TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA UHUSIANO WAKE NA KATIBA MPYA YA TANZANIA. Waraka uliowasilishwa na Nd. Ibrahim Mzee Ibrahim, Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, na Katibu wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi, katika semina ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi juu ya Wajibu wa Wajumbe katika Bunge la Katiba, iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Coconut Beach Resorts, Marumbi Zanzibar, tarehe 2-3 Disemba 2013. Waraka huu umechapishwa kwa ufadhili wa Mradi wa Kuimarisha Vyombo vya Kutunga Sheria – Legislature Support Project (LSP) unaoratibiwa na UNDP.
39
Embed
TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA NA … · Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2010. Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo kwa masharti kwamba kufanyike
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
TAFAKURI KUHUSU SERIKALI YA
UMOJA WA KITAIFA NA
UHUSIANO WAKE NA KATIBA
MPYA YA TANZANIA.
Waraka uliowasilishwa na Nd. Ibrahim Mzee
Ibrahim, Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar,
na Katibu wa Zamani wa Baraza la
Wawakilishi, katika semina ya kuwajengea
uwezo Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
juu ya Wajibu wa Wajumbe katika Bunge la
Katiba, iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli
ya Coconut Beach Resorts, Marumbi
Zanzibar, tarehe 2-3 Disemba 2013.
Waraka huu umechapishwa kwa ufadhili wa
Mradi wa Kuimarisha Vyombo vya
Kutunga Sheria – Legislature Support
Project (LSP) unaoratibiwa na UNDP.
1
Utangulizi
Katika mada hii tutajaribu kueleza kuhusu
mambo matatu makubwa. Tutaanza na
historia ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja
wa Kitaifa hapa Zanzibar. Tutafafanua
masharti yaliyomo kwenye Katiba ya
Zanzibar ya 1984 kama ilivyorekebishwa
mnamo mwaka 2010 kuhusu Serikali ya
Umoja wa Kitaifa. Tutamalizia kwa kugusia
mambo ya kuyatafakari katika muktadha wa
katiba mpya ya Tanzania.
2
Azimio la Baraza la Wawakilishi
Baraza la Wawakilishi la Zanzibar mnamo
tarehe 28 na 29 Januari 2010 lilijadili hoja ya
mapendekezo ya kuundwa kwa Serikali ya
Umoja wa Kitaifa Zanzibar. Hoja hiyo
iliwasilishwa kwenye Baraza la Wawakilishi
na Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi wa
Jimbo la Mgogoni Pemba Mheshimiwa
Abubakar Khamis Bakary.
Katika hoja hiyo, Wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi waliombwa kupongeza na
kuridhia mazungumzo ya maridhiano
yaliyofanyika tarehe 5 Novemba 2009 baina
ya aliyekuwa Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mheshimiwa Dr. Amani Abeid Karume
ambaye alikuwa pia ni Makamo Mwenyekiti
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar,
na Mhe. Seif Shariff Hamad – Katibu Mkuu
wa chama cha Civic United Front (CUF).
Aidha, wajumbe waliombwa wakubali
3
kuanzishwa kwa Serikali ya Umoja wa
Kitaifa Zanzibar baada ya Uchaguzi Mkuu
wa Oktoba 2010.
Baraza la Wawakilishi liliikubali hoja hiyo
kwa masharti kwamba kufanyike kura ya
maoni kwa ajili ya kutafuta ridhaa ya
wananchi kuhusu jambo hilo na Serikali ilete
mswada wa sheria kwenye Baraza ili
utengenezwe utaratibu wa kisheria wa
kuendesha kura ya maoni. Maamuzi hayo ya
Baraza yalipitishwa kwa azimio lilokuwa na
vifungu 12.
Kwenye majadiliano ya Baraza la
Wawakilishi kuhusu azimio hilo, ilielezwa na
wajumbe mbali mbali kuwa maridhiano ya
kisiasa baina ya CCM na CUF yamefikiwa ili
kuondoa migogoro na mivutano ya kisiasa
Zanzibar iliyodumu kwa muda mrefu tangu
kurejeshwa kwa mfumo wa siasa za vyama
4
vingi Tanzania na hususan Zanzibar kuanzia
mwaka 1992.
ya kisiasa
Uchaguzi wa kwanza katika mfumo wa
vyama vingi tangu baada ya Mapinduzi ya
1964 ulifanyika mwaka 1995 ambapo
mivutano ya kisiasa ilijitokeza wazi wazi
baina ya vyama viwili vikuu vya siasa hapa
Zanzibar yaani CCM na CUF. Uhasama na
chuki za kisiasa zilishika kasi. Chama cha
upinzani CUF kilikataa kuyatambua matokeo
ya uchaguzi wa Rais na pia kilikataa
kumtambua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi ambaye wakati huo
alikuwa Mheshimiwa Dr. Salmin Amour
Juma.
