ISSN 0856 - 3861 Na. 1202 MUHARRAM 1437, IJUMAA , NOVEMBA 6 - 12, 2015 BEI TShs 800/=, Kshs 50/= Sauti ya Waislamu www.annuurpapers.co.tz au facebook:[email protected]Uk. 20 Ameapishwa, ameanza kazi Kikwete imekuwa ‘lam yalbathuu illa…’ ‘Hatutoi labda mtupindue’ - Asha Bakari Hiki ndicho kilichofanyika Zanzibar Sio yale aliyosema Jecha Salim Jecha “NAMWAMBIA (Ismail) Jussa hatutoi (Serikali), labda mtupindue. Serikali ya kimapinduzi haichukuliwi kwa karatasi, hilo nawabainishia”- Asha Bakari. “Hata wapinzani washinde kwa kura, CCM hatuko tayari kutoa Serikali. Vifaru na makombora ya kivita yapo kwa ajili ya kuhakikisha hilo.”- Salmin Awadh Salmin. ASHA Bakari Makame ‘Hapa kazi tu’ ilete haki, neema kwa wote 'Mbele kwa mbele’ iwe fuata nyao za Robin… Kulikamata kambaku kwa mapembe yake 'Mwisho wa usanii' RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli. Changamoto kwa Shein Kinachosubiriwa sasa ni ‘Mwafaka wa 5’ Kikwete atoka Ikulu na ‘zigo’ la lawama Uk. 20 ANNUUR REAL.indd 1 11/5/2015 3:35:59 PM
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Hiki ndicho kilichofanyika ZanzibarSio yale aliyosema Jecha Salim Jecha
“NAMWAMBIA (Ismail) Jussa hatutoi (Serikali), labda mtupindue. Serikali ya kimapinduzi haichukuliwi kwa karatasi, hilo nawabainishia”-Asha Bakari.
“Hata wapinzani washinde kwa kura, CCM hatuko tayari kutoa Serikali. Vifaru na makombora ya kivita yapo kwa ajili ya kuhakikisha hilo.”- Salmin Awadh Salmin.
ASHA Bakari Makame
‘Hapa kazi tu’ ilete haki, neema kwa wote
'Mbele kwa mbele’ iwe fuata nyao za Robin…Kulikamata kambaku kwa mapembe yake
'Mwisho wa usanii'
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.
Changamoto kwa SheinKinachosubiriwa sasa ni ‘Mwafaka wa 5’Kikwete atoka Ikulu na ‘zigo’ la lawama
Fethullah-Gulen“ALLAH – hapana Mola anayestahili kuabudiwa kwa haki asiyekuwa Yeye aliye hai mwenye kudumu katika kuyasimamia mambo”. [Al-Baqarah 255]
Ndiyo, Yeye ndiye mwenye k u a b u d i w a m p w e k e . Hapana mwenye kuabudiwa asiyekuwa Yeye. Hapatikani m w e n y e k u a b u d i w a asiyekuwa Yeye kwa sababu vilivyopo vyote tokea tangu mpaka milele, havikuwa isipokuwa ni vivuli kutokana na nuru ya kupatikana kwake na sura zote za ulimwengu ni muonekano kutokana na nuru yake na kila kilichopo na kila chenye kuwa, kitu hicho ni mdhihiriko mdogo unaochukua kupatikana k w a k e , k u t o k a n a n a usimamizi wake Mwenyezi Mungu mtukufu.
K u p a t i k a n a k w a k e Mwenyezi Mungu mtukufu,
Baqara: 255kunatokana na nafsi yake na uhai wake na usimamizi wake unatokana na dhati yake. Kila kilichopo kisicho kuwa Yeye kinatoka kwake na ni katika kudhihiri kwa sifa zake na majina yake mazuri.
Ye ye n d i ye a l i ye h a i m we n ye k u ya s i m a m i a mambo ambaye hakipatikani kitu chochote ambacho kimesimama kwa nafs i yake, pasi na kutegemea kwake. Na hakuwezekani kwa kitu chochote kilichopo, kudumisha kupat ikana kwake pasi na Yeye. Na hakuwezekani kuleta tafsiri yoyote na ufafanuzi wa fumbo la maisha, pasi na kuchukua usimamizi wake, Mwenyezi Mungu mtukufu, ambao una maana ya kuwa kusimama kwake ni kwa dhati yake na kusimama kila kitu ni kwa sababu yake – kwa mazingatio ya jambo hilo. Na hakuwezekani kabisa kusimamisha msingi wowote ulio sahihi wenye kukubaliwa na akili, kwa ajili ya kuufasiri ulimwengu wa kupatikana wala kudumu k wa u l i m w e n g u h u u , isipokuwa kwa sababu yake. Yeye ndiye dhati iliyopo, iliyotukufu na haya majina mawili yanatokana na jina lake tukufu.
Mambo yote na matukio yote ni udhihirikaji katika k u d h i h i r i k a k wa k e n a u l i m w e n g u n i k i t a b u katika kudhihirika huko. Kumewekwa mbele ya binadamu ili wakifikirie kufikiri kwa mtu anayetaka kukitwalia kitabu hiki na kukisoma. Manabi i na Mitume wao wako katika nafasi ya waelekezaji na
wafasiri wa kitabu hiki. Na vitabu vya mbinguni ni mfasiri bora sana wa kitabu hiki na hasa Qur’an tukufu. Ki tabu cha u l imwengu ambacho kinayanyakua macho kutokana na yale ambayo kimeyakusanya na yenye uhai na namna nyingi mno na balagha.
Anasema mjumbe wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) kuhusu ayat Al Kursiy kwamba hiyo ni aya kubwa sana kat ika ki tabu cha Mwenyezi Mungu na ni aya muhimu sana: “Na ndani yake, mna aya hiyo kubwa ya aya za Qur’an nayo ni aya Al-Kursiyy”. Umuhimu huu unakuja kutokana na haya yafuatayo:
1 . U m u h i m u k w a upande wa yale ambayo umeyakusanya aya hii ambayo inafundisha kumpwekesha Mwenyezi Mungu kwenye kutakata na ina kuwa ni tafsiri ya “sifa za Mwenyezi Mungu mtukufu”. Aya hii kwa sura ya jumla ni mfano wa surat, Al-Ikhlasi. Mtume (s.a.w.) alikuwa anasoma Surat Al-Ikhlas, katika kipindi cha Makkah ikiwa ni majibu ya kila swali linaloelekezwa kwake kuhusu Mwenyezi Mungu mtukufu. Kwa hakika kila sura katika Qur’an tukufu inamiliki thamani kubwa sana, isipokuwa daraja la ubora wake linatofautiana kutokana na yale ambayo yamekusanywa na sura hiyo.
2 . U n a f u n g a m a n a
umuhimu vile vile kutokana na majibu ambayo si ya kawaida ambavyo inayotoa kwa wale wenye kuzisoma aya na sura hizi na sura hiyo na aya zinakubaliana moja kwa moja na kiwango cha kuelewa kwa msomaji kutokana na upana wa upeo wake na kina cha ulimwengu wake wa ndani. Hakika nyenzo muhimu ambayo inafanya kazi yake katika jambo hili ni kuuelekeza moyo kwa Mwenyezi Mungu kwa imani ya kina sana. Kwa sababu ya kuliweka wazi jambo hili Mtume (s.a.w.) katika hadithi yake kuhusiana na mwezi wa Ramadhani na amesema:
“ M w e n y e k u f u n g a Ramadhani kwa kumwamini Mwenyezi Mungu na kwa kumtakasia nia, atasamehewa yale yaliyotangulia katika madhambi yake”.
Inadhihirika kutokana na maelezo haya kwamba k u m t a k a s i a M we n ye z i Mungu ndicho kiini cha matendo yote na msingi wake na roho yake. Al-Qayyoum – jina hili, linaelekea kwenye dhati ya Mwenyezi Mungu mtukufu na wakati huo huo linaelekea kwenye matendo yake kuhusiana na dhati yake Mwenyezi Mungu mtukufu. Jina hili linaelezea utangu wa Mwenyezi Mungu mtukufu na kubaki kwake. Ama upande wenye kuelekea kwenye matendo yake , upande huo ni kuelekea kwake kudumu kwa vilimwengu.
Kwa sababu kudumu kwa vilimwengu kunafungamana na kudumu kwake Mwenyezi Mungu mtukufu. Na yote yanayotajwa, katika kudumu – kwa vilimwengu, miongoni mwa kanuni na mfumo na kadhalika, hayo ni mambo ya mazingatio na kiwango. Na hakuwezekani kubaki kwa vilimwengu, kwa mfano wa kanuni hizi za kiwango na mazingatio. Tukitaka kuyapanua maelezo haya t u t a s e m a : K wa h a k i k a kunalazimu, kupatikana yule ambaye atazitekeleza kanuni hizi na atakayezielekeza kwenye kutenda naye ni Mwenyezi Mungu mtukufu.
Ibn Al-Arabi ana raai nyengine katika maudhui haya na tunaona kuwa ni jambo lenye faida kutaja hapa. Anasema Ibnu Al-Arabi kuwa kwa hakika zile hakika za vitu ni msemo unaoelezea kuhusu kudhihirika kwa majina ya Mwenyezi Mungu. Kwa msingi huo kupatikana katika uhakika, ni kukosekana, isipokuwa kudhihirika huku kunakuja hali ya kufuatana, kumoja nyuma ya kwingine kwa sura yenye kutiririka, kwa sifa ya kuwa tunaona kwa kudhihir ika huko, vitu vinapatikana na kule kudhihirika kunatawala juu ya kupatikana kwake. Na lau angetaka Mwenyezi Mungu kudhihirika huko, kitambo kimoja tu, vitu vyote vingeondoka na vingetoweka.
Ndiyo, kama alivyosema msani i ambaye n i mtu wa Tasawwuf Suleiman Jalabia. Alisema kuuambia u l i m we n g u k u wa “ N a lau, angesema: Ondoka ungeondoka ulimwengu.”
PROFESA Ibrahim Lipumba, amewataka wadau wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara na Visiwani kutoirejesha Zanzibar katika machafuko ya kisiasa ya mwaka 2000, na kusababisha vifo na wakimbizi.
Prof. Lipumba, ameyasema hayo Jumapili ya wiki iliyopita akizunguzma na Waandishi wa Habari katika Ofisi Kuu za Chama Cha Wananchi CUF, Buguruni Jijini Dar es Salaam, akizungumzia sintofaham ya kufutwa uchaguzi Mkuu wa Visiwani Zanzibar.
Mwanas iasa huyo na mtaalamu wa maswala ya Uchumi Duniani, alisema anazungumza kama mzalendo na kilicho msukuma zaidi ni uzoefu wake wa kisiasa nchini na uzalendo ili kuhakikisha nchi yake inabakia katika hali ya usalama.
Alisema, anaamini kuwa maamuzi ya Mwenyekiti wa ZEC, Zanzibar kufuta uchaguzi huo na kutoa sababu zenye maswali mengi kuliko majibu ni shinikizo kutoka kwa watu wa CCM, jambo ambalo ni hatari kwa mustakabali wa Visiwa hivyo na Tanzania kwa ujumla.
“Ndugu zangu wa CCM, msiturudishe katika matatizo
Kauli ya Prof. Lipumba kwa CCMNa Bakari Mwakangwale
ya mwaka 2000, ni wazi kabisa Wazanzibar hawako tayari kurudi huko kitendo cha kurudia uchaguzi kwa shinikizo si jambo la busara wakati wao (Wazanzibar ) waliofanya waliopiga kura hawajaulalamikia uchaguzi huo.
Sinikizo zitolewe katika suala hili kwa sababu yule bwana (Mwenyekiti wa ZEC) hawezi tu kwenda kutangaza alivyotangaza bila kuwa na shinikizo nyumna yake kutoka kwa watu wa Chama na Serikali”. Amesema Prof. Lipumba.
Prof. Lipumba, akawataka wale wanaoweka shinikizo la kufutwa uchaguzi wa mwaka huu, wakumbuke matukio yaliyotokea baada ya uchaguzi wa mwaka 2000, ambapo majimbo 16 ya Mkoa wa Mjini Magharibi, uchaguzi ulifutwa na ulirudiwa kwa shinikizo.
Al isema, matokeo ya maamuzi hayo ya shinikizo yalipelekea Wazanzibar zaidi ya 60, kuuwawa na baadaye Visiwa hivyo vikazalisha wakimbizi zaidi ya elfu mbili, kufatia maandamano ya amani yaliyofanyika Januari
27, 2001, kutokana na mvutano wa kisiasa uliosababishwa na CCM huku chama chake cha CUF, kikipinga.
“Tusirudie ya mwaka 2000, kwa mashinikizo ya watu kwani uchaguzi huu wa Oktoba 25, 2015, umeenda vizuri na wasimamizi wa nje wameona kuwa hapakuwa na ta t izo wala hakuna aliyeulalamikia kwa dosari yoyote ni wazi Mwenyekiti wa ZEC, amefanya maamuzi h a y o k w a s h i n i k i z o . ” Amesema Prof. Lipumba.
Akisahuri nini kifanyike k u i n u s u r u Vi s i wa v ya Zanzibar kuingia katika machafuko, Prof. Lipumba, alisema, jambo la maana linaloweza kulimaliza tatizo hilo ni Tume ya Uchaguzi Z a n z i b a r , k u l i a n g a l i a suala hilo kwa kuzingatia Katiba na Sheria, kwamba Mwenyekiti wa ZEC, peke yake hana mamlaka ya kufuta uchagaguzi Mkuu wa Zanizbar.
Prof. Lipmba, alisema ieleweke kuwa Zanzibar imeingia katika maridhiano ya
kidemokrasia, huku akimtaka Dk. Ali Mohammed Shein kukumbuka, mwaka 2010, alitangaza kuwa mshindi kwa kupata asilimia 50 na Maalimu Seifu wa CUF, asilimia 49.8.
Alisema, matokeo hayo ya l i sababisha mvutano mkubwa kwani kura karibia zilifungana lakini Maalim Seif, alikubali kushindwa kwa pointi, sasa akasema ni wakati wake Dk. Shein na CCM yake kukubali matokeo na waonyeshe ukomavu wa kisiasa, kwa kukubali maamuzi ya Wazazibar.
Alisema, haoni sababu ya CCM, kuogopa matokeo hayo ambayo yanaonyesha dalili ya Chama Tawala kuanguka kwa sababu Katiba ya Zanzibar i m e e l e z a k u we p o k wa muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, kwa kushirikisha chama chochote kilichoshiriki katika uchaguzi, na kupata zaidi ya asilimia tano ya kura za wananchi kitakuwa na sifa ya kushiri katika Serikali hiyo.
Aidha, alisema katika suala hili zisiletwe hoja za kuwadanganya Watanzania
na tukaingia katika matatizo yasiyo kuwa na sababu kwa madia kuwa CUF, itavunja M u u n g a n o , i k i t a w a l a Zanzibar, kwani kifungi cha sheria kinachoelezea suala hilo kinaeleza kuwa Zanzibara na Tanganyika zimeungana kuanzisha dola moja kwa maana hiyo suala la Muungano ni suala la Kikatiba (Articles of Union).
Wakati huo huo, kuibuka kwa aliyekuwa Mwenyekiti huyo wa CUF, katika ofisi cha chama hicho hapo Buguruni, kwa mara ya kwanza tokea a a c h i e wa d h i f a wa k e , umewafurahisha wanachama wa chama hicho baada ya kukusanyika kwa wingi na kumlaki huku kila mmoja akionyesha shauku ya kutaka kusalimiana naye, ambapo walisema wamefurahia ujio wake katika ofisi hizo na kuzungumza na vyombo vya habari.
Wal isema, wao kama wanachama kwa kuzingatia mchango wake katika CUF, watazidi kumkumbuka na kumuheshimu, kwani bado wanamapenzi makubwa na msomi huyo, pamoja na kwamba amechukua maamuzi ya kujiuzuru wakati bado wanamuhitaji awe kiongozi wao.
“Namwambia (Ismail) Jussa hatutoi (Serikali), l a b d a m t u p i n d u e . Serikali ya kimapinduzi h a i c h u k u l i w i k wa k a r a t a s i , h i l o nawabainishia”-Asha Bakari.
“ H a t a wa p i n z a n i washinde kwa kura, CCM hatuko tayar i kutoa Serikali. Vifaru n a m a k o m b o r a y a kivita yapo kwa ajili ya kuhakikisha hilo.”- Salmin Awadh Salmin.
Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar umefutwa na Tume ya Taifa ya U c h a g u z i Vi s i wa n i humo (ZEC), ambayo pia imetangaza kurudiwa kwa uchaguzi huo . Sababu zilizotolewa na Mwenyekiti wa ZEC, bwana Jecha Salim Jecha, wakati akifuta uchaguzi huo ni nyepesi mno na wala hazina mashiko. Jecha alishinikizwa na wenye mamlaka ya Zanzibar kufanya kile alichofanya!
Wa s w a h i l i w a n a m s e m o , " u k i m u o n a mbwa yuko juu ya mti, basi ujue hakupanda m w e n y e w e " . Wa t u wote wanaofuat i l ia kwa karibu siasa za Z a n z i b a r , wa n a j u a kwamba maneno yale si ya Jecha. Yeye katumika tu kuvuruga uchaguzi wa Zanzibar, ambao kwa mujibu wa waangalizi wa ndani na nje, ulikuwa umeenda vizuri.
N i w a k u m b u s h e kidogo kuhusu Bunge Maalumu la Kat iba mwezi April mwaka jana kule Dodoma. Mjumbe wa Bunge hilo kupitia C C M , A s h a B a k a r i Makame a l impasha m j u m b e m we n z a k e kutoka CUF, Ismail Jussa Ladhu. Alisema hivi:
“Namwambia (Ismail) Jussa hatutoi (Serikali), l a b d a m t u p i n d u e . Serikali ya kimapinduzi h a i c h u k u l i w i k wa k a r a t a s i , h i l o nawabainishia”.
T u m e w a h i p i a kumsikia al iyekuwa Mnadhimu Mkuu wa CCM kwenye Baraza la Wawakilishi, marehemu Salmin Awadh Salmin, akitamka kwamba hata wapinzani washinde
kwa kura, wao CCM hawako tayari kutoa Ser ika l i na akaf ika mahali pa kusema kuwa vifaru na makombora ya kivita yapo kwa ajili ya kuhakikisha hilo.
Ukizingatia kauli hizo, ambazo zimetolewa hadharani na makada wazito wa CCM, bila ya kukemewa, basi unajua kwanini uchaguzi wa Zanzibar umefutwa mwaka huu. Maalim Sei f Shari f f Hamad alikuwa ameshinda, isipokuwa wale wenye 'Hati Miliki' ya kutawala Zanzibar hawako tayari kuona hilo likitokea. Bora wafute matokeo, kuliko kumtangaza Seif mshindi!
K a m a k a w a i d a y a m a d h a l i m u , sasa wanahangaika kuhalalisha udhalimu wao, kwa kuhamisha mazingatio ya watu kutoka kwenye tatizo la msingi la Zanzibar a m b a l o n i w a o . Wamekuwa wakianzisha mijadala potofu kuhusu s i a s a z a Z a n z i b a r , kupitia mavuvuzela
yao yaliyomo kwenye vyombo vya habari!
Inasemekana kuwa tangu mwaka 1995, c h a g u z i z a v ya m a vingi zilipoanza, CCM hai jawahi kushinda Zanzibar . Imekuwa ikitumia hila, hadaa n a u b a b e k u p o r a maamuzi ya wananchi wa visiwa hivyo. Na mgogoro wa kisiasa unaofukuta Zanzibar, msingi wake hasa uko hapo. Mara zote ZEC imekuwa ikimtangaza a l iyeshindwa kuwa mshindi!
Na mpaka uchaguzi w a m w a k a 2 0 1 0 , muasisi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na kiongozi wa Kamati ya Maridhiano, Mzee Hassan Nassor Moyo, amekuwa aki tamka bayana kwamba ni yeye ndiye aliyetumwa na Rais Amani Karume kumshawishi Maalim Seif Sheriff Hamad akubali matokeo yoyote ambayo yangelitangazwa na ZEC mwaka huo.
Naye Maalim Seif alikubali kwa kuzingatia
umuhimu wa amani ya nch i pamoja na Maridhiano yaliyofikiwa kati ya CUF na CCM. S a s a u c h a g u z i wa mwaka huu, Maalim Seif alitangaza mapema kuwa hatakubali tena kuporwa ushindi wake. Ndiyo maana tunashuhudia viroja hivi vya kufuta matokeo! Wamekwama!
N i m e o n a nizungumzie kidogo kuhusu ukweli halisi wa siasa hizi zinazoitwa za 'Kidemokrasia' na Katiba zinazotokana na mfumo huo, ili wasomaji wangu waweze kuakisi kwa usahihi yale yanayotokea Zanzibar hivi sasa. Jambo la msingi ni kufahamu k wa m b a d h a n a ya 'Demokrasia' siyo halisi kama tunavyoaminishwa na watetezi wake. Ni ulaghai tu unaolenga k u w a n d a m i z a wa n y o n g e , k u p i t i a matumaini hewa.
Na kupitia Katiba inayotawala Zanzibar n a Ta n z a n i a B a r a , k a m we m a b a d i l i k o yatakayoifanya nguvu ya umma itawale nchi hizo hayatapatikana. C C M i t a e n d e l e a kutawala Watanzania, h a t u w e z i k u s e m a milele, lakini mpaka hapo watakapochoka wenyewe!
Tumefundishwa tangu shule za msingi kwamba 'Demokrasia' ni mfumo wa utawala wa Watu, unaowekwa na Watu kwa ajili ya Watu hao. Hiyo ndiyo dhana kuu inayotawala mfumo wa 'Demokrasia', ambayo sisi kama taifa tunaufuata na Katiba inayotuongoza imeuzingatia.
Lakini waasisi wa Siasa za Kidemokrasia duniani, wanaamini k w a m b a u k i w a p a wananchi mamlaka kamili kupitia Katiba, b a s i u n a h a t a r i s h a taas i s i yenyewe ya 'Demokrasia.' Wananchi hao wanaweza kuitupilia mbal i 'Demokras ia ' kwa kutumia nguvu waliyonayo kikatiba.
Kwa hiyo, walinzi halisi wa 'Demokrasia'
ni genge dogo tu la watu wanaonufaika na mfumo unaotawala na wala siyo wananchi kama inavyoaminishwa. Genge hili halitaki kabisa mabadiliko na limethibiti siasa za nchi kupitia Katiba na nguvu za Dola.
Ni vyema wananchi wakaelewa kwamba katika mifumo ya tawala za 'Kidemokrasia', si kweli kwamba wananchi ndiyo wenye mamlaka ya k u t u n g a K a t i b a itakayolinda maslahi yao. Katiba inatungwa na kikundi kidogo tu cha watu, na maslahi ya kikundi hicho ndiyo ya n a y o l i n d wa k wa gharama ya umma. Tu m e s h u h u d i a h i l i D o d o m a k w e n y e Bunge Maalumu la Katiba mwaka jana, a m b a p o m a o n i y a wananchi yametupwa, y a m e i n g i z w a y a watawala!
Pamoja na kwamba K a t i b a n i M u a f a k a wa K i t a i f a , l a k i n i Katiba pia ni chombo cha utawala. Kikundi kidogo kinachotawala nchi, huwa hakipendi mabadiliko yanayoweza kutishia utawala wao. Wanapendelea zaidi Katiba i takayolinda utawala wao milele! Wananchi wanaburuzwa tu kwa kutumia hila, h a d a a , v i t i s h i o , propaganda, danganya toto na ubabe.
Tumeshuhudia jinsi 'Demokrasia' ilivyopora haki ya Wananchi wa Misri, Uturuki, Algeria, Tunisia, Iraq, Afghanistan na Palest ina. Hakuna asiyejua kwamba wananchi wa nchi hizo wakipewa mamlaka kamili lazima watachagua utawala wa Kiislamu. Lakini kwanini nchi hizo za 'Kidemokrasia', hazitawaliwi Kiislamu l e o ? Wa n a n c h i wa k e hawana mamlaka yoyote. Hiyo ndiyo kanuni ya 'Demokrasia'!
Genge la watawala linaamini kwamba katika m f u m o wa S i a s a z a 'Kidemokrasia', Katiba ni chombo tu cha watawala kuwabana watawaliwa, i n g a w a k w e n y e ma jukwaa ya s iasa wanahadaa kwamba wananchi ndiyo wenye mamlaka yote.
KIFARU cha jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikirandaranda katika mitaa ya Chake Chake, Pemba hivi karibuni.
Ofisi zetu zipo: Manzese Tip TopUsangi House, barabara ya Morogoro, D'Salaam
RAIS John Pombe Joseph Magufuli ameanza kazi rasmi baada ya kuapishwa j a n a k a t i k a s h u g h u l i iliyofana.
Pamoja na kuhudhuriwa na Marais wa nchi mbalimbali na wageni wengi waalikwa kutoka nchi za nje, umati mkubwa wa wananchi ulihudhuria kushuhudia hafla hiyo ya kihistoria.
Na kutokana na umuhimu na uzito wa tukio la kupishana ma-Rais, anayetoka Ikulu na anayeingia, jana ilitangazwa kuwa siku ya mapumziko.
Kama ilivyo ada, vikosi vya majeshi yetu vilifanya g wa r i d e l a k u f a n a n a kuhitimisha kwa kula kiapo cha utii kwa Rais, huku Rais Magufuli naye akila kiapo cha kuwatumikia wananchi na kuilinda Katiba ya nchi.
Wakati Magufuli anaingia Ikulu, anapishana mlangoni na Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye anaelekea katika ‘benchi’ la Marais Wastaafu.
Kama ilivyokuwa kauli zake wakati wa kampeni, kinachotarajiwa kwa Rais Magufuli ni uchapakazi na utumishi kwa wananchi wa kiwango cha hali ya juu.
Hapana shaka ukiacha yale yaliyoainishwa katika Ilani ya CCM ambayo yanakuwa kama ndio mwongozo wa utendaji wake, ikiwemo utekelezaji wa ahadi za Chama chake kwa wananchi, kuna yale ambayo Rais Magufuli binafsi amejinasibu kuwa atayafanya.
M a t a r a j i o n i k u w a utekelezaji huo utaanza mara moja ili angalau kuanza na ‘mguu wa kulia’. Kuwapa wananchi matumaini.
Yapo ambayo CCM na Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete aliahidi kuyafanya, na katika hayo huenda yapo ambayo hakujaaliwa kuyatekeleza na labda angetaka muda zaidi ili aweze kuyafanya.
Miaka mitano au kumi yaweza kuonekana kuwa mingi, lakini ukishtuka utadhani ilikuwa jana tu ulipongia Ikulu, miaka 5 au 10 imemalizika.
Uliyopanga kufanya labda hujagusa hata robo yake na wananchi wanakulilia. Au umefanya mengi, lakini ya kukuletea lawama na laana kutoka kwa wananchi.
Sasa bora wa kul i l ie wakitaka uwaongeze katika mema uliyowafanyia, kuliko wakulilie huku mwenyewe ukijuta na kujilaumu kuwa hujafanya lolote la maana katika uliyowaahidi. Au
Ameapishwa, ameanza kaziKikwete imekuwa ‘lam yalbathuu illa…’Mheshimiwa Magufuli alizingatie hilo
umeharibu na kuvuruga hata yale machache mazuri uliyoyakuta.
W a i s l a m u k a t i k a m a f u n d i s h o y a o wanaambiwa kuwa Siku ya Hukumu itakapofika, wale ambao waliishi katika maisha ya dhambi watajuta kwa nini waliumbwa binadamu.
W a t a s e m a , “ l a i t i ningalikuwa udongo nisipate adhabu hii inayoningoja hivi sasa.” (78:40)
Kat ika munasaba wa kuingia Ikulu, hapana shaka itakuwa ni katika Dua na Dhamira ya Rais Magufuli, kufurahia utumishi wake katika nafasi ya Urais na sio kinyume chake.
Lakini la kuzingatia pia ni kuwa muda haumngoji mtu.
K a d i r i a t a k a v y o i s h i mwanadamu, lakini siku ya kuondoka kwake duniani, anaona kama hakuishi ila siku moja au nusu siku tu.
Na ndio pale Qur’an i n a p o s e m a , “ S i k u watakapokiona (Kiama-Siku ya Hukumu) watakuwa kama kwamba hawakukaa (ulimwenguni) ila jioni moja au mchana wake tu.” (79:46)
B a s i k a m a n d i v y o itakavyokuwa siku ya kufa na siku ya Hukumu, basi ni hivyo hivyo katika kukaa Ikulu.
Walipita Wazee wetu, Mwalimu Nyerere, Benjamini William Mkapa, Alhaji Alli Hassan Mwinyi na sasa Jakaya Mrisho Kikwete, lakini siku wanaondoka Ikulu, si ajabu waliona kama hawakukaa ila kidogo tu.
Bado wangali wanatamani ‘utamu’ wa kukaa Ikulu (madaraka), lakini muda wao umekwisha.
Utamu huu wa madaraka, ndio huwafanya baadhi ya ma-Rais kufanya vitimbi kudumu Ikulu ili waendelee kupigiwa saluti, barabara zisafishwe kwa ving’ora wakipita, na mbwembwe za walinzi kila upande. Wenye ‘visirani’ ndio usiseme, w a e n d e l e e k u w a o n e a baadhi ya watu, ambao kwa sababu moja au nyingine wal iwahesabu kuwa ni maadui.
Sasa maadhali nchi yetu ishaj i jengea utamaduni wa kuondoka kistaarabu kila baada ya muda fulani, uungwana ni kutumia muda vizuri kufanya yaliyo mema kwa mujibu wa matarajio ya wananchi na kwa manufaa ya nchi.
WAKATI hali bado ikiwa haijatengemaa, huku juhudi zikifanyika za kukutana viongozi wa serikali na v ya m a k u s h u g h u l i k i a mtafaruku ul io tokana na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salum Jecha, kufuta uchaguzi mkuu Zanzibar, w a t a a l a m w a s h e r i a wameeleza kuwa muda wa Dk. Ali Mohamed Shein kutumikia madaraka yake kama Rais wa Zanzibar umemalizika kikatiba.
Kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, Rais wa sasa wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, amemaliza muda wake wa kuiongoza serikali ya Zanzibar na kwamba, iwapo ataendelea kuongoza Wazanzibar baada ya kipindi chake kukoma, atakuwa anakwenda kinyume na Katiba.
Hayo yamebainishwa na Chama cha Wanasheria Zanzibar (ZLS), wiki hii na kwamba, pia kuendelea kuwa na serikali isiyokuwa na Baraza la Wawakilishi pia ni tatizo kubwa na ni kinyume na katiba.
Rais wa chama hicho Bw. Awadh Ali Said, alisema kuwa maudhui ya Ibara 28 (1) ya katiba ya Zanzibar, ni kumpa uwezo wa kikatiba Rais kuendelea kuongoza ili kutoa nafasi ya maandalizi ya kula kiapo kwa Rais anayefuata tu, na si kuendelea kukaa madarakani bila ya kufanyika kwa uchaguzi au kwa sababu ya uchaguzi kufutwa.
Aidha Bw. Said alisema kitendo cha nchi kuendeshwa muda mrefu bila ya Baraza l a Wa w a k i l i s h i k a m a yalivyo mazingira ya sasa yanavyoonyesha, ni tatizo.
A l i s e m a , K a t i b a ya Zanzibar imeruhusu hali ya kuendesha nchi bila ya Baraza la Wawakilishi ni kwa muda usiozidi siku tisini (90) tu, tangu siku Baraza lilipovunjwa.
“ K w a m a z i n g i r a tuliyonayo, siku tisini (90) zinazokubalika kikatiba, z inaishia Novemba 12, 2015 kwa kuwa Baraza la Wawakil ishi l i l ivunjwa Agosti 13, 2015,” alifafanua.
R a i s h u y o w a Z L S alionyesha pia hatari ya Zanzibar kuwa na Rais ambaye yuko juu ya Sheria na Katiba katika mazingira yaliyopo sasa.
Alisema kuwa Ibara ya 37 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 inayolipa M a m l a k a B a r a z a l a Wawakilishi kuondoa kinga ya Ra is kutosh i tak iwa anapokuwa madarakani kama inavyotolewa na Ibara ya 36 ya Katiba.
Dk. Shein amemaliza muda wake kikatibaNa Mwandishi Wetu
Dk. Ali Mohamed Shein
Aliongeza kuwa katika mazingira yaliyopo hivi sasa ambapo ifikapo tarehe 12 Novemba, 2015, Baraza la Wawakilishi halitakuwapo na haliwezi kuitishwa kikatiba, ni wazi kuwa ikiwa Rais atafanya matendo yoyote yenye kuvunja katiba ya nchi na kukiuka kiapo chake, hakutakuwa na mamlaka nyingine yoyote yenye uwezo wa kuhoji matendo ya Rais.
Alidai hali hiyo inatoa fursa na ina tengeneza hatari ya kuwa na Serikali inayoongozwa ‘kidikteta’.
Sakata hilo la Zanzibar kwa mara ya pili limemwibua mwenyekiti wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, a k i m t a k a R a i s J a k a ya Kikwete kumaliza tatizo la Zanzibar kwa kuiamuru ZEC kumtangaza mshindi wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 ili kuliepusha Taifa lisiingie kwenye machafuko.
A k i z u n g u m z a n a waandishi wa habari hivi karibuni, Lipumba alisema ni muhimu Rais Kikwete akahakikisha anatekeleza hilo kabla ya kumaliza muda wake, badala ya kumwongezea matatizo na mzigo rais mpya, Dk. John Magufuli aliyeapishwa jana.
“ D k . J o h n M a g u f u l i a taapishwa kuwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Vi k o s i v ya U l i n z i n a Usalama vya Tanzania, Kikwete usimwongezee Magufuli matatizo, yaliyopo ya n a m t o s h a , ” a l i s e m a L ipumba ambaye wik i iliyopita akizungumzia pia mgogoro huo akiitaka ZEC imtangaze mshindi.
Aidha kuapishwa kwa Dk. Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni dhahiri kwamba kitakachofuatia kuanzia hapo ni kumteua Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano na kufuatiwa na kuteua Baraza la Mawaziri, ambalo kimsingi litajumuisha pia na baadhi ya Mawaziri kutoka Zanzibar, hasa kwa zile wizara za muungano.
Prof. Lipumba alisema, vigogo wa Tanzania na Zanzibar wasisubiri hadi maafa yatokee ndipo waanze kuchukua hatua, watumie muda huu kuyazuia.
“Nayakumbuka mauaji ya wafuasi wa CUF yaliyotokea mwaka 2001 na wengine kukimbil ia uhamishoni Shimoni nchini Kenya, n i m e o n a k u k a a k i m ya kutaleta madhara katika nchi hii,” alitahadharisha.
Tayari hali hiyo ya utata wa kisheria katika mamlaka ya Zanzibar kwa sasa imezua wasiwasi kiasi hata Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdan Omar Makame, ameshasema kuwa kutokana na taarifa hizo za wanasiasa na watu
wengine, huenda wananchi watakuwa huru kufanya watakavyo na kuvunja sheria.
Makame alisema ni vyema kipindi hiki kuhubiri amani na kuwa na subira kuiachia ZEC ambayo ndiyo yenye dhamana na mamlaka ya kutangaza tarehe ya kurejewa kwa uchaguzi na si mtu mwingine.
K a m i s h n a M a k a m e alinukuu kifungu cha 28 (1) cha Katiba ambacho pia wanasheria wa ZLS walikitoa na kumwomba Rais wa Zanzibar kuchukua tahadhari , i l i asiwe wa kwanza kuvunja Katiba ya Zanzibar kwa kuvuka tarehe ya mwisho kuwapo madarakani.
Kifungu cha 28 (1) cha Katiba kinasema, “Kufuatana na Katiba hii mtu ataendelea kuwa Rais mpaka (a) Rais anayefuata ale kiapo cha kuwa Rais, au (b)afariki wakati akiwa Rais, au (c) hapo atakapojiuzulu; au (d) iwapo amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ; au (e) kwa sababu yoyote nyingine ameacha kuwa kiongozi kwa mujibu wa vifungu vingine vya katiba hii.
“ I k u m b u k w e k u w a k u t o k u w a p o R a i s w a nchi kama inavyodaiwa, haimaanishi sheria hazipo na watu wafanye watakavyo. Kuna makosa ukiyafanya moja kwa moja sher ia itachukua mkondo wake ikiwamo kufanya kitendo cha uvunjifu wa amani, kufanya maandamano au mikusanyiko ya watu isiyo halali,” alisema kamishna huyo.
Wakati hali ya mashaka i k i t a m a l a k i Z a n z i b a r , Wazanz ibar wanao ish i nchini Uingereza (ZAWAUK) wamepanga kuandamana hadi katika ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini humo kupinga yale yaliyotokea Zanzibar wakati wa uchaguzi Mkuu.
Aidha Wazanzibar hao kwa mujibu wa taarifa iliyonakiliwa na mtandao
Dk. Shein amemaliza muda wake kikatibaInatoka Uk. 4wa Mzalendonet, walifikia makubaliano katika kikao kilichofanyika Jumatatu wiki hii Novemba 01, 2015, ambacho kilijadili mwenendo mzima wa hali ya kisiasa nyumbani Zanzibar na matokeo ya uchaguzi ambayo hayakukamilika kutangazwa.
W a z a n z i b a r waliohudhuria katika kikao hicho, wengi walipitisha a z i m i o l a k u f a n y i k a maandamano hadi katika ofisi za ubalozi wa Tanzania Uingereza na kufikisha barua kwa wabunge wa Uingereza kuhusu suala hilo.
Kuna kila dalili kwamba t a y a r i w a p o a m b a o wameshawasilisha barua hizo kwa wabunge wa Uingereza na kuwataka kufikisha ujumbe wao kwa Waziri Mkuu wa Uingereza Bw. David Cameroon, ili kuingilia kati mzozo uliopo baina ya vyama vya CCM na CUF kuhusu kufutwa uchaguzi mkuu.
A i d h a s u a l a l a m a a n d a m a n o b a d o lilielezwa kuwa bado lipo kama lilivyopangwa, lakini imetolewa kwanza nafasi kwa viongozi Tanzania kuendelea na mazungumzo hadi kufikia ufumbuzi wa mzozo huo.
Imeeleza taarifa hiyo kuwa wakati viongozi wa Z AWA U K wa k i f u a t i l i a kwa karibu mazungumzo hayo, iwapo itaonekana hakuna dalili za maendeleo yeyote ya maridhiano, basi Wazanzibar hao wataendelea na maandamano ya siku tatu mfululizo katika Balozi za Tanzania nchini Uingereza kama yalivyopangwa na kukubaliana.
Kuna taarifa kuwa jeshi la Polisi Scotland Yard Special Events, limeshafikishiwa taarifa ya maandamano h a y o n a m a a n d a l i z i yalikashamilika.
Mwishoni mwa mwezi wa Oktoba 2015, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ilitoa ushauri wake kwa ZEC, kuhusiana na tangazo la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Bw. Jecha Salim Jecha, alilolitoa Oktoba, 28 2015 kupitia vyombo vya habari, la kufuta matokeo ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Zanzibar Oktoba 25, 2015 na kuahirisha mchakato mzima wa uchaguzi hadi hapo Tume hiyo itakapotoa taarifa ya kufanyika tena uchaguzi huo.
K a t i k a t a a r i f a y a Mwenyekiti wa Tume hiyo ya Haki za Binadamu Bw. Bahame Tom Nyanduga, ilitoa ushauri kuwa baada ya kupitia Ibara na vifungu mbali mbali vya Katiba zote mbili na sheria husika, yaani katiba ya Jamhuri ya Muungano na Katiba ya Zanzibar, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora (THBUB) ilijiridhisha kwamba ina uwezo wa kuishauri Tume
ya Uchaguzi ya Zanzibar kuhusiana na masuala kadhaa yaliyojitokeza katika Tamko la Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar.
Tume hiyo ilieleza kuwa Ibara ya 21 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, na Ibara 21 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 [1]
RAIS wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein (kushoto), Makamu wake wa kwanza, Maalim Seif Sharif Hamad.
zikisomwa pamoja, zinatoa uhuru wa kila raia kushiriki katika shughuli za uongozi wa Serikali kwa kupitia uwakilishi wa kuchaguliwa na kuchagua kwa uhuru na haki.
Ilieleza kuwa pia kifungu cha 42(6) cha Sheria ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar [2] kinaipa Tume (ZEC)
mamlaka ya kushughulikia matatizo ya uchaguzi na kuyapatia ufumbuzi kwa utaratibu ulioanishwa katika kifungu hicho.
THBUT ilisema kuwa kifungu hicho kinabainisha mamlaka ya Tume (ZEC) kutangaza matokeo ndani ya siku tatu na endapo kuna matatizo yamejitokeza katika
mchakato wa uchaguzi, ZEC inatakiwa kuyatafutia ufumbuzi, na baada ya hapo matokeo yatatangazwa ndani ya siku tatu.
Aidha THBUB ilieleza kupitia sababu zilizotolewa n a M w e n y e k i t i J e c h a n a k u b a i n i k w a m b a mambo yote yaliyotajwa, y a n a w e z a k u t a t u l i w a iwapo Makamishna wa ZEC wataweka tofauti zao pembeni, na wakafanya kazi kwa pamoja kwa nia njema.
Hivyo THBUB ilishauri kwamba tofauti ama kasoro za kiutendaji zilizotajwa zinaweza kutatuliwa kwa kuhakiki waliopiga kura kwa mujibu wa daftari, na kwa kuzingatia sheria zilizopo na kwamba, THBUB inapenda kumshauri Mwenyekiti wa ZEC kutafakari upya uamuzi wake wa kufuta uchaguzi na matokeo yake yote.
Katika hitimisho la taarifa hiyo, THBUB il isisit iza umuhimu wa kila mdau wa uchaguzi kuzingata sheria, katika mchakato mzima, kwani bila kufanya hivyo misingi ya utawala bora itakuwa imevunjwa, na hivyo inaweza kusababisha uvunjifu wa haki za binadamu na kwamba, wao wapo tayari tayari kushirikiana na ZEC kuchunguza tuhuma zote zilizotajwa na Mwenyekiti Jecha na kuzitafutia ufumbuzi wa haraka ili kulinda haki za binadamu na misingi ya utawala bora.
ALIYEKUWA mgombea Ubunge kupitia Chama Cha CUF, Kondo Juma Bungo, amesema yeye pamoja na wapiga kura wa Jimbo la Mbagala, wanaimani wameshinda uchaguzi huo.
Kwa maana hiyo, alisema h i v i s a s a y u p o k a t i k a m c h a k a t o wa k we n d a Mahakama Kuu Jijini Dar es Salaam, kupinga mgombea wa CCM, katika jimbo hilo kutangazwa kuwa ndiye mshindi.
“Napenda niseme, sina kanuni ya kukata tamaa katika kudai haki katika hali yoyote na haswa nikiamini kuwa nipo katika haki, nitahakikisha uchaguzi wa Jimbo la Mbagala unarudiwa kama alivyo tangaza na M k u r u g e n z i , k a b l a ya kumtangaza mgombea wa CCM.” Alisema Kondo.
A l i s e m a , h a k u n a l i n a l o s h i n d i k a n a k wa Mwenyezi Mungu, ikiwa tu utaonyesha jitihada za kudai na kupigania haki, n a M w e n y e z i M u n g u hapendi wale wanaokubali kudhulumiwa haki zao bila kuonyesha jitihada zozote.
Akiwashukuru wananchi wa jimbo la Mbagala na kila aliyemuunga mkono tokea alipotia nia ya kugombea U b u n g e , a l i s e m a k wa ujumla hana tamko ambalo litawakilisha hisia halisi ya
Sheikh Bungo kwenda mahakamaniNa Bakari Mwakangwale
thamani yao kwake zaidi ya shukrani zake kwao kwani wote walisema wapo nyuma yake katika suala hilo.
“ Z a i d i , n a p e n d a kuwashukuru wananchi wa J imbo la Mbaga la , h a k i k a wa m e n i c h a g u a tena kwa kura nyingi na hakika nimeshinda na wao wameshinda pia, lakini kilichotokea nimeporwa haki yangu na haki ya wapigiga kura kwa ujumla.” Amesema Kondo Bungo.
Akielezea sinto fahamu iliyotekea katika Jimbo lake, mpaka kuamuliwa kurudiwa uchaguzi kisha baadae kutangazwa mgombea wa CCM, kuwa ndiye mshindi, Kondo, alisema kwa ujumla
uchaguzi umevurugwa na Watendaji wa Halimashauri pamoja na wasimamizi wa uchaguzi.
Alisema, wameharibu uchaguzi kutokana na kuficha nyaraka za matokeo kwa kuwanyima baadhi ya mawakala wake fomu za matokeo, hata hivyo alidai walipopit ia karatasi za watendaji hao walizobandika katika vituo vya kupigia kura zinaonyesha yeye ameshinda.
“Utata ulipozuka katika k u h a k i k i , n d i p o a k a j a Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, naye alipoelezwa a l ik i r i kwel i uchaguzi umeharibiwa na kwamba itabidi urudiwe na akaahidi
mbele ya Waandishi wa Habari, kuwa uchaguzi wa Jimbo la Mbagala umefutwa na utarudiwa na kututaka wahusika wote kurejea katika kituo cha majumuisho ya kura ili kutoa tamko ni lini uchaguzi utarudiwa hayo ndiyo yalikuwa makubaliano kwa ujumla.” Alisema Kondo Bungo.
Hata h ivyo , a l i sema katika hali ya kushangaza na kusikitisha siku iliyofuata asubuhi walipofika kituoni hapo kama walivyoelezwa n a M k u r u g e n z i w a Temeke, walikuta matokeo y a m e s h a b a n d i k w a yakionyesha mgombea wa CCM, kuwa ndiyo mshindi.
ALIYEKUWA mgombea Ubunge kupitia Chama Cha CUF, Kondo Juma Bungo.
A: KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOLWALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA I, 2015
WAVULANAS/N NAME
1 ABBAS ANAS SAID2 ABBAS HAJI ALI3 ABDALLAH SADIK FAKI4 ABDIRRAHMANI MOHAMMED ELMI5 ABDUL-ALAWI GENDO6 ABDUL-AZIZ AMIN7 ABDULI ADAM MSANGI8 ABDULKADIR SALIM KARATA9 ABDULMUSTAFA MUHAMED
10 ABDULRAHMANI MUSSA MSANGI11 ABDULSEIF HUSSEIN KATERANYA12 ABDULWAHAB SHAZIL MOHAMED13 ABUBAKAR MAJALIWA NGONJI14 ABUBAKI IDD MALEGELI15 AHMAD MBWIZA ISSA16 AHMADI HASSANI SEMPOLI17 AJMI ABDALLAH SALEH18 ALI HUSENI MADENGE19 ALKAMAL SADIKI KIUNGULIA20 ALLY HASSAN MSHEHE21 ALLY ISSA KILINDO22 ALLY MAKAME ABASI23 AMHMED SAIDI CHUDI 24 AMIRI JUMA KULEWA25 ANSWARI RIDHIWANI MSANGI26 AQRAM ABDALLAH MSANGI27 ARIF JUMA KHAMIS28 ASHRAF FAKHI ADAM 29 ATHUMANI JUMA ALLY30 BAKARI MUSSA KAMBWELA31 FADHILI HAJI HAMIDU32 HAMISI MAKANGE SAKO33 HAMISI SELEMANI HAMISI34 HASHAMU HAMADI BAKARI35 HASHIMU MUHIDINI RAMADHANI36 HASSAN DHAHIR MSOFE37 HASSAN KOMBO HABIBU38 HASSANI RAMADHAN NGEZE39 HILALY ISSAH SWEDY40 HUDHAIFA SADAT HASHIM41 HUSEIN SALIM MWAIMU42 HUSSENI ABBASI MRUMA 43 IBARAHIMA RAMADHANI MSASU44 IBRAHIM ABBAS JUMA45 IBRAHIM NASIBU LYOKA46 IBRAHIMU SHABANI SALUM47 IDDI BAKARI HAMISI
48 IDDI HASSAN MBAGA49 IDDI RAMADHANI MMBAGA50 IKRAM JUMANNE ZUBEIR51 IS-HAKA MOHAMED LUPATU52 IS-HAQA VUAI HAJI53 ISMAIL IBADA SWALEHE54 ISSA IDI NUHU55 ISSA KHALFAN IDD56 ISSA RAJABU ITIEGE57 ISSA SHABANI MCHOMVU58 JAMALI MSITIRI MALONGWE59 JUMA ALLY MFINANGA60 KARIMU HAMISI JUMANNE 61 KHALIDI KOMBO SIWA62 KURIA MOHAMED MIRAJI63 LUGENDO ADINANI MKOMWA64 MASSA HUSSEINI KAHEMA65 MAULID ABDALLAH MSUYA66 MAYA ABBASI MWALIMU67 MBARAKA MUSSA MWINGIRA68 MOHAMED HUSENI KIBAURA69 MSHEWA ABBASI MUNIRI70 MUNA ABUBAKAR MUNA71 MUSA ABDALLAH BADI72 MUSSA YASINI GOMA73 MWAITA MUHAMED MWAITA74 NAJM KASSIM MSABA75 OMARY BAKARI MSAMI76 OTHMANI MUSA KIWERU77 RAHMAN ABUBAKAR SAID78 RAJABU MUSSA NDAWALE79 RAMADHAN MAULID JUMA80 RAMADHAN VUAI HAJI81 RAMADHANI ALLY SHEMAZIGE82 RAMADHANI HAJI CHIGGA83 RAMADHANI MMBAGA MBAGA84 RASHID MIRAJI MLINDOKO85 SAIDI ADAM MAGOGO86 SALIMINI JUMA KIMU87 SALUM MOHAMMED88 SAMIR MASOUD OMAR89 SELEMAN JABIR SHEKANDI90 SHABAN SHAFII KEJJO91 SHABANI RAMADHAN MADAMBO92 SHABANI VICTOR MZIRAY93 SHABIR FAIZ WALIH SHABUOIN94 SHARIFU ISSA MAKANGE95 SULEIMAN SALUM MSABAHA96 SULTANI MUHAMED SULEYMANI
97 SWALEHE MASSOUD SALIM98 TARIQ AHMED KAKERE99 TARIQ KHALID HASSAN
TA R E H E 2 1 M a c h i 2015 ilikuwa siku ya kuadhimisha mwaka wa 50 wa kuondoa ubaguzi duniani (50th anniversary of the International C o n v e n t i o n o n t h e Elimination of All Forms of Racial Discrimination (ICERD). Hii ni siku maarufu kwa jina la: “International Day for the Elimination of Racial Discrimination.”
Na ujumbe wa mwaka huu ulikuwa: “Learning from historical tragedies to strengthen the global fight against racism.”
Ukiwa na maana ya kuwahimiza watu kusoma kutokana na yaliyojiri katika historia, ili pasiwe na kurudia makosa na wakati huo huo kuongeza juhudi katika kukabiliana na uovu wa ubaguzi.
Katika ujumbe wake kwa siku hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kufuta ubaguzi (Committee on the Elimination of Racial Discr imination) , Jose Francisco Cali Tzay, alitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuvunja ukimya juu ya uovu wa ubaguzi na wajifunze kutoka historia ili wasiruhusu tena uovu huo dhidi ya binadamu kutendeka katika zama hizi.
“Nchi za Ulaya zilibuni sera za kibaguzi dhidi ya watu wengine zikajipa ubora na haki juu ya wengine ili zipate kisingizio na sababu ya kuwatawala na kuwanyonya wengine, n a s a s a w a n a t a k a kupanua zaidi ‘ubora’ na ukandamizaji wao kwa wengi zaidi (jambo ambalo halikubaliki). Amesema Jose Francisco Cali Tzay k a t i k a u j u m b e wa k e mwaka huu.
“There is only one race around the world and that is the human race, so in theory there is no basis for racial discrimination.”
Amesema Cali Tzay a k i m a a n i s h a k u w a (maadhali watu wote wameumbwa na Mungu), kimsingi kuna taifa na kabila moja tu: nalo ni binadamu (human race). Kwa maana hiyo, hakuna sababu wala kisingizio c h a n a m n a y o y o t e kinachoweza kuhalalisha ubaguzi dhidi ya watu wengine.
Katika moja ya kauli na maandiko yake, Cali Tzay anasema kuwa japo huwezi kusema kuwa chimbuko la ubaguzi ni ubepari/ubeberu, lakini mfumo huo
‘Hapa kazi tu’ isiwe kufunga MasheikhSema ‘Hapana’ kwa usanii wa ugaidi'Mbele kwa mbele’ iwe fuata nyao za Robin…Kulikamata kambaku kwa mapembe yake
Na Omar Msangi
msingi wake ni unyonyaji na kutaka faida hata kwa kudhulumu wengine. K w a h i y o , u b a g u z i h u s t a w i s a n a p e n ye ubeberu. Na mabeberu hawaishi kubuni mbinu za kufanikisha agenda zao za siri huku wakijifanya kuwa wasamaria wema.
Kwa upande wake ‘Shaheed’ Malcolm X anasema kuwa, "You Can't Have Capitalism Without Racism".
K wa m a a n a k u wa unapokuwa na mfumo wa kibepar i , huwezi kuepuka ubaguzi, uonevu na ukandamizaji kwa misingi ya rangi/taifa. Na kwamba ili kulinda mfumo wao, mabeberu wamekuwa wakitumia jeshi, polisi na vikosi maalum vilivyovutishwa bangi la kuwachukia na kupambana na kila wanaopakaziwa ubaya na mabwana zao ‘mabeberu’.
Kutokana na wito wa Malcolm X, wapinga ubaguzi nchini Marekani wamekuwa wakiandaa h a f l a m b a l i m b a l i yakiwemo makongamano na maandamano kupinga harakati na mipango ya mataifa yanayotajwa kuwa tajiri zaidi duniani G20. Na mwaka huu wameitisha maandamano New York na miji mingine, siku moja kabla ya mkutano wa G20 (G20 Summit)utakaofanyika Uturuki baadae mwezi huu.
“November 15 A People’s R e s p o n s e t o t h e G 2 0 Summit”, ni maandamano a m b a y o w a a n d a a j i wanasema ni muhimu kwa sababu yataainisha hisia na hasira za walimwengu dhidi ya watu wachache wanaohodhi mal i na rasilimali za dunia huku wakiwatia wengine katika dhiki na tabu ya kudumu ya umasikini.
W a a n d a a j i w a m a a n d a m a n o h a y o waliojipa jina “People’s Power Assembly” wanasema k u wa b i l a ya k u j a l i nini itakuwa agenda ya mkutano wa G20 mwaka huu hapo Novemba 16, lakini la kuzingatia ni kuwa mabebebru hawa n d i o wa n a s a b a b i s h a mauwaji na mateso kwa watu wasio na ajira, walio na ajira kulipwa mishahara midogo, kukosekana kwa huduma za kijamii, na baya zaidi hivi sasa wameibuka na mpango wa vita na mauwaji katika nchi mbalimbali duniani wakitaja Iraq, Libya, Syria, Yemen na mauwaji ya kikatili dhidi ya Waarabu, Wa a f r i k a , Wa i s l a m u na watu wa Asia, kwa kisingizio cha kupambana na magaidi.
Pengine hili la kuvamia nchi kuondoa uongozi na hili la kuuwa watu kwa kisingizio cha ugaidi ndio tulizungumzie hapa kama ujumbe maalum kwa Rais wetu Mheshimiwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli aliyeapishwa jana kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano katika Jamhuri ya Tanzania.
Hivi karibuni aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza Tony Blair na baadhi ya wanasiasa wa Marekani, wamenukuliwa wakisema k u w a u l i m w e n g u ungekuwa salama zaidi
ukiwa na Saddam Hussein na Muammar Gaddafi wakiwa viongozi wa nchi zao. Kwa maneno mengine wanakiri kuwa walifanya makosa kuwapiga na kuwaondoa madarakani v i o n g o z i h a o , k w a kisingizio chochote kile kilichotolewa wakati ule.
Akizungumzia suala la Iraq, Bair alikiri kwamba walifanya makosa na waliongopa walipodai kuwa Saddam ana silaha za maangamizi . Kwa lugha ya kidiplomasia alisema kuwa habari za ki-intelijensia walizotegemea zilikuwa urongo mtupu.
“I apologise for the fact that the intelligence we received was wrong. I also apologise for some of the mistakes in planning and, certainly, our mistake in our understanding of what would happen once you removed the regime.”
Alisema Blair wakati akihojiwa na CNN ambapo alikiri pia kuwa yeye na Bush ndio sababu ya kuibuka kwa ‘magaidi wa IS’ na anaomba msamaha k w a k u s a b a b i s h a ‘Jahannam’ katika Iraq na Libya.
Lakini Blair ni mwongo n a b a d o a n a e n d e l e a kusema uwongo na hivyo kuomba kwake msamaha ni kiini macho. Ndani ya nafsi anafurahi kwamba yao yamefanikiwa. Ni mwongo kwa sababu yeye na mwenzake Bush ndio waliopika hizo taarifa anazosema za uwongo za ki-intelijensia ikiwemo ile barua ya kughushi juu ya uranium kutoka Niger. (Tazama: Niger Yellow Cake Forgery, "CIA man denies Niger-Iraq uranium link na Niger upset by uranium slur.)
Tutakumbuka kuwa B l a i r n a w e n z a k e , walipotaka kumng’oa M u a m m a r G a d d a f i kwa masi lahi yao ya kibeberu, walisingizia k u w a w a n a k w e n d a kuwanusuru watu wa Benghazi kutokana na kile walichodai kuwa ni mipango ya mauwaji ya hilaki (genocidal designs) ya Gaddafi dhidi ya watu wa mji huo. Obama akasema wanakwenda Libya “to prevent a “bloodbath’’ in Benghazi.
L a k i n i k a m a anavyosema Profesa Alan J. Kuperman (Professor of public affairs at the University of Texas), yote ilikuwa ni urongo mtupu. (Tazama: False pretense for war in Libya? Tazama pia: The Wickedness of Foreign Policy-By Sheldon Richman.)
Robert Finlayson Cook (Robin Cook)
Mwenyekiti wa Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Kufuta ubaguzi (Committee on the Elimination of Racial Discrimination), Jose Francisco Cali Tzay
‘Hapa kazi tu’ isiwe kufunga MasheikhInatoka Uk. 9
Lakini zaidi, japo Blair ana j i tah id i kukwepa kusema wazi baadhi ya vitu, lakini ukweli wa mambo ni namna mbili:
Moja ni hili walilosema Jose Francisco Cali Tzay na Malcolm X kwamba ‘ m a b e b e r u ’ h u t u m i a visingizio ili kuhalalisha ubabe wao, unyonyaji na dhulma zao juu ya wengine. Itakumbukwa kuwa kat ika ukoloni mkongwe, wal i tumia Biblia, hata kuzipa meli za kubebea watumwa jina la Yesu kuhalalisha unyama wao na ukatili wao wa kukamata Waafrika na kwenda kuwatumikisha kitumwa kwao. (Tazama: The First British Slave Ship To Reach The Americas Was Called The Good Jesus!)
Katika zama hizi za ‘utawala wa ma- neo-conservatives (aka neo-cons au neocons)’, ambao ndio walipanga kuvamia Iraq na kusambaratishwa Somalia, Libya na sasa S y r i a , wa n a c h o t a k a mabeberu ni kitu kinaitwa ‘World Hegemony’. Na katika kulifanikisha hili, wamebuni mkakati wa kupambana na ugaidi. Mkakati huu wa kutumia ugaidi wa kupanga (false flag terror attacks, hoax, na frauds), wamejipa ukiranja na usamaria mwema wa kuwasaidia walimwengu kupambana na magaidi ( w a n a o w a u n d a w a o w e n y e w e ) . N a kwa k i s ing iz io h ik i , wanasambaza makucha yao ya kijeshi kila mahali kuikamata dunia. Na ndio maana unaona kila unapoingia ugaidi, hakuna namna ya kuuondoa. K i la mnavyosa id iwa kikachero, kipolisi, vifaa na ujuzi, ndivyo magaidi wanavyozidi kushamiri. Ndio tatizo linaloikumba Nigeria, Somalia na Kenya hivi sasa. Ufupi wa maneno n i k a m a a l i v y o wa h i kusema Robert Finlayson C o o k ( R o b i n C o o k ) , kwamba hao wanaodaiwa k u wa n i m a g a i d i n i ‘vijana watumishi’ wa m a b e b e r u . K a m a n i kupambana, mtakuwa mnapambana na hewa na kuumiza watu wenu bure na mwisho wa yote nchi inasambaratishwa.
Robin Cook anasema: “The truth is no Islamic army or any terrorist group by the name Al Qaida and any intell igence off icer knows about this. But there is a propaganda campaign to make the public believe in the presence of an identified entity
Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Blairrepresenting the “devil” only in order to drive the TV watchers to accept a unified international leadership for a war against terrorism. The country behind this propaganda is the USA.”
Na mahali pengine anasema tena: “The so called al-Qaida that we see are actually Kharjee along with Mossad, CIA and RAW led and trained mercenary gangs like TTP who pose as Islamic Jihadists and create justification for global information war and propaganda to launch a new war against another Muslim country.”
Leo kuna Masheikh na Waislamu wapo ndani w a k i t u h u m i w a k w a vi tendo vya k igaidi . Uki t i zama mlo longo
wa matukio ya kigaidi ulimwenguni na sera hizi za ma-neocons na yaliyokwishaelezwa na Robin Cook, utaona kuwa Masheikh na Waislamu hao ni wahanga tu wa mikakati hii ya mabeberu. Na tujue kuwa nchi hii kamwe haiwezi kusumbuliwa n a w a n a o d a i w a k u w a m a g a i d i , i l a wale waliobuniwa na kuandal iwa chini ya mpango huu wa ma-neocons.
K u l e N e w Y o r k wanafanya maandamano chini ya kibwagizo: ‘Say No to Racism’, "You Can't Have Capitalism Without Racism".
S a s a w a k a t i Mheshimiwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli akiapishwa kuwa Rais wa
Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Tanzania, lazima tuseme “Hapana kwa Usanii huu wa Ugaidi’. Usanii na ‘hoaxes’ ambazo zimesababisha watu wetu kuwekwa ndani kwa zaidi ya miaka miwili bila ya kesi zao kuzungumzwa na kutolewa uamuzi.
K a m a t u n a h i s i tuna ubavu, mahali pa kuelekeza ujasiri wetu ni kulikamata kambaku kwa mapembe yake . Kambaku ambalo tayari Robin Cook ashatutajia. Tuliambie hatutaki hizi ‘false flag terror attacks’ na ‘hoaxes’ za Al Shabaab, Boko Haram na Al Qaidah, sio kuwaumiza wananchi wetu.
Na la kufahamu hapa ni kuwa kama tutameza ndoano hii ya ‘ma-neocons’ na ubeberu wao, basi tutakuwa wabaya kuliko wale tunaowatuhumu na kuwashikilia kwa ugaidi. Kwanza ni kuwa sote, wenye mamlaka na wao tutakuwa tunatumiwa n a m t u m m o j a , k i l a mmoja kwa namna yake. Lakini pili, tufahau kuwa mwisho wa kutumiwa huko ni kiangamiza nchi. Ni kuwaletea tabu watu wetu. Tizama mauwaji yanayodaiwa ya kigaidi Somalia, Kenya na Nigeria. H a k u n a m wa n a n c h i mwenye salama.
L a k i n i t u j u e p i a kwamba, tofauti na Blair na Bush wakiomba msamaha hivi sasa juu ya Iraq, nchi zao zipo salama. Na kama ni agenda za ubeberu wao ushafanikiwa. Waliokula
hasara ni wananchi wa Iraq na hata viongozi wao waliotumiwa katika mkakati huo wakamuona Saddam ni adui yao au wale waliomuona Gaddafi ni adui badala ya kuungana k u z i k a b i l i n j a m a z a mabeberu na NATO yao. Sisi yakitukuta yanatukuta ndani ya Tanzania na kama ni kusambaratika, inasambaratika Tanzania.
Amesema Jose Francisco Cali Tzay akiwaambia m a b e b e r u m a b a g u z i kuwa:
“There is only one race around the world and that is the human race, so in theory there is no basis for racial discrimination.”
Pengine na sisi tuseme tukimwambia Rais wetu Dr Magufuli:
‘ T a n z a n i a k u n a watu namna moja tu: “Watanzania.”
Na ndio maana nchi hii imedumu katika amani na kuitwa kisiwa cha amani.
Hakuna gaidi wala msal i t i wa kutuletea magaidi ndani ya nchi yetu na hata akijaribu hawezi kufanikiwa.
K i l i c h o p o n i k i l e a l i c h o s e m a R o b e r t F i n l a y s o n C o o k . Propaganda na michezo i n a y o p a n d i k i z wa n a mabeberu ma-neocons. Sasa namna ya kukabiliana na michezo na ‘HOAX’ hizo, sio kuwakamata Masheikh na kuwatesa ‘Shimoni’ na ‘Guantanamo’.
Wakati “International Day for the Elimination of Racial Discrimination” ya mwaka huu inatupa ujumbe usemao:
“ L e a r n i n g f r o m historical tragedies to strengthen the global fight against racism.”
Basi kwetu iwe kusoma kutoka yanayowakuta Nigeria katika kupambana na Boko Haram na kiroja cha “Bring Back Our Girls” tukiwianisha na yale anayotuambia Robin Cook kwamba tunafanyiwa mchezo wa kuigiza katika hii vita dhidi ya ugaidi.
Tujue kuwa salama ya nchi hii ipo katika kutambua michezo hii na kujua namna ya kucheza nayo bila ya kuwadhuru watu wetu na nchi yetu.
Kama ni “hapa kazi tu”, basi ionekane pia katika eneo hili.
Isijekuwa “hapa kazi tu”, kufanyia kazi mikakati na njama za mabeberu.ENZI za utumwa Marekani.
Makala tatu mfululizo zitaangaza Misikiti na fadhila zake. Aidha Misikiti katika Mji Mkongwe wa Zanzibar.
Fadhila za MsikitiM s i k i t i n i n y u m b a
tukufu na n i mwahal i Muislamu anatakiwa kila siku awe anafika kwenye Msikiti kukamilisha sala 5. Msikiti ni sehemu ambayo huwakusanya Waislamu katika kufanikisha mambo yao yote ya akhera na ya k i l i m we n g u . A i d h a n i sehemu ambayo Mtume (SAW) akiweka mikutano ya Waislamu na sehemu kuu ya Waislamu kupanga mipango yao yote. Hivi sasa tunaelezwa kuwa Misikiti ni sehemu ya kusali na sio zaidi ya hayo na kuwapelekea Waislamu kuingia katika mtego huo wa kuhakikisha kuwa zaidi ya kusali kwenye Misikiti kinachoongezwa ni kusomeshwa darsa na hio darsa nayo kufikia baadhi ya waumini katika Misikiti yao kufanya mchujo wa walimu gani ndio wanayostahiki kusomesha darsa katika Msikiti yao, bila ya kuangalia kigezo na uwezo wa mwalimu ambaye wanamteua.
Ndani ya Misikiti kwa sasa kuna siasa za aina yake ambapo inawasukuma uongozi wa Misikiti kuratibu mambo sio katika misingi tunayotakiwa. Maana ya Msikiti
Nini maana ya Msikiti? Kilugha Msikiti ni kila sehemu inayosujudiwa. Kwa upande wa sheria Msikiti ni sehemu yoyote ya ardhi iliyokusudiwa na mwenyewe kwa ajili ya kuwa Msikiti (kusaliwa) pamoja na kuiweka wakfu sehemu hiyo. Yaani ili sehemu ya ardhi iitwe Msikiti na kuchukuwa hukumu za Msikiti, basi ni lazima mmiliki wa ardhi hiyo atamke kuwa sehemu hiyo ni wakfu kwa ajili ya Msikti na lengo ni kuweza kuutumia kila muumini kwa kusali na kuweza kusaliwa sala za Jamaa. Wajanja wengi hunyakua ardhi za watu kwa kisingizio cha ujenzi wa Msikiti kisha Misikiti hio ikawekwa maduka na wao kufaidika.
Zimekuja hadi th i za Mtume zinazotufahamisha k u wa k i l a s e h e m u ya ardhi inafaa kuwa Msikiti. Imepokelewa na Sahaba Jabir (RA) kuwa, amesema Mtume (SAW) " Imejaaliwa sehemu ya ardhi ni Msikiti kwangu (na kwa umma wangu), na kuwa ni safi."
Eneo lolote lile la ardhi inaweza ikawa ni Msikiti. Muislamu akasali, mfano
Misikiti katika Mji Mkongwe wa Zanzibar (1)
MSIKITI wa Makkah.
MSIKITI wa Madinah
MSIKITI wa Aqsa.Muislamu akiwa safirini na akataka kusali, anaweza akasali popote pale, muhimu pawe ni pasafi kutokana na najisi. Ama katika baadhi ya umma zilizotangulia, wao walikuwa hawawezi k u t e k e l e z a i b a d a z a o isipokuwa wakiwepo katika sehemu maalumu.
Mafunzo yanayopatikana katika hadithi hii nikuwa Muislamu hatakiwi kuacha sala kwa hali yoyote ile, wala
hana kisingizio kwa kusema hana maji ya kujitoharisha au hawezi kusali mpaka afike Msikitini. Hata hivyo, nafasi ya Msikiti itabakia kuwepo na ni bora kwa anayeweza kufika Msikitini akafanya ibada zake humo kuliko kusali popote tu, na bila ya shaka atakayekuwa na ufahamu huu wa kukataa kwenda Msik i t in i bas i atakuwa amekosea.
Msikiti upi ulijengwa
mwanzo duniani? Msiki t i wa mwanzo
kujengwa duniani ni Msikiti wa Makka (Al-Qaba) kama a l i v y o s e m a M we n ye z i Mungu katika Qran: "Hakika Msikiti wa kwanza kuwekwa kwa watu (duniani ) ni Msikiti wa Makka " (Al-Imran 3: 96).
Imepokewa hadithi kutoka kwa Sahaba Abi Dharri radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake amesema: "Nilimuuliza Mtume (S.A.W) ni Msikiti gani wa mwanzo uliojengwa duniani? Akanijibu ni Msikiti wa Makka, nikamuuliza kisha upi, akasema kisha ukajengwa Msikiti wa Al-Aqsa. (Bukhari na Muslim.)
Msikiti wa Makka (Al-Qaba tukufu) ndio Msikiti wa mwanzo kujengwa duniani, na aliyeujenga Msikiti huo ni Nabii Ibrahim rehema na amani juu yake, kisha ukajengwa Msikiti wa Al-Aqsa na mjukuu wake Nabii Yaakub bin Is-haq bin Ibrahim, ama Nabii Suleiman yeye hakuujenga kwa maana ya kuasisi bali yeye aliufanyia matengenezo upya Msikiti wa Al-Aqsa. Fadhila za kujenga Msikiti
Kuna fadhila kubwa kwa mwenye kujenga Msikiti. Kuna mapokezi mengi yamepokewa kutoka kwa Mtume (SAW) kuelezea fadhila za mwenye kujenga Msikiti, na muhimu kati ya hadithi hizo ni ile iliyopokewa kutoka kwa Sahaba Syd Uthman bin Affan (RA). Imepokewa kuwa wakati Sahaba Uthman alipotaka kuutanua Msikiti wa Mtume (SAW) baadhi ya watu walikataa kuungana nae juu ya fikra hii na kutaka Msikiti wa Mtume uwachwe kama ulivyokuwa, akawajibu kuwa "Nimemsikia Mtume (saw) akisema mwenye kujenga Msikiti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu basi Mwenyezi Mungu atamjengea mtu huyo nyumba peponi ." (Bukhari na Muslim). Aidha imepokewa kutoka kwa Sahaba Uthman kuwa amemsikia Mtume (SAW) akisema "Mwenye kujenga Msikiti, Mwenyezi Mungu atamjengea mtu huyo nyumba peponi mfano wake, yaani ya Msikiti alioujenga.” Hapa tunatakiwa tukiwa na uwezo tujitahidi kujenga Misikiti wala sio kujenga Misikiti kwa ushindani mfano pao kwa papo. Ni dhahiri Allah katuahidi kuwa utapojenga Msikiti jazaa yako ni kwenda Peponi, lakini tujuwe nazo fedha za kujengea Misikiti zinatakiwa ziwe safi, kiwanja sio cha ghilba na ujenzi uwe wa dhati kwa mwenye kutaka kuujenga. Mtume (SAW) hakuwahimza watu wajenge Misikiti tu, bali yeye ndiye wa mwanzo kuonyesha mfano katika suala hili, na haya tunayapata pale Mtume (S.A.W) alipowasili Madina kwa mara ya kwanza kutoka Makka (Hijra) alipofika tu
jambo la kwanza aliamrisha ujengwe Msikiti, nae akawa ni mmoja kati ya hao wajenzi alikuwa akibeba matofali kama waumini wengine.
Pia tunatakiwa tuimarishe Misikiti kwa ibada mbali mbali, kwani Mtume (SAW) amesema kuwa "Watu wa aina saba watapata kivuli siku ya kiama siku isiyokuwa na kivuli isipokuwa hicho, na mmoja kati ya hao saba ni mtu ambaye moyo wake umeshikamana na Misikiti”, ikimaanisha anautukuza Msikiti na kufanya ibada kwa wingi zikiwemo Sala, Itikafu na mengineyo kama kusoma Qur’an.
Na amesema Mtume (SAW) "Sehemu iliyobora mbele ya Mwenyezi Mungu ni Mis ik i t i na sehemu zinazomchukiza Mwenyezi Mungu ni Masoko" (Muslim). Kwenye masoko hakuna utulivu na kwenye masoko k u n a m a b a l a a m e n g i yanatokea jaribu kuchunguza mwenyewe.Misikiti iliyobora zaidi
Baada ya kufahamu nafasi na utukufu wa Misikiti hapa duniani na kwamba ni nyumba tukufu kuliko nyumba nyengine pia hiyo Misikiti imetofautiana kwa utukufu kuna mingine ina fadhila zaidi ikiwa ni Misikiti mitatu, wa kwanza ni Msikiti wa Makka kisha Msikiti wa Mtume (SAW) Madina, kisha Msikiti wa Kudsi. Mja hutakiwa kufanya ziara zaidi ya Misikiti hio mitatu, na kwa sasa hapa Tanzania kuna kikundi kinakwenda Umra na kuunganisha na Msikiti wa Al-Aqsa na kuna kikundi Zanzibar nacho kimepanga kwenye mfungo Sita kufanya Umra na kwenda Al-Aqsa. Tumuombe Allah atujaalie na sisi kupata fursa hio. Ameen, jambo kubwa ni kutia nia.
"Mtume (SAWA) amesema sala moja katika Msikiti wangu wa (Madina ) ni bora kuliko Msikiti mwengine kwa mara elfu isipokuwa Msikiti wa Makka " Imamu (Bukhari na Muslim.) Sala moja katika Msikiti wa Makka ni bora kuliko sala laki moja katika Msikiti mwengine na sala moja katika Msikiti wa Mtume (S.A.W) ni bora kuliko sala elfu moja katika Msikiti mwengine na sala moja katika Msikiti wa Al-Aqsa ni bora kuliko sala mia tano katika msikiti mwengine.
Ama Misikiti isiyokuwa hiyo miatu basi yote ni sawa katika fadhila za sala wala hakuna ulio bora kuliko mwengine kwa dhati ya Msikiti .
( M a k a l a i f w a t a y o itaangalia Mji Mkongwe wa Zanzibar na Misikiti iliyomo katika sehemu hii.)
12 AN-NUURMUHARRAM 1437, IJUMAA NOVEMBA 6 - 12, 201512 MAKALA
Kwa habari mbalimbali zinazohusu matukio n a h a r a k a t i z a kupigania Uhuru wa Tanganyika, picha za matukio, Waislamu na harakati za Uhuru, watu mashuhuri walioshiriki katika harakati hizo kabla na baada ya Uhuru tembelea Blog ya Mwanahistoria, Sheikh Mohammed Sa lum Said: - http: / /www.mohammedsaid.com
WAKATI hali ya visiwa vya Zanzibar ikiwa katika mashaka, baadhi ya wananchi wameonyesha kusikitishwa na kitendo cha serikali ya Jamhuri ya Muungano kumimina askari wa JWTZ katika M a k a z i ya r a i a n a kuwaweka roho juu.
“Hali hii inatuvunja moyo sana wananchi wa Zanzibar, kweli nchi hii inaendeshwa kwa misingi ya kisheria au kiubabe ? Mbona kule Tanganyika Kikwete hakuyafanya haya ya kuliingiza Jeshi katika makazi ya raia na kuwafanya raia wa Zanzibar kuishi kwa hofu.”
Baadhi ya wananchi wa Zanzibar walihoji kuwa Je, kumwagwa majeshi na zana zao visiwani humo, ndio kul inda amani au kuwanyima Wa z a n z i b a r u h u r u wao wa kidemokrasia w a k u c h a g u a m t u wanayemtaka wenyewe?
Kwa jinsi hali ilivyo kwa sasa, wananchi wengi wa Zanzibar wameonekana k u m l a u m u R a i s wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kutapakaa vikosi hivyo vya JWTZ katika mitaa ya Z a n z i b a r , j a m b o ambalo limezua hofu kwa Wazanzibar katika kipindi hiki ambacho Tume ya Uchaguzi imefuta Uchaguzi Mkuu visiwani humo.
K w a m b a k i n a c h o t a f s i r i wa n a Wazanzibar kwa kitendo hiki cha kusambazwa askari wa Jeshi la Wananchi visiwani humo wakati Wazanzibar wametulia tuli, ni ubabe na dharau kwa Zanzibar kunatokana na nafasi yake ya Amiri Jeshi Mkuu huku bara ikiwa haiathiriki kitu.
Kufuatia hali hiyo, w e n g i w a m e h o j i k w a m b a k w a n i n i serikali ilikubali mfumo wa vyama vingi, lakini watawala wakishindwa wanakakataa kuondoka n a k u z u a k i l e kinachotafsiriwa sasa kama kupindua kijeshi.
Imeelezwa kwamba kinachofanyika Zanzibar hivi sasa, kwa kuwepo majeshi mitaani na uraiani hali ya kuwa wananchi wa Zanzibar wametulia, ni kama kupindua nchi kijeshi.
“Inshallah Mwenyezi Mumgu ampige laana huyo anayepanga na kutuharibia uchaguzi na
Jeshi sio ufumbuzi wa mgogoro ZanzibarNa Makame Silima
ASKARI wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakishiriki kupiga watu Zanzibar kufuatia kumalizika kwa uchaguzi Mkuu visiwani humo na kufutwa na Tume ya Uchaguzi (ZEC).kutukosesha haki yetu na kukandamiza raia kwa kutumia cheo chake vibaya.”
“Yaarabii tufungulie kheri na uwangamize m a d h a l i m u n a wanaotucheza shere, na uikwamishe mipango yao miovu ki la pale wanapokaa wakipanga”. Alisikika akilalama mkazi mmoja wa Zanzibar.
Tayar i Chama cha W a n a n c h i ( C U F ) kimesema kuwa ufumbuzi wa mgogoro wa Zanzibar hauwezi kupatikana kwa kutumia nguvu au vitisho vya kuingiza vifaru na magari ya maji ya kuwasha kama inavyofanyika sasa, bali kinachotakiwa ni kukaa katika meza ya majadiliano.
Tamko hilo limetolewa na mgombea urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati a k i z u n g u m z a n a waandishi wa habari mjini hapa.
M g o m b e a h u y o aliwataka wafuasi wa CUF na wananchi kuendelea kuwa na subira wakati viongozi wao wakiwa katika jitihada za kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo (kidhati? Au usanii?)
A l i s e m a m g o g o r o uliojitokeza Zanzibar ni mgogoro wa kisiasa baada ya haki ya kidemokrasia ya wananchi kupindishwa, n d i o m a a n a C U F inamtaka Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC) afute uamuzi wake, amalizie kazi iliyobakia ya kuhakiki matokeo na kutangaza mshindi.
“Tatizo lililopo ni la kisiasa na ufumbuzi wake si vifaru wala kuongeza ulinzi, linahitaji njia ya mazungumzo kumalizika kwake,” alisema.
Aidha, Maalim Seif aliwataka wanachama kuendelea na utulivu kutokana na juhudi zinazofanywa na Jumuiya za Kimataifa kuonesha mwelekeo wa kupatikana ufumbuzi wa mgogoro wa uchaguzi wa Zanzibar.
A l i s e m a C U F i n a imani kwamba ufumbuzi wa haki wa suala hilo hauko mbali (hata kwa kupatikana mwafaka mwingine wa Anyauko!!!) na Wazanzibari wataona mafanikio ya demokrasia yatakayojengwa nchini. Alisema haki lazima i tendeke (hata kama haitaonekana kutendeka) katika uchaguzi uliopita.
“Sisi tumepata moyo na imani kwamba ufumbuzi wa haki wa suala hili h a u k o m b a l i ( h a t a ikibidi kusubiri uchaguzi mwingine 2020!!! Si mbali) na Wazanzibari wataona mafanikio ya demokrasia yetu tunayoijenga katika nchi yetu,” alisisitiza Maalim Seif.
A l i w a o m b a Wa z a n z i b a r i w o t e wanaopenda amani wawe waangalifu sana na taarifa za uongo zinazotolewa za kuchochea kufanya vurugu kwa kisingizio kuwa zimetolewa na viongozi wa CUF wakati ni uongo.
“Nitumie fursa hi i k u w a s h u k u r u w a l e wote wanaofanya juhudi kubwa kuona ufumbuzi wa haki na wa amani unapatikana kwa tatizo hili lililosababishwa na mtu mmoja, aliyeamua kuacha waj ibu wake na kutumikia maagizo ya kikundi cha watu wabinafsi”, alisema.
Aidha, alisema Rais wa Jamhuri ya Muungano Jakaya Kikwete na Rais
wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, bado wana nafasi kubwa ya kuhakikisha wanaivusha Zanzibar kwa kumaliza mgogoro wa uchaguzi uliojitokeza kwa amani na utulivu.
“Kwa mara nyingine tena natoa wito kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais Dk. Shein kuchukua dhamana ya uongozi na kwa pamoja tushirikiane kuikwamua Zanzibar na Tanzania katika mkwamo huu”, alisema.
K u h u s u v y o m b o vya ulinzi na usalama v i l i v y o j a a v i s i wa n i Z a n z i b a r k wa s a s a , Maal im Sei f a l isema vina wajibu mkubwa wa kusaidia kupatikana ufumbuzi wa tatizo walilo nalo badala ya kuongeza wasiwasi kwa wananchi waliotulia.
Akizungumzia kuhusu uamuzi wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Jecha Salim Jecha, kufuta matokeo ya
uchaguzi wa Zanzibar, alisema kuwa wamepata taarifa kuwa Mwenyekiti huyo ameitisha kikao cha Tume na kuwataka Makamishna kuunga mkono uamuzi wake huo alioutangaza pekee wa kufuta matokeo ya uchaguzi.
A l i s e m a k u w a n i vyema Mwenyekiti huyo akatambua kwamba, hata akiwatumia baadhi ya Makamishna kumuunga mkono, bado uamuzi huo hautakuwa halali kwa sababu haumo katika uwezo uliopewa Tume; si katiba wala sheria ya uchaguzi.
“Kwa ufupi suala hili halina njia nyingine ya kulimaliza zaidi ya kukamil isha kazi ya kufanya majumuisho, kuhakiki matokeo na kumtangaza mshindi wa uchaguzi”, alisema Maalim Seif.
M a a l i m S e i f aliwahakikishia viongozi na wanachama wa CCM kwamba hawana sababu ya kuwa na hofu na maamuzi ya Wazanzibari waliyoyafanya Oktoba 2 5 m w a k a h u u n a kwamba, kama kuna tofauti zozote za kisera na kimtazamo baina yao zinaweza kuzungumzwa na maelewano kufikiwa.
“ N a w a h a k i k i s h i a viongozi na wanachama wa CCM na Wazanzibari wote kwamba hakutakuwa na ulipizaji kisasi au kufukua makaburi kwa mambo yaliyopita, sote tutafanya kazi pamoja bila ya kujali tofauti za itikadi za kisiasa, asili, kabila au dini zetu, Zanzibar ni moja na itabaki kuwa moja,” alisisitiza Maalim Seif.
Kuhoji yanilazimu, wanelimishe wajuzi,Pamwe na wataalamu, wa mambo ya uchaguzi,Makani yanapokimu, mawili haya kwa wazi,Haki, uhuru vi wapi, katika zetu chaguzi?
Nina kubwa sana hamu, ya wake upambanuzi,Toka kwa wanofahamu, mambo haya kwa ujuzi,Wanijaze mafuhumu, nipate kuyamaizi,Haki, uhuru vi wapi, katika zetu chaguzi?
Kwa wa kwao ufahamu, pamoja na upembuzi,Wa mambo haya kawimu, mintarafu uchaguzi,Wanidhukuru sehemu, yadhihiripo kwa wazi,Haki, uhuru vi wapi, katika zetu chaguzi?
Wasikika 'kituhumu, si jana wala si juzi,Mambo haya mahashumu, wananchi waziwazi,I ombwe yake hatamu, katika zetu chaguzi,Haki, uhuru vi wapi, katika zetu chaguzi?
Kadhalika walaumu, ya tume ya uchaguzi,Mazonge ya kuhujumu, uhuru wa uchaguzi,Pamwe haki kudhulumu, yao katika chaguzi,Haki, uhuru vi wapi, katika zetu chaguzi?
Kaditamati nudhumu, nawahimiza wajuzi,Tena na wataalamu, wa mambo ya uchaguzi,Kwa wao utaalamu, watupe ufafanuzi,Katika zetu chaguzi, haki, uhuru vi wapi?
ABUU NYAMKOMOGI-MWANZA.
MAZONGE YA UCHAGUZIMazonge ya uchaguzi, Zenji tuloshuhudiya,Mazonge ya uchaguzi, si ya kimya kukaliya,Mazonge ya uchaguzi, kwa walo na njema niya, Mazonge ya uchaguzi, wapaswa kuyakemeya,Kwa kila alohusika, vikali awajibishwe.Mazonge ya uchaguzi, khasara yametutiya,Mazonge ya uchaguzi, tumeyo iso huriya,Mazonge ya uchaguzi, hoja izotunadiya,Mazonge ya uchaguzi, si hoja bali udhiya,Kwa kila alohusika, vikali awajibishwe.Mazonge ya uchaguzi, khasara yametutiya,Mazonge ya uchaguzi, wale wanoyateteya,Mazonge ya uchaguzi, si kunga nawashakiya,Mazonge ya uchaguzi, mui wamedhamiriya, Kwa kila alohusika, vikali awajibishwe.Mazonge ya uchaguzi, khasara yametutiya,Mazonge ya uchaguzi, mafukara tunaliya,Mazonge ya uchaguzi, gharama kuteketeya,Mazonge ya uchaguzi, nani wa kuzifidiya?Kwa kila alohusika, vikali awajibishwe.Mazonge ya uchaguzi, khasara yametutiya,Mazonge ya uchaguzi, si ya kuyapuuziya,Mazonge ya uchaguzi, si ya kuyanyamaziya,Mazonge ya uchaguzi, si ya kuyavumiliya,Kwa kila alohusika, vikali awajibishwe.Mazonge ya uchaguzi, khasara yametutiya,Mazonge ya uchaguzi si ya watu kuteteya,Mazonge ya uchaguzi, si ya watu kuchekeya,Mazonge ya uchaguzi, si ya watu kucheleya,Hatua twazingojeya, kwa kila alohusika.ABUU NYAMKOMOGI-MWANZA.
HAKI, UHURU VI WAPI?
KAMA tulivyoona katika s e h e m u ya k wa n z a , kuna watoto wa ahadi wawil i , a l ioahidiwa Nabii Ibrahimu, mwanae anayetoka katika viuno vya Ibrahimu, ni mmoja, na wa pili alitokana na Amri ya Mwenyezi Mwenyezi Mungu. Katika watoto hao wawili, huyo wa pili ndiye ambaye baadhi ya watoto wake walipata ile baraka ‘kama ni baraka!’ ya kwenda ugenini, na utumwani kwa miaka 400, ‘kama tutaiita baraka-au laana.’ Na hao ndio kizazi cha Yakobo au Israeli. Sasa kwa mujibu wa Biblia, Isaka alikuwa na mkewe akiitwa Rebeka binti Labani. Mama huyo, kwa mujibu wa Biblia, alikaa muda mrefu, hakupata mtoto. Ikaaminika kuwa ni tasa; na alipopata m i m b a , i k a m t i a msukosuko tumboni m p a k a a k a m w o m b a M w e n y e z i M u n g u : Hapo ndipo tunaanza kumfahamu Israeli na ‘Israiliyati’; na vitimbi vyao.
“ I s a k a a k a m w o m b a BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba. Watoto wakashindana tumboni mwake . Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda k u m w u l i z a B WA N A . BWANA akamwambia , Matai fa mawil i yamo tumboni mwako, Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili, Na mkubwa atamtumikia mdogo.” (Mw. 25:23.)
Kama hizo tutazitizama kuwa ni Baraka au ni laana itategemea uelewa wa Neno la Maungu wa ‘Israeli’. ‘Israiliyati’ hizo ndizo zinazo tumika kudhulumu wana damu katika mataifa, kama tutakavyoona badae.
M o j a y a m a m b o yaliyojenga msingi wa kujitukuza, kibubusa na kuwajengea waumini uvivu wa kufikiri hadi wakati huu wa taaluma mbalimbali za elimu ya viumbe na uumbaji, na ufafanuzi wake; bado kila kitu waumini ni ‘amina’. Mambo yaliyotokea siku ya kuzaliwa Yakobo na kaka yake Esau, ni haya:
“Siku zake za kuzaa zilipotimia! tazama! mapacha walikuwamo tumboni mwake. Wa kwanza akatoka, naye alikuwa mwekundu mwili wote kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau. Baadaye ndugu yake akatoka,
Khabari ya Israel ‘Taifa teule’-2Na Khatibu J. Mziray na mkono wake umemshika
Esau kisigino. Akaitwa jina lake Yakobo.” (Mw 25:24-26.)
K w a i m a n i y a mafundisho ya Ukristo, ni kuwa, ishara hiyo ya Yakobo kumshika Esau kisigino, ni kuashiria kuwa yeye ndiye angepaswa kuwa mzaliwa wa kwanza, yaani awe ndiye kaka yake Esau badala ya kuwa mdogo wake. Na ndivyo vile vita vilivyokuwa vikipiganwa tumboni mama yao alipokuwa mja- mzito. Lakini hapo juu aya zinatwambia kuwa, Esau alizaliwa, na ni ‘mwekundu mwili wote’ na- akapewa jina la ‘Esau’ na zile ‘Israiliyati’ hazikukosa mchango wake humo.
Kwa sis i Waislamu na hata Wakristo wenye imani kikweli, wanaamini kuwa Manabii, Mitume, w a m e e p u s h w a n a mambo ya hila, ghilba, u t o v u wa n i d h a m u , bali ni wanyeyekevu, wapole wenye huruma, watiifu, waadilifu, n.k. Pia watoto wanaozaliwa m a p a c h a , k wa k i a s i wanavyopendana na kuhurumiana, inatokea mmoja akaugua hata na mwenzake anajisikia kuugua. Lakini sivyo Biblia inavyo tufundisha, hasa kwa kigezo cha manabii hawa wawili, yaani Yakobo na Esau nduguye:-
K w a m u j i b u w a Biblia, Isaka na mkewe w a l i g a w a n y i k a k i upendo kwa watoto wao, kila mmoja alimpenda w a k w a k e . A n d i k o linalotufundisha hivyo, l i n a t u o n g o z a k a t i k a maadili yenye manufaa gani kama si kutujengea maadili ya uhasama katika kizazi chetu, na ndiyo maana kizazi cha wana wa Israeli hakiambiliki, kumbe ni hizo ‘Israiliyati’ zilizopandikizwa ndani ya Neno la Mwenyezi Mungu.
“Basi Isaka akampenda Esau, kwa sababu alikula mawindo yake, na Rebeka akampenda Yakobo. Yakobo akapika chakula cha dengu. Esau akaja kutoka nyikani, naye alikuwa amechoka sana. Esau akamwambia Yakobo, Tafadhali, unipe hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo walimwita jina lake Edomu. Yakobo akamwambia, Kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza. Esau akasema, Tazama, mimi ni karibu kufa, inanifaa nini haki hii uzazi? Yakobo akamwambia, Uniapie kwanza. Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa
wa kwanza. Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.” (Mw 25:28-34).
Utukufu wa Yakoo, na wana wa I s rae l i , unaoelezewa na kusifiwa katika Biblia, umejengwa hivyo. Je, kwa somo hilo tunajifunza nini na nini cha kuiga ili tuwe mfano wa Isaka na Yakobo na kweli Mwenyezi Mungu a l i k u b a l i k u m f a n ya Yakobo kuwa mkubwa, yaani mzaliwa wa kwanza k w a k u b a d i l i s h a n a ukubwa na chakula?
Lakini Biblia inasema: “Na i k iwa nduu yako amekuwa masikini, na mkono wake umelegea kwako, ndipo utamsaidia, atakaa nawe kama mgeni, na msafiri. Usitake riba kwake wala faida, bali mche Mungu wako, ili ndugu yako akae nawe. Usimpe fedha yako upate riba, wala usimpe vyakula vyako kwa kujitakia faida. Mimi ndimi BWANA, Mungu wako,…” (Walawi 25:35-38.)
Tunachojifunza hapo ni kuwa Isaka na mkewe R e b e k a wa l i wa g a wa watoto wao makundi mawili yaliyohasimiana; kiasi kwamba inaonekana kuwa, Rebeka alikuwa hamwogopi Mwenyezi M w e n y e z i M u n g u , jambo l i l i lomwathir i Yakobo mwanawe (kwa mujibu wa Biblia). Na mibaraka hiyo kama wao wanavyoamini, ndiyo hii inaendelea kusifiwa, hata pale wana wa Israeli wanapo fanya unyama wa kishetani wafuasi wao tena viongozi wa dini badala ya kusikitika wanafurahia, badala ya kuona kuwa hizo ni laana.
Tunaambiwa kuwa Isaka alipokuwa mzee, na macho yakawa hayaoni, alimwagiza Esau kuwa amtafutie chakula kizuri ili ampe Baraka za mwisho, kulingana na alivyojihisi umri wake. Lakini wakati Isaka anamwagiza Esau, Rebeka mkewe alikuwa akisikia. Kutokana na mgawanyiko wa mapenzi kwa watoto wao, Rebeka alitaka Baraka zile ziende kwa Yakobo badala ya Isaka; hivyo akafanya hila. Msomaji, usidhani kuwa nafundisha Biblia, la, bali nataka wasomaji watumie akili zao kupima huo utukufu wa wana wa Israeli, na huyo mungu wa Israeli; na huo uadilifu wa Mungu wa Israeli kama andiko linavyosema:
“Ikawa Isaka alipokuwa m z e e , n a m a c h o ya k e yamepofuka asione, akamwita Esau mwanawe mkubwa,
Inaendelea Uk. 17
1.MAMA MLEZI (MATRON) BWENI LA WASICHANA,UMRI KUANZIA MIAKA 40.
2.MLEZI BWENI LA WAVULANA (WARDEN),UMRI KUANZIA MIAKA 40.
3.FUNDI UMEME, UJENZI NA SEREMALA, WENYE UJUZI NA UZOEFU
Pambana na ujinga kuwasomesha watoto wako katika shule za WEC -Kibaha kuanzia Nursery,Msingi, Sekondari na ualimu. Bweni na kutwa. Simu 0715959522/0786959522
1 HAFSWA ALLY NGAMBA KE2 JUMA ISSA MZEE ME3 MUUNGUJA IBRAHIM MURAD KE4 NASSOR HAMISI HEMED ME5. SAIDA JUMA MAJENGO KE
S/N JINA KAMILI JINSIA1 ZULFA RAMADHANI KE2 REHEMA HAMIS SAIDI KE3 BAYHAQIYYU MWAYA ME4 HAWA RAMADHANI KE5 ASHURA IDD RAMADHANI KE6 REHEMA MOZES HENJELWALE KE7 ASHURA MKOMA AMASI KE8 MWANAHARUSI HASSAN KE9 MARIAM RASHID ABDALLAH KE10 YUSUF OMARY MASOUD ME
WALIOFANYA MTIHANI KITUO CHA NYASAKA NA KUCHAGULIWA KITUO CHA KIRINJIKO 11 MWAJUMA MWINYI KONDO KE
12 TAMIMA M. MWAZBANI KE13 ZAINAB J. SWED KE14 RASHID HUSSEIN RAMADHANI ME15 NURU ALLY SHILLINGI KE16 JAMILA ALI RAJABU KE17 ZENA ABDALLAH RAMADHANI KE18 AISHA RAMADHANI MUSSA KE19 ZAMZAM SHAIBU ALLY KE20 SAUDA HASSAN SAIDY KE21 MWANAHARUSI MWINSHEHE KE22 ISSA RASHIDI NIPARA ME
MAELEKEZO MUHIMU.1.AMBAO HAWAONI MAJINA KATIKA SHULE WALIYOOMBA WAANGALIE KATIKA ORODHA YA SHULE NYINGINE. 2.WALIOCHGALIWA WAFUATILIE BARUA ZAO KATIKA VITUO WALIPOFANYIA MTIHANI.3.AMBAO HAWAKUCHAGULIWA WAJIANDAE KUFANYA MTIHANI KWA MARA YA PILITAREHE 28/11/2015 KATIKA VITUO WALIPOFANYIA MTIHANI WA KWANZA (BILA MALIPO)
4. KWA MAELEZO ZAIDI PIGA SIMU KWA MKURUGENZI WA ELIMU NA.0654613086AU KWA WAKUU WA SHULE KAMA IFUATAVYO:-AMBASHA ISLAMIC HIGH SCHOOL:0679 449668/0772916933 -KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL:0784 296424 -NYASAKA ISLAMIC SECONDARY SCHOOL 0786 417685 - MKUZO ISLAMIC HIGH SCHOOL0654876317 -UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOOL.0687820895 KWA KOZI FUPI: MAELEKEZO MUHIMU.WALIOCHAGULIWA WAFUATILIE BARUA KUJIUNGA KUANZIA IJUMAA IJAYO.
Changamoto kwa Shein Kikwete na Dr MagufuliInatoka Uk. 20ni kufuata Katiba, hivi sasa Zanzibar haina Rais halali na itakuwa pia haina Baraza la Wawakilishi hali itakayozidisha zaidi mgogoro wa kikatiba.
F a t m a K a r u m e , a l i s i k i t i k i a h a l i iliyotamalaki Zanzibar ya kusambazwa wanajeshi na vifaa vizito vizito vya kijeshi hali inayotisha w a n a n c h i n a h i v y o kukwaza shughuli za kiuchumi na maisha ya kawaida.
Lakini akasema pia hiyo inakuwa ni kana kwamba wananchi wa Zanzibar w a n a a d h i b i w a k w a kutekeleza haki yao ya kupiga kura na kuchagua viongozi wanaowataka.
Lakini pia akasema, a n a s h a n g a z w a n a ‘uhuni’ wanaofanyiwa Wazanzibari, kwamba japo walipiga kura tano, lakini z inazoonekana kuwa ni chafu, ni za Rais wa Zanzibar na Wawakilishi/Madiwani pekee, ila za Rais wa Tanzania/Wabunge safi, wakati mpiga kura ni huyo huyo, kituo ni hicho hicho na msimamizi ni huyo huyo.
Lakizi kubwa zaidi, kura zilishahesabiwa na matokeo kukubaliwa na mawakala wa wagombea (vyama) halikadhalika kusainiwa na msimamizi wa uchaguzi (ZEC) na fomu za matokeo kubandikwa katika vituo husika kama sheria inavyotaka.
Akasema, kwa maana nyingine ni kuwa ZEC inafuta uchaguzi baada ya kuendesha upigaji kura na kutoa matokeo na kuyakubali kwa kusaini kuwa ni halali.
Katika ujumla wake, wanasiasa hao wanasema kuwa, kwanza Wazanzibari wameporwa haki yao kinyume cha katiba na sheria na kwa kufanywa hivyo, nchi imeingizwa katika mgogoro mkubwa wa kikatiba, japo watawala wanafanya kiini macho wakidanganya umma kwamba kilichofanyika ni ‘halali’ na wao kuendelea kuwepo madarakani ni halali pia.
Mwanasheria Awadh katika kulitizama suala hili amekwenda mbali zaidi akisema kuwa anachoona h a ya n i m a t o k e o ya ukaidi wa kung’ang’ania muungano wa serikali mbili.
Akifafanua akasema, Rais wa Zanzibar ni mjumbe katika Baraza la Mawaziri la Tanzania.
S a s a m a a d h a l i anayeingia madarakani
DKT. Ali Mohamed Shein
ni Rais kutoka CCM, pengine inakuwa vigumu k wa C C M k u k u b a l i Maalim Seif, kama Rais wa Zanzibar (CUF) kuingia katika Kebineti ya serikali ya CCM ya Jamuri ya Muungano.
Na kwamba kinyume chake inakuwa hivyo hivyo.
K a m a C H A D E M A ndio ingeshinda urais wa muungano, huenda nao wangesita kuruhusu Dr. Shein kutoka CCM kuingia katika kebineti yao.
Hii ni mara ya pili kwa Mwanasheria Fatma Amani Abeid Karume kuzungumzia mgogoro huu wa uchagzu mkuu Zanzibar ambapo wiki iliyopita alihojiwa na DW na kuwatupia lawama wakuuu wa vyombo v y a u s a l a m a k u w a ndio waliopora haki ya Wazanzibari.
Katika mahojiano hayo alisema kuwa, kisheria, Jecha hana mamlaka ya kufuta uchaguzi wowote wa Zanzibar kwa sababu Uchaguzi ni haki ya watu wa Zanzibar na hakuna mtu anaweza kufuta haki yao hiyo.
“(Jecha) Kasema tu yeye kwamba kafuta. Ikiwa huna mamlaka, utafuta v ip i uchaguzi? Yeye
kajitamkia (tu) anavyotaka yeye.”
“Sote tumepiga kura. Kura zetu zipo na hakuna mtu anaweza kuifuta hiyo.”
A l i s e m a F a t m a n a kueleza kuwa kabla ya Jecha kutangaza kufuta uchaguzi, jeshi la Tanzania, TPDF (JWTZ), walizingira ‘ Tu m e ya U c h a g u z i Zanzibar’.
“Tuseme ukweli sio Jecha, kwa sababu Jecha hana jeshi. Jecha hana P o l i s i . Wa z a n z i b a r i tumenyimwa haki yetu si na Jecha.”
“Tumenyimwa haki yetu na wale watu waliotuma Jeshi pale na kutuma polisi pale.”
A l i s e m a F a t m a Karume akisisitiza kuwa wanaowanyima haki yao Wazanzibari waliopiga kura s io Mwenyekit i wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha.
K a m a n i k u s e m a , Jecha kasema tu, lakini hana mamlaka na kama n i k u l a u m i wa J e c h a atalaumiwa kwa kutumiwa dhidi ya maslahi na haki ya Wazanzibari.
Wa k a t i h u o h u o , wananchi mbalimbali w a m e u n g a n a n a M wa n a s h e r i a F a t m a
Karume wakisema kuwa kwa hakika wa kulaumiwa n i Amri Jesh i Mkuu aliyetuma Jeshi Zanzibar.
K a t i k a m a o n i y a wananchi hao wanasema k u wa ” Wa z a n z i b a r i watamkumbuka sana Kikwete kwa kuwanyima haki yao ya msingi ya k u c h a g u a k i o n g o z i wanayemtaka.”
“Tutamkumbuka vyema kwa kusimamia zoezi zima la kupindua demokrasia Zanzibar kwa nguvu .
Tutamkumbuka kwa kufanya hivyo bila ya kujali matokeo na athari ya k u wa n y i m a h a k i Wazanzibari.”
“ T u t a m k u m b u k a kwa kutudhih i r i sh ia kuwa huu muungano k w a W a z a n z i b a r i n i wa k u k a n d a m i z a ( W a z a n z i b a r i ) . . .ametunyima uhuru wetu wa kuamua. Amekejeli mawazo na maamuzi ya Wazanzibari.”
“ K w a u f u p i a m e t u d h a r a u k a b i s a Wazanzibar kwa kiwango cha hali ya juu kabisa na kutuonesha kuwa sisi hamna lolote wala u m u h i m u w o w o t e kwa Tanzania, (ni kana kwamba anatuambia) ‘tutafanya tunavotaka, t u m e k u h o d h i n i n a kuwatawala na hamna haki zozote za kujiamulia mambo yenu’.”
“Sisi ni wanyonge..., ni Mungu peke yake atatulipia na kutulinda. Allah ni Muweza na ni vyake vyote viliomo kwenye ardhi na mbingu..na Yeye
ndie mwenye kutoa na kunyima. Tunamuangukia Yeye atupe nguvu na kutunusuru.”
Huo ni moja ya ujumbe unaowakilisha maoni ya baadhi ya wananchi wa Zanzibar ambao umekuwa ukisambazwa kupitia mitandao ya kijamii.
Kwa upande mwingine, Ra is mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete alifanya mazungumzo na Maalim Seif katika Ikulu Jijini Dar es Salaam juzi.
Hata hivyo, habari kutoka ndani ya chama cha CUF zinasema kuwa hakuna lolote la muhimu lililoafikiwa isipokuwa ‘mazungumzo ya kawaida’ tu.
H a b a r i z i n a s e m a , k i n a c h o o n e k a n a n i kutafuta ‘muafaka wa 5’ na kurudiwa uchaguzi ili kuhakikisha kuwa ‘kosa halifanyiki tena kuruhusu CCM kushindwa’.
Katika hali ambayo i m e w a s h a n g a z a wengi , v iongozi hao wameonekana wakifurahi na kucheka muda wote wa maongezi yao (kwa mujibu wa picha zilizopatikana) wakati jambo lenyewe ni zito huku mitaa ya Unguja na Pemba ikiwa imejinamia kwa huzuni, kukata tamaa na kutokujua nini majaaliwa yao.
Lakini za idi n i i le kukutana wao wawili tu, na wakati huo huo hali ikizidi kuwa tete kwa wananchi mitaani ambapo bado jeshi, polisi na vikosi wanaranda.
J e c h a a l i s e m a k u t o k a n a n a k a s o r o nyingi z i l izo j i tokeza kat ika uchaguzi huo kwa mamlaka aliyopewa anafuta uchaguzi huo na Tume hiyo italazimika kufanya uchaguzi mengine upya, kauli hiyo imepigwa na baadhi ya wanasiasa na wanasheria mbali mbali nchini.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wanasheria hao wamesema kwamba Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi hana mamlaka ya kisheria kufuta matokeo ya uchaguzi.
K w a m a a n a h i y o amefanya jambo batili kikatiba na kisheria na kwa hakika inahuzunisha k w a m b a s e r i k a l i inayowachagiza wananchi kufuata sheria, ndiyo
inaonekana nyuma ya pazia katika jinai na hatia hii kubwa inayoweza kuleta machafuko katika nchi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku.
akamwambia, Mwanangu. Naye akamwitikia, mimi hapa. Akasema, Tazama, sasa mimi nimekuwa mzee wala sijui siku yangu ya kufa kwangu. Basi, nakuomba , chukua mata yako, podo lako na upinde wako, ukaende nyikani uniwindie mawindo; ukanifanyie chakula kitamu namna i l e n i ipendayo, ukaniletee, ili nile; na roho yangu ikubariki, kabla sijafa.” (Mw. 27:1-4.)
Z i l e ‘ I s r a i l i y a t i ’ n i l izokuwa nikisema zinajitokeza hapo, wakati Isaka ameishi mpaka amezeeka na kupofuka macho, alikuwa anajua kuwa mwanae wa kanza ni Isaka, lakini andiko lilitwambia kuwa ukubwa wake wa mzaliwa wa kwanza al iubadil isha na chakula chekundu cha dengu; na Yakobo aliridhika kuwa ndiye mkuwa akampa chakula cha dengu na mkate.
“Na Rebeka akasikia, Isaka aliposema na Esau m w a n a w e … . . R e b e k a a k a m w a m b i a Ya k o b o mwanawe, akisema, Angalia, n imems ik i a baba yako akisema na Esau, ndugu yako, akisema,…mbele za BWANA… basi, mwanangu, sikiliza sauti yangu kama nitakavyokuagiza. Enenda sasa kundini unitwalie wana-mbuzi wawili walio wema, nami nitawafanya chakula kitamu kwa baba yako, namna ile aipendayo. kisha utampelekea baba yako, apate kula, ili akubariki kabla ya kufa kwake.” (Mw. 27:5-10.)
Katika andiko la hapo juu, Isaka hakumwambia Esau nikubariki ‘mbele za BWANA’, maneno hayo ameyasema Rebeka; a k i m a a n i s h a k u w a anayeidhinisha Baraka au laana, zimpate mtu ni BWANA, yaani Mwenyezi
Mungu; ikimaanisha kuwa Rebeka ni mcha Mungu; Je! hivyo ndivyo?
“Yakobo akamwambia Rebeka mamaye, Esau n d u g u ya n g u n i m t u mwenye malaika, na mimi ni mtu laini. Labda baba yangu atanipapasa, nami nitakuwa machoni pake kama mdanganyifu; nami nitaleta juu yangu laana wala si mbaraka. Mamaye akamwambia, Laana yako naiwe juu yangu, mwanangu, usik ie sauti yangu tu, enenda ukaniletee wana-mbuzi. Akaenda, akawatwaa, akamletea mamaye. Mamaye akafanya chakula kitamu namna ile aliyopenda babaye. Kisha Rebeka akatwaa mavazi mazuri ya Esau mwanawe mkubwa, aliyokuwa nayo nyumbani, akamvika Yakobo mwanawe mdogo. Na ngozi za wana-mbuzi akamvika mikononi, na katika ulaini wa shingo yake. Naye akampa Yakobo mwanawe mikononi mwake hicho chakula kitamu, na mkate a l ioufanya .” (Mw.27:11-17).
Aya hizo hapo juu zinatudhihirishia kuwa, ubadilishanaji wa ukubwa wa Esau kwa udogo wa Yakobo ni hekaya za alinacha; ndiyo maana Rebeka mama yao hazijui, yeye anacho jua, ni kuwa Esau ndiye mwanawe mkubwa, na Yakobo ni mwanawe mdogo. Hapo j u u n i l i e l e z a k u wa , Rebeka alionesha kuwa anamtambua ‘BWANA’ yaani Mwenyezi Mumnu’ lakini kwa maelezo ya aya hizo hapo juu, inaonekana kuwa Rebeka hana habari na uwezo wa ‘BWANA’ yaani Mwenyezi Mungu;
na inaonekana ndiye aliyechangia silka ya wana wa Israeli tunayoishuhudia hadi sasa, ya uongo na ulaghai n.k. Ni vipi Yakobo alaaniwe na baba yake, lakini laana impate mamayake? Wasomaji, naandika kisa hiki kutoka katika Biblia, kwa kirefu kwa kuwa, hi i ndiyo moja ya misingi mikuu w a n a y o s i f i w a n a y o wana wa Israeli, kuwa imewajengea utukufu kwa Mwenyezi Mungu, na wakawa taifa teule. Fatilia mahojiano ya Yakobo na baba yake Mzee Isaka:
“Akaja kwa baba yake, akasema, Babangu. Akasema Mimi hapa, Unani wewe, m w a n a n g u ? Ya k o b o akamwambia babaye, Mimi ni Esau, mzaliwa wako wa kwanza, nimefanya kama ulivyoniambia. Ondoka, tafadhali, ukae kitako, ule mawindo yangu, ili roho yako inibariki. Isaka akamwuliza m wa n a we , I m e k u wa j e umepata upesi namna hii, mwanangu? Akasema, Kwa sababu BWANA, Mungu wako, amenifanikisha. Isaka akamwambia Yakobo, Karibu, tafadhali, ili nikupapase, mwanangu, nione kwamba wewe ndiwe mwanangu Esau, ama siyo. Basi Yakobo akamkaribia Isaka, babaye, naye akampapasa, akasema, Sauti ni sauti ya Yakobo, lakini mikono ni mikono ya Esau. Wala hakumtambua, kwa maana mikono yake ilikuwa kama mikono ya Esau yenye malaika; basi akambariki. Akamwuliza, Wewe ndiwe kweli mwanangu Esau? Akasema , Ndimi. Akasema Niletee karibu nami nipate kula mawindo ya mwanangu,
ili roho yangu ikubariki. Akasogeza karibu, naye akala; kisha akamletea mvinyo, akanywa, Isaka, baba yake, akamwambia, Njoo karibu sasa, ukanibusu, mwanangu. Akakaribia akambusu. Naye akasikia harufu ya mavazi yake, akambariki akasema… (Mw.27:18-27.) (Soma hukumu ya mdanganyifu, Walawi 6:1-7):
“BWANA akanena na Musa, na kumwambia , Mtu awaye yote akifanya dhambi, na kuasi juu ya BWANA, akamdanganya mwenziwe katika jambo la amana, au la kunyang’anya, au kumwonea mwenziwe; au kuzumbua kitu kilichopotea na kutenda la uongo juu yake, na kuapa kwa uongo; katika mambo hayo yote mojawapo atakalol i tenda mtu, na kufanya dhambi kwalo; ndipo itakapokuwa, akiwa amefanya dhambi, na kupata hatia, atarudisha hicho alichokipata kwa kunyang’anya, au kitu kile alichokipata kwa kuonea, au ile amana aliyowekewa, au kitu kile kilichopotea alichokizumbua yeye, au kitu chochote ambacho amekiapia uongo; atakirudisha hata kwa ukamilifu wake, kisha ataongeza na sehemu ya tano zaidi juu yake; naye atampa huyo mwenyewe, siku hiyo ambayo atakapohukumiwa kuwa mwenye hatia. Kisha ataleta sadaka yake ya hatia kwa BWANA, ni kondoo mume wa katika kundi lake, mkamilifu, sawasawa na hesabu utakayomwandikia, kuwa sadaka ya hatia, na kumpa kuhani; na huyo kuhani atafanya upatanisho kwa ajli yake mbele za Bwana, naye atasamehewa; katika jambo lo lote alifanyalo hata akapata kuwa mwenye hatia
kwalo.” (Lawi 6:1-7.)Aya hizo zinatuonesha
wazi , zile ‘israiliyati’ n i l i z o z i z u n g u m z i a hapo mwanzo. Mzee Isaka hana habari kuwa, mwanawe Esau, amekuwa mdogo kwa Yakobo, na kuwa Yakobo amekuwa mkubwa kwa Esau; na Yakobo anakiri, kuwa yeye ni mdogo kwa Esau, ndiyo maana anatafuta Baraka za Esau kwa hila. Kwa kumdanyanya babayao. Jambo jingine , ni kuwa, kama Yakobo a l ikuwa na mapenzi na baba yake kwanini Mzee Isaka asimwambie amchinjie mbuzi; i la akamwambia Esau kuwa amtafut ie mawindo? Kinachosikitisha zaidi ni kuwa, Isaka na Yakobo wanatambuliwa kuwa ni Manabii na Mitume maarufu wa Mwenyezi Mungu, lakini kwa riwaya hizo zinawaondoa katika k i i g i z o c h a k u i g wa ; unategemea nini kwa mafundisho hayo, kwa waumini wako vijana, hata na watu wazima?
“Tazama, harufu ya mwanangu Ni kama harufu ya shamba al i lol ibariki Bwana. Mungu na akupe ya umande wa mbingu, na manono ya nchi, Na wingi wa nafaka na mvinyo. Mataifa na wakutumikie Na makabila wakusujudie, Uwe bwana wa ndugu zako, Na wana wa mama yako na wakusujudie. N a a t a k a y e k u b a r i k i abarikiwe.” (Mw. 27:28-29.)
Ukisikia kuwa wana wa Israeli ni taifa teule, takatifu na kuna mungu wa Israeli, ni yule mungu a n a ye b a r i k i d h a m b i kama hizo zilizofanywa na Rebeka na Yakobo mwanawe.
CHAMA Cha Wananchi CUF, kimeelezea kusikitishwa na matukio ya kuwatia hofu wananchi na kuhatarisha amani ya nchi.
A k i z u n g u m z a n a waandishi wa habari katika o f i s i z a C h a m a h i c h o Mtendeni Zanzibar, Naibu K a t i b u M k u u wa C U F Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui, ameyataja matukio hayo kuwa ni pamoja na miripuko inayoelezwa kuwa ni mabomu katika maeneo ya Mkunazini na Michenzani.
A m e y a t a j a m a t u k i o mengine kuwa ni uvamizi uliofanywa katika kisiwa cha Tumbatu ambao ulipelekea nyumba nne kutiwa moto na nyengine kadhaa kuvunjwa, sambamba na kupigwa na kujeruhiwa kwa wananchi 16 wa kisiwa hicho.
A k i f a f a n u a k u h u s u matukio ya miripuko, Mhe. Mazrui ameishauri Serikali
Wanaotega mabomu wakamatweNa Mwandishi Wetu
k u wa t a f u t a wa l i o t e g a m a b o m u h a y o k w a kutumia picha za kamera za ulinzi za CCTV ambazo zimesambazwa katika eneo lote la Mji Mkongwe.
A m e s e m a , b i l a y a kuchukuliwa kwa hatua, wananchi wataendelea kuamini kuwa matukio hayo yamepangwa makusudi kwa lengo la kuwatia hofu w a n a n c h i w a s h i n d w e kuendelea na shughuli zao za kimaisha.
Wakati hayo yakiendelea, Mhe. Mazrui amesema juhudi kubwa zimeanza na zinaendelea vyema kwa kuzishirikisha jumuiya na taasisi za ndani na nje ya nchi, zikiwa na lengo la kukwamua mkwamo wa kisiasa unaoikumba Zanzibar hivi sasa. NAIBU Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui.
Nimeamua kuijibu makala ya Khatib J Mziray toleo na 1231 ilihusu “KHABARI YA ISRAEL TAIFA TEULE LA MUNGU”. Sikusudii k u l u m b a n a n a y e , i l a k w a k u w a a m e n u k u u vifungu kadhaa vya Biblia, kuna ulazima wa kuweka mambo sawa.
S i s i w a u m i n i w a “ n j i a i l e ” t u m e a g i z wa kuishindania imani mara moja tu kwasababu baada ya maisha ya hapa duniani aaminiye hatakuwa na nafasi tena ya kuishindania (kuipigania imani). Yuda a l i y e k u w a n d u g u w a kuzaliwa tumbo moja na Yesu, anaandika “wapenzi nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, niliona imenilazimu kuwaandikia ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu. Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola na Bwana wetu Yesu kristo”(Yuda 1-3).
Yesu aliwapa mitume wake changamoto hii, “Je, atakaporudi tena mwana w a A d a m u a t a i k u t a i m a n i d u n i a n i ? ” Ye s u anazungumzia imani asilia i l iyoanzia kwa Adamu Baba yetu wa kwanza, imani ambayo hakuilinda akaanguka dhambini. Imani hiyo ikal indwa vi l ivyo na Ibrahimu hadi Mungu ak amk ubal i , akamwita I b r a h i m u b a d a l a y a Abrahamu, kumaanisha Baba wa imani na Baba wa Mataifa yaani wanadamu wengine watakaoamini nje ya uzao wa kimwili wa Ibrahimu (Waisraeli).
Imani ya Ibrahimu ni somo pana linastahili kuandikiwa vitabu hata zaidi ya vitano. Yesu alipokuwa duniani hakuanzisha imani mpya, bali aliilinda, akaipigania imani ile ile aliyokabidhiwa Adamu lakini ikamponyoka. Imani ile ile iliyomfanya Nabii Nuhu ajenge safina kwa miaka mia, ndiyo i l iyomfanya Abrahamu ajitenge na ukoo wake, awaachane ndugu zake na kuishi hali ya upweke.
Tofaut i ya Ibrah imu n a A d a m u n i k wa m b a Ibrahimu aliilinda imani hadi mwisho. Mungu akamkubali akasema, “ Ibrahimu hakika nimethibitisha kwamba unaniamini na unanicha mimi Mungu wako iwapo hukunizuilia mwana wako wa pekee.” Mungu akamwapia Ibrahimu akisema, “nimeapa kwa nafsi yangu nitakubariki, nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia.”
Neno hili la Mungu lilitimia alipozaliwa Yesu kupitia ukoo wa Ibrahimu kwani mataifa yote ya dunia yanajibarikia kwa jina lake, hayabarikiwi kupitia dola ya Israeli, hili inabidi liwekwe bayana. Yesu ana sifa nyingine ya kuitwa mzao wa mwanamke, kuzaliwa kwake kulitimiza unabii ambao Mungu aliutoa
Itikadi siyo imani wala imani haina itikadiNa Mwinjilisti Kamara Kusupa
kwa kinywa chake akiwa Edeni, alipomwambia nyoka wa zamani aitwaye Ibilisi “nami nimeweka uadui kati ya uzao wake na uzao wako, “mzao wake” atakuponda kichwa.
M i a k a 7 0 0 k a b l a ya kuzaliwa Yesu, Nabii Isaya alitabiri akisema, “tazama bikira atachukua mimba naye atamzaa mwana nao watamwita jina lake Imanueli maana yake ni Mungu pamoja nasi wanadamu.”
Imani ile ile ya Ibrahimu ndiyo iliyomfanya Musa asimame mbele ya Farao (Firauni) na kumpa ujumbe “BWANA asema uwaachilie watu wangu.” Imani hiyo haikulindwa na Israeli kama taifa, wala haikulindwa na Waisraeli kama watu binafsi ukiacha manabii kama ELiya. Huyu nabii Eliya Mungu a l i m p a i s h a m b i n g u n i hakuonja mauti, jina Eliya maana yake ni “commitment to faith” yaani mtu aliyejitoa na kuyasalimisha maisha yake kwa ajili ya imani.
Dhana ya Israeli kuwa taifa teule la Mungu imetokana na ukweli uliopotoshwa, kilichoandikwa ndani ya Bibl ia ni ukweli lakini k i n a c h o h u b i r i w a n a wanadamu wanaonasibisha maandiko matakatifu na matendo mabovu ya dola ya Israeli ya sasa ni uwongo na upotoshaji wa ukweli. Upotoshaji huo una lengo la kuhalal isha ubeberu wa Kiyahudi dhid i ya Wapalestina huko Mashariki ya Kati.
K u h u s i s h a s i a s a z a M a s h a r i k i ya K a t i n a kilichoandikwa ndani ya B i b l i a , n i k u e n d e l e z a yasiyofaa ambayo Yuda alionya mapema kwamba ni mambo ya watu waliojiingiza kwa siri. Watu makafiri wenye kumkana Mola na Bwana Yesu. Watu wabadilio neema ya Mungu na kuigeuza kuwa ufisadi.
S i u t e t e i U k r i s t o , b a l i n a u t e t e a u k w e l i u n a o f u n u l i w a k a t i k a Biblia. Inahitaji moyo wa m w e n d a w a z i m u m t u kuutetea Ukristo ulioingia Afrika kutoka Ulaya na Marekani. Marekani na Ulaya Mangaribi zimeruhusu ndoa za jinsia moja, Mkristo anaweza kufanyiwa upasuaji akabadilisha sura (plastic surgery), akabadilisha jinsia kutoka mwanaume akawa mwanamke, bado akaendelea kutambuliwa na kanisa lake analoshiriki kumwabudu Mungu.
Wa l i o m wa m i n i Ye s u waliitwa “watu wa njia ile” kutokana na kutofautiana na Wayahudi walioifuata Torati ya Musa. Walioamini walitofautiana na Wayahudi kuanzia namna yao ya kuishi hadi namna yao ya kusali na kuabudu.
Jina la Wakristo lilianza kutumika Antiokia mj i uliokuwa maarufu kwa biashara na uliokuwa na mchanganyiko wa watu wa nasaba (race) zote, Wayahudi, Wayunani , Warumi na Wakushi (Waafrika).
W a t u w a n j i a i l e
walikuwako hata kabla ya Yesu kuja ulimwenguni. Manabii wa kale waliisisitizia juu ya njia ile. Nabii Isaya aliyeishi miaka mia saba kabla ya kuzaliwa Yesu, aliandika “Na hapo patakuwako na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu, wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao tu, watu wasaf ir io , wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo. Hapo hapatakuwa na Simba, wala mnyama mkali hatapanda juu yake, wala hawataonekana hapo, b a l i w a l i o k o m b o l e w a n d i o w a t a k a o k w e n d a katika njia hiyo. Na hao waliokombolewa na BWANA watarudi watafika Sayuni wakiimba na furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao nao watapata kicheko na furaha, huzuni na kuugua zitakimbia.”(Isaya 35:8 – 10).
H i y o n d i y o n j i a ya mbinguni aliyoonyeshwa Yakobo mjuu wa Ibrahimu a m b a y e a l i b a d i l i s h wa jina kutoka Yakobo lenye maana ya mtu mjanja na m d a n g a n y i f u a k a i t wa Israeli, huyu ndiye Baba wa Waisraeli kutokana na watoto wake 12 ambao waliongezeka na kuwa kabila 12 za Israeli.
K w e n y e k i t a b u c h a Mwanzo 28:10 -22 Musa a m e a n d i k a h a b a r i y a Yakobo alivyoonyeshwa njia ile, baada ya Yakobo kumfanyia nduguye kitendo tunachoweza kukifananisha n a u t a p e l i ” m a a n a alidanganya akamwibia mbaraka nduguye Esau waliyezal iwa mapacha, aliamua kuikimbia hasira ya Esau kaka yake. Yakobo akiwa njiani kwenda Harani kwa mjomba wake, alifika sehemu iliyoitwa Luzu, jua lilipomchwea, aliviringisha jiwe akalilalia kama mto. Akiwa usingizini akaona ngazi imeteremshwa duniani na kilele chake kinafika m b i n g u n i a k a m w o n a BWANA ambaye alimwambia “Mimi ni BWANA Mungu wa Ibrahimu Baba yako n a M u n g u w a I s a k a , nchi hii ulalayo nitakupa wewe na uzao wako. Uzao wako utaenea upande wa M a n g a r i b i , M a s h a r i k i , K u s i n i n a K a s k a z i n i , tazama mimi nipo pamoja nawe, ni takul inda ki la uendako, nami nitakuleta tena mpaka nchi hii, kwa maana s i takuacha hata ni takapokufanyia hayo niliyokuambia.” Yakobo alipoamka akasema mahala hapa panatisha, bila shaka hapa ni nyumba ya Mungu na ndipo lilipo lango la mbinguni, akapaita Betheli.
Yakobo akiwa kwa mjomba wake alioa binamu zake wawili akazaa watoto kumi na wawili, hatimaye aliamua kuirudia nchi ya Baba yake I saka . Wakat i anarudi alihofia kushambuliwa na Esau kutokana na utapeli aliomfanyia, maana alipata s a l a m u k wa m b a E s a u anakuja kukulaki akiwa na Jeshi la watu 400.
Yakobo akajitenga peke yake akaomba akisema,
“ee Mungu wa Baba yangu Isaka ni kweli nilivuka mto huu nikiwa na fimbo yangu tu lakini sasa nina mali na watoto nakuomba uniokoe na mkono wa ndugu yangu Esau.” Akiwa kwenye maombi yaliyotokana na hofu ya kupigwa vita ndipo Malaika alipomtokea katika umbo la mwanadamu, Yakobo akamshika kwa nguvu akisema sikuachii hadi unibariki.
Mkanganyiko wa maneno m a l a i k a , M u n g u n a m t u mmoja, yanatokana na ukweli kwamba Mungu aliyekuwa akiwatoke Ibrahimu, Isaka na Yakobo hana umbile maalumu. Wakati Mungu anakwenda kuiteketeza Sodoma alipita kwenye hema ya Ibrahimu, aliandamana na malaika wawili lakini wote watatu wakiwa katika umbile la mwanadamu, ndio maana Ibrahimu aliweza kuwakaribisha akawaandalia chakula, akamchinja ndama na mkewe Sara akaoka mikate isiyo na chachu wakala.
Mungu alipomtokea Musa katika umbile la moto alisema “mimi ni Mungu wa Baba zako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.
K i t e n d o c h a M u n g u kujitambulisha kwa Musa kama Mungu wa Ibrahimu hakina maana kwamba aliwakana wanadamu wengine akawafanya si wake wala hakusema hahusiki nao. Dhana ya Israeli kuitwa Taifa teule ililetwa na wanadamu (Wayahudi) wenye ubinafsi, ambao walitaka kuhalalisha mabaya yasiyohalalishika.
Huko mbelen i tu taona j insi Yesu al ivyofarakana na Wayahudi kwasababu mafundisho yake yalipingana na itikadi ya Usayuni au “Zionism”. Nihitimishe mada yangu kwa kugusia kifupi suala la Ukristo wa It ikadi au “Ideological Christianity.”
Je, Itikadi au “Ideology” ni nini? Ideology inatokana na neno “idea” ni hali ya kuyainua juu mawazo fulani au fikra, zinapewa uzito usiostahili na msisitizo mkuu hadi kuyaingiza kwenye imani yakahubiriwa kama yotokayo kwa Mungu.
Ukristo wa itikadi uliingia Afrika kwa sura nyingi zenye athari tofauti, “Christianity that comes to Africa in different forms with difference effects.” Tuangalie sura nne ya kwanza naiita “Christian colonialism.” Wazungu wa Ulaya Mangaribi walipoleta ukoloni walitanguliza Ukristo kama chambo. Wamishenari walihubiri habari za Mungu wa upendo huruma na msamaha.
Lakini kwenye kipindi chote cha utawala wa Wazungu b a r a n i A f r i k a , u k o l o n i haukuonyesha upendo wowote kwa Mwafrika. Mbaya zaidi ukoloni ukafungamanishwa na Ukristo ukafanywa kitu kimoja. Ndio maana historia haionyeshi kanisa kupinga utumwa wala kupinga ukoloni.
Iko sura ya pili ya Ukristo wa itikadi naiita “Christian Capitalism” miaka ya themanini Tai fa kubwa la Marekani liliandaa mkakati wake wa kuangusha Ukomunisti na kuisambaratisha dola ya Urusi (USSR) likatanguliza mbele kipaumbele cha Injili. USA ilitupumbaza wengi tukadhani inatimiza neno la Yesu alilosema
kabla ya mwisho kuja, habari njema za ufalme wa Mungu (Injili) itahubiriwa Ulimwenguni kote iwe ushuhuda. Tuliamini kwamba Marekani inataka dunia “iinjilishwe” lakini wahubiri wengi kutoka Marekani na Ulaya Mangaribi walisisitizia Injili ya mafanikio (injili ya kumtajirisha aaminiye), wakasisitizia wokovu kamili kumaanisha aliyeokoka hateswi na magonjwa na umaskini. Wengine waliita “the health and wealthy gospel” wakimaanisha ni injili ya afya na utajiri, hata kama mafundisho yao hayakusema moja kwa moja yanataka mwanadamu aishi chini ya mfumo gani, lakini yaliashiria kuuhalisha ubepari kama mfumo unaompa binaadamu uhuru. Kwa njia hiyo
wakahalalisha “capitalism” kuitawala dunia. Hatimaye niliitilia shaka “doctrine” hii kwani kila nilipomzamia Yesu n i l imwona kama mjamaa aliyejiweka mbali na aina zote za unyonyaji.
Ukomunisti ulipoanguka Marekani ikaanza kuonyesha sura yake halisi, ikathibitisha kwamba mradi wa “kuinjisha” dunia (to evangelize the world) ilikuwa mbinu ya kupenya kwenye mataifa ili kuangusha usoshalisti duniani.
Sasa Marekani na Ulaya Mangaribi wako mstari wa mbele kuishinikiza Afrika ikubaliane na machukizo ya ushoga na ndoa za jinsia moja, maadamu makanisa ya Ulaya na Marekani yamekubali machukizo hayo hatimaye serikali dhaifu za Afrika zitakubali.
S u r a ya t a t u n a i i t a “Christian Zionism.” Hii ni itikadi inayoshabikiwa zaidi na Wakristo wenye imani ya kilokole, chimbuko lake ni maandiko pale M u n g u a l i p o m wa m b i a Ibrahimu nitakubariki na akubarikie atabarikiwa naye akulaaniye atalaanika. Narudia tena kusisitiza kwamba yaliyoandikwa katika Biblia ni ya kweli lakini yanatafsiriwa vibaya, anayethubutu kuitwaa dola ya sasa ya Israeli na kuiweka mahala pa Ibrahimu, Yakobo na Daudi (watu waliokwenda vizuri na Mungu) atakuwa anaitafutia dola ya Israeli uhalali usiokuwako hapa duniani wala huko mbinguni. Mungu haridhii uovu wala dhuluma ya aina yoyote, ndio maana Waisraeli wa kale walipozidisha dhambi Mungu a l iwaadhibu kwa kuwafukuza kwenye nchi yao.
Itikadi siyo imani wala imani ya kweli haibebi itikadi ambazo chimbuko lake ni mawazo ya watu wenye ubinafsi, kwa hiyo waaminio katika “Zionism”, wanafumbia macho mambo mengi. Kwanza wanafumbia m a c h o u k w e l i k w a m b a Wayahudi walimkataa Yesu hadi leo hawamkubali kuwa ni mwana wa Mungu.
W a n a f u m b i a m a c h o ukweli kwamba mbaraka wa Mungu ni kwa Ibrahimu na wazao wake, Mungu ndiye aliyemwambia Ibrahimu “kwa habari ya Ishimaeli nimekusikia nimembariki naye atakuwa taifa atazaa maseyidina kumi na wawili.” Maneno ya Mungu hayatanguki, katika uzao wa Ishmaeli ndiko walikotoka Waarabu na katika uzao wa Isaka ndiko walikotoka Waisraeli, kumbe taifa la Mungu ni lipi na lisilo la Mungu ni lipi?
ISLAMIC PROPAGATION CENTREP.O. BOX 55105, Dar es Salaam; Phone: 022 2450069, 0784 267762, 0654 613086 Fax: 022 2450822, website:wwwipc.org.tz
Nafasi za kujiunga na Kidato cha I, 2016
ARUSHA: Ofisi ya Islamic Education Panel, Jambo Plastic, ghorofa ya 2 mkabala na Msikiti Mkuu wa Bondeni simu 0715 438676. KILIMANJARO: MOSHI: Msikiti wa Riadha simu 0686 938077, SAME: Juhudi Studio mkabala na Benki ya NMB Same simu 0757 013344. Kirinjiko Islamic Secondary School simu 0784 296424.TANGA: Twalut Islamic Centre – Mabovu Darajani simu 0713 014469/0768 087112. KOROGWE Shemea Shop: 0715 690008. LUSHOTO Mandia: 0782 257533. HANDENI Mafiga: 0782 105735.MWANZA: Nyasaka Islamic Secondary School simu 0717 417685/0786 417685. Ofisi ya Islamic Panel – Mtaa wa Rufiji
mkabala na Msikiti wa Al-Amin simu 0714 097362.MUSOMA: Ofisi ya Islamic Education Panel Mtaa wa Karume, nyumba Na. 5 simu 0787 868611/0716 810002.SHINYANGA: Msikiti wa Majengo na Manispaa ya Shinyanga Mjini simu 0768 895484/0655 608139. KAHAMA: Ofisi ya AN-NUUR karibu na Msikiti wa Ibadhi simu 0782 994738/0754 994738.DAR ES SALAAM: Ubungo Islamic High School simu 0687 820895.MOROGORO: Msikiti wa Ijumaa simu 0782 529263.DODOMA: Hijra Islamic Eng. Med Primary School simu 0718 661992.SINGIDA: Ofisi ya Islamic Education Panel karibu na Nuru
Snack Hotel simu 0786 425838/0784 928039.MANYARA: Ofisi ya Islamic Education Panel Masjid Rahma simu 0784 491196.KIGOMA: Idhihari karibu na Msikiti wa Legeza Mwendo Mwanga simu 0717 383400/0754 569661. KIBONDO: Kibondo Islamic Nursery School simu 0784 442860. KASULU: Murubona Islamic Secondary School simu 0714 710802. Msikiti wa Mugera Mwandika simu 0763 945704/0714 717727.LINDI: Wapemba Store simu 0653 705627.MTWARA: Amana Islamic Secondary School simu 0787 231007.SONGEA: Kwa Kawanga karibu na Msikiti wa NURU simu 0713 249264. Mkuzo Islamic High School simu 0654 876317.MBEYA: Ofisi ya Islamic Education Panel Uhindini simu 0785 425319. Rexona Video mkabala na Mbeya RETCO simu 0713 200209/0785 425319.RUKWA: Sumbawanga: Ofisi ya Islamic Education Panel mkabala na shule ya Msingi Kizwite simu 0717 082073.TABORA: Kituo cha Kiislamu Isevya simu 0718 556355. NZEGA: Dr. Mbaga: 0784 576922.IRINGA: Ofisi ya Islamic Education Panel Masjid Hidaya simu 0714 522122.PEMBA: Kizimbani: Wete Islamic School simu 0777 870601.UNGUJA: Madrasatul-Fallah simu 0777 432331. Pand Book Shop: 0777 462056 karibu na uwanja wa Lumumba.MAFIA: Karibu na Msikiti Mkuu Ofisi ya Ust. Yusuph Ally: 0773 580703.
Wahi kuchukua fomu sasa
Kirinjiko Islamic High School - Same Mkuzo Islamic High School - SongeaAmbasha Islamic High School-Pemba
Nyasaka Islamic Sec. School - Mwanza Ubungo Islamic High School - Dar es SalaamWaislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za Kidato cha Kwanza 2016 kwa shule zifuatazo:
Ambasha Islamic High - Bweni tu - Pemba: 0777 870601/0786 573938 Kirinjiko Islamic Sec. Sch. - Bweni tu - Same: 0784 296424 Mkuzo Islamic High School - Bweni tu -Songea: 0654 876317/0783 079146 Nyasaka Islamic Sec. School - Bweni tu - Mwanza: 0786 417685/0713 749020 Ubungo Islamic High School - Kutwa na Bweni - DSM: 0687 820895/0716 960456
Mlete mwanao apate elimu na malezi bora ya kimwili, kiroho, na kiakili
1. Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wa-toto elimu bora ya sekondari na kuwalea kwa misingi na maadili mema ya Kiislamu.2. Masomo yanayofundishwa ni haya yafuatayo: Elimu ya Dini ya Kiislamu, Usomaji Qur’an na mafunzo yake, Lugha ya Kiarabu, Kiswahili, English, Basic Mathematics, Physics, Chemistry, Biology, Geography, History, Civics, Book - Keeping na Commerce.3. Mtihani wa kujiunga utafanyika tarehe 28/11/2015 saa
MUDA WA KUCHUKUA FOMU UMEONGEZWA HADI 28/11/2015
2:00 asubuhi katika vituo mbalimbali kote nchini.4. Muombaji anaweza kufanya mtihani katika kituo chochote.5. Mwisho wa kuchukua fomu ni tarehe 28/11/2015.6. Fomu za Maombi zinapatikana katika vituo vilivy-oorodheshwa hapa chini kwa malipo ya shilingi 10,000/=7. Pia, fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Kwa atakayepata fomu kupitia tovuti (download) ata-takiwa kuilipia siku ya mtihani.
Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Ltd, Dar es Salaam.
MUHARRAM 1437, IJUMAA NOVEMBA 6 - 12, 2015
TA A S I S I y a Mwalimu Nyerere imeitaka Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kufanya kazi kwa kuzingatia katiba na sheria za nchi na kuacha kutanguliza mbele maslahi binafsi ya kisiasa.
A k i z u n g u m z a n a vyombo vya habari mjini Musoma, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Mzee Joseph Butiku, amesem a amekerwa na tabia ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kusitisha uchaguzi na kushindwa kuwatangazia wananchi kiongozi wao waliomchagua, huku ikishindwa kuheshimu matakwa ya wananchi waliopiga kura katika visiwa vya Zanzibar.
Taasisi hiyo imeitaka Tume ya Uchaguzi ya
Mzee Butiku aishushia lawama nzito ZECNi muafaka wa tano! 2020 hatukubali...Salma Alghaythiyah wa Tanzania na Mbunge
ziliyosimamiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Tanzania (NEC) na kura tatu za kumchangua Rais wa Zanzibar, Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi na Diwani.
Wakati matokeo ya uchaguzi yalitangazwa katika majimbo 32 na baadhi ya wagombea kukabidhiwa matokeo yao ambayo yalibandikwa v i t u o n i n a b a a d h i y a m a t o k e o h a y o kutangazwa kwenye kituo kikuu cha kutangazia matokeo katika Hoteli ya B wa wa n i , g h a f l a zoezi hilo likasitishwa na kufutwa kabisa mnapo O c t o b a 2 8 a m b a p o Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salum Jecha alipojitokeza kwenye kituo cha televisheni cha taifa.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyemaliza muda wake Dkt. Jakaya Kikwete. Mazungumzo hayo yaliyochukua muda wa dakika 50 yalifanyika Jumatano wiki hii Ikulu ya Rais Jijini Dar es Salaam kuanzia saa 4:24 asubuhi na kumaliza saa 5:14. Kicheko hiki kina tafsiri gani kwa wananchi walioporwa kura zao kwa kufutwa uchaguzi halikadhalika vipigo vinavyoendelea mitaani?
Zanzibar kufanya kazi kwa uweledi na kuheshimu maamuzi ya wananchi na sio kwa kutanguliza mbele maslahi binafsi ya kisiasa hatua ambayo inaweza kusababisha machafuko na umwagaji wa damu katika visiwa vya Unguja na Pemba.
Aidha Mzee Butiku amewataka wananchi wa Zanzibar kutokubali tena
kurudia upigaji wa kura hadi hapo yatakapotolewa maelezo ya kuridhisha na wahusika waliosababisha uchaguzi huo kufutwa pia waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria
Mzee Butiku amesema k w a s a b a b u h i y o amewataka viongozi k u h e s h i m u s h e r i a na katiba ya nchi na kwamba chama ambacho
kinadhani kimeshindwa katika uchaguzi huo kikubali matokeo badala ya kuifanya Zanzibar ni mali ya chama fulani pekee.
Uchaguzi wa Tanzania umefanyika Oktoba 25 mwaka huu ambapo W a z a n z i b a r i n a o wamepiga kura tano ikiwemo ile ya Rais wa Jamhuri ya Muungano
WANASHERIA Fatma Amani Abeid Karume na Awadh Ali Said, wametoa changamoto kwa mamlaka husika, kutaja chapo kifungu kimoja tu cha Katiba ya Zanzibar na Sheria za Tume ya Uchaguzi Zanzibar, ambacho kinampa Mwenyekiti wa Tume, Jecha Salim Jecha na ZEC kwa ujumla, uwezo na mamlaka ya kufuta uchaguzi.
Wamesema, hilo ni muhimu kabla hata kuja katika malumbano ya Urais wa Dr Shein wakati muda wake ukiwa umemalizika.
Wanasheria hao ambao ni mawakili katika Mahakama Kuu, wamesema kuwa kilichofanyika ni kupora haki ya wananchi kinyume kabisa na katiba na sheria na kwamba ni kielelezo kwamba viongozi wamekosa kabisa sifa ya kuwahimiza wananchi kufuata sheria na katiba kwa sababu wao wenyewe wamekuwa ndio wa mwanzo kuzivunja na kutokujali.
Wakizungumza katika kipindi kilichorushwa na Channel Ten juzi usiku, wamesema kuwa kama
Changamoto kwa SheinKikwete na Dr Magufuli
Na Mwandishi Wetu
Inaendelea Uk. 16
Inaendelea Uk. 16
Kinachosubiriwa sasa ni ‘Mwafaka wa 5’Kikwete atoka Ikulu na ‘zigo’ la lawama