeye ataingilia kati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningeomba Bungehili litoe kauli, matendo haya ambayo yanafanyika kwaWateule ambao wanateuliwa na Mheshimiwa Rais,wakidhalilisha Mhimili wa Bunge, wao wapo juu ya sheria?Katiba imetoa mgawanyiko wa madaraka, kwamba kunakazi za Serikali, kuna kazi za Bunge na kuna kazi zaMahakama. Hata hivyo, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
66
Wilaya anafika mahali anamwambia kuanzia sasa sioMtumishi wa Umma na hilo jambo limerudiwa mara kwamara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mwongozo waBunge hili ili tufuate utaratibu, tufuate sheria na Katiba ili kilamtu afanye kazi katika mazingira na mipaka ya kazi yakekwa mujibu wa sheria.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naminaomba mwongozo wako, kwa suala hili ambalo lipo mbeleyetu ambalo Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwambahakuna Wakuu wa Mikoa wa ambao wameweza kufanyakitendo hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkuu wa Mkoa wa ManyaraMheshimiwa Mnyeti, amewavua nafasi zao za Ukuu wa Shulena kuwasimamisha kwa madai kwamba hawajatimizawajibu wao Walimu Wakuu katika Shule za Simanjiro, Kitetona Babati Vijijini. Hivi karibuni, Mheshimiwa Rais wa Jamhuriwa Muungano wa Tanzania alitoa kauli katika vyombo vyahabari kwamba michango mashuleni sio lazima, vyakulamashuleni sio lazima na kwa hali ya kawaida Wakuu hawawa Shule wanaovuliwa nafasi zao sio kwamba waowanasababisha watoto wafeli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe mwongozo wako,ni kwa nini Serikali inatudanganya kwamba hakuna Wakuuwa Wilaya na Wakuu wa Mikoa ambao wanawasimamishakazi watumishi wakati hali hiyo ikiendelea hususan katikaMkoa wa Manyara? Naomba mwongozo wako. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsanteni.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
67
Waheshimiwa Wabunge, Kanuni ya 68(7) ya kuombeamwongozo sote tunaifahamu, kuhusu jambo lililotokeaBungeni mapema ili Spika atoe ufafanuzi kama jambo hilolinaruhusiwa au haliruhusiwi na Kanuni hizi. Hiyo ndiyo Kanuniambayo imeombewa mwongozo. Nijumuishe, inaonekanahaya yametokana na jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri.(Makofi)
Twende vizuri tu Waheshimiwa Wabunge, kwanzakuna uamuzi wa Spika kuhusiana na majibu ya nyongezakutokidhi kile kiwango ambacho Mbunge anaona kwambahakikufikiwa. Hasa uamuzi wa Spika ni kwamba anayewezakulalamika kwamba swali lake halikujibiwa kikamilifu, nimwenye swali na aliyeuliza maswali ya nyongeza kwa swalihilo na sio mwingine. Wale tunaouliza maswali ya nyongezahuwezi ukasema yale majibu aliyopewa muuliza swalihayajitoshelezi. Kwa hiyo, Waheshimiwa hilo tuelewanekabisa.
MJUMBE FULANI: Ulinipa nafasi.
MWENYEKITI: Mheshimiwa, wewe hukuwa mwenyeswali la msingi kama unadhani yaliyosemwa humu Bungenina Serikali hayatoshelezi, wewe uliza swali lako litajibiwa naSerikali. (Makofi)
(Hapa baadhi wa Waheshimiwa Wabungewalikuwa wakiongea bila mpangilio)
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, ndiyo maanalazima Kanuni hizi tuendelee kuzisimamia sisi wenyewe. Yotehaya Mheshimiwa Masoud, Mheshimiwa Waitara naMheshimiwa mliojigeuza, mimi nimemuita Paressomkajigeuza, mkakaribishana tu, nimevumilia tu hayo yote,lakini nayakubali tu kwamba na ninyi mna haki ya kuyasemahaya lakini mimi nawanyoosha kwenye mstari wa Kanuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, huo ndiyomwongozo wangu, tumekaa vizuri na suala hilo. Sasatunaendelea, Katibu.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
68
NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI:
MISWADA YA SHERIA YA SERIKALI
Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwaWatumishi wa Umma kwa Mwaka 2017
(The Public Service Social Security Fund Bill 2017)
(Kusomwa Mara ya Pili)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi yaWaziri Mkuu, karibu uwasilishe Muswada, Karibu sana.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE,KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU): MheshimiwaMwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni ya 86(2) ya Kanuni zaKudumu za Bunge, Toleo la Mwaka 2016, naomba kutoa hojakwamba Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamiikwa Watumishi wa Umma wa Mwaka 2018 (The Public ServiceSocial Security Fund Act, 2018) kama ulivyochapishwa upyasasa usomwe Mara ya Pili na Bunge lako Tukufu lijadili nahatimaye lipitishe Muswada huu kuwa sehemu ya sheria zanchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kutoa maelezokuhusu Muswada huu, naomba nianze kwa kumshukuruMwenyezi Mungu kwa kutujalia uzima na afya njema nakutuwezesha kuendelea kutekeleza majukumu yetu ndani nanje ya Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana wewemwenyewe binafsi kwa kunipa nafasi ya kuwasilishaMuswada huu mbele ya Bunge lako Tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ni Mkutano waKwanza tangu mwaka huu uanze, naomba nikutakie weweMheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Spika na Wenyevitiwengine wa Bunge pamoja na Mheshimiwa Naibu Spika naWabunge wengine wote kheri ya mwaka mpya wa 2018.(Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
69
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, naomba nichukuenafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Doto Biteko, kwakuteuliwa na kuaminiwa na Rais kuwa Naibu Waziri waWizara ya Madini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naombaniwapongeze Waheshimiwa Wabunge wapya, MheshimiwaDkt. Damas Ndumbaro, Mbunge wa Songea Mjini;Mheshimiwa Justin Monko, Mbunge wa Jimbo la SingidaKaskazini; na Mheshimiwa Dkt. Stephen Kiluswa, Mbunge waJimbo la Longido kwa kuchaguliwa na wananchi waMajimbo yao na kisha kuapishwa kuwa Wabunge wa Bungehili. Nawatakia utendaji mwema katika kutekelezamajukumu yao ya Kibunge ndani na nje ya Bunge hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi yapekee kumshukuru sana Dkt. John Pombe Magufuli, Rais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miongozoanayoendelea kutupatia ambayo imetuwezesha kufanikishauandaaji wa Muswada ambao uko mbele yako leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sanaMheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu waJamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maelekezo yakeyaliyotuwezesha kufanikisha kuandaa Muswada huu. Aidha,nawashukuru sana Waheshimiwa Naibu Mawaziri wanguMheshimiwa Anthony Peter Mavunde na Mheshimiwa StellaIkupa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Ndugu EricShitindi na watendaji wengine wote toka Ofisi ya Waziri Mkuukwa msaada mkubwa waliotupatia katika maandalizi yaMuswada huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kutambua kazikubwa iliyofanywa na Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti waSekta ya Hifadhi ya Jamii kuanzia hatua ya utafiti zilizopelekeakufikia hatua hii ya leo. Nawashukuru sana SSRA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa namna ya pekee,nawashukuru sana Viongozi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamiina naomba kwa hisani yako niwataje kwa majina viongozi
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
70
Watendaji Wakuu wa Mifuko hiyo, Mheshimiwa Sanga,Mheshimiwa Eriyo, Profesa Kiharara, Mheshimiwa Msangi naNdugu yetu Adam. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile natoa shukrani zadhati kwa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA)wakiongozwa na Rais wa Shirikisho hilo Ndugu yangu TumainiNyamhokya kwa kazi nzuri waliyoifanya katika kupelekeakufanikiwa kwa kuwepo kwa Muswada huu. Aidha, nashukurusana Chama cha Waajiri Tanzania (ACTE) kikiongozwa namama yetu mpendwa Mama Janeth Nyimbo kwa kufanyakazi nzuri ya kutoa ushauri katika kufanikisha Muswada huu.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho lakini sio kwaumuhimu, nilishukuru sana Shirika la Kazi Duniani kwaushirikiano mkubwa walionyesha katika hatua zote zamajadiliano ya hoja na mpaka kutufikishia kuweza kuletaMuswada wa kuunganisha Mifuko na hatimaye Muswada huukuingia katika Bunge lako. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikupongeze tenakwa mara nyingine, lakini nimpongeze pia Spika wa Bungeletu, Naibu Spika na Wenyeviti Wabunge kwa jinsimnavyoendelea kutekeleza majukumu ya Bunge kwa ufanisimkubwa. Aidha, namshukuru sana kaka yangu GeorgeMasaju, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Ndugu GersonMdemu, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na watumishiwote wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ushaurina ushirikiano wao waliotupatia wakati wa uandaaji waMuswada. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa dhati pianimshukuru sana Mheshimiwa Profesa Kabudi, Waziri waKatiba na Sheria kwa kazi kubwa aliyoifanya katikakusimamia shughuli za maandalizi ya Muswada huu ndaniSerikali, lakini tulishirikiana pamoja na Mheshimiwa Dkt.Harrison Mwakyembe na Ndugu yangu George Mkuchika,wote kwa pamoja Mawaziri hawa tulifanya nao kazi usiku
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
71
na mchana na hatimaye kazi hii leo imeweza kuja mbele yaBunge lako Tukufu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa namna ya pekee,naishukuru sana Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma naMaendeleo ya Jamii chini ya uongozi mahiri wa Mwenyekitiwa Kamati hiyo Mheshimiwa Peter Joseph Serukamba,Mbunge wa Kigoma Kaskazini, akisaidiwa na MheshimiwaAzzan Zungu, Mbunge wa Jimbo la Ilala ambaye ni MakamuMwenyekiti wa Kamati pamoja na Wajumbe wote wa Kamatihiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli wametupaushirikiano na ambao umetupelekea kuchambua na kupitiaMuswada huu na hatimaye tarehe 22 Januari, Kamatiilikamilisha kupitia na kuchambua Muswada wa Sheria waHifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma na kuridhiaMuswada huu uendelee kwa hatua ya kusoma Mara ya Pilina ya Tatu katika Mkutano huu wa Bunge. Hakika ushauri,maoni na mapendekezo ya Kamati yametusaidia sana sanakuboresha Muswada kupitia marekebisho ambayoyamefanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kilichofanywa na Mwenyekitiwa Kamati hii na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bungeya Huduma na Maendeleo ya Jamii katika Muswada huu nijambo la kihistoria. Kwa dhati kwa niaba ya Serikalitutaheshimu sana kazi nzuri iliyofanywa na Kamati hii. Hii nikutokana na namna Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamatiwalivyoungana na kujitoa kwa pamoja bila kujali itikadi zaokatika kuchambua, kurekebisha na kuboresha Muswada huuili kuhakikisha kwamba unakidhi lengo lililokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maboresho makubwayaliyofanywa na Kamati yamepelekea kupokea maagizo yaKamati na Muswada huu kuchapwa upya ili kujumuishamaboresho yote na hivyo kuleta urahisi wa usomaji waMuswada wenyewe. Mwenyezi Mungu awabariki sana kwakazi hii nzuri mliyoifanya. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
72
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa kuwatunamaliza sasa mwaka wa mwisho wa utendaji wa Kamatiza Kudumu za Bunge, naomba nichukue nafasi hiikuzipongeza na kuzishukuru Kamati za Kudumu za Bunge zotekwa ushirikiano mkubwa waliotuonesha ndani ya Ofisi yaWaziri Mkuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nafasi ya pekee,nawashukuru sana Wenyeviti na Makamu Wenyeviti waKamati zifuatazo za Bunge ambao tulifanya nao kazi katikakipindi hiki cha awamu ya kwanza ya Kamati za Kudumu zaBunge ndani ya Bunge lako Tukufu. Kamati ya Katiba na Sheriana Kamati ya UKIMWI lakini vilevile Kamati yako ya SheriaNdogo. Hakika walitupa ushirikiano mkubwa na walioneshakwamba wanajali na kuhitaji kuboresha utendaji wa Serikalikwa ujumla kwa manufaa ya nchi yetu yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nitakwenda kwenyemadhumuni ya Muswada. Muswada uliopo mbele yakounapendekezwa kutungwa kwa Sheria ya Mfuko wa Hifadhiya Jamii kwa Watumishi wa Umma wa mwaka 2018. Sheriahii inapendekeza kuunganisha Mifuko ya Pension ya PSPF, LAPF,GEPF na PPF na kuanzisha mfuko mmoja wa hifadhi ya jamiimahsusi kwa ajili ya Watumishi wa Umma kote nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na kuanzishamfuko mpya, sheria inayopendekezwa inafanya marekebishomakubwa (consequential amendment) kwenye Sheria yaMfuko wa Taifa ya Hifadhi ya Jamii (NSSF) ili kuufanya Mfukohuo kuwahudumia wafanyakazi wa sekta binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Muswada huu piaunapendekeza kufuta sheria zinazoanzisha Mifuko ya Pensheniambayo ni Sheria ya Mafao ya Pensheni kwa Watumishi waUmma (PSPF), Sheria ya Mafao ya Pensheni kwa Watumishiwa Serikali za Mitaa (LAPF), Sheria ya Mafao ya Pensheni kwaMashirika ya Umma (PPF) na Sheria ya Mafao ya Kustaafu(GEPF). Aidha, Sheria ya SSRA pia itarekebishwa ili kuendanana mabadiliko haya.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
73
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya kuunganisha Mifukoya Pensheni inalenga kukidhi kilio cha muda mrefu chawafanyakazi kuhusu kuunganisha Mifuko hiyo ili kupunguzagharama za uendeshaji, kuondokana na ushindani usio natija baina ya Mifuko ya Pensheni ambayo kimsingi inatoamafao yanayofanana na hatimaye kuboresha mafao yawanachama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chimbuko la hoja yakuunganisha Mifuko ya Pensheni nchini ni madai ya mudamrefu ya wadau mbalimbali wa sekta ya hifadhi ya jamii,hasa wafanyakazi ambao katika nyakati tofauti kupitiavyama vyao waliomba na kuishauri Serikali kuunganishaMifuko hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi cha miakaminne mfululizo kuanzia mwaka 2014, 2015, 2016 na 2017,Shirikisho la Vyama Nchini (TUCTA) wakati wa Maadhimishoya Siku ya Wafanyakazi Duniani na katika vikao baina yaona Serikali wamekuwa wakiomba Serikali kuunganisha Mifukoya Pensheni i l i kuondoa changamoto mbalimbalizinazotokana na uwepo wa Mifuko mingi ya Pensheniinayotoa mafao yanayofanana na kupunguza gharama zauendeshaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, mwaka 2016katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani katikarisala yao TUCTA waliwasilisha kwa Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John PombeMagufuli ombi lao la kuunganisha Mifuko ya Pensheni nchini.Mheshimiwa Rais alikubali ombi hilo na kuiagiza Ofisi ya WaziriMkuu kuharakisha mchakato wa kuunganisha Mifuko hiyo.Hatua hii pia inakwenda sambamba na mapendekezo yaILO ambayo kupitia tathmini ilishauri Mifuko ya Pensheni nchiniiuanganishwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuitikia kilio chamaombi ya wadau wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii hatua yakuunganisha Mifuko hii pia ni sehemu ya utekelezaji wa Ibara
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
74
174 ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka2015 inayoielekeza Serikali kuimarisha Sekta ya Hifadhi ya Jamiikwa manufaa ya Watanzania wote kwa ujumla na hasawafanyakazi wanaostaafu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuunganisha Mifukokutasaidia kupunguza gharama za uendeshaji kutokaviwango vya asilimia 19 mpaka asilimia tisa iliyowekwa naMdhibiti wa Sekta; kuondoa gharama za ushindani usiokuwana tija; kupunguza migogoro baina ya Mifuko; kuboreshamafao ya wanachama ikiwemo kuongeza mafao mapyayaliyokuwa yakihitajika sana miongoni mwa wanachama;kuongeza tija katika sekta ya hifadhi ya jamii na kukuzauchumi wa nchi kwa ujumla. Aidha, hatua ya kuunganishaMifuko itasaidia kuimarisha uwiano wa idadi ya wanachamawachangiaji na wastaafu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya sheria hiiinayopendekezwa uwiano ya idadi ya wanachamawachangiaji na wastaafu ilikuwa wastani wa 1:5 kwa Mfukoambao ulikuwa chini kabisa. Baada ya kupitishwa kwa sheriahii inayopendekezwa na Bunge lako Tukufu tunatarajiauwiano wa idadi ya wanachama wachangiaji na wastaafuitaendelea kuongezeka kufikia kiwango cha kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kidogo mambomuhimu yaliyozingatiwa katika Muswada huu. Kabla yakueleza mpangilio wa Muswada huu, naomba uniruhusunibainishe kwa ujumla mambo muhimu ambayoyamezingatiwa katika Muswada wetu mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inayopendekezwakwa sasa inaweka mfumo madhubuti utakaomhakikishiamwanachama kulipa mafao ya msingi kama inavyoelekezwana Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977,Ibara ya 11(1) nitanukuu:-
“Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu unaofaa kwaajili ya kufanikisha utekelezaji wa haki ya mtu kufanya kazi na
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
75
kupata msaada wa jamii wakati wa uzee, wakati wa maradhiau hali ya ulemavu na katika hali nyingine za mtu kuwahajiwezi”. Mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inayopendekezwainabainisha kwa uwazi jumla ya mafao saba yatakayolipwana Mfuko huu, mafao hayo ni pamoja na:-
(i) Fao la Pensheni;
(ii) Fao la warithi;
(iii) Fao la ulemavu;
(iv) Fao la uzazi;
(v) Fao la ukosefu wa ajira;
(vi) Fao la ugonjwa; na
(vii) Fao la kufiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inaweka utaratibubora na ulio rahisi wa wanachama wa mifukoinayounganishwa kuhamia kwenye mfuko mpya pasipokuathiri mafao yao na uendelevu wa Mfuko mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, sheria inapendekezakutumia utaratibu wa cut-off date ambapo wanachama waumma waliopo NSSF na wanachama waliopo katika sektabinafsi ambao kwa sasa wanachangia kwenye mifukoinayounganishwa hawatahamishwa na badala yakeutaratibu mpya wa mifuko miwili utaanza kwa wanachamawatakaoajiriwa baada ya sheria mpya kuanza kutumika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inaweka bayanakwamba mafao na michango ya wanachama haitatozwakodi kama ilivyokwishabainishwa hata katika sheria nyingineza kodi. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
76
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inaainisha viwangovya uchangiaji na namna ya uchangiaji katika Mfuko mpyaambapo viwango vya uchangiaji itakuwa ni asilimia 20,mwajiri atachangia asilimia 15 na mwajiriwa atachangiaasilimia tano (5) tu ya mshahara wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inaweka mfumomadhubuti utakaohakikisha mwanachama anapata mafaokwa wakati kama ifuatavyo:-
Itautaka Mfuko kumlipa mwanachama aliyekidhivigezo mafao yake hata kama mwajiri hajawasilishamichango na baadaye Mfuko utafuatilia michango ambayohaijawasilishwa kutoka kwa mwajiri. Hii inatokana na ukwelikwamba jukumu la kufuatilia michango siyo jukumu lamwanachama. Wakati ukifika mwanachama alipwemichango yake hata kama mwajiri hajafuatilia michangoyake kunakohusika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inaweka adhabu yatozo ya asilimia tano (5) kwa Mfuko utakapocheleweshamafao ya mwanachama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inaweka mfumo rahisina mfupi wa mashauri ya madai ya michango Mahakamani,ambapo mwajiri aliyeshtakiwa kwa kutowasilisha michangoya mwanachama, hatakuwa na fursa ya moja kwa moja yakujitetea Mahakamani mpaka atakapowasilisha dhamanaya fedha taslimu sawa na kiasi cha michango yamwanachama anayodaiwa na mwanachama huyo.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii itamwezeshamwanachama kutumia mafao yake kujipatia mikopo yanyumba na shughuli nyingine za kiuchumi kwa riba nafuu.Hatua hii itawasaidia wanachama kujiandaa na maishakabla ya kustaafu. Baada ya sheria hii kupita, Ofisi yanguitaandaa utaratibu ambapo mikopo itakayotolewa,itatolewa na benki ambayo Mifuko itakuwa na hisa na
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
77
mikopo hiyo kwa wafanyakazi hao ambao ni wanachamaitakuwa ni mikopo yenye riba nafuu il i kuhakikishawanachama hawapati tena shida ya kujiandaa na maishakabla ya kustaafu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii inaainisha kwauwazi haki na stahili za warithi pale mwanachama aumstaafu anapofariki. Masharti katika eneo hili yanalengakuondoa changamoto mbalimbali zinazotokana na sheriaza sasa za Mifuko kutokuwa wazi katika eneo la haki na stahiliza warithi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inayopendekezwainaondoa kilio cha muda mrefu cha wastaafu katika utumishiwa umma kuhusu kukoma kwa mafao ama pensheni palemstaafu anapofariki dunia. Sheria inayopendekezwaitaruhusu wategemezi kuendelea kupokea mafao kwa kipindicha miezi 36 baada ya mstaafu kufariki dunia. Tofauti na ilivyosasa ambapo mwanachama akifariki tu, malipo hukomamara moja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inapendekezakuboresha masharti kuhusu fao la uzazi ambapo pamoja nakupata fedha taslim baada ya kujifungua, mwanachamapia atapata huduma ya matibabu kabla na baada yakujifungua endapo huduma hizo hazilipwi na Mfuko wa Taifawa Bima Afya, Aidha, mwanachama atakuwa na fursa yakupata fao hilo mara nne katika kipindi chake chote chaajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria inayopendekezwaitaanzisha fao la upotevu wa ajira ili kuondoa changamotoya muda mrefu ya wanachama kujitoa kwenye Mifuko yaHifadhi ya Jamii. Fao hili litatolewa kwa wanachamawaliopoteza ajira baada ya kukidhi vigezo vilivyoainishwandani ya sheria. Vigezo hivyo ni pamoja na hivinitakavyovisoma:-
- Mwanachama awe amechangia kwa kipindikisichopungua miezi kumi na nane;
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
78
- Awe ni Mtanzania; awe hajaacha kazi kwamatakwa yake mwenyewe;
- Mwanachama huyo awe hajafikia umri wakupata pensheni au kiinua mgongo au mafao mengine yamuda mrefu;
- Awe ametoa uthibitisho kwa Mkurugenzi Mkuukuwa hajaweza kupata kazi nyingine na awe hajafikisha umriwa miaka 55.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii inaongeza wigo wawanachama wa Mfuko mpya kwa kuwatambuawafanyakazi wote waliopo kwenye mashirika ambayo Serikaliina hisa kuwa wanachama wa Mfuko huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria pia inaanisha muundowa Bodi ya Wadhamini ili kuzingatia uwakilishi wa waajiri nawafanyakazi. Sheria hii pia inaboresha masharti kuhusu mafaoya Majaji na Viongozi wengine Waandamizi wa Serikaliambao wanashika nafasi za kikatiba kwa kutenganishamafao yao ya pensheni na stahili nyingine wanazopatawakati wa kustaafu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la maboresho hayani kuhakikisha sheria inayopendekezwa inajikita kwenyemasuala ya pensheni tu stahili nyingine za viongozi hawazitahamishiwa kwenye sheria zao za utumishi. Hatua hiiinalenga kuondoa uwezekano wa fedha za Mfuko kutumikakulipa stahili zisizohusiana na mafao ya pensheni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii inatoa fursa kwamwanachama anayetumikia kifungo jela kushirikishwa juuya namna bora ya mafao yake yatakavyotumika ikiwa nipamoja na kutunza familia yake akiwa anaendeleakutumikia kifungo kwa kuiandikia Bodi ya Mfuko na Bodiitafanyia maamuzi kuzingatia taarifa ya mfungwa husika.Sheria hii pia imeainisha kipindi cha mpito na mambo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
79
yanayopaswa kusimamiwa na kutekelezwa katika kipindihicho cha mpito ni kama haya yafuatayo:-
- Kutambua na kulinda haki, stahili na mafaoya wanachama wa Mifuko inayounganishwa na kuhakikishakwamba yanahamishiwa kwenye Mfuko mpya kwa usalama;
- Kutambua na kusimamia uhamishaji warasilimali na miradi ya Mifuko inayounganishwa;
- Kutambua na kulinda haki za wanachamakatika Mifuko ya hiari inayoendeshwa na Mifukoinayounganishwa;
- Kuandaa muundo mpya wa Mfuko mpyaikiwa ni pamoja na kuweka mfumo utakaosimamia usalamawa ajira za watumishi wa Mifuko inayounganishwa;
- Kufanya marekebisho katika Sheria ya NSSF ilikuwezesha Mfuko huu kuhudumia wafanyakazi wote waliokokatika sekta binafsi. Aidha, kwa mujibu wa sheriainayopendekezwa, Mfuko wa NSSF utatoa hifadhi ya jamiikwa sekta isiyo rasmi (informal sector).
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii inalenga kuimarishamfumo wa usimamizi na udhibiti wa sekta ili kuiwezeshaMamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA)kuendelea kusimamia Sekta ya Hifadhi ya Jamii katikakuhakikisha kwamba mabadiliko hayataathiri kwa namnayoyote ile haki na maslahi ya wanachama na wastaafu.Vilevile kuhakikisha ushiriki wa sekta katika miradi iliyopo nailiyopangwa kufanywa haiathiriwi na mabadiliko haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kufanikisha lengo hili,sheria inapendekeza kufanya marekebisho Sheria yaMsimamizi na Mdhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii ili pamojana mambo mengine kuipa nguvu ya kisheria miongozombalimbali inayotolewa na Mamlaka hiyo kwa kuitakakutangazwa katika Gazeti la Serikali ili iweze kutambulikarasmi kama sehemu ya Sheria Ndogo za nchi yetu ya Tanzania.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
80
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nitakwenda kwenyempangilio wa Muswada. Sheria hii inayopendekezwaimegawanyika katika sehemu kuu kumi na moja. Sehemu yaKwanza, inaweka masharti ya utangulizi yakiwemo jina lasheria inayopendekezwa, matumizi yake na tafsiri ya manenoyaliyotumika katika sheria inayopendekezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Pili inapendekezamasharti yanayoanzisha mpango wa hifadhi ya jamii kwawatumishi wa umma wenye lengo la kutoa mafaombalimbali ya hifadhi ya jamii kwa watumishi wa umma.Sehemu hii pia inaainisha wanachama na masharti yauanachama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Tatuinapendekeza kuanzishwa kwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamiikwa Watumishi wa Umma kwa madhumuni ya kutoa mafaoya hifadhi ya jamii kwa watumishi wa umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Nneinapendekeza masharti kuhusu usimamizi na uangalizi waMfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa umma. Sehemuhii inaanzisha Bodi ya Wadhamini ya Mfuko na kuainishamajukumu na mamlaka ya Bodi hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, sehemu hii inawekamasharti kuhusu uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko nautaratibu wa ajira kwa watumishi wengine wa Mfuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Tano inawekamasharti kuhusu usajili wa wanachama, kiwango chamichango ya kila mwezi na utaratibu wa uwasilishaji wamichango kwenye Mfuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chini ya sehemu hii, Muswadaunapendekeza masharti kuhusu usajili na utunzaji wa taarifana kumbukumbu za wanachama, usajili wa wanachama,kiwango na utaratibu wa uchangiaji, usalama wa michangona masharti mengine yanayofanana na hayo.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
81
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Sita ya Muswadainaainisha masuala yanayohusiana na mafaoyatakayotolewa na Mfuko wa Watumishi wa Umma. Kwamadhumuni hayo, Muswada unaainisha kwa kina mashartikuhusu umri wa kustaafu na masharti ya sifa za kupatapensheni kwa wanachama na wategemezi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa masharti yasehemu hii mafao yanayopendekezwa kutolewa chini yasheria mpya ni pamoja na mafao ya pensheni, ulemavuusiotokana na kazi, warithi kwa kuboresha muda na utaratibuwa kutoa fao hilo, fao la uzazi, fao la upotevu wa ajira nafao la ugonjwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Saba yaMuswada inaweka masharti kuhusu fedha. Sehemu hiiinapendekeza masharti kuhusu vyanzo vya mapato vyaMfuko, bajeti ya mwaka, hesabu za Mfuko na ukaguzi wahesabu. Masharti kuhusu tathmini na uwekezaji wa fedha zaMfuko pia yameainishwa katika sehemu hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Nane inawekamasharti kuhusu mashauri ya kisheria pamoja na makosa naadhabu mbalimbali. Chini ya sehemu hii, Muswada unawekamasharti kuhusu urejeshwaji wa michango ambayohaijalipwa, vipaumbele vya malipo ya michango, wajibu wawajumbe na masuala yanayohusu kesi dhidi ya Bodi yaWadhamini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Tisa inahusumasharti ya jumla yakiwemo ujumuishwaji wa vipindi vyauchangiaji, kulinda maslahi ya wanachama na watumishi,ukaguzi na mamlaka ya Waziri kutengeneza Kanuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Kumi inawekamasharti ya mpito na ufutwaji wa sheria mbalimbali. Sehemuhii inaweka masharti yanayotambua mikataba na mashaurimbalimbali dhidi ya Mifuko inayounganishwa kuwayatahamishiwa katika Mfuko mpya. Aidha, sehemu hii piainaweka masharti yanayolenga kulinda maslahi ya
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
82
wanachama, wastaafu, warithi wa Mifuko inayounganishwayasiathiriwe wakati wa kuunganisha Mifuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sehemu ya Kumi na Mojainaweka masharti kuhusu marekebisho yatokanayo(consequential amendment). Katika sehemu hii, sheriambalimbali zinapendekezwa kufanyiwa marekebisho. Sheriahizi ni:-
(i) Sheria ya Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta yaHifadhi ya Jamii;
(ii) Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii;Sheria ya Utumishi wa Umma;
(iii) Sheria ya Tume ya Utumishi wa Polisi naMagereza na Sheria ya Mafao ya Hitimisho la Marupurupu yaMajaji.
Lengo la marekebisho katika sheria hizi ni kutambuana kuhamishia katika sheria hizo stahili za baadhi ya viongoziambao hulipwa sambamba na mafao ya uzeeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hitimisho. Baada ya maelezohaya, naomba sasa Bunge lako Tukufu liujadili Muswada huuwa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi waUmma wa mwaka 2018 na kuridhia usomwe kwa Mara yaPili na Mara ya Tatu na hatimaye kuwa sehemu ya sheria zanchi yetu ya Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NAMICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.
(Hoja ilitolewa iamuliwe)
MWENYEKITI: Ahsante. Hoja imetolewa na imeungwamkono. Tunakushukuru sana Waziri kwa jinsi ulivyoiwasilishahoja yako na maeneo ya msingi ulivyoyaweka wazi.
83
ISSN O856 – 01001
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
BILL SUPPLEMENT
No. 1 26th January, 2018
to the Gazette of the United Republic of Tanzania No.4 Vol. 99 dated 26th January, 2018
Printed by the Government Printer, Dodoma by Order of Government
payable under this Act shall not be capable of being
assigned or transferred or otherwise ceded or of being
pledged or hypothecated. (2) Subject to subsection (1), a pension or other
benefits granted under this Act may be assigned or
transferred for the purposes of satisfying: (a) debt due to the Government; (b) a mortgage created pursuant to section 42; or (c) an order of any court for the periodical payment
of the sums of monies towards the maintenance
of the spouse, former spouse or child of a
member. (3) A pension, gratuity or any allowance granted
under this Act, shall not be attached, sequestered or
levied upon for or in respect of any debt, mortgage or
claim other than a claim of income tax due to the
Government but, the Director General shall make
arrangement necessary for satisfying it or any debt arising
from, discharging a mortgage created or an order of the
court issued consequent upon a loan granted to a
member. Unclaimed
benefits 48.-(1) Where any benefit remains unclaimed for a
period of three years from the date of death or any other
cause, the whole amount shall be credited to a special
reserve account. (2) Where any benefits remains unclaimed for ten
years, the account shall be frozen and the amount
standing in the account shall be transferred to the reserve
account. (3) Notwithstanding subsections (1) and (2), the
Board may on application by the member or any other
beneficiary, order that a member be paid in accordance
with the provisions of this Act.
PART VII
FINANCIAL PROVISIONS
Sources of
funds 49.-(1) The sources of funds shall, without prejudice to
section 6, include - (a) employee and employers' contributions; (b) monies accrued from investments; (c) such sums as may be appropriated by the
with the provisions of the Act; (e) monies accrued from grants and donations; and (f) such sum as may in any manner become
payable to or vested in the Fund. (2) The funds shall be applied for- (a) payment of benefits; (b) investments of the Fund; (c) administration of the Fund; and (d) other uses as may be allowed for better
administration of the Act. (3) The administration expenses of the Fund shall not
exceed limit prescribed by the Authority. Fund to be
held by
Board
50.-(1) For the avoidance of doubt, it is hereby
declared that the monies in the Fund shall, for the
purposes of this Act and all other written laws, be deemed
to be funds held by the Board in trust for the members of
the Scheme and shall be administered by the Board in
accordance with the provisions of this Act. (2) Notwithstanding subsection (1), it shall be lawful
for the Board to authorise payments out of the Fund for
any of the purposes for which payments out of the Fund
are expressly authorised by the Act. Annual
budget
estimates
51.-(1) The Director General shall, before the
commencement of any financial year, prepare or cause
to be prepared for the consideration of the Board
estimates of the revenue and expenditure of the Fund for
the ensuing financial year. (2) The Board shall, after receiving the estimates
report under subsection (1), consider and adopt the
estimates subject to such modifications and amendments
as the Board may consider appropriate. (3) The annual budget estimates shall contain
provisions for all the estimated expenditure during the
ensuing financial year and in particular- (a) for payment of benefits to members; (b) for payment of salaries, allowances and other
expenses in respect of the Board, committees of
the Board and the staff of the Fund; (c) for payment of construction, improvement,
(b) a copy of the report regarding the activities of the
Fund in the preceding financial year. Reserve
account 55.-(1) The Board shall establish, maintain and
manage a Reserve Account into which shall be paid- (a) all portion of the income from the investments; (b) all contributions collected pursuant to this Act; (c) any other money received by the Fund pursuant
to sections 6 and 49; (d) other monies authorised to be paid into the
Reserve Account by any provisions of this Act;
and (e) fines and penalties which may be paid under this
Act. (2) The payment into and out of the Reserve
Account shall be determined by the Board. Exemption
from tax 56.-(1) All contributions and benefits payable under
this Act shall not be subject to income tax. (2) Subject to tax laws, stamp duty and value added
tax shall not be payable on any receipt, contract,
instrument or other document given or executed by the
Board on behalf of the Fund or by any person in respect of
benefits or refunds of contributions under this Act.
Cap.189
(3) Notwithstanding subsection (2), nothing in this
section shall be construed to exempt any person from
liability to pay stamp duty on any power of attorney or on
any document otherwise liable under the Stamp Duty Act. Actuarial
valuation
report
57.-(1) The Board shall, at intervals of three years or at
any other intervals as the Authority may direct and subject
to guidelines issued by the Authority, cause the assets and
liabilities of the Fund to be evaluated by an actuary. (2) Notwithstanding subsection (1), the Board may,
owing to the nature and circumstances of the business of
the Fund, request to the Authority for the waiver of the
requirement under subsection (1). (3) A report of the valuation shall be submitted to the
Authority and the Minister. (4) Upon receipt of the report, the Authority may
direct the Fund to take measures as may be necessary to
necessary for better management of the Fund, regulation
and monitoring of the activities of the Fund. (3) Financial reports referred to under subsection (1)
shall contain- (a) financial position of the Fund at that time; (b) assets and liabilities; (c) results of the Fund's operations; (d) statement of cash flow; and (e) other information as may be required by the
Authority.
PART VIII
LEGAL PROCEEDINGS, OFFENCES AND PENALTIES Contribution
s to be debt
to Board
62.-(1) Every statutory contribution and other
contributions payable under this Act shall be a debt due
to the Board, and may be recovered by way of summary
suit at the instance of the Director General at any time
within twelve years after the date on which it was due. (2) In a case where a defendant applies for leave to
defend, the trial court shall, before granting leave, require
the defendant to deposit a sum equal to the contributions
being claimed in the suit as security for due performance
of the decree that may be entered against the
defendant. Certificates
as evidence 63. A copy of entry in the accounts of the Fund or
other extract from the record of the Fund shall, when
certified by the Director General or any other member
nominated by the Board in that behalf in writing under the
seal of the Board, be received in all courts as prima facie
evidence of the truth of the contents therein and of the
debt due to the Fund by any person. Summary
recovery 64.-(1) Any action for recovery of contributions and
additional contributions may be instituted by the Board of
Trustees, and where an action is instituted before any
court, any officer of the Fund or an advocate appointed
by the Fund in that behalf may appear and conduct the
proceedings.
Cap. 33
(2) Every contribution and additional contributions
due to the Fund may be recovered by a summary suit
under order XXXV of the Civil Procedure Code at any time
within twelve years after the date on which it is due.
apprenticeship with an employee;” (iv) the definition of the term “medical board”; (v) the definition of the term “salary”; (b) adding in its alphabetical order the following new
definitions: “actuary” means a person who is
professionally qualified as an actuary
and approved by the Minister in the
manner prescribed in the regulations; “merged schemes” means the PPF Pension
Scheme, the Public Services Pension
Scheme, GEPF Retirement pension
benefit Scheme and LAPF Pension
Scheme merged by the Public Service
Social Security Act, 2018” Amendment
of section 6 95. The principal Act is amended in section 6, by
deleting paragraphs (a) and (b) and substituting for them
the following: “ (a) employed in the private sector; (b) self-employed; (c) a foreigner employed in Mainland Tanzania; (d) employed in an international organisation
operating in Mainland Tanzania; and (e) any other category of persons as may be
specified by the Minister upon
recommendation of the Authority.” Repeal of
section 20A 96. The principal Act is amended by repealing
section 20A. Amendment
of section 21 97. The principal Act is amended in section 21, by
deleting paragraph (g) and substituting for it the following: “(g) unemployment benefit;” Amendment
of section 22 98. The principal Act is amended in section 22, by:
(a) deleting the words “and (d)” and substituting for
them the phrase “(d) and (f); (b) designating the contents of section 22 as
subsection (1); (c) adding immediately after subsection (1) as
designated a new subsection (2) as follows: “(2) The benefit under section 21(1)(f)
unemployment benefit; (iv) the manner of identifying members
who qualify for unemployment
benefit; (v) the manner and procedure of
converting members contribution
from mandatory scheme to
supplementary scheme; (vi) the manner and modality of
graduating from supplementary
scheme to mandatory scheme; and (vii) any other matter relating to
unemployment benefit.” Amendment
of section 58 127. The principal Act is amended in section 58 by
deleting the word “internal” appearing in subsection (2).
________
SCHEDULE
______
(Made under Section 10 (1))
PROVISIONS RELATING TO THE BOARD
Compositio
n of Board 1.-(1) The Board shall be composed of-
(a) a Chairman who shall be appointed by the President; (b) a member representing the Ministry responsible for social security;
(c) a representative from the Ministry responsible for local government
authorities; (d) a representative of the Ministry responsible for finance; (e) a law officer representing the Attorney General; (f) two members representing most representative employers organisation; (g) two members representing the most representative employees
organisation; and (h) one member appointed by the Minister from amongst persons who
possess knowledge and experience in social security matters. (2) The members referred to under paragraph (b) to (g) shall be
appointed by the Minister upon recommendation by the respective
institutions. (3) In appointing members under paragraph (1)(g) the Minister shall
ensure that the members are appointed from different associations. Inability to
attend
meetings
2.-(1) Where any member appointed pursuant to paragraph
1 ( 1 ) is by reason of illness, infirmity or absence from the United Republic
unable to attend any meeting of the Board, the Minister may appoint a
temporary member in his place and the temporary member shall cease to
Sehemu ya Kumi na Moja inaweka masharti kuhusu marekebisho
yatokanayo. Katika Sehemu hii, sheria mbalimbali zikiwemo Sheria ya
Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii, Sheria ya Mfuko wa Taifa wa
Hifadhi ya Jamii, Sheria ya Utumishi wa Umma, Sheria ya Tume ya Jeshi
la Polisi na Magereza na Sheria ya Marupurupu ya Majaji
zinapendekezwa kurekebishwa kwa lengo la kuwianisha masharti ya
Sheria hizo na masharti ya Sheria inayopendekezwa.
Dodoma, KASSIM MAJALIWA MAJALIWA
22 Januari, 2018 Waziri Mkuu
146
SCHEDULE OF AMENDMENT TO BE MOVED BY KASIM MAJALIWA
MAJALIWA, THE PRIME MINISTER AT THE SECOND READING OF THE BILL
ENTITLED “THE PUBLIC SERVICE SOCIAL SECURITY FUND ACT, 2018 __________
Made under S.0. 86(10)
___________
A Bill entitled “The Public Service Social Security Fund Act, 2018” is amended
generally as follows:
A: By deleting Clause 97 and substituting for it the following:
“Amend-
ment of
section 21
97. The principal Act is amended in section 21, by
deleting paragraph (f) and substituting for it the following:
(f) unemployment benefit;”
B: In Clause 105, by deleting the phrase “section 40” and substituting for it the
phrase “sections 39 and 40”.
Dodoma, KMM
31st January, 2018 PM
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
147
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea,sasa namwita Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Hudumana Maendeleo ya Jamii ili aweze kutoa taarifa ya Kamatiyake. Mheshimiwa Peter Serukamba, karibu.
