Top Banner
1 Fataawa Za Wanachuoni [13] Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©
30

Fataawa Za Wanachuoni (13)

Oct 30, 2014

Download

Documents

wanachuoni


1

.·«·-|· .,···
Fataawa Za Wanachuoni

[13]


Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush
©





2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili
kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji
elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya
Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.
Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida
Welcome message from author
This document is posted to help you gain knowledge. Please leave a comment to let me know what you think about it! Share it to your friends and learn new things together.
Transcript
Page 1: Fataawa Za Wanachuoni (13)

1

������� ���

Fataawa Za Wanachuoni

[13]

Imefasiriwa Na Kutayarishwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za Wanachuoni (13)

2

Dibaji:

Hizi ni Fataawa za wanachuoni mbali mbali ambazo nimezikusanya ili

kuweza kuwasahilishia ndugu zetu Waislamu na khaswa wale watafutaji

elimu. Fataawa ni mchanganyiko kuhusiana na masuala mbali mbali ya

Tawhiyd, ´Aqiydah, Manhaj, Fiqh na mengineyo.

Hivyo, ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) ziweze kuleta faida kwa ndugu

zetu Waislamu, na ninamuomba Allaah (´Azza wa Jalla) Ajaalie kazi hii niwe

nimeifanya kwa kutafuta Radhi Zake (Subhaanahu wa Ta´ala), na Amlipe kila

Aliyeisambaza kwa ndugu mwengine na Awalipe ndugu wasomaji wote kwa

jumla.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.

Page 3: Fataawa Za Wanachuoni (13)

3

Fataawa zilizomo ni hizi zifuatazo:

1. Kunywa Kwenye Kikombe Cha Dhahabu

2. Je, Ni Lazima Kwa Mke Kufanya Kazi Za Nyumbani?

3. Hukumu Ya Kusherehekea Krismasi Na Sikukuu Za Makafiri

4. Hukmu Ya Filamu Zinazolingania Katika Kheri Na Fadhila

5. Kufurahi Kwa Kufa Mwanachuoni IbnJibriyl

6. Anaekufa Huku Kaacha VitabuMbalimbali Vya Dini

7. Hatari Ya Mawasiliano Ya Wachumba

8. Jamaa´at-ut-Tabliygh Wanahitajia Jihaad

9. Kufasiri Vitabu Bila Ya Idhini Ya Mwandishi

10. Kunywa Katika Kikombe Cha Dhahabu

11. Swalat-ul-Kusuuf Msikitini Au Nyumbani?

12. Baba Hataki Kuswali Anadai Anajua Zaidi Yangu

13. Kumtembelea Mtu Ambaye Haswali

14. Habbat Sawdaa (Haba Soda) Ni Dawa Ya Kila Ugonjwa

15. Hukumu Ya Jina La ”al-Haadiy”

16. Je, Du´aa Hii Yatosheleza Du´aa Zingine Zote?

17. Je, Inajuzu Mwanamke Kuvaa Suruwali Pana Isiyobana?

18. Je Kumuona Mtume Usingizini Ni Bishara Njema?

19. Kuomba Wafu Ni Shirki Kubwa Au Ndogo?

20. Kumpa Mtu Jina La "Mwenye Kumjua Allaah"

21. Kupokea Zawadi Ya Pesa Za Haramu

22. Kupunguza Ndevu Au Kufukuzwa Kazini?

23. Kusomea Maji Ruqyah Kisha Kuyaoga

24. Msafiri Kujumuisha Swalah Ya Ijumaa Na ´Aswr

25. Tofauti Ya Sunnah Na Ada Ya Mtume (و��م ���� ��)

26. Upi Msimamo Wa Mwanamke Kwa Madu´aat Wapotevu?

27. Wale Wanaotumia Mantiki Na Falsafa Katika Hadiyth

28. Wanachuoni Wa Hedhi Na Nifasi

29. Wale Wanaokaa Na Ahl-ul-Bid´ah Wamelaaniwa

30. Neno "Jins-ul-´Amal" Limetoka Kwa Murji-ah

31. Mwanamke Kwenye Nifasi Akitwaharika Kabla Ya Siku Arubaini

32. Mwanamke Anaetaka Kuzaa Kapitwa Na Swalah Nyingi, Afanye

Nini?

Page 4: Fataawa Za Wanachuoni (13)

4

33. Mishaary Raashiyd al-´Afaasy Na Anashiyd Zake

34. Kwa nini Mwanamke Hafai Kumuonesha Mwanamke

Wa Kikafiri Nywele Zake?

35. Kipote Kitakachookoka Na Moto

Wanachuoni waliomo ni hawa wafuatao:

1. ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

2. Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

3. Swaalih bin Swaalih bin Fawzaan

4. Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy

5. Zayd bin Muhammad bin Haadiy al-Madkhaliy

Page 5: Fataawa Za Wanachuoni (13)

5

Bismillaahi Rahmaani Rahiym

1. Kunywa Kwenye Kikombe Cha Dhahabu

Swali:

Swali kutoka Ireland. Je, inajuzu kunywa kwenye chombo cha dhahabu?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Jibu hapana! Chombo cha dhahabu haijuzu kukinywiya humo kitu.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=itDh565ss1s

2. Je, Ni Lazima Kwa Mke Kufanya Kazi Za Nyumbani?

Swali:

Je, mwanamke ni lazima kupika na kutandika kitanda nyumbani kwa ajili ya

mume wake?

