Top Banner
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA TAMKO LA SHERIA ZA KIMILA (MKONDO WA UKOO WA MAMA) Mei, 2013
43

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Oct 31, 2019

Download

Documents

dariahiddleston
Welcome message from author
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
Page 1: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIATUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA

TAMKO LA SHERIA ZA KIMILA (MKONDO WA UKOO WA MAMA)

Mei, 2013

Page 2: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

 

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA

Anuaniyasimu"TUMESHERIA ". S. L. P 3580, Simu 2111387/2123533/4 DAR ES SALAAM Nukushi Na. 2123534/2123793 Tovuti: www.lrct.go.tz Baruapepe: [email protected] Unapojibutafadhalitaja: Kumbukumbu Na. CA.71/72/01 28 Februari, 2013. Mh. Mathias M. Chikawe (MB), Wizara ya Katiba na Sheria, S.L.P 70069, DAR ES SALAAM.

KUH: BARUA YA KUKABIDHI RIPOTI YA TUME KUHUSIANA NA UTAFITI WA SHERIA ZA MILA KWA MAKABILA

YANAYOFUATA MKONDO WA UKOO WA MAMA

Tume ya Kurekebisha Sheria kwa mujibu wa mamlaka iliyonayo chini ya kifungu cha 4(2) na 9(1) cha Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria, Sura ya 171 [Mapitio Toleo la 2012] ikiongozwa na msukumo wa hitaji la mapitio ya aina hii ndani ya Tume yenyewe, imefanya utafiti kwenye Sheria za Mila kwa Makabila yanayofuata mkondo wa ukoo wa mama.

Utafiti huu uliojumuisha taasisi na wadau mbalimbali, umefanyika katika mikoa ya Lindi (Wilaya za Ruangwa na Nachingwea), Mtwara (Wilaya za Masasi na Nanyumbu), Morogoro (Wilaya za Ulanga, Kilombero, Kilosa na Mvomero), na Ruvuma (Wilaya za Namtumbo na Tunduru).

Dhumuni kubwa la kufanya mradi huu ni kubainisha sheria za mila ambazo hazikujumuishwa katika Tamko la Kimila zilizomo kwenye Gazeti la Serikali Namba 279 la mwaka 1963 na kujumuisha sheria za mila ambazo hazikinzani na Katiba, haki za binadamu na sheria yoyote ya nchi.

Page 3: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Baada ya utafiti kukamilika, na Kwa mujibu wa kifungu cha 14(1) cha Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria, Tunapenda kukabidhi kwako Taarifa ya Tamko la Sheria za Kimila kwa makabila yanayofuata mkondo wa ukoo wa mama.

Wako,

MWENYEKITI

Ms. Esther J. Manyesha Jaji (mstaafu) Ernest L.K. Mwipopo KAMISHNA WA KUDUMU KAMISHNA WA KUDUMU

Prof. Sufian H. Bukurura Mr. Albert A. Msangi KAMISHNA WA KUDUMU KAMISHNA WA KUDUMU Dr. Eve HawaSinare Dr. Benedict T. Mapunda KAMISHNA WA MUDA KAMISHNA WA MUDA

Mh. Jaji Aloysius B. Mujulizi............................................................

.................................................

.................................................

.................................................

.................................................

.................................................

.................................................

Page 4: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

i

MAELEZO JUU YA UTAFITI WA SHERIA ZA MILA

1.0 UTANGULIZI

2.0 MISINGI YA SHERIA ZA TANZANIA

Tume ya Kurekebisha Sheria imeamua kuendeleza mradi wa utafitii wa sheria za kimila kwa makabila yote ya Tanzania. Utafiti huu ulianza mwaka 2006 ambapo Tume ilianza kufanya utafiti wa sheria za mila katika baadhi ya Mikoa na Wilaya za Tanzania. Dhumuni kuu la kufanya utafiti wa Sheria za mila ilikuwa kuchambua sheria za mila kwa nia ya kutambua mapungufu ambayo yanaweza kusababisha kukosekana kwa haki na kuvunjwa kwa haki za binadamu.

Utafiti wa sheria za mila umefanyika katika awamu mbili. Awamu ya kwanza ilihusisha kupitia Matangazo ya Sheria za Mila ya mwaka 1963 ili kubaini vipengele vinavyokinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na hatimaye kupendekeza kufutwa kwa vipengele hivyo vya sheria ya mila. Sheria zilizoguswa zaidi katika awamu ya kwanza ni zile zilizorasimishwa mwaka 1963, ambazo zilihusu zaidi makabila ambayo uasilia na urithishwaji huegemea upande wa baba. Hata hivyo, kwakuwa yako makabila hapa nchini ambayo uasilia na urithishwaji huegemea upande wa mama, imeonekana kuwa ni vyema na busara kuzitambua na kuziandika sheria za makabila hayo ambazo hazikushulikiwa mwaka 1963.

Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria za Bunge, Sheria za Mapokeo (Common laws, equity and statutes of general application) na Sheria za Mila na Kiislamu. Hivyo basi, sheria za kimila ni mojawapo ya sheria zenye umuhimu mkubwa katika kutatua mashauri ya watu mahakamani.

Page 5: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

ii

Sheria za mila zinatambuliwa kama chanzo cha sheria zinazotumika katika mahakama za Tanzania Bara kupitia Sheria inayohusika na matumizi ya sheria [The Judicature and Application of Laws Act Cap.358] Sheria za mila kama chanzo cha sheria, pamoja na vyanzo vingine, zimekuwa zikipotea kwa kuwa sheria nyingine zimekuwa zikitungwa kwenye maeneo ambayo yalikuwa yakiratibiwa au kutawaliwa na sheria za mila. Sheria za mila hutumika kwenye mashauri ya madai pekee kati ya wanajamii wanaotoka kwenye jamii moja au wanajamii wanaotoka kwenye jamii tofauti lakini sheria za mila zinafanana kwa mujibu wa mila na desturi zao.

Halmashauri za wilaya zimepewa jukumu la kutambua sheria za mila katika maeneo yao na kupendekeza kwa serikali kuhusiana na sheria zipi za mila zinatakiwa kutangazwa kama sheria na kutumika na mahakama ndani ya Halmashauri husika, ili kuondoa mashaka yanayoweza kutokea ikiwa sheria husika hazikutambuliwa na kuandikwa. Hakuna hata halmashauri moja hapa Tanzania iliyotekeleza wajibu wake huu wa kuzitambua na hatimaye kuzitangaza sheria za mila zinazotakiwa kutumika katika wilaya husika.

Sheria za mila zinajengwa kwenye jamii na jamii hubadilika kulingana na mabadiliko yanayotokea kwenye jamii. Mabadiliko hayo huathiri sheria za mila na mara nyingine kuzifanya zipitwe na wakati na kuonekana hazikidhi tena haja na mahitaji ya jamii husika.

Tume iliona haja kubwa kwa sasa kufanya utafiti wa sheria za kimila kwa kugawa mradi huu katika Makundi makuu mawili:-

3.0 UTAFITI WA SHERIA ZA KIMILA

i. Tume imefanya uchambuzi wa sheria zote za kimila ambazo zinakinzana na Katiba ya Tanzania, Muswada wa Haki za Binadamu

Page 6: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

iii

Katika kutambua na kuandika sheria za mila zinazofuata ukoo wa mama, Tume ilifanya utafiti wa mahojiano na makabila yanayofuata mkondo wa ukoo wa mama (matrilineal) katika Mikao ifuatayo; Lindi (Wilaya za Ruangwa na Nachingwea), Mtwara (Wilaya za Masasi na Nanyumbu), Morogoro (Wilaya za Kilombero, Kilosa, Mahenge na Mvomero) na Ruvuma (Wilaya za Namtumbo na Tunduru). Tume ilifanya mahojiano na wananchi katika wilaya zilizotajwa hapo juu ili kubaini na kuzitambua sheria za mila zinazotumika kwenye maeneo yao, hasa sheria zinazohusiana na ndoa, mirathi na jando. Pia wananchi walipata fursa ya kueleza ni sheria zipi ambazo wanafikiri zinafaa kuendelea kutumika na zile ambazo wanafikiri zimepitwa na wakati.

i. (Bill of HumanRights) Uchambuzi huu uliisaidia Tume kuangalia na kutambua sheria zote ambazo ni kandamizi hasa kwa akina mama na watoto, pia uchambuzi huu uliisaidia Tume kupendekeza kuwa sheria zote za mila ambazo ni kandamizi zinafutwa katika sheria ya mila ya mwaka 1963.

ii. Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania imefanya jitihada ya kuziandika sheria za kimila za mkondo wa ukoo wa mama. Dhumuni kuu la kufanya utafitii huo ni baada ya kubaini kuwa Sheria ya Mila ya mwaka 1963 (Customary law (Declaration) order, 1963) haijajumuisha sheria za mila za makabila yanayofuata ukoo wa mama kwa kuzingatia kuwa kuna watanzania wanaofuata ukoo wa mama na wana mila na desturi zao tofauti na koo zinazofuata mkondo wa ukoo wa baba. Pia kuna nchi nyingi duniani zinazofuata ukoo wa upande wa mama kwahiyo sio kitu kigeni.

