Page 1
al-Masa'ilu 'l-Islamiyyah(Sheria za Kiislamu)
Kwa Mujibu wa Fatwa za
Ayatullah al-Udhma
Sayyid Sadiq Husaini Shirazi
Mtarjumi:
Abdul Karim J. Nkusui
Kimechapishwa na:
Ahlul Bayt Centre (ABC)
S.L.P. - 7169, Arusha. Tanzania
na
Sayed Al-Shohada Charitable Committee
S.L.P. - 15338, Kuwait
Page 2
Haki ya kunakili imehifadhiwa na:
Sayed Al-Shohadaa Charitable Committee
Kimetafsiriwa na:
Ustadh Abdul-Karim Nkusui
Barua Pepe: [email protected]
Toleo la kwanza: Augasti, 2008
Nakala: 3000
Kimechapishwa na:
Ahlul Bayt Centre (ABC)
S.L.P. - 7169, Arusha. Tanzania
na
Sayed Al-Shohada Charitable Committee
S.L.P. - 15338, Kuwait
Simu: +965 255 2560
Nukushi: +965 963 5403
DA’IYYAH - KUWAIT
Page 3
YALIYOMO
Hukumu za Taqlid. “ Kufuata”.........................................................2
Hukumu za Tohara............................................................................6
Hukumu za Maji..............................................................................11
Hukumu za kujisaidia......................................................................13
Istibra...............................................................................................16
Adabu za kujisaidia.........................................................................17
Najisi...............................................................................................18
Njia za kuthibitisha Najisi...............................................................25
Namna ya kunajisika vitu vilivyo Tohara........................................26
Mas’ala............................................................................................28
Vinavyotoharisha.............................................................................30
Kupungua theluthi mbili za juisi ya zabibu mbivu.........................34
Hukumu za vyombo.........................................................................39
Kuosha mikono miwili....................................................................40
Kupaka kichwa................................................................................41
Kupaka miguu mwili.......................................................................41
Udhu wa Irtimasi “kuzamisha”........................................................42
Masharti ya udhu.............................................................................43
Hukumu za udhu..............................................................................45
Page 4
D
Al-Masailul Islamiyah
Mambo ambayo yanapasa udhu.....................................................47
Vinavyobatilisha udhu.....................................................................48
Hukumu za udhu wa Jabirah (Bandeji)...........................................48
Josho za wajibu................................................................................49
Hukumu za Janaba...........................................................................50
Mambo ambayo ni haramu kwa mwenye Janaba...........................51
Mambo yaliyo makuruhu kwa mwenye Janaba..............................52
Mas’ala katika kuoga Janaba.........................................................53
Josho la mpangilio...........................................................................53
Josho la kuzama...............................................................................55
Hukumu za kuoga............................................................................55
Istihadha........................................................................................ . 58
Hukumu za Istihadha...................................................................... 59
Hedhi...............................................................................................65
Hukumu za Hedhi........................................................................... 68
Vigawanyo vya Hedhi.....................................................................72
Wenye Ada ya wakati na Idadi....................................................... 73
Nifasi.............................................................................................. 84
Kuoga josho la kugusa maiti...........................................................86
Hukumu za muhtadhari “anayekata roho”.......................................88
Hukumu baada ya mauti................................................................. 89
Page 5
E
Al-Masailul Islamiyah
Hukumu za kuosha maiti.................................................................91
Hukumu za kumkafini maiti............................................................93
Hukumu za tahaniti “kupaka”..........................................................95
Hukumu za swala ya maiti...............................................................95
Namna ya kuswali swala ya maiti...................................................97
Yaliyo Sunna katika swala ya maiti................................................98
Hukumu za kuzika...........................................................................99
Tayamamu.....................................................................................105
Hukumu za swala...........................................................................110
Swala za wajibu.............................................................................111
Swala za wajibu za kila siku......................................................... 111
Wakati wa Swala ya Adhuhuri na Alasiri..................................... 112
Wakati wa Swala ya Magharibi na Isha....................................... 113
Wakati wa swala ya Asubuhi.........................................................113
Hukumu za wakati wa swala ....................................................... 115
Swala za Sunna..............................................................................119
Swala ya Usiku..............................................................................120
Swala ya Ghufaila......................................................................... 121
Hukumu za Kibla...........................................................................121
Kusitiri mwili katika Swala...........................................................122
Page 6
Masharti ya vazi la mwenye kuswali............................................123
Sharti la kwanza...........................................................................123
Sharti la pili..................................................................................124
Sharti la tatu..................................................................................125
Sharti la nne..................................................................................125
Sharti la tano.................................................................................126
Sharti la sita..................................................................................127
Sehemu ambazo hazilamu tohara ya mwaili wa mwenye kuswali.127
Yaliyosunna katika vazi la mwenye kuswali.................................129
Yaliyo makuruhu katika vazi la mwenye kuswali.........................129
Sehemu ya mwenye kuswalio.......................................................129
Shari la kwanza..............................................................................130
Sharti la pili...................................................................................130
Sharti la tatu...................................................................................131
Sharti la nne...................................................................................131
Sharti la tano..................................................................................131
Sharti la sita...................................................................................131
Sharti la saba..................................................................................131
Sharti la nene.................................................................................132
Sharti la tisa...................................................................................132
Hukumu za misikiti. .................................................................... 133
F
Page 7
Sharti la tano
Takbira ya kuhirimia swala.......................................................... 138
Sehemu Ambazo ni wajibu kukata Swala................................... 158
Shaka.............................................................................................157
Shaka zisizotiliwa maanani...........................................................160
Shaka ya kitu baada ya kupita sehemu yake.................................160
Shaka baada ya salamu..................................................................163
Mwingi wa shaka...........................................................................163
Shaka ya Imamu na Maamuma.....................................................163
Shaka zisizobatilisha swala........................................................... 167
Swala ya Ihtiyati............................................................................171
Sijida ya kusahau......................................................................... 172
Namna ya kuleta sijida ya kusahau.............................................. 174
Swala ya msafiri............................................................................176
Hukumu za makazi na kukaa siku kumi...................................... 183
Wajibu wa mtoto mkubwa kulipa swala zilizowapita wazazi waw-
ili....................................................................................................188
Swala ya Jamaa..............................................................................190
Hukumu za Jamaa......................................................................... 192
Sunna za swala ya Jamaa...............................................................193
Swala ya majanga..........................................................................197
G
Page 8
Swala ya majanga..........................................................................197
Swala ya Idd mbili “Al-fitri na Al-adhihaa”.................................200
Hukumu za Saumu.........................................................................202
Panyeto”Kuchezea utupu”.............................................................207
Kumzulia uongo Mwenyezi Mungu, Mtume (s.a.w.w) na Maimamu
(a.s)................................................................................................207
Kufika vumbi zito kwenye koo.................................................... 209
Kuzamisha kichwa kwenye maji...................................................210
Kubaki na Janaba au hedhi au Nifasi mpaka Alfajiri...................211
Hukumu ya vitenguzi.....................................................................216
Mambo ambayo ni wajibu kupa kadhaa na kutoa kafara...............217
Kafara za Saumu...........................................................................217
Mambo ambayo ni wajibu kulipa kadha ya saumu bila kafara......220
Hukumu za Saumu ya kadhaa....................................................... 222
Hukumu za Saumu ya msafiri........................................................224
Njia za kuthibiti mwanzo wa mwezi............................................226
Saumu ambazo ni Haramu na makuruhu ....................................277
Hukumu za Khumsi.......................................................................230
Hukumu za Zaka............................................................................231
Hukumu za Hija.............................................................................235
Umra Tamatui................................................................................238
H
Page 9
Umra ya Mufrad............................................................................245
Hukumu za ndoa........................................................................... 248
Hukumu za Talaka.........................................................................260
Hukumu za kuchinja mnyama na kumuwinda kwake.................. 265
Njia ya kisheria ya kuchinja..........................................................266
Masharti ya kuchinja ....................................................................267
Hukumu za kuwinda kwa silaha...................................................269
Hukumu za kula na kunywa..........................................................273
Mambo ya Sunna wakati wa kula.................................................274
Hukumu za miradhi.......................................................................277
Talaqin ya maiti.............................................................................283
I
Page 10
UTANGULIZI
Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema mwenye kurehe-
mu, rehema na amani zimwendee kipenzi chetu Mtume Muhammad
(saww) na Aali zake wema, ama baad.
Taasisi ya Sayed Shohadaa (as) kwa moyo mkunjufu na furaha
kubwa inawaletea wasomaji wa lugha ya Kiswahili na hususan
kuitajirisha maktaba ya Kiswahili kwa Muhtasari wa Sharia ya
Kiislam kwa mujibu wa fat’wa za Ayatollah Al - Udhmaa As Sayed
Swadiq Al-Hussein As Shirazi - Mwenyezi Mungu aidumishe kazi
yake.
Tarjama hii ilioko mikononi mwako ni matunda ya jitihada na juhu-
di kubwa za waalimu wa Madrasatul - Wahdah Singida ambao
wametumia muda wao mwingi ili kufanikisha kazi hii nzuri; Kwa
hawa na kwa kila aliyeshiriki kwa namna moja au nyingine katika
kufanikisha kazi hii tunatoa shukrani zetu za dhati na tunawaombea
kila la kheri kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu awalipe malipo mema.
Imamu Swadiq Shirazi ametumia lugha rahisi na nyepesi jambo
ambalo tunamatumaini kuwa litawasaidia wasomaji na kuwafanyia
sahali katika kufuatilia na kujua hukumu za mas’ala ambayo aghlabu
wanayahitajia katika maisha yao ya kila siku bila ya ugumu wowote.
Tarjama hii imetoa kipaumbele katika mas’ala ambayo ni muhimu
zaidi kwa waumini ili kuwarahisishia kujua Sharia ya dini yao husu-
san mas’ala ya Swala, saumu, ndoa, talaka, mirathi n.k. Ni matara-
jio yetu kuwa wasomaji wetu watakipokea kwa mikono miwili na
J
Al-Masailul Islamiyah
Page 11
watanufaika kwa kupata utatuzi wa mas’ala mengi mbali mbali kwa
njia nyepesi zaidi.
Tarjama hii haikuzingatia utaratibu wa namba za mas’ala kama
yalivyo katika kitabu cha asili bali mtiririko wa namba ni kulingana
na mas’ala yaliyochaguliwa, hivyo ukitaka kufuatilia lazima urejee
katika maudhui tajwa katika nakala ya asili ndio utajua namba ya
mas’ala husika. Nia yetu katika tarjama hii ni kutoa mas’ala ambayo
ni muhimu zaidi katika jamii pia hatukutaka kitabu kiwe ni kikubwa
sana.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu atie wepesi na baraka katika kazi
hii ili iwafikie waumini kwa haraka kwani Yeye ndio mwenye
kuombwa msaada na taufiq
Wasalaam
S.S.Magwe
Sayed Shohadaa Trust
4 Rabiul Akhir 1428AH - 22 April 2007
K
Al-Masailul Islamiyah
Page 12
L
DIBAJI
Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema
Mwenye kurehemu.
Shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe, rehema na
amani zimwendee kipenzi cha nyoyo zetu Mtume wetu Muhammad
(s.a.w.w.) na kizazi chake chema, masahaba wake na wote waliomfuata
kwa wema hadi Siku ya Kiyama.
SAYYED SHUHADAA CHARITABLE COMMITTEE ni taasisi ya
kidini inayojishughulisha na mambo ya waislamulimwenguni katika nyan-
ja mbalimbali za maisha yao ya kila siku. Pamoja na kujali sana mambo
ya waislamu pia inatoa kipaumbele katika suala la elimu kwa vijana wa
kiislamu na kuwaendeleza ili kuwajenga katika maadili mema ya kumtu-
mikia Mwenyezi Mungu na hatimaye wawe ni viongozi wazuri watakao-
hudumia jamii ya Kiislam na kuijenga kiroho, kimaadili na hatimaye
kuwawezesha kufikia lengo lao la kuwepo hapa dunia kwa wepesi.
Sambamba na hayo taasisi yetu pia inajishughulisha na mambo yafuatayo
katika jamii:-
- Ujenzi wa Miskiti
- Ujenzi wa Madrasa
- Kuwaangalia wazee wasiojiweza
- Kusaidia watoto yatima
- Kuwasaidia maskini
- Kutoa misaada ya kibinadamu wakati wa majanga
- Kukusanya na kugawa nudhur, kafara, chinjo katika mwezi wa Dhul-Hajj
na kutoa futari katika mwezi wa Ramadhani
- Kuendesha Majlis za Muharram na minasaba mbalimbali ya kidini kama
Page 13
M
vile kuadhimisha Maulidi na Wafayaat ( vifo na mazazi )
- Kuchapisha vitabu mbalimbali vya kidini kama vile Misahafu, Juzuu
Amma, vitabu vya fikra, dua n.k.
- Na kuendesha na kusimamia semina mbalimbali za kidini.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu atupe wepesi na atufanyie sahali katika
kufanikisha malengo yetu haya tuliyojiwekea, kwani Yeye ndiye
wakuombwa msaada
Wabillahi Tawfiq.
Page 16
2
Al-Masailul Islamiyah
HUKUMU ZA TAQLID
“KUFUATA”
1.Mas’ala: Niwajibu itikadi ya mwislamu katika Usul- Dini “misingi ya
dini” iwe ni kutokana na dalili na hoja, na wala haijuzu humo kufanya
taqlid, kwa maana ya kwamba mtu asikubali maneno ya yeyote bila ya
dalili. Lakini katika hukumu za kidini na matawi yake ni wajibu ama awe
ni mujitahid anayeweza kuchambua hukumu kutoka katika naswi “ Aya au
Hadith” na ama awe ni mwenye kufanya taqlid kwa maana ya kwamba
afanye amali kutokana na fat’wa za mujitahid ambaye ametimiza mashar-
ti na ama awe anafanya amali kwa njia ya kufanya ihtiyat “tahadhari” kwa
namna ambayo atapata yakini kwamba ametekeleza wajibu. Kwa mfano
kama jopo la mujitahid limetoa fat’wa kuharamisha jambo na jopo jingine
limetoa fat’wa ya uhalali wa jambo hilo basi anachukua tahadhari ya kuto-
lifanya jambo hilo au kama baadhi wametoa fat’wa ya wajibu wa kufanya
amali na wengine wakatoa fat’wa ya kuwa kwake sunna basi anachukua
tahadhari ya kufanya jambo hilo. Na ambaye sio mujitahidi wala hawezi
kufanya ihtiyat “tahadhari” ni wajibu kwake kumfuata Mujitahid na
kufanya amali kulingana na fat’wa zake.
2: Kufanya taqlid katika hukumu ni kufanya amali kwa mujibu wa fat’wa
ya mmoja wa Mujitahidina. Ni wajibu Mujitahidi awe ni mwanaume,
baleghe, mwenyeakili timamu, Shia Ithina Asharia, mtoto wa halali, awe
hai, huru na mwadilifu. Mwadilifu ni mtu anayefanya yaliyo wajibu na
kuacha yaliyoharamu kwa kiasi kwamba lau kama ukiulizia hali yake kwa
jirani yake au kwa wanayeishi naye au watu wa mahali anapofanyia kazi
basi wangekupa habari za wema wake, na kwa tahadhari mujitahid huyo
awe ni mjuzi zaidi katika zama zake katika kufahamu hukumu na
kuzichambua.kuliko mujtahid mwengine
Page 17
3
Al-Masailul Islamiyah
3: Mujitahid na mjuzi zaidi anafahamika kwa moja kati ya njia tatu:-
i – Mtu mwenyewe kupata yakini ya hilo, kwa yeye mwenyewe kuwa
ni kati ya wenye elimu na anaweza kumtambua mujitahid na mjuzi
zaidi kwa ujuzi wake.
ii - Wajuzi wawaili waadilifu kutoa taarifa juu ya hilo ambao
wanaweza kumtambua Mujitahid na mjuzi zaidi kwa sharti
wasipinge taarifa yao wajuzi wengine wawili.
iii Washuhudie hilo jopo la watu wenye elimu na ujuzi kati ya wanao
weza kumtambua Mujitahid na mjuzi zaidi na wanaoaminiwa, na
hukumu iliyo na nguvu zaidi ni kutosheleza taarifa ya mtu mmoja
ikiwa ni mkweli.
4. Ikiwa ni vigumu kumtambua mjuzi zaidi inalazimu kwa tahadhari ya
wajibu kumfuata anayedhaniwa kuwa yeye ni mjuzi zaidi, vivyo hivyo
atamfuata ambaye anadhana dhaifu juu ya kuwa kwake mjuzi zaidi na
anajua kutokuwepo kwa mjuzi zaidi mwingine asiyekuwa yeye kwa
tahadhari ya sunna, ama kama kundi litalingana katika ujuzi basi atam-
fuata mmoja kati yao, lakini ikiwa mmoja wao ni mchamungu zaidi basi
atamfuata yule mcamungu zaidi bila ya wengine kwa tahadhari ya
sunna.
5. Inawezekana kupata fat’wa na rai ya mujitahidi kwa moja kati ya njia
nne zifuatazo :-
Kusikia moja kwa moja kutoka kwa mujitahidi.
Kusikia kutoka kwa waadilifu wawili wakinukuu fat’wa ya Mujitahidi.
Kusikia kutoka kwa wanaoaminika na kutegemewa katika kunukuu kauli
yake.
Kupatikana fat’wa katika kitabu chake cha fat’wa, katika muundo unaole-
ta tumaini juu ya usahihi wa yaliyomo humo na usalama wake kutokana
Page 18
4
Al-Masailul Islamiyah
na makosa.
6. Maadamu mwenye kufanya taqlid hajapata yakini ya kubadilika fat’wa
ya Mujitahidi na rai yake inajuzu kwake kufanya amali kulingana na
yaliyomo ndani ya kitabu chake cha fat’wa lakini akidhania juu ya
kuwepo mabadiliko katika fat’wa yake sio wajibu kuchunguza
isipokuwa kama dhana inakubalika kiakili.
7. Mujitahid mjuzi zaidi akitoa fat’wa katika mas’ala haijuzu kwa anaye
mfuta kumfuata mujitahidi mwingine katika mas’ala hayo kwa tahadha-
ri ya wajibu, lakini kama hajatoa fat’wa bali amesema. “ Kwa tahadha-
ri afanye kadha.” Kwa mfano akisema: “ kwa tahadhari alete tasbihi nne
mara tatu” inalazimu kwa mwenye kuqalid kufanya kulingana na tahad-
hari hii au afanye kulingana na fat’wa ya mujitahid mwingine, ikiwa
mujitahidi mwingine amesema inatosha kuileta mara moja basi anawe-
za kuileta mara moja, na hukumu ni hiyo hiyo ikiwa Marjii anayemfua-
ta atasema. “Mas’ala haya ni mahala pa kutafakari au ni mahala pa
mushkeli.”
8. Mujitahidi akitoa tahadhari baada ya kutoa fat’wa katika mas’ala mfano
mtu akisema “Chombo kilichonajisika kinatoharika kwa maji ya kuru
“birika” mara moja ingawa ni bora kukiosha mara tatu” haijuzu kwa
anayemfuata mujtahid kumrejea mujitahidi mwingine katika mas’ala
hayo na hii inaitwa tahadhari ya sunna.
9. Haijuzu kumfuata mujitahid aliyekufa kwa anayeanza taqlid, ama akifa
mujitahid ambaye mtu anamfuata inajuzu kwake kubaki katika taqlid ya
mujitahid aliyekufa katika mas’ala yote ambayo mwenye kuqalid
hajayafanya wakati wa uhai wa mujitahid.
10. Mtu akifanya amali fulani kwa fat’wa ya mujitahid, kisha mwenye
kufanya taqlid katika mas’ala hayo kwa fat’wa ya mujitahid aliye hai
baada ya kufa marja wake wa kwanza haitajuzu kwake kubadili kuto-
ka katika fat’wa ya mujitahid aliye hai kwenda kwenye fat’wa ya mar-
Page 19
5
Al-Masailul Islamiyah
jaa wake wa awali aliyekufa katika mas’ala hayo. Vivyo hivyo ikiwa
mujitahid hakutoa fat’wa katika mas’ala hayo bali akatoa tahadhari na
mwenye kuqalid akafanya kulingana na tahadhari hiyo kwa muda hai-
juzu kwake kurejea katika fat’wa ya mujitahid aliyekufa.
11. Inajuzu kubadili taqlid kutoka kwa mujitahid aliyekufa kwenda kwa
mujitahid hai na wala haijuzu kubadili kutoka kwa mujitahid hai kwen-
da kwa mujitahid mwingine hai kwa tahadhari, isipokuwa ikiwa muji-
tahid wa pili ni mjuzi zaidi kuliko mujitahid wa kwanza au wa kwanza
akipoteza sifa ya uadilifu.
12. Ni wajibu kwa mukalafu “aliye baleghe na mwenyeakiili tiomamu”
kujifunza mas’ala ambayo aghlabu anayahitaji.
13. Yakitokea mas’ala ambayo mtu hajui hukumu yake ikiwa inawezeka-
na kusubiri ni wajibu wake kusubiri hadi apate fat’wa ya marjaa
anayemfuata na ikishindikana afanye kilicho wajibu kwake kwa
kuchukua tahadhari kama kuna uwezekano.
14. Kama mtu akinukuu fat’wa ya mujitahid kwa yeyote fat’wa ikibadili-
ka sio lazima kwake kumjulisha mabadiliko hayo, lakini akijua kuwa
alikosea katika kunukuu fat’wa ni lazima kumjulisha yale aliyoyanu-
kuu kwake kama kuna uwezekano.
15. Mukalafu akifanya amali kwa muda bila ya taqlid amali yake itasihi
ikiwa itaafikiana na fat’wa ya mujitahid ambaye ilikuwa ni wajibu
kwake kumfuata au ikiafikiana na fat’wa ya mujitahid ambaye imepa-
sa kumfuata, ingawa kwa tahadhari iafikiane na mujitahid anayetaka
kumfuata au akijua kwa njia nyingine kuwa amali zake zimeafikiana na
hali halisi na kwamba ametimiza wajibu wake.
16. Taqlid inahusu hukumu zote, katika ibada, mikataba, wajibu, haramu,
sunna, makuruhu na mubaha.
Page 20
6
Al-Masailul Islamiyah
HUKUMU ZA TOHARA
Maji halisi na mudhafu
17. Maji ama ni mutlaq ‘halisi’ na ama ni mudhafu. Mudhafu ni ambayo
yamekamuliwa kutoka kwenye kitu, mfano maji ya komamanga, maji
ya waridi au yaliyochanganywa na kitu mfano maji yaliyochanganywa
na udongo n.k kiasi kwamba hayaitwi maji tu, na halisi ni yasiyoku-
wa hayo, nayo yamegawanyika sehemu tano:-
maji ya “kuru” birika
maji machache
maji yanayotiririka
maji ya mvua
maji ya kisima
Maji ya birika
18. Kuru “birika” ni ambalo lina ujazo wa shibiri 3 upana, urefu na kina au
ambalo jumla ya ujazo wake ni shibiri 27.
19. Maji ya birika hayanajisiki kwa kukutana tu na damu au mkojo au kitu
chochote kilicho najisi au kilichonajisika mfano nguo iliyonajisika ila
yakibadilika na kuchukua rangi ya najisi au harufu yake au ladha yake
na hayanajisiki ikiwa hayajabadilika.
20. Maji ya birika hayanajisiki ikiwa yatabadilika bila ya kupatwa na
najisi.
21. Kilicho najisi mfano damu kikikutana na maji yanayozidi kuru na
baadhi ya rangi yake ikabadilika au harufu yake, ikiwa yaliyobakia ni
Page 21
7
Al-Masailul Islamiyah
machache kuliko kiwango cha kuru yote yatanajisika na ikiwa yaliy-
obakia ni kiwango cha kuru au zaidi ya kuru hayatanajisika yote bali
kiasi kilichobadilika tu.
22. Ikiwa maji ya bomba yameungana na birika maji yaliyonajisika yata-
toharika, lakini hayatohariki ikiwa yatadondokewa na matone tu, ila
kikiwekwa kitu kwenye bomba ili maji yake yaungane kabla hayajawa
matone na kuungana na maji yaliyonajisi, na kwa tahadhari ya sunna
yachanganyike maji ya bomba na maji yaliyonajisika.
23. Kama akiosha kitu najisi kwenye bomba la maji yaliyoungana na biri-
ka, maji yanayodondoka kutoka kitu kilicho najisi yatakuwa tohara
kama yataunganika na birika na hayajachukua rangi ya najisi au ladha
yake au harufu yake na ikiwa humo hakuna viini vya najisi.
24. Kama kitaganda kiasi cha maji ya birika na yaliyobaki yakawa sio
kiwango cha birika maji yaliyobaki yatanajisika kama yatakutana na
najisi, vivyo hivyo yatanajisika kila yatakapo yeyuka kutoka katika
barafu.
25. Maji ambayo yameshakuwa kuru ikitokea shaka kuwa yamepungua
kiasi cha kuru au laa basi hukumu yake ni kuru yaani ni tohara na
yanatoharisha na wala hayanajisiki kwa kukutana na najisi, na ambayo
yalikuwa sio kuru ikitokea shaka kuwa yamekuwa kuru au laa basi
hayatakuwa na hukumu ya kuru na kwa tahadhari ya lazima afanye
utafiti katika maudhui haya kisha aratibu atoe hukumu iliyotajwa
ikiwa hali halisi haitabainika.
26. Birika linathibitika kwa njia moja kati ya tatu:-
Mtu binafsi kupata yakini juu ya hilo
Watu wawili waadilifu watoe habari au mtu mmoja mkweli
Atoe habari ya hilo ambaye maji yako chini ya usimamizi wake kama vile
mwangalizi wa bafu akisema: Maji yaliyopo katika tanki la bafu ni birika
Page 22
8
Al-Masailul Islamiyah
Maji machache
27. Maji machache ni maji ambayo hayatiririki ardhini na wala hayafikii
kiasi cha birika.
28. Maji machache yakimwagwa kwenye kitu najisi au yakikutana na naji-
si yananajisika, lakini kama yatamwagiwa kutoka juu, juu ya kitu kili-
cho najisi au kwa mkupuo, kina najisika kiasi kilichokutana na najisi tu
na kinachobakia kitakuwa tohara.
29. Maji machache yakimwagiwa kwenye kitu kilicho najisi ili kuondoa
kiini cha najisi humo, kisha maji yakajitenga nacho maji yanayojiten-
ga yatakuwa najisi na inalazimu kwa tahadhari ya sunna ajiepushe na
maji ambayo yanamwagiwa juu ya kitu kilicho najisika baada ya kuon-
doka kiini cha najisi humo.
30. Maji yanayooshewa sehemu ya haja kubwa na ndogo yatakuwa tohara
na wala hakitonajisika kitu kinacho kutana nayo kama masharti mata-
no yatatimia pamoja na kuchukua tahadhari:-
Kama hayatachukua rangi ya najisi, harufu yake au ladha yake.
Ikiwa hayatapatwa na najisi nyingine.
Ikiwa hayatapatwa na chembechembe za kinyesi zinazoonekana.
Ikiwa mkojo au kinyesi hakijatoka pamoja na damu.
Ikiwa haja ndogo au kubwa haitavuka sehemu yake ya kawaida inayoju-
likana.
Maji yanayotiririka
31. Maji yanayotiririka ni ambayo yanatoka ardhini na yanatiririka kama
maji ya chemchem na mifereji.
32. Maji yanayotiririka hata kama ni machache ni kama kuru yakipatwa na
najisi yatakuwa tohara maadam hayajabadilika rangi yake au harufu
Page 23
9
Al-Masailul Islamiyah
yake au ladha yake kwa sababu ya najisi.
33. Najisi ikikutana na maji yanayotiririka kitanajisika kiasi cha maji kili-
chobadilika kwa sababu ya najisi tu, na ambayo yameunganika na
chemchem miongoni mwayo yatakuwa tohara hata kama ni machache
kuliko kuru. Ama maji mengine ya mto ikiwa yatakuwa katika kiwan-
go cha kuru au yakichanganyika na chemchem kwa njia ya maji
ambayo hayajabadilika yatakuwa tohara vinginevyo yatakuwa najisi.
34. Chemchem inayobubujika masika na inaacha kububujika wakati wa
kiangazi hukumu yake wakati inapotiririka ni hukumu ya maji yanay-
otiririka.
35. Maji ya chemchem ambayo hayatiririki lakini yanatoka kila yanapoc-
hotwa hukumu yake ni hukumu ya maji yanayotiririka, kwa maana
kwamba hayanajisiki kwa kukutana tu na kiini cha najisi maadamu
hayajabadilika rangi yake au ladha yake au harufu yake kwa sababu ya
najisi.
36. Maji yaliyotuama karibu na mto unaoungana nayo hukumu yake ni
hukumu ya maji yanayotiririka.
37. Maji ya hodhi za bafuni ikiwa yameungana na tanki basi ni kama maji
yanayotiririka katika hukumu, hata kama ni machache kuliko kuru,
kwa sharti tanki liwe na kiwango cha kuru.
38. Maji ya bomba ambayo yako katika bafu na majengo, ambayo yanami-
minika katika bomba na karo ikiwa yanaungana na kuru - kama vile
jokofu za maji ya kunywa- hukumu yake ni hukumu ya maji yanay-
otiririka.
39. Maji yanayotiririka juu ya ardhi lakini hayana chanzo toka ardhini
yakiwa chini ya kiwango cha kuru na yakakutana na najisi yatanajisi-
Page 24
10
Al-Masailul Islamiyah
ka, ama ikiwa yanatiririka toka juu kwenda chini au kwa mkupuo na
yakakutana na najisi chini maji yaliyo juu hayatanajisika.
Maji ya mvua
40. Maji ya mvua yakinyeshea kitu kilicho najisi ambacho hakina kiini cha
najisi, kitu kilichonyeshewa na mvua kitatoharika, matone ya mvua
hayatoshelezi bali iwe kwa kiasi kwamba inaitwa mvua na inatiririka
ardhini na kwa tahadhari ya sunna mvua iwe ni kwa kiasi inatiririka
katika ardhi ngumu.
41. Hailazimu kukamua nguo, godoro n.k , sawa sawa likioshwa kwa maji
ya mvua au mengineyo.
42. Mvua ikinyeshea kiini cha najisi na kikasambaa hadi sehemu nyingine
matone yatakuwa tohara ikiwa hayaambatani na chembechembe za
najisi, harufu yake, rangi yake, au ladha yake, mvua ikinyeshea damu
na kusambaa ikiwa katika cheche kuna chembechembe za damu, haru-
fu yake au ladha yake zitakuwa najisi.
43. Mvua ikinyeshea paa la nyumba au juu ya jengo na ikawa juu yake
kuna kiini cha najisi maji yanayotiririka chini ni tohara hata kama
yatakuwa yamepata kiini cha najisi maadam mvua inaendelea kunye-
sha. Ama baada ya kukatika akijua kuwa maji yanayotiririka kutoka
kwenye paa yamepatwa na najisi basi yatakuwa najisi.
44. Ardhi iliyonajisi inatoharika kwa kunyeshewa na mvua , ikiwa mvua
itanyeshea ardhi kisha maji yakapenya katika sehemu iliyo najisi chini
ya paa sehemu hiyo itatoharika.
45. Udongo ulionajisi ambao kwa kunyeshewa na mvua unakuwa tope
utakuwatohara.
46. Maji ya mvua yakikusanyika sehemu yakaosha kitu kilichonajisika
Page 25
11
Al-Masailul Islamiyah
wakati wa kunyesha mvua kitu hicho kinatoharika hata kama maji
yaliyokusanyika ni chini ya kuru, hii ni kwa sharti yasichukue rangi ya
najisi, harufu yake wala ladha yake.
47. Mvua ikinyeshea godoro tohara lililotandikwa juu ya ardhi iliyo najisi
na maji yakatiririka juu ya ardhi, ardhi najisi inatoharika na godoro hal-
itanajisika.
Maji ya kisima
48. Maji ya kisima yanayotoka ndani ya ardhi ni tohara hata kama ni
machache kuliko kuru maadam hayajabadilika rangi yake au harufu
yake au ladha yake kutokana na najisi, lakini ni sunna yanapokutana na
baadhi ya najisi yatolewe kiasi kilichotajwa katika vitabu vikubwa.
49. Najisi ikimwagiwa katika kisima ikabadili rangi yake au harufu yake
kama mabadiliko hayo yataondoka basi maji yakisima yatatoharika
ingawa kwa tahadhari ya sunna yachanganyike na maji mapya yanay-
otoka katika kisima.
50. Maji ya mvua au maji yoyote yakikusanyika katika shimo na yakawa
ni machache kuliko kuru yananajisika kwa kukutana na najisi.
HUKUMU ZA MAJI
51. Maji mudhafu(ambayo maana yake imeelezwa katika mas’ala 17) hay-
atoharishi kitu najisi na wala haisihi kutawadhia wala kuoga josho.
52. Maji mudhafu vyovyote yatavyokuwa mengi (lakini si kwa wingi wa
kisima cha mafuta) yananajisika kwa kukutana tu na najisi lakini kama
maji mudhafu yakikingwa kutoka juu, kwenye ya kitu najisi, yatana-
jisika yaliyokutana na najisi tu, bila ya kunajisika yaliyo juu, mfano
Page 26
12
Al-Masailul Islamiyah
kama maji ya waridi yakimwagwa kutoka kwenye birika juu ya mkono
ulio na najisi yananajisika yaliyofika kwenye mkono na ambayo haya-
jafika yatakuwa tohara, vivyo hivyo lau yakisukumwa kutoka chini
kwenda juu kwa msukumo wa bomba na yakakutana na yaliyo juu
yaliyonajisika sehemu ya chini haitonajisika.
53. Maji mudhafu yakichanganyika na maji ya kuru au maji yanayotiriri-
ka kiasi ambacho hayasemwi kuwa ni mudhafu yanatoharika.
54. Maji ambayo yalikuwa mutlaq na wala hayajulikani kama yamegeuka
na kuwa mudhafu au laa yatahukumiwa kuwa ni mutlaq kwa maana
kwamba yanatoharisha najisi na inafaa kutawadha na kuoga kwayo.
Ama ambayo yalikuwa mudhafu mwanzo na wala haijulikani kabla ya
hapo yalikuwa mutlaq au ni mudhafu hayatoharishi kilichonajisika, na
kutawadha na kuoga kwayo ni batili lakini yakiwa kwa kiwango cha
kuru au zaidi yakikutana na najisi hayahukumiwi kuwa ni najisi.
55. Maji ambayo hayajulikani kuwa ni mutlaq au mudhafu wala haijulikani
je hapo kabla yalikuwa mutlaq au mudhafu, hayatoharishi kitu kilicho
najisika, na kutawadha na kuoga kwayo ni batili, lakini yakiwa kwa
kiwango cha kuru au zaidi yake na yakakutana na najisi hayahukumi-
wi kuwa yamenajisika.
56. Maji ambayo yamekutana na najisi mfano mkojo na damu yakabadili-
ka rangi yake au harufu yake au ladha yake kwa sababu hiyo yatana-
jisika hata kama yanatiririka au yako katika kiwango cha kuru, lakini
yakibadilika rangi yake au harufu yake au ladha yake kwa sababu ya
ukaribu wake na najisi iliyo nje – kama ikiwa mzoga umetupwa karibu
ya maji hayo ukabadili harufu ya maji – dhahiri ni kutonajisika kwake
na wala si wajibu kufanya tahadhari ingawa ni bora kufanya hivyo.
57.Maji ambayo yamekutana na najisi mfano wa mkojo na damu rangi
yake ikibadilika au harufu yake au ladha yake kwa sababu ya hiyo najisi
Page 27
13
Al-Masailul Islamiyah
yananajisika japo yawe yanatiririka au kufikia kiwango cha kuru, laki-
ni endapo itabadilika rangi yake au harufu yake au ladha yake kwa ajili
ya ukaribu wake na najisi iliyo nje yake, kama vile utupwe mzoga
karibu na maji ukabadilisha harufu ya maji- kwa hukumu yenye nguvu
-hayanajisiki wala si lazima kufanya ihtiyati- tahadhari- japokuwa ni
bora.
58. Maji ambayo yameingia najisi mfano wa damu au mkojo ikabadilisha
harufu yake au ladha yake au rangi yake,yatatoharika yakikutana na
kuru au na maji yanayotiririka au yakinyeshewa na mvua moja kwa
moja au upepo ukipeperusha maji ya mvua na kuyaingiza humo au
maji ya mvua yametiririkia humo kutoka kwenye bomba la maji ya
mvua, hayo yote yatatimia kwa sharti ya kutoweka mabadiliko wake.
59. Mabaki ya maji yaliyonywewa na mbwa, nguruwe au kafiri ni najisi na
ni haramu kuyanywa, ama mabaki ya maji yaliyonywewa na mnyama
ambaye ni halali kuliwa ni tohara na sio makuruhu kuyanywa. Ama
mnyama aliye haramu kuliwa mabaki yake ni tohara ,lakini ni maku-
ruhu kuyanywa isipokuwa mabaki ya paka sio makuruhu kuyanywa.
60. Endapo kitu kilichonajisika kitaoshwa ndani ya kuru au maji yanay-
otiririka maji yanayoatuka kutoka kwenye kitu kilichooshwa yatakuwa
tohara.
HUKUMU ZA KWENDA HAJA
61. Ni wajibu- kwa mwanadamu- kustiri uchi wake - mbele ya kila aliye-
baleghe, wakati wa kujisaidia na mbele ya mtu mwingene hata kama
anayemuona ni mahram yake, kama vile dada yake, mama yake n.k.
Ni wajibu kustiri uchi mbele ya kichaa, mtoto mwenye kutambua zuri
na baya, lakini sio lazima kwa mke kusitiri uchi wake mbele ya mume
wake au kinyume chake.
62. Si wajibu kusitiri utupu kwa kitu makhsusi bali hata akiusitiri kwa
Page 28
14
Al-Masailul Islamiyah
mkono wake inatosha.
63. Ni wajibu asielekee kibla wala kukipa mgongo wakati wa kujisaidia,
yaani sehemu ya mbele ya mwili wake; tumbo lake, kifua chake na
magoti yake yasielekee kibla au kinyume chake.
64. Endapo mwenye kujisaidia ameelekea kibla au amekipa mgongo haito-
tosha kwa kupindisha utupu wake mbali na upande wa kibla katika
hali zote mbili. Na ikiwa hakuelekea kibla wala kukipa mgongo afanye
ihtiyati ya wajibu kutoielekeza tupu yake upande wa kibla au kinyume
chake.
65. Na kwa tahadhari ya sunna asielekee mwenye kujisaidia wala
asielekeze mgongo kibla wakati wa kufanya istibraa (ambayo maelezo
yake yatakuja katika mas’ala 73) na wakati wa kujitoharisha sehemu ya
mkojo na ya haja kubwa pia.
66. Akilazimika kuelekea kibla au kukipa mgongo ili asionekane kwa
asiyekuwa mahram yake hakuna ubaya kukielekea kibla au kukipa
mgongo ,vivyo hivyo hakuna ubaya akilazimika kukielekea kibla au
kukipa mgongo kwa ajili ya sababu nyingine.
67. Hailazimu kuchukua tahadhari ya kutomkalisha mtoto mchanga kwa
namna ambayo atakuwa ameelekea kibla isipokuwa uharamu wa hilo
uwe kwa upande mwingine, na kama mtoto mwenyewe akielekea
kibla au akakipa mgongo hailazimu kumkataza kwa hilo.
68. Ni haramu kujisaidia katika sehemu tano:-
Vichochoro visivyopitika kama wenyewe hawaruhusu hilo,
vivyo hivyo katika njia zinazopitika (zisizo fungwa) katika
hali ya dharura kwa mpita njia. Miliki ambayo hairuhusiwi
kujisaidia humo.
Sehemu zilizowaqfu kwa watu mahsusi mfano katika madrasa za kidini
Page 29
15
Al-Masailul Islamiyah
n.k. Juu ya kaburi la muumini kama hilo litamdhalilisha .Sehemu za hes-
hima ambazo haifai kujisaidia kutokana na heshima yake.
69. Sehemu ya haja kubwa haitohariki isipokuwa kwa maji katika hali tatu,
baadhi ya hizo ni kwa tahadhari:-
Kama itagusa sehemu ya haja kubwa najisi kutoka sehemu nyingine.
Kama itatoka pamoja na haja kubwa najisi nyingine kama vile damu.
Kama haja kubwa itavuka sehemu ya haja kubwa zaidi ya inavyojulikana.
Ama isiyokuwa katika hali zisizokuwa hizi inajuzu kutoharisha sehemu ya
haja kubwa kwa maji au tambara au mawe n.k, kama utakavyokuja ufafa-
nuzi wake ingawa kuosha kwa maji ni bora zaidi.
70. Sehemu ya haja ndogo haitohariki isipokuwa kwa maji na kama ikio-
shwa katika kuru au maji yanayotiririka mara moja baada ya kumalizi-
ka mkojo inatosha, lakini kwa maji machache inalazimu kuiosha mara
mbili na ni bora kuiosha mara tatu.
71. Inajuzu kutoharisha sehemu ya haja kubwa kwa mawe, changarawe na
mfano wake yakiwa makavu na tohara, na hakuna mushikeli ikiwa
yana unyevuvyevu kidogo kiasi kwamba hauhamii kwenye sehemu ya
haja kubwa, lakini ni wajibu afute kwa mawe yasiyopungua matatu na
asafishe sehemu ya haja kubwa mara moja au mara mbili.
72. Kwa tahadhari yasunna mawe yawe matatu au matambara ya kufutia
sehemu ya haja kubwa yawe matatu, jiwe kubwa lenye pembe tatu au
tambara refu moja linatosha, na kama najisi haitatoka kwa vipande
vitatu inamlazimu aongeze ambayo yatatosha kusafisha na kuondoa
najisi yote, na hakuna mushikeli katika kubakia chembechembe ndogo
sana zisizoonekana.
73 Haijuzu kufutia sehemu ya haja kubwa kwa vitu ambavyo ni wajibu
kuviheshimu, mfano karatasi ambayo ina jina la Mwenyezi Mungu,
manabii au mawasii (as) ,na kwa tahadhari ya sunna asifute kwa mifu-
Page 30
16
Al-Masailul Islamiyah
pa wala kwa vinyesi vya wanyama, kama ataondoa haja kubwa kwa
vitu hivi ataasi na kupata dhambi, lakini dhahiri ni kwamba sehemu ya
haja kubwa itatoharika.
74. Akipata shaka kuwa sehemu ya haja kubwa imetoharika au laa, ni waji-
bu atoharishe, ama ikiwa ni kawaida yake kutoharisha sehemu ya haja
ndogo au kubwa haraka,basi ni kwa tahadhari ya sunna atoharishe.
75. Akishuku baada ya swala kwamba alitoharisha sehemu ya haja kubwa
kabla ya swala au laa, swala yake aliyoswali itasihi, lakini inamlazimu
kutoharisha kwa ajili ya swala zinazofuata, na kama atashuku ndani ya
swala ni wajibu akate swala na kutoharisha, ama ikiwa ni ada yake
kutoharisha sehemu ya haja mara tu baada ya haja basi itakuwa ni
sunna kufanya tahadhari kwa kutoharisha, na wala hatakakata swala
kwa ajili ya tahadhari hii ya sunna.
ISTIBRAA
76. Istibraa ni kitendo cha sunna wanachokifanya wanaume baada ya
kumaliza haja ndogo ili kuwa na yakini ya kutobakia mkojo katika njia
yake, na ina viwango, vilivyo bora zaidi ni kutoharisha sehemu ya haja
kubwa kwanza kama atakwenda haja kubwa baada ya mkojo kukatika,
kisha anakamua kwa kidole cha mkono wake wa kushoto kuanzia kati-
ka njia ya haja kubwa hadi kwenye shina la dhakari mara tatu kwa
nguvu, kisha anaweka kidole gumba juu ya dhakari na kidole cha sha-
hada chini yake kisha anakamua kwa nguvu hadi kwenye kichwa cha
dhakari mara tatu.
77. Maji yanayotoka kwa mwanaume baada ya kumchezea mwanamke
yanayoitwa madhii ni tohara, vivyo hivyo maji yanayotoka baada ya
manii ambayo huitwa wadhii ni tohara, vilevile maji yatokayo aghlab
baada ya mkojo ambayo huitwa wadii ni tohara kama hayajapatwa na
Page 31
17
Al-Masailul Islamiyah
mkojo. Na mtu akifanya istibrai baada ya mkojo kisha akatokwa na
maji na akashuku kuwa ni mkojo au moja kati ya maji haya yaliyotaj-
wa basi yatakuwa tohara.
78. Mtu akishuku je, amefanya istibrai baada ya haja ndogo au laa, na aka-
tokwa na majimaji hajui ni najisi au ni tohara, hukumu yake ni najisi
na udhu wake unabatilika, lakini kama ni kawaida yake kufanya isti-
brai baada ya kukojoa. Au akishuku kuwa amefanya istibrai kwa njia
sahihi au laa, na yakatoka kwake maji maji hajui ni tohara au laa, yata-
kuwa tohara na udhu wake haubatiliki.
79. Ambaye hajafanya istibarai akiwa na yakini baada ya kupita muda
baada ya kukojoa kwamba hakuna mkojo katika njia ya mkojo, kisha
akaona maji maji na akashuku kuwa ni tohara au laa, yatakuwa tohara
na udhu wake hautabatiliki.
80. Kwa kuacha istibrai maji maji yanayoshukiwa kuwa ni mkojo yata-
hukumiwa kuwa ni najisi na yanatengua tohara, hata kama kuacha
kwake ni kwa dharura au kwa kughafilika.
81. Mwanamke hafanyi istibrai kutokana na mkojo, kama ataona maji maji
na akakushuku kuwa ni tohara au laa, basi yatakuwa tohara na udhu
wake au josho halitobatilika lake.
ADABU ZA KWENDA HAJA
82. Ni sunna wakati wa kujisaidia akae katika sehemu ambayo haonwi na
mtu yeyote, na atangulize mguu wa kushoto wakati wa kuingia choo-
ni, na atangulize mguu wa kulia wakati wa kutoka chooni.
83. Ni makuruhu kuelekea jua na mwezi wakati wa kujisaidia, lakini kara-
Page 32
18
Al-Masailul Islamiyah
ha hii hutoweka akifunika tupu yake kwa kitu, na vivyo hivyo ni
makuruhu katika hali ya kujisaidia kuuelekea upepo, na ni makuruhu
kujisaidia katika njia, vichochoro, mbele ya majumba, chini ya miti ya
matunda, kula wakati wa kujisaidia, kukaa muda mrefu chooni na
kujitoharisha mahali pa haja kubwa kwa mkono wa kulia na vile vile
kuongea katika hali ya kujisaidia, na hakuna mushkeli kumtaja Mungu
au kuongea kwa dharura.
84. Ni makuruhu kukojoa katika ardhi ngumu, katika mashimo ya wadu-
du na katika maji hususan ikiwa yametuama, vivyo hivyo ni makuru-
hu kukojoa kwa kusimama. Lakini si makuruhu kukojoa wima katika
sehemu ambazo zimewekwa marumaru na changarawe zake.
85. Ni makuruhu kubana mkojo au haja kubwa, bali ni haramu ikiwa kuba-
na huku kutadhuru mwili madhara makubwa.
86. Ni sunna mtu kujisaidia haja ndogo kabla ya swala kisha atawadhe, au
kuoga na kuswali, vivyo hivyo ni sunna kujisaidia haja ndogo kabla ya
kulala, kabla ya kujaamiiana na baada ya kutoka manii.
NAJISI
87. Najisi ni kumi na moja:-
1. mkojo 4. mzoga 7. nguruwe 10. Pombe za kisasa
2. kinyesi 5. damu 8. kafiri 11. jasho la mnyama anayekula vinyesi
3. manii 6. mbwa 9. pombe za kienyeji
1 na 2 :Mkojo na kinyesi
88. Mkojo na kinyesi cha binadamu na cha kila mnyama aliye haramu
kuliwa ni najisi, lakini mkojo na kinyesi cha mnyama aliye haramu
kuliwa ambaye damu yake haitoki kwa kasi wakati wa kuchinjwa ni
tohara. Na vivyo hivyo mfano wa mbu, nzi -wanyama- wasio na
Page 33
19
Al-Masailul Islamiyah
nyama. Ama mkojo na kinyesi cha mnyama aliye halali kuliwa ni toha-
ra.
89. Ni sunna kujiepusha na vinyesi vya ndege wasioliwa na hasa mkojo wa
popo na kinyesi chake.
90. Mkojo na kinyesi cha mnyama anayekula vinyesi ni najisi, vivyo hivyo
mkojo na kinyesi cha mnyama aliyeingiliwa na binadamu, vile vile
mkojo wa mnyama aliyenyonya kwa nguruwe na kunawiri kutokana na
maziwa yake.
3:Manii
91. Manii ya mwanadamu na ya mnyama anayetoka damu kwa kasi waka-
ti wa kuchinjwa ni najisi.
92. Maji ya aina tatu madhii, wadhii na wadii ni tohara.
4:Mzoga
93. Mzoga wa mnyama mwenye damu itokayo kwa kasi ni najisi, sawa
sawa amejifia mwenyewe au amechinjwa kwa njia isiyokuwa ya kisha-
ria. Samaki ambapo hana damu itokayo kwa kasi mzoga wake ni toha-
ra hata kama akifia kwenye maji.