MHE. PETER J. SERUKAMBA – MWENYEKITI WA KAMATIYA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII: MheshimiwaMwenyekiti, napenda kuchukua nafasi hii kuwasilisha maoni,ushauri na mapendekezo ya Kamati kuhusu Muswada waSheria wa Mfuko wa Hifadhi Jamii kwa Watumishi wa Ummawa mwaka 2017 (The Public Service Social Security Fund, 2017).Uwasilishaji huu wa maoni na mapendekezo ya Kamati nikwa mujibu wa Kanuni ya 86(5) ya Kanuni za Bunge zaKudumu, Toleo la Januari 2016.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kuanza shughuli hiimuhimu ya uchambuzi wa Muswada, Kamati ilipata fursa yakupokea maelezo ya kina kuhusu Muswada wa Sheriainayopendekezwa yaliyowasilishwa mbele ya Kamati naWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi,Vijana na Wenye Ulemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagamaambaye alieleza kuhusu madhumuni, sababu na mpangiliowa Muswada huu siku ya tarehe 16 Januari 2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maelezo hayo ya kinayalitanguliwa na semina ya kutoa uelewa mpana kwaWajumbe wa Kamati kuhusu dhana nzima ya Mfumo waHifadhi ya Jamii pamoja na chimbuko la hoja ya kuunganishaMifuko hii. Semina hiyo iliyotolewa na wataalam wa masualaya Hifadhi ya Jamii iliwawezesha Wajumbe wa Kamati kuwakatika nafasi nzuri, kuelewa dhana nzima ya msingi wauunganishwaji wa Mfuko na sababu za mapendekezo yasheria hii ambayo wajumbe waliweza kuwa na nafasi nzuriya kuchambua, kuweza kutoa maoni, ushauri namapendekezo ya kuboresha Muswada.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dhana na chimbuko la Mfukowa Hifadhi ya Jamii. Kabla ya kuendelea, napenda kutoamaelezo machache kuhusu dhana na chimbuko la Mfuko
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
148
wa Hifadhi ya Jamii kwa ujumla wake nikioanisha na Mfukowa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, dhana ya Mfuko wa Hifadhiya Jamii ni kwa ajili ya kumwezesha mwanajamii aweze kuishimaisha yenye thamani na staha ndani yake na kumpa uwezowa kuendelea kumudu maisha yake wakati wote hasa paleanapokumbwa na majanga katika maisha kama vile kukosaajira, kuugua, kuacha kazi kwa sababu ya umri yaani uzee,likizo ya kujifungua, ulemavu na majanga mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi ya jamii ni haki yamsingi ambayo inatambulika kimataifa na viwango vyakevimeainishwa katika Mkataba wa Shirika la Kazi Dunia (ILO)102 wa mwaka 1952 pamoja na pendekezo lake la 201 lamwaka 2012. Tanzania kama nchi mwanachama iliridhia nakusaini mkataba huo, basi haina budi kuufuata na kuwekasheria na taratibu il i kuhakikisha unakuwepo mfumomadhubuti wa kutoa huduma hiyo kwa wananchi wake.Aidha, Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Binadamu wamwaka 1948, Kifungu cha 22 nacho kimeainisha suala laHifadhi ya Jamii kwa wananchi wake katika nchi yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, inatambulika kwamba kwamujibu wa utaratibu wa mkataba wowote lazima upateridhaa ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nautekelezaji wa maridhio ya Bunge hilo utafanya mapitishoya sheria mbalimbali zikiwemo sheria zilizokuwa zinasimamiaMifuko inayopendekezwa na sheria hii kufutwa ambayo niMifuko mitano. Kwa maana ya Sheria ya Mfuko wa NSSF yamwaka 1997; Sheria ya Usimamizi wa Mfuko wa GEPF, 2012;Sheria ya Mfuko wa LAPF; Sheria ya Mfuko wa PPF; na Sheriaya Mfuko wa PSPF. Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania imetambua Hifadhi ya Jamii kama sehemu ya hakiya kila mwananchi wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, chimbuko la uunganishwajiwa Mifuko hiyo ilitokana na maombi ya watumishi wa ummakupitia Vyama vyao vya Wafanyakazi na kuwasilishwa katikaShirika la Vyama vya Wafanyakazi yaani TUCTA ambapo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
149
walieleza mapendekezo hayo wakati wa Maadhimishombalimbali ya Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani ambayohufanyika kila mwaka Mei Mosi. Aidha, wakati wamaadhimisho hayo kuanzia mwaka 2014 (Mbeya), 2016(Dodoma), 2017 (Kilimanjaro), TUCTA ambao ndio sauti yawafanyakazi nchini imekuwa ikitoa mapendekezo hayo kwaMgeni Rasmi mara nyingi amekuwa ni Mheshimiwa Raiskwamba Mifuko hiyo iunganishwe kwa ajili ya kuweka uwianowa makato pamoja na maslahi mbalimbali yatolewayo naMifuko hiyo kwa wanachama na watumishi wa umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, madhumuni yauunganishwaji wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii. Muswada waSheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Watumishi wa Ummawa mwaka 2017 unalenga kupendekeza kutungwa kwaSheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Ummakwa malengo ya kutoa mafao ya hifadhi ya jamii kwawatumishi walio katika utumishi wa umma, kufuta Sheria yaMfuko wa Mafao ya Hitimisho la Kazi la Watumishi wa Umma,Sura 407; Sheria ya Mfuko wa Pensheni wa LAPF, Sura 407;Sheria ya Mfuko wa Pensheni ya PPF, Sura 372; Sheria ya Mfukowa Pensheni wa GEPF, Sura 51 kwa ajili hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Muswadaunapendekeza pia marekebisho katika Sheria ya Mfuko waHifadhi ya Taifa wa Jamii kwa madhumuni ya kuwekamasharti kuhusu mafao ya hifadhi ya jamii kwa watumishiwalio katika sekta binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu imekuwa ikitimizamajukumu ya utoaji wa huduma ya hifadhi ya jamii kwawatumishi wa umma na watumishi walio katika sekta binafsikupitia Mifuko mbalimbali kama ambavyo imetajwa hapoawali kwa maana ya PSPF, LAPF, GEPF pamoja na PPF kwamujibu wa sheria za uanzishwaji wake na ina-save kwawatumishi walio katika sekta binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa maelezo yaSerikali na uchambuzi uliofanywa na Kamati imebainikakwamba kuunganishwa kwa Mifuko hii ya Hifadhi ya Jamii
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
150
kutakuwa na manufaa mengi kwa wananchi nawanachama wa Mifuko pamoja na Taifa kwa ujumla wakekama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kupunguza gharamambalimbali za uendeshaji wa Mifuko. Kamati imebainikwamba kuunganisha Mifuko hiyo, gharama nyingizitapungua zikiwemo gharama zifuatazo:-
Kupungua kwa idadi ya gharama za Bodi yaWadhamini; kupunguza gharama za Menejimenti ya Mifuko;kupunguza gharama za uendeshaji wa Ofisi za Mikoa naKanda; kupunguza gharama za mifumo ya TEHAMA;kupunguza gharama za ushindani na kupunguza kwamigogoro baina ya Mifuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamotohii Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA)imekuwa ikilazimika kuendesha zoezi la uhakiki(reconciliation) kwa michango ya wanachama ambalo hilinalo lil ikuwa linatumia gharama kubwa kusababishaongezeko la gharama hizo katika gharama za uendeshajiwa Mifuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uboreshaji na uimarishaji wahuduma kwa wanachama. Kamati imebaini kwambakuunganishwa kwa mifuko hii kutapelekea huduma kwawanachama kuwa bora na imara kwa mujibu wa Sheria,Kanuni na Miongozo iliyopo itakayoendelea kutolewa naMamlaka kuhusu utoaji wa huduma hizo kwa wateja waMifuko. Sheria hii inayopendekezwa imeainisha vifungumbalimbali vinavyolinda maslahi ya wanachama ikiwa napamoja na Kifungu namba 20 cha Muswada kinachotoamasharti ya kuzuia wanachama kuhusishwa na ucheleweshajiwa michango ambalo ni jukumu la mwajiri la kuhakikishamichango ya mwajiriwa inapelekwa kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuboresha huduma zawanachama, Kifungu cha 43(3) kinampa haki kamilimwanachama kuweza kudai kulipwa fidia na Mfuko
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
151
ambapo kama Mfuko huo utamcheleweshea stahiki yake yamafao ndani ya siku 90 na kubainika kwamba ucheleweshajihuo haujasababishwa na mwanachama bali ni Mfuko husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vifungu vya Sheria vyaUsimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii imeboreshwa ili kuipaMamlaka uwezo wa kuchukua hatua stahiki kwa watumishiwa Mifuko ambao watakiuka masharti ya kisheria namaelekezo ya Mamlaka. Kwa kufanya hivyo, huduma zawateja wa Mifuko hazitaathirika kwa namna yoyote ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uchambuzi wa Muswada.Kwa mujibu wa Kanuni ya 84(2) ya Kanuni za Bunge, Toleo la2016, mnamo tarehe 17 na 18 Kamati ilifanya mkutano wawadau kwa lengo la kupokea maoni (public hearing) kwakusaidia Kamati kufanya uchambuzi wa Muswada huu.Wadau mbalimbali walifika katika mkutano huo ambao nipamoja na:-
National Organization for Legal Aids; Legal andHuman Rights Centre; Chama cha Wanasheria Tanzania;Chama cha Walimu Tanzania; Chama cha Waajiri; Chamacha Wafanyakazi (TUCTA); Chama cha Wahadhiri wa VyuoVikuu vya Tanzania na Shirika la Kazi (ILO). Aidha, wadauwengine walitoa maoni yao kwa maandishi wakiwemoChama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA) na Chama chaWafanyakazi wa Mahakama ambayo yamesaidia Kamatikuboresha Muswada huu na kutoa maoni na ushauri huu leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na hoja nzitozilizoibuliwa, siku ya tarehe 19 ilikuwa ni siku ya kufanyamaridhiano ya Serikali kupata ushauri elekezi (consultation)ili kuwa na dhana ya uwajibikaji wa pamoja. Kamati ikaonani busara kuwapa nafasi Serikali. Napenda kulieleza Bungelako Tukufu kuwa katika mashauriano ya hoja mbalimbalizikiwemo zile zilizohitaji ushauri elekezi, Serikali ilikubalianana Kamati kwamba marekebisho yote yatawasilishwa naSerikali kwenye Jedwali la Marekebisho (Schedule ofAmendments) kama Kamati ilivyopendekeza.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
152
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumshukuru sanaMheshimiwa Spika na wewe kwa kusaidia Kamati kutekelezawajibu wake, naipongeza Serikali kwa kuwa wasikivu nakupokea maoni, ushauri na mapendekezo yaliyotolewa naKamati kuyapokea kwa ajili ya kuyafanyia kazi. Ni imani yanguna Kamati nzima kwamba tumeisaidia Serikali na wananchiwa Tanzania katika kuiboresha sheria hii ambayo ipo katikamchakato wa kutungwa kwa aji l i ya manufaa yawafanyakazi wa nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kuchukua fursahii kumshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa JenistaMhagama kwa namna ambavyo amekuwa akitoaushirikiano wa dhati kwangu mimi pamoja na Kamati nzima.Kwa jinsi alivyokuwa msikivu, mwelewa na hata paletulipohitaji ufafanuzi wa Serikali alitoa ushirikiano bila kusitawakati wa kuuchambua na kuujadili Muswada huu. Kwakweli Mheshimiwa Jenista ni mfano wa kuigwa, hongera sanadada yangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni na mapendekezo yaKamati. Napenda kutoa maoni na ushauri na mapendekezoya Kamati kama ifuatavyo kwa lengo la kuboreshaMuswada. Kamati imebaini makosa ya uchapaji, spelling andgrammatical errors na inashauri marekebisho yafanywe kwamaeneo yote yenye makosa ili kuweka maana stahiki katikavifungu vilivyoonekana kuwa na makosa ya uchapishwaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati inapendekezakifungu cha tatu (3) kuhusu Interpretation kufuta neno‘leader’ katika maana ya neno qualifying period na badalayake kuweka neno ‘member’. Aidha, kifungu hicho Kamatiinashauri kufuta marejeo namba 87 kwa maana yatransitional period badala yake kitumike kifungu namba 86ili kuondoa makosa ya uchapaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kifungu cha tatu (3)cha tafsiri ya maneno mbalimbali l iongezwe neno‘Parliamentary Service’ kwa maana Public Service i l ikutambua utumishi wa Bunge ni mtumishi wa umma na ni
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
153
mwanachama wa mfuko huu unaopendekezwa kuanzishwa.Aidha, kuongezwa tafsiri ya maneno kama vile Special lumpsum, pension, unemployment benefit, funeral benefit andsickness benefit ambayo yametumika hajapatiwa tafsiri yakekatika orodha ya maneno yaliyotafsiriwa kwa Muswada huu.Aidha, Kamati inashauri maneno haya yapatiwe tafsiri piazijumuishwe katika Kanuni ambazo zitatungwa na Wazirimwenye dhamana kwa ajili ya utekelezaji wa sheria hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati inapendekeza pianeno ‘month’ tafsiri iliyopewa iboreshwe kwa kuwa siyo mieziyote ina siku thelathini kama ilivyotafsiriwa, kuna mweziambao siku ni ishirini na nane, ishirini na tisa na mingine sikuthelathini na moja. Kamati inapendekeza isomeke calendarmonth or a written calendar badala ya a period of thirty daysconsecutively kama ilivyotafsiriwa katika Muswada.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kifungu hicho hichocha tatu (3) katika tafsiri ya neno ‘qualifying pensionableservice’ kuna neno continuous katika vipengele vyote yaani“a” na “b”, kwa kuwa mwanachama anaweza akawahajafanya kazi kwa kipindi fulani kutokana na sababumbalimbali na baadaye akarejea kazini katika sekta yaumma au katika sekta binafsi, ambapo atakapofikia umriwa kustaafu akawa anastahili kulipwa mafao yake kwakujumlisha muda aliotumikia na kuchangia katika Mfuko wahifadhi ya jamii. Aidha, katika tafsiri ya neno ‘totalization’neno ‘fully contributed’ lifafanuliwe ili lisiweze kuletamkanganyiko na liweze kueleweka sawasawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika tafsiri ya neno ‘salary’Kamati inashauri neno hilo litafsiriwe vyema na ikiwezekanatafsri inayotumika na Msimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya jamii(SSRA) itumike. Kamati inashauri marupurupu mengine kamavile posho zisijumuishwe katika tafsiri hiyo kwani posho hizohubadilika mara kwa mara kadiri inavyoonekana inafaa.Aidha, Kamati inashauri pia maneno “Employers Association”na “Employees Association” yaongezwe katika orodha yatafsiri ya meneno.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
154
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika orodha ya tafsiri yamaneno kuna neno la ‘full pension’ kwa kuwa tafsiri hiyohaijakamilika kama ambavyo imetafsiriwa na Sheria ya SSRA.Kamati inashauri tafsiri hiyo izingatie tafsiri itakayorejewakatika kanuni za ukokotozi zitakazotengenezwa kwa ajili yautekelezaji wa sheria hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, neno ‘Actuarialvaluation’ limepewa tafsiri yake katika orodha ya manenona limetumika katika kifungu cha 91(a)(i) kwa maana tofautina tafsiri iliyopo katika maneno mengine. Kamati inashauritafsiri hiyo iangaliwe upya ili kuondoa mkanganyikounaoweza kujitokeza katika matumizi yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika tafsiri ya neno‘qualifying period’ Kamati inapendekeza neno ‘leader’ lifutwena badala yake litumike neno ‘member’ i l i kufanyamarekebisho ya kiuandishi na kuleta tafsiri sahihi kwa kuwawachangiaji wa Mfuko huo wa Hifadhi ya Jamii wotewanatambulika kama wanachama (members) na siyokiongozi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, katika tafsiri ya neno‘transition period’ kumefanyika marejeo ya kifungu cha 87kinachozungumzia provision regarding employees Cap.298,Kamati inashauri ibadilishwe na badala yake marejeoyafanyike katika kifungu cha 86 ambacho kinazungumziatransition period.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha sita (6)kinachohusu Establishment of the Fund. Katika Kifungu kidogo6(1)(c), Kamati inashauri kifutwe na kiandikwe upya ilikuondoa mkanganyiko uliopo katika kifungu hicho tajwa nakifungu cha 80(2) na 105 vya Muswada huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 15 kinachohusuAppointment of the Director General wa Mfuko huu. Kifungucha 16(2) kinachohusu other staff of the fund.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
155
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 18 kinachohusucontributions, Kamati inapendekeza kufuta manenoyanayosomeka ‘such amount as the Minister may, by orderin the Gazette, determine’. Katika Kifungu cha 18(8) Kamatiinapendekeza kuondoa neno ‘may’ na kuweka neno ‘shall’.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 19 kinachohusuAdditional contributions for delayed remittance ofcontributions by employer. Kifungu 19(1) kina mkanganyikona kifungu 18(3) katika kuainisha nani ni mwajiri. Kamatiinashauri kifanyiwe kazi ili kuondoa mkanganyiko huo. Aidha,katika kifungu hicho rejea ifanyike katika Kifungu cha 18(6)badala ya kifungu cha 21(2) na kifungu 19(3). Kifungu cha 19kinachohusu Additional contributions for delayed remittanceof contributions by employer.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 29(1)kinachohusu Benefits payable, Kamati inashauri iongeze ainambili ya mafao kutoka nane (8) yanayotolewa na Mfuko hadikufikia kumi (10) kwa kuongeza fao la education benefit nagratuity benefit.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 33 kinachohusuinvalidity benefit. Kifungu cha 37 kinachohusu “Survivorsbenefits”, kifungu 37(1) (a) na (b). Kifungu cha 38 kinachohusuBasis and duration of survivor’s pension.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 40 kinachohusupensions, gratuity and allowances for persons holding certainpublic office. Kamati inapendekeza viongozi waliotajwakatika kifungu hiki aongezwe Katibu wa Bunge (Clerk ofNational Assembly) kwenye orodha ya viongozi wanaopatamafao maalum kwa kuwa nafasi hiyo ni nafasi ya kikatibakama ilivyoainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muunganowa Tanzania ya Mwaka 1977, Ibara ya 87 (1) ambapoimetamka uwepo wa Katibu wa Bunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Katika kifungu hikikuongezwe neno ‘and Security’ kati ya neno ‘Intelligence’na neno ‘service’ ili kuweza kurekebisha jina la Mkurugenzi
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
156
wa Idara ya Intelijensia kuweza kuleta maana sahihi ya cheohicho katika sheria hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 47(2)(c)kinachohusu Prohibition on cession and attachment ofbenefits, Kamati inashauri kiangaliwe upya ili kuondoaubaguzi wa jinsia kwani kimemtaja mke na kuacha mume.Aidha, marekebisho yafanyike ili kumtambua mnufaikajipasipo kuainisha jinsi ya mnufaika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kifungu cha 56 kinahusuexemption from tax. Kifungu cha 57(4) Actuarial ValuationReport, Kamati inashauri neno ‘may’ lifutwe na kuweka neno‘shall’ ili kuweza kuwa na sharti la lazima kwa Mamlaka yaUsimamizi wa Mifuko kuchukua hatua stahiki kwa ajili yakurekebisha upungufu uliobainika kwenye taarifa ya mtaalamwa uthamini wa hali halisi ya Mifuko (Actuarial Valuation) yahifadhi ya jamii. Kwa kubaki hivyo, mamlaka inapewamwanya wa kuamua kuchukua hatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni ya jumla. Umuhimuwa SSRA kuongezewa majukumu ya usimamizi ya hifadhi yajamii. Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003ilipelekea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniakutunga Sheria Na.8 ya mwaka 2008 pamoja na mambomengine ilitoa masharti ya kuanzishwa kwa Mamlaka yaUsimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (Social SecurityRegulatory Authority).
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majukumumengine, Mamlaka hii ya usimamizi ilipewa jukumu lakusimamia Mifuko yote ya Hifadhi ya Jamii kwa kutoamiongozo ya utendaji sahihi, kusimamia utendaji wa Mifuko,kutetea na kulinda maslahi mbalimbali ya wanachama,kutoa ushauri wa kisera kwa Waziri mwenye dhamana, kusajiliwasimamizi wa uwekezaji wa fedha za Mifuko ya jamii namajukumu mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ina maoni kuwa,bado kuna majukumu mengi na makubwa kwa Mamlaka
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
157
hii ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii kwa kuwamajukumu hayo bado yapo ikizingatiwa kwamba Mifuko hiiinakwenda kuunganishwa hivyo Mamlaka inapaswakuhakikisha kumbukumbu za wanachama wa Mifuko yotezinabaki vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati inapendekeza piamasuala yote yanayohusiana na hifadhi ya jamii, iwekwechini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii.Kamati inaishauri Serikali kuhakikisha Mifuko ya Bima ya Afyaikiwemo Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF), Bima ya Afyaya Jamii (CHF) na mifuko mingine yenye dhana ya hifadhi yajamii iwekwe chini ya msimamizi mmoja. Kwa kufanya hivyo,kutaondoa mkanganyiko na unufaikaji wa mafao zaidi yamara moja ikiwemo fao la matibabu na fao la ugonjwayanayotolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii na Mfuko waTaifa wa Bima ya Afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watumishi wanaotokakatika Mifuko hiyo kuwahahakikishia ajira zao. Kamati inaonakuwa kuunganishwa kwa Mifuko hii kutapelekea suala la ajiraza wafanyakazi katika Mifuko hiyo kuathirika na wenginekupoteza nafasi zao za awali na hata kupoteza ajira zaokabisa. Kamati inashauri, Wizara yenye dhamana ikishirikianana Mifuko husika pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Sektaya Jamii kuhakikisha wanalinda ajira za wafanyakazi haobila kujali nafasi zao za awali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni imani ya Kamati kuwa,kuanzia sasa ofisi za Mifuko hii zitakuwa hadi ngazi ya Wilayaambako wanachama wengi wapo wakiwemo Walimu,Wauguzi, Askari na kada nyingine mbalimbali hasa kutokakatika sekta ya umma. Hivyo basi Kamati inasisitiza watumishiwote waliokuwa katika Mifuko hiyo ajira zao zilindwe kwamujibu wa Sheria na Kanuni za Utumishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanachama katika Mifukohiyo wasihame na michango yao ili kuiwezesha Mifuko hiyokujiendesha. katika kuhakikisha Mifuko hii inakuwa na mudamrefu wa uhai wake, ni maoni ya Kamati kwamba, katika
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
158
uunganishaji na usajili wa wanachama wa Mifuko uanze nawafanyakazi wapya katika sekta zote mbili kwa maanakwamba, mara baada ya sheria hii kusainiwa na MheshimiwaRais, basi wafanyakazi watakaoajiriwa katika sekta zote mbiliwaanze kutenganishwa usajili wao ili mfanyakazi wa sektaya umma asajiliwe katika Mfuko wa umma na mfanyakaziwa sekta binafsi asajiliwe katika Mfuko wa sekta binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati inashauri kwa wakatihuu, wanachama waliopo katika Mifuko hiyo minneinayounganishwa wote wabaki katika Mfuko wa umma nawale waliopo katika mfuko wa NSSF waendelee kuchangiahuko bila kujali ni mfanyakazi wa sekta gani, utaratibu huuunafahamika kama cut-off date ya mwanachama. Kwakufanya hivyo, kutasaidia kuboresha uwiano wawanachama wastaafu kutoka uwiano wa 1:5 hadi kufikiauwiano wa 1:10, kutapunguza idadi ya wanachama kuanzakufuatilia taarifa zao wakati wa kupata stahiki za mafaoyakiwemo mafao ya uzazi na kustaafu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, sababu kubwa zaidini kwamba michango ya wanachama hao imewekezwakatika miradi mbalimbali iliyogharamiwa na michango yaoambapo kuwahamisha na uwekezaji huo itailetea usumbufuSerikali na wanachama wake pia na kwa mfumo ulivyomakusanyo ya michango ya watumishi sasa (currentcollections) ndiyo inambeba kwa kumlipa mtumishianayestaafu leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ifafanue fao laupotevu wa ajira (Unemployment Benefit).
Mheshimiwa Mwenyekiti, mifuko kufuatilia michangoya wanachama kwa waajiri. Mara baada ya mwajiriwakupeleka taarifa zake kwa mwajiri na kuanza kulipwamshahara wake huanza kukatwa michango yake kwa ajiliya kupeleka michango yao. Kamati inashauri Mifuko hiyoiweke utaratibu wa kufuatilia michango hiyo kwa waajiri ilikifungu cha kulipa faini kilichopo katika sheria hii kiwezekutumika vizuri.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
159
Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyakazi katika kampuniyenye hisa za Serikali kuchangia katika mfumo wa umma.Nchi yetu imekuwa na kampuni za aina mbalimbali zile zabinafsi na kampuni ambako Serikali imeingia ubia namwekezaji. Kamati inashauri Kampuni zote ambako Serikaliina hisa zake bila kujali kiasi cha umiliki wa hisa hizo, ikiwemoTBL, TCC, Airtel na Kampuni nyingine, wafanyakazi wake wotewawe wanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwaWatumishi wa Umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo,kutaweza kuimarisha Mfuko huu lakini pia kuweza kulindamaslahi ya wananchi wetu ambao ni waajiriwa katikakampuni hizo kwa kuhakikisha kwamba ni kwa kiasi ganiwafanyakazi wa Kitanzania wananufaika na Kampuni hizona kuwekewa hazina yao ya kijamii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kulipa madeni yamifuko. Mifuko inayounganishwa kwa sheria hii imekuwaikiidai Serikali madeni makubwa ya kuanzia mwaka 2000 nakurudi nyuma ilipoamua kuwalipa wastaafu mafao licha yaSerikali kutopeleka mafao ya watumishi hao katika Mifukowanakonufaika nayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kukamilisha utoaji wa faola elimu. Katika Mifuko hii inayounganishwa kwa sheria hii,kuna Mifuko iliyokuwa inatoa fao la elimu kwa wanachamana hata wategemezi wa wanachama wa Mifuko hiyo. Aidha,kwa mujibu wa kifungu cha 29(1) cha orodha ya mafaoyanayoainishwa na Mfuko huu fao la elimu limeachwa nakwamba halitatolewa tena kwa wanachama wa Mfuko huu.Kamati inaunga mkono hoja ya kuondolewa kwa fao la elimukatika orodha ya mafao kwani sasa Serikali inaihudumia jamiinzima ya Tanzania kwa kutoa elimu bila malipo kuanzia elimuya msingi. Nashauri kama itakuwa hivyo basi wale waliokuwawananufaika, waendelee kunufaika mpaka waishe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria iwatambue Katibu waBunge na Makatibu Wakuu wa Wizara. Katiba ya Jamhuri ya
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
160
Muungano wa Tanzania imemtambua Katibu wa Bungekatika Ibara ya 87(1) kwamba kutakuwa na AccountingOfficer.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati inashauri sheria hiiiwajumuishe Makatibu Wakuu wote wa Wizara ili wawezekunufaika na Mfuko huu wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishiwa umma. Kwa kufanya hivyo, kutaondoa dhana yamatumizi mabaya ya madaraka yao kwa manufaa binafsina kutalinda hadhi ya maisha na utu wao mara baada yaajira zao kukoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, kwa mara nyinginetena napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru wewe binafsi,kwa kunipa nafasi ya kuwasilisha maoni, ushauri namapendekezo ya Kamati kuhusu Muswada huu Mfuko waHifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hiikumpongeza sana Mheshimiwa Jenista Mhagama, NaibuMawaziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Mheshimiwa AnthonyMavunde na Mheshimiwa Ikupa Stella Alex, Katibu Mkuu EricShitindi na watendaji wote wa Wizara kwa ushirikianowalioipa Kamati na kupelekea kuwasilisha vyema Muswadahuu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hiikuwashukuru tena wadau wote waliofika mbele ya Kamatikuwasilisha maoni yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa namna ya kipekeenawashukuru sana Wajumbe wa Kamati kwa kazi nzuri yenyeumahiri wakati wote wa uchambuzi wa Muswada huu.Wajumbe wamefanya kazi nzuri ya kuhakikisha uchambuziwa Muswada huu unakuwa wenye tija kwa maslahi ya Taifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda sana kumshukuruKatibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai, Mkurugenzi waIdara ya Kamati za Bunge Ndugu Athuman B. Hussein naKaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Kamati Ndugu Chacha
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
161
Nyakega pamoja na Katibu wa Kamati hii Ndugu AgnesNkwera na Msaidizi wa Kamati Ndugu Waziri Kizingiti kwakuratibu vyema shughuli za Kamati na kuhakikisha taarifa hiiinakamilika kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, namshukuru KaimuMshauri Mkuu wa Mambo ya Sheria wa Bunge Ndugu PiusMboya pamoja na wasaidizi wake Ndugu LeorcardKapongwa, Ndugu Maria Mdulugu na Ndugu NestaKawamala kwa uchambuzi wa kisheria walioufanya kuisadiaKamati.
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Mwenyekiti,hasa na kwa kuzingatia muda.
MAONI, MAPENDEKEZO NA USHAURI WA KAMATI YAKUDUMU YA BUNGE YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMIIKUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MFUKO WA HIFADHI YAJAMII KWA WATUMISHI WA UMMA WA MWAKA 2017 (THE
PUBLIC SERVICE SOCIAL SECURITY FUND, 2017) KAMAILIVYOWASILISHWA MEZANI
____________________
1.0 UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hiikuwasilisha Maoni, Ushauri na Mapendekezo ya Kamati kuhusuMuswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwaWatumishi wa Umma wa Mwaka 2017 (The Public ServiceSocial Security Fund, 2017). Uwasilishaji huu wa maoni namapendekezo ya Kamati ni kwa mujibu wa Kanuni ya 86 (5)ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari 2016.
Mheshimiwa Spika, Kwa kuzingatia Kanuni ya 119 yaKanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari 2016, uliipaKamati ya Kudumu ya Huduma na Maendeleo ya Jamiijukumu la kushughulikia Muswada huu wa Sheria. Naomba
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
162
kutoa shukrani zangu za dhati kwa kuendelea kuonesha imanikubwa kwa Kamati ninayoiongoza na kuipa kazi ya kuufanyiakazi Muswada na kuwasilisha maoni na mapendekezo mbeleya Bunge lako Tukufu. Nina imani Kamati imefanya kazi kwaweledi mkubwa na kuweza kuutendea haki Muswada nakuisaidia Serikali kwa manufaa ya nchi yetu.
Mheshimiwa Spika, kabla ya kuanza shughuli hiyomuhimu ya uchambuzi wa Muswada, Kamati ilipata fursa yakupokea Maelezo ya kina kuhusu Muswada wa Sheriainayopendekezwa yaliyowasilishwa mbele ya Kamati na Ofisiya Waziri Mkuu-Waziri, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na WatuWenye Ulemavu Mheshimiwa Jenister Joakim Mhagama, (Mb)ambaye alieleza kuhusu Madhumuni, Sababu na Mpangiliowa Muswada huu siku ya tarehe 16 Januari, 2018. Maelezohayo ya kina yalitanguliwa na Semina ya kutoa uelewampana kwa Wajumbe wa Kamati kuhusu dhana nzima yaMfuko wa Hifadhi ya Jamii pamoja na chimbuko la hoja yakuunganisha mifuko hii. Semina hiyo ilitolewa na wataalamuwa masuala ya Hifadhi ya Jamii iliwawezesha wajumbe wakamati kuwa katika nafasi nzuri ya kuuelewa dhana na msingimzima wa uunganishwaji wa mifuko na sababu zamapendekezo ya sheria hii ambapo Wajumbe waliwezakuwa katika nafasi nzuri ya kuuchambua na kuweza kutoaMaoni, Ushauri na Mapendekezo ya kuuboresha Muswada.
2.0 DHANA NA CHIMBUKO LA MFUKO WAHIFADHI YA JAMII
Mheshimiwa Spika, Kabla ya kuendelea napendakutoa maelezo machache kuhusu Dhana na Chimbuko laMfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa ujumla wake ikioanishwa naMfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma.
Mheshimiwa Spika, Dhana ya Mfuko wa Hifadhi yaJamii ni kwa ajili ya kumuwezesha mwanajamii aweze kuishimaisha yenye thamani na staha ndani yake na kuwapauwezo wa kuendelea kumudu maisha yake wakati wote nahasa pale akapokumbwa na majanga katika maisha yakekama vile kukosa ajira, kuugua, kuacha kazi kwasababu ya
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
163
umri (uzee), likizo ya kujifungua, ulemavu na majangamengine.
Mheshimiwa Spika, hifadhi ya jamii ni haki ya msingiambayo inatambulika kimataifa na viwango vyakevimeainishwa katika Mkataba wa Shirika la Kazi Duniani(ILO) Na.102 wa Mwaka 1952 pamoja na pendekezo lakeNa.201 la Mwaka 2012 na Tanzania kama nchi mwanachamaaliliridhia kwa kusaini Mkataba huo, basi nchi haina budikuufuata kwa kuwekwa utaratibu wa kuhakikishakunakuwepo na mfumo madhubuti wa kutoa huduma hiyokwa wananchi wake. Aidha, Mkataba wa kimataifa wa hakiza binadamu wa Mwaka 1948 kifungu cha 22 nachokimeainisha suala la Hifadhi ya Jamii kwa wananchi wakekatika nchi yeyote.
Mheshimiwa Spika, inatambulika kwamba, kwamujibu wa utaratibu Mkataba wowote lazima upate ridhaaya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na katikautekelezaji wa maridhio hayo Bunge liliweza kufanyamapitisho ya Sheria mbalimbali zikiwemo Sheria zilizokuwazinasimamia Mifuko inayopendekezwa na Sheria hii kufutwaambayo ni Mifuko mitano (5) kwa maana ya sheria ya mfukowa NSSF ya Mwaka 1997, Sheria ya usimamizi wa mfuko waGEPF ya mwaka 2012, Sheria ya mfuko wa LAPF, Sheria yamfuko wa PPF na Sheria ya Mfuko wa PSPF.
Mheshimiwa Spika, Katiba ya Jamhuri ya Muunganowa Tanzania ya Mwaka 1977 ibara ya 11(1) pia imetambuaHifadhi ya jamii kama sehemu ya haki ya kila mwananchiwa Tanzania. Kwa kufanya hivyo Muswada huu umetoamapendekezo ya aina nane (8) za Mafao ikiwemo fao lakustaafu, fao la urithi kwa mtumishi atakayefariki na kuachawategemezi wake, fao la pensheni endapo mtumishiatafikisha miaka 60 kazini na ndiyo ukomo wa utumishi kwamujibu wa sheria, fao la uzazi kwa mtumishi atakayejifunguamtoto akiwa bado kazini, fao la upotevu wa ajira, fao laugonjwa endapo mtumishi ataugua ugonjwa ambaoutamsababishia kushindwa kuendelea kufanya kazi katikautumishi wa umma na kupata kipato chake cha kila siku,
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
164
fao la kifo na fao la mazishi kwa mwanachama wake. Aidha,utolewaji wa mafao hayo hautaingiliana kati ya unufaikajiwa fao moja na fao lingine kwa wakati mmoja kwa mujibuwa usimamizi wa sheria hii inayopendekezwa.
Mheshimiwa Spika, chimbuko la uunganishwaji waMifuko hiyo lilitokana na maombi ya watumishi wa Ummawenyewe kupitia vyama vyao vya wafanyakazi nakuwasilishwa na Shirikisho la Vyama vya wafanyakazi yaaniTUCTA ambapo walieleza mapendekezo hayo wakati wamaadhimisho mbalimbali ya Sikukuu ya wafanyakazi Dunianiambayo hufanyika kila mwaka tarehe 01 Mei ijulikanayokama Mei Mosi.
Aidha, wakati wa maadhimisho hayo kuanzia mwaka2014 jijini Mbeya, 2016 Mjini Dodoma, 2017 Mjini Moshi –Kilimanjaro TUCTA ambayo ndiyo sauti ya wafanyakazi nchini,imekuwa ikitoa mapendekezo hayo kwa mgeni rasmi (maranyingi amekuwa Mheshimiwa Rais) kwamba Mifuko hiyoiunganishwe kwa ajili ya kuweka uwiano wa makato pamojana maslahi mbalimbali yatolewayo na mifuko hiyo kwawanachama hasa watumishi wa Umma.
Mheshimiwa Spika, mbali na sababu ya kuwekauwiano wa makato na maslahi ya mwanachama katikamifuko ya hifadhi ya jamii, mapendekezo mengineyaliyokuwa yakitolewa ni pamoja na kupunguza gharamaza uendeshaji. Aidha, mapendekezo yao yalikuwa ni kuwepokwa mifuko miwili tu, mmoja ukihudumia sekta ya Umma nawa pili kwa ajili ya sekta binafsi. Licha ya kupunguza gharamapia kuondokana na ushindani usio na tija baina ya mifukoiliyopo na kuifanya Sekta ya Hifadhi ya Jamii kuwa bora zaidikwa wanachama wake.
Mheshimiwa Spika, Serikali ilitueleza kwamba, katikakusikiliza hoja ya wafanyakazi wa umma iliamua kulichukuapendekezo hilo na kulifanyia kazi. Aidha, kabla ya kutekelezamapendekezo ya uunganishaji wa mifuko ya Hifadhi ya jamiiambacho kimekuwa ni kilio cha wafanyakazi wengi waumma hapa nchini kwa muda mrefu Serikali ilifanya utafiti
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
165
wa kuona jinsi gani mifuko hiyo inaweza kuunganishwa nanini faida zake, lakini pia kuwashirikisha wadau mbalimbaliwakiwemo wafanyakazi wenyewe kupitia majukwaa auvyama vyao, waajiri na hata baadhi ya idara za Serikali,kupeleka Waraka wa Baraza la Mawaziri pamoja na kuandaaMuswada wa Sheria wa kuunganisha Mifuko ya Hifadhi yaJamii na kuunda Mifuko miwili kama ilivyokwisha kuelezwahapo awali. Muswada huo ulisomwa kwa mara ya Kwanzambele ya Bunge lako Tukufu siku ya tarehe 17 Novemba, 2017.
3.0 DHUMUNI LA MUSWADA NA UUNGANISHWAJIWA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII
Mheshimiwa Spika, Muswada wa Sheria ya Mfuko waHifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma wa Mwaka 2017(The Public Service Social Security Fund, 2017) unalengakupendekeza kutungwa kwa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi yaJamii kwa Watumishi wa Umma kwa malengo ya kutoamafao ya hifadhi ya jamii kwa watumishi walio katikaUtumishi wa Umma na kufuta sheria ya Mfuko wa mafao yaHitimisho la kazi kwa Watumishi wa Umma, Sura 407 Sheriaya Mfuko wa Pensheni wa LAPF, Sura 407 Sheria ya Mfuko waPensheni wa PPF, Sura 372 na Sheria ya Mfuko wa Pensheniwa GEPF, Sura 51 kwa ajili hiyo. Aidha, Muswadaunapendekeza pia marekebisho katika Sheria ya Mfuko waTaifa wa Hifadhi ya Jamii kwa madhumuni ya kuwekamasharti kuhusu mafao ya hifadhi ya Jamii kwa watumishiwalio katika sekta binafsi.
Mheshimiwa Spika, Nchi yetu imekuwa ikitimizamajukumu ya utoaji wa huduma ya Hifadhi ya Jamii kwawatumishi wa Umma na Watumishi walio katika Sekta binafsikupitia mifuko mbalimbali kama ambavyo imetajwa hapoawali kwa maana ya PSPF, LAPF, GEPF pamoja na PPF kwamujibu wa Sheria za uanzishwaji wake na NSSF kwa watumishiwalioko katika sekta binafsi.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa maelezo ya Serikalina uchambuzi uliofanywa na Kamati imebainika kwamba,kuunganishwa kwa Mifuko hii ya Hifadhi ya Jamii kutakuwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
166
na manufaa mengi kwa wanachama wa mifuko hiyopamoja na Taifa kwa ujumla wake kama ifuatavyo;
3.1 Kupunguza gharama mbalimbali zauendeshaji wa Mifuko
Mheshimiwa Spika, Kwa mujibu wa Sheria ya mifukoili uweze kutoa huduma bora kwa wanachama wake lazimauingie gharama za kuendesha mfuko huo. Kwa hali ilivyosasa mifuko mitano (5) inayowahudumia wafanyakazi katikasekta zote mbili na inatoa mafao ambayo kwa kiasi kikubwayanafanana, na kwa mujibu wa mfumo wa uendeshaji wakila mfuko unapaswa kuwa na mfumo wa kitaasisi ambapomifumo hiyo inapelekea gharama kubwa za uendeshaji wamifuko husika. Kwa sasa nchi yetu ina mifuko mitano (5) kamaambavyo imetajwa hapo awali na mifuko hiyo ilikuwainatumia kiasi kisichopungua shilingi Bilioni 235.8 kwa mwakakwa ajili ya uendeshaji wa mfuko husika kwa wanachamakatika ofisi za kanda na mikoa.
Mheshimiwa Spika, Kamati imebaini kwamba kwakuunganisha mifuko hiyo gharama nyingi zitapunguazikiwemo gharama zifuatazo;
i) Kupungua kwa idadi na gharama ya Bodiya wadhamini
Mheshimiwa Spika, Sheria zinazoisimamia Mifuko hii ilitoamasharti ya kuanzishwa kwa bodi ya wadhamini kwa kilamfuko. Kamati imebaini kwamba katika uendeshaji waMifuko hii kila mfuko ulikuwa na bodi yake ya wadhaminiyenye wajumbe wasiopungua tisa (9), kwa mantiki hiyo kwamifuko yote wajumbe waliopo ni takribani 45. Wajumbehawa wanapaswa kulipwa kila baada ya miezi mitatu (3)ada ya ujumbe (Directors Fees) pamoja na gharama nyinginekwa mujibu wa miongozo ya Msajili wa Hazina, ambapogharama za bodi hizi zilikuwa ni kubwa ikilinganishwa nauhalisia. Jedwali namba 1 linaonesha gharama za uendeshajiwa bodi ya udhamini kwa kipindi cha miaka mitatu (3)kuanzia Mwaka wa Fedha wa 2013/2014 hadi 2015/2016.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
167
Jedwali Na. 1Gharama za uendeshaji wa Bodi ya Wadhamini kwa
Mwaka 2013/2014 hadi 2015/2015 (Tsh.Bilioni)
Chanzo: Taarifa ya SSRA
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa jedwali lamatumizi ya fedha kwa bodi ya wadhamini kwa mifuko yotemitano (5) ni kiasi cha shilingi Bilioni 1.67 kwa mwaka kwawajumbe wasiozidi 45 kama ada ya ujumbe wa bodi namalipo mengine. Ambapo baada ya Kamati kufanyauchambuzi wake wa kina ikabaini kwamba, katika mifukoinayounganishwa (Mifuko minne) ili kupata mfuko wa Hifadhiya Jamii wa watumishi wa umma, Bodi ya wadhamini kwawajumbe wake 36 ilikuwa inatumia kiasi cha shilingi Bilioni4.46 kwa wastani wa kiasi cha shilingi Bilioni 1.115 kwamwaka kwa ajili ya kuhudumia Bodi ya wadhamini yenyewajumbe watano (9) kwa kila mfuko.
Mheshimiwa Spika, Kwa kuunganisha mifuko hiiitapunguza gharama za Bodi ya wadhamini kwani katikamifuko hiyohiyo kumekuwa na utofauti mkubwa wa gharamakati ya bodi moja na nyingine. Kwa mfano mwaka 2014/2015mfuko wa LAPF ilitumia kiasi cha shilingi Bilioni 1.8 wakatimfuko wa GEPF ilitumia kiasi cha shilingi Bilioni 0.3 tofauti yashilingi Bilioni 1.5 sawa na asilimia 83.3 kwa gharama zauendeshaji wa Bodi ya wadhamini, Kamati ilijiuliza je,miongozo kutoka kwa Msajili wa Hazina ya usimamizi nauendeshaji wa Bodi za mifuko ya Hifadhi ya jamii ni tofautikulingana na aina ya mfuko? Na je, majukumu ya Bodiyanatofautiana kati ya mfuko mmoja na mwingine?
M F U K O L A P F P P F P S P F N S S F G E P F W A S T A N I
M W A K A G H A R A M A Z A U E N D E S H A J I Z A K ILA
M F U K O
2 0 1 3 /2 0 1 4 0 .8 1 .9 1 .4 3 .6 0 .3 1 .0 6
2 0 1 4 /2 0 1 5 1 .8 2 .6 1 .8 3 .9 0 .3 2 .0 8
2 0 1 5 /2 0 1 6 1 .5 1 .6 1 .7 4 .2 0 .4 1 .8 8
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
168
Mheshimiwa Spika, Kamati inaendelea kusisitizakwamba hii ilikuwa ni gharama kubwa sana kwa bodi hizona ikumbukwe kwamba hizi ni fedha za wanachama nafaida inayopatikana kutokana na uwekezaji wa fedha zawanachama hao katika miradi mbalimbali. Kamati ilionagharama hizi ni kubwa na utofauti wake ni mkubwa, hivyobasi kwa ajili ya kupunguza gharama hizo Kamati inaungamkono hoja ya Serikali ya kuunganisha mifuko hiyo mine (4)na kuwa mfuko mmoja na mfuko wa NSSF kwa ajili yawatumishi wa sekta binafsi.
ii) Kupungua kwa gharama za menejimenti yaMifuko
Mheshimiwa Spika, Kamati imebaini kwamba,maamuzi ya Serikali kuunganisha mifuko hii ya Hifadhi ya Jamiikutoka Mifuko Mitano (5) hadi miwili kutapunguza gharamaza uendeshaji katika suala zima la menejimenti. Kwa kuwepomifuko mitano ya hifadhi ya jamii ilikuwa inalazimu kila mfukokuwa na timu yake ya menejimenti ambapo kila mfukoulikuwa na timu yake ya uongozi akiwemo Mkurugenzi Mkuuna wastani wa wakurugenzi wa Idara mbalimbali sita (6) kwaajili ya uendeshaji wa mfuko husika. Kwa uwepo wawakurugenzi hao ambao ni wajumbe wa menejement kilamjumbe alistahili kupata mshahara na stahiki mbalimbali kwamujibu wa sheria za mifuko husika, rejea Jedwali namba 2.
Jedwali Na. 2Mishahara na stahili za viongozi wa Menejimenti (Tsh.
Bilioni)
Chanzo: Taarifa ya SSRA
M FU K O LA P F P PF PSP F N SSF G EP F W A STA N I K W A M W A K A
M W A K A G H A R A M A ZA U EN D ESH A JI K W A K ILA M FU K O
2 0 13/20 14 1 .7 3 .7 2 .8 7 .3 0 .5 3 .2 0
2 0 14/20 15 3 .6 5 .2 3 .5 7 .8 0 .7 4 .1 6
2 0 15/20 16 3 .1 3 .1 3 .4 8 .4 0 .9 3 .7 8
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
169
Mheshimiwa Spika, matumizi ya fedha yamenejimenti kwa wajumbe wake, mishahara na stahili katikamifuko hii mitano ilikuwa ni makubwa na ambayo yalikuwayanapanda kila mwaka, mathalani, mfuko wa LAPF mwaka2013/2014 ilitumia kiasi cha shilingi Bilioni 1.7 ikilinganishwana mwaka 2014/2015 ambapo mfuko ulitumia kiasi cha shilingiBilioni 3.6 ambalo ni ongezeko la shilingi Bilioni 1.9 sawa naasilimia 52.7 kwa mwaka huo. Aidha, mifuko yote matumiziya menejimenti kwa mwaka wa fedha 2013/2014 hadi Mwakawa Fedha wa 2014/2015 gharama za uendeshaji wa ilikuwani kwa wastani wa shilingi Bilioni 0.96 ambayo sawa naasilimia 23 ya ongezeko ikilinganishwa na matumizi yamenejimenti kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014.
Mheshimiwa Spika, Kamati inaona matumizi haya nimakubwa sana na hakuna sababu ya kuendelea kuwa namifuko mingi ambayo kimsingi haina tija kwa wanachamana taifa kwa ujumla, kwani fedha hizo zilizokuwa zinatumikani michango ya wanachama ambao wanajiwekea akibayao ya maisha kwa dhana ya hifadhi ya jamii.
iii) Kupunguza gharama za kuendesha ofisi zaMikoa na Kanda
Mheshimiwa Spika, mujibu wa uendeshaji wa mifukohii ya hifadhi ya jamii inayopendekezwa kufutwa na sheriahii, ili kufanikisha utekelezaji wa utoaji wa huduma bora kwawanachama wake mifuko ilianzisha ofisi mbalimbali ikiwemoza Kanda na Mikoa. Kwa mujibu wa taarifa za msimamiziwa mifuko ya hifadhi ya jamii mifuko yote ina jumla ya ofisi114 zinazojumuisha ofisi za makao makuu, kanda, mikoa nawilaya. Mifuko yote ina ofisi katika mikoa ya Dar es salaam,Arusha, Mwanza, Tanga, Mbeya na Iringa. Aidha, mifuko yaNSSF, LAPF, GEPF na PPF ina ofisi katika mikoa yote na baadhiya wilaya nchini.
iv) Kupunguza gharama za mifumo ya Tehama
Mheshimiwa Spika, Kati ya gharama nyingi zauendeshaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii ni pamoja na eneo
M FU K O LA P F P PF PSP F N SSF G EP F W A STA N I K W A M W A K A
M W A K A G H A R A M A ZA U EN D ESH A JI K W A K ILA M FU K O
2 0 13/20 14 1 .7 3 .7 2 .8 7 .3 0 .5 3 .2 0
2 0 14/20 15 3 .6 5 .2 3 .5 7 .8 0 .7 4 .1 6
2 0 15/20 16 3 .1 3 .1 3 .4 8 .4 0 .9 3 .7 8
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
170
la Tehama kwa ajili ya uendeshaji wa mifuko hiyo. Kwakuunganisha mifuko hii kutaweza kupunguza gharama zakulipia mifumo hiyo ya Tehama kwa zaidi ya asilimia 60. Nimatumaini ya Kamati kwamba, mifuko hii ikiunganishwagharama zilizoainishwa hapo awali na nyingine nyingizitaendelea kupungua na kuweza kuimarisha maisha yamifuko hii.
v) Kupunguza Gharama za Ushindani
Mheshimiwa Spika, kamati ilibaini kwamba, mfumowa sasa unaruhusu kufanya ushindani kwa ajili ya kujipatiawanachama. Ili mfuko husika uweze kumudu ushindani huoulikuwa unalazimika kufanya matangazo kwa njiambalimbali za habari kama vile matangazo ya Televisheni,machapisho ya vipeperushi, matangazo ya radio na hatakuandaa makongamano yaligharimu fedha nyingi za mifuko.Kwa mujibu wa kumbukumbu za msimamizi wa mifuko yahifadhi ya jamii, kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 kila mfukoulitumia kiasi cha shilingi Bilioni 1.0 katika ushindani wakujitafutia wanachama. Kamati ina maoni kwamba kwakuunganisha mifuko hii dhana ya ushindani baina ya mifukoitapungua kama siyo kuondoka kabisa na kupunguzagharama za kujinadi ili kuvutia wanachama.
