-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
i
YALIYOMO
Maelezo Ukurasa
SURA YA KWANZA
...................................................... ..1
1.0. UTANGULIZI
......................................................... 1
SURA YA PILI
...............................................................
5
2. O Muhtasari wa takwimu za uhalifu 2007. ...................
5
2.2 Uchambuzi wa matukio kwa aina ya uhalifu ..............
8
2.2.1 Makosa dhidi ya maadili ya jamii
............................. 8
2.2.2. Makosa ya kuwania mali
...................................... 12
2.2.3 Makosa dhidi ya
binadamu..............................................15
2.3. Uhamiaji haramu
................................................ 20
2.4 Makosa ya Jinai yalivyoripotiwa na jinsi
yalivyoshughulikiwa........................................................25
2.5. Makosa yaliyotendwa na wakimbizi Januari –
Desemba 2007. ..................................................
29
SURA YA TATU
............................................................ 33
3.0 Ajali za Barabarani
.............................................. 33
3.1 Mchanganuo wa Makosa ya Usalama Barabarani .... 33
3.2 Mikakati iliyopo kukabiliana na Tatizo la Ajali za
Barabarani:
........................................................ 38
SURA YA NNE
.............................................................
42
4.0 Matukio ya kushtua
............................................. 42
i Arusha
...............................................................
42
ii Mgomo wa Mahabusu ..........................................
42
iii kinondoni (dsm/kin/pe/01/2007) ..........................
43
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
ii
iv Uvamizi wa Benki tawi la mwanga .........................
43
v Kilimanjaro
......................................................... 44
VI kuchoma jengo la shule moto ...............................
44
SURA YA TANO
........................................................... 45
5.0 Uchambuzi wa Makosa makubwa na madogo ya Jinai
ikilinganishwa na Idadi ya Watu. ...........................
45
SURA YA SITA
............................................................ 65
6.0 MAPENDEKEZO
6.1 HITIMISHO .......ERROR! BOOKMARK NOT DEFINED.
Orodha ya Jedwali
Jedwali Na. 1.2: Mchanganuo wa Makosa Makubwa na
madogo ya Jinai na Usalama Barabarani Januari
hadi Desemba 2006/2007 .....................................
5
Jedwali Na. 2.2: Makosa dhidi ya Maadili ya Jamii – 2006
na 2007
..............................................................
9
Jedwali Na. 3.2: Makosa dhidi ya Mali kwa 2006 na 2007 ....
13
Jedwali Na. 4.2: Makosa dhidi ya binadamu kwa 2006
na 2007
............................................................ 16
Jedwali Na. 6.2: Namna Makosa ya Jinai yalivyoshughulikiwa
kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2007
kimkoa
.............................................................
26
Jedwali Na. 7.2: Makosa yaliyotendwa na Wakimbizi ..........
30
Jedwali Na. 7.2.1: Namna Makosa yaliyotendwa na
Wakimbizi yalivyoshughulikiwa kwa kipindi cha
Januari – Desemba 2007 ....................................
31
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
iii
Jedwali Na. 1.3: Matukio ya Ajali Barabarani kwa kipindi
cha Januari hadi Desemba 2007 .......................... 34
Jedwali Na. 2.3: Mchanganuo wa Makosa ya Ajali za
Usalama Barabarani Januari hadi Desemba ........... 35
Jedwali Na. 3.3: Mchanganuo wa Watu Walioathirika
kwa Ajali Barabarani ..........................................
36
Jedwali Na. 4.3: Matukio ya usalama barabarani (ajali)
kuanzia 2002 - 2007 ..........................................
39
Jedwali Na. 5.3: Mabadiliko ya Matukio ya Usalama
Barabarani kwa Asilimia kwa Mwaka 2002 – 2007 .. 40
Jedwali Na. 3.5: Makosa ya Jinai kwa Idadi ya Watu,
Eneo na Idadi ya Askari ......................................
53
Jedwali Na. 6.5: Mtiririko wa Makosa makubwa ya Jinai
kuanzia mwaka 2002 hadi 2007 .......................... 58
Jedwali Na. 7.5: Idadi ya watu mwaka 2002 hadi 2007 .......
63
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 1 - 65
SURA YA KWANZA
1.0. Utangulizi Tanzania ni moja ya nchi zilizo katika jumuiya
ya Afrika
Mashariki na ina eneo la kilomita za mraba 887,460 (Sq
km). Ipo kati ya nyuzi za Longitudo 29 na 41 kwa
upande wa Mashariki na nyuzi za Latitudo 1 na 12 kwa
upande wa Kusini. Kwa upande wa Mashariki imepakana
na bahari ya Hindi, Kusini nchi ya Msumbiji, Kusini
Magharibi nchi za Zambia na Malawi, Magharibi nchi za
Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo
(DRC), na kwa upande wa Kaskazini nchi za Uganda na
Kenya.
Tanzania ni moja ya nchi zinazofuata utawala wa sheria,
hivyo serikali yake inaendeshwa kidemokrasia. Katika
kutekeleza hili Wizara mbalimbali zimeundwa ili kuweza
kukidhi matakwa ya wananchi wake. Moja ya Wizara hizo
ni Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, ambayo inaundwa
na Idara tano ambazo ni Jeshi la Polisi, Magereza,
Uhamiaji, kikosi cha Zimamoto na Utawala.
Jukumu la Jeshi la Polisi ni kulinda usalama wa raia na
mali zao, kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa,
kukamata wahalifu na kuwafikisha katika vyombo vya
sheria ili washughulikiwe kwa mujibu wa sheria na
taratibu zilizowekwa. Lengo kuu ni kuhakikisha kuwa hali
ya amani na utulivu inadumishwa. Ili kutekeleza
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 2 - 65
majukumu yake ipasavyo, Jeshi la Polisi limegawanywa
katika Idara, vikosi na vitengo. Idara hizo ni Upelelezi wa
Makosa ya Jinai, Utawala na Fedha, Mafunzo na
Uendeshaji, ofisi ya kamishina wa Polisi Zanzibar na ofisi
ya kamishina Kanda Maalumu D’Salaam. Aidha kuna
vikosi ambavyo ni pamoja na Usalama Barabarani, Kikosi
cha Kutuliza Ghasia, Kikosi cha Wanamaji, Polisi Anga,
Polisi Reli, Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Wizi wa
Mifugo ( STPU), Kikosi cha Tazara na vikosi vingine
mbalimbali vilivyo chini ya Makao Makuu ya Polisi kama
vile Kikosi cha Band, Kikosi cha Matengenezo ya Magari
na Kikosi cha Mbwa na Farasi. Lengo kubwa la
mgawanyo huo ni kuwa na usimamizi wa karibu katika
utekelezaji wa majukumu ya kila siku kwa kila Idara,
Kitengo au Kikosi husika.
Idara ya upelelezi wa makosa ya Jinai ina utaratibu wa
kufuatilia na kupima taarifa za uhalifu zilizoripotiwa na
jinsi zilivyoshughulikiwa katika vituo vyote vya Polisi
nchini. Utaratibu huo huliwezesha Jeshi la Polisi
kutambua mwenendo wa uhalifu ulivyo katika nchi
mzima, na hivyo kuwa na uwezo wa kutabiri matukio ya
uhalifu na hivyo kubuni na kupanga mikakati ya
kukabiliana na uhalifu na wahalifu katika wakati uliopo
na ujao.
Hii ni Taarifa ya Uhalifu nchini kwa mwaka wa 2007.
Hivyo taarifa hii itaangalia matukio ya uhalifu
yaliyoripotiwa katika kipindi cha Januari hadi Desemba
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 3 - 65
2007 yakilinganishwa na Januari hadi Desemba 2006,
vyanzo vya makosa hayo na juhudi zinazofanywa
kukabiliana na uhalifu nchini kwetu.
1.1 Hali ya Uhalifu kwa Mwaka 2007
Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007, Matukio
ya uhalifu yaliyoripotiwa katika vituo vya Polisi nchini
kote yalikuwa 740,213 ikilinganishwa na kipindi cha
Januari hadi Desemba 2006 ambapo matukio yalikuwa
538,497. Idadi hii ya matukio inajumuisha matukio ya
Jinai, ajali na makosa ya usalama barabarani. Matukio
haya yanaonyesha ongezeko la matukio 201,716 sawa
na asilimia 37.3.
Kuongezeka kwa matukio haya kumechangiwa na
sababu mbalimbali, zikiwemo kukua kwa sayansi na
teknolojia, utandawazi, ukosefu wa ajira, umasikini,
ukuaji wa miji (Urbanisation), ongezeko la makazi holela,
kuibuka na kuongezeka kwa imani za kishirikina na
wimbi la ongezeko la baadhi ya wakimbizi wanaojiingiza
katika vitendo vya uhalifu. Pia udhaifu wa baadhi ya
sheria zetu ambazo zimepitwa na wakati na hivyo
kuhitaji marekebisho ya msingi, udhaifu wa watendaji
katika mfumo mzima wa udhibiti wa sheria na utoaji
haki.
Katika kukabiliana na changamoto zinazoletwa ongezeko
la uhalifu kama ilivyoainishwa na takwimu hapo juu,
Idara ya Upelelezi wa Jinai. Idara inaendelea na
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 4 - 65
mchakato wa kubuni mikakati mbali mbali
itakayoiwezesha Idara kudhibiti hali hiyo ambalo ndio
jukumu la msingi la Idara. Mikakati inayobuniwa inaenda
sambamba na mihimili mikuu mitatu ya kisera ya Jeshi la
Polisi katika kuboresha huduma inayotolewa kwa
wananchi na Jeshi la Polisi ambalo ni kulinda usalama wa
raia na mali zao na kuhakikisha utengamano unakuwepo
kwa kusimamia sheria. Mihimili ya kisera ya Polisi
ambayo ndio dira ya idara katika kubuni mikakati yake ni
• Weledi (Professionalism), • Usasa (Modernisation), na • Ulinzi
shirikishi (Commuinity Policing).
Idara kwa kutumia falsafa tajwa hapo juu, inaimarisha
vitengo vyake ili vitekeleze majukumu ya kupambana na
kudhibiti uhalifu kwa viwango ambavyo jamii ya
watanzania wa leo wanavitarajia. Mafunzo ya kada mbali
mbali katika fani ya upelelezi wa jinai yanaimarishwa ili
kujenga weledi ambao ni ujuzi utakaosaidia kuharakisha
upelelezi wa kesi kwa ufanisi, Upatikanaji wa zana za
kisasa za upelelezi na utendaji wa kazi kuanzia kwa
wapelelezi na wachunguzi katika maabara ya Polisi
ambapo usasa utatumika katika kushughulikia kesi za
jinai na ushirikishwaji wa wadau mbali mbali katika
jitihada za kukabiliana na uhalifu. Kwa kufahamu kuwa
matatizo mengi ya uhalifu yanatokana na jamii yenyewe,
Idara inafanya juhudi za kushirikiana na taasisi rasmi za
udhibiti, taasisi za kijamii na za kimataifa kuhakikisha
mapambano dhidi ya uhalifu yanapata msukumo
unaostahili.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 5 - 65
SURA YA PILI
2. O Muhtasari wa Takwimu za Uhalifu 2007. Jumla ya matukio yote
ya uhalifu kwa mwaka huu ni
740,213 kwa nchi nzima, matukio yaliyochukua nafasi
kubwa ni yale ya jinai. Katika aina hii ya makosa,
matukio 509,462 yaliripotiwa ambayo ni sawa na 68.8%
ya matukio yote. Matukio ya usalama barabarani
yalikuwa 230,751 sawa na 31.2% ya matukio yote.
Taarifa ya matukio ya jinai na usalama barabarani
imefafanuliwa katika jedwali Na. 1.2
Jedwali Na. 1.2:
2..1 Mchanganuo wa Makosa Makubwa na madogo ya Jinai na Usalama
Barabarani Januari hadi Desemba 2006/2007
Januari– Desemba
2006
Januari – Desemba
2007
Tofauti
2007-2006
Asilimia
2007-2006
JINAI
MADOGO 359,848 420,935 61,087 17.0
MAKUBWA 68,781 88,527 19,746 28.7
JUMLA 428,629 509,462 80,833 18.9
USALAMA BARABARANI
MADOGO 91,681 205,600 113,919 124.2
MAKUBWA 18,187 25,151 6,964 38.2
JUMLA 109,868 230,751 120,883 110.0
JUMLA KUU 538,497 740,213 201,716 37.3
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 6 - 65
Uchambuzi wa Matukio ya Uhalifu Nchini
Uhalifu wa makosa ya jinai umegawanyika katika
makundi makuu matatu:
• Makosa dhidi ya mali • Makosa dhidi ya binadamu • Makosa dhidi
ya maadili ya jamii.
Jumla ya makosa makubwa ya jinai yaliyoripotiwa katika
vituo mbalimbali vya Polisi katika kipindi cha Januari
hadi Desemba 2007 ni 88,527 ikilinganishwa na makosa
68,781 yaliyoripotiwa kwa kipindi kama hicho cha
Januari hadi Desemba 2006 ambalo ni ongezeko la
makosa 19,746 sawa na 28.7%.