Page 7: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Utafiti huu ulifanyika kwa awamu mbili katika wilaya zilizohusika na utafiti huu. Hatua ya kwanza ilikuwa ni kuzibaini sheria za mila katika wilaya husika. Tume ilifanya mahojiano na wazee wa makabila yaliyoko kwenye wilaya husika na viongozi wa Halmashauri za wilaya kwenye wilaya zilizotajwa hapo juu. Katika hatua hii wazee wa makabila husika waliitarifu Tume sheria mbalimbali za mila wanazotumia katika meneo yao, hasa katika maeneo ya ndoa, mirathi na jando. Baada ya kukamilisha utafiti,Tume ilichambua zilizopatikana kwenye utafiti huu na hatimaye, kupitia taarifa zilizopatikana, kutayarisha rasimu ya kanuni inayobainisha sheria zinazotumika katika wilaya zilizohusika.

Katika hatua ya pili Tume ilirudi tena katika wilaya husika na kuendesha warsha na mikutano na wadau mbalimbali kupitia rasimu ya kanuni. Wadau, hasa wazee wa mila na viongozi katika halmashauri hizo, walipata nafasi ya kupitia rasimu ya kanuni iliyotayarishwa na kutoa maoni yao juu ya kanuni hizo. Katika warsha hizo rasimu ya kanuni ilikubaliwa na maboresho kupendekezwa ambayo Tume iliyafanyia kazi. Baada ya maboresho Tume imetayarisha rasimu ya Kanuni za Sheria za Mila kwa makabila yanayofuata mkondo wa mama.

Tume imeshakamilisha kuandika Sheria za Kimila za makabila yanayofuata mkondo wa ukoo wa mama. Sheria hizi zitasaidia mahakama zilizomo kwenye wilaya husika kutoa hukumu zenye haki kwa kuzingatia taratibu na destruri ambazo hazikinzani na Katiba ya Jamhuri ya Muungano na Muswada wa Haki za Binadamu (Bill of Human Rights). Hii itatokana na kwamba sheria zote za mila ambazo ziko kinyume na Katiba na haki za binadamu hazikujumuishwa katika sheria zilizoandikwa kama sheria za mila kwa makabila yanayofuata mkondo wa ukoo wa mama. Mahakama kupitia sheria hizi za mila zitawezeshwa kuzipata sheria za mila kwa urahisi bila hata kuhitaji wazee wa baraza

iv

Page 8: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

au wazee wenye utaalamu wa sheria za mila. Pia itakuwa rahisi kwa Halmashauri za wilaya zilizopo katika maeneo husika kupendekeza kuboreshwa au kurekebishwa kwa sheria husika kama zitaona kuwa kulingana na wakati uliopo sheria husika zimepitwa na wakati.

Ni matumaini ya Tume ya Kurekebisha Sheria kuwa uandikwaji wa sheria za mila kwa makabila yayofuata ukoo wa mama utakuwa ni wa manufaa kwa taifa, hasa katika utoaji wa haki na utawala wa sheria. Jamii na mahakama zitanufaika kwa upatikanaji rahisi wa sheria za mila na hivyo kutenda haki kwa mujibu wa sheria kama zilivyoandikwa katika Halmashauri za wilaya husika. Tume ya Kurekebisha Sheria inatumaini kwamba huu utakuwa ni mwanzo kwa Halmashauri nyingine za wilaya kuchukua hatua ili kuhakikisha kuwa sheria za mila zilizomo kwenye Halamashauri hizo zinatambuliwa na kuandikwa ili kurahisisha upatinakaji wake na kuhakikisha zinaendana na wakati uliopo.

4.0 HITIMISHO

v

Page 9: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

TAMKO LA SHERIA ZA KIMILA (MKONDO WA UKOO WA MAMA), 2012

SEHEMU YA KWANZAVIFUNGU VYA AWALI

1. Jina fupi.2. Utumikaji3. Tafsiri.

SEHEMU YA PILIMAHARI

4. Ulipaji wa mahari5. Nafasi ya mahari katika ndoa na muda wa kulipa mahari6. Kubadilisha mifugo iliyolipwa kama mahari kuwa fedha7. Vitu vinavyojumuishwa kwenye mahari.8. Mahari ilipwayo na ndugu upande wa bwana harusi9. Mahari ilipwayo baada ya baba wa msichana kufariki bila wosia10. Namna ya kulipa mahari

SEHEMU YA TATUNDOA

11. Mashahidi wa ndoa12. Kumbukumbu za ndoa ya kimila13. Umri wa kuoa na kuolewa14. Vizuizi vya ndoa 15. Ndoa ya mke zaidi ya moja 16. Mume aliyetorokwa au kutelekezwa na mke17. Mke aliyetelekezwa na mume

vi vi

Page 10: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA NNETALAKA NA KUTENGANA

18. Sababu za kuvunja ndoa19. Matunzo kwa mke baada ya ndoakuvunjwa20. Matunzo kwa watoto baada ya ndoa kuvunjwa21. Mashtaka ya ugoni

SEHEMU YA TANOHALI YA MTOTO

22. Matunzo ya mtoto wa mwanamke asiyeolewa ambaye ni marehemu.23. Matunzo ya mtoto wa kambo.24. Taratibu za kumhalalisha mtoto.25. Matunzo ya mimba.26 Taratibu na vigezo vya kuasili mtoto27. Kupokea mahari ya mtoto wa nje ya ndoa

SEHEMU YA SITAURITHI

28. Makundi ya urithi.29. Warithi wa kundi la kwanza.30. Warithi wa kundi la pili.31. Warithi wa kundi la tatu.32. Mrithi wa mali ya mume aliyeacha mke mmoja.33. Warithi wa mali ya mke.34. Warithi wa mali ya mtoto wa kike ambaye hakuolewa.35. Haki ya mtoto wa kambo urithi.36. Taratibu za kubadilisha warithi.

ii viivii

Page 11: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA SABAWOSIA

37. Haki ya kutoa wosia.38. Aina ya wosia.39. Umri wa mtoa wosia.40. Taratibu za kutoa wosia.41 Wosia wa mdomo.42. Utaratibu wa kubadilisha wosia wa mdomo.43. Utaratibu au unaofuatwa pale mashahidi wa wosia wanapokuwa wote wamefariki au hawapo.44. Wosia wa maandishi. 45. Wosia kwenye mgawanyo wa mali.46. Utaratibu unaofuatwa kwa mtu aliyefariki bila kuacha wosia.47. Kukataliwa kwa wosia.48. Kupotea kwa wosia.49. Sababu za kumnyima mrithi, urithi.50. Taratibu za kutunza kumbukumbu za wosia.51. Taratibu za kubadilisha warithi walioandikwa kwenye wosia.52. Taratibu za kugawa mali za marehemu ambaye hakuacha wosia.53. Utaratibu wa kusajili vifo.54. Kutunza kumbukumbu za vifo.