´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy:

Ada za kiarabu na za Waislamu wengine katika wanawake ni kwamba wao

ndio wanaofanya kazi mbalimbali katika manyumba yao; kama kufua nguo,

kuangalia watoto n,k. Hili ni jambo wanaliweza baina ya Waislamu na

waarabu. Hatotoka mwanamke katika hilo. Kuna Wanachuoni wanaosema

kwamba hana ulazima wa chochote katika makazi, bali lililo la wajibu kwake

ni ile sababu ya mwanamme kumuoa. Akifanya kazi hizo basi yuko na ujira

Page 6: Fataawa Za Wanachuoni (13)

6

na kafuata Maswahabah wanawake wema [... sauiti imekatika ...] ufahamu

katika Dini.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=BkKE5lN0K2c

3. Hukumu Ya Kusherehekea Krismasi Na Sikukuu Za Makafiri

Swali:

Baadhi ya Waislamu wanasherehekea sikukuu ya kuzaliwa - yaani krismasi

kama wanavyoiita, tunaomba nasaha?

Imaam Ibn Baaz:

Haijuzu kwa Muislamu mwanamme na mwanamke kushirikiana na

Manaswara au Mayahudi au makundi mengine katika sikukuu zao. Ni wajibu

kuacha hilo kwa kuwa [Mtume yu wasema]:

"Mwenye kujifananisha na watu basi yeye ni miongoni mwao."

Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katukataza kushirikiana nao,

kuchukua tabia zao. Ni juu ya muumini mwanamme na mwanamke

kujiepusha na hilo wala wasihudhurie katika sikukuu zao kwa chochote. Kwa

kuwa sikukuu zao zinakhalifu Shari´ah ya Allaah isitoshe ni maadui wa

Allaah. Kwa hiyo haijuzu kushiriki humo wala kusaidizana nao wala

kuwasaidia kwa lolote; si kwa [kunywa] hata chai, kahawa na kadhalika. Pia

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala):

�وى و� ��و�وا ��� ا� م وا�دوان و��و�وا ��� ا��ر� وا���

”Na saidianeni katika wema na uchaji Allaah. Wala msisaidiane katika

dhambi na uadui.” (05:02)

Page 7: Fataawa Za Wanachuoni (13)

7

Kushirikiana na makafiri katika sikukuu zao ni aina ya kusaidiana katika

dhambi na uadui. Ni wajibu kwa Waislamu wote wanamme na wanamke

kuacha hilo. Wala mtu asidanganyike na wayafanyayo watu; bali ni wajibu

aangalie alifanyalo - Uislamu na yale iliyokuja nayo na atekeleza amri za

Allaah na Mtume Wake wala asidanganyike na mambo ya watu. Hakika watu

wengi hawajali na Shari´ah ya Allaah, kama alivyosema Allaah (´Azza wa Jall)

katika kitabu Chake kitukufu:

� وإن �ط+ أ( ر )ن '& ا%رض �#�"وك �ن ��ل

“Na ukiwatii wengi katika hawa waliomo duniani watakupoteza na Njia ya

Allaah.” (06:116)

و)� أ( ر ا����س و�و 1ر0ت �)ؤ)��ن

“Na wengi wa watu si wenye kuamini hata ukijitahidi vipi.” (12:103)

Ni wajibu kutekeleza Shari´ah, haijuzu kuichukulia sahali. Muislamu hufanya

vitendo na kauli zake na za watu kwa mujibu wa Qur-aan na Sunnah za

Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ikiwa yataafikiana nayo

(Qur-aan na Sunnah) basi yatakubaliwa hata watu wakiyaacha. Na

wakiyakhalifu au wakayachukia watu, yatarudishwa (hayatokubaliwa) hata

watu wakiyafanya.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=O7jikWCbou0

4. Hukmu Ya Filamu Zinazolingania Katika Kheri Na Fadhila

Swali:

Page 8: Fataawa Za Wanachuoni (13)

8

Huyu anauliza hukumu ya filamu ambazo zinalingania katika kheri na

fadhila?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kheri na fadhila bila ya filamu. Hawakuwa Salaf wakicheza filamu. Hizi ni

katika desturi ambazo zimetujia kutoka nje. Wala hatutumii filamu kwa

Da´wah. Si katika mfumo wa Da´wah kucheza filamu, kamwe.

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa &

http://www.youtube.com/watch?v=axQeeDqdIbs

5. Kufurahi Kwa Kufa Mwanachuoni IbnJibriyl

Swali:

Baadhi ya wanafunzi walifurahi kwa kufa Shaykh Ibn Jibriyn (Rahimahu

Allaah). Je, kitendo hichi ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili halijuzu. Haijuzu kufurahi kwa kifo cha Waislamu wote kwa jumla.

Haijuzu kwa kuwa hili ni kashfa katika Uislamu. Tusemeje kwa kifo cha

mwanachuoni? Haijuzu hili kuwa wanafurahi kwa mauti ya mwanachuoni

katika Wanachuoni wa Kiislamu. Hili linatokana ima kwa ujinga au unafiki -

A´udhubi Allaah.