94. Vitu visivyokuwa na uhai vinavyotokana na mnyama mfano sufi,
nywele, manyoya, mifupa na meno, vyote ni tohara isipokuwa vinavyo
tokana na mbwa na nguruwe.
95. Ikiwa sehemu ya mwili wa mwanadamu hai au mnyama hai mwenye
kutoka damu kwa kasi wakati wa kuchinjwa itajitenga, basi nyama au
kipande au kitu kingine chenye uhai ni najisi.
96. Magamba mepesi yanayojitokeza kwenye midomo au mahali pengine
Page 34
20
Al-Masailul Islamiyah
mwilini na ikiwa wakati wa kuanguka kwake umewadia, ni tohara japo
akiyang’oa - mtu - kwa hiyari, lakini ni bora kujiepusha kwa ihtiyati ya
sunna na magamba haya endapo yatang’olewa kabla ya wakati wa
kuanguka kwake.
97. Yai litokalo tumboni mwa kuku aliyekufa, endapo gamba lake la juu
litakuwa gumu ni tohara, lakini ni wajibu kulitoharisha kwa tahadha-
ri.
98. Kitoto kichanga cha kondoo au mbuzi kikifa kabla hakijala nyasi, kha-
mira (mazima aliyoyanyonya ambayo yako katika fuko la chakula)
iliyomo tumboni mwake ni tohara, lakini ni lazima kuitoharisha kwa
tahadhari.
99. Dawa ya mitishamba ya rojorojo, manukato, mafuta, rangi na sabuni
zinazoagizwa toka nchi zisizokuwa za kiislamu, hukumu yake ni toha-
ra maadamu tu mtu hajapata yakini ya unajisi wake.
100. Nyama, mafuta na ngozi zinazouzwa katika soko la waislamu ni toha-
ra, vivyo hivyo vilivyo katika miliki ya waislamu, lakini ikifahamika
kuwa mwislamu amevichukua kwa kafiri bila ya kuchunguza kuwa ni
kutoka kwa mnyama aliyechinjwa kisheria au laa, basi ni najisi.
5. Damu.
102. Damu ya binadamu na kila mnyama atokaye damu kwa kasi wakati
wa kuchinjwa ni najisi, na damu ya mnyama asiyetoka damu kwa kasi
wakati wa kuchinjwa mfano samaki, mbu au ambaye anashukiwa,
asiyejulikana kuwa anatoka damu kwa kasi wakati wa kuchinjwa au
laa, kama vile nyoka ni tohara.
103. Mnyama ambaye ni halali kuliwa akichinjwa kisharia na ikatoka
Page 35
21
Al-Masailul Islamiyah
damu inayotakiwa kutoka, damu iliyobakia ndani ni tohara na inaju-
zu kula nyama yake bila ya kuiosha kutokana na damu, isipokuwa
shingo yake inapasa kuiosha halafu iliwe, lakini ikiwa kiasi cha
damu kutoka nje kitarejea hadi ndani ya nyama kutokana na kupu-
mua, au kichwa cha mnyama kuwa juu wakati wa kuchinja, damu
hiyo itakuwa najisi, ni wajibu kufanya tahadhari kufanya tahadhari
kwa kujiepusha na damu iliyobakia ndani ya mnyama aliye haramu
kuliwa kama atachinjwa kisheria.
104. Damu chache ambayo inaonekana katika yai la kuku ikiwa ganda lake
jepesi la juu halijapasuka, ikiwezekana kuitoa damu hiyo bila ya
kuchanganyika na yai basi yai litakuwa tohara.
105. Damu chache ionekanayo wakati wa kukamua maziwa wakati mwin-
gine inanajisisha maziwa – kwa tahadhari -
106. Damu inayotoka baina ya meno ikichanganyikana na majimaji ya
kinywa na kwisha ni tohara, lakini kwa tahadhari ya sunna asiyame-
ze.
107. Damu ambayo inaganda chini ya ngozi kwa sababu ya pigo kali, kama
haitosemekana kuwa ni damu basi ni tohara, na ikisemekana kuwa ni
damu basi ni najisi, na katika hali hii ngozi ikichanika au ukucha uki-
toboka inalazimu kutoa damu iliyoganda kwa ajili ya udhu na josho,
kama kutolewa hakutakuwa na tabu, na kama kutasababisha adha
inalazimu kuosha pembezoni mwake kwa namna ambayo haitasaba-
bisha kunajisika, kisha aweke kitambaa au mfano wake kisha anapa-
ka juu ya kitambaa na anatayamamu vile vile kwa tahadhari.
108. Kama hawezi kutambua kuwa hii damu iliyo chini ya ngozi imegan-
da au ni nyama imekuwa katika hali hiyo kutokana na kupigwa basi
itakuwa tohara.
109. Bonge la damu likitumbukia katika chakula wakati kimechemka,
Page 36
22
Al-Masailul Islamiyah
katika chakula wakati kimechemka chakula chote kitanajisika na chombo
chake vile vile, na mchemko, joto au moto sio katika vitu vinavyotohari-
sha.
110. Maji ya njano yanayoonekana pembezoni mwa jeraha wakati wa
kukifungua kinapo pona, kama hatajua kuchanganyika kwake na
damu ni tohara, vivyo hivyo utando unaokuwa juu ya jeraha wakati
kinapopona na hufanya tabaka jeusi juu yake, hilo tabaka jeusi ni
tohara. kwa istihala « kubadilika.»
6 na 7 - Mbwa na nguruwe
111. Mbwa na nguruwe wa nchi kavu ni najisi hata nywele zao, mifupa yao
ma makucha yao na unyevunyevu wao. Lakini mbwa na nguruwe wa
majini ni tohara.
112. Wanyama wote walio haramu kuliwa ila mbwa na nguruwe inakuba-
lika kuchinjwa, kwa maana kuwa kama watachinjwa kisheria wataku-
wa tohara ingawa hawatakuwa halali kuliwa.
8- Kafiri
113. Kafiri ni najisi, naye ni ambaye anakanusha kuwepo kwa Mwenyezi
Mungu na anayemshirikisha au anaepinga utume wa Muhammad
(saww), vivyo hivyo kila anayekanusha wajibu katika wajibu wa dini,
mfano swala na saumu ambayo waislamu wanaizingatia kuwa ni
sehemu ya dini kwa sharti kuwa inalazimu kukanusha kwake huko
kumkanusha Nabii (saww), na awe anajua kuwa hii ni katika wajibu
wa dini, vinginevyo haitohukumiwa kuwa ni kafiri ingawa ni sunna
kufanya tahadhari kujiepusha naye. Na anayepinga siku ya kiyama na
madhambi makubwa, wajibu, nasibi, ghulati na khawariji wao wako
katika hukumu ya kafiri.
Page 37
23
Al-Masailul Islamiyah
114. Ahlul- kitab, kama vile manaswara, mayahudi na majusi kwa - tahad-
hari ya wajibu ni kujiepusha nao katika sehemu zisizokuwa za dharu-
ra na shida, hata kama hawajanajisika kwa kunywa pombe, kula mizo-
ga na nyama ya nguruwe au kutumia kwao najisi zingine.
115. Mwili wote wa kafiri hata nywele, kucha na unyevunyevu vyote ni
najisi.
116. Ikiwa mzazi wa mtoto asiyebaleghe, mama yake, babu yake, bibi
yake, wote wakiwa ni makafiri basi mtoto pia atakuwa najisi, au ikiwa
mmoja wa hawa ni mwislamu basi mtoto atakuwa tohara.
117. Asiyejulikana kuwa ni kafiri au mwislamu akiwa katika nchi ya kiis-
lamu basi ni tohara, na hukumu zote za Uislamu zitatekelezwa kwake,
inajuzu kuoa mwislamu na kuzikwa katika makaburi ya waislamu.
118. Yeyote katika waislamu akimtukana Nabii (saww), Fatma Zahra au
mmoja wa maimamu kumi na mbili au akiwafanyia uadui basi ataku-
wa ni najisi.
9 -Pombe
119. Pombe na kila kileo cha asili ya majimaji ni najisi hata kama ataki-
gandisha kwa njia yoyote ile, ama kikiwa hakina asili ya majimaji
mfano bangi na hashishi ni tohara hata kama kikitumbukizwa kitu
humo ili iwe maji maji.
120. Polishi inayotumika kwa kupaka na kung’arisha milango, viti, meza
n.k. kama haijathibitika kuwa ni kileo basi ni tohara.
121. Zabibu mbivu au maji ya zabibu mbivu ikichemka yenyewe, ni hara-
mu kuila au kuinywa ni, lakini ni tohara na wala haijuzu kuitumia
(kuila na kuinywa) ila ikiwa siki, vivyo hivyo inaharamishwa kuitu-
Page 38
24
Al-Masailul Islamiyah
mia ikiwa itachemshwa kwa njia ya kupikwa, na haijuzu kuitumia ila
baada ya kupungua theluthi mbili kwa kuichemsha kwa moto.
122. Tende, zabibu kavu na kishimishi na juisi zake, ni halali kama zita-
chemka zenyewe ingawa kwa tahadhari ya sunna hususani katika
zabibu na kishimishi ni kujiepusha kutumia.
10 - Bia.
123. Bia nacho ni kinywaji kinachotengenezwa kwa shairi ni najisi, lakini
maji yanayochukuliwa kutoka kwenye shairi kulingana na maelezo ya
daktari kwa ajili ya tiba na ambayo yanaitwa “maji ya shairi” vivyo
hivyo shairi inayopikwa katika mchuzi na shurbati ni tohara.
11 - Jasho la mnyama anayekula vinyesi
124. Kwa tahadhari ni wajibu kujiepusha na jasho la mnyama aliyezoea
kula vinyesi vya watu, na jasho la kila mnyama anayekula vinyesi vya
watu.
Jasho la janaba lililotokana na haramu
125. Jasho la janaba iliyotokana na haramu sio najisi ingawa ni bora
kuchukua tahadhari, ni sawasawa jasho limetoka wakati wa jimai au
baada yake, kwa mwanaume au kwa mwanamke, kwa zinaa au kwa
liwati, kwa kumwingilia mnyama au kwa kufanya punyeto. Na
punyeto ni mtu binafsi kukusudia kujitoa manii.
126. Mtu akimwingilia mke wake katika wakati ambao ni haramu kwake
kumwingilia, mfano akimwingilia wakati wa funga ya mwezi wa
Ramdhani au katika hedhi, kwa tahadhari ya sunna ajiepushe na jasho
lake.
Page 39
25
Al-Masailul Islamiyah
127. Mwenye janaba linalotokana na haramu akitayamamu badala ya
kuoga kutokana na udhuru, kisha akatoka jasho baada ya kutayama-
mu, inajuzu kwake kuswali pamoja na nalo, lakini udhuru wake ukii-
sha kisha akatoka jasho haifai kwake kuswali na jasho hilo na ni juu
yake kujiepusha nalo kwa tahadhari ya sunna hadi aoge.
128. Akipata janaba kwa njia ya haramu kisha akamwingilia mke wake
kwa njia ya halali, kisha akapata janaba kwa njia ya haramu, basi -
kwa tahadhari ya sunna - ajiepushe na jasho lake vile vile.
NJIA ZA KUTHIBITISHA NAJISI
129. Najisi inathibitika kwa moja ya njia tatu:-
Mtu binafsi kuwa na yakini kwa kunajisika kitu, akidhani kunajisika kitu,
hailazimu kwake kujiepusha nacho, hakuna mushkeli kula katika migaha-
wa na magenge ambayo watu wamezoea na wanakula humo ambao hawa-
jali tohara na najisi ikiwa hajapata yakini kuwa chakula anachopewa ni
najisi.
Mmiliki au mtumiaji wa chombo anapotoa taarifa juu ya unajisi wa kitu,
kama vile mke au mtumishi akisema chombo hiki au kitu hiki kilichopo
mkononi na chini ya uangalizi wake ni najisi, basi inamlazimu kujiepusha
nacho, na hii inaitwa habari ya mmiliki.
Kutoa taarifa watu wawili kwa unajisi wa kitu, vivyo hivyo akitoa taarifa
mtu mmoja mkweli kuhusu unajisi wa kitu inamlazimu kujiepusha nacho-
kwa ilivyo na nguvu zaidi.
130. Ikiwa hajui unajisi wa kitu au utohara wake kwa kutokujua kwake
mas’ala, mfano kutojua kuwa jasho la janaba ya haramu ni najisi au
ni tohara, ni wajibu wake aulize ili ajue hukumu, lakini akipata shaka
juu ya unajisi wa kitu au kutokuwa kwake najisi pamoja na kujua
kwake mas’ala, mfano akishuku kuwa hii ni damu au sio damu? Au
Page 40
26
Al-Masailul Islamiyah
akiwa hajui kuwa hii ni damu ya kiroboto au damu ya binadamu, basi
itakuwa tohara.
131. Kitu najisi ambacho anashaka kuwa kimekuwa tohara au laa kitabaki
kuwa ni najisi, na kitu tohara ambacho anashuku kuwa kimenajisika
au laa ni tohara, na kama anaweza kujua utohara wake au unajisi wake
haitomlazimu kuchunguza.
132. Akijua kuwa moja kati ya vyombo viwili au nguo mbili imenajisika,
na zote mbili alikuwa anazitumia na wala hajui ipi ndio imenajisika,
ni wajibu ajiepushe nazo zote, lakini ikiwa hajajua kwa mfano, kuwa
nguo yake ndio imenajisika au nguo ambayo haitumii kabisa na
ambayo ni nguo ya mwingine, haitomlazimu kujiepusha na nguo
yake.
NAMNA YA KUNAJISIKA VITU VILIVYO TOHA-
RA
133. Kitu najisi kikikutana na kitu tohara na vyote viwili au kimoja wapo
kina unyevunyevu kiasi kwamba unyevunyevu wa kimoja wapo una-
hamia kwa kingine, kitu tohara kinanajisika, ikiwa unyevunyevu ni
mdogo sana kiasi kwamba hausambai kwa kingine hakitonajisika.
134. Kitu tohara kikikutana na kitu najisi na akashuku je vyote au kimoja
wapo kilikuwa na unyevunyevu, kitu tohara hakitanajisika.
135. Kama kuna vitu viwili haijulikani kipi ni najisi na kipi ni tohara,
kimoja wapo kikigusa kitu tohara chenye unyevunyevu, kitu tohara
hakitanajisika, na kama kitu tohara kitagusa vyote viwili kitanajisika.
136. Ardhi, kitambaa na mfano wake kikiwa kimeloana inanajisika sehe-
Page 41
27
Al-Masailul Islamiyah
mu ambayo inagusana na najisi, na iliyobaki itakuwa tohara vivyo
hivyo tikiti maji, tango n.k.
137. Mafuta, jamu na mfano wake ikiwa kwa namna ambayo kama ita-
chukuliwa, kiasi nafasi iliyopo itajaa haraka basi itanajisika yote kwa
kukutana tu na najisi, na ikiwa nafasi iliyopatikana kwa kupunguza
haijai haraka basi hainajisiki kwa kupatwa na najisi, isipokuwa sehe-
mu iliyokutana na najisi hadi nafasi hiyo ijae baadae, hivyo kinyesi
cha panya kikidondokea katika hali hii ya pili itanajisika sehemu
iliyogusana na kinyesi tu na iliyobaki itakuwa tohara.
138. Nzi au anayefanana naye katika wadudu akitua juu ya kitu najisi che-
nye unyevu nyevu, kisha akaruka na kutua juu ya kitu kingine toha-
ra, chenye unyevunyevu kitu tohara kina najisika kama itajulikana
kuwa nzi ana chembechembe za viini vya najisi,vivyo hivyo akipata
yakini juu ya kugandamana najisi katika mguu wa mnyama kisha
akapata shaka kuwa imeondoka au laa, ama ikiwa hakujua basi ni
tohara.
139. Sehemu ya mwili ikinajisika na ikawa na jasho, kisha jasho najisi
likatiririka kwenda sehemu nyingine, sehemu iliyofikiwa itanajisika,
na ikiwa halitiririka hadi sehemu nyingine basi sehemu ya mwili
iliyobaki itakuwa tohara.
140. Kamasi na makohozi yanayotoka puani na mdomoni yakiwa na damu
sehemu iliyogusana na damu ni najisi na iliyobaki ni tohara, kikitoka
kitu nje ya pua au kinywa sehemu ambayo anajua kuwa imegusana na
sehemu iliyonajisika ni najisi, na sehemu ambayo anashuku katika
kukutana na sehemu iliyonajisika itakuwa tohara.
141. Birika ambalo ndani yake kuna maji na chini yake kuna tundu iki-
wekwa juu ya ardhi iliyonajisika, na maji yatokayo kwenye lile tundu
yanajikusanya chini yake kiasi cha kuzingatiwa kuwa maji yaliyo
Page 42
28
Al-Masailul Islamiyah
ndani ya birika na yale ya chini ni mamoja yaliyo ndani ya birika pia
yatakuwa yamenajisika. Na yakitiririka juu ya ardhi au yakipenya
humo, endapo tobo la birika likiwa limeungana na ardhi iliyonajisi
kiasi chakuwa inazuwia kububujika kwa majimaji ya ndani ya birika,
yatahukumiwa kuwa yamenajisika pia, lakini ikiwa tundu haikuunga-
na na ardhi iliyonajisika na wala hayahesabiki maji yaliyomo ndani ya
birika na yaliyo nje ni mamoja au maji yaliyo katika birika yakitoka
kwa nguvu na msukumo, yaliyo ndani ya birika hayatokuwa najisi.
142. Mtu akiingiza kitu mwilini na kikakutana na najisi, baada ya kukitoa
kikiwa hakikuchafuka na najisi, kitakuwa tohara. Akiingiza bomba
mahali pa kutokea haja kubwa au akidunga sindano au kisu na kitu
mfano wa viwili hivyo mwilini na baada ya kukitoa hakikuchafuka na
najisi hakitokuwa najsi, na vivyo hivyo mate au kamasi yakutanapo
na damu mdomoni na puani, kisha yakitoka bila ya kuchafuka na
damu yatakuwa tohara.
143. Kitu kilichonajisika kinanajisisha kama vile kiini cha najisi isipoku-
wa haitolazimu juu yake hukumu zake zote mfano kitu kikinajisika
kwa mkojo, inalazimu kurudiarudia kukitoharisha kama maji ni
machache na wala hailazimu kurudia rudia kwa kitu kilichokutana na
kitu kilichonajisika kwa mkojo.
MAS’ALA
144. Inaharamishwa kuitia najisi hati na maandishi ya Qur’an tukufu na ni
wajibu kuondoa najisi kwayo haraka pindi inaponajisika, lakini liki-
najisika jalada lake ni wajibu kulitoharisha ikiwa kuacha kwake kuna-
lazimu kuidharau, vivyo hivyo inaharamishwa kutia najisi (jalada
lake) na ni wajibu kutoharisha haraka msikiti, sehemu takatifu, turba
ya Imamu Hussein na hukumu ni hiyo hiyo katika turba ya Mtume
Page 43
29
Al-Masailul Islamiyah
Mtukufu na Maasumina wengine kwa tahadhari.
145. Ni haramu kuweka Qur’an juu ya najisi mfano damu, na mzoga hata
kama ni mkavu kama itahesabiwa kuwa ni kudharau Qaur’an na ni
wajibu kuiondoa katika vitu hivyo haraka.
146. Inaharamishwa kuiandika Qur’an kwa wino najisi hata kama ni heru-
fi moja na kama akiandika ni wajibu kuifuta kwa kifuto au mfano
wake.
147. Ni haramu kumpa kafiri Qur’an tukufu kama hiyo itasababisha kuid-
harau Qur’an na ni wajibu kuichukua Qur’an kutoka kwake.
148. Karatasi ya Qur’an tukufu au kitu kingine ambacho ni wajibu kuki-
heshimu kama vile karatasi ambayo imeandikwa jina la Mwenyezi
Mungu, Nabii, Imamu au Fatma Zahra likiangukia chooni ni wajibu
kulitoa na kulitoharisha hata kama hilo litalazimu kutoa gharama, na
kama haiwezekani kuitoa basi kwa tahadhari ya wajibu aache kukitu-
mia choo hicho hadi apate yakini ya kuyeyuka na kumalizika maan-
dishi ya karatasi hiyo, vivyo hivyo turba ya Imamu Huseini ikiangu-
kia chooni na ikashindikana kuitoa ni wajibu kuacha kujisaidia katika
choo hicho hadi turba iyeyuke na kumalizika.
149. Ni haramu kula na kunywa najisi au kilichonajisika kama vile maji
yaliyonajisika, vivyo hivyo inaharamishwa kumlisha mwingine hata
kama ni mtoto lakini mtoto mwenyewe akila najisi si wajibu kumzuia
ikiwa najisi hiyo haina madhara kwake.
150. Hakuna mushakeli kuuza au kuazima kitu kilichonajisika ambacho
inawezekana kukitoharisha ikiwa muuzaji au mwazimishaji atatoa
taarifa juu ya unajisi wake.
151. Mtu akiona mtu anakula najisi au anaswali na nguo najisi haimlazimu
kumwambia.
Page 44
30
Al-Masailul Islamiyah
152. Ikiwa sehemu ya godoro, mto au nyumba yake ni najisi na akaona
mgusano wa nguo za wanaoingia katika nyumba hiyo au miili yao au
kitu kingine na sehemu najisi nayo ikiwa na unyevunyevu ni lazima
kwake kuwaeleza kwa tahadhari ya wajibu ikiwa wamekuwa wageni
wake na wamekuja kwa wito wake.
153. Mwenye nyumba akijua wakati wa kula unajisi wa chakula ni wajibu
wake kuwaeleza wageni wake, ama akijua hilo mmoja wa wageni sio
lazima kwake kuwaeleza wengine.
VINAVYOTOHARISHA
154. Vinavyotoharisha vitu vilivyonajisika ni kumi na mbili:-
1. Maji 5. Kupungua theluthi mbili za juisi ya zabibu mbivu
2. Ardhi 6. Kuhama 8. Kuondoka kiini cha najisi
3. Jua 7. Uislamu 9. Kumtoharisha mnyama anayezoea
kula kinyesi
4. Kubadilika 10. Kufuata 11. Kutoweka kwa mwislamu
12. Kutoka damu kiwango kinachojulikana kwa mnyama.
MAJI
155. Maji yanatoharisha vitu kwa sharti nne:-
1- Yawe halisi
2- Yawe tohara
3- Yasiwe mudhafu wakati wa kutoharisha kitu kilicho najisika
4- Kusibaki baada ya kutoharisha kitu kilichonajisika kiini cha
najisi
156. Utoharishaji wa vitu vilivyonajisika kwa maji machache unasharti
zingine maelezo yake yatakuja baadae.
Page 45
31
Al-Masailul Islamiyah
157. Ni wajibu katika kutoharisha chombo kilichonajisika kioshwe kwa
maji machache mara tatu kwa tahadhari, na inatosha kukiosha mara
moja katika kuru au maji yanayotiririka lakini chombo kilicho lamb-
wa na mbwa au alichonywea humo ni wajibu kwanza kukisugua kwa
mchanga tohara kisha kukitoharisha katika kuru au maji yanayotiriri-
ka mara mbili ama chombo kilicho dondokewa na ute wa mbwa au
maji maji yake ni bora kukisugua kwa mchanga na kukiosha mara
tatu.
158. Ikiwa mdomo wa chombo ambacho mbwa amelamba ni mfinyu na
ikashindikana kusugua ndani ya chombo kwa udongo itamlazimu iki-
wezekana kuzungusha tambara kwenye kijiti na kusugua ndani ya
chombo kwa mchanga kwa njia hiyo hiyo ikishindikana anamwagia
mchanga katika chombo na kutikisa kwa nguvu hadi mchanga ufike
sehemu zote za ndani.
159. Chombo ambacho kimelambwa nguruwe au kunywa humo ni wajibu
kukiosha kwa maji machache mara saba na inatosha kukiosha katika
kuru au maji yanayotiririka mara moja na wala hailazimu kusugua
kwa mchanga ingawa ni bora kusugua kwa mchanga.
160. Ikitakiwa kusafisha chombo kilichonajisika kwa pombe kwa maji
machache inatosha mara tatu ingawa kwa tahadhari ni bora zaidi
kukiosha mara saba kwa maji machache.
161. Mitungi na vyombo vya urembo vilivyotengenezwa kwa udongo ulio-
najisika au ambavyo maji najisi yamepenya ndani yake vikiwekwa
kwenye kuru au maji yanayotiririka na maji yakaenea sehemu zote
vitakuwa vimetoharika na ikitakiwa kutoharishwa ndani yake pia
inalazimu vibakie katika kuru au maji yanayotiririka kwa muda ili
maji yaenee sehemu zote za ndani.
162. Chombo kilicho najisi inawezekana kukitoharisha kwa maji
Page 46
32
Al-Masailul Islamiyah
machache kwa njia mbili:-
1. Kwa kujaza chombo maji kisha anayamwaga mara tatu.
2. Au kuweka kiasi cha maji kisha anayazungusha humo kiasi cha
kufika sehemu zote zilizonajisika kisha anayamwaga na anaru-
dia mara tatu.
.
163. Kitu kikinajisika kwa mkojo wa mtoto mchanga ambaye hajaanza
kula chakula na hajanyonya maziwa ya nguruwe au kafiri, kikimwa-
giwa maji mara moja kiasi kwamba maji yanafika sehemu zote zili-
zonajisika kinatoharika lakini ni sunna kufanya tahadhari kwa
kumwgia maji mara mbili
2-Ardhi
164. Ardhi inatoharisha nyayo na viatu kwa sharti tatu :-
1. Ardhi iwe tohara
2. Iwe kavu
3. Kiini cha najisi kiondoke kama vile damu, mkojo au kilichonajisika
kama vile udongo ulionajisika ambao umegandamana katika sehemu za
nyayo au viatu kwa kutembea juu ya ardhi au kusugua juu yake kama
ambavyo inamlazimu katika kutoharisha kwa ardhi, ardhi iwe ni udon-
go au jiwe, vile vile sehemu ya chini ya nyayo au kiatu haitohariki kwa
kutembea juu ya godoro au jamvi, ama jiwe, changarawe, sementi iliyo-
tengenezwa kwa changarawe hukumu yake ni hukumu ya ardhi inato-
harisha.
165. Ni bora katika kutoharisha chini ya nyayo au viatu atembee juu ya
ardhi hatua kumi na tano au zaidi hata kama najisi itaondoka kwa
hatua chache kuliko hizo.
3 - Jua
166. Jua linatoharisha ardhi, majengo na mfano wake kama vile milango,
Page 47
33
Al-Masailul Islamiyah
madirisha ya majengo yakinajisika vivyo hivyo hutoharisha misumari
iliyopigiliwa ukutani na hiyo ni kwa masharti matano baadhi yake ni
kwa tahadhari:-
1. Kitu najisi kiwe na unyevuunyevu kiasi kikigusana na kitu unyevu
nyevu wake unahamia kwake, kikiwa kikavu inalazimu kukiloanisha ili
kikaushwe na jua.
2.Kiini cha najisi kiondoshwe kabla ya kupigwa jua.
3. Jua lisizuiliwe na kitu, kama jua litazuiliwa na pazia, mawingu n.k na
likakausha (kitu hicho) hakitohariki, lakini kama mawingu au pazia ni
jepesi sana kiasi halizuii jua hakuna mushkeli.
4. Jua peke yake likaushe kitu najisi, jua halitotoharisha kama litasaidiwa
na upepo katika kukausha lakini hakuna mushikeli ikiwa upepo ni
mdogo sana kiasi inasemwa kimekaushwa na jua.
5. Jua likaushe jengo ambalo najisi imepenya kwa mara moja yaani kwa
mchomozo mmoja, ama jua likipiga juu ya ardhi na jengo lililonajisika
na likikausha nje ya jengo na ardhi kisha likapiga mara ya pili na
likakausha ndani yake itatoharika nje tu na ndani patabaki kuwa najisi.
4. Kubadilika
167. Kitu najisi kikibadilika kiasi kwamba kinaonekana katika sura ya kitu
tohara kinakuwa tohara na hii inaitwa “kubadilika”ni sawa kubadili-
ka ni kwa kiini cha najisi au kitu kilichonajisika mfano ubao uliona-
jisi kubadilika na kuwa majivu au mbwa kuzikwa katika ardhi ya
chumvi na kugeuka chumvi lakini hakitohariki ikiwa uhakika wa kitu
haujabadilika mfano ngano kuwa unga au kutengenezwa mkate au
maziwa yaliyonajisi kutengenezwa jibini au mgando.
168. Pombe ikibadilika yenyewe na kuwa siki au kwa kubadilishwa mfano
kuweka siki au chumvi humo inakuwa tohara.
169. Siki iliyotengenezwa kwa zabibu mbivu, kishimishi au tende najisi ni
najisi kwa tahadhari ya wajib
Page 48
34
Al-Masailul Islamiyah
5 - Kupungua theluthi mbili za juisi ya zabibu mbivu
170. Maji ya za bibu mbivu hayanajisiki ikiwa yatachemshwa kwa moto
lakini ni haramu kuyanywa, na yakichemka na kupungua theluthi
mbili na ikabaki theluthi moja ni halali kuinywa, lakini ikichemka
yenyewe haiwi halali kuinywa isipokuwa ikigeuka siki.
171. Zikipungua theluthi mbili za juisi ya zabibu bila ya kuchemshwa
kama iliyobaki itachemka yenyewe au kwa moto ni haramu kuinywa
na ikitakiwa kuwa halali inalazimu kuchemshwa hadi ipungue the-
luthi mbili.
172. Punje ya zabibu ikitumbukia katika kitu kilichochemshwa kina-
chochemka kwa moto na punje ikichemka pamoja nacho sio wajibu
kujiepusha nacho.
173. Ikitakiwa kutengenezwa jamu katika viungu na masufuria tofauti
tofauti hakuna mushikeli katika kutumia mwiko katika chungu amba-
cho juisi yake imechemka katika viungu ambavyo havijachemka na
vikichemka vyote asitumie mwiko kwa sababu ya uharamu -katika
viungu ambavyo havijapungua theluthi mbili kwenye viungu
ambavyo vimepungua thelutghi mbili pamoja na kutobadilika,
vinginevyo hakuna mushkeli
6 - Kuhama
174. Inatoharika damu ya binadamu au mnyama anayetoka damu kwa kasi
wakati wa kuchinjwa ikihama kwenda katika mwili wa mnyama
asiyetoka damu kwa kasi na ikahesabika kuwa ni katika damu yake na
hii inaitwa “kuhama”, ama damu ambayo anainyonya luba kwa
mwanadamu ambapo haitwi damu ya luba bali damu ya binadamu
Page 49
35
Al-Masailul Islamiyah
inakuwa ni najisi.
175. Mtu akiua kunguni kwenye mwili wake na hajui kuwa damu iliy-
otoka ya kunguni au ni ambayo ameinyonya kutoka kwake basi ni
tohara, vivyo hivyo akijua kuwa ni katika damu ya kunguni lakini
imeshakuwa ni sehemu ya mwili wake, ama ikiwa muda wa kuiny-
onya na kumuuwa kwake ni mchache sana kiasi kwamba inasemwa
kuwa hii damu ni damu ya binadamu au haijulikani kuwa ni damu ya
kunguni au damu ya binadamu itakuwa najisi kwa tahadhari.
7 - Uislamu
176. Kafiri akitamka shahada yaani akisema “Ash hadu an laa ilaaha ila
llah wa ash hadu anna Muhammadan rasulullah” anakuwa mwislam.
Mwili wake, mate yake, makamasi yake na jasho lake vinatoharika
baada ya kuslim. Lakini ikiwa kuna kiini cha najisi katika mwili
wake wakati wa kusilimu kwake itamlazimu kuondoa najisi na kuto-
harisha sehemu yake bali kiini cha najisi kikiondoka kabla ya kusil-
imu kwake kwa tahadhari ya sunna atoharishe sehemu iliyonajisika.
177. Kafiri akitamka shahada mbili na wala haijulikani kuwa uislamu
umeingia katika moyo wake au laa ni tohara lakini ikijulikani kuwa
uislam haujaingia moyoni ni najisi lakini mnafiki ambaye hajasilimu
kwa moyo lakini anatekeleza uislamu kivitendo ni tohara.
8. Kufuata
178. Kufuata: Ni kutoharika najisi kwa njia ya kutoharika kitu kilichona-
jisi kama vile kutoharika watoto kafiri wasiobaleghe kwa kusilimu
mmoja wa wazazi wawili au babu na bibi.
179. Pombe ikiwa siki chombo chake kinatoharika kwa kufuata kwake
hadi sehemu iliyofikia pombe vile vile kifuniko, kitambaa kina-
Page 50
36
Al-Masailul Islamiyah
chowekwa kwenye mdomo wa chombo kama kitalowana kwa unye-
vunyevu huo lakini sehemu ya nje ya chombo hicho ikilowana kwa
pombe hiyo- kwa tahadhari ya sunna- ni kujiepusha nacho baada ya
kugeuka siki.
180. Ubao au jiwe ambalo amelazwa juu yake maiti na nguo ambayo ina-
funika mwili wake na mkono unaomuosha vyote vinatoharika baada
ya kukamalizika josha.
181. Anayetoharisha kitu mkono wake unatoharika baada ya kutoharika
kitu hicho kilichonajisika.
182. Maji yanayobaki katika nguo au mfano wake baada ya kuitoharisha
kwa maji machache na baada ya kutengana na maji ya kuoshewa ni
tohara.
9. Kuondoka kiini cha najisi
183. Mwili wa mnyama unatoharika - na unajumuisha viungo vyote vya
mwili wa mnyama hadi mdomo kwa upande wa ndege- kwa kuondo-
ka najisi kwake ikitapakaa najisi mfano damu au kilichonajisika
mfano maji, kisha kiini cha najisi au kilichonajisika kikaondoka una-
toharika, vivyo hivyo inatoharika sehemu ya ndani ya mwanadamu
kama vile tumbo, ndani ya pua na kinywa kwa kuondoa kiini cha
najisi kwayo, damu ikitoka baina ya meno na ikamalizika katika maji
maji ya kinywa haitomlazimu kutoharisha ndani ya kinywa vivyo
hivyo meno ya bandia yakinajisika ingawa ni bora zaidi kuyatohar-
isha.
184. Vumbi au mchanga najisi ukiangukia kwenye nguo au godoro au
mfano wake kisha akakung’uta au kutikisa kwa namna ambayo vumbi
najisi inaondoka kwa (kufanya hivyo) itakuwa tohara.
10. Kumtoharisha mnyama anayekula vinyesi
Page 51
37
Al-Masailul Islamiyah
185.Mkojo na kinyesi cha mnyama - aliyezoea kula vinyesi vya binadamu
- ni najisi na ikitakiwa kumtoharisha ni lazima kumzuia mnyama huyo
kwa muda kutokana na kula vinyesi kiasi ambapo hatoitwa mnyama
anayekula vinyesi, na alishwe malisho tohara kwa muda huo.
186. Ngamia anazuiliwa siku arobaini, ng’ombe siku thelathini, kondoo na
mbuzi siku kumi, bata siku saba au siku tano na kuku ni siku tatu, na
mnyama atazuiwa kula najisi na alishwe chakula tohara katika muda
huu na lau ikithibiti anuani ya(mnyama mla kinyesi) baada ya muda
huu pia ni lazima azuiwiliwe kula najisi kwa muda mwingine ili asi-
itwe baada ya muda huo - mnyama anayekula kinyesi.
11. Kutoweka kwa mwislamu
187. Mwili wa mwislamu ukinajisika au nguo yake na kitu chake kingine
kama vile vyombo, godoro n.k. ambavyo viko katika milki yake kisha
akatoweka pamoja na vitu hivyo, vitu hivi vinahukumiwa kuwa ni
tohara kama yatatimia masharti sita baadhi yake ni kwa tahadhari:-
1. Mwislamu atapaswa aitakidi unajisi wa kitu hicho ambacho kimetia
najisi mwili wake au nguo yake n.k, ikiwa itagusa nguo yake au mwili
wake maji ya zabibu iliyochemka naye haitakidi kuwa ni najisi kisha
akatoweka basi kutoweka(kughibu) kwake hakutoharishi.
2. Mwislamu Ajue kufika najisi kwenye mwili wake au nguo yake au
kinacho shabihiana na hivyo.
3. Mwislamu aonekane baada ya kutoweka kwake anatumia vitu hivyo
katika amali ambazo zinatakiwa kuwa na tohara mfano kama anaswali
kwa nguo hiyo iliyonajisika.
4. Mwislamu mwenyewe kutambua kuwa tohra inatakiwa katika amali
Page 52
38
Al-Masailul Islamiyah
hiyo ikiwa hatambui ulazima wa tohara kwa vazi la mweye kusali na
akasali kwa nguo hiyo haiwezi kuzingatiwa kuwa nguo hiyo ni tohara
kwa sabau ya kutoweka kwake.
5. Mwislamu huyo achukue jukumu la kutoharisha kitu hicho, akipata
yakini kwamba hajakitoharisha kitu hicho hakitazingatiwa kuwa ni
tohara, ama ikiwa hakuna tofauti baina ya tohara na najisi kwa mtazamo
wa mwislamu huyo basi kukizingatia kuwa ni tohara wakati huo ni
mahali pa mushikeli.
6. Mwislamu huyo awe baleghe - kwa tahadhari.
12. KUTOKA DAMU KWA KIWANGO KINACHOJULIKANA
KWA MNYAMA
188. Mnyama aliyehalali kuliwa akichinjwa kwa njia ya kisharia na kuto-
ka kwake damu kwa kiwango cha kawaida kinachojulikana, damu
iliyobaki katika mwili wake itakuwa tohara.
MAS’ALA
189. Mtu binafsi kuwa na yakini kwamba kitu kilichokuwa najisi kime-
shatoharika au wakitoa taarifa ya hilo watu wawiliwaadilifu inahuku-
miwa kuwa ni tohara, vivyo hivyo kama atatoa taarifa aliyetoharisha
kitu kilichokuwa najisi kama atapata matumaini kwa kauli yake au
ikiwa ndio mmiliki.
190. Mwakilishi wa mtu katika kutoharisha nguo yake kama atasema nguo
hii imetoharika basi nguo hiyo itakuwa tohara.
191. Mwenye wasiwasi (mwingi) naye ni ambaye hapati yakini kwa uto-
hara wakati wa kutoharisha kitu najisi inajuzu kwake kutosheka na
dhana au afanye kama wanavyotoharisha watu wa kawaida kwa kitu
najisi.
Page 53
39
Al-Masailul Islamiyah
HUKUMU ZA VYOMBO
192. Chombo kilichotengenezwa kwa ngozi ya mbwa au nguruwe wa nchi
kavu au mfu ni najisi na inaharamishwa kulia na kunywea humo,
haifaikutawadhia wala kuogea na wala hakitumiki katika amali
ambayo tohara ni sharti humo bali kwa tahadhari ya sunna asitumie
ngozi ya mbwa au nguruwe au mfu hata kwa visivyokuwa vyombo.
193. Inaharamishwa kulia na kunywea katika vyombo vya dhahabu na
fedha na kwa tahadhari ya sunna ni kuacha kuvitumia kabisa hata
katika mapambo.
194. Chombo kilichopo katika milki ya asiyekuwa mwislamu ni tohara
maadamu mtu hajapata yakini ya unajisi wake.
195. Hakuna mushikeli kutumia vyombo vilivyochovywa dhahabu na
fedha.
UDHU
196. Yaliyo wajibu katika udhu ni: Nia, kuosha uso, kuosha mikono
miwili, kupaka maji utosini na juu ya miguu miwili.
KUOSHA USO
197. Ni wajibu kuosha uso kwa mapana na marefu kuanzia kwenye mao-
teo ya nywele hadi mwisho wa kidevu, na upana ni sehemu iliyozun-
gukwa na kidole gumba na kidole cha kati na kama hajaosha sehemu
katika kiasi hicho udhu wake utabatilika na ili apate yakini ya kufika
maji hadi kwenye kiasi hicho inamlazimu kuosha sehemu ya pembe-
zoni mwake vile vile.
Page 54
40
Al-Masailul Islamiyah
198. Kama uso wa mtu au kiganja chake ni kikubwa au kidogo kuliko
maumbile ya watu wa kawaida inamlazimu atazame kiwango wana-
choosha nyuso zao watu wa umbile la kawaida na mikono yao kisha
aoshe, hukumu ni hiyo hiyo ikiwa nywele za utosi wa kichwa chake
zimevuka mpaka wa kawaida na kuteremka hadi kwenye paji au
ikiwa hana nywele kwenye utosi wa kichwa chake ni wajibu kuosha
paji la uso kwa kiwango cha watu wenye maumbile ya kawaida.
199. Ni wajibu kuosha uso na mikono miwili kuanzia juu kwenda chini
kama akiosha kuanzia chini kwenda juu udhu wake utabatilika.
200. Akiloanisha kiganja chake na akapaka kwacho uso wake na mikono
yake na ikiwa kiwango cha maji maji ya kiganja ni kwa kiasi kwam-
ba maji yanatiririka kidogo usoni na mikononi wakati wa kupaka
kwake inatosha.
KUOSHA MIKONO MIWILI
201. Baada ya kuosha uso ni wajibu kuosha mkono wa kulia kisha mkono
wa kushoto kuanzia kwenye kiwiko hadi kwenye ncha za vidole.
202. Ili kuwa na yakini kuwa ameosha kiwiko aoshe juu yake kidogo.
203. Anayeosha viganja vyake hadi kwenye vifundo viwili kabla ya
kuosha uso ni wajibu wake aoshe mikono yake hadi kwenye ncha za
vidole, na akiosha mikono yake hadi kwenye vifundo viwili na wala
asioshe viganja viwili udhu wake unabatilika.
204. Muosho wa kwanza wa uso na mikono miwili ni wajibu na wa pili ni
sunna, wa tatu na kuendelea ni haramu, ama ni muosho upi ni wa
kwanza au wa pili au wa tatu hiyo inategemea nia ya mwenye
kutawadha, kama atamwagia maji mara kumi kwa nia ya muosho wa
Page 55
41
Al-Masailul Islamiyah
kwanza hakuna mushikeli na zote zinazingatiwa kuwa ni muosho wa
kwanza, na kama ataosha uso mara tatu kwa maana ya miosho mitatu
basi muosho wa tatu utakuwa haramu.
KUPAKA KICHWA
205. Baada ya kuosha uso na mikono miwili ni wajibu kupaka utosi wa
kichwa kwa unyevunyevu uliobaki kwenye kiganja, na kwa tahadhari
ya wajibu apake kwa kiganja cha kulia kuanzia juu kwenda chini.
206. Robo ya utosi wa kichwa inayoelekeana na uso ndio sehemu ya kupa-
ka, hivyo inatosha kupaka mahali na sehemu hiyo na kwa kiasi cho-
chote ingawa ni wajibu kupaka kiwango cha upana wa kidole, na kwa
tahadhari ya sunna urefu uwe kwa urefu wa kidole na upana uwe kwa
upana wa vidole vitatu vilioungana.
207. Sio wajibu kupaka ngozi ya kichwa bali inasihi kupaka juu ya nywele
za kichwa, lakini kama nywele za utosi wa kichwa chake ni ndefu
sana kiasi kwamba kama akizichana zitafika usoni au zinaangukia
sehemu ya pili kama za wanawake ni wajibu apake kwenye maoteo
ya nywele.
KUPAKA MIGUU MIWILI
208. Baada ya kupaka kichwa ni wajibu kupaka juu ya miguu miwili kwa
unyevunyevu ule ule wa udhu uliobakia katika viganja viwili kuanzia
kwenye ncha za nywele hadi kwenye kongo mbili, na kwa tahadhari
ya sunna ni kupaka hadi kwenye maungio ya mguu.
209. Kwa tahadhari ya sunna atangulize kupaka mguu wa kulia kabla ya
mguu wa kushoto vivyo hivyo apake mguu wa kulia kwa mkono wa
kulia na mguu wa kushoto kwa mkono wa kushoto.
Page 56
42
Al-Masailul Islamiyah
210. Katika kupaka kichwa na sehemu ya juu ya miguu miwili ni wajibu
kupitisha mikono juu ya sehemu hizi, kama ataweka kiganja chake
juu ya kichwa chake na miguu yake, kisha akavuta kichwa na miguu
badala ya kupitisha mikono yake udhu wake utabatilika.
211. Ni wajibu sehemu ya kupakwa iwe kavu, ikiwa itakuwa na unyevu
nyevu kiasi ambacho unyevu nyevu wake unaathiri, unyevunyevu wa
kiganja hiyo itakuwa kinyume na tahadhari ya wajibu, lakini hakuna
mushkeli ikiwa unyevunyevu ni kidogo sana kiasi kuwa
utapoonekana unyevu nyevu utasemwa kuwa ni unyevunyevu wa
kiganja.
212. Kama unyevu nyevu wa kiganja utakauka na usibaki wa kupa kwayo,
haijuzu kuchukua unyevunyevu kutoka nje bali ni wajibu kuchukua
katika sehemu za udhu na kupaka kwa unyevunyevu huo.
213. Kupaka juu ya soksi na khuf ni batili, lakini hakuna mushkeli kupaka
juu yake ikiwa ni kutokana na baridi kali au hofu kutokana na wezi na
wanyama wakali na hakuweza kuvua soksi zake, na ikiwa juu ya soksi
kuna najisi inamlazimu kuweka kitu tohara juu yake kisha apakae, na
kwa tahadhari ya wajibu atayamamu vile vile.
214. Kama juu ya miguu kuna najisi na wala hawezi kutoharisha kwa ajili
ya kupaka juu yake itamlazimu kutayamamu.
UDHU WA IRTIMASI “KUZAMISHA”
215. Udhu wa itrimasi: Ni mwenye kutawadha kuzamisha uso wake na
mikono yake kwenye maji na kuutoa kwa nia ya udhu, na akiweka nia
wakati wa kuzamisha uso wake na mikono yake katika maji na
akabakia na nia yake hadi wakati wa kuitoa kwenye maji na akaende-
lea na nia yake hadi wakati wa kuutoa katika maji udhu wake unasi-
hi, vivyo hivyo unasihi udhu wake kama atazamisha mkono wake wa
Page 57
43
Al-Masailul Islamiyah
kulia katika maji kwa nia ya udhu wa irtimasi na akaosha mkono wa
kushoto kwa nia ya udhu usio wa irtimasi.
216. Katika udhu wa irtmasi vile vile ni wajibu kuosha uso na mikono
kuanzia juu kwenda chini, anuie udhu wakati wa kuzamisha uso wake
na mikono yake katika maji, ni wajibu aingize uso wake kuanzia
kwenye paji la uso katika maji na mikono yake kuanzia kwenye
kiwiko, na anuie udhu wakati wa kutoa sehemu hizi kwenye maji, ni
wajibu atoe uso wake kuanzia upande wa paji na atoe mikono yake
kuanzia kwenye kiwiko.
217. Hakuna mushikeli kutawadha baadhi ya viungo vyake kwa irtmasi na
vingine kwa njia isiyokuwa ya irtimasi.
MASHARTI YA UDHU
218. Ili udhu usihi kuna masharti kumi na mbili:-
1. Maji ya udhu yawe tohara
2. Maji yawe halisi na sio mudhafu
3. Maji, chombo na sehemu anayotawadhia viwe mubaha “halali”
4. Chombo cha kutawadhia kisiwe cha dhahabu au fedha.
5. Viungo vya udhu viwe tohara wakati wa kuosha na kupaka
6. Wakati uwe unatosha kwa udhu na swala
7. Atawadhe kwa nia ya kujikurubisha, yaani kutekeleza amri ya
Mwenyezi Mungu mtukufu kama atatawadha kwa ajili ya kupa-
ta ubaridi au kwa nia nyingine udhu wake unabatilika.
219. Sio lazima kutamka nia ya udhu au kuipitisha katika moyo bali
inatosha kuwa mwangalifu wakati wa kutawadha kiasi kwamba lau
akiulizwa swali ghafla nini anachofanya angesema natawadha.
8. Achunge utaratibu katika vitendo vya udhu yaani aanze kwa
Page 58
44
Al-Masailul Islamiyah
kuosha uso, mkono wa kulia, mkono wa kushoto, kupaka kich-
wa, kisha kupaka miguu miwili kama hatafuata utaratibu huu
udhu wake utabatilika.
9. Afanye vitendo vya udhu kwa mfuatano.
220. Kama atatenganisha baadhi ya vitendo vya udhu kwa muda kiasi
ambacho atakapotaka kuosha au kupaka kiungo kinachofuata viungo
vilivyotangulia vitakuwa vimeshakauka udhu wake utabatilika.
221. Kama atafuatisha baina ya viungo vya udhu kimoja baada ya kingine
bila ya kuchelewesha lakini unyevunyevu wa viungo vilivyotangulia
ukakauka kwa sababu ya joto la mwili udhu wake utasihi.
10. Atawadhe mwenyewe yaani aoshe uso wake, mikono yake na
apake sehemu za kupaka bila ya msaada wa yeyote na mtu
akimtawadhisha au akimsaidia katika kufikisha maji kwenye
uso wake au mikono yake au akapaka kichwa chake au miguu
yake, udhu wake utabatilika.
222. Asiyeweza kutawadha mwenyewe ni wajibu amuweke mtu wa kum-
tawadhisha na kama akitaka ujira ampe akiweza, lakini mwenye kuta-
wadhishwa anuie nia ya udhu na apake kwa mikono yake sehemu za
kupaka, kama hawezi amuweke mtu atakayeshika mikono yake na
kupaka kwayo sehemu za kupaka, na kama hilo haliwezekani ni waji-
bu mwakilishi wake achukue unyevunyevu kutoka katika kiganja cha
mwenye kutawadhishwa na apake kwayo sehemu zake za kupaka.