SEHEMU YA NANEUGAWAJI WA MALI YA URITHI

55. Taratibu za kumteua msimamizi.56. Taratibu za kugawa mali inayohamishika na isiyohamishika.57. Kazi za msimamizi.58. Malipo ya msimamizi.59. Kushughulikia malalamiko yanayotokana na ugawaji mali.

iiiviii

Page 12: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

60. Taratibu za ulipaji wa madeni ya marehemu.61. Ugawaji wa ardhi ya marehemu.62 Taratibu za kugawa mifugo ya marehemu.63. Taratibu za kurithi mali ya marehemu aliyoiacha kama zawadi.64. Utunzaji wa Kumbukumbu za ugawaji naki mali ya marehemu

SEHEMU YA TISAARDHI YA UKOO

65. Taratibu za kumteua mtunzaji wa ardhi ya ukoo.

SEHEMU YA KUMIJANDO NA UNYAGO

66. Kamati ya Jando na Unyago.67. Muda wa kufanya jando na unyago.68. Taratibu za kufanya jando na unyago.69. Mafundisho yanayotolewa kwenye jando na unyago70. Sherehe za jando na unyago zisizozingatia umri71. Tohara .

SEHEMU YA KUMI NA MOJAWAJANE

72. Kosa la kumrithi mjane.73. Matunzo ya mjane mwenye watoto74. Matunzo ya mjane ambaye hana watoto.

iv ix

Page 13: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA KUMI NA MBILIUANGALIZI

75. Namna au aina za uangalizi.76. Uangalizi wa watoto.77. Wajibu wa mwangalizi.78. Uangalizi wa mali ya mrithi asiyekuwepo.79. Uangalizi wa mtu ambaye hawezi kujitegemea.80. Uangalizi wa familia na mali ya mtu aliyesafiri kwa muda mrefu.

SEHEMU YA KUMI NA TATUUSULUHISHI WA MIGOGORO

81. Wahusika wa usuluhishi. 82 . Nafasi ya familia kwenye usuluhishi.83 . Nafasi ya wazee kwenye usuluhishi.84 . Nafasi ya ukoo kwenye usuluhishi.85 . Nafasi ya Baraza la wazee kwenye usuluhishi.86. Usuluhishi unaposhindikana.87. Ushahidi wakati wa usuluhishi.88. Adhabu.

x

Page 14: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA KWANZA VIFUNGU VYA AWALI

Jina fupi 1. Hili ni Tamko la Sheria za Kimila (Mkondo wa Ukoo wa Mama), 2012

Utumikaji 2. Tamko hili litatumika katika Wilaya ya Kilombero, Kilosa,UlangaMvomero,Namtumbo,Tunduru, Ruangwa,Nachingwea,Masasi, na Nanyumbu .

Tafsiri 3. Kwa mujibu wa Tamko hili, isipokuwa pale lita kapotafsiriwa vinginevyo-“Baraza la Ukoo” maana yake ni kikao cha ukoo kilichoitishwa ili kushughulikia mambo mbalimbali yaliyoainishwa na Tamko hili;.“ndoa” itakuwa na maana sawa kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971; “mahari’ maana yake ni malipo ya mifugo, fedha au mali ya aina yoyote inayotolewa au kuahidiwa kutolewa kwa madhumuni ya kufunga ndoa iliyokusudiwa; “msimamizi” maana yake ni msimamizi wa mirathi ya marehemu;“ mwangalizi” maana yake ni mwangalizi wa watoto waliofiwa na baba;“wosia” maana yake ni kauli au maandishi yanayotolewa na mtu wakati wa uhai wake kwa hiari yake kuonyesha jinsi gani angependa mali yake igawanywe baada ya kufa kwake.

1

Page 15: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA PILIMAHARI

Ulipaji wa mahari. 4. (1)

(2)

Nafasi ya mahari 5. (1) katika ndoa na mudawa kulipa mahari.

(2)

Kubadilisha mifugo 6. - (1)au mali nyingineiliyolipwa kamamahari kuwa fedha. (2)

Ulipaji wa mahari ni jukumu la bwana harusi kuhakikisha kuwa mahari inalipwa kwa mpangilio uliokubaliwa, na kwamba inafikishwa kwa mtu anayestahili kupokea mahari hiyo.

Aina ya mahari itategemea uamuzi na uwezo wa wazazi wa bwana harusi na bibi harusi kadri watakavyokubaliana.

Kwa mujibu wa mila na desturi, ulipaji wa mahari ni tendo linalohalalisha ndoa yeyote itakayofungwa kwa taratibu za kimila na wazazi wa bwana harusi na bibi harusi wanaweza kukubaliana muda na jinsi mahari itakavyolipwa.

Kutolipwa kwa mahari haitakuwa sababu ya kuzuia ndoa kufungwa kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971.

Mzazi, mjomba au ndugu mwingine wa bibi harusi atawajibika kupokea mahari. Baada ya mzazi, mjomba au ndugu mwingine wa bibi harusi kupokea mifugo au mali ya aina yoyote iliyolipwa kama mahari, hatakuwa na haki ya kudai kubadilisha mahari hiyo

2

Page 16: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

kuwa fedha baada ya harusi kufanyika au kurudisha mahari husika kwa sababu ya kasoro yoyote.

Thamani ya mfugo au mifugo ya aina yoyote ile itakayobadilishwa kuwa fedha kwa ajili ya ulipaji wa mahari itategemea bei ya ngombe wa mahari kwa eneo husika.

Mahari inaweza kulipwa kwa kutumia mifugo, zana, nguo,fedha au mali nyingine kulingana na makubaliano ya upande wa bwana harusi na bibi harusi ambapo upande wa bibi harusi utakuwa na uamuzi wa mwisho kuchagua aina ya vitu vya mahari.

Ndugu au ukoo wa bwana harusi wanaweza kukubaliana kuchangia kulipa mahari ya bwana harusi lakini jukumu la bwana harusi au wazazi wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa mahari inalipwa kwa mpangilio uliokubaliwa na pande husika na mahari inafikishwa kwa mtu anayestahili kupokea mahari hiyo.

Iwapo msichana anaolewa baada ya baba yake kufariki bila kuacha wosia, mahari yake kwa mujibu wa mila hupokelewa na baba mkubwa au mjomba na kama baba mkubwa au mjomba hayupo mahari yatapokelewa na ndugu mwingine anayestahili kupokea kwa mujibu wa mila husika.

Utaratibu wa kupokea mahari utapangwa na upande wa bibi harusi ingawa pande zote mbili zinaweza kukubaliana.

(3)

Vitu vinavyo 7.jumuishwakwenyemahari.

Mahari 8.ilipwayona nduguupandewa bwanaharusi.

Mahari 9.ilipwayobaada yababa wamsichanakufariki bila wosia.

Namna ya 10. (1)kulipa mahari.

3

Page 17: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

(2)

(3)

(4)

(5)

(6)

(7)

(8)

(9)

(10)

Mahari yote inaweza kulipwa mara moja kabla ya harusi kulingana na makubaliano ya upande wa bwana harusi na bibi harusi.

Harusi itafanyika kulingana na makubaliano baada ya kulipwakwa sehemu ya kwanza ya mahari

Iwapo bwana harusi atachelewesha malipo ya mahari iliyobaki, baba wa msichana ana haki ya kupeleka madai yake mbele ya Baraza la Ukoo.

Mzazi hataruhusiwa kumrudisha msichana nyumbani kwasababu mume wake hajamaliza kulipa sehemu ya mahari, vinginevyo mzazi atakuwa anavunja sheria na anastahili kulipa fidia.

Mume na mke baada ya harusi wana uhuru wa kuhamia popote hata kama mahari haijalipwa yote.

Endapo ndoa ikivunjika kutokana na sababu zilizosababishwa na mke, ndugu waliopokea mahari wana wajibu wa kurudisha mahari kutegemea na muda ambao mke amekaa kwa mume wake na iwapo amezaa mtoto.

Kutorudishwa kwa mahari hakutamzuia msichana aliyeolewa kuachana na mume wake.

Mahari italipwa mbele ya mashahidi wa upande wa bwana harusi na bibi harusi.