Chanzo: http://alfawzan.ws/node/2034

http://www.youtube.com/watch?v=uOWhuy9lQJc

Page 9: Fataawa Za Wanachuoni (13)

9

Tarehe: 1430-08-18/2009-08-09

6. Anaekufa Huku Kaacha VitabuMbalimbali Vya Dini

Swali:

Muulizaji kutoka Ireland, je vitabu ambavyo vipo maktabah ni katika elimu

ambayo itakuja kumfaa mtu baada ya kufa kwake?

´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy:

Bila shaka, vitabu vya faida kama vya tafsiri, hadiyth, fiqh, syrah ya Mtume,

´aqiydah na vitabu vingine vya Kiislamu akifariki mtu na kukaja mtu baada

yake sawa ndugu au wengineo, hakika yuko na ujira mbele ya Allaah

(Tabaarak wa Ta´ala) kwa elimu ya manufaa aliyoacha.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=b-4Jbk_ySkU

7. Hatari Ya Mawasiliano Ya Wachumba

Swali:

Je, inajuzu kuwasiliana wawili wanaotaka kuchumbiana kwa idhini ya walii

wake (mwanamke)?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Page 10: Fataawa Za Wanachuoni (13)

10

Hili halitakiwi kuwa moja kwa moja (yaani bila mipaka). Kwa kuwa

wakiwasiliana baina yao, mawasiliano mengi hakuaminiki huenda kukatokea

mawasiliano ya vitendo. Baada ya mawasiliano ya vitendo la kufuatia ni

mawasiliano ya kimwili. Hiki ni kitu kimeshajaribiwa na ni maarufu.

"Hawi mwanamme na mwanamke ispokuwa Shaytwaan huwa watatu wao."

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=caM_dg_KkwM

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action

8. Jamaa´at-ut-Tabliygh Wanahitajia Jihaad

Swali:

Muulizaji kutoka Ufaransa anauliza. Ipi Tafsiyr ya kauli ya Allaah

(Subhaanahu wa Ta´ala):

8 �د�ون إ�� ا�6�ر و�5)رون ���)روف و�3�ون �(م أ)� �ن ا�)�(ر و��(ن )�

“Na uwe kutokana na nyinyi umma unao lingania kheri na unao amrisha

mema na unakataza maovu.” (03:104)

Vipi tutawaradi Jama´at-ut-Tabliygh ambao hutumia Aayah hii?

Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Jama´at-ut-Tabliygh wanahitaji (kupigwa) Jihaad. Jama´at-ut-Tabliygh ni

makhurafi, wanaitakidi Usufi. Muasisi wake alikuwa akikaa kwenye kaburi la

"Kankoohi" kiasi cha nusu saa nzima. Alikuwa akikaa na kusema "Allaah

kahudhuria." Anasema Allaah kahudhuria kwenye kaburi la mtu yule.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=caM_dg_KkwM

Page 11: Fataawa Za Wanachuoni (13)

11

9. Kufasiri Vitabu Bila Ya Idhini Ya Mwandishi

Swali:

Ipi hukumu ya kufasiri (vitabu) bila ya kuomba idhini kwa wamiliki - yaani

mwandishi - kwa ajili ya biashara? Je, inajuzu kuuza na kununua vitabu hivi?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Kwa hakika haifai kwenda kinyume, inatakiwa kuomba idhini kwa

mwandishi au mmiliki. Wala haifai masuala yakawa vurugu. Vurugu

haipelekei kwenye chochote isipokuwa shari.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=7LfbMFmUK0I

10. Kunywa Katika Kikombe Cha Dhahabu

Swali:

Swali kutoka Ireland. Je, inajuzu kunywa kwenye chombo cha dhahabu?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Jibu hapana! Chombo cha dhahabu haijuzu kukinywiya humo kitu.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=7LfbMFmUK0I

Page 12: Fataawa Za Wanachuoni (13)

12

11. Swalat-ul-Kusuuf Msikitini Au Nyumbani?

Swali:

Swalat-ul-Kusuuf (Swalah ya kupatwa jua au mwezi) inaswaliwa nyumbani

au Jamaa´ah Msikitini na ipi kauli yenye nguvu katika hili?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Swalat-ul-Kusuuf inaswaliwa Msikitini na inaswaliwa nyumbani. Wanawake

wanaiswali nyumbani na wanaume wanaiswali Msikitini.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=2_ieB2FuyMo

12. Baba Hataki Kuswali Anadai Anajua Zaidi Yangu

Swali:

Baba yake haswali na anapomnasihi anasema: "Mimi najua zaidi yako wewe."

Unaninasihi nini kuamiliana naye?

´Allaamah al-Fawzaan:

Yaani hajui hata Swalah? Anajua zaidi yako wewe kisha hajui hata Swalah?

