Top Banner
TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA UHUSIANO WAKE NA KATIBA MPYA YA TANZANIA. Waraka uliowasilishwa na Nd. Ibrahim Mzee Ibrahim, Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, na Katibu wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi, katika semina ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi juu ya Wajibu wa Wajumbe katika Bunge la Katiba, iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Coconut Beach Resorts, Marumbi Zanzibar, tarehe 2-3 Disemba 2013. Waraka huu umechapishwa kwa ufadhili wa Mradi wa Kuimarisha Vyombo vya Kutunga Sheria Legislature Support Project (LSP) unaoratibiwa na UNDP.
39

TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

Aug 31, 2019

Download

Documents

dariahiddleston
Welcome message from author
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
Page 1: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA

UMOJA WA KITAIFA NA

UHUSIANO WAKE NA KATIBA

MPYA YA TANZANIA.

Waraka uliowasilishwa na Nd. Ibrahim Mzee

Ibrahim, Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar,

na Katibu wa Zamani wa Baraza la

Wawakilishi, katika semina ya kuwajengea

uwezo Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi

juu ya Wajibu wa Wajumbe katika Bunge la

Katiba, iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli

ya Coconut Beach Resorts, Marumbi

Zanzibar, tarehe 2-3 Disemba 2013.

Waraka huu umechapishwa kwa ufadhili wa

Mradi wa Kuimarisha Vyombo vya

Kutunga Sheria – Legislature Support

Project (LSP) unaoratibiwa na UNDP.

Page 2: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

1

Utangulizi

Katika mada hii tutajaribu kueleza kuhusu

mambo matatu makubwa. Tutaanza na

historia ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja

wa Kitaifa hapa Zanzibar. Tutafafanua

masharti yaliyomo kwenye Katiba ya

Zanzibar ya 1984 kama ilivyorekebishwa

mnamo mwaka 2010 kuhusu Serikali ya

Umoja wa Kitaifa. Tutamalizia kwa kugusia

mambo ya kuyatafakari katika muktadha wa

katiba mpya ya Tanzania.

Page 3: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

2

Azimio la Baraza la Wawakilishi

Baraza la Wawakilishi la Zanzibar mnamo

tarehe 28 na 29 Januari 2010 lilijadili hoja ya

mapendekezo ya kuundwa kwa Serikali ya

Umoja wa Kitaifa Zanzibar. Hoja hiyo

iliwasilishwa kwenye Baraza la Wawakilishi

na Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa

Jimbo la Mgogoni Pemba Mheshimiwa

Abubakar Khamis Bakary.

Katika hoja hiyo, Wajumbe wa Baraza la

Wawakilishi waliombwa kupongeza na

kuridhia mazungumzo ya maridhiano

yaliyofanyika tarehe 5 Novemba 2009 baina

ya aliyekuwa Rais wa Zanzibar na

Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi

Mheshimiwa Dr. Amani Abeid Karume

ambaye alikuwa pia ni Makamo Mwenyekiti

wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar,

na Mhe. Seif Shariff Hamad – Katibu Mkuu

wa chama cha Civic United Front (CUF).

Aidha, wajumbe waliombwa wakubali

Page 4: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

3

kuanzishwa kwa Serikali ya Umoja wa

Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu

wa Oktoba 2010.

Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo

kwa masharti kwamba kufanyike kura ya

maoni kwa ajili ya kutafuta ridhaa ya

wananchi kuhusu jambo hilo na Serikali ilete

mswada wa sheria kwenye Baraza ili

utengenezwe utaratibu wa kisheria wa

kuendesha kura ya maoni. Maamuzi hayo ya

Baraza yalipitishwa kwa azimio lilokuwa na

vifungu 12.

Kwenye majadiliano ya Baraza la

Wawakilishi kuhusu azimio hilo, ilielezwa na

wajumbe mbali mbali kuwa maridhiano ya

kisiasa baina ya CCM na CUF yamefikiwa ili

kuondoa migogoro na mivutano ya kisiasa

Zanzibar iliyodumu kwa muda mrefu tangu

kurejeshwa kwa mfumo wa siasa za vyama

Page 5: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

4

vingi Tanzania na hususan Zanzibar kuanzia

mwaka 1992.

ya kisiasa

Uchaguzi wa kwanza katika mfumo wa

vyama vingi tangu baada ya Mapinduzi ya

1964 ulifanyika mwaka 1995 ambapo

mivutano ya kisiasa ilijitokeza wazi wazi

baina ya vyama viwili vikuu vya siasa hapa

Zanzibar yaani CCM na CUF. Uhasama na

chuki za kisiasa zilishika kasi. Chama cha

upinzani CUF kilikataa kuyatambua matokeo

ya uchaguzi wa Rais na pia kilikataa

kumtambua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti

wa Baraza la Mapinduzi ambaye wakati huo

alikuwa Mheshimiwa Dr. Salmin Amour

Juma.