11. Asiwe na kizuizi cha kutumia maji
12. Katika viungo vya udhu kusiwe na kizuizi cha kuzuia maji
kufika kwenye ngozi
Page 59
45
Al-Masailul Islamiyah
HUKUMU ZA UDHU
223. Ambaye anashuku sana katika vitendo vya udhu au sharti zake,
mfano utohara wa maji au uhalali wake au kwa ghasb(bila ya ridhaa
ya mwenyewe), ni wajibu asizingatie shaka yake.
224. Akishuku kuwa udhu wake umebatilika au laa, atahukumu kubaki
kwa udhu wake, lakini kama hajafanya istibrai baada ya haja ndogo
kisha akatawadha, na kisha akaona unyevunyevu baada ya udhu hajui
ni mkojo au kitu kingine, udhu wake utabatilika.
225. Anayeshuku kuwa ametawadha au laa, ni wajibu atawadhe.
226. Anayejua kuwa ametawadha kisha akapatwa na kinachobatilisha
udhu kama vile mkojo na wala hajui kipi kimetangulia, ikiwa ni kabla
ya swala ni wajibu atawadhe, na ikiwa ni ndani ya swala anaivunja na
kutawadha tena, na ikiwa ni baada ya swala , basi swala yake aliy-
oiswali itasihi, lakini atawadhe kwa swala zinazofuata.
227. Akishuku baada ya swala kuwa ametawadha kabla ya swala au laa,
swala yake aliyoisali itasihi, lakini ni wajibu atawadhe kwa swala
zinazofuata
228. Akishuku katikati ya swala kuwa ametawadha kabla ya kuingia
kwenye swala au laa, swala yake inabatilika na ni wajibu atawadhe
kisha aswali.
229. Akishuku baada ya swala kuwa udhu wake umebatilika kabla ya
swala au baada ya yake, swala yake aliyoswali itasihi.
230. Mwenye ugonjwa wa salasi (kutoka mkojo) au mabutun “asiyeweza
kuzuia haja kubwa” akitambua kuwa ugonjwa wake utampa fursa
mwanzo wa wakati wa swala hadi mwisho kwa kiasi cha kutosha
udhu na swala, ni wajibu aswali katika wakati huo, na kama fursa
Page 60
46
Al-Masailul Islamiyah
hiyo haitoshi isipokuwa kufanya vitendo vya swala ni wajibu kufanya
vitendo vya wajibu tu na kuacha ya sunna kama vile kunuti, adhana
na kukimu.
231. Kama maslusi au mabtun hapati fursa ya kiasi cha kutawadha na
kuswali, bali mkojo au haja kubwa inadondoka wakati wa swala mara
nyingi, kama sio vigumu kwake basi atawadhe kila mara, aweke
chombo cha maji karibu naye na atawadhe kila unapotoka mkojo au
haja kubwa na akamilishe swala, lakini kwa tahadhari ya sunna aswali
swala ya pili kwa udhu mmoja hata kama udhu wake utabatilika
katikati ya swala asijali.
232. Maslusi au mabtun ambaye hawezi kujizuia kama itamuwia vigumu
kutawadha kila mara ni lazima kwake aswali kila swala kwa udhu
mmoja.
233. Ni wajibu kwa ambaye ana maradhi ya kutokwa na upepo afanye
kama anavyofanya maslus au mabtun, vivyo hivyo kwa asiyeweza
kujizuia na usingizi.
234. Maslusi ambaye anadondokwa na mkojo mfululizo ni wajibu ajihi-
fadhi mkojo usiruke hadi kwenye sehemu zingine za mwili wake kwa
kuweka kifuko chenye pamba au vitu vingine, na kwa tahadhari ya
wajibu atoharishe kifuko ambacho kina najisi, vivyo hivyo sehemu ya
haja ndogo kabla ya kila swala ikiwa hakuna usumbufu, na vivyo
hivyo inalazimu kwa mabatun.
235. Sio wajibu kwa maslusi au mabtun kulipa swala ambazo ameziswali
katika maradhi yake baada ya kupona kama atakuwa ameziswali
kama inavyotakiwa, lakini akipona ndani ya wakati wa swala ni bora
airudie swala aliyoiswali katika wakati huo.
Page 61
47
Al-Masailul Islamiyah
MAMBO AMBAYO YANAPASA UDHU
236. Udhu ni wajibu kwa mambo matano:-
1. Swala za wajibu isipokuwa swala ya maiti
2. Sijida au tashahud iliyosahauliwa
3. Tawafu ya wajibu katika ka’aba tukufu
4. Akiweka nadhiri, kiapo au kumwahidi Mwenyezi Mungu kuwa
atatawadha
5. Akiweka nadhiri au akitaka kugusa, maandishi ya Qur’an kwa
mwili wake.
237. Sio wajibu kutawadha kwa ajili ya sijida ya kusahau isipokuwa
kutawadha katika sehemu hii ni jambo zuri.
238. Udhu ni wajibu ikiwa mtu atataka kutoharisha Qur’an iliyonajisika au
akitaka kuitoa chooni, lakini kama kuchelewa kuitoa itakuwa ni kuid-
harau Qur’an afanye upesi kuitoa bila ya udhu.
239. Ni haramu kugusa maandishi ya Qur’an kwa mwili bila ya udhu, na
kwa tahadhari ya wajibu asiguse kwa nywele zake isipokuwa zikiwa
ndefu, lakini hakuna mushikeli kugusa tarjama ya Qur’an ya lugha
yoyote.
240. Ni haramu kugusa jina la Mwenyezi Mungu kwa lugha yeyote bila ya
udhu, na kwa tahadhari ya wajibu asiguse jina la Nabii mtukufu na
Maimamu Masumini na Faatmah Zahra(a.s).
VINAVYOBATILISHA UDHU
241. Mambo yanayobatilisha udhu ni saba:-
1. Mkojo
Page 62
48
Al-Masailul Islamiyah
2. Kinyesi
3. Upepo unaotoka katika sehemu ya haja
kubwa
4. Usingizi unaoshinda usikivu na kuona kiasi kwamba sikio hali-
sikii wala jicho halioni
5. Kila kinachoondoa akili kama vile ulevi, kichaa au kuzimia.
6. Istihadha utakuja ufafanuzi wake
7. Kila kinachowajibisha kuoga kama vile janaba na kugusa maiti
kwa tahadhari.
HUKUMU ZA UDHU WA BANDEJI
Bandeji ni ile ambayo inafungiwa jeraha au sehemu iliyoumia.
242. Ikiwa katika sehemu za udhu kuna jeraha, kidonda au mvunjiko na
hakuna kitu juu yake, na maji hayamdhuru ni wajibu atawadhe kama
kawaida.
243. Ikiwa sehemu kati ya sehemu za udhu kuna jeraha, kidonda au mvun-
jiko, na ikawa wazi na ikawa kumwagia maji juu yake kunadhuru,
lakini hakumdhuru kupitisha mkono wenye unyevunyevu juu yake,
basi kwa tahadhari ya wajibu ni kupitisha mkono wenye unyevunye-
vu juu yake, na kama hiyo pia inadhuru, au jeraha ni najisi haiweze-
kani kutoharisha, itamlazimu kuosha sehemu inayozunguka jeraha
kuanzia juu hadi chini, na kwa tahadhari ya wajibu aweke kitambaa
tohara juu ya jeraha na kupaka juu yake kwa mkono wenye unyevu-
nyevu, na ikiwa haiwezekani kwake kutoharisha itamlazimu kuosha
pembezoni mwa jeraha kisha atayamamu kwa tahadhari ya sunna.
244. Kama juu ya jeraha, kidonda au mvunjiko kuna bandeji, kama kuna
uwezekano wa kufungua na kusafisha na maji hasidhuru, ni wajibu
Page 63
afungue na atawadhe kama kawaida, ni sawasawa bandeji iwe usoni,
mkononi, utosini au juu ya mguu.
245. Kama bandeji itafunika uso wote au mkono wote au mikono yote, ni
wajibu atawadhe udhu wa bandeji, na kwa tahadhari ya wajibu ataya-
mamu.
246. Kama bandeji imefunika viungo vyote vya udhu basi kwa tahadhari
ya wajibu atawadhe udhu wa bandeji na atayamamu vile vile.
247. Ikiwa katika viungo vya udhu hakuna jeraha, kidonda au mvunjiko,
lakini maji yanamdhuru ni wajibu atayamamu, na kwa tahadhari ata-
wadhe udhu wa bandeji.
248. Josho la bandeji ni kama udhu wa bendeji, lakini kwa tahadhari ya
wajibu aoge josho wa bandeji kwa utaratibu, hata kama anaweza
kuoga kwa kuzamia pamoja na masharti ambayo ni, tohara ya kiungo
na kutodhurika kwa maji, kama hayatapatikana masharti ya kuoga
kwa kuzamia basi aoge kwa utaratibu.
JOSHO ZA WAJIBU
249. Josho za wajibu ni saba:-
Kuoga josho la janaba
Kuoga josho la hedhi
Kuoga josho la nifasi
Kuoga josho la istihadha
Kuoga ikiwa umegusa maiti
Kuosha maiti.
Miogo ambayo inakuwa wajibu kwa sababu, kama vile nadhiri,ahadi n.k.
HUKUMU ZA JANABA
49
Al-Masailul Islamiyah
Page 64
249. Janaba inapatikana kwa njia mbili:-
Kujamiana.
Kutokwa na manii, sawasawa akiwa usingizini au akiwa macho, yawe
yametoka machache au mengi, kwa kutamani au bila ya kutamani, kwa
hiyari au bila hiyari.
250. Ikiwa mtu atatokwa na unyevunyevu na ikawa hajui kuwa ni manii
au mkojo, ikiwa umetoka kutokana na matamanio, kwa nguvu na
kulegea kwa mwili baada ya kutoka kwake, basi hukumu yake ni
hukumu ya manii, na kama alama hizi tatu hazitokuwepo zote au
baadhi, basi hayatakuwa na hukumu ya manii, lakini kwa mtu
ambaye ni mgonjwa sio lazima unyevu nyevu huo utoke kwa nguvu,
ukitoka kwa shahawa na mwili kulegea baada ya kutoka basi
yatakuwa ni manii hata kama hayatatoka kwa nguvu.
251. Mtu akiingiza uume kwa kiasi cha kichwa au zaidi, ni sawasawa
aliyeingiliwa awe Mwanamke au mwanamume “Allah atulinde na
haya” iwe kwa mbele au nyuma, awe amebalehe au laa, manii ya
toke au laa, basi wote wawili watapata janaba na ni wajibu waoge.
252. Ikiwa mtu atashuku kuwa ameingiza uume kwa kiasi cha kichwa au
laa, sio wajibu wake aoge.
253. Akiingilia Mnyama – Mwnyezi Mungu atulinde na hayo - na akatok-
wa na manii kuoga kunatosheleza, na kama hajatokwa na manii na
alikuwa na udhu kabla ya kumwingilia mnyama, pia inatosha kuoga
peke yake, na kama alikuwa hana udhu basi ni kwa tahadhari ya
wajibu aoge na kutawadha.
254. Kama manii yatatikisika katika sehemu yake na hayakutoka, kisha
akashuku kuwa je, manii yametoka au laa, sio wajibu wake kuoga.
50
Al-Masailul Islamiyah
Page 65
255. Mtu ambaye hawezi kuoga lakini anaweza kutayamamu, basi ina-
juzu kwake kumwingilia mke wake hata kama ni baada ya kuin-
gia wakati wa swala.
256. Kama mtu ataona manii katika nguo zake na anajua kuwa yameto-
ka kwake, kisha hajaoga, ni wajibu aoge, na ni wajibu alipe swala
ambazo ana yakini kuwa ameziswali baada ya kutokwa na hayo
manii na kabla ya kuoga. Lakini swala ambazo anadhani kuwa
ameziswali baada ya kutokwa na manii sio lazima kuzilipa.
MAMBO AMBAYO NI HARAMU
KWA MWENYE JANABA
257. Ni haramu kwa mwenye janaba mambo matano:-
Kugusa andiko la Qur’an tukufu au jina la Allah (swt) kwa mwili, na kwa
tahadhari ya wajibu asiguse majina ya Manabii, Maimamu waliotoharika
pia na Fatma Zahara (as).
Kuingia katika Msikiti Mtukufu wa Makka na msikiti wa Nabii (saww),
ni haramu hata kupita kwenye mlango na kutokea mlango mwingine.
Kusimama na kubakia ndani ya Msikiti mwingine, na vile vile katika
sehemu takatifu za Maimamu waliotoharika (as), lakini hakuna mushke-
li kupita mlangoni na kutokea mlango mwingine, na pia inajuzu kuingia
kwa ajili ya kuchukua kitu.
Kuingia msikitini kwa kusudi la kuweka kitu, bali ni haramu kwa tahad-
hari ya wajibu kuweka kitu ndani hata bila ya kuingia ndani.
51
Al-Masailul Islamiyah
Page 66
Kusoma aya ya sajida katika moja ya sura “a’zaim” tukufu, nazo ni sura
za Qur’ani ambazo zina sajida ya wajibu nazo ni:-
Suratus Sajdah nayo ni sura ya 32
Sura ya Fuswilat nayo ni sura ya 41
Sura ya Najim nayo ni sura ya 53
Sura ya Alaq nayo ni sura ya 96
258. Ni haramu kwa mwenye janaba kusoma aya ya Sajida, bali ni kwa
tahadhari ya sunna asisome hata herufi moja katika sura hizi nne.
MAMBO YALIYO MAKURUHU
KWA MWENYE JANABA
259. Ni makuruhu kwa mwenye janaba mambo tisa yafuatayo:-
Kunywa na kula, lakini akitawadha au akiosha mikono yake kabla ya
kula na kunywa hapatakuwa na karaha
Kusoma aya za Qur’ani zaidi ya aya saba zisizokuwa katika sura za
sajida
Kugusa kwa mwili pembezoni mwa Qur’ani; jalada lake na baina ya maan-
dishi yake
Kuweka Qur’an tukufu na kuibeba
Kulala, lakini hakuna karaha akitawadha, au akitayamamu badala ya kuoga
kama hana maji
Kupaka hina n.k
Kujipaka mafuta
Kufanya jimai baada ya kujiotea usingizini.
52
Al-Masailul Islamiyah
Page 67
MAS’ALA KATIKA KUOGA JOSHO LA JANABA
260.Kuoga josho la janaba ni sunna, na ni wajibu kwa ajili ya swala ya
wajibu n.k. Lakini sio lazima kuoga janaba kwa ajili ya swala ya maiti,
sajida ya kushukuru na sajida za Qur’an za wajibu, lakini ni bora kwa
tahadhari ya sunna kuoga kwa ajili ya swala ya maiti.
261. Sio lazima wakati wa kuoga kunuwia wajibu au sunna, inatosha
kunuwia kujikurubisha kwa Allah (swt) na kutekeleza amri yake.
262. Akiwa na yakini kuwa wakati wa swala umeingia na akanuwia kuoga
josho la wajibu, kisha ikambainikia kuwa ameoga kabla ya wakati
basi kuoga kwake kutasihi.
263. Josho la wajibu au sunna linagawanyika sehemu mbili:-
- Josho la mpangilio
- Josho la kujizamisha.
JOSHO LA MPANGILIO
264. Katika josho la mpangilio ni wajibu kuanza kichwa na shingo kwan-
za, kisha upande wa kulia kisha upande wa kushoto kwa nia ya kuoga,
na kama mwili wote uko ndani ya maji au chini ya bomba, atanuwia
kuoga kwa kuanza na kichwa na shingo kisha upande wa kulia kisha
upande wa kushoto. Kama atafanya kinyume na utaratibu huu kwa
makusudi au kutokujua mas’ala, basi kwa tahadhari ya wajibu josho
lake litabatilika.
265.Unapoosha upande wa kulia ni wajibu kuosha nusu ya kitovu na nusu
ya sehemu ya siri na nusu nyingine unaiosha unapoosha upande wa
kushoto, na kwa tahadhari ya sunna kuosha kitovu na sehemu ya siri
53
Al-Masailul Islamiyah
Page 68
yote wakati unapoosha pande zote mbili.
266. Ili kupata uhakika kuwa umeosha sehemu zote tatu yaani kichwa,
shingo, upande wa kulia na upande wa kushoto, ni lazima kuzidisha
kila sehemu unapoosha. Bali kwa tahadhari ya sunna kuosha upande
wa kulia wote na upande wa kulia wa shingo na upande wa kushoto
wote pamoja na upande wa kushoto wa shingo.
267. Mtu akijua baada ya kuoga kuwa hajaosha sehemu katika mwili na
hajui ni wapi, basi lazima aoge kwa mara nyingine kwa tahadhari ya
wajibu.
268. Kama mtu akijua baada ya kuoga kuwa hajaosha sehemu katika
mwili, kama sehemu hiyo ipo upande wa kushoto inatosha aoshe
upande wa kushoto tu, na ikiwa itakuwa upande wa kulia ni kwa
tahadhari ya sunna baada ya kuiosha hiyo sehemu, aoshe upande wa
kushoto kwa mara nyingine, na kama itakuwa kichwani au shingoni
ni lazima aoshe hiyo sehemu, kisha upande wa kulia, kisha upande wa
kushoto kwa mara nyingine.
269. Kama atashuku kabla ya kumaliza kuosha upande wa kushoto
inatosheleza kuosha sehemu anayoishuku, lakini akishuku kuwa
hajaosha sehemu katika upande wa kulia basi ni kwa tahadhari ya
sunna kuosha sehemu aliyoishuku kisha aoshe upande wa kushoto
kwa mara nyingine, na akishuku kuwa hajaosha sehemu ya kichwa na
shingo, basi ni kwa tahadhari ya sunna baada ya kumaliza kuosha
hiyo sehemu, aoshe upande wa kulia kisha upande wa kushoto.
JOSHO LA KUZAMA
270. Katika josho la kuzamia ni wajibu maji yaenee mwili mzima kwa
mara moja, kama atazama katika maji kwa nia ya kuoga josho la
kuzama ni wajibu anyanyue miguu yake juu ya ardhi.
54
Al-Masailul Islamiyah
Page 69
271. Katika josho la kuzamia sio lazima wakati wa nia baadhi ya mwili
uwe nje ya maji, bali anaweza kunuwia na mwili wote ukiwa ndani ya
maji.
272. Kama akijua baada ya kuoga josho la kuzamia kuwa kuna baadhi ya
sehemu za mwili hazijafikiwa na maji, sawasawa amejua hizo sehe-
mu au laa, ni wajibu arudie kuoga.
273. Kama wakati hautomtosha kuoga josho la mpangilio, lakini unam-
tosha kuoga josho la kuzamia, ni lazima aoge kwa kuzama.
274. Mwenye kufunga saumu ya wajibu au akihirimia hija au umra, hai-
juzu kwake kuoga kwa kuzama katika hali ya saumu au ihramu. Lakini
akioga kwa kusahau kuoga kwake utasihi.
HUKUMU ZA JOSHO
275. Katika kuoga josho la kuzamia ni lazima mwili wote uwe tohara,
lakini katika joshoo la mpangilio sio lazima mwili wote uwe na
tohara, na kama mwili wote utakuwa na najisi kisha akatoharisha kila
sehemu kabla ya kuiosha inatosheleza.
276. Mtu akizini kama akitaka kuoga kwa maji ya moto, na mwili wake
ukatoa jasho ,basi sio lazima aoge kwa maji ya baridi, japo ni bora
aoge kwa maji ya baridi.
277. Katika kuoga janaba usipoosha hata unywele mmoja wa mwili josho
lake litabatilika, lakini sio wajibu kuosha sehemu ambazo
hazionekani mfano ndani ya sikio na pua.
278 Sehemu ambayo inashukiwa kuwa ni ya ndani au ya nje ya mwili ni
lazima ioshwe kwa tahadhari.
55
Al-Masailul Islamiyah
Page 70
279. Kama sikio lina shimo pana kwa kiasi kwamba kunaonekana ndani,
ni wajibu kuiosha na kama haionekani ndani sio lazima ioshwe.
280. Ni wajibu kuondoa kila uchafu unaozuia maji kufika mwilini, na
kama ataoga kabla ya kuhakikisha kuwa kuna kizuizi au laa, kisha
akabaini kuwa kizuizi hakijatoka, josho lake litabatilika.
281. Kama atashuku wakati wa kuoga, shaka inayokubalika kwa wenye
akili timamu, kuwa je kuna kizuizi kinachozuia maji kufika mwilini
au laa, basi ni wajibu afanye uchunguzi ili kuhakikisha kuwa hamna
kizuizi.
282. Katika kuoga ni lazima kuosha nywele ndogondogo ambazo zinah-
esabika kuwa ni sehemu ya mwili, na wala sio wajibu kuosha nywele
ndefu zaidi, bali ikiwezekana maji kufika mwilini bila ya kulowana
nywele josho litasihi. Lakini kama haitawezekana kufika maji mwili-
ni mpaka uoshe nywele ni wajibu kuziosha nywele ili maji yafike
mwilini.
283. Masharti yote ambayo yanafanya udhu usihi, mfano maji kuwa na
tohara na kuwa ya halali, vilevile masharti haya yanazingatiwa katika
kuoga, lakini sio lazima kuanza kuoga kuanzia juu mpaka chini,
vilevile sio lazima katika josho la mpangilio kuosha upande unaofua-
ta kwa haraka bila ya kuchelewesha,bali anaweza kuchelewesha
baada ya kuosha kichwa na shingo kisha baadaye aoshe upande wa
kulia na baada ya muda aoshe upande wa kushoto.
284. Anayeshindwa kuzuia mkojo au haja kubwa, kama maradhi yake
yatampa ahueni kidogo kwa kiwango cha kuoga na kuswali tu, basi ni
wajibu afanye haraka kuswali bila ya kuchelewesha, na vivyo hivyo
hukumu ni hii kwa mwanamke mwenye damu ya istihadha.
56
Al-Masailul Islamiyah
Page 71
285. Mtu akikusudia kutomlipa malipo mwenye bafu au akinuwia kutolipa
taslimu josho lake litabatilika.
286. Kama mwenye bafu anaridhia malipo ya kuoga yacheleweshwe, laki-
ni mwenye kuoga akanuwia kutolipa kabisa au atalipa lakini katika
mali ya haramu, josho lake litakuwa na mushkeli.
287. Kama mtu akitaka kulipa malipo ya mwenye bafu katika mali ya hara-
mu au ambayo haijatolewa khumsi, joshoo lake litabatilika isipokuwa
mwenye bafu akiridhia kutochukua chochote.
288. Kama akishuku kuwa ameoga au laa ni wajibu aoge, lakini akishuku
baada ya kuoga kuwa ameoga sawasawa au laa, sio lazima arudie
kuoga.
289. Kama atatokwa na mkojo wakati anaoga, basi atakamilisha kuoga
kisha atatawadha au ataacha na kuanza kuoga upya kwa nia ya wajibu
ulio juu yake na kutawadha pia.
290. Kama akioga kwa ajili ya swala kwa kudhania kuwa wakati unam-
tosha kuoga na kuswali, kama wakati utatosha kuswali rakaa moja au
zaidi ndani ya wakati swala yake inasihi.
291. Mwenye janaba akishuku kuwa ameoga au laa, swala zake alizoswali
zitakuwa sahihi, lakini aoge kwa ajili ya swala zingine.
292. Mwenye kuwajibika kuoga josho nyingi, inajuzu aoge josho moja
kwa nia ya josho zote, au aoge kila mmoja kwa nia yake.
293. Kama ataandika kwenye mwili wake aya ya Qur’an au jina la Allah
ni wajibu kufuta kama itawezekana, na ikishindikana ni lazima
atawadhe na kuoga josho la kuzamia, na kama atataka kutawadha na
kuoga josho la mpangilio ni lazima maji yafike mwilini bila ya mkono
wake kugusa sehemu iliyoandikwa katika mwili wake.
57
Al-Masailul Islamiyah
Page 72
294. Aliyeoga josho la janaba hatawadhi kwa ajili ya swala, ama josho
zingine za wajibu na sunna ni wajibu atawadhe kwa ajili ya swala,
kwa sababu josho hizi hazitoshelezi udhu, isipokuwa josho la wa jan-
aba tu.
ISTIHADHA
295. Damu ya istihadha ni moja ya damu ambazo zinatoka kwa
mwanamke, na mwanamke ambaye anatokwa na damu hii anaitwa
mustahadha.
296. Damu ya istihadha mara nyingi huwa ya njano, baridi, haichomi wala
haitoki kwa nguvu, inawezekana ikawa nyeusi au nyekundu ya moto
na nzito na inatoka kwa nguvu na kuchoma.
297. Istihadha inagawanyika sehemu tatu: Chache, wastani na nyingi.
Chache: Ni ambayo hailoanishi pamba anayoiweka mwanamke katika
uke.
Wastani: Ni ambayo inaloanisha na kupenya ndani ya pamba lakini
haitokezi nje ya kitambaa anachofungia pamba ili kuzuia damu isisambae
mwilini mwake.
Nyingi: Ni ambayo inapenya ndani ya pamba na kutokeza nje kwenye
kitambaa anachofungia pamba.
HUKUMU ZA ISTIHADHA
58
Al-Masailul Islamiyah
Page 73
298. Katika istihadha chache ni wajibu mwanamke atawadhe katika kila
swala, abadilishe pamba na kutoharisha nje ya uke kama damu
itakuwa imefika.
298. Katika istihadha ya wastani ni wajibu mwanamke aoge katika swala
ya asubuhi josho la istihadha, kisha abadilishe pamba na kutoharisha
nje ya uke kama damu itakuwa imefika, na kama hataoga katika swala
ya asubuhi kwa makusudi au kwa kusahau ni wajibu kwake aoge kati-
ka swala ya Adhuhuri na Alasiri na kama hataoga kwa ajili ya
Adhuhuri na Alasiri basi aoge kabla ya swala ya Magharibi na Isha,
sawa sawa damu iwe imekatika au laa.
299. Katika istihadha nyingi ni wajibu aoge katika swala ya Asubuhi,
Adhuhuri na Alasiri, Magharibi na Isha yaani josho tatu, kisha abadil-
ishe pamba na kutoharisha nje ya uke. Na kama atatenganisha baina
ya Magharibi na Isha ni wajibu aoge kwa ajili ya swala ya Isha.
300. Damu ya istihadha ikiendelea kutoka mpaka karibu na wakati wa
swala, na kama mwanamke bado hajaoga na kutawadha, basi ni lazi-
ma kwake aoge na kutawadha wakati wa swala.
301. Mwenye istihadha ya wastani na nyingi ambaye ni wajibu kwake
kutawadha na kuoga, kama atatanguliza kutawadha au kuoga inasihi.
302. Mwenye istihadha chache ikiwa ya wastani baada ya sala ya Asubuhi
ni wajibu aoge kwa ajili ya sala ya Adhuhuri na Alasiri, na istihadha
ya wastani ikiwa nyingi baada ya sala ya Adhuhuri na Alasiri ni
wajibu aoge kwa ajili ya sala ya Magharibi na Isha.
303. Mwenye istadha chache au ya wastani ikiwa itakuwa nyingi baada ya
swala ya Asubuhi ni wajibu aoge kwa ajili ya swala ya Adhuhuri na
Alasiri, na aoge kwa mara nyingine kwa ajili ya swala ya Magharibi
59
Al-Masailul Islamiyah
Page 74
na Isha.
304. Mwenye istihadha ya wastani au nyingi akioga kwa ajili ya swala ya
Asubuhi kabla ya kuingia wakati, josho lake litabatilika, lakini haku-
na tatizo kama ataoga kwa ajili ya swala ya usiku karibu na adhana
ya Alfajiri, na akaswali swala ya usiku, kisha wakati wa swala ya
Asubuhi ukaingia na akafanya haraka kuswali.
305. Mwanamke mwenye istihadha ni wajibu atawadhe katika kila swala,
iwe ya sunna au ya wajibu, na vile vile akitaka kurudia swala kwa
tahadhari au akitaka kurudia swala aliyoiswali furada kuiswali jamaa,
ni lazima afanye vitendo vyote anavyotakiwa kuvifanya mustadha.
Lakini sio lazima afanye vitendo anavyotakiwa kuvifanya mustadha
ikiwa anaswali rakaa ya Ihtiyati, sajda iliyosahauliwa, tashahudu
iliyosahauliwa na sajda ya kusahau, kama atavifanya hivi baada ya
swala bila kuchelewesha.
306. Ni lazima kwa mustahadha baada ya damu kukatika afanye vitendo
vya mustadha katika swala ya kwanza atakayotaka kuswali, baada ya
hapo sio lazima kuvifanya hivyo vitendo kwa ajili ya swala zingine.
307. Mustahadha kama hatambui yupo katika kundi gani ni lazima ajipime
ili ajijue yupo kundi gani, ataingiza pamba ukeni na kusubiri kidogo
kisha aitoe na baada ya kujua yuko kundi gani basi itakuwa ni isti-
hadha yake.
308.Mwenye istihadha akianza kusali bila ya kujua yupo kundi gani, kama
atakusudia kujikurubisha kwa Allah na akafanya vitendo vya mwenye
istadha chache sala yake itasihi, na kama hatakusudia kujikurubisha
kisha hajafanya wadhifa wake, akafanya wadhifa wa kundi lingine
mfano yeye ni wastani akafanya wadhifa wa chache sala yake itabati-
lika.
60
Al-Masailul Islamiyah
Page 75
309. Mwenye istihadha kama hawezi kujua yuko katika kundi gani, mfano
hajui kuwa yeye yuko katika chache au wastani, basi ni lazima afanye
wadhifa wa istihadha chache, na kama hajui kuwa yuko katika isti-
hadha ya wastani au nyingi basi ni lazima afanye wadhifa wa isti-
hadha ya wastani, lakini kama alikuwa anajua yuko katika kundi gani
kati ya haya matatu, basi itabidi awe katika hilo kundi la zamani.
310. Damu ya istihadha ikibakia tumboni haibatilishi josho wala udhu,
na ikitoka hata kama ni chache inabatilisha udhu na josho.
311. Mwanamke mwenye istihadha kama hataona damu inajuzu asali
haraka na udhu alionao.
312. Mwenye istihadha akijua kuwa damu haijatoka tangu alipoanza
kutawadha au kuoga, inajuzu kwake kuchelewesha sala mpaka
wakati atakapokuwa tohara.
313. Mwenye istihadha akijua kuwa atatoharika kabisa kabla ya kumal-
izika wakati wa swala, au itakatika kwa muda wa kuweza kuswali
basi ni kwa tahadhari ya wajibu asubiri mpaka huo wakati na
kuswali atakapotoharika.
314. Kama itaonekana dhahiri kuwa damu imekatika na baada ya udhu na
kuoga , na mustahadha akajua kuwa akichelewesha swala kwa muda
wa kuweza kutawadha na kuoga atatoharika kabisa, ni wajibu
acheleweshe swala na arudie kutawadha na kuoga baada ya kuto-
harika, kisha aswali, na kama wakati utakuwa mfinyu sio lazima
arudie kutawadha na kuoga kwa mara nyingne, bali inajuzu aswali
na udhu na josho lile ile.
315. Mwenye istihadha nyingi na ya wastani anapotoharika kabisa ni
wajibu aoge, lakini kama akijua kuwa damu haijatoka kabla hajao-
ga sio lazima arudie kuoga.
61
Al-Masailul Islamiyah
Page 76
316. Ni wajibu kwa mwenye istihadha chache baada ya udhu, na mwenye
istihadha nyingi na ya wastani baada ya kutawadha na kuoga wasali
bila ya kuchelewa, lakini hakuna tatizo kutoa adhana kukimu na
kusoma dua kabla ya swala, pia inajuzu kufanya mambo ya sunna
kama vile kunuti n.k.
317. Mwenye istihadha kama akichelewesha kusali baada ya kuoga, ni
lazima arudie kuoga na kusali bila ya kuchelewa.
318. Kama damu ya istihadha itaendelea kutoka bila ya kusimama, ni
lazima kwa tahadhari ya sunna kama hataogopa madhara kabla ya
kuoga na baada ya kuoga achukue pamba na kuingiza ukeni ili
kuzuia damu isitoke nje, lakini kama damu itakuwa haitiririki kila
wakati ni lazima baada ya udhu na kuoga azuie damu, na kama
atafanya uzembe kujihifadhi na akaacha damu inatoka ni lazima kwa
tahadhari ya sunna arudie kuoga na kutawadha na arudie swala kama
ameswali.
319. Kama damu haitakatika wakati wa kuoga, josho litasihi, lakini
mwenye istihahadha ya wastani akiwa mwenye istihahadha nyingi
wakati akioga, ni lazima aanze kuoga upya kwa tahadhari.
320. Kwa tahadhari ya sunna kwa mwenye istihahadha kuzuia damu isi-
toke mchana kutwa ambao atafunga saumu kwa kadiri atakavy-
oweza.
321. Mwenye istihahadha ambaye ni wajibu aoge, saumu yake itasihi
kama ataoga jinsi inavyotakiwa, mfano akioga kwa ajili ya swala
ya magharibi, kisha akaoga josho za mchana kwa ajili ya swala za
wajibu za siku hiyo. Lakini kama hataoga kwa ajili ya swala ya
magharibi na Isha na akaoga kwa ajili ya swala ya usiku kabla ya
adhana ya alfajir,i na akaoga josho za mchana kwa ajili ya swala
62
Al-Masailul Islamiyah
Page 77
zake, saumu yake itasihi na kama atakuwa mustahadha baada ya
swala ya alasiri na hajaoga saumu yake itasihi.
322. Mwenye istihadha chache ikiwa ya wastani au nyingi kabla ya swala,
ni lazima afanye wadhifa wa istihadha ya wastani au nyingi, na
kama istihadha ya wastani ikiwa nyingi lazima afanye wadhifa wa
istihadha nyingi, na kama alikuwa ameoga kwa ajili ya istihadha ya
wastani haitosadia, bali ni wajibu arudie kuoga kwa ajili ya istihad-
ha nyingi.
323. Kama istahadha ya wastani itakuwa nyingi katikati ya swala basi ni
kwa tahadhari ya wajibu avunje swala, kisha aoge na kutawadha na
afanye vitendo vingine vya wajibu vya mwenye istihadha nyingi,
kisha aswali, na kama wakati hautatosha kutawadha na kuoga, ni
wajibu kwake atayamamu mara mbili, tayamamu moja ni badala ya
kuoga na nyingine ni badala ya kutawadha, na kama wakati hau-
tatosheleza kuoga na kutawadha basi ni wajibu kwake atayamamu
badala yake, na kama ataoga itabidi atayamamu badala ya udhu, na
kama atatawadha itabidi atayamamu badala ya kuoga, na kama
wakati hautatosha kwa vyote viwili, haijuzu kukata swala, bali
ataikamilisha kisha atalipa kwa tahadhari ya sunna.
324. Kama damu ikikatika katikati ya swala na mustadha hajui kuwa
imekatika tumboni au laa, kama atajua baada ya swala kuwa imekati-
ka ni wajibu kwake arudie kuoga, kutawadha na kuswali kwa mara
nyingine.
325. Kama mwenye istihadha nyingi ikiwa ya wastani, ni wajibu afanye
wadhifa wa istihadha nyingi katika swala ya kwanza, na wadhifa wa
wastani kwa swala zinazofuatia. Mfano mwenye istihadha nyingi
ikiwa ya wastani kabla ya adhuhuri, ni wajibu aoge kwa ajili ya
swala ya adhuhuri na atatawadha kwa ajili ya swala ya magharibi na
Isha, lakini kama hajaoga kwa ajili ya swala ya adhuhuri na ikawa
63
Al-Masailul Islamiyah
Page 78
wakati unamtosha kuswali swala ya alasiri tu, basi ni wajibu kwake
aoge kwa ajili ya swala ya alasiri, na kama hataoga kwa ajili ya
swala ya alasiri pia, ni wajibu aoge kwa ajili ya swala ya
magharibi, na kama hataoga kwa ajili ya swala ya magharibi pia na
wakati ukawa hautoshi, basi ni wajibu aoge kwa ajili ya swala ya
Isha.
326. Kama damu ya istihadha nyingi itakatika kabla ya kila swala, kisha
akaona damu, ni wajibu aoge katika kila swala kwa tahadhari ya
wajibu.
327. Kama istihadha nyingi itakuwa istihadha chache ni wajibu kwake
afanye wadhifa wa istihadha nyingi katika swala ya kwanza, kisha
atafanya wadhifa wa istihadha chache katika swala zinazokuja, na
vile vile istihadha ya wastani ikiwa istihadha chache, atafanya wad-
hifa wa istihadha ya wastani katika swala ya kwanza, kisha atafanya
wadhifa wa istihadha chache katika swala zingine.
328. Kama mustahadha ataacha kufanya moja ya wadhifa wake wa
wajibu, kama vile kuacha kubadilisha pamba basi swala yake inabati-
lika.
329. Mwenye istihadha chache kama anataka kufanya kitendo ambacho
ni sharti awe na udhu, mfano anataka kugusa maandiko ya Qur’an,
kama itakuwa ni baada ya swala basi ni wajibu kwake atawadhe.
330. Mustahadha kama ataoga josho za wajibu wake ataruhusiwa kuingia
msikitini, kusimama ndani yake, kusoma sura zenye sajda za wajibu
na kuonana kimwili na mume wake, hata kama hatafanya vitendo
vingine ambavyo ni wajibu avifanye kwa ajili ya swala, mfano
kubadilisha pamba na kitambaa.
331. Mwenye istihadha nyingi au ya wastani kama akitaka kusoma sura
yenye sajida ya wajibu au kuingia msikitini kabla ya swala, basi ni
64
Al-Masailul Islamiyah
Page 79
kwa tahadhari ya wajibu aoge, na vile vile mume wake akimtaka
waonane kimwili, lakini akitaka kugusa Qur’ani ni wajibu kwake
atawadhe pia.
332. Swala ya majanga ni wajibu kwa mustahadha na ni wajibu kwake
afanye vyote ambavyo ni wajibu katika swala za kila siku.
333. Kama mustahadha atawajibika kuswali swala ya majanga katika
wakati wa swala za kila siku, ni wajibu kwake afanye kwa ajili ya
swala ya majanga kila kinachokuwa wajibu kwake kwa ajili ya
swala za kila siku, hata kama akitaka kuswali moja baada ya
nyingine na wala haijuzu kuswali swala zote mbili kwa josho moja.
334. Mustahadha kama akitaka kulipa swala zilizompita ni wajibu afanye
katika kila swala vyote ambavyo ni wajibu kwake kwa ajili ya swala
za adaa (swala zinazoswaliwa kwa wakati).
335. Mustahadha akijua kuwa damu inayotoka kwake sio damu ya jera-
ha au jipu na wala sio damu ya hedhi au nifasi kisheria, ni wajibu
afanye wadhifa wa mustahadha, bali hata akishuku kuwa ni damu ya
istahadha au ni katika damu zingine, kama haitakuwa na alama za
damu zingine, basi ni lazima kwake afanye wadhifa wa mustahad-
ha kwa tahadhari ya wajibu.
HEDHI
336. Damu ya hedhi ni damu ambayo inatoka kwenye mfuko wa uzazi
wa mwanamke katika kila mwezi kwa siku maalumu.
337. Damu ya hedhi mara nyingi huwa ni ya moto, nzito nyeusi au
nyekundu, inatoka kwa nguvu na inachoma.
338. Wanawake wa kikuraishi hukoma kutokwa na damu ya hedhi
wanapofikisha umri wa miaka sitini, na wasio kuwa makuraishi
hukoma kutokwa na damu ya hedhi wanapofikisha umri wa miaka
65
Al-Masailul Islamiyah
Page 80
hamsini, na kama wataona damu baada ya hapo haitakuwa damu ya
hedhi hata kama ikiwa na alama za damu ya hedhi, bali itakuwa ni
damu ya istihadha.
339. Damu ambayo anaiona binti kabla hajatimiza miaka tisa au anay-
oiona mwanamke baada ya kufikia umri wa kutotokwa na hedhi
haitokuwa hedhi.
340. Mwanamke mwenye mimba na mwenye kunyonyesha anaweza
kupata hedhi.
341. Binti ambaye hajui kuwa ametimiza miaka tisa au laa, kama akiona
damu ambayo haina sifa za hedhi haitokuwa hedhi, na kama itakuwa
na sifa za hedhi basi itakuwa ni hedhi, inawezekana akawa ame-
timiza miaka tisa.
342. Mwanamke ambaye anashuku kuwa amekoma kutokwa na damu ya
hedhi au laa, na wala hawezi kujua umri wake ni miaka mingapi?
Kama ataona damu na wala hajui kuwa ni hedhi au laa, ni wajibu
ajalie kuwa hajakoma kutokwa na damu ya hedhi.
343. Muda wa hedhi haupungui siku tatu wala hauzidi siku kumi, kama
akiona damu kwa muda wa chini ya siku tatu hata kama ikiwa kido-
go haitakuwa hedhi, na muda mchache unaotenganisha baina ya
hedhi mbili ni siku kumi.
344. Ni wajibu siku tatu za hedhi ziwe kwa mfululizo, kama ataona damu
kwa muda wa siku mbili kisha akatoharika siku moja, kisha akaona
damu siku ya tatu, basi haitokuwa hedhi, ni juu yake kwa tahad-
hari ya sunna aache yaliyokatazwa katika hedhi na afanye vitendo
vya istihadha, yaani aache kuonana kimwili, kuingia msikitini,
kugusa maandiko ya Qur’ani, kugusa jina la Allah na kusoma sura
zenye sajida za wajibu, na wakati huo huo afanye yaliyo wajibu kwa
66
Al-Masailul Islamiyah
Page 81
mustahadha, kutawadha, kuoga n.k, katika kila swala.
345. Sio lazima damu kutoka katika siku zote tatu, bali inatosha kuwepo
damu ndani ya uke, lakini akitoharika katikati ya siku tatu kwa
muda mfupi na muda huo uwe mfupi sana kwa kiasi kwamba
itasemwa kuwa damu ilikuwa ndani ya uke katika muda wa siku tatu
basi itakuwa hedhi.
346. Sio lazima aone damu katika usiku wa kwanza na usiku wa nne kwa
muda wa siku tatu, lakini ni lazima isikatike usiku wa pili na usiku wa
tatu, kama ataona damu kuanzia adhana ya Asubuhi ya siku ya kwan-
za na ikakatika wakati huo huo wa siku ya nne na haijakatika usiku
wa pili, wa tatu na wa nne, itakuwa ni hedhi.
347. Kama ataona damu kwa muda wa siku tatu mfululizo kisha akato-
harika, na kama ataona damu baada ya hapo na siku zote alizoona
damu na alizotoharika kama hazizidi siku kumi, basi zote zitakuwa
hedhi.
348. Kama ataona damu zaidi ya siku tatu na chini ya siku kumi na wala
hajui kuwa ni damu ya jipu au jeraha au damu ya hedhi, basi ni
wajibu aijalie kuwa ni hedhi, sawasawa atakuwa na yakini kuwa ni
hedhi au anashaka katika hilo.
349. Kama ataona damu na hajui kuwa ni damu ya jeraha au hedhi kabla
ya kupita siku tatu, basi kwa tahadhari ya wajibu afanye ibada zake na
aache kila kinachokuwa wajibu kuachwa na mwenye hedhi mpaka
itakapojulikana hali halisi.
350. Kama ataona damu kisha akashuku kuwa ni damu ya hedhi au ni
damu ya istihadha, basi ni wajibu aijalie kuwa ni hedhi, kama itakuwa
na alama za hedhi.
67
Al-Masailul Islamiyah
Page 82
351. Kama ataona damu na akawa hajui kuwa ni damu ya hedhi au ni damu
ya bikira, basi ni wajibu afanye uchunguzi kwa kuingiza pamba ndani
ya uke na kusubiri kidogo kisha aitoe, kama damu haikuingia ndani
ya pamba bali ikachovya pembeni basi itakuwa ni damu ya bikira, na
kama damu itaingia ndani ya pamba yote basi itakuwa ni damu ya
hedhi, na hii ni ikiwa damu ya bikira sio nyingi inayoweza kufanana
na ya hedhi.
352. Kama ataona damu chini ya siku tatu na akatoharika, kisha akaona
damu kwa muda wa siku tatu zingine, basi damu ya mara ya pili ni
hedhi na ya kwanza sio hedhi hata kama itakuwa katika ada yake.
HUKUMU ZA HEDHI
353. Ni haramu kwa mwenye hedhi mambo yafuatayo:-
Ibada ambazo ni wajibu kutawadha au kuoga au kutayamamu, lakini ibada
ambazo hazihitaji udhu au kuoga au kutayamamu mfano swala ya maiti,
anaweza kuiswali akiwa katika hali ya hedhi.
Mambo yote ambayo ni haramu kwa mwenye janaba.
Jimai ni haramu kwa mwanaume na mwanamke, hata kwa kiasi cha kuin-
giza kichwa cha uume na kutotoka manii, bali ni kwa tahadhari ya wajibu
asiingize kichwa hata kidogo na asimwingilie mwanamke mwenye hedhi
kwa nyuma, lakini hakuna tatizo kumbusu.
354. Ni haramu kuonana kimwili kama hedhi itaendelea zaidi ya ada yake,
lakini ni wajibu azijaalie siku hizo kuwa ni hedhi, kama ataona damu
zaidi ya siku kumi ni wajibu ajalie ada za jamaa zake wa karibu kuwa
ni hedhi yake, na itakuwa haramu kwa mume wake kumuingilia.
355.Siku za hedhi zinagawanyika sehemu tatu
68
Al-Masailul Islamiyah
Page 83
1 – Siku za mwanzo
2 - Siku za katikati
3 - Siku za mwisho
356. Kama mume wake atamwingilia kwa mbele katika siku za mwanzo
atatoa dinari moja kumpa fukara, na akimwingilia siku za katikati ata-
toa nusu dinari, na siku za mwisho atatoa robo dinari. Pia atatoa
kafara kama atamwingilia kwa nyuma akiwa katika hedhi.
357. Ni kwa tahadhari ya sunna kwa mwanamume kutoa kafara kama aki-
jua kuwa mke wake ana hedhi naye akamwingilia, lakini
akimwingilia katika hali ya hedhi naye hajui hatawajibika kutoa cho-
chote.
358. Sio wajibu kafara iwe ni dinari bali inaweza ikawa thamani yake.
369. Kama thamani ya kafara itatofautiana wakati alipomwingilia mke
wake mwenye hedhi na wakati wa kumpa fukara, ni wajibu atoe
thamani ya wakati anapompa fukara.
360. Kama mwanaume atamwingilia mke wake mwenye hedhi katika siku
za mwanzo za hedhi na za katikati na za mwisho itabidi atoe kafara
katika kila kundi kafara yake.
361. Mwanaume akimwingilia mke wake mwenye hedhi na akatoa kafara,
kisha akarudia tena kumwingilia atatoa kafara kwa mara nyingine.
362. Mwanaume akimwingilia mke wake mwenye hedhi zaidi ya mara
moja na hajatoa kafara wakati huo, basi ni kwa tahadhari ya sunna
atoe kafara moja katika kila mara aliyomwingilia.
363. Kama mwanaume atajua katikati ya jimai kuwa mke wake ana hedhi,
ni wajibu aache haraka na kama hataacha atalipa kafara kwa tahadhari
69
Al-Masailul Islamiyah
Page 84
ya sunna.
364. Mwanaume akizini na mwanamke mwenye hedhi au akimwingilia
mwanamke ajinabia (asiyekuwa halali kwake) mwenye hedhi kwa
kudhania kuwa ni mke wake, basi ni kwa tahadhari ya sunna atoe
kafara.
365. Mtu ambaye hawezi kulipa kafara aombe msamaha kwa Allah (swt)
hii ikiwa hana uwezo kuanzia mwanzo, lakini kama alikuwa anauwe-
zo kisha akawa hana uwezo, basi kwa tahadhari ya sunna akipata
uwezo alipe kafara.
366. Talaka ya mwanamke akiwa katika hedhi ni batili.
367. Mwanamke akisema mimi nina hedhi au nimetoharika kutokana na
damu ya hedhi, kauli yake itakubalika ikiwa haijulikani kuwa ni
muongo.
368. Kama mwanamke atatokwa na hedhi wakati wa kuswali swala yake
itabatilika.
369. Kama mwanamke atashuku kuwa ametokwa na hedhi wakati wa
swala au laa, swala yake inasihi, lakini akijua kuwa alitokwa na hedhi
wakati wa swala basi swala yake itabatilika.
370. Baada ya mwanamke kutoharika kutokana na hedhi ni wajibu aoge
kwa ajili ya swala na ibada zingine ambazo ni sharti kuwa na udhu,
au kuoga, na kuoga josho la hedhi ni kama josho la janaba, lakini aki-
taka kuswali ni wajibu atawadhe kabla ya kuoga au baada ya kuoga.
371. Baada ya mwanamke kutoharika kutokana na damu ya hedhi akipewa
talaka inasihi hata kama bado hajaoga, vilevile inajuzu kwa mume
wake kumwingilia kabla ya kuoga, lakini kwa tahadhari ya sunna
aoshe uke wake kabla ya jimai, na kwa tahadhari ya sunna ajiepushe
na jimai kabla ya kuoga, ama mambo mengine ambayo yana-
70
Al-Masailul Islamiyah
Page 85
haramishwa wakati wa hedhi mfano, kubakia msikitini, kugusa
maandiko ya Qur’an ambayo ni sharti awe na udhu haitakuwa ruhusa
kwake mpaka aoge au atawadhe.