Kwa ujumla uhalifu wa makosa ya jinai kwa kipindi cha
Januari hadi Desemba 2007 umepanda ikilinganishwa na
Januari hadi Desemba 2006, kama takwimu za hapo juu
zinavyoonesha. Kuongezeka kwa takwimu za idadi ya
makosa ya jinai kumesababishwa na sababu kadhaa za
kiuchumi na kijamii kama inavyofahamika uhalifu ni
tatizo ya kijamii, pamoja na ukweli kwamba utendaji wa
makosa pia uliongezeka, Hata hivyo,pia ongezeko la
kitakwimu linaloonekana sasa limetokana pia na
mikakati ya Jeshi la Polisi kuwashirikisha wananchi kwa
kutumia falsafa ya Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi.Hii
imechangia kwa kiasi kikubwa kukuza uhusiano na
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 7 - 65
wananchi na hivyo kuwa huru kutoa taarifa za uhalifu
kwa Jeshi la Polisi bila woga.Taarifa za wananchi
zimesaidia Jeshi la Polisi kuchukua hatua zilizopelekea
ongezeko la mashauri yaliyoripotiwa kwenye vituo vya
Polisi.
Tatizo la upungufu wa askari (Staff strengths) ndani ya
Jeshi la Polisi unachangia kuongezeka kwa matukio
mengi ya uhalifu, kwani yapo maeneo katika nchi yetu
ambayo kwa kipindi kirefu yamekosa huduma ya Polisi
kutokana na uhaba wa askari ikilinganishwa na idadi
halisi ya wananchi (Population) katika maeneo husika,
hivyo uwiano kati ya idadi ya askari na wananchi
wanaowahudumia na ukubwa wa maeneo kwa mraba,
kutoshabihiana. Mathalani, uwiano wa kimataifa ni askari
Polisi 1 kwa watu 400 hadi 700. Na wastani kwa nchi
zilizoendelea ni askari Polisi 1 kwa watu 250 hadi 350;
lakini katika nchi yetu wastani wa uwiano ni kwa askari
Polisi 1 kwa watu 1300. Uwiano huu ni mkubwa mno
kuwawezesha askari wetu kutoa huduma itakayoridhisha
wananchi wote. Aidha, Kukosekana kwa uwepo wa askari
katika baadhi ya maeneo ya nchi yetu, ni kichocheo kwa
wahalifu kutimiza azma yao bila kuhofia hatua za
kisheria dhidi yao.
Ni imani ya Jeshi la Polisi, kwamba serikali kwa kadri ya
uwezo wa kiuchumi utakavyoruhusu itapunguza tatizo
hili kwa kuongeza idadi ya askari wanaoajiriwa.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 8 - 65
Graph 1.2.1
2.2 Uchambuzi wa Matukio kwa aina ya Uhalifu
2.2.1 Makosa dhidi ya Maadili ya Jamii Haya ni makosa
yanayokiuka maadili mema ya jamii,
kama vile matumizi na usafirishaji wa madawa ya
kulevya, rushwa n.k. Makosa haya kuongezeka au
kupungua kwake hutegemea sana juhudi za Polisi katika
kukusanya taarifa na kuendesha misako ya mara kwa
mara. Juhudi hizo zikiimarishwa ukamataji wa makosa
hayo huongezeka pia.
Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007 jumla ya
makosa 14,036 dhidi ya maadili ya jamii yaliripotiwa
ambayo ni ongezeko la makosa 4,004 sawa na aslimia
39 ikilinganishwa na taarifa ya mwaka 2006 kama
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 9 - 65
inavyoonekana katika Jedwali nambari 2.2
Jedwali Na. 2.2: Makosa dhidi ya Maadili ya Jamii - 2006 na
2007
Makosa Januari– Desemba
2006 Januari – Desemba
2007 Tofauti
Asilimia(%)
Madawa ya kulevya 377 318 - 59 -15.65 Bhangi 5,020 5,521 501
9.98 Mirungi 296 471 175 59.12 Nyara za serikali 720 791 71 9.86
Magendo 60 39 - 21 -35.00 Rushwa 37 34 - 3 -8.11 Pombe ya moshi
2,690 5,937 3,247 120.71 Mitambo ya pombe ya moshi - 133 133 0
Kupatikana na risasi - 189 189 0 Kupatikana na silaha 832 585 247
29 Kupatikana na bomu - 18 18 0 JUMLA 10,032 14,036 4,004 39
Graph 2.2.1
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 10 - 65
Mikakati iliyopo kukabiliana na Makosa ya Maadili
ya Jamii
Kama ilivyoelezwa hapo juu, ongezeko la makosa ya
maadili ya jamii kwa mwaka 2007 kulinganisha na
mwaka 2006 linatokana na sababu kuu mbili: Kwanza,
haya ni makosa ambayo yanatokana na juhudi za polisi
katika kufanya misako na operesheni mbali mbali, hivyo
ongezeko la takwimu linaweza kusababishwa na
ongezeko la ufanisi wa Polisi katika utekelezaji wa
majukumu yao, pili ongezeko linaweza kusababishwa na
ongezeko halisi la shughuli za uhalifu katika makosa
haya; Hali ambayo inatokana na matatizo ya utendaji wa
Polisi kutokana na athari za upungufu wa vitendea kazi
ambapo Jeshi la Polisi hufanya kazi katika mazingira
magumu na hivyo kuathiri kwa kiwango kikubwa cha
ufanisi.
Makosa ya kupatikana na Bangi na Pombe ya Gongo ni
makosa yaliyokithiri kutokana na sababu za kiuchumi.
Kilimo cha mashamba makubwa ya bangi kinaendelea
kushamiri nchini kwa kuwepo kwa soko la ndani na nje.
Jeshi la Polisi limeendelea kuharibu mashamba ya bangi
katika Mikoa ya Mara, Arusha, Morogoro, Shinyanga,
Iringa na Mbeya. Aidha, Madawa ya kulevya toka nje ya
Tanzania kama vile Heroine kutoka Asia na Cocaine
kutoka Amerika ya Kusini yameendelea kuonekana
nchini kwetu na kuwa kero. Vijana wa Kitanzania
wanaendelea kujihusisha na biashara hii nje ya nchi yetu
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 11 - 65
na kutia doa jina la nchi yetu na kuleta athari kubwa
nchini.
Kwa kuzingatia hali ya ongezeko la makosa ya maadili
ya jamii, Jeshi la Polisi litaendelea na kukabiliana na
changamoto hiyo kwa kuishirikisha Jamii katika
mapambano haya,
Kwani makosa yanayoongoza kwa mbali ki -takwimu ya
kupatikana na Pombe ya Moshi na Bangi ni makosa
yaliyoenea kwenye jamii zetu na yanatokana na hali
halisi ya kiuchumi wa jamii husika. Utatuzi wake
utafanikiwa si kwa juhudi za Polisi pekee, bali wanajamii
wote hususan wale waliopewa jukumu la kuongoza
serikali kuanzia za mitaa hadi taifa kwa kubuni mikakati
mbadala ya kiuchumi, Jeshi la Polisi litaendelea na
misako ya mara kwa mara katika juhudi za kudhibiti
tatizo hili. Aidha, viongozi wa kijamii wanajukumu kubwa
katika kuiandaa jamii kufuata maadili mema ya jamii
yenyewe.
Jeshi la Polisi kwa upande wake litaendelea kuimarisha
ukusanyaji wa taarifa za kiintelijensia kuhusu wahalifu
wanaojihusisha na makosa haya,na hususan yale yenye
kuvuta hisia za jamii kama madawa ya kulevya toka nje
ya nchi na rushwa. Kwa kutumia wananchi na wadau
mbali mbali, Jeshi litaweza kuendesha operesheni sahihi
za kudhibiti makosa haya. Hata hivyo ni mategemeo ya
Jeshi la Polisi kwamba, ufanisi katika udhibiti wa makosa
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 12 - 65
haya utapatikana iwapo Jeshi litajengewa uwezo wa ki –
zana za kutendea kazi.
2.2.2. Makosa ya kuwania Mali
Makosa ya kuwania mali ni makosa ambayo hufanywa na
mtu kwa utashi wake ambapo mhalifu huwa na nia ya
kupata mali kwa kumdhulumu mtu mwingine. Mara
nyingine aina hii ya makosa hutendwa kwa kutumika
nguvu kupita kiasi na kuleta madhara makubwa yasiyo
tarajiwa kwa mtu au mali. Baadhi ya makosa haya ni
Unyang’anyi wa kutumia silaha, Unyang’anyi wa kutumia
nguvu, Wizi wa magari, Wizi wa pikipiki, Wizi katika
Taasisi za fadha hasa (Mabenki, Maduka ya kuuza na
kununua fedha), Wizi wa Silaha, Kuchoma nyumba
moto, Kuharibu mali n.k.
Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007 jumla ya
makosa 60,913 yaliripotiwa, na kipindi cha Januari hadi
Desemba 2006 jumla ya makosa 51,034 yaliripotiwa.
Kuna ongezeko la makosa 9,879 sawa na asilimia 19.4%
aidha takwimu zinaonyesha kuwa wizi katika benki
umeongezeka kwa makosa 17 mwaka 2007
ikilinganishwa na makosa 6 kwa mwaka 2006 sawa na
asilimia 283.3%. Wizi wa magari umepungua kwa
makosa 33 kwa mwaka 2007 ikilinganishwa na makosa
287 ya mwaka 2006 sawa na asilimia 11.5 kama
inavyoonyeshwa kwenye Jedwali Na. 3.2.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 13 - 65
Jedwali Na. 3.2: Makosa dhidi ya Mali kwa 2006 na 2007
Makosa Januari– Desemba Januari – Desemba
Tofauti
2006 2007 Asilimia(%)
Wizi wa silaha 72 104 32 44.4 Unyang"anyi wa k/silaha 1,028
1,108 80 7.8 Unyang"anyi wa k/nguvu 4,620 7,198 2,578 55.8 Uvunjaji
20,413 20,904 491 2.4 Wizi 18,107 21,708 3,601 19.9 Wizi wa
pikipiki 118 222 104 88.1 Wizi wa magari 287 254 -33 -11.5 Noti
bandia 389 487 98 25.2 Wizi wa mifugo 3,904 5,153 1,249 32 Wizi k/
mabenki 6 23 17 283.3 Wizi k/ mashirika ya umma 0 383 383 0 Wizi k/
vyama vya ushirika 0 18 18 0 Wizi k/ serikali za mitaa 0 27 27 0
Wizi k/ serikali kuu 0 129 129 0 Kuchoma nyumba moto 2090 2943 853
40.8 Ajali ya moto 0 252 252 0 Jumla 51,034 60,913 9,879 19.4
Graph 3.2.1
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 14 - 65
Uchambuzi wa Makosa ya kuwania Mali na Mikakati
ya kukabiliana na Makosa hayo
Kuna ongezeko la jumla la makosa ya kuwania mali
mwaka 2007 ukilinganisha na mwaka 2006 kwa asilimia
20%. Ukiacha upungufu katika wizi wa magari, takriban
makosa yote katika sehemu hii yanaonekana
kuongezeka. Makosa ya Uvunjaji na wizi yanaendelea
kuongoza kwa mbali katika tawimu za uhalifu nchini
kwetu. Hali hii ina uhusiano wa moja kwa moja na hali
halisi ya kiuchumi ya wananchi wetu na nchi kiujumla.
Ukosefu wa ajira za uhakika ndio msukumo unaopelekea
wananchi kujitosa katika uvunjaji ili kuweza kukidhi
mahitaji ya msingi.
Ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili si rahisi kupatikana
kwa kuzingatia ufumbuzi wa matatizo ya kiuchumi kitaifa
na kimataifa si rahisi pia. Tatizo la makosa ya uvunjaji
na wizi hustawi pale ambapo mazingira yanashawishi
wahalifu kutekeleza azma yao. Maeneo yenye giza,
miundo mbinu mibovu kama vile ujenzi holela hufanya
kazi ya udhibiti wa uhalifu wa aina hii kuwa ngumu.Hata
hivyo Idara atazidi kupanga mikakati ya kuimarisha
hatua za kuzuia kwa kusisitiza doria katika maeneo
yaliyokithiri kwa matatizo kwa uvunjaji na wizi.
Udhibiti wa silaha haramu mipakani, Kuimarisha
mafunzo ya stadi za teknolojia za kisasa zinazotumiwa
na wahalifu wa kisasa kuiba, Kushirikiana na wadau
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 15 - 65
rasmi na wananchi, ni miongoni mwa mikakati ya Idara
katika kukabiliana na makosa haya. Katika ngazi ya
Taifa, kuna mafanikio yaliyoonekana kwa kuwatumia
wadau katika mapambano ya uhalifu wa kuwania mali
hasa ujambazi wa kutumia silaha. Juhudi zinaelekezwa
kwenye ngazi ya mikoa na wilaya, ili mtandao wa
ushirikiano wa wadau rasmi uweze kupanuka nchini
kote, na hivyo kuleta matokeo chanya katika udhibiti wa
makosa haya.