Ni wajibu wa mzazi, mjomba au mlezi wa bibi arusi na bwana harusi kuona kwamba mahari imelipwa mbele ya mashahidi kutoka kwa bwana harusi na bibi harusi.

4

Page 18: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA TATUNDOA

Mashahidi wa ndoa.

Kumbukumbuza ndoa za kimila

Umri wa kuoana kuolewa.

Vizuizi vya ndoa.

Ndoa ya mkezaidi ya mmoja.

Ndoa za kimila zitashuhudiwa na mashahidi wasiopungua wawili wa umri usiopungua miaka kumi na nane na wenye akili timamu kwa mujibu wa Sheria ya Ndoa, 1971.

Ndoa lazima iandikishwe kwa kufuata sheria za nchi ikiwa ni pamoja na kulipa ada husika.

Halmashauri ya wilaya kwa kuzingatia ushauri wa Msajili wa ndoa wa Wilaya itaweka kumbukumbu za ndoa za kimila zilizofungwa katika halmashauri husika.

Halmashauri ya wilaya husika itaweka utaratibu wa kuratibu ufungaji wa ndoa za kimila katika halmashauri husika.

Umri wa kuolewa na kuoa utakuwa kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971.

Mzazi au mlezi wa mtoto anayesoma shule ya msingi au sekondari atakuwa ametenda kosa iwapo atashindwa kumzuia mtoto huyo kufunga ndoa au kutoa taarifa mapema kwenye vyombo vya sheria ili mtoto husika azuiwe kufunga ndoa kabla ya kumaliza shule.

Vizuizi vya ndoa vitakuwa kama vilivyoainishwa katika Sheria ya Ndoa,1971,

Ndoa inaweza kuwa ya mke mmoja au zaidi ya mmoja.

11.

12. (1)

(2)

(3)

13. (1)

14.

15. (1)

(2)

5

Page 19: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Mumealiyetorokwaau kutelekezwa na mke.

Mke aliyetorokwaau aliyetelekezwana mume.

Mwanaume mwenye wake zaidi ya mmoja anawajibika kuwatunzawake wote kwa usawa.

Endapo mke amemtoroka au kumtelekeza mume wake, wazazi wa mke watamjulisha mume wa mke huyo kuwa mke wake amekimbilia kwa wazazi wake.

Mara baada ya kumjulisha mume aliyetorokwa au kutelekezwa na mke, wazazi wa mke aliyetoroka watafikisha suala hilo mbele ya Baraza la Ukoo na Baraza la Ukoo litawaita mume na mke ili kuwasuluhisha.

Iwapo mwanamke atakuwa ametoroka na kwenda sehemu nyingine tofauti na kwa wazazi wake, mume wake atalazimika kuwajulisha wazazi wa mke wake na atakuwa na jukumu la kumtafuta mke wake kwa kadiri atakavyoweza.

Mke aliyetelekezwa au kutorokwa na mume wake atalifikisha shauri lake mbele ya Baraza la Ukoo wa mume huyo ili litafutiwe ufumbuzi kwa mujibu wa sheria za kimila.

Baraza la Ukoo linaweza kutoa uamuzi wowote stahili ikiwa ni pamoja na kushauri Baraza la Ukoo kumtafuta mume wake kwa kadiri atakavyoweza.

(2)

(2)

(3)

(2)

16 (1)

17.-(1)

6 6

Page 20: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA NNETALAKA NA KUTENGANA

Sababu zakuvunjaNdoa.

Mume na mke wanaweza kutengana au kuachana kufuatana na utaratibu uliowekwa na Sheria ya Ndoa, 1971.

Endapo mume au mke anataka kuvunja ndoa waliooana kimila, wazo hilo litafikishwa kwanza mbele ya Baraza la Ukoo wa mume na wa mke na wanandoa wataitwa ili Baraza lijaribu kutafuta suluhu na kuinusuru ndoa yao.

Endapo haitawezekana kwa sababu yoyote ile kuitishakikao cha Baraza la Ukoo kwa mujibu wa kanuni hii, wazo la kuvunjwa kwa ndoa litawasilishwa mbele ya baraza lolote la usuluhishi ambalo limeundwa kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na Bunge.

Pale Baraza la usuluhishi litakaposhindwa kuwashawishi wanandoa kuinusuru ndoa yao kwa maelewano Baraza litatayarisha taarifa ya kushindwa kwake kuwasuluhisha wanandoa na taarifa hiyo itawasilishwa mahakama ya mwanzo ili kufungua kesi ya madai ya talaka.

Sababu za kimila zinazoweza kusababisha Baraza la Ukoo kupendekeza kupelekwa shauri mahakamani ni pamoja na-

(a) mwanandoa kushindwa kutimiza tendo la ndoa;(b) ugoni; (c) ukatili wa mmoja wa wanandoa;(d) mmoja wa wanandoa kushindwa kumtunza mwenzi wake;

18. (1)

(2)

(3)

(4)

(5)

77

Page 21: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Matunzo kwamke baada ya ndoa kuvunjwa.

Matunzo kwa watoto baada ya ndoa kuvunjwa.

Mashtaka ya ugoni.

(e) ulemavu wa akili wa mmoja wa wanandoa unaohatarisha maisha ya mwanandoa au watoto;(f) mmoja wa wanandoa kukataa kumfuata mwenzi wake aliyehamia sehemu nyingine bila ya kuwa na sababu ya msingi;(g) mke au mume kukataa kufanya tendo la ndoa na mwenzi wake mara kwa mara bila ya sababu ya msingi; au (h)sababu nyingine yoyote ambayo Baraza la Ukoo au Baraza la usuluhishi litaona inatosha kupendekeza kuvunja ndoa husika.

Matunzo kwa mke baada ya ndoa kuvunjwa itakuwa kama ilivyoainishwa na Sheria ya Ndoa, 1971.

Matunzo ya watoto baada ya ndoa kuvunjwa itakuwa kama itakavyoamuliwa na mahakama kwa kufuata Sheria ya Bunge.

Mashtaka ya ugoni yatafikishwa mbele ya Baraza la Ukoo la mume au mke anayelalamika na Baraza la Ukoo linaweza kuamuru kulipa fidia kwa muathirika.

Mashtaka yoyote ya uzinzi au madai ya fidia hayawezi kutiliwa nguvu mpaka uwepo ushahidi wa kutosha kuonyesha kwamba tendo la uzinifu limefanyika.

Wanandoa tu watakuwa na uwezo wa kufungua madai ya kuvunjwa kwa ndoa.

Mashtaka juu ya kuachana yanaweza kufikishwa mbele ya Baraza la Ukoo

19.

20.

(2)

(3)

(4)

21.-(1)

8 8

Page 22: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

kama kuna uhakikisho juu ya tendo la uzinzi.

Baraza la Ukoo liachiwe kufikiria na kuamua kama ushahidi ulioletwa mbele yake ni ushahidi wa kutosha kwa ugoni au kama unahitaji kuthibitishwa zaidi.

Iwapo mume au mke anarudi baada ya kuondoka kwa muda mrefu naanamkuta mwenzi wake wa ndoa anakaa kinyumba na mtu mwingine, anaweza kudai talakapamoja na fidia yaugoni bila ya kuhitaji uhakikisho zaidi.

Iwapo mume anarudi na kumkuta mke wake amebeba mimba au amezaa mtoto ambaye hawezi kuwa wake kwa sababu ya kutokuwepo kwake, anaweza kufanya yafuatayo:

kudai fidia ya ugoni,kukataa kumpokea mtoto yule kama wake na kumsamehe mke wake, na mtoto anakuwa wa ujombani;

kudai fidia ya ugoni,kukataa kumpokea mtoto yule kama wake na kumsamehe mke wake, na mtoto anakuwa wa ujombani;kudai fidia ya ugoni, kumkubali mtoto kuwa wake au;kumsamehe mke wake;kudai fidia ya ugoni kumuacha mke wake na mtoto wa ugoni anakuwa wa ujombani;kuwasilisha shauri katika Mahakama ya Mwanzo.