Aidha, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi

wa Upande wa Upinzani (CUF) walisusia

vikao vya Baraza kwani walihudhuria vikao

hivyo kwa kupangilia ili wasipoteze sifa tu za

Page 6: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

5

kuwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi

kwa mujibu wa Katiba. Vile vile, Wajumbe

wa Baraza la Wawawkilishi wa Upande wa

Upinzani walikuwa hawazungumzi wala

kuchangia chochote kwenye mijadala

iliyoendeshwa kwenye vikao vya Baraza.

Katika mwendelezo wa matukio hayo, wakati

Rais alipokuwa akienda kulihutubia Baraza,

wajumbe wa CUF walikuwa wakitoka nje ya

ukumbi wa mkutano wa Baraza.

Matokeo ya chaguzi zilizofanyika 1995, 2000

na 2005 yalionyesha waziwazi kwamba jamii

ya Zanzibar imegawika pande mbili kisiasa

zenye wafuasi wengi kila upande kiasi

ambacho kukaribiana sana kwa matokeo ya

chaguzi hizo kunaufanya upande ulioshindwa

kuyatilia mashaka na kutoyakubali matokeo

hayo. Mwaka 1995 mgombea urais kutoka

CCM alipata kura 50.2% wakati mgombea

urais kutoka CUF alipata kura 49.8%.

Mwaka 2000 mgombea urais kutoka CCM

Page 7: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

6

alipata kura 56% na mgombea urais kutoka

CUF alipata 44%. Mwaka 2005 mgombea

urais kutoka CCM alipata kura 53% wakati

mgombea urais kutoka CUF alipata kura

47%. Hata mwaka 2010 mgombea urais wa

CCM alipata kura 50.1% na mgombea urais

wa CUF alipata kura 49.1%.

Hali ya matokeo kukaribiana ilijitokeza pia

kwenye chaguzi za wajumbe wa Baraza la

Wawakilishi kwani mwaka 1995 CCM

ilipata majimbo 26 na CUF ilipata majimbo

24. Baadae, baada ya idadi ya majimbo ya

Pemba kupungua na idadi ya majimbo ya

Unguja kuongezeka, mwaka 2000 CCM

ilipata majimbo 35 na CUF ilipata majimbo

15. Mwaka 2005 CCM ilipata majimbo 31

wakati ambapo CUF ilipata majimbo 19.

Mwaka 2010 CCM imepata majimbo 28

wakati CUF imepata majimbo 22.

Page 8: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

7

Mgogoro wa kukataa kutambua na

kuyakubali matokeo katika chaguzi hizo

uliathiri uchumi wa nchi, Washirika wa

Maendeleo waliisusia na kuiwekea vikwazo

Zanzibar na uliwagawa wananchi wa Unguja

na Pemba kisiasa na hata kwenye mambo yao

ya kawaida ya kijamii kama vile harusi na

maziko.

Uchaguzi wa mwaka 2000 na wa mwaka

2005

Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000 ulifanyika

katika mazingira yale yale ya chuki na

uhasama wa kisiasa. Kwa mara nyengine tena

chama cha CUF kilikataa kuyatambua

matokeo ya uchaguzi na pia kilikataa

kumtambua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti

wa Baraza la Mapinduzi Dr. Amani Abeid

Karume. Baada ya uchaguzi, Wajumbe wa

Baraza la Wawakilishi wa upande wa

upinzani (CUF) hawakuhudhuria kabisa

vikao vya Baraza la Wawakilishi na

Page 9: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

8

hawakwenda Barazani hata kuapa kiapo cha

uaminifu.

Kutokana na hali hiyo, baada ya mikutano

mitatu ya Baraza kupita bila ya wajumbe hao

kuhudhuria kwenye vikao vya Baraza,

walipoteza sifa za kuwa wawakilishi na

hivyo kupoteza viti vyao kwenye Baraza la

wawakilishi. Matukio ya kuhuzunisha pia

yalitokea tarehe 26 na 27 Januari 2001 kwa

baadhi ya wananchi kupoteza maisha yao na

wengine kwenda ukimbizi kwenye nchi jirani

ya Kenya.

Uchaguzi Mkuu mwengine ulifanyika mwaka

2005 na kwa mara nyengine tena Chama cha

Wananchi CUF kilikataa kuyatambua

matokeo ya uchaguzi wa Rais na pia kilikataa

kumtambua Rais Amani Abeid Karume.

