Prepeared by hebron venance UFUGAJI WA NGURUWE Nguruwe ni mnyama mwenye faida, ni rafiki kwa mazingira na hahitaji gharama kubwa. Katika nchi nyingi zinazo endelea ikiwemo Tanzania kiasi kikubwa cha nyama kinatokana na wanyama wenye matumbo Zaidi ya moja kama ng’ombe, mbuzi, kondoo, nk. Kutokana na kukua na kuongezeka kwa kasi kwa idadi ya watu kunaumuhimu mkubwa wa mabadiliko ya vyanzo vya nyama ili kuweza kukidhi mahitaji ya idadi kubwa ya ongezeko hilo la watu. Moja ya chazo kizuri na kinacho weza kupunguza uhaba wa nyama kwa muda mfupi ni pamoja na nguruwe ambao wanakuwa kwa muda mfupi, wanatupatia protini nyingi, gharama zake za uzalishaji si kubwa sana kwani wanatumia aina nyingi za vyakula kulingana na mazingira husika na pia wanaweza kuzaliana kwa vingi kwa muda mfupi. Mfano nguruwe anaweza kufikisha kilo 90-120 akifugwa vizuri ndani ya miezi sita(6) na hivyo tayari kwa kuchinjwa kwaajili ya nyama, na kwa mzao mmoja anaweza kuzaa vitoto 9-14 ambapo kwa mwaka anazaa mara mbili hivyo twaweza kupata vitoto 14-24 kwa mwaka.
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
Prepeared by hebron venance
UFUGAJI WA NGURUWE
Nguruwe ni mnyama mwenye faida, ni rafiki kwa mazingira na hahitaji gharama kubwa. Katika nchi nyingi zinazo
endelea ikiwemo Tanzania kiasi kikubwa cha nyama kinatokana na wanyama wenye matumbo Zaidi ya moja kama
ng’ombe, mbuzi, kondoo, nk. Kutokana na kukua na kuongezeka kwa kasi kwa idadi ya watu kunaumuhimu
mkubwa wa mabadiliko ya vyanzo vya nyama ili kuweza kukidhi mahitaji ya idadi kubwa ya ongezeko hilo la
watu. Moja ya chazo kizuri na kinacho weza kupunguza uhaba wa nyama kwa muda mfupi ni pamoja na nguruwe
ambao wanakuwa kwa muda mfupi, wanatupatia protini nyingi, gharama zake za uzalishaji si kubwa sana kwani
wanatumia aina nyingi za vyakula kulingana na mazingira husika na pia wanaweza kuzaliana kwa vingi kwa muda
mfupi. Mfano nguruwe anaweza kufikisha kilo 90-120 akifugwa vizuri ndani ya miezi sita(6) na hivyo tayari kwa
kuchinjwa kwaajili ya nyama, na kwa mzao mmoja anaweza kuzaa vitoto 9-14 ambapo kwa mwaka anazaa mara
mbili hivyo twaweza kupata vitoto 14-24 kwa mwaka.
Prepeared by hebron venance
Jamii nyingi hapa Tanzania huchukulia nguruwe kama mnyama mchafu na asiyefaa kuwa karibu naye na hata kwa
matumizi kama lishe. Zaidi, nyama yake inapendwa na haina madhara kwa afya na inapendekezwa kuliwa zaidi
kuliko nyama nyekundu. Unaweza kuanzisha mradi wa nguruwe kwa gharama ndogo lakini baada ya kipindi cha
miezi tisa tu ukaanza kujipatia kipato kutokana na ufugaji huo.
Ufugaji
Kwa kawaida nguruwe wanafugwa na watu wa kada zote, wafugaji wadogo wadogo na hata wakubwa. Aina hii ya
ufugaji huweza kumpatia mkulima kipato pamoja na lishe kwa familia, na hauhitaji gharama kubwa.
AINA ZA NGURUWE
Hampshire (USA)
Wana rangi ya dhahabu – nyeusi na msitari mweupe kuzunguka mabega.