(5)

(6)

(7)

(a)

(b)

(c)

(d)

99

Page 23: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Iwapo aliyesafiri ni mume au mke atalazimika kukata shaurimaramoja juu ya mimba au mtoto aliyemkuta na iwapo bado hatakikukata shauri na anaendelea na maisha yake ya ndoa kama desturi, itachukuliwa kwamba mume au mke amesamehe yote.

Iwapo mke anarudi na kumkuta mume ana mtoto ambaye ni matokeo ya ugoni anaweza kufanya yafuatayo:

kudai fidia ya ugoni na kutaka waachane;kudai fidia ya ugoni, kumkubali mtoto kuwa wake na kumsamehe mume wake.

(8)

(9)

(a)

(b)

10 10

Page 24: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA TANOHALI YA MTOTO

Matunzo ya mtoto wa mwanamke asiyeolewa ambaye ni marehemu.

Matunzo ya mtoto wa kambo.

Taratibu za kumhalalisha mtoto.

Matunzo ya mimba ya mtoto wa nje ya ndoa.

Taratibu na vigezo vya kuasili mtoto.

Mtoto aliyezaliwa na mwanamke ambaye hakuolewa na amefariki atatunzwa na ukoo wa mama yakeau ukoo wa baba yake kulingana na mahakama maalum ya watoto.

Baba anayeishi na mtoto wa kambo ana wajibu wa kumtunza mtoto huyo.

Mtoto ambaye hakuzaliwa ndani ya ndoa na ambaye baba yake hajulikani atakuwa sehemu ya ukoo wa mama.

Baba anaweza kuhalalisha mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa kwa kumuoa mama yake.

Baba anaweza kumhalalisha mtoto wake bila ya kumuoa mama yake kwa kulipa fidia baada ya makubaliano ya pande zote mbili.

Mama atawajibika kuthibitisha madai kuhusiana na mtu anayedaiwa kuwa baba wa mtoto.

Mwanaume aliyempa mimba msichana ana wajibu wa kutoa gharama zote za matunzo wakati wa mimba, kuzaliwa kwa mtoto pamoja na matunzo ya mtoto huyo akishazaliwa.

Mtoto ataasiliwa kwa mujibu wa taratibu zilizoainishwa na Sheria ya Mtoto, 2009.

22.

(2)

(3)

(4)

23.

25.

26.

24.-(1)

1111

Page 25: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Kupokea mahari ya mtoto wa nje ya ndoa.

SEHEMU YA SITAURITHI

Makundi ya urithi.

Warithi wa kundi la kwanza.

Warithi wa kundi la pili.

Warithi wa kundi la tatu.

Warithi wa mali ya marehemu aliyeacha mke moja.

Mahari ya msichana aliyezaliwa nje ya ndoa ambaye baba yake mzazi hakumhalalisha itapokelewa na jamaa wa ukoo wa mama yake wakiongozwa na mjomba wa mtoto huyo.

Watoto wote wa marehemu wana haki ya kurithi mali ya marehemu baba yao kwa usawa.

Mke au wake wa marehemu wana haki ya kurithi mali ya marehemu.

Endapo marehemu hakuacha mke wala mtoto warithi wa mali ya marehemu watakuwa ni wazazi na ndugu zake.

Kundi la kwanza la warithi ni mke au mume wa marehemu.

Kundi la pili la warithi ni la watoto wa marehemu.

Kundi la tatu la warithi ni kaka, dada, wazazi wa marehemu na nduguwengine kulingana na ukaribu wao kwa marehemu.

Warithi wa mali ya marehemu ni mke wake na watoto kama ameacha watoto.

Endapo marehemu hakuacha watoto, mjane wa marehemu atarithi nusu ya mali ya marehemu na nusu nyingine itarithiwa na ndugu wa marehemu.

27.

28. (1)

(2)

(2)

(3)

29.

30.

31.

32. (1)

12 12

Page 26: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Warithi wa mali ya mke.

Warithi wa mali za mtoto wa kike ambaye hakuolewa.

Haki ya mtoto wa kambo urithi.

Taratibu za kubadilisha warithi.

SEHEMU YA SABAWOSIA

Haki ya kutoa wosia.

Aina ya wosia.

Warithi wa mali ya mwanamke aliyeolewa watakuwa ni mume na watoto wake.

Warithi wa mali za mwanamke ambaye hakuolewa ni watoto wake.

Endapo marehemu hakuacha watoto warithi wa mali yake watakuwa ni wazazi wake.

Endapo wazazi wa marehemu hawapo wajomba au jamaa wa upande wa mama yake watarithi mali yake.

Mtoto wa kambo ana haki ya kurithi mali ya mama yake wa kambo kwa wosia.

Mtoto wa kambo ana haki ya kurithi mali ya baba yake wa kambo kwa wosia.

Warithi wanaweza kubadilishwa kama kuna sababu za msingi kupitia kikao cha ukoo na kikao hicho ndicho kinaweza kubadilisha mpangilio wa warithi.

Kila mtu ana haki ya kutoa wosia kuonyesha ni jinsi gani angependa mali yakeigawanywe baada ya yeye kufariki.

Wosia unaweza kuwa wa maandishi au wa mdomo.

33.

36.

37.

38.

(2)

(2)

(3)

34. -(1)

35. (1)

1313

Page 27: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Umri wa mtoa wosia.

Taratibu za kutoa wosia.

Wosia wa mdomo.

Utaratibu wa kubadilisha wosia wa mdomo.

Mtu yeyote aliye chini ya umri wa miaka kumi na nane hawezi kutoa wosia.

Wosia wowote ni lazima ushuhudiwe na mashahidi maalumu ambao lazima wawepo wote kwa wakati mmoja.

Mashahidi wa wosia watachaguliwa na mwenye kutoa wosia mwenyewe.

Mke au wake wa mwenye kutoa wosia waliopo nyumbani lazima washuhudie pamoja na mashahidi wengine waliochaguliwa.

Mtu yeyote atakayerithi mali yeyote kutoka kwenye wosia hatakiwi kuwa shahidi wa kushuhudia wosia, isipokuwa kama shahidi ameteuliwa na mtoa wosia.

Wosia wa mdomo lazima ushuhudiwe na mashahidi wasiopungua wanne ukiwahusisha watu wa ukoo wasiopungua wawili na watu wasio wa ukoo huo wasiopungua wawili.

Endapo mtoa wosia ataamua kugawa mali yake upya itamlazimu atoe wosia mpya.

Wosia wa mdomo utabadilishwa na mtoa wosia kwa kutoa wosia mwingine mbele ya mashahidi aliowachagua mwenyewe.

Mke au wake wa mwenye kutoa wosia waliopo nyumbani lazima washuhudie kubadilishwa kwa wosia huo wa mdomo.

Wosia huo ni lazima ushuhudiwe na mashahidi wasiopungua wanne wakiwemo watu wa ukoo wasiopungua

39.

(2)

(3)

(4)

(2)

(2)

(3)

40. - (1)

41. (1)

42. (1)

1414 14

Page 28: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Utaratibu unaofuatwa pale mashahidi wa wosia wanapokuwa wote wamefariki auhawapo.

Wosia wa maandishi.

wawili na watu wasio wa ukoo huo wasiopungua wawili.

Ikiwa mashahidi wa wosia wamefariki wote kabla ya mwenye kutoa wosia kufariki, itakuwa ni jukumu la mtoa wosia kuchagua mashahidi wengine na kutoa wosia mwingine, ikiwa hajafanya hivyo basi urithi utagawanywa kwa kufuatautaratibu wa urithi usio na wosia.

Ikiwa mashahidi wengine wamefariki na mashahidi walio hai bado hawapungui wawili, wosia huo utafuatwa.

Wosia wa maandishi unatakiwa uwe na tarehe.

Wosia wa maandishi lazima ushuhudiwe na mashahidi wanaojua kusoma na kuandika.

Mashahidi wa wosia lazima wachaguliwe na mwenye kutoa wosia.