372.Kama maji hayatoshi kutawadha na kuoga, lakini yanatosha ama
kuoga au kutawadha, basi ni wajibu aoge na atayamamu badala ya
udhu kwa tahadhari ya wajibu, na kama hayatoshi kuoga, basi ni
wajibu atawadhe halafu atayamamu badala ya kuoga, na kama hana
maji kabisa ni wajibu atayamamu mara mbili, moja ni badala ya kuoga
na nyingine ni badala ya udhu.
373. Mwanamke mwenye hedhi halipi swala za kila siku zilizopita wakati
wa hedhi, lakini ni wajibu alipe saumu za wajibu zilizompita wakati
wa hedhi.
374. Mwanamke akijua kuwa wakati wa swala umeingia na kama
akichelewesha swala atatokwa na hedhi, basi ni wajibu kwake aswali
haraka.
375. Kama atachelewesha swala mpaka wakati ukapita kwa kiwango cha
swala kisha akapata hedhi, ni wajibu ailipe hiyo swala, mwanamke
ambaye sio msafiri kama akichelewesha swala ya Adhuhuri kuanzia
mwanzo wa wakati kisha akapata hedhi baada ya kupita muda wa
kuweza kuswali rakaa nne, ni wajibu kwake ailipe, na kwa
mwanamke msafiri akichelewa kwa kiwango cha rakaa mbili ni
wajibu ailipe.
376.Kama mwanamke atatoharika mwisho wa wakati wa swala, na wakati
ukatosha kuoga na kutawadha na maandalizi mengine kwa ajili ya
swala na kuswali rakaa moja au zaidi ndani ya wakati, ni wajibu aswali
na kama hataswali ni wajibu ailipe
377. Kama wakati hautoshi kuoga na kutawadha lakini ukatosha kutaya-
71
Al-Masailul Islamiyah
Page 86
mamu na kuswali, ni wajibu aswali hiyo swala, na vilevile kama wad-
hifa wake ni kutayamamu ni wajibu atayamamu na kuswali swala
hiyo.
378. Mwanamke mwenye hedhi akishuku kuwa wakati unamtosha kuswali
au laa, ni wajibu aswali swala hiyo.
379. Kama hajaswali kwa kudhania kuwa wakati haumtoshi kuswali rakaa
moja na kufanya maandalizi mengine, kisha ikabainika kuwa wakati
ulikuwa unatosha basi ni wajibu ailipe swala hiyo.
380. Ni sunna kwa mwanamke mwenye hedhi unapofika wakati wa swala
ajisafishe, abadilishe pamba na kitambaa kisha atawadhe au atayama-
mu kama hataweza kutawadha, kisha akae katika sehemu ya kuswalia
akielekea kibla na asome dhikiri, dua na kumswalia Mtume (saww)
381. Ni makuruhu kwa mwenye hedhi kusoma Qur’an tukufu, kuwa nayo,
kuibeba na kugusa pembeni mwa maandiko, vilevile ni makuruhu
kwake kupaka hina na n.k
VIGAWANYO VYA HEDHI
382. Wanawake wenye kutoka hedhi wamegawanyika katika sehemu sita;
1). Mwenye ada ya wakati na idadi:
Yaani anaona damu ya hedhi katika miezi miwili mfululizo kwa wakati
maalumu na kwa idadi maalumu mfululizo mwanzo wa mwezi mpaka siku
ya saba.
2).Mwenye ada ya wakati:Yaani anaona damu ya hedhi katika miezi
miwili mfululizo kwa wakati maalumu, lakini idadi inatofautiana katika
mwezi wa kwanza na wa pili mfano; Anaona damu katika mwezi wa kwan-
za kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka siku ya saba, na mwezi wa pili
kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka siku ya nane.
72
Al-Masailul Islamiyah
Page 87
3). Mwenye ada ya idadi: Yaani idadi ya hedhi katika miezi miwili inalin-
gana, lakini wakati wa kuona damu katika miezi miwili unatofautiana
mfano: Anaona damu katika mwezi wa kwanza kuanzia siku ya tano
mpaka siku ya kumi na mwezi wa pili kuanzia siku ya kumi na mbili
mpaka siku ya kumi na saba.
4). Asiokuwa na ada maalumu sio ya wakati wala ya idadi: Hapo
mwanzo alikuwa nayo lakini imeharibika, na wala haijatulia nakupata ada
mpya.
5). Anayeanza: Naye ni ambaye anaona damu kwa mara ya kwanza.
6). Aliyesahau ada yake.
WENYE ADA YA WAKATI NA IDADI
383. Wenye ada ya wakati na idadi wanagawanyika sehemu tatu:-
Mwanamke ambaye anaona damu ya hedhi katika miezi miwili mfululizo
kwa wakati maalumu na anatoharika kwa wakati maalumu mfano: Anaona
damu katika miezi miwili mfululizo kuanzia mwanzo wa mwezi na anato-
harika siku ya saba, ada yake inakuwa kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka
siku ya saba.
Mwanamke ambaye hatohariki kutokana na damu lakini anaona damu kati-
ka miezi miwili mfululizo na kwa siku maalumu damu yenye sifa ya hedhi,
lakini damu ambayo anaiona baada ya siku maalumu inakuwa na sifa za
damu ya istihadha. Mfano anaona damu yenye sifa ya hedhi kuanzia
mwanzo wa mwezi mpaka siku ya nane katika miezi yote miwili, kwa hiyo
hii ni ada yake kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka siku ya nane.
Mwanamke ambaye anaona damu ya hedhi katika miezi miwili mfululizo
kwa wakati maalumu na inaendelea kwa muda wa siku tatu au zaidi kisha
73
Al-Masailul Islamiyah
Page 88
anatoharika siku moja au zaidi, kisha anaona damu kwa mara nyingine,
kama siku alizoona damu, na siku alizotoharika hazizidi siku kumi katika
kila miezi miwili, basi siku zote hizo zitakuwa ni ada yake mfano: Akiona
damu katika mwezi wa kwanza kuanzia mwanzo mpaka siku ya tatu, na
katika mwezi wa pili akiona kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka siku ya
tatu, kisha akatoharika kwa muda wa siku tatu au zaidi au pungufu ya tatu,
kisha akaona damu kwa mara nyingine kama siku alizoona damu, na siku
alizotoharika hazizidi siku tisa, kwa hiyo ada ya huyu mwanamke ni siku
tisa.
384. Mwanamke mwenye ada ya wakati na idadi kama akiona damu kabla
ya ada au baada ya ada kwa siku mbili au tatu kwa kiasi kwamba
itasemwa kuwa hedhi yake imetangulia au imechelewa, ni wajibu
kwake afanye wadhifa wa hedhi (afanye anayo yafanya mwenye
hedhi) hata kama damu haitakuwa na sifa za hedhi, na kama atajua
baadae kuwa haikuwa ni damu ya hedhi mfano: Akitoharika kabla ya
siku tatu basi ni wajibu kwake alipe ibada zilizompita.
385. Mwanamke mwenye ada ya idadi na wakati:-
kama akiona kabla ya ada yake na ikaendelea mpaka kwenye siku za ada
yake na baada ya ada, kama siku zote alizoona damu hazizidi siku kumi
basi zote zitakuwa ni hedhi.
Na kama zitazidi siku kumi basi damu aliyoiona katika siku za ada yake
zitakuwa ni hedhi, na damu ambayo aliona kabla na baada ya ada itakuwa
ni damu ya istihadha, na ni wajibu alipe ibada zilizopita katika siku zili-
zotangulia ada au baada ya ada.
Kama siku za ada na zilizotangulia ada hazizidi siku kumi basi zote
zitakuwa ni hedhi.
Na kama siku zitazidi siku kumi basi siku za ada peke yake zitakuwa ni
hedhi na damu aliyoiona kabla ya ada itakuwa ni damu ya istihadha, na ni
74
Al-Masailul Islamiyah
Page 89
wajibu alipe ibada zilizompita.
Kama ataona damu katika siku za ada na baada ya siku za ada kama siku
zote hazitazidi siku kumi basi zote ni hedhi, na kama zitazidi siku kumi
basi siku za ada peke yake zitakuwa ni hedhi na zilizobaki ni istihadha.
386. Mwenye ada ya wakati na idadi :-
Kama ataona damu katika baadhi ya siku za ada yake na akaona kabla ya
ada, kama siku zote hazitazidi siku kumi, basi zitakuwa ni hedhi.
Na kama zitazidi siku kumi, basi siku alizoona damu katika siku za ada
yake zitakuwa ni hedhi, hata kama siku hizo zitakuwa chache au nyingi
kuliko ada yake, na zilizobaki zitakuwa ni istihadha.
Kama akiona katika baadhi ya siku za ada yake na baada ya ada na siku
zote hazizidi kumi basi zote ni hedhi.
Na kama siku alizoona damu zinazidi siku kumi ni wajibu ajalie siku zili-
zoingiliana na ada yake azifanye kuwa ni hedhi na zilizobaki ni istihadha.
387. Mwanamke mwenye ada ya wakati na idadi, kama akiona damu siku
tatu au zaidi kisha akatoharika, kisha akaona damu kwa mara
nyingine, na muda uliotenganisha baina ya damu mbili ni pungufu ya
siku kumi, kisha siku alizoona damu na siku alizotoharika zinazidi
siku kumi, mfano: aone damu kwa muda wa siku tano, kisha anaona
damu kwa mara ya pili kwa muda wa siku tano zingine, kwa hali hii
kutakuwa na sura zifuatazo:-
Damu aliyoiona kwa mara ya kwanza yote au baadhi ilingane na siku za
ada yake na wala hailingani na damu atakayoiona baada ya kutoharika na
siku za ada yake, basi hapa ni wajibu ajaalie kuwa ya kwanza ni hedhi na
ya pili ni istihadha.
75
Al-Masailul Islamiyah
Page 90
Damu ya kwanza isilingane na siku za ada yake, damu ya pili yote au baad-
hi ilingane na siku za ada yake, hapa ni wajibu aifanye damu ya pili kuwa
ni hedhi na damu ya kwanza kuwa istihadha.
Baadhi ya siku za kwanza na za pili kulingana na siku za ada yake, na
damu ya kwanza iliyolingana na siku za ada isipungue siku tatu na damu
yote iliyolingana na ada na siku alizotoharika zisizidi siku kumi, na kwa
hali hii siku zote zitakuwa ni hedhi, na iliyotangulia ada na iliyochelewa
itakuwa ni istihadha. Mfano kama ada imeanza siku ya tatu ya mwezi
mpaka siku kumi na akaona damu katika moja ya miezi kuanzia mwanzo
mpaka siku ya sita, kisha akatoharika kwa muda wa siku mbili, kisha
akaona damu mpaka siku ya kumi na tano ya mwezi, basi atajaalia siku ya
tatu mpaka ya kumi ni hedhi na kuanzia siku ya kwanza mpaka siku ya
tatu, na kuanzia siku ya kumi mpaka siku ya kumi na tano ni istihadha.
Baadhi ya damu ya kwanza na ya pili ikilingana na siku za ada lakini baad-
hi ya damu ya kwanza iliyolingana na ada iwe pungufu ya siku tatu, basi
ni wajibu kwake katika hali hii ajiepushe na vilivyoharamu kwa mwenye
hedhi katika siku za damu mbili na siku alizotoharika, na wakati huo huo
atafanya vitendo vya mustadha na kufanya ibada kama ilivyo tajwa katika
hukumu za mustadha.
388. Mwenye ada ya wakati na idadi, kama hataona damu katika wakati wa
ada yake na akaiona wakati mwingine kwa kiwango cha ada yake, ni
wajibu aifanye kuwa hedhi, sawa sawa iwe kabla ya ada au baada ya
ada.
389. Mwenye ada ya wakati na idadi kama ataona damu wakati wa ada
yake lakini idadi ikawa pungufu au zaidi ya ada ya hedhi, na damu
aliyoiona kabla ya ada ikiwa na idadi ya ada, na kama kitenganishi
baina ya damu ni siku kumi au zaidi, atajaalia damu mbili kuwa ni
76
Al-Masailul Islamiyah
Page 91
hedhi, na kama siku za damu mbili na siku alizotoharika hazizidi siku
kumi basi zote zitakuwa ni hedhi.
390. Mwenye ada ya wakati na idadi kama akiona damu zaidi ya siku
kumi, basi damu aliyoiona katika siku za ada itakuwa ni hedhi hata
kama haina sifa za hedhi, na damu aliyoiona baada ya siku za ada ni
istihadha hata kama ina sifa za hedhi, mfano: mwanamke ambaye ada
yake ni kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka siku ya saba, kama akiona
damu kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka siku ya kumi na mbili, ata-
jaalia siku saba za mwanzo kuwa ni hedhi na siku tano za mwisho
kuwa ni istihadha.
391. Wenye ada ya wakati wanagawanyika sehemu tatu:-
mwanamke ambaye anaona damu ya hedhi katika miezi miwili mfululizo
kwa wakati maalumu kisha anatoharika baada yake siku kadhaa, lakini
idadi ya siku katika kila mwezi inatofautiana. Mfano anaona damu katika
miezi miwili mfululizo kuanzia mwanzo wa mwezi, na mwezi wa kwanza
mpaka siku ya saba na mwezi wa pili mpaka siku ya nane, basi huyu ada
yake ni kuanzia mwanzo wa mwezi.
Mwanamke ambaye hatohariki kutokana na damu lakini damu ambayo
anaiona katika miezi miwili mfululizo kwa wakati maalumu inakuwa na
sifa ya hedhi, na damu anayoiona katika siku zingine inakuwa na sifa za
istihadha na idadi ya siku anazoona damu yenye sifa za hedhi katika miezi
miwili hailingani. Mfano damu anayoiona kuanzia mwanzo wa mwezi
mpaka siku ya saba ya mwezi wa kwanza na mwezi wa pili kuanzia mwan-
zo wa mwezi, mpaka siku ya nane inakuwa na sifa za hedhi na inayobaki
inakuwa na sifa za istihadha.
Mwanamke ambaye anaona damu ya hedhi katika miezi miwili mfululizo
kwa wakati maalumu kwa siku tatu au zaidi, kisha anatoharika kisha
anaona damu kwa mara nyingine, lakini idadi ya siku alizoona damu mbili
na alizotoharika hazizidi siku kumi, lakini katika mwezi wa pili inazidi
77
Al-Masailul Islamiyah
Page 92
siku hizi au zinapungua kuliko mwezi wa kwanza mfano: katika mwezi wa
kwanza idadi ya siku ni nane na mwezi wa pili ni siku tisa, na huyu pia
mwanzo wa mwezi utakuwa ni ada yake.
392.Mwenye ada ya wakati kama akiona damu, kabla ya ada au baada kwa
siku mbili au tatu, ikiwa hedhi imetangulia au imechelewa ni wajibu
kwake afanye wadhifa wa hedhi hata kama hiyo damu haina sifa za
hedhi, na kama atatambua baadae kuwa haikuwa damu ya hedhi
mfano: akitoharika kabla ya siku tatu, ni wajibu alipe ibada zilizompi-
ta, nani bora kwake aache yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na
kufanya yaliyo wajibu kwa mustahadha.
393. Mwenye ada ya wakati, kama akiona damu zaidi ya siku kumi na
akawa hawezi kutambua siku za hedhi kwa njia ya alama basi itabidi
ajalie ada ya jamaa zake wa karibu kuwa ni hedhi yake. Sawa sawa
jamaa zake wawe wa upande wa baba au wa mama, wako hai au maiti
kwa sharti ada zao wote ziwe sawa, lakini ada zao zikitofautiana
mfano: baadhi yao ni siku tano na baadhi yao ni siku saba, basi ina-
juzu kwake kujaalia ada ya waliowengi kuwa ni ada yake.
394. Mwenye ada ya wakati ambaye anafanya ada ya jamaa zake wa
karibu kuwa ni hedhi yake, basi ni wajibu afanye siku ambayo ilikuwa
mwanzo wa ada yake katika kila mwezi kuwa ni mwanzo wa hedhi
yake mfano: Mwanamke ambaye alikuwa anaona damu kila mwanzo
wa mwezi na anatoharika siku ya saba au ya nane, na kama ataona
damu katika moja ya miezi kwa muda wa siku kumi na mbili na ada
ya jamaa zake ni siku saba ni wajibu afanye siku saba kuanzia mwan-
zo wa mwezi kuwa ni hedhi na inayobaki kuwa istihadha.
395. Mwanamke ambaye ni wajibu kwake aifanye ada ya jamaa zake wa
karibu kuwa ni hedhi yake, kama hana jamaa au wakatofautiana ada
zao ni wajibu kila mwezi kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka siku ya
saba afanye kuwa ni hedhi na inayobaki kuwa istihadha lakini kama
78
Al-Masailul Islamiyah
Page 93
alama za hedhi zitakuwa katika siku za katikati au za mwisho ni nyin-
gi zaidi kuliko siku zingine, basi ni wajibu afanye mwanzo wa siku
saba kuanzia katikati au kuanzia mwisho.
396. Wenye ada ya idadi wanagawanyika sehemu tatu:-
mwanamke ambaye idadi ya siku za hedhi yake katika miezi miwili mful-
ulizo zinakuwa sawa, lakini wakati wa kuona damu katika miezi miwili
unatofautiana, basi katika hali hii atajaalia siku zote alizoona damu kuwa
ni hedhi mfano: Kama akiona damu katika mwezi wa kwanza kuanzia
mwanzo mpaka siku ya tano, na katika mwezi wa pili kuanzia siku ya tano
na katika mwezi wa pili kuanzia siku ya kumi na moja mpaka siku ya kumi
na tano, ada yake itakuwa ni siku tano.
Mwanamke ambaye hatohariki kutokana na damu, lakini yeye anaona
damu katika miezi miwili mfululizo na katika siku maalumu damu yenye
sifa za hedhi na katika siku zingine anaona damu yenye sifa za istihadha,
na idadi ya siku amabzo ameona damu yenye sifa za hedhi katika miezi
inalingana lakini wakati unatofautiana. Katika hali hii siku zenye sifa za
hedhi zinakuwa ni ada yake mfano: Akiona damu kuanzia mwanzo wa
mwezi mpaka siku tano na katika mwezi unaofuatia kuanzia siku tano na
damu katika mida yote miwili inakuwa na sifa za hedhi na inayobaki
inakuwa na sifa za istihadha basi ada yake itakuwa siku tano.
Mwanamke anayeona damu katika miezi miwili mfululizo kwa muda wa
siku tatu au zaidi kisha akatoharika kwa muda wa siku moja au zaidi, kisha
akaona damu kwa mara nyingine lakini wakati wa kuona ukatofautiana
katika miezi miwili, kama idadi ya damu mbili na siku alizotoharika hazi-
jazidi siku kumi na idadi ya siku katika miezi miwili iko sawa, basi siku
alizoona damu na siku alizotoharika zinakuwa ni ada yake mfano: kama
akiona damu kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka siku ya tatu kisha akato-
harika kwa muda wa siku mbili kisha akaona damu kwa muda wa siku tatu
zingine, na katika mwezi wa pili akiona damu kuanzia siku ya kumi na
moja mpaka siku ya kumi na tatu, kisha akatoharika kwa muda wa siku
79
Al-Masailul Islamiyah
Page 94
mbili au zaidi au pungufu kisha akaona damu kwa mara nyingine na siku
zote hazijazidi siku nane basi ada yake itakuwa siku nane.
397. Mwenye ada ya idadi kama akiona damu zaidi ya ada yake na ikazidi
kumi itakuwa kama ifuatavyo:-
Kama damu yote itakuwa ina sifa moja ni wajibu ajalie idadi ya siku
kuanzia wakati alipoona damu kuwa ada yake na inayobaki istihadha.
Kama sifa za damu zitatofautiana baadhi ikawa na sifa za hedhi na
nyingine za istihadha, kama damu yenye sifa za hedhi idadi yake italingana
na ada yake ni wajibu ajalie siku hizo kuwa ni hedhi na zinazobaki kuwa
istihadha.
Kama siku ambazo damu itakuwa na sifa za hedhi zinazidi siku za ada yake
atajalia idadi ya ada yake kuwa ni hedhi peke yake na inayobaki kuwa isti-
hadha.
Kama siku ambazo damu itakuwa na sifa za hedhi ni pungufu kuliko siku
za ada yake, ni wajibu aongeze siku zingine katika siku za ada yake kuwa
ni hedhi yake na zinazobaki ni istihadha.
398. Mwenye utata:Ni mwanamke ambaye anaona damu katika miezi
kadhaa lakini hana ada thabiti sio ya idadi wala ya wakati, kama
ataona damu zaidi ya siku kumi na damu yote ina sifa moja kama ada
ya jamaa zake wa karibu ni siku saba, basi afanye siku saba kuwa ni
hedhi na inayobaki kuwa ni istihadha, na kama ada yao ni chache
mfano: Ni siku tano, ataifanya kuwa ni hedhi na kwa tahadhari ya
sunna aache yaliyo haramu kwa wenye hedhi na kufanya wadhifa wa
mustadha, katika tofauti baina ya siku saba na ada zao, na kama ada
ya jamaa zake wa karibu ni zaidi ya siku saba, mfano ada yao ni siku
tisa kwa hiyo yeye atafanya siku saba kuwa ni hedhi na siku mbili zili-
zobaki ataacha yaliyoharamu kwa wenye hedhi na kufanya wadhifa
wa mustadha kwa tahadhari ya sunna.
80
Al-Masailul Islamiyah
Page 95
399. Mwenye utata kama ataona damu zaidi ya siku kumi, na baadhi ya
damu ina sifa ya hedhi na nyingine ina sifa ya istihadha, kama damu
yenye sifa ya hedhi ni pungufu ya siku tatu au zaidi ya siku kumi ni
wajibu afanye kama tulivyotaja katika mas’ala yaliyopita, lakini kama
damu yenye sifa ya hedhi sio pungufu ya siku tatu wala zaidi ya siku
kumi basi yote itakuwa ni hedhi.
400. Anayeanza: Ni mwanamke ambaye anaona damu kwa mara ya kwan-
za, kama ataona damu zaidi ya siku kumi yenye sifa moja, basi ni
wajibu afanye ada ya jamaa zake wa karibu kuwa ni ada yake ambayo
ni siku saba na zinazobaki kuwa ni istihadha.
401. Anayeanza kama ataona damu zaidi ya siku kumi baadhi yake ina sifa
ya hedhi na nyingine ina sifa ya istihadha, kama damu yenye sifa ya
hedhi ni zaidi ya siku tatu na haijazidi siku kumi basi yote itakuwa ni
hedhi, lakini akiona damu kabla ya siku kumi kuisha damu yenye sifa
ya hedhi pia, mfano: Akiona damu nyeusi kwa muda wa siku tano, na
damu ya njano kwa muda wa siku tisa, kisha akaona damu nyeusi kwa
muda wa siku tano zingine, basi ni wajibu afanye ada ya jamaa zake
wa karibu kuwa ni hedhi yake na nyingine ni istihadha.
402. Anayeanza akiona damu zaidi ya siku kumi, na baadhi ya damu ina
sifa ya hedhi na nyingine ina sifa ya istihadha kama siku ambazo zina
sifa za hedhi ni chache kuliko siku tatu au zaidi ya siku kumi, basi ata-
jalia ada ya jamaa zake wa karibu kuwa ni hedhi yake na inayobaki
kuwa ni istihadha.
403. Aliyesahau: Ni mwanamke ambaye amesahau ada yake, kama ataona
damu zaidi ya siku kumi, ni wajibu ajalie siku ambazo zina sifa ya hedhi
kuwa ni hedhi, na ikiwa hataweza kupambanua kwa njia ya sifa na alama
ni wajibu ajaalie siku saba za mwanzo kuwa ni hedhi na zinazobaki kuwa
ni istihadha.
81
Al-Masailul Islamiyah
Page 96
404. Anayeanza, mwenye utata, aliyesahau na mwenye ada ya idadi, kama
wataona damu yenye sifa ya hedhi au wakawa na yakini kuwa damu
itaendelea kwa muda wa siku tatu, ni wajibu kwao waache ibada, na
ikibainika baadae kuwa haikuwa ni hedhi ni wajibu kwao walipe
ibada zilizowapita, na kama hawajawa na yakini, na damu haikuwa na
sifa ya hedhi, basi ni lazima kwa tahadhari ya wajibu wafanye wad-
hifa wa mustadha kwa muda wa siku tatu na waache yaliyoharamu
kwa wenye hedhi, na kama hawatatoharika kabla ya siku tatu ni
wajibu waifanye kuwa ni hedhi.
405. Mwenye ada: Sawa sawa awe ni wa idadi au wakati au idadi na
wakati, kama wataona damu katika miezi miwili mfululizo inatofau-
tiana na ada zao kwa idadi au wakati au idadi na wakati na ilikuwa ni
ya aina moja katika miezi miwili katika idadi au wakati au katika
idadi na wakati, atarejea ada yake aliyoiona katika miezi hii miwili
Mfano: Kama alikuwa anaona damu kuanzia mwanzo wa mwezi mpaka
siku ya saba, kisha anatoharika lakini yeye akaona katika miezi miwili
mfululizo kuanzia siku ya kumi mpaka siku ya kumi na saba, kisha akato-
harika basi ada yake itakuwa kuanzia siku ya saba mpaka siku ya kumi na
saba.
406. Makusudio ya mwezi mmoja ni kuanzia kuonekana damu mpaka siku
ya thelathini, na wala sio mwanzo wa mwezi, labda hedhi ianze
mwanzo wa mwezi.
407. Mwanamke ambaye anaona damu katika mwezi mara moja, kama
ataona damu mara mbili na damu zote mbili zina sifa ya hedhi, kama
siku alizotoharika ni chache kuliko siku kumi ni wajibu azifanye
damu mbili kuwa ni hedhi.
408. Kama akiona damu kwa muda wa siku tatu au zaidi, damu yenye sifa
ya hedhi, kisha akaona damu kwa muda wa siku kumi au zaidi, damu
yenye sifa ya istihadha, kisha akaona baada ya muda wa siku tatu,
82
Al-Masailul Islamiyah
Page 97
damu yenye sifa ya hedhi, basi ni wajibu ajalie damu ya kwanza na ya
pili zilizokuwa na sifa ya damu ya hedhi kuwa ni hedhi.
409. Mwanamke akitoharika kutokana na hedhi kabla ya siku kumi, na
akajua kuwa hakuna damu tumboni mwake, basi ni wajibu aoge kwa
ajili ya ibada zake, na akipta dhana kwamba ataona damu kwa mara
nyingine kabla ya siku kumi kwisha. Lakini kama atakuwa na yakini
kuwa ataona damu kwa mara nyingine kabla ya siku kumi kwisha,
basi asioge, bali damu ya kwanza na ya pili na siku ambazo zinakuwa
baina ya damu mbili zote zitakuwa ni hedhi.
410. Kama mwanamke akitoharika kabla ya siku kumi kwisha, na akadha-
nia kuwa bado kuna damu ndani ya tumbo, ni wajibu achukue pamba
na kuingiza ndani ya uke na asubiri kidogo kisha aitoe pamba, kama
pamba itakuwa ni safi basi ataoga na kufanya ibada, na kama pamba
haitakuwa safi mfano: Ikawa na rangi ya njano, haitakuwa ni hedhi
isipokuwa kama itakuwa katika siku za ada yake, bali hiyo itakuwa ni
istihadha. Lakini kama pamba itakuwa na damu na haikuwa katika
siku za ada yake au ada yake ni siku kumi, basi ni wajibu asubiri kama
atatoharika kabla ya siku kumi ataoga, laa sivyo ataoga mwanzo wa
siku ya kumi kama atatoharika mwanzo wa siku ya kumi, lakini kama
damu yake itazidi siku kumi na ada yake ni pungufu ya siku kumi,
kama akijua kuwa atatoharika kabla ya siku kumi au mwanzo wa siku
kumi basi asioge, na kama akidhania kuwa damu itaendelea mpaka
siku ya kumi basi kwa tahadhari aache ibada ikiwa damu ina sifa ya
hedhi, japo ni bora kuacha yaliyoharamu kwa mwenye hedhi na
kufanya wadhifa wa mustahadha, na kama atatoharika kabla ya siku
ya kumi au mwanzo wa siku ya kumi basi yote itakuwa ni hedhi, na
kama damu itazidi siku kumi basi ni wajibu afanye ada yake kuwa ni
hedhi na inayobaki kuwa ni istihadha, na atalipa ibada zilizompita
katika siku zilizozidi ada yake.
411. Kama atafanya baadhi ya siku kuwa ni hedhi kisha asifanye ibada,
83
Al-Masailul Islamiyah
Page 98
halafu akatambua baadae kuwa haikuwa ni hedhi ni wajibu kwake
alipe swala na saumu zilizompita katika siku hizo, na kama atafanya
ibada kwa kudhania kuwa hana hedhi kisha akagundua kuwa alikuwa
na hedhi, basi ni wajibu kwake alipe saumu alizofunga katika siku
hizo.
NIFASI
412. Damu inayoanza kutoka baada ya sehemu ya mtoto kutokeza nje
kutoka tumboni na ikakatika kabla ya siku kumi au mwanzo ni mwa
siku kumi ni damu ya nifasi au “uzazi”.
413. Damu anayoiona mwanamke kabla ya kutokeza sehemu ya mtoto nje
kutoka tumboni sio damu ya nifasi.
414.Ili kuwa na uhakika wa damu ya nifasi sio lazima mtoto awe amekami-
lika kuumbwa, hata kama kikitoka kipande cha damu au mwanamke
mwenyewe akijua kuwa kilichotoka kama kingebakia tumboni
kingekuwa binadamu au wakunga wanne wakimwelezea kuwa kili-
chotoka kama kingebakia tumboni kingekuwa binadamu basi damu
atakayoiona kwa muda wa siku kumi ni damu ya nifasi.
415. Damu ya nifasi haizidi siku kumi.
416. Kama akishuku kuwa kilichotoka kwake kama kingebakia tumboni
kingekuwa ni binadamu au laa, basi ni kwa tahadhari ya wajibu
afanye uchunguzi. Kama akibakia katika hali ya shaka basi damu
inayotoka sio damu ya nifasi kisharia.
417. Ni haramu kwa mwenye nifasi kubakia msikitini, kugusa maandishi
ya Qur’an tukufu kwa mwili na kila kilichokuwa haramu kwa
mwenye hedhi, na mengineyo, kama ambavyo ni wajibu kwake
84
Al-Masailul Islamiyah
Page 99
vilevile ni sunna kwake na makuruhu kwake yote ambayo ni wajibu
au sunna au makuruhu kwa wenye hedhi.
418. Haisihi kwa mwanamke kupewa talaka akiwa katika hali ya nifasi,
isipokuwa kwa masharti yatakayotajwa katika hukumu za talaka, pia
ni haramu kumwingilia kimwili, na kama mume wake atamwingilia
katika hali hiyo basi ni kwa tahadhari ya sunna atoe kafara kama
ilivyoelezwa katika hukumu za hedhi.
419. Ni wajibu kwa mwanamke aoge baada ya kutoharika kutokana na
damu ya nifasi kisha afanye ibada, na kama ataona damu kwa mara ya
pili, kama damu zote mbili na siku alizotoharika hazizidi siku kumi au
zikawa kumi basi zote zitakuwa ni nifasi, na kama alikuwa amefunga
katika siku alizotoharika ni wajibu alipe hiyo saumu.
420. Kama mwanamke akitoharika kutokana na damu ya nifasi na akadha-
nia kuwa kuna damu tumboni mwake, ni wajibu aingize pamba ukeni
na kusubiri kidogo, kama haijachovya chochote basi aoge kwa ajili ya
ibada zake.
421. Kama damu ya nifasi itazidi siku kumi, kama atakuwa na ada katika
hedhi basi atajalia kiwango cha ada yake kuwa nifasi na inayobaki
kuwa istihadha, na kama hana ada katika hedhi, atajalia kuanzia siku
ya kwanza mpaka ya kumi ni nifasi na siku zinazobaki kuwa istihad-
ha.
422. Mwanamke ambaye ada ya hedhi yake ni chini ya siku kumi, kama
ataona damu ya nifasi zaidi ya ada yake ya hedhi ni wajibu ajaalie
kiwango cha ada yake kuwa nifasi, na baada ya hapo aache ibada kwa
muda wa siku moja kwa tahadhari ya wajibu, na baada ya siku moja
mpaka siku ya kumi ni sunna kwake kufanya wadhifa wa mustahad-
ha, na kuacha kila kilichokuwa haramu kwa mwenye nifasi, na kiasi
kitakachozidi kumi itakuwa istihadha, na ni wajibu ajaalie siku baada
85
Al-Masailul Islamiyah
Page 100
ya ada yake mpaka siku ya kumi kuwa istihadha, na atalipa ibada zili-
zompita katika siku hizo, mfano: mwanamke ambaye anakuwa na ada
katika hedhi siku sita ,kama ataona damu katika nifasi zaidi ya siku
sita ni wajibu ajalie siku sita kuwa ni nifasi na aache ibada katika siku
ya saba kwa tahadhari ya wajibu, na katika siku ya nane, tisa na kumi
ni sunna afanye wadhifa wa mustahadha mfano: Mwanamke ambaye
ada yake katika kila mwezi ni kuanzia siku ya ishirini mpaka ishirini
na saba, kama atajifungua siku ya kumi na damu ikaendelea kutoka
kwa muda wa mwezi au zaidi ya mwezi bila ya kukatika, ni wajibu
kwake ajalie siku ya kumi mpaka siku ya kumi na saba kuwa ni nifasi,
na baada ya kupita siku kumi zilizotajwa na kama damu anayoiona ni
katika siku za ada yake basi ni hedhi, sawa sawa iwe na sifa za hedhi
au laa.
423. Mwanamke ambaye hana ada katika hedhi, kama ataona damu baada
ya kujifungua kwa muda wa mwezi au zaidi, basi kumi la mwanzo ni
nifasi na kumi la pili ni istihadha, na atakayoiona baada ya hapo kama
ina sifa za hedhi basi ni hedhi la sivyo ni istihadha.
KUOGA JOSHO LA KUGUSA MAITI
424.Kama mtu atagusa mwili wa maiti uliopoa na haujaoshwa kwa mwili
wake ni wajibu kwake aoge josho la kugusa maiti, ni sawa sawa awe
amegusa usingizini au akiwa macho, kwa kutaka au laa, bali ni wajibu
kuoga kama amegusa ukucha kwa ukucha au mfupa kwa mfupa, laki-
ni sio wajibu kuoga kama atagusa mzoga wa mnyama.
425. Sio wajibu kuoga kama mtu atagusa maiti ya binadamu ikiwa hau-
japoa mwili wote, hata kama atagusa sehemu iliyopoa.
426. Kama mtu akigusa mwili wa maiti kwa unywele au akagusa unywele
wa maiti kwa mwili au akagusa unywele wa maiti kwa unywele wake,
kama nywele hazitakuwa ni ndefu sana kupita kiasi basi ni wajibu
86
Al-Masailul Islamiyah
Page 101
aoge.
427.Ni wajibu kuoga josho la kugusa maiti, kama akigusa maiti ya mtoto
hata kama ikiwa ni kichanga cha miezi minne (umri wa kuwa tum-
boni), vilevile ataoga kwa tahadhari ya sunna, kama atagusa kichanga
chini ya miezi minne inamaana kuwa, akizaliwa mtoto mwenye umri
wa miezi minne akiwa maiti, kama mwili wake utakuwa wa baridi
wakati wa kutoka basi ni wajibu kwa mama yake aoge josho la kugusa
maiti kwa tahadhari ya wajibu, na kama umri wake utakuwa chini ya
miezi minne sio wajibu kwa mama aoge.
428.Mtoto ambaye amezaliwa baada ya mama yake kuwa maiti, kama
mwili wa mama yake utakuwa umepoa wakati wa kuzaliwa basi ni
wajibu kwa mtoto aoge josho la kugusa maiti akibaleghe kwa tahad-
hari.
429.Kama mtu akigusa maiti ambayo tayari imeshaoshwa josho zote
mitatu sio wajibu kwake kuoga josho la kugusa maiti.
430.Kama kichaa au mtoto akigusa maiti ni wajibu kwa kichaa aoge
akipona na kwa mtoto akibaleghe.
431. Kama sehemu ya mwili wa mtu aliye hai ikikatika au maiti ambaye
haijaoshwa na sehemu iliyokatika ina mfupa, na mtu akaigusa kabla
ya kuoshwa ni wajibu kwa aliyegusa aoge josho la kugusa maiti, laki-
ni kama sehemu iliyokatika haina mfupa sio wajibu aoge.
432. Ni kwa tahadhari ya wajibu kuoga josho la kugusa maiti, ukigusa
mfupa usiokuwa na nyama na haujaoshwa, sawa sawa umekatika
kutoka kwa maiti au kwa mtu hai, na vile vile ni lazima aoge akigusa
jino lililong’ooka kutoka kwa maiti kama maiti bado haijaoshwa,
lakini sio lazima aoge akigusa jino lililong’ooka kutoka kwa mtu hai,
na halina nyama au likiwa na nyama kidogo sana.
433. Josho la kugusa maiti ni sawa na kuoga janaba katika namna, lakini
87
Al-Masailul Islamiyah
Page 102
mtu akioga josho la kugusa maiti akitaka kuswali ni wajibu kwake
atawadhe pia.
434.Kama atagusa maiti nyingi au akagusa maiti moja mara nyingi basi
inamtosheleza kuoga josho moja.
435. Hakuna tatizo kwa mwenye kugusa maiti ambayo haijaoshwa, kusi-
mama msikitini, kufanya jimai au kusoma sura zenye sajda ya wajibu,
lakini ni wajibu aoge na atawadhe kama akitaka kuswali n.k.
HUKUMU ZA MUHTADHARI
“ANAYEKATA ROHO”
436. Mwislamu anayekuwa katika hali ya kutokwa na roho ni wajibu
alazwe chali, nyayo za miguu yake zielekee kibla, sawa sawa awe ni
mwanaume au mwanamke, mkubwa au mdogo kama haitowezekana
kulazwa kwa mgongo, basi ni wajibu alazwe kwa mgongo kwa kadiri
itakavyowezekana, na kama haitawezekana kulazwa kwa kifua kifud-
ifudi ni wajibu akalishwe akielekezwa kibla na kama ikishindikana
hivyo pia ni lazima alazwe kwa upande wa kulia au wa kushoto
akielekezwa kibla.
437. Ni kwa tahadhari ya sunna kumwelekeza maiti kibla kama ilivy-
oelekezwa katika mas’ala iliyotangulia mpaka amalize kumuosha,
lakini akimaliza kumuosha ni bora alazwe kwa kama anavyolazwa
wakati anaposaliwa, mpaka atakapozikwa.
438. Kumuelekeza muhtadhari upande wa kibla ni wajibu kwa kila mwis-
lamu na wala haihitaji idhini ya mwenyemamlaka na maiti, na kama
baadhi (ya watu) watafanya haitakuwa wajibu kwa wengine.
439. Ni sunna kumsomea muhatadhari shahada mbili, majina ya maimamu
kumi na mbili n.k.
88
Al-Masailul Islamiyah
Page 103
440. Ni sunna kumsomea dua muhtadhari.
441.Ni sunna kumuweka muhtadhari kwenye sehemu ya kuswalia pindi
anapozidiwa na uchungu wa kutokwa na roho.
442.Ni sunna kumsomea muhtadhari surat Yaasini, Swafaati, Ahzaabu,
Ayatul – kursiyi na Aya ya 54 katika surati A’raafu na Aya tatu za sura-
tul Baqara bali amsomee kila atachoweza katika Qur;an ili apate kus-
tarehe.
443. Ni makuruhu kumuacha muhtadhari peke yake, vile vile ni makuruhu
kumwekea kitu kizito juu ya tumbo, pia ni makuruhu kwa wenye
janaba na wenye hedhi kuhudhuria sehemu aliyopo muhtadhari,
kuongea, kulia sana, pia ni makuruhu wanawake kuachwa peke yao
sehemu aliyopo muhtadhari.
HUKUMU BAADA YA MAUTI
444. Ni sunna baada ya kufa kufumbwa macho ya maiti, mdomo wake na
kunyooshwa mikono yake na miguu yake, kisha afunikwe kwa shuka,
na kama atafariki usiku ni sunna kuwashwa taa katika sehemu
ambayo maiti ipo, pia waumini wapewe taarifa ili waje wasindikize
jeneza na wafanye haraka kuzika, lakini ni wajibu wasubiri mpaka
wapate yakini kuwa amefariki, vile vile ni wajibu kuchelewesha kuzi-
ka kama maiti ni mwanamke mweye mimba, na tumboni kwake kuna
mtoto hai apasuliwe upande wa kushoto kisha mtoto atolewe na
washone.
446.Ni wajibu wa kila mwislamu balaghe kuosha maiti ya mwiislamu, kui-
kafini, kuiswalia na kuizika hata kama maiti sio ya mwinathna
Asharia, na kama baadhi watafanya mambo haya basi haitakuwa waji-
89
Al-Masailul Islamiyah
Page 104
bu kwa wengine.
Kama mtu ataanza kumwandaa maiti sio lazima kwa watu wengine kufa-
nya hivyo, lakini kama hatakamilisha basi itakuwa ni wajibu kwa wengine
kukamilisha.
447. Kama mtu atakuwa na yakini kuwa fulani ana mwandaa maiti, sio
wajibu kwake kufanya maandalizi, lakini akishuku au akidhani hivyo
basi ni wajibu kwakwe afanye hivyo.
448. Kama atatambua kuwa maiti amekosewa kuoshwa, kukafiniwa,
kuzikwa au kuswaliwa, ni wajibu arudie hayo kwa mara nyingine,
lakini akishuku au akidhania kuwa mambo hayo sio sahihi, sio lazima
kwake kufanya bali ajaalie kuwa ni sahihi.
449. Ni wajibu kuchukua idhini kwa walii wa maiti ili kumuosha kumka-
fini, kumswalia na kumzika.
450. Walii wa mwanamke ni mume wake na baada yake ni wanaume
wanaomrithi maiti kwa utaratibu uliopo katika mirathi.
451. Kama mtu atasema mimi ni walii au walii wa maiti au walii wa maiti
amenipa idhini ya kuosha maiti, kukafini na kuzika, kama watu
wataamini maneno yake na hakuna mtu aliyedai hivyo, basi ataachi-
wa afanye hivyo.
452. Mtu kama atabainisha mtu wa kumuosha kabla hajafa, kumkafini,
kumswalia na kumzika basi kwa tahadhari ya sunna achukue idhini
ya walii wa maiti, na wala sio lazima kwa mtu aliyeidhinishwa na
maiti kwa ajili ya maandalizi yake kukubaliwa wasia wake, lakini
wasia ukikubaliwa ni wajibu afanye hivyo.
HUKUMU ZA KUOSHA MAITI
90
Al-Masailul Islamiyah
Page 105
453. Ni wajibu kuosha maiti josho tatu:-
Kwa maji yaliyochanganywa na sidri “majani ya mkunazi”
Kwa maji yaliyochanganywa na kafuri “karafuu maiti”
Kwa maji halisi.
454. Ni wajibu sidri na kafuri zisiwe nyingi sana mpaka kufanya maji
kuwa mudhafu vile vile ni wajibu zisiwe chache sana.
455. Kama sidri na kafuri haitoshi kwa kiwango kinachotakikana basi kwa
tahadhari ya wajibu ichanganywe na maji kiasi.
456. Mtu aliyevaa ihramu kwa ajili ya hija au umra kisha akafariki kabla
ya kukamilisha twawafu ya hija ni wajibu asioshwe na maji yaliy-
ochanganywa na kafuri, badala yake ataoshwa na maji halisi
457. Kama itakosekana kafuri na sidri au moja wapo au zikawa za wizi,
basi ni wajibu maiti aoshwe badala ya kila josho kwa maji halisi.
458.Ni wajibu anayeosha maiti awe ni muislamu wa madhehebu ya Shia
Ithinasharia, awe amebaleghe, awe na akili timamu, awe anajua
mas’ala ya kuosha pamoja na hukumu zake kama maiti hatakuwa ni
shia ithina asharia basi sio lazima kwa anayeosha kuwa ni shia ithi-
nasharia.
459. Ni wajibu kwa muoshaji akusudie kujikurubisha kwa Allah (swt)
wakati wa kuosha, yaani aoshe maiti kwa kujikurubisha kwa Allah
(swt) na kutekeleza amri yake (swt)
460. Ni wajibu maiti ya mtoto mwislamu ioshwe hata kama ni mtoto wa
zinaa, ama kuoshwa kwa kafiri na watoto wake kukafiniwa na kuzik-
wa haijathibiti katika sharia, mtu ambaye alikuwa na kichaa kuanzia
utotoni mpaka akabaleghe ni lazima aoshwe kama wazazi wake ni
waislamu au mmoja wao, lakini kama wote sio waislamu haijuzu
91
Al-Masailul Islamiyah
Page 106
kuoshwa.
461.Ni wajibu kuosha kichanga chenye umri wa miezi minne au zaidi, laki-
ni kama kina umri chini ya miezi minne basi ni lazima afungwe na
kitambaa na azikwe bila ya kuoshwa.
462.Inajuzu kwa mwanaume kuosha maiti ya binti mwenye umri chini ya
miaka mitatu, vilevile inajuzu kwa mwanamke kuosha maiti ya mtoto
wa kiume ambaye umri wake haujavuka miaka mitatu.
463.Ni haramu kwa mwanaume kuosha maiti ya mwanamke, vilevile ni
haramu kwa mwanamke kuosha maiti ya mwanaume, lakini inajuzu
kwa mwanamke kuosha maiti ya mume wake, na mume pia kuosha
maiti ya mke wake, japo kwa tahadhari ya sunna mwanamke asimu-
oshe mume wake na mwanaume asimuoshe mke wake.
464. Kama hatopatikana mwanaume wa kuosha maiti ya mwanaume basi
inajuzu kwa mama yake, dada yake, shangazi yake, mama mdogo au
mkubwa wamuoshe.
465. Ni bora mwili wa maiti usifunikwe wakati wa kuoshwa isipokuwa
sehemu za siri ikiwa waoshaji na maiti ni jinsia moja.
466. Ni haramu kuangalia uchi wa maiti ila kwa mume na mke inajuzu
kuangalia na kama muosha maiti ataangalia uchi wa maiti atapata
dhambi, lakini haibatilishi josho la maiti.
467.Kama kuna sehemu najisi katika mwili wa maiti ni lazima itoharishwe
kabla hajaoshwa, na kwa tahadhari ya sunna mwili wa maiti wote uwe
na tohara kabla ya kuoshwa.
458.Namna yan kuosha maiti ni kama namna ya kuoga janaba kwa utarat-
ibu, na kwa tahadhari ya wajibu maiti asioshwe josho la kuzama, ikiwa
josho la utaratibu unawezekana.
92
Al-Masailul Islamiyah
Page 107
469. Mtu akifa akiwa na janaba au hedhi sio lazima aoshwe josho la jana-
ba au la hedhi, bali inatosha aoshwe josho la maiti tu.
470. Sio haramu kuchukua malipo kwa ajili ya kuosha maiti ikiwa ni kwa
ajili ya kulingania, vinginevyo ni wajibu kutochukua, na kama ata-
muosha maiti kwa lengo la kuchukua malipo josho halitabatilika,
lakini sio haramu kuchukua malipo kwa ajili ya baadhi ya vitu kama
vile kuleta maji, sidri (majani ya mkunazi) au kafuri maiti.
471. Kama hakuna maji ya kuoshea maiti au kuna kizuizi cha kutumia maji
basi inatosha kumtayamimisha maiti, tayamamu moja badala ya josho
zote tatu, japo ni kwa tahadhari ya sunna kumtayamimisha tayamamu
tatu, kila tayamamu badala ya josho moja.
472. Katika kumtayamimisha maiti ni wajibu kwa aliye hai kupiga ardhi
kisha apake uso wa maiti na apake migongo ya viganja vya maiti.
HUKUMU ZA KUMKAFINI MAITI
473. Ni wajibu kumkafini maiti mwislamu kwa vipande vitatu vya nguo.
474. Kipande cha kwanza ni wajibu kianzie kwenye kitovu mpaka kwenye
magoti, lakini ni bora zaidi kianzie kifuani mpaka kwenye nyayo, na
cha pili ni wajibu kianzie mabegani mpaka kwenye miundi, na ni bora
mpaka kwenye nyayo, na cha tatu ni wajibu kiwe kirefu zaidi kwa
kiasi kwamba kinaweza kufunika mwili wote kwa urefu na upana.
475. Mali ya kununulia sanda ya maiti inachukuliwa kwenye theluthi ya
mali yake.
476. Sanda ya mke ni juu ya mume wake hata kama mke ni tajiri, vile vile
ni wajibu kwa mume kumtolea sanda mke wake aliyempa talaka
rejea- kama yatakavyokuja maelezo yake katika hukumu za talaka -
93
Al-Masailul Islamiyah
Page 108
ikiwa atafariki kabla ya kumalizika eda yake, na ikiwa mume sio
baleghe au akiwa kichaa ni wajibu kwa walii wa mume kutoa sanda
kutoka katika mali ya anayemsimamia.