Mheshimiwa Spika, Kamati inasisitiza kwamba,pamoja na dhana ya ushindani kuondoka kutokana nauunganishwaji wa mifuko hii, ni muhimu Serikali ikatambuakwamba dhana ya ushindani itaendelea kuwepo katikamifuko hii miwili ya hifadhi ya jamii, kwani kuna wananchiwengine ambao hawapo katika sekta ya binafsi au sekta yaumma watapenda kujiunga na mifuko hiyo kwa mfumo wauchangiaji wa hiari (Supplementary Schemes) ambapomfumo huu unaruhusu mwananchi kuchagua mfukoaupendao na kuchangia kwa hiari.
3.2 Kupunguza kwa Migogoro baina ya Mifuko
Mheshimiwa Spika, kutokana na utitiri wa mifuko yahifadhi ya jamii ilipelekea hali ya mifuko hiyo kuingia katika
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
171
migogoro ya kugombaniana wanachama kutokana nabaadhi ya wanachama kuandikishwa katika mfuko zaidi yammoja na kupelekea usumbufu mkubwa wakatimwanachama huyo anapostaafu na kuanza kufuatiliamafao yake. Na kwakuwa mifuko hii ilikuwa inafanya kazikipekee (Independent Operation) bila kuingiliana na mfukomwingine kimfumo wa uendeshaji, hivyo kupelekea baadhiya wanachama kukosa stahiki zao kama mwanachamahalali wa mfuko.
Mheshimiwa Spika, Kutokana na changamoto hii,Mamlaka ya usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA)imekuwa ikilazimika kuendesha zoezi la uhakiki (Re-concilliation) wa michango ya wanachama ambalo nalolilikuwa linatumia gharama kubwa na kusababisha ongezekola gharama hizo katika gharama za uendeshaji wa mifuko.Hivyo basi, ni dhahiri kuwa uunganishwaji wa mifuko hiikutaondoa changamoto ya wanachama kujiandikisha katikamifuko mingi ambayo ingeweza kuleta migogoro wakati wautekelezaji wa utoaji wa huduma kwa ufanisi mkubwa.
3.3 Uboreshaji na uimarishaji wa huduma kwawanachama
Mheshimiwa Spika, Kamati imebaini kwamba,kuunganishwa kwa mifuko hii kutapelekea huduma kwawanachama kuwa bora na imara kwa mujibu wa Sheria,Kanuni na Miongozo iliyopo na itakayoendelea kutolewa naMamlaka kuhusu utoaji wa huduma hizo kwa wateja wamfuko. Sheria hii inayopendekezwa imeainisha vifungumbalimbali vinavyolinda maslahi ya mwanachama ikiwa nipamoja na Kifungu cha 20 cha Muswada kinachoainishamasharti ya kuzuia mwanachama wa mfuko kuhusishwa naucheleweshwaji wa michango yake ambalo ni jukumu lamuajiri kuhakikisha michango ya mwajiriwa wakeinapelekwa katika mfuko kwa wakati na badala yake muajiriachukuliwe hatua.
Mheshimiwa Spika, katika kuboresha huduma kwawanachama, Kifungu cha 43(3) kinampa haki kamili
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
172
mwanachama kuweza kudai kulipwa fidia na mfuko endapomfuko huo utamcheleweshea stahiki yake ya mafao ndaniya siku sitini (60) na kubainika kwamba ucheleweshaji huohaujasababishwa na mwanachama bali ni mfuko husika.
Mheshimiwa Spika, pamoja na vifungu hivyo Sheriaya Msimamizi wa mIfuko ya Hifadhi ya Jamii imeboreshwa ilikuipa mamlaka uwezo wa kuchukua hatua stahiki kwawatumishi wa mfuko ambao watakiuka masharti ya Sheriana maelekezo ya mamlaka, kwa kufanya haya yote hudumakwa wateja wa mfuko hazitaathirika kwa namna yoyote ile.
Mheshimiwa Spika, kutokana na manufaa hayoyaliyoainishwa na Kamati yakiwemo kuwepo kwa taarifa zawanachama wa nchi nzima katika mifumo miwili tu badalaya kutawanyika katika mifumo mitano (5), kupungua kwagharama za uendeshaji wa mifuko, kuondoa dhana yaushindani uliokuwa unajitokeza ambao kwa wakatimwingine ulikuwa hauna tija kwa wanachama na hata nchi,Kamati imebaini kwamba, Sekta ya Hifadhi ya Jamii itawezakudhibitiwa na kusimamiwa kwa urahisi, kuboresha uwekezajiutakaotokana na fedha za Hifadhi ya Jamii, kumalizamalalamiko ya wanachama kutokana na sababumbalimbali na kuwapa uhakika wa maisha wafanyakaziwakati na baada ya ajira zao kukoma kwa sababu yoyoteile, hoja ya kuunganisha mifuko hii ni njema kabisa kama tuitasimamiwa ipasavyo.
4.0 UCHAMBUZI WA MUSWADA
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 84 (2)ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la Januari 2016, mnamotarehe 17 na 18 Januari, 2018 Kamati ilifanya Mkutano naWadau kwa lengo la kupokea Maoni yao (Public Hearing) ilikuisadia Kamati katika Uchambuzi wa Muswada huu.
Mheshimiwa Spika, Wadau mbalimbali walifikakatika Mkutano huo Wadau hao ambao walifika mbele yaKamati ni pamoja na National Organization for Legal Aids,Legal and Human Rights Centre (LHRC), Chama cha
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
173
Wanasheria Tanzania (Tanganyika Law Society (TLS), Chamacha Walimu Tanzania (CWT), Chama cha Waajiri Tanzania,Chama cha Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Chama chaWahariri wa Vyuo Vikuu Tanzania (THTU), Shirika la Kazi Duniani(ILO), Aidha Wadau wengine walitoa maoni yao kwamaandishi wakiwemo Chama cha Wanasheria wanawake(TAWLA) na Chama cha wafanyakazi wa mahakama walitoamaoni yao kwa njia ya maandishi ambayo yamesaidia Kamatikuboresha Muswada huu na kuiwezesha Kamati kutoa maonina ushauri unaotolewa leo.
Mheshimiwa Spika, kutokana na hoja nzitozilizoibuliwa na Kamati wakati wa majadiliano, Serikaliiliiomba Kamati siku ya tarehe 19 Januari, 2018 ambayoilikuwa ni siku ya kufanya mashauriano na Serikali kupataushauri elekeze (Consultation) ili kuwa na dhana ya uwajibikajiSerikalini (Collective Responsibility) na Kamati ikaona ni busarakuwapa nafasi hiyo ili kupata majibu sahihi na yenye kujengakutoka kwao kwa muktadha mzima wa Muswada huu.
Mheshimiwa Spika, kwa kibali chako, uliiruhusuKamati kuendelea na kazi kwa siku ya Jumamosi tarehe 20Januari, 2018 ili kufanya mashauriano na Serikali kwa lengola kuzingatia maoni ya Kamati na Maoni ya wadaumbalimbali yaliyotolewa kwa ajili ya maboresho na ambayoKamati iliona ni mazuri kwa ajili ya uboreshaji wa Mfuko waHifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma.
Mheshimiwa Spika, napenda kulieleza Bunge lakoTukufu kuwa, katika mashauriano ya hoja mbalimbalizikiwemo zile zilizohitaji ushauri elekezi Serikali ilikubaliana naKamati kwamba marekebisho yote yatawasilishwa na Serikalikwenye Jedwali la marekebisho (Schedule of Ammendments)kama Kamati ilivyokuwa imependekeza.
Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru sana wewe,kwa kuisaidia Kamati kutekeleza wajibu wake naninaipongeza Serikali kwa kuwa wasikivu na kupokeaMaoni, Ushauri na Mapendekezo yaliyotolewa na Kamati na
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
174
kuyapokea kwa ajili ya kuyafanyia kazi. Ni imani yanguna Kamati nzima kwamba, tumeisaidia Serikali na wananchiwa Tanzania katika kuiboresha Sheria hii ambayo ipo katikamchakato wa kutungwa kwa ajili ya manufaa yawafanyakazi wa nchi hii.
Mheshimiwa Spika, naomba pia kuchukua fursa hiikumshukuru na kumpongeza sana Mheshimiwa JenisterMhagama Waziri, kwa namna ambavyo amekuwa akitoaushirikiano wa dhati kwangu mimi pamoja na Kamati nzima,kwa jinsi alivyokuwa msikikivu, muelewa na hata paletulipohitaji ufafanuzi wa Serikali Mheshimiwa Waziri alitoabila kusita wakati wa kuuchambua na kuujadili muswadahuu. Kwakweli Mheshimiwa Jenister ni mfano wa kuigwa,hongera na asante sana.
5.0 MAONI, MAPENDEKEZO NA USHAURI WAKAMATI
Mheshimiwa Spika, napenda kutoa Maoni, Ushaurina Mapendekezo ya Kamati kama ifuatavyo kwa lengo lakuboresha Muswada huu:-
5.1 MAONI KUHUSU VIFUNGU
a) Mheshimiwa Spika, Kamati imebaini makosaya uchapaji na sarufi (spelling and grammatical errorrs) nainashauri Marekebisho yafanyike kwenye maeneo yote yenyemakosa hayo ili kuweka maana stahiki katika vifungu hivyovilivyoonekana kuwa na makosa ya kiuchapishaji.
b) Mheshimiwa Spika, Kamati inapendekezaKifungu cha 3 kuhusu Interpretation kufuta neno “leader”katika maana ya neno “qualifying period” na badala yakekuweka neno “member”. Aidha, katika kifungu hicho hichoKamati inashauri kufuta marejeo namba 87 katika maanaya neno “transition period” na badala yake kitumike kifungunamba 86 ili kuondoa makosa ya kiuchapaji.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
175
c) Katika Kifungu cha 3 cha tafsiri ya manenombalimbali “Interpretation” iongezwe neno “Parliamentaryservice” katika maana ya “public services” ili kutambuaUtumishi wa Bunge kuwa ni mtumishi wa Umma na nimwanachama wa mfuko huu unaopendekezwa kuanzishwa.Aidha, kuongezwe tafsiri ya maneno kama vile “SpecialLumpsum”, “Pension”, unemployment benefit, “funeral benefit”na “sickness benefit” ambayo yametumika na hayajapatiwatafsiri yake katika orodha ya maeneo yaliyotafsiriwa katikaMuswada huu. Aidha, kamati inashauri maneno hayayapatiwe tafsiri pia zijumuishwe katika Kanuni ambazozitatungwa na Waziri mwenye dhamana kwa ajili yautekelezaji wa Sheria hii.
Kamati inapendekeza pia neno “Month” tafsiriiliyopewa iboreshwe kwakuwa siyo miezi yote ina sikuthelathini (30) kama ilivyotafsiriwa, kuna mwezi ambao sikuni ishirini na nane (28), ishirini na tisa (29) na mingine mpakasiku thelathini na moja (31). Kamati ianapendekeza isomeke“Calendar Month or a written calendar” badala ya “a periodof thirty days consecutively” kama ilivyotafsiriwa katikaMuswada.
Mheshimiwa Spika, katika kifungu hicho hicho cha 3katika tafsiri ya neno qualifying pensionable service kunaneno continuous katika vipengele vyote yaan “a” na “b”,kwakuwa mwanachama anaweza akawa hajafanya kazikwa kipindi fulani kutokana na sababu mbalimbali nabaadae akarejea kazini katika sekta ya umma au katika sektabinafsi, ambapo atakapofikia umri wa kustaafu akawaanastahili kulipwa mafao yake kwa kujumlisha mudaaliotumikia na kuchangia katika mfuko wa hifadhi ya jamii.Aidha, katika tafsiri ya neno “Totalization” neno “fullycontributed” lifafanuliwe ili lisiweze kuleta mkanganyiko naliweze kueleweka sawasawa.
Mheshimiwa Spika, Katika tafsiri ya neno “Salary”Kamati inashauri neno hilo litafsiriwe vyema na ikiwezekanatafsri inayotumika na Msimamizi wa mifuko ya hifadhi ya jamii(SSRA) itumike. Kamati inashauri malupulupu mengine kama
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
176
vile posho zisijumuishwe katika tafsiri hiyo kwani posho hizohubadilika mara kwa mara kadiri inavyoonekana inafaa.Aidha, Kamati inashauri pia maneno “Employers Association”na “Employees Association” yaongezwe katika orodha yatafsiri ya meneno mbalimbali ili kutambua na kuweka bayanamaana ya vyama hivyo vya waajiri na waajiriwa.
Mheshimiwa Spika, katika orodha ya tafsiri yamaneno kuna neno la “full pension” kwa kuwa tafsiri hiyohaijakamilika kama ambavyo imetafsiriwa na Sheria ya SSRA.Kamati inashauri tafsiri hiyo izingatie tafsiri itakayorejewakatika kanuni za ukokotozi zitakazotengenezwa kwa ajili yautekelezaji wa Sheria hii. Aidha, neno “Actuarial valuation”limepewa tafsiri yake katika orodha ya maneno na limetumikakatika kifungu cha 91(a)(i) kwa maana tofauti na tafsiriiliyopo katika orodha ya maneno. Kamati inashauri tafsiri hiyoiangaliwe upya ili kuondoa mkanganyiko unaowezakujitokeza katika matumizi yake.
Mheshimiwa Spika, katika tafsiri ya neno “qualifyingperiod” Kamati inapendekeza neno “leader” lifutwe nabadala yake litumike neno “member” ili kufanya marekebishoya kiuandishi na kuleta tafsiri sahihi kwa kuwa wachangiajiwa mfuko huo wa hifadhi ya jamii wote wanatambulikakama wanachama (members) na siyo kiongozi.
Aidha, katika tafsiri ya neno “transition period”kumefanyika marejeo ya kifungu cha 87 kinachozungumzia“provision regarding employees Cap.298, Kamati inashauriibadilishwe na badala yake marejeo yafanyike katika kifungucha 86 ambacho kinazungumzia “Transition Period”.
d) Kifungu cha 6 kinachohusu “Establishment ofthe Fund” katika Kifungu kidogo 6(1)(c) Kamati inashaurikifutwe na kiandikwe upya ili kuondoa mkanganyiko uliopokatika kifungu hicho tajwa na kifungu cha 80(2) na 105 vyamuswada huu.
e) Kifungu cha 15 kinachohusu “Appointment ofthe Director General” wa mfuko huu, Kamati inashauri kifutwe
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
177
na kuandikwa upya ili masharti yake yaweze kumuondoaMkurugenzi huyo kabla ya kipindi chake cha miaka mitano(5) kuisha kwa mujibu wa Sheria. Aidha, Sheria iainishe vipindivya Mkurugenzi Mkuu kushika wadhfa huo yaana kwa vipindiviwili tu (two terms) kulingana na utendaji bora wa kazi yakepamoja na masharti mengine kuzingatiwa.
f) Kifungu cha 16(2) kinachohusu “Other staffof the Fund” Kamati inashauri maneno yanayosomeka “undersubsection (2) yafutwe kwani hayana msingi wowote kuwepokatika kifungu hicho kwakuwa kinachoainishwa kipo katikakifungu hicho hicho kidogo.
g) Kifungu cha 18 kinachohusu “Contributions”Kamati inapendekeza kufuta maneno yanayosomeka “suchamount as the Minister may, by order in the Gazette,determine” kwakuwa Waziri mwenye dhamana na Mfuko waHifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma amepewaMamlaka makubwa ambayo yanaweza kutumika vibayadhidi ya michango ya wanachama na hasa maamuziambayo yanaweza kuwa kandamizi kwa watumishi waumma.
Mheshimiwa Spika, katika Kifungu cha 18(8) Kamatiinapendekeza kuondoa neno “May” na kuweka neno “Shall”ili kuweka masharti kuwa endapo Bodi itajiridhisha kwambamichango ya mwanachama ilikatwa na mwajiri hakupelekakatika mfuko basi Bodi ilazimike kuingiza michango hiyokatika mfuko wa mawanachama na gharama hizo ziwe juuya mwajiri pamoja na adhabu kwa mujibu wa sheria hii.
h) Kifungu cha 19 kinachohusu “Additionalcontributions for delayed remittance of contributions byemployer” kifungu 19(1) kina mkanganyiko na kifungu 18(3)katika kuainisha nani ni mwajiri, Kamati inashauri kifanyiwekazi ili kuondoa mkanganyiko huo. Aidha, katika kifungu hichorejea ifanyike katika Kifungu cha 18(6) badala ya kifungu cha21(2) kama ilivyo katika muswada ili kuondoa makosa yakiuchapaji. Aidha, kiongezwe kifungu cha 19(3) kinachowekasharti la Mkurugenzi wa mfuko kulazimika kutoa taarifa kwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
178
mwanachama kila ifikapo mwisho wa mwaka wa fedha waSerikali yaani mwezi Juni.
i) Mheshimiwa Spika, Katika kifungu cha 19kinachohusu “Additional contributions for delayed remittanceof contributions by employer” Kamati inapendekezakiongezwe kifungu cha 19(3) na kisomeke kama ifuatavyo,“The Director General shall make available to each membera statement of his contributions at the end of each financialyear”. Kamati iina maoni kuwa ni vyema kuweka sharti hili ilikuhakikisha linakuwa ni jukumu la Mkurugenzi wa mfukokuwapa wanachama taarifa za michango yao kila mwishowa mwaka badala ya kusubiri maombi kutoka kwamwanachama kama ambavyo inapendekezwa katikaMuswada.
Mheshimiwa Spika, Kwa kuweka sharti hili kutasaidiakuwapa taarifa wanachama wa mfuko kila mwaka nakupunguza usumbufu na malalamiko yanayotokana namwajiri kutopeleka michango ya mwanachama kwa wakatina kupelekea mtumishi anapostaafu kuanza kusumbukakupata haki yake ya msingi ya uzeeni aliyoitumikia kwa miakamingi katika utumishi wake.
j) Kifungu cha 29 (1) kinachohusu “Benefitspayable” Kamati inashauri iongeze aina mbili ya mafaokutoka nane (8) yanayotolewa na mfuko hadi kufikia kumi(10) baada ya kuongeza fao la elimu (education benefit) naFao la mkono wa kwaheri (gratuity benefit).
k) Kifungu cha 33 kinachohusu “Invaliditybenefit” kamati inashauri Serikali ifafanue vizuri ili kiwezekueleweka katika sheria hii na pia masharti ya kustahili kulipwayaondolewe, kwani kil ivyoandikwa sasa kinaletamkanganyiko wa mtumishi ambaye amepata ulemavu kazinina hakutarajia kupata ulemavu huo chini ya muda ambaoanastahili kulipwa fao hilo.
l) Kifungu cha 37 kinachohusu “Survivorsbenefits” kifungu 37(1) (a) na (b) katika vifungu hivyo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
179
ametajwa mjane “widow” kama mnufaikaji wa mafaoendapo mume wake aliyekuwa mwanachama atafariki basiataendelea kunufaika na uchangiaji wa mume wake nakipengele hicho hakijamtambua mgane (widower) aliyefiwana mke wake ambaye alikuwa mwanachama wa mfukokuendelea kunufaika. Kamati inashauri liongezwe neno“widower” ili mgane aweze kutambulika na sheria hii kamammoja wa wanufaika endapo mkewe atafariki.
m) Kifungu cha 38 kinachohusu “Basis andduration of survivors pension” Kamati inashauri kifanyiwemarekebisho ya utambuzi wa umri wa mtoto na kuongezakutoka miaka 15 hadi miaka 18 ambayo inatambulika nasheria ya mtoto. Aidha, wanufaika wote kwa maana yamgane, mjane au mtoto walipwe mafao kwa kutumiakanuni kama ilivyo kwa mwanachama wa mfuko kwa kuwaangekuwa hai angenufaika kwa kutumia kanuni husika yamfuko ambayo itawekwa kwenye Kanuni za sheria hii.
n) Kifungu cha 40 kinachohusu “Pensions, gratuityand allowances for persons holding certain public office”Mheshimiwa Spika , Kamati inapendekeza viongoziwaliotajwa katika kifungu hiki aongezwe Katibu wa Bunge(Clerk of National Assembly) kwenye orodha ya viongoziwanaopata mafao maalum kwa kuwa nafasi hiyo ni nafasiya kikatiba kama ilivyoainishwa katika Katiba ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 Ibara ya 87 (1)ambapo imetamka uwepo wa Katibu wa Bunge. Aidha,Katika kifungu hiki kuongezwe neno “ and Security” kati yaneno “Intelligence” na neno service ili kuweza kurekebishajina la Mkurugenzi wa Idara ya Intelijensia kuweza kuletamaana sahihi ya Cheo hicho katika sheria hii.
o) Kifungu cha 47 (2)(c) kinachohusu “Prohibitionon cession and attachment of benefits”, Kamati inashaurikiangaliwe upya il i kuondoa ubaguzi wa jinsi kwanikimemtaja mke na kuacha mume. Aidha marekebishoyafanyike ili kumtambua mnufaikaji pasipo kuainisha jinsi yamnufaika.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
180
p) Kifungu cha 56 kinachohusu “Excemption fromTax” Kifungu hiki kimeelezea ukatwaji wa kodi lakini kamatiina maoni kuwa kifungu hiki hakijawekwa sawa kwakuwahakifafanui kuwa nani atapaswa kukatwa kodi hiyo ni mfukoau michango ya mwezi au mafao ya mkupuo anayolipwamwanachama. Aidha, Serikali ikakiandike upya kifungu hikiili kiweze kuainisha kwamba atakayekatwa kodi ni mfukokutokana na uwekezaji wake kwa kutumia fedha zawanachama na kodi hiyo isikatwe kwa mwanachama wamfuko.
q) Kifungu cha 57(4) kati ya vifungu vinavyohusu“Actuarial Valuation Report” Kamati inashauri neno “may”lifutwe na kuweka neno “shall” ili kuweza kuwa na sharti lalazima kwa mamlaka ya usimamizi wa mifuko kuchukuahatua stahiki kwa ajili ya kurekebisha mapungufu yaliyobainikakwenye taarifa ya mtaalamu wa uthamini wa hali halisi yamifuko (Actuarial Valuation) ya hifadhi ya jamii. Kwa kubakihivyo, mamlaka inapewa mwanya wa kuamua kuchukuahatua au isichukue hatua.
5.2 MAONI YA JUMLA
i) Umuhimu wa SSRA kuongezewa majukumu yaUsimamizi ya Hifadhi ya Jamii
Mheshimiwa Spika, Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamiiya Mwaka 2003 ilipelekea Bunge la Jamhuri ya Muunganowa Tanzania kutunga Sheria Na.8 ya Mwaka 2008 pamojana mambo mengine ilitoa masharti ya kuanzishwa kwaMamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SocialSecurity Regulatory Authority). Pamoja na majukumumengine Mamlaka hii ya Usimamizi ilipewa jukumu lakusimamia Mifuko yote ya hifadhi ya jamii kwa kutoamiongozo ya utendaji sahihi, kusimamia utendaji wa mifuko,kutetea na kulinda maslahi mbalimbali ya wanachama,kutoa ushauri wa kisera kwa waziri mwenye dhamana, kusajiliwasimamizi wa uwekezaji wa fedha za mifuko ya jamii namajukumu mengine mengi.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
181
Mheshimiwa Spika, Kamati ina maoni kuwa, badokuna majukumu mengi na makubwa kwa Mamlaka hii yaUsimamizi wa Sekta ya hifadhi ya jamii kwa kuwa majukumuhayo bado yapo ikizingatiwa kwamba mifuko hii inakwendakuunganishwa hivyo Mamlaka inapaswa kuhakikishakumbukumbu za wanachama wa mifuko yote zinabaki kuwasahihi na huduma zinaendelea kutolewa kwa wanachamawanaostahili katika mifuko hiyo. Kuunganishwa kwa mifukohii kusiwe sababu au kigezo cha huduma kusimama. HivyoUangalizi wa SSRA ni muhimu sana kwa wakati huu kulikowakati mwingine wowote. Aidha, katika kuanza kutekelezaSheria hii, Serikali inahitaji kufanya tathmini ya hali halisi yamifuko (Acturial Valuation) yote ili iweze kuandaa kikokotoo(Formular) ambapo kazi hii inahitaji kusaidiwa na mamlakahusika ambayo ni SSRA.
Mheshimiwa Spika, Kamati inapendekeza piamasuala yote yanayohusiana na Hifadhi ya Jamii, iwekwechini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii.Kamati inaishauri Serikali kuhakikisha Mifuko ya Bima ya Afyaikiwemo Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF), Bima ya Afyaya Jamii (CHF) na mifuko mingine yenye dhana ya hifadhi yajamii iwekwe chini ya msimamizi mmoja. Kwa kufanya hivyokutaondoa mkanganyiko na unufaikaji wa mafao zaidi yamara moja ikiwemo fao la matibabu na fao la ugonjwayanayotolewa na Mfuko wa Hifadhi ya jamii na Mfuko waTaifa wa Bima ya Afya.
ii) Watumishi wanaotoka katika mifuko hiyokuwahahakikishia ajira zao
Mheshimiwa Spika, Kamati inaona kuwakuunganishwa kwa mifuko hii kutapelekea suala la ajira zawafanyakazi katika mifuko hiyo kuathirika na wenginekupoteza nafasi zao za awali na hata kupoteza ajira zaokabisa. Kamati inashauri, Wizara yenye dhamana ikishirikianana mifuko husika pamoja na Mamlaka ya Usimamizi wa Sektaya Jamii kuhakikisha wanalinda ajira za wafanyakazi haobila kujali nafasi zao za awali. Wizara ifanye tathmini ya idadiya wafanyakazi wenye sifa wanaohitajika kwa ajili ya
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
182
kuhakikisha wanabaki katika ajira na kuhakikisha uanzishwajiwa Mifuko hii unakuwa wa ufanisi mkubwa bila kuletataharuki yoyote kwa wafanyakazi na wanachama wake.
Mheshimiwa Spika, ni imani ya Kamati kuwa, kuanziasasa ofisi za mifuko hii zitakuwa hadi ngazi ya wilaya ambakowanachama wengi wapo wakiwemo walimu, wauguzi,askari na kada nyingine mbalimbali hasa kutoka katika Sektaya Umma. Hivyo basi Kamati inasisitiza watumishi wotewaliokuwa katika mifuko hiyo ajira zao zilindwe kwa mujibuwa Sheria na Kanuni za utumishi wa umma.
iii) Wanachama katika mifuko hiyo wasihame namichango yao ili kuiwezesha mifuko hiyo kujiendesha
Mheshimiwa Spika, Katika kuhakikisha mifuko hiiinakuwa na muda mrefu wa uhai wake, ni maoni ya Kamatikwamba, katika uunganishaji na usajili wa wanachama wamifuko ianze na wafanyakazi wapya katika Sekta zote mbilikwa maana kwamba, mara baada ya Sheria hii kusainiwana Mheshimiwa Rais, basi wafanyakazi watakaoajiriwa katikasekta zote mbili waanze kutenganishwa usajili wao ilimfanyakazi wa Sekta ya umma asajiliwe katika mfuko waumma na mfanyakazi wa Sekta binafsi asajiliwe katika mfukowa Sekta binafsi.
Mheshimiwa Spika, Kamati inashauri kwa wakati huu,wanachama waliopo katika mifuko hiyo minneinayounganishwa wote wabaki katika mfuko wa umma nawale waliopo katika mfuko wa NSSF waendelee kuchangiahuko bila kujali ni mfanyakazi wa Sekta gani, utaratibu huuunafahamika kama Cutt off date ya mwanachama.
Mheshimiwa Spika, Kwa kufanya hivyo, kutasaidiakuboresha uwiano wa wanachama wastaafu kutoka uwianowa 1:5 hadi kufikia uwiano wa 1:10, kutapunguza idadi yawanachama kuanza kufuatilia taarifa zao wakati wa kupatastahiki za mafao yakiwemo mafao ya uzazi na kustaafu.Aidha, sababu kubwa zaidi ni kwamba michango yawanachama hao imewekezwa katika miradi mbalimbali
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
183
iliyogharamiwa na michango yao ambapo kuwahamishana uwekezaji huo itailetea usumbufu Serikali na wanachamawake pia na kwa mfumo ulivyo makusanyo ya michangoya watumishi sasa (Current Collections) ndiyo inambeba kwakumlipa mtumishi aliyestaafu.
iv) Serikali ifafanue Fao la upotevu wa ajira(Unemployment Benefit)
Mheshimiwa Spika, Katika uchambuzi wa Muswadahuu, Kamati ilibaini kwamba katika orodha ya mafao kunafao la upotevu wa ajira (Unemployment Benefit) kwamwanachama ambaye amechangia michango kwa kipindikisichopungua miezi 18, hajaacha kazi kwa hiari pamoja namasharti mengine, atalipwa asilimia 33.3 ya mshahara wakekwa kipindi cha miezi sita (6), ambalo kimsingi Kamatiinakubaliana nalo.
Mheshimiwa Spika, Kamati inashauri fao hilolifafanuliwe vizuri ili umma uweze kuelewa kwani kumekuwana upotoshwaji mkubwa katika jamii kuwa sasa watanzaniawote waliokosa ajira watalipwa fao la ukosefu wa ajira. Hatahivyo, Kamati inashauri Serikali kubadili jina la fao hilo kuitwaFAO LA UKOSEFU WA AJIRA na badala yake liitwe FAO LAUPOTEVU WA AJIRA kwa maana kwamba mtu alikuwamwajiriwa na mwanachama wa mfuko, ila kutokana nasababu zilizokuwa nje ya uwezo wake amepoteza ajira yake.Kwa kufanya hivyo Serikali itakuwa imefuta dhana potofuiliyoko kwa wananchi ya kwamba waliokosa ajira wote kwaSheria hii wanaingizwa katika orodha ya wanufaika wamafao kupitia fao la ukosefu wa ajira.
v) Mifuko kufuatilia michango ya wanachamakwa Waajiri
Mheshimiwa Spika, Mara baada ya mwajiriwakupeleka taarifa zake kwa mwajiri na kuanza kulipwamshahara wake huanza kukatwa michango yake kwa ajiliya kupeleka katika mfuko wa hifadhi ya jamii ambalo ni
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
184
jukumu la muajiri kuhakikisha michango hiyo inapelekwakatika Mfuko husika kwa wakati. Aidha, imezoeleka kwambamuajiri ndiye anapaswa kupeleka michango hiyo na endapohaijapelekwa kwa wakati mfuko haufanyi juhudi yoyote ileya kufuatilia michango ya mwanachama wake. Hali hiiinapelekea kutengeneza mazingira ya usumbufu kwamwajiriwa wakati wa kufuatilia stahiki yake na hasa marabaada ya kustaafu na kuonekana kuna baadhi ya miezimakato hayo hayakupelekwa na mwajiri.
Mheshimiwa Spika, Kamati inashauri mifuko iwekeutaratibu wa kufuatilia michango hiyo kwa waajiri ili kifungucha kulipa faini kilichopo katika sheria hii kiweze kutumikavizuri na ikawa sehemu ya mapato kwa mfuko.
vi) Wafanyakazi wa Kampuni zenye hisa zaSerikali kuchangia katika Mfuko wa Umma
Mheshimiwa Spika, Nchi yetu imekuwa na kampuniza aina mbalimbali zile za binafsi na kampuni ambako serikaliimeingia ubia na muwekezaji. Kamati inashauri Kampuni zoteambako Serikali ina hisa zake bila kuja kiasi cha umiliki wahisa hizo, ikiwemo TBL, TCC, Airtel na Kampuni nyingine,wafanyakazi wake wote wawe wanachama wa Mfuko waHifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma. Kwa kufanyahivyo, kutaweza kuimarisha mfuko huu lakini pia kuwezakulinda maslahi ya wananchi wetu ambao ni waajiriwakatika kampuni hizo kwa kuhakikisha kwamba ni kwa kiasigani wafanyakazi wakitanzania wananufaika na Kampunihizo na kuwekewa hazina yao ya kijamii.
vii) Serikali kulipa madeni ya Mifuko
Mheshimiwa Spika, mifuko inayounganishwa kwasheria hii imekuwa ikiidai serikali madeni makubwa ya kuanziaMwaka 2000 na kurudi nyuma (Pre 1999) ilipoamua kuwalipawastaafu mafao licha ya Serikali kutopeleka mafao yawatumishi hao katika mifuko wanakonufaika nayo. Hali hiiimepelekea mifuko hiyo kuendesha kwa hasara kubwa na
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
185
madeni makubwa na wakati mwingine kuwasababishawanachama hasa wastaafu kuwekwa kwenye foleni yakusubiri pensheni zao kwa foleni. Aidha, Serikali imekuwaikchukua fedha za mifuko kwa njia ya kukopa na kufanyamiradi mbalimbali ya maendeleo kwa nchi, mikopo hiyonayo imegeuka kuwa changamoto mojawapo inayoikabiliMifuko iayounganishwa kwa Sheria hii.
viii) Kukamilisha utoaji wa fao la elimu
Mheshimiwa Spika, Katika Mifuko hii inayounganishwakwa Sheria hii, kuna mifuko iliyokuwa inatoa fao la elimukwa wanachama na hata wategemezi wa wanachama wamifuko hiyo. Aidha, kwa mujibu wa kifungu cha 29(1) chaorodha ya mafao yanayoainishwa na mfuko huu fao la elimulimeachwa na kwamba halitatolewa tena kwa wanachamawa mfuko huu. Kamati inaunga mkono hoja ya kuondolewakwa fao la elimu katika orodha ya mafao kwani sasa Serikaliinaihudumia jamii nzima ya Tanzania kwa kutoa elimu bilamalipo kwa elimu ya msingi yaani kuanzia Shule ya Msingihadi Kidato cha nne kuanzia mwaka 2016.
Mheshimiwa Spika, Kamati inashauri, Serikali, kamahaitaongeza fao la elimu, basi Serikali iruhusu mifuko hiikuendelea kutoa fao hilo la elimu kwa wale wanachamawalioko tayari katika mfumo wa kupewa fao hilo ili wawezekumalizia masomo yao badala ya kuwakatika na kuwezakukatisha ndoto zao. Ikumbukwe kwamba kuna watotoambao wamepoteza wazazi wao na kutokana na fao hilikuwepo wameweza kuendelea na masomo katika shulewalizokuwepo wakati wa uhai wa wazazi au walezi wao.
ix) Sheria iwatambue Katibu wa Bunge na MakatiWakuu wa Wizara
Mheshimiwa Spika, Katiba ya Jamhuri ya Muunganowa Tanzania imemtambua Katibu wa Bunge katika Ibaraya 87 (1) kwamba kutakuwa na Katibu wa Bunge ambayeatakatoka miongoni mwa watumishi wenye madaraka ya
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
186
juu Serikalini. Aidha, katika utendaji wa Wizara Mtendaji Mkuuni Katibu Mkuu (Accounting Officer) wa Wizara husika.
Mheshimiwa Spika, Sheria hii inayopendekezwa kwaajili ya Mfuko wa Jamii kwa Watumishi wa Umma imelengakuwapa huduma watumishi wote waliopo katika Sekta yaUmma wakiwemo Makatibu Wakuu wa Wizara ambaowanateuliwa miongoni mwa watumishi wa ummawaliohudumu kwa muda mrefu na kukatwa michango yaowakiwa watumishi katika ngazi za chini kabla ya ukatibumkuu. Aidha, Makatibu Wakuu ndiyo maafisa masurufu nani wasimamizi wa watumishi wengi walio chini yao(Subirdinates) ambao wamejumuishwa katika Mfuko waHifadhi ya jamii lakini wasimamizi wao hawajapewa fursahii muhimu sana kwa maisha yao.
Mheshimiwa Spika, Kamati inashauri sheria hiiiwajumuishe Makatibu Wakuu wote wa Wizara ili wawezekunufaika na Mfuko huu wa Hifadhi ya jamii kwa watumishiwa umma. Kwa kufanya hivyo kutaondoa dhana ya matumizimabaya ya madaraka yao kwa manufaa binafsi nakutalinda hadhi ya maisha na utu wao mara baada ya ajirazao kukoma.
6.0 HITIMISHO
Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine tena napendakuchukua nafasi hii kukushukuru wewe binafsi, kwa kunipanafasi ya kuwasilisha Maoni, Ushauri na Mapendekezo yaKamati kuhusu Muswada huu Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwaWatumishi wa Umma wa Mwaka 2017.
Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kumpongezasana Mhe. Jenister Joachim Mhagama (Mb), Waziri Ofisi yaWaziri Mkuu, Sera, Bunge, Vijana, Kazi, Ajira na Watu wenyeUlemavu Mhe. Anthony Mavunde (Mb), Naibu Waziri, Mhe.Ikupa Stella Alex, (Mb), Ndg. Katibu Mkuu, Ndg. Erick Shitindina watendaji wote wa Wizara kwa ushirikiano walioipaKamati na kuwasilisha vyema Muswada huu mbele ya Kamati
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
187
pamoja na kutoa ufafanuzi wa kina kila ulipohitajika.Namshukuru pia Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Watendajiwake kwa kazi nzuri waliyofanya ya kutoa kutoa mwongozomahiri wa kisheria wakati wote wa uchambuzi wa Muswada.
Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kuwashukurutena Wadau wote waliofika mbele ya Kamati kuwasilishaMaoni yao. Aidha, nawashukuru hata Wadau ambaowalishindwa kufika mbele ya Kamati kutokana na sababumbalimbali lakini waliweza kutuma maoni yao kwaMaandishi. Napenda kuwaeleza kuwa Michango yaoimesaidia kupata sheria hii muhimu kwa Maslahi mapana yaWatumishi wa Umma na hata Taifa.
Mheshimiwa Spika , kwa namna ya kipekeenawashukuru sana Wajumbe wa Kamati kwa kazi nzuri yenyeumahiri wakati wote wa uchambuzi wa Muswada huu.Wajumbe wamefanya kazi nzuri ya kuhakikisha uchambuziwa Muswada huu unakuwa wenye tija kwa maslahi ya Taifazima. Napenda kuwatambua Wajumbe wa Kamati yaKudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kwamajina kama ifuatavyo:-
1. Mhe. Peter J. Serukamba, Mb Mwenyekiti2. Mhe. Mussa A. Zungu, Mb M/Mwenyekiti3. Mhe. Hussein Mohamed Bashe, Mb Mjumbe4. Mhe. Peter Ambrose Lijualikali Mjumbe5. Mhe. Joseph Osmund Mbilinyi, Mb Mjumbe6. Mhe. Kasuku Samson Bilago, Mb Mjumbe7. Mhe. Lucia Ursula Michael Mlowe, Mb Mjumbe8. Mhe. Dkt. Jasmine Tiisekwa, Mb Mjumbe9. Mhe. Ahmed Ally Salum, Mb Mjumbe10. Mhe. Susan Anselm Lyimo, Mb Mjumbe11. Mhe. Juma Selemani Nkamia, Mb Mjumbe12. Selemani Said Bungara, Mb Mjumbe13. Mhe. Zitto Zuberi Kabwe, Mb Mjumbe
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
188
14. Mhe. Boniphace Mwita Getere, Mb Mjumbe15. Mhe. Bernadetha K. Mushashu, Mb Mjumbe16. Mhe. Jaku Hashim Ayoub, Mb Mjumbe17. Mhe. Grace Victor Tendega Mjumbe18. Mhe. Sikudhani Yassin Chikambo Mjumbe19. Mhe. Hussein Nassor Amar Mjumbe20. Mhe. Juma A. Juma Mjumbe21. Mhe. Sonia Juma Magogo Mjumbe22. Mhe. Nuru Awadh Bafadhili Mjumbe23. Mhe. Rehema Juma Migira Mjumbe
Mheshimiwa Spika, napenda sana kumshukuru Katibuwa Bunge Ndg. Stephen Kagaigai, Mkurugenzi wa Idara yaKamati za Bunge Ndg. Athuman B. Hussein na KaimuMkurugenzi Msaidizi wa Kamati Ndg. Chacha Nyakegapamoja na Katibu wa Kamati hii Ndg. Agnes Nkwera naMsaidizi wa Kamati Ndg. Wazir Kizingiti kwa kuratibu vyemashughuli za Kamati na kuhakikisha Taarifa hii inakamilika kwawakati. Aidha, namshukuru Kaimu Mshauri Mkuu wa Mamboya Sheria wa Bunge Ndg. Pius T. Mboya pamoja na wasaidiziwake Ndg. Leorcard Kapongwa, Ndg. Maria Mdulugu naNdg. Nesta Kawamala kwa Uchambuzi wa kisheriawalioufanya kuisadia Kamati.
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na naombakuwasilisha.
Peter Joseph Serukamba, MbMWENYEKITIJanuari, 2018
MWENYEKITI: Tunaendelea, tupokee sasa maoni yaMsemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kuhusu Ofisi ya WaziriMkuu, karibu Mheshimiwa Ester Bulaya.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
189
MHE. ESTER A. BULAYA – MSEMAJI MKUU WA KAMBIRASMI YA UPINZANI BUNGENI KWA OFISI YA WAZIRIMKUU(SERA, BUNGE, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU:Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijasoma naomba niwekerekodi sawa kwamba wazo la kuunganishwa kwa Mifukolilitoka Kambi Rasmi ya Upinzani na lilikuwa ni hoja ya mudamrefu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maoni ya Kambi Rasmi yaUpinzani kuhusu Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi yaJamii kwa Watumishi wa Umma wa mwaka 2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ni mara yanguya kwanza kwa mwaka huu wa 2018 kusimama hapa kutoamaoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu Muswadawa sheria uliopo mezani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa heshima,nichukue fursa hii kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwakutulinda sote na kutuvusha salama katika mwaka uliopitawa 2017 na kutujalia kuuona mwaka huu mpya wa 2018tukiwa salama. Kwa sababu hiyo, nakutakia wewe naWaheshimiwa Wabunge wote, kheri ya mwaka mpya.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Zaburi ya 1:1 na 3 inasemakwamba, heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasiohaki; wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. Nayeatakuwa kama mti uliopandwa kandokando ya vijito vyamaji, uzaao matunda yake kwa majira yake, wala jani lakehalinyauki; na kila alitendalo litafanikiwa. Mzaburianaendelea kusema katika mstari wa nne (4) kwamba, sivyowalivyo wasio haki, hao ni kama makapi yapeperushwayona upepo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeanza na nukuu hiyo yaBiblia Takatifu ili itutie nguvu sisi tulioonewa…
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
190
MWENYEKITI: Mheshimiwa hebu keti kidogo.
Waheshimiwa Wabunge, jana nilisema na leonalazimika kusema tena, hizi taarifa pamoja na kwambatunatoa maoni yetu lakini ni taarifa ambazo lazima zizingatieKanuni kwa kutumia lugha za kibunge. Nilisema jana nanimekusihi Mheshimiwa Ester, nimekuandikia ki-note kwambastick kwa hayo ambayo yamo kwenye hotuba hii. Paragraphhizo ambazo zimeondolewa sasa naamrisha usizisome.Baada ya hiyo uliyosoma kwenye Zaburi ufuate sasa unasemaMheshimiwa Spika, baada ya salamu hizo, endelea kuanziahapo. Karibu.