Huu ni ujinga mkubwa - A´udhubillaah. Au ni mjuzi mpotofu. Na ni juu yake

kuendelea nasaha naye akimukhofisha Allaah, akimukhofisha Allaah (´Azza

wa Jalla). Akikataa na yeye (mtoto) ni mwenye uwezo wa kuishi mwenyewe

Page 13: Fataawa Za Wanachuoni (13)

13

afanye hivyo, lakini aendelee kuwasiliana naye kwa wema na Ihsaan. Hata

kama atakuwa anaishi nyumba nyingine.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=YvSIjQzHbwI

13. Kumtembelea Mtu Ambaye Haswali

Swali:

Niko na baba mdogo ambaye anavuta sigara na wala haswali Msikitini Swalah

ya Ijumaa tu na (Swalah) zilizobaki anaswali nyumbani kwake bila ya

kuhifadhi wakati. Je, ni wajibu kwangu kuwasiliana naye, kumtembelea na

kumtolea Salaam kwa kuwa anasema usininasihi wala usiongee na mimi kwa

nasaha kamwe?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana usimtembelei maadamu anasema maneno haya basi ni kafiri, wala

hakubali nasaha. Muache!

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=YvSIjQzHbwI

14. Habbat Sawdaa (Haba Soda) Ni Dawa Ya Kila Ugonjwa

Swali:

Habbat Sawdaa (haba soda) imethibiti katika chakula chake kitu kama athari

au Hadiyth Swahiyh, sisi tunasoma baadhi ya maongozo (tukaona hivyo)?

Page 14: Fataawa Za Wanachuoni (13)

14

´Allaamah al-Fawzaan:

Imethibiti ya kuwa ina tiba ya kila ugonjwa isipokuwa mauti tu. Iko na dawa

kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ama jinsi ya

kuitumia itatokana na mt. (Mtu) anaweza kuitumia kwenye kinywaji, chakula,

akaitumia wakati wa kula au akainywisha maji au mfano wa hayo.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=4el_PeDIkDE

15. Hukumu Ya Jina La ”al-Haadiy”

Swali:

Je, inajuzu kuitwa kwa jina la “al-Haadiy”?

´Allaamah al-Fawzaan:

´Abdul-Haadiy hili ndio maarufu. al-Haadiy pekee ni (Jina la) Allaah.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=v2lHcGsbT1o

16. Je, Du´aa Hii Yatosheleza Du´aa Zingine Zote?

Swali:

Je, inachukuliwa hii Du´aa ni kubwa na yatosheleza kwa Du´aa zingine zote

zilizobaki, nayo ni:

Page 15: Fataawa Za Wanachuoni (13)

15

���� د ��� و��م و���دك ا�����ون ا���م إ�� أ���ك ن ��ر � ���ك ���ك

“Ewe Allaah mimi nakuomba katika ya kheri aliyokuomba nayo Mtume

Wako Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na waja Wako

wema.”

´Allaamah al-Fawzaan:

Du´aa hii ni kubwa lakini haitoshelezi Du´aa zilizobaki, bali kila Du´aa ajuazo

mtu aombe kwazo. Ni katika kujizidishia kheri wala asisimamie kwa

(kuomba) Du´aa moja tu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

hakusimamia (kwa kuomba) Du´aa moja; bali alikuwa akiomba kwa hii mara

fulani, na wakati mwingine kwa hii.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=ewVV1GR-iEs

17. Je, Inajuzu Mwanamke Kuvaa Suruwali Pana Isiyobana?

Swali La Kwanza:

Ipi hukumu ya kuvaa suruwali kwa mwanamke? Na je, kuna tofauti ikiwa

pana au nyembamba?

´Allaamah al-Fawzaan:

Katika mji wetu si ada ya wanawake kuvaa suruwali, na wanawake wanavaa

kutokana na wavaavyo wanawake wa mji. Haijuzu khaswa kayika mji huu

(Saudi Arabia) kuvaa suruwali. Hata katika miji mingine, kwa kuwa suruwali

inabainisha mwili wa mwanamke wala haisitiri stara kamili. Na huenda fitina

ya suruwali ikawa kubwa. Kwa kuwa inadhihirisha yaliyomo ndani.

Mwanamke ajiepushe kuvaa suruwali, hususan katika mji huu kwa kuwa hii

Page 16: Fataawa Za Wanachuoni (13)

16

si katika ada ya mji huu. Mwenye kuvaa mavazi yanayokwenda kinyume na

makubaliano (ya waislamu) basi yuko katika makemeo makali (kwa Mola

Wake).

Swali La Pili:

Vipi akivaa yuko nyumbani?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hata nyumbanni (haijuzu). Kwa kuwa ataanza kuivaa nyumbani kisha hatua

baada ya hatua ataanza kuivaa hata barabarani.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=165rIMROtGY

18. Je Kumuona Mtume Usingizini Ni Bishara Njema?

Swali:

Je, maono ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) usingizini katika

umbo lake huchukuliwa ni bishara kwa yule aliyemuona au kwamba ni katika

watu wa Peponi?

Imaam Ibn Baaz:

Ikiwa mtu atamuona kwa sura yake kama ilivyotangulia basi ni kheri – In

Shaa Allaah - lakini haizingatiwi kuwa ni kuokoka, au mafanikio, uchaji

Allaah n,k. Kwa kuwa kuna waliomuona Mtume (Swalla Allaah ´alayhi wa

sallam) kipindi cha uhai wao makafiri na wanafiki na haikuwafaa kitu muono

huu. Alimuona Abu Jahl na akafa kwenye kufuru wakati aliuawa katika vita

Page 17: Fataawa Za Wanachuoni (13)

17

vya Badr. Alimuona Ibn Rabiy´ah na Shaybah bin Rabiy´ah na wakauawa juu

ya ukafiri wao. Alimuona anko wake Abu Twaalib na akafa juu ya ukafiri.