Mkakati mwingine ni kuimarisha mfumo wa kuyatambua
magenge ya uhalifu na kuweza kuzuia kabla ya
utekelezaji wa azma yao, hii itawezekana kwa
kuimarisha mfumo wa utafutaji wa habari za uhalifu na
wahalifu kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa na hii
itawezekana kwa kuimarisha vitengo vya Intelijensia.
Hata hivyo, baadhi ya mikakati ya idara inahitaji uwezo
wa kiuchumi wa kitaifa kugharimia na hivyo kuleta
ufanisi unaotarajiwa ni matumaini yetu serikali kwa
upande wake utaona umuhimu wa kulinda mali za
wananchi wake na athari zake ki usalama na hivyo kutoa
kipaumbele katika kugharamia hatua hizo.
2.2.3. Makosa dhidi ya Binadamu:
Makosa dhidi ya binadamu ni makosa ambayo huathiri
utu wa binadamu na maisha yake. Makosa hayo ni
Mauaji, Kulawiti, kubaka, wizi wa watoto, kutupa watoto,
usafirishaji haramu wa binadamu, na uhamiaji haramu.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 16 - 65
Hivi karibuni kumejitokeza hujuma dhidi ya walemavu
hususan albino, na baadhi ya wananchi kuchunwa ngozi
kwa sababu za imani potofu za kishirikina, ili wahusika
wafanikiwe katika harakati za kujasiria mali.
Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007 jumla ya
makosa 13,578 yaliripotiwa wakati Januari hadi
Desemba 2006 makosa 7,715 yaliyoripotiwa sawa na
ongezeko la makosa 5,863 ambayo ni asilimia 75.9
Aidha, mwaka 2007 yameongezeka makosa 917 ya
mauaji ambayo ni sawa na asilimia 37.2 ongezeko hili
linajumuisha mauaji yaliyoambatana na imani za
ushirikina. Jedwali 4.2 linaonyesha takwimu
Jedwali Na. 4.2: Makosa dhidi ya binadamu kwa 2006 na 2007
Makosa
Januari – Desemba Januari – Desemba
Tofauti
2006 2007 Asilimia(%)
Mauaji 2,612 3,583 971 37.2
Kubaka 4,278 8,894 4,616 107.9
Kulawiti 512 567 55 10.7
Wizi wa watoto 38 71 33 86.8
Kutupa watoto 86 157 71 82.6
Wahamiaji haramu 189 306 117 61.9
Jumla 7,715 13,578 5,863 75.9
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 17 - 65
Graph Na. 4.2.1
Uchambuzi wa vyanzo vya Makosa na Mikakati ya
Udhibiti
Kulingana na takwimu kuna ongezeko la makosa dhidi ya
binadamu mwaka 2007 ikilinganishwa na mwaka 2006.
Makosa ya mauaji yaliongezeka kwa asilimia 37.2
Makosa ya kubaka kwa asilimia 107. Makosa ya kulawiti
kwa asilimia 10.8, na asilimia 86. 2 kwa kosa la kutupa
watoto, asilimia 82.6 kwa makosa ya wizi wa watoto, na
asilimia 61.9 kwa kosa la Uhamiaji Haramu.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 18 - 65
Uchambuzi wa vyanzo vya makosa ni kama ifuatavyo:
Mauaji:
Sababu kubwa za mauaji ni kuwania mali kama vile
katika matukio ya ujambazi, uporaji na wizi wa mifugo
na imani za ushirikina. Mikoa ya Mwanza, Kagera,
Shinyanga, Tabora na Dar es salaam zimeongoza kwa
mauaji na sababu inayoongoza ni kuwania mali
ikifuatiwa na ushirikina. Sababu hii ya ushirikina
inatokana na ufinyu wa elimu ya wananchi wetu na
ufukara na tamaa ya utajiri wa haraka. Kutokana na
ufinyu wa elimu bado wananchi wanahadaiwa na
waganga wa jadi wanaoshawishi kutenda mauaji aidha
kwa kisasi au tamaa ya utajiri wa haraka.
Mauaji mengine yanatokana na wivu wa mapenzi,
kuwania mali, ugomvi wa kawaida, ulevi ama kuficha
uhalifu. Ongezeko la takwimu za mauaji linaashiria kuwa
bado kuna kazi kubwa ya serikali kutilia mkazo katika
sekta ya elimu. Ni elimu pekee itakayoweza kupanua
ufahamu wa watu na hivyo kuchukua hatua sahihi katika
mwenendo wa maisha yao na kuachana na imani potofu.
Aidha,Kwa kushirikiana na wadau wengine kama vile
waganga wa jadi viongozi wa dini mbalimbali ambao kwa
namna moja ama nyingine wana mchango mkubwa
kufanikisha kudhibiti uhalifu huo.
Kubaka:
Sababu kubwa inayosababisha kosa hili ni kujiridhisha
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 19 - 65
kimapenzi, Imani za kishirikina, ulevi uliokithiri wa
pombe au madawa ya kulevya, na uduni wa kipato. Hata
hivyo ongezeko la takwimu za kosa hili pia
limesababishwa na mabadiliko ya kisheria ambapo
makosa ambayo awali hayakuwa na hadhi ya kosa la
kubaka sasa yameingizwa katika kifungu hiki mfano kosa
la kufanya mapenzi na mtoto wa shule sasa ni kubaka
hata kama kulikuwa hakuna matumizi ya nguvu. Athari
zake ni ongezeko la kitakwimu la makosa haya. Pia
ongezeko hili linaonesha bado jamii yetu inahitaji
kiwango cha juu cha maadili ili kupata suluhu la udhibiti
wa tatizo hili.
Kulawiti:
Sababu hazitofautiani sana na kosa la kubaka na
ongezeko linaonesha kiwango cha mmong’onyoko wa
maadili katika jamii yetu.
Wizi watoto:
Sababu ni kutaka watoto kwa wasioweza kuzaa,
kukomoana na visasi na imani za kishirikina.
Kutupa watoto:
Sababu za kijamii, kuogopa kukaripiwa na ndugu kwa
wasichana wadogo, mimba zisizotarajiwa na kupangwa,
kutelekezwa na wanaume waliowapa mimba. Zipo pia
sababu za kiuchumi kwa wanaojiuza kutotaka kulea
mtoto; sababu za kiafya kwa wanaopata kichaa cha
mimba nk.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 20 - 65
2.3 Uhamiaji Haramu
Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007 jumla ya
wahamiaji haramu 2,644 wa mataifa mbalimbali
walikamatwa, ikilinganishwa na wahamiaji haramu 189
waliokamatwa katika kipindi kama hicho mwaka 2006.
Takiwimu hizo zinaonyesha kuna ongezeko la wahamiaji
haramu 117 ambao ni sawa na asilimia 61.90%.
Idadi kubwa ya wahamiaji haramu waliokamatwa nchini
wanatoka katika mataifa ya Somalia na Ethiopia. Aidha
wapo wahamiaji haramu waliotoka katika mataifa ya
Congo, Rwanda, India, Iran, Burundi, Malawi na
Pakistan.
Uchunguzi umebaini kwamba wahamiaji wengi haramu
wanaokamatwa huingia nchini kupitia mikoa ya Mbeya,
Kilimanjaro, Mtwara, Tanga, Arusha na Mara wakiwa
safarini kuelekea Afrika Kusini, Ulaya na Marekani kama
inavyoonyeshwa kwenye jedwali 5.2 hapa chini.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 21 - 65
Jedwali Na. 5.2
Mkoa Walioka-matwa
Idadi
ya Kesi
UTAIFA
Somalia Pakistan
Ethiopia
Kenya
Burundi India Congo Mozambiq Zimbabwe
Jumla ya Waliokamatwa
M F M F M F M F M F M F M F M K M F M F
Arusha 28 98 24 40 - 27 - - - - 165 25
D’salaam 14 - 14 - - - - - 145
Iringa 14 248 94 2 1 - - - - 344 1
Kagera 1 - - 11 - - - - 11 -
K’njaro 5 111 22 - - - - 133 -
Mbeya 19 200 162 - - - - 362 -
Pwani 36 159 235 2 - - - - 396 -
Tanga 32 212 49 - 4 - - - - 267 2
Lindi 1 32 1 13 - - - - - 46 -
Mtwara 6 169 4 47 2 1 1 3 16 - - - 243 -
Mara 35 2 2 56 - - - - 60 -
Singida 1 1 - - - - - 1 -
Kigoma 77 - - 400 17 - - - - 400 17
Ruvuma 24 - 26 - - - 26 -
Rukwa 2 - 10 - - - - 10 -
Tabora 1 13 - - - - - 13 -
Dodoma 1 - - 541 14 - - - - - -
Morogoro 1 5 - - - - - - -
Mwanza 4 - - 10 - - - - 10 -
Reli 4 - 12 - - - - 12 -
Jumla 306 1250 25 58 - 661 64 34 1 946 32 42 - - - 2644 44
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 22 - 65
Graph Na. 5.2.1
Uchambuzi wa Takwimu za Idadi ya kesi za
Wahamiaji Haramu
Kesi za wahamiaji haramu huhusisha wageni wanaotoka
nchi zao na kuingia nchini mwetu bila kufuata utaratibu
wa kisheria. Tawimu zilizopo zinaonesha kuwa mikoa ya
mipakani ya Kigoma, Arusha, Pwani, Mbeya, Mara,
Ruvuma, Tanga, Mtwara inaongoza kwa kukamatwa
wahamiaji haramu wengi. Hali hii inasababishwa na
mikoa hiyo kuwa njia ya kuingilia na kutokea nchini
mwetu. Aidha, matatizo ya kisiasa eneo la maziwa
makuu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Burundi
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 23 - 65
imepelekea Mkoa wa Kigoma kuongoza. Upande
mwingine matatizo ya kiusalama na kiuchumi eneo la
Pembe ya Afrika imepelekea Mikoa ya Arusha, Pwani,
Mara na Tanga kuongoza kwa idadi ya kesi.
Uchambuzi wa Tatizo la Wahamiaji Haramu
Kosa hili ni moja ya uhalifu unaokuja kwa kasi katika
miaka ya karibuni. Wahamiaji wengi wanaokamatwa
nchini ni wale wanaotoka katika nchi za pembe ya Afrika
ambako kuna migogoro ya kisiasa na matatizo
makubwa ya kiuchumi. Nchi za Somalia na Ethiopia
zinaongoza kwa kutoa wahamiaji haramu nchini kwetu.
Wengi wa wahamiaji hawa wanaitumia nchi yetu kama
mapito ya safari yao kwenda Afrika Kusini ambako kuna
imani kwamba kuna kazi nyingi kufuatia nchi hiyo kuwa
mwenyeji wa mashindano ya Kombe la Dunia mwaka
2010.
Takwimu zinaonesha kwamba wageni wengi huingia
kupitia mikoa ya kaskazini ya Arusha, Tanga,
Kilimanjaro, Mara na ukanda wa Pwani ukiongozwa na
mkoa wa Pwani. Aidha, takwimu zinaonesha kwamba
Watu hao huelekea Mikoa ya Kusini ya nchi yetu ya
Mtwara, Mbeya na Rukwa. Aidha, takwimu zinaonesha
ukamataji umefanywa katika mikoa ya barabara kuu
ziendazo kusini ya Lindi na Iringa.Hii inaonesha wazi
wageni kutoka Ethiopia na Somalia wanatumia nchi yetu
kama mapito.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 24 - 65
Mikakati ya Kupambana na Makosa dhidi ya
Binadamu
Makosa dhidi ya binadamu ni makosa yanayoleta
mshtuko na athari kubwa kwa jamii kwa muda mrefu.
Ongezeko la takwimu kiujumla linatokana na sababu za
kimaadili na kiuchumi kutokana na hali halisi ya jamii
yetu. . Makosa haya hayawezi kudhibitiwa na Polisi
pekee yanahitaji jamii nzima kushughulikia. Jeshi
linaendelea kubuni na kupanga mikakati ya kuhakikisha
uhalifu dhidi ya binadamu unadhibitiwa. Msisitizo sasa
uko kwenye kujenga ushirikiano na wadau na wananchi.
Kwa kuwashirikisha viongozi wa kijamii kama vile wa
madhehebu ya dini na vyama vya kijamii (NGO).
Pamoja na hayo, Jeshi limeanzisha mkakati wa
kuutambua mtandao wa waganga wa kienyeji ( wapiga
ramli) ambao huwapotosha wananchi kutenda makosa
haya kwa imani kuwa wameathiriwa na wahanga wa
matendo hayo au watapata utajiri kwa kutenda makosa
hayo.