Mashahidi wa wosia wanatakiwa wasipungue wawili, mmoja wa ukoo na mmoja asiye wa ukoo wake ikiwa mtoa wosia anajua kusoma na kuandika; na mashahidi wasipungue wanne ambao wawili watakuwa ni wa ukoo wake na wawili watakuwa sio wa ukoo wake, endapo mtoa wosia hajui kusoma na kuandika.

Mtoa wosia analazimika kuweka saini yake kwenye wosia wa maandishi endapo anajua kusoma na kuandika na endapo hajui kusoma na kuandika ataweka alama ya kidole gumba, baada ya kusomewa, kuhakikisha na kuuridhia wosia huo kupitia mashahidi wake.

43 . (1)

4 4 . - ( 1 )

(2)

(2)

(3)

(4)

(5)

15 1515

Page 29: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Wosia kwenye mgawanyo wa mali.

Utaratibu unaofuatwa kwa mtu aliyefariki bila kuacha wosia.

Kukataliwa kwa wosia.

Mashahidi wa wosia washuhudie saini au alama ya mwenye kutoa wosia, na mashahidi waweke saini zao katika wosia.

Karatasi ya wosia isijazwe wala isiongezwe chochote na mtu mwingine yeyote.

Wosia wa maandishi hauwezi kufutwa au kubadilishwa na wosia wa mdomo, ila wosia wa mdomo unaweza kubadilishwa au kufutwa na wosia wa maandishi, wakiwepo mashahidi wote walio hai na wanaoweza kupatikana walioshuhudia wosia wa mdomo.

Mwenye kutoa wosia atakuwa na mamlaka ya mwisho kuhusu mali yake. (2) Ikiwa mwenye kutoa wosia anausia sehemu tu ya mali yake, mali inayobaki bila kutajwa kwenye wosia itagawanywa kufuatana na masharti ya urithi usio na wosia.

Iwapo marehemu hakuacha wosia, Baraza la Ukoo litakaa na kumteua msimamizi ambaye atasimamia mirathi ya marehemu kwa mujibu wa mila na desturi kwa kufuata makundi yaliyoainishwa na Tamko hili.

Wosia unaweza kukataliwa endapo itathibitishwa kuwa mtoa wosia alitoa wosia huo akiwa hana akili timamu kwa sababu ya ulemavu wa akili, ugonjwa, ulevi, hasira ya ghafla kurubuniwa au ulaghai.

Wosia ambao hautakidhi masharti yaliyoainishwa katikaTamko hili hautatambulika kuwa ni wosia halali.

4 5 . - ( 1 )

(6)

46.

(2)

47. (1).

(7)

(8)

16 16

Page 30: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Kupotea kwa wosia.

Sababu za kumnyima mrithi, urithi.

Taratibu za kutunza kumbukumbu za wosia.

Taratibu za kubadilisha warithi walioandikwa kwenye wosia.

Taratibu za kugawa mali ya marehemu ambaye hakuacha wosia.

Utaratibu wa kusajili vifo.

Kutunza kumbukumbu za vifo.

Iwapo wosia umepotea na mtoa wosia yuko hai, atalazimika kuandaa wosia mwingine.

Ikiwa wosia umepotea na mtoa wosia amefariki, urithi utasimamiwa kama vile mtu huyo hakuwa na wosia.

Mtu atakayemnyima mrithi, urithi atalazimika kutamka bayana kwenye wosia wake pamoja na sababu zilizopelekea kufikia uamuzi huo.

Halmashauri ya wilaya itaweka utaratibu wa kutunza kumbukumbu za wosia wa maandishi na pia kuwateua maafisa wanaoweza kuhifadhi wosia katika Halmashauri husika katika ngazi ya Kata, kitongoji, mtaa nakijiji.

Mtoa wosia atabadilisha majina ya warithi baada ya kuita mashahidi walioshuhudia wosia huo kama watakuwa wamefariki au hawapatikani basi mtoa wosia ataandaa wosia mpya.

Baraza la Ukoo litafanya maamuzi ya ugawaji wa mali ya marehemu ambae hakuacha wosia kwa kufuata sheria za mila za kabila husika.

Itakuwa jukumu la wanafamilia kupeleka taarifa za vifo katika Serikali ya kijiji kwa ajili yakusajiliwa.

Serikali ya kijiji itahusika na kusajili na kutunza kumbukumbu zote za vifo.

48.

49.

50.

51.

52.

53.

(2)

54.-(1)

1717

Page 31: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA NANEUGAWAJI WA MALI ZA URITHI

Taratibu za kumteua msimamizi.

Taratibu za kugawa mali inayohamishika na isiyohamishika.

Serikali ya kijiji itaweka utaratibu wa kuratibu uwekaji wa kumbukumbu za vifo ndani ya kijiji husika.

Serikali ya kijiji baada ya kupokea kumbukumbu hizo itawasilisha nakala za kumbukumbu hizo kwenye Kata na hatimaye kwenye Halmashaurihusika.

Kutakuwa na msimamizi atakayewajibika kusimamia mirathi ya marehemu.

Msimamizi atateuliwa na Baraza la Ukoo au kikao cha familia kwa kuzingatia vigezo vifuatavyo :(a) uaminifu;(b) heshima;(c) nidhamu;(d) uadilifu;(e) busara; na(f) uelewa wake.

Baada ya uteuzi wa msimamizi, Baraza la Ukoo au kikao cha familia kitaandaa muhtasari wa kikao hicho na kuufikisha kwenye Mahakama ya mwanzo, pamoja na cheti cha kifo, kwa ajili ya uteuzi rasmi wa Msimamizi.

Iwapo kutakuwa hakuna wosia, mali zote za marehemu zisizohamishika na zinazohamishika zitagawanywa kwa kuzingatia makundi yaliyokubaliwa yakiwa ni watoto wa marehemu, mjane au wajane, wazazi wa marehemu na ndugu wengine.

(2)

(3)

(2)

(3)

56.

55. -(1)

18 18

Page 32: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Kazi za msimamizi.

Malipo ya msimamizi.

Kushughulikia malalamiko yanayotokana na ugawaji mali.

Taratibu za ulipaji wa madeni ya marehemu.

Msimamizi wa mali atakuwa na kazi zifuatazo:(a)

(b) (c)

(d)

(e)

(f)

Msimamizi wa ugawaji mali hatalipwa kitu chochote, nje ya kurudishiwa gharama alizotumia katika kusimamia mirathi husika.

Iwapo msimamizi atakuwa amefanya kazi vizuri itakuwa ni hiyari ya warithi wa marehemu kumpa kitu chochote wanachoona kinafaa kama shukrani yao kwake.

Iwapo kuna malalamiko yeyote yanayotokana na ugawaji mali kikao cha ukoo kitakaa na kushughulikia malalamiko hayo.

Iwapo marehemu ameacha madeni yoyote, baada ya msiba wadeni wote wa marehemu wanatakiwa kupeleka madai yao yote kwa msimamizi.

Kikao cha ukoo kitajadili uhalali wa madeni au madaiyaliyoletwa na kuyajumlisha yote kwa pamoja.

57.

59.

(2)

(2)

kuwatambua warithi halali wa marehemu; kukusanya mali;kuhakikisha mali zinagawiwa sawa kwa warithi wote bila upendeleo wa aina yeyote ile na kwa wakati;kuhakiki kama waliogawiwa wameridhika na gawio walilopata na kama kuna tatizo la ugawaji mali msimamizi ndiye atakayelitatua kwa ngazi ya awali;kulipa madeni ya marehemu kama yapo; nakudai madeni ya marehemu kama yapo.

58. -(1)

60. (1)

1919

Page 33: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Ugawaji wa ardhi ya marehemu.

Taratibu zakugawa mifugo ya marehemu.

Taratibu za kurithi mali ya marehemu aliyoiacha kama zawadi.

Utunzaji wa Kumbukumbu za ugawaji mali ya marehemu.

Msimamizi akishirikiana na familia ya marehemu watawajibika kulipa madeni yote kwa kutumia mali ya marehemu.

Iwapo mali ya marehemu haitoshi kulipa madeni yake yote Baraza la Ukoo litakutana na kuamua namna ya kulipa madeni hayo. .