Alimuona Abu Lahab na akafa juu ya ukafiri. Alimuona ´Abdullaah ibn

´Ubayd kiongozi wa wawanafiki na akafa juu ya ukafiri. Muono wa mtu

ambaye hapewi uzito katika uongofu wake au Uislamu wake au mafanikio

kwa watu wake; isipokuwa (yule) atayemuamini akamsadikisha na kumfuata

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Yapewa uzito zaidi ikiwa

atamuona usingizini. Atayemuona usingizini naye ni muumini mchaji Allaah;

hutarajiwa kheri mtu huyo ikiwa atamuona kwa sura yake ya kweli. Ama

atayemuona na haamini Shari´ah yake na hafuati yale aliyokuja nayo, hakika

muono huu hautomfaa kitu bali ni hoja dhidi yake, sawa akimuona kihakika

au usingizini. Kama walivyomuona wale makafiri katika uhai wake Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na haikuwafikisha kumuamini bali

iliwazidishiwa kuwa wanyonge. Na Allaah Atukinde kwa hilo. Hali kadhalika

kwa yule atayemuona usingizini hamuamini wala hafuati yale aliyokuja nayo,

haitomfaa kitu muono huu bali itakuwa ni hoja dhidi yake.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=fudgl4fkrbc

19. Kuomba Wafu Ni Shirki Kubwa Au Ndogo?

Swali:

Ipi kauli za wanachuoni kwa yule anayetaka Du´aa kutoka kwa wafu? Je, hili

linaingia katika Shirki kubwa au ndogo?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Bila shaka hili ni katika Shirki kubwa. Kwa kuwa anaitakidi kama maiti

anamsikia. Na Allaah (Ta´ala) katwambia kuwa maiti hawasikii.

Page 18: Fataawa Za Wanachuoni (13)

18

ن '& ا���ور و)� أ�ت �) )+ )�

”Wala wewe siwakuwasikilizisha walio makaburini.” (35:22)

Huyu anataka kutoka kwa wafu nini? Akiamini kuwa wanamsikia, pia

akiamini uwezo wao katika kitendo hichi, hii ni batili bali ni Shirki kubwa

inayomtoa mtu katika Uislamu. Anaeitakidi hivi ni (Shirki kubwa) inayomtoa

katika Uislamu.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=5Nu-mEnjAKo

20. Kumpa Mtu Jina La "Mwenye Kumjua Allaah"

Swali:

Inajuzu kutoa jina "Mwenye kumjua Allaah" kwa baadhi ya watu wema?

´Allaamah al-Fawzaan:

Huku ni kumtakasa mtu. Mwenye kumjua Allaah huku ni kutakasa na hili ni

maarufu kwa Suufiyyah.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=V333ryRJB4A

21. Kupokea Zawadi Ya Pesa Za Haramu

Swali:

Page 19: Fataawa Za Wanachuoni (13)

19

Je, inajuzu kupokea zawadi (inayotokana na) pesa za Haramu au

kuchanganyikana (nayo)?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Ni bora zaidi kutoikubali, bora zaidi kutoikubali.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=JpY4zl8Hl-s

22. Kupunguza Ndevu Au Kufukuzwa Kazini?

Swali:

Dada huyu anauliza mume wake anafanya kazi katika taasisi ya kutengeneza

pasta kama vile tambi na kadhalika, wamemuomba kupunguza ndevu zake ili

aweze (kuendelea) kufanya kazi. Je, inajuzu kwake kufanya hivyo na kama

hakufanya hivyo watamfukuza kazini?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Asiwatii, hichi ni kitu kimeumbwa fasi yake (kwa mwanamme), wala

asipunguze.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=r1yWnaIL2fM

23. Kusomea Maji Ruqyah Kisha Kuyaoga

Page 20: Fataawa Za Wanachuoni (13)

20

Swali:

Mimi nasomea maji Ruqyah ya Kishari´ah halafu nayanywa na kuyaoga. Je, ni

sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna ubaya. Ni vizuri kuoga maji ya Ruqyah. Na Allaah Anajua Zaidi.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=UyxhG1FwOz0

24. Msafiri Kujumuisha Swalah Ya Ijumaa Na ´Aswr

Swali:

Je, msafiri siku ya Ijumaa anajumuisha mwa zile nyakati za mwanzo au

anachelewesha?

´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy:

Msafiri siku ya Ijumaa akijiwa na wakati wa Ijumaa naye yuko katika safari,

anaweza kujumuisha (na ´Aswr). Sawa ikiwa ni wakati ule wa Ijumaa au

akichelewesha (hadi wakati wa Swalah ya ´Aswr]. Kwa kuwa hakuswali

Ijumaa. Ama kwa mfano anataka kuswali Ijumaa na kujumuisha na ´Aswr

hapana (haijuzu).