(Hapa baadhi wa Waheshimiwa Wabungewalikuwa wakiongea bila mpangilio)
MHE. ESTER A. BULAYA – MSEMAJI MKUU WA KAMBIRASMI YA UPINZANI BUNGENI KWA OFISI YA WAZIRIMKUU(SERA, BUNGE, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU:Mheshimiwa Mwenyekiti na Mtemi wangu ninayekuheshimusana, kwa sababu hutaki hata Maandiko ya Biblia niliyoya-quote niyasome na huyaamini nitaamua kuyaondoa ila mimininayaamini ndio maana nimeyaandika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya salamu hizo naquote hizo za Biblia ulizozikataa za utangulizi, sasa naombanitoe maoni ya jumla kuhusu Muswada wa Sheria ya Hifadhiya Jamii uliopo mbele yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Jamii ni haki yakila Mtanzania. Haki hii imeanishwa katika Katiba ya Jamhuriya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 11(1) na Sera ya Taifa yaHifadhi ya Jamii ya mwaka 2003. Haki hii pia imeiainishwakwenye Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Binadamu wamwaka 1948 pamoja na Mikataba ya Shirika la Kazi Duniani(ILO), Ibara ya 102 ya mwaka 1952.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
191
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi ya jamii ni haki yakila mtu na si kwa wale tu walio katika sekta iliyo rasmi, kwasababu mpaka sasa kulingana na takwimu za Sensa ya Watuna Makazi zilizotolewa mwaka 2012 ni kwamba idadi yaWatanzania wote ni milioni 44.9 ambao kati yao, ni watumilioni 1.7 tu ndio waliojiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii,hii ikiwa ni asilimia 6.5 tu ya nguvukazi yote ya watu milioni23.7.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu hizo, Tanzaniahaiwezi kujitokeza kifua mbele na kujidai kwamba jamii yakeimehifadhika. Sababu kubwa asilimia ndogo ya watuwaliojiunga na skimu za hifadhi za jamii ni ufinyu wa ajirakwa sekta za umma na sekta binafsi. Kambi Rasmi ya Upinzaniina mtazamo kwamba badala ya Serikali kung’ang’aniakuweka sheria za kupunguza na kuibana mifuko ya jamii,ingepanua fursa za ajira kwa Watanzania na kuwekamazingira wezeshi kwa sekta binafsi kuajiri kwa wingi ilikupunguza umasikini wa kipato kwa Watanzania, lakini pili,kuhakikisha kwamba wafanyakazi wanaweka akibaitakayowasaidia pindi umri wao wa kufanya kaziutakapokoma. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo yote,jambo la msingi ambalo Kambi ya Upinzani inaamini nikwamba akiba ni kitu kinachomsaidia mtu wakati wa shidaau wa matatizo na siyo kitu cha kufanikisha mazishi ya mtuhuyo baada ya kufariki kutokana na kushindwa kutatuliwakwa matatizo au shida iliyokuwa ikimkabili. Kwa sababu hiyo,Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali, pamoja naWabunge wote kwa ujumla, kuhakikisha kwamba mifukoya jamii chini ya sheria hii inaweka mazingira ya wanachamakuweza kunufaika na michango yake wakati wowoteanapopata shida kubwa kabla ya kustaafu na siyo kuwekamasharti magumu ya kumfanya mwanachama ashindwekunufaika na michango yake mpaka wakati wa kustaafu.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi kwa sababuikiwa hatutaweka utaratibu wa kumfanya mwanachama
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
192
kunufaika na michango yake wakati anapopata shida akiwahai, yamkini tunaweza kuwa tunatengeneza mazingira yakuwachangisha wanachama fedha za kuja kugharamiamazishi yao na siyo kuwasaidia kuboresha maisha yao. Hii nibayana kwa kuwa umri wa kuishi kwa Mtanzania sasa hiviunakadiriwa kuwa ni miaka 61 na takribani umri huo huomtumishi anapaswa kustaafu na kulipwa mafao yake. Kwalogic ndogo, mafao hayo ni ya kumzikia na siyo yakumtegemeza kuishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Mamlaka ya Udhibitina Uhifadhi wa Jamii (SSRA) inasema kwamba hadi Juni, 2015,Mifuko ya Hifadhi ya Jamii hapa nchini ilikuwa na jumla yawanachama 2,132,000 kufikia Juni, 2016 wanachamawaliongezeka kufikia 2,464,000. hii ni kutokana na ushindaniuliopo baina ya mifuko. Watu hao ni wale waliopo katikaajira ya sekta iliyo rasmi tu na nguvu kazi kubwa iliyobaki yatakribani 20,000,000 inashughulika na sekta isiyo rasmi na wotewako katika hali hatarishi kwa vile hawana kinga yoyote yahifadhi ya jamii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zinaonesha kuwaPPF hadi Juni, 2015 ilikuwa na jumla ya watumishi 352, PSPFilikuwa na watumishi 186, LAPF ilikuwa na watumishi 195 namifuko hiyo yote ina matawi zaidi ya kumi nchi nzima. Hapani dhahiri kwamba kutokana na kile kinachoitwa downsizingili kazi zifanyike kulingana na nafasi zitakazotengenezwa namfuko mpya wa taasisi inayoanzishwa kwa mujibu wa sheriahii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali na hilo, kunaushindani kwa mifuko kutoa mafao yanayofanana. Mfano,fao la Bima ya Afya linalotolewa na Mfuko wa Bima ya Afyana fao la kuumia ukiwa kazini linalotolewa na Mfuko Maalumwa Fidia ya Wafanyakazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuangalia mafaoyatakayotolewa chini ya sheria hii, ni dhahiri kwambaushindani wa mafao baina ya mifuko utaendelea kuondoabaadhi ya mafao na kuyaacha kwenye mifuko ambayo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
193
haijafutwa kwa mujibu wa sheria hii. Maana yake nikumzidishia mzigo wa makato mtumishi wa umma ambayemshahara wake ni mdogo, kwani inamlazimu kuchangiamifuko miwili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maelezo yaMheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya Hifadhi ya Jamiikwenye Kamati iliyochambua Muswada huu, alisema kuwapamoja na mambo mengine, ni kuboresha mafao yawanachama. Hili ni jambo jema kama litaonekana katikaMuswada huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mafao ya wanachamayanaboreshwa kwa kuwa na kikokotoo (formula)kinachojulikana na kukubalika baina ya wahusika wote kwamaana ya wanachama. Tukumbuke kuwa fedha hizo siyomali ya Serikali, bali ni mali ya wanachama na Serikali kupitiakwenye sheria hii ni mtunzaji na mwendelezaji wa fedha hizo.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Muswada umetoa kitukinachoitwa full pension na ikatolewa tafsiri yake, kwa bahatimbaya sana hiyo ndiyo ilikuwa ni kikokotoo au kanuni auformula, lakini wadau waliipinga, kwani badala ya kuboreshamafao ilikuwa inayakandamiza. Kabla ya kuunganisha mifukohii, mifuko mingi ilikuwa na vikokotoo kama vile PSPF 540 na580 kwa waajiriwa walioanza kazi baada ya 2014; LAPF 540,PPF na GEPF 580.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile moja ya sababukuu ya kuunganisha mifuko hii ni kuboresha mafao yawafanyakazi, hivyo tunatarajia sheria hii ije na kikokotoo chachini ya 540 au 580 na kionekane kwenye muswada huu washeria na siyo kwenye kanuni za Mheshimiwa Waziri na SSRA.Hivyo hatutarajii kabisa kupunguza kile kilichokuwepo badalaya kukiboresha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hoja nyingi zinajengwakuhusu uimara wa mifuko na mabadiliko ya kupunguzamafao kwa kutumia kanuni, lakini hoja hizi ni dhaifu kama
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
194
Serikali itaacha kuchota fedha za wanachama na kuwekakatika miradi ambayo haikufanyiwa upembuzi yakinifu namwisho wa siku miradi hushindwa kutoa kile kilichokusudiwakama ambavyo ilioneshwa katika taarifa ya ukaguzi wa CAGkuhusiana na utendaji wa mashirika hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa hiyo ya mwaka 2015/2016 inasema kwamba watumishi wa umma wa mwakaunaoishia tarehe 30 Juni, 2014 ilionesha kuwa mfuko una jumlaya fedha shilingi trilioni 1.3 na deni halisi lilikuwa shilingi trilioni12.46, hivyo kufanya upungufu wa shilingi trilioni 11.1. Taarifaya sasa inaonesha Mfuko wa PSPF unaidai Serikali kiasi chashilingi trilioni tatu. Madeni haya yanatokana na mikopo yamoja kwa moja, dhamana na michango ambayohaikuwahusisha kulingana na matakwa ya kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali bado ni ile ile yaCCM, je, ni kitu gani kitakachotoa uthibitisho kuwa tabiahiyo ya Serikali itabadilika katika sheria hii inayotungwa ilikuondokana na tabia yake ya kukopa moja kwa mojakwenye mifuko na kushindwa kurejesha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hili jambo la kuachamambo muhimu yanayohusu maisha ya watu kwenye kanuniambayo kwanza ni jukumu la Waziri au Serikali. Hii siyo sahihikabisa. Inatakiwa suala muhimu kwa maisha ya wafanyakazikama hili liamuliwe na Bunge zima kwa kujadiliwa na kufikiamwisho, kwani Wabunge ndiyo walinzi wa wananchiikiwemo wanachama wa mifuko ya hifadhi. Mfano, kifungucha 18(2)(b): “or such amount as the Minister may by order inthe Gazette determine...” Kifungu cha 29(2).
Mheshimiwa Mwenyekiti, hifadhi ya jamii ni kinga yamaisha kwa wanachama wake mara tu baada ya kutokakwenye ajira na mfuko uliokuwepo ambao ulikuwa unawapawanachama kuchagua kulingana na aina ya mafaoyaliyokuwa yanatolewa na mfuko husika. Hivyo basi, KambiRasmi ya Upinzani inaona itakuwa jambo la busara kamawanachama waliopo sasa katika mifuko waendelee nautaratibu walioingia nao mikataba ya kupatiwa huduma na
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
195
utaratibu mpya wa mifuko miwili uwahusu wanachamawapya au watumishi wapya katika sekta za umma na binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja hii ya wanachamakuhama na sera ya mafao waliyojiunga nayo kwenye mifukoiliyovunjwa, imepewa mwanga kidogo kwenye kifungu cha80(4) cha muswada huu, lakini bado kuna hoja, kama ndivyohivyo, ni kweli kuwa mafao yaliyokuwepo kwa mifukoinayounganishwa bado yataendelea kutolewa kwawanachama wa zamani katika mifuko mipya inayoanzishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa takwimu zilizotolewana wadau ni kwamba PPF ambayo asilimia 75 ya wanachamawake ni kutoka sekta binafsi, asilimia 25 ndiyo sekta za umma.Kwa hiyo basi, katika kuunganisha mifuko, ilitakiwa NSSF naPPF kuwa taasisi moja ambayo ingetumika kama sektabinafsi, badala yake asilimia 25 za wanachama ambao wakosekta za umma ndio wameunganishwa na wenzao katikamifuko mingine na iliyobaki, asilimia 75 wanahamishiwa NSSF.Hapa kuna shida ya kimahesabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, madhumuni ya muswadahuu unapendekeza kutunga sheria ya kutoa mafao ya hifadhiya jamii kwa watumishi walio katika utumishi wa umma nakufuta sheria zilizopo zilizokuwa zinatoa huduma hiyo kwawatumishi hao. Ni kweli kwamba Mifuko hiyo ya Pensheni yaPSPF, LAPF, GEPF na PPF, mbali ya kutoa huduma kwawatumishi wa umma, pia ilikuwa inatoa huduma kwa watuambao sio watumishi wa umma. Kwa maana nyingine nikuwa taasisi hizo zina wanachama wasiokuwa watumishiwa umma na pia kuna watumishi wa umma ambaowalikuwa ni wanachama wa NSSF.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muktadha huo, ilikuondoa mtafaruku unaoweza kujitokeza kutokana nauanzishwaji wa sheria hii, Kambi Rasmi ya Upinzani inaonakuwa muda wa mpito uliowekwa kwenye muswada huukatika kifungu cha 86 kinaweza kusababisha usumbufu nahivyo kuleta matatizo miongoni mwa wanachama, kwaniwatu wanaostaafu kila wakati na wengine tayari wako
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
196
kwenye kusubiri mafao yao. Hivyo, kwa kipindi hicho champito cha miezi sita ni wapi watatakiwa kudai aukuhudumiwa ili wapatiwe stahiki zao? Ni bora kuwekwamuda maalum wa kufanya uhamisho wa wanachama wotewanaotakiwa kuhamishwa kutoka mfuko wa awali kwendamfuko mpya ili kuondoa usumbufu ambao utajitokeza katikautekelezaji wa zoezi hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama muswadaunavyosema kuwa unafuta mifuko minne ambayo ilikuwainatoa huduma kwa watumishi wa umma na kuunda mfukommoja kwa lengo kuu la kupunguza matumizi yasiyokuwaya lazima na pale pale kuleta tija kiutendaji kwa kutoamafao na pensheni zilizolingana kwa watumishi wa umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kifungu cha (3) chamuswada kinachohusu tafsiri ya maneno mbalimbaliyaliyotumika kwenye muswada, neno “authority” au kwakiswahili “mamlaka” kwa maana iliyotolewa kuwa ni Mdhibitiwa Mifuko (SSRA) limetumika mara kadhaa katika vifungumbalimbali vya muswada. Kwa mujibu wa kifungu cha 6(1)cha Sheria ya SSRA kinasema kazi kubwa ya mamlaka itakuwani kusimamia na kudhibiti utendaji wa mifuko ya hifadhi. Hiiilikuwa sahihi kutokana na kuwepo kwa mifuko mingiambayo ilikuwa inashindana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi Rasmi ya Upinzaniinaona kuwa dhana pana ya Serikali ni kuwa mifuko miwiliambayo haishindani katika kutoa mafao na kwa mfumo huuunaoanzishwa na Muswada wa Sheria hii ni kuwa utakuwana bodi inayopewa mamlaka kwa mujibu wa kifungu cha 8na kifungu cha 9 katika kusimamia uendeshaji wa mfuko.Hivyo basi, itakuwa haina tija yoyote kwa Mdhibiti kudhibititaasisi ambazo hazina ushindani wa aina yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo KambiRasmi ya Upinzani inashauri kuanzisha mchakato wa kuifutaMamlaka ya Udhibiti wa Hifadhi za Jamii kwani kuendeleakuwepo ni kuongeza gharama zisizokuwa za lazima kwamfuko, kwani sheria inailazimisha mifuko kuchangia asilimia
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
197
kadhaa kwa mamlaka kila mwaka ili mamlaka ifanye kazizake. Jambo hilo lilikuwa sahihi pale ambapo kulikuwa namifuko zaidi ya mitano ya hifadhi ambayo il ikuwainashindana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 8 kwa ujumlawake kinasema kuwa bodi itakuwa ni chombo huru chenyeuwezo wa kushtaki au kushtakiwa, kununua na kuuza malizake zisizohamishika na zinazohamishika, kukopa aukukopesheka na kuingia kwenye mikataba, lakini piainasema, Mwanasheria Mkuu wa Serikali atatakiwa kuingiliapale ambapo bodi itakuwa imeshitaki au kushitakiwa. Kwakuwa bodi ni chombo au taasisi huru na yenye uwezo wakuingia mikataba ya aina yoyote, ni kwa nini inapotakiwakushtakiwa ni lazima utaratibu wa kushitaki Serikali ufuatwe?(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu hiki kinahalalisha kilekitu kinachopigiwa kelele mara kwa mara na watendajikufanya kazi kwa kutojali, kwa kuwa kuna kinga ya Serikali.Kambi Rasmi ya Upinzani inashauri kuwa ili kuleta uwajibikajikila mtu awajibike kulingana na matendo yake. Hakunakifungu chochote kinachosema kuwa kabla ya kukopa aukukopesheka, kununua au kuuza mali au kuingia kwenyemikataba ya kibiashara ni lazima Mwanasheria Mkuu atoeruhusa. Hivyo, kwa nini wakishalikoroga wanataka kinga yaMwanasheria Mkuu wa Serikali? Kambi Rasmi ya Upinzaniinaungana na wadau waliopendekeza kufutwa kwa kifungucha 8(3), (4) na (5).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 24 chamuswada kinatoa ruhusa kwa mwanachama kujitoa katikamfuko, lakini kwa sharti la kupata kibali cha bodi, baada yabodi kujiridhisha kuwa mwanachama amekidhi matakwayaliyowekwa. Jambo hili linaweza kuwa zuri hasa kwawatumishi wa mikataba ya muda mfupi, kwani sasa hivi siyolazima kuzeekea kazini eti unafanya kazi Serikalini. Kunawatumishi wa Serikali kwa muda wa miaka mitano kamavile alivyo Rais na timu yake ya wasaidizi na pindi anapoingiaRais mwingine naye anaingia na timu yake ya wasaidizi,
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
198
waajiriwa wa kwenye migodi na madini ambao wanafanyakazi kwa mikataba na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia Sheria ya Hifadhiya Jamii ya wenzetu wa Kenya, Sheria Namba 45 ya mwaka2013, kifungu cha 45, ina fao la kujitoa na haina mgogorokabisa. Umuhimu wa kuwa na fao la kujitoa kama Sheria yaPPF na PSFP pamoja na NSSF zilivyokuwa zinahitaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukumbuke kwamba kanunizilizoletwa na SSRA kujaribu kuzuia fao hili zilileta mtafarukumkubwa sana kwa wanachama hasa wale waliokuwawameajiriwa katika sekta ya madini na Mheshimiwa Waziriwa sasa ambaye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hudumaza Jamii alikubaliana na wanachama na hoja binafsizilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge; Mheshimiwa JohnMnyika na Mheshimiwa Selemani Jafo kuhusiana na fao hili;na Mheshimiwa Spika Anna Makinda kwa kushauriana naMwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii, walikubaliMheshimiwa Selemani Jafo afanye utafiti wa kuleta taarifaBungeni.
Mheshmiwa Mwenyekiti, hivyo, kwa taarifa hiyo,Kambi Rasmi ya Upinzani ina uhakika kuwa fao hilo badolinahitajika na ni muhimu sana kwa wanachama wa mifukoya hifadhi kuwa nalo. (Makofi)
Mheshmiwa Mwenyekiti, kifungu cha 29 kinachoelezamafao yatakayokuwa yanatolewa na mfuko huu, kifungukidogo (e) kimesema kuwa kutakuwa na fao la kutokuwana ajira (an employment benefit). Hata hivyo fao hilihalijatolewa ufafanuzi wowote kwenye sheria, zaidi yakueleza kwamba Waziri mwenye dhamana atalitungiakanuni.
Mheshmiwa Mwenyekiti, Kambi Rasmi ya Upinzaniinaitaka Serikali ieleze kwa kina fao hili ni lipi? Linagusa kundilipi? Kwa masilahi yapi? Tunayasema haya kwa sababuinasemekana kwamba fao hili lina lengo la kuchukua nafasiya fao la kujitoa. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
199
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi Rasmi ya Upinzaniinaona kwamba umuhimu mkubwa wa kuwa na fao lakujitoa kama ilivyokuwa linatolewa na mifuko iliyokuwepo,bado ni la msingi na lazima, kwani mwanachama anakuwatayari ana akiba yake na hivyo huo unakuwa ni mtaji wakumtoa kwenye umaskini wa kipato.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 29(1)(f) kinatoafao la ugonjwa. Kambi Rasmi ya Upinzani inaomba ipatiweufafanuzi wa hili. Fao la ugonjwa na tofauti yake…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda waMzungumzaji)
MWENYEKITI: Ni kengele ya pili, Mheshimiwa.
MHE. ESTER A. BULAYA – MSEMAJI MKUU WA KAMBIYA UPINZANI KUHUSU OFISI YA WAZIRI MKUU: MheshimiwaMwenyekiti, naomba nimalizie sentensi. Ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tunaona ni njia yakutaka kuliita fao la afya ili lisiingiliane na kile kinachotolewana NHIF. Kama lengo ni kupunguza gharama za uendeshajina hivyo kuwa na matumizi mazuri ya fedha za wanachama,ni bora kama ambavyo tulieleza hapo awali, mafaoyanatolewa na Mfuko wa Bima ya Afya yawekwe pia kwenyemfuko huu unaoanzishwa na sheria hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na ufinyu wamuda, naomba yote ambao yamebakia, sijayasoma yaingiekwenye Hansard.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipanafasi, ila nasikitika kwa kutokubali Zaburi na wewe niMkristo. (Makofi)
MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI KUHUSU MUSWADAWA SHERIA YA MFUKO WA HIFADHI YA JAMII KWAWATUMISHI WA UMMA WA MWAKA 2017 - KAMA
ILIVYOWASILISHWA MEZANI
(The Public Service Social Security Fund Act, 2017)
(Yanatolewa chini ya kanuni ya 86(6) ya kanuni zaBunge, Toleo la mwaka 20016)
A. UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kwa mwaka huu wa2018 kusimama hapa kutoa maoni ya Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni kuhusu Muswada wa Sheria uliopo mezani,naomba kwa heshima, nichukue fursa hii kumshukuru sanaMwenyezi Mungu kwa kutulinda sote na kutuvusha salamakatika mwaka uliopita wa 2017 na kutujalia kuuona mwakahuu mpya wa 2018 tukiwa salama. Kwa sababu hiyo,nakutakia wewe Mheshimiwa Spika, na WaheshimiwaWabunge wote, heri ya Mwaka Mpya.
Mheshimiwa Spika,Zaburi ya 1 mstari wa kwanza na wa tatu inasema kwamba:“Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki, walahakusimama katika njia ya wakosaji, wala hakuketi barazanipa wenye mizaha. Naye atakuwa kama mti uliopandwakando ya vijito vya maji, uzaao matunda yake kwa majirayake, wala jani lake halinyauki; na kila atendalo litafanikiwa.Mzaburi anaendelea kusema katika mstari wa nne kwamba:“Sivyo walivyo wasio haki, hao ni kama makapiyapeperushwayo na upepo”
[MANENO YAMEONDOLEWA KWA MAELEKEZO YA KITI]
Mheshimiwa Spika,baada ya salamu hizo za utangulizi sasa naomba nitoe maoniya jumla kuhusu Muswada wa Sheria ya Hifadhi ya Jamii uliopombele yetu.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
201
Mheshimiwa Spika,Hifadhi ya Jamii ni haki ya kila Mtanzania. Haki hii imeanishwakatika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibaraya 11(1) na Sera ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii ya mwaka 2003.Haki hii pia imeiainishwa kwenye mkataba wa kimataifa wahaki za binadamu wa mwaka 1948 pamoja na mikataba yashirika la kazi duniani (ILO) ibara ya 102 ya mwaka 1952.
Mheshimiwa Spika,Hifadhi ya Jamii ni haki ya kila mtu na si kwa wale tu waliokatika sekta iliyo rasmi . Kwa sababu mpaka sasa kulinganana takwimu za sensa ya watu na makazi zilizotolewa mwaka2012 ni kwamba idadi ya watanzania wote ni milioni 44.9ambao kati yao watu milioni 1.7 tu ndio waliojiunga namifuko ya hifadhi ya jamii, hii ikiwa ni asilimia 6.5 tu ya nguvukazi yote ya watu milioni 23.7
Mheshimiwa Spika,kwa takwimu hizo, Tanzania haiwezi kujitokeza kifuambelena kujidai kwamba jamii yake imehifadhika. Na sababukubwa asilimia ndogo ya watu waliojiunga na scheme zahifadhi za jamii ni ufinyu wa ajira kwa sekta za uma na sektabinafsi. Kambi Rasmi ya Upinzani ina mtazamo kwambabadala ya Serikali kung’ang’ana kuweka sheria zakupunguza na kuibana mifuko ya jamii ingepanua fursa zaajira kwa watanzania na kuweka mazingira wezeshi kwasekta binafsi kuajiri kwa wingi ili kupunguza umasikini wakipato kwa watanzania lakini pili kuhakikisha kwambawafanyakazi wanaweka akiba itakayowasaidia pindi umriwao wa kufanya kazi utakapokoma.
Mheshimiwa Spika,pamoja na hayo yote, jambo la msingi ambalo Kambi Rasmiya Upinzani inaamini, ni kwamba; akiba ni kitukinamchomsaidia mtu wakati wa shida au matatizo; na siokitu cha kufanikisha mazishi ya mtu huyo baada ya kufarikikutokana na kushindwa kutatuliwa kwa matatizo au shidailiyokuwa ikimkabili. Kwa sababu hiyo, Kambi Rasmi yaUpinzani inaitaka Serikali pamoja na wabunge wote kwajumla kuhakikisha kwamba mifuko ya jamii chini ya sheria hii
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
202
inaweka mazingira ya mwanachama kuweza kunufaika namichango yake wakati wowote anapopata shida kubwakabla ya kustaafu na sio kuweka masharti magumu yakumfanya mwanachama ashindwe kunufaika na michangoyake mpaka wakati wa kustaafu.Mheshimiwa nasema hivi kwa sababu ikiwa hatutawekeutaratibu wa kumfanya mwananchama kunufaika namichango yake wakati anapopata shida akiwa hai, yamkinitunaweza kuwa tunatengeneza mazingira ya kuwachangishawanachama fedha za kuja kugharamia mazishi yao na siokuwasaidia kuboresha maisha yao. Hii ni bayana kwa kuwaumiri wa kuishi kwa mtanzania sasa hivi unakadiriwa kuwani miaka 61; na ni takribani umri huo huo mtumishi anapaswakustaafu na kulipwa mafao yake. Kwa logic ndogo, mafaohayo ni ya kumzika sio ya kumtegemeza aishi.
Mheshimiwa Spika,Aidha, Mamlaka ya uthibiti wa hifadhi ya jamii (ssra) inasemakwamba hadi juni, 2015 mifuko ya hifadhi za jamii hapa nchiniilikuwa na jumla ya wanachama 2,132,350. Na kufikia Juni,2016 wanachama waliongezeka na kufikia 2,464,399, hii nikutokana na ushindani uliopo baina ya mifuko na watu haoni wale walipo katika ajira ya sekta iliyo rasmi tu na nguvukazi kubwa iliyobakia ya takribani milioni 20 inashughulikana sekta isiyo rasmi na wote wako katika hali hatarishi kwavile hawana kinga yeyote ya hifadhi ya jamii.
Mheshimiwa Spika,Takwimu zinaonesha kuwa PPF hadi juni 2015 ilikuwa na jumlaya watumishi 352, PSPF ilikuwa na watumishi 186, LAPF ilikuwana watumishi 195 na mifuko hiyo yote ina matawi zaidi yazaidi 10 nchi nzima. Hapa ni dhahiri kwamba kutakuwa nakile kinachoitwa “down sizing” ili kazi zifanyike kulingana nanafasi zitakazo tengenezwa na mfumo mpya wa taasisiinayoanzishwa kwa mujibu wa sheria hii. Mbali ya hilo kunaushindani kwa mifuko kutoa mafao yanayofanana, mfano;fao la bima ya afya linalotolewa na Mfuko wa Bima ya afya-National Health Insurance Fund- (NHIF) na fao la kuumiaukiwa kazini linatolewa na mfuko maalumu wa fidia yawafanyakazi –Workers Compensation Fund (WCF)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
203
Mheshimiwa Spika,Kwa kuangalia mafao yatakayotolewa chini ya sheria hii nidhahiri kwamba ushindani au duplication ya mafao bainaya mifuko itaendelea au kuondoa baadhi ya mafao nakuyaacha kwenye mifuko ambayo haijafutwa kwa mujibuwa sheria hii maana yake ni kumzidishia mzigo wa makatomtumishi wa umma ambaye mshahara wake ni mdogo,kwani ina mlazimu kuchangia mifuko miwili.
Mheshimiwa Spika,Katika maelezo ya Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana naHifadhi za jamii kwenye kamati iliyouchambua muswada huualisema kuwa, pamoja na mambo mengine ni kuboreshamafao ya wanachama. Hili ni jambo jema kama litaonekanakatika muswada huu.
Mheshimiwa Spika,Mafao ya wanachama yanaboreshwa kwa kuwa nakikokotoo (formula) ambacho kinajulikana na kimekubalikabaina ya wahusika wote, kwa maana ya wanachama.Tukumbuke kuwa fedha hizi sio mali ya Serikali bali ni mali yawanachama na Serikali kupitia kwenye shirika hili ni mtunzajina muendelezaji wa fedha hizo.
Mheshimiwa Spika,Muswada ulikuwa umetoa kitu kinachoitwa “full pension” nakikatolewa tafsiri yake na kwa bahati mbaya sana hiyo ndiyoilikuwa ni kikokotoo au Kanuni au formula, lakini wadauwaliipinga kwani badala ya kuboresha mafao ilikuwainayakandamiza. Kabla ya kuunganisha mifuko hii, mifukomingi ilikuwa na vikokotoo tofauti kama vile: pspf 540 na(580 kwa wajiriwa walioanza kazi baada ya 2014, lapf 540,PPF na gepf 580. Kwa vile moja ya sababu kuu za kuunganishamifuko hii ni kuboresha mafao ya wafanyakazi, hivyotunatarajia sheria hii ije na kikotoo cha chini ya 540 au 580 nakionekane kwenye muswada huu wa sheria na sio kwenyekanuni za Mheshimiwa Waziri na SSRA. Hivyo hatutarajiikabisa kupunguza kile kilichokuwepo badala ya kukiboresha.Kuna hoja nyingi zinajengwa kuhusu uimara wa mifuko namabadiliko ya kupunguza mafao kwa kutumia kanuni, lakini
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
204
hoja hizo ni dhahifu kama Serikali itaacha kuchota fedha zawanachama na kuwekeza katika miradi ambayohaikufanyiwa upembuzi yakinifu na mwisho wa siku mradiunashindwa kutoa kile kilichokusudiwa kama ambavyoilioneshwa katika taarifa za ukaguzi na CAG kuhusiana nautendaji wa mashirika hayo. Taarifa hiyo ya mwaka 2015/16inasema kwamba;“Taarifa ya tathmini ya uwezo wa wa Mfuko wa Pensheni yaWatumishi wa Umma ya mwaka unaoishia tarehe 30 Juni 2014ambayo iliandaliwa na Muhana & Co Actuaries & Consultantsilionyesha kuwa Mfuko una jumla ya fedha za Shilingi milioni1,306,707; na deni halisi lilikuwa Shilingi trilioni 12.46 Hivyokufanya upungufu wa shilingi trilioni 11.15. Taarifa ya sasainaonesha Mfuko wa PSPS unaidai serikali kiasi cha Tsh. 3 Trilion.Madeni haya yanatokana na mikopo ya moja kwa moja,dhamana, na michango ambayo haikuwasilishwa kulinganana matakwa ya kisheria”.
Mheshimiwa Spika,Serikali bado ni ile ile ya CCM, je ni kitu gani kitakachotoauthibitisho kuwa tabia hiyo ya Serikali itabadilika katika Sheriahii inayotungwa ili kuondokana na tabia yake ya kukopamoja kwa moja kwenye mifuko na kushindwa kurejesha?
Mheshimiwa Spika,Kuna hili jambo la kuacha mambo muhimu yanayohusumaisha ya watu kwenye kanuni ambazo kwazo ni jukumu laWaziri(Serikali), hii sio sahihi kabisa inatakiwa suala muhimukwa maisha ya wafanyakazi kama hili liamuliwe na Bungezima kwa kujadiliana na kufikia mwisho kwani wabunge ndiowalinzi na wawakilishi wa wananchi ikiwemo wanachamawa mifuko ya hifadhi. Mfano kifungu cha 18(2) (b) ……. Orsuch amount as the minister may, by order in the Gazettedetermine”, kifungu cha 29(2) n.k
Mheshimiwa Spika,Hifadhi ya jamii ni kinga ya maisha kwa wanachama wakemara tu baada ya kutoka kwenye ajira, na mfumouliokuwepo ambao ulikuwa unawapa wanachamakuchagua kulingana na aina ya mafao yaliyokuwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
205
yanatolewa na mfuko husika. Hivyo basi Kambi Rasmi yaUpinzani inaona litakuwa jambo la busara kamawanachama waliopo sasa katika mifuko waendelee nautaratibu walioingia nao mikataba ya kupatiwa huduma,na utaratibu mpya wa mifuko miwili uwahusu wanachamawapya au watumishi wapya katika sekta ya umma na binafsi.
Mheshimiwa Spika,Hoja hii ya wanachama kuhama na sera ya mafao walijiunganayo kwenye mifuko inayovunjwa imepewa mwanga kidogokwenye kifungu cha 80(4) cha muswada huu. Lakini badokuna hoja kama ndio hivyo ni ukweli kuwa mafaoyaliyokuwepo kwa mifuko inayounganishwa badoyataendelea kutolewa kwa wanachama wa zamani katikamifuko mipya inayoanzishwa?
Mheshimiwa Spika,Kwa takwimu zilizotolewa na wadau ni kwamba PPF ambayoasilimia 75 ya wanachama wake ni kutoka sekta binafsi naasilimia 25 ndio sekta ya umma, kwa hiyo basi katikakuunganisha mifuko ilitakiwa NSSF na PPF kuwa taasisi mojaambayo ingehudumia sekta binafsi. Badala yake asilimia 25za wanachama ambao wako sekta ya umma ndiowameunganishwa na wenzao katika mifuko mingine nailiyobakia 75% wanahamishiwa NSSF. Hapa kuna shida yakimahesabu!!!!!
B. MAPITIO YA MUSWADA
Mheshimiwa Spika,Madhumuni ya muswada huu unapendekeza kutungwa kwasheria ya kutoa mafao ya hifadhi ya jamii kwa watumishiwalio katika utumishi wa umma, na kufuta sheria zilzopozilizokuwa zinatoa huduma hiyo kwa watumishi hao.
Mheshimiwa Spika,Ni ukweli kwamba mifuko hiyo ya Pensheni ya PSPF, LAPF,GEPF na PPF mbali ya kutoa huduma kwa watumishi waumma pia mifuko hiyo ilikuwa inatoa huduma kwa watuambao sio watumishi wa umma. Kwa maana nyingine ni
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
206
kuwa taasisi hizo zina wanachama wasiokuwa watumishiwa umma na pia kuna watumishi wa umma ambaowalikuwa ni wanachama wa NSSF.
Mheshimiwa Spika,Kwa muktadha huo ili kuondoa mtafaruku unaowezakujitokeza kutokana na uanzishwaji wa sheria hii, KambiRasmi ya Upinzani inaona kuwa muda wa mpito uliowekwakwenye muswada katika kifungu cha 86 kunawezakusababisha usumbufu na hivyo kuleta matatizo miongonimwa wanachama kwani watu wanastaafu kila wakati nawengine tayari wako kwenye kusubiri mafao yao, hivyo kwakipindi hicho cha mpito wa miezi sita ni wapi wanatakiwakudai au kuhudumiwa ili wapatiwe stahiki zao?
Ni bora kuwekwe muda maalum wa kufanya uhamisho kwawanachama wote wanaotakiwa kuhamishwa kutoka mfukowa awali kwenda mfuko mpya, ili kuondoa usumbufu ambaoutaweza kujitokeza katika utekelezaji wa zoezi hilo.
Mheshimiwa Spika,Kama muswada unavyosema kuwa unafuta mifuko minneambayo ilikuwa inatoa huduma kwa watumishi wa ummana kuunda mfuko mmoja, kwa lengo kuu la kupunguzamatumizi yasiyokuwa ya lazima na pale pale kuleta tijakiutendaji kwa kutoa mafao na pensheni zinazolingana kwawatumishiwa umma.
Mheshimiwa Spika,Katika kifungu cha 3 cha muswada kinachohusu tafsiri yamaneno mbalimbali yaliyotumika kwenye muswada, neno“authority” au kwa Kiswahili mamlaka na kwa maanailiyotolewa kuwa ni mdhibiti wa mifuko yaani (SSRA)limetumika mara kadhaa katika vifungu mbalimbali vyamuswada. Kwa mujibu wa kifungu cha 6(1) cha sheria yaSSRA kinasema kazi kubwa ya Mamlaka itakuwa ni kusimamiana kuthibiti utendaji wa mifuko ya hifadhi. Hii ilikuwa sahihikutokana na uwepo wa mifuko mingi ambayo kwayo ilikuwani shindani.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
207
Mheshimiwa Spika,Kambi Rasmi ya Upinzani inaona kwa kuwa dhana pana yaSerikali ni kuwa na mifuko miwili ambayo haishindani katikakutoa mafao, na kwa mfuko huu unaoanzishwa namuswada wa sheria hii, ni kuwa utakuwa na bodi inayopewamamlaka kwa mujibu wa kifungu cha 8 na kifungu cha 9katika kusimamia uendeshaji wa mfuko. Hivyo basi itakuwahaina tija yoyote kwa mdhibiti kudhibiti taasisi ambazo hazinaushindaji wa aina yoyote.
Mheshimiwa Spika,Kwa maana hiyo, Kambi Rasmi ya Upinzani inashaurikuanzisha mchakato wa kuifuta mamlaka ya udhibiti wahifadhi za jamii kwani kuendelea kuwepo ni kuongezagharama zisizokuwa za lazima kwa mfuko, kwani sheriainailazimisha mifuko kuchangia asilimia kadhaa kwamamlaka kila mwaka ili mamlaka ifanye kazi zake. Jambohilo lilikuwa sahihi pale ambapo kulikuwa na mifuko zaidi yamitano ya hifadhi ambayo ilikuwa inashindana.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 8 kwa ujumla wake kinasema kuwa Bodi itakuwani chombo huru chenye uwezo wa kushitaki au kushtakiwa,kununua na kuuza mali zake zisizohamishika nazinazohamishika, kukopa au kukopesha na kuingia kwenyemikataba. Lakini pia inasema Mwanasheria Mkuu wa Serikaliatatakiwa kuingilia pale ambapo bodi itakuwa imeshtakiau kushtakiwa.
Mheshimiwa Spika,Kwa kuwa bodi ni chombo huru au taasisi huru na yenyeuwezo wa kuingia mikataba ya aina yoyote, ni kwaniniinapotakiwa kushtakiwa ni lazima utaratibu wa kuishtakiSerikali ufuatwe? Kwa mujibu wa sheria ya Mwenendo waMashtaka (Government Proceeding ACT)ili upeleke shauri lakomahakamani ni lazima utimize matakwa ya kifungu cha 6(2)kinachosema kuwa;
“No suit against the Government shall be instituted,and heard unless the claimant previously submits tothe Government Minister, Department or officer
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
208
concerned a notice of not less than ninety days of hisintention to sue the Government, specifying the basisof his claim against the government, and he shall senda copy of his claim to the Attorney General. Noticeof intention to sue, as the first procedure to suethe government, a notice of not less than ninety daysof his intention to sue the Government, beforecommencing proceedings in court”,
Kwa utaratibu maalum ili kukidhi matakwa ya sharia hiyo,kwa wanachama wa kawaida ambao kwa njia moja aunyinge wanakuwa na mikataba na mashirika haya, ni kwelihaki itapatikana?
Mheshimiwa Spika,Kifungu hiki kinahalalisha kile kitu kinachopigiwa kelele kilamara cha watendaji kufanyakazi kwa kutokujali, kwa kuwakuna kinga ya Serikali. Kambi Rasmi ya Upinzani inashaurikuwa ili kuleta uwajibikaji kila mtu awajibike kulingana namatendo yake. Hakuna kifungu chochote kinachosema kuwakabla ya kukopa au kukopesha, kununua au kuuza mali aukuingia kwenye mikataba ya kibiashara ni lazimaMwanasheria Mkuu wa Serikali atoe ruhusa. Hivyo kwaniniwakishalikoroga wanataka kinga ya Mwanasheria Mkuu waSerikali?
Mheshimiwa Spika,Kambi Rasmi ya Upinzani inaungana na wadauwaliopendekeza kufutwa kwa vifungu vidogo vya 8(3), 8(4)na 8(5).
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 11 cha muswada kinachosema kuhusu“Management of the Fund”, kifungu hicho kinasomeka kuwa;
“The Board shall be responsible for theadministration and management of thefund………”
Kambi Rasmi ya Upinzani inaona kwamba Bodi yawakurugenzi jukumu lake ni kusimamia (supervisory role) na
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
209
sio la uendeshaji (administrative and management role).Jambo hili limegusiwa katika kifungu cha 15(3) kinachosemakwamba;
“the Director General shall,subject to the directionsof the Board, be responsible for the day to dayadministration of the Fund”.
Hii ni sawa sawa kabisa na Bunge linavyofanya kazi zakedhidi ya Serikali. Kwa muktadha huo Kambi Rasmi ya Upinzaniinaona kifungu hicho kitoe jukumu la uendeshaji kwaMkurugenzi na timu yake ya utendaji badala ya Bodi yaWakurugenzi. Kila mmoja ahukumiwe kwa nafasi yake namgawanyo wa madaraka uwe wazi, tukumbuke kuwaMtendaji Mkuu na Mwenyekiti wa bodi kwa mujibu wa sheriahii wote ni wateule wa Rais, rejea kifungu cha 8(1) kwenyeJedwali la kwanza kifungu cha 1(1) (a) na kifungu cha 15(1).
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 15(4) cha muswada kinasema kuwa; “TheDirector General shall hold office for a term of five yearsand……”. Hapa limetumika neno “shall”, hii ni kinga ya nguvuhadi kipindi cha miaka mitano kifike kama bado yuko haina mwenye afya njema. Maana yake hata kama utendajikazi wake utakuwa upo chini ya kiwango kwa tafsiri panasio rahisi kutenguliwa. Japokuwa kifungu cha 15(2) kinasemaatapewa masharti ya kazi, lakini mktaba au masharti ya kazihayawezi kwenda tofauti na sheria iliyopitishwa na Bunge.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 24 cha muswada kinatoa ruhusa kwamwanachama kujitoa katika mfuko, lakini kwa sharti lakupata kibali cha Bodi, baada ya bodi kujiridhisha kuwamwanachama amekidhi matakwa yaliyowekwa. Jambo hililinaweza kuwa zuri hasa kwa watumishi wa mikataba yamuda mfupi, kwani sasa hivi kazi sio lazima kuzeekea kazinieti unafanya kazi Serikalini, kuna watumishi wa Serikali kwamuda wa miaka mitano kama vile alivyo Rais na timu yakeya wasaidizi na pindi anapoingia Rais mwingine naeanaingia na timu yake ya wasaidizi, waajiriwa wa kwenye
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
210
migodi ya madini ambao wanafanya kazi kwa mikataban.k. Mheshimiwa Spika, ukiangalia sheria ya hifadhi ya jamiiya wenzetu wa Kenya kwa sheria Na.45 mwaka 2013 kifungucha 45 ina fao la Kujitoa na haina mgogoro kabisa.
Mheshimiwa Spika,Umuhimu wa kuwa na fao la kujitoa kama sheria ya PPF naPSPF pamoja na NSSF zilivyokuwa zinahitaji, tukumbukekwamba kanuni zilizoletwa na SSRA kujaribu kuzuia fao hilizilileta mtafaruku mkubwa sana kwa wanachama hasa walewaliokuwa wameajiriwa katika sekta ya madini, naMheshimiwa Waziri wa sasa akiwa Mwenyekiti wa Kamati yaHuduma za Jamii ulikubaliana na wanachama na hoja binafsizilizoletwa na waheshimiwa John Mnyika na Mhe SelemaniJaffo kuhusiana na fao hili na Mheshimiwa Spika Annemakinda kwa kushauriana na Mwenyekiti wa Kamati yahuduma za Jamii walikubali Mheshimiwa Selemani Jaffoafanye utafiti na kuleta taarifa Bungeni. Hivyo, kwa taarifahiyo Kambi Rasmi ya Upinzani ina uhakika kuwa fao hilo badolinahitajika na ni muhimu sana kwa wanachama wa mifukoya hifadhi kuwa nalo.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 27 kinasomeka kuwa kuwa kuwa na kitu kinaitwa“Special lumpsum” lakini vitatolewa vigezo vya wanaostahilihiyo “Special Lump sum”, kama ambavyo hapo awaliniliongelea kuhusu wafanyakazi walio katika sekta za madinina watumishi ambao utumishi wao Serikali unaendana namihula ya Serikali kuwa madarakani kabla ya kufanyika kwauchaguzi. Kama hakutakuwa na kazi inayotakiwa kuendeleana mtumishi huyo anaacha utumishi wa umma, ninikinatakiwa kifanyike kuhusiana na mafao yake? Je ni kweliataendelea kulipwa mafao ya kutokuwa na ajira hadikutimiza umri wa kulipwa pensheni? Au kifungu cha 27 (d)kinachosema kuwa “has retired on abolition of his office”.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 29 kinachoeleza mafao yatakayokuwayanatolewa na mfuko huu, kifungu kidogo cha (e) kimesemakuwa kutakuwa na fao la kutokuwa na ajira (unemployment
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
211
benefit). Hata hivyo fao hili halijatolewa ufafanuzi wowotekwenye sheria,zaidi ya kuelekeza kwamba waziri mwenyedhamana atalitungia Kanuni. Kambi rasmi ya upinzaniinaitaka serikali ieleze kwa kina fao hili ni lipi , litagusa kundilipi na kwa maslahi yepi? Tunayasema haya kwa sababuinasemekana kwamba fao hii lina lengo la kuchukua nafasiya fao la kujitoa ( withdrawal benefit).
Mheshimiwa Spika,Kambi Rasmi ya Upinzani inaona kwamba umuhimu mkubwawa kuwa na fao la kujitoa kama lilivyokuwa linatolewa namifuko iliyokuwepo bado ni la msingi na lazima kwanimwanachama anakuwa tayari na akiba yake na hivyo huounakuwa ni mtaji wa kumtoa kwenye umasikini wa kipato.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 29(1) (f) kinatoa fao la Ugonjwa au “sicknessbenefit”, Kambi Rasmi ya Upinzani inaomba ipatiwe ufafanuziwa hili fao la ugonjwa na tofauti yake na fao la afya. Hapatunaona ni njia ya kukataa kuliita fao la afya ili isiingiliane nakile kinachotolewa na NHIF. Kama lengo ni kupunguzagharama za uendeshaji na hivyo kuwa na matumizi mazuriya fedha za wanachama ni bora kama ambavyo tulielezahapo awali Mafao yanayotolewa na Mfuko wa Bima ya Afyayawekwe pia kwenye mfuko huu unaoanzishwa na shariahii.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 32(1) cha sheria kinasema kuwa mwanachamaana haki ya kupata mafao la uzazi, jambo ambalo ni jemasana, lakini maelezo yake yanabagua wanachama. Ukwelini kuwa wanachama wanaume nao wanawake zao ambaonao wanakuwa katika mchakato wa uzazi kamawanachama wanawake. Ili kuweka uwiano ulio sawa kwawanachama wa jinsia zote ni muhimu kukawepo na faolitakalokuwa ni kwa wanaume kama mafao hayo ya uzazini maalum kwa wanachama wa jinsia ya kike tu, i l iwanachama wanawake na wanaume wanufaike na fao lauzazi.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
212
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 45(1) cha muswada kinaipa Bodi mamlaka yakugawa pensheni ya mwanachamba ambaye atakuwaanatumikia kifungo kwa kadri itakavyoona inafaa hadi paleatakapomaliza kutumikia adhabu yake ya kifungo. KambiRasmi ya Upinzani iungane na wadau kwamba mtu kuwagerezani haina maana kuwa hauna uwezo wa kuelewa nivipi mali zako zitumike na ni nani wanastahili na nanihawastahili. Hivyo basi, tunashauri kifungu hicho kiondoemamlaka ya kugawa pensheni yake kwa bodi na yarudishwekwa mhusika mkuu wa pensheni.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 46 kinataja nafasi za utumishi wa umma kuwawao inawapasa kupata kibali maalum kutoka kwaMheshimiwa Rais kuhusiana na mafao yao, lakini kada zotehizo zinafuata sharia ya utumishi wa umma katika kutimizamajukumu yao japokuwa ni wateule wa Rais. Kamaambavyo tumeeleza hapo awali kwamba fao la kujitoa nimuhimu, na kama kanuni/kikokotoo cha pension au mafaokitakuwa shirikishi na kuwekwa wazi kuna umuhimu gani waRais kutoa kibali?