477. Sanda ya maiti sio wajibu kwa jamaa zake wa karibu.
478. Haijuzu kumkafini maiti na ngozi ya mzoga na sanda ya wizi hata
kama hakuna kitu kingine cha kumkafinia.
479. Haijuzu kumkafini maiti na sanda yenye najisi, hariri na kitambaa
kilichochovya dhahabu, ila katika dharura.
480. Haijuzu kumkafini maiti na sufi au nywele za mnyama ambaye ni
haramu kuliwa.
481. Kama sanda itanajisika na najisi ya maiti au na najisi nyingine, ni
wajibu itoharishwe au ikatwe sehemu yenye najisi hata kama maiti
atakuwa amewekwa kaburini, na kama haitawezekana kutoharishwa
au kukatwa ni wajibu abadilishiwe sanda nyingine ikiwezekana.
482. Mtu akihirimia kwa ajili ya Hija au Umra kisha akafa ni wajibu
akafiniwe kama wengine, wala hakutakuwa na tatizo kufunika uso na
kichwa.
483. Ni sunna kwa mtu wakati wa uhai wake kuandaa sanda, sidri na kafu-
ri (kwa ajili yake pindi atakapo kufa).
HUKUMU ZA TAHANITI “KUPAKA”
94
Al-Masailul Islamiyah
Page 109
484. Ni wajibu kumpaka maiti kafuri maiti katika viungo vyake vya kusu-
judi
baada ya kumuosha.
485. Ni kwa tahadhari ya wajibu kupaka kafuri kuanzia paji la uso, kigan-
ja cha kulia na cha kushoto, goti la kulia na la kushoto, kidole gumba
cha kulia na cha kushoto.
486. Ni bora kumpaka maiti kafuri kabla ya kumkafini.
487. Mtu akihirimia Hija au Umra, kisha akifa kabla ya kumaliza sa’ayi na
kunyoa haijuzu kumpaka kafuri.
488.Mwanamke ambaye amefiwa na mume wake, kama akifa kabla ya
kumaliza eda basi ni wajibu apakwe kafuri.
489.Kama kafuri haitapatikana ya kutosha basi sio lazima kupakwa.
HUKUMU ZA SWALA YA MAITI
490. Ni wajibu kumswalia maiti hata kama ni mtoto, kama wazazi wake ni
waislamu au mmoja wao ni mwislamu na awe maiti huyo ametimiza
umri wa miaka sita.
491. Ni wajibu kumswalia maiti, baada ya kuoshwa, kupakwa kafuri na
kukafiniwa.
492. Sio lazima kwa anayetaka kuswali swala ya maiti awe na udhu au
aoge au atayamamu, japo ni bora awe na udhu au aoge na atayama-
mu.
493. Ni wajibu kwa anayetaka kuswali swala ya maiti aelekee kibla, kama
ilivyo wajibu kumlaza maiti kwa mgongo, kichwa chake kiwe upan-
95
Al-Masailul Islamiyah
Page 110
de wa kulia wa mwenye kuswali na miguu yake iwe upande wa
kushoto wa mwenye kuswali.
494. Ni wajibu sehemu anayoswaliwa maiti isiwe ya kunyang’anya, pia ni
wajibu sehemu ya mwenye kumswalia isiwe juu zaidi ya sehemu ya
maiti.
495. Ni wajibu kwa mwenye kuswalia maiti asiwe mbali na maiti, lakini
kama maiti anaswaliwa jamaa hakuna tatizo mtu kuwa mbali na maiti,
kwa sharti safu za jamaa ziwe zimeungana.
496. Ni wajibu pasiwe na kizuizi baina ya maiti na mwenye kumswalia,
lakini hakuna tatizo kama maiti itakuwa kwenye sanduku n.k.
497. Ni wajibu mwenye kuswali swala ya maiti asimame usawa wa maiti,
lakini hakuna tatizo kwa mwenye kuswali jamaa kusimama pembeni
mwa maiti.
498. Ni wajibu kusitiri sehemu za siri za maiti wakati wa kumswalia, na
kama itashindikana kukafiniwa basi ni wajibu kusitiri sehemu za siri
hata kama ni kwa ubao au jiwe n.k.
499. Ni wajibu kuswali swala ya maiti kwa kusimama na iwe ni kwa ajili
ya kujikurubisha kwa Allah, na kubainisha katika nia maiti unayem-
swalia.
500. Mtu ambaye hawezi kuswali swala ya maiti kwa kusimama inajuzu
kuswali akiwa amekaa.
501. Ni makuruhu kurudia rudia kuswali swala ya maiti mmoja, lakini
hakuna karaha kurudiarudia kuswali swala ya maiti ya mwenye elimu
au mcha Mungu.
96
Al-Masailul Islamiyah
Page 111
502. Kama maiti itazikwa bila ya kuswaliwa kwa makusudi au kwa kusa-
hau au kwa udhuru au ikijulikana baada ya kuzikwa kuwa swala ili-
kuwa ni batili, basi ni wajibu kuswali swala ya maiti, maiti akiwa
kaburini maadamu kaburi halijafutika kabisa.
NAMNA YA KUSWALI SWALA YA MAITI
503. Swala ya maiti ina takbira tano.
Takbira ya kwanza: Baada ya nia anasema “Ash hadu an laa ilaaha ila
llahu wa anna Muhammadan rasulullah”
Takbira ya pili anasema: Allahumma swali alaa Muhammad wa Aali
Muhammad waswali alaa jami’il – ambiyaai wal mursaliina”
Takbira ya tatu atasema: “ Allahumma ighfir lil muuminina wal muumi-
naat”
Takbira ya nne atasema: “Allahumma ighfir lihaadhal mayit” kama ni
mwanaume na akiwa mwanamke anasema “ Allahumma ighfir lihaadhihil
mayitah” kisha analeta takibira ya tano na swala inamalizika.
Katika takbira ya nne ikiwa maiti ni mtoto atasema: “ Allahumma ij’alhu
liabawayhi walanaa salafan wafartwan waajran” na kama hali yake haiju-
likani kuwa ni mwanaume au ni mwanamke atasema: “ Allahumma ighfir
liladhiyna tabuu watabi’u sabiylaka waqihim adhabal jahiym” na kama ni
mnafiki atalaaniwa katika takbira ya nne.
504. Ni wajibu kusoma takbira na dua kwa kufuatiliza ili hali swala isiha-
ribike.
505. Ni lazima kwa maamuma katika swala ya maiti naye asome takbira na
dua haitoshelezi Imamu peke yake kusoma.
97
Al-Masailul Islamiyah
Page 112
506. Sio sharti kuwa na tohara wakati wa kuswali swala ya maiti, bali
inajuzu kwa mwenye kuswali, kuswali bila ya udhu na kuoga.
MAMBO YA SUNNA KATIKA SWALA YA MAITI:-
Mwenye kuswali awe na udhu, au aoge au atayamamu.
Imamu asimame usawa wa maiti wakati wa kumswalia maiti, na kama mtu
atamswalia furada pia asimame katikati ikiwa maiti ni mwanaume, ikiwa
maiti ni mwanamke asimame usawa wa kifua cha maiti.
Mwenye kuswali asiwe amevaa viatu.
Anyanyue mikono kila anaposoma takbira.
Mwenye kuswali asimame karibu sana na maiti, kwa kiasi upepo ukitikisa
nguo yake inaweza kugusa jeneza.
Ni sunna swala ya maiti kuswaliwa jamaa.
Imamu wa jamaa asome takibira na dua kwa sauti na maamuma wasisome
kwa sauti.
Maamuma asimame nyuma ya Imamu hata kama ni mmoja.
Amuombee maiti na waumini msamaha kwa Allah (swt) kwa wingi.
10.Aseme kabla ya swala “Aswalaatus swalaat, swalaat” mara tatu(badala
ya kukimu).
11.Swala ya maiti iswaliwe katika sehemu ambayo watu wamezoea
kuswalia maiti mara kwa mara.
12.Mwanamke mwenye hedhi akitaka kuswali swala ya maiti asimame
98
Al-Masailul Islamiyah
Page 113
nyuma peke yake.
507. Inasihi kuswali swala ya maiti msikitini, na ingawa ni makuruhu laki-
ni sio makuruhu katika msikiti mtukufu wa Makka.
HUKUMU ZA KUZIKA
508.Ni wajibu maiti izikwe kwa kiasi kwamba harufu isienee, na wanya-
ma wasiweze kutoa mwili ndani ya ardhi, na kama itahofiwa kuwa
wanyama watafukua maiti basi ni lazima kaburi lijengewe.
509. Kama haiwezekani maiti kuzikwa, inajuzu kuwekwa kwenye jengo
au sanduku badala ya kuzikwa.
510. Ni wajibu maiti alazwe kwa upande wa kulia ili sehemu ya mbele
ielekee kibla
511. Kama mtu atafia kwenye meli ikawa mwili hautoharibika itabidi izik-
we ardhini na kama mwili utaharibika itabidi afungiwe kitu kizito
kisha izamishwe ndani ya maji
512. Mwanamke kafiri akifa na mtoto akafia tumboni au ikiwa bado
hajawa na uhai, kama baba wa mtoto ni mwislamu basi ni wajibu
mwanamke azikwe kwa kulazwa kwa upande wa kushoto ili mtoto
aliye tumboni aelekee kibla.
513. Haijuzu mwislamu kuzikwa katika makaburi ya makafiri, na haijuzu
kafiri kuzikwa katika makaburi ya waislamu.
514. Haijuzu kuzika mwislamu katika sehemu ambayo inasababisha
udhalili mfano, katika sehemu ambayo uchafu unatupwa.
99
Al-Masailul Islamiyah
Page 114
515. Haijuzu kuzika katika ardhi ya kunyang’anya au waqfu, mfano ardhi
ya msikiti.
516. Haijuzu kuzika katika kaburi lingine, isipokuwa liwe ni la zamani
sana na limekwisha.
517. Sehemu yoyote ya mwili ikitengana na mwili ni lazima izikwe pamo-
ja na mwili, ni sunna katika uhai wa mtu anapokata kucha au kung’o-
ka meno ayazike.
518. Kama mtu atafia ndani ya kisima na haiwezekani kutolewa, basi ni
wajibu kisima kifukiwe na kuwa kaburi lake.
519. Kama mtoto atafia tumboni na kubakia kwake tumboni kukawa ni
hatari kwa maisha ya mama yake ni wajibu atolewe haraka.
520. Mwenye mimba akifariki na mtoto tumboni yuko hai ni wajibu apa-
suliwe upande wa kushoto kisha mtoto atolewe na kisha ashonwe
MAMBO YALIYO SUNN KATIKA KUZIKA
521.Ni sunna kuchimba kaburi sawa na urefu wa mtu wa kawaida
522. Ni sunna kuchimba kaburi kwa mustatili, na kuwekwa alama juu yake
ili kutofautisha na makaburi mengine, baada ya kumaliza kuzika ni
sunna kumwagia maji juu ya kaburi na kuweka vidole kaburini kisha
unasoma suratul Qadri mara saba na kumuombea msamaha maiti.
523. Ni sunna kubeba maiti ndani ya jeneza na kumwingiza kaburini tarat-
ibu na kusoma dua zilizopokelewa (kwenye kitabu) kabla ya kuzika
na baada ya kuzika, na kufungua sanda, baada ya kuwekwa katika
mwanandani shavu la maiti liwekwe juu ya ardhi na chini ya kichwa
chake pawekwe udongo, na kuwekwa udongo au tofali nyuma ya
mgongo wake ili asirudi nyuma, na kulala chali, na kabla ya kufuni-
100
Al-Masailul Islamiyah
Page 115
ka mwanandani mzikaji apige bega la kulia la maiti, na anaweka
mkono wake wa kushoto juu ya bega la kushoto la maiti, na mdomo
wake ukaribie sikio la maiti, na kumtikisa kwa nguvu, kisha asome
talakini “talakini itakuja mwisho wakitabu Inshaallah.”
524.Ni sunna kuomboleza baada ya kuzika lakini kama muda umepita sana
ni bora kuacha kuomboleza ili usifanye msiba kurudia upya, ni sunna
kupeleka chakula kwenye nyumba ya msiba kwa muda wa siku tatu.
525. Ni sunna kwa mtu kufanya subira anapofiwa na jamaa zake wa
karibu, hasa anapofiwa na mtoto wake, ni sunna kusema “Innaa lilaah
wainnaa ilaihi raajiuuna” ni sunna kumsomea maiti Qu’ran tukufu na
kumwomba Allah haja zako katika kaburi la baba yako na la mama
yako, pia ni sunna kulijengea ili lisiharibike.
526 .Haijuzu kwa mtu kujirarua katika msiba, isipokuwa katika misiba ya
maasumina inajuzu kila aina ya maombolezo.
527. Haijuzu kupasua mifuko katika misiba isipokuwa katika msiba wa
baba na wa kaka, japokuwa ni bora kuacha pia.
528. Mwanamke kama atajirarua uso wake au akang’oa unywele wake basi
ni wajibu wake aache mtumwa huru, au alishe mafakiri kumi au
awape mavazi, na vile vile kwa mwanaume kama atachana mfuko au
nguo zake katika msiba wa mke wake au mtoto wake.
529. Ni bora kufanya tahadhari kutolia kwa sauti, lakini misiba ya maa-
sumini inajuzu kulia kwa sauti
SWALA YA WAHSHA
530. Ni sunna kuswali swala ya wahsha kwa ajili ya maiti baada ya kuzi-
101
Al-Masailul Islamiyah
Page 116
ka kwa usiku wake, ni rakaa mbili unasoma katika rakaa ya kwanza
baada ya Al-hamdu ayatul kursiyi, mara moja, na katika rakaa ya pili
unasoma baada ya Al-hamdu suratul- Qadir mara kumi, na baada ya
swala unasoma Allahumma Swali alaa Muhammadi Waali
Muhammad, wab’athi thawabahaa ilaa Qabri Fulani na ni bora utaje
jina la maiti(mahala pa fulani).
531. Kama maiti atacheleweshwa kuzikwa au atapelekwa nchi nyingine,
basi swala ya wahsha isicheleweshwe mpaka usiku atakaozikwa
Kufukua kaburi
532. Ni haramu kufukua kaburi la mwislamu hata kama liwe ni la mtoto au
kichaa, lakini hakuna tatizo ikiwa mwili umekwisha kabisa na kuwa
udongo.
533. Ni haramu kufukua makaburi ya manabii, maimamu, watoto wao
mashahidi maulamaa, na watu wema hata kama imepita miaka mingi.
538. Sio haramu kufukua kaburi kwa mambo yafuatayo:-
Kama maiti atazikwa katika sehemu ya kunya’nganya na mwenyewe
hajaridhia kuzikwa maiti hapo.
Kama maiti atakafiniwa na sanda ya kunyang’anganya na mwenyewe
hajaridhika.
Kama maiti atazikwa bila kuoshwa au kukafiniwa au akioshwa kimakosa
au hajaelekezwa kibla.
Kama kuna haja ya kumuona maiti ili kuthibitisha haki.
Kama atazikwa katika sehemu inayo sababisha kudhalilika, mfano katika
102
Al-Masailul Islamiyah
Page 117
makaburi ya makafiri au katika sehemu ya kutupia takataka.
Kama kufukuliwa kaburi ni kwa ajili ya jambo la kisharia muhimu zaidi
kuliko uharamu wa kufukua kaburi, mfano kutolewa mtoto hai aliye tum-
boni mwa mama yake aliyezikwa naye.
Ikiogopewa kuwa wanyama watafukua na kuitoa maiti nje ya kaburi au ita-
sombwa na maji au adui ataichukua.
Kama maiti hajazikwa pamoja na sehemu ya mwili wake iliyojitenga naye
na ikatakiwa kuzikwa pamoja naye, lakini kwa tahadhari ya wajibu sehe-
mu hiyo iwekwe bila ya kuonekana mwili wa maiti
Josho za sunna
539. Josho la Ijumaa: Wakati wake ni kuanzia adhana ya alfajiri mpaka
adhuhuri ya siku ya Ijumaa, na ni bora kuoga adhuhuri ikikaribia
Josho la mwanzo wa usiku wa kwanza wa Ramadhani, na kila usiku wa
witiri, mfano usiku wa tatu, wa tano, wa saba na wa tisa.
Ni sunna kuoga kuanzia usiku wa ishirini na moja mpaka mwisho wa
Ramadhani, sunna hii imetiwa mkazo zaidi katika usiku wa kwanza, usiku
wa kumi na tano, usiku wa kumi na saba, usiku wa kumi na tisa, usiku wa
ishirini na moja, usiku wa ishirini na tatu, usiku wa ishirini na tano, usiku
wa ishirini na saba, usiku wa ishirini na tisa katika mwezi wa Ramdhani
mtukufu.
Josho la siku ya Iddul -fitri na Iddul - Adhuha, na wakati wake ni kuanzia
adhana ya alfajiri mpaka magharibi, lakini ni bora kuoga kabla ya swala
ya Idd.
Josho la usiku wa kuamkia siku ya Idd ndogo na kubwa.
103
Al-Masailul Islamiyah
Page 118
Josho la siku ya nane na ya tisa katika mwezi wa Dhul Hija, na ni bora
kuoga siku ya tisa kabla ya Adhuhuri.
Josho la siku ya kwanza, siku ya kumi na tano, siku ya ishirini na saba, na
siku ya mwisho katika siku ya mwezi wa Rajab.
Josho la siku ya Iddul - Ghadiri na ni bora kuoga kabla ya Adhuhuri
Josho la siku ya nne na siku ya ishirini katika mwezi wa Dhul -Hija.
Josho la siku ya Nairuzi, siku ya kumi na tano ya mwezi wa shambani na
siku ya tisa na siku ya kumi na saba ya mwezi na Rabiul-awal na siku ya
ishirini na tano ya mwezi wa Dhul Qa’ad.
Kuosha mtoto anapozaliwa.
Mwanamke kuoga baada ya kutumia manukato ambayo sio ya mume
wake.
Kuoga kwa mtu ambaye amekunywa pombe na akalala akiwa amelewa.
Kuoga josho la kugusa maiti ambaye hajaoshwa.
Josho la mtu ambaye hajaswali swala ya majanga kwa makusudi, hasa
swala ya kupatwa kwa jua na mwezi.
540. Ni sunna kuoga kwa mtu ambaye ameenda kuona mtu aliyesulubiwa,
lakini akimuona ghafla au ikiwa ameenda kutoa ushahidi sio lazima
kuoga.
541. Ni sunna kuoga kabla ya kuingia Makka, Msikiti mtukufu wa
Makka, Ka’aba, tukufu, na katika mji wa Madinatul Munawara, na
katika msikiti wa Mtume (saww) na katika sehemu takatifu za maima-
mu na ni sunna kuoga kwa ajili ya Ihramu.
542. Ni sunna kuoga kwa ajili ya kuwazuru Maimamu watukufu (as) iwe
104
Al-Masailul Islamiyah
Page 119
kwa mbali au kwa karibu, na ni sunna kuoga kwa ajili ya kuomba haja
zako kwa Allah (swt), vile vile ni sunna kuoga kwa ajili ya kutubu na
kupata uchangamfu wa ibada.
543. Kama ikiwajibika kwa mtu kuoga josho nyingi za wajibu au baadhi
yake ni wajibu inatosha kuoga josho moja kwa nia ya josho zote.
TAYAMAMU
544. Ni wajibu kutayamamu badala ya kutawadha na kuoga katika
mambo saba:-
Kukosekana maji
Kama hutaweza kufika yaliko maji
Ikiwa maji yanamdhuru
Akihofia kiu
Maji aliyonayo kutotosha isipokuwa kutoharisha mwili na nguo
Maji yakiwa sio halali
Wakati wa swala ukiwa mfinyu.
Jambo la kwanza:
545.Mtu akiwa nyumbani ni wajibu atafute maji hadi akate tamaa, ndio
atayamamu.
546. Kama mtu ataacha kutafuta maji mpaka wakati wa swala ukabakia
mfinyu kisha akatayamamu, atakuwa ameasi lakini swala yake
itakuwa sahihi.
547. Mtu kama ana maji yanayotosha kutawadha au kuoga, na akajua
kuwa akiyamwaga hatapata maji, kama itakuwa ndani ya wakati wa
swala, basi ni haramu kuyamwaga, pia ni bora asiyamwage kabla ya
wakati wa swala
105
Al-Masailul Islamiyah
Page 120
548. Mtu akijua kama hatapata maji kisha akabatilisha udhu wake baada
ya kuingia wakati wa swala, au akamwaga maji baada ya kuingia
wakati wa swala, atakuwa ameasi na kupata dhambi lakini swala
yake itasihi akitayamamu.
Jambo la pili:
549. Kama hutaweza kufika katika sehemu ambayo ina maji kwa sababu
ya uzee, basi ni wajibu utayamamu, pia ni wajibu utayamamu kama
kutumia maji kuna kudhuru.
550. Kama italazimika kununua ndoo au kamba ya kuvutia maji au
kukodisha basi ni wajibu anunue au akodishe.
551. Kama mtu hatapata maji mpaka akope hela za kununulia maji, basi ni
wajibu akope ili anunue maji.
552. Kama kuchimba kisima hakumpatii taabu basi ni wajibu achimbe illi
apate maji
553. Kama mtu atakupa maji bila masimango huna budi kuyachukua na
kutawadhia, lakini kama kuna masimango ni lazima usiyachukue
Jambo la tatu:
554. Akihofia kwamba kutumia maji kutamdhuru au akihofia maradhi
yake yatachukua muda mrefu au yatazidi au itakuwa vigumu kutibika
kwa sababu ya kutumia maji, basi ni wajibu atayamamu, lakini kama
maji yaliyochemshwa hayamdhuru ni wajibu atawadhe au aoge kwa
kutumia maji ya moto.
555. Sio lazima apate yakini kuwa maji yatamdhuru, bali hata akidhania
kuwa maji yatamdhuru na akawa na hofu basi ni wajibu atayamamu.
106
Al-Masailul Islamiyah
Page 121
556. Mwenye ugonjwa wa macho kama maji yanamdhuru ni wajibu ataya-
mamu.
557. Kama atatayamamu kwa sababu ya kuwa na yakini kuwa maji
yatamdhuru, kisha akatambua kabla ya swala kuwa maji hayamdhu-
ru, tayamamu yake itabatilika, na akijua hivyo baada ya swala ni bora
arudie swala yake akiwa na udhu au aoge, na alipe ikiwa wakati
umepita.
558. Mtu akijua kuwa maji hayamdhuru kama ataoga au kutawadha, kisha
akajua baadae kuwa maji yanamdhuru basi josho lake na udhu wake
utasihi.
Jambo la nne:
559. Kama akihofia kutumia maji katika kutawadhia au kuogea atakufa
yeye au familia yake au rafiki yake au mtumishi, au kila aliye wajibu
kwake kuokoa maisha yake kutokana na kiu kali, basi ni wajibu ataya-
mamu badala ya kutawadha au kuoga.
560. Kama ana maji yaliyonajisika yanatosha kunywa yeye na familia yake
na yaliyotohara kwa ajili ya udhu au kuoga, basi ni wajibu maji yaliy-
otohara yawe ni ya kunywa na atayamamu kwa ajili ya swala, na aki-
taka kumnywesha mnyama wake maji amnyweshe maji yaliyonajisi-
ka.
Jambo la tano:
561. Kama mwili au nguo ikinajisika na maji aliyonayo ni machache,
mfano akitawadhia au kuogea hayatabaki, basi ni wajibu kwake ato-
harishe nguo au mwili wake kwa hayo maji kisha atayamamu kwa
ajili ya swala.
107
Al-Masailul Islamiyah
Page 122
Jambo la sita:
562. Kama ana maji au chombo ambacho ni haramu kutumia, mfano maji
au chombo cha kunyang’anya basi ni wajibu atayamamu badala ya
kuoga au kutawadha.
563. Kama wakati wa swala utakuwa mfinyu kama akitawadha au kuoga
swala yote itakuwa nje ya wakati au baadhi, basi ni wajibu atayama-
mu.
Jambo la saba:
564. Kama atachelewesha swala kwa makusudi mpaka wakati ukawa hau-
toshi kutawadha au kuoga, atakuwa ameasi na kupata dhambi lakini
swala yake itakuwa sahihi.
565. Kama akishuku kuwa je wakati utabakia kwa ajili ya swala kama
atatawadha au kuoga, basi ni wajibu atawadhe au aoge.
Vitu ambavyo inasihi kutayamamu
566. Inasihi kutayamamu kwa udongo, mchanga na changarawe, yaani
vipande vipande vya udongo au vya mawe.
567. Inasihi kutayamamu kwa kutumia ukuta wa udongo, na ni bora
kuchukua tahadhari usitayamamu na ardhi au udongo mbichi na
wakati huo huo kuna mkavu.
Namna ya kutayamamu badala ya udhuNia.
Kupiga kwa viganja viwili kwa pamoja juu ya kitu ambacho kinasihi
kutayamamia
108
Al-Masailul Islamiyah
Page 123
Kupaka paji la uso lote kwa viganja viwili kwa kuanzia kwenye maoteo ya
nywele mpaka juu ya pua.
Kupaka juu ya kiganja cha kulia kwa tumbo la kiganja cha mkono wa
kushoto kisha kupaka juu ya kiganja cha kushoto kwa tumbo la kiganja cha
mkono wa kulia, kuanzia kwenye vifundo mpaka kwenye ncha za vidole.
Namna ya kutayamamu badala ya kuoga
Katika tayamamu badala ya kuoga atanuia na kupiga ardhi kwa viganja
vyake kisha anapaka paji la uso, kisha atapaka mgongo wa kiganja cha
mkono wa kulia, kisha atapaka mgongo wa kiganja cha mkono wa
kushoto, kisha atapiga udongo tena na kupaka viganja vya mikono yake
kama ilivyotangulia.
Hukumu za kutayamamu
568. Ni wajibu kupaka paji la uso na mikono kwa kuanzia juu na kupele-
ka chini, na ni wajibu kutayamamu kwa kufuatilizia kiungo hadi kiun-
go kingine.
569. Ni wajibu wakati wa kutayamamu kubainisha nia kuwa unatayamamu
badala ya udhu au kuoga, pia ni wajibu kubainisha kuwa unatayama-
mu badala ya josho gani, josho la janaba au josho la hedhi n.k.
570. Ni wajibu wakati wa kutayamamu paji la uso na viganja vya mkono
viwe tohara.
571. Mtu ambaye hawezi kutayamamu mwenyewe ni wajibu atayaya-
mamishwe.
572. Mtu ambaye ametayamamu kwa sababu ya udhuru, kisha udhuru huo
109
Al-Masailul Islamiyah
Page 124
ukaondoka basi tayamamu yake itabatilika.
573. Mambo ambayo yanatengua udhu yanatengua tayamamu pia.
574.Mtu ambaye hawezi kuoga, kama akiwajibika kuoga josho nyingi basi
tayamamu moja inamtosheleza
HUKUMU ZA SWALA
575. Swala ni katika amali iliyo bora kabisa katika dini na iliyo na
umuhimu mkubwa, bali swala ni nguzo ya dini, kama swala yako
itakubaliwa basi amali zako zingine zitakubaliwa, na ikikataliwa na
amali zako zingine hazitakubaliwa, mfano wa swala ni sawa na mtu
anayeoga kila siku mara tano, ambaye uchafu hautabaki katika mwili
wake. Vile vile mtu akiswali swala tano za faradhi atatakasika
kutokana na madhambi na machafu.
Na inapasa kwa mtu kuziswali swala zake mwanzo wa nyakati zake na
mwenye kuzipuzia swala zake na kuzembea ni sawa na mtu asiyeswali,
na atastahili adhabu akhera.
Mtume (saww) amesema: “ Hayupo katika dini yangu mwenye kupuuzia
swala yake”. Na Mtume (saww) amesema: “Hatapata maombezi yangu
mwenye kupuuzia swala yake, na wala hataingia katika hodhi yangu”.
Siku moja Mtume (saww) alikuwa msikitini, akaingia mtu mmoja na
akawa akishughulika na kuswali, lakini bila ya kutimiza rukuu yake na
sijda yake. Mtume (saww) akasema: “Huyu anadonoadonoa kama kun-
guru, lau akifa na hii ndio swala yake atakufa nje ya dini yangu”.
Basi inamlazimu mtu adumishe swala zake sana asiziswali harakaharaka,
110
Al-Masailul Islamiyah
Page 125
na amnyenyekee Mola wake wakati wa swala, kwa hofu na heshima, na
ajue kwamba kuna ambaye anaongea nae ,na ajue kwamba yuko mbele
ya utukufu wa Mwenyezi Mungu na ufalme wake, awe dhalili na mnyonge,
na lau mwenye kuswali akiyajua haya wakati wa swala, basi nafsi yake
itayasahau mengine yote, na atajihisi kwamba yuko mbele ya Mwenyezi
Mungu (swt) kama ilivyotokea kwa kiongozi wetu Amirul Muuminina Ali
(as) walipoweza kumtoa mshale mguuni mwake bila ya yeye kuhisi wala
kutambua.
Hivi ndivyo yampasa mwenye kuswali atubie na kutaka istighifar kwa
Mola wake na kuelekea kwa Mola wake na kuacha madhambi na maasi
ambayo yanazuia kukubaliwa swala yake. Kama vile hasadi na kibri,
kusengenya, kula haramu na ulevi, na kuacha kuzuia kutoa khumsi na
zaka, bali kuacha maasi yote kwa ujumla. Pia yampasa aache vitendo
vyenye kupunguza thawabu za swala. Asisimame katika swala huku
akisinzia au akiswali huku akijizuia mkojo usimtoke au asiangalieangalie
juu, na hali yuko katika swala. Anatakiwa afanye vitendo vyenye
kumzidishia thawabu katika swala yake. Kama kuvaa pete ya akiki, kuvaa
nguo safi, kujipaka manukato, kupiga mswaki na kuchana nywele.
SWALA ZA WAJIBU576. Swala za wajibu ni:
1. Swala za kila siku
2. Swala za matukio (majanga)
3. Swala ya maiti
4. Swala ya tawafu ya wajibu ka’aba
5. Swala ya kuwalipia wazazi ambayo ni wajibu kwa mtoto mkub-
wa wa kiume
6. Swala inayokuwa wajibu kwa mtu kwa kuweka nadhiri au
ahadi au kiapo au kuajiriwa(kuswali kwa niaba ya mtu).
SWALA ZA WAJIBU ZA KILA SIKU
111
Al-Masailul Islamiyah
Page 126
577. Swala za wajibu za kila siku ni tano, swala ya Adhuhuri na Alasir,
kila moja ina rakaa nne, na swala ya magharibi yenye rakaa tatu, na
swala ya Isha yenye rakaa nne, na swala ya asubuhi yenye rakaa
mbili.
Ni wajibu kupunguza swala zenye rakaa nne katika safari kwa masharti
ambayo ufafanuzi wake utaelezwa. Na maana ya kupunguza ni kuziswali
swala zenye rakaa nne, rakaa mbili mbili.
WAKATI WA SWALA YA ADHUHURI
NA ALASIRI
578.Swala ya Adhuhur na Alasir zina wakati mahsusi, na zina wakati wa
kushirikiana, ama wakati ulio mahsusi kwa swala ya adhuhuri ni pale
linapopinduka jua mpaka unapomalizika muda wa kiwango cha
kuswali swala ya Adhuhur. Basi ikiwa mtu yeyote ataiswali swala ya
Alasiri katika wakati huu kwa kusahau, swala yake itakuwa ni
batili. Ama wakati mahsusi kwa swala ya Alasir ni ule uliobakia
mpaka kuzama jua kwa kiwango cha kuweza kuswali rakaa nne za
Alasiri, kama mtu hakuswali swala ya Adhuhuri mpaka wakati huu
basi swala yake itakuwa ni kadhaa na ni juu yake kuiswali swala ya
alasiri muda huu, kisha ailipe swala ya adhuhuri.
Ama wakati wakushirikiana baina ya Adhuhuri na Alasiri ni muda ulio
baina ya wakati mahsusi kwa swala ya adhuhuri, na muda mahsusi wa
swala ya alasiri kiasi kwamba akiiswali swala ya alasiri katika muda
huu wa kushirikiana kabla ya kuiswali swala ya adhuhuri kwa kusahau,
swala yake itasihi na itahesabika kuwa ameswali alasiri, na ni wajibu wake
kuiswali adhuhuri baada yake.
579. Mtu akishughulika na kuswali swala ya alasiri kabla ya kuiswali
swala ya adhuhuri kwa kusahau, kisha akafahamu katikati kwamba
112
Al-Masailul Islamiyah
Page 127
amekosea ikiwa hili litakuwa katika wakati wa kushirikiana baina ya
swala ya adhuhuri na alasiri ni wajibu kwake kubadili nia kwa kutia
nia ya swala ya adhuhuri, yaani yeye atanuia hali yuko katika swala
ya kwamba yote aliyofanya, na anayoyafanya sasa hivi na atakayoy-
afanya yatakuwa ni ya swala ya adhuhuri, na baada ya kukamilisha
swala ya adhuhuri, ataswali swala ya alasiri, ama ikiwa haya yote
aliyoyafanya ni katika wakati mahsusi kwa swala ya adhuhuri, basi
yote aliyoyafanya yatakuwa ni batili, sawasawa amefahamu makosa
yake katikati ya swala au baada ya swala.
WAKATI WA SWALA YA MAGHARIBI
NA ISHA
590. Magharibi huingia pale unapoondoka wekundu wa mashariki, nao ni
unaoonekana upande wa mashariki linapozama jua.
591. Kila swala ya magharibi na isha ina wakati wake mahsusi na zina
wakati wa kushirikiana baina ya swala hizi mbili. Ama wakati mah-
susi kwa swala ya magharibi ni mwanzo wa swala ya magharibi
mpaka kumalizika muda kwa kiwango cha kuiswali swala ya
magharibi, kiasi ambacho lau mtu msafiri akiswali swala ya isha
katika muda huu kwa kusahau swala yake itabatilika.
Ama wakati wa kushirikiana kati ya swala hizi mbili ni kati ya wakati
mahsusi kwa swala ya magharib na wakati mahsusi wa swala ya isha kiasi
kama mtu hakuiswali swala ya magharibi mpaka wakati huu itawajibi-
ka kuiswali swala ya isha kwanza kisha ataswali magharibi.
Ama wakati wa kushirikiana kati ya swala hizi mbili ni baina ya wakati
mahsusi kwa swala ya magharibi na wakati mahsusi kwa swala ya isha,
kiasi ambacho lau mtu akiiswali swala ya isha katika wakati huu wa
kushirikiana kabla ya kuswali magharibi kwa kusahau, kisha akafahamu
kuwa amekosea, swala yake itasihi na itamlazimu kuiswali swala ya
113
Al-Masailul Islamiyah
Page 128
magharibi baada ya hapo.
592. Muda mahsusi na wa kushirikiana tuliouelezea katika mas’ala yaliy-
otangulia, unatofautiana kulingana na watu, kuhusu msafiri lau
ukipita muda wa mwanzo wa adhuhuri kwa kiwango cha kuswali
rakaa mbili, basi unaingia muda wa kushirikiana, ama kuhusu mtu
ambaye si msafiri ni lazima kwake upite muda wa mwanzo wa
adhuhuri kwa kiasi cha kuswali rakaa nne ndio ufike muda wa
kushirikiana.
593. Ikiwa mtu atashughulika kwa swala ya isha kabla ya swala ya
magharibi kwa kusahau na akafahamu katikati ya swala kuwa
amekosea, ikiwa atakuwa ameiswali swala yote au baadhi yake kati-
ka muda wa kushirikiana na ikawa hakuingia katika rukuu ya rakaa
ya nne, itamuwajibikia kubadilisha nia yake kwenda katika swala ya
magharibi, na atazingatia aliyoyasoma na kuyafanya ni ya swala ya
magharibi na hivyo itambidi akae ikiwa alikuwa amesimama pasi na
kwenda kwenye rukuu ya rakaa ya nne na kukamilisha swala, kisha
ataswali swala ya isha baada ya hapo. Na ikiwa atakuwa amekwenda
kwenye rukuu ya rakaa ya nne ni wajibu kukamilisha swala kisha
ataswali swala ya magharibi baada ya hapo.
Ama akiiswali swala katika wakati mahsusi kwa swala ya magharibi,
kama lau akiwa ni msafiri na akaswali Qaswir, swala yake itabatilika na
atawajibika kuswali swala ya magharibi kisha swala ya isha kwa
mpangilio.
594. Muda wa mwisho wa swala ya isha ni katikati ya usiku, hivyo ni laz-
ima tuanze kuhesabu usiku pindi jua linapozama mpaka adhana ya
alfajiri na sio kwa kuchomoza jua. Mwisho wa muda wa swala ya
magharibi na isha kwa mtu mwenye dharura au aliyesahau au kwa
aliyekuwa amelala au aliyechelewesha swala yake kwa ajili ya hedhi
ni mpaka adhana ya alfajiri.
114
Al-Masailul Islamiyah
Page 129
595. Lau akichelewesha swala ya isha mpaka katikati ya usiku bila udhu-
ru, basi ni bora zaidi kuswali hata kabla ya swala ya alfajiri bila ya
nia ya adaai wala kadhaa
WAKATI WA SWALA YA ASUBUHI
596. Baada ya kutokeza weupe upande wa mashariki unaoelekea juu,
ambao unaitwa alfajiri ya mwanzo ya uongo, kisha weupe huu
hupanuka zaidi, wakati huo huwa alfajiri ya pili, “alfajiri ya kweli”
ama mwisho wa swala ya alfajiri ni kuchomoza kwa jua.
HUKUMU ZA WAKATI WA SWALA
597. Haijuzu kuanza kuswali mpaka uwe na uhakika wa kuingia muda wa
swala au baada ya kupewa tarifa na watu wawili waadilifu ya kuin-
gia wakati wa swala au kupata taarifa kwa mtu mmoja mwenye
kuaminika.
598. Ikiwa mtu hawezi kupata uhakika wa kuingia wakati wa swala kwa
kuwa yeye ni kipofu au kwa sababu ya mawingu au vumbi au kwa
sababu yuko ndani ya jela, ni wajibu kwake kuchelewesha swala
yake mpaka apate uhakika wa kuingia kwa wakati.
599. Ikiwa mtu atapewa taarifa na watu wawili waadilifu au akapata
uhakika mwenyewe wa kuingia wakati wa swala, akaanza kushughu-
lika na swala, kisha ikambainikia kwamba wakati wa swala bado
haujaingia basi swala yake itabatilika na vivyo hivyo itabatilika aki-
jua baada ya swala kwamba ameswali swala hiyo kabla ya kuingia
wakati, lakini akitambua kuingia wakati akiwa ndani ya swala, au
akatambua baada ya swala kwamba wakati wa swala umeingia na
yeye yuko ndani ya swala, swala yake itasihi.
115
Al-Masailul Islamiyah
Page 130
600. Ikiwa mtu atapata uhakika wa kuingia wakati wa swala na akaanza
kuswali, kisha akashuku na hali yuko ndani ya swala kuwa je wakati
umeingia au bado? Basi swala yake itakuwa na mushkeli, ama akiwa
na yakini wakati wa kuswali na ana uhakika wa kuingia wakati wa
swala itasihi, lakini akijua kuwa swala yote ameiswali nje ya wakati
au akiwa hajui kuwa ameiswali ndani ya wakati au nje ya wakati
swala yake itabatilika, bali hata akijua kwamba wakati umeingia
akiwa anaswali ni wajibu arudie swala kwa tahadhari.
601 Mtu ambaye ana muda wa kuweza kuswali rakaa moja, ni wajibu
kwake kuiswali swala kwa nia ya adaai, lakini haijuzu kwake
kuichelewa swala kwa makusudi mpaka muda uwe mfinyu namna
hii.
602.Mtu ambaye si msafiri ikiwa ana muda wa kuweza kuswali rakaa tano
kabla ya kuzama jua ni wajibu kuswali swala ya adhuhuri na alasiri
wakati huo, lakini ikiwa muda ni mchache zaidi ya huo, itamuwa-
jibikia kuswali swala ya alasir peke yake, kisha ataiswali adhuhuri
kadha na vivyo hivyo atakapobakiwa na muda wa kuswali rakaa nne
kufikia nusu ya usiku, itampasa kuswali magharibi na isha katika
muda huo, lakini muda ukiwa ni mchache zaidi ya huo, itambidi
kuswali isha peke yake, kisha baada ya hapo ataswali swala ya
magharibi kadhaa, ila mwenye dharura ameongezewa muda mpaka
adhana ya alfajiri.
603.Msafiri aliyebakiwa na muda wa kuweza kuswali rakaa tatu kabla ya
kuingia magharibi, ni wajibu kuiswali swala ya adhuhuri na alasiri
katika muda huo. Na ikiwa muda ni mchache zaidi ya huo itamuwa-
jibikia kuiswali alasiri peke yake kisha ataswali adhuhuri kadha, na
ikiwa mtu amebakiwa na muda wa kuswali rakaa nne tu na kuingia
nusu ya usiku ni wajibu kuswali magharibi na isha wakati huo ama
akibakiwa na muda wa kuweza kuswali rakaa moja au zaidi ya rakaa
moja ndio ifike katikati ya usiku itamuwajibikia kuswali magharibi
haraka kwa nia ya adaai.
116
Al-Masailul Islamiyah
Page 131
Ni sunna kwa mtu kuswali swala mwanzo wa wakati, na riwaya nyingi
zimepokelewa zikiusia jambo hili na kutilia mkazo sana na fadhila zina
kuwa nyingi zaidi kila swala inaposwaliwa mwanzo wa wakati wake ila
ikiwa kuchelewesha ni kwa ajili ya kutaka fadhila za kitu fulani, mfano
kusubiria mpaka aweze kuswali swala ya jamaa. Kama mtu ana udhuru
kiasi ambacho akitaka kuswali mwanzo wa wakati analazimika kutaya-
mamu kwa ajili ya swala au kuiswali swala kwa nguo iliyo na najisi,
ikiwa atajua kwamba udhuru wake utabakia mpaka mwisho wa wakati ita-
juzu kwake kuiswali swala mwanzo wa wakati, lakini akijua kuwa udhu-
ru wake utaondoka itamuwajibikia kusubiri mpaka udhuru wake uondoke
na kama udhuru wake haujaisha ataswali mwisho wa wakati, na wala hait-
omlazimu kusubiri kiasi cha kutokubakiwa na muda, ila kwa kiwango cha
kuweza kufanya wajibu wa swala bila ya mustahabu. Bali inajuzu
kuziswali swala katika muda wenye wasaa, ambapo anaweza kufanya
mustahabu mfano kuadhini, kukimu, kusoma kunuti pamoja na kutayama-
mu.
604. Mtu ambaye hajui taratibu za swala, hukumu za shaka na kusahau na
akashuku kuwa atatatizwa na moja wapo, ni wajibu kuchelewesha
swala yake mpaka mwisho wa wakati, ili aweze kujifunza lakini
akiwa na uhakika kwamba ataweza kukamilisha swala kwa njia sahi-
hi inajuzu kuswali mwanzo wa wakati, na kama hakutokewa na
mas’ala ambayo haelewi hukumu yake swala yake itasihi na aki-
tokewa na mas’ala ambayo hajui hukumu yake inajuzu afanye kwa
moja ya njia anazozijua na kukamilisha swala yake kisha ni wajibu
kwake kuuliza hukumu ile baada ya swala na kuirudia swala kama
aliiswali kinyume.
605. Ikiwa wakati wa swala ni mpana, na mwenye deni akamdai deni
lake ni wajibu kwake kumlipa deni lake kwanza kama itawezekana
kisha aendelee na swala, na vivyo hivyo ukimtokea wajibu mwingine
wa haraka, mfano akiona najisi msikitini, ni wajibu kusafisha msikiti
kwanza kisha ataswali na kama ataswali kwanza kisha aondoshe
117
Al-Masailul Islamiyah
Page 132
najisi atakuwa ametaasi, lakini swala yake itakuwa sahihi.
SWALA AMBAZO NI WAJIBU KUZISWALI
KWA MPANGILIO
606. Ni wajibu kuiswali swala ya alasiri baada ya swala ya adhuhuri na
swala ya isha baada aya swala ya magharibi, na kama ataswali alasiri
kabla ya adhuhuri au isha kabla ya magharibi kwa makusudi basi swala
yake itabatilika.
607. Akianza kuswali kwa nia ya swala ya adhuhuri na wakati huo
akakumbuka kuwa ameswali adhuhuri haijuzu kwake kubadilisha nia
kwenda kwenye swala ya alasir na vivyo hivyo hukumu ni hii kati-
ka swala ya magharibi na isha.
608. Akipata uhakika akiwa katika swala ya alasiri kwamba hajaswali
adhuhuri, basi ni wajibu kwake kubadilisha nia kwenda kwenye
swala ya adhuhuri na kama akikumbuka baada ya hapo kwamba
ameswali adhuhuri kabla, itamlazimu kubadili nia yake kwenda
kwenye swala ya alasiri na swala yake itasihi ikiwa hakufanya kitu
katika swala iliyotangulia, kwa kusudio mahsusi kwa ajili ya
adhuhuri.
609. Ikiwa atashuku akiwa katika swala ya alasiri kwamba ameswali
swala ya adhuhuri, au laa, ni wajibu abadili nia yake kwenda kwenye
swala ya adhuhuri kisha ataswali alasiri lakini ikiwa wakati ni
mfinyu sana kiasi ambacho lau atatimiza swala na kutaka kuswali
alasiri wakati wa magharibi utaingia, itamuwajibikia kukamilisha
swala kwa nia ya alasiri na kwa sura hii ni juu yake ailipe adhuhuri
118
Al-Masailul Islamiyah
Page 133
nje ya wakati kwa tahadhari.
610. Akishuku katika swala ya isha kabla ya kwenda rukuu ya rakaa ya
nne, kwamba ameswali magharibi kabla ya hapo au laa, ikiwa
wakati ni mfinyu kiasi ambacho lau akikamilisha swala itaingia
nusu ya usiku ni wajibu kukamilisha swala kwa nia ya isha, ama kama
wakati unawasaa inamuwajibikia kubadili nia kwenda swala ya
magharibi na kukamilisha rakaa tatu, kisha baada ya hapo ataswali
swala ya isha.
611. Akishuku ndani ya swala ya isha baada ya kufika kwenye rukuu ya
rakaa ya nne, kwamba ameswali magharibi kabla ya hapo au laa, ita-
muwajibikia kukamilisha swala yake kisha ataswali magharibi baada
ya hapo.
Kama atarudia swala aliyoiswali kabla kwa tahadhari, na katikati ya swala
akakumbuka kwamba hakuswali swala ambayo ilikuwa ni wajibu
kuiswali kabla ya hii swala, haijuzu kubadili nia yake kwenda kwenye
swala iliyotangulia, mfano kama alikuwa anarudia swala ya alasiri kwa
tahadhari na akakumbuka wakati huo kwamba hajaswali adhuhuri, haijuzu
kubadili nia yake kwenda kwenye adhuhuri.
612. Haijuzu kubadili nia kutoka kadha kwenda kwenye adai, wala kutoka
swala ya sunna kwenda kwenye swala ya wajibu.
Ikiwa wakati wa swala za adai, ni mpana inajuzu kubadilisha nia kutoka
swala za adai kwenda swala za kulipa ndani ya swala kama itawezekana
kubadilisha kwa mfano, kama mtu anaswali adhuhuri inajuzu kwake
kubadili nia yake kwenda swala ya asubuhi maadamu hajaingia katika
rakaa ya tatu.
SWALA ZA SUNNA
119
Al-Masailul Islamiyah
Page 134
613. Swala za sunna ni nyingi na pia huitwa swala za “nawafil” na zili-
zotiliwa mkazo katika sunna za kila siku “zilizowekwa kwa
mpangilio” nazo ni za kila siku isipokuwa siku ya Ijumaa, ni rakaa
34 katika utaratibu ufuatao:-
-Sunna ya adhuhuri rakaa nane
-Sunna ya alasiri rakaa nane
-Suna ya magharibi rakaa nne
-Suna ya isha rakaa mbili
-Sunna ya swala ya usiku rakaa kumi na moja
SWALA YA USIKU
614. Wakati wa swala ya usiku unaanzia katikati ya usiku mpaka adhana
ya alfajiri, na ni bora zaidi kuswali swala ya usiku karibu na adhana
ya alfajiri.
615. Msafiri au mtu ambaye hawezi kuswali swala ya usiku baada ya
katikati ya usiku inajuzu kwake kuswali mwanzo wa usiku.
616. Swala ya usiku ina rakaa kumi na moja, rakaa nane kati ya hizo ni
sunna ya usiku, rakaa mbili ni shufaa, na rakaa moja ni witiri, na
katika kila rakaa mbili kuna salam ila rakaa ya witiri yenyewe peke
yake ina salam.
617. Ni sunna katika swala ya usiku kusoma sura ndefu katika rakaa ya
kwanza na sura fupi katika rakaa ya pili na ni sunna katika sunna ya
shufaa na witiri kusoma suratul – Falaq, Nnasi na Tauhidi au kuso-
ma suratu Tauhid katika rakaa zote.
618. Ni sunna katika kunuti ya witiri kuwaombea waumina 40 aseme:
“Ewe Mwenyezi Mungu msamehe fulani na fulani” uwataje kwa
120
Al-Masailul Islamiyah
Page 135
majina yao, na aseme mara 70 “Astaghafirullaha rabbii waatuubu
ilaihi” na aseme mara saba “hadhaa maqamul – aaidhi bika mina
nnaari” na aseme mara 300 “al’afuwa”.