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=LnH8ZX-t8tE

Page 21: Fataawa Za Wanachuoni (13)

21

25. Tofauti Ya Sunnah Na Ada Ya Mtume (و��م ���� ��)

Swali:

Ipi kipimo (kujua) Sunnah za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa

kuwa watu wengi wamekuwa wakikazia katika mambo mengi na wanasema

na hili ni katika Sunnah; kwa mfano kuvaa kilemba, kuendesha farasi, nywele

ndefu. Na je, kila alichofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

inakuwa Sunnah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Aliyofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yako aina mbili:

1. Aina ya kwanza aliyoyafanya kwa minajili ya kuyaweka katika Shari´ah,

haya ni Sunnah ima ni (jambo) la wajibu au Mustahaba.

2. Ama aliyoyafanya kwa minajili (ilikuwa ni) ada yake; kama vile nguo,

kilemba, mavazi, kanzu, kikoi, haya ni katika ada yake na si ya Kiibaadah.

Nii ni ada yake.

Haya si Sunnah bali yanaingia katika mambo ya Mubaha na si katika mambo

ya Kiibaadah.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=OHuYbKOSAEg

26. Upi Msimamo Wa Mwanamke Kwa Madu´aat Wapotevu?

Swali:

Muulizaji mwanamke anauliza, upi msimamo wa mwanamke Muislamu

kutokana na Madu´aat (walinganiaji) wapotevu?

Page 22: Fataawa Za Wanachuoni (13)

22

´Allaamah al-Fawzaan:

Mwanamke na mwanaume msimamo wao ni kutoa nasaha katika jambo hili

na kukataza dhidi ya Madu´aat wapotevu na kutoa tahadhari (kwa watu)

dhidi yao, ili asije kudanganyika mwenye kudanganyika.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=HMN1UVyF6m8

27. Wale Wanaotumia Mantiki Na Falsafa Katika Hadiyth

Swali:

Mwenye kusema Hadiyth zinaweka dhana kuthibiti kwake - Hadiyth za

Ahaad wala hazichukui. Je, anaingia katika tishio la Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, anaingia katika tishio la Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa

kuwa wana makusudio mabaya. Makusudio yao watangulize dalili za

kimantiki, na falsafa waziweke mahala pa Hadiyth. Haya ndio makusudio

yao. Wanasema dalili za kimantiki ndio za mwisho (kutegemewa), na dalili za

Hadiyth ni za kudhania. Wanatanguliza za kukata shauri (falsafa & mantiki)

kabla ya hizi za dhana (Hadiyth). Ni kinyume chake, Hadiyth ndio za mwisho

(baada ya Qur-aan) na kanuni za kimantiki ndio za kudhania. Kwa kuwa ni

fikra za kibinaadamu zinapatia na kukosea. Ama Sunnah hakosei (Mtume)

kamwe, ikiwa (ni Hadiyth) sahihi hakosei - yeye kalindwa na madhambi.

Chanzo: http://www.youtube.com/watch?v=0PyVOzLVFSM

Page 23: Fataawa Za Wanachuoni (13)

23

28. Wanachuoni Wa Hedhi Na Nifasi

Swali:

Tunaomba uwanasihi baadhi ya wanafunzi au vijana wanaowafedhehesha

baadhi ya wanachuoni kwa kukusudia au bila ya kukusudia. Wanapoambiwa

kurejea kwa wanachuoni wakati wa fitina na mfarakano wanasema hawa

wanachuoni ni wanachuoni wa hedhi na nifasi. Hata mimi nilisikia hivyo

Shaykh. Tunaomba nasaha huenda ikaleta manufaa.

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

Ni wajibu kwa mtu kumcha Allaah (´Azza wa Jalla) na asimdharau mtu

mwengine.

�3 ا��ذ�ن آ)�وا � � 6ر :وم ن :وم � � أن �(و�وا �� أ�" 3�م )� 6�را )�

”Enyi mlioamini! Wanaume wasiwadharau wanaume wenzao, huenda hao

wakawa bora kuliko wao.”(49:11)

Na mtu ahifadhi ulimi wake kwa kuwa ulimi ni kiungo hatari sana kwa mtu.

Kasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia Mu´aadh bin

Jabal:

"Je, nikueleze kitu kinachomiliki vyote hivyo? Akasema "ndio ewe Mtume wa

Allaah." Akaushika ulimi wake na kusema: "Uhifadhi huu [ulimi]" Akasema

"Ewe Mtume wa Allaah kwani tutachukuliwa kwa yale tuyasemayo?" Hivyo

akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): Akukose mama yako ewe

Mu´aadh! Je kipi kitachowafanya watu kutupwa Motoni kwa nyuso zao

isipokuwa ni kwa sababu ya ndimi zao.”

Na mwanachuoni mwenye ujuzi wa hedhi na nifasi ni mwanachuoni katika

mipaka ya Allaah na Shari´ah miongoni mwa Shari´ah za Allaah. Na hedhi na

Page 24: Fataawa Za Wanachuoni (13)

24

nifasi ni katika masuala magumu sana kwa wanafunzi kutokana na Ikhtilaaf

nyingi zilizomo humo. Na mwanachuoni kwa hilo ni mwanachuoni kigogo.

Mtu hasemi hilo kwa njia ya dharau. Hedhi na nifasi yanaingia humo mambo

mengi; kama ´Ibaadah, muda wa kusubiri, Talaka na mengineyo. Si jambo

sahali.

Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn

Tarehe: Liqaa' al-Baab al-Maftuuh (74 B)

http://www.youtube.com/watch?v=toPN9LCFwi4

29. Wale Wanaokaa Na Ahl-ul-Bid´ah Wamelaaniwa

Swali:

Je, imewekwa katika Shari´ah kwa Muislamu mwenye msimamo kukaa,

kuwapenda na kufurahi na wafanya maasi na wale wenye kutumbukia

kwenye Bid´ah zisizokuwa kufuru wakati hawatumbukia katika haya

madhambi? Au ni wajibu kuwasusa kwa hali zote isipokuwa tu kama

atawakataza atapokutana nao?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kuchanganyika na wafanya madhambi, washirikina, makafiri, wanafiki

linahitaji ufafanuzi. Ikiwa atachanganyika nao kwa ajili ya kuwalingania kwa

Allaah, kuwapa nasaha na kuwabainishia huku akitaraji huenda wakatubia na

kujirejea, hili limeamrishwa. Ni kulingania (Da´wah) kwa Allaah. Ama

kuchanganyika nao kwa ajili ya kuwa kijamii nao na kufurahi nao na

hawahukumu wala kuwakataza hili halijuzu. Hii ni njia ya Baniy ´Israaiyl

ambao wamelaaniwa na Allaah.

(��وا ��دون (?روا )ن ��& إ را<�ل ��� � �ن داوود و�� ��ن ا��ذ�ن (��وا � ا�ن )ر�م ذ�ك �)� 0�وا و��(ر '�وه ��<س )� (��وا �?�ون ����ھون �ن )"

Page 25: Fataawa Za Wanachuoni (13)

25

”Walilaaniwa waliokufuru miongoni mwa Wana wa Israili kwa ulimi wa

Dawuud na wa ´Iysa mwana wa Maryam. Hayo ni kwa sababu waliasi na

wakawa wanapindukia mipaka. Walikuwa hawakatazani maovu waliyokuwa

wakiyafanya. Hakika ni maovu yalioje mambo waliyokuwa wakiyafanya!”

(05:78-79)

Hii ndio sababu.

Mtu asiwe sawa na watu (kama hawa). Akiona maasi. Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam anasema):

"Yeyote yule atakayeona kitendo kiovu mwache akiondoe (abadilishe) kwa

mkono wake, ikiwa hawezi basi kwa ulimi wake (alikemee au kukataza), na

ikiwa hawezi basi kwa moyo wake. [Muslim]

Ukikikataza kwa moyo wako (yaani kuchukia) usikae nao. Jetenge nao mbali.

Na ukikaa nao, wewe hukuwakataza kwa moyo wako. Asli ni kwamba

hukumu ya kukaa na wafanya madhambi na wengineo wanaokwenda

kinyume, lina ufafanuzi. Yule mtu ambaye katika kuchanganyika nao kuna

maslahi ya kidini, kama kuwanasihi na kuwabainishia na kuwalingania kwa

Allaah - hili ni wajibu. Ama yule anayekaa nao, akala nao, akanywa nao na

akafurahi nao - huyu amelaaniwa kwa ulimi wa Dawuud na ´Iysa mwana wa

Maryam na Mtume Muhamad (Swalla Allahu ´alayhi wa sallam).

Kasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Naapa mtaamrishana mema na kukatazana mabaya, na mtamzuia mfanya

madhambi na kumfanya ashikamane na haki. La sivyo Allaah Atazifanya

nyoyo zenu kuambatana nyote halafu Awalaani kama alivyowalaani."

Ni lazima kuweka tanbihi ya kitu kimoja. Kuwalingania kwa Allaah (Da´wah)

wafanya madhambi, washirikina na makafiri ni lazima kuwa na elimu. Ama

kwa mjinga, haiwezekani akachanganyika nao. Kwa kuwa hana elimu ya

kuwabainishia na kuwanasihi. Au anaweza kuwalingania kwa Allaah kwa

ujinga, halitozidisha isipokuwa shari. Ni wajibu mtu awe na elimu kwa kiasi

ambacho anaweza kuamrisha, kuwakataza na kuwafanyia Da´wah kwa

Page 26: Fataawa Za Wanachuoni (13)

26

Allaah kwa Baswiyrah. Kumbukeni hili! Kwa yule asiyekuwa na elimu

asijiingize katika hili. Ajiweke mbali.

´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

Chanzo: http://alfawzan.ws/node/2033

http://www.youtube.com/watch?v=51_E7jpx4gY

Tarehe: 1430-08-17/2009-08-08

30. Neno "Jins-ul-´Amal" Limetoka Kwa Murji-ah

Swali:

Je, ni sahihi kauli: "Jins-ul-´Amal” ni lafdhi ya Bi´dah haikuwepo kwa Salaf; na

ni lafdhi ya utata yenye maana nyingi na ni bora kuiacha?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hatujui neno hili katika maneno ya ´Ulamaa wetu na ´Ulamaa wa Salaf. Sijui

tofauti ya Jins-ul-´Amal na kitendo. Inasemwa "Kitendo" na si "Jins-us-´Amal".