Iwapo marehemu alikuwa anaishi au kutumia ardhi ya ukoo, ardhi hiyo haitagawiwa kama sehemu ya urithi, bali itaendelea kuwa ardhi ya ukoo husika.

Iwapo marehemu alikuwa akiishi au kutumia ardhi yake mwenyewe, ardhi hiyo itahesabiwa kama mali nyingine za marehemu katika kugawa mali zake.

Mifugo itagawiwa kama mali nyingine kwa warithi wa marehemu.

Mali ya marehemu aliyoaicha kama zawadi itaendelea kuwa mali ya yule aliyepewa zawadi hiyo, isipokuwa kama zawadi hiyo ilitolewa bila ridhaa ya marehemu.

Halmashauri ya Wilaya itakuwa na jukumu la kutunza kumbukumbu za mgao wa mali ya marehemu kwa mujibu wa sheria zilizotungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

(3)

(4)

(2)

62.

63.

64.

61. (1)

20 20

Page 34: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA TISAARDHI YA UKOO

Taratibu za kumteua mtunzaji wa ardhi ya ukoo.

SEHEMU YA KUMIJANDO NA UNYAGO

Kamati ya Jando na Unyago.

Kutakuwa na mtunzaji wa ardhi ya ukoo atakayewajibika kusimamia matumizi endelevu ya ardhi ya ukoo.

Uteuzi wa mtunzaji wa ardhi ya ukoo utafanyika chini ya Baraza la Ukoo.

Ardhi ya ukoo itatunzwa na kiongozi wa ukoo na itatumiwa kwa manufaa ya wana ukoo wote.

Mtunzaji wa ardhi ya ukoo anapokuwa hawezi kutimiza majukumu yake ama kwa sababu ya ugonjwa, uzee, kukosa uadilifu au kifo Baraza la Ukoo litakaa na kumteua mtunzaji ardhi ya ukoo mwingine.

Kila Halmashauri ya wilaya itaunda Kamati ya Jando na Unyago itakayojumuisha viongozi wa jadi wasiopungua saba chini ya uenyekiti wa Afisa Utamaduni wa Halmashauri husika na viongozi wengine kutoka idara za afya, elimu na ustawi wa jamii zilizopo katika halmashauri husika.

Kamati ya Jando na Unyago itapanga ratiba za shughuli za jando na unyago kwa kuzingatia maslahi ya vijana husika pamoja na kuhakikisha kuwa ratiba za shule haziathiriwi na shughuli za jando na unyago.

65 . (1)

(2)

(3)

(4)

(2)

66. (1)

21 21

Page 35: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Muda wa kufanya jando na unyago.

Taratibu za jando na unyago.

Mafundisho yanayotolewa kwenye jando au unyago.

Sherehe za Jando na Unyago zisizozingatia umri.

Kamati ya Jando na Unyago itahakikisha kuwa, vijana wanaoshiriki katika jando au unyago wanakuwa na umri stahili kuhudhuria mafunzo ya jando au unyago, na shughuli za jando au unyago zinazingatia misingi ya afya ya mtoto.

Sherehe za jando na unyago zitafanyika wakati wa kipindi cha mavuno na wakati watoto watakuwa likizo ya shule.

Shughuli zote za jando na unyago zitafanyika katika mazingira ya usafi na ni lazima zizingatie kanuni za afya dhidi ya magonjwa ya kuambukiza na madhara mengine yoyote.

Mtoto atafanyiwa jando au unyago anapotimiza umri wa miaka tisa wakati wa kipindi cha mavuno wakati akiwa likizo ya shule.

Mafundisho yanayotolewa kwenye jando au unyago ni-(a)

(b)

(c) (d)

(e) (f)

Itakuwa ni kosa kwa mujibu wa Tamko hili kwa mtu, watu au kikundi cha aina yoyote kufanya sherehe za jando au unyago kwa mtoto ambaye hajatimiza umri ulioainishwa kwenye Tamko hili na wakati ambao si wa likizo za shule.

(3)

(2)

67. (1)

68.

69.

kuheshimu wazazi na jamii kwa ujumla;kufanya kazi kwa bidii na kuwa wakakamavu;elimu ya afya; kupenda elimu na kupenda maendeleo;ujasiri;nauvumilivu

70.

2222 22

Page 36: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Tohara

SEHEMU YA KUMI NA MOJAWAJANE

Kosa la kumrithi mjane.

Matunzo ya mjane mwenye watoto.

Matunzo ya mjane ambaye hana watoto.

Tohara kwa wanaume itatakiwa kufanyika chini ya wataalamu wa afya walioidhinishwa na Halmashauri ya Wilaya.

Itakuwa ni kosa kwa mtu yeyotekumrithi mjane au kufanya utaratibu au taratibu zitakazopelekea kutimiza lengolake ya kumrithi mjane.

Iwapo marehemu ameacha mali matunzo ya mjane mwenye watoto yatakuwa juu yake mwenyewe kwa kutumia maliiliyoachwa na marehemu mume wake.

Iwapo marehemu hakuwa na mali basi matunzo ya mjanewenye watoto yatakuwa chini ya uangalizi wa wanafamilia mpaka pale mjaneatakapokuwa na uwezo wa kujitunza mwenyewe au atakapoolewa na mume mwingine.

Mjane ambaye hana watoto atapata sehemu ya urithi wake na kuruhusiwa kurudi kwao iwapo ataridhia yeye mwenyewe na atatunzwa na wazazi wake.

Iwapo mjane hataridhia kurudi kwao atakuwa na haki ya kukaa kwenye nyumba ya familia yake na kurithi mali za marehemu mume wake kwa utaratibu uliowekwa kwenye Tamko hili, isipokuwa ardhi ya ukoo ambayo atakuwa na haki ya kuitumia hadi atakapokufa au atakapoolewa na mwanaume mwingine.

71.

72.

(2)

(2)

73. (1)

74. (1)

23 2323

Page 37: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

SEHEMU YA KUMI NA MBILIUANGALIZI

Namna au aina za uangalizi.

Uangalizi wa watoto.

Wajibu wa mwangalizi.

Uangalizi ni wa aina zifuatazo-(a)

(b)

(c)

(d)

Mwangalizi wa watoto wadogo waliofiwa na baba yaoatateuliwa na Baraza la Ukoo.

Ikiwa mzaliwa wa kwanza ni mtu mzima, mwenye akili timamu, hekima na tabia nzuri, atateuliwa kuwa mwangalizi wa wadogo zake.

Ikiwa mzaliwa wa kwanza hafai kuwa mwangalizi wa watoto atateuliwa ndugu mwingine wa ukoo wa marehemu kuwa mwangalizi wa watoto kwa kuzingatia uwezo wa ndugu huyo wa kuwatunza watoto hao..

Ikiwa marehemu alikuwa na wake wengi, kila mzaliwa wa kwanza toka kila nyumba atafikiriwa kwanza kuwa mwangalizi wa wadogo zake katika nyumba yao.

Mwangalizi ataelezwa na Baraza la Ukoo wajibu wake wa uangalizi na kama hakuelezwa, ni juu yake kupata maelekezo ya wajibu wake kutoka kwa Baraza la Ukoo.

uangalizi wa mtoto aliyefiwa na baba wakati akiwa na umri chini ya miaka kumi na nane;uangalizi wa mali ya mrithi ambaye hayupo wakati wa kurithishwa; uangalizi wa mtu ambaye hawezi kujitegemea kwa sababu ya umaskini, ulemavu, uzee au maradhi;uangalizi wa mke na mtoto wa mtu anayekwenda safari ndefu.

75.

(2)

(3)

(4)

76.- (1)

77. (1)

2424 24

Page 38: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Kazi ya mwangalizi itakuwa ni kuwatunza watoto na mama yao, nakuangalia mali yao isipotee wala isiharibike na mambo yote ya nje yanayohusu familia hiyo.

Mwangalinzi anawajibu wa kuangalia mali ya watoto walio chini yaulinzi wake, bila ya kuichanganya na mali yake na mali yake lazima ijulikane wazi.