Tunaamini tunaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa
makosa haya baada ya kutolewa elimu kama
ilivyoainishwa hapo juu. Kwa makosa yanayohusisha
kuwania mali, Jeshi linaendelea na mikakati yake ya
kupunguza matukio hayo kwa kuimarisha doria na ulinzi
wa maeneo muhimu.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 25 - 65
Aidha, kwa kosa la Uhamiaji Haramu Jeshi limeunda
Task Force inayowashirikisha watendaji kutoka vyombo
vingine vya udhibiti kama vile idara ya Uhamiaji, TRA,
TISS ili kushughulikia tatizo hili. Mafanikio
yaliyopatikana ni pamoja na kuanza kuyabaini magenge
ya wahalifu wanaofanya biashara ya kusafirisha watu
katika nchi za Kenya, Ethiopia,Tanzania na Afrika kusini.
Tatizo hili linahusisha nchi zaidi ya moja na mikakati
yetu inalenga kushirikisha nchi majirani ili tuwe na
ufumbuzi wa pamoja.
2.4 Makosa ya Jinai yaliyoripotiwa na jinsi
yalivyoshughulikiwa kwa kipindi cha Januari hadi
Desemba 2007.
Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007, jumla ya
kesi 88,527 ziliripotiwa nchi nzima. Kati ya hizo, kesi
30,946 zilipelekwa mahakamani; kesi 6,390 zilifanikiwa
mahakamani; kesi 2,287 zilishindwa mahakamani; kesi
9,790 zilifungwa na kesi 37,376 ziko chini ya upelelezi.
Aidha kesi zilizokataliwa Polisi kwa sababu mbalimbali ni
1,738. Mchanganuo wa namna kesi hizo
zilivyoshughulikiwa kwa kila mkoa ni kama
inavyoonekena katika jedwali nambari 6.2.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 26 - 65
Jedwali Na. 6.2: Namna Makosa ya Jinai yalivyoshughulikiwa kwa
kipindi cha Januari hadi Desemba 2007 kimkoa
Mkoa
Kesi Kesi Kesi zilizo Kesi Kesi zilizoko Kesi Kesi
Zilizoripotiwa Zilizokataliwa Chini ya upelelezi Zilizofungwa
Mahakamani Zilizofanikiwa Zilizoshindwa
Arusha 4,167 289 1,550 523 1,414 331 60
Dar es Salaam 6,584 355 2,073 1,299 2,431 399 27
Dodoma 2,709 23 1,010 719 660 270 27
Iringa 5,153 9 2,275 645 1,903 291 30
Kagera 4,782 43 1,631 482 2,212 338 76
Kigoma 3,415 15 1,612 621 1,061 71 35
Kilimanjaro 5,076 91 2,303 934 1,510 112 126
Lindi 3,841 30 1,130 383 1,922 98 278
Manyara 2,705 - 1,196 84 1,200 125 100
Mara 3,991 - 1,842 184 1,630 229 106
Mbeya 2,638 170 710 340 558 650 210
Morogoro 6,764 361 3,764 107 2,032 407 93
Mtwara 1,971 31 799 200 562 347 32
Mwanza 5,729 - 2,169 155 2,654 582 169
Pwani 4,001 79 1,572 320 1,665 258 107
Rukwa 2,920 52 1,164 513 857 299 35
Ruvuma 4,884 30 2,846 264 1,623 56 65
Shinyanga 4,339 29 1,442 712 962 616 578
Singida 1,888 27 762 233 652 178 36
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 27 - 65
Mkoa
Kesi Kesi Kesi zilizo Kesi Kesi zilizoko Kesi Kesi
Zilizoripotiwa Zilizokataliwa Chini ya upelelezi Zilizofungwa
Mahakamani Zilizofanikiwa Zilizoshindwa
Tabora 5,454 93 3,099 546 1,505 164 47
Tanga 3,468 - 1,583 244 1,304 291 46
JUMLA - BARA 86,479 1,727 36,532 9,508 30,317 6,112 2,283
- - - - -
Kaskazini Unguja - - - - - -
Kusini Unguja - - - - - -
Mjini Magharibi - - - - - -
Kaskazini Pemba - - - - - -
Kusini Pemba - - - - - -
JUMLA - VISIWANI 1,564 11 618 242 479 214 -
VIKOSI VINGINE 484 - 226 40 150 64 4
JUMLA - TANZANIA 88,527 1,738 37,376 9,790 30,946 6,390
2,287
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 28 - 65
Uchambuzi wa jinsi makosa yalivyoshughulikiwa
Takwimu hizi, zinaonesha wazi kuna changamoto za
msingi kuhakikisha kuwa ufanisi katika upelelezi wa kesi
unaimarishwa. Kwani ni asilimia 7 tu ambayo kesi zake
zimefanikiwa kwa watuhumiwa kupatikana na hatia,
asilimia 42 kesi hizo bado upelelezi kukamilika, asilimia
34 kesi bado zipo mahakamani. Wakati asilimia 11.5 kesi
hizo zimefungwa kwa sababu mbalimbali kama vile
kukosekana ushahidi n.k. Ingawa ni asilimia 3 ya kesi
hizo watuhumiwa waliachiwa huru na mahakama.
Hali tajwa hapo juu inatokana na sababu kadhaa; uhaba
wa askari wapelelezi, uhaba wa vitendea kazi, ujuzi
mdogo wa baadhi ya wapelelezi wetu na zingine zilizo
nje ya Idara kama vile ucheleweshaji wa taarifa za
kitaalamu, kukosekana kwa mashahidi muhimu, uhaba
wa watumishi na majengo ya mahakama.
Mikakati ya kukabiliana na hali hiyo inabuniwa kila mara,
kuwepo kwa kamati za kusukuma kesi mahakamani
katika ngazi ya mikoa na wilaya ni moja ya mikakati
hiyo.(Case Flow Management Committees) ambapo
tathmini ya vyanzo vya ucheleweshaji wa kesi hufanywa
na hatua kuchukuliwa kuharakisha upelelezi na usikilizaji
wa kesi .
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 29 - 65
Kwa upande wake Jeshi linaendelea na mipango wa
kuongeza idadi ya wapelelezi na mafunzo ya wapelelezi
hao ili kukuza ufanisi wa upelelezi wa kesi.
2.5 Makosa yaliyotendwa na wakimbizi Januari –
Desemba 2007. Katika jitihada za kukabiliana na uhalifu, Jeshi
la Polisi
pia limetupia macho makambi ya wakimbizi yaliyoko
mikoa ya Tabora, Kigoma, Rukwa, na Kagera. Lengo ni
kuhakikisha sheria na taratibu za nchi zinafuatwa na
wageni hao.
Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007 jumla ya
makosa 713 yaliripotiwa na kushughulikiwa kama jedwali
Na. 7.2 na Na. 7.2.1
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 30 - 65
Jedwali Na. 7.2: Makosa yaliyotendwa na Wakimbizi
MAKOSA TABORA RUKWA KIGOMA KAGERA JUMLA
MAKOSA DHIDI YA BINADAMU Mauaji 0 0 26 0 26 Kubaka 5 4 42 0 51
Kulawiti 0 1 1 0 2 Kujeruhi 6 7 16 0 29 Kutoa mimba 0 0 1 0 1
Kutorosha watoto 0 Kumtaja mtu mchawi 1 1 0 0 2 Kipingo 0 0 1 0 1
Kujaribu kujiua 0 0 1 0 1 Shambulio la kudhuru mwili 0 1 0 0 1
JUMLA 12 14 88 0 114 MAKOSA DHIDI YA MALI Unyang'anyi wa kutumia
silaha 0 1 32 0 33 Unyang'anyi wa kutumia nguvu 5 1 30 0 36
Uvunjaji 5 0 16 0 21 Wizi wa mifugo 0 0 22 0 22 Kuchoma nyumba moto
3 6 1 0 10 Kuharibu mali 1 0 0 0 1 Wizi 11 1 22 0 34 Kupatikana na
dawa za binadamu 0 0 1 0 1 Kupatikana na mali ya wizi 2 0 1 0 3
Wizi wa kuaminiwa 1 1 0 0 2 Kupatikana na noti bandia 0 0 3 0 3 K/
na mashine ya kutengenezea noti 0 0 1 0 1 Kujipatia mali kwa njia
ya udanganyifu 3 0 0 0 3 K/ na madini bandia 0 0 1 0 1 JUMLA 31 10
130 0 171 MAKOSA DHIDI YA MAADILI YA JAMII Kupatikana na bhangi 6 2
3 0 11 Pombe ya moshi 2 0 14 0 16 Kupatikana na silaha 0 5 3 0 8
Kupatikana na risasi 0 0 3 0 3 Kupatikana na nyara za serikali 0 16
1 0 17 Kutishia kuua 8 1 0 0 9 Kuingia kambini bila kibali 0 1 0 0
1 Kuingia kwa jinai 0 2 0 0 2 Kutumia lugha ya matusi 0 0 6 0 6
Shambulio 16 1 40 0 57 Uzembe na uzururaji 2 0 0 0 2 Kufanya fujo 4
0 0 0 4 Kutoroka kambini 1 58 196 0 255 Kuingia kwenye hifadhi za
Taifa 0 14 18 0 32 Kumzuia mwanafunzi asiende shule 2 0 1 0 3
Kutorosha wakimbizi 0 0 1 0 1 Kupigana hadharani 1 0 0 0 1 JUMLA 42
100 286 0 428 JUMLA KUU 85 124 504 0 713
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 31 - 65
Jedwali Na. 7.2.1: Namna Makosa yaliyotendwa na Wakimbizi
yalivyoshughulikiwa kwa kipindi cha Januari – Desemba 2007
Mkoa Idadi ya kesi
Yaliyopata mafanikio Zilizoshindwa Zinazoendelea Zilizo chini
Yaliyofungwa na polisi Yaliyopelekwa
Mahakamani Mahakamani Mahakamani Mahakamani ya upelelezi NFA U
Refused
Tabora 85 44 12 4 28 31 - 10 - Rukwa 124 114 42 8 64 4 1 4 1
Kigoma 504 417 262 24 131 50 11 26 - Kagera - - - - - - - - - Jumla
713 575 316 36 223 85 12 40 1
Uchambuzi wa Makosa yaliyotendwa na Wakimbizi
Makosa yanayotendwa na wakimbizi yamebakia katika mikoa mitatu
nchini Tabora,
Rukwa na Kigoma. Takwimu za mkoa wa Kagera zinaonesha kutokuwa
na makosa yeyote hii inatokana na uamuzi wa serikali kuyafunga
makambi katika mkoa huo na wakimbizi kurejea nyumbani Rwanda baada
ya hakikisho la amani. Tunatarajia hali
kama hiyo kujitokeza Kigoma na baada ya wakimbizi kurejea nchini
kwao baada ya Kikundi cha mwisho cha waasi wa Burundi kurejea baada
ya mkataba wa amani, na nia
ya serikali kuyafunga makambi hayo.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 32 - 65
Kosa linaloongoza kitakwimu ni kutoroka kambini.
Wakimbizi wengi hupenda kutoroka na kujichanganya na
jamii ya watanzania katika harakati za kujitafutia riziki
badala ya kuendelea kubanwa na masharti ya kambini.
Aidha, kukosekana kwa vitambulisho vya uraia nchini
Tanzania ni moja ya vitu vinavyowahamasisha wakimbizi
kujaribu kujichanganya na raia. Sababu nyingine ni
hatua ya Tanzania kutangaza kuyafunga makambi ya
wakimbizi mkoani Kigoma, hatua ambayo haijaridhiwa
na baadhi ya wakimbizi na hivyo kujaribu kutoroka
kutoka makambini kwa kuhofia kurudishwa nchini kwao
bila hiari yao.
Katika kushughulikia kesi za wakimbizi, Idara imepata
mafanikio makubwa katika kushughulikia Makosa
yaliyotendwa na wakimbizi kwa kadri ya takwimu
zilizopo kati ya kesi 575 zilizofikishwa mahakamani kesi
316 zilipata mafanikio kwa watuhumiwa kupatikana na
hatia. Hii ni zaidi ya asilimia 50 ambao ni juu ya wastani
wa Taifa Hali inatokana na ukweli kwamba watuhumiwa
wanaishi katika makambi na ni rahisi kupatikana kwa
ushahidi na mashahidi kwa kuwa makambi wanayoishi
yanadhibitiwa na Jeshi la Polisi.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 33 - 65
SURA YA TATU
3.0 Ajali za Barabarani
3.1 Mchanganuo wa Makosa ya Usalama
Barabarani
Ajali za barabarani bado ni tatizo kubwa katika nchi yetu.
Watu wengi wasio na hatia wameendelea kupoteza
maisha na kupata athari za kudumu kwa maisha yao na
mali kutokana na ajali za barabarani.
Takwimu zinaonesha kwamba kuna ongezeko mara dufu
ya makosa ya usalama barabarani katika kipindi cha
januari hadi disemba 2007 ikilinganishwa na kipindi
kama hiki 2006. Jumla ya matukio 230,751 yaliripotiwa
katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007 wakati
jumla ya matukio 109,868 yaliyoripotiwa katika kipindi
kama hicho cha Januari hadi Desemba 2006. Hilo ni
ongezeko la matukio 120,883 sawa na 110%.