Kunasemwa "Kitendo." Kitendo ni katika Imani. Imani ni kauli kwa ulimi na

Itikadi katika moyo na vitendo vya mwili, na hawakusema "Jins-ul-´Amal."

Lafdhi hii haina asili na huenda imetoka kwa Murji-ah.

´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

Chanzo: http://alfawzan.ws/node/2033

http://www.youtube.com/watch?v=yZ90SMogswA

Tarehe: 1430-08-17/2009-08-08

31. Mwanamke Kwenye Nifasi Akitwaharika Kabla Ya Siku Arubaini

Page 27: Fataawa Za Wanachuoni (13)

27

Swali:

Je, damu baada ya (siku) arubaini kwa wenye nifasi huchukuliwa ni

Istihaadhah? Na vipi ikiwa atatwaharika kabla ya (siku) arubaini?

´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy:

Akitwaharika kamili (vizuri) mwanamke kabla ya siku arubaini, ni wajibu

kwake Swalah na Swawm kawaida kama wanawake wengine. Hata kama

itakuwa siku ishirini, hata chini ya hapo au zaidi huchukuliwa... wala

asiangalie siku arubaini. Na (damu) ikikatika siku arubaini na kutwaharika

(vizuri), na aghlabu huwa hivi kwa wanawake.

Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kasema nifasi siku arubaini,

kwa kuwa ndo huwa aghlabu kwa wanawake. Lakini anaweza kutwaharika

chini ya siku hizo, na damu inaweza kuendelea zaidi ya siku arubaini.

Ikiendelea kumtoka damu ndani ya siku arubaini, hukumu yake ni hukumu

ya wenye nifasi. Na ikiendelea zaidi ya siku arubaini, basi hiyo ni Istihaadhah

(damu ya ugonjwa). Na mwenye Istihaadhah hukumu yake ni kama hukumu

ya waliotwahara - ´Ibaadah n,k hatofautiani na waliotwahara katika

wanawake.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action

http://www.youtube.com/watch?v=lF3toS5rCtk

32. Mwanamke Anaetaka Kuzaa Kapitwa Na Swalah Nyingi, Afanye Nini?

Swali:

Page 28: Fataawa Za Wanachuoni (13)

28

Muulizaji kutoka Ubeljiji, mwanamke alikwenda kwa daktari kwa ajili ya

kujifungua saa kumi asubuhi, na hakujifungua ila saa tisa kabla ya ´Aswr na

hajaswali Dhuhr. Je, ana madhambi na vipi atalipa faradhi hizi?

´Allaamah Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy:

Ikiwa katika muda huu tangu alipoenda kwa daktari na kujifungua alikuwa

akitokwa na damu au na kitu aina ya damu, hana juu yake kitu wala hafai

kuswali. Na kama alikuwa twahara hakutokwa na kitu, ni wajibu kwake

kulipa Swalah zilizompita naye alikuwa twahara.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action

http://www.youtube.com/watch?v=GNir-FntYRY

33. Mishaary Raashiyd al-´Afaasy Na Anashiyd Zake

Swali:

Ipi rai yenu, tunataka kutoka kwa Mishaary Raashiyd al-´Afaasy (dalili sahihi

za kuimba Anashiyd) katika Swahiyh al-Bukhaariy?

Shaykh Mahir Qahtwaaniy:

Hizi ni katika Bid´ah zake maarufu kwake, anataka kutumia Hadiyth za katika

al-Bukhaariy kwa kuimba kwake. Bila shaka ni mtu wa Bid´ah mpotofu. Ni

wajibu kujiepusha na njia zake ambazo hawakuwahi kuafikiana nazo Salaf.

Chanzo: http://youtu.be/_T3RcEBU8UE

Page 29: Fataawa Za Wanachuoni (13)

29

34. Kwa nini Mwanamke Hafai Kumuonesha Mwanamke Wa Kikafiri Nywele Zake?

Swali:

Ipi dalili ya uwajibu wa mwanamke kufunika nywele zake mbele ya

wanawake wa kikafiri?

´Allaama Zayd bin Muhammad al-Madkhaliy:

Dalili ni kuwa wanawake wa kikafiri mara nyingi wanafanya khiyana katika

amaanah. Huenda akaenda kusifia umbile la huyu mwanamke Muislamu

kwa mtu ajinabi, ikapelekea katika madhara. Ama kwa yule ambaye atakuwa

na wanawake makafiri ambao ni waaminifu, hakuna ubaya akaonesha uso

wake - khaswa ikiwa kumetokea dharurah.

Chanzo: http://z-salafi.com/v2/action

35. Kipote Kitakachookoka Na Moto

Imaam Ibn ´Uthaymiyn:

"Kipote kitakachookolewa, Ahl-us-Sunnaah wal-Jamaa'ah, na wala

haitomfaidikisha mtu yeyote isipokuwa (kwa kufuata Manhaj/ufahamu) wa

Salafiyyah. Wale walioshikamana na njia ya Mtume wa Allaah (Swalla

Allaahu 'alayhi wa sallam) na Maswahabah zake."

Chanzo: http://youtu.be/qwkaa5CVljg

Page 30: Fataawa Za Wanachuoni (13)

30

Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu Muhammad, na ahli zake na

Maswahabah zake na watakaowafuata kwa wema mpaka siku ya Qiyaamah.