Mheshimiwa Spika,Kifungu hicho kikisomwa pamoja na sharia ya SSRA kifungucha 38A(A) kuwa mhusika ni lazima aandike barua kwenyekamati na barua hiyo iambatane na mapendekezo kutokakwa majiri wake wa mwisho wakati anaacha kazi.Tukumbuke kwamba kada zote zil izotajwa kwenyemusdwada katika kifungu cha 46 ni wasaidizi wa Rais hivyokatika hili Rais anakuwa na nafasi mbili, moja ni ushauri napale ni kutoa maamuzi. Hii sasa ni jambo la ajabu katikautendaji wa sheria.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 56(1) cha muswada kinachosema kuwa;
“No income tax on the contributions and benefitispayable under the scheme shall be levied on the fund”
Kwa maana kwamba, mfuko ndio hautatakiwa kulipa kodilakini mafao ya wanachama yatakayokuwa yanalipwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
213
yatatakiwa kukatwa kodi ya mapato, Kambi Rasmi yaUpinzani inashukuru kwani Serikali katika kikao na wadauilikubali kuondoa maneno, “on the fund”.
Mheshimiwa Spika,Kuendelea kuwepo kwa maneno hayo ni kwambawanachama watakuwa wanalipishwa michango mara mbilikwenye mishahara yao jambo ambalo lilikuwa ni kinyumecha utaratibu wa kikodi.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 57(1) cha muswada kinailazimisha Bodikumtafuta mthamini kufanya tathmini ya mfuko kila baadaya miaka mitatu kulingana na kanuni zilizotolewa na Mdhibiti.Kifungu cha 57(2) kinasema kuwa bodi inaweza kumuombamdhibiti ili akubaline na bodi kutokufanyika kwa uthaminiwa mfuko kama kifungu cha 57(1) kinavyotaka. MheshimiwaSpika, madhara ya kutokufanyika kwa tathmini kwa wakatiinaweza kupelekea madhara ya kufilisika kwa mfuko kamaambavyo ulivyokuwa mfuko wa PSPF. Hivyo basi, KambiRasmi ya Upinzani inataka kifungu hicho cha 57(2) kifutwe.
Mheshimiwa Spika,Kifungu cha 57(3) kinasema kuwa taarifa ya tathmini ya uborawa mfuko inapelekwa kwa mdhibiti na Waziri badala yamsimamizi wa mfuko ambaye ni Bodi. Kambi Rasmi yaUpinzani inaona kuwa itakuwa ni vyema na taarifa toka kwamdhamini juu ya ubora wa mfuko nakala ipewe Bodisambamba na Mdhibiti na Waziri i l i kabla ya hatuakuchukuliwa bodi na Mtendaji Mkuu vijitathmini utendajiwake.
Mheshimiwa Spika,Vifungu vya 66 na 67 vya muswada vinatoa uhuru kwaMkurugenzi Mkuu(ambaye anafanya kazi kwa maelekezo yaBodi) wa PSSSF kuomba kibali cha Mahakama ili kukamatamali za mwajiri na kuzinadi ili kulipia michango ambayoalitakiwa kulipa lakini akashindwa kulipa. Wakati kifungu cha72 kinazuia mali za mfuko kukamatwa na kunadiwa bila yakuwepo kibali cha Waziri. Kambi Rasmi ya Upinzani inauliza,
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
214
sheria hii waajiri wote ni taasisi za Serikali na taasisi za Serikalinyingi kuzishtaki ni lazima Mwanasheria Mkuu wa Serikaliahusishwe. Aidha, Mfuko kwa muktadha huo ni kwanini malizake zisikamatwe kama kutakuwa na amri ya kufanya hivyo?Kambi Rasmi ya Upinzani inaona hii ni “double Standard”inayowekwa katika muswada huu.
Mheshimiwa SpikaKifungu cha 89(d), 108(h) na kifungu cha 112(b) kinachofanyamarekbisho ya jedwali la pili la sheria ya Utumishi wa ummakwa kufuta kifungu cha 26 cha sheria na kukiandika upya.Kifungu hicho kinasema kuwa;
“one motor vehicle given once,of a value notexceeding such amount as the President may fromtime to time determine”
Kambi Rasmi ya Upinzani inaona kuwa kifungu hiki ambachokinawaweka Waheshimiwa Majaji wastaafu kutegemeafadhila za Rais, jambo hili kwa mtazamo wetu linawezakutumika kama kigezo cha kuwalazimisha kufanya yaleambayo Mheshimiwa Rais anataka yafanyike katika kadhianzima ya utoaji wa haki. Hivyo basi tunaona sheria imtoeRais na itamke aina ya gari au Jaji Mkuu aliyepo ndiye awemhusika mkuu katika hilo.
Mheshimiwa Spika,Baada ya kusema hayo, kwa niaba ya Kambi Rasmi yaUpinzani, naomba kuwasilisha.
…………………………….Esther A. Bulaya(Mb)
Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani-Ofisi yaWaziri Mkuu (Sera,Bunge,Kazi, Vijana, Ajira
na Wenye Ulemavu)31/1/2018
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, nina tangazo,wakati natangaza wageni, sikumtangaza kiongozi mmojatuliyenaye hapa na kwa sababu ya muswada huu na ule
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
215
utatu wetu katika shughuli za wafanyakazi nchini, napendanitambue uwepo wa Dkt. Aggrey Mlimuka, MkurugenziMtendaji wa ATE, karibu sana.
Waheshimiwa Wabunge, asubuhi baada ya kipindicha maswali, mliona tulichua muda ambao tungelikuwakatika shughuli hizi mapema. Kwa maana hiyo, nitakujakutumia madaraka yangu niongeze muda wa 30, tufanyekazi ya kibunge. Hii kazi ya leo ni muhimu sana. Sasa natakaniwahoji, kwamba badala ya kutumia kuchangia kwa dakika15 kila mmoja wetu mtakaopata nafasi, kwa kuwa mkowachache, mnaonaje kama tutachangia kila mmoja wetukwa dakika saba?
(Hoja ilitolewa iamuliwe)(Hoaja iliamuliwa na Kuafikiwa)
MWENYEKITI: Sasa wachangiaji tulionao hapa natakatuelewane. Waheshimiwa tulionao hapa, tutatumia mudahuo kidogo tulionao. Tutaanza na Mheshimiwa Mwenyekitiwetu wa Kamati, Mheshimiwa Serukamba, atafuatiwa naMheshima Stephen Masele na Mheshimiwa Kasuku Bilago.Muda ninavyouona, hatutafika, lakini tuone, maana nusu saanitaiongeza lakini tutafika tu. Tuanze na hawa watatu.
Mheshimiwa Serukamba.
MHE. PETER. J SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru kwa kunipa nafasi ya kwanza na naomba kwanzaniishukuru Serikali kwa kuleta muswada huu. Kipekee kabisanamshukuru Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma historia yamuswada huu, ilianza mwaka 2004 huko, lakini wotehawakufanya decision hii, Rais huyu amechukua maamuzihaya magumu lakini maamuzi mazuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nilitaka kusemakwamba sheria hii tunayotunga leo, Mifuko ya Hifadhi yaJamii, guarantor ni Serikali, tusije tukasahau hili. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
216
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kusoma standardza ILO, minimum ya pensheni ya ILO ni asilimia 40; UlayaMagharibi ni asilimia 42 mpaka asilimia 74; Ulaya Mashariki niasilimia 46 mpaka asilimia 63. Latin America ni asilimia 46mpaka 77; Tanzania kwa wale ambao labda hawajui ni katiya nchi chache zenye kiwango kikubwa sana cha pensheni.Tanzania ni asilimia 72.5. Tumewazidi wengi katika continenthii. Naipongeza sana Serikali kwenye hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nimeamua kusemahili kwanza? Nataka tuelewane, sisi Kamati tumewaombaSerikali wako wachache watesema otherwise, lakiniunanimously Kamati tulisema formula iwekwe kwenye kanuni.Sababu zetu ni moja, mbili, tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya kwanza,tumesema watakapotunga sheria hii wakafanya actuarialvaluation. Actuarial valuation inafanywa na SSRA, siyo namifuko yenyewe. Huweze kumwambia mtu aku-access wewemwenyewe. Regulatory akafanye hiyo kazi, access hiyomifuko, baada ya pale wakutane kwenye utatu mtakatifu,waweze kuandaa formula na lazima formula hii iwezeshemifuko hii kuendelea kuwapo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefanya maamuzihaya kwa sababu ya kutatua matatizo tuliyokuwa nayo iliwafanyakazi wa Tanzania wasipate shida. Kwa hiyo, badonaomba Serikali ifanye kazi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu, nimemsikiliza dadayangu wa upinzani, aliyekuwa anasoma, nadhani hajasomamuswada huu mpya. Serikali imeamua haitahamishamember yeyote. Members watabaki kule walikokuwa.Wanasheria wenzangu mnajua, hatutungi retrospective law.Waajiriwa wapya ndio watakwenda kwenye hiyo mifukomipya. Hii ni kwa sababu ungewahamisha leo,unawahamisha na contribution, investment zao unafanyaje?Liabilities zao anabaki nazo nani? Kwa hiyo, ilikuwa ni lazimawabaki, halafu tuweke cutoff, wale wanaokuja mbele,wataingia kwenye sheria hizi. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
217
Mheshimiwa Mwenyekiti, umuhimu wa SSRA, watuwanaweza wasilione, ndiyo maana tumependekeza mifukoyote ya hifadhi ya jamii iwe chini ya mtu mmoja, NHIF iendehuko, CHF iende huko na mifuko yote ili kuwe na regulatorambaye anasimamia shughuli hii. Kwa hiyo, ni muhimu sanakwa ajili ya maendeleo ya mfuko wa jamii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo tumelisemakwenye kamati na naomba personally niliseme, ni suala laMakatibu Wakuu. Makatibu Wakuu ndio Maafisa Masurufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe umekaa Serikalini;kwa kweli niwapongeze kwanza hata hao Makatibu Wakuuna watu wa Serikali. Maana wangekuwa wanajifikiria wao,wasingeileta hii sheria. Kwa sababu sheria hii ilikuwa inawa-benefit wao, hasa waliokuwa kwenye PSPF. Kwa sababu yakuangalia mbali, kuangalia Taifa, wameileta hii sheria.Naomba sana Makatibu Wakuu wenyewe hawafiki 20.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaongelea yule ambayeamefanya kazi mpaka siku ya kustaafu ni Katibu Mkuu. Hawandio wanatunza pesa, otherwise tusipowa-consider, naombaSerikali mkatafakari, wataanza kujitafutia pensheni yaopembeni. Tunazuia haya, maana haiwezekani mimi ni KatibuMkuu, aliye chini yangu amekuwa taken care, badohatueleweki.
Naiomba Serikali iende kulitafakari namnatunachoweza kufanya kuhusu Makatibu Wakuu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu umesematupunguze muda, ukiangalia sheria hii, kwanza naipongezaSerikali kwa sababu karibu amendments zote ambazoKamati tulitoa, kwa kweli zimeingizwa. Unaweza ukaona aliyena ule muswada wa Oktoba na huu, tofauti ni kubwa sana.Serikali imeanzisha mafao mapya, lakini imehakikisha mafaoyanayotolewa mifuko yote ni sawa, lakini under section 29inasema, bodi ikiona inataka kuanzaisha fao lingine, waondiyo wataangalia wataweka. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
218
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni suala la walewaliokuwa wana-benefit hasa kwenye fao la elimu. KamaSerikali inaona hilo fao hapana, naombeni wale watotoambao wazazi wao labda hawapo, ni maskini, wamefariki,waliokuwa wanasomeshwa kwenye arrangement hizo,tusiwaache barabarani. Wale ni watoto wa Tanzania,twende tuhakikishe mifuko hiyo inayowachukua, iendeiwafanyie kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naiomba Serikaliihakikishe inasimamia wafanyakazi wote wasipoteze ajirazao. Naamini wakifanya job evaluation, wakaangalia mifukoyote miwili, wakaangalia NHIF, wakaangalia WorkersCompensation, bado unaweza ukawa-rearrangewafanyakazi walioko kwenye hii mifuko yote na kila mtuakapata kazi na kama Taifa tukaenda mbele. Baada yakusema hayo, naunga mkono hoja hii na niwaombaWaheshimiwa Wabunge, tunaandika historia, tunatungasheria ambayo itafanya hifadhi ya jamii Tanzania iendeleekuwepo kwa muda mrefu sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Serukamba.
Waheshimiwa Wabunge, kwa mamlaka niliyonayonaongeza muda wa nusu saa kuanzaia saa 7.00 mchanahadi saa 7.30 mchana ili tuvutevute wachangie na wengine.Mheshimiwa Masele atafuatiwa na Mwalimu Bilagoni naMheshimiwa Zitto ajiandae.
MHE. STEPHEN J. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti,nami nianze kwa kuipongeza Serikali kwa kuleta Muswadahuu. Kipekee kabisa, nampongeza sana Mheshimiwa Wazirina timu yake ya Manaibu Waziri, kwa kuwa wasikivu nakupokea ushauri ambao sisi Waheshimiwa Wabungetumekuwa tukiutoa kwa Serikali kupitia Kamati. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza mambo mawili;la kwanza, maamuzi ya Serikali ya kuiacha NSSF ku-deal na
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
219
private sector pamoja na informal sector. Utafahamukwamba kwa population ya Tanzania, Watanzania wengiwako kwenye informal sector na wengi hawaratibiwi namfuko wowote. Kwa hiyo, maamuzi haya yanaifanya sasaWatanzania walio wengi ambao wako kwenye informalsector kupata fursa ya kuratibiwa na mifuko hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitazama kabisa NSSF iki-deal na informal sector itaweza kutoa mafao ambayoyatawanufaisha Watanzania wengi ambao ni wanyonge naambao hawana uwezo mkubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sheria hii, walewatumishi ambao ni wa Serikali na walioko kwenye mifukohii ambayo tunaiunganisha kupitia Muswada huu ambaotutatunga sheria, watafaidika na mafao mengi ambayo yakokwenye minimum requirements za ILO. Mimi nitajielekezasehemu moja hasa kwenye section number 29 ambapo kunaorodha ya mafao ambayo yapo kwenye Muswada huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitazama orodha hii, kunafao la matibabu halipo. Vilevile ukitazama kwenye sheriailiyoanzisha NSSF, tukiichukulia kama ni standard, fao lile lipo.Sasa nilikuwa naomba kushauri Serikali…
MWENYEKITI: Mheshimiwa Masele, samahani nikohapo kwenye section 29.
MHE. STEPHEN J. MASELE: Section 29, ukiangalia palesubsection (1)(a) “retirement benefits, survivors benefits,invalidity benefits, maternity benefits, unemployment benefits,sickness benefits and death gratuity.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa napendekezaSerikali ilete amendments iongeze medical benefits amahealth insurance benefits ili watumishi wa umma ambaowatakuwa wakichangia kwenye mfuko huu mpyatutakaouanzisha waweze kunufaika na fao hili moja kwamoja bila kuchangia tena kwenye NHIF. Ziko hoja
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
220
zinazungumzwa kwamba Watumishi Umma wote watakuwawananufaika na health Insurance kupitia NHIF.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizama kwa makini,unaona kwamba watumishi hawa wa Umma watakuwawanachangia mara mbili; wanakatwa kwenye NHIF iliwaweze kupata huduma, lakini kwa kuwa wao wako chiniya mfuko huu, pia watakatwa huku ambapo wakikatwahuku, moja kwa moja wana-qualify kupata huduma ya afya.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilikuwa naishauriSerikali, ilete mabadiliko hapa, iongeze medical insurance;na kupitia kukatwa huko kwa watumishi wa umma, huumfuko sasa upeleke hizo fedha kule NHIF ili ukagharamiematibabu ya wanachama ama members ambao watakuwani wanachama wapya wa mfuko huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivyo,tutakuwa tumewaondolea wanachama ama Watumishi waSerikali ama watumishi wa umma kuchangia mara mbili. Hiviilivyo, watakaochangia kwenye mfuko huu watakuwawanakatwa na upande wa NHIF ili wale members piawatakatwa. Kwa hiyo, mtumishi huyu atakuwa anakatwamara mbili kwa jambo lile lile ambalo anaweza kulipata kwakuchangia katika mfuko huu ambao tunatunga sheria leo.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naishauri Serikali naninaamini Mheshimwa Waziri na Mwanasheria Mkuu,watalizingatia hil i, walete mabadiliko i l i tuwezekuwaondolea michango ya mara mbili watumishi wa umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu ulikuwaumeegemea hapo. Naomba niunge mkono muswada huu,naomba Serikali izingatie maoni haya ili kuwaondolewamzigo watumishi wa umma. Nashukuru sana.
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Masele kwamchango wako mzuri, una mantiki. Acha Serikali iuangalie
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
221
kwa undani zaidi. Mheshimiwa Mwalimu Kasuku Bilago,Mheshimwa Zitto na Mheshimiwa Benardetha Mushashu.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante sana kwa nafasi hii. Kwanza ni-declare interestkwamba mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Huduma naMaendeleo ya Jamii, kwa hiyo, nimeusoma muswada huusana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yote katika yote, i l ituutendee haki muswada huu ni lazima kikokotoo kiingiekwenye kanuni. Kama kikokotoo hakitaingia kwenyemuswada huu kikaenda kwenye kanuni, Mheshimiwa Wazirianaweza akaja na yake ambayo hayatakuwa na maslahikwa wafanyakazi waliokuwa wakiyapata kwenye mifukoiliyopita. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu ya kufutwa kwa fullpension, ile tafsiri ya full pension ni baada ya kuona kikokotoocha 100 kwa 580 kinapigiwa kelele hakikubaliki kubaliki. Kwahiyo, ikaonekana kiondolewe halafu eti mtu akafanyaactuarial valuation ndiyo aweze ku-determine kikokotoo, nihatari sana. Mfanyakazi hawezi kuingia kwenye scheme;unamwingiza mfanyakazi kwenye scheme hajui mwisho wasiku atanufaikaje na scheme hii? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hiki kitu kiwe in black andwhite kwenye sheria. Hizi sheria tunazo-merge zote zilikuwazina formula. Kabla hujajiunga unaangalia formula ya PSPFinanifaa kwa kiasi gani? Formula ya NSSF inanifaa kwa kiasigani? Formula ya PPF, kwa hiyo, mfanyakazi anasema shouldI go to PSPF or NSSF or PPF? Baada ya kuona maslahi yanayomuhusu. Sasa tukienda kuficha kwenye kanuni, halafu sheriaiwe kimya kabisa, haina mafao yoyote, haionyeshi mwishowa siku itatusaidia nini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili halileti afyana kama Waziri anaona, ili kikokotoo kifahamike ni baadaya actuarial valuation, alitakiwa afanye actuarial valuationndiyo alete hoja ya kuunganisha kwamba hawa nimewaona
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
222
wakiungana, nimeridhika kwamba watakuwa na afya yakutosha kunufaisha wafanyakazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unakuja unaunganishaambapo hujui kwamba baada ya actuarial valuationwatakuwa na afya kiasi gani? Ukikuta baada ya kuungana,hali zao ni mbovu, ni mbaya kabisa, tutarudi humu tena kujakushughulikia hii kitu? Kwa hiyo, hilo naliomba kabisaWaheshimiwa Wabunge tukubaliane, tusipitishe sheriaambayo iko kimya, yaani hata leo tukitoka, unakwendakumuuliza mwenzako ambaye ni mfanyakazi aliyekonyumbani, hivi tutafaidikaje na huu mfuko? Nikistaafunitalipwa bei gani? Huwezi kumwambia bei atakayolipwa.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, kuna hiicutoff point ambayo inataka wafanyakazi waliokuwa katikasekta fulani wabaki huko tu-board na hawa wapya kwenyemfuko huu mpya. Basi ikiwezekana, vikokotoo vyaowalivyokuwa navyo vibaki. Kila watu wa board in kwenyemfuko huo na vikokotoo vyao. Kwa hiyo, waliokuwa na 540,waendelee na 540 yao mpaka watakapo-phase out,waliokuwa na 580 nao waingie humo wa-board in mpakawatakapomaliza. Kikokotoo kipya kitakachokuja kianze nawafanyakazi wapya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na nia njema kabisaya kuunganisha mifuko hii, tusisahau baadhi ya benefitsambazo zilikuwa kwenye mifuko ya zamani. Mfanyakazialiyekuwa ana-benefit kwenye mfuko aliokuwanaotusiipoteze ile benefit kwa sababu tu ya kuanzisha mfukompya. Mfuko mpya kama tunauanzisha na tunapotezabaadhi ya benefits, haina sababu ya kuunganishwa.Kuunganishwa kuboreshe kutoka pale tulipokuwa kwendasehemu nyingine bora zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa fao la elimulimeondolewa wakati mifuko mingine ilikuwa inatoa hilo fao.Fao la afya (health insurance) nalo linaondolewa wakatil i l ikuwepo. Sasa hivi vitu tusipoviangalia vitatuletea
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
223
confusion. Sasa mtu anajiuliza, huu mfuko mpya unanifaakweli au haunifai? Kwa sababu hata kuwa na option, yaanini kama tunatengeneza kitu ambacho utake, usitakeutaingia tu. Kwa hiyo, hiki ni kitu cha hatari sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 19 ambachokimtoza fine anayechelewesha makato, mwajiri ambayeamechelewesha makato. Tukubaliane ile fine inayotozwaimnufaishe na mfanyakazi yaani at the end of the daywanapo-calculate mafao yake, waangalie tulinufaikaje nafine? Isiwe fine tu inaunufaisha mfuko halafu memberhatanufaika nayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 18(2) kwenye (b)pale, kuna mahali ambapo tunazungumzia viwango vyakutoza, asilimia tano kwa mfanyakazi na asilimia 15 kwamwajiri. Pale chini pamesema hivi, baada ya kusoma (b):“or such amount as the Minister may by order published inthe Gazette determine taking into consideration of theactuarial valuation.” Maana yake nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna siku watafanyaactuarial valuation waone labda mfuko una afya mbaya,Waziri akaamua kuongeza makato. Inawezekana, yaani hiiinampa room Waziri kuongeza makato wakati tulishawekakwenye sheria ni 5% by 15% ya Mwajiri. Hivi kwa nini tusiondoehiki kifungu? Yaani kila siku akiamka tu akiona mifuko inaafya mbaya, anakwenda kuongeza makato. Mfanyakazianaishi bila ya kuwa na uhakika atamaliza anakatwa kiasigani? Kama ni 5% ibaki 5% na 15 ibaki 15. Kama anaiongeza,aiongeze kwa mwajiri, Mtumishi abaki na ile ile ya kwake.(Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante sana kwa mchango wako.Mheshimiwa Zitto Kabwe, atafuatiwa na MheshimiwaMashashu.
MHE. ZITTO Z. R. KABWE: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia muswada huumuhimu sana. Nadhani katika mambo ambayo tunaweza
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
224
tukasema kwamba tumeyafanya katika Bunge hili la Kumina Moja ni pamoja na muswada huu kwa sababu niMuswada ambao una mabadiliko makubwa sana ambayotunakwenda kuyafanya katika mfumo mzima wa hifadhi yajamii ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo moja la jumlaambalo napenda nilizungumze, ni kwamba hapa tumekaatunazungumzia jambo la 9% tu ya work force ya Tanzania.Kwa sababu mfumo wetu wa hifadhi ya jamii katika nchiyetu unagusia watu tu ambao wameajiriwa katika sektarasmi ambao ni watu 2,100,000. Watu 700,000 walioajiriwana Serikali na Mashirika yake na watu 1,400,000 ambaowameajiriwa na sekta binafsi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuna haja hukosiku za usoni tunakokwenda tujaribu kuona ni namna ganiambavyo tutakuwa na utekelezaji wa kisera na kisheria katikahifadhi ya jamii ili tuweze kuwafikia Watanzania wengi zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii napenda kutoa mfanohuu sana kwa watu wa korosho. Leo hii korosho ine bei nzurisana na wananchi wamepata fedha nyingi sana, lakini keshona keshokutwa bei ya Soko la Dunia ikiporomoka, watuwatalia kwa sababu hatuna mfumo wa hifadhi ya jamii kwawakulima ambapo tungeweza kuwapa wakulima fao la beipale ambapo bei zimekuwa zimetetereka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo jambo la msingisana ambalo ni lazima tulitazame lazima tuondokekuzungumzia 9% ya watu, tuje kuzungumzia Watanzaniawengi zaidi ambao hawaguswi kabisa na schemes za hifadhiya jamii ambazo tunazo katika nchi yetu hivi sasa
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ambalo napendakulizungumzia, limegusiwa kidogo na Mheshimiwa Masele,Mbunge wa Shinyanga Mjini kuhusiana na SHIB (Fao laMatibabu). Katika sheria hii mpya kuna hiyo provision yasickness benefit ambayo ndani ya sheria haijaelezwa inakuwanamna gan? Kwa sababu ni miongoni mwa vifungu viwili
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
225
ambavyo Serikali inasema Waziri na SSRA watavitoleaufafanuzi wakati mafao mengine yote ndani ya sheriayamewekewa ufafanuzi wa namna gani ambavyoitatekelezwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kustaajabishakidogo, ukienda kwenye consequential amendmentsambazo Serikali inazo ndani ya muswada huu, section 97,Serikali inafanya amendment ya Sheria ya NSSF. Sheria ya NSSFsection 21 inatoa health insurance benefit kwa wanachamawa NSSF. Sheria hii ambayo Serikali inaileta hapa, inaondoahealth insurance benefit kwa wanachama wa NSSF. Hili nijambo la hatari, kwa sababu sasa hivi NSSF ina zaidi yawanachama 600,000. Kwa hiyo, Serikali hii inakwendakutunga sheria kuwaondoa watu 600,000 kwenye takwa lakisheria la health insurance. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naelewa mkanganyikoambao Serikali imeupata kwamba inataka health insurancezote ziwe provided for na NHIF, inaeleweka. Tunachopaswakukifanya kwenye sheria ni kuweka provision inayosemakwamba fao hilo la health insurance litatolewa na NHIF, kwaNSSF kuchukua ile michango ambayo imefanyiwa mahesabuna actuarial kwamba ni percent ngapi ya michango ambayoinalipia health insurance, michango ile ipelekwe NHIF.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ukiwa na kadi yaNSSF wewe ni mwanachama wa NSSF, automaticallyunakuwa mwanachama wa NHIF. Hii ndiyo njia bora zaidiambayo Serikali ilipaswa kufanya na inapaswa kufanya.Nawashauri Waheshimiwa Wabunge, kama amendment hiihaitaletwa, tusiipitishe sheria hii kwa sababu tunakwendakuwaondoa watu 600,000 kutoka kwenye health insurance.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo moja tu ambalo nivizuri pia Serikali ifahamu kufuatia hoja ambayo MheshimiwaBilago, Mbunge wa Kakonko amezungumza kwambatunapotunga Sheria za Pensheni, wale ambao tayariwanafaidika na sheria sasa hivi, hawapaswi kufanywa kuwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
226
worse off. Wale wapya ambao wanaingia wakati sheriainatungwa, ndio wanapaswa kuendana na yale mashartimapya. Kwa hiyo, ni muhimu sana jambo hili l iwezekueleweka vizuri ili tusiweze kuwafanya watu wetu kuwakatika hali mbaya zaidi badala ya kuwaboresha zaidi.(Makofi)
Jambo la mwisho na ambalo limezungumzwa naMsemaji wa Kambi ya Upinzani, ni jambo ambalo sisi kamaTaifa ni lazima tuli-face, hatuna namna ya kulikwepa kamaambavyo tumelikwepa kwa miaka minne iliyopita, ni hikikinachoitwa fao la kujitoa au kujitoa kwenye mafao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huko nje vijana wengi sanawanataka fao hili liwepo kwamba hiyo ni innovation ambayoipo Tanzania. Inaeleweka kabisa dhamira ya Serikali yoyote,dhamira ya dola yoyote ni kujenga mazingira ambayo unamfumo madhubuti wa hifadhi ya jamii. Mfumo ambaohautakufanya baadaye uwe na wazee ambao hawanapension. Lazima ujenga hayo mazingira. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuja nainnovation ya unemployment benefit. Tumeijadili sana hiikwenye Kamati na Serikali imeongeza kifungu cha 35kuifafanua. Maelezo ambayo Serikali imetupa ya kwambawafanyakazi ambao wanatoka kwenye mafao, ambaowamekosa kazi walipwe asilimia 33 ya mshahara kwa mudawa miezi sita. Baada ya miezi sita fedha ile inayobakia iingiekwenye supplementary scheme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hayo ndiyo maelezoambayo Serikali imeyaeleza kwenye Kamati, haijayawekakwenye sheria kama mafao mengine namna ambavyoyamefafanuliwa kwenye sheria, ila ndiyo maelezo ambayotumepewa na masharti yamewekwa kwenye section 35. Miminadhani tulitazame hili jambo vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inalazimisha Mwajirikuchangia asilimia 10 ya mshahara wa mfanyakazi kwenyemfuko…
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
227
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda waMzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa BenardethaMushashu, atafuatiwa na Mheshimiwa Constantine Kanyasu.
MHE. BENARDETHA MUSHASHU: MheshimiwaMwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanzanampongeza sana Mheshimiwa Waziri, Naibu Mawaziri,Katibu Mkuu pamoja na Wakurugenzi Wakuu wa mifuko kwakuandaa na kutuletea huu muswada. Naipongeza sanaSerikali, nimeangalia huu muswada waliotugawia leoasubuhi, naona wamezingatia maoni ya wadau pamoja namarekebisho makubwa yaliyofanywa na Kamati. Ahsantenisana Serikali kwa kuwa wasikivu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, muswada huu unalengakuunganisha hii mifuko yote mitano tukabakia na mifukomiwili, mmoja wa Umma na mwingine wa binafsi kwa lengola kuboresha mafao ya wafanyakazi. Kwa hiyo, ni kitu kizuri,nakiunga mkono.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia Ibara ya 18 yamuswada huu inayozungumzia michango kwamba mwajiriatachangia asil imia 15 ya mshahara na mwajiriwaatachangia asilimia tano; lakini ukiangalia 18(b) hii imempaWaziri mamlaka ya kuweza kubadilisha viwango kadriatakavyoona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikitokea tukawa na Waziriwakati fulani ambaye hajali wafanyakazi, unaweza ukakutahuyu Waziri ameamua kupanga kwamba contribution yamfanyakazi iende mpaka asilimia 30. Hii inaweza ikawa shida,kwa sababu kwenye mshahara huo huo labda ukute alikuwani mwanafunzi anakatwa Bodi ya Mikopo, anakwata PAYE,anakatwa na vitu vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nafurahi kwambasasa hivi kwenye kipengele hicho wamebadilisha wakasemakwamba mpaka ifanywe actuarial valuation. Sasa nataka
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
228
nimuulize Mheshimiwa Waziri kwamba hiyo actuarialvaluation inafanywa kwenye mfuko au inafanywa kwamfanyakazi aonekane ana nguvu kiasi gani ya kuwezakuchangia? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ibara ya 20 inazungumzia juuya michango isiyowasilishwa. Hali ilivyo sasa hivi ni kwambaunakuta wastaafu wengi wanapostaafu, wanalipwa mafaokidogo sana kwa sababu michango ilikatwa kutoka kwenyemishahara yao, lakini haikuwasilishwa kwenye mifuko. Katikakipengele cha 20 kimeainisha kwamba huyu mtu sasa awemichango yake imeshawasilishwa kwenye mifuko auhaijawasilishwa, mfuko utatakiwa umlipe mafao yake yotena ule mfuko wenyewe ndiyo uendelee kudaiana na mwajiriHiki ni kitu kizuri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nilikuwa napendekezailivyoandikwa pale kwenye kipengele cha 20 kinachosema;“Where the Director General is satisfied that an employee’scontribution has been deducted from his earnings, but theemployer has failed to remit the contribution together withthe paid employer’s contributions to the fund, he shall treatthe unremitted contributions as wholly or partially paid tothe purpose...” Nilikuwa napendekeza neno “partially”liondoke pale, linaleta ukakasi kusudi tuhakikishe kwambahuyu mwajiriwa atalipwa mafao yake yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ibara ya 29 inazungumziamafao atakayopata mwanachama; ni mafao saba.Naipongeza Serikali kwa sababu wameweka mafao ya yuleambaye atakuwa amestaafu, lakini vile vile kuna namnaambapo huyu hajafikia umri wa kustaafu, atafaidika.Napenda kuuliza kwamba kuna invalidity benefits ambayoinahusu watu wenye ulemavu. Ni kitu gani kitalipwa na hiimifuko ya hifadhi ya jamii na kitu gani kitalipwa na WorkersCompensation Fund?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitu kinaitwaunemployment benefit, nawashukuru sana kwa kuliweka hilifao. Kwa mara ya kwanza katika Tanzania tutakuwa sasa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
229
tumetoa faraja kwa mtu aliyepoteza ajira. Pia naombaMheshimiwa Waziri atufafanulie zaidi, ni kitu gani huyu mtuanategemewa kupata kwenye unemployment benefit?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ibara ya 56 inazungumzia juuya msamaha wa kodi kwenye mafao. Hii ibara imekaa vizurikwa sababu huyu mtu amehangaika, sasa amefikia kustaafu,ukute na ile pension yake ya kila mwezi au ile gratuityanayoipata ikatwe kodi. Kwa hiyo, kipengele hiki kimesomekakwamba huyu mtu hatakatwa kodi. Kwa hiyo, naipongezaSerikali kwa kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ila ningependa kuona,inaweza ikatokea wakatunga Sheria za Kodi ambazozinalazimisha sasa kwamba ile pension ambayo iko kwenyesheria hii iende kukatwa kodi. Napenda kuona kwenyemuswada huu au sheria hii waweke kipengele kinacholindapension ya mfanyakazi kwamba hata zikitungwa sherianyingine za kodi zisilazimishe pension ya mfanyakazi kukatwakodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, msingi wa muswada huu nimapendekezo ya wafanyakazi na mategemeo yawafanyakazi ni kwamba mifuko hii iunganishwe; gharamaza uendeshaji zipungue, kusudi wao waweze kupata mafaomakubwa zaidi. Sasa bahati mbaya kikokotoo kweli hakipokwenye huu muswada na Mheshimiwa Waziri anasemawatakiweka kwenye kanuni. Napendekeza kanunizikishatungwa zipelekwe mbele ya Kamati itakayokuwainahusika hizi… (Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda waMzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa. MheshimiwaKanyasu.
MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: MheshimiwaMwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza naombaniwapongeze sana Kamati kwa namna ambavyo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
230
wameutendea haki muswada huu. Nilipousoma mwaka 2017na nilipokuja kusikiliza marekebisho, nimeona Kamatiwamefanya kazi kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sanaMheshimiwa Waziri na Naibu Mawaziri pamoja na Watendajiwote katika Wizara hii. Kama walivyosema wenzangu,kimsingi tunaiona nia ya Serikali ya kuunganisha mifuko hiina kuondoa gharama za uendeshaji kama ambavyozimetajwa katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri naMwenyekiti wa Kamati. Kwa hiyo, tunaiona hiyo nia na hilolengo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu hapa, nilidhanibaada ya Serikali kuondoa gharama hizo ambazo tumezionakwenye maelezo ya Mheshimiwa Waziri, basi zingekuja chinizikawa na faida kwa mwanachama wa mfuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyomalizia kusemaMheshimiwa Mama Mushashu, kwa kweli tulitarajia kuonakwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri kwamba mwisho wasiku sasa haya mafao yanakwenda kuongezeka kwa asilimiangapi au yanakwenda kuimarika kwa asilimia ngapi? Sasalinabaki kuwa kwenye Pandora box kitu ambacho nadhanitutahitaji pia baadaye kuanza kuhangaika na MheshimiwaWaziri. Kwa ujumla wake, napongeze sana, marekebishoyamezingatia sana maoni ya wadau.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, katika section 35 kamawalivyosema wenzangu, ni vizuri sana kufikiria kuhusu medicalinsurance na fao la elimu. Hivi tunapozungumza, watumishiwengi ambao walikuwa wamesoma Diploma, hawapatimikopo tena kwenye Bodi ya Elimu na wengi walikuwawanakimbilia kwenye mifuko hii kwenda kuomba mikopona baadaye wanakwenda vyuoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakapokuwa tume-mergena tukaliondoa hili kama ambavyo iko sasa, maana yake nikwamba liko kundi la watu hawatasoma tena kulingana nagharama za elimu zilivyo juu. Kwa hiyo, ni vizuri sana kwenye
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
231
section 29 kurudisha fao hili la elimu, kwa sababu mifukoilikuwa inatoa na wanachama walikuwa wakijiunga katikamifuko hii kwa sababu waliona kuna kitu wanakihitaji kwenyemfuko huo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine naipongeza sanaSerikali kwenye section 43. Mafao ya wastaafu yalikuwayanaweza kuchelewa mpaka mwaka mzima na hakuna mtualiyekuwa anajali. Ninao mfano wa watu ambaonimewasaidia, walicheleweshewa mafao yao kwa zaidi yamiezi sita, miezi nane na wako wengine mpaka leowanasubiri na hakuna interest, wala hakuna mtu aliyekuwaanajali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuweka provision hiikatika section 42 na 43 maana yake tunaweka commitmentkwa mifuko hii kuhakikisha kwamba hii miezi sita yamaandalizi na hizi siku 60 zilizotajwa katika sheria wasipolipawajue kwamba watalipa kwa interest. Interest haimasaidiisana mstaafu, kwa sababu mstaafu akili yake ikimpelekeakufikiri kustaafu, mara nyingi hufikiri aweze kupata malipoyake na kuendelea na maisha yake mengine. NaipongezaSerikali kwa kuweka commitment hii kwa sababu itatusaidiasana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine mimi natoka kwenyemaneo ya wachimbaji na mgogoro wangu mkubwa sikuzote umekuwa ni fao la kujitoa. Ninaishukuru Serikali, maelezoaliyoyasema Mwenyekiti wa Kamati na Mheshimiwa Waziri,yanaleta picha kwamba kuna namna inalishughulikia. Hivitunavyozungumza, wako wafanyakazi wengi waliokokwenye madini ambao wana zaidi ya miaka mitano, ambaowanasubiri sheria hii ili iwafungue namna ya kuendeleambele, kwa bahati mbaya sana haijawa clear bado. Badoimekuja ikiwa imefumbwa fumbwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba sanaMheshimiwa Waziri, wapiga kura wangu wanatakakufahamu sasa hasa wale ambao tayari wako nje wanasubiri
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
232
utaratibu kwa ahadi ya Rais aliyoitoa kule Kilimanjaro, ni ninikinafuata baada ya hapa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulimsikia Mwenyekiti waKamati anasema kutakuwa na hiyo asilimia 33 kwa miezisita na baadaye kuangalia kama hakuna tena ajira nyingine,basi mtu analipwa pesa yake, anaondoka. Tulione hili kwenyeutaratibu ili liwasaidie watu kuweza kujipanga na maishayao mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, tufahamukwamba tunapoiunganisha mifuko hii tunaondoa ushindanikwa kupunguza gharama, pia kuna madhara ya kuondoaushindani. Mara nyingi sana huko nyuma kabla ya mifuko hiikuwa mingi, pia hata customer care ilikuwa very poor. Lazimatulitambue hili kwamba baada ya mifuko hii kuunganishwa,watu watakuwa hawana option; wa umma watakwendahuku na wa upande wa binafsi atakwenda huku. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kukosekana kwa optionkunaweza kukawafanya watendaji wakalala usingizi. Kwahiyo, lazima tuweke mfumo ambao utaendelea kuifanyamifuko hii kuendelea kuhakikisha kwamba inajali hudumaza members wake, lakini pia inatoa huduma kulingana namikataba ambayo ipo.
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, kwa sababuya muda, kwa sasa ndiyo tuishie hapo.
Waheshimiwa Wabunge, nawashukuru sana. Kituambacho mimi kukaa hapa leo nimejisikia vizuri sana, nimichango yenu wote mmejielekeza kwenye muswada.Mmechangia ya jumla, lakini unakwenda kwenye Muswada,kwa sababu katika hatua hii ndiyo muhimu sana.Tutakapoingia sasa kwenye Kamati ya Bunge Zima, issues zoteambazo mlidhani kwamba Serikali ipate nafasi ya kuziona,zimo kwenye muswada huu.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
233
Waheshimiwa Wabunge wote, nawashukuruni sanamliopata nafasi ya kuchangia. Ni matarajio yangu nawengine watakaofuata wachache ambao watapata nafasijioni na wenyewe wafuate nyayo hizi. Hizi ndiyo shughuli zaWabunge, tunapofika kutunga sheria. Nawashukuruni sanakwa hilo.
Sasa baada ya kusema hayo, sina matangazo, lakininiwatangaze tu wale ambao tutaanza nao mchana iliwakajiweke vizuri. Tutaanza na wawili wa mwanzo, kwasababu tutashauriana na Serikali kwa jinsi ya mudanitakavyoona saa 11.00, lakini kwa uamuzi tuliochukua wadakika saba, ile saa moja itatupatia kama wachangiaji nane.Siyo haba lakini tutaona.
Sasa niwataje tu hawa wa mwanzo; tutakuwa naMheshimiwa Allan Kiula, Mheshimiwa Mtolea na MheshimiwaPascal Haonga. Tuanze na hao, halafu tutaona baadae.
Waheshimiwa Wabunge, baada ya kusema hayo,nasitisha shughuli za Bunge hadi saa 11.00 jioni.
(Saa 7.30 mchana Bunge lilisitishwa hadi saa 11.00 jioni)
(Saa 11.00 jioni Bunge lilirudia)
Mwenyekiti (Mhe. Andrew J. Chenge) Alikalia Kiti
MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, tukae.
Waheshimiwa Wabunge, nilikuwa nimewataja waletutakaoanza nao. Tunaanza na Mheshimiwa Allan Kiula,atafuatiwa na Mheshimiwa Abdallah Mtolea na MheshimiwaPascal Haonga. Tutaona muda unavyokwenda.
MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naminichukue nafasi hii kukushukuru kwa kuweza kunipatia nafasiya kuweza kuchangia muswada huu muhimu. Pil i,naipongeza Wizara na watendaji wote waliofanyia kaziMuswada huu kwa sababu umekuja kwa wakati muafaka
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
234
kabisa. Kwa hiyo, wale wanaoona kama ungeahirishwa auhaujatimia, mimi nasema muswada huu umetimia na ndiyowakati wake kuwasilishwa na ninasema umechelewa sanakuletwa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi hizo,lakini yako mambo kadhaa ambayo inabidi tuyaangalie sisikama Bunge na kuyatolea maamuzi. Mambo mengiyameshazungumzwa na Waheshimiwa Wabunge wenzangu,lakini nami nitajazia baadhi ya sehemu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ile section 19 inazungumziasuala zima la mwajiri kama atakuwa hajapeleka michango,yaani fursa ya mwajiri kutokupeleka michango. Uhalisia sasahivi ni kwamba inapotokea hali kama hii uyo mfanyakaziambaye amestaafu anastahili kulipwa mafao yake, huwaanapata shida kubwa. Kwa hiyo, hatutakiwi kutoa nafasiau fursa ya mwajiri kuchelewesha michango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sheria ingesematu kama mwajiri anatakiwa apeleke michango kwa wakatiinapo-fall due, basi, tukaishia hapo hapo. Kwa sababunafahamu kwamba kwenye mifuko wako ma-inspectorambao ndio kazi yao kufuatilia michango hii. Kwa hiyo, siyokazi ya mwanachama kufuatilia mchango. Kwa hiyo, hilo nijambo la muhimu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kipengele namba 22kinasema: “money paid in excess.” Hili lilivyoingia tu kidogolilinipa ukakasi, kwa sababu kama sasa hivi tuko kwenyemambo ya teknolojia (IT), kwa nini michango iende in excesshalafu tuanze kuangalia inarudishwa kwa utaratibu upi? Kwahiyo, hili jambo lingeweza kuangaliwa kwa sababu waowanaopeleka michango wanatakiwa wawe makini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, liko jambo lingine kwenyekuunganisha mifuko ambalo na lenyewe lipo lakini sijalionavizuri, labda Waziri mhusika atalifafanua. Wako wafanyakaziambao walikuwa wafanyakazi, wameshachangia kwenyemifuko hii inayounganishwa, lakini sasa hivi sio wafanyakazi
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
235
na hawachangii, lakini pesa zao bado zipo kwenye mifukona hawajachukua. Walikuwa wanasubiri muda wa miaka60 au 55 waweze kudai mafao yao. Sasa sijaona kwenyetransition au hili jambo litakuwa handled vipi? Wako wengisana wa namna hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia i le section 29inayozungumzia ile list ya mafao, Waheshimwia Wabungewameshazungumza suala la health benefit, ni jambo muhimusana likawekwa. Bunge hili lisikubali kupitisha sheria hii kamahilo jambo halitawekwa, kwa sababu jambo hilo ni muhimuna tumeona faida zake na wananchi wanahangaika. Mifukomingine ilianzisha involuntary contribution, lakini kwenyeinvoluntary contribution watu wanapata mafao na limewezakusaidia sana Watanzania. Kwa hiyo, ni fao muhimu naambalo ni muhimu likawekwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuunganisha mifuko,huko nyuma tulizungumza kwamba litapunguza gharamaza uendeshaji. Kwa maana hiyo tulitarajia kwamba gharamazilizopungua na wanachama wakiwa pooled kwenye mfukommoja, kutakuwa na ongezeko la kuondoa michango nakwa sababu michango hii itawekezwa ina maana kutakuwana ongezeko la uwekezaji. Kwa hiyo, mafao kama healthbenefit na mengineyo, fao la elimu wamezungumza, nimuhimu yakawekwa kwa sababu ni jambo ambalolinawezekana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine muswada huuumezungumzia suala la kwamba mafao hayatatozwa kodi.Sheria ya Kodi (Income Tax Act) section 10 (3) nafikiri inaelezakwamba iwe ina-override mambo yote. Kwa hiyo, jambohili labda Mheshimiwa Waziri aliweke vizuri ili atuhakikishiekwamba kodi haitatozwa kwenye mafao ya mwisho. Ni rahisitu, ni kuongezea pale kwamba “not withstanding”,tunaongezea maneno pale, mambo yanakaa vizuri. Kwasababu ni matarajio kwamba kwa kuunganisha mifuko,kutakuwa na manufaa zaidi na ndiyo imani ya Wabungekwamba kutakuwa na manufaa zaidi.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
236
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu ndioulikuwa huo na ningependa kusisitiza hayo mambomachache. Nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Kiula kwamchango wako, lakini pia kwa kututunzia muda.Mheshimiwa Mtolea.
MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nami nakushukuru, lakini namshukuru sana Mwenyezi Mungualiyenipa nguvu ya kusimama hapa na kukupa nguvu weweya kuniona na kunipa nafasi niweze kuchangia kidogo katikaMuswada ambao uko mbele yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli zilikuwa kelele zetuza muda mrefu sana kutaka marekebisho haya yaje ili tuwezekufanya maboresho katika hii mifuko ili Watanzania waliowengi wale ambao wapo katika ajira waweze kuonamwanga wa maisha yao ya kesho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulihitaji kweli kupunguzautitiri wa mifuko, lakini tulihitaji kuboresha maslahi yaliyomokwenye mifuko iliyopo. Sasa tungeweza kuipongeza Serikalikwa kuleta muswada, lakini kuuleta muswada peke yakebila kuzingatia vile vilio vyenyewe vilivyokuwa vikipigiwakelele na sisi Wabunge kwa niaba ya Watanzania, haisaidiisana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utakuja kugundua kwambakuna mafao mapya ambayo yanaanzishwa, lakini kunamafao ya muhimu yaliyokuwepo yameondolewa. Sasa hilisiyo jambo jema sana, kwa sababu lengo ilikuwa nikupunguza malalamiko ya watu. Sasa huwezi kupunguzamalalamiko ya watu kwa kuondoa vile vitu vizuri ambavyovilikuwa vikiwagusa katika maisha yao ya kila siku.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaona hapa limeondolewalile fao la afya (health benefit). Utagundua kwamba katikakipindi kilichopita ambapo fao la kujitoa lilikuwa limeondoka,wanufaika hawa walikuwa angalau wanaenda wanapata
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
237
ile huduma ya afya. Sasa hivi hilo fao limeondolewa,kinaletwa kitu kinachoitwa unemployment benefits ambayona yenyewe inaelea juu juu, hujui mtu huyu mnufaika atapatakitu gani? Unaambiwa kwamba kujua ni namna ganiitakokotolewa, Waziri atakuja kutunga regulations. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi ndio wenye kazi yakutunga sheria na siyo vizuri tukatunga sheria ya kumruhusuWaziri aende akatunge sheria. Tunatakiwa tumalizie hapa,tuwekewe hiyo hesabu ya kukokotoa ili tujue mtu akiwaamepoteza ajira, wakati anatafuta ajira, anapata kiasi gani?Tunajijua wenyewe, ukiiacha tu hivi na kusema Waziriatatunga regulations, inaweza kuchukua miaka mitatu auminne hapa hiyo regulation haijatungwa. Tuna hiyo mifano.Sasa hapa hata ile kazi yetu ya Kibunge ya kutunga sheriayenyewe haikamiliki katika kuweka mafao ambayo yanaeleakiasi hiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaona kifungu cha 31(2)kinatambua kwamba kuna Mtanzania kwa namna moja aunyingine atalazimika kuondoka hapa nchini, ama ataachakazi au atapata kazi kwenye nchi nyingine na sheriainatambua kabisa kwamba mtu huyu anaweza akaendaakarudi au akaenda asirudi. Mnatuletea hiyo special lumpsum benefit na yenyewe ni kiasi gani? Mtu kama anaondokanchini, bado unataka akuachie hela yake, ufanye nayo nini?Kwa nini humpi hiyo hela yake akaondoka nayo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unaona muswadaumekuja na mambo mengi ambayo hayajakamilika, yaanivitu viko nusu nusu. Miswada ya namna hii kwa kwelihaitusaidii. Vilevile inatunyima fursa na sisi kama Wabungekuitunga sheria ambayo tukimaliza tu, Mtanzania atakuwaanaguswa moja kwa moja. Sasa hata tukishaipitisha hii leohapa, bado kazi kubwa anaachiwa Waziri. Kwa hiyo, sisitunakuwa bado hatujafanya ile kazi yetu ya kimsingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, ukienda kwamfano pale kifungu cha 57(1) kinasema hivi, kwa ufupi tunikisome. Anasema: “The board shall at interval of three year
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
238
or at any other intervals...” sitaki kuendelea huko. Hivi ukisema“the body shall’, halafu unasema at interval of three year orany intervals;” sasa hapo “shall” ilikuwa na kazi gani? Kwasababu unapoweka “shall” ni lazima ukasisistize lile jambo,lakini kumbe jambo lenyewe bado linaendelea kubaki nidiscretion ya mtu ambaye atafanya hayo maamuzi. Kwa ninitunatumia “shall”? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mmekwenda mbali zaidimkaongeza kifungu kingine cha 57(2), mnazidi kusisitiza hilohilo kwamba kumbe hii actuarial valuation siyo jambo lamsingi kwenu. Sasa kama siyo jambo la msingi, kwa ninimnalirudia, mnaliandika halafu mnalitoa? Mngechaguamoja au kuliweka au kutoliweka kuliko kufanya namna hii.Maana yake hapa tutaonekana sasa kama tumekujakupitisha mafao ya kijanja kijanja hivi, jambo ambalo siyozuri kwa Bunge letu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nashauri, hikikifungu, maana yake hata kwenye drafting tu ya mambohaya ya kisheria hapa inatudhalilisha. Kwa hiyo, mnawezamkaenda kuifanyia marekebisho au mkaondoa kabisa hiyosub-section two, kama hamtaki ku-edit hiyo sub-section one.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nazidi kusisitiza kwambakitendo cha kutokuwa na kikokotoo katika Muswada huukimeondoa ile maana nzima ya sisi kuja kutunga sheria nakuwasaidia hao wanufaika wa hii wa mifuko ili wajue ni kitugani watakipata baada ya kuwa wamepoteza ajira kablaya kutimiza hiyo miaka 50. Fao lao la kujitoa bado linahitajikasana na kelele za Watanzania katika hili hazitaisha.Nakushukuru sana. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante sana. Nakushukuru kwamchango wako. Tunaendelea na Mheshimiwa PascalHaonga, atafuatiwa na Mheshimiwa Hawa Mchafu.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru sana. Ninaomba na mimi niweze kuchangiamuswada wa kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
239
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshauriMheshimiwa Waziri, yale yote ambayo Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni imewasilisha ni vizuri akayachukua naakayafanyia kazi kwa sababu yana faida kubwa sana.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine kamaulivyotangulia kuzungumza tunapokuwa tunatunga sheriaza nchi yetu, ni vizuri basi hata yale ambayo yanatoka kwamtu ambaye ni wa upande mwingine, ili mradi tu kama yanamaslahi mapana kwa Taifa letu, ni vyema tukayafanyia kazi.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba niungane namchangiaji Mwalimu Kasuku Bilago kuhusu ile formulakutokuwekwa kwenye muswada huu. Mara nyingi sana wotetunajua kwamba mara nyingi sana kanuni zimekuwa nikichaka cha Serikali kujifichia. Mara nyingi sana zimekuwa nikanuni ambazo Waziri peke yake anaenda kujifungia,anaangalia nifanye nini, nadhani siyo sahihi hata kidogo. Kwahiyo, nashauri kama alivyotangulia kuongea mzungumzajiwa kwanza kwamba jambo hili ni vema basi, kwa maanaya formula ingeweza kuweka kwenye muswada na badalaya Waziri kwenda mwenyewe kupeleka kwenye kanuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna Mbunge ambayeanashiriki kwenye kutunga hizo kanuni. Sasa Wazirianapokuwa amekosea na yuko peke yake na ukiwa pekeyako ni rahisi kukosea, kwa hiyo, ushauri wangu ni kwambatu ni vizuri ingeweza kuletwa formula hapa tukajadili kwapamoja, tujue sasa hawa wastaafu wetu watanufaika vipituweze kujadiliana kwa maslahi mapana ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme tu jambolingine kwamba hata ile denominator ambayo inatumikakwa sasa ile 540 kwa 580 bado unaweza ukaona kwambasiyo nzuri kwa wastaafu wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo 540 ipo tangu kipindicha ukoloni, ni ya muda mrefu sana. Kwa hiyo, kama lengo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
240
ni kui-merge mifuko hii ili kuboresha mafao ya wastaafu, basiingekuwa ni vema tungeboresha hata tuweke denominatorya 520. Tukiweka denominator ya 520 wastaafu wetuwatanufaika vizuri, watapata pension ya kutosha na mwishowa siku tutakuwa angalau na sisi tumeingia historia yakutengeneza ya kwetu kuliko ile ambayo tulitengenezewana Wakoloni miaka hiyo ambayo ni 540 ambayo siyo nzuri,inawanyonya watumishi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Waziri, kwa hiyo, nashauri hapaMheshimiwa Waziri katika jambo ambalo ukilifanya naaminiutakuwa umetendea haki Watanzania ni pamoja na kuwekahii denominator 520 ambayo itakuwa ni jambo jema nawastaafu wetu wataenda kupata pension ya kutosha namwisho wa siku wataishi bila stress hapo watakapokuwawamestaafu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ni jamboambalo linahusu wale watumishi ambao wako kwenyemifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii. Huyu MheshimiwaWaziri anahusika na mambo ya kazi na ajira, siyo ajabu keshona keshokutwa akaleta tatizo lingine la ajira. Kwa sababuhawa watu wameajiriwa kwenye mifuko mbalimbali,atakapokuwa ana-windup atuhakikishie hapa kwamba je,wale ambao wameajiriwa kwenye mifuko mbalimbaliwatachukuliwa kupelekwa kwenye mfuko mpya, hii mifukoambayo itakuwa imeunganishwa? Kwa sababutusipolichukulia vizuri hili, mwisho wa siku wale wotewalioajiliwa watakuwa wamepoteza ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwenye kupoteza ajira,tunaweza tukapoteza watu wengi sana. Kwa mfano,ukichukua PSPF, iko karibu kila mkoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ngazi ya mkoa kunamtu mmoja anaitwa Afisa Mfawidhi, pia kuna kuna mwingineanaitwa Afisa Mfawidhi Msaidizi na kuna madereva. Sasahawa wapo kwenye kila ngazi ya mkoa, je, watawachukuawote hawa kwenda kuwapeleka kenye mifuko mingine hiiau ndiyo watakuwa wameshawatelekeza?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
241
Unapowatelekeza maana tafsiri yake ni kwamba badala yakutatua tatizo, unakuwa umesababisha tatizo kubwa laukosefu wa ajira. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kwambabaada ya mwanachama kufariki wategemezi watanufaikakwa miezi 36 tu. Sasa jambo hili labda naomba MheshimiwaWaziri atusaidia mwishoni hapa, criteria ipi ilitumika kusemakwamba hawa wategemezi anufaike kwa miezi 36? Kwanini isiwe miaka mitano? Kwa nini isiwe miaka 10? Kwa niniisiwe miaka nane? Maana yake hii miezi 36 ni sawa na miakamitatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Waziriatuambie ni criteria ipi ilitumika kuweka miezi 36 na siyo miakamitano au 10 na kadhalika? Atuambie aliangalia kitu gani?Kwa sababu siku moja nimewahi kumsikia akisema mifukoyetu itafika mahali itakosa fedha za kujiendesha. Sasa kamaitakosa fedha na kuna mtu alikuwa anachangia, tusijetukawatesa wategemezi ambao mara nyingi unajua kabisawengi wanakuwa wanateseka kwa sababu tu watu waowaliokuwa wanafanya kazi wamefariki, tunakuja kuachamiezi 36 tu. Kwa kweli hii naomba tu watusaidie, kwa niniisiwe miaka mitano au 10?
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusumadeni makubwa ambayo mifuko hii inaidai Serikali. Kwenyehotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani tumesikia wote kwambakwa mfano PSPF waidai Serikali karibu shilingi trilioni tatu.Sasa kama hili jambo ndivyo ilivyo, hebu tuambiwe vizuri:Je, hii mifuko italipwa hizi fedha kabla ya kwendakuiunganisha au yale madeni yatahamishwa kutoka kwenyemifuko tuliyokuwa nayo sasa kwenda kwenye ile mifukomingine ambayo sasa tutakuwa tumeshaipata ile miwili kwamaana ya PSSF na ile mingine ya NSSF? Kwa hiyo, kamatutahamisha madeni, hiyo pia tutataka tuambiwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kama hayo madeniyakihamishiwa kule kwenye mifuko mingine hii mipya, kama
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
242
Serikali itaendela kukopa mifuko hii, hii mifuko haita-survivekwa muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni vizuri Serikaliikaangalia utaratibu mwingine wa kutafuta fedha kulikokwenda kukopa kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii. Inafikamuda watumishi wengi wanataka kustaafu, Serikaliimeshakopa fedha wanahangaika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli Serikali…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda waMzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante sana. Ahsante kwa mchangowako. Tunaendelea Mheshimiwa Hawa Mchafu, atafuatiwana Mheshimiwa Masele na Mheshimiwa Mwita Mwikabweajiandae. (Makofi)
MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia Muswadauliopo mbele yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya uchache wamuda, niende moja kwa moja kwenye Ibara ya 29 ambayoimeweka orodha ya mafao pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuiomba Serikaliyangu ione sasa umuhimu ili iweze kuja na amendmentiongeze fao la elimu. Kwa mujibu wa ILO, minimum standardya haya mafao ni tisa, sisi hapa tuna saba, haitakuwa mbayasana tukiongeza fao la elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tukiacha hivyo, Serikaliya Awamu ya Tano ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John PombeMagufuli, tayari inatoa elimu bila malipo kuanzia darasa lakwanza mpaka kidato cha nne. Kwa hiyo, itapendeza kamamfuko utatoa fao la elimu ili kuweza kusaidia kwa Kidatocha tano na cha sita, mwanafunzi huyu akimaliza, anakutana
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
243
na Bodi ya Mkopo kuweza kupata mkopo kuendelea naelimu yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa pili ukohapo hapo kwenye Ibara ya 29 kuhusiana na unemploymentbenefit. Naipongeza sana Serikali kwa kuona umuhimu wakuja na fao hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu sananchini kwetu kumekuwa na taharuki au sintofahamu yawithdrawal benefit. Kwa hiyo, naipongeza sana Serikali kwakuliona hili. Ukichukua ripoti ya Upinzani ambapo katikaukurasa wake wa 12, wao wanavyoona, fao la kujitoalinaenda kuchukua nafasi ya withdrawal benefits. Hivi ni vituviwili tofauti, unapuzungumzia withdrawal benefit ama faola kujitoa kwanza kwa mujibu wa ILO, hakuna fao la kujitoaau hakuna withdrawal benefit. Kwa wao hilo siyo fao,ukienda kwenye orodha ya mafao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unapozungumziawithdrawal benefit, tafsiri au maana yake mwanachamaaliyechangia kwa muda wa miaka nane akaja akapatajanga la kupoteza ajira, maana yake anaenda kwenye ulemfuko anatoa yale mafao yake. Baada ya mwaka mmojaau miaka miwili, akipata ajira anaenda tena kuanza sifuriama kuanza moja. Sasa hapo tunamsaidia mwanachamaama tunamuumiza huyu mwanachama? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuja na hili fao launemployment benefit litaenda kuwasaidia wenzetu ambaokatikati ya ajra yake amepata bahati mbaya ya kupotezaajira.
TAARIFA
MHE. HALIMA J. MDEE: Taarifa.
MWENYEKITI: Taarifa.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
244
MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti,nilikuwa tu nataka kumpa taarifa Mheshimiwa Mchafu, nimuhimu akasoma vizuri taarifa ya Kambi Rasmi ya Upinzani.Kambi Rasmi ya Upinzani hakuna mahali popote kwenyehotuba tulikosema withdrawal benefit ni sawa naunemployment benefit. Hakuna mahali tuliposema, kwa hiyo,ni muhimu arejee vizuri ili kutokupotosha maelezo. (Makofi)
MWENYEKITI: Mheshimiwa Hawa Mchafu, unaikubalitaarifa au unaikataa?
MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti,siipokei taarifa yake, achukue ripoti yake, sitaki kupotezamuda, dakika ni saba. Asome mstari wa mwisho.Imeandikwa tu kwa kiswahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najaribu kuwapa elimu yawithdrawal benefit. Unapoenda kumwambia mtu aka-withdraw mafao yake unacho…
MHE. HALIMA J. MDEE: (Hapa hakutumia kipaza sauti).
MHE. HAWA M. CHAKOMA: Hiyo siyo sababu, naweumekaa mwaka mmoja exile ndiyo maana huelewi ninitunafanya humu ndani. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, unapomwambiamwanachama aka-withdraw mafao yake aliyochangia kwamiaka nane, unaenda kumuumiza huyu mwanachama. Kwasababu ili u-qualify kupata pension ni miaka 15. Kwa hiyo,kama leo ana-withdraw mafao yake, akija baada ya miakamiwili akipata ajira, tafsiri yake anaanza sifuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikalikwa kuja na unemployment benefit, maana huyumwanachama ikitokea bahati mbaya amepoteza ajira,kutokana na fao hili, ataenda atalipwa asilimia 33.3 yamichango yake kwa muda wa miezi sita. Ikipita miezi sitaikitokea hajapata ajira, atahamishwa kutoka kwenyemandatory scheme atapelekwa kwenye supplementary au
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
245
voluntary scheme. Ataendelea kupewa michango yake kwamuda wa miezi 18 tukiamini baada ya hiyo miaka miwiliatakuwa amepata ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali yangu sasaiboreshe tu hapa kwa kuangalia baada ya ile miezi sita naile miezi 18 ambayo amehamishiwa kwenye voluntaryscheme, ikitokea amepata ajira, je, tutamrudisha tena kulekwenye mandatory? Tukimrudisha, tunaanzaje kuhesabu?Kwa hiyo, naiomba Serikali yangu ikiweke hicho kifungu kizurikabisa cha unemployment benefit ili kuweza kuwasaidiawatumishi wa Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye Ibara ya 35.Ibara hii pia inazungumzia suala hili la unemployment benefit.Ili tukae vizuri kabisa na tuondokane na hizi kelele zawithdraw, naona kile kifungu cha 35(2)(e) ambachokinasema; “proves to the Director General that he has notsecure, another employment.” Ni ngumu sana kuli-prove hilikwmaba sijapata ajira. Hili limekaaje? Naomba MheshimiwaWaziri atakapokuja ku-windup, alitolee ufafanuzi hili ilikuondoa huo ukakasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tuzungumze kuhusianana suala la formula kuwepo kwenye muswada huu. Suala lakutumia moja chini ya 520 ama moja chini ya 540 ama 580hatukurupuki tu kwa utashi wa kiasiasa na tukasema twendetutumie hii. Ni lazima tukafanye actuarial report, hii ndiyoitatuongoza tunaenda na mtindo gani ambapo tutaangalianamba ya wachangiaji, namba ya wastaafu, namba yauwekezaji na kadhalika. Hiyo ndiyo itakayosema tunaendakwenye formula ipi? Siyo tu mtu unaamka unataka ile formulaambayo unaitaka wewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kile kinachosemekana kanakwamba Serikali imekuja na merging as if haijafanya actuarialreport, no, Serikali imefanya. Pengine labda mwendemkasome, mkatafute. Tukienda na hii 100 chini ya 540 maanayake, contribution rate iende ikapande mpaka asilimia 35?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
246
Sasa are we ready kwa wafanyakazi wetu wachangie kutokaasilimia 20 mpaka…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda waMzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante. (Makofi)
Nakushukuru sana kwa mchango wako. MheshimiwaMwita Mwikwabe, atafuatiwa na Mheshimiwa MussaMbarouk.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Asubuhi wakatiunamalizia kipindi cha asubuhi, uliwapongeza WaheshimiwaWabunge kwa kuchangia vizuri na ukasema katika utungajiwa sheria ni jambo muhimu sana, ni muhimu watuwakajielekeza kwenye hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kujielekeza hukokwenye hoja, ni pale ambapo mimi kama Mbunge nasemayangu. Tukianza kusema Mbunge wa upande huu ametoahoja wewe unamjibu kama Serikali, kwa kweli hatuendimbele. Nadhani hilo ni jambo la msingi sana kuzingatia.Tuache Serikali iwajibu hoja ambazo wamepewa il iwatusaidie twende mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hii sheria, kimsingihuko mtaani na wananchi wetu na hasa watu ambaowanafanya shughuli za kimikataba wanatarajia kwambasheria hii inapopitishwa leo wapate ahueni ya kupata tibaya malalamiko mengi ambayo wanayo mtaani kule. Kunawatu ambao wanafanya kazi migodini, wameachishwa kazi,hawana ajira wamekuwa blacklisted maeneo mengiwanataka hii suluhu wapate wafao yao waanze maishamengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu ambaowameajiriwa wakamaliza mkataba wao, fedha zao
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
247
wamezuiliwa, wanaambiwa ni baada ya miaka 55,wanatarajia tupate majibu hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naona ni jamboambalo ni muhimu sana na ndiyo maana Wabungewakaomba hii sheria ilipaswa ipewe siku mbili mpaka tatukujadiliwa kwa sababu tunajadili maisha ya watu wetukatika Taifa hili. Hapa ndiyo mahali pekee tunawezakuwasaidia. Sasa nitashangaa tunaanza kulumbana kwa vituambavyo havina maana sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ibara ya 27(b) kamawenzangu walivyozungumza kwamba inatajwa kutakuwana kulipa mafao ya jumla, lakini hapa ambacho tungeomba,tungetaka formula ambayo itatumika kutengeneza fedhahizi ijulikane kwenye sheria. Tunataka hii iingizwe kwenye sheriatufahamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu mtindo wa kumwambiaWaziri atakaa peke yake, atengeneze sheria, halafu atatoakiasi gani kwa kweli ni kama tunawaambia watu kwambahuo utaratibu watapata fedha lakini hawajui kiasi gani nahakuna namna ambayo tutarudi kuja kujadili tena hapa. Kwahiyo hili jambo lingewekwa kwenye sheria na formula hapatuzi-testify kwamba kama mtu anapewa milioni kumi, formulahiyo inampa outlet shilingi ngapi, ijulikane hapa! Lakini hilijambo kulificha kwenye kanuni kule, Waziri aende akakaena wenzake atengeneze halafu alete, sisi Wabungehatutamhoji, hatutaiona ataweka kwenye gazette,wananchi wetu hawataona, wataendelea kupiga kelele nakulalamika mtaani bila majibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, jambo hil ikwakweli ni kubwa kwelikweli lilipaswa liwekwe wazi kilaMtanzania ajue na Wabunge wajue, tupitishe kitu ambachotunakijua kwamba hii formula, inawezekana. Kamainashindikana, wataalam wa hesabu tupo hapa, tulete,tusaidiane, tuitoe hadharani ijulikane ili watu wapate majibu,hakuna sababu ya kuficha formula hii ya kupata fedha yaWatanzania wetu ambazo kimsingi ni jasho lao. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
248
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, niliona kwenyeBodi pale ambayo wameweka kwenye schedule nambamoja, provisions relation rating to the Board. Hapa kunamambo yafuatayo; moja, wametaja Wajumbe wote, sikuonakama watazingatia gender balance katika eneo hili.Wametaja nafasi, lakini kwa sababu kwa namna yakuboresha kwamba angalau jinsia nyingine ishirikishwe, kwakulazimisha il itakiwa itajwe kwamba katika Bodiitakapokuwa ina-appoint hawa wahusika, watazingatiagender. Hilo jambo sikuliona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, wamesemakutakuwa na uwakilishi wa taasisi ambazo zina ajira kubwa,most employee organizations. Hapa unapozungumzia ajirakatika nchi hii, kuna watu ambao wana mahitaji maalum,sikuona uwakilishi wao katika eneo hili kwamba angalauwale wenye mahitaji maalum na wenyewe angalau mtummoja ambaye atawawakilisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maanawasipokuwepo hapa, madai yao mbalimbalihayatazungumzwa. Watazungumza mtu kama mimi ambayesina mahitaji maalum, nina viungo kamili, sina ulemavuwowote. Hawa watu wanahitaji wapate mtu hapa wakuwasemea kwenye Bodi hii kwa kuzingatia mahitaji yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho, hii sheriaambayo inayojadiliwa leo kwamba inapitishwa, ndiyo sheriaambayo kila Mbunge, message ambazo mnatumiwakwamba watu wanalalamika mtaani hawana haja,wanataka fedha zao; wale watu wanauliza, kwa nini miminifanye kazi, nimemaliza miaka sita au kumi, unaniambianisubiri miaka 55, nina watoto ninasomesha; na mwingine nimgonjwa, angefanya biashara aanze maisha yake mengine.Kwa nini unamlazimisha? Yaani kazi ya ajira imekuwa tenani utumwa kwake, analazimishwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, jambo hili nadhaniMheshimiwa Waziri na Serikali kwa ujumla na Wabunge waBunge hili Tukufu ni muhimu tujielekeze tukitoka humu ndani,
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
249
wananchi wanaolalamikia fedha zao ambazo wamefanyiakazi tusiwalazimishe matumizi yao. Tuwa-guide lakini tutoetiba ya jumla katika jambo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anajua,mara nyingi tumekwambia sana watu wanalalamika mtaani,tupate majibu! Kwa mtindo ambao nauona huu ambapowatu wanajigeuza kuwa upande wa Serikali, kazi ya Bungetunatunga sheria, sisi tunaishauri Serikali, tunaiwajibisha.Humu ndani tumejigeuza, tumejipa vyeo, Mawaziri, Kamati,tunazungumza hapa. Ndiyo picha inayoonekana hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani mimi Mbunge hakunatofauti na Waziri, wala hakuna habari ya chama hapa. Hapani kwamba sisi Wabunge tuisimamie Serikali, wananchi wetuwanalalamika, sheria hii inawaumiza, wanataka fedha zaowajenge nyumba, wakopeshwe, watibiwe na wasomeshe.(Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante sana. Nakushukuru kwa kuokoana muda pia. Naelekea kwa Mheshimiwa Mussa Mbarouk,halafu bado nina muda kidogo. Baada ya MheshimiwaMbarouk nitamwita Mheshimiwa Sonia Magogo.
Mheshimiwa Mbarouk, huwezi kusema, hujawa tayari!Mimi nimekuita, kama huwezi kusema nafasi imepotea.Mheshimiwa Sonia Magogo.
MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante kwa kunipa nafasi ya kuchangia…
MWENYEKITI: Samahani kidogo. Mheshimiwa Halima,naomba utulivu tu Bungeni. Msijibishane huko, kama una hojaielekeze kwenye kiti. Mheshimiwa Sonia.
MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante. Kwanza kabisa, napenda kuipongeza Serikali kwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
250
kuleta muswada huu wa kuunganisha mifuko. Ninaona niwakati muafaka kabisa kwa kuwa hiki kilikuwa ni kilio chamuda mrefu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kuipongezaSerikali, nil ikuwa napenda kutoa angalizo, kwa viletunakwenda kuunganisha mifuko na kunakuwa kunamonopolization, kwa hiyo hakuna ushindani kati ya mfukommoja na mfuko mwingine kama ilivyokuwa mwanzo,napenda kuishauri Serikali iwe makini sana katika hudumazinazokwenda kutolewa na mifuko hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanzo kulikuwa na mafaoambayo yanatolewa ambayo yalikuwa yanatumika kamakichocheo cha kuvutia wanachama kutoka mfuko mmojakwenda mfuko mwingine. Vilevile mifuko ilikuwa inajitahidikila mfuko utoe huduma bora zaidi ya mwingine ili kuwezakuvutia wanachama zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokwenda kuweka hilisuala la kuwa na mifuko miwili ambapo mwanachamahatakuwa na nafasi ya kuchagua aende mfuko gani, nilikuwanaishauri Serikali iwe makini sana kuhakikisha kwambawanachama hawa hawapati usumbufu katika hudumawanazokwenda kuzipata. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ningependakuongelea kuhusu suala la fao la unemployment ambalolimekuwa introduced kwenye muswada. Hili fao kwa kwelinami naliunga mkono. Mimi ni mmoja wapo wa watuambao walikuwa wanatoa huduma kwenye Mifuko yaHifadhi ya Jamii.
Kwa hiyo, wakati mwingine nilikuwa nakutana nawanachama ambao walitamani kuwepo na fao kama hiliili liweze kuwasaidia kulinda credit zao pindi watakapostaafu.Kwa kuwa kulikuwa hakuna hili fao, ilibidi kipindi kingine wa-withdraw hata bila kupenda pamoja na kwamba walikuwabado wana credit chache ili waweze ku-qualify kuwapensioners.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
251
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunakwenda kulitoahili fao la unemployment, naishauri Serikali iangalie hili faolinakwenda kutolewaje na litawasaidiaje wale waathirikawa hii unemployment kwa kipindi kile ambacho watakuwahawana kazi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huo huo naishauriSerikali iangalie, kuna makundi kadhaa ambayo sidhani kamahii unemployment benefit ambayo ni sehemu tu ya mafaoitaweza kuwasaidia. Mathalani wale wanaofanya kazi kwamikataba mifupi na hawana tena room ya kwenda kupatakazi sehemu nyingine na vilevile kuna wengine ambaowanapata ugonjwa ambao kwa ripoti ya Daktari unaonakabisa huyu mtu hawezi kuja kuendelea na kazi au labda ilepesa angeweza kusaidiwa kupata, ingeweza kumsaidiakatika matibabu au shida anayoipitia.
Kwa hiyo, naiomba Serikali, pamoja na kuondoa faola withdrawal, lakini naomba waangalie makundi. Kuna kesiambazo ukiliweka hili fao la unemployment na wakashindwakupata ile pesa yao, bado tutakuwa hatujawatendea haki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambachoningependa kuishauri Serikali, kwa kuwa sasa hivitunakwenda kuwa na mifuko miwili, sioni tena sababu yamfuko mmoja unakata asilimia 15 kwa asilimia tano na mfukomwingine unaendelea kukata asilimia 10 kwa asilimia 10.Naiomba Serikali, kwa kuwa sasa hivi tunakwenda kuwa namifuko miwili, mifuko yote iwe uniform; wote wawewanakata asilimia 15 kwa mwajiri na asilimia tano inakatwakutoka kwa mfanyakazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwa upande wamafao, nilikuwa naishauri Serikali iyapite upya mafao ambayowameyapendekeza. Ukiangalia vitu vikubwa ambavyovinamuumiza mwanachama, ni elimu na afya na miminapendekeza kama wenzangu waliotangulia kwambatuangalie fao la elimu. Fao la elimu ni muhimu sana kwawanachama na tutakwa tumewasaidia kutua mzigo navilevile tutakuwa tunatengeneza kizazi ambacho baadaye
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
252
kitakuja kuwa wanachama wetu wa Mifuko ya Hifadhi yaJamii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naishauri Serikali kwasababu tayari wafanyakazi watakuwa ni wanachama waNSSF, sioni sababu tena ya yule mwanachama kukatwa pesakwa aji l i ya matibabu ya NHIF. Kwa hiyo, ni vyemamwanachama ambaye atakuwa tayari yuko kwenye Mifukoya Hifadhi ya Jamii akaunganisha moja kwa moja kupitia ilemichango yake kikawa ndiyo kigezo cha yeye kumfanyaatibiwe kupitia NHIF. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambachonaomba kuishauri Serikali ni hili suala la kusema kwambaMfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Umma utachanganywa nayale makampuni ya private. Kwangu mimi hili naona kamalitakuja kuleta mkanganyiko, kwa sababu terms za publicservice ukiangalia na private ziko tofauti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama hawawafanyakazi wa Private Sector watakwenda kwenye PublicSector baadaye itakuja kuleta shida hata kwenye suala launemployment, kwa sababu terms zao hawa, anaacha kazihapa leo, anahamia hapa. Kwa hiyo, itakuwa badala yaku-concentrate kuendeleza hii mifuko, kila siku itakuwa niku-deal na hilo fao la unemployment.
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa kwamchango wako. Tunaendelea, Mheshimiwa Richard Mbogo.(Makofi)
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante. kwanza naomba nishukuru kwa hii nafasi.Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kutupa uhaimpaka dakika hii.
Naomba nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwakufanya kazi na Kamati hii na wameweza kufanya vizuri sanakwanza kwa kuchukua maoni ya Kamati na kuwezakuyafanyia kazi na kwa ushahidi, ukiangalia muswada huu
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
253
hatuna schedule of amendment mezani za Wizara, inaoneshajinsi gani walikuwa wasikivu na wameweza kuchukua maoniya Kamati na wadau mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo machache tu;la kwanza ambalo naomba nisisitize upande wa Serikali,kwamba baada ya kuunganisha hii mifuko, naomba sanatuangalie suala la kulinda hizi ajira za watumishi waliopokatika hii mifuko. Kama tukiangalia suala la wastaafuwangapi ambao ni wafanyakazi ndani ya hii mifuko, basituzilinde ajira kwa watu waliopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pil ilimezungumziwa kuhusu suala la kujitoa. Kuna sekta nyingineambayo hatujaiangalia kwa umakini. Kwa mfano, mtu labdaana miaka 50, anajitoa katika mfuko kwa sababu tuamepata ajira au kwa mfano, mtu amechaguliwa kuwaMbunge, anaenda kwenye sheria nyingine ya wastaafu kwaupande wa kisiasa, ambapo kuingia kwenye hii mifukoinakuwa ni hiari.
Sasa kwa mtu ambaye ameacha kazi, ameingiakwenye Ubunge, kwa nini mtu kama huyo asifikiriwe kwenyefao la kujitoa aliye tofauti zaidi ya kukaa miezi sita ile nakusubiri na kuingia kwenye ule mfuko ambao ali-serve. Kwahiyo, tuangalie na maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la michango kwaupande wa asilimia tano kwa 15. Tumeona kwamba kunahiari, mtu anaweza akaongeza lakini azidi asilimia 50. Sasani bora kwa wakati mwingine tunaweza kubadilisha, tuachetu asilimia tano kwa 15; asilimia tano kwa mwajiriwa naasilimia 15 kwa mwajiri, kuliko ile section 18(6) ambayoimeweka uhiari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine la section 25,tumezungumzia kuhusu umri wa kustaafu. Umri wa hiari nimiaka 55 na umri wa lazima ni miaka 60. Tukumbuke kwambani jana tu tumeipitisha ile sheria kwa zile kada za Madaktarina Wahadhiri, lakini sasa huku kwenye mifuko hakuna haja
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
254
ya kuongeza kipengele kikatambua ile sheria ambayotumepitisha jana kuhusu hizo kada za Madokta pamoja naWahadhiri ambao ni Maprofesa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda section 39(1),inazungumzia endapo mnufaika ambaye ni mstaafuamefariki kwamba warithi watalipwa kiasi alichokuwaanalipwa cha mwezi cha huyu mstaafu, watalipwa kwamiezi 36. Sasa endapo mtu amestaafu ana miaka 62, bahatimbaya amefariki, halafu beneficiaries wanalipwa miezi 36:Je, kama mtu kastaafu kwa lazima miaka 60 halafuakaendelea kuishi mpaka miaka 75, angeweza kulipwashilingi ngapi katika hiyo miaka 15 ya uhai wake?
Mheshimiwa Mwneyekiti, leo hii beneficiariestunawapa fao la miezi 36 tu. Hatuoni katika probabilityambayo tunaiangalia hapa, kwa namna nyingine hatujuisasa siyo Mungu wa kujua kwamba lini mtu atakufa, lakininashauri tuweke categories tuwe na range kama tatu; kamamtu amefariki ana zaidi ya miaka 70 ndiyo hiyo miezi 36, lakinikama mtu amefariki kati ya miaka 60 na 65, hii miezi yakuwalipa hawa wanufaika iongezeke ifike hata miezi 72 au60 ili wanufaika waweze kufaidika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, tunaunganishahii mifuko, lakini imezungumziwa kwenye hii sheria, bahatinzuri imebeba vizuri suala la kama la makato haya ya lazimahayakuwasilishwa katika hii mifuko, yeye mwajiriwa itakuwasiyo mzigo wake. Kuna mashirika mengine ya Serikali,mengine yaliweka madeni na hasa hizi statutory deductionsza nyuma, sasa Serikali inabeba vipi? Kwa mfano, Air Tanzaniaunakuta ilikuwa inadaiwa na TRA, inadaiwa na mifuko,inadaiwa na SACCOS mbalimbali, kama za wanahewa, sasamadeni kama haya yanabebwaje kuja kwenye hii mifuko?
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo,naunga mkono hoja. Ahsante sana.
MWENYEKITI: Ahsante sana kwa mchango wako.Mheshimiwa Hussein Bashe.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
255
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru kwa kunipa fursa. Kwanza nitumie nafasi hiikuipongeza sana Serikali kwa kukubali kufanya mabadilikoambayo Kamati imewashauri kwa kipindi cha siku nane. Kwakuwa Kamati ya Bunge inafanya kazi kwa niaba ya Bunge,haya yanayokuja katika muswada huu, kwa asilimia zaidi ya99 Kamati imeshiriki katika mabadiliko haya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nayasema haya kwa dhatikabisa na yapo mabadiliko ambayo tumeyafanya. Moja,uwepo wa unemployment benefit; pili, mabadiliko kwenyekifungu cha 29 ambacho kinaelezea mafao na kuipamamlaka bodi kuweza kufanya maamuzi juu ya aina yamafao ambayo bodi husika itaona inaweza kuyaongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa kuna cry kubwaya public juu ya withdraw benefit. Sisi tumeangalia nini?Tuliangalia sustainability ya mifuko hii. Sote tunafahamumifuko ya hifadhi hii kama ingeendelea kwa utaratibuambao tumekuwa nao, kuna mfuko kama PSPF uhai wakeulikuwa hauna zaidi ya miaka miwili, ulikuwa unaanguka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, denominator ya 540 ilikuwani dialogue kubwa, lakini sisi kama Kamati vilevile tulionakwamba tu-provide nafasi kwa Serikali na kuiruhusu kutumiakanuni kwenda kuweka equation na kwa kufuata utaratibuwa utatu kwa maana ya waajiriwa, vyama vya wafanyakazi,waajiri na Serikali katika mchakato wa kutengeneza kanuniili mjadala wa equation itakayotumika kama benefit yawafanyakazi iweze kuwa considered.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumeangalia sualala ku-safeguard interest za mifuko ya hifadhi kwa maana yainvestment. Kumekuwa kuna uwekezaji mwingi sana ambaoulikuwa ukifanyika huko nyuma ambao umepoteza fedhaza wastaafu. Kwa sheria hii, Management, Board of Directorswatakuwa accountable juu ya uwekezaji wowoteutakaofanyika na wataadhibiwa mpaka kifungo cha miakamitano juu ya uwekezaji wowote watakaofanya. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
256
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliamua mapendekezo yaSerikali yalikuwa ni kwamba wafanyakazi walioko kwenyeprivate sector, wanaolipa katika mifuko ya kiserikali kamaPPF wahame na michango yako. Uhai wa mifuko ungekwisha!Tuliamua kuweka demarcation na kusema kwamba kuanziasasa mashirika yote ya umma ambayo Serikali ina interestyachangie katika mfuko wa umma. Hii ni ili kuweza kuipauhai mifuko hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kabisa kwambamaamuzi ya kisiasa ambayo yalikuwa yakifanyika hukonyuma katika mifuko ya hifadhi, hayatafanyika tena naSerikali. Tumeitaka Serikali kwamba watakapotunga kanuni,ziletwe kwenye Kamati ya Bunge ili Kamati ya Bunge iwezekuzipitia kanuni zile, ili tuone maslahi ya wafanyakazi kamayameweza kutazamwa inavyotakiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo moja tu ambalonaendelea kuiomba Serikali na tumeiomba hata kwenyeKamati, sheria hii imetambua watu wa kada mbalimbaliambao wapo Kikatiba, ambao wametwajwa na sheria,lakini Makatibu Wakuu wameachwa kwa hoja kwambaMakatibu Wakuu ni wengi, lakini vilevile waliokuwaconsidered ni wale waliotajwa katika Katiba tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kila Executiveni Permanent Secretaries. Kwa hiyo, ni vizuri kabisa PermanentSecretaries wakaweza kuwa considered kama alivyotajwaIGP, kama alivyotajwa Chief Secretary, kama alivyotajwaKatibu wa Bunge na sheria hii, ili hawa watu ambao ndiocustodian wa taasisi zetu za umma waweze kuwa na uhakikawa kesho yao.
Mheshimiwa Mwenekiti, otherwise nimalizie tu kusemajambo moja kwamba attitude iliyooneshwa na Wizara katikamchakato wa kuipitisha sheria hii ni very positive attitude.Tunaamini Serikali inapoenda kutunga kanuni ambazozitatumika ku-govern sheria hii na kufanya utekelezaji washeria hii, kanuni zile zitatungwa katika misingi ile ile ambayosheria hii imepitia. Misingi ya dialogue, misingi ya kusikiliza
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
257
vyama vya wafanyakazi, misingi ya kusikiliza vya waajiri ilituweze kuwa na sheria ambayo itaipa uhai mifuko yetu yahifadhi ya jamii. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Bashe.Mheshimiwa Rehema Migilla. Mheshimiwa Mbarouk.
Nawashukuruni sana. Nahamia kwenye upande wamapito ya mwenye hoja. Kwa sababu ya Ofisi ya Waziri Mkuu,Naibu Mawaziri hawa wawili; Mheshimiwa Ikupa naMheshimiwa Mavunde, tutaanza na Mheshimiwa Ikupa Alexdakika kumi, halafu Mheshimiwa Mavunde dakika 20; namtoa hoja mwenyewe nadhani dakika 30 zitakuwa zimekaavizuri ndani ya muda wetu wa saa moja. Tunaanza naMheshimiwa Ikupa, dakika kumi, karibu.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (WALEMAVU):Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia hiinafasi. Awali ya yote naomba niunge mkono hoja hiiambayo iko mbele yetu na moja kwa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada kuunga mkono hojahii na kama ambavyo hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu imeelezea, hiki kilikuwa ni kilio chawafanyakazi kwa muda mrefu sana kama ambavyoimeelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, faida zake kwenye hotubaimeelezwa pia kwamba ni kwa nini sasa hii mifukoinaunganishwa ama kwa nini wafanyakazi walikuwa wakililiakwamba mifuko hii iunganishwe?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ilitokana na kwambakulikuwa kuna utofauti mkubwa wa mafao kati ya mfukommoja na mwingine, lakini pia gharama za uendeshaji wahii mifuko na mengine mengi ambayo yameongelewakwenye hii hotuba.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
258
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitafafanua kwa ufupi tu faola kifo. Fao hili ni fao ambalo linatolewa pale ambapomtumishi bado anakuwa yuko kwenye utumishi na bahatimbaya akafariki. Fao hili limewekwa siyo kama tunatakawatu wafe kabla ya umri, lakini kwa hali ilivyo ni lazimaliwepo kwa sababu ni hali ambayo imekuwa ikijitokeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili fao ni zuri kwa maanaya kwamba kwa jinsi ambavyo limewekwa, yaaniwanufaikaji pale ambapo huyu mtumishi anapofariki akiwakwenye utumishi. Ukiangalia kwenye hii sheria inafafanuakabisa na inaonesha kwamba ni akina nani ambaowanakuwa ni wanufaika pale ambapo mtumishi anafarikiakiwa bado kwenye utumishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaona kuna watoto, lakinipia kuna mjane, kwa maana ya mgane ama mjane; piakwa upande wa watoto wanaendelea kuhudumiwa mpakapale wanapofikisha umri wa miaka 21. Pia watoto hawaama mtoto anaweza akaendelea kuhudumiwa endapoatakuwa na ulemavu wa aina yoyote. Kwa hiyo, huyuataendelea kuhudumiwa kwa muda wake wote, yaani kwamaisha yake yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili fao ni zuri kwamaana kwamba linanufaisha wale ambao wanakuwawamebaki ama ambao walikuwa ni wategemezi waMarehemu. Siyo hilo tu, kama Marehemu alikuwa hana mkewala watoto wanaomtegemea, lakini ana wazazi, hili faopia linakuwa lina umuhimu kwake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba WaheshimiwaWabunge wenzangu, muunge mkono hoja hii iliyoko mbeleyetu ili iweze kupitishwa kwa maslahi mapana ya Watanzaniawote na kwa maslahi mapana ya nchi yetu kwa ujumla.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayanaomba niendelee kuunga mkono hoja hii. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
259
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Wazirikwa mchango wako mzuri. Tunaendelea, MheshimiwaMavunde, una dakika zako 20.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANANA AJIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napendakuchukua fursa hii kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabungewote waliochangia kwa michango yenu ambayo kwanamna moja ama nyingine imekuwa ni sehemu ya kuboreshamuswada huu wa sheria ambao umewasilishwa mbele yaBunge lako Tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ulivyosema asubuhi,hata sisi ambao tulikuwa tunasikil iza michango yaWaheshimiwa Wabunge, unasikia kabisa ni michangoambayo inakwenda kuongeza thamani, ni michangoambayo iko very positive; na tunaamini kabisa kama Serikaliiko michango ambayo tumeona ina umuhimu na sisitutaichukua kwa ajili ya kuona namna bora ya utekelezajiwa sheria hii hapo baadaye.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na jamboambalo siyo muhimu sana lakini ni kwa sababu yakumbukumbu. Nataka niweke kumbukumbu sawa. WakatiMsemaji wa Kambi ya Upinzani hajaanza kusoma hotubayake, alizungumza ya kwamba ikumbukwe kwamba hojahii ya kuunganisha mifuko ni hoja ambayo imeletwa naupinzani na akawataja baadhi ya Wabunge ambaowaliianzisha hoja hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumbukumbu tu iliBunge lako liweke kumbukumbu sawa, nimepatamkanganyiko mkubwa sana wakati nasoma taarifa hii namkanganyiko wenyewe ni kwamba sehemu moja inakubali,sehemu nyingine inakataa. Wakati maelezo ya msemajianasema kwamba hoja hii imeanzia kwao, lakini ukisomaukurasa wa pili, aya ya pili, naomba ninukuu kidogo tu kwaajili ya kuweka kumbukumbu sawa. Msemaji wa Kambi Rasmiya Upinzani anasema; “Kambi Rasmi ya Upinzani inamtazamo kwamba badala ya Serikali kung’ang’ana kuweka
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
260
sheria za kupunguza na kuibana mifuko ya jamii, ingepanuafursa za ajira kwa Watanzania na kuweka mazingira wezeshikwa sekta binafsi kuajiri kwa wingi ili kupunguza umasikiniwa kipato kwa Watanzania.”