Hivyo katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2007
watu waliokufa kutokana na ajali hizo ni watu 3,071
ikilinganishwa na watu 2,657 waliokufa kwa kipindi kama
hicho cha Januari hadi Desemba 2006, sawa na
ongezeko la watu 414 sawa na 15.6%. Aidha katika ajali
hizo jumla ya watu 16,119 walijeruhiwa katika kipindi
cha Januari hadi Desemba 2007 ikilinganishwa na watu
16,456 waliojeruhiwa kwa kipindi kama hicho cha
Januari hadi Desemba 2006, ikiwa ni pungufu ya
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 34 - 65
majeruhi 337 sawa na 2.05%. Katika kipindi cha Januari
hadi Desemba 2007 ajali zilizosababisha vifo ni 3065
ikilinganishwa na ajali 3,028 za Januari hadi Desemba
2006 ikiwa ni pungufu la matukio 37 sawa na 1.22%
kama jedwali Na. 1.3 linavyoonesha hapa chini.
Jedwali Na. 1.3: Matukio ya Ajali Barabarani kwa kipindi cha
Januari hadi Desemba 2007
Matukio
Januari – Desemba Januari – Desemba
Tofauti
Asilimia 2006 2007
Ajali za barabarani 18,187 25,151 7024 38.6
Ajali za vifo 3,028 3,065 37 1.22
Waliokufa 2,657 3,071 414 15.6
Waliojeruhiwa 16,456 16,119 337 2.05
Pamoja na mchanganuo wa takwimu za makosa ya ajali
za barabarani, ufuatao ni ufafanuzi wa matukio ya ajali,
ajali za vifo, watu waliokufa na majeruhi kutokana na
ajali hizo kwa mikoa kwa kipindi cha Januari hadi
Desemba 2007 ikilinganishwa na kipindi kama hicho cha
Januari hadi Desemba 2006 kama inavyoonesha katika
jedwali Na. 2.3 na 3.3 hapa chini kama ilivyotokea
katika mikoa yote.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 35 - 65
Jedwali Na. 2.3: Mchanganuo wa Makosa ya Ajali za Usalama
Barabarani Januari hadi Desemba
Mkoa
AJALI ZA BARABARANI AJALI ZA VIFO
Jan– Des Jan– Des Jan– Des Jan– Des
2006 2007 Tofauti Asilimia 2006 2007 Tofauti Asilimia
Arusha 487 1458 971 199.4 82 129 47 57.3
D'salaam 7377 6557 -820 -11.1 365 290 -75 -20.5
Dodoma 97 403 306 315.5 73 73 0 0
Iringa 371 324 -47 -12.7 168 123 -45 -26.8
Kagera 442 452 10 2.3 92 96 4 4.3
Kigoma 396 317 -79 -19.9 47 47 0 0
K'njaro 785 961 176 22.4 140 91 -49 -35
Lindi 79 119 40 50.6 31 29 -2 -6.5
Manyara 198 18 -180 -90.9 35 29 -6 17.1
Mara 412 362 -50 -12.1 68 85 17 25
Mbeya 848 1058 210 24.8 153 228 75 49
Morogoro 952 1144 192 20.2 140 137 -3 -2.1
Mtwara 459 330 -129 -28.1 32 38 6 18.8
Mwanza 857 6741 5884 686.6 172 167 -5 -2.9
Pwani 849 1053 204 24 167 197 30 18
Rukwa 172 311 139 80.8 32 35 3 9.4
Ruvuma 836 367 -469 -56.1 36 87 51 141.7
Shinyanga 474 663 189 39.9 69 77 8 11.6
Singida 315 249 -66 -21 36 70 34 94.4
Tabora 407 374 -33 -8.1 54 44 -10 -18.5
Tanga 450 305 -145 -32.2 145 120 -25 -17.2
Reli 0 758 0 0 0 60 0 0
Tazara 0 0 0 0 0 0 0 0
V/ndege 0 0 0 0 0 0 0 0
Zanzibar 924 827 -97 10.4 891 824 -67 7.5
Jumla 18,187 25,151 7,024 38.6 3028 3065 37 1.2
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 36 - 65
Jedwali Na. 3.3: Mchanganuo wa Watu Walioathirika kwa Ajali
Barabarani
Waliokufa Waliojeruhiwa
Mkoa 2006 2007 Tofauti Asilimia 2006 2007 Tofauti Asilimia
Arusha 112 148 36 32 345 511 166 48
D'salaam 410 272 -138 -34 4897 4429 -468 -10
Dodoma 84 95 11 13 76 440 364 479
Iringa 168 148 -20 -12 552 504 -48 -9
Kagera 101 107 6 6 620 339 -281 -45
Kigoma 48 149 101 210 498 438 -60 -12
Kilimanjaro 175 162 -13 -7 1020 266 -754 -74
Lindi 31 38 7 23 55 72 17 31
Manyara 48 39 -9 18.7 445 330 -115 -25.8
Mara 78 85 7 9 542 438 -104 -19
Mbeya 194 476 282 145 911 841 -70 -8
Morogoro 186 184 -2 -1 821 1204 383 47
Mtwara 32 38 6 19 378 411 33 9
Mwanza 196 188 -8 -4 948 562 -386 -41
Pwani 282 244 -38 -13 1392 1688 296 21
Rukwa 28 38 10 36 283 96 -187 -66
Ruvuma 65 94 29 45 342 308 -34 -10
Shinyanga 79 96 17 22 54 434 380 704
Singida 36 79 43 119 226 231 5 2
Tabora 67 44 -23 -34 412 371 -41 -10
Tanga 168 132 -36 -21 741 483 -258 -35
Reli 0 67 0 0 0 769 0 0
Tazara 0 0 0 0 0 0 0 0
V/ndege 0 0 0 0 0 0 0 0
Zanzibar 69 824 -755 -86 897 954 +57 6.3
Jumla 2,657 3,071 414 15.5 16,456 16,119 -337 -2
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 37 - 65
Kutokana na Takwimu zinavyoonyesha hapo juu mikoa
inayoongoza kwa matukio ya ajali ni Mwanza, D’ salaam,
Arusha, Morogoro, Mbeya, Pwani na Kilimanjaro. Aidha
uzito wa kazi unajionyesha zaidi katika mikoa ya Iringa,
Rukwa, Shinyanga, Kigoma, Tabora, Dodoma, Mwanza,
Singida, Kagera, Mtwara na Ruvuma kutokana na
ukubwa wa maeneo na uhaba wa askari wa Usalama
barabarani.
Graph 3.3.1: Matukio ya Ajali kwa kipindi cha Januari
hadi Desemba 2006/2007 Kimkoa
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 38 - 65
Pamoja na sababu mbalimbali zinazochangia ajali za
barabarani, takwimu zetu zinaonesha kuwa vyanzo
vikubwa vya ajali hapa nchini ni:
i Uzembe wa madereva, ukiwemo uendeshaji wa kasi usiozingatia
sheria na alama za barabarani.
ii. Ubovu wa magari au yaliyo chini ya viwango
vinavotakiwa kubeba abiria au mizigo iii. Ubovu na ufinyu wa
barabara zilizopo nchini iv Usimamizi usioridhisha wa usalama
barabarani,
zikiwemo sheria, mfumo mzima wa uendeshaji wa shughuli za
usafirishaji hapa nchini.
3.2 Mikakati iliyopo kukabiliana na Tatizo la Ajali
za Barabarani:
Katika kudhibiti matatizo ya usalama barabarani, Jeshi
linaendelea na mkakati wa kushirikiana na wadau
wengine kama SUMATRA, TANROADS, Shule za udereva
nk, ili kusaidiana kuhakikisha wananchi wanafuata
taratibu na wanaelemishwa kuhusu taratibu hizo.
Mikakati iliopo ni kama ifuatavyo:
• Kutunza kumbukumbu za makosa ya barabarani ili kubaini
wahalifu sugu na kuwafutia leseni zao.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 39 - 65
• Kutoa elimu kwa watumia barabara kama waenda kwa miguu,
madereva na wamiliki wa
magari.
• Mradi wa ‘Safiri Salama’ unaowahamasisha wananchi kutoa
taarifa za ukiukwaji wa sheria
kwa Polisi kwa njia ya simu.
• Kuhimiza doria za barabarani.
• Kudhibiti mwendo kasi wa magari kwa kutumia ratiba za
mabasi.
Ni imani ya Jeshi la Polisi, wananchi wakijenga
utamaduni na nidhamu ya kuheshimu taratibu na sheria
zilizopo, na endapo wadau watatekeleza wajibu wao
vyema udhibiti wa ajali za barabarani utawezekana.
Baada ya kuangalia matukio ya Usalama Barabarani kwa
mwaka 2007, hatuna budi kuangalia matukio hayo kwa
mwaka 2002 hadi 2007 ili kupata mwelekeo wa wakati
ujao na namna ya kuyadhibiti. Jedwali Na. 4.3
linaonyesha.
Jedwali Na. 4.3: Matukio ya usalama barabarani (ajali) kuanzia
2002 - 2007
Matukio 2002 2003 2004 2005 2006 2007
Ajali za Barabarani 16,412 17,614 18,031 17,220 18,187
25,151
Ajali/ Vifo 1,714 1,841 1,994 2,149 3,028 3,065
Waliokufa 2059 2,240 2,442 2,509 2,657 3,071
Waliojeruhiwa 16,197 17,912 22,825 17,434 16,456 16,119
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 40 - 65
Graph Na. 4.3.1
MCHORO 3: MATUKIO YA AJALI BARABARANI TANZANA 2002-2007
0
5,000
10,000
15,000
20,000
25,000
30,000
2002 2003 2004 2005 2006 2007
Miaka
Idad
i ya
Aja
li
AJALI AJALI ZA VIFO
Jedwali Na. 5.3: Mabadiliko ya Matukio ya Usalama Barabarani kwa
Asilimia kwa Mwaka 2002 – 2007
Matukio
Tofauti ya matukio ( Asilimia)
2002 2003 2004 2005 2006 2002 _ 2007
Ajali za Barabarani 7.3 2.4 -4.5 5.6 33.6
53.2
Ajali/ Vifo 7.4 8.3 7.8 43.2 -27.8 78.8
Waliokufa 8.8 9.0 2.7 5.9 8.5 49.1
Majeruhi 10.6 27.4 -23.6 -5.6 -9.9 -0.5
Kama jedwali Na. 7.5 sura ya tano linalohusu idadi ya
watu kuanzia mwaka 2002 hadi 2007. Mwaka 2002 hadi
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 41 - 65
2007 kumekuwa na ongezeko la idadi ya watu kwa
asilimia 14.5. Katika kipindi cha Jan – Des 2002 idadi ya
watu waliokufa kutokana na ajali barabarani 2,059, Jan –
Des 2007 idadi ya watu waliokufa kutokana na ajali
barabarani ni 3,071 hiyo ni sawa na ongezeko la 49.1.
Kwa mantiki hiyo inaonekena kuwa kumekuwa na
ongezeko kubwa zaidi la idadi ya vifo vinavyotokana na
ajali barabarani ikilinganishwa na ongezeko la watu
ambalo ni dogo. Angalia Jerdwali Na. 4.3, na. 5.3.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 42 - 65
SURA YA NNE
4.0 Matukio ya Kushtua
i Arusha
Kukamatwa Mashine ya kutengenezea Master Card.
Tarehe 13/09/2007, Polisi mkoani Arusha walikamata
raia wawili wa Kenya na Mtanzania mmoja wakiwa na
mashine ya kutengenezea master card za malipo ya
Backlays na kadi maalumu za kuchukulia fedha benki za
Backlays ya Uingereza, Marekani na Afrika kusini.
Watuhumiwa wote wamefikishwa mahakamani.
ii Mgomo wa Mahabusu
Kati ya tarehe 2 na 6 mwezi wa Agost mwaka 2007,
mahabusu wa gereza la Ukonga, Segerea na Keko kwa
pamoja walifanya mgomo wa kutoingia mahakamani
baada ya kufikishwa mahakamani hapo na gari la Polisi.