Page 10: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

9

Jitihada za Usuluhishi

Jitihada za usuluhishi zilianza kwa

Muwafaka wa Mwanzo kusainiwa tarehe 9

Juni 1999 baina ya CCM na CUF ili kufanya

mazungumzo ya kutatua hali iliyojitokeza

baada ya uchaguzi mkuu wa 1995

(Muwafaka wa Kwanza: Mhe. Mkema na

Mhe. Mloo). Kamati ya Pamoja ya CCM na

CUF yenye Wajumbe wa Baraza la

Wawakilishi kumi na nne, yaani saba kutoka

kila upande, iliundwa ili kufanya

mazungumzo chini ya usuluhishi wa Katibu

Mkuu wa Jumuiya ya Madola wa wakati huo

Chief Emeka Anyaokou. Kamati hiyo ilianza

kazi mwezi wa Septemba 1999 na kumaliza

mchakato wa mazungumzo mnamo mwezi

wa Julai 2000 na kuwasilisha ripoti Serikalini

yenye mapendekezo ya mambo

yanayohitajika kufanywa ili kutekeleza

muwafaka huo wa kisiasa.

Page 11: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

10

Serikali iliandaa Mswada wa Marekebisho ya

Katiba na kupelekwa kwenye Baraza la

Wawakilishi, lakini mswada huo haukupita

kwani ulikataliwa na Wajumbe wa Baraza la

Wawakilishi kutoka Chama cha Upinzani

CUF ambao walikuwa hawakuridhika na

marekebisho yaliyokuwemo kwenye mswada

huo. Kwa wakati huo Wajumbe wa upande

wa Chama Tawala CCM idadi yao ilikuwa

haitimii theluthi mbili ya Wajumbe wote wa

Baraza iliyohitajika kwa ajili ya kupitisha

marekebisho hayo ya Katiba yaliyotokana na

muwafaka wa kwanza.

Muwafaka wa pili kati ya CCM na CUF

ulisainiwa tarehe 10 Oktoba 2001

(Muwafaka wa Pili: Mhe Mangula na Mhe

Seif Shariff) na baadae mnamo tarehe 30

Novemba 2001 Sheria Nambari 10 ya 2001

ilipitishwa na Baraza la Wawakilishi kwa

madhumuni ya kuunda Tume ya Pamoja ya

Rais ya Kusimamia Utekelezaji wa

Page 12: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

11

Muwafaka wa Kisiasa baina ya CCM na

CUF. Tume hiyo ilikuwa na Wajumbe kumi

ambapo watano ni kutoka CCM na watano

kutoka CUF.

Kifungu cha 5 (2) (b) cha Sheria hiyo

Nambari 10 ya 2001 kilitamka wazi wazi

kwamba miongoni mwa majukumu na kazi

za Tume hiyo ni kuanzisha na kufanya

mazungumzo yatayoshirikisha CCM na CUF

kwa madhumuni ya kufungua maeneo

mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo

uwezekano wa kuunda serikali ya umoja wa

kitaifa kwa ridhaa ya wananchi na kwa haja

ya kuamua mustakbala wa Zanzibar katika

nyanja za uchumi, demokrasia na mambo

mengineyo1.

1 Section 5(2)(b) of an Act No. 10 of 2001,

among the functions of the Joint Presidential

Supervisory Commission is to “initiate and

engage in dialogue involving CCM and CUF with

the aim of opening different areas of co-operation

which includes the possibility of forming a

Page 13: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

12

Matokeo ya mazungumzo ya Tume hiyo

ndiyo yaliyopelekea kufanyika kwa

Marekebisho ya Nane na Marekebisho ya

Tisa ya Katiba ya Zanzibar mnamo mwaka

2002 na 2003, ili kuingiza kwenye Katiba

yale mambo yaliyokubalika kwenye

muwafaka huo. Hata hivyo, suala la serikali

ya umoja wa kitaifa halikuingizwa kwenye

marekebisho ya Katiba wala halikutekelezwa.

Mabadiliko makubwa yaliyofanyika kwenye

Katiba kupitia Marekebisho ya Nane na ya

Tisa yalikuwa ni kuweka Muundo wa Tume

ya Uchaguzi inayojumuisha Makamishna

kutoka kwenye vyama vya siasa na pia

kuweka utaratibu wa Mheshimiwa Rais

kuteua angalau watu wawili kuwa Wajumbe

wa Baraza la Wawakilishi kutoka upande wa

government of national unity by consent of the

people, and the need to determine the future of

Zanzibar in the spheres of politics, democracy and

other matters”

Page 14: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

13

upinzani, miongoni mwa nafasi kumi za

uteuzi wa Wajumbe wa Baraza la

Wawakilishi ambazo zipo kwa mujibu wa

Katiba. Halikadhalika, Uchaguzi Mdogo

ulifanyika ili kujaza nafasi za Uwakilishi za

Majimbo ya Pemba yaliyokuwa wazi tangu

2001 kutokana na Wawakilishi wa Upinzani

kupoteza sifa kwa kutohudhuria vikao. Hatua

hizo zilileta utulivu kidogo hadi kufikia

uchaguzi wa mwaka 2005.

Baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais

wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi

kwenye hotuba yake ya tarehe 30 Disemba

2005 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano

wa Tanzania, alionyesha nia ya dhati ya

kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa Zanzibar

unaojitokeza kila mara baada ya uchaguzi

Mkuu. Katika kutekeleza azma hiyo, Kamati

ya pamoja ya CCM na CUF iliundwa.

Page 15: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

14

Kamati hiyo iliongozwa na Makatibu Wakuu

wa vyama hivyo, na ikafanya mazungumzo

ya kina kule Bagamoyo na kutoa

mapendekezo yake kwa vyama husika

likiwemo suala la uanzishwaji wa serikali ya

umoja wa kitaifa Zanzibar.

Kwa upande wa CCM, mapendekezo hayo

yalipowasilishwa kwenye Halmashauri Kuu

ya Taifa (NEC) katika kikao cha tarehe 29

hadi 30 Machi 2008 kilichofanyika Butiama

yalikubaliwa lakini NEC ya CCM iliona

kuwa suala la uanzishwaji wa Serikali ya

Umoja wa Kitaifa ni vyema, kwa uzito na

umuhimu wake, lipelekwe kwa wananchi

moja kwa moja ili kupata ridhaa yao kwa njia

ya kura ya maoni. Chama cha CUF kwa

wakati ule hakikuridhishwa na uamuzi huo

wa NEC ya CCM na kikatangaza rasmi

kujiondoa kwenye mazungumzo.

Page 16: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

15

Hatua hiyo ilipelekea kukwama tena kwa

mazungumzo ya muwafaka ambao

ungelikuwa ni muwafaka wa tatu tangu

kuanza tena kwa siasa za vyama vingi hapa

Zanzibar. Muwafaka huo ulififia baada ya

CUF kujitoa kwenye mazungumzo kufuatia

maamuzi ya NEC ya CCM Butiama.

Historia hii fupi ya miafaka hapa Zanzibar

baada ya kuanza tena kwa siasa za vyama

vingi, inaonyesha kwamba Muwafaka wa

kwanza wa 1999 chini ya Uongozi wa Dr.

Salmin Amour Juma haukutekelezwa hata

kidogo. Muwafaka wa pili wa 2001 chini ya

Uongozi wa Dr. Aman Abeid Karume

ulitekelezwa kwa kiasi fulani kwa kufanywa

marekebisho ya Katiba ya Zanzibar ya 1984

(Marekebisho ya Nane 2002 na Marekebisho

ya Tisa 2003). Hata hivyo, siasa za chuki

zilirejea na kujitokeza tena kwenye Uchaguzi

Mkuu wa 2005.

Page 17: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

16

Kwa bahati nzuri muwafaka huu wa tatu

ulifufuka Novemba 2009 baada ya

mazungumzo ya tarehe 5 Novemba 2009

baina ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na

Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr.

Amani Abeid Karume na Mheshimiwa

Katibu Mkuu wa Chama wa Wananchi CUF

Maalim Seif Sharif Hamad.

Muwafaka huu wa Tatu ulianza kuonyesha

dalili za matumaini ya mafanikio kwa sababu

suala la ushirikiano katika madaraka (power

sharing) kwa njia ya uundwaji wa Serikali ya

Umoja wa Kitaifa lilipewa kipaumbele.

Mwafaka huu sasa unajulikana kwa umaarufu

kama “Maridhiano”.

Kamati ya Watu Sita

Kifungu cha Kumi na moja 11 cha Azimio la

Baraza kilielekeza kuundwa kwa Kamati ya

Watu Sita ya Kusimamia Utekelezaji wa

Maamuzi ya Baraza kuhusu hoja ya

Page 18: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

17

uanzishwaji wa Serikali ya umoja wa kitaifa

hadi kukamilika kwake. Kwa mujibu wa

Kifungu hicho, Kamati hiyo ilitakiwa iwe na

Wajumbe watatu kutoka upande wa chama

kinachounda Serikali (CCM) na watatu

kutoka upande wa Upinzani.

Spika wa Baraza la Wawakilishi Mheshimwa

Pandu Ameir Kificho aliunda Kamati hiyo

kwa kuteua Wajumbe Sita, kama

ilivyoelekezwa kwenye kifungu tulichokitaja

hapo juu. Wajumbe watatu miongoni mwao

walichaguliwa kutoka CCM – Chama

kinachounda Serikali; na Wajumbe wengine

watatu walichaguliwa kutoka CUF ambacho

kilikuwa Chama cha Upinzani ndani ya

Baraza la Wawakilishi kwa wakati huo.

Wajumbe wa kamati hiyo walipokutana

walichagua Mwenyekiti wa Kamati na

Makamo Mwenyekiti wa kamati kutoka

miongoni mwao.Wajumbe hao sita

walioteuliwa na Mheshimiwa Spika kuunda

Page 19: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

18

kamati ya watu sita kwa mujibu wa

maelekezo ya Azimio la Baraza ni:-

1 Mhe. Ali Mzee Ali CCM Mwenyekiti

2

Mhe. Abubakar Khamis

Bakary CUF

Makamo

Mwenyekiti

3 Mhe. Ali Abdalla Ali CCM Mjumbe

4 Mhe. Haji Omar Kheri CCM Mjumbe

5

Mhe. Nassor Ahmed

Mazrui CUF Mjumbe

6 Mhe. Zakiya Omar Juma CUF Mjumbe

Sekretarieti ya Kamati ilikuwa ni Ndugu

Ibrahim Mzee Ibrahim, aliyekuwa Katibu wa

Baraza la Wawakilishi na Ndugu Mdungi

Makame Mdungi (aliyekuwa Mkuu wa Idara

Page 20: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

19

ya Utawala) Afisi ya Baraza la Wawakilishi.

Kamati ya Watu Sita ilijifunza ndani ya nchi

na nje ya nchi na ilitoa elimu kwa jamii

Unguja na Pemba.

Kura ya Maoni

Sheria Nambari 6 ya 2010 kuhusu uendeshaji

wa kura ya maoni ilipitishwa na Baraza la

Wawakilishi mnamo mwezi wa Machi 2010

na kutiwa saini na Mheshimiwa Rais mnamo

mwezi wa Aprili 2010. Wananchi wa

Zanzibar walipiga kura ya maoni siku ya

Jumamosi tarehe 31 Julai 2010. Kura hiyo

ilikuwa na lengo la kutafuta ridhaa ya

wananchi katika kuamua iwapo wanalikubali

wazo la kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa

Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu

wa Oktoba 2010.

Kupigwa kwa kura hiyo ya maoni ilikuwa ni

utekelezaji wa kifungu nambari mbili cha

Azimio la Baraza ambacho kilieleza kwamba

Kimsingi, Baraza limekubali kwamba ipo

Page 21: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

20

haja ya kufanywa kura ya maoni

(referendum) itayowashirikisha wananchi

moja kwa moja katika kupata ridhaa ya

wananchi kuhusu uanzishwaji wa mfumo na

muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa

Zanzibar.

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ilitangaza

matokeo ya kura ya maoni siku ya Jumapili

ya tarehe 01/08/2010. Matokeo hayo yalitoa

ushindi wa kura za NDIO kwa aslimia

66.40% dhidi ya kura za HAPANA asilimia

33.90%.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 11(1) cha

Sheria ya Kura ya Maoni Nambari 6 ya 2010,

ushindi wa Kura ya Maoni utaamuliwa kwa

wingi wa kura. Hivyo, kwa mujibu wa

matokeo hayo, Wazanzibari waliopiga kura

ya NDIO kuunga mkono kuundwa kwa

Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar baada

Page 22: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

21

ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010

walishinda.

Kwa mujibu wa kifungu cha sheria

kilichotajwa hapo juu, Serikali ililazimika

kuyakubali matokeo yoyote ya Kura ya

Maoni. Hivyo, Serikali mpya ikaundwa

baada ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa

Oktoba 2010 ambayo ikatambulika kuwa ni

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye

Muundo wa Umoja wa Kitaifa kama

inavyoelekeza Katiba ya Zanzibar kwenye

kifungu cha 9(3), baada ya kufanyiwa

marekebisho. Marekebisho hayo yalifanywa

kwenye Mkutano wa Ishirini na Moja wa

Baraza la Saba la Wawakilishi mnamo

mwezi wa Ogasti 2010.

Madhumuni ya Serikali ya Umoja wa

Kitaifa

Kifungu cha tano cha Azimio la Baraza la

Wawakilishi lililotajwa hapo juu kilisisitiza

Page 23: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

22

kwamba Serikali ya Umoja wa Kitaifa

itakayoundwa Zanzibar itaendelea kuheshimu

na kuthamini misingi mikuu ya Mapinduzi ya

tarehe 12 Januari 1964. Katika mjadala

uliofanyika kwenye Baraza la Wawakilishi

ilibainishwa kuwa misingi hiyo ni ile

iliyotajwa na kuwekwa kisheria kwenye

Dikrii Nambari 6 ya 1964. Misingi hiyo ni

Usawa, Maridhiano, na Umoja.

Baada ya kufanyika kwa Kura ya Maoni

tarehe 31 Julai 2010 na baada ya kufanywa

kwa Marekebisho ya Kumi ya Katiba ya

Zanzibar ya 1984, Katiba imeanisha kuwepo

kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye

muundo wa Umoja wa Kitaifa ambayo

itajumuisha mawaziri kutoka vyama tofauti

vya siasa kulingana na uwiano wa viti

ambavyo vyama vya siasa vimepata kwenye

Baraza la Wawakilishi.