SWALA YA GHUFAILA
619. Miongoni mwa swala za sunna ni swala ya Ghufaila ambayo
huswaliwa baina ya Magharibi na Isha, nayo ina rakaa mbili na
huswaliwa kama ifuatavyo: Utasoma katika rakaa ya kwanza baada
ya Al hamdu “waddhannuun idhi dhahaba mughadhiban” iliyoko
katika sura ya 88 aya 87 na katika rakaa ya pili baada ya Al hamdu
“wa’indahu mafaatihul ghayib” mpaka mwisho wa aya iliyoko kati-
ka sura ya 6 aya ya 59
Na atasema katika kunuti “Allaahumma innii as,aluka bimafaatihil –
ghayibi allatii laa yaalamuhaa illa anta an tuswalliya alaa Muhammad
waali Muhammad” kisha unataja haja zako, kisha unasema “Allahumma
anta waliyu ni’imatiy wal- qaadiru alayi twalabatii ta’alamu haajatiy
faas’ aluka bihaq Muhammad waaalihi alaihi wa alaihimu ssalam lammaa
qadhwaytahaa lii”
HUKUMU ZA KIBLA
620.Kibla ni ka’aba tukufu iliyoko katika Mji wa Makka hivyo ni wajibu
kwa mwenye kuswali akiwa Makka kuilekea ka’aba yenyewe lakini
mtu alioko mbali aelekee upande wa kibla, vivyo hivyo kwa jambo
ambalo ni sharti kuelekea kibla kama vile kuchinja mnyama.
621. Mwenye kuswali swala zake za wajibu kwa kusimama ni wajibu
kuelekea kibla kwa uso wake, kifua chake, tumbo lake na sehemu
ya mbele ya miguu yake na kwa tahadhari ya sunna vidole vyake pia
vieleke kibla. Anayeswali kwa kukaa akishindwa kukaa katika hali ya
121
Al-Masailul Islamiyah
Page 136
kawaida kuweka tumbo na miguu yake katika ardhi, ni wajibu
aelekeze uso wake, kifua chake na tumbo lake kibla, na kwa tahadhari
na miundi yake ielekee kibla.
622. Mtu ambaye hawezi kuswali kwa kukaa ni wajibu aswali kwa kulala
kwa ubavu wa kulia kwa kuelekeza sehemu ya mbele ya mwili wake
kibla, na kama hakuweza, basi aswali hali amelala kwa ubavu wa
kushoto, na akishindwa alale kwa mgongo kwa kuelekeza matumbo
ya miguu yake kibla.
623. Mwenye kutaka kuswali ni wajibu afanyejitihada ya kujua kwa yaki-
ni upande wa kibla, na inajuzu ategemee kauli ya watu wawili
waadilifu au mtu mmoja mkweli.
624. Kama akishindwa kupata yakini kwamba kibla kiko upande upi, na
hakupata mtu wa kuaminika wa kumwambia upande wa kibla, itam-
lazimu atumie dhana kwa kutazama mihrabu za miskiti ya waislam au
makaburi yao au njia zingine zitakazomuwezesha kujua upande wa
kibla.
625. Ambaye hakupata uhakika kibla kipo upande upi akitaka kufanya
amali isiyo kuwa swala ambayo ni wajibu kuelekea kibla, mfano aki-
taka kuchinja mnyama itamlazimu awe na dhana ulipo upande wa
kibla na akishindwa hilo atamchinja kumwelekeza upande wowote
atakaoafiki katika hali ya dharura juu ya amali hiyo.
KUSITIRI MWILI KATIKA SWALA
626. Ni wajibu kwa mwanaume kusitiri mwili wake katika swala hata
kama hakuna mtu yeyote anayemuona, na ni bora kusitiri kuanzia
kitovuni mpaka magotini.
627. Na ni wajibu kwa mwanamke wakati wa swala kusitiri mwili wake
wote hata kichwa na nywele, na kwa tahadhari ya sunna kusitiri chini
122
Al-Masailul Islamiyah
Page 137
ya unyayo wake pia, lakini si lazima kusitiri vile viungo vinavy-
ooshwa katika udhu, yaani uso na viganja vya mikono mpaka kongo
mbili, na vile vile migongo ya miguu mpaka kwenye kongo mbili
lakini ili awe na yakini kwamba amesitiri yaliyowajibu kusitiriwa ni
wajibu kusitiri sehemu za pembeni za uso na kusitiri kongo za
viganja.
628. Kama mtu hakusitiri uchi wake katika swala kwa makusudi swala
yake inabatilika.
inajuzu kwa mwenye kuswali kusitiri uchi wake wakati wa swala kwa
karatasi au majani ya miti na ikiwa ana kitu kingine ambacho anaweza
kusitiri uchi wake kwa tahadhari ajisitiri kwa kitu hicho.
Inajuzu kwa mwenye kuswali kusitiri uchi wake kwa udongo.
VAZI LA MWENYE KUSWALI
629. Kuna masharti sita kwa vazi la mwenye kuswali:-
Lazima liwe tohara
Liwe la halali
Lisiwe limetokana na mizoga
Lisiwe limetokana na vitu vya wanyama ambao ni haramu kuliwa
Lisiwe la hariri halisi au dhahabu, ikiwa mwenye kuswali ni mwanaume,
ufafanuzi wake utakuja.
SHARTI LA KWANZA
630. Ni wajibu nguo ya mwenye kuswali iwe tohara na lau akiswali kwa
nguo au mwili ulio na najisi kwa makusudi swala yake inabatilika.
Mwenye kuswali na nguo au mwili ulio najisi naye hajui kwamba kuswali
katika hali ile inabatilisha swala, swala yake itasihi.
123
Al-Masailul Islamiyah
Page 138
631. Kama hajui unajisi wa kitu kwa kutokujua mas’ala, mfano kama
hajui unajisi wa damu, kisha akaswali na nguo iliyo na najisi ya
damu swala yake inasihi.
632. Kama hajui kwamba mwili wake au nguo yake ina najisi na akatam-
bua hilo baada ya swala, swala yake itasihi.
633. Akiona damu katika mwili wake au vazi lake na akawa na uhakika
kwamba ile si katika damu zilizonajisi, mfano akiwa na uhakika
kwamba damu ile ni ya kunguni au ya mbu, na akafahamu baada ya
swala kwamba damu ile ni katika damu zilizo najisi ambazo hazifai
kuswali nazo, swala yake aliyoiswali itasihi.
634. Ambaye hana nguo nyingine isipokuwa hiyo yenye najisi, ni wajibu
kuswali na nguo hiyo, hasa kama hataweza kuvua nguo yake kwa
sababu ya baridi na mfano wa hilo swala yake itasihi.
635. Ambaye ana nguo mbili na akafahamu kwamba mojawapo ya nguo
zake mbili ina najisi, lakini hafahamu ni ipi kati ya hizo iliyo na
najisi, kama muda ni wasaa ni wajibu kuswali na nguo zake mbili,
mfano akitaka kuswali adhuhuri na alasir ataswali nazo katika kila
nguo moja, katika nguo hizo mbili lakini kama wakati hautoshi, ita-
muwajibikia kuswali na nguo mojawapo atakaeitaka lakini na kwa
tahadhari alipe swala hiyo baada ya wakati katika nguo tohara.
SHARTI LA PILI
636. Ni wajibu nguo ya mwenye kuswali iwe ya halali, na mwenye kujua
uharamu wa kuvaa nguo ya kunyang’anya lau akiswali na nguo ya
wizi au nguo yenye uzi au vifungo au kitu kingine cha kunyang’anya
swala yake inabatilika na hukumu hii pia ni kwa mtu ambaye hajui
na mwenye kupuuzia.
124
Al-Masailul Islamiyah
Page 139
637. Anayejua uharamu wa kuvaa nguo ya kunyang’anya, lakini hajui
kubatilika kwa swala ya mwenye kuswali kwa nguo hiyo, kama
ataswali kwa nguo hiyo ya kunyang’anya kwa makusudi swala yake
itabatilika.
638. Kama hakujua au akisahau kwamba nguo yake ni ya wizi na
akaswali na nguo hiyo, swala yake itasihi lakini kama mtu
mwenyewe akinyang’anya nguo kisha akasahau kwamba nguo hii ni
ya kunyang’anya basi kwa tahadhari arudie swala hiyo kwa nguo
halali.
639. Kama mtu akiswali kwa nguo ya kunyang’anya kwa kulinda maisha
yake au kwa ajili ya nguo hiyo isiweze kubwa swala yake itasihi.
640. Akinunua nguo na pesa ambayo haijatolewa khumsi au zaka, na
akaswali na nguo hiyo, swala yake itakuwa na mushkeli
SHARTI LA TATU
641. Ni wajibu vazi la mwenye kusali lisiwe limechanganywa na vitu
vinavyotokana na mizoga ya wanyama ambao hutoka damu kwa kasi
wakati wa kuchinja kama vile mbuzi, na kwa tahadhari pia asiswali
na vazi lililotengenezwa na vitu vya mizoga ya wanyama ambao
damu zao hazitoki kwa kasi kama vile samaki na nyoka.
SHARTI LA NNE
642. Ni wajibu vazi la mwenye kuswali lisiwe limetokana na vitu vya
wanyama ambao ni haramu kuliwa na swala itabatilika kutokana na
vitu hivyo hata kama vazi hilo lina unywele mmoja.
643. Kama vazi lake lina kitu chochote kinachotokana na mate au mako-
hozi au kitu kingine chenye unyevunyevu unaotokana na wanyama
125
Al-Masailul Islamiyah
Page 140
walio haramu kuliwa kama vile paka, kama vina unyevunyevu swala
yake itabatilika na vikiwa ni vikavu na najisi yake imeshaondoka
swala yake itasihi.
644. Akishuku kwamba vazi hili limetengenezwa kutokana na wanyama
ambao ni halali kuliwa au walioharamu kuliwa, itajuzu kuswali na
vazi hilo sawasawa limetengenezwa katika nchi za kiisalamu au
zisizokuwa za kiisalmu. Akiswali na nguo ambayo hajui au akisa-
hau kwamba imetokana na mnyama ambaye ni haramu kuliwa swala
yake itasihi.
SHARTI LA TANO
645. Ni haramu kwa mwanaume kuvaa nguo yenye nyuzi zilizochovya
dhahabu au vifungo vya dhahabu na itabatilisha swala, lakini haku-
na mushkeli katika hilo kwa wanawake katika swala na nje ya
swala. Ni haramu kwa mwanaume kujipamba kwa mapambo ya
dhahabu mfano kuvaa mikufu ya dhahbu shingoni au kuvaa pete au
saa ya dhahabu mkononi, na vitu vinayobatilisha swala, na ni
wajibu kujiepusha na kuvaa fremu za miwani kama ni za dhahabu,
lakini hakuna tatizo kujipamba mapambo ya dhahabu kwa
wanawake katika swala na nje ya swala.
646. Ikiwa mwanaume atasahau kwamba pete yake au vazi lake ni la
dhahabu, au akashuku na akaswali kwa pete au vazi hilo, swala yake
inasihi, lakini katika hali ya kushuku ni wajibu kwake afanye utafi-
ti na vivyo hivyo ni wajibu kufanya utafiti katika mas’ala mengine
yaliyobakia mbali na haya tuliyoyaeleza.
126
Al-Masailul Islamiyah
Page 141
SHARTI LA SITA
647. Ni wajibu vazi la mwenye kuswali lisiwe limetokana na hariri hal-
isi hasa akiwa mwanaume na ni haramu pia kuvaa nje ya swala,
ama kofia, mkanda na mfano wa hivyo ni kinyume na tahadhari.
648. Nguo ambayo haifahamiki kuwa ni ya hariri halisi au laa, haina
mushkeli kuivaa wakati wa swala, hakuna tatizo katika leso iliy-
otengenezwa kwa hariri ikiwa ndani ya mfuko wa mwenye kuswali
na haitabatilisha swala. Hakuna tatizo kwa wanawake kuvaa hariri
ndani ya swala au nje ya swala. Hakuna kizuizi wakati wa dharura
kuvaa nguo ya kunyang’anya au iliyotengenezwa kwa hariri au
kuchanganywa na dhahabu au kutengenezwa kutokana na vitu vya
mizoga na inajuzu kuswali navyo.
SEHEMU AMBAZO HAZILAZIMU TOHARA YA
MWILI NA NGUO KWA MWENYE KUSWALI
649. Inasihi swala kwa kiwiliwili au nguo yenye najisi katika sehemu tatu:-
Ikiwa mwili au nguo ya mwenye kuswali itachafuka kwa damu iliyotoka
kwenye jeraha au kidonda au jipu kutoka katika mwili wake.
Mwili wake au nguo yake ikichafuka kwa damu iliyotoka kwa kiwango
kidogo sana.
Kama atalazimika kuswali kwa mwili au nguo iliyo na najisi.
650. Swala inasihi swala katika hali mbili ikiwa nguo za mwenye kuswali
tu zina najisi.
Ikiwa mavazi yake ni madogo mfano wa soksi au kofia vina najisi.
Ikinajisika nguo ya mwanamke anaelea kwa mkojo wa mtoto mchanga.
127
Al-Masailul Islamiyah
Page 142
651. Kama katika mwili wa mwenye kuswali au nguo yake kuna jereha
au kidonda au jipu , itajuzu kwake kuswali kwa nguo hiyo mwilini
madamu jeraha au kidonda au jipu halijapona ikiwa kutoharisha
mwili au nguo au kubadilisha kwake kutakuwa na ugumu na pia
ikiwa katika mwili au nguo kuna matapishi yaliyotoka kwa
kuchanganyikana na damu au dawa iliyowekwa kwenye jeraha ikatia
najisi. Mtu ambaye mwili wake umejeruhiwa akiona katika mwili
wake au nguo yake damu na akawa hajui ni damu ya jeraha lake au
ni damu nyingine inajuzu kwake kuswali katika hali hiyo.
652. Ikiwa kwenye mwili wa mtu kuna majeraha mengi na yakawa
yamekaribiana kiasi cha kuhesabika kuwa ni jeraha moja hakuna
mushikeli kuswali na damu yake maadamu hajapona lakini kama
yametengana kiasi cha kuhesabika kila jeraha mahali pake basi kila
jeraha likipona itamlazimu kutoharisha nguo au mwili kwa ajili ya
swala kutokana na damu hiyo.
653. Ikiwa katika mwili au nguo ya mwenye kuswali kuna damu ya hedhi
au istihadha au nifasi au damu ya mbwa au nguruwe au damu ya
kafiri au mizoga swala yake itabatilika na pia kama kuna damu ya
mnyama ambaye ni haramu kuliwa, lakini hakuna tatizo katika
swala pamoja na damu zingine kama damu ya mtu au damu ya
mnyama aliye halali kuliwa japo itaenea sehemu za mwili wake au
nguo yake kwa sharti iwe damu yote hiyo ni chache sana.
YALIYO SUNNA KATIKA VAZI LA
128
Al-Masailul Islamiyah
Page 143
MWENYE KUSWALI
654. Ni sunna katika vazi la mwenye kuswali mambo mengi miongoni
mwa hayo ni kuvaa kilemba, kuvaa joho, kuvaa nguo nyeupe, kuvaa
nguo iliyo safi zaidi, kujipaka manukato na kuvaa pete ya akiki.
YALIYO MAKURUHU KATIKA VAZI LA
MWENYE KUSWALI
655. Yaliyo makuruhu katika vazi la mwenye kuswali ni mengi, miongo-
ni mwa hayo ni kuvaa nguo nyeusi, ila kwa ajili ya kukumbuka misiba ya
maasumina (as) sio makuruhu bali ni sunna, na kuvaa nguo chafu, yenye
kubana, nguo za mwenye kunywa pombe, nguo za mtu ambaye hajiepushi
najisi, nguo yenye picha, nguo isiyo na vifungo na kuvaa pete yenye
picha.
SEHEMU YA MWENYE KUSWALI
656. Sehemu ya mwenye kuswali ina masharti tisa nayo ni:-
1. Iwe ya halali.
2. Iwe imetulizana isitikisike
3. Aweze kutimiza swala yake humo
4. Asiwe amekatazwa kubaki mle
5. Isiwe kusimama au kukaa sehemu ile ni haramu
6. Aweze kusimama, kurukuu na kusujudu humo
7. Asiwe mbele au amelingana na kaburi la maasum(as)
8. Sehemu hiyo isiwe na najisi yenye unyevunyevu
9. Paji lake la uso liwe limelingana na magoti yake na ncha za
dole gumba vya miguu yake.
129
Al-Masailul Islamiyah
Page 144
Sharti la kwanza
657.Ni wajibu sehemu ya mwenye kuswali iwe ya halali, mwenye kuswali
katika sehemu iliyo nyang’anywa swala yake ni batili hata kama
ataswali juu ya godoro au kitanda lakini hakuna mushkeli kuswali
chini ya dari ya unyang’anyi na hema la unyang’anyi.
658. Mwenye kukaa katika sehemu ya msikiti kisha akaja mtu na akam-
nyanganya sehemu yake hiyo na akaswali, swala yake itakuwa na
mushkeli.
659. Kama mtu akijua kuwa sehemu hii ni ya kunyang’anya na hajui
kuwa kuswali katika sehemu hiyo kunabatilisha swala, kisha
akaswali hapo basi swala yake itabatilika kama hakufahamu kwa
kupuuzia. Mwenye kuwa na udhuru, na akaswali juu ya mnyama
kama mnyama huyo tandiko lake alotandikiwa juu ya mgongo wake
au ikiwa kiatu chake ni cha kunyang’anya swala yake ni batili, pia
hukumu ni hii hii kwa mwenye kuswali swala za sunna juu ya mnya-
ma huyo.
Sharti la pili
660. Ni wajibu sehemu ya mwenye kuswali iwe yenye kutulizana na
kama atalazimika kuswali katika sehemu yenye kutikisika kwa
sababu ya ufinyu wa wakati au sababu nyingine, mfano kuswali
katika gari au treni au ndege, itamuwajibikia kutokusoma wakati wa
mtikisiko na kutotulizana kwa mwili kama ataweza kufanya hivyo, hii
ni kama hataharibu utaratibu wa swala la sivyo asome wakati wa
mtikisiko, pia kama gari litageuka kutoka upande wa kibla kuelekea
upande mwingine ni wajibu yeye ageukie kibla.
Hapakatazwi kuswali katika gari au meli na vinginevyo vikiwa vimesima-
ma.
130
Al-Masailul Islamiyah
Page 145
Sharti la tatu
661. Ni wajibu kwa mwenye kuswali aweze kumaliza swala, haijuzu
kuanza kuswali katika sehemu ambazo huna uhakika kwamba
utaweza kutimiza swala hapo, kwa sababu ya mvua au msongamano
au upepo mkali, lakini lau atashuku katika hilo au akawa na uhaki-
ka wa kutimiza swala, itajuzu kuanza kuswali, na ikikamilika swala
itasihi.
Sharti la nne
662.Nisharti asiswali katika sehemu ambayo ni haramu kubakia humo
kama vile kuswali chini ya dari inayokaribia kuanguka na kubomoka.
Sharti la tano
663. Ni sharti mtu asiswali juu ya kitu kilichokatazwa kusimama juu yake
au kukaa kama vile mswala ulioandikwa jina la Mwenyezi Mungu.
Sharti la sita
664. Ni wajibu asiswali katika paa liloinama sana kiasi kwamba hawezi
kusimama vizuri chini yake ama akilazimika kuswali katika sehemu
hii ni lazima asimame, arukuu na asujudu kadri atakavyoweza.
Sharti la saba
665. Ni wajibu asilitangulie kaburi la Mtume na maimamu wakati wa
kuswali vivyo hivyo asiswali kwa kulingana nalo kwa tahadhari ya
wajibu.
131
Al-Masailul Islamiyah
Page 146
Sharti la nane
666. Ni wajibu sehemu ya mwenye kuswali isiwe na najisi yenye unyevu
nyevu unaohamia kwenye mwili wake au nguo yake na swala itabati-
lika ikiwa sehemu ya kusujudia ina najisi hata kama ni kavu na kwa
tahadhari ya sunna sehemu ya mwenye kuswali isiwe najisi kabisa.
Sharti la tisa
667. Ni wajibu sehemu ya paji lake wakati wa kusujudu isiwe juu au chini
zaidi kuliko. magoti yake na ncha za vidole gumba zaidi ya vidole
vinne vilivyounganishwa.
668. Si lazima mwanamke kusimama mbali ya mwanaume katika swala
isiyokuwa ya jamaa, wala mahali anaposujudia kuwa mbali kidogo
na mahali aliposimama mwanaume, ingawa ni bora kufanya hivyo.
669. Ni makuruhu kwa mwanamke kusimama mbele ya mwanaume au
kuwa sawasawa naye katika swala na kuanza kuswali pamoja lakini
haiwalazimu kurudia swala kama wakifanya hivyo. Kama kuna kizui-
zi kati ya mwanaume na mwanamke kiasi ambacho mmoja hamuo-
ni mwenzake au kati yao kuna umbali wa mita tano, au mmoja wao
kasimama sehemu ya juu sana kiasi ambacho haitasadikishwa kutan-
gulia kwa mwanamke au kuwa sawasawa, basi karaha huondoka. Ni
haramu kwa mwanaume na mwanamke ambao sio mahramu kukaa
chumba kimoja bila ya kuwa na mtu mwingine wa tatu na bila ya
kuonekana na yeyote, na kwa tahadhari ni kwamba swala yao hai-
tasihi katika sehemu hiyo, lakini kama mmoja ataswali na mwingi-
ne akaingia, swala yake haina mushkeli.
670. Kuswali sehemu ya kupigia muziki kama haihesabiki kuwa ni kusai-
dia kufanya katika maasi haina mushkeli.
132
Al-Masailul Islamiyah
Page 147
SEHEMU ZILIZO SUNNA KUSWALI HUMO
671. Umepokewa msisitizo mkubwa katika sharia ya kiislamu kuhusu
kuswali katika misikiti na msikiti uliobora zaidi ni msikiti wa Makka,
kisha msikiti wa Mtume Madina kisha msikiti wa Al Kufa kisha msi-
kiti wa Al Aqswaa kisha kila msikiti mkuu wa kila mji, kisha msikiti
wa kila mtaa, kisha msikiti wa soko.
672. Ni bora kwa wanawake kuswali nyumbani lakini wakiweza kujilin-
da na wanaume ajinabiya basi itakuwa ni bora kuswali misikitini.
HUKUMU ZA MISIKITI
673. Ni haramu kutia najisi ardhi ya msikiti, dari yake, paa lake na sehe-
mu za ndani za kuta, na ni wajibu kwa atakayefahamu unajisi wa
moja ya sehemu hizo kuiondosha najisi haraka na kwa tahadhari ya
wajibu ni kwamba imeharamishwa kutia najisi sehemu za nje za msi-
kiti, na ikinajisika ni wajibu kwake kuiondosha haraka.
674. Kama hakuweza kusafisha msikiti au akihitajia msaada na hakupata
haitamuwajibikia kusafisha, lakini ni wajibu kwake kwa tahadhari ya
wajibu kumwambia mwenye uwezo wa kusafisha.
675. Sehemu ya msikiti ikinajisika na ikawa haiwezekani kutoharishwa
kwake ila kwa kuchimba shimo, basi ni wajibu kuchimbwa na ikila-
zimu kuvunja sehemu kwa ajili ya kutoharisha inajuzu kuvunja
sehemu hiyo. Ni haramu kutia najisi makaburi ya maimam, na lau
mojawapo likinajisika ni wajibu kulitoharisha. Ni haramu kuingiza
kiini cha najisi msikitini kama vile damu kama kutaudhalilisha msi-
kiti bali kwa tahadhari ya sunna kutoingiza kiini cha najisi msiki-
tini hata kama si kwa ajili ya kuudhalilisha msikiti lakini sio haramu
kuingiza kitu kilicho najisika msikitini, ila kama itakuwa ni kwa ajili
133
Al-Masailul Islamiyah
Page 148
ya kuudhalilisha msikiti.
676. Haikatazwi kuweka mahema misikitini kwa ajili ya maatam na maji-
lisi za maombolezo ya maimamu. Pia haikatazwi kutundika na kui-
pamba kwa vitambaa vyeusi na kuingiza vitu vya kupikia chai kama
havitaleta madhara na havizui watu kuswali humo.
677. Haijuzu kuuza ardhi ya msikiti ikiwa msikiti umebomoka pia kuun-
ganisha na njia kuu au kuunganisha na milki ya mtu mwingine.
678. Ni haramu kuuza madirisha ya msikiti na milango yake na vitu vingi-
ne na kama msikiti ukibomoka basi ni wajibu kwa kiongozi wa kisha-
ria kuvitoa vitu na kuvitumia kuimarisha msikiti huo, na kama hai-
wezekani kuvitumia katika msikiti huo, ni wajibu kuvitoa katika misi-
kiti mingine, na ikishindikana katika misikiti mingine, itajuzu kuviu-
za kwa ajili ya kuimarisha misikiti mingine.
679. Inachukiza kuwaruhusu wasio na akili na watoto kuingia msikitini, ila
watoto kama kuingia kwao ni kwa ajili ya kujifunza swala na Qur’ani
na mas’ala ya kisharia, malezi, mafunzo ya kiislam na mengineyo,
pia inachukiza kwa mwenye kula vitunguu maji na saumu kama haru-
fu ya mdomo wake itawaudhi watu.
KUADHINI NA KUKIMU
680. Ni sunna kwa mwanaume na mwanamke kuadhini na kukimu kabla
ya swala za wajibu za kila siku, bali haifai kuacha kukimu lakini
kabla ya kuanza kuswali swala za wajibu zisizokuwa za kila siku
mfano swala za majanga ni sunna kusema mara tatu “As swalaatu
aswalatu aswalat”(badala ya kukimu).
781. Adhana ina vipengele ishirini navyo ni:-
Allahu akbar x 4
134
Al-Masailul Islamiyah
Page 149
Ashahadu an llaa ilaaha illa llaah x 2
Ash hadu anna Muhammadan rasulullah x 2
Ash hadu anna Alliyyan waliyullah x 2
Hayya alaa swalaat x 2
Hayya alaal falah x 2
Hayya alaa khairil – amal x 2
Allah akbar x 2
Laa ilaaha illa llah x 2
683. Na iqama ina vipengele 19 yaani kwa kuondosha takbira mbili za
mwanzo na tahalili moja ya mwisho na kuongezea qadi qaamatis
swalaat mara mbili baada ya “Hayya alaa khairil – amali”
684. Haifai kutenganisha sana kati ya sentensi na vipengele vya adhana na
kukimu na akitenganisha sana kuliko kawaida basi atapaswa arudie
tena upya.
685. Akirudiarudia kwa kughani adhana na kukimu kiasi kwamba inakuwa
kama wimbo katika vikao vya upuuzi na michezo inakuwa ni hara-
mu.
686. Hakuna adhana katika swala za aina tano:-
Swala ya alasiri siku ya Ijumaa
Swala ya alasiri siku ya arafa, nayo ni siku ya 9 ya mfungo 3
swala ya isha usiku wa Idul -Adhuhaa kwa aliyoko muzdalfa
Swala ya alasiri na isha kwa mwenye istihadha
Swala ya alasiri na isha kwa asiyeweza kuzui mkojo au haja
kubwa, katika swala hizi huondoka adhana kama hakutenganisha
kati ya swala hiyo na Swala iliyotangulia.
687. Pakiadhiniwa na kukimiwa kwa swala ya jamaa, hawataadhini wala
kukimu wale watakaounga jamaa hawatolazimika kuadhini wala
kukimu tena.
688. Hakuna kukimu kama mtu akikuta watu wanaswali jamaa au jamaa
135
Al-Masailul Islamiyah
Page 150
imemalizika na watu hawajaondoka katika safu, na akataka kuswali
peke yake au kuswali swala ya jamaa nyingine kwa masharti
matatu:-
Iwe pameadhiniwa na kukimiwa katika swala iliyotangulia
Isiwe swala ya jamaa iliyotangulia ni batili kuungana jamaa mbili ya
mwanzo na inayofuatia katika sehemu moja.
689. Ni sunna kwa anayechaguliwa kuadhini na kukim awe mwadilifu,
anayefahamu nyakati za swala mwenye sauti ya juu na aadhini kati-
ka sehemu iliyonyanyuka.
MAMBO YALIYOWAJIBU KATIKA SWALA
690. Wajibati za swala ni kumi na moja:-
Nia
Kisimamo
Takbira ya kuhirimia swala
Rukuu
Sijida
Kusoma
Dhikir
Tashahud
Kutoa salam
10.Kufuata utaratibu
11.Kufuatanisha
691. Baadhi ya wajibati za swala ni nguzo kwa maana kama mwenye
kuswali akiicha au akizidisha kwa makusudi au bila ya kukusudia
swala yake inabatilika, na baadhi ya wajibati siyo nguzo, kwa maana
kwamba swala inabatilika kwa kupunguza au kuzidisha kwa makus-
dui wala haibatiliki kwa kusahau.
692. Nguzo za swala ni tano
136
Al-Masailul Islamiyah
Page 151
Nia
Takbira ya kuhirimia
Kisimamo wakati wa takbira ya kuhirimia na kisimamo kilichoun-
gana na rukuu (yaani kabla ya kurukuu)
Rukuu
Sijida mbili
NIA
693. Ni wajibu kwa mwenye kuswali atie nia katika swala kwa kujikuru-
bisha kwa Mwenyezi Mungu, na kutekeleza amri yake, wala hailaz-
imu kupitisha moyoni au kuitamka kwa ulimi wake, bali yatosha
kufahamu kwamba yeye anaswali rakaa nne za swala ya adhuhuri
kwa ajili ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu.
694. Akinuia katika swala ya adhuhuri au alasiri kwamba anaswali rakaa
nne lakini hakubainisha kwamba ni adhuhuri au alasiri basi swala
yake itakuwa na mushikeli na ni wajibu kwa ambaye ana kadha ya
adhuhuri na akataka kuswali adhuhuri kwa wakati au kadha katika
wakati wa adhuhuri kubainisha kwamba anaswali kadha au adaa
(kwa wakati).
695. Ni wajibu kwa mwenye kuswali kubakia na nia yake tangu mwanzo
wa swala hadi mwisho na akighafilika wakati wa swala, kiasi lau
akiulizwa unafanya nini? Ikawa hajui aseme nini, swala yake ita-
batilika.
137
Al-Masailul Islamiyah
Page 152
TAKBIRA YA KUHIRIMIA
696. Takbira ya kuhirimia yaani kusema: “Allah akbar” ni wajibu katika
kila mwanzo wa swala nayo ni nguzo katika swala na ni wajibu kufu-
atanisha kati ya neno “Allah” na neno “Akbar” pia ni wajibu kuy-
atamka kwa lugha ya kiarabu sahihi, na lau akitamka kwa kiarabu
chenye makosa au kwa lugha isiyokuwa ya kiarabu, takbira yake
haitasihi.
697. Ni wajibu kwa mwenye kuswali kutulizana wakati wa kuleta takbira
ya kuhirimia, na kama akihirimia na hali anatikisika kwa makusudi,
takbira yake inabatilika.
698. Ni wajibu kuhirimia, na kusoma Al hamdu, sura, dhikiri na dua kwa
kiasi cha kusikia mwenyewe, kama ni kiziwi au asiyesikia vizuri au
kwa sababu ya makelele mengi, ni wajibu kuhirimia kwa kiasi
ambacho kama si kizuizi angesikia.
699. Bubu na mwenye matatizo ya ulimi yanayomfanya asiweze kutamka
takbira kwa njia sahihi, ni wajibu kutamka kwa namna atakayoweza,
na kama hakuweza kutamka chochote, itamlazimu kutamka kimoyo
moyo, na aashirie katika kuhirimia kwa kutikisa ulimi wake kwa
namna atakavyoweza.
700. Ni sunna kunyanyua mikono mpaka kwenye usawa wa masikio
wakati wa kuhirimia na katika takbira zingine wakati wa swala.
KISIMAMO
701. Kisimamo wakati wa kuhirimia na kisimamo kabla ya kwenda
kurukuu, visimamo hivi ni nguzo mbili, lakini kisimamo wakati wa
kusoma Al hamdu na sura na kisimamo baada ya rukuu si nguzo laki-
138
Al-Masailul Islamiyah
Page 153
ni akiviacha kwa kusahau swala yake itasihi.
702. Ni wajibu kusimama kabla ya kuhirimia swala na baada ya kuhirimia
kwa kiwango cha kuwa na uhakika kwamba amehirimia wakati wa
kisimamo.
703. Akisahau kurukuu na akakaa baada ya Al hamdu na sura kisha
akakumbuka kwamba hajarukuu ni wajibu kusimama na kisha
arukuu, na akirukuu bila ya kusimama kwanza, swala yake inabatili-
ka kwa sababu hajasimama kabla ya rukuu.
704. Ni wajibu asitikise mwili wake wakati wa kisimamo na asiegemee
upande mmoja wala asiegemee kitu chochote, lakini hakuna tatizo lau
akifanya mambo haya kwa dharura, kama ambavyo hakuna tatizo
kama atatikisa miguu yake wakati wa kuinama kwenda kwenye
rukuu.
705. Akishindwa kusimama wakati wa kuswali ni wajibu kukaa na
akishindwa kukaa pia, ni wajibu kwake kulala lakini asisome cho-
chote mpaka atulizane.
KUSOMA
706. Ni wajibu kusoma Al hamdu na sura kamili katika rakaa mbili za
mwanzo katika swala za wajibu za kila siku. Kama wakati utakuwa ni
mfinyu na akalazimika kutokusoma sura, mfano lau ataogopa kuibi-
wa au kudhuriwa na wanyama wakali au litamsibu jambo jingine
kama atasoma sura, basi ni wajibu kwake asisome sura.
707. Akisoma sura kabla ya kusoma Al hamdu kwa makusudi swala yake
itabatilika. Na akifanya hivyo kwa kusahau na akakumbuka wakati
huo, itamlazimu kuacha sura kisha atasoma Al hamdu kisha atasoma
sura kuanzia mwanzo.
139
Al-Masailul Islamiyah
Page 154
708. Akisahau kusoma Al hamdu na sura au akasahau mojawapo kisha
akakumbuka baada ya kufika kwenye rukuu swala yake itasihi.
709. Akikumbuka kabla ya kuinama kwenye rukuu kwamba hakusoma Al
hamdu na sura ni wajibu kuzisoma, pia akikumbuka kwamba haku-
soma sura peke yake, ni wajibu kuisoma, lakini akikumbuka katika
hali ile kwamba hakusoma Al hamdu ni wajibu kuisoma Al hamdu
kwanza kisha atairudia sura mara nyingine, na atafanya hivyo akijua
baada ya kuinama na kabla ya kufika katika rukuu kuwa hakusoma
Al hamdu na sura au mojawapo atarejea katika kisimamo na kusoma
Al hamdu aliyoisahau.
710. Akikusudia katika swala ya wajibu kusoma mojawapo ya sura zenye
sijda ya lazima swala yake itabatilika.
711. Ni wajibu kwa mwanaume kudhihirisha Al hamdu na sura katika
swala ya asubuhi, magharibi na isha na ni wajibu kwa mwanaume na
mwanamke kutokudhihirisha katika swala ya adhuhuri na alasiri.
712. Ni wajibu kwa mwanaume kudhihirisha kila neno la sura ya Al hamdu
na sura atakayoisoma katika swala ya asubuhi, magharibi na isha hata
herufi ya mwisho.
713. Inajuzu kwa mwanamke kutokudhihirisha au kudhuhirisha Al hamdu
katika swala ya asubuhi, magharibi na isha lakini hatodhihirisha
kama sauti yake itasikika na mtu ambaye si mahramu yake.
714. Mwanaume akikusudia kutokudhihirisha katika swala ambayo ni
wajibu kudhihirisha swala yake itabatilika lakini lau akifanya hivyo
kwa kusahau au kutokujua swala yake itasihi, na akifahamu kuwa
amekosea wakati wakusoma Al hamdu na sura, haimlazimu kurudia
aliyosoma kwa kukosea.
140
Al-Masailul Islamiyah
Page 155
715. Akisoma kwa sauti ya juu sura ya Al hamdu na sura kinyume na sauti
zilizozoeleka, kama akisoma kwa kupiga makelele ya juu, swala yake
itabatilika.
716. Ni wajibu kujifunza swala ili asisome kwa makosa na ambaye hawezi
kujifunza kutamka sawa sawa, ni wajibu kuswali kwa njia atakay-
oweza lakini ni vizuri kuswali jamaa.
717. Ni sunna katika swala zote kusoma suratul – Qadir katika rakaa ya
kwanza na suratu tauhid katika rakaa ya pili.
718. Inachukiza kwa mtu kuacha kusoma suratu tauhid katika swala zake
za kila siku.
719. Inachukiza kuisoma suratu tauhid yote kwa pumzi mmoja bila ya
kusimama kwenye vituo.
720. Inachukiza kusoma katika rakaa ya pili sura aliyoisoma katika rakaa
ya kwanza isipokuwa kama atasoma suratu tauhid.
RUKUU
721. Ni wajibu kuinama baada ya kusoma katika kila rakaa kwa kiwango
cha kumuwezesha kushika magoti yaani kuweka viganja vya mikono
yake magotini.
722. Hakuna tatizo akiinama kwa kiwango cha kushika magoti hata kama
hakuweka viganja vyake juu ya magoti yake
723. Ni wajibu kuinama kuwe kwa nia ya kurukuu na akiinama kwa lengo
lingine kama kuweka kitu au kukinyanyua haitojuzu kuhesabiwa
kuwa ni rukuu.
730. Akirukuu kwa namna isiyoeleweka, kwa mfano lau akiinama kwa
kuelemea upande wa kulia au wa kushoto, rukuu yake haitosihi hata
141
Al-Masailul Islamiyah
Page 156
kama mikono yake itafika kwenye magoti.
731. Ni bora kusema katika rukuu “Subhanallah” mara tatu au “Subhana
rabbiyal – adhiim wabihamdih” mara moja lakini kama muda ni
mfinyu au wakati wa dharura yatosha kusema “Subuhanallah” mara
moja.
732. Ni wajibu dhikri ya rukuu iwe kwa kufuatana na kwa kiarabu sahihi
na ni sunna kuikariri mara tatu au tano au zaidi.
733. Ni wajibu mwili wa mwenye kuswali kutulizana wakati wa kurukuu
kiasi cha kuweza kuitamka dhikri ya wajibu na pia wakati wa kutam-
ka dhikri ya sunna.
734. Akinyanyua kichwa chake makusudi kabla ya kukamilisha dhikiri ya
wajibu swala yake inabatilika.
735. Akisahau kurukuu na akakumbuka kabla ya kufika katika sijda ni
wajibu kusimama kisha alete rukuu na lau akisimama kwenye rukuu
kwa kuinama swala yake itabatilika.
736. Akikumbuka kuwa hakurukuu na hilo ni baada ya kuwa ameshafika
chini au baada ya kunyanyua kichawa chake kutoka kwenye sijda ya
kwanza, itamlazimu asimame wima kisha arukuu, kisha alete sijda ya
swala, kisha sijida ya sahau baada ya swala na kwa tahadhari arudie
swala yake mara ya pili.
KUSUJUDU
737. Ni wajibu kwa mwenye kuswali kuleta sijida mbili baada ya rukuu,
katika kila rakaa za wajibu na sunna, maana ya kusujudu ni kuweka
paji la uso na matumbo ya viganja, magoti na vidole gumba vya
142
Al-Masailul Islamiyah
Page 157
miguu juu ya ardhi.
738. Sijda mbili ni nguzo, kama mwenye kuswali akiziacha katika swala
ya wajibu kwa makusudi au kwa kusahau au akizidisha sijda mbili
zingine, swala yake itabatilika.
739. Akipunguza au akizidisha moja ya sijida mbili kwa makusudi swala
yake itabatilika
740. Kama hakuweka paji la uso wake ardhini kwa makusudi au kwa kusa-
hau sijda hiyo haitahesabika hata kama ameweka sehemu zingine za
kusujudia ardhini, lakini akiweka paji lake ardhini na hakuweka viun-
go vingine vya kusujudia sijda yake itasihi.
741. Ni wajibu kutulizana kwa mwili katika sijida kiasi cha kuleta dhikiri
ya wajibu na pia katika dhikiri ya sunna.
742. Akikusudia kuleta dhikri ya sijda kabla ya kufikisha paji la uso wake
ardhini na kutulizana mwili wake au akanyanyua kichwa chake kabla
ya kutimiza dhikri ya sijda kwa makusudi swala yake itabatilika.
743. Akileta dhikri ya sijida kabla ya kufikisha paji lake ardhini na mwili
wake kutulizana kwa kusahau na akafahamu makosa yake kabla ya
kunyanyua kichwa katika sijda atarudia dhikri na swala yake itasihi.
745. Akitambua baada ya kunyanyua kichwa katika sijda kwamba amele-
ta dhikri kabla ya kutulizana mwili wake au amenyanyua kichwa
kabla ya kutimiza dhikri ya sijida swala yake itasihi.
746. Akikusudia kunyanyua mojawapo ya viungo saba vya sijda wakati
wa kuleta dhikri ya sijda, swala yake inabatilika lakini hakuna tatizo
akinyanyua moja ya viungo vya sijda isipokuwa paji la uso katika
hali isiyokuwa ya kuleta dhikri ya swala kisha akarejesha kiungo
hicho ardhini mara nyingine.
143
Al-Masailul Islamiyah
Page 158
VITU VINAVYOSIHI KUSUJUDIA JUU YAKE
747. Ni wajibu kusujudu juu ya ardhi na vinavyotokana na ardhi
“isipokuwa vile vinavyoliwa au kuvaliwa” kama vile mbao na majani
ya miti, wala haisihi kusujudu juu ya vitu vyenye kuliwa, kama vile
matunda na vyenye kuvaliwa kama vile pamba na vitu vya madini
kama vile dhahabu.
748. Haikatazwi kusujudu juu ya jani la zabibu likiwa kavu, kama sio kavu
na liko katika muda wa kuweza kuliwa, haitajuzu kusujudu juu yake.
749. Inasihi kusujudu juu ya vitu vinavyoota katika ardhi na vyenye kuli-
wa na wanyama kama vile majani, pumba n.k
750. Kilicho bora zaidi kusujudia ni turba ya Imam Hussein (as) kisha
udongo wa kawaida kisha jiwe kisha mimea.
751. Kama hana kitu chenye kusihi kusujudia juu yake au anacho lakini
akawa hawezi kusujudu juu yake kwa sababu ya baridi kali au joto
kali, basi kama ana nguo iliyotengenezwa kwa pamba au katani, ni
wajibu kwake kusujudu juu ya nguo yake, na ikiwa nguo yake ime-
tokana na vitu vingine ni wajibu kusujudu juu ya viganja vya mikono
yake au kitu cha madini kama vile pete ya akiki lakini ni bora asisu-
judu juu ya viganja vyake kama kunauwezekano wa kusujudu juu ya
kitu cha madini.
Kusujudu katika ardhi ambayo haitulizani ni batili.
752. Hakuna tatizo katika swala yake kama akifahamu baada ya kusujudu
kwamba amesujudu katika vitu ambavyo havisihi kusujudu juu yake.
753. Ni haramu kumsujudia asiyekuwa Mwenyezi Mungu na wanayofanya
144
Al-Masailul Islamiyah
Page 159
baadhi ya waumini kwa kuweka mapaji ya nyuso zao katika dharihi
ya makaburi ya Maimamu watukufu hilo ni kwa ajili ya kumshuku-
ru Mwenyezi Mungu na hakuna mushkeli humo, ama kubusu ukuta
wa makaburi ya Maimamu jambo hilo linajuzu bali ni sunna na hilo
sio sijida
SUNNA ZA SIJDA NA MAKURUHU ZAKE
753. Ni sunna katika sijida mambo yafuatayo:-
Mwenye kuswali aseme Allahu akbar akiwa amesimama kabla ya kwenda
kusujudu, baada ya kunyanyua kichwa chake katika rukuu na kusimama
wima, pia kwa mwenye kuswali kwa kukaa baada ya kukaa wima.
Mwanaume kutanguliza mikono yake ardhini kwanza wakati wa kwenda
kusujudu kisha magoti yake.
Kuweka pua yake juu ya turba au kitu chenye kusihi kusujudia juu yake.
Kuviunganisha vidole vya mikono yake na kuiweka mikono yake usawa
wa ndwele za masikio yake kiasi kwamba ncha za vidole vyake vinakuwa
vimeelekea kibla
Kuomba katika sijida yake na kumwomba Mwenyezi Mungu kumkidhia
haja zake na aombe kwa dua hii “ Yaa khairal – masiuliina wa yaa khairal
– mu’utwiina, urzuqunii warzuqu iyaalii min fadhilika fainnaka dhul fad-
hilil adhiym”
Kukalia paja la kushoto anapotoka katika sijda na kuweka mgongo wa
mguu wa kulia juu ya tumbo la mguu wa kushoto.
Alete takibira baada ya kukaa katika kila sijda na mwili wake utulizane.
Aseme “Astaghafirullaha rabii waatubu ilaihi” Baada ya kukaa kutoka
sijda ya kwanza na mwili wake utulizane.
Arefushe sijida yake
Aweke mikono yake juu ya mapaja anapokaa
145
Al-Masailul Islamiyah
Page 160
Alete takbira anapokwenda sijida ya pili katika hali ya kutulizana
Amswalie Mtume na kizazi chake katika sijida yake
Aweke mikono yake ardhini anapotaka kusimama
Mwanaume asikutanishe viwiko vya mikono yake na tumbo lake na asi-
ikutanishe na mbavu zake lakini mwanamke alaze viwiko vyake na tumbo
lake ardhini na kuvibana viungo vya mwili wake.
754. Inachukiza kupuliza sehemu ya kusujudia kwa ajili ya kuondosha
vumbi na lau ikitoka kutokana na kupuliza lafudhi ya herufi mbili
mfano akisema fuu, kwa makusudi swala yake itabatilika.
SIJDA ZA QUR’AN ZILIZO WAJIBU
755. Sijda za wajibu zinapatikana kila moja katika sura nne nazo ni:-
surat Najmi: aya ya 62, Al Alaq aya ya 19, Fusswilat aya ya 37 na As
Sajida aya ya 15 kila sura ina aya moja ya sijida ya wajibu na zinabainish-
wa katika misahafu mitukufu na ni wajibu kwa mtu atakapo isoma au
kuisikia asujudu baada ya kukamilika kusomwa aya kwa haraka, na kama
atasahau kusujudu wakati ule ule, basi asujudu akikumbuka.
Inawajibika kusujudu kama ikisomwa aya kamili ama lau ikisomwa nusu
haitolazimu kusujudu.
756.Akisikia aya ya sijda ikisomwa na mtoto ambaye hatofautishi jambo la
kheri na la shari au akasikia kwa mtu ambaye hakukusudia kusoma
Qur’ani, kwa tahadhari ya sunna asujudu, na pia akisikia aya ya sijda
katika kanda za kaseti au redioni.
Yatosha katika sijida ya Qur’an ya wajibu kuweka paji la uso ardhini kwa
lengo la kusujudu hata kama hakusoma dhikri lakini ni sunna kusoma
dhikri na ni bora kusema: “Laa ilaaha illa llahu haqan haqan, laa ilaha
illa llahu imanan wataswidiyqan, laa illaha illallaahu ubudiyatan
wariqan, sajadtu laka ya Rabi ta’abbudan wariqqan laa mustankifan
146
Al-Masailul Islamiyah
Page 161
walaa mustakbiran bal anaa abdun dhalilun dhaiifun khaaifun mustaji-
irun”
TASHAHUD
757. Ni wajibu kukaa katika kila rakaa ya pili ya swala za wajibu na kati-
ka rakaa ya tatu ya swala ya magharibi na rakaa ya nne ya swala ya
adhuhuri, alasiri na isha na hilo ni baada ya kukaa kutoka sijida ya
pili, na kusema hali umetulizana mwili wake “Ash hadu an laa ila
ha illa llaahu wahadahu laa sharika lahu waash hadu anna
Muhammadan abduhu warasuluhu Allahumma swali alaa
Muhammadin waali Muhammadi”
758. Ni wajibu kuyasoma maneno ya tashahudi kwa kiarabu sahihi na kwa
kufuatana kama inavyofahamika.
759. Akisahau tashahud na akasimama kisha akakumbuka kabla ya
kurukuu kuwa hajaleta tashahud atakaa na kuleta tashahudi kisha
atasimama na kusoma yaliyo wajibu katika rakaa hiyo na kukamilisha
swala kisha ataleta sijda sahau baada ya swala kwa kusimama pasipo
mahala pake na akikumbuka ndani ya rukuu au baada ya salamu
atailipa tashahudi na kuleta sijia mbili za sahau kwa ajili ya tashahu-
di iliyo sahauliwa.
759. Ni sunna kwa mwanamke kubananisha mapaja yake wakati wa
tashahudi.
KUTOA SALAM
760. Mwenye kuswali atasema baada ya tashahud katika rakaa ya mwisho
ya swala na akiwa amekaa na kutulizana mwili wake “Assalaam
alaika ayyuha nnabiyyu warahmatullah wabarakatuh assalam
alainaa waalaa ibaadillah sswalihiyna assalaam alaikum warahmat-
147
Al-Masailul Islamiyah
Page 162
ullah wabarakatuh”.
761. Akisahau salam na akawa hakukumbuka ila baada ya kumalizika
swala ni wajibu kwa tahadhari alete sijda mbili za sahau na ni vizuri
zaidi kuirudia swala yake.