Mahabusu hao walikuwa wakilalamika kuwa kesi zao
zinacheleweshwa kwa makusudi. Kiini cha mgomo huo
kilitokana na kuona kuwa kesi ya aliyekuwa Mkuu wa
Mkoa wa Tabora MH. DITOPILE MZUZURI ambaye
alituhumiwa kwa shitaka la mauaji ya dereva wa
daladala aitwaye Hassan Mbonde kesi yake imekamilika
katika muda mfupi ambapo shauri lake lilipelekwa
Mahakama kuu linaendelea huko na mshitakiwa yupo nje
kwa dhamana na lilichukua muda wa miezi sita tu
kukamilisha upelelezi. Matokeo ya mgomo huo
ulisababisha pia mahabusu wa mikoa ya Arusha,
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 43 - 65
Mwanza, Butimba Luanda – Mbeya kugoma katika kipindi
hichohicho.
iii Kinondoni (dsm/kin/pe/01/2007)
Jalada la uchunguzi
Mnamo tarehe 02/01/07 saa 11.00 katika kiwanda cha
kutengeneza nondo kiitwacho Iron and steel Ltd
kilichopo eneo la Mikocheni zilipatikana taarifa kwamba
katika eneo la kukusanya vyuma chakavu kiwandani
hapo kuna vyuma vinavyofanana na mabomu. Vyuma
hivyo vilikaguliwa na timu ya wataalamu wa mabomu
kutoka Jeshi la Polisi na Jeshi la wananchi wa Tanzania
na katika ukaguzi huo mabomu 20 ya aina mbalimbali
yaligundulika ikiwa ni pamoja na mabomu aina ya
PROPELLER 11, ROCKET PROPELLER 6, WAR HEAD OF
ROCKET RONGER 1 na MOTOR BOMB 2. Mabomu hayo
hayakuleta madhara na Upelelezi unaendelea.
iv Uvamizi wa Benki Tawi la Mwanga
Mnamo tarehe 11/07/2007, saa 19.40 Wilayani Mwanga
Mkoani Kilimanjaro majambazi waliokuwa na silaha
walivamia Banki ya NMB na kupora kiasi cha Shs
234,200,000 baada ya kumuua askari namba E. 6825 PC
Michael na kumjeruhi askari namba F.6973 PC Naftan.
Katika tukio hilo jambazi mmoja raia wa Kenya
aliyefahamika kwa jina la Kamau Peter Ndung’u aliuawa.
Aidha watuhumiwa 20 walikamatwa wakiwemo
wanawake (5), Watuhumiwa wote wamefikishwa
mahakamani tarehe 02/10/2007.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 44 - 65
v Kilimanjaro
Kuuawa kwa Majambazi ya Kenya
Tarehe 06/09/2007, Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro
liliwauwa kwa kuwapiga risasi raia 14 wa Kenya akiwamo
mwanamke mmoja waliosadikiwa kuwa ni majambazi
waliokuwa na silaha. Majambazi hao wanadaiwa kupanga
njama za kupora fedha katika benki ya EXIM Mjini Moshi.
Tukio hilo lilitokea majira ya usiku katika eneo la maili
sita. Majambazi 11 kati ya waliouawa walitambuliwa kwa
majina yafuatayo: Saimon s/o Maina 43 yrs, Moses s/o
Kamau 47yrs, David s/o Mbuna 53yrs, Peter s/o Wawom,
Willium s/o Kamau 36yrs, Philipo s/o Wanjiku 38yrs,
Ludovick s/o Kavuki 27yrs, John s/o Bukuku 47yrs,
Zacharia s/o Kamathiro, Jeremiah s/o Machania, Hannah
d/o Kungwava na wengine watatu hawakuweza
kutambuliwa. Katika mapambano hayo hakuna askari
aliyejeruhiwa ila kulikuwa na uharibifu wa gari la Polisi.
vi Kuchoma Jengo la Shule moto
Mnamo tarehe 07/05/2007 saa 1.30 shule ya Sekondari
Msangano iliyoko kata ya Msangano, wilaya ya Mbozi,
Mkoa wa Mbeya, ilichomwa moto wanafunzi wa shule
hiyo mbali ya uhalibifu huo walimshambulia mwalimu
MATAMANGA. Chanzo cha vurugu hiyo ni tuhuma dhidi
ya kiranja mkuu wa shule hiyo ERNEST S/O SIMKOKO
kumpa mimba mwanafunzi mwenzie aitwaye ELIMA D/O
SIMBEYE. Thamani ya mali iliyoharibiwa inakadiriwa
kufikia Tshs 20,000,000/=.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 45 - 65
SURA YA TANO
5.0 Uchambuzi wa Makosa Makubwa na Madogo
ya Jinai.
Uchambuzi wa Makosa Makubwa na Madogo
ya Jinai ikilinganishwa na Idadi ya Watu.
Katika kufanya uchambuzi ili kujua ni kwa kiwango gani
makosa yameongezeka na pengine kujua ni sababu gani
zinazochangia ongezeko hilo, hatuna budi kufanya
uchambuzi wa kina juu ya ongezeko la watu katika nchi
kulinganisha idadi ya watu na askari Polisi. Aidha, ni
vema pia uwiano huo wa askari ukalinganishwa kwa kila
Mkoa na idadi ya watu, ukubwa wa Mkoa na kiwango cha
makosa katika mkoa. Sambamba na hilo, uchambuzi huu
umekwenda mbali zaidi katika kuangalia hali ya kiuchumi
ya watu kwa kuangalia vipato vya watu, ongezeko la
umaskini, na ukuwaji wa uchumi kulinganisha na
makosa. Bila kusahau ulinganisho huo na makosa ya
Usalama Barabarani.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 46 - 65
Kulingana na sensa ya mwaka 2002 idadi ya watu kwa mwaka 2007
ilikadiriwa kuwa ni 39,446,061 wakati idadi
ya askari Polisi nchi nzima ni 29,463. Kwa maana hiyo Takwimu
zinaonyesha kuwa askari mmoja anahudumia
kiasi cha watu 1,339 ambapo kwa kawaida askari mmoja anatakiwa
ahudumie watu 250. Ongezeko hili linachangia kwa sehemu kubwa
kuongezeka kwa uhalifu Kutokana
na tatizo la askari polisi kuhudumia jamii kwa kiwango cha
chini, tatizo hili haliishii katika ngazi za Taifa
linaendelea hadi ngazi za Mikoa, Wilaya na hata vijijini.
Ukiangalia taarifa ya uhalifu utagundua kuwa mkoa wa D’salaam
unaongoza kwa idadi ya makosa yaliyoripotiwa
ukifuatiwa na mkoa wa Mwanza, Morogoro, Kilimanjaro, Arusha,
Tanga, Kagera, Tabora na Iringa. Aidha pamoja
na kuwa Dar es salaam kuwa na kiwango cha juu cha makosa, kuna
mikoa inayoelemewa zaidi na kazi ambayo ni Shinyanga, Tabora,
Manyara, Kagera, Mbeya,
Mwanza, Rukwa, Ruvuma, Mtwara, Tanga, Kigoma, Iringa na Singida.
Hali hii inatokana na tofauti ya
ukubwa wa maeneo kwa kila mkoa ambapo takwimu zinaonyesha kuwa
mtawanyiko wa askari katika mikoa hiyo ni mdogo sana ikilinganishwa
na mkoa wa D’
salaam na mikoa ya Zanzibar.kama jedwali Na. 1.5
linavyoonyesha hapo chini.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 47 - 65
Jedwali Na. 1.5
Mkoa Makosa Yote
Jinai 2007 Mkoa Watu /
Mkoa Askari /
Mkoa Makosa Yote Jinai / Askari Askari Km2 100
Dar es Salaam 124,331 Shinyanga 4,190 Dar es Salaam 451.4 Mwanza
238.7 Mwanza 47,738 Tabora 3,359 Jumla - visiwani 192.8 Kilimanjaro
194.1 Morogoro 28,243 Manyara 2,766 Kilimanjaro 9.8 Jumla -
visiwani 151.2 Manyara 28,093 Kagera 2,727 Mwanza 6.8 Tanga 77.6
Mbeya 26,846 Mbeya 2,428 Mara 4.3 Mtwara 74 Kilimanjaro 25,232
Mwanza 2,394 Mtwara 3.3 Kagera 71.9 Arusha 24,847 Rukwa 2,347 Tanga
3.1 Arusha 69 Tanga 20,965 Ruvuma 2,222 Arusha 3.1 Manyara 61.1
Kagera 20,852 Mtwara 2,221 Kagera 2.9 Mara 58.4 Tabora 17,328 Tanga
2,170 Dodoma 2.8 Mbeya 44.7 Iringa 16,447 Kigoma 2,082 Pwani 2.3
Morogoro 39.8 Ruvuma 15,001 Iringa 2,056 Kigoma 2.1 Kigoma 35
Dodoma 13,915 Singida 2,004 Mbeya 1.7 Dodoma 33.9 Kigoma 12,956
Lindi 1,815 Morogoro 1.6 Pwani 29.4 Mara 12,850 Mara 1,717
Shinyanga 1.6 Iringa 28.9 Mtwara 12,580 Dodoma 1,704 Iringa 1.4 Dar
es Salaam 27.5 Shinyanga 12,426 Morogoro 1,700 Singida 1.3
Shinyanga 24.4 Rukwa 12,266 Arusha 1,353 Manyara 1 Ruvuma 23.4
Singida 10,669 Pwani 1,315 Ruvuma 0.9 Tabora 22.8 Lindi 10,508
Kilimanjaro 1,201 Rukwa 0.8 Singida 21.8 Pwani 9,687 Dar es Salaam
638 Tabora 0.8 Rukwa 17.8 Jumla - visiwani 3,720 Jumla - Visiwani
244 Lindi 0.7 Lindi 15.9 Tanzania Bara 503,780 Tanzania Bara 1,802
Tanzania bara 2.4 Tanzania Bara 23.7 Jumla - Tanzania 509,462 jumla
- Tanzania 1,339 Jumla - tanzania 3.3 Jumla - Tanzania 17.3
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 48 - 65
Uchambuzi wa Makosa Makubwa ya Jinai kwa Idadi ya Watu, Eneo na
Idadi ya Askari.
Katika kuangalia makosa makubwa ya jinai kwa nchi nzima takwimu
zinaonyesha kwamba mikoa inayoongoza
kwa makosa yaliyoripotiwa kwa kipindi cha Januari hadi Desemba
2007 ni Morogoro, D’salaam, Mwanza, Tabora, Iringa, Kilimanjaro,
Ruvuma, Kagera, Shinyanga, Arusha
na Pwani. Pamoja na mikoa hiyo kuongoza kuna mikoa inayoelemewa
na kazi kama vile Shinyanga, Tabora,
Manyara, Kagera, Mbeya, Mwanza, Rukwa, Ruvuma, Mtwara, Tanga,
Kigoma, Iringa, Singida. Kuelemewa kunatokana na sababu za ukubwa
wa maeneo katika
mikoa hiyo na uhaba wa askari kama jedwali Na. 2.5 na
3.5 yanavyoonyesha hapo chini.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 49 - 65
Jedwali Na. 2.5
Mkoa
Makosa Makubwa Jinai
2007 Mkoa Watu / Askari Mkoa Askari / Km2
100 Mkoa
Makosa makubwa ya
Jinai / Askari
Morogoro 6,764 Shinyanga 4,190 Dar es Salaam 451.4 Tabora
8.8
Dar es Salaam 6,584 Tabora 3,359 Jumla - Visiwani 192.8 Ruvuma
8.6
Mwanza 5,729 Manyara 2,766 Kilimanjaro 9.8 Lindi 8.0
Tabora 5,454 Kagera 2,727 Mwanza 6.8 Iringa 6.4
Iringa 5,153 Mbeya 2,428 Mara 4.3 Manyara 6.0
Kilimanjaro 5,076 Mwanza 2,394 Mtwara 3.3 Morogoro 5.8
Ruvuma 4,884 Rukwa 2,347 Tanga 3.1 Kagera 5.7
Kagera 4,782 Ruvuma 2,222 Arusha 3.1 Shinyanga 5.3
Shinyanga 4,339 Mtwara 2,221 Kagera 2.9 Pwani 5.3
Arusha 4,167 Tanga 2,170 Dodoma 2.8 Rukwa 5.1
Pwani 4,001 Kigoma 2,082 Pwani 2.3 Kigoma 4.4
Mara 3,991 Iringa 2,056 Kigoma 2.1 Mara 4.2
Lindi 3,841 Singida 2,004 Mbeya 1.7 Mwanza 4.2
Tanga 3,468 Lindi 1,815 Morogoro 1.6 Tanga 4.1
Kigoma 3,415 Mara 1,717 Shinyanga 1.6 Kilimanjaro 4.0
Rukwa 2,920 Dodoma 1,704 Iringa 1.4 Arusha 3.7
Dodoma 2,709 Morogoro 1,700 Singida 1.3 Mtwara 3.5
Manyara 2,705 Arusha 1,353 Manyara 1.0 Singida 3.0
Mbeya 2,638 Pwani 1,315 Ruvuma 0.9 Mbeya 2.6
Mtwara 1,971 Kilimanjaro 1,201 Rukwa 0.8 Dodoma 2.4
Singida 1,888 Dar es Salaam 638 Tabora 0.8 Dar es Salaam 1.5
Jumla - Visiwani 1,564 Jumla - Visiwani 244 Lindi 0.7 Jumla -
Visiwani 0.3
Tanzania Bara 86,479 Tanzania Bara 1,802 Tanzania Bara 2.4
Tanzania Bara 4.1
Jumla - Tanzania 88,527 Jumla - Tanzania 1,339 Jumla - Tanzania
3.3 Jumla - Tanzania 3.0
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 50 - 65
5.2 Uchambuzi wa Mahusiano (correlation
analysis)
Uchambuzi wa mahusiano kati ya veriebo mbali mbali
ulifanyika ili kuangalia kiwango cha ushabihiano
(association) kati yao.