Ikiwa Mwangalizi hatimizi wajibu wake, Baraza la Ukoo lina uwezo wa kumwondoa na kuteua mwingine.

Mwangalizi haruhusiwi kuuza mali alizokabidhiwa kwa niaba ya watoto, isipokuwa tu kama ni kwa munufaa ya watoto husika na lazima apate kibali cha kikao cha familia kufanya hivyo.

Mwangalizi atashughulika na mambo yote ya nje yanayohusu nyumba ile ya kusimamia mashauri, malipo ya kodi na ushuru, ada ya shule na kuhudhuria minada ya mifugo.

Mazao na mifugo vitatumika nyumbani kwa manufaa ya watu wa nyumbani.

Mwangalizi anaweza kuuza au kubadilisha mifugo kwa faida au mahitaji ya nyumbani.

Mashtaka au madai juu ya uangalizi yanaweza kuletwa na mjane, mtoto wa marehemu au ndugu yeyote wa ukoo kwenye Baraza la Ukoo.

Mashtaka au madai hayo hayatapokelewa mahakamani ikiwa hayakufikishwa kwanza kwenye Baraza la Ukoo.

(2)

(3)

(4)

(5)

(6)

(7)

(8)

(9)

(10)

25 2525

Page 39: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Uangalizi wa mali ya mrithi asiyekuwepo.

Iwapo mwangalizi atafariki, Baraza la Ukoo litateua mtu mwingine kuwa mwangalizimwanagalizi.

Mzaliwa wa kwanza atakapofikia miaka ishirini na moja (21) au atakapooa na kama ataonekana kuwa anafaa, Baraza la Ukoo litamteua kuwa mwangalizi wa wadogo zake.

Watoto walio chini ya uangalizi watakapofikia umri wa miaka ishirini na moja watatoka katika uangalizi.

Ikiwa hakuna ndugu yeyote wa ukoo wa watoto, Barazala Ukoo wa mama litateua mwangalizi toka kwenye ukoo wao.

Ikiwa hakuna ndugu yeyote wa ukoo, mahakama kufuatiamaombi ya mtu yeyote inaweza kumweka mtu mwingine asiye wa ukoo kuwa mwangalizi wa watoto.

Ikiwa mmoja wa warithi hayupo wakati wa kurithi, ndugu mwingine wa ukoo wake atateuliwa kuangalia mali hiyo mpaka mrithi huyo atakaporudi au kwa kipindi ambacho ataona kuwa kinafaa kama mrithi ataonekana kutorudi.

Mwangalizi wa mrithi asiyekuwepo atateuliwa na Baraza la Ukoo na anapoteuliwa ataelekezwa na Baraza la Ukoo wajibu wake wa uangalizi na kama hakuelezwa ni juu yake kupata maelezo ya wajibu wake kutoka kwenye Baraza la Ukoo.

(11)

(12)

(13)

(2)

(14)

15)

78 .- (1)

2626 26

Page 40: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Mtoto mkubwa kati ya warithi waliopo atafikiriwa kwanza na Baraza la Ukoo ikiwa kwa maoni yao ni mwenye akili timamu, hekima na mwenye tabia nzuri, ndiye atakayeteuliwa kuwa mwangalizi wa mali ya mrithi asiyekuwapo.

Ikiwa warithi wote hawapo au kwa maoni ya Baraza la Ukoo wataona haiwezekani kuteua mmoja wao kuwa mwangalizi wa mali ya mrithi asiyekuwepo, Baraza la Ukoo litateua mwangalizi yeyote toka kwenye ukoo ule kuangalia mali yote ya mrithi.

Mwangalizi wa mrithi asiyekuwepo akipoteza au akiharibu mali ya mrithi anaweza kudaiwa.

Mwangalizi wa mrithi asiyekuwepo hawezi kuchanganya mali ya urithi pamoja na mali yake yaani mali ya mrithi lazima ijulikane wazi.

Mwangalizi hawezi kutumia mali ya mrithi asiyekuwepo, isipokuwa kwa manufaa ya mrithin asiyekuwepo au kwa ajili ya gharama zinazohusiana na mali husika.

Mazao na mali ya mrithi asiyekuwepo zinaweza kuuzwa ili kutimiza shida za nyumbani kwa mrithi iwapo ameridhia mwenyewe.

Mwangalizi wa mrithi asiyekuwepo hatapata mshahara au malipo maalumu kwa kazi anayofanya, isipokuwa atakuwa na haki ya kurudishiwa gharama alizotumia kuhusiana na mirathi hiyo.

3.

4.

5.

6.

7.

8.

9.

27 2727

Page 41: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Uangalizi wa mtu ambaye hawezi kujitegemea.

Uangalizi wa familia na mali ya mtu aliyesafiri kwa muda mrefu.

SEHEMU YA KUMI NA TATUUSULUHISHI WA MIGOGORO

Wahusika wa usuluhishi.

Baraza la Ukoo linaweza kumwondoa mwangalizi wa mrithi asiyekuwepo ikiwa hatimizi wajibu wake na kuweka mwingine, kufuatia madai au mashtaka ya ndugu yeyote wa mrithi asiyekuwepo.

Ikiwa hakuna mtu yeyote kutoka kwenye ukoo wa mrithi asiyekuwepo na kufuatia maombi ya mtu yeyote, mahakama kufuatia maombi ya mtu huyo inaweza kuweka mtu mwingine asiye wa ukoo kuwa mwangalizi wa mali ya mrithi asiyekuwepo.

Mtu ambaye hawezi kujitegemea kwa sababu ya ulemavu, uzee na maradhi atawekwa chini ya uangalizi wa mtu wa ukoo wake.

Mwangalizi huyu atateuliwa na Baraza la Ukoo, na wajibu wake utakuwa sawa na ule wa mwangalizi wa mtoto katika Tamko hili.

Ikiwa mume ana kwenda safari ya muda mrefu, atashauriana na familia yake kuhusu uangalizi wa watoto, mali ama familia kwa ujumla.

Usuluhishi wa migogoro kwa njia ya mila utasimamiwa na vyombo vifuatavyo:(a) familia;(b) kikao cha ukoo;(c) baraza la wazee; na (d) mahakama.

10.

11.

80.

81.

(2)

79. (1)

28 28

Page 42: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba

Nafasi ya familia kwenye usuluhishi.

Nafasi ya wazee kwenye usuluhishi.

Nafasi ya ukoo kwenye usuluhishi.

Nafasi ya Baraza la wazee kwenye usuluhishi.

Usuluhishi unaposhindikana.

Ushahidi wakati wa usuluhishi.

Adhabu

Familia ndiyo hatua ya kwanza katika suala zima la usuluhishi wa migogoro.

Katika ngazi ya familia na ukoo, wazee ni wahusika wakuu katika usuluhishi wa migogoro yote.

Iwapo mgogoro hautapata usuluhishi katika ngazi ya familia, kikao cha ukoo kitakaa na kuutafutia usuluhishi mgogoro huo.

Iwapo mgogoro hautapata usuluhishi katika kikao cha ukoo, baraza la wazee litakaa na kuutafutia usuluhishi mgogoro huo.

Iwapo usuluhishi umeshindikana katika ngazi ya familia, kikao cha ukoo na baraza la wazee, utaratibu utakaofuata utakuwa ni kupeleka shauri mahakamani, Baraza la Kata au Baraza la Usuluhishi wa Ndoa kwa migogoro ya ndoa.

Wahusika katika mgogoro wa kimila wana haki ya kuitamashahidi wao wakati wa usuluhishi.

Uamuzi utakaotolewa katika usuluhishi, utazingatia ushahidi uliotolewa.

Iwapo mtu atapatikana na kosa kwa mujibu wa Tamko hili ataamuriwa kulipa fidia kulingana na uzito wa kosa husika

82.

83.

84.

85.

88.

86.

(2)

87. (1)

2929

Page 43: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TUME YA ... - lrct.go.tz 2013.pdf · Misingi ya sheria za Tanzania ambazo zinatumika katika mashauri ya kesi mbalimbali mahakamani inajumuisha Katiba