Aidha, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
wa Upande wa Upinzani (CUF) walisusia
vikao vya Baraza kwani walihudhuria vikao
hivyo kwa kupangilia ili wasipoteze sifa tu za
5
kuwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi
kwa mujibu wa Katiba. Vile vile, Wajumbe
wa Baraza la Wawawkilishi wa Upande wa
Upinzani walikuwa hawazungumzi wala
kuchangia chochote kwenye mijadala
iliyoendeshwa kwenye vikao vya Baraza.
Katika mwendelezo wa matukio hayo, wakati
Rais alipokuwa akienda kulihutubia Baraza,
wajumbe wa CUF walikuwa wakitoka nje ya
ukumbi wa mkutano wa Baraza.
Matokeo ya chaguzi zilizofanyika 1995, 2000
na 2005 yalionyesha waziwazi kwamba jamii
ya Zanzibar imegawika pande mbili kisiasa
zenye wafuasi wengi kila upande kiasi
ambacho kukaribiana sana kwa matokeo ya
chaguzi hizo kunaufanya upande ulioshindwa
kuyatilia mashaka na kutoyakubali matokeo
hayo. Mwaka 1995 mgombea urais kutoka
CCM alipata kura 50.2% wakati mgombea
urais kutoka CUF alipata kura 49.8%.
Mwaka 2000 mgombea urais kutoka CCM
6
alipata kura 56% na mgombea urais kutoka
CUF alipata 44%. Mwaka 2005 mgombea
urais kutoka CCM alipata kura 53% wakati
mgombea urais kutoka CUF alipata kura
47%. Hata mwaka 2010 mgombea urais wa
CCM alipata kura 50.1% na mgombea urais
wa CUF alipata kura 49.1%.
Hali ya matokeo kukaribiana ilijitokeza pia
kwenye chaguzi za wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi kwani mwaka 1995 CCM
ilipata majimbo 26 na CUF ilipata majimbo
24. Baadae, baada ya idadi ya majimbo ya
Pemba kupungua na idadi ya majimbo ya
Unguja kuongezeka, mwaka 2000 CCM
ilipata majimbo 35 na CUF ilipata majimbo
15. Mwaka 2005 CCM ilipata majimbo 31
wakati ambapo CUF ilipata majimbo 19.
Mwaka 2010 CCM imepata majimbo 28
wakati CUF imepata majimbo 22.
7
Mgogoro wa kukataa kutambua na
kuyakubali matokeo katika chaguzi hizo
uliathiri uchumi wa nchi, Washirika wa
Maendeleo waliisusia na kuiwekea vikwazo
Zanzibar na uliwagawa wananchi wa Unguja
na Pemba kisiasa na hata kwenye mambo yao
ya kawaida ya kijamii kama vile harusi na
maziko.
Uchaguzi wa mwaka 2000 na wa mwaka
2005
Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2000 ulifanyika
katika mazingira yale yale ya chuki na
uhasama wa kisiasa. Kwa mara nyengine tena
chama cha CUF kilikataa kuyatambua
matokeo ya uchaguzi na pia kilikataa
kumtambua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi Dr. Amani Abeid
Karume. Baada ya uchaguzi, Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi wa upande wa
upinzani (CUF) hawakuhudhuria kabisa
vikao vya Baraza la Wawakilishi na
8
hawakwenda Barazani hata kuapa kiapo cha
uaminifu.
Kutokana na hali hiyo, baada ya mikutano
mitatu ya Baraza kupita bila ya wajumbe hao
kuhudhuria kwenye vikao vya Baraza,
walipoteza sifa za kuwa wawakilishi na
hivyo kupoteza viti vyao kwenye Baraza la
wawakilishi. Matukio ya kuhuzunisha pia
yalitokea tarehe 26 na 27 Januari 2001 kwa
baadhi ya wananchi kupoteza maisha yao na
wengine kwenda ukimbizi kwenye nchi jirani
ya Kenya.
Uchaguzi Mkuu mwengine ulifanyika mwaka
2005 na kwa mara nyengine tena Chama cha
Wananchi CUF kilikataa kuyatambua
matokeo ya uchaguzi wa Rais na pia kilikataa
kumtambua Rais Amani Abeid Karume.