Uchambuzi wa takwimu umeonyesha kuwa idadi ya
makosa katika eneo ina uhusiano mkubwa na idadi ya
watu katika eneo husika (correlation coefficient of
0.486 at 95% confidence level). Kadiri idadi ya watu
inavyoongezeka, ndivyo idadi ya makosa
inavyoongezeka. Idadi ya makosa vile vile
imeonekana kuwa na uhusiano mkubwa na idadi ya
uwandikishaji wa watoto wa shule za sekondari
(correlation coenfficient of 0.488).
Kama inavyojulikana, idadi ya watu inajidhihirisha
wazi kuwa inahusiana kwa kiwango kikubwa na idadi
ya maskini (correlation coefficient of 0.739) na
uwandikishwaji wa vijana katika shule za sekondari
(correlation: 0.488).
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 51 - 65
Kwa upande mwingine, kiwango cha uhamiaji mijini
nacho kina uhusiano mkubwa na idadi ya askari
mijini, pato la mtu na uwandikishwaji wa vijana
katika shule za sekondari. Kwa mfano, mahusiano
kati ya kiwango cha uhamiaji mijini na pato la mtu ni
wa kiwango kikubwa (correlation: 0.774) kama ulivyo
uhusiano kati ya uhamiaji mijini na uwandikishwaji
wa vijana katika shule za sekondari (correlation:
0.513)
Tukiangalia idadi ya askari katika eneo, inaonekana
kuwa inahusiana kwa kiasi kikubwa na uhamiaji
mijini, umaskini, pato la mtu na uwandishwaji wa
vijana katika shule za sekondari. Uchambuzi
unaonyesha kuwa mahusiano ya idadi ya askari na
uhamiaji mijini ni chanya (positive) labda kwa sababu
askari wengi wako mijini ukilinganisha na idadi yao
vijijini. Lakini ukiangalia uhusiano wa idadi ya askari
na umaskini, inaonekana kwamba mahusiano yao ni
hasi (correlation: -0.472). Hii inaweza kuwa na
maana kuwa idadi ya askari inapoongezeka katika
sehemu, shughuli za kiuchumi katika eneo hilo
zimepanda kwa maana ya kwamba umaskini
unapungua. Jedwali hapa chini linatueleza mahusiano
ya kitu kimoja na kitu kingine.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 52 - 65
Id
adi y
a m
ako
sa
Idad
i ya
wat
u
Kiw
ang
o
miji
ni
Uku
waj
i miji
Idad
i ya
aska
ri
Um
aski
ni
Idad
i ya
mas
kin
i
Pat
o la
mtu
Sec
on
dar
y
enro
llmen
t
Idadi ya makosa 1 0.486* 0.044 0.08 0.084 -0.355 0.194 0.332
0.488*
Idadi ya watu 0.486* 1 0.222 -
0.189 0.709 -0.347 0.739** 0.06 0.571**
Kiwango mjini 0.044 0.222 1 0.001 0.794** -0.383 -0.114 0.774**
0.513*
Ukuwaji miji 0.08 -0.189 0.001 1 -0.071 0.143 -0.045 0.089
0.187
Idadi ya askari 0.084 0.709 0.794** -
0.071 1 -
0.472* 0.038 0.719** 0.747**
Umaskini -0.356 -0.347 -0.383 0.143 -0.472* 1 0.339 -0.504*
-0.482*
Idadi ya maskini 0.194 0.739** -0.114
-0.045 0.038 0.339 1 -0.366 0.115
Pato la mtu 0.332 0.06 0.774** 0.089 0.719** -0.504 -0.366 1
0.621**
Secondary enrollment 0.488* 0.571** 0.513* 0.187 0.747** -0.482
0.115 0.621** 1
• Vile vile idadi ya askari katika eneo imeonekana kuwa na
mahusiano chanya na uwandikishwaji wa vijana
shule za sekondari (correlation: 0.747). Labda uwepo
wa askari katika eneo unahamasisha uwandikishwaji
wa vijana katika shule za sokondari. Uhusiano kama
huu haukujionyesha dhahiri kwa shule za misingi.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 53 - 65
Jedwali hapa chini linaonyesha majumuisho ya uchambuzi wa makosa
ya jinai kwa idadi
ya watu na idadi ya askari kwa kila mkoa, Tanzania bara na
visiwani.
Jedwali Na. 3.5: Makosa ya Jinai kwa Idadi ya Watu, Eneo na
Idadi ya Askari
Mkoa Makosa 2007 2007 Eneo Idadi ya watu Idadi ya Idadi ya
Makosa/ Makosa/ Makosa/
Ya Idadi ya Idadi ya (km2) Kwa askari Watu Askari Eneo Askari
Watu Jinai Watu Askari Mmoja Km2100 Km2100 Km2100 Kumi 100,000
Arusha 4,167 1,522,974 1126 36,000 1,353 4,230 3 12 37 274 Dar
es Salaam 6,584 2,881,548 4514 1,000 638 288,155 451 658 15 228
Dodoma 2,709 1,951,071 1145 41,000 1,704 4,759 3 7 24 139 Iringa
5,153 1,649,199 802 57,000 2,056 2,893 1 9 64 312 Kagera 4,782
2,293,093 841 29,000 2,727 7,907 3 16 57 209 Kigoma 3,415 1,601,020
769 37,000 2,082 4,327 2 9 44 213 Kilimanjaro 5,076 1,535,976 1279
13,000 1,201 11,815 10 39 40 330 Lindi 3,841 869,521 479 66,000
1,815 1,317 1 6 80 442 Manyara 2,705 1,241,994 449 46,000 2,766
2,700 1 6 60 218 Mara 3,991 1,631,031 950 22,000 1,717 7,414 4 18
42 245 Mbeya 2,638 2,423,636 998 60,000 2,428 4,039 2 4 26 109
Morogoro 6,764 1,975,160 1162 71,000 1,700 2,782 2 10 58 342 Mtwara
1,971 1,246,089 561 17,000 2,221 7,330 3 12 35 158 Mwanza 5,729
3,265,729 1364 20,000 2,394 16,329 7 29 42 175 Pwani 4,001 991,586
754 33,000 1,315 3,005 2 12 53 403 Rukwa 2,920 1,349,579 575 69,000
2,347 1,956 1 4 51 216 Ruvuma 4,884 1,268,738 571 64,000 2,222
1,982 1 8 86 385 Shinyanga 4,339 3,411,022 814 51,000 4,190 6,688 2
9 53 127 Singida 1,888 1,258,545 628 49,000 2,004 2,568 1 4 30 150
Tabora 5,454 2,086,048 621 76,000 3,359 2,745 1 7 88 261 Tanga
3,468 1,837,660 847 27,000 2,170 6,806 3 13 41 189
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 54 - 65
Mkoa Makosa 2007 2007 Eneo Idadi ya watu Idadi ya Idadi ya
Makosa/ Makosa/ Makosa/
Ya Idadi ya Idadi ya (km2) Kwa askari Watu Askari Eneo Askari
Watu Jinai Watu Askari Mmoja Km2100 Km2100 Km2100 Kumi 100,000
Jumla - Bara 86,479 38,291,219 21,249 885,000 1,802 4,327 2 10
41 226 Kaskazini Unguja 160,240 470 34,094 34,094 - - Kusini Unguja
105,456 854 12,348 12,348 - - Mjini Magharibi 447,716 230 194,659
194,659 - - Kaskazini Pemba 224,951 574 39,190 39,190 - - Kusini
Pemba 216,479 332 65,205 65,205 - - Jumla - Visiwani 1,564
1,154,842 4742 2,460 244 46,945 193 64 3 135 Vikosi Vingine 484
3472 - 1 Jumla - Tanzania 88,527 39,446,061 29463 887,460 1,339
4,445 3 10 30 1,992
5.3 Uchambuzi wa Matukio makubwa ya Usalama Barabarani
Kuhusiana na takwimu za Usalama barabarani, takwimu zinaonyesha
kuwa kuna
mikoa ambayo inaelemewa na kazi kutokana na uhaba wa askari
pamoja na
ukubwa wa maeneo katika kudhibiti matukio ya Usalama barabarani.
Mikoa hiyo
ni Iringa, Mwanza, Arusha, Tanga, Mara, Kagera, Morogoro, Mbeya,
Rukwa,
Ruvuma, Pwani, Shinyanga, Mtwara, Dodoma na Lindi. Jedwali Na.
4.5 na 5.5
yanaonyesha hapo chini.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 55 - 65
Jedwali Na. 4.5
Mkoa Matukio Usalama Barabarani 2007
Mkoa Watu / Askari Mkoa Askari / Km2 100 Mkoa Matukio Barabarani
/
Askari
Mwanza 28,338 Iringa 56,869 Dar es Salaam 30.0 Iringa 442.8
Arusha 23,832 Rukwa 49,984 Jumla - Visiwani 13.2 Mwanza 298.3
Morogoro 19,971 Shinyanga 48,729 Kilimanjaro 0.9 Arusha 273.9 Mbeya
16,181 Kigoma 44,473 Mwanza 0.5 Tanga 165.8 Pwani 15,319 Tabora
41,721 Pwani 0.4 Mara 154.2 Iringa 12,842 Dodoma 40,647 Mara 0.3
Kagera 150.9 Dar es Salaam 12,621 Mwanza 34,376 Tanga 0.3 Morogoro
138.7 Jumla - Visiwani 11,988 Singida 34,015 Mtwara 0.3 Mbeya 136.0
Tanga 11,608 Kagera 32,297 Kagera 0.2 Rukwa 133.3 Mara 10,951
Mtwara 28,979 Arusha 0.2 Ruvuma 130.5 Kagera 10,715 Ruvuma 28,835
Morogoro 0.2 Pwani 119.7 Shinyanga 7,928 Lindi 26,349 Mbeya 0.2
Shinyanga 113.3 Kilimanjaro 7,434 Tanga 26,252 Shinyanga 0.1 Mtwara
108.1 Ruvuma 5,744 Mara 22,972 Manyara 0.1 Dodoma 105.4 Dodoma
5,057 Manyara 2,178 Dodoma 0.1 Lindi 100.1 Mtwara 4,649 Mbeya
20,367 Kigoma 0.1 Singida 90.5 Rukwa 3,598 Arusha 17,505 Singida
0.1 Kigoma 88.9 Singida 3,347 Morogoro 13,716 Ruvuma 0.1 Tabora
66.1 Lindi 3,304 Kilimanjaro 13,017 Tabora 0.1 Kilimanjaro 63.0
Tabora 3,303 Dar es Salaam 9,605 Iringa 0.1 Dar es Salaam 42.1
Kigoma 3,202 Pwani 7,747 Lindi 0.1 Jumla - Visiwani 36.9 Manyara
192 Jumla - Visiwani 3,553 Rukwa 0.0 Manyara 3.4 Vikosi Vingine
8,627 Tanzania Bara 210,136 Tanzania Bara 22,458 Tanzania Bara 0.2
Tanzania Bara 123.2 Jumla - Tanzania 230,751 Jumla - Tanzania
19,432 Jumla - Tanzania 0.2 Jumla - Tanzania 113.7
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 56 - 65
Jedwali Na. 5.5
Mkoa Matukio Ajali
Barabarani 2007 Mkoa Watu / Askari Mkoa
Askari / Km2 100 Mkoa
Ajali Barabarani /
Askari
Mwanza 6,741 Iringa 56,869 Dar es Salaam 30 Mwanza 71 Dar es
Salaam 6,557 Rukwa 49,984 Jumla - Visiwani 13.2 Dar es Salaam 21.9
Arusha 1,458 Shinyanga 48,729 Kilimanjaro 0.9 Arusha 16.8 Morogoro
1,144 Kigoma 44,473 Mwanza 0.5 Rukwa 11.5 Mbeya 1,058 Tabora 41,721
Pwani 0.4 Iringa 11.2 Pwani 1,053 Dodoma 40,647 Mara 0.3 Shinyanga
9.5 Kilimanjaro 961 Mwanza 34,376 Tanga 0.3 Mbeya 8.9 Jumla -
Visiwani 827 Singida 34,015 Mtwara 0.3 Kigoma 8.8 Shinyanga 663
Kagera 32,297 Kagera 0.2 Dodoma 8.4 Kagera 452 Mtwara 28,979 Arusha
0.2 Ruvuma 8.3 Dodoma 403 Ruvuma 28,835 Morogoro 0.2 Pwani 8.2
Tabora 374 Lindi 26,349 Mbeya 0.2 Kilimanjaro 8.1 Ruvuma 367 Tanga
26,252 Shinyanga 0.1 Morogoro 7.9 Mara 362 Mara 22,972 Manyara 0.1
Mtwara 7.7 Mtwara 330 Manyara 22,178 Dodoma 0.1 Tabora 7.5 Iringa
324 Mbeya 20,367 Kigoma 0.1 Singida 6.7 Kigoma 317 Arusha 17,505
Singida 0.1 Kagera 6.4 Rukwa 311 Morogoro 13,716 Ruvuma 0.1 Mara
5.1 Tanga 305 Kilimanjaro 13,017 Tabora 0.1 Tanga 4.4 Singida 249
Dar es Salaam 9,605 Iringa 0.1 Lindi 3.6 Lindi 119 Pwani 7,747
Lindi 0.1 Jumla - Visiwani 2.5 Manyara 18 Jumla - Visiwani 3,553
Rukwa 0 Manyara 0.3 Vikosi Vingine 758 Tanzania Bara 23,566
Tanzania Bara 22,458 Tanzania Bara 0.2 Tanzania Bara 13.8 Jumla -
Tanzania 25,151 Jumla - Tanzania 19,432 Jumla - Tanzania 0.2 Jumla
- Tanzania 12.4
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 57 - 65
5.4 Mtiririko wa Makosa Makubwa ya Jinai 2002
hadi 2007.