MPANGILIO
762. Akiacha mpangilio wa swala kwa makusudi mfano akasoma sura
kabla ya Al hamdu au akasujudu kabla ya kurukuu swala yake ita-
batilika.
763. Akisahau nguzo miongoni mwa nguzo za swala kwa mfano akale-
ta sijida mbili kabla ya kuleta rukuu swala yake itabatilika.
764. Akisahau nguzo na akaleta kinachofuatia ambacho si nguzo, kwa
mfano akisahau sijida mbili na akaleta tashahudi ni wajibu alete
nguzo aliyoisahau kisha atarudia kusoma aliyoyasoma mwanzo
kimakosa au kwa kusahau.
765. Akisahau ambayo si nguzo na akaleta nguzo inayofuata, kwa mfano
lau akisahau Al hamdu na akashughulika na rukuu swala yake itasi-
hi.
766. Akileta sijida ya kwanza kwa kuamini kuwa ni sijida ya pili itah-
esabika kuwa ni sijda ya kwanza au akileta sijida ya pili k0wa
kuamini kuwa ni sijda ya kwanza itahesabika kuwa ni sijida ya pili na
swala yake itasihi.
KUFUATANISHA
767. Ni wajibu kwa mwenye kuswali kuchunga mfuatano wa swala yaani
alete vitendo vya swala kama vile kurukuu, kusujudu na tashahud kwa
kufuatana na bila ya kutenganisha, pia achunge na afuatanishe katika
dhikir ambazo anazisoma kama inavyofahamika, na lau atatenganisha kati
148
Al-Masailul Islamiyah
Page 163
ya mambo haya kiasi ambacho haitasemwa kwamba anaswali, swala
yake itabatilika.
768. Akitenganisha kati ya herufi na manaeno ya swala kwa kushau laki-
ni kutenganisha huko sio kwa kiasi cha kufuta utaratibu wa swala
kama hakushughulika na nguzo inayofuata ni wajibu kurudia kiso-
mo cha herufi na maneno yale kwa kufuatanisha na kwa njia yenye
kufahamika na lau kama ameshughulika na nguzo iliyofuata swala
yake itasihi.
769. Kurefusha rukuu na sijida na kusoma sura ndefu hakuvunji wala
hakuharibu mfuatano wake.
KUNUTI
770. Ni sunna kusoma kunuti katika swala zote za wajibu na za sunna na
hilo ni kabla ya kwenda rukuu ya rakaa ya pili bali ni vizuri
kutokuacha kunuti katika swala za wajibu na ni sunna kusoma kunuti
katika swala ya witiri japokuwa ni rakaa moja.
771. Katika kila rakaa ya swala ya ijumaa kuna kunuti na katika swala za
majanga kuna kunuti tano, na katika swala ya Iddi rakaa ya kwanza
ina kunuti tano na rakaa ya pili ina kunuti nne, na ni bora kutokuacha
kunuti za swala ya Iddil- Fitri na Adhuhaa.
772. Ni Sunna kwa mwenye kuswali kudhihirisha kunuti yake lakini ni
makuruhu kwa anayeswali jamaa kudhihirisha kunuti yake kama
Imamu atasikia sauti yake.
KUMSWALIA MTUME (SAWW)
773. Ni sunna kumswalia Mtume na watu wa nyumbani kwake pindi
149
Al-Masailul Islamiyah
Page 164
usikiapo majina yake matukufu kama Muhammadi, Ahmadi au sifa
yake kama Mustwafaa au lakabu yake kama Abul – Qasim na hata
akisikia dhamiri inayomkusudia Mtume hata kama yupo kwenye
swala.
774. Ni sunna kuandika “kumtamkia rehema Mtume” pindi unapoandika
majina yake matukufu na pia kumtakia rehema Mtume na watu wa
nyumbani kwake anapowataja.
775. Namna ya kumtakia rehema Mtume ni kusema: “Allahuma swali
alaa Muhammadi wa Aali Muhammadi”
VINAVYO BATILISHA SWALA
776. Vitu vinavyobatilisha swala ni kumi na mbili:-
Kukosekana sharti miongoni mwa masharti ya swala.
Kutenguka udhu au josho
Kuweka mkono juu ya mwingine “juu ya tumbo”
Kusema “amina” baada ya Al hamdu
Kukipa kibla mgongo
Kuzungumza
Kukohoa
Kulia kwa ajili ya mambo ya kidunia
Kufutika sura ya swala
Kula na kunywa
Baadhi ya vifungu vya shaka
Ziada au upungufu katika nguzo za swala na zinginezo kwa ujumla.
YA KWANZA
777. Cha kwanza katika vinavyobatilisha swala ni kukosekana katikati
ya swala sharti miongoni mwa masharti yake, mfano atambue
katikati ya swala kuwa sehemu anayoswalia ni ya unyang’anyi na
150
Al-Masailul Islamiyah
Page 165
hawezi kuhamia katika sehemu iliyohalali bila ya kufanya mambo
mengi ya kufuta sura ya swala.
YA PILI
778. Cha pili katika vinavyobatilisha swala ni kupatwa katikati ya swala
na moja ya vitenguzi vya udhu au josho, kwa kukusudia au kusahau
au kwa dharura mfano kutokwa na mkojo.
779. Al- masluus– Anayetokwa na mkojo kila wakati, au al – mabtun –
anayetokwa na haja kubwa mara kwa mara wakifanya kutokana na
wadhifa wao ambao tumeutaja katika hukumu za udhu swala zao
hazitabatilika. Na vile vile Mustahadha swala yake itasihi akitokwa
na damu katika swala akizingatia hukumu za istahadha.
780. Mwenye kughafilika na akalala bila ya hiyari kama hatajua amelala
ndani ya swala au baada ya swala, ni lazima arudie swala kwa
tahadhari ya wajibu ndani ya muda, na ni sunna alipe nje ya wakati.
781. Akitambua kuwa amelala kwa kutaka kwake na akasahau kuwa
amelala baada ya swala au katikati ya swala, swala yake itasihi.
782. Atakapoamka usingizini katika hali ya sijda na akashuku kuwa
amelala katika sijda ya mwisho ya swala au katika Sijida ya
kushukuru, “Baada ya swala” ni lazima arudie swala kwa tahadhari
ya wajibu ndani ya wakati, na ni sunna airudie nje ya wakati
YA TATU
783. Cha tatu katika vinavyobatilisha swala ni “takfiri” nayo ni kuwe-
ka moja ya mikono miwili juu ya mwingine kama wafanyavyo
wasiokuwa Shia.
151
Al-Masailul Islamiyah
Page 166
784. Akiweka mkono juu ya mwingine ni lazima arudie swala na hata
kama hatafanya mfano wa takfiri zao, lakini hakuna tatizo kama
atafanya hivyo kwa kusahau, au kwa dharura au akifanya hivyo kwa
kujikuna na mfano wake.
YA NNE
785. Cha nne katika vinavyobatilisha swala ni kusema “Amin” baada ya
kusoma Al – hamdu ,na akisema hivyo kwa kusahau au taqiya swala
yake haitobatilika.
YA TANO
786. Cha tano katika vinavyobatilisha swala ni kukipa kibla mgongo kwa
kukusudia au kusahau au kwa kutokujua au akigeukia kulia au
kushoto mwa kibla, bali hata kwa makusudi kwa kiasi kwamba
haisemekani kuwa ameelekea kibla swala yake inabatilika hata kama
hajageuka kulia au kushoto.
787. Akigeuza kichwa chake mwelekeo wa kibla kwa kukusudia au kwa
kusahau kiasi kwamba anaweza kuona nyuma swala yake inabati-
lika, lakini akigeuza uso wake kidogo kwa kukusudia au kwa kusa-
hau swala yake haibatiliki
YA SITA
788. Cha sita katika vinavyobatilisha swala ni kutamka neno lenye
herufi mbili au zaidi hata kama halina maana lakini akifanya
hivyo kwa kusahau swala yake haibatiliki.
789. Akitamka neno lenye herufi moja na lenye maana mfano “Qi” amba-
cho ni kitendo cha amri ambacho kinatokana na “waqaa, yaqii” kwa
maana ya hifadhi, akifahamu maana ya kitendo hiki na akakusudia
kutamka, swala yake inabatilika, kwa tahadhari ya wajibu arudie
152
Al-Masailul Islamiyah
Page 167
swala hata kama hakukusudia maana yake lakini alikuwa anatam-
bua kuwa maana yake ni hiyo.
790. Hakuna tatizo katika kukohoa, kucheua na kupiga miayo kwenye
swala, lakini kauli “akh” “ah” na zingine zenye herufi mbili zin-
abatilisha swala kama zikitamkwa kwa kukusudia.
791. Hakuna tatizo akitamka neno kwa kukusudia utajo mfano akisema:
“Allahu Akbar” kwa sauti ya juu ya kumzindua mwenzake katika
jambo fulani, na akitamka neno kwa kukusudia uzinduzi wa kufa-
hamisha jambo fulani na bila kukusudia kuwa ni dhikri swala ita-
batilika.
792. Hakuna tatizo kusoma Qur’an katika swala isipokuwa sura za
“Azaim” zenye sijida za lazima ambazo utajo wake umeshapita kati-
ka hukumu za janaba, na pia hakuna tatizo katika kutaja majina ya
Mwenyezi Mungu katika swala, na pia hakuna tatizo kwenye dua,
kwa tahadhari ya wajibu asiombe dua ila kwa kiarabu.
793. Hakuna tatizo katika kurudiarudia sehemu katika suratul - Hamdu au
sura au mengineyo miongoni mwa dhikri za swala mara nyingi kwa
tahadhari, pia hakuna tatizo akirudia rudia bila ya kukusudia au
kutenganisha, lakini akirudia rudia kitu kwa sababu ya wasiwasi
swala yake itaharibika kwa tahadhari
SALAMU KATIKA SWALA
794. Mwenye kuswali hatakiwi amsalimie yeyote lakini anaposalimiwa
ni wajibu arudishe salamu kama alivyosalimiwa , yaani arudishe
salamu kwa matamshi yale yale, mfano akiambiwa “Asalam
Alaykum” mwenye kuswali arudishe salamu kwa kusema “ Asalamu
Alaikum” lakini akisema “Alaikum Salam” kwa tahadhar aseme
“Asalam Alaykum”
153
Al-Masailul Islamiyah
Page 168
795. Ni wajibu kurudisha salamu haraka katika swala au nje ya swala, na
akichelewa k`urudisha salamu kwa kukusudia au kwa kusahau kwa
muda kiasi kwamba akirudisha salamu haitahesabika kuwa ni
jawabu la ile salamu akiwa katika swala asirudishe salamu na akiwa
nje ya swala si wajibu kurudisha salamu.
796. Si wajibu alete jawabu la salamu kwa nia ya dua kwa kunuia kwa
kauli yake “Assalam alaikum” kuomba amani kutoka kwa Mwenyezi
Mungu kwa yule aliyemsalimia lakini inajuzu alete kwa kusudio la
kurudisha salamu.
797. Mwanamke akimsalimia mwanaume ajinabi katika swala au
mwanaume akimsalimia mwanamke ajinabiya katika swala au ikiwa
mwenye kusalimia ni mtoto wa kiume aliyepevuka, inajuzu kwa
mwenye kuswali bali ni wajibu wake arudishe salamu.
798. Mwenye kuswali asiporudisha salamu atakuwa ameasi na amepata
dhambi lakini swala yake inasihi.
799. Mtu akimsalimia mwenye kuswali kwa kukosea maneno kama ita-
hesabika kuwa ni salamu au kama atakosea katika matamshi yake
ni wajibu arudishe salamu na isipohesabika kuwa ni salamu si
wajibu kurudisha, bali haijuzu kurudisha salamu ndani ya swala.
800. Si wajibu kuitikia salamu kwa anayesalimia kwa mzaha au kejeli pia
haijuzu kumwitikia katika swala.
801. Mtu akisalimia kundi la watu ni wajibu kwa watu wale kuitikia sala-
mu, pia inatosha akiitikia mmoja wao.
802. Mtu anaposalimia watu na akaitikia asiyekusudiwa kurudisha salamu
haitaporomoka kwa waliokusudiwa bali ni wajibu wao kurudisha
salamu.
154
Al-Masailul Islamiyah
Page 169
803.Mtu anaposalimia watu na mwenye kuswali akaitilia shaka kuwa
msalimiaji alimkusudia yeye au hakumkusudia, haijuzu kwa mwenye
kuswali kurudisha salamu, na pia akitambua kuwa msalimiaji
alimkusudia lakini wakajibu wengine inatosha, na akitambua kuwa
msalimiaji alimkusudia yeye halafu hakujibu hata mmoja ni lazima
yeye arudishe salamu.
804.Kuanza kusalimia ni sunna na imetiliwa mkazo kuwa mwenye kipan-
do aanze kumsalimia asiye na kipando, aliyesimama kwa aliyekaa na
mdogo amsalimie mkubwa ama kuitikia salamu ni wajibu.
805. Zikigongana salamu za watu wawili kwa tahadhari kila mmoja
aitikie salamu ya mwingine.
806. Ni sunna kurudisha salamu kwa iliyobora zaidi nje ya swala, mfano
mtu akisema “salam Alaykum” ajibu kwa kusema “salam alaikum
warahmatu llaahi”
YA SABA
807. Cha saba katika vinavyobatilisha swala ni kucheka kwa sauti, kwa
kukusudia au kwa dharura, ama akicheka kwa kusahau hakuna tatizo
katika swala, isipokuwa asitoke katika sura ya swala, ama
kutabasamu haibatilishi swala.
808. Ikibadilika hali yake kwa ajili ya kujizuia kudhihirisha sauti ya
kicheko mfano, rangi yake kuwa nyekundu kwa tahadhari ya sunna
arudie swala yake, lakini akitoka katika sura ya swala hapo atawa-
jibika kurudia swala.
YA NANE
809. Cha nne katika vinavyobatilisha swala ni kukusudia kulia kwa sauti
kwa ajili ya mambo ya kidunia, kwa tahadhari ya wajibu asilie kwa
155
Al-Masailul Islamiyah
Page 170
ajili mambo ya kidunia hata bila ya sauti lakini hakuna tatizo kulia
kwa ajili ya kumnyenyekea Mwenyezi Mungu au kwa ajili ya
mambo ya akhera kwa sauti ya juu au ya chini bali hili ni katika
vitu vizuri na pia inajuzu kwa dhahiri kulia kwa misiba ya Mtume
na watu wa nyumbani kwake “as.”
YA TISA
810. Cha tisa katika vinavyobatilisha swala ni kufanya kitendo kina-
chofuta sura ya swala kama kupiga makofi sana au kuruka sana
n.k. kwa kukusudia au kusahau lakini hakuna tatizo kufanya kitu
kisichofuta sura ya swala kama kuashiria kwa mkono.
811. Akinyamaza kwa muda mrefu kwenye swala kiasi kwamba haise-
mekani kuwa anaswali swala yake inabatilika.
812. Akileta kitendo katika swala au akinyamaza kwa muda, akitilia
shaka kuwa imefutika sura ya swala au laa swala yake inasihi.
YA KUMI
813. Kumi katika vinavyobatilisha swala ni kula na kunywa, akila au kun-
ywa katika swala kiasi kwamba haisemekani kuwa anaswali swala
yake inabatilika kwa kukusudia au kwa kusahau.
814. Anayetaka kufunga ikiwa anajishughulisha na swala ya witiri kabla
ya adhana ya alfajiri na akawa na kiu na akahofia kuingia Al fajiri
kama atakamilisha swala ya witiri na atabanwa na kiu inaruhusiwa
anywe maji katika swala kama maji yatakuwa mbele yake au karibu
kwa hatua chache na ajihadhari na vinavyobatilisha swala kama vile
kukipa kibla mgongo na mengineyo.
156
Al-Masailul Islamiyah
Page 171
815. Akimeza mabaki ya chakula yaliyokuwepo katika meno au
mdomoni haibatiliki swala. Ikibaki sukari na yanayofanana na
sukari mdomoni kisha yakayeyuka katika swala kidogo kidogo na
kuingia tumboni pia swala haibatiliki
YA KUMI NA MOJA
816. Cha kumi na moja katika vinavyobatilisha swala ni kutilia shaka
katika swala za rakaa mbili, tatu au katika rakaa mbili za awali kati-
ka swala za rakaa mbili
YA KUMI NA MBILI
817. Cha kumi na mbili katika vinavyobatilisha swala ni kupunguza au
kuongeza nguzo miongoni mwa nguzo za swala na pia kuongeza au
kupunguza kwa kukusudia visivyokuwa nguzo lakini ziada ya takbi-
ratul ihram kwa kusahau haibatilishi swala.
818. Akitilia mashaka baada ya kumaliza swala kuwa ameleta kina-
chobatilisha swala au laa swala yake inasihi.
YALIYO MAKURUHU KATIKA SWALA
819. Ni makuruhu kugeuza uso wake kulia na kushoto au kufumba macho
au kugeuza macho kulia na kushoto au kuchezea ndevu au mikono
au kuliza (kubinya au kuvunja) vidole au kutema mate au kuangalia
hati ya Qur’an au kitabu au maandishi ya pete katika swala, vile vile
kunyamaza katikati ya kusoma Al – hamdu au sura nyingine au
kunyamza kwa ajili ya kusikiliza maneno ya mtu, bali ni makuruhu
kuleta chochote kinachotoa unyenyekevu na umakini unaotakiwa
katika swala.
157
Al-Masailul Islamiyah
Page 172
820. Ni makuruhu kuswali wakati umebanwa na usingizi au mkojo au haja
kubwa na pia kuvaa soksi zinazobana miguu katika swala.
SEHEMU AMBAZO NI WAJIBU
KUKATA SWALA
821. Haijuzu kukata swala kwa hiyari, lakini hakuna kizuizi kukata swala
kwa ajili ya kuhifadhi mali au kuondoa madhara ya kimali na
kimwili.
822. Kama haiwezekani kwa mwenye kuswali kuhifadhi nafsi yake au
kuhifadhi ambao anawajibika kuwahifadhi, au kuhifadhi mali
ambayo ni wajibu kuihifadhi bila ya kukata swala, na pia ni maku-
ruhu kukata swala kwa kuhifadhi mali isiyokuwa na muhimu.
823. Akijishughulisha na swala katika muda mpana kisha akadaiwa na
anayemdai, ikiwezekana kulipa deni bila ya kukata swala alipe hali
ya kuwa katika swala, na kama haitawezekana kulipa deni bila ya
kukata swala, basi ni wajibu akate swala ili alipe deni, na kama
hatakata swala, swala yake itasihi japo kuwa atakuwa ameasi, kwa
kutokulipa deni.
824. Akifahamu katikati ya swala kunajisika msikiti, kama wakati wa
swala ni mfinyu ni wajibu akamilishe swala, na kama wakati ni
mpana ikiwezekana kutoharisha msikiti italazimu kuvunja swala, na
ikiwezekana kutoharisha msikiti baada ya swala basi haitaruhusiwa
kukata swala, na ikiwa kubakia najisi msikitini kunasabisha udhalili
kwa msikiti katika sura hii ni wajibu kukata swala ili atoharishe msik-
iti, kisha aswali na pia ni wajibu kukata swala kama haitawezekana
kutoharisha msikiti baada ya swala.
158
Al-Masailul Islamiyah
Page 173
825. Mwenye kuwajibikiwa kukata swala kisha akaacha kukata na
akakamilisha atakuwa ameasi japokuwa swala yake itasihi.
826. Akikumbuka kabla ya kuinama kwa kiasi cha rukuu kuwa amesa-
hau adhana na iqama kama wakati utamruhusu ni sunna akate swala
kwa ajili ya kuleta adhana na iqama.
SHAKA
827. Shaka za swala zimegawanyika katika mafungu 23 nane kati ya hizo
zinabatilisha swala na sita ni wajibu zisizingatiwe na tisa hazibatilishi
swala.
828. Shaka zinazobatilisha swala ni kama zifuatazo:-
Shaka ya idadi ya rakaa katika swala za rakaa mbili kama swala ya asub-
uhi au swala ya msafiri lakini akitilia shaka katika idadi ya rakaa katika
swala za sunna zenye rakaa mbili na swala ya ihtiyati swala haibatiliki
kwa sababu yake.
Shaka katika idadi ya rakaa katika swala yenye rakaa 3
Akishuku katika swala ya rakaa nne kuwa ameswali rakaa moja au zaidi
Akishuku katika swala ya rakaa nne kabla ya kukamilisha sijida ya pili
kuwa ameswali rakaa mbili au zaidi.
Shaka baina ya rakaa mbili au tano au rakaa mbili au zaidi ya tano.
Shaka baina ya tatu na sita au tatu na zaidi ya sita .
Shaka katika idadi ya rakaa kiasi kwamba hajui rakaa ngapi ameswali.
Shaka baina ya rakaa nne na sita au baina ya rakaa nne na zaidi ya sita
kabla ya kukamilisha sijida ya pili lakini kama akishuku baada ya sijida
159
Al-Masailul Islamiyah
Page 174
ya pili baina ya nne na sita au baina ya nne na zaidi ya sita kwa tahadhari
ajengee kuwa ameswali rakaa nne kisha akamilishe swala, baada ya hapo
alete sijida mbili za kusahau baada ya swala na pia arudie swala.
829. Mwenye kuswali akitokewa na moja ya shaka zinazobatilisha swala
inaruhusiwa kukata swala au afikirie mpaka sura ya swala ifutike na
akate tamaa ya kupata uhakika wa rakaa alizoziswali.
SHAKA ZISIZOTILIWA MAANANI
830. Shaka ambazo ni wajibu zisizingatiwe na wala zisitiliwe maanani ni
kama zifuatazo:-
Shaka ya kitu baada ya kupita sehemu yake mfano apate shaka katika
rukuu kuwa amesoma Al – hamdu au laa.
Shaka baada ya salamu
Shaka baada ya kupita muda wa swala
Mwingi wa shaka
Shaka ya Imam katika idadi ya rakaa wakikumbuka maamuma katika idadi
ya rakaa, na vile vile shaka ya maamuma kama Imam akikumbuka idadi ya
rakaa.
Shaka katika swala za sunna.
1 – SHAKA YA KITU BAADA YA KUPITA
SEHEMU YAKE
831. Akishuku katikati ya swala kuwa ameleta baadhi ya vitu
vilivyokuwa ni wajibu au hakuvileta mfano – akitilia shaka kuwa
amesoma Al – hamdu au laa, kama hajajishughulisha na yanayokuja
160
Al-Masailul Islamiyah
Page 175
baada ya Al hamdu au baada ya alichokuwa akikishuku basi asizin-
gatie shaka yake.
832. Akitilia shaka katikati ya kusoma aya kuwa amesoma aya iliyopita au
laa au akitilia shaka katika aya anayoisoma kuwa amesoma mwanzo
wa aya au laa asizingatie shaka yake.
833. Akitilia shaka baada ya kurukuu na kusujudu kuwa ameleta baadhi ya
mambo ya wajibu katika swala kama vile dhikri, utulivu wa mwili au
laa, asizingatie shaka yake.
834. Akitilia shaka wakati anakwenda katika sijida kuwa ameleta rukuu
au laa au alisimama wima baada ya rukuu au laa asizingatie shaka
yake.
835. Akitilia shaka katika hali ya kunyanyuka kuwa ameleta sijida au
tashahudi au laa, asizingatie shaka yake.
836. Mwenye kuswali kwa kukaa au kulala akitilia shaka katikati ya
kusoma Al- hamdu au tasbihi nne kuwa ameleta tashahudi au sijida
au laa ni wajibu asizingatie shaka yake.
837. Kama akishuka katika kuleta sijida au tashahudi kabla ya kusoma
Al – hamdu au tasbihi, lazima alete alicho kitilia shaka.
838. Akishuku katika kutekeleza moja ya nguzo za swala kama atakuwa
ameshapita hiyo sehemu aliyoishuku basi asizingatie shaka yake,
kinyume na hapo kama alichotilia shaka atakumbuka baadae kuwa
alishaleta nguzo ya swala, basi swala yake itabatilika kwa kuongeza
nguzo ya ziada.
839. Akishuku katika kutekeleza kitu kisichokuwa ni nguzo kama atakuwa
amepita hiyo sehemu asizingatie hiyo shaka la sivyo ataleta alichoki-
161
Al-Masailul Islamiyah
Page 176
tilia shaka, akikumbuka baada ya kuisoma kuwa alishaisoma kabla ya
hapo swala yake inasihi, kwa kutozidisha nguzo, na ataleta sijida
mbili za kusahau kwa tahadhari ya wajibu.
840. Akishuku katika kuleta moja ya nguzo za swala, kama amejishughul-
isha na ambacho kinafuata baada ya nguzo hiyo asizingatie shaka
yake mfano akitilia shaka katikati ya tashahudu kuwa ameleta sijida
mbili au laa, asizingatie shaka yake, ama akikumbuka kuwa hakule-
ta hiyo nguzo aliyoisahahu na kama atajishughulisha na nguzo
nyingine swala yake itakuwa imebatilika mfano akikumbuka kabla ya
kurukuu katika rakaa ifuatayo kuwa hajaleta sijida mbili katika rakaa
iliyopita basi alete hizo sijida mbili, na kama atakumbuka katikati ya
rukuu au baada ya rukuu swala yake inabatilika.
841. Akitilia shaka katika kutekeleza jambo ambalo si nguzo katika
matendo ya swala, na akajishughulisha na kitendo kifuatacho baada
ya hicho ni wajibu asizingatie shaka yake kwa mfano akitilia shaka
katika kusoma sura kuwa amesoma Al – hamdu au laa, ni wajibu
asizingatie shaka yake ama akikumbuka kuwa hakuleta kile kitendo
kabisa kama hajajishughulisha na kitendo ambacho ni nguzo ni
wajibu alete kitendo hicho alichokisahau, na kama atajishughulisha
na nguzo swala yake inasihi, kwa hiyo akikumbuka akiwa katika
kunuti kuwa hakusoma Al – hamduu ni wajibu asome Al – hamdu na
akikumbuka katika hali ya rukuu swala yake inasihi.
842. Akishuku kuwa ametoa salamu ya swala au laa, au akishuku kuwa
ameileta kwa usahihi au laa, kama shaka hizo mbili ni baada ya
kujishughulisha na nyuradi zinazofuatia baada swala kama vile dua au
kuanza swala nyingine, au baada ya kuleta kinachovunja swala na
kutoka katika hali ya mwenye kuswali au akawa anajiona kuwa hali
yake iko nje ya swala, basi asizingatie shaka yake ama shaka yake
ikiwa kabla ya vitu hivi ni wajibu atoe salamu upya.
162
Al-Masailul Islamiyah
Page 177
2 SHAKA BAADA YA SALAMU
843. Akishuku baada ya salamu kuwa swala yake imesihi au laa, mfano
akitilia shaka kuwa amerukuu baada ya salamu, au akashuku baada ya
salamu katika swala ya rakaa nne kuwa ameswali rakaa nne au tano
asizingatie shaka yake, lakini ikiwa pande mbili hizi za shaka zin-
abatilisha swala mfano akishuku baada ya salamu katika swala ya
rakaa nne kuwa ameswali rakaa mbili au tano swala yake inabatilika.
3. SHAKA BAADA YA KUPITA WAKATI
844. Akishuku baada ya kupita muda kuwa ameswali au laa, akidhani
kuwa hakuswali kabisa, haimlazimu kuswali lakini akitilia shaka
kabla ya wakati kwisha kuwa ameswali au laa au akidhani kuwa
hakuswali kabisa ni wajibu aswali hata akidhani kuwa ameswali.
845. Akishuku baada ya kupita wakati kuwa ameswali kwa usahihi au laa
asizingatie shaka yake.
846. Akitambua baada ya kupita wakati wa adhuhuri na alasiri kuwa
ameswali rakaa nne tu, na hatambui kuwa ameziswali kwa nia gani ya
adhuhuri au alasiri ni wajibu aswali rakaa nne zingine za kadha kwa
nia ya yanayomuwajibikia.
847. Akitambua baada ya kupita wakati wa swala ya Magharibi na Isha
kuwa ameswali moja wapo kati ya swala hizi na hajui ameswali
rakaa tatu au nne ni wajibu alipe kadha ya Magharibi na Isha pamo-
ja.
4- MWINGI WA SHAKA
848. Mtu akishuku mara tatu katika swala moja au akishuku katika swala
tatu zinazofuatana kwa mfano asubuhi, adhuhuri na alasiri atahesabi-
163
Al-Masailul Islamiyah
Page 178
ka kuwa ni mwingi wa shaka kwa hiyo haimlazimu kuzingatia shaka
yake kama wingi wa shaka zake unasababishwa na hasira, woga au
fikra nyingi.
849. Mwingi wa shaka akishuku katika kutekeleza jambo ikiwa jambo hilo
halibatilishi swala atajengea kuwa ametekeleza, mfano akishuku
kuwa amerukuu au laa atajengea kuwa amerukuu, na kama ikiwa
kutekeleza hilo jambo linabatilisha swala basi inabidi ajengee kuwa
hajafanya, mfano akishuku kuwa ameleta rukuu moja au zaidi ya
moja,anajengea kuwa hajaleta zaidi ya moja kwa sababu ziada ya
rukuu inabatilisha swala.
850. Mwingi wa shaka akishuku katika sehemu moja tu katika swala,
akishuku katika sehemu nyingine nje ya ile inatakiwa afanye kama
afanyavyo mwingi wa shaka, mfano akiwa mwingi wa shaka katika
sijida, kuwa amesujudu au laa, na akatilia shaka katika rukuu lazima
afanye kama anavyofanya mwingi wa shaka yaani atarukuu kama
alikuwa amesimama na hatazingatia shaka yake kama itakuwa baada
ya kwenda sijida.
851. Mwingi wa shaka akishuku katika swala maalumu pasina zingine
mfano akiwa anakithirisha shaka katika swala ya adhuhuri pasina
zingine na akishuku kwenye swala zingine kama swala ya alasiri kwa
mfano mwisho wa swala atafanya kama anavyofanya mwenye shaka
ya kawaida.
852. Mwingi wa shaka akishuku katika swala katika sehemu maalumu
pasina sehemu nyingine kama vile sehemu yenye makelele akiswali
sehemu nyingine ikamtokea shaka ni wajibu afanye kama afanyavyo
mwenye shaka ya kawaida.
853. Mwenye kushuku kwa sababu ni mwingi wa shaka ni wajibu afanye
kama afanyavyo mwenye shaka ya kawaida na mwingi wa shaka
164
Al-Masailul Islamiyah
Page 179
asizingatie shaka yake maadamu hana uhakika wa kurudi katika hali
ya watu wa kawaida
954. Mwenye kushuku katika nguzo miongoni mwa nguzo za swala kisha
akawa hajazingatia shaka yake, kisha akakumbuka kuwa hakuileta ile
nguzo kama hajajishughulisha na nguzo nyingine ni wajibu alete
nguzo aliyoisahau, na ikiwa ameanza kujishughulisha na nguzo
nyingine swala itakuwa imebatilika, mfano akishuku kuwa amerukuu
au laa, akawa hajazingatia shaka yake, akikumbuka kabla ya sijida
kuwa haja rukuu, ni wajibu alete rukuu aliyoisahau ama akikumbuka
katika sijida ya pili swala yake inabatilika.
855. Mwingi wa shaka akishuku katika kuleta kisichokuwa nguzo na
akawa hajazingatia shaka yake, akikumbuka kuwa hajaleta kabisa kile
alichokuwa anakishuku, kama atakuwa hajapita hiyo sehemu lazima
akilete na kama atakuwa amepita hiyo sehemu swala yake inasihi,
mfano akishuku kuwa amesoma Al- hamdu au laa kisha akawa
hajazingatia shaka yake akikumbuka katika kunuti kuwa hajasoma Al
– hamdu ni wajibu asome Al – hamdu na akikumbuka katika rukuu
swala yake inasihi.
5- SHAKA YA IMAMU NA MAAMUMA
856. Imamu akishuku katika swala ya jamaa katika idadi ya rakaa mfano
akishuku kuwa ameswali rakaa tatu au nne, ikiwa maamuma
wanauhakika kuwa ameswali rakaa nne na wakamfahamisha Imamu
kuwa ameswali raka nne inamlazimu Imamu akamilishe swala, na
haitamlazimu kuswali swala ya ihityati, vile vile Imamu akiwa na
uhakika katika idadi maalumu za rakaa na maamuma akishuku katika
idadi ya rakaa ni lazima kwa maamuma asizingatie shaka yake.
6- SHAKA KATIKA SWALA YA SUNNA
857. Akishuku katika swala za sunna, ikiwa upande wa wingi wa shaka
165
Al-Masailul Islamiyah
Page 180
unabatilisha swala atajengea katika uchache mfano ikimtokea shaka
katika sunna ya asubuhi kuwa ameswali rakaa mbili au tatu itamlaz-
imu ajengee kuwa ameswali rakaa mbili na ikiwa upande wa wingi
wa shaka haubatilishi swala, mfano akishuku kuwa ameswali rakaa
mbili au moja atafanya njia yoyote anayotaka yaani anaweza
kujengea kuwa ameswali rakaa mbili na kukamilisha swala au kujen-
gaea kuwa ameswali rakaa moja na kumalizia rakaa ya pili na swala
inasihi.
858. Upungufu wa nguzo unabatilisha swala ya sunna lakini ziada yake
haibatilishi swala, akisahau moja ya vitendo vya swala ya sunna na
hakukumbuka ila baada ya kuingia katika nguzo, atakuwa na haki ya
kuleta alichokisahau na kurudia ile nguzo mara nyingine mfano
akikumbuka katika rukuu kuwa hakusoma Al- hamdu na akawa ames-
imama wima basi utambidi asome Al- hamdu na kurukuu mara ya pili.
859. Akishuku katika kuleta moja ya matendo ya swala ya sunna iwe ni
katika nguzo au isiyokuwa nguzo itatakiwa alete alichokishuku,
maadamu hajapita sehemu yake na asizingatie shaka yake kama
atakuwa amepita hiyo sehemu.
860. Akidhani katika sunna ya rakaa mbili kuwa ameleta rakaa tatu au
zaidi ya tatu asizingatie dhana yake na swala itasihi na kama atadhani
kuwa ameleta rakaa mbili au chini ya mbili kwa tahadhari ya sunna
atafanya kutokana na dhana yake mfano akidhani kuwa ameswali
rakaa moja basi atakamilisha swala yake kwa kumalizia rakaa ya pili.
861. Akifanya katika swala ya sunna ambayo yanasababisha sijida ya
kusahahu au akisahau sijida au tashahudu, haitamlazimu baada ya
swala alete sijida sahau au kuleta kadha ya sijida iliyosahaulika au
tashahudi iliyosahaulika, na ingawa kwa tahadhari alete alichokisa-
hahu baada ya swala.
166
Al-Masailul Islamiyah
Page 181
862. Akishuku kuwa ameswali swala ya sunna au laa kama swala hiyo
haitakuwa ya muda maalum kama swala ya “Jafari Twayaar” ata-
jengea kuwa hajaswali na vile vile atajengea kuwa hajaswali akitia
shaka katika swala za sunna za kila siku ambazo zinakuwa na muda
maalumu na ikiwa shaka yake ni kabla ya kupita muda na kama aki-
tilia shaka baada ya muda kupita basi hatazingatia shaka yake.
7. SHAKA ZISIZOBATILISHA SWALA
863. Ni wajibu kwa mwenye kuswali kutafakari haraka akishuku katika
idadi ya rakaa katika swala za rakaa nne na hiyo ni katika sura tisa, na
kama fikra yake itampelekea kupata yakini au dhana katika moja ya
pande mbili basi itabidi achukue ambayo inampelekea kupata yakini
au dhana yake katika upande huo na kukamilisha swala, na kama
mawazo yake na fikira zake hazitampa jawabu maalum basi atafanya
kutokana na kanuni ambazo ufafanuzi wake utakuja baadae
SURA YA KWANZA
864. Akishuku baada ya kunyanyua kichwa katika sijida ya pili kuwa
ameswali rakaa mbili au tatu katika sura hii ni wajibu ajengee kuwa
ameswali rakaa tatu, atasimama na kuleta rakaa nyingine na kukamil-
isha swala kisha ataleta baada ya swala rakaa moja ya swala ya ihtiy-
ati kwa kusimama na rakaa mbili kwa kukaa vilevile kama
utakavyokuja ufafanuzi wake baadaye
SURA YA PILI
865. Akishuku kati ya rakaa mbili au nne baada ya kunyanyua kichwa kati-
ka sijida ya pili hapo ni wajibu ajengee kuwa ameswali rakaa nne na
kukamilisha swala akiwa amekaa kisha ataleta rakaa mbili za swala ya
ihtiyati baada ya swala kwa kusimama kwa tahadhari
167
Al-Masailul Islamiyah
Page 182
SURA YA TATU
866. Akishuku kati ya rakaa mbili, tatu na nne baada ya sijida ya pili yaani
hajui kuwa ameswali rakaa mbili, tatu au nne katika hali hii atajengea
kuwa ameswali rakaa nne na atakamilisha swala hali ya kuwa amekaa
kisha ataleta rakaa mbili za swala za ihtiyati kwa kusimama na rakaa
mbili kwa kukaa pia.
SURA YA NNE
867. Akishuku kati ya rakaa nne na tano baada ya kunyanyua kichwa
katika sijida ya pili, atajengea kuwa ameswali rakaa nne na kukamil-
isha swala hali ya kuwa amekaa na ataleta sijida mbili za kusahau
baada ya swala.
868. Ikitokea moja ya shaka hizi nne baada ya kuleta dhikri katika sijida
ya pili kabla ya kunyanyua kichwa katika sijida ya pili, basi atafanya
kutokana na hukumu za shaka zilizotajwa na atarudia swala kwa
tahadhari ya sunna na kama atarudia swala tu inatosha.
SURA YA TANO
869. Akishuku kati ya rakaa tatu na nne katika sehemu yeyote ya swala,
lazima ajengee kuwa ameswali rakaa nne na akamilishe swala, kisha
alete rakaa moja ya ihtiyati kwa kusimama au rakaa mbili kwa kukaa
kwa tahadhari
SURA YA SITA
870. Akishuku kati ya rakaa nne na tano akiwa katika hali ya kusimama,
lazima akae na atoe tashahudi na salamu na kukamilisha swala, kisha
ataleta rakaa moja ya ihtiyati kwa kusimama au mbili kwa kukaa na
kwa tahadhari ya wajibu alete sijida mbili za kusahau kwa ajili ya
kisimamo cha ziada.
168
Al-Masailul Islamiyah
Page 183
SURA YA SABA
871. Akishuku kati ya rakaa tatu au tano katika hali ya kusimama itamlaz-
imu akae na atoe tashahudi na salamu na kukamilisha swala kisha
alete rakaa mbili za ihtiyati kwa kusimama kwa tahadhari na kuleta
sijida mbili za kusahau kwa ajili ya kisimamo cha ziada kwa tahad-
hari ya wajibu.
SURA YA NANE
872. Akishuku kati ya rakaa tatu, nne na tano katika hali ya kisimamo ita-
mlazimu akae na atoe tashahudi na salamu na ataleta baada ya salamu
sijida mbili za kusahau na kwa tahadhari ya wajibu alete sijida zingine
za kusahau kwa ajili ya kisimamo cha ziada.
SURA YA TISA
873. Akishuku kati ya rakaa tano na sita katika hali ya kisimamo itamlaz-
imu akae na alete tashahudi na salamu na ataleta baada ya salamu siji-
da mbili za kusahau na kwa tahadhari ya wajibu alete sijida zingine
mbili za kusahau kwa ajili ya kisimamo cha ziada
MAS’ALA MENGINE
874. Mwenye kuswali ikimtokea shaka isiyobatilisha swala itamlazimu
asikate swala kwa tahadhari, ama akianza swala nyingine baada ya
kuvunja ya mwanzo basi swala yake ya pili itasihi.
875. Ikimtokea moja ya shaka zinazosababisha swala ya ihtiyati,
akikamilisha swala yake na akianza swala nyingine bila ya kuleta
169
Al-Masailul Islamiyah
Page 184
swala ya ihtiyati na akawa ameanza swala mpya kabla ya kuleta
kinachobatilisha swala, kama kugeuza uso pembeni mwa kibla,
swala yake ya pili itabatilika pia kwa tahadhari, ama akijishughulisha
na swala ya pili baada ya kuleta kinachobatilisha swala ya kwanza
swala ya pili itasihi.
876. Inapomtokea mwenye kuswali moja ya shaka zisizobatilisha swala ni
wajibu atulie na kufikiria kwa haraka kama ilivyotangulia, lakini aki-
tambua kuwa hatasahau kitu kwa kuchelewa kidogo inajuzu kwake
kufikiri kidogo baadae, mfano akishuku naye yuko katika sijida ina-
juzu kuahirisha kufikiria hadi baada ya sijida.
877. Dhana yake ikielemea moja kati ya pande mbili za shaka katika jambo
moja, kisha dhana yake ikalingana katika pande zote mbili kwa
mtazamo wake, ni wajibu afanye kulingana na hukumu za shaka na
pande zote mbili zikilingana kwa mtizamo wake tangu mwanzo basi
atajengea kutokana na kuelemea kwa moja ya dhana yake, na ni
wajibu afanye kilichowajibu kwake, lakini dhana yake ikielemea
moja ya pande mbili ni wajibu achukue upande ambao swala yake
itasihi na kukamilisha swala.
878. Ambaye hajui kuwa dhana yake imeelemea upande mmoja au pande
zote mbili, ni wajibu afanye kulingana na hukumu za shaka.
879. Akishuku katika tashahudi au baada ya kunyanyuka kuwa ameleta
sijida mbili au laa, kisha ikamtokea hapo hapo shaka isiyobatilisha
swala, ikitokea baada ya kukamilisha sijida mbili, mfano akishuku
kuwa ameswali rakaa mbili au tatu atafanya kulingana na wadhifa
tulioutaja na swala yake itasihi.
880. Akishuku katika hali ya kusimama kati ya rakaa tatu na nne au baina
ya rakaa tatu, nne na tano, na akakumbuka kuwa hajaleta sijida mbili
katika rakaa iliyopita swala yake inabatilika.
170
Al-Masailul Islamiyah
Page 185
881. Ikiondoka shaka yake kisha ikamtokea shaka nyingine, mfano mwan-
zo alishuku kati ya rakaa mbili na tatu kisha akashuku mara ya pili
baina ya tatu na nne, atafanya kulingana na shaka yake ya pili.
882. Akishuku baada ya swala kuwa ameshuku kati ya rakaa mbili au nne
au kati ya tatu na nne ni wajibu afanye kwa shaka zote mbili.
883. Mwenye kuswali kwa kukaa akiweza kusimama katika kuleta swala
ya ihtiyati ni wajibu ailete kwa kusimama.
SWALA YA IHTIYATI
884. Ambaye amewajibikiwa na swala ya ihtiyati ni wajibu anuie kwa
haraka baada ya kumaliza swala, atahirimia na kusoma Al – hamdu tu
atarukuu na kuleta sijida mbili na akiwa katika wale waliowajibiki-
wa na rakaa moja ya ihtiyati ataleta tashahudi baada ya sijida mbili
na kutoa salamu, ama aliyewajibikiwa na rakaa mbili za ihtiyati atasi-
mama baada ya sijida mbili na kuswali rakaa ya pili, kisha ataleta
tashahud na kutoa salamu.
885. Katika swala ya ihtiyati hakuna sura wala kunut na lazima asidhi-
hirishe sauti wakati wa kusoam Al- hamdu wala asidhihirishe nia yake
na kwa tahadhari asidhihirishe hata bismillah pia.
886. Akitambua kabla ya swala ya ihtiyati kuwa swala yake ilikuwa sahi-
hi haimlazimu kuleta swala ya ihtiyati na akitambua hivyo katikati ya
swala ya ihtiyati haimlazimu kuikamilisha, bali inajuzu kuikatisha
popote alipo.
887. Akishuku kati ya rakaa mbili, tatu na nne katika hali ya kuleta rakaa
mbili za ihtiyati katika hali ya kusimama kabla ya kurukuu katika
rakaa ya pili kwamba swala yake ilikuwa ni rakaa tatu lazima akae na
kukamilisha swala ya ihtiyati rakaa moja.
171
Al-Masailul Islamiyah
Page 186
888. Akishuku kuwa ameleta swala ya ihtiyati ambayo alitakiwa aswali au
laa, ikiwa ni baada ya wakati hatazingatia shaka yake, na kama wakati
bado upo na hakujishughulisha na kitu kingine na hajasimama sehe-
mu aliyokuwa anaswalia, na hakuleta kinachobatilisha swala itamlaz-
imu alete swala ya ihtiyat,i na kama ameleta kinachobatilisha au ame-
tenganisha kati ya swala aliyoiswali na shaka hiyo muda mrefu
hatazingatia shaka yake.
889. Akizidisha nguzo katika swala ya ihtiyati au akileta rakaa mbili
badala ya rakaa moja, swala yake ya ihtiyati inabatilika na ni wajibu
kurudia swala upya.
890. Hukumu ya dhana katika idadi ya rakaa ni hukumu ya yakini, ila
dhana ikiwa ni ya kitu kinachosababisha kubatilisha swala katika hali
hii, dhana haitakuwa na hukumu ya yakini, ama dhana katika vitendo
vya swala ingawa haiko mbali na kuiunganisha na yakini, lakini
pamoja na hivyo inalazimu kwa tahadhari ya sunna baada ya kuizin-
gatia dhana akamilishe amali na arudie swala
891. Hakuna tofauti katika hukumu ya shaka, kusahau na kudhani katika
swala za kila siku na swala zingine za wajibu, mfano akishuku katika
swala za majanga kuwa ameleta rakaa moja au mbili, kwa kuwa
swala ya majanga ina rakaa mbili hivyo shaka hiyo inabatilisha swala.
SIJIDA YA KUSAHAU
892. Ni wajibu kuleta sijida mbili za kusahau baada ya salamu kwa namna
ambayo ufafanuzi wake utakuja na hii ni kwa mambo matano:-
(i) Akizungumza katikati ya swala kwa kujisahau
(ii) Akitoa salamu sehemu isiyokuwa ya salamu, mfano akitoa
salamu katika rakaa ya kwanza kwa kujisahau
(iii) Akisahau moja ya sijida mbili
(iv) Akisahau tashahudi
172
Al-Masailul Islamiyah
Page 187
(v) Akishuku baada ya sijida mbili katika swala ya rakaa nne
kuwa ameswali rakaa nne au tano.
893. Akikaa kwa kujisahau katika mahali pa kusimama, mfano akikaa kati-
ka hali ya kusoma Al-hamdu na sura kwa kukosea, au akasimama
katika mahali pa kukaa kama akisimama katika mahali pa tashahudi
kwa kujisahahu, itamlazimu kwa tahadhari ya wajibu alete sijida
mbili za kusahau, na kwa tahadhari ya wajibu alete sijida mbili za
kusahau katika kila ziada au upungufu.
Na hukumu za hali hizi zitatajwa katika mas’ala yajayo.
894. Mwenye kuswali akizungumza kwa kujisahau au akadhani kuwa
swala yake imekamilika, ni wajibu alete sijida mbili za kusahau.
895. Si wajibu kusujudu sijida ya kusahu kwa kutamka herufi ambayo
imesababishwa na kukohoa, kucheua na mengineyo, lakini akisema
Ah, au Akh, kwa kusahau ni wajibu alete sijida mbili za kusahau.
896. Mwenye kurudia kusoma vizuri kwa kukosea mara ya kwanza, haita-
mlazimu alete sijida ya kusahau kwa kukosea.
897. Akizungumza muda mrefu katika swala kwa kujisahau yatahesabika
maneno yake hayo kuwa ni neno moja inatosha alete sijida ya kusa-
hau baada ya swala.
898. Mwenye kuleta tasbihi nne zaidi ya mara tatu kwa kujisahau haitam-
lazimu alete sijida ya kusahau.
899. Akileta salamu nje ya sehemu ya salamu, mfano alete salamu tatu
zisizotajwa, inatosha alete sijida mbili za kusahau mara moja tu.
900. Asipoleta sijida mbili za kusahau baada ya salamu kwa kukusudia
173
Al-Masailul Islamiyah
Page 188
atakuwa ameasi na atawajibika alete kwa haraka, na kama hataleta ni
lazima azilete wakati wowote atakapokumbuka na si lazima arudie
swala.
901. Akishuku kuwa imewajibika kwake sijida mbili za kusahau au laa,
haitamlazimu alete chochote.
902. Akitambua kuwa hakuleta moja ya sijida mbili za kusahau, itamlaz-
imu alete sijida zingine mbili za kusahau.
NAMNA YA KULETA SIJIDA YA KUSAHAU
903. Namna ya kusujudu sijida ya kusahau: Baada ya salamu anuie nia ya
sijida ya kusahau na kuweka paji la uso juu ya kinachosihi kusujudu
juu yake na kusema “Bismillah wa billah wa swala llahu alaa
Muhamadi wa aali Muhammad” au aseme “Bismillah wa billah
allahuma swali alaa muhamadi wa aali Muhamadi”. Na ni bora
aseme “Bismillah wabillah asalamu alayka ayuh nabiyu warahmatu
llah wabakatuh” Kisha anakaa kisha anasujudu tena na kusoma moja
ya dhikri hapo juu, atakaa na kuleta tashahudi na kutoa salamu moja.
KADHA YA SIJIDA AU TASHAHUDI ZILIZOSA-
HAULIKA
904. Ni sharti katika kadha ya sijida au tashahudi zilizosahaulika mambo
yote yanayoshurutishwa katika swala kama vile, tohara ya mwili na
mavazi na masharti mengineyo.
905. Akisahau sijida mara nyingi, mfano akisahau sijida katika rakaa ya
kwanza na sijida katika rakaa ya pili ni wajibu azilipe baada ya swala
174
Al-Masailul Islamiyah
Page 189
ya pamoja na kuleta sijida mbili za kusahau kwa kila moja na hailazi-
mu kuainisha, ama akisahau sijida katika rakaa ya kwanza na ya mwi-
sho au akasahau tashahudi mbili, kwa tahadhari ya wajibu alete sijida
ya mwisho aliyoisahau kwanza, kisha analeta tashahudi na salamu na
baada ya hapo atalipa sijida ya kwanza, na vivyo hivyo itamlazimu
alete tashahudi iliyosahaulika mwisho na kutoa salamu, kisha atalipa
tashahudi ya kwanza, haya yote ni katika hali ya kutoleta kinachoba-
tilisha swala kwa kukusudia au kusahau, ama akileta kinachobatilisha
swala kwa kukusudia au kusahau ni lazima arudie swala.
906. Asipotambua kuwa amesahau tashahudi au sijida atawajibika kulipa
zote mbili pamoja, na hakuna tatizo kutanguliza moja kati ya hizi
mbili.
907. Akishuku kuwa amesahau tashahudi au sijida au laa, hatawajibika
kulipa kadha.
908. Akishuku kuwa baada ya swala alileta sijida au tashahudi zilizosa-
haulika au laa, ikiwa wakati bado upo itabidi arudie kulipa, na kama
wakati wa swala umeisha hatawajibika kuzilipa.
UPUNGUFU NA ZIADA KATIKA SEHEMU ZA
SWALA NA MASHARTI YAKE
909. Akizidisha au kupunguza katika wajibati za swala kwa kukusudia
swala yake inabatilika.
910. Akitambua katikati ya swala kuwa josho lake au udhu wake ulikuwa
batili au alijishughulisha na swala bila ya udhu au josho, swala yake
inabatilika, atairudia kwa udhu au josho, na akitambua baada ya swala
ni wajibu airudie kwa udhu au josho ikiwa wakati bado upo, na kama
175
Al-Masailul Islamiyah
Page 190
wakati umekwisha ni lazima alipe kadha.
911. Akikumbuka kabla ya salamu kuwa amesahau rakaa katika mwisho
wa swala ni wajibu alete hiyo rakaa kwa haraka.
912. Akikumbuka baada ya salamu kuwa amesahau rakaa au zaidi ya
rakaa, akifanya kinachobatilisha swala kwa kusahau au kukusudia,
mfano kukipa kibla mgongo, swala yake inabatilika, na kama hajafa-
nya kinachobatilisha swala ni wajibu alete kwa haraka alichokisahau.
913. Akitambua kuwa ameswali kabla ya wakati au ameswali kwa kukipa
mgongo kibla au kuelekea kulia au kushoto mwa kibla ni wajibu aru-
die swala ndani ya wakati na kuilipa kama wakati umeisha
SWALA YA MSAFIRI
914. Ni wajibu kwa msafiri kupunguza katika swala za rakaa nne yaani
“Adhuhuri, Alasiri na Isha” na ataswali rakaa mbili badala ya rakaa
nne na hiyo ni pindi yakipatikana masharti nane yafuatayo:-
1. Masafa ya safari yawe ni farsakha nane ( kilometa 45)
2. Akusudie tangu mwanzo wa safari kukata farsakha nane
3. Asibadili nia yake
4. Asipitie katika mji wake, na asikusudie kukaa siku kumi
5. Asisafiri kwa ajili ya mambo ya haramu.
6. Asiwe ni katika watu wanaohamahama ambao hawatulii sehemu
moja.
7. Safari isiwe ndio kazi yake
8. Afike kwenye sehemu anayoruhusiwa kisheria kupunguza.
SHARTI LA KWANZA
176
Al-Masailul Islamiyah
Page 191
915. Inatakiwa masafa anayosafiri yasipungue farsakha nane za kisheria na
farsakha moja ni sawa na kilometa tano na nusu takribani.
916. Mwenye kufikisha jumla ya masafa yake kwenda na kurudi farsakha
nane, akisafiri na kurudi siku hiyo hiyo, mfano akisafiri mchana aka-
rudi usiku wake, kama hayajapungua masafa ya kwenda farsakha nne
ni wajibu apunguze swala zake, lakini ikiwa kwenda ni farsakha tatu
na kurudi ni farsakha tano, dhahiri atapunguza swala zake, ingawa ni
kwa tahadhari ya sunna ni kukusanya baina ya kupunguza na kuka-
milisha.
917. Ikiwa safari yake kwenda na kurudi ni farsakha nane, na kama safari
yake haichukui siku kumi, kama akisafiri leo na akarudi kesho au
baada ya kesho au chini ya siku kumi ni wajibu apunguze swala zake
na asifunge bali atalipa kadha kama yuko katika mwezi wa
Ramadhani.
918. Ikiwa masafa hayajafika farsakha nane au msafiri hakujua kuwa safa-
ri yake inafika farsakha nane au haifiki hatapunguza swala zake. Ama
akishuku safari yake imefikia farsakha nane au haikufika, ni wajibu
wake afanye uchunguzi ili apate uhakika, na akipata habari kutoka
kwa waadilifu wawili au mmoja au inajulikana baina ya watu kiasi
cha kupata matumaini kuwa safari yake imefikisha farsakha nane
basi atapunguza swala zake.
919. Mwenye kupata uhakika kuwa safari yake imefika farsakha nane
kisha akapunguza swala zake, baada ya hapo akatambua kuwa safari
yake haikufikia farsakha nane, itamuwajibikia arudie swala za rakaa
nne ndani ya wakati au kadha kama wakati umepita.
920. Ikiwa safari ina njia mbili moja inafikisha farsakha nane na nyingine
haifikishi farsakha nane, akisafiri kwa ile njia inayofikisha farsakha
nane atapunguza swala, na kama atatumia njia ambayo haifikishi far-
sakha nane atakamilisha swala zake.
177
Al-Masailul Islamiyah
Page 192
921. Ikiwa mji anaoishi una ukuta mwishoni mwa mji ni lazima aanze
kuhesabu masafa ya kisheria hapo, yaani farsakha nane kuanzia kwe-
nye ukuta wa mji, na kama hauna ukuta ni wajibu aanze kuhesabu
masafa ya kisheria mwisho wa nyumba za mji.
SHARTI LA PILI
922. Ni sharti akusudie kukata masafara ya farsakha nane kuanzia mwan-
zo wa safari, na kama atasafiri masafa ambayo hayafiki farsakha nane
kisha baada ya kufika hapo akakusudia kwenda sehemu nyingine
kiasi kwamba akijumlisha masafa mawili yatafikisha farsakha nane,
kwa kuwa hakukusudia tangu mwanzo wa safari kukata masafa haya
ni wajibu akamilishe swala yake.
923. Asiyejua kuwa safari yake itafikisha masafa kiasi gani, mfano akisa-
firi kwa ajili ya kutafuta kitu kilichopotea na hajui atasafiri masafa
kiasi gani mpaka akipate, ni wajibu akamilishe swala zake, na kama
wakati wa kurudi atasafiri farsakha nane au zaidi ni wajibu apunguze
swala zake.
924. Msafiri hapunguzi swala zake mpaka aazimie mwanzo wa safari
kukata masafa ya farsakha nane. Mwenye kukusudia kukata masafa
ya farsakha nane kama atapata rafiki, kama atakuwa na matumaini ya
kumpata rafiki ni wajibu apunguze swala zake, na kama hana matu-
maini ya kumpata rafiki atakamilisha swala.
925. Mwenye kukusudia kukata masafa ya farsakha nane ni wajibu aanze
kupunguza anapofikia kwenye sehemu asiyoona ukuta au kusikia
sauti ya adhana, na kama atasafiri kidogo sana kiasi kwamba haisadi-
ki kuwa ni msafiri ni wajibu wake akamilishe swala na kwa tahadha-
ri ya sunna apunguze swala
178
Al-Masailul Islamiyah
Page 193
926. Ikiwa katika safari yake anamfuata mtu mfano mtumishi akisafiri
kwa kumfuata bwana wake, kama atatambua kuwa safari itafikisha
farsakha za kisheria atapunguza swala, na kama hatambui kwa tahad-
hari amuulize bwana wake.
SHARTI LA TATU
927.Ni sharti msafiri asibadilishe azima yake ya kukata masafa ya kisheria
njiani, akibadilisha lengo lake kabla ya kutimiza farsakha nne au aki-
sitasita baina ya kuendelea na safari au kurudi atawajibika kukamili-
sha swala.
928. Akibadili nia yake baada ya kumaliza farsakha nne ikiwa aliazimia
kukaa huko au kurudi baada ya siku kumi au akawa hana mwelekeo
baina ya kurudi au kubakia ni wajibu akamilishe swala.
929. Akibadili nia yake baada ya kumaliza farsakha nne na akawa ameazi-
mia kurudi siku ile ile ni wajibu kwake kupunguza hata kama akiru-
di kabla ya siku kumi.
930. Mtu akitoka kwenda sehemu maalum na akawa amekata sehemu fula-
ni ya masafa, baada ya hapo akakusudia kwenda sehemu nyingine,
kama jumla ya masafa ya sehemu anayoaanzia hivi sasa kwenda
sehemu ya pili aliyoikusudia mwishoni ni farsakha nane atapunguza
swala zake.
SHARTI LA NNE
931. Ni sharti msafiri asipitie kwenye mji wake kabla ya kufika farsakha
nane na asikae sehemu siku kumi au zaidi, kama atataka kupitia kwe-
nye mji wake kabla ya kukamilisha masafa ya kisheria au akitaka
kukaa sehemu siku kumi atakamilisha swala zake.
179
Al-Masailul Islamiyah
Page 194
932. Asiye jua kuwa atapitia kwenye mji wake, au laa au atakaa zaidi ya
siku kumi au laa, ni wajibu akamilishe swala zake.
SHARTI LA TANO
933. Ni sharti asisafiri kwa ajili ya maasi au kitu cha haramu, kama atasa-
firi kwa ajili ya haramu kama vile kuiba, ni wajibu akamilishe swala
yake na vile vile atakamilisha swala kama safari yenyewe ni ya hara-
mu mfano kama inamdhuru au safari ya mke bila idhini ya mumewe,
au safari ya mtoto aliyekatazwa na wazazi wake pamoja na kupatika-
na maudhi kwa kuwakhalifu kwao ikiwa safari ya hawa sio ya waji-
bu. Lakini safari ya hija ya wajibu ni wajibu wapunguze katika swala
zao.
934. Ambaye safari yake sio ya haramu au hakusafiri kwa jambo la hara-
mu anapunguza swala zake hata akifanya maasi katika safari hiyo,
mfano kusengenya au kunywa pombe.
935. Akisafiri kwa ajili ya kuacha wajibu ni wajibu akamilishe swala
zake, aliyekuwa na deni na akawa na uwezo wa kulipa deni hilo
kisha akasafiri ili asilipe deni ni wajibu akamilishe swala, lakini
kama hakusafiri kwa ajili ya kuacha wajibu ni wajibu apunguze
katika swala zake, hata kama itaafikiana na kuacha wajibu kwa
sababu hiyo au italazimu hivyo.
936. Ikiwa safari yake si ya haramu lakini chombo alichosafiria ni cha
unyang’anyi au ardhi aliyotembelea juu yake ilikuwa ya
unyang’anyi atapunguza swala, na kwa tahadhari ya sunna akusanye
baina ya kupunguza na kukamilisha.
937. Mwenye kusafiri pamoja na dhalimu na ikiwa si lazima asafiri nae,
au amesafiri kwa ajili ya kumsaidia dhalimu ni wajibu akamilishe
180
Al-Masailul Islamiyah
Page 195
swala. Ama kama kuna ulazima wa kusafiri nae au safari yake na
dhalimu ni kwa ajili ya kuwasaidia watakao dhulumiwa atapunguza
swala.
938. Ambaye amesafiri si kwa ajili ya maasi akikusudia katikati ya safa-
ri kumalizia masafa yaliyobakia kwa ajili ya maasi ni wajibu akami-
lishe swala zake, lakini swala zake alizoziswali kwa kupunguza
kabla ya hapo zitasihi.
SHARTI LA SITA
939. Ni shartia asiwe katika watu wa kuhamahama ambao wanahamahama
na wasio kuwa na makazi maalumu wanatembea na nyumba zao
wanapoona maji au majani wanapiga kambi hapo na yanapokwisha
huhama na kwenda sehemu nyingine hawa ni wajibu kukamilisha
swala zao.
940. Akisafiri mmoja wa watu hawa kwa ajili ya kutafauta malisho ya
wanyama wao hata kama safari yake ikifikia masafa ya kisheria ni
wajibu wake akamilishe swala hata kama hana mifugo yake.
941. Akisafiri miongoni mwa watu wanao hama hama kwa ajili ya hija,
ziara au biashara na mengineyo atapunguza swala zake.
SHARTI LA SABA
942. Ni sharti safari isiwe ni kazi yake na kama shughuli yake ni utingo,
dereva au baharia na wengineo atakamilisha swala kama safari yake
si ya kwanza, lakini katika safari ya kwanza atapunguza swala zake
hata kama safari yake itakuwa ndefu kiasi gani.
943. Ambaye safari ni kazi yake katika baadhi ya misimu ya mwaka,
kama vile dereva ambaye huendesha gari lake kiangazi au masika ni
181
Al-Masailul Islamiyah
Page 196
wajibu akamilishe swala katika safari.
944. Ambaye shughuli yake ni safari akibaki kwenye mji wake siku kumi
au zaidi ni wajibu apunguze swala zake katika safari yake ya kwan-
za ambaye atasafiri baada ya kukaa siku kumi.
945. Mtalii katika miji ambayo hajaifanya kuwa ni makazi yake ni wajibu
akamilishe swala.
946. Ambaye safari si kazi yake na akawa anasafiri mara nyingi katika
miji au vijiji kwa ajili ya kuchukua bidhaa ni wajibu apunguze swala
zake.
SHARTI LA NANE
947. Ni sharti msafiri afike katika sehemu inayoruhusiwa kupunguza,
yaani awe mbali na mji kiasi kwamba haoni ukuta wa mji au hasikii
adhana.
948. Akisafiri na akifika sehemu anasikia adhana, lakini haoni ukuta wa
mji au anaona ukuta, lakini hasikii adhana akitaka kuswali atakami-
lisha swala.
949. Msafiri anayerudi kwenye mji wake ni wajibu akamilishe swala zake
pindi aonapo ukuta wa mji wake au asikiapo adhana, na msafiri
anayetaka kukaa sehemu siku kumi akiona kuta za sehemu hiyo au
akisikia adhana yake nilazima akamilishe swala.
950. Msafiri anayerudi kwenye mji wake ni wajibu akamilishe swala zake
anapoona ukuta wa mji wake au kusikia adhana, na pia msafiri
ambaye anataka kukaa kwenye sehemu siku kumi ataanza kukamili-
sha swala anapoona ukuta au kusikia adhana ya mahali anapoenda.
182
Al-Masailul Islamiyah
Page 197
951. Akisafiri katika sehemu isiyokuwa na nyumba wala ukuta akifika
kwenye sehemu ambayo kwa kawaida kama kungelikuwa na nyumba
au ukuta zisingeonekana nilazima apunguze swala yake.
952. Ikiwa macho, masikio na sauti ya adhana si ya kawaida ni lazima
apunguze swala katika sehemu ambayo macho ya kawaida hayaoni,
au masikio ya kawaida hayasikii au sauti ya adhana ya kawaida haisi-
kiki.
953. Mwenye kwenda kwenye mji wake ni lazima akamilishe swala aona-
po ukuta wa mji au kusikia adhana.
HUKUMU ZA MAKAZI NA KUKAA
SIKU KUMI
954. Mwenye kuchagua mji kwa ajili ya kuishi utahesabiwa kuwa ni mji
wake hata kama hajazaliwa sehemu hiyo.
955. Akikusudia kuishi kwenye mji kwa muda maalum usiokuwa mji wake
kisha akahama hapo, haitahesabiwa kuwa ni mji wake ila anapotaka
kubaki muda mrefu kama mwaka au zaidi, kwa wanafunzi na wana-
chuo wanaosafiri kwa ajili ya kusoma huo mji unakuwa ni mji wao,
kwa hiyo wanalazimika kukamilisha swala na kufunga, na vivyo
hivyo hukumu ya Askari ambao wanapangiwa kukaa sehemu muda
mrefu.
956. Mahali ambapo amekusudia kuishi miaka minne au mitano itahesa-
bika kuwa ni mji wake, ikitokea safari kisha akarudi kwenye huo mji
atawajibika kukamilisha swala.
183
Al-Masailul Islamiyah
Page 198
957. Mwenye sehemu mbili mfano akikaa sehemu moja miezi sita na sehe-
mu nyingine miezi sita, sehemu zote mbili zitahesabika kuwa ni miji
yake, na vile vile hukumu hii itakuwa kwa mwenye kuchagua miji
mingi kuwa makazi yake.
958. Akifika sehemu ambayo ilikuwa ni mji wake wakati uliopita lakini
alihama, hakamilishi swala hata kama bado hajapata mji mwingine.
959. Msafiri ambaye hajakusudia kuishi siku kumi lakini amenuia endapo
atapata rafiki sehemu nzuri atakaa siku kumi atapunguza swala zake.
960. Msafiri akikusudia kubaki sehemu siku kumi akibadilisha kusudio
lake la kubaki siku kumi kabla ya kuswali swala ya rakaa nne au
akawa hana mwelekeo kati ya kubaki au kuondoka ni wajibu apungu-
ze swala zake, na kama ataondoka hiyo sehemu au alikosa mwelekeo
baada ya kuswali swala ya rakaa nne, ni lazima akamilishe swala
maadamu yuko huko.
961. Msafiri akijishughulisha na swala kwa nia ya kukupunguza na kati-
kati ya swala akaazimia kukaa siku kumi ni lazima akamilishe swala.
962. Msafiri aliyekusudia kukaa sehemu siku kumi akikaa zaidi ya siku
kumi ni lazima akamilishe swala zake na haimlazimu kunuia upya
kukaa siku kumi zingine.
963. Msafiri aliyekusudia kukaa sehemu siku kumi ni wajibu wake kufun-
ga saumu za wajibu na za sunna na kuswali swala ya ijumaa.
964. Msafiri ambaye amebaki sehemu siku thelathini kwa kukosa mwele-
keo kuwa ataondoka lini, ni wajibu wake akamilishe swala baada ya
siku thelathini hata kama atakaa kidogo.
184
Al-Masailul Islamiyah
Page 199
965. Msafiri ambaye hana mwelekeo kwa muda wa siku thelathini ni lazi-
ma akamilishe swala zake baada ya siku thelathini, kama siku thela-
thini amekaa sehemu moja, ama ikiwa zimeisha kwa kukaa sehemu
mbalimbali atapunguza swala zake hata baada ya siku thelathini.
MAS’ALA MENGINEYO
966. Inajuzu kwa msafiri akamilishe swala zake katika msikiti mtakatifu
wa Makka, msikiti wa Mtume, msikiti wa Kufah na kwenye kaburi la
Imamu Hussein (as) akiswali nje ya sehemu hizi au akiswali sehemu
ambayo iko na umbali kidogo kiasi cha mita ishirini na tano kwa
tahadhari ya sunna apunguze swala zake.
967. Anayetambua kuwa msafiri ni wajibu wake apunguze swala zake aki-
kamilisha kwa kujisahau swala yake inabatilika.
968. Msafiri asiyejua kuwa ni wajibu kwake kupunguza swala akikamili-
sha swala yake inasihi.
.
969. Akijisahau kuwa ni msafiri akakamilisha swala akitambua ndani ya
wakati atarudia swala yake na akitambua baada ya wakati halazimiki
kuswali kadha.
970. Ni sunna kwa msafiri baada ya kila swala aseme mara thelathini
“Subhana llah, wal hamdulillah, walaa ilaha ila llahu wa llah akbar”
imetiwa mkazo kuisema baada ya swala ya adhuhuri, alasiri na ishaa
na ni bora alete dhikri hii baada ya swala hizi mara sitini.
SWALA YA KADHA
971. Ambaye hakuswali swala ya wajibu katika wakati wake ni wajibu
185
Al-Masailul Islamiyah
Page 200
ailipe hata kama alikuwa amelala wakati wote wa swala au wakati
umepita kwa sababu alikuwa amelewa, au kazimia, lakini mwanamke
halipi kadha za swala zilizompita katika hali ya hedhi na nifasi.
972. Akitambua baada ya wakati wa swala kuwa swala aliyoiswali ilikuwa
ni batili ni wajibu aswali kadha.
973. Ambaye ana kadha za swala zilizompita ni lazima asizembee wala
kupuuzia lakini sio wajibu kuzilipa kwa haraka.
974. Swala za kila siku zikimpita ambazo huwa na utaratibu kama adhu-
huri, alasiri au magharibi na ishaa katika siku moja ni wajibu azilipe
kwa utaratibu, ama nje na hapa ni kwa tahadhari ya sunna achunge
utaratibu.
975. Akitaka kulipa swala nyingi zisizo za kila siku kama swala za matu-
kio ambazo zimempita mara nyingi na akataka kulipa kadha za swala
za kila siku, si lazima kulipa kadha kwa utaratibu.
976. Akipitwa na swala ya adhuhuri kisha siku nyingine akapitwa na swala
ya alasiri au akapitwa na zote mbili na akawa hajui ni ipi iliyotangu-
lia kumpita, inatosha alete swala mbili za rakaa nne nne kwa kunuia
kuwa swala ya kwanza ni kadha ya siku ya kwanza na ya pili ni kadha
ya siku ya pili.
977. Akitambua kuwa amepitwa na swala ya rakaa nne na hatambui kuwa
ni adhuhuri au alasiri inatosha alete swala ya rakaa nne kwa nia ya
swala iliyompita.
978 Akipitwa na swala tano na hajui ya kwanza kumpita ni ipi itabidi azin-
gatie utaratibu ufuatao: Kwanza ataswali swala tisa kwa utaratibu,
ataanza na swala ya asubuhi, adhuhuri, alasiri, magaharibi na ishaa
kisha arudie upya swala ya asubuhi, adhuhuri, alasiri na magharibi na
vile vile akipitwa na swala sita itabidi aswali swala kumi kwa utarati-
186
Al-Masailul Islamiyah
Page 201
bu huu huu na akipitwa na swala saba ataswali swala kumi na moja.
979. Mwenye kutambua kuwa amepitwa na swala ya asubuhi mara nyingi
au swala ya adhuhuri mara nyingi na hajui kuwa imepita mara ngapi
mara tatu au tano au sita, akilipa kadha kwa kiasi kidogo inatosha, na
kama anajua idadi yake lakini akasahau itabidi alete kadha ambayo
inampa uhakika, kama akiwa na uhakika kuwa swala ya asubuhi hai-
jampita zaidi ya mara kumi basi kwa tahadhari ya sunna inabidi alete
kadha ya swala ya asuhubi mara kumi.
980. Haijuzu kwa mtu mwingine kulipa kadha za swala zilizompita aliye
hai hata kama ameshindwa kuzilipa.
981. Inajuzu kuswali swala za kadha na jamaa hata kama swala ya imamu
ni adaa au kadha, hailazimu swala ya maamuma iafikiane na swala ya
imamu, hakuna tatizo kama akilipa kadha ya swala ya asubuhi na
imamu anaswali swala ya adhuhuri au alasiri.
982. Ni sunna kumhimiza mtoto na kumzoesha swala na ibada mbali
mbali, bali ni sunna pia kumhimiza kulipa swala zilizompita na inaju-
zu kwa watoto kusimisha swala ya jamaa na imamu wao awe ni
mtoto.
WAJIBU WA MTOTO MKUBWA KULIPA SWALA
ZILIZOWAPITA WAZAZI WAWILI
187
Al-Masailul Islamiyah
Page 202
983. Ni wajibu kwa mtoto mkubwa kulipa kadha ya swala na saumu zili-
zompita baba yake, bali na hata mama pia kama hazikumpita kwa
kuasi na wakawa na uwezo wa kuzilipa, bali ni wajibu kulipa kadha
za wazazi wawili baada ya kufa kwao au kuajiri mtu wa kulipa kadha
zilizowapita, na zikiwapita swala na saumu bila ya udhuru wowote
kwa tahadhari mtoto mkubwa awalipie.
984. Mtoto mkubwa akishuku kuwa wazazi wake walipitwa na swala au
saumu sio wajibu wake kulipa kadha.
985. Kama mtoto mkubwa hafahamiki basi watoto wote watagawiwa
yaliyowapita wazazi wao au achaguliwe mmoja wao.
986. Kama maiti ameusia kuwa aajiriwe mtu wa kulipa yaliyompita haita-
wajibika kwa mtoto mkubwa baada ya aliye ajiriwa kulipa kadha kwa
njia sahihi.
987. Mtoto akitaka kulipa yaliyowapita wazazi wake ni lazima alipe kuto-
kana na wadhifa wake, mfano kudhihirisha sauti katika swala ya asu-
buhi na magharibi na isha hata kama analipa kadha ya mama yake.
988. Ikiwa mtoto mkubwa hajabaleghe au alikuwa ni kichaa wakati waza-
zi wake wanakufa atalipa kadha baada ya kubaleghe, na kichaa ata-
walipia atakapopona, na akifa mtoto mkubwa kabla ya kubaleghe
hatawajibika mtoto anayefuata.
989. Akifa mtoto mkubwa kabla ya kuwalipia wazazi wake si wajibu kwa
mtoto anayefuata kulipa.
KUTOA UJIRA KWA AJILI YA SWALA
ZA KADHA
188
Al-Masailul Islamiyah
Page 203
990. Inajuzu kumwajiri mtu kwa ajili ya kulipa swala au ibada zingine na
kama atajitolea mtu bila ya ajira itasihi.
901. Ni wajibu kwa mwenye kuiajiri nafsi yake katika kulipa swala za
maiti awe ni mujitahidi au mwenye kujua hukumu za swala kwa uele-
wa na taqlidi sahihi.
902. Ni wajibu kwa muajiriwa amuainishe anayemuwalikilisha wakati wa
nia na si lazima atambue jina lake, na inatosha anuie hivi: “Ninaswali
kwa niaba ya yule nilioajiriwa kwa jili yake kwa kujikurubisha kwa
Mwenyezi Mungu”.
903. Akiajiriwa mtu kwa ajili ya kulipa kadha ya maiti ikifahamika kuwa
hajalipa kabisa au hajalipa kwa usahihi ni wajibu atoe ajira tena kwa
mwingine ikiwa ni wajibu kwake kuajiri.
904. Akishuku kuwa muajiriwa amelipa au laa, akisema muajiriwa kuwa
nimelipa na ni mkweli inatosha, na akishuku kuwa ametekeleza vili-
vyo au laa, si lazima aajiri upya mtu mwingine.
905. Haijuzu kumwajiri mtu mwenye udhuru kama vile mwenye wadhifa
wa kutayamamu au mwenye kuswali kwa kukaa n.k
906. Inajuzu mwanamke kulipa kadha za mwanaume pia inajuzu kwa
mwanaume kumlipia mwanamke na kila mmoja anafanya kulingana
na wadhifa wake.
SWALA YA JAMAA
907. Ni sunna kuswali swala za kila siku kwa jamaa na imetiliwa mkazo
kwenye swala ya asubuhi, magharibi na isha na hasa kwa aliyekaribu
na msikiti na mwenye kusikia adhana.
189
Al-Masailul Islamiyah
Page 204
908. Mtu mmoja akiswali nyuma ya Imamu malipo ya kila rakaa ni sawa
na mwenye kuswali swala mia na hamsini, na kama watu wawili
watamfuata malipo yao ni sawa na kuswali swala mia sita, na idadi
inapoongezeka na malipo pia huongezeka mpaka kufikia kumi, wana-
pozidi kumi kama mbingu itakuwa ni katarasi na bahari kuwa wino na
miti kuwa kalamu kisha waandishi wawe ni majini, watu na malaika
hawataweza kuandika thawabu za rakaa moja.
909. Haijuzu kutohudhuria swala ya jamaa na haijuzu kuacha swala ya
jamaa bila ya udhuru.
910. Ni sunna kwa mtu kungoja jamaa, na swala ya jamaa baada ya waka-
ti wa mwanzo ni bora kuliko swala ya furada katika mwanzo wa
wakati.
911. Hakuna tatizo Imamu au Maamuma akitaka kurudia swala aliyokwi-
sha iswali kwa jamaa mara nyingine.
912. Ambaye hutokewa na wasiwasi katika swala ya furada na wasiwasi
wake huisha anaposwali jamaa itamlazimu kwa tahadhari ya wajibu
aswali jamaa.
913. Haijuzu kuswali swala za sunna kwa jamaa ila swala ya kuomba
mvua au swala ya wajibu iliyokuwa sunna kwa sababu fulani, kama
vile swala ya Iddil- ftiri, Iddil – Adhuha ambazo ni wajibu kwa kud-
hihiri Imamu (as) na ni sunna kwa kutokuwepo kwake, inajuzu kuzis-
wali jamaa.
914. Asiyetambua kuwa Imamu wa jamaa anaswali swala za kila siku
ambazo ni wajibu au swala ya sunna haijuzu kumfuata.
915. Safu za swala zikifika kwenye mlango wa msikiti swala inasihi kwa
yule aliyeswali mbele ya mlango.
190
Al-Masailul Islamiyah
Page 205
916. Ambaye amesimama kwenye sehemu ambayo hapati mawasiliano na
safu ya mbele na kama hapati mawasiliano kwa imamu kwa kupitia
maamuma wengine kulia na kushoto, haijuzu kwake kujiunga na
imamu.
917. Hakuna tatizo kama sehemu ya maamuma iko juu zaidi kuliko sehe-
mu ya imamu.
918. Akitenganisha mtoto mwenye kutambua zuri na baya katika safu
moja, kama hawatambui kubatilika swala yake inajuzu kujiunga na
jamaa.
919. Akitambua kuwa swala ya imamu ni batili, kama akitambua kuwa
imamu hana udhu haijuzu kumfuata hata kama imamu hajajua hilo.
920. Akitambua maamuma baada ya swala kuwa imamu hakuwa muadili-
fu au alikuwa kafiri au swala yake ilikuwa batili kwa sababu mion-
goni mwa sababu mfano hakuwa na udhu swala inasihi.
921. Akinuia maamuma swala ya furada bila ya udhuru au pamoja na
udhuru baada ya Al – hamdu na sura haimlazimu kusoma Al hamdu
na sura lakini akinuia furada kabla ya kumaliza Al- hamdu na sura
inabidi asome kiasi ambacho imamu amesoma, na kwa tahadhari aru-
die kuzisoma kwa nia ya kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu.
922. Akishuku maamuma kuwa amenuia swala ya furada au laa ni wajibu
ajengee kuwa hajanuia nia ya furada na ataendelea na swala ya
jamaa.
YALIYOLAZIMA KWA IMAMU
WA JAMAA
191
Al-Masailul Islamiyah
Page 206
923. Lazima imamu wa jamaa awe baleghe, mwenye akili na awe ni shia
ithna asharia muadilifu, awe mtoto wa halali, awe anaswali swala kwa
usahihi, ni lazima imamu awe ni Mwanaume kama atafuatwa na
wanaume na hakuna tatizo kwa mtoto kufuatwa na watoto na pia
mwanamke kufuatwa na wanawake.
924. Mwenye kuwa na uwezo wa kuswali kwa kusimama haijuzu kumfua-
ta aliyekaa au aliyelala, ambaye anaswali kwa kukaa haijuzu kum-
fuata aliye lala, inajuzu kwa anayeswali kwa kulala amfuate aliyekaa
na aliyekaa kwa aliyesimama.
925. Inajuzu kumfuata imamu ambaye nguo yake ina najisi au wadhifa
wake ni kutayamamu au kwa udhu wa bandeji kama kuswali kwake
na nguo yenye najisi au tayamamu au udhu wa bandeji ni kwa saba-
bu ya udhuru.
926. Inajuzu kumfuata maslusi na mabtuni na pia inajuzu asiye kuwa mus-
tahadha kumfuata mustahadha.
927. Kwa tahadhari ya sunna wasifuatwe wenye ukoma na balanga na
yeyote.
HUKUMU ZA JAMAA
928. Ni wajibu kwa maamuma kumuainisha imamu katika nia, lakini hai-
lazimu kumjua imamu kwa jina inatosha kusema ninamfuata imamu
anayetuongoza.
929. Ni wajibu kwa maamuma alete vipengele vyote vya swala yeye mwe-
nyewe ila kusoma Al- hamdu na sura hiyo ni kazi ya imamu.
930. Ni wajibu kwa maamuma asisome Al- hamdu na sura katika swala za
asubuhi, magharibi na ishaa kama anasikia sauti ya imamu na hata
kama hasikii sauti ya imamu vizuri na kama hasikii kabisa lazima
192
Al-Masailul Islamiyah
Page 207
asome kwa kutodhihirisha sauti.
931. Akirukuu kabla ya imamu kwa kujisahau na akajua kuwa nikirudi
katika kisimamo sitamuwahi imamu katika kusoma, akisuburi mpaka
imamu amkute kwenye rukuu swala yake inasihi. Na pia swala yake
inasihi kama atanyanyua kichwa chake kutoka kwenye rukuu kwa
lengo la kumfuata imamu kisha akarukuu na imamu mara ya pili.
932. Haijuzu kumfuata imamu akileta kunuti kwa kusahau katika sehemu
isiyo ya kunuti au akileta tashahudi katika sehemu isiyo ya tashahudi
kama ambavyo katika hali hii haijuzu kurukuu kabla ya imamu kuru-
kuu bali atasubiri kisha atakamilisha yaliyo bakia pamoja naye ila
akikusudia furada inajuzu kumkhalifu imamu.
SUNNA ZA SWALA YA JAMAA
933. Ni sunna kwa mamuma wa kiume asimame kulia mwa imamu na
kama maamuma ni wa kike atasimama kulia mwa imamu kiasi
kwamba sehemu yake ya kusujudia itakuwa sawa na magoti ya
imamu au miguu ya imamu kama maamuma ni mwanaume na mwa-
namke au mwanaume na wanawake wengi ni sunna maamuma wa
mwanaume asimame kulia mwa imamu na wanawake wasimame
nyuma ya imamu na kama ni wanaume wengi na wanawake wengi ni
sunna wanaume kuwa nyuma ya imamu na wanawake kuwa nyuma
ya wanaume.
934. Ikiwa imamu na maamuma ni wanawake ni bora wasimame kwa
usawa asitangulie imamu kwa maamuma.
935. Ni sunna kwa imamu kusimama katikati ya safu na wasimame wenye
elimu na ucha Mungu nyuma yake katika safu ya kwanza
936. Ni sunna safu ziwe zimenyooka na bila ya kuwepo na mwanya wala
193
Al-Masailul Islamiyah
Page 208
kitenganishi chochote.
937. Ni sunna kwa waumini kusimama baada ya kauli ya imamu “Qad
Qaamati swaalat”
938. Ni sunna kwa imamu kuchunga udhaifu wa maamuma asirefushe
rukuu, kunuti na sijida ila akitambua kuwa wote wanapendezwa na
hali hiyo.
939. Ni sunna akitambua imamu kuongezeka kwa maamuma mwingine
arefushe rukuu mara mbili zaidi kisha asimame hata kama akitambua
kuongezeka mwingine.
VILIVYO MAKURUHU KATIKA
SWALA YA JAMAA
940. Ni makuruhu kwa maamuma kusimama peke yake katika safu moja
ikiwa katika safu zingine kuna sehemu zilizo wazi.
941. Ni makuruhu kwa maamuma kuleta baadhi ya dhikri kwa sauti kiasi
kwamba imamu anasikia.
942. Ni makuruhu kwa msafiri ambaye anapunguza swala zake kama
adhuhuri, alasiri na ishaa afuatwe na asiye kuwa msafiri na pia ni
makuruhu kwa asiye kuwa msafiri kumfuata msafiri.
SWALA YA IJUMAA
943. Swala ya ijumaa ni wajibu akiwepo Imamu (as) badala ya adhuhuri,
194
Al-Masailul Islamiyah
Page 209
lakini katika zama ya ghaiba ya Imamu inakuwa ni wajibu wa hiari,
yaani mtu anakuwa na hiari katika siku ya Ijumaa kuswali adhuhuri
au kuswali ijumaa lakini kwa tahadhari ya sunna akiswali ijumaa kati-
ka wakati huu wa ghaiba ya Imamu aswali na adhuhuri pia.
944. Swala ya Ijumaa ina rakaa mbili mfano wa swala ya asubuhi na
imamu adhihirishe sauti yake katika kusoma Al- hamdu na sura na
imetiliwa mkazo asome suratul- jum’a katika rakaa ya kwanza na
suratul – munaafiquun katika rakaa ya pili, na ni sunna katika swala
ya ijumaa kuleta kunuti mbili katika rakaa ya kwanza kabla ya rukuu
na katika rukuu ya rakaa ya pili baada ya rukuu. Ni wajibu asirukuu
baada ya kunuti ya rakaa ya pili na akirukuu baada ya kunuti swala
inabatilika.
945. Shaka katika idadi ya rakaa kwenye swala ya ijumaa inabatilisha
swala.
946. Ni sharti katika swala ya ijumaa yanayoshurutishwa katika swala za
kila siku kwa kuongeza yafuatayo:-
1. Iswaliwe jamaa na si furada.
2. Iwe idadi ya wenye kuswali - imamu na maamuma - wawe saba
waliobaleghe kwa uchache na kwa tahadhari ya wajibu katika hao
asiwepo msafiri anayepunguza swala ikiwa imamu na mamuma ni
watano swala inasihi.
3. Imamu ahutubie kabla ya swala khutuba mbili kwa ufafanuzi uta-
kaokuja inshaallah.
4. Ikiwa kuna sehemu mbili za swala za ijumaa ni wajibu masafa
baina ya ijumaa mbili hizo yawe ni kilometa tano na nusu
5. Kama maamuma watatawanyika katikati ya khutuba ya swala au
195
Al-Masailul Islamiyah
Page 210
kabla ya kuanza swala na idadi ikawa chini ya watu wanne swala
ya ijumaa haitasihi ni wajibu waswali adhuhuri, na wakitawanyi-
ka katikati ya swala ni wajibu kwa imamu kukamilisha ijumaa
kisha aswali adhuhuri.
947. Ni lazima vizingatiwe vitu vifuatavyo katika khutuba mbili:-
- Kumhimidi Mwenyezi Mungu – kumshukuru
- Kumtakia rehma Mtume “Muhammad (saww) na kizazi chake kituku-
fu
- Awalinganie watu katika kumcha Mwenyezi Mungu na kumuogopa
- Asome sura kamili katika khutuba ya kwanza
- Kuwatakia rehma maimamu na kuwataja kwa majina katika khutuba
ya pili
- Kuwaombea waumini maghfira
948. Ni lazima kumuhimidi Mwenyezi Mungu na kumtakia rehma Mtume
Muhammadi (saww) na kizazi chake katika khutuba kwa lugha ya
kiarabu lakini mawaidha na kuwalingania inajuzu kwa lugha ya
waliohudhuria.
949. Ni lazima kwa imamu asome khutuba mbili mwenyewe, asisome
mwingine kama ambavyo anatakiwa azisome akiwa amesimama
kisha atenganishe khutuba ya pili kwa kukaa kikao kidogo na adhi-
hirishe sauti ya khutuba kwa uchache wasikie watu wanne
waliokamilisha masharti, na inapaswa waliohudhuria wote wasikie
khutuba mbili.
950. Ni lazima kwa maamuma kwa ubora kusikiliza khutuba ya imamu, na
wasizungumze mazungumzo yanayowafanya wasimsikilize imamu
na wala wasiswali swala za sunna na wakae mkao wa swala,
wasigeuke kulia na kushoto na wala wasigeuke geuke, na hakuna tati-
zo katika mambo haya baada ya khutuba na kabla ya swala.
196
Al-Masailul Islamiyah
Page 211
951. Kama maamuma hawatasikiliza khutba mbili na wakawa wamegeuka
kulia na kushoto watakuwa wamefanya kinyume na tahadhari lakini
swala yao inasihi.
952. Si wajibu swala ya Ijumaa kwa asio baleghe, vichaa na wazee, wag-
onjwa, vipofu, wanawake, wasafiri na wanaokaa mbali na sehemu ya
kuswalia kwa farsakha mbili wala kwa yule ambaye ni vigumu
kuhudhuria katika swala wala katika wakati wa mvua, lakini mmoja
wa hawa akihudhuria swala yake inasihi.
953. Inajuzu kwa aliyechelewa khutba mbili ahudhurie ijumaa na kuswali,
na pia akimkuta imamu yuko kwenye rukuu ya rakaa ya pili itakuwa
rakaa yake ya kwanza na akitoa salamu imamu atasimama kwa ajili
ya rakaa ya pili na kukamilisha swala na ijumaa itakuwa imesihi.
SWALA YA MAJANGA
954. Ni wajibu kuswali swala ya majanga ambayo tutataja namna yake
baadaye kwa sababu ya mambo yafuatayo:-
1. Kupatwa kwa Jua, hata kama itapatwa sehemu tu na hajaogopa
yeyote
2. Kupatwa kwa Mwezi, hata kama itapatwa sehemu tu na hakuo-
gopa yeyote
3. Tetemeko, hata kama hakuogopa yeyote
4. Radi, ngurumo, kimbunga, kuvuma kwa upepo mweusi na
mwekundu n.k. ikiwa watu wengi wataogopa
955. Vikitokea vitu vingi ambavyo ni wajibu kuswali swala ya majanga ni
wajibu aswali kwa kila tukio swala ya janga mfano: Ikitokea kupatwa
kwa jua na likatokea tetemeko ni wajibu kuswali swala ya majanga
mara mbili.
197
Al-Masailul Islamiyah
Page 212
956. Mwenye kuwajibikiwa na swala nyingi za majanga, mfano likipatwa
jua mara tatu na hakuswali kwa muda wake haitamlazimu wakati wa
kadha kuainisha ni swala ipi anayoiswali bali inatosha kuswali idadi
ya swala kulingana na idadi ya majanga yaliyompita.
957. Ni wajibu kuleta swala ya majanga tangu linapoanza kupatwa jua au
mwezi na kwa tahadhari ya sunna asicheleweshe hadi weupe uanze
kutokea.
958. Akiwajibikiwa na swala ya majanga katika wakati wa swala za kila
siku, kama wakati utakuwa ni mpana atachagua yeyote ya kutan-
guliza, na kama wakati utakuwa ni mfinyu itabidi aswali swala
ambayo muda wake ni mfinyu na kama wakati wa swala mbili hizi ni
mfinyu atatanguliza swala ya kila siku.
959. Akitambua katikati ya swala ya kila siku kuwa wakati wa swala ya
majanga ni mfinyu na wakati wa swala ya kila siku ni mpana
atakatisha swala ya kila siku na kuswali swala ya majanga.
960. Ikitokea kupatwa kwa jua, mwezi, tetemeko na mwanamke yuko kati-
ka hedhi au nifasi hatawajibikiwa na swala ya majanga wala kadha
yake lakini kwa tahadhari ya sunna aswali baada ya kutoharika.
NAMNA YA KUSWALI SWALA YA
MAJANGA
961. Swala ya majanga ina rakaa mbili na kila raka kuna rukuu tano namna
yake ni hii: “Alete takbira baada ya nia atasoma Al- hamdu na sura
kamili na kurukuu kisha anasimama na kusoma Al- hamdu na sura
kamili atafanya vivyo hivyo hadi mara tano na baada ya kusimama
kutoka kwenye rukuu ya tano anaenda kwenye sijida mbili kisha
anasimama kwa ajili ya rakaa ya pili, anafanya kama alivyofanya kati-
198
Al-Masailul Islamiyah
Page 213
ka rakaa ya kwanza na kuleta tashahudi na kutoa salamu.
962. Katika swala ya majanga inajuzu baada ya nia na kusoma Al- hamdu
agawanye sura kwenye vifungu vitano atasoma aya au zaidi ya aya
kisha anarukuu kisha ananyanyuka anasoma kifungu cha pili cha sura
bila ya kusoma Al- hamdu kisha anarukuu vivyo hivyo mpaka rukuu
ya tano mfano: asome baada ya Al-hamdu (bismillah rahmani rahim”
kama anataka kusoma suratul – Ikhalas kisha anarukuuu kisha
ananyanyuka anasoma Qul huwallahu ahad – kisha anarukuu kisha
ananyanyuka anasoma Allahhu swamadu – anarukuu kisha anasoma
lam yalid walam yuulad kisha anarukuu kisha ananyanyuka anasoma
Walam yakun lahuu kufuwan ahad – anarukuu rukuu ya tano baada ya
kunyanyuka hapo anaenda kwenye sijida mbili kisha ananyanyuka
kwa ajili ya rakaa ya pili na anafanya kama alivyofanya kwenye rakaa
ya kwanza.
963. Ni sunna kuleta takbira kabla ya kurukuu na baada yake ama baada
ya rukuu ya tano na ya kumi ni sunna kusema “Samia llahu liman
hamidah”
964. Ni sunna kuleta Qunuti kabla ya rukuu ya pili, ya nne, ya sita, ya nane
na ya kumi na akileta Qunuti moja kabla ya rukuu ya kumi inatosha.
965. Kila rukuu katika rukuu za swala za majanga ni nguzo zinabatilisha
swala kwa kuongezeka kwake au kupungua kwa kukusudia au kusa-
hau.
966. Ni mustahabu kuleta swala ya majanga kwa jamaa na hapo
haitawalazimu maamuma kusoma Al- hamdu na sura .
199
Al-Masailul Islamiyah
Page 214
SWALA YA IDD MBILI “AL – FITRI
NA AL – ADHIHAA”
967. Swala ya Idd mbili ni wajibu katika zama za kuwepo Imamu “as” na
ni lazima iswaliwe jamaa na ni sunna katika zama za “ghaiba”
kuswaliwa jamaa au furada.
968. Wakati wa swala ya Idd ni mwanzo wa kuchomoza jua mpaka jua
linapopetuka.
969. Ni sunna kuswali swala ya Idd ya adhuhaa baada ya kunyanyuka jua
kama ilivyo kwenye swala ya Iddil – fitri na atoe zaka kisha aswali
Idd.
970. Swala ya Idd mbili ina rakaa mbili kwanza analeta takbira ya ihram
kisha baada ya kusoma Al-hamdu na sura analeta takbira tano
anakunuti baada ya kila takbira, analeta takbira nyingine na kurukuu
kisha analeta sijida mbili, kisha anasimama kwa ajili ya rakaa ya pili
baada ya Al hamdu na sura analeta takbira nne na anakunuti baada ya
kila takbira kisha analeta takbira ya tano na kurukuu kisha analeta
sijida mbili baada ya rukuu na analeta tashahudi na kutoa salamu.
971. Na inatosha kuleta dua yeyote katika kunuti za idd mbili lakini ni bora
alete moja ya hizi dua mbili “Allahuma Ahlul kibriai wal
adhama.waahalul juudi wal jabarut waahalul ‘af’wi wa rahma
waahlu taqwaa walmaghifra as’aluka bihaqi hadhal yaumi alladhii
ja’al tahu lili muslimiina I’ydan, wali Muhammadin swala llahu alay-
hi waalihi dhukhran wa sharafan wakaramatan wa mazidaan, an
tuswaliya alaa muhammadin waali Muhammad, wa an tud khilanii fii
kuli khayrin adkhalta fiihi Muhammad waala muhammad wa
antukhirjanii min kuli suui akhrajta minhu muhammadan waala
200
Al-Masailul Islamiyah
Page 215
Muhammadi swalawatuka alayhi wa alayhimu allahumma inii
as’aluka khayran maasaalaka minihu Ibaaduka swaalihuuna wa
waa’udhubika mimaa istadha minhu ibaadukal mukhliswuna”
972. Ni sunna kuleta khutba mbili katika ghaiba ya Imamu baada ya swala
na ni bora kutaja hukumu za fitri katika Iddil- fitri na hukumu za
kuchinja katika iddil adhiha
973. Hakuna katika idd mbili hizi sura maalumu ya kusoma lakini ni bora
asome katika rakaa ya kwanza suratu Shamsi (nayo ni sura ya 91)
na katika rakaa ya pili suratul ghashiya (nayo ni sura ya 88) au
asome katika rakaa ya kwanza suratul A’alaa (nayo ni sura ya 87)
na katika rakaa ya pili suratul Shamsi.
974. Ni sunna kuswali swala ya Idd mbili uwanjani lakini Makka ni
sunna kuswaliwa ndani ya msikiti mtukufu .
975. Ni sunna baada ya swala ya magharibi na isha, katika usiku wa idd il-
fitri na baada ya swala ya asubuhi na vile vile hata baada ya swala ya
Idd alete hizi takbira.
“Allahu akbaru Allahu akbaru laa ilaaha ila llaha wa llahu akbaru
walilahil hamdu,al-hamdu lilahi alaa maahadaanaa walahu shukri alaa
maa aulaanaa”
976. Na takbira ya Iddul – adhuhaa atesema baada ya kauli ya “alