Top Banner
ISSN 0856 - 3861 Na. 1117 JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA , MACHI 21-27, 2014 BEI TShs 500/=, Kshs 50/= Sauti ya Waislamu www.annuurpapers.co.tz Facebook:[email protected] Abiria 239 wapo wapi? Ni siku ya 14 toka walipopotea Wapo walitoweka 1,945 hadi leo Kuna wale wa baharini wa 1,872 Masheikh wa Uamsho wafutiwa mashitaka Msaidizi wa Sheikh Rogo ashambuliwa Mombasa Polisi wadai kuanza msako kwa wahusika Sheikh Farid Hadd Ahmed. NDEGE ya Shirika la Ndege la Malaysia Air Line inayosadikiwa kupotea. Habari kamili Uk. 8 Sheikh Azzan Hamdan Wasiwasi wazidi Zanzibar baadhi watuhumu usaliti Vibonzo vyasambazwa mtandaoni Seif Khatib arejea siasa za ‘Upemba’ Pamoja na kauli ya Jussa...... Uk. 4
16

ANNUUR 1117

Nov 26, 2015

Download

Documents

zanzibariyetu
Welcome message from author
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
  • ISSN 0856 - 3861 Na. 1117 JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA , MACHI 21-27, 2014 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

    Sauti ya Waislamuwww.annuurpapers.co.tz Facebook:[email protected]

    Abiria 239 wapo wapi?Ni siku ya 14 toka walipopoteaWapo walitoweka 1,945 hadi leoKuna wale wa baharini wa 1,872

    Masheikh wa Uamsho

    wafutiwa mashitaka

    Msaidizi wa Sheikh Rogo ashambuliwa Mombasa

    Polisi wadai kuanza msako kwa wahusika Sheikh Farid Hadd Ahmed.

    NDEGE ya Shirika la Ndege la Malaysia Air Line inayosadikiwa kupotea. Habari kamili Uk. 8

    Sheikh Azzan Hamdan

    Wasiwasi wazidi Zanzibarbaadhi watuhumu usalitiVibonzo vyasambazwa mtandaoniSeif Khatib arejea siasa za Upemba

    Pamoja na kauli ya Jussa......

    Uk. 4

  • 2 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014AN-NUUR

    S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM.

    www.annuurpapers.co.tz E-mail: [email protected] zetu zipo: Manzese Tip Top

    Usangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

    Tahariri/Habari

    UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOOL inatangaza program maalum ya maandalizi ya kujiandaa kurudia Mtihani wa kidato cha NNE 2014.Program hii itaanza tarehe 15/03/2014 hadi tarehe 15/10/2014. Jumatatu hadi ijumaa kuanzia saa 2:00 kamili asubuhi hadi saa 9:00 Alasir.

    Masomo yatakayofundishwa ni:-Elimu ya dini ya Kiislamu, English language, Lugha ya kiarabu, Basic Mathematics, Civics, History, Geography, Kiswahili, Physics, Chemistry, Biology, Commerce na Book Keeping.

    ADA: Ni Tshs 500,000/= (Laki Tano) tu. Inalipwa yote kabla ya kuanza programu.

    Fomu za Kujiunga zinapatikana shuleni BURE baada ya kulipa ada.Mlete mwanao apate Elimu yenye tija itakayomwezesha kufanya mtihani wake vizuri.

    Kwa mawasiliano zaidi piga simu namba:0712 974428

    Wabllah tawfiq MKUU WA SHULE

    Ubungo Islamic high SchoolP.o. Box 55105 Tel: 2450069, 0712 974428, fax: 2450822 Dar es salaam.

    E-mail: [email protected]

    MAANDALIZI YA KUJIANDAA KURUDIA MTIHANI WA KIDATO CHA 4, 2014

    S I K U y a J u m a n n e w i k i hii, Mwenyekiti w a T u m e y a Mabadi l iko ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba, aliwasilisha mbele ya Bunge Maalum la Katiba, rasimu ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

    J a j i Wa r i o b a a m e w a s i l i s h a rasimu hiyo ya Katiba mpya mbele ya wajumbe wa Bunge maalum, baada ya wajumbe hao kufanikiwa kupi t i sha kwa kiasi kikubwa, k a n u n i z a kuliongoza Bunge hilo, jambo ambalo limetoa fursa kwa wa j u m b e s a s a k u a n z a r a s m i kuijadili rasimu ya katiba hiyo.

    K w a k u w a sasa Bunge hili maalum limeanza kuijadili rasimu ya Katiba Mpya, ni wajibu wetu kutoa indhari au kukumbushana mambo kadhaa ya msingi.

    K a m a inavyofahamika, K a t i b a n d i o m w o n g o z o mkuu wa dola au

    mamlaka yeyote ya kidemokrasia.

    L a k i n i z a i d i , k a t i b a n i k wa ajili ya wananchi husika na wao ndio wanaostahili kutoa maoni wawe na katiba ya aina gani kwa maslahi yao na Taifa kwa ujumla.

    K w a m s i n g i huo, tunawataka wabunge wa bunge maalum la katiba, k u h a k i k i s h a k w a m b a wanajadili rasimu hiyo ya kat iba m p y a , h u k u w a k i t a m b u a kuwa rasimu hiyo ndio hasa maoni ya wananchi wa Tanzania.

    Hatutara j i na wala halitakuwa jambo la busara kama wajumbe hao watatumia nafasi za kuwawakilisha wa wa n a n c h i , kuweka pembeni au kujadili kwa u c h a c h e j u u ya maoni hayo y a w a n a n c h i yaliyomo ndani ya rasimu, na kuanza kulumbana juu ya maslahi ya vyama, taasisi au makundi yaliyowachagua.

    T u n a s e m a haya kwa kuwa d a l i l i m b a y a

    z i n a z o a s h i r i a kuwepo agenda n a m i s i m a m o y a k i g o n j w a , z i l i s h a a n z a k u j i t o k e z a katika hatua ya awali kabisa ya kujadili kanuni za kuliongoza bunge hilo maalum la katiba.

    M i v u t a n o y a k i c h a m a , k i m a k u n d i ilionekana dhahiri, ikiwa ni ishara tosha kwamba u t a k a p o a n z a m j a d a l a w a rasimu yenyewe, maslahi ya wenye maoni yao kwenye r a s i m u y a n aweza kutotiliwa maanani.

    T u s e m e t u k wa m b a k u n a haja ya wajumbe k u t a m b u a kwamba, katiba

    w a n a y o i t a k a watanzania sio mali ya chama wala taasisi au kikundi cha watu. Ni mali ya watanzania wote.

    Hatuna maana ya wajumbe wawe waitikiaji wa kila kinachojadiliwa katika Bunge hilo, Lah. La msingi ni kuwa na fikra y a k i z a l e n d o kwamba, rasimu ya katiba ndio maoni yenyewe y a w a n a n c h i yaliyokusanywa na kuchambuliwa n a k u w e k w a pamoja.

    W a j u m b e wayajadili wakiwa na fikra kwamba wanajadili yale yaliyotokana na wananchi wenywe. Tu n a c h o k a t a a n i w a j u m b e

    kutanguliza fikra za kimaslahi ya vyama au taasisi z a o b a da l a ya maslahi ya umma kat ika kujadi l i rasimu hiyo.

    T u m a a m i n i kabisa kwamba hata wajumbe wa Bunge hili maalum l a k a t i b a , n a o walipewa nafasi ya kutoa maoni yao ndani ya rasimu wakati Tume ya Jaji Warioba ilipokuwa inakusanya maoni y a w a n a n c h i n a h a t i m a y e kupatikana rasimu kamili.

    N a f a s i y a o sasa ni kujadili y a l i m y o m o kwenye rasimu, sio kuja na maoni yao mapya kwa misingi binafsi i s i y o k u w a n a m a s l a h i k w a umma.

    Bunge la katiba lizingatie maoni ya wananchi

  • 3 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Habari

    Masheikh wa Uamsho wafutiwa mashitakaV I O N G O Z I w a Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam (JUMIKI) wamefutiwa mashitaka yaliyokuwa yakiwakabali katika mahakama ya wilaya ya Mwanakwerekwe, ya kufanya mkusanyiko bila ya kibali , kesi iliyofunguliwa Mei mwaka juzi visiwani Zanzibar.

    Uamuzi wa kuwafutia mashitaka viongozi hao umetolewa na Hakimu wa Mahakama hiyo Ame Msaraka Pinja, baada ya kuonekana k u wa wa s h i t a k i wa hawana hatia katika kesi iliyokuwa imefunguliwa na M kurug enz i wa Mashitaka Zanzibar DPP.

    A k i t o a k u h u m u k a t i k a k e s i h i y o , Hakimu Pinja alisema kuwa, kutokana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo na mashahidi wanne wa upande wa mashitaka, na kwa kusikiliza utetezi wa washitakiwa wenyewe, ambao waliithbitishia mahakama kwamba k a t i k a m k u s a n y i k o w a o h a w a k u w a wakizungumzia mambo ya d in i , i s ipokuwa w a l i z u n g u m z i a M u u n g a n o w a T a n g a n y i k a n a Zanzibar, imeonekana k u wa wa s h i t a k i wa h a wa k u h i t a j i k u wa n a k i b a l i c h o c h o t e cha kisheria kabla ya kuandaa mkusanyiko huo kwa vile walikuwa wakizungumzia mambo ya Muungano.

    K wa m s i n g i h u o , mahakama il itupilia m b a l i s h i t a k a lililofunguliwa dhidi ya Masheikh hao.

    H a k i m u P i n j a aliongeza kuwa baada ya mahakama kupitia jalada la kesi hiyo, imeona k u wa wa s h i t a k i wa hawana hatia, hivyo i n a w a a c h i a h u r u washitakiwa kwa sababu kosa waliloshitakiwa, halikuhitaji kibali cha

    Na Mwandishi Wetu

    Mufti kabla ya kuandaa mkusanyiko huo.

    Kufuat ia hukumu hiyo, Hakimu huyo wa mahakama ya wilaya ya Mwanakwerekwe alisema kuwa iwapo

    upande wa mashitaka w a S e r i k a l i k a m a haujaridhika na uamuzi wa mahakama hiyo, unaweza kukata rufaa mahakama ya mkoa ndani ya siku thelathini

    tangu kutolewa kwa hukumu ya mahakama hiyo.

    W a t u h u m i w a waliokuwa wakikabiliwa na kesi hiyo ni Sheikh Farid Hadd Ahmed,

    Sheikh Mussa Juma Issa, Sheikh Haji Sadif Haji, Sheikh Suleima Juma Suleiman,Sheikh Fikirini Mjawaliwa Fikirini na Sheikh Abdallah Said Ali.

    A w a l i M a s h e i k h h a o wa l i f u n g u l i wa mashitaka mahakamani h a p o y a k u f a n y a mihadhara ya Kiislamu bila kibali cha Mufti, jambo ambalo lilidaiwa kuwa ni kinyume cha kifungu cha 6(1)(2) cha kanuni za kuidhinisha na kuratibu mihadhara zinazotengenezwa chini ya kifungu 15(1) ya sheria Namba 9 ya mwaka 2001, kifungu cha 10(1)(c) na kifungu cha 14(2) cha sheria namba 9 ya mwaka 2001.

    Ilidawa kuwa Mei 26 mwaka juzi majira ya saa 3:30 katika viwanja vya Lumumba wilaya y a M j i n i U n g u j a , w a s h i t a k a i w a h a o walifanya mihadhara ya Kiislamu bila ya kuomba kibali cha Mufti wa Zanzibar, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

    Msaidizi wa Sheikh Rogo ashambuliwa MombasaMOMBASA

    Sheikh Ali Bahero, a m b a y e a l i k u w a msaidizi wa ulamaa wa Kiislamu aliyeuawa kwa kupigwa risasi h u k o M o m b a s a K e n y a , m a r e h e m u Sheikh Aboud Rogo Mohammed, amekutwa akiwa ameloa damu baada ya kushambuliwa m j i n i M o m b a s a , limeripoti gazeti la Daily Nation la Kenya.

    Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Mombasa, G e o f f r e y M a y e k , a m e s e m a p o l i s i walikwenda kufuatilia ripoti ya tukio moja huko Chuo cha Gateaway na walipofika, walipata taarifa za tukio hilo na kumkuta Sheikh huyo

    akiwa hoi huku kalowa damu.

    I m e d a i w a k u w a kufuatia tukio hilo, Polisi mjini Mombasa walianzisha msako dhidi ya vijana waliodaiwa k u f i k i a 4 0 a m b a o imeelezwa kuwa asubuhi ya Alhamisi ya Machi 13 mwaka huu, walitumia mawe na vitu vyenye ncha kali kumshambulia Sheikh huyo katika eneo la Majengo, ikidawa k u wa S h e i k h h u y o kuhitilafiana na vijana hao.

    S h e i k h B a h e r o alipelekwa Hospitali ya Jocham, ambako inasemekana kuwa hali yake inaendelea nzuri.

    "Hadi sasa hakuna aliyekamatwa kwani vijana hao walikimbia

    lak in i tumeanzisha uchunguzi juu ya suala hilo," alisema mkuu wa kituo Mayek.

    M k u u h u y o a m e d a i w a k u s e m a k u w a w a t a c h u k u a maelezo zaidi kutoka k w a S h e i k h h u y o mara tu atakapoweza kuzungumza na polisi.

    W a t u h u m i w a w a l i r i p o t i w a k u m s h a m b u l i a p i a mwal imu mkuu wa shule, ambaye alijaribu kuingilia kati kumuokoa Sheikh Bahero.

    " T u n a s h u k u kwamba vi jana hao w a l i o m s h a m b u l i a S h e i k h B a h e r o wamepandikizwa siasa kali , lakini bado ni mapema kwangu mimi k u wa u n g a n i s h a n a

    ghasia za Masjid Mussa," aliongeza Mkuu wa kituo cha polisi huko Mombasa Bw. Mayek, akirejea vurugu zilizosababisha kumwagika damu kati ya polisi na vijana wa Kiislamu wanaodaiwa kupandikizwa siasa kali katika msikiti huo mapema mwezi wa Februari.

    S h e i k h B a h e r o amekuwa akifundisha kwenye Madrasa Fathil Adhym na madrasa ya Kisauni , na p ia a l iwahi kukamatwa na polisi muda mfupi n a p o l i s i m w a k a 2 0 1 1 a k i t u h u m i wa kuwaandikisha vijana kwa ajili ya al-Shabaab, tuhuma ambazo Sheikh huyo alizikana.

    VIONGOZI wa UAMSHO katika picha ya pamoja.

  • 4 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Makala

    M A D A I m a z i t o w a m e r u s h i w a wanasiasa wa Zanzibar wanaopigania kubaki k w a m u u n d o w a muungano wa serikali mbili.

    Madai yanayotolewa

    Pamoja na kauli ya Jussa...

    Wasiwasi wazidi Zanzibarbaadhi watuhumu usaliti

    Vibonzo vyasambazwa mtandaoniSeif Khatib arejea siasa za Upemba

    Na Mwandishi Wetu ni kuwa wanaoipigia debe sera ya Serekali mbili wana agenda ya siri ya kuidalali Zanzibar kwa kulinda maslahi yao binafsi.

    M i o n g o n i m w a wanaotajwa kushika bango la serikali mbili ni pamoja na Mheshimiwa

    Seif Khatibu na Ali Karume.

    M a o n i ya n a m n a hii yanakuja kufuatia juhudi za baadhi ya wanasiasa wa Bara na Visiwani, hasa kutoka Chama Cha Mapinduzi, CCM, kutamka wazi kuwa wanapigania kuendelea na mfumo wa muungano wa serikali mbili.

    Akizungumzia suala hilo, Mjumbe wa Bunge la Katiba na aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa R a i s ( M u u n g a n o ) , Mheshimiwa Mohamed Seif Khatibu amesema muundo wa Serikali tatu, hautaisaidia nchi, bali ni njia ya mzunguko ya kuvunja Muungano.

    Alisema hayo mjini Dodoma hivi karibuni akiongea na baadhi ya vyombo vya habari ambapo al ibainisha kuwa, kuna kila sababu ya kulinda Muungano a m b a o u n a p e l e k e a Watanzania Bara na Zanzibar, kuishi kwa uhuru bila kubaguana.

    Mohamed Seif Khatib akitoa maoni yake, anaonekana kurejea yale yale ya kale ya kuwagawa Wazanzibari kat ika makundi ya Wapemba na Waunguja pale a l i p o s e m a k u w a W a p e m b a n d i o wanaotaka muungano wa Mkataba.

    Na kwamba lengo ni kuvunja muungano na kisha kudai kuwa

    h a t a w a n a o s e m a serikali tatu, haisaidii kuimarisha muungano zaidi ya kuwa ni njia ya mzunguko ya kuuvunja.

    Akionyesha kuwa Zanzibar ndiyo inayo f a i d i z a i d i k a t i k a muungano kuliko Bara akasema kuwa hata usafi ri unatoa fursa zaidi kwa Zanzibar kuliko Bara usafi ri wa boti ni mara nne kwa siku.

    Na kwamba fursa nyingi zinapatikana Bara kama maeneo ya kulima na kufuga. Zanzibar unapata eka 3, lakini ukija Bara unapata hata eka 10,000. Kuna masuala ya afya ambayo yanatolewa bila kubagua.

    Kwa mujibu wa madai hayo yaliyosambazwa k a t i k a b a a d h i y a mitandao ya kijamii, i n a e l e z wa k u we p o k w a m a d a l a l i w a kuiangamiza Zanzibar kupi t ia mfumo wa Serekali mbili.

    Inadaiwa kuwa mfumo huo unainawir i sha B a r a ( Ta n g a n y i k a ) i l iyojivika ngozi ya Tanzania huku Zanzibar ikizidi kupokonywa

    Inaendelea Uk. 16

    P.O. BOX 72045, Dar es Salaam, TANZANIA. TEL+255 0655 654900, +255 752 245446. Email: [email protected], Web: www.tampro.org

    CAREER GUIDANCE KWA WAHITIMU WA KIDATO CHA SITA

    JUMUIYA YA WATAALAMU WA KIISLAMU TANZANIA (TAMPRO) INAWAALIKA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA KUHUDHURIA KATIKA CAREER GUIDANCE JUU YA UOMBAJI WA UNDERGRADUATE SCHOLARSHIPS NJE YA NCHI. PIA, FURSA ZA UFADHILI ZILIZOPOKELEWA NA TAMPRO ZITATANGAZWA. SIKU: IJUMAPILI TAREHE 30/03/2014 MUDA: SAA 3:00 ASUBUHI 6:00 MCHANA WASICHANA SAA 8:00 MCHANA 10:00 JIONI - WAVULANA MAHALA: CHUO CHA UALIMU SAFINA, BOKOBASI HAYA, DAR ES SALAAM PIA WALIOSOMA ELIMU YA DINI YA KIISLAMU WAKIWA NA VYETI WANAOMBWA WAHUDHURIE. TAFADHALI UKIIPATA TAARIFA HII WAARIFU NA WENGINE KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NASI KWA NAMBA: 0716 234391, 0652 212672, 0688 130828 AU EMAIL:

    [email protected], [email protected]

    Ngoi Kayeko MKURUGENZI MTENDAJI

    NB: KUTAKUWA NA CHAKULA CHA MCHANA KWA WASHIRIKI WOTE

    BW. Seif KhatibuBW. Ismail Jussa

  • 5 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Habari za Kimataifa

    SERIKALI ya Canada i m e t a n g a z a r a s m i kuondoa wanajeshi wake wote waliokuwa nchini Afghanistan, hivyo kuhitimisha ushiriki wake katika harakati mapambano nchini Afghanistan.

    Hatua hiyo imekuja baada ya kufungwa mafunzo ya kijeshi kwa Wanajeshi wa Serikali ya Karzai kwenye uwanja wa Ndege mjini Kabul.

    Bendera ya Canada iliteremshwa rasmi siku ya Jumatano iliyopita baada ya kufanyika sherehe fupi kwenye kambi ya wanajeshi wa wa NATO mjini Kabul.

    Kwa muda wa miaka 12 Serikali ya Canada imekuwa mshirika wa

    Shehena ya kwanza ya misaada ya kibinadamu kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kwa Waislamu wa Jamhuri ya Afr ika ya Kat i imewasili kwa nde3ge maalum katika kambi ya wakimbizi wa nchi hiyo iliyopo nchini Chad.

    S h e h e n a h i y o iliyotumwa na Jumuiya ya Hilali Nyekundu ya Iran, inajumuisha mahema, mablanketi, d a w a n a v y a k u l a i m e t u m w a k w a

    Maimamu na walimu wa madrasa wapatao mia moja kutoka maeneo mbalimbali ya Zanzibar, wa m e s h i r i k i k a t i k a kongamano maalum la Kiislamu lililoandaliwa na Kituo cha Kiislam cha Markaz Changombe cha jijini Dar es Salaam kwa kushirikana na Ofisi ya Mufti ya Zanzibar, lililofanyika Jumamosi iliyopita visiwani humo.

    M a d a z a m d a h a l o h u o u l i o k u w a n a anuani ya umuhimu wa mazungumzo ka t ika kupiga vita ubabe na ugaidi, ziliwasilishwa na Mashekhe wa Markaz na wa Zanzibar miongoni mwao wakiwa ni Mufti wa Zanzibar Sheikh Swaleh Omari Kaabi na Katibu wa Mufti Sheikh Fadhili Solaga, ambaye aliongoza Kongamao hilo.

    Wengine ni Mkurugenzi wa Markaz Changombe ya Dar es Salaam Dk. Osama Mahmoud Ismail ambaye alizungumzia juu ya umuhimu wa mazungumzo ka t ika kuzungumzia Uislamu sahihi.

    Aidha aliandaa mada

    Canada yaondoa majeshi yake Afghanistanvita vinavyoendelea nchini Afghanistan. Hata hivyo baada ya k u k a m i l i s h a k a z i ya kuondoa v ikos i vyake vi l ivyodumu

    Afghanistan kwa miaka mitatu, sasa imetamka r a s m i k u w a o n d o a wanajeshi wake.

    C a n a d a i l i t u m a w a n a j e s h i w a k e

    Afghanistan mwaka 2001 kushir iki vi ta dhidi ya wapiganaji wa Taliban, ambapo vituo vyao vilikuwa kwenye mikoa ya kusini mwa

    Afghanistan, hususan mkoa wa Kandahar.

    Mpaka sasa Canada i m e k i r i k u p o t e z a wanajeshi 158 katika vita nchini Afghanistan.

    Misaada kwa Waislamu wa Jamhuri ya kati yawasili Chadwakimbizi wa Kiislamu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wanaopewa hifadhi nchini Chad.

    Umoja wa Mataifa n a m a s h i r i k a y a kimatai fa ya kutoa misaada ya kibinadamu, yamekuwa na wasiwasi kuhusu uwezekano wa kujitokeza balaa la njaa na mauaji ya kimbari yanayofanywa na wanamgambo wa Kikristo wa Anti Balaka dhidi ya Wais lamu nchini humo.

    Markaz wafunda Maimamu ZanzibarNa Mwandishi Wetu juu ya umuhumu wa

    m s a m a h a n a k u p i g a vita ubabe kwa kueneza utamaduni wa Uislamu katika jamii.

    M a d a n y i n g i n e z i l i z o wa s i l i s h wa n a k u j a d i l i w a k a t i k a kongamano hilo ni somo kuhusu kuvuka mipaka sio tabia ya Uislamu na suala la ulazima wa kuwahifadhi watoto wasiingie katika ufahamu mbaya.

    Dk. Osama alitoa fikra ya mwanzo juu ya maana ya msamaha wa Uislamu, ambapo alisema kwamba unalingania upole na ulaini na wala haulinganii ubabe wala kuvuka mipaka na ugaidi. Alisema masuala hayo yote yapo nje ya mtazamo wa Uislamu.

    S h e i k h A b u b a k a r i Suleiman, mmoja wa walimu wa Markaz ya Kimisri alitoa fikra zake juu ya malezi ya watoto katika ufahamu sahihi na kuwaepusha na ufahamu mbaya. Alisema iwapo jamii itafumbia macho suala la malezi sahihi, basi hali itazidi kuharibika.

    Hivyo alishauri uwepo m j a d a l a wa k i n a i l i kulipatia ufumbuzi tatizo la malezi katika jamii.

    Elimu sahihi ni moja ya hoja zilizojadiliwa katika kongamano hilo

    kama ilivyonukuliwa aya ya Mwenyezi Mungu anaposema Waulizeni wanaojua kama nyinyi haumjui

    Aidha wajumbe katika kongamano hilo walitaka kujua pia maana ya ugaidi. Dk. Ismail alisema ugaidi ambao wanauzungumzia watu wengi duniani

    siku hizi, hauna maana nyingine isipokuwa ni kuwatisha watu wenye amani na kuwaogopesha waliotulia na kuwatikisa na kuondoa amani katika miji ambayo ipo katika utulivu.

    Alisema yote hayo ni makosa makubwa katika Uislamu na kinyume

    cha makusudio ya kuja Uislamu.

    Mwisho wa kongamano Sheikh Swaleh Omari Kaabi, Mufti wa Zanzibar alifunga mdahalo kwa kuishukuru Markaz ya Kimisri nchini Tanzania kwa kutoa elimu sahihi ya dini na chuo cha Azhari Sharif kwaz kuwasomesha watanzania.

    Kituo cha kiislamu cha Misri nchini Tanzania (Markaz) kimefanya kongamano la Kidini Zanzibar mada ilikuwa umuhimu wa mazungumzo katika kupiga vita ubabe na ugaidi kongamano hili limefanyika hivi karibuni.

    RAIS wa Mpito JAK, Catherine Samba Panza.

  • 6 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Makala

    AFRICA MUSLIMS AGENCY

    )TANZANIA OFFICE( DIRECT AID

    aid.org-Tanzania@directMAIL: -P.O.BOX 9211 DSM E TANZANIA OFFICEAFRICA MUSLIMS AGENCY,DIRECT AID 787486666MOBILE: 255 [email protected]

    Africa Muslims Agency -Direct Aid -is an international organization based in Kuwait with regional offices in a number of African countries. The organization is mainly concerned with uplifting the standards of the needy

    through education. Thus it has set up a number of schools from primary to universities in a number of African countries.

    To accomplish its set goals it looks forward to recruit intellectuals in the field of education to fill the available vacancies.

    Job Title: Education Supervisor Job Station: Tanga and Moshi Available Positions: 2 posts

    Roles and Responsibilities Complies with state administrative regulations and Board of Education policies Adheres to school and local school system procedures and rules Demonstrates timeliness and attendance for assigned responsibilities Maintains accurate, complete, and appropriate records and files reports promptly Preparing weekly and monthly reports and ensure timely submission of reports to the administration Assist in recruitment and in service training of teachers Evaluate teaching techniques and suggest means of improving them Visit classrooms to see effectiveness of teaching and teaching materials. Conduct seminars and workshops to teachers to demonstrate new teaching methods, teaching materials

    and teaching. To provide to teachers teaching materials and all necessary equipments for teaching process.

    Qualifications

    A holder of degree in education with any specification Has at least two years in teaching or similar position with good track record Must be willing and available to work in Tanga or Moshi

    Strong leadership, communication, interpersonal, and organizational skills Computer application skills. Experience in working with donor funded projects. Excellent written and oral communication skills in English and Kiswahili, including report writing. Excellent networking and organizational skills Self motivated person

    Mode of Application Send your Application including application letter, CV and copies of certificates to:

    The Director Africa Muslims Agency

    P o Box 9214

    Dar es Salaam

    aid.org-tanzania@directOr Email:

    Deadline: Two weeks after first advertisement.

    Wasiwasi wazidi Zanzibarbaadhi watuhumu usaliti

    Inatoka Uk. 4utambulisho wake hal i inayotishia uwepo wake kama nchi.

    M a d a i h a y o katika mmoja wa mitandao ya kijamii, yameambatanishwa n a k i b o n z o kinachoonyeshwa unaodaiwa kuwa u h u s i a n o w a Ta n g a n y i k a n a Zanzibar katika hali hii ya mfumo wa serikali mbili.

    Tukija katika mfumo huu wa Muungano tulio n a o w a m i a k a 5 0 , we n ye wa o madalali husema huu ni Muungano wa pekee duniani tuenzi, tuulinde na tuudumishe kwa nguvu zetu zote.

    Sasa tujiulize ndugu zangu Wana wa Zanzibar, ni nchi gani au mshirika gani alio ungana na

    kama tuliungana na Tanganyika kwa nini inapigwa vita Tanganyika kurudi? Hii ndiyo agenda ya kunyongwa na kuuliwa Zanzibar kimbinu na wauaji wakubwa sio watu wa mbali ni hao hao Wazanzibar wenyewe wenye kusaka tonge kwa migongo ya nchi.

    Hayo ni baadhi ya madai ya baadhi ya watu wanaotaka m a b a d i l i k o k a t i k a m u u n d o w a m u u n g a n o w a k i r u s h a tuhuma kwamba wanaongangania m f u m o u l i o p o wana agenda ya siri ambayo hatimaye ni kufanya Zanzibar i p o t e z e k a b i s a uwepo wake.

    T u s i s a h a u kuwa kutokuitetea Z a n z i b a r y e t u

    n a t u k a w a n a mgawanyiko, basi wabeba lawama wakubwa watakua ni madalali ambao t u n a m j u a m o j a baada ya mwengine, k w a i r a b u n a katu hatutokuja k u w a s a m e h e , wacha watumie m a d a r a k a y a o vibaya lakini wajue tu kuwa madaraka ni kitu cha kupita, h a w a t o k u w a viongozi maisha.

    Inadaiwa kuwa huenda Katiba ya sasa ya Zanzibar, i n a y o t a m b u a uwepo wa Zanzibar kama nchi yenye m i p a k a y a k e , i tapanguliwa il i ilingane na Katiba Mpya ya Muungano w a S e r i k a l i mbili kama ndio utakaopita Dodoma ambao kwa hali yoyote, utaondoa

    hadhi ya Zanzibar na kuirejesha kuwa sehemu ya nchi Tanzania, ambayo ndiyo hiyo hiyo Tanganyika.

    Yako mambo tayari yanapikwa jikoni na tutakuja k u j u t a m b e l e n i Wazanzibar ikiwa v i o n g o z i w e t u w a Z a n z i b a r w a t a s h i n d w a kuitetea Zanzibar.

    Imehitimisha na k ut ah adhar i sha moja ya taar i fa iliyotolewa katika mtandao wa kijamii n a k u o n g e z a ikisema:

    Ikiwa Wananchi w a Z a n z i b a r tutacheka cheka t u n a v i o n g o z i w a k o r o f i w a Zanzibar wenye kujali maslahi yao binafsi bila kujali nch i ye tu , bas i tujuwe wananchi wa Zanzibar itakua tumepoteza nchi.

    N a k a t i b a Mpya inakuja na marekebicho ya Ardhi kwa Zanzibar kuwa Mtanzania yoyote anaweza kuishi popote bila kubughudhiwa na... tumemsikia Waziri k a t i k a m a s u a l a ya Muungano Bi Samia Suluhu kuwa kero moja katika kero zinazokuja kufanyiwa kazi ni Wa - Ta n g a n y i k a wajiitao Watanzania kuja kumiliki ardhi Zanzibar.. na katiba ya Muungano ndio itakua kinga yao.

    Mtoa maoni huyo anasema hayo kwa kuzingatia maneno ya Mheshimiwa J a j i W a r i o b a kuwa Katiba ya Muungano ndiyo itakayokuwa juu zaidi kuliko katiba zote, ya Zanzibar (na ya Tanganyika).

    mwenzake halafu mwenzake akaingia kizani na baada ya kuitwa arudi akaja mtu mwengine?

    W a m e h o j i baadhi ya watu w a k i m a a n i s h a k u w a a s i l i y a M u u n g a n o n i Ta n g a n y i k a n a Zanzibar, lakini wakati Zanzibar ipo, Tanganyika i n a k u j a k a m a Tanzania, ikiwa kama mzazi na mwana aliyezaliwa na Tanganyika na Zanzibar.

    H i v i k w e l i s i s i t u l i u n g a n a na Tanzania au Tanganyika? Na

    BALOZI Ali Karume.

  • 7 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Makala/Tangazo

    TANGAZO

    NAFASI ZA MASOMO SUDAN 2014/2015.

    Ofisi ya Munazzamat Al-Daawa Al- Islamiya ( MDI) iliyopo Mbezi Beach-Tangi Bovu jijini Dar es Salaam, inapenda kuwatangazia nafasi za masomo kwa wale wote wanaotaka kujiunga na Chuo Kikuu cha INTERNATIONAL UNIVERSITY OF AFRICA, Khartoum Sudan. Kozi zinazotolewa ni;

    1. Shahada ya kwanza katika Medicine, Pharmacy, Dentist, Nursing, Laboratory Sciences, Natural resources, Petroleum and Minerals, Engineering, Electronics & electrical Engineering, Computer Science, Pure Science, Applied chemistry, Microbiology, Geology, Physics na Computer with Mathemtics.

    2. Shahadaya kwanza katika Law & Sharia, Islamic studies, Economics, Administration, Political Science, Education Administration and technology, Curriculum & Methods of Teaching, Arts (Mass communication, Arabic, Geography, History, and General Psychology).

    3. Ualimu ngazi ya Diploma Fomu za maombi zinapatikana kwa Tsh 10,000/= tu, kuanzia tarehe 29 March mpaka tarehe 10 April 2014 DAR ES SALAAM: katika ofisi ya Munazzamat iliopo Tangibovu- Mbezi Beach. MWANZA: Msikiti wa Rufiji uliopo Mtaa wa Rufiji na ZANZIBAR: katika ofisi ya Munazzamat (Kituo cha kusaidia mayatima) kilichopo eneo la Mpendae kwa mchina mwisho, mkabala na skuli ya Kijangwani, saa 3:00 asubuhi mpaka saa 7:00 mchana. Kutakuwa na Mtihani (Oral Interview) tarehe na mahali utapewa pale utakapochukulia fomu. Sifa za mwombaji:- Awe amemaliza kidato cha Nne na sita au Thanawiya kwa kupata daraja la kwanza, la pili au la tatu.Pia mwombaji lazima alete Vyeti halisi (Original academic certificates) Result sleep haikubaliwi. Kwa maelezo zaidi piga simu:- Makao makuu, Dar es Salaam: 0786 806662 au 0652 806662 au 0715249015 au 0787 121283 Kituo cha Zanzibar simu no: 0777415835 au 0715 415835. Kituo cha Mwanza simu no: 0688 216644 au 0782 382434 au 0762 498913

    Mr. Khamisi M. Liyenike K.n.y. Mkurugenzi, MDI, TZ

    Na Rafaat Salah al-Din, Mchambuzi wa masuala ya Afrika

    (Jumamosi, February 22, 2014)

    Chini ya mkataba wa Libreville wa mwezi Januari mwaka jana, m o j a y a m a m b o muhimu yaliyotajwa ni kuwa Uislamu uwe na nafasi muhimu miongoni mwa dini z i n a z o t a m b u l i w a rasmi, hivyo siku kuu mbili kwa Waislamu, Idd el Hajj (au Idd el Adha) na Idd el Fitr

    Nini kilisababisha mkasa Jamhuri ya Afrika ya Kati? (2)zitambulike rasmi kuwa ni za kusherehekewa, na s iku hizo ziwe s i k u k u u k i t a i f a . Waislamu wasitishiwe au kupata misukosuko ya kisheria hasa pale wanapohitaji kupata hati za vitambulisho, kwani kutoa hati ya kusafiria kwa Muislamu ilikuwa haiwezekani, ila kwa taabu.

    Mtu aliyesimamia mapendekezo hayo alikuwa mjumbe wa kundi la Seleka. Bw. H a s s a n O t h m a n , ambaye ni mmoja wa viongozi wa Waislamu

    n a m w a n a z u o n i mwenye shahada ya pili ya uchumi kutoka C h u o K i k u u c h a Bangui, lakini akapotea baada mazungumzo k u m a l i z i k a k a t i k a hali ya kutatanisha n a k i l i c h o m p a t a hakijafahamika hadi sasa.

    I s i t o s h e , s e r i k a l i haikuchukul ia kwa umakini madai haya na haikuyatekeleza kama ilivyokubaliwa katika makubaliano ya Libreville, na hii ikaipeleka nchi katika uhasama wa wazi.

    Hivyo, vikundi viwili v i k a u n g a n a k a t i k a mfungamano uitwao Seleka - au mkataba' katika lugha ya Sengo ya eneo hilo - kupitia kuungana na kula kiapo kuiondoa madarakani serikali ya Bangui. Kwa msingi wa hatua hiyo, mfungamano mpya wa Seleka ukapata kuungwa mkono kwa nguvu na wassi wa Sudani Kusini na Chad, kwa masharti kuwa mfungamano huo utawaunga mkono wapinzani hao dhidi ya serikali hizo wakichukua madaraka.

    Cheche ya kwanza: Azimio la Umoja wa M a t a i f a l i l i t o l e wa asubuhi ya mauaji (ya

    Wais lamu) kuunda serikali mpya l icha ya kuwa askari wa Ufaransa wal ikuwa wameshafika Jamhuri ya Afrika ya Kati kabla ya kuruhusiwa na Baraza la Usalama.

    Cheche ya kwanza ya mapigano ilianza Machi 2013, na wapiganaji w a S e l e k a w e n g i wa k i wa Wa i s l a m u walifaulu kumwondoa m a d a r a k a n i R a i s Mkristo Francois Bozize, ambaye sasa anaungwa mkono na wapiganaji wa Pinga Balaka wa Kikristo ambao wanaungwa mkono na Ufaransa.

    Kwa makisio kadhaa, wapiganaji wa Seleka wako kiasi cha askari 25,000 wakiongozwa na rais wa kwanza Muislamu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Michel D j o t o d i a , a m b a y e alisimikwa kama rais wa mpito Agosti 18, 2013 baada ya majeshi yake ya Seleka kuukamata mji mkuu na Ikulu, kulazimisha kuondoka kwa Rais Francois Bozize.

    Serikal i ya mpito iliundwa kutokana na mawaziri 29, ikiwa ni pamoja na mawaziri wa nchi, na kwa mara ya kwanza katika historia

    Inaendelea Uk. 9

  • 8 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Makala

    Abiria 239 wapo wapi?NI wiki ya pili leo, siku 14 kamili, toka ndege ya Malaysia, Boeing 777-200 ER ipotee.

    Ikiwa na abiria 239, ndege hiyo Flight no. MH 370 ilipotea Machi 8, ikiwa njiani kuelekea Beijing, China ikitokea Kuala Lumpur.

    Juhudi za kuitafuta

    Na Mwandishi Wetu

    njia ambayo haikuwa ndiyo ya kawaida kupita kuelekea Beijing.

    Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri Mkuu wa Malaysia, Najib Razak, Jumamosi, iliyopita, mawasiliano

    mwa Bahari ya Hindi na pengine ikaishiwa mafuta na kuanguka baharini.

    K a m a n i h i v y o wanasema, i takuwa vigumu sana kuipata kutokana na kina cha

    been no trace of the plane, nor any sign of wreckage.

    Wanasema wataalamu wakimaanisha kuwa, kawaida ndege ikishapaa na kufika angani na kuchukua uelekeo wa inakokwenda, si kawaida

    safari yake Novemba 7, 1872 kikitoka New York kuelekea Genoa, Italy kikiwa na abiria 10.

    Wiki nne baadae, c h o m b o h i c h o kilionekana kikielea Rasi ya Gibralta (Strait of Gibraltar), bila ya abiria wake.

    Mizigo yote ilikuwepo, kasoro watu na boti ya uokozi wakati wa dharura (lifeboat). Mpaka hivi leo haijajulikana nini kiliwasibu abiria wale.

    What's the deal with the Bermuda Triangle? Hili ni swali linalosimulia kisa kingine ambapo ndege za k iv i ta za Marekani zikiwa na watu 14 zilipotea Desemba 1945 pwani ya kusini mwa Florida.

    Askari wengine 13 waliotumwa kwenda kuwatafuta waliopotea, n a o w a l i t o w e k a b i l a k u j u l i k a n a walipotokomea hadi hii leo.

    Eneo hi lo ambalo l i n a f a n y a p e m b e t a t u ( t r i a n g l e ) i n a y o u n g a n i s h a Bermuda, Florida na Puerto Rico, hutajwa kama lenye miujiza.

    Ni katika eneo hilo ambapo ndege mbili za abiria za Uingereza na Amerika ya Kusini (British South American Airways), zilitoweka mwaka 1948 na 1949.

    Hakuna mabaki ya ndege hizo na abiria wake yaliyoonekana hadi hii leo.

    Inasemekana zipo pia meli za mafuta zilipata kutoweka katika eneo hilo.

    Kutokana na rekodi h i y o , v i t a b u v i n g i vimeandikwa kuelezea eneo hilo kuwa ni la maajabu.

    Miongoni mwa vitabu hivyo ni "The Devil's Triangle," "Limbo of the Lost," na "The Riddle of the Bermuda Triangle."

    Maelezo yanayotolewa k a t i k a m a a n d i k o mbalimbali ni kuwa hilo ni eneo la miujiza au lenye viumbe wa ajabu ambao inakuwa ndio sababu ya kutoweka kila meli/ndege na watu wanaopita hapo.

    ndege hiyo zikihusisha wataalamu na vyombo m a a l u m , k u t o k a Marekani na China, hadi sasa hazijaonyesha dalili yoyote ya kutambua ilikopotelea ndege hiyo.

    S i b a h a r i n i wa l a nch i kavu ambapo rada na vifaa maalum v i m e t a m b u a , j a p o uwepo wa dalil i za mabaki ya ndege hiyo kama i l ianguka au vinginevyo.

    I n a e l e z w a k u w a masaa kadhaa baada ya ndege hiyo kuruka, ilipoteza mawasiliano na waongoza ndege na ikawa haionekani kabisa katika rada.

    Baadae ikafahamika kuwa ndege ilibadili mwelekeo na kuchukua

    yaliyonaswa kupitia satellite yanaonyesha kuwa ndege ilibadili m w e l e k e o , l a k i n i bila kuonyesha hasa ilikoelekea.

    Inaaminika kuwa mitambo ya mawasiliano na waongoza ndege i l iz imwa makusudi ndani ya ndege hiyo, na hivyo kuibua wasiwasi kuwa huenda ndege hiyo ilitekwa.

    Lakini hata kama ilitekwa, bado swali linakuwa imekwenda wapi?

    Ta a r i f a z a a wa l i z a w a c h u n g u z i wa K i m a r e k a n i n a Uingereza zinasema kuwa huenda ndege hiyo iligeuza mwelekeo na kuelekea kusini

    bahari hiyo.Bahari ya Hindi ina

    kina cha urefu wa futi 12,000 sawa na maili 2 (kilometa 3.5).

    Kina hicho ni kirefu kuliko kile cha bahari ya Atlantic ambapo i l i c h u k u a m i a k a miwili (2) kugundua yalipokuwa mabaki ya ndege ya Ufaransa (Air France) il iyotoweka mwaka 2009.

    It is extremely rare for a modern passenger aircraft to disappear once it has reached cruising altitude, as MH370 had. When that does happen, the debris from a crash is usually found relatively quickly, close to its last known position.

    In this case, there has

    kabisa kupotea katika rada, na hata ikipata ajali ikianguka, basi inakuwa wepesi kuona mabaki yake.

    N i k u t o k a n a n a hali hiyo, kitendawili kinachozunguka iliko ndege hiyo na abiria w a k e , k i m e f a n y a watu kurejea matukio ya nyuma na kuibua matukio mengine kama hayo katika historia a m b a p o , z i l i w a h i kupotea ndege na meli mpaka sasa hazijulikani zilipo na watu wake.

    Moja ya matukio yanayotajwa ni l i le l i l i l o p e w a j i n a l a The ghost ship Mary Celeste.

    Hiki ni chombo cha baharini kilichoanza

    NDEGE ya Shirika la Ndege la Malaysia Air Line inayosadikiwa kupotea.

  • 9 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Makala

    Nini kilisababisha mkasa Jamhuri ya Afrika ya Kati? (2)Inatoka Uk. 7

    ya nchi hiyo wizara 14 zilitolewa kwa mawaziri Waislamu. Na zaidi, wizara moja muhimu ilikabidhiwa kiongozi wa Waislamu Nouraddin Adam. Rais Djotodia, ambaye alikuwa na timu ya washauri ambao wengi ni Waislamu, al ikutana na kundi la wafanyabiashara, wabunge na wanazuoni Waislamu na kutokana nao baraza la mawaziri liliundwa.

    Mnamo Septemba 13, 2013 Rais Djotodia alivunja rasmi kundi la wapiganaji wa Seleka na kutangaza kuingizwa kwa baadhi yao katika jeshi la taifa.

    Viongozi wa nchi za magharibi walichukiwa n a n g u v u a m b a y o Wais lamu wal ipata c h i n i ya D j o t o d i a kwani ras l imal i za fedha hazikuwa tena c h i n i ya m a wa z i r i wa Kikristo, ambao walikuwa wanatumia raslimali hizo na nafasi zao kujenga makanisa n a s e m i n a r i . H i i inathibitisha kuwa kuna msukumo wa kidini katika uingiliaji kijeshi wa Ufaransa katika koloni lake la zamani la JAK.

    Uingiliaj i kati wa kimataifa ulifanyika kuzuia hatua zilizokuwa z i n a c h u k u l i w a n a Wais lamu kuingiza madai yao ya uhuru na haki za msingi kuhusiana na makubal iano ya Libreville. Njama hizo ziliongozwa na Ufaransa ambayo ilipata kibali cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuingilia kati nchini humo, ikaingiza kiasi cha askari 1,600 hapo Desemba 5, 2013, Rais Hollande akatembelea

    kwa muda mfupi Bangui hapo Desemba 10.

    Vikosi vya Ufaransa vilijiunga na askari 6,000 wa kulinda amani wa Kiafrika walisambazwa kote nchini. Kulikuwa na hisia kuwa majeshi ya Ufaransa yangeingia ili kumwondoa Rais Djotodia al iyekuwa a n a u n g w a m k o n o n a S e l e k a b i l a k u m w a g a d a m u , lakini hawakufanya hivyo. Badala yake, askari wa Ufaransa wa l i wa n ya n g ' a n ya silaha wapiganaji wa Seleka, bila majadiliano yoyote ya kisiasa na mfungamano wa Seleka au kuweka mipaka kwa vitendo vya mgambo wa makundi mengine ambayo hayana tofauti kat ika vi tendo vya kinyama ukilinganisha n a S e l e k a ; h a l a f u , serikali ya Djotodia ilidhaifishwa kijeshi na hapakuwa na uungwaji mkono wa kisiasa kwa chama chochote.

    Waislamu waachwa b i l a u l i n z i : H a t u a z i l izochukul iwa na askari wa Ufaransa ziliwaacha Waislamu bila ulinzi mbele ya mgambo wa Kupinga

    Balaka. Mfungamano wa Seleka haikubaki madarakani kwa muda mrefu, hadi makundi mengine kuanza kuunda mgambo kuanzia ngazi ya v i j i j i k u j i l i n d a , ambayo ni pamoja na kundi la wakulima wa Kikristo lililoitwa anti-Balaka, wapinzani wa mapanga.

    M a k u n d i k a m a hayo yaliinuka kutoka m i o n g o n i m w a wafuasi wa Rais Bozize k u a n z i a S e p t e m b a 2013 katika eneo la kaskazini magharibi y a J A K k u f u a t i a vitendo vya kiharamia v i l i v y o f a n y w a n a w a p i g a n a j i w a mfungamano wa Seleka na kwa nia ya kuhamisha madaraka kwa rais Mkristo. Halafu ikafuata alfajiri ya Desemba 5, 2013 ambako serikali iliangushwa kitaaluma kwa ushirika wa askari wa Ufaransa, Cameroon na Sudan Kusini, na kuungwa mkono na makasisi.

    Waislamu waliuawa k a t i k a m a e n e o ya Boeing kulifanya jeshi la JAK lielekeze macho kwingine, na kuondoka k a t i k a m a e n e o

    lili lokuwa linalinda kuzunguza Ikulu, hali ambayo i l iwezesha makundi ya mgambo pinzani na askari wa kukodiwa kuvamia Ikulu na majumba ya redio na televisheni, na kutangaza kuangushwa kwa seriakali kwa njia za kijeshi.

    Askari wa Ufaransa walikuja kukamilisha lilichokuwa kinahitajiwa kuliwezesha tukio hilo lisipingike kokote. Na k u w e k a m a p a m b o ya mwisho, azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likatolewa asubuhi ya mauaji hayo kuunda serikali mpya, ingawa vikosi vya Ufaransa vilishafika JAK kabla ya kupitishwa kwa azimio la Baraza la Usalama.

    Askari wa Ufaransa waliingia miji ya Bouar na Berberati ambayo ina utajiri wa dhahabu na almasi, na Ufaransa i l i p o g u n d u a k u wa maangusho ya kijeshi i l i y o u n g a m k o n o yalikuwa yameshindwa, ilianza kutangaza kuwa kuna vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya Waislamu na Wakristo nchini humo, na kuwa

    askari wa Ufaransa waliingia tu ili kuzuia m a c h a f u k o h a y o kuendelea, na kuwa jumuia ya kimataifa iunge mkono juhudi hizo.

    H a l a f u , h a p o D e s e m b a 9 , 2 0 1 3 askari wa Ufaransa, wa k i s h i r i k i a n a n a wa nchi za Afr ika, waliwapokonya silaha zaidi ya wapiganaji elfu saba wa Seleka na kuweka silaha zao katika makambi tofauti ya jeshi jijini Bangui. Hatua hizo ziliwachukiza Waislamu k w a n i w a p i g a n a j i wa Seleka walikuwa wanawapa ulinzi kiasi fulani dhidi ya mgambo wa Kikristo. Hivyo, Waislamu waliandaa upinzani wa hapa na pale katika mitaa ya jiji hilo kulaani upendeleo w a U f a r a n s a k w a upande wa Wakristo, na kuweka v izuiz i vya mawe na matairi kupinga kusambazwa kwa askari wa Ufaransa. Walisema pia kuwa hatua hizo zinawaacha Wa i s l a m u wa k i wa hawana ulinzi mbele ya mgambo wa Kupinga Balaka.

    Hapo Januari 10, 2014, Jumuia ya Uchumi ya Nchi za Afrika ya Kati (ECCAS) i l i tangaza kujiuzulu kwa Rais Michel Djotodia na akaenda uhamishoni alikotaka mwenyewe, nchini Benin. Halafu, Waziri Mkuu Nicolas T i a n g a y e a m b a y e hakuwa anaelewana na Djotodia, akajiuzulu. H a l a f u B u n g e likamtangaza Catherine Samba-Panza hapo Januari 20 2014 kutoka orodha ya wagombea w a n a n e k u w a mwanamke wa kwanza kuwa rais wa mpito.

    UKATILI wa Anti-Balaka dhidi ya Waislamu Afrika ya Kati.

  • 10 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Makala

    KILA sifa njema na shukrani zote anastahiki M w e n y e z i M u n g u , M o l a w a v i u m b e wote, kwa neema zake a l i z o t u n e e m e s h a , z i n a z o o n e k a n a n a zisizoonekana.

    K a t i k a m a k a l a h i i nitajaribu kubainisha misingi ya tabia katika mtazamo wa dini na namna ya utekelezaji wake katika maisha ya kila siku. Katika kufanya hivyo, nitanukuu aya za Qur'ani pamoja na Hadithi, na baadhi ya fikra na mitazamo ya wanafikra na wasomi katika masuala ya dini na tabia.

    Mwanadamu ni kiumbe mwenye hali mbili za roho na kiwiliwili. Mbali ya kuwa na sifa sawa na walizonazo viumbe wa jamii ya wanyama, lakini pia ana sifa teule na muhimu zinazompambanua na kumtofautisha na viumbe hao.

    Miongoni mwa sifa hizo ni akili, hiyari na utashi wa kimaumbile. Mwanadamu ana karama maalumu yenye nguvu kubwa ya utambuzi wa mambo iitwacho akili, ambayo ina uwezo wa kugundua kanuni kuu za ulimwengu. Kutokana na kugundua kanuni hizo na kuweza kuutumikisha ulimwengu wa maumbile kwa ajili ya maslahi na manufaa yake, mwanadamu amejaaliwa katika kuumbwa kwake kuwa na nyenzo zote zinazohitajika kwa ajili ya ukamilifu wa kiroho na kimaumbile.

    M w e n y e z i M u n g u amempa mwanadamu i lhamu ya kutambua kheri na shari; kwa maana kwamba amemuonyesha ni ipi njia ya uongofu na ipi ya upotofu.

    Kwa kutumia akili na maumbile yake pamoja na muongozo wa Mitume. M w e n y e z i M u n g u Mtukufu ameiashir ia hali hii ya mwanadamu katika Surat Shams Aya ya 7-10, pale aliposema: Na kwa nafsi na kwa aliyeitengeneza. Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake. Hakika amefanikiwa aliyeitakasa ( n a f s i ) . N a h a k i k a amekhasiri aliyeiviza

    Kwa maneno hayo mwanadamu ana uwezo

    Dini kiunganishi kati ya Mwenyezi Mungu na mwanadamuNa Hemed S. Marhoon

    wa kuzipambanua njia mbili hizo, kwa maana u k a m i l i f u h a s a w a mwanadamu hupatikana kwa njia ya hiyari na uelewa. Mwanadamu ni kiumbe mwenye uwezo wa kuchagua na kwa sababu ya kuwa na nguvu hii, huweza kuchagua mahala pake pa kuishi, aina ya maisha anayotaka, dini, kazi yake n.k.

    Kwa kuzingatia kuwa mwanadamu amejaaliwa kuwa na akili ya kuamua, anao uwezo wa kudhibiti matashi na mielekeo yake yote na kuiweka chini ya amri na muongozo wa akili na dini, na kwa njia hiyo kuimarisha shakhsia yake ya kiutu na sifa za ukamilifu wake wa kiroho. Kwa maneno mengine ni kwamba, mwanadamu anaweza kuwa mmiliki wa nafsi yake na kujivua na matashi na matamanio ya mambo yanayomzuia kufikia kwenye ukamilifu wa kiroho, ambayo ndiyo aina bora na yenye thamani zaidi ya uhuru.

    Watu wengi wenye kupendelea mabadiliko ya duniani wameikana dini kwa sababu wanaamini kuwa dini na maisha ya sasa haviendi pamoja. Wanafikiri kuwa kudumaa, kutuama na kutobadilika ni sifa za lazima za mtu mshika dini. Kwa maneno mengine, wanafikiri kuwa hali kama hizo katika dini zinatokana na kutokuwepo

    k wa m a b a d i l i k o n a kwamba, kudumisha hali ya kizamani ndio tabia za dini.

    Kuijenga nafsi ya mtu na kuirekebisha fikra na tabia yake kwa kiasi kikubwa inategemea msaada wa mtu binafsi na jamii, ni jambo muhimu sana na lenye uzito mkubwa kwa jamii yoyote ile.

    Umuhimu wa jambo hili ni mkubwa kiasi kwamba ikiwa mtu atajifunza na kuhitimu elimu zote na kuwa na udhibit i wa nyenzo zote za ulimwengu wa maumbile, lakini kama atashindwa kuidhibiti nafs i yake hatoweza kufikia ukamilifu halisi wa kiutu.

    Hali halisi ilivyo katika jamii nyingi za watu inaonyesha kuwa, suala la malezi ya kitabia ya watu limetupwa na kusahaulika. Licha ya marembo na mapambo yote ya nje ya kuwapumbaza watu yanayoonekana katika ustaarabu wa Magharibi, mmongonyoko wa tabia umekuwa sababu ya kuzuka hali mbaya ya masaibu na kuzifanya jamii za nchi hizo zikabiliwe na majanga ya kila namna ya kimaadili.

    S a b a b u k u b wa ya kupewa mgongo thamani za asili za kiutu, kushamiri ufuska, maingiliano holela ya kijinsia na uhuru usio na mipaka katika jamii za Magharibi, kumeifanya

    misingi ya asili ya maisha ya mwanadamu isahaulike kabisa.

    Ta t izo l a k up uuza suala la malezi ya kitabia, linagusa takribani jamii zote zisizojali maadili ya dini na linashuhudiwa pia ndani ya baadhi ya jamii za kidini zikiwemo nchi za Kiislamu. Na chimbuko hasa la tatizo hili linatokana na ufahamu usio sahihi wa kuuelewa n a k u u j a l i u p a n d e mmoja tu wa hakika ya mwanadamu.

    Katika hali hii na wakati huu, njia ya kumuokoa mwanadamu ni kurejea kwenye mafundisho ya dini. Na ni kwa sababu hiyo ndio maana Mtume wa mwisho wa Mwenyezi Mungu, Nabii Muhammad (SAW) amelieleza lengo la kutumwa kwake kuwa ni kukamilisha fadhila za tabia njema na akafanya juhudi kubwa ya kueneza mafundisho ya tabia kwa maneno na matendo.

    Mwanadamu ni kiumbe a m b a ye u u m b a j i wa ulimwengu umefanywa kwa a j i l i yake yeye , licha ya taarifa chungu nzima zilizokusanywa kuzungumzia sifa na hali ulizonazo mwili wa mwanadamu.

    M w e n y e z i M u n g u (S.W) amelielezea jambo hili katika Kitabu chake kitukufu, Surat Baqara Aya 164, pale aliposema: Hakika katika kuumbwa

    kwa mbingu na ardhi, na kuhitilafiana usiku na mchana, na merikebu zipitazo baharini pamoja na viwafaavyo watu, na maji al iyoyateremsha Mwenyezi Mungu kutoka mawinguni, na kwa hayo akaihuisha ardhi baada ya kufa kwake, na akaeneza h u m o k i l a a i n a y a wanyama, na mabadiliko ya pepo, na mawingu yanayoamrishwa kupita baina ya mbingu na ardhi, bila shaka zimo ishara kwa watu wenye kuzingatia

    Licha ya Magharibi k u p a t a m a e n d e l e o makubwa na ya kila aina, lakini imeghafilika na hakika moja muhimu, nayo ni kwamba maendeleo yote haya ya teknolojia, s a ya n s i n a v i wa n d a pamoja na mashine zote na umuhimu na maajabu yake, vyote hivyo vinapasa vichukuliwe kuwa ni nyenzo tu. Na nyenzo hizi zitumike kwa ajili ya mwanadamu na kwa ajili ya kumuinua yeye ili kumfikisha kwenye ukamilifu na utukukaji wa kitabia.

    Eric Froum, Mtaalamu wa Elimu Nafsia na Sayansi Jamii wa Ki jerumani anasema kuhusiana na suala hili kuwa: "Sisi katika Ulimwengu wa Magharibi n a h a s a M a r e k a n i tumefikwa na janga la kupoteza utambulisho. Sababu ni kuwa katika jamii za viwanda, hakika za watu zimebadilishwa kuwa sawa na kitu; na kitu nacho hakina utambulisho wowote. Ustaarabu wa M a g h a r i b i u m e f i k i a mahala ambapo mapenzi ya vitu vya kimaada, yaani vile visivyo na roho yameenea, na matokeo yake ni kujitokeza namna fulani ya hisia za kutojali na kupoteza hamu na mapenzi juu ya maisha ya mwanadamu na athari zake.

    Katika nadharia hii mwanadamu anafanywa k u wa n d i o m h i m i l i mkuu wa ulimwenguni, fikra yoyote inayohusu masuala ya Metafizikia kama wahyi na dini za mbinguni inapingwa na kutupiliwa mbali. Mfumo huo unaitakidi kuwa uokovu wa mwanadamu u n a p a t i k a n a k u p i t i a f ikra ya mwanadamu mwenyewe tu, na moja kati ya dhana ya mfumo huo ni kwamba ulimwengu wa maumbile ni kitu kilichozuka chenyewe, n a m w a n a d a m u n i s e h e m u m o j a w a p o ya ulimwengu huu wa maumbile ambao kutokea kwake kumetokana na mwenendo wa mabadiliko unaoendelea.

    Itaendelea toleo lijalo

  • 11 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Makala

    MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, amelieleza Bunge la Katiba kwamba pamoja na mambo mengine, suala la muundo wa Serikali tatu ndilo lililochukua sehemu kubwa ya maoni ya wananchi.

    Hayo yamebainishwa J u m a n n e w i k i h i i katika Bunge maalum l i n a l o e n d e l e a m j i n i D o d o m a , w a k a t i M w e n y e k i t i h u y o akiwasilisha rasimu ya Katiba Mpya bungeni humo.

    A l i s e m a s u a l a l a muundo wa Muungano na serikali tatu limechukua nafas i kubwa kat ika mjadala tangu Tume ilipozindua rasimu ya kwanza, likitanguliwa na suala la haki za binadamu.

    Katika suala hili la Muungano, Tume ilipokea

    WANANCHI wa Kuwait kupitia taasisi ya Africa Muslims Agency/ Direct Aid, wametoa msaada wa vi tu mbalimbali unakadiriwa kuwa na thamani ya shi l ingi milioni sitini (60,000,000) z a K i t a n z a n i a , k wa waathirika wa mafuriko yaliyotokea katika vijiji vya Magole na Mateteni, wilaya ya Kilosa mkoa wa Morogoro hivi karibuni.

    Akikabidhi msaada huo kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Joel Bendera , Mwaki l i shi Mkazi wa Shirika hilo hapa nchini Dk. Adam Osman, alisema wananchi wa Kuwait wametoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya kuwafariji waathirika wa mafuriko hayo baada ya kuguswa na hali ngumu ya kimaisha inayowakabili katika makazi yao.

    M s a a d a h u o umejumuisha tani nne za unga wa mahindi, tani nne za mchele, tani mbili za maharage, tani moja

    Kuwait watoa msaada kwa waathirika wa mafuriko KilosaNa Mwandishi Wetu. ya sukari, lita elfu moja

    za mafuta ya kupikia, jozi mia nne za nguo aina ya Khanga, blanket mia moja, magodoro mia moja (100), mabegi mia moja ya shule yenye vifaa mbalimbali vya shule ndani yake, aina mbalimbali za dawa za binadamu na mikeka mia mbili.

    A i d h a D k . A d a m , aliahidi kuwa taasisi yake itachimba visima sita vya maji safi na salama ili kutatua tatizo la maji linalowakabili waathirika wanaoishi katika makazi ya muda.

    A k i p o k e a m s a a d a huo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Bw. Joel N. Bendera, kwa niaba ya waathirika aliwashukuru wananchi wa Kuwait kupitia taasisi ya Africa Muslims Agency/ Direct Aid, kwa msaada huu ambao kwa kiasi kikubwa utawasaidia waathirika hao.

    A i d h a a l i m u o m b a mwakilishi mkazi wa Shirika hilo hapa nchini Dk. Adam Osman kufikisha

    shukurani za serikali ya Tanzania kwa niaba ya waathirika, kwa wananchi wa Kuwait walioguswa na hali ya ndugu zao wa

    Tanzania waliokumbwa na maafa hayo ya mafuriko.

    Bw. Bendera alitumia fursa hiyo kuziomba taasisi nyingine na watu

    binafsi, kuiga mfano wa Africa Muslims Agency/ Direct Aid kutoa misaada kwa wenye kuhitaji kwani bado inahitajika.

    Serikali tatu lachukua sehemu kubwa ya maoni ya wananchiNa Bakari Mwakangwale mawazo ya kila aina, Tume ilianza kazi kwa

    madhumuni ya kupata maoni ya wananchi ili kuboresha Muungano, wa n a n c h i wa l i j i k i t a kwenye muundo kama njia ya kuondoa kero. Alisema Jaji Warioba.

    Jaji Warioba aliyewahi kuwa Wazir i Mkuu n a M a k a m u wa P i l i wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, alisema baada ya kukusanya maoni waliangalia takwimu na kuzichanganua.

    Akianisha mchanganuo w a m a o n i h a y o y a wananchi kwa asilimia, a l i s e m a a s i l i m i a 6 1 , walipendekeza muundo wa serikali tatu, asilimia 24 walipendekeza muundo wa serikali mbili ambapo wale waliopendekeza muundo wa Serikali moja walikuwa asilimia 13.

    A m a k wa u p a n d e wa Zanzibar, alisema asilimia 60, walipendekeza Muungano wa Mkataba na asilimia 34 ya wananchi

    walipendekeza serikali mbili huku asilimia 0.1 wakipendekeza serikali moja.

    Aidha Jaji Warioba, a l i s e m a T u m e p i a ilipata maoni ya Taasisi mbalimbali pamoja na vyama vya siasa, asasi za kiraia na Jumuiya za kidini, ambazo kwa pamoja nazo zilipendekeza muundo wa serikali tatu.

    M w e n y e k i t i h u y o al iongeza kuwa hata baadhi ya Taasis i za Serikali, ama moja kwa moja au kwa tafsiri ya mapendekezo yao pia zilipendekeza au kukubali muundo wa Serikali tatu.

    Kwa mfano alisema, Baraza la Wawakilishi Zanzibar, limependekeza kuwepo kwa mamlaka H u r u y a Z a n z i b a r , M a m l a k a H u r u y a Tanganyika na Mamlaka ya Muungano na iwekwe wazi kat ika maeneo, uwezo, nguvu utendaji na mipaka ya kila mamlaka.

    A l i s e m a B a r a z a l a

    Makamu Ofisi ya Rais l i l ipendekeza kuhusu muundo wa serikali, huku akinukuu mapendekezo hayo kwamba Kuwe na Rais mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wakuu wa Serikali washirika wa Muungano wapewe vyeo vingine kulingana na hadhi na mamalaka zao.

    K w a u p a n d e w a Baraza la Ofisi ya Waziri Mkuu, alisema yenyewe i l ipendekeza kuhusu uongozi wa Taifa, kwamba kuwe na Rais wa Jamhuri wa Muungano, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano Waziri Mkuu wa Serikali ya Tanganyika, pamoja na Waziri Mkuu wa Serikali ya Zanzibar.

    Hata hivyo Jaji Warioba alisema, baada ya kuona t a k w i m u n a s a b a b u zilizotolewa na wananchi na taasisi, Tume iliamua kufanya utafiti wa kina k u h u s u m u u n d o wa Muungano na matatizo yake tangu Muungano ulipoundwa mwaka 1964.

    Alisema wakati huo lugha ya Tanganyika

    kuvaa koti la Muungano ilianza kusikika, ambapo mwaka 1984, kulitokea kile kilichoitwa kuchafuka kwa hali ya hewa Viwani Zanzibar.

    Alifafanua kwamba msingi wa machafuko hayo ilikuwa ni mpango ya baadhi ya viongozi wa Zanzibar, kutaka Serikali tatu ingawa jaribio hilo halikufanikiwa, ambapo Zanzibar ilitunga katiba mpya mwaka huo.

    Katiba hiyo iliweka m a s h a r t i k w a m b a , sher ia za Muungano zipelekwe kwenye Baraza la Wawakilishi kabla ya kutumika Zanzibar na mwaka 1991 Tume ya Nyalali , i l ipendekeza muundo wa serikali tatu.

    A l i s e m a i n g a w a p e n d e k e z o h i l i halikukubalika, Zanzibar iliamua kuwa na bendera pamoja na nembo yake na baadaye sharti likawekwa kwamba, meli zinazoingia k w e n y e b a n d a r i y a Zanzibar ni lazima zitumie bendera ya Taifa zenye nembo ya Zanzibar.

    SEHEMU ya msaada uliotolewa na wananchi wa Kuwait kupitia taasisi ya Africa Muslims Agency/ Direct Aid, kwa waathirika wa mafuriko yaliyotokea katika vijiji vya Magole na Mateteni, wilaya ya Kilosa mkoa wa Morogoro hivi karibuni.

  • 12 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Mashairi/Makala

    Inatoka Uk. 16

    Kundecha ninakuunga, mkono kwa ulonena, Jumanne ulolonga, Bungeni i nzito sana, si kauli ya varanga, ina adhimu maana, Kweli lisanulhali, afswahu kwamaqali ! Bilhaki hukukenga, utendi watakikana, Kwa kanuni mlotunga, kwa utendi zitafana, Kwa kufika mkolenga, kwalo mkishikamana, Kweli lisanulhali, afswahu kwa maqali ! Thakili mbele kusonga, kwa uneni kuzozana,Sahali mbele kusonga, kwa utendi kushindana, Utendi mkiujenga, Bunge lenu litafana, Kweli lisanulhali, afswahu kwa maqali ! Utendi kwa kuuchunga, atawajazi Rabbana, Na kwao mkijitenga, chukizo kwa Subhana, Ikabu itawazonga, kiama ya Maulana, Kweli lisanulhali, afswahu kwa maqali ! Khamsa beti nafunga, lengo si tumbi kunena, Bali mkono kuunga, kauli chanya mwanana, Kundecha aloilonga, filosofiye i pana, Swadakta kwa ulonena, Kundecha haukukenga !

    ABUU NYAMKOMOGI

    BUNGE LA KATIBA (SWADAKTA, SHEIKH KUNDECHA !)

    Upo ukumbusho kutoka Flight MH370h a w a k u j i t o k e z a n a kusema wanataka nini, na wala hapakuwa na ushahidi kama Wairan hao wana uhusiano na kundi lolote lile.

    Pia wapo waliosema k u w a i n a w e z e k a n a imetekwa na viumbe vya ajabu, pengine wakiwemo m a s h e t a n i , h i y o n i mitizamo yao hata, wewe unaweza kuwa na wa kwako juu ya suala hili.

    Wapo pia wanaosema kuwa imepotea tu na huenda ikaonekana hata kama watu wamekufa au wako hai ila itaonekana.

    Tu s i w a s a h a u p i a wale wanaoamini kuwa Allah (sw) ameamua kuwaonesha waja wake kuwa yeye yupo na lile alitakalo ndilo alifanyalo, kama anavyotuambia k a t i k a Q u r a n ; N a ( M w e n y e z i M u n g u ) anapotaka kufanya jambo lolote, basi huliambia tu kuwa basi mara moja likawa (Quran 36:82).

    Wanaamini hivyo kuwa Allah (sw) kasema liwe na ndio hivyo linakuwa, ili kutukumbusha uwepo wake kwani binadamu tumejisahau, dhambi, ubabe, dhulma na mambo mengine maovu ndio tumeyaweka mbele.

    Inaelezwa kuwa hata waganga wa kienyeji wametumika kugundua ndege hii iko wapi, lakini matokeo yakawa hasi, hii ni kuonesha kukata tamaa na teknolojia zao.

    Hayo ndiyo mawazo machache na yenye nguvu katika kesi hii inayogonga vichwa vya magazeti, redio, runinga na hata vijiwe kama si vibaraza vya kunywea kahwa, hiyo ndio hadithi ya mjini.

    Mimi sipingi wazo lolote kati ya hayo kwani yo te yanawezekana . Nimeamua kuleta fikra na mawazo ya watu tofauti kuanzia wasomi na hata tu watu wa barabarani, ambao nikikutana nao nawauliza mawili matatu juu ya hili.

    K a t i y a m e n g i niliyokutana nayo wakati naandaa makala hii, ni maneno ya watu katika mitandao ya ki jamii , wapo waliohoji kuwa sasa zile sentensi za kusema kuwa dunia ni kama kijiji zina maana gani?

    Wanahoji hayo kwani tayari walichokiona ni kuwa kwa teknologia ya sasa, ilikuwa isitimie hata saa 12 tayari ndege

    ingekuwa imeshaonekana kutokana na maendeleo makubwa ya kisayansi na teknolojia.

    M a t a i f a y e n y e teknolo j ia za k isasa yanatafuta ndege hiyo ambayo mpaka namalizia kuandika makala hii, bado hakuna taarifa za kuonekana, wanasema hawajapata dalili zozote kama ipo wapi.

    Kwa tukio hilo tu, wanasema inawezekana kwa kiasi fulani dunia inaweza is iwe ki j i j i . K u t o k a n a n a k i l e kinachoitwa kuwepo t e k n o l o j i a ya k we l i duniani, basi kulitakiwa t u w a s e m e , n d e g e imeanguka au imetekwa ama imetuwa mtaa fulani, hizo ni fafanuzi za watu ambazo nimezikuta katika mitandao ya kijamii.

    Nirudi katika ile aya ya mwanzo inayosema kuwa Pengine hili litakuwa ni somo kwa wanadaum kuwa akili na ubunifu wao sio chochote wala lolote mbele ya Mwenyezi M u n g u a n a p o a m u a kuwaonyesha uwezo wake.

    Kama wapo wanaoamini kuwa viumbe wa ajabu ndio wameichukua hiyo ndege, basi na hata wao wapo chini ya uwezo wa Mungu.

    Hivyo Mungu hufanya lolote atakalo kwa njia yoyote aitakayo, halafu kwako wewe ikawa ni mt ihani ufaulu ama ushindwe.

    Mungu ameamua kutoa somo kama nilivyosema anatukumbusha kuwa yeye yupo.

    N i j a m b o l a kushangaza kuwa dunia i l iyojaa ki la a ina ya teknoloj ia ,wanaadam wanaotoka nje ya dunia na kurudi wanashindwa kuiyona ndege iliyopotea duniani. Kweli hapa yapo mazingatio kwa wenye akaili.

    Nimetumia neno wenye akili, kwasababu ndio wanaokumbuka kama Allah (sw) alivyosema kat ika maneno yake matukufu yaani Quran; Na hawakumbuki i la wenye akili. (Quran 2:269).

    Sasa huenda wenye akili wakakumbuka na wasio na akili hawatokumbuka k a m a A l l a h ( s w ) alivyokwisha sema.

    Na hata Flight MH370 e n d a p o i t a o n e k a n a lakini ukumbusho tayari

    utakuwa umeshawafikia binadam, mambo mengi duniani yanatoa ishara ya uwepo wake, hata janga hili nalo ni hivyo hivyo. Kinachonipa zaidi mdomo wa kusema hivyo ni kutokana na teknolojia tulizonazo, hapa Allah anatuonesha kuwa yeye yupo juu zaidi ya hizo teknolojia tulizonazo.

    N a amet u k uk uk a y u l e a m b a ye k a t i k a mkono wake kuna uweza (Ufalme) juu ya kila kitu. Na kwake Mola wenu n y o t e m t a r e j e s h w a (Quran 36:83)

    Huu ndio ufalme au uwezo wa Mungu juu ya teknolojia tulizonazo nchi zisizopungua 26 zinaitafuta ndege moja kwa kutumia vifaa vya kisasa tena ndani ya dunia hii, ama kweli huu ndio uwezo wake Allah (sw).

    Sema Oh Mnakanusha yule (Mwenyezi Mungu) aliyeumba ardhi na katika siku mbili na mnamfanyia washirika? Huyu ndiye Mola wa ulimwengu wote (Quran 41:9)

    Huyo ndiye Mola wa ulimwengu wote anazijua chochoro sisi tusizo zijua anajua wapi pa kuificha n a s i t u k a t u mi a k i l a tulichonacho kutafuta mwisho tukashindwa, Mola wa ul imwengu kwahiyo kila sehemu kipembe, tambarare , majangwa, mapango n.k yeye ndiye anajua zaidi.

    Kwa hili nimuombe Al lah ( sw) a tu jaa l ie tufunguke macho na t u e l e w e u m u h i m u wake na uwezo wake juu ya dunia hii, wenye kudhulumu wengine w a a c h e , w a s i o m j u a Mungu wamtambue kwa hili lililotokea.

    Pia tumuombe Allah (sw) atuondoshee viburi juu ya viumbe wenzetu na wale wenye matatizo Allah awaondoshee, hali kadhalika wale walio kwenye dimbwi la vita na umwagaji damu Allah (sw) awajaalie mapatano.

    Nimalizie kwa aya hii ya Quran;

    K a t i k a k u u m b wa mbingu na ardhi na kutofautiana kwa usiku na mchana ,ziko (dalili) hoja (za kuonesha kuwepo kwa Mwenyezi Mungu mmoja) kwa watu wenye akili (Quran 3:190)

    E m a i l : rashidalmendhry@yahoo.

    Jumatatu tumeona, cheche za nari Bungeni Nilopata kuunena, huko nyuma nudhumuniSi jambo la kunong'ona, natamka hadharani Msipouziba ufa, mtajajenga ukuta !

    Ni wajumbe walosana, zalo Bungelo kanuni Na kuzipasisha sana, kwa nderemo 'mjengoni' Na kisha kupongezana, wiki jana si zamaniMsipouziba ufa, mtajajenga ukuta !

    Thuma tena kuzikana, hao hao kulikoniKwa kuzidi kuvutana, najiuliza kwanini Kanuni walozisana, maanaye hasa nini Msipouziba ufa,mtajajenga ukuta !

    Migombo na kusigana, na lufufu tafraniYote tusingeyaona, kwa utii wa kanuniKwa kanuni kuzikana, wajitia matatani Msipouziba ufa, mtajajenga ukuta !

    Wajumbe mlozisana, kanuni haja sioni Kukithiri kulumbana, kwa lembelembe uneni Mwapaswa kushikamana na utendi wa kanuniMsipouziba ufa, mtajajenga ukuta !

    Kumbukeni wiki jana, aloinena Bungeni Kundecha ya kiungwana, kauliye ishikeni Utendi hukidhi sana, haja kuliko uneni Msipouziba ufa, mtajajenga ukuta !

    Lengo si mzo kunena, bali kukuhimizeni Pamwe na kukumbushana, mzopitisha kanuni Kwa vifijo wiki jana, ebu zizingatieniMsisubiri kujenga, ukuta zibeni ufa!

    ABUU NYAMKOMOGI SAFARINI MOROGORO.

    BUNGE LA KATIBA (CHUPUCHUPU)

  • 13 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Makala/Tangazo

    KWA mujibu wa Shirika la Afya duniani, tohara (kutahiri) inatakiwa kuwa ni sehemu muhimu katika vita ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi. Watafiti wa masuala ya afya wanadai k u w a k i t e n d o c h a kutahiri kinampunguzia mwanamme uwezekano wa kuambukizwa virusi vya ukimwi anapokutana kingono na mwanamke aliyeathirika kwa kiasi cha asilimi sitini (60%)!

    Katika kitabu chake, al Khitaan, Dk. Muhammad Ali al Baar, ambaye ni mwanachama wa Chuo cha Kifalme cha Madaktari Bingwa wa Upasuaji cha Uingereza, na mshauri kwenye idara ya Tiba za Kiislamu katika Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Mfalme Fahdi katika Chuo Kikuu cha Mfalme Abdul Aziz, kule Jeddah Saudi Arabia, ametaja faida za ziada za tohara inayofanywa kwa watoto wakiwa wangali wadogo kama ifuatavy

    1. Ni kinga dhidi ya maambukizi ya kwenye uume sehemu ya nje;

    2. Ni kinga dhidi ya maambukizi ya kwenye uume sehemu ya ndani (kwenye njia ya mkojo). Ta f i t i z i m e o n y e s h a kuwa asilimia tisini na tano (95%) ya watoto wanaopata maambukizi katika njia ya mkojo ni wale ambao hawakutahiriwa.

    3 . N i k i n g a d h i d i ya saratani ya kwenye uume. Tafiti mbalimbali z i m e b a i n i s h a k u w a saratani ya kwenye uume ni kama haipo kabisa miongoni mwa wanaume ambao wametahiriwa. K a t i k a n c h i m b a z o viwango vya kutahiriwa viko chini kama China, Uganda, na Puerto Rico, saratani za kwenye uume ni kati ya 12-22% ya saratani zote zinazowakumba w a n a u m e !

    4. Ni kinga dhidi ya magon jwa mengi ya zinaa. Watafiti wamebaini kwamba magonjwa ya

    ToharaNa Juma Kilaghai zinaa kama vile gonoria, kaswende, muasho, na

    kadhalika, husambaa kwa kiwango kikubwa zaidi kwa wanaume wasio tahiriwa ikilinganishwa na wale waliotahiriwa.

    5. Ni kinga dhidi ya saratani ya kizazi kwa w a n a w a k e . T a f i t i zimebaini kuwa wake wa wanaume waliotahiriwa wako katika hatari ndogo zaidi ya kupata saratani ya kizazi, ikilinganishwa na wake wa wanaume ambao hawajatahiriwa.

    K w a k u w a h u y o aliyetuumba yote haya anayajua, bila ya shaka ndio maana akafanya k u t a h i r i wa k u wa n i miongoni mwa ibada kubwa kabisa. Mwenyezi Mungu muumba katika Quran 16:123 anatuambia: Kisha tukakufunulia kuwa ufuate mila ya Ibrahim (aliyekuwa) mtii kamili, wala hakuwa miongoni m w a w a s h i r i k i n a .

    I n a j u l i k a n a k u w a s e h e m u m u h i m u ya mila ya Ibrahim ilikuwa ni kutahiriwa. Mtume M u h a m m a d ( S AW ) kuhusu tohara amesema:

    K u n a m a m b o matano ambayo ni ya asili kwa mwanaadamu: K u t a h i r i wa , k u n y o a nywele za k inenani , kukata kucha, kuonyoa nywele za makwapani, na kunyoa sharubu.

    U k w e l i w a k a u l i hii ya Mtume (s.a.w) u n a d h i r i s h w a n a uchunguzi wa tabia za baadhi ya makabila ya asili ya bara la Afrika, kwa mfano Wamaasai na Wakurya. Kitendo cha kuingia jando (kutahiri) kwa makabila hayo ni mila yenye nguvu mno ambayo chimbuko lake halijulikani. K i n a c h o j u l i k a n a n i kwamba mila hii ilikuwepo kwa makabila haya kabla kabisa ya kufikiwa na Uislamu; hivyo makabila haya hayawezi kuambiwa kuwa yamejifunza mila hii kutoka kwenye Uislamu. Kwa hisani ya Ukurasa wa Herbal Impact katika Facebook

    UNIVERSITY COLLEGE OF EDUCATION ZANZIBAR INTERNATIONAL UNIVERSITY OF AFRICA KHARTOUM

    STUDENTS ADMISSION 2014/2015

    The University College of Education invites qualified applicants to apply for the following programs:

    Certificate Programs 1. Information Technology 2. Early Childhood Education 3. Arabic Language 4. Teaching English 5. NTA Level 4 (Science) 6. NTA Level 5(Science)

    Duration and Admission Requirements:1. One year duration for the Certificate program.2. Candidate should have a minimum of four passes in Tanzania Certificate of Secondary School Education OR NVA level 3 as established by VETA or equivalent.3. For NTA Level 4(Science), Candidates should have a minimum of four passes in Secondary School Education Certificate with at least two passes in any science subject.4. For NTA Level 5, candidates should have NTA Level 4 certificate.5. Be a full time student.6. Provide a medical fitness certificate from UCEZ dispensary or any other dispensary approved by UCEZ dispensary.

    Diploma Programs with Education1. English Language 2. NTA level 6(Ordinary Diploma in Science) 3. Computer Science 4. Information TechnologyDuration and Admission Requirements:1 Two years duration.2. Candidate should have at least one principle pass and two subsidiary passes in Advanced Certificate of Secondary School Education. ORFull Technician Certificate with a minimum average of grade D in addition to four passes at O Level. OR NTA level 4 certificate besides four passes at Secondary School Education.3. For Computer Science, a subsidiary pass in mathematics shall be an added advantage.4. Be a full time student.5. Provide a medical fitness certificate from UCEZ dispensary or approved by UCEZ dispensary.

    Mode of Study:Courses shall be conducted in semester system for both certificate and diploma programs.All classes start from 2.00pm to 8.00pm from Monday to Friday. Weekend Session (Saturdays and Sundays) from 08.00 am to 3.00pm

    Commencement date: 21st April, 2014

    Fees Structure:Diploma Programs Tsh. 600,000/=Additional Fees for Computer Courses Tsh 100,000/=NTA Level 4 Certificate Courses:Tuition Fees (Science) Tsh. 500,000/=Additional fees Tsh. 200,000/=Certificate Course:Tuition Fees Tshs. 500.000/=Additional fees for Science students. Tshs. 200,000/=

    Additional Fees:Application form Tshs. 15,000/=Accommodation (optional) Tshs. 180,000/= per annumRegistration Tshs. 30,000/=Student Union Tshs. 25,000/=Computer Services Tshs. 40,000/=Examination fees Tshs. 30,000/=Graduation Tshs. 30,000/=Medical Checkup Tshs. 10,000/=

    Fees is payable in installments.The College reserves the rights to change these fees at any time.Application forms are obtained from:Academic Office, University College of Education Zanzibar at Chukwani P.O. Box 1933 Zanzibar Mobile: 0773774838 OR 0772912181 Email: [email protected] forms are also available from the following offices;- - Africa Muslims Agency, MabaoniChake Chake Pemba: Tel: 024-2452337- Africa Muslims Agency, Tabata - Dar es Salaam: Tel: 022-2807843- Africa Muslims Agency, Kaloleni -Moshi- Africa Muslims Agency, Pongwe- Tanga.From our website: www.ucez.ac.tz

    Application fee should be paid through the following account numbers:- (i) The peoples Bank of Zanzibar (Islamic Banking division) Account No. 51120100002450- Mwanakwerekwe, Zanzibar(ii) Barclays Bank Account No. 003 4000387

    All completed forms together with payment receipts should be returned to the Academic Office, University College of Education Zanzibar.

    The deadline for receiving applications is 4th April, 2014. For further information contact:

    Registrar,University College of EducationP.O BOX 1933, Zanzibar

    MOBILE: 0778698127E.mail:[email protected]

    Visit our main campus at Chukwani, West District, Unguja, two kilometers from the new Parliament Building.

  • 14 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014TANGAZO

    Waislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za kidato cha Tano kwa shule zifuatazo:

    KIRINJIKO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL SAME KILIMANJARO NYASAKA ISLAMIC SECONDARY SCHOOL MWANZA UBUNGO ISLAMIC HIGH SCHOO L DAR ES SALAAM

    Shule hizi ni za Kiislamu zenye lengo la kuwapa wanafunzi taaluma ya hali ya juu na malezi bora ya Kiislamu.Shule hizi ni za bweni za mchanganyiko wa wavulana na wasichana .Zipo Combinations za SAYANSI,ARTS na BIASHARA. Pia wanafunziwote wanafundishwa Islamic Knowledge,Introduction to Arabic na Compyuta..Muombaji awe na Crediti tatu na Pass mbili au zaidi katika mtihani wa kidato cha nne..Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi 10,000/= katika vituo vilivyoorodheshwa hapa chini.

    Arusha - Ofisi ya Islamic Education Panel -Jambo Plastic Ghorofa ya 2 mkabala na msikiti Mkuu Bondeni - 0763 282 371/ 0784 406 610.Kilimanjaro - Moshi: Msikiti wa Riadha 0654 723 418 - Same: Kirinjiko Islamic Secondry School: 0784 296424/0655 697 075Tanga - Uongofu Bookshop: - 0784 982525/ - Lushoto: Mandia Shop - 0782257533Mwanza - Nyasaka Islamic Secondary School 0717 417685/0786 417685 - Mtaa wa Rufiji: Ofisi ya Islamic Education Panel mkabala na Msikiti Al-Amin 0785 086 770.Mara - Musoma: Ofisi ya Islamic Ed Panel -Mtaa wa Karume,Nyumba Na. 0782 868611/0716810002.Kagera - Bukoba: Alhuda Caf Kwa mzee Kinobe karibu na ofisi za TRA. - 0688 479 667 Shinyanga - Msikiti wa Majengo 0718 866869 - Kahama ofisi ya AN NUUR Karibu na msikiti wa Ibadhi: 0753 993930 Dar es Salaam - Ubungo Islamic High School 0712 974428/0684306650 - Manzese :Ofisi ya Annur 0655 677683Morogoro - Wasiliana na Ramadhani Chale :0715704380Dodoma - Hijra Islamic Primary School : 0716 544757/0712 325086Singida - Ofisi ya Islamic Ed. Panel karibu na Nuru snack Hotel 0714285465 Manyara - Babati:Ofisi ya Islamic Ed. Paneli Masjid Rahma 0784 491196Kigoma - Msikiti wa Mwanga Kigoma: 0753 355224. - Kibondo Islamic Nursery School: 0784 442860. - Kasulu: Murubona Isl.SS. 0714710802.Lindi - Wapemba Store: 0784 974041/0786 959663.Mtwara - Amana Islamic S.S 0715 465158.Songea - Msikiti wa NURU 0715 681701/0716791113 - Mkuzo Islamic High School. 0716 791113Mbeya - UYOLE: Duka la vifaa vya Kiislamu nje ya Msikiti wa Uyole 0713 200209 - Rexona Video mkabala na Mbeya RETICO: 0713 200209Rukwa - Sumbawanga: Masjid TAQWA 0717082 073Tabora - Kituo cha Kiislamu Isevya: 0784 944566Iringa - Madrastun Najah: 0714 522 122Pemba - Wete: Wete Islamic Education Center: 0777 432331Unguja - Madrasatul Fallah: 0777125074- Mafia - Ofisi ya ust. Yusufu Ally jirani na msikiti mkuu 0653705627

    6. Pia fomu zinapatikana kwenye Tovuti: wwwipctz.org. ikumbukwe kuwa watakao pata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha

    USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA!

    MKURUGENZI

    WABILLAH TAWFIIQ

    ISLAMIC PROPAGATION CENTREP.O Box 55105,Phone: 0222450069, 0784 267762, 0755 260087 & Fax 022 2450822, Dar es Salaam website :www.ipctz.org

    NAFASI ZA KIDATO CHA TANO 2014/2015

  • 15 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014Habari/Tangazo

    NAFASI ZA DIPLOMA YA UALIMU WA KIARABU JULAI,2014 Waislamu kote nchini mnatangaziwa nafasi za Diploma ya Ualimu wa Lugha ya Kiarabu katika chuo cha Ualimu Kirinjiko kilichopo Same mkoani KilimanjaroLengo la kozi hii ni kuwandaa walimu mahiri wa kufundisha somo la lugha ya Kiarabu katika shule za sekondari na shule za msingi.Muda wa kozi hii ya aina yake ni miaka miwili na itaanza Julai ,2014.Muombaji anatakiwa awe na sifa zifuatazo:

    (a) Awe amehitimu katika chuo cha mafunzo ya Dini na Kiarabu kwa angalau kiwango cha IIdad au zaidi (b) Awe amemaliza kidato cha nne na kupata crediti katika somo la Lugha ya Kiarabu au(c) Awe anayeweza kusoma ,kuandika ,kusikiliza na kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha hata kama hana sifa (a) na (b).

    Waombaji wote watafanyiwa usaili tarehe 10-11,Mei 2014 katika chuo cha Ualimu Ubungo Islamic-Dar Es Salaam .

    Fomu za Maombi zinapatikana kwa gharama ya shilingi ELFU TANO katika vituo vilivyoorodheshwa katika Tangazo la kujiunga na Kidato cha Tano lililopo katika ukurasa wa 14 wa gazeti hili.

    Pia Fomu zinapatikana kwenye Tovuti: www.ipctz.org. Ikumbukwe kuwa watakaopata fomu kupitia tovuti (download) watatakiwa kuzilipia wakati wa kuzirejesha.

    USIKOSE NAFASI HII ADHIMU WAHI KUCHUKUA FOMU SASA!

    Wabillah Tawfiiq

    MKURUGENZI

    ISLAMIC PROPAGATION CENTREP.O Box 55105,Phone: 0222450069, 0784 267762, 0755 260087 & Fax 022 2450822, Dar es Salaam website :www.ipctz.org

    Wenye asili ya Kisomali wana wakati mgumu KenyaInatoka Uk. 16

    kaunti za Garissa, Wajir na hata Mandera, mara kwa mara huripot i juu ya kunyanyaswa k we n ye v i t u o v ya ukaguzi barabarani.

    A l i s e m a k u w a haikubaliki kuwatenga wa t u wa j a m i i ya Kisomali kwa sababu tu wanahisiwa kuwa wanaweza kuchochea hali ya kutoridhika na kutotii.

    Al i sema jami i ya K i s o m a l i i m e k u wa ikiteswa na makundi ya kigaidi, kama vile ambavyo wananchi wengine wanavyoteswa, na kulaumiwa kwa kutofanya chochote kuzuia ghasia hizo.

    Alisema watu wa J a m i i ya K i s o m a l i hawajawahi kusifiwa, l a k i n i w a m e k u w a wakiwasaidia maafisa wa usalama wa Kenya k u t e g u a h u j u m a zinazotishia usalama wa watu.

    "Baadhi ya Wasomali wanaweza kujitolea kutoa taarifa, badala ya maafisa wa usalama kuzifanyia kazi, yule mtu aliyetoa taarifa ndiye anayeshikiliwa na kuhojiwa kinyume cha sheria." Alinukuliwa akisema mbunge huyo.

    M b u n g e w a Kamukunji, ambaye n a y e n i m w e n y e asili ya kisomali Bw. Yusuf Hassan Abdi, ambaye ali jeruhiwa katika mashambulizi ya guruneti mwaka jana karibu na msikiti mmoja kwenye kiunga cha Eastleigh, alisema wamekuwa wakitumia vi tuo vya redio na televisheni kutangaza ujumbe wa amani kwa l u g h a ya K i s o m a l i kuufikia umma.

    M b u n g e A b d i , a n a w a s h a j i i s h a r a i a k u l a k i a n a n a kuzishirikisha jamii n y i n g i n e k w e n y e shughuli mbalimbali.

    Alisema kwa nj ia hiyo, jamii ya Kisomali

    katika eneo la Eastleigh, ambalo analiwakilisha, mara kwa mara hufanya shughuli zinazohusisha jamii nyingine kama vile usafi wa mazingira na mikutano ya dini tofauti.

    Sheikh Mukhtar Abdi,

    Imamu wa Msikiti Nur katika mji wa Mandera, alisema viongozi wa dini pia wamekuwa wakitekeleza sehemu yao ya kuchukua jukumu kwa mchango wao muhimu wa uongozi.

    "Sisi kuhubiri amani na Qur'an kama ilivyo. "Qur'an haitetei vurugu na sisi tunawaambia watu katika mkutano yetu kujiepusha na ghasia." Alisema .

    SAMANTHA Lewithwaite anayehusishwa na tukio la Westgate.

  • 16 AN-NUURJAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 201416 MAKALA

    Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na POA Printing Works LTD, S.L.P. 4605, Dar es Salaam.

    AN-NUUR16 JAMADUL AWWAL 1435, IJUMAA MACHI 21-27, 2014

    Soma AN-NUUR

    kila Ijumaa

    PENGINE hili litakuwa ni somo kwa wanaadamu kuwa akili na ubunifu wao sio chochote wala lolote mbele ya Mwenyezi M u n g u a n a p o a m u a kuwaonyesha uwezo wake.

    Ni aya kutoka katika gazeti moja maarufu hapa nchini, wakiwa na maana kuwa, kupotea kwa ndege ya abiria nchini Malaysia tangu Ijumaa iliyopita, i n a w e z e k a n a k u w a Mungu anaonesha uwezo wake mbele ya ubunifu wa hali ya juu walionao binadamu sasa.

    Ndege ya Malaysia Airlines Flight aina ya Flight MH370, iliruka kwenye uwanja wa ndege

    TAKRIBANI miezi sita baada ya shambulizi katika jengo la maduka la Westgate na kundi la al Shabaab la Somalia, Wakenya wenye asili ya Kisomali nchini K e n ya wa m e k u wa wakionekana kama w a k o s a j i k w a kuhusishwa na al-Shabaab, huku mara kwa mara wakikabiliwa na ubaguzi katika maisha ya kila siku.

    W a k e n y a h a o wamekuwa wakijitahidi k u k a b i l i a n a n a mashaka yalipo juu yao, wanasambaza ujumbe wa kujizuia na fujo, akina mama, wabunge, wa l i m u , v i o n g o z i wa kidini na vijana wamekuwa wakijaribu kuondoa taswira hiyo katika jamii ya watu wa Kenya.

    Suleiman Hassan Abdi, mwenye umri w a m i a k a 2 3 n a mwafunzi wa sheria katika Chuo Kikuu cha Nairobi, alisema jamii ya Kisomali imekuwa ikionewa sana kwa kukabiliwa na dhana potofu, ingawa jamii nyingine pia zinahusika na mambo ya kigaidi.

    " J a m i i n z i m a inabebeshwa lawama kwa sababu ya makosa ya watu wachache. Lakini hatujakaa kitako na kupakata mikono," alinukuliwa akisema Abdi, mkazi wa Kaunti ya Wajir.

    Kijana huyo anasema kuwa Maulamaa wenye asili ya Kisomali na hata katika hotuba za Makhatibu misikitini,

    Wenye asili ya Kisomali wana wakati mgumu KenyaWajitahidi kuondoa taswira ya ugaidi Na Bosire Boniface, Garissa wamekuwa wakijitahidi kuelimisha umma na kupeleka ujumbe wao

    wa jamii ya Kiislamu hususan wale wenye a s i l i y a k i s o m a l i kutojihusisha na vurugu misikitini na sehemu nyengine katika jamii.

    " K a t i k a h o t u b a misikitini, viongozi wa kidini wanasema k w a m b a m a t e n d o y o t e y a k i g a i d i yanayowalenga raia ni haramu kwenye Uislamu na kwamba i n a k a t a z w a k w a Muislamu kushirikiana n a m t u a u k u n d i linalohusika na kitendo chochote cha ugaidi au ghasia," alisema.

    Vijana kwa upande w a o w a m e k u w a wakituma ujumbe huo huo katika mitandao ya kijamii na kujiingiza k w e n y e m i d a h a l o yenye maana, zote hizo zikiwa ni jitihada za kuuelewesha umma juu ya taswira waliyo nayo dhidi ya watu wa jamii ya Kisomali nchini Kenya.

    Mbunge wa jimbo la Garissa, Aden Duale, a n a s e m a a n a u n g a mkono na anashajiisha juhudi hizo za kijamii.

    Anasema Wasomali wengi nchini Kenya ni raia wanaofuata sheria, wanaopingana na matendo ya ghasia na siasa kali," alisema.

    Hata hivyo, matokeo y a j i t i h a d a z a o yanaathiriwa vibaya na mtazamo unaongaliwa jamii hiyo ya Kisomali nchini humo.

    M b u n g e h u y o alisema kuwa Wasomali wanaosafiri kutoka

    Upo ukumbusho kutoka Flight MH370Inawezekana dunia sio kama kijiji

    Na Rashid Abdallah, MUM

    jijini Kuala Lampur saa 6 :41 us iku kuelekea Beijing, China ikiwa na abiria 227 na wafanyakazi 12, jumla ni watu 239.

    Muda mfupi tu baada ya kuruka, ikapoteza mawasiliano na vituo vya kuongozea ndege na kuonekana mara moja katika rada za nchi ya Vietnam.

    Rada kubwa za kijeshi t a y a r i z i m e e n d e l e a k u t u m i k a b i l a y a mafanikio, ndege za kivita na meli za kivita huku si chini ya mataifa 26 yakiwa na vifaa vya kisasa, yanaisaka ndege hiyo.

    Ilitarajiwa itue Ijumaa saa 12:30 asubuhi Beijing, lakini hali haikuwa hivyo pale ndugu na jamaa waliposubiri kwa muda

    mrefu ndugu zao hao ili wawapokee, lakini baada ya mawasiliano kufanyika kutoka Beijing kwenda M a l a y s i a wa k a p e wa taarifa ya kupotea kwa ndege hiyo.

    Imeshatafutwa tayari katika eneo lote la nchi ya Malaysia, kusini mwa bahari ya China, pwani ya nchi za jirani ghuba ya Thailand n.k, lakini matokeo yamekuwa hasi.

    Awali wapo waliosema kuwa ndege hiyo ilitekwa kwani kuligunduliwa Wairan wawili waliosafiria hati za wizi, zilizoibwa m wa k a 2 0 1 2 n c h i n i Thailand.

    Lakin i taar i fa h iz i z i l i k a n u s h w a n a Interpool kwani watekaji

    Inaendelea Uk. 12 Inaendelea Uk. 15

    Sheikh Ali Bahero, ambaye alikuwa msaidizi wa marehemu Sheikh Aboud Rogo Mohammed, amekutwa akiwa ameloa damu baada ya kushambuliwa mjini Mombasa.