Uchambuzi wa makosa makubwa ya jinai ni kuanzia
mwaka 2002 hadi 2007 unaonyesha ongezeko la jumla
ya 7% kama jedwali 2.6 linavyoonyesha hapo chini.
Taarifa zinaonyesha kuwa makosa dhidi ya binadamu
yanaongoza kwa ongezeko la 89.1 kuanzia 2002 hadi
2007.
Hata hivyo, kumekuwa na pungufu ya 5.8% kwa makosa
dhidi ya mali hali inayoonyesha jitihada kubwa ya Jeshi
la Polisi kudhibiti aina hiyo ya uhalifu. Punguzo kubwa la
makosa ya jinai lipo katika kosa la magendo ambalo
limepungua kwa 96.7% hali inayoashiria kutoweka
kabisa kwa makosa hayo kutokana na sera za soko huria
na utandawazi. Hata hivyo inabidi vyombo vinavyohusika
na ushuru wa Forodha kuwa macho na makini zaidi
katika kudhibiti uingizaji bidhaa nchini. Mabadiliko ya
ongezeko/ pungufu ya viwango vya aina mbalimbali za
makosa makubwa ya jinai kuanzia 2002 hadi 2007
yanaonekana katika mchoro uliopo baada ya jedwali 6.5
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 58 - 65
Jedwali Na. 6.5: Mtiririko wa Makosa makubwa ya Jinai kuanzia
mwaka 2002 hadi 2007
Kosa 2002 2003 2004 2005 2006 2007
Asilimia
2002 2003 2004 2005 2006 2002 _ 2007
Makosa dhidi ya binadamu Mauaji 2,612 2,778 2,926 2,775 2,612
3,583 6.4 5.3 -5.2 -5.9 37.2 37.2 Kubaka 3,721 3,089 4,621 3,997
4,278 8,894 -17 49.6 -13.5 7 107.9 139 Kulawiti 490 488 541 420 512
567 -0.4 10.9 -22.4 21.9 10.7 15.7 Wizi wa watoto 47 94 48 40 38 71
100 -48.9 -16.7 -5 86.8 51.1 Kutupa watoto 144 314 134 84 86 157
118.1 -57.3 -37.3 2.4 82.6 9 Jumla 7,014 6763 8,270 7,316 7,526
13,272 -3.6 22.3 -11.5 2.9 76.3 89.2
Makosa dhidi ya mali Wizi wa silaha 68 84 70 55 72 104 23.5
-16.7 -21.4 30.9 44.4 52.9 Unyang"anyi wa k/silaha 1,237 1,111
1,175 1,080 1,028 977 -10.2 5.8 -8.1 -4.8 -5 -21 Unyang"anyi wa
k/nguvu 6,640 4,600 7,460 6,783 4,620 7,329 -30.7 62.2 -9.1 -31.9
58.6 10.4 Uvunjaji 29,707 26,748 22,928 20,812 20,413 20,904 -10
-14.3 -9.2 -1.9 2.4 -29.6 Wizi 15,318 16,161 17,080 18,000 18,107
21,708 5.5 5.7 5.4 0.6 19.9 41.7 Wizi wa pikipiki 166 180 174 129
118 222 8.4 -3.3 -25.9 -8.5 88.1 33.7 Wizi wa magari 235 186 361
309 287 254 -20.9 94.1 -14.4 -7.1 -11.5 8.1 Noti bandia 707 722 742
653 389 487 2.1 2.8 -12 -40.4 25.2 -31.1 Wizi wa mifugo 7,430 7,102
5,080 3,528 3,904 5,153 -4.4 -28.5 -30.6 10.7 32 -30.6 Wizi k/
mabenki - 7 11 3 6 23 57.1 -72.7 100 283.3 Wizi mashirika umma 281
409 - - - 383 45.6 -100 36.3 Wizi v/ushirika - 15 - - - 18 -100
Wizi s/mitaa 85 30 - - - 27 -100 Wizi s/kuu 87 104 - - - 129 19.5
-100 48.3 48.3 Kuchoma nyumba moto 2,669 2,556 4,033 1,916 2,090
2,943 -4.2 57.8 9.1 10.3 10.3 Ajali ya moto - - - - - 252 Jumla
64,630 60,015 59,114 53,268 51,034 60,913 -7.1 -1.5 -9.9 -4.2 19.4
-5.8
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 59 - 65
Kosa 2002 2003 2004 2005 2006 2007
Asilimia
2002 2003 2004 2005 2006 2002 _ 2007
Makosa dhidi ya Maadili ya Jamii Kupatikana na silaha 623 678
731 635 832 585 8.8 7.8 -13.1 31 -29.7 -6.1 Madawa ya kulevya 277
280 355 207 377 318 1.1 26.8 -41.7 82.1 -15.6 14.8 Bhang 3,661
4,034 4,088 2,552 5,020 5,521 10.2 1.3 -37.6 96.7 10 50.8 Mirungi
233 254 210 311 296 471 9 -17.3 48.1 -4.8 59.1 102.1 Nyara za
serikali 764 1,168 755 672 720 791 52.9 -35.4 -11 7.1 9.9 3.5
Magendo 1,183 342 99 89 60 39 -71.1 -71.1 -10.1 -32.6 -35 -96.7
Rushwa 29 22 24 18 37 34 -24.1 9.1 -25 105.6 -8.1 17.2 Pombe ya
moshi 4,288 4,586 4,292 4,005 2,690 5,937 6.9 -6.4 -6.7 -32.8 120.7
38.5 Mitambo ya gongo - - - - - 133 Ku[patikana na risasi - - - - -
189 Kupatikana na bomu - - - - - 18 Uhamiaji haramu - - - - 189 306
Jumla 11,058 11,364 10,554 8,489 10,221 14,342 2.8 -7.1 -19.6 20.4
40.3 29.7 Jumla kuu Jinai 82,702 78,142 77,938 69,073 68,781 88,527
-5.5 -0.3 -11.4 -0.4 28.7 7
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 60 - 65
Makosa ya jinai kwa ujumla wake kwa kipindi cha
Januari hadi Desemba 2003 yamepungua kwa 5.5%,
Januari hadi Desemba 2004 yamepungua kwa 0.3%,
Jan – Des 2005 yamepungua kwa asilimia 11.4, Jan –
Des 2006 yamepungua kwa 0.4%, Jan - Des 2007
makosa yameongezeka kwa 28.7%. Kwa wastani
kuanzia mwaka 2002 hadi 2007 uhalifu umeongezeka
kwa 7% Kama inavyoonekena katika mchoro hapa
chini.
Graph Na. 4.5.1
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 61 - 65
Graph Na. 4.5.2
Katika kipindi cha Januari hadi Desemba 2002 hadi
Januari - Des 2007 kumekuwepo na kupanda na
kupungua kwa uhalifu kama graph zinavyoonyesha hapo
juu.
Kwa ujumla uhalifu wa makosa ya jinai kwa kipindi cha
Januari hadi Desemba 2007 umepanda ukilinganisha na
kipindi cha Januari hadi 2006. Aidha pamoja na sababu
za jumla za kuongezeka kwa matukio pia kupanda huko
kumetokana na juhudi za Jeshi la Polisi katika kufanya
misako mbalimbali katika kupambana na uhalifu huo.
Kuna mikakati mbalimbali imefanywa ya kuutokomeza
uhalifu, misako ya ndani ya Wilaya- kati ya wilaya na
wilaya - ndani ya mkoa na mkoa ili kuweza kudhibiti
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 62 - 65
uhalifu kuhamia maeneo mengine baada ya kufanya
uhalifu eneo fulani. Vilevile vikosi vya doria
vimeimarishwa hivyo makosa mbalimbali yamekuwa
yakikamatwa, utumiaji wa pikipiki sehemu zisizofikiwa
kirahisi, pia matumizi ya Helikopta yamesaidia
kukamatwa kwa makosa ambayo hapo awali
yasingeweza kukamatwa.
Pia Taasisi zingine zimekuwa na ushirikiano wa karibu na
Polisi katika utendaji wa kila siku wa shughuli za
kukabiliana na uhalifu na wahalifu, mfano; Taasisi ya
TRA, Usalama wa Taifa, Mamlaka ya Bandari Tanzania,
Mali asili na Utalii, n.k Ushirikiano umeimarika hivyo
kumekuwapo na vyanzo vingi vya kupata taarifa za
uhalifu na wahalifu.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 63 - 65
Jedwali Na. 7.5: Idadi ya watu mwaka 2002 hadi 2007
Mkoa 2002 2003 2004 2005 2006 2007 Eneo Km2
Dodoma 1,692,000 1,739,456 1,790,306 1,843,169 1,896,786
1,951,071 41,000 Arusha 1,288,000 1,334,076 1,380,830 1,428,034
1,475,489 1,522,974 36,000 Kilimanjaro 1,377,000 1,406,470
1,437,755 1,470,168 1,503,014 1,535,976 13,000 Tanga 1,636,000
1,672,581 1,711,722 1,753,284 1,795,284 1,837,660 27,000 Morogoro
1,753,000 1,794,815 1,838,386 1,883,437 1,929,087 1,975,160 71,000
Pwani 885,000 903,816 924,289 946,158 968,637 991,586 33,000 Dar es
Salaam 2,487,000 2,564,394 2,642,708 2,721,926 2,801,675 2,881,548
1,000 Lindi 787,000 801,189 816,769 834,171 851,764 869,521 66,000
Mtwara 1,124,000 1,145,655 1,169,215 1,194,588 1,220,248 1,246,089
17,000 Ruvuma 1,114,000 1,141,066 1,170,676 1,202,430 1,235,161
1,268,738 64,000 Iringa 1,491,000 1,520,891 1,552,796 1,585,501
1,617,696 1,649,199 57,000 Mbeya 2,063,000 2,127,641 2,197,141
2,270,711 2,346,388 2,423,636 60,000 Singida 1,087,000 1,118,874
1,152,422 1,187,409 1,222,810 1,258,545 49,000 Tabora 1,710,000
1,777,420 1,849,101 1,925,106 2,004,115 2,086,048 76,000 Rukwa
1,136,000 1,173,159 1,213,309 1,256,828 1,302,278 1,349,579 69,000
Kigoma 1,674,000 1,356,497 1,413,199 1,473,100 1,535,700 1,601,020
37,000 Shinyanga 2,797,000 2,907,776 3,025,241 3,149,179 3,277,784
3,411,022 51,000 Kagera 2,028,000 1,982,612 2,054,392 2,130,668
2,210,217 2,293,093 29,000 Mwanza 2,930,000 2,891,952 2,980,930
3,073,881 3,168,904 3,265,729 20,000 Mara 1,363,000 1,410,328
1,460,984 1,515,358 1,572,068 1,631,031 22,000 Manyara 1,038,000
1,075,022 1,114,591 1,156,334 1,198,051 1,241,994 46,000 Jumla -
Bara 33,460,000 33,845,690 34,896,762 36,001,440 37,133,156
38,291,219 885,000 Kaskazini Unguja 137,000 140,911 145,403 150,143
155,066 160,240 470 Kusini Unguja 94,000 96,480 98,727 100,934
103,191 105,456 854 Mjini Magharibi 390,000 401,337 412,761 424,366
435,992 447,716 230 Kaskazini Pemba 185,000 192,446 199,914 207,773
216,174 224,951 574 Kusini Pemba 175,000 182,718 190,448 198,690
207,348 216,479 332 Jumla - Visiwani 981,000 1,013,892 1,047,253
1,081,906 1,117,771 1,154,842 2,460 Jumla - Tanzania 34,441,000
34,859,582 35,944,015 37,083,346 38,250,927 39,446,061 887,460
Chanzo: Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania, 2007 Tanzania in
figures.
-
Taarifa ya Hali ya Uhalifu Nchini Januari hadi Desemba 2007
Uk. 64 - 65
Kutokana na takwi