“Pil i, ni kuhakikisha kwamba wafanyakaziwanawekewa akiba itakayowasaidia pindi umri wao wakufanya kazi utakapokoma.”
Mheshimiwa Mwenyekiti, unaona kabisacontradiction hapa kwamba mwanzoni anasema hoja hiiimetokea Upinzani, lakini ukisoma katika ripoti hiiwanashangaa kwa nini tunaendelea kung’ang’anakupunguza idadi ya mifuko?
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa katika kumbukumbu hiiibaki sawa ni kwamba hoja hii kama walivyosemawachangiaji waliopita, ni hoja ambayo imeletwa naShirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) na sisi kamaSerikali tuliona ina umuhimu mkubwa ndiyo maanatumeichukua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuweka hiyokumbukumbu sawa, niko katika hotuba ya Kambi Rasmi yaUpinzani. Moja ya jambo ambalo limesemwa katika taarifahii, limezungumzwa vyema kabisa kwamba tusiunganishemifuko hii na badala yake tupanue fursa za ajira na kuwekamazingira wezeshi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri mtoa hoja alielezeaumuhimu wa kuunganisha mifuko hii na namna ambavyoitakwenda kuboresha mazingira ya wafanyakazi katika nchiyetu ikiwemo pamoja na mafao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja inayozungumzwahapo na Kambi Rasmi ya Upinzani ni kutuambia kwambabadala ya kuunganisha mifuko, ni afadhali mtengeneze fursazaidi za ajira kuliko kufanya jambo hili, ambayo inapinganana hoja ambayo aliitoa Mheshimiwa Zitto Kabwe yakuongeza wigo wa sekta ya hifadhi ya jamii.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
261
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali tunaaminikabisa uunganishaji wa mifuko hii inakwenda kuongeza tijakubwa sana kwa wafayakazi wa nchi hii, lakiniunapozungumzia suala la kuweka mazingira wezeshi nakuongeza fursa za ajira, mipango ya Serikali iko dhahiri,inafahamika. Tunayo miradi mikubwa katika nchi yetuambayo itakwenda kutengeneza ajira nyingi sana ikiwemoujenzi wa reli ya kati (standard gauge), likiwemo bomba lamafuta. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ukienda katikafalsafa ya uchumi wa viwanda ambayo inakwenda naufungamanisho na maendeleo ya watu moja kati ya mamboambayo tunayapigia kelele sana katika uchumi wa viwandani pamoja na kusaidia upatikanaji wa ajira hasa katika kundikubwa hili la vijana. Kwa hiyo, sioni kabisa kwamba ile hojailiyoletwa hapa ya kusema kwamba, tuendelee kutengenezanafasi tu za ajira na mifuko hii isiunganishwe, sikuona kamaina umuhimu mkubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya jambo lingineambalo katika ripoti hii katika Taarifa ya Kambi Rasmi yaUpinzani wamesema ni msemaji anazungumza kwambalazima mwanachama huyu anayechangia basi anufaike namichango yake kwa sababu kuna wengine unakuta hatamichango hii hawajaitumia na tayari ameshafariki nahajaona utamu wa michango yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri Msemaji leo waKambi Rasmi ya Upinzani, Dada yangu Mheshimiwa Ester,kidogo alipitiwa leo na kama hakupitiwa basi hakuusomavizuri muswada huu wa sheria. (Makof)
Mheshimiwa Mwenyekiti, muswada huu wa sheriaambao tunaupendekeza katika kifungu cha 29, imeainishwabayana mafao ambayo yatakwenda kutolewa. Hata katikaprevious position, kwa sheria zilizopo hivi sasa mwanachamaananufaika na mafao mbalimbali ambayo muda mwinginetunayasema ni mafao ambayo hata kabla hajafikia muda
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
262
wake wa kustaafu, lakini anayapata kuanzia hivi sasa.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano mafao ya uzazi,mafao ya kuumia kazini, ugonjwa na mikopo. Kwa hiyo,unapozungumza hoja ya kwamba, michango yake imsaidiendio inavyomsaidia katika namna hii na ndio maana katikamuswada wa sheria ambayo tunaipendekeza kifungunamba 29 kimeeleza bayana aina ya mafao ambayo sheriahii inayapendekeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini alikwenda mbali zaidiakazungumza kuhusu suala la life expectancy ya miaka 61.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Taarifa hii ya KambiRasmi ya Upinzani…
MWENYEKITI: Wheshimiwa Wabunge, samahahi sanaMheshimiwa Naibu Waziri. Waheshimiwa Wabunge, Idara yaHansard inashindwa ku-capture anayosema Mheshimiwakwa sababu tunachangia na sisi kwa mashauriano. Naombauende chini na ndio shughuli za Kibunge, msikilize mwenzako,yeye alikusikiliza. Tuendelee.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANANA AJIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, hoja yanguni kwamba, katika Taarifa hii ya Kambi Rasmi ya Upinzaniimezungumzwa hoja ya kwamba umri wa kuishi Mtanzaniahivi sasa unakadiriwa kuwa ni miaka 61 kwa hiyo, na ndiomaana ilikuja hoja kwamba ni afhadhali mtu anufaike namafao yake haya kabla kwa sababu sio wote ambaowanakuwepo katika mda huo ambao aliusema hapaMheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nimpe tu taarifakidogo kwamba, najua alikwenda kuchukua takwimu hiikatika Taarifa ya NBS ambayo inazungumzia General LifeExpectancy ambayo hii inamhusisha mpaka mtoto wa umriwa chini ya mwaka mmoja. Lakini nataka nimsaidie taarifanyingine ambayo itamsaidia pia katika taarifa nyingine
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
263
ambazo zinakuja. Ni kwamba kwa mujibu wa ActurialValuation Report ambayo il ifanywa na ILO ambayoinazungumzia kuhusu wastani wa kuishi wa mstaafu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wastani wa kuishi wamstaafu kwa mujibu wa taarifa ile inasema, mstaafu wakiume ana uwezo wa kuishi miaka 20.9, lakini wa kike kwamiaka 22.3. Lakini kubwa zaidi kuliko yote tukichukulia kwamfano tu wa PSPF ambao mpaka hivi sasa una takribani yawastaafu 72,000 ni wastaafu asilimia nne tu waliofariki mpakaleo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imezungumzwa pia katikataarifa hii kwamba hoja ya kwa nini tunamuingizaMwanasheria Mkuu pindi pale Bodi inaposhitakiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sera yaHifadhi ya Jamii ya mwaka 2003 inamtamka Serikali kamandiye guarantor. Mwanasheria Mkuu wa Serikali anaingia kwasababu ya kulinda maslahi ya Serikali. Ndio maana kwamujibu wa sheria inayopendekezwa kifungu cha 60 kinatoawajibu wa Serikali kama sehemu ya guarantee kwa mfukohuu, maana yake ni nini; maana yake ni kwamba Serikalilazima ilinde maslahi yake katika mfuko huu. Ikitokea jambololote limetokea mfuko huu una-colapse mwisho wa sikumzigo mzito inabeba Serikali na ndio maana MwanasheriaMkuu wa Serikali likitokea jambo lolote la kushitakiwa kwaBodi hii anaingia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kifungu hiki cha 60,inakwenda mbali zaidi ikitokea kwamba, kuna jambo ambalolinasababisha insufficience katika fund kwenye mfuko huu,Mfuko Mkuu wa Serikali unaguswa kwa namna moja, kwahiyo, ndio maana nafasi ya Mwanasheria Mkuu inakuwepokatika Sheria hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imezungumzwa pia, hojahapa na Waheshimiwa Wabunge ambayo na sisi kamaSerikali tunaikubali ya kuongeza wigo wa ku-cover mpakainformal sector na hoja hii, ukiifuatilia katika ripoti iliyotolewa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
264
mwaka 2014 inaitwa Intergrated Labour Force Survey inasema,nchi yetu ya Tanzania tuna takribani ya nguvu kazi ya watumilioni 22.3. Watu milioni 22.3 maana yake ni watu kuanziamiaka 15 na kuendelea mbele ambao ndio the working agepopulation (watu wenye uwezo wa kufanya kazi).
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa mujibu watakwimu zilizofanyika, utafiti uliofanyika inaonyesha kwamba,ni asilimia 10 tu ya nguvu kazi yetu ndio wapo katika hifadhiya jamii. Ndio maana na sisi tunakubaliana na hoja hiikwamba, ni lazima, kama Serikali, tuje na mipango madhubutiya kuhakikisha kwamba, tunaendelea kuwa-cover watuwengi zaidi kuingia katika mfumo wa hifadhi ya jamii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hayo yamefanyika pia katikamarekebisho ya kifungu cha 30 cha Sheria ya SSRA ambayoimekwenda kutambua wafanyakazi wa sekta isiyo rasmikama wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii. Lakinivilevile kwa sheria hii ambayo leo tunaijadili hapa ndani naikipitishwa inakwenda kupeleka mabadiliko katika Sheria yaNSSF ambapo NSSF sasa inapewa jukumu mahususi lakushughulika na private sector na informal sector.
Kwa hiyo, katika mpango na mkakati wa Serikali wakuhakikisha kwamba, kupitia NSSF tunaifikia informal sectorkwa eneo kubwa zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini na sera yetuimezungumza jambo hilo. Ukisoma sera yetu, Sera ya Hifadhiya Jamii ya mwaka 2003, kifungu cha 3(2)(b) na chenyewekinaelezea umuhimu wa kuwepo na informal sector katikacoverage ya social security hasa katika maeneo ya kilimo,uvuvi, madini na biashara ndogondogo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu cha 95 chaMuswada kinakwenda kurekebisha kifungu cha 6 cha Sheriaya NSSF kuongeza maneno ya mtu aliyeajiriwa katika sektabinafsi na mtu ambaye amejiajiri ikiwa ni sehemu ya kwendakutekeleza takwa hili la kusaidia coverage ya informal sectorkwenye hifadhi ya jamii.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
265
Mheshimiwa Mwenyekiti, imezungumzwa pia hojahapa ambayo imewagusa Waheshimiwa Wabunge wengisana kuhusiana na Fao la Bima ya Matibabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa umuhimu wa fao hilitumeshuhudia Wabunge wengi wamkisimama wakilisemajambo hili. Niseme tu kama Serikali kwa kufahamu umuhimuwa jambo hili, tusingekuwa tayari kuliondoa kwa sababu nijambo ambalo kwa kiwango kikubwa sana linagusa maishaya Watanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kilichotokea ilikuwa tu nimakosa ya kiuchapaji na ndio maana tumerekebisha. Faohili la Bima ya Matibabu lipo palepale na marekebisho yetuya Jedwali ambalo linakuja na Serikali lengo lake ni kupitiakifungu cha 97 kwenda kufuta kifungu cha 21(f) cha Sheriaya NSSF na kuingiza badala yake unemployment benefit,lakini kukiacha kifungu 21(g) cha sheria ile ambachokinazungumzia masuala ya Bima ya Afya ya Matibabu. Kwahiyo, jambo hili halijaondoka lipo palepale na kwa kweli,tunawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa concernyenu kubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ilizungumzwa pia, hoja naMheshimiwa Mtolea, Mheshimiwa Mtolea alikwenda specifickwenye kifungu namba 57 na akawa anastaajabishwa namatumizi ya neno shall ambalo kwa tafsiri yake anasema nikama inatoa discretion.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nafikiri rafiki yangumwanasheria msomi Mheshimiwa Mtolea hakujielekezavyema katika kifungu hicho. Kifungu hiki cha 57 kipo wazikinasema, neno alilolisema yeye la shall katika kifungu hikicha 57 neno hili linalenga kuweka sharti la lazima kwa bodikuandaa ripoti ya uthamini kila baada ya miaka mitatu.(Makofi)
Kwa hiyo, ukisoma vizuri pale utaona imezungumzwashall, lakini kwenye zile koma zile imekwenda kutoa jukumukule mbele kwa hiyo, Mheshimiwa Mtolea ukikisoma vizuri
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
266
bado hakijaharibu maana. Na uzuri katika Kifungu cha 57(2)imekwenda kueleza pia, kwamba, iwapo itatokea kwamba,kuna sababu za msingi za Bodi kutokuandaa ripoti ya Uthaminiinaweza kuomba waiver kwa mujibu wa kifungu hicho kwahiyo, nafikiri kabisa hapa Mheshimiwa Mwanasheria MsomiMheshimiwa Mtolea hakujielekeza vyema katika kifungu hiki.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimebakiza hoja moja yamwisho, hoja hii imesemwa na Kambi Rasmi ya Upinzani nabaadhi ya Wabunge kwamba, hawaoni tena umuhimu waSSRA kwa sababu mifuko hii inakwenda kuunganishwa,itakuwa miwili, kutakuwa hakuna ushindani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera yetu ya Hifadhi ya Jamiiinajielekeza katika taa ya tatu ambazo naomba nizitaje kwaufupi, taa ya kwanza inazungumzia kuhusu social assistance,taa ya pili inazungumzia kuhusu mandatory schemes na taaya tatu inazungumzia kuhusu voluntary schemes. Sasa sisi kwahoja inayosemwa hapa ni kwamba tayari tuna mifuko mwiliSSRA anabaki kufanya kazi gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niweke vyemakabisa hapa, hii mifuko miwili ambayo tunaizungumzia ipokwenye taa ya pili ya mandatory scheme, lakini tunayo taaya tatu ambayo ni ya voluntary scheme. Iko mifukomidogomidogo mingi sana, hauwezi leo kumuondoa SSRAukaacha mifuko hii ikajiendesha yenyewe, hapo ndipo hasaumuhimu wa SSRA unaingia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sio hivyo tu ukiachamifuko hii miwili hapa kinachozungumzwa inazungumzwaSera ya Hifadhi ya Jamii ambayo ndani yake pia inajumuishamifuko mingine ikiwemo Mfuko wa CHF, ukiwemo Mfuko waNHIF, ukiwepo Mfuko wa WCF. Hii yote pia inahitaji kuwaregulated kwa hiyo, hayo hasa ndio yanafanya na kuletarelevancy ya kwa nini SSRA iwepo. Lakini pia bado chombohiki ni muhimu kuwepo katika kushughulikia malalmiko yawanachama hasa katika kipindi hiki cha mabadilikomakubwa sana.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
267
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia, hata uzoefu wanchi za jirani Kenya wana mifuko mikubwa miwili, kama kaziambayo tutakwenda kuifanya hapa, lakini Kenya wana kitukinaitwa Retirement Benefit Authority ambayo kazi yakekubwa ni kama kazi inayofanywa na SSRA. Sasa kwa Kenyamifuko iko miwili, lakini Kenya wana voluntary schemes zaidiya 10,000 ndio maana wenyewe wakaona umuhimukwamba pamoja na mifuko hii mikubwa miwili, lakini badomifuko hii midogo lazima iwe ina mtu wa kui-regulate. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayonichukue fursa hii tena kuwashukuru sana WaheshimiwaWabunge kwa michango yao. Na kwa kweli, Muswada huuunakwenda kutibu matatizo mengi sana yaliyokuwayanakabili wananchi wafanyakazi wa Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi tu niseme naungamkono hoja. Asante sana. (Makofi)
MWENYEKITI: Asante sana Naibu Waziri, MheshimiwaMavunde kwa mchango wao. Sasa nimuite mtoa hoja,Mheshimiwa Jenista Mhagama, Waziri wa Nchi, Ofisi ya WaziriMkuu. (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE,KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: MheshimiwaMwenyekiti, kwanza kabisa ninaomba nichukue nafasi hiiniwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote ambaowamepata nafasi ya kuchangia muswada huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge waliopata nafasiya kuchangia muswada huu ni pamoja na Kamati yaKudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, lakinipamoja na Maoni ya Upinzani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile Wabungewalioweza kuchangia kwa kuzungumza hapa Bungeni niWaheshimiwa Wabunge 17 na waliochangia kwa maandishini Wabunge watano. Naomba niwashukuru sana Wabungekwa michango yao.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
268
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nianze kwa kusemakwamba, nichukue nafasi ya pekee kwa niaba ya Serikalikuwahakikishia wafanyakazi wote wa Tanzania kwamba,Serikali yao inawapenda sana na niwaombe sanawafanyakazi wa Tanzania wasifikiri kuletwa kwa muswadahuu wakayasikiliza maneno ya uchonganishi kutoka mahalikokote kwamba muswada huu una lengo la Serikalikudhulumu maslahi ya wafanyakazi, si kweli, kwa sababuwafanyakazi wanajua chanzo cha muswada huu ni nini. Kwahiyo, naomba niwahakikishie tuko pamoja wafanyakazi wotena tunaendelea kuwaheshimu na tutaendelea kufanya kazinao kwa maslahi ya Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa kilichonifurahishakatika majadiliano ya muswada huu ni kwamba Wabungewaliochangia wengi wamedhihirisha kabisa kwamba,wanaunga mkono muswada wetu ikiwa ni pamoja naMsemaji wa Kambi ya Upinzani na yeye anasema hoja hiihata wao waliitafakari tafakari hivi. Kwa hiyo, hiyoinadhihirisha kabisa kwamba kwa kweli, WaheshimiwaWabunge wa Kambi zote mbili wanaunga mkono hoja hii,ninawashukuru sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesema toka asubuhikwamba, haki ya hifadhi ya jamii katika nchi yetu ya Tanzaniaimwekwa katika misingi ifuatayo; msingi wa kwanza niMkataba wa ILO Namba 102, lakini msingi wa pili niPendekezo Namba 202 la mwaka 2012 ambalo linawekautaratibu na mfumo wa ulipaji wa mafao katika nchi zotewanachama wa Umoja wa Mataifa. Pendekezo namba 202linatoa nafasi kwa kila nchi mwanachama kuangalia mafaoyale ambayo yametajwa na ILO katika muongozo namkataba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi inao uwezo wakuamua kutengeneza aina ya mifumo na sheria ambazozitatafsiri mahitaji ya hifadhi ya jamii katika nchi husika nandio maana sisi katika Katiba yetu ya Jamhuri ya Muunganowa Tanzania Ibara ya 11(1) kimejieleza wazi mamlaka ya nchiyetu haina budi sasa kwa kutafsiri miongozo hiyo, lakini vilevile
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
269
kwa kutafsiri mikataba tunao uwezo wa kutunga sheriambalimbali zitakazowahifadhi Watanzania watakapokutanana majanga yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, muswada wa leo niutekelezaji wa mikataba, lakini ni utekelezaji wamapendekezo ya Shirika la Kazi Ulimwenguni. Kwa hiyo, waleWabunge waliounga mkono ninawashukuru sana kwasababu tunaendana na Umoja wa Mataifa unavyotaka nahasa Shirika la Kazi Ulimwenguni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema mwanzotunapoendelea kuyatekeleza matakwa haya wote tunaonakwamba sekta ya hifadhi ya jamii katika nchi yetu ya Tanzaniaimeendelea kuwa na mabadiliko makubwa na imeendeleakuchangia katika kukua kwa Taifa letu ukiachia mbali sualazima la kuwahifadhi wananchi wa Tanzania wakiwemowafanyakazi kwa kutumia misingi ambayo tumejiwekeakisheria lakini kwa kuzingatia sera ambayo tumeiunda yahifadhi ya jamii katika nchi yetu ya Tanzania. Na hivyo hivyoimetupelekea tukakutana leo kwenye Bunge lako tukufu,tukaja kuangalia umuhimu wa kuunganisha mifuko namifuko hii tunapoiunganisha leo ziko sababu za kimsingi zakuunganisha mifuko hii nitarejea kwa ufupi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Kazi Ulimwengunililishatuagiza baada ya kufanya utathimini wa mifukolilishatoa mapendekezo ya kuishauri nchi yetu ya Tanzaniatoka mwaka 2013 kufikiria namna bora ya kuboresha sektaya hifadhi ya jamii kwa kuiunganisha mifuko hii ya hifadhi yajamii ambayo nchi yetu ya Tanzania ilionekana ina mifukomingi kulinganisha na nchi nyingine. Shirika la KaziUlimwenguni kama mdau mkubwa anayesimamia vigezo vyahifadhi ya jamii katika mataifa mbalimbali na yeye alitushaurihivyo. Lakini na sisi kupitia mdhibiti wa sekta katika nchi yetuya Tanzania tuliona kwamba iko hoja ya msingi ya kuhakikishakwamba mifuko hii tunaiunganisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema manenohayo ya utangulizi sasa nitajikita katika kujibu hoja za
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
270
Waheshimiwa Wabunge lakini ambazo zimezungumzwa kwaujumla. Labda nianze na hoja ambayo ni hoja kubwa sana.Ninaona Bilago mwalimu mwenzangu na jirani yake HaongaKambi Rasmi ya Upinzani wameizunguza kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na hoja yao kubwakikokotoo ambacho kinatakiwa kielekeze mfumo wa malipoya pensheni kiingizwe kwenye sheria. Hiyo ndiyo hoja kubwa,na Mheshimiwa kaka yangu Bilago mwalimu mwenzanguamekwenda mbali zaidi akasema ni lazima kikokotoo chamoja chini ya mia tano arobaini (1/540) kijionyeshe paledhahiri. Lakini alipokuja kuchangia jirani yake ndugu yanguHaonga akasema tena hiyo moja chini ya mia tano arobaini(1/540) haitoshi twende moja chini ya mia tano ishirini(1/520). (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kusema mamboyafuatayo; ningeomba sana wafanyakazi tusiwapotoshe,wafanyakazi tusiwajengee mtazamo kwamba Bunge hili ndiloBunge linaloweza kuwahurumia sana katika suala la mafaoyao. Ninasema hivyo kwa sababu gani ninazo sababu zamsingi. Kabla hatujafikia kuunganisha hii mifuko nimesemapale mwanzo ILO walifanya tathimini wa sekta ya hifadhi yajamii katika nchi yetu ya Tanzania. Wamefanya utathiminimwaka 2010; wamefanya utathimini mwaka 2016nilitegemea kaka yangu Haonga anapokuja kuleta hilopendekezo na kaka yangu Bilago na Kambi Rasmi ya Upinzaniwasingeishia kwenye eneo la kikokotoo peke yake,wangeenda mbele kwenye zile findings zote ambazo zililetwabaada ya kufanya utathimini wa mifuko. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaambieWaheshimiwa Wabunge wenzangu yafuatayo; baada yakufanya utathimini wa mifuko mwaka 2010 na 2016 yafuatayondiyo yaliyojitokeza; la kwanza, ni funding level ya mifukoyote katika nchi ya Tanzania. Mfuko wa NSSF ambaokikokotoo chake ni moja chini ya mia tano themanini(1/580);mwaka 2010 funding level yake ilikuwa asilimia 75.8 mwaka2016 funding level ikaendelea kupanda. Mfuko wa PPFwalipofanya utathimini wa mfuko mwaka 2010 funding level
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
271
ya PPF ilikuwa asilimia 47.1 mwaka 2016 ikawa 49.6. LAPFambayo inatumia kikokotoo cha moja kwa mia tanoarobaini (1/540) funding level ilikuwa asilimia 46.7 mwaka 2010ilipofika mwaka 2016 kwa sababu ya kikokotoo cha mojachini ya mia tano arobaini funding level ya LAPF ikaanzakushuka na ikafika asilimia 27.7. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, PSPF mwaka 2010 fundinglevel ilikuwa asilimia 10.1 ilipofika mwaka 2016 funding levelikawa asilimia 6.2. Lakini hatukuishia hapo matokeo yautathimini baada ya kupata hizi findings wakatoa ushauri,ushauri wa wazi kabisa tukitaka kuendelea na kikokotoo chamoja chini ya mita tano arobaini (1/540) kwa mfuko wa LAPFna mfuko wa PSPF ni lazima contribution rate itoke asilimia20 iende asilimia 30.
Sasa ninataka kumuuliza kaka yangu Bilagoanapopendekeza kikokotoo cha moja chini ya mia tanoarobaini achotaka kuwaambia wafanyakazi wa Tanzaniaanakubaliana na mapendekezo ya ILO yaliyofanywa mwaka2010 na 2016 kwamba sasa kikokotoo kiondoke asilimia 20kiende asilimia 30. (Makofi)
Ninaomba nitoe ufafanuzi wa maana ya asilimia 30.Mfanyakazi huyo sasa akipelekwa asilimia 30 ina maanamwajiri atachangia asilimia 15 mfanyakazi atachangiaasilimia 15 na mwenye kalamu aanze kushika karamu yakeaorodheshe. Mfanyakazi atachangia asilimia 15 ya Mfukowa Pensheni, atachangia asilimia 15 ya Bodi ya Mikopo,atachangia asilimia tatu ya Mfuko wa Bima ya Afya wa Taifaatachangia mbili, Chama cha Wafanyakazi, achangieasilimia tisa ya Kodi ya Mapato, achangie asilimia tano labdaya mkopo ambao ameukopa labda binafsi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli kwa asilimia 15 kwafunding level ya moja chini ya mia tano arobaini (1/540)ambayo itampelekea mfanyakazi huyu kukatwa makatoambayo yanazidi Sheria ya Utumishi wa Umma vigezovilivyowekwa. Mfanyakazi huyu mshahara wake utabakitakribani kama asilimia 23 tu.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
272
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuliona hilo lakini piakwa kuyatazama na mengine ambayo nitayasema TUCTA(Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi) ambao hoja hii ndiyohoja yao pamoja na Kamati walikuja Serikalini na ushahidiwao ninao hapa, wakaomba Bunge lisiwaamulie kikokotoo,hayo ndiyo maoni ya TUCTA na TUCTA ndiyo wenye sheriayao na ndiyo waliyoiomba Serikali na ndiyo wadau nambamoja. Kikokotoo hiki turudi kwenye kanuni na kwa kuzingatiasheria za kazi tulizo nazo na utaratibu wetu wa collectivebargaining katika dhana ya Utatu tuende tukatafakari jambohili kwa pamoja na mwisho wa siku tukubaliane sisi kule nawadau wa mfuko huu kikokotoo kiwe ni kikokotoo kipi.
Waheshimiwa Wabunge, ninawaomba sana kamatutaamua sisi kuwapangia wafanyakazi tutakuwatumewapangia wafanyakazi na contribution rate ambayoitakuwa ama inawaumiza ama haitawasaidia. Kwa hiyo, kwakufanya hivyo tutakuwa hatujawatendea haki wafanyakaziwa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaomba sana nduguzangu wa upinzani muelewe kabisa hoja hii kwa msingi huoambao nimeusema. Sheria yetu sisi tumeamua kuwekabayana kikokotoo ili tusiwaumize wafanyakazi kibakie kuwaasilimia 20 mfanyakazi achangie asilimia tano, Serikaliinachangie asilimia 15. (Makofi)
Sasa kaka yangu Bilago unapotaka kung’ang’aniatwende katika mfumo huo kabla hatujarudi kukaa pamojana kutafakari na kuwabebesha hao wafanyakazi mzigowakuchangia asilimia 30 unawasaidia ama unawaingizakwenye matatizo zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaomba sanaWaheshimiwa Wabunge jambo hili ni jambo zito wala siyojambo la kuliamua tuhumu ndani wenye Maulid yao niwafanyakazi wa Tanzania watakaokutana na Waziri wa Kazi.Na Maulid kaka Bilago siyo ya kwako usiyavalie kanzu, achawenye maulid wayafanyie kazi, tutarudi. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
273
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabungemmesema hapa kwamba hamumwamini Waziri wenyedhamana kurudi kukaa na wadau katika kutengenezavikokotooo. Waziri wa Kazi haongozwi na sheria moja katikanchi ya Tanzania. Uzoefu wa Kimataifa na mikatabaniliyoisema Waziri wa Kazi anaongozwa na sheria nyingi, mimininaongozwa na Sheria Namba 7 ya mwaka 2014. Sheria hiyoinaunda Baraza la LESCO na Baraza la LESCO kazi yake nikumshauri Waziri kama kubadilisha sheria lazima nitarudikwenye Baraza la LESCO na Baraza la LESCO lina Wajumbeambao ni wafanyakazi, mwajiri lakini na Serikali tunakuwamle ndani kwa pamoja na hiyo niwaondoe tu shaka kwambajambo hilo tutalifanya kwa pamoja na wafanyakazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niongeze pia katikakufanya pia utathimini wa mifuko tulichogundua hii mifukoambayo inatumia kikokotoo cha moja kwa mia tanoarobaini (1/540) imeendelea kushuka hata kwa uwiano nauwiano wa walipwaji wa pensheni. Standard za kimataifainatakiwa katika mfuko mwanachama mmoja aliyesitaafuachangiwe fedha ya kustaafu na wanachama 25, lakinitukirudi kwa sababu ya kikokotoo kile kile, mifuko ambayokikokotoo chake ni hicho ambacho Kaka Bilago unasematwende tu hata bila kufanya utathimini tuamue tu unaonakwamba wameshindwa kufikia standard hizi za Kimataifa.Mfuko wa PSPF uwiano ni mwanachama mmoja kwawanachama watano tu. Lakini ukienda kwenye mfuko waLAPF ni mwanachama mmoja kwa wanachama 19. Lakiniukienda kwenye mfuko wa NSSF ni mwanachama mmojakwa wanachama 32.
Kwa hiyo, unaona kabisa hali ya sekta ilitakiwatufanye maamuzi haya, ninarudia kusema WaheshimiwaWabunge tupitisheni sheria tutakwenda kufanya actuarialmpya. Kwa sababu hata hapa tunapoongea wakowanachama ambao mpaka sasa wanaendelea kujiunga namifuko hii na wako wanachama wanaostaafu. Sasa niulizehivi tukiamua tu hapa ndani hawa wanachamawanaojiunga leo. Wanachama wanaoendelea kustaafuwakati sisi tuko na huo muswada, hao nao tutafanya nini.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
274
Kwa hiyo, ndiyo maana tunasema tumalize sheria hii, turuditukafanya actuarial yetu tutapata picha nzuri tutatengenezaregulation kwa taratibu wa sheria za kazi tulizonazo, tunaSheria Namba 6 na Sheria Namba 7 na hizi zote zitatusaidiakutuhakikishia kwamba jambo hili tunalifikisha salama nawafanyakazi. Wafanyakazi nieleweni Waziri wenu nipohakuna kitakachoharibika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, limezungumzwa fao lakukosa ajira, kwanza niwashukuru Wabunge wote ambaowameunga mkono fao hili ninawashukuru sana. Fao hilinisema labda maneno machache ya utangulizi, kwenyemafao ambayo yanatambulika na Umoja a Mataifa hakunafao la kujitoa. Fao hili la kujitoa liliingizwa na mifuko yetu mingikwa kulazimishwa ama sheria ama kulitoa fao bila kuwa namandate za kisheria kwa sababu ya ushindani kwenye sekta.Lakini hakuna fao la kujitoa katika mafao duniani halipo.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali sikivu ya MheshimiwaDkt. John Pombe Magufuli baada ya kusikiliza kilio chawafanyakazi kwa muda mrefu na hasa wafanyakazi wakwenye migodi ndiyo maana tumekuja na fao hili sasaunemployment benefit ili tutibu tatizo la wafanyakazi hao.Nilitegemea Wabunge leo mngeshangilia sana fao hili kwasababu linaenda kusaidia sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesema hivi fao hilikwenye sheria tumelipa masharti, baada ya kulipa mashartikaka yangu Mtolea alisema kitu kizuri sana hapa ni lazimawakati wa kuliangalia hili fao la kujitoa tukajue aina zawafanyakazi walioko katika sekta mbalimbali na tujuewatalipwa je hayo mafao yao kwenye hili fao la kukosa ajirakama mbadala wa fao la kujitoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili utaweza kulifanyatu kama utarudi kwenye regulation ukamaliza utathimini wakowa mfuko ukaangalia mahitaji halisi ya wafanyakazi kwenyefao hili la kosefu waajira na baada ya hapo ukalitengenezeamfumo wa malipo mzuri ambao utakuwa endelevu.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
275
Ninaomba Waheshimwa Wabunge muamini hapa tulipofikatumefika kwa sababu tumefanya kazi kwa pamoja naShirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini na hii siyo hojaya Serikali peke yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imezungumzwa hofu yahatima ya wafanyakazi ambao wako kwenye mifuko yetumpaka sasa. Kifungu cha 87 kiko wazi kabisa na sisi tumesemakwamba hatuwezi kuwaacha Watanzania wenzetu ambaowamehudumia kwenye sekta ya hifadhi ya jamii kwa miakahii yote eti kwa sababu ya kuunganisha mifuko tukawaachawapotee tu hapana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, idadi ya wafanyakaziwaliopo kwenye sekta mpaka sasa mpaka Septemba mwakajana ni wafanyakazi 2,147. Lakini idadi ya wanachama haina wanachama wastaafu mpaka mwezi Septemba, 2017ilikuwa ni 1,448,861. Baada ya kuunganisha hii mifuko kwatakwimu sahihi ambazo tunazo idadi ya wafanyakazi kwenyemfuko wa umma watakuwa 988 na idadi ya wafanyakazikwenye mfuko binafsi watakuwa 1,159. Sasa ili uweze kujuawafanyakazi hawa unawachukua ama huwachukui ni lazimauzingatie uwiano wa wafanyakazi na uwiano wawanachama na wastaafu katika kila mfuko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefanya hiyo kazi kwakiasi cha kutosha na naomba niwaombe wenzetu Wabungewa Upinzani hatujaja hapa tumekurupuka, jamani tumefanyakazi kwa ajili ya wafanyakazi wa nchi hii ya Tanzania. Ni tofautina mtu aliyekutana tu na muswada huu bila kujua kaziiliyofanyika. SSRA baada ya kuangalia sekta itakavyokuwahuko mbele tunapokwenda tumegundua uwianounaonatakiwa kwa mfuko wa umma utakuwa ni 1:675 nakwa hali hiyo wafanyakazi wote 988 watahitajika na tutahitajiziada ya wafanyakazi 114. (Makofi)
Kwa hiyo, hiyo tu inatosha kabisa kukuambia kwambapamoja na kifungu cha 87 lakini bado sekta itahitajiwafanyakazi wa ziada na hivyo basi ninaomba niwahakikishiewafanyakazi, ambao wako kwenye sekta ya jamii mpaka
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
276
sasa tumeshafanya hesabu yao, tunajua waliko, tunajuawanafanya nini, na sisi tumejipanga kuwachukua il iwaimarishe sekta ya hifadhi ya jamii.
Lakini hata hivyo kwenye sekta ya hifadhi ya jamiibado tunayo mifuko mingine tunao Mfuko wa Bima ya Afyawa Taifa unahitaji wafanyakazi, tunao Mfuko wa Fidia kwaWafanyakazi wanapoumia kazini tunahitaji wafanyakazi namfuko huo wa private wa NSSF tuliouanzisha unahitajiwafanyakazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kifungu cha 87ninaomba niwahakikishie kabisa kabisa ndugu zanguWabunge wafanyakazi wako salama. Labda kutokee jamboambalo kati ya hao wafanyakazi lazima utakuta kunawengine labda maadili yao hayafanani na sekta yetu nainawezekana tu lazima watakuwa wapo, ama aina mojaau nyingine ya mfanyakazi ambaye hatakuwa anaendanana sekta tunayokwenda kuijenga. Sheria za utumishi waumma zimeweka ufafanuzi wa kila jambo na kwa namnahiyo basi tutaweza kusonga mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, i l itolewa hoja hapakwamba hii mifuko wakati mwingine imekuwa inakufa kwasababu ya madeni.
Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakanitulikuwa na madeni ya aina tatu kwenye mifuko ya hifadhiya jamii. Deni la kwanza kubwa ambalo ni la msingi lilikuwani malimbikizo ya michango ya wanachama yenye thamanishilingi za kitanzania trilioni 1.3, naomba kuwaarifu Wabungefedha hiyo yote imekwisha kulipwa kwenye mifuko, fedhayote trilioni 1.3 tumekwisha kuilipa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumebakiza madenimengine ambayo ni lazima yahakikiwe lakini vilevileyatengenezewe mfumo wa kuyalipa. Lakini wakati tunafanyautathimini wa mfuko tulijiuliza swali lingine moja la msingi,je, madeni haya ni sababu ya mfuko kama wa PSPFkutokufanya vizuri?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
277
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo hapa taarifa yautathimini ambayo imejionyesha wazi. Ukiacha hata hayomadeni mengine kwa mfano ukauacha mfuko wa PSPF kamavile una kila kitu, mfuko huo maisha yake ni mafupi sana naMfuko wa PSPF ulitakiwa uwe umekwisha kufa mwaka 2018hata kama madeni yangekuwa yamelipwa yote. Lakinivilevile Mfuko wa LAPF na Mfuko wa GEPF ulikuwa unakufamwaka 2049 na mifuko hiyo ndiyo ile mifuko ambayopendekezo lake ilikuwa ichangiwe sasa kiwango chauchangiaji kifike asilimia 30. Lakini Mfuko wa PPF maisha yakeyalikuwa yanakwenda mpaka mwaka 2075 kwa kikokotoocha moja chini ya mia tano na themanini (1/580). Mfuko waNSSF uhai wake ni miaka 75 mpaka 85.
Sasa Waheshimiwa Wabunge ukishapata data kamahizi utabebaje hoja ambayo haina uchambuzi wa kitafitikama uchambuzi ninaoutoa hapa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikwenda mbali zaiditukajiuliza hivi kwenye Mfuko wa PSPF wale wanachamaambao wako kwenye mfuko huo, kwa mwezi wanachangiashilingi ngapi na malipo ya pensheni zao kwa mwezi ni shilingingapi, tulilolikuta michango yao kwa mwezi ni shilingi bilioni44 lakini mafao wanayolipwa ni shilingi bilioni 77. SasaWaheshimiwa Wabunge hebu fanya huo ulinganishi na kwasababu kikokotoo kilikuwa kimewekwa kwenye sheriaunapokuja na matokeo sasa ya utathimini wa mfuko haliilikuwa ni tete ya kutokuelewana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachotaka sasa hivi turudikama nilivyosema tukakae kwa pamoja, tujue mwenendomzima wa namna tutakavyofanya kwa kukubaliana nawafanyakazi wenyewe na hiyo itatusaidia kutuweka mahalipazuri zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie kuwaombaWaheshimiwa Wabunge kwamba suala zima la deni lamalimbikizo la michango ambalo lilikuwa kwa Serikali nabaada ya kulipwa, inakupa nafasi ya kutathimini sekta namifuko ilivyo hali yake ilivyo na nini cha kufanya, lakini sasa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
278
kwa kutumia sheria ulizonazo za kazi ni lazima urudi ukakaena wafanyakazi wenyewe na mkishafanya utathimini mtakaamtakubaliana, mtaelewaa na safari itakuwa salama zaidi.Ninaamini kwa maneno haya hata Mheshimiwa Bilago sasaananielewa vizuri na nitamshukuru kama ataelewa hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema mwanzotumepata pendekezo toka kwa Mheshimiwa Bashe linalohusukuangalia kifungu cha 40 na 41 na kuona ni namna ganitunaweza kufanya ili kuona Makatibu Wakuu nao wanakuwaconsidered kwenye mfuko wetu na kwenye sheria ambazozinaenda kueleza mfumo wa mafao yao. Jambo hiliWaheshimiwa Wabunge naomba mtuachie ili turudi natukalitafakari na tuone ni watu wengine wa aina gani ambaowatashiriki na wao watahitaji kushirikishwa katika kufanyautathimini na kuja na pendekezo ambalo litabeba dhanazima ya mahitaji halisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nimalizie na fao laelimu tumewasikia Waheshimiwa Wabunge.Tutakachokifanya kwa sababu kifungu cha 29(3)kinatuelekeza kuangalia namna nzuri ya kuendelea kulipamafao, kwanza niwahakikishie watoto wote ambaowanalipiwa fao la elimu hakuna mtoto atakayeachakuendelea kulipiwa fao la elimu, hiyo tutaendelea kuwalipiana kama tutaona fao hili baada ya utathimini ni fao ambaloni zuri ambalo linaweza kuwasaidia wanachama kwakutumia kifungu cha 29(3) tutafanya hivyo na ninaomba sanaWaheshimiwa Wabunge muwe na imani na sisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, michango iliyoletwa naWabunge ni mingi niseme tu labda tutaijibu ile ambayotutashindwa kuijibu, tutaijibu kwa kutumia maandishi.
Nimalizie kwa kusema Waheshimiwa WabungeMuswada huu ni muswada unaowahusu wafanyakazi wanchi Tanzania na kwa kuwa muswada huo toka tulipoanzatumefanya kazi ya kutosha kwa kushirikiana na wafanyakaziwenyewe kupitia Shirikisho la Vyama vya WafanyakaziTanzania yaani TUCTA. Na kwa kuwa TUCTA wenyewe kwenye
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
279
barua niliyonayo na maoni haya wameridhia vipengeleambavyo vipo kwenye muswada huu. Ninawaomba sanaWaheshimiwa Wabunge kwa kuwa shughuli hii ina wenyewena wenyewe ni wafanyakazi wa Tanzania, yale tuliyomesematunakwenda kujadiliana na wafanyakazi, mridhie mtuachetukajadiliane na wafanyakazi na tutayarudisha ndani yaBunge. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaomba sana tusijetukatumia nafasi hii kuwaamulia wafanyakazi mamboambayo ama hawatoyapenda ama yatakiuka misingi nataratibu zetu za kisheria za kutekeleza matakwa yawafanyakazi kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema hayoniwashukuru sana sana Waheshimiwa Wabunge wote kwamara nyingine ninawaomba sana muunge mkono muswadahuu. Muswada huu umefanyiwa kazi nzuri sana na Kamati,muswada huu unahitajika sana na wafanyakazi wa Tanzania,muswada umeweka mafao mengine mapya mengi ambayowafanyakazi walikuwa wanayahitaji, muswada huu hatmayake ni makubaliano kati wafanyakazi na Serikali yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuyasema haya,sasa naomba kutoa hoja. (Makofi)
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NAMICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.
MWENYEKITI: Ahsante sana, hoja imetolewa,imeungwa mkono na Wabunge zaidi ya kumi. Katibu.
NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI:
KAMATI YA BUNGE ZIMA
MWENYEKITI: Kamati ya Bunge Zima!
Waheshimiwa Wabunge, tukae. Katibu!
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
280
MISWADA YA SHERIA YA SERIKALI
Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwaWatumishi wa Umma wa mwaka 2017
(The Public Service Social Security Fund Bill, 2017)
Ibara ya 1Ibara ya 2
(Ibara zilizotajwa hapo juu zilipitishwa na Kamati ya BungeZima bila mabadiliko yoyote)
Ibara ya 3
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwalimu Bilago, tukokwenye eneo la tafsiri.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante, kwenye kifungu hicho cha 3 naomba niisome; “Inclause three by adding the word full pension and giving itinterpretation as follows; means an annual amount equal toone divided by 540 of a members monthly pensionableemolument for each completed monthly of each hispensionable service multiplied by annual pensionableemolument and this also shall be a competition formula.”(Makofi)
MWENYEKITI: Mheshimiwa
MHE. KASUKU S. BILAGO. Naomba nieleze sababu.
MWENYEKITI: Hebu ngoja kidogo, unachopendekezayaani maana yake ndio unaanza na maneno means si ndiounakuja kuishia nayo wapi zile comma, mabano.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,kifungu hiki kilifutwa.
MWENYEKITI: Nakuelewa sasa nataka tu maanaumeingiza this also shall be a competition formula.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
281
MHE. KASUKU S. BILAGO. Baada ya hii definitioninayoongezeka ya hii full pension na ndiyo hiyo hiyo sasaitumike kama formula.
MWENYEKITI: Haya.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Ndiyo maneno hayo natakayaongezeke hapo kwenye three.
MWENYEKITI: Maelezo sasa
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,maana nzima ya dhana ya kuunganisha hii mifuko na kwamaelezo Waziri ilikuwa ni kuboresha mafao ya wafanyakazi.Mafao ya wafanyakazi yaliyokuwepo kwenye mifukoyalikuwa na formula zake. Sheria nzima hii kifungu hikikinalenga kuingiza formula kwenye muswada ili sheriainapotungwa iwe tayari ina kikokotoo chake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati hii full pensioninafutwa, ilifutwa kwa maana kwamba haikutajwa mahalipopote lakini ina-appear kifungu cha 30. Kifungu cha 30kinaendelea kuitaja full pension wakati haina definitionmahali popote.
Kwa hiyo, iingizwe na kwa maana tu kwamba ili sheriainatungwa sasa iwe na kikokotoo cha 1/540 na kamahaitaingizwa na kwa maelezo ya Waziri tunayoyasikiayanalenga kwenda kuipunguza 540 waathirika ni wale wotewaliokuwa wanalipwa kwa kikokotoo walichoingia nachomkataba wa ajira. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba wao wa ajirawaliingia kwa 540; sasa kama 500 inapotea na kwa maelezoya Waziri niliyopata sasa hivi, inaenda kupotea baada yaactuarial evaluation na nimeshauri kabla ya kufanya actuarialevaluation hakukutakiwa kuja bill humu Bungeni walitakiwawawe wamekaa wote na TUCTA na hao wafanyakazi nawatu gani ili watuletee walisha-determine kikokotoo halisikitakachotumika kwenye sheria hii. (Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
282
Mheshimiwa Mwenyekiti, vinginevyo kuleta ikiwa hivihivi kimya na tunaipitisha kimya wanaomba tuwaaminiwakati mwingine huwa hawaaminiki hii ni kuwaumizawafanyakazi. Kwa hiyo, hatuwezi kwenda kwa kuaminianatu tuwaamini tutunge sheria ambayo itawasaidiawafanyakazi.
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,nitatoa hoja kama sitaridhika na majibu wa Waziri.