Uzoefu wa chaguzi zilizopita unaonyesha

kwamba kwa hapa Zanzibar ni vyama vya

Page 24: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

23

CCM na CUF tu ndivyo vimekuwa vikipata

viti kwenye Baraza la Wawakilishi. Kifungu

cha 9 (3) cha Katiba kinaeleza kwamba

“Muundo wa Serikali ya Mapinduzi ya

Zanzibar utakuwa ni wa Umoja wa Kitaifa na

utendaji wa kazi zake utafanywa katika

utaratibu utakaohakikisha kuendelezwa kwa

umoja nchini na lengo la kufikia demokrasia”

Serikali ya Umoja wa kitaifa inafanana na

serikali ya mseto kwa kuwa aina zote hizo

mbili za serikali zinashirikisha mawaziri

kutoka vyama tofauti vya siasa lakini

zinatofautiana katika sababu za kuwepo kwa

serikali hizo. Serikali ya mseto inatokana na

kutokuwepo kwa mshindi mwenye wingi wa

viti vya kutosha kwenye Bunge/ Baraza kwa

ajili ya kuunda serikali wakati ambapo

serikali ya umoja wa kitaifa haitokani na

kutokuwepo kwa mshindi mwenye viti vya

kutosha kwenye Bunge bali inatokana na

matatizo mahsusi katika nchi husika,

matatizo ambayo utatuzi wake umewekwa

Page 25: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

24

kwenye Katiba kwamba ni kuwa na serikali

inayoshirikisha vyama mbali mbali vya siasa.

Kwa kawaida katika nchi nyingi kunapokuwa

na serikali ya mseto ambayo ina mawaziri

kutoka kwenye vyama viwili au zaidi vya

siasa, bado kunakuwepo vyama vyengine

ndani ya Bunge ambavyo hufanyakazi ya

upinzani. Lakini Serikali ya Umoja wa

Kitaifa huwa na hali tofauti, na hiyo ni kwa

sababu hujumuisha mawaziri kutoka vyama

vyote vya siasa vyenye uwakilishi kwenye

Bunge/ Baraza; kwa maneno mengine ni

kwamba Serikali ya Umoja wa Kitaifa ni

serikali ya vyama vyote vya siasa vilivyomo

Bungeni na kunakuwa hakuna Upande wa

Upinzani kwani vyama vyote vilivyomo

Bungeni/Barazani huwa vimo pia serikalini

kwa maana kwamba vimetoa mawaziri.

Page 26: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

25

Mabadiliko ya Kanuni na Taratibu za

Baraza kutokana na kuanzishwa kwa

Serikali ya Umoja wa Kitaifa

Katika mazingira ya sasa ya kikatiba kwa

Zanzibar ambapo mawaziri wanapatikana

kutoka kwenye vyama vyote vya siasa

vilivyomo kwenye Baraza la Wawakilishi,

ina maana kuwa hakuna chama cha siasa

ndani ya Baraza la Wawakilishi

kinachofanyakazi ya upinzani kama chama

kwani vyama vyote vilivyomo kwenye

Baraza kwa kiasi fulani viko upande wa

serikali kwa sababu vimetoa mawaziri. Kwa

maneno mengine ni kwamba kwa sasa

hakuna Kiongozi wa Upinzani wala Upande

wa Upinzani ndani ya Baraza la Wawakilishi

wala mawaziri vivuli.

Majukumu ya wajumbe wote wa Baraza la

Wawakilishi kutoka vyama mbali mbali

ambao si mawaziri wala si manaibu mawaziri

ni kuikosoa na kuiwajibisha serikali. Hii ina

Page 27: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

26

maana kwamba yale majukumu yaliyokuwa

yakitekelezwa na Upande wa Upinzani

pamoja na ''backbenchers'' wa chama tawala

sasa yanahamia rasmi kwa ''backbenchers''

wa vyama vyote vilivyomo kwenye Baraza la

Wawakilishi.

Kulikuwa na hofu (hasa kwa wataalamu

mbalimbali wa nchi za Ulaya na asasi za

kiraia) kwamba kutokuwepo kwa kambi

rasmi ya upinzani kwenye Baraza

kutasababisha kudumaa kwa demokrasia na

kupwaya au kudorora kwa Baraza. Lakini,

uzoefu wa miaka mitatu ya Serikali ya

Umoja wa Kitaifa haukuonyesha hivyo.

Kilichoonekana ni kuimarika kwa

demokrasia, wajumbe wa Baraza wamekuwa

huru zaidi kutoa maoni yao na

''backbenchers'' wote kwa pamoja

wanashirikiana kuiwajibisha serikali. Mfano

uliowazi ni kuundwa kwa kamati teule nne

na matokeo yake yameanza kuonekana.

Page 28: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

27

Masharti yaliyomo kwenye Katiba

kufuatia Marekebisho ya Kumi

Muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa

kwa mujibu wa Marekebisho ya Kumi ya

Katiba ni kuwa na Rais mtendaji, Makamo

wa Kwanza wa Rais atakaeteuliwa na Rais

baada ya kushauriana na chama cha siasa

kilichopata nafasi ya pili katika matokeo ya

kura ya uchaguzi wa Rais, Makamo wa Pili

wa Rais atakaeteuliwa na Rais kutoka

miongoni mwa wajumbe wa Baraza la

Wawakilishi kutoka katika chama cha siasa

anachotoka Rais. Pia, Rais kwa kushauriana

na Makamo wote wawili atataeua Mawaziri

kutoka miongoni mwa wajumbe wa Baraza la

Wawakilishi kwa kuzingatia uwiano wa viti

vya majimbo kwa vyama vya siasa vilivyomo

ndani ya Baraza la Wawakilishi.

Vifuatavyo ni baadhi ya vifungu vilivyomo

katika Katiba ya Zanzibar kufuatia

marekebisho ya Kumi ya Katiba hiyo:-

Page 29: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

28

Kutamkwa kwamba muundo wa

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni

wa Umoja wa Kitaifa (Kifungu cha 9

(3) cha Katiba).

Kuanzishwa kwa wadhifa wa

Makamo wa Kwanza na Makamo wa

Pili wa Rais na kufutwa kwa wadhifa

wa Waziri Kiongozi (Kifungu cha 39

(1) cha Katiba).

Mawaziri kuteuliwa na Rais kutoka

miongoni mwa wajumbe wa Baraza

la Wawakilishi kwa kuzingatia

uwiano wa viti vya majimbo kwa

vyama vya siasa vilivyomo ndani ya

Baraza la Wawakilishi (Vifungu vya

42 (2) na 43 (2) vya Katiba).

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

chini ya mamlaka ya Rais ndiyo

itakuwa na uwezo wa kufanya

maamuzi juu ya sera za serikali „kwa

Page 30: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

29

ujumla (Kifungu cha 43 (5) cha

Katiba).

Kutamkwa bayana kwamba Zanzibar

ni nchi, na mipaka yake, na ni moja

ya nchi mbili zinazounda Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania, na uwezo

wa Rais kuigawa Zanzibar katika

Mikoa na Wilaya na maeneo

mengine, na kutamkwa kuwa Rais

wa Zanzibar ni Mkuu wa nchi ya

Zanzibar (Vifungu vya 1, 2, 2A, na

26).

Kuweka masharti kuwa baadhi ya

vifungu vya Katiba haviwezi

kurekebishwa na Baraza la

Wawakilishi hadi kwanza kufanywe

kura ya maoni (Kifungu kipya cha

80A). Mfano wa vifungu

visivyoweza kurekebishwa

isipokuwa ifanywe kwanza kura ya

Page 31: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

30

maoni ni vifungu vyote vilotajwa

hapo juu kwenye sehemu hii.

Taratibu muhimu za Uendeshaji Serikali

ya Umoja wa Kitaifa

Serikali ya Umoja wa kitaifa kwa kawaida

huendeshwa kwa kufuata taratibu zile zile

muhimu za uendeshaji serikali zikiwemo

zifuatazo:

Uwajibikaji wa Pamoja (Collective

Responsibility) wa mawaziri mbele

ya Baraza la Wawakilishi (Kifungu

cha 43 (5) cha Katiba).

Mawaziri kutoka vyama mbali mbali

vya siasa wanawajibika kufuata na

kuheshimu matakwa ya kudhibiti na

kutotoa siri za Baraza la Mawaziri

(Confideniality) (Kifungu cha 46 cha

Katiba na Sheria ya Viapo).

Wajibu wa mawaziri kuwa wawazi,

wakweli na kutoa majibu au maelezo

Page 32: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

31

sahihi mbele ya Baraza la

Wawakilishi (Transparency,

Truthfulness and Accuracy). (Kanuni

za Baraza la Wawakilishi)

Uwajibikaji binafsi wa kila waziri

katika Baraza la Wawakilishi kwa

majukumu ya wizara anayoiongoza

hususan kuhusu sera, maamuzi na

matendo ya wizara hiyo (Individual

or Ministerial Responsibility)

(Kifungu cha 50 (1) cha Katiba).

Kutenganisha siasa (sera) na

Utendaji (Dichotomy of politics and

administration) (Kifungu cha 50 (1)

cha Katiba).

Wajibu wa kila waziri kutokuwa na

mgongano wa kimaslahi (Conflict of

Interest) baina ya majukumu yake ya

kazi ya uwaziri na maslahi yake

binafsi.(Kifungu cha 83 (3) cha

Katiba).

Page 33: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

32

Wajibu wa kila waziri kutenganisha

utekelezaji wa majukumu yake ya

uwaziri na majukumu yake ya

uwakilishi wa jimbo lake la

uchaguzi.