9
Jitihada za Usuluhishi
Jitihada za usuluhishi zilianza kwa
Muwafaka wa Mwanzo kusainiwa tarehe 9
Juni 1999 baina ya CCM na CUF ili kufanya
mazungumzo ya kutatua hali iliyojitokeza
baada ya uchaguzi mkuu wa 1995
(Muwafaka wa Kwanza: Mhe. Mkema na
Mhe. Mloo). Kamati ya Pamoja ya CCM na
CUF yenye Wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi kumi na nne, yaani saba kutoka
kila upande, iliundwa ili kufanya
mazungumzo chini ya usuluhishi wa Katibu
Mkuu wa Jumuiya ya Madola wa wakati huo
Chief Emeka Anyaokou. Kamati hiyo ilianza
kazi mwezi wa Septemba 1999 na kumaliza
mchakato wa mazungumzo mnamo mwezi
wa Julai 2000 na kuwasilisha ripoti Serikalini
yenye mapendekezo ya mambo
yanayohitajika kufanywa ili kutekeleza
muwafaka huo wa kisiasa.
10
Serikali iliandaa Mswada wa Marekebisho ya
Katiba na kupelekwa kwenye Baraza la
Wawakilishi, lakini mswada huo haukupita
kwani ulikataliwa na Wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi kutoka Chama cha Upinzani
CUF ambao walikuwa hawakuridhika na
marekebisho yaliyokuwemo kwenye mswada
huo. Kwa wakati huo Wajumbe wa upande
wa Chama Tawala CCM idadi yao ilikuwa
haitimii theluthi mbili ya Wajumbe wote wa
Baraza iliyohitajika kwa ajili ya kupitisha
marekebisho hayo ya Katiba yaliyotokana na
muwafaka wa kwanza.
Muwafaka wa pili kati ya CCM na CUF
ulisainiwa tarehe 10 Oktoba 2001
(Muwafaka wa Pili: Mhe Mangula na Mhe
Seif Shariff) na baadae mnamo tarehe 30
Novemba 2001 Sheria Nambari 10 ya 2001
ilipitishwa na Baraza la Wawakilishi kwa
madhumuni ya kuunda Tume ya Pamoja ya
Rais ya Kusimamia Utekelezaji wa
11
Muwafaka wa Kisiasa baina ya CCM na
CUF. Tume hiyo ilikuwa na Wajumbe kumi
ambapo watano ni kutoka CCM na watano
kutoka CUF.
Kifungu cha 5 (2) (b) cha Sheria hiyo
Nambari 10 ya 2001 kilitamka wazi wazi
kwamba miongoni mwa majukumu na kazi
za Tume hiyo ni kuanzisha na kufanya
mazungumzo yatayoshirikisha CCM na CUF
kwa madhumuni ya kufungua maeneo
mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo
uwezekano wa kuunda serikali ya umoja wa
kitaifa kwa ridhaa ya wananchi na kwa haja
ya kuamua mustakbala wa Zanzibar katika
nyanja za uchumi, demokrasia na mambo
mengineyo1.
1 Section 5(2)(b) of an Act No. 10 of 2001,
among the functions of the Joint Presidential
Supervisory Commission is to “initiate and
engage in dialogue involving CCM and CUF with
the aim of opening different areas of co-operation
which includes the possibility of forming a
12
Matokeo ya mazungumzo ya Tume hiyo
ndiyo yaliyopelekea kufanyika kwa
Marekebisho ya Nane na Marekebisho ya
Tisa ya Katiba ya Zanzibar mnamo mwaka
2002 na 2003, ili kuingiza kwenye Katiba
yale mambo yaliyokubalika kwenye
muwafaka huo. Hata hivyo, suala la serikali
ya umoja wa kitaifa halikuingizwa kwenye
marekebisho ya Katiba wala halikutekelezwa.
Mabadiliko makubwa yaliyofanyika kwenye
Katiba kupitia Marekebisho ya Nane na ya
Tisa yalikuwa ni kuweka Muundo wa Tume
ya Uchaguzi inayojumuisha Makamishna
kutoka kwenye vyama vya siasa na pia
kuweka utaratibu wa Mheshimiwa Rais
kuteua angalau watu wawili kuwa Wajumbe
wa Baraza la Wawakilishi kutoka upande wa
government of national unity by consent of the
people, and the need to determine the future of
Zanzibar in the spheres of politics, democracy and