MWENYEKITI: Haya ngoja upewe maelezo tena.Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE,KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: MheshimiwaMwenyekiti, pamoja na kutokuelewa vizuri mfumo wauandishi alioutumia na hasa katika kuweka comma ina inaina inasumbua kidogo kuielewa, sasa unapata shida yakuielewa, lakini hata hivyo, nitarudi kwa Mheshimiwa Bilagokumwambia yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naendelea kumsihisana Mwalimu Bilago, anapopendekeza hiki kikokotoonimesema toka mwanzo, anafahamu pia utathimini wamifuko uliofanyika, sambamba na kikokotoo hicho kulikuwana vitu gani vingine vya msingi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu anapotakakukirudisha kikokotoo hiki kwa utathimini ambao umekwishakufanyika na nataka kumkatalia kwamba anasemahatujafanya utathimini. Tumeshafanya na nimesematumefanya mwaka 2010; tumefanya mwaka 2016 na tunajuatunachokifanya. Sasa mapendekezo ya kikokotoo hikiyanaendana sambamba na kuongeza contribution ratekwenda 30%. Sasa naomba kujua Mheshimiwa Bilago,umeshajadiliana na wafanyakazi na mmeshakubalianakwamba contribution rate ya 30% wafanyakazi wanaouwezo wa kuilipa?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
283
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tulipokaa naTUCTA na kuangalia utathimini ulivyo, tukakubaliana kwapamoja na hawa wafanyakazi ambao ndiyo wenye Mfukona hao ndiyo wenye hizo pension zao. Wakaomba sana ilituendane sambamba, ili sheria hii iwe na manufaa yakikokotoo chenye tija kwao, turudi kwenye regulationtukajadiliane alafu tumalize huo mjadala, tuwe na kikokotoohalisia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, unapoendeleakuweka kikokotoo kwenye sheria, pale ambapo mfukoutakuwa umekuwa ama umepungua kwa hiyo kila siku kaziitakuwa ni kurudi kufanya tena mashauriano? Kwa sababuwenye uhitaji wa huu mfuko wamesharidhiana na sisi, nanimewaambia hata Mheshimiwa Bilago alikuwepo kwenyeKamati, TUCTA walisema nini na ninayo document ya TUCTAhapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwasihi WaheshimiwaWabunge, tuacheni Serikali kwa kutumia sheria za Kazitulizonazo. Tukakae na wenye muswada wao wafanyakazi,wakiridhia kikokotoo kiende 30% tutarudisha hiyo moja chiniya 540. Lakini wakisema kwamba tuitazame industry nzimatutafanya yale ambayo mwisho wa siku yatakuwa na tijakwa wafanyakazi. Mimi na Serikali yangu tunawajaliwafanyakazi na ndiyo maana tunataka kuwapa nafasi yamajadiliano. (Makofi)
MWENYEKITI: Kabla Mheshimiwa haujaendelea, hebuisaidie Kamati. Endapo Kamati itakubaliana na pendekezolako kwamba tuwe na definition hiyo, nichukue basi kwenyemain body ya muswada ni wapi tunatumia neno hilo iliwakuelewe vizuri.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante, kifungu cha 30 kimeelezea vizuri kabisa kwambaitakuwepo full pension na itakuja kwenye movement yanguya pili, kwa hiyo kwa sababu ipo kwenye section 30 iki -appear kwenye distribution kwenye fasili ni sahihi zaidi. Lakinisambamba na hilo Mwenyekiti kama kuunganisha mifuko
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
284
kunaokoa gharama, gharama hizo hizo ndizo zinawezazikashusha uendeshaji ulikuwa mkubwa, kwa hiyo,inakwenda kumuweka Waziri pazuri zaidi kulikokung’ang’ania kwamba gharama zitakuwa kubwa mifukoitakufa mapema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sioni sababu ya kamatunaokoa gharama ma-MD wote wanastaafu, tutakuwa naMD mmoja tu. Kwa hiyo, naomba nitoe hoja MwenyekitiWabunge waweze kunisaidia kujadili hoja hii.
MWENYEKTI: Kwenye Kamati hakuna taarifa,Mheshimiwa sijavaa miwani yangu, niwie radhi kwa nyumahapo nani? Haya tuitendee haki hoja ya MheshimiwaMwalimu Bilago. Tunaanza na Mheshimiwa Grace Tendega.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Ahsante MheshimiwaMwenyekiti kwa kunipa nafasi. Naunga mkono hoja yaMheshimiwa Bilago kama alivyoelekeza .
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tukijadili katikaKamati yetu kulikuwa na full pension ambayo ilikuwa nidefinition imewekwa vizuri kabisa pale, ikiwa inaonyesha nimoja kati ya 580 na katika hiyo tunaona kwamba katikakifungu cha 30 maelekezo tuliyopewa ni kwamba itafutwawataielekeza kwenye Kanuni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Lakini, katika hii, billiliyoletwa tumeiona bado ipo pale na kikokotoo chake badoimewekwa full pension na kwenye definition hakuna. Kwahiyo, naunga mkono Mheshimiwa Bilago anavyosemakwamba tuiweke lakini kikokotoo kiwe 540 kama ambavyo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
285
wadau walikuwa wametoa mapendekezo na kwa sababumifuko hii lengo lake ni kuboresha maslahi ya wafanyakazina kwa sababu tunataka tuwaboreshee ni vema wakapatakikokotoo ambacho walikuwa wakikitumia mwanzoni kulikosasa hivi tukiweka kikokotoo cha 580. (Makofi)
Kwa hiyo, naunga mkono hoja ili hiyo full pensioniwekwe kwenye definition na iwekwe badala ya 580 iwe 540.Kusema kwamba actuarial valuation itafanyika tena naMheshimiwa Waziri amesema kwamba walikwishafanyaactuarial valuation, sawa actuarial valuation kama ilifanywalakini anasema tutaweza kushusha tukiweka kwenye kanuniinaweza ama ikapata ama ikashuka. Kwa nini mmewahishabill ikaja kabla ya kuweka actuarial valuation?
Kwa hiyo, nilikuwa nadhani jambo jema kwambatungemaliza kabisa actuarial valuation, ndiyo bill ije tuwezekuijadili na kujua hicho kikokotoo. Bila kuweka kikokotookwenye hii bill …(Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda waMzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante sana kwa mchango wako,Mheshimiwa Richard Mbogo.
MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,hoja ya Serikali ndiyo inapashwa kuungwa mkono kwasababu kwanza Wajumbe ambao wanachangia hapawalikuwa kwenye Kamati husika. Sijui nashangaa kwaninihawakumaliza kule. Narudi kwenye hoja, kifungu cha 30kimetoa ruksa ya kwenda kwenye regulations na kule kwenyeregulations kwa maelezo mazuri ambayo yametolewa naSerikali kwamba wadau watashirikiswa wote naWaheshimiwa Wabunge unavyofanya actuarial evaluationsio kwanza evaluation ni valuation. Factors zipo nyingi zakuangalia na inafanywa na wataalam husika, sasa katikavigezo vya kwenda kuangalia lazima uangalie mtu huyu kwamiaka aliyofanya kazi amestaafua amewekeza shilingingapi?
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
286
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, makatoambayo amechangia ni Milioni 15, katika formula ambazomtakazozileta ambazo hazina tija anapewa labda milioni40. Hii milioni 25 zimewekezwa wapi mpaka akafikisha pale?Ndiyo matokeo yake Mifuko inakuwa kwamba sio stahimili,kwa hiyo, naunga mkono hoja ya Serikali, Kifungu kibaki hivyohivyo. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Susan Lyimo.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti,nakushukuru, na mimi ninaunga hoja mkono ya MheshimiwaBilago kwa sababu kuu mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisikiliza maelezo yaMheshimiwa Waziri amekiri kwamba wamefanya actuarialvaluation, sasa suala ni kwamba kama wameshafanyawamegundua hii mifuko life span yake ni muda gani? Nakama wameshagundua hiyo prediction kwani kurudi baadaya miaka 50 kwa mfano, kurudi tukabadilisha sheria kutakuwana shida gani? Kwa hiyo, nasema kikokotoo hiki ni muhimusana kwa sababu kitaonesha ni jinsi gani huyu mtu, huyupensioner mwisho wa siku anapata kiasi gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wewe najua ni mtaalam waSheria kwa sababu hili jambo kwenye Kamati, ukiangaliamuswada wetu wa awali hii tafsiri ilikuwepo na hicho kifungu30 kinaelezea full pension. Sasa kama hakipo kwenyeinterpretation, hatuoni kwamba hili ni tatizo kubwa?
Kwa hiyo, ninachosema ni kwamba kwa kuwawamefanya valuation, kama bado maana nimeongea naWaziri bado anasema wanataka kufanya thorough actuarialvaluation. Kama wanataka kufanya hiyo thorough kwa niniwametuletea muswada kabla hawajakamilisha hiyothorough valuation ili sasa wananchi wajue kikokotoo chaoau wafanyakazi ni cha nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme huu muswada sio niwafanyakazi lakini sisi Wabunge ndiyo tunajua pia ni mambo
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
287
gani ambayo tunataka tuwasaidie wafanyakazi wa nchi hii.Kwa hiyo, nadhani kuna kila sababu ya kuhakikisha kwambahiki kikokotoo kinakuwa interpreted kama ilivyokuwa awalina watu waje, wafanyakazi hao waelewe wanapoingiakwenye hii mifuko watapata nini baada ya kustaafu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
MWENYEKITI: Ahsante sana. Mheshimiwa Waitara.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nashukuru na naunga mkono hoja ya Mwalimu Bilago,mwalimu mwenzangu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Waziri anazungumzamwanzoni na alipokuja kumaliza amepiga siasa sana kwakweli. Kwa sababu anajichanganya. Wewe umesemaumeshakutana na Wafanyakazi mmekubaliana, tunatakamakubaliano hayo hapa. Kwa nini hayawekwi no, hayo siomakubaliano. Unasema mrudi mkajadili eti mlishakutanamkajadili mkakubaliana, mnarudi kujadili kitu gani tena?Karatasi hiyo Mheshimiwa Waziri unayo peke yako, yaaniunaweza ukaamua ukaichana na ukabadilisha unachotakakufanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yetu ni kwamba kamaissue yakusema kwamba inaweza ikapanda ikashuka sio hojaki-mathematics. Kihesabu inahesabugi wote kama ni mojaya 540 umesema mshahara wake ni X ukizidisha utapataproduct pale mbele. Haina shida, yaani hii ndiyo hoja ambayoukiwa na formula huna malalamiko yoyote na mfanyakaziyoyote. Kwa sababa formula inafahamika value yakeikibadilika thamani imeshuka, imepanda anajua yaani hunamgogoro naye. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ya kutunga sheriaambako hatutakua na nafasi ya kuja kujadiliana mrudikujadili kwa kweli maana yake ni kwamba ama kazihaijafanywa au kazi imefanywa unaficha ukweli au Bungehalitungi kitu hakieleweki. Na kwa kweli sina muda mrefu
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
288
sana sijawahi kuona sheria ambayo tunapitisha hapawakajadiliane waandae wenyewe ukaache na wadau. Nahoja ya kutuambia kwamba hii ni kazi eti hii sheria niwafanyakazi wenye ngoma hizi ni mbwembwe za mtaani,haina maana yoyote humu ndani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni Sheria tujadiliane kwamaana na mujibu wa sheria tutunge, hao wafanyakazihawawezi kutunga ndiyo maana wameleta kwenye Bunge.Kwa hiyo, tufanye kazi ya Kibunge tusifanye kazi ambayo kunamaswali ya kuuliza, formula ilipaswa iwekwe hapa tupitisheili tusiweze kuuliza.
Kwa hiyo, naunga mkono hoja ya Mwalimu Bilagona Mheshimiwa Waziri na Wabunge wenzake wa CCMwasilete msimamo ambao kimsingi haupo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunajadili mambo yamsingi ni bora tukaweka siasa pembeni na tukaweka maslahiya Taifa mbele. Nimemsikiliza kwa makini shemeji yangukutoka Kigoma na kule kuna msemo unasema maghamboBukhebukhe (mambo ni polepole). Kilio hiki, cha wafanyakazinaomba niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge, kilasherehe za Mei Mosi zinapofanyika, moja ya kilio kikubwa chawafanyakazi katika Taifa letu ni kuleta ombi la kuunganishamifuko hii kwa pamoja. Maombi haya yamekuwa yakitoka,kwa bahati nzuri Mtemi Chenge Mheshimiwa Mbunge weweunajua mimi nimelelewa katika chama hiki na nimekuwamstari wa mbele katika kushiriki shughuli mbalimbali za Serikali.
Kwa hiyo, hoja yangu ni kuonesha hisia kwa wenzetuwageni ambao wanakurupuka na waliodandia treni kwambele. Sisi tuliingia wakati treni ile ikianza safari, enzi ya MwinyiMheshimiwa Mwinyi, Mheshimiwa Jakaya Kikwete,
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
289
Mheshimiwa Mkapa na sasa juzi Mheshimiwa Dkt. JohnPombe Joseph Magufuli, ni namna wafanyakazi wanautashina ushawishi mkubwa wa kuona mifuko hii inaunganishwakwa pamoja. Tukipata msingi wa jambo hil i kuwaumetokana na wafanyakazi wenyewe, ndipo tutakapojengahoja ya msingi ya kuona namna ni gani tatizo hili tunalitatua.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tu pia nikufahamishekuwa wenzetu ni wavivu wa kusoma. Hata, katika nyumbaza Ibada tunazokwenda, nyaraka nyingi ambazowanatakiwa kuzisoma waumini wanakuwa wavivu nawanaishia kulalamika. Wenzetu hawajasoma, ukisoma ripotiya ILO actuarial valuation ya mwaka 2016...
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa …(Makofi/Vigelegele)
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Naunga mkono hojaya Serikali. (Makofi)
MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: MheshimiwaMwenyekiti, nataka ni nioneshe kwa nini siungi mkono hojaya Mheshimiwa Bilago.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili uweze kupata kikokotoolazima uwe na guidelines, na ili ufanye actuarial valuationlazima uongozwe na guidelines, na guidelines zinapatikanapale tu ambapo utakuwa umeiunganisha hii mifuko naukisha unganisha hii mifuko utapata new guidelines ambazozitakueleza sasa unawezaje kutengeneza hiyo formula.(Makofi)
Sasa mifuko haijaunganishwa ili ije na hizi guidelinesmpya, unapataje hiyo denominator unaipataje sasa. LakiniMheshimiwa Bilago hapa ametumia ujanja mkubwa, na miminikupongeze we ni mjanja. Anataka kuturudisha nyumba
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
290
tuiharibu kabisa hii Sheria yote, sasa sidhani kama kuna mtuyupo tayari hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kazi iliyofanyika nikubwa na Kamati imefanya kazi kubwa. Natakanikuhakikishie kwamba hauwezi ukapata hicho kikokotookwa sababu hiyo section 30 imekuwa coached katikautaalam ambao sasa inatengeneza sheria nzuri zaidi kulikoile ilivyokuwa zamani. Maana inasema itazingatia TheRegulatory Authority Act, section number 25A ambayoinaelezea namna ya kupiga hizo hesabu. Sasa ukishazingatiahiyo ile maana yake utakuwa salama zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti nimalizie, hivi dhana yakwamba Sheria Ndogo ni mbaya inatoka wapi? Yaanikwamba by-laws sio sheria nzuri! Hapana kwa sababu Bungehili lina Kamati inayoshughulikia sheria ndogo na kwambazikitungwa zinaletwa huku huku Bungeni zinaangaliwakwamba zimezingatia Katiba, zimezingatia Sheria nyingine,zimezingatia matakwa na maelekezo ya wakati wa utungajiwa sheria zingine ikiwemo sheria hii. Maana lazimatunapotaka kutafsiri sheria ndogo lazima tuianzie kwenyesheria mama zinazozalisha kutungwa kwa Sheria hii. Katibainasema, sheria nyingine zinasema ndiyo unapoi-verifykwamba hii Sheria hii imekidhi matakwa ya utungwaji wakehata kama inatungwa na Executive. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo dhana hii yakuondoa mfumo ambao upo kwamba hatuaminiani kwa kiasihicho…
MWENYEKITI: Ahsante sana MheshimiwaSimbachawene. Mheshimiwa Haonga.
MHE. GEORGE B. SIMBACHAWENE: Naunga mkonomsimamo wa Serikali. (Makofi)
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nimegundua kwa nini kuna watu walipoteza Uwaziri kwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
291
sababu haya mawazo…(Makofi) [Maneno Haya Siyo Sehemuya Taarifa RAsmi za Bunge]
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mheshimiwa Haonga.
KUHUSU UTARATIBU
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Kuhusu Utaratibu.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti,hiyo.
MWENYEKITI: Futa kauli hiyo.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti,nimeifuta hiyo, nimeshaifuta.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya Mwalimu Bilagohapa ni kwamba hicho kikokotoo (denominator 540)kiingizwe kwenye kanuni. Na kama tunakubali kwamba kunaby -laws kwa nini sasa tusikubali kuiweka hiyo kama ikiletamatatizo baadaye tunaweza pia kutoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutunga sheria mkishatungasheria kwenye Bunge hili, hizi sheria wakati mwingine zikishatumika tukiona kwamba kuna shida baadaye hamna ubayawowote kuja kurudi tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo ni maslahi mapanaya watumishi. Watumishi wetu amezungumza MheshimiwaMhagama pale, watumishi wetu wamekuwa wakilalamikasana Mheshimiwa Mhagama wanalalamika sana kwasababu pension yao inaonekana kwamba wanapata kidogokwa sababu ya kile kikokotoo, sasa kumruhusu Waziri pekeyake akakae peke yake chumbani na anatengeneza kile kitu,halafu tunadanganywa kwamba anaenda kukaa na walewawakilishi kwa mfano vile Vyama vya Wafanyakazi hii siosahihi.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
292
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme tukwamba Mheshimiwa Jenista Mhagama naomba ukubali tu,kwamba tuingize kikokotoo hiki cha 540 ili tuwasaidiewatumishi wetu wamelalamika wa muda mrefu sana kamaikaleta matatizo bado tutarudi tu nafasi hiyo bado tunayo,Ahsante sana lilikuwa ndilo hilo tu.
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante, kwanza siungi mkono hoja ya Mheshimiwa Bilago,lakini pia nimeshangaa kidogo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili tumelijadili sanakwenye Kamati, na naomba leo niseme mbele ya Bunge hili,walioleta maoni ya kuomba kikokotoo kisiwekwe kwenyesheria ni watu wa TUCTA. Sasa huyu nani ambaye kiatu asichovaa yeye kinamuhangaisha? Na waliokuja na hoja hukuwepokwenye kamati usipige kelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, waliokuja na hoja hapa yakikokotoo hiki ni chama kimoja ATE wakawajibu msiturudishenyuma na TUCTA wakawajibu msiturudishe nyuma, tukakaakama kamati tukakubaliana tukasema jambo hili liondolewekwenye sheria. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, funding level ya PSPF ilikuwaimefika asilimia 6.2 maana yake ni nini? Maana yake nikwamba leo ukiwaambia PSPF tunafunga hawawezi kulipaliability zaidi ya asilimia 6.2.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeambiwa PSPF ilipofikailikuwa mtu akistaafu anachangiwa na watu watano. LakiniILO inasema ili mtu apate pension lazima achangiwe na watu
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
293
25, mnataka tukae hapa Bunge hili na sisi tuwe sehemu yakutunga sheria inaenda kuua mifuko naomba nisiwe sehemuya sheria hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wanasema actuarialvaluation hakuna, actuarial valuation mwaka 2010 ilikuwepo,actuarial valuation 2016 na unaona wanakimbia suala lakuongeza asil imia 30 hamna anayesema. Wewe niMwenyekiti wa Kamati Ndogo unajua Serikali ikishatungakanuni wanazileta kwenye kamati yako, kwa hiyo bado roleya Bunge ipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wewe unajuaumekuwa Attorney General wa nchi hii huwezi Waziriukatunga kanuni peke yako chumbani, ukishamaliza kutungakanuni unawapelekea wadau. (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa umechangiavizuri.
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti,naomba niwashawishi Wabunge tusikubali hoja ya MwalimuBilago. (Makofi)
MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekitinashukuru, nadhani kama Serikali imefanya actuarialvaluation kama wanavyosema, jukumu la msingi lilikuwabaada ya hiyo valuation kikokotoo ni kiasi gani, mkiwekekikokotoo kiwe kizuri ama kiwe kibaya ili Wafanyakazi waWatanzania waweze kupima utendaji kazi wenu kwenye hiimifuko kwa kipindi cha miaka 56 ya utawala. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili, jukumu la Bungeni kutunga sheria, Kamati imefanya kazi nzuri, lakini kazikubwa ambayo Kamati imefanya ni kutoa mamlakamakubwa kwa Waziri na kwa SSRA kwenye mambo ya msingisasa Waziri tu anisaidie, kama kikokotoo ilikuwa ni shida kwa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
294
nini kwenye muswaada wa kwanza mlikionyesha kikokotoo?(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mbaya zaidi Kifungucha 57 kipitie. Kifungu cha 57(1), 57(2) kina ainisha wazi kabisakwamba actuarial valuation ambayo inatusaidia kujua assetsna liability ya shirika letu likoje, uhai wa shirika ikoje. Hapaimeonekana kwamba inaweza isifanyike soma kifungu cha57(1) kimetoa mandatory kufanya miaka mitatu, lakinikikaenda mbele sana au muda mwingine wowote. Kifungukidogo cha (2) kinasema kabisa kwamba bodi inawezaikaomba ruhusa na ikiomba ruhusa actuarial isifanyike.
Sasa tupo kwenye mazingira ambayo actuarialvaluation ndio itatu–guide, lakini sheria hii hii inatoa kificho,kwa hiyo, matokeo yake mashirika yetu yatakuwayanaendeshwa tukitaka kwenda kutaka wataalam wamasuala ya risk ili tujue assets na liability kuna kifungu kinasemasio lazima tuangalie. Kwa hiyo, tutafunika kombe mwanaharamu apite mifuko inazidi kupata, wananchi wanazidikuumia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu sio sahihi kusema etiTUCTA, wametuambia, nchi hii ina Vyama vya Wafanyakazivingapi? Kwa hiyo, TUCTA wakija ndio wame representwafanyakazi wote?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, niseme hivi,nashukuru Mheshimiwa Serukamba alisema hivi the law doesnot apply retrospective ulisema vizuri, hoja nyingine yaMwalimu inasema, kwa wale wafanyakazi ambao waliingiamikataba, mikataba wakasema… (Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda waMzungumzaji)
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti,mgawanyiko juu ya 540 ama 580 ulikuwa ni dialogue yaalmost siku mbili ndani ya Kamati na tukafikia consensus kwaactuarial valuation iliyofanyika, Serikali ikafanye tena baadaya kuunganisha mifuko yote kuangalia asset and liability iliiweze ku-determine itumike denominator ya ngapi? Tuliulizaswali why 540, why not 520, why not 400, why not 580? Swalihili litaenda kujibiwa baada ya kufanyika kwa evaluation yamifuko hii baada ya kuunganisha assets and liability. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili MheshimiwaDada yangu Halima ametumia kifungu cha 57 tukisome tuwote na mimi nilipata mchanganyiko kama wa kwake.Kinasema; “The board shall at interval of three years or at anyother intervals as the authority...” na tunapo zungumziaauthority tunamzungumzia regulator SSRA, “...may direct andsubject to guidelines issued by the authority...” zipo clearguideline zilizokuwa issued na authority ya SSRA namna ganiya kufanya valuation. (Makofi)
Lakini sub section (2) ambayo inasemanotwithstanding subsection (1) the board may not shall owingto the natural and circumstances. This is very clear, suala yaactuarial valuation liko very clear na linasimamiwa nautaratibu wake, kwa hiyo, we expect Serikali haitovunjasheria, lakini kama tunakuja Bungeni tunataka kupitisha sheriaambayo sote tunafahamu kwamba itaenda kuua hii mifukowe are not going to be fair for this country na kikubwa nikutokuaminiana, lakini ipo kamati ndogo ya sheria ambayoina jukumu la kupitia hizi kanuni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwenye mchakatohuu kuna utatu mtakatifu wa mwajiri, Serikali na Vyama vyaWafanyakazi, hatuamini kwamba Serikali itaenda kutungakanuni bila kupitia mchakato huu wa kisheria ulioko,hatudhani kwamba Mheshimiwa Jenista atajifungiachumbani lakini niseme na niseme hapa kwenye Bunge hili,hakuna njia nyingine we have two choices kufanya maamuzikwa moyo tukaue mifuko, hii tunayotaka ya kwenda kuweka540 ambayo leo PSPF ime-suffer na ina create shimo la zaidi
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
296
ya 300 billion shilling a year. This is the only best way ambayotunayo kama nchi kusaidia mifuko hii na kusaidia wafanyakaziwa nchi hii. (Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda waMzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante, Waheshimiwa Wabunge, ilituweke mambo sawa kifungu cha 57(1) kama mnatakatukisome mimi nitawasomea mkielewe tu, tunasema hivi; Theboard shall sikiliza sasa, The Board shall cause asset liability ofthe fund to be evaluated by an actuary. Lini ndiyo unarudiat intervals of three years or at any other intervals as authoritymay direct any subject guideline issued by the authority.(Makofi)
Ukisoma ndio maana comma hizi zina maana sanaile shall inabaki pale pale interval lini wafanye na kuzingatiasasa utaratibu ambao regulator ameweka, bila kujali kifungukidogo cha kwanza board yaweza, yaweza sio lazima, sasakatika mazingira yanayokutegemea na hali ya biashara ndionil ikuwa nasema ukiisoma kwa namna hiyo walamkanganyiko wowote hasa. Nimuite MheshimiwaMwanasheria Mkuu sasa naye aseme yale ya kisheria ili tuwezesasa kuiamua hoja hii kabla sijamwita mtoa hoja.
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: MheshimiwaMwenyekiti, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungukuniwezesha kuchangia kwenye hoja hii, na ninaunga mkonomoja kwa moja hoja ya Serikali kama ilivyo kwenye muswadahuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama wote tunavyofahamumuswada huu una maslahi makubwa sana kwa wafanyakazi,ni muswada ambao moja kwa moja unagusa maslahi
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
297
muhimu ya wafanyakazi na wafanyakazi wana taasisimuhimu ya kuwasemea na taasisi hiyo ni Shirikisho laWafanyakazi la Chama cha Wafanyakazi Tanzania (TUCTA).
Mheshimiwa Mwenyekiti, na Bunge lako Tukufu,limeweka utaratibu kwenye kanuni ya 84(2) kwenye kamatikuwashirikisha wadau kwenye mchakato wa kuunda sheriana Shirikisho hili wameitwa wameleta maoni haya lazimatuheshimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii siyo sheria ya kwanzaambayo tumewashirikisha wadau, kila sheria inatungwatunawashirikisha wadau, leo kwa sababu tuna hoja fulanitofauti tunasema tunataka ku-down play role ya wadaukwenye hii tena wadau ambao wameleta haiwezekani sisitukaguswa sana na maslahi ya wadau/wafanyakazi walekuliko wafanyakazi wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni hili, kwanza sio kilaneno kwenye sheria lazima lipate tafsiri sasa utatunga sheriaya aina gani hiyo kama full pension kwa mfano unatafutatafsiri, can’t you take it seven so much literary, lakini kamaunataka tafsiri pia ipo kwenye kifungu chenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kifungu chenyewe cha 30kinaitoa hiyo tafsiri kama unaitaka tafsiri ya full pension sema;a full pension naisoma a members who has attained the ageof retirement and has contributed to the fund for the periodof not less than one hundred and eight months shall be entitledto a full pension constituted of commuted pension andmonthly pension calculated and payable in accordance withthe formula prescribed in regulations this is in itself a definition.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani hii yenyewe ni tafsiriinakupa tafsiri ndio, kwa sababu formula si ndio formulainakuongoza inakupa tafsiri, that is it na hii siyo sheria yakwanza pia inayotoa mamlaka kwa Waziri kwendakutengeneza formula, tunatunga sheria chungu mzima.(Makofi)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
298
Mheshimiwa Mwenyekiti, cha pili, hizi sheria ndogohizi ni sehemu ya sheria ni sawa ni sehemu ya sheria mamakwa mujibu wa kifungu cha 41 na cha 42 cha Sheria ya Tafsiriya sheria na sababu za msingi zimetolewa na MheshimiwaWaziri na Wabunge wamesema kwa nini hii haiwezikuwekwa hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme hivi kwamba mojakama ambavyo Katiba ya nchi inatafsiriwa na sheria hizimama, kanuni ndizo zinatafsiri sheria na hiyo inasababishautekelezaji wa sheria.
Kwa hiyo, baada ya kusema hayo ninaunga mkonohoja hii ya Serikali kama ilivyo kwenye muswada na hili la piliibara 57 ya muswada kiti chako kimeitolea tafsiri sahihi kamaambavyo na Serikali imeshakwisha kutoa na ni kwa hekimayako kwa sababu tungetegemea kwamba kama kungekuwana schedule of amendment ambayo imekuwa moved kujadiliibara ya 57 then could have considered in this one accordingly.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aendelee kukubariki sanakwa hekima uliyonayo baada ya mwongozo huu ambaonakubaliana nao naomba kuwashauri WaheshimiwaWabunge wote tuunge mkono hoja hii, huu ni muswadamuhimu kwa maslahi ya wafanyakazi na watumishi wotewa umma. Ninayezungumza, pia ni mtumishi wa umma namimi najulikana kama kitu hiki kingekuwa cha hovyoningekataa tu hapa hapa, na mimi nawafanyakazi Ofisi yaMwanasheria Mkuu wa Serikali pale. (Makofi)
Kwa hiyo, hoja hizi za Mheshimiwa Waziri ameelezasana wakati wa winding up, Waheshimiwa Wabungewanaounga mkono hoja hii ya Serikali wamelifafanua vizurisana, Mheshimiwa Mwenyekiti umetoa mwongozo kwambakwa mara nyingine kwa nidhamu kubwa sana naombakuishauri Wabunge wote tukubali hii hoja ya Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata ukikubali tu assumingkwamba tunakubali hivi proposal hii ina kichwa wala miguu,hii definition yenyewe hii hapa …
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
299
MWENYEKITI: Tulianza nayo. (Kicheko)
MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI: Ahsante sanaMheshimiwa Mwenyekiti Mungu akubariki sana, naungamkono hoja ya Serikali. (Makofi)
MHE. HALIMA J. MDEE: Kuhusu Utaratibu.
MWENYEKITI: Ahsante sana AG, ahsante sana. HapanaWaheshimiwa Wabunge tupo kwenye process ya msingi sanahapa, na mniwie radhi sometimes na mimi naghafirikakidogo.
Lakini tuone sasa, narudia na yamesemwa na ninyimliokuwa mnachangia, Bunge hili haliwezi likafanya kazi zotena ndio maana tunafanya kazi nyingi kwenye Kamati,mmeipongeza sana Kamati ya Kudumu ya Huduma yaMaendeleo ya Jamii kwa kazi nzuri ambayo inaonekana, kwasiku nane kama ripoti inavyosema wamefanya kazi natunaona.
Sasa kwa vile muswada huu pia una maslahi mapanaya wafanyakazi wa nchi hii, ndio maana ule utatu waoumeshirikishwa kikamilifu na mpaka wakafika kwenye eneola sasa la kikokotoo wakasema bwana hapa twende hatuakwa hatua ndio ninavyoliona mimi kwa maelezo ya Serikalihasa sisi kama Bunge sasa hivi tupo kwenye kamatitusipoisikiliza au kuyasikiliza maoni na mapendekezo yaKamati ya Kudumu ya Bunge iliyoleta taarifa yake Bungenitutakuwa tunafanya vitu ambavyo kusema kweli ni … miminaomba tulione hili, na sitaki kushawishi Kamati hii ya BungeZima lakini nataka mlione hili kwamba…(Makofi)
Waheshimiwa Wabunge, Kamati hizi zinafanya kazikubwa ya kuchambua haya kwa niaba ya Bunge ili sasa unlesskuna hoja ambayo wame-over look ndiyo unaweza sasaMbunge ukasema hapa Mheshimiwa Spika, Mwenyekiti sualahili halijakaa vizuri naomba ni-move amendment. Hiyo ni hakiyako lakini kama limefanyiwa kazi kama katika hali ambayotunayo sasa hivi, mimi nadhani tuendelee kuheshimu taarifa
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
300
za Bunge zinazowasilishwa Bungeni. Niliona niyaseme hayosasa nitamwita mwenye hoja aweze kuhitimisha hoja yakehalafu twende mbele tuiamue.
Sasa naongeza muda kwa mamlaka niliyonayo kwanusu saa, tumalize kazi iliyo mbele yetu.
Mheshimiwa Mwalimu Bilago.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante, tunaingia kwenye historia ya kutunga sheriainayokwenda kumaliza mafao ya wafanyakazi na kama kunamtu anapingana na hili kwa kuiona sheria ina maslahimapana, upana wa maslahi ungeonekana kama kunaformula. Kama hakuna formula unajuaje huo upana wamaslahi? Na ninawahakikishia Wabunge wenzangu, walewafanyakazi waliokuwa wanalipwa 540 denominate nahawataipata. Hiyo dhambi tutabeba wote humu. Kamaitakuja 540 waliokuwa wanalipwa 580 watashangilia. Lakinikwa dalili zilizopo hakuna 540, itakuwa above that naninawashangaa Wabunge wa CCM kabla ya leo tulikuwatunaelewana hili vizuri tu, sasa leo sijui mmelishwa nini!Walikuwa wanasema hili tutakomaa nalo hawawezikukomaa leo. (Makofi/Kicheko)
Naomba kwa wingi wenu, niombe kwa sababu yawingi wenu tuliamue hili kwa kura mimi ni-keep record yakutetea wafanyakazi wa nchi hii mpaka mwisho.
MWENYEKITI: Ahsante sana. Sasa nawahoji kuhusuhoja ya Mheshimiwa Mwalimu Bilago. (Makofi)
(Hoja ilitolewa iamuliwe)(Hoja iliamuliwa na Kukataliwa)
(Ibara iliyotajwa hapo juu ilipitishwa na Kamati ya BungeZima bila mabadiliko yoyote)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
301
Ibara ya 4Ibara ya 5Ibara ya 6Ibara ya 7Ibara ya 8Ibara ya 9Ibara ya 10Ibara ya 11Ibara ya 12Ibara ya 13Ibara ya 14Ibara ya 15Ibara ya 16Ibara ya 17Ibara ya 18Ibara ya 19Ibara ya 20Ibara ya 21Ibara ya 22Ibara ya 23Ibara ya 24Ibara ya 25Ibara ya 26Ibara ya 27Ibara ya 28
(Ibara zilizotajwa hapo juu zilipitishwa na Kamati ya BungeZima bila mabadiliko yoyote)
Ibara ya 29
MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti,kwa kuwa Serikali yenyewe ilikiri ni typing error peke yake basinimeondoa.
(Ibara iliyotajwa hapo juu ilipitishwa na Kamati ya BungeZima bila mabadiliko yoyote)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
302
Ibara ya 30
MWENYEKITI: Mheshimiwa Bilago.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante. Kifungu cha 30 inasema hivi; by deleting the wordsprescribed by the Authority pass one to section 2 A of theSocial Security (Regulatory Authority) Act. Nilitaka isome hivikama mngekuwa mnakubaliana na mambo mazuri; “Amember who has attained the age of retirement and hascontributed to the fund for the period of not less than Onehundred and eight month shall be entitled to a full pensionconstituted of a commuted pension and a monthly pensioncalcuted and payable in accordance with the formulaprescribed in the regulations,” ingeishia hapo.
Haya maneno ya prescribed by the authority pursuantto section 25A of Social Security (Regulatory Authority) Actyangefutika na kwa vile yangefutika haya maneno basi hiiingekuja kufanana na ile tuliyokuwa tume-define kwenye fullpension. Kwavile ile imegoma kwa wingi wenu basi na hiiniiache haitakuwa na maana kama hii itaondoka na ilehaikuwepo tena.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Bilago, kwanza utungajiwa sheria tu tuelewane, ukiishia tu the regulations hainamaana, inapoteza kabisa maana. Hatuwezi kutunga sheriaambazo hazieleweki kwa watumiaji na hili ni Bunge hapandio tunatunga sheria. Hata kama ungekuwa una-accepthiyo uliyoanza nayo huwezi ukaishia hapo. Made na nanilazima ziwe made by a certain authority ambalo Bunge hililinakasimu madaraka ya kwenda kutengeneza kanuni hizo.
Kwa hiyo, lazima utaje Waziri, sasa Wazirianazitengeneza zile kwa mujibu upi, inakuelekeza sasa nendakwenye sheria nyingine inaitwa The Social Security RegulatoryAuthority Act kifungu cha 25A, ndio tunachohama. Tena niuandishi rafiki kabisa. Hivyo usifike huko kwamba kwa sababuhili limekufa na hili sasa hapana, hapana, hapana. Kwauandishi wa sheria mapendekezo yako hayawezi kukubalika
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
303
kwa sababu yatakuwa yanapoteza maana tuinayokusudiwa. (Makofi)
(Ibara iliyotajwa hapo juu ilipitishwa na Kamati yaBungeZima bila mabadiliko yoyote)
Ibara ya 31Ibara ya 32Ibara ya 33Ibara ya 34Ibara ya 35Ibara ya 36Ibara ya 37Ibara ya 38Ibara ya 39Ibara ya 40Ibara ya 41Ibara ya 42Ibara ya 43Ibara ya 44Ibara ya 45Ibara ya 46Ibara ya 47Ibara ya 48Ibara ya 49Ibara ya 50Ibara ya 51Ibara ya 52Ibara ya 53Ibara ya 54Ibara ya 55Ibara ya 56Ibara ya 57Ibara ya 58Ibara ya 59Ibara ya 60Ibara ya 61Ibara ya 62Ibara ya 63Ibara ya 64
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
304
Ibara ya 65Ibara ya 66Ibara ya 67Ibara ya 68Ibara ya 69Ibara ya 70Ibara ya 71Ibara ya 72Ibara ya 73Ibara ya 74Ibara ya 75Ibara ya 76Ibara ya 77Ibara ya 78Ibara ya 79Ibara ya 80Ibara ya 81Ibara ya 82Ibara ya 83Ibara ya 84Ibara ya 85Ibara ya 86Ibara ya 87Ibara ya 88Ibara ya 89Ibara ya 90Ibara ya 91Ibara ya 92Ibara ya 93Ibara ya 94Ibara ya 95Ibara ya 96
(Ibara zilizotajwa hapo juu zilipitishwa na Kamati ya BungeZima bila mabadiliko yoyote)
Ibara ya 97
(Ibara iliyotajwa hapo juu ilipitishwa na Kamati yaBungeZima pamoja na Marekebisho yake)
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
305
Ibara ya 98Ibara ya 99Ibara ya 100Ibara ya 101Ibara ya102Ibara ya103Ibara ya 104
(Ibara zilizotajwa hapo juu zilipitishwa na Kamati ya BungeZima bila mabadiliko yoyote)
Ibara ya 105
(Ibara iliyotajwa hapo juu ilipitishwa na Kamati ya BungeZima pamoja na Marekebisho yake)
Ibara ya 106Ibara ya 107Ibara ya 108Ibara ya 109Ibara ya 110Ibara ya 111Ibara ya 112Ibara ya 113Ibara ya 114Ibara ya 115Ibara ya 116Ibara ya 117Ibara ya 118Ibara ya 119Ibara ya 120Ibara ya 121Ibara ya 122Ibara ya 123Ibara ya 124Ibara ya 125Ibara ya 125
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
306
Ibara ya 126Ibara ya 127
(Ibara zilizotajwa hapo juu zilipitishwa na Kamati yaBungeZima bila mabadiliko yoyote)
Jedwali la 1
(Jedwali lililotajwa hapo juu lilipitishwa na Kamati yaBunge Zima bila mabadiliko yoyote)
NDG. JOSHUA CHAMWELA - KATIBU MEZANI:Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa Taarifa kuwa Kamatiya Bunge Zima imekamisha kazi yake.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE,KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: MheshimiwaMwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni ya 89(1) ya Kanuni zaKudumu za Bunge Toleo la Januari 2016 napenda kutoataarifa kwamba Kamati ya Bunge zima imeupitia MuswadaIbara kwa Ibara na kuukubali pamoja na marekebishoyaliyofanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hojakwamba Muswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamiikwa Watumishi wa Umma wa mwaka 2018 yaani The PublicService Social Security Fund Act 2018 kama ulivyorekebishwakatika Kamati ya Bunge Zima sasa ukubaliwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.
WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NAMICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
307
MWENYEKITI: Ahsante. Hoja imetolewa na imeungwamkono na zaidi ya Wabunge kumi. Nitawahoji sasa muiamuehoja hiyo. (Makofi)
(Hoja ilitolewa iamuliwe)(Hoja iliamuliwa na Kuafikiwa)
MWENYEKITI: Katibu!
NDG. THEONEST RUHILABAKE – KATIBU MEZANI:
Muswada wa Sheria kwa ajili ya kutunga Sheria yaMfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma kwamadhumuni ya kutoa Mafao ya Hifadhi ya Jamii kwaWatumishi Walio katika Utumishi wa Umma na kufuta Sheriaya Mfuko wa Mafao ya Hitimisho la Kazi kwa Watumishi waUmma, Sheria ya Mfuko wa Pensheni wa LAPF, Sheria ya Mfukowa PPF na Sheria ya Mfuko wa Pensheni wa GEPF pamojana mambo mengine yanayohusina na hayo (A Bill for an Actprovide for establishment of Public Service Social SecurityScheme to provide for contribution and to the payments ofsocial security benefits in respect of the service of the employeein The Public Service Retirement Benefit Act, The LAPF PensionFund Act, The GEPF Retirement Benefits Act and The PPF PensionFund Act and to provide for other related matters).
(Kusomwa Mara ya Tatu)
(Muswada wa Sheria wa Serikali Ulipitishwa na Bunge)
MWENYEKITI: Ahsante, hapo ndio tumepitisha huuMuswada wa Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwaWatumishi wa Umma kwa mwaka 2017 (The Public ServiceSocial Security Fund Bill 2017) ndio umepitishwa na Bunge rasmikatika hatua yetu ya Bunge kama National Assembly.Itaenda kwa hatua za Kikatiba na kwa mujibu wa Kanunikwa Mheshimiwa Rais kama sehemu ya pili ya Bunge kwaidhini yake.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
308
Kwa hiyo, nichukue nafasi hii kuwashukuruni sana ninyiWaheshimiwa Wabunge kwa kazi ya kihistoria mliyoifanyaleo, mtakumbukwa kwa Bunge la Kumi la Kumi na Mojamtakumbukwa na Taifa hili kwamba mlifanya maamuzi yaMsingi sana katika maslahi mapana ya watumishi wa ummakatika mifuko hii na ninaamini kazi hii na jasho lililotolewatangu kwenye Kamati husika na wadau mbalimbali kwambajasho hilo halikupotea bure.
Niishukuru sana Serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi yaWaziri Mkuu kwa kazi kubwa aliyofanya. Wataalam wotewaliokuwa nyuma ya hii, a lot of thinking and hardworkimeendana na kazi hii. Ofisi ya Mwanasheria Mkuu na timuyako yote, nawashukuru sana na mimi huwa sifichi, si mchoyokwa kutoa au kumegea wenzako.
Waheshimiwa Wabunge, mimi nimemwambia AGmchana tulipomkuta anatoka, katika Miswada michacheambayo nimeona imeandikwa vizuri na kwa mtiririko ambaounauona kabisa hupotei msituni ni huu, nawashukuruni sana.(Makofi)
Tunatarajia sasa hayo ambayo yanaenda kukamilishakatika kupitia Kifungu cha 30 kuandaa zile kanuni yatafanyikakwa ushirikishi ule ule ambao umetufikisha katika hatua hiina Kanuni maana sasa hivi Bunge limekasimu madarakayake, kwa Waziri mwenye dhamana ya mifuko hiiakatengeneze kanuni ni Bunge limekasimu, lakini halijajivuamadaraka yake ya kuangalia ni nini kinachoendakutekelezwa katika kukasimu.
Kwa hiyo, tunaamini watakapokamilisha Kanuni hiyoau Kanuni hizo zitawasilishwa humu humu Bungeni na baadaya pale kwa taratibu za kawaida zitapelekwa kwenye Kamatiya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo watazipitia na kamawataona kuna masuala ambayo hayajakaa vizuri wataiitaSerikali kwenye Kamati na kama haijakaa vizuri watatoataarifa Bungeni kwamba tumegundua kitu ambachoni tofauti na matarajio yetu katika kupata kile kikokotoo.
NAKALA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
309
Lakini siamini kwamba itakuwa hivyo kwa sababu wataalamninaowafahamu ndani ya Serikali na Mifuko ni wengi na niwazuri na weledi ni wa hali ya juu sana. (Makofi)
Tuliongeza muda tumefika hapo vizuri, MheshimiwaBilago nakushukuru as a Parliamentarian umefanya kazi nzurina wote mliojenga hoja. (Makofi)
Sasa kwenye taratibu hizi wengi wape, umeyasemaya kwako, Kamati imesikia na Watanzania wamesikia, lakinikwa sababu hoja hii ni ya msingi na Serikali imeyaeleza vizurikwanini hoja yako haukuweza kuichukua, siyo kwa sababuya wingi tu wa upande huu hapana, ile mantiki yenyewe.Kwa hiyo, niwashukuruni sana, sina mengine ya ziada kwaleo sina matangazo. (Makofi)
Nimalizie tu kama nilivyoanza kwa kuwashukurunisana kwa ushirikiano mlionipatia kwa siku ya leo kwakufanikisha kazi iliyokuwa mbele yetu.
Baada ya kusema hayo naahirisha shughuli za Bungehadi kesho siku ya Alhamisi Saa Tatu Asubuhi.
(Saa 2.05 Usiku Bunge liliahirishwa hadi siku ya Alhamisi,Tarehe 1 Februari, 2018 Saa Tatu Asubuhi)