Marufuku kwa waziri yoyote

kutumia mali au rasilimali za serikali

ikiwemo watendaji wa serikali kwa

ajili ya shughuli za chama cha siasa.

Wajibu wa kila waziri kuhakikisha

kwamba uteuzi anaoufanya kwa ajili

ya nyadhifa mbali mbali haufanyi

kisiasa bali kwa mujibu wa sifa na

kwa mujibu wa matakwa ya sheria na

taratibu zilizopo (Kifungu cha 69 (4)

(a) cha Katiba).

Ni mwiko kwa kiongozi kupokea

kipato cha kificho, au rushwa au

kushiriki katika mambo yoyote ya

magendo (Kifungu cha 69 (4) (b) cha

Katiba.

Page 34: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

33

Vyeo vyote vya madaraka ni

dhamana na vipo kwa faida na

manufaa ya umma na wale wote

walio na madaraka watawajibika ama

moja kwa moja kwa umma au kupitia

vyombo vya uwakilishi (Kifungu cha

10 (h) cha Katiba).

Mambo ya kuyatafakari

(i) Rasimu ya katiba mpya

imeelekeza kwamba mambo

yasiyo ya muungano yako

mikononi mwa washirka wa

muungano na yatawekwa

kwenye katiba zao. Hii

inamaanisha kuwa Mfumo

wa Serikali ya Umoja wa

Kitaifa uliomo kwenye

Katiba ya Zanzibar kwa

ujumla hautoathirika.

Page 35: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

34

(ii) Rasimu ya katiba mpya ya

Tanzania imefuata utaratibu

kama ule wa Katiba ya

Zanzibar wa kutamka

kwamba baadhi ya mambo

kwenye katiba hiyo

hayawezi kufanyiwa

marekebisho mpaka kwanza

ifanywe kura ya maoni.

Mambo hayo ni kuongeza au

kupunguza jambo lolote la

muungano, na uwepo wa

jamhuri ya Muungano wa

Tanzania.

(iii) Jee ipo haja ya kuwa na

utaratibu wa Serikali ya

Umoja wa Kitaifa katika

katiba mpya ya Tanzania?

(iv) Marekebisho ya Nane ya

Katiba ya Zanzibar

yalianzisha utaratibu wa

Page 36: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

35

kuwa na Tume ya Uchaguzi

yenye uwakilishi wa vyama

vya siasa. Jee tunakubaliana

na utaratibu uliopendekezwa

wa kuunda Tume Huru ya

Uchaguzi ya Tanzania kwa

utaratibu uliopendekezwa

kwenye rasimu ya awali ya

Tume ya Mabadiliko ya

Katiba bila ya kuwa na

uwakilishi wa vyama vya

siasa kwenye Tume hiyo?

(v) Endapo kutakuwa na

mabadiliko katika baadhi ya

mambo kwenye katiba mpya

ya Tanzania, itakuwaje kwa

upande wa Zanzibar kwa

mambo ambayo

hayabadilishiki isipokuwa

kwanza ipigwe kura ya

maoni? Kwa mfano:

Page 37: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

36

(a) Kifungu cha 26 cha Katiba ya

Zanzibar hakiwezi kufanyiwa

marekebisho mpaka kwanza kufanyike

kura ya maoni. Kifungu cha 26 (2) (d)

kinataja miongono mwa sifa za mtu

kuweza kuwa Rais ni kuwa mwanachama

na mgombea aliyependekezwa na chama

cha siasa kilichosajiliwa kwa mujibu wa

Sheria ya Vyama vya Siasa ya 1992.

Endapo suala la mgombea binafsi

litakubalika na kuingizwa kwenye katiba

mpya ya Tanzania kwa chaguzi za

muungano, jee kwa upande wa chaguzi

za Zanzibar tutafanyaje? Tutafanya kura

ya maoni na kurekebisha katiba au bado

tutaendelea kuzuia mgombea binafsi?

(b) Mapendekezo ya rasimu ya awali ya

katiba mpya ya Tanzania yalipendekeza

mawaziri wa serikali ya muungano

wasiwe wabunge. Tumeona kwamba

vifungu vya 42 (2) na 43 (2) vya Katiba

ya Zanzibar vimeweka utaratibu kwamba

Page 38: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

37

mawaziri watateuliwa kutoka miongoni

mwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi

na vifungu hivyo navyo haviwezi

kubadilishwa isipokuwa kwanza ifanywe

kura ya maoni, jee ikitokea hivyo

tutafanya kura ya maoni au tutabakia na

mfumo wetu tuliouzowea?

Page 39: TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike

38

TAFAKURI KUHUSU

SERIKALI YA UMOJA

WA KITAIFA NA

UHUSIANO WAKE NA

KATIBA MPYA YA

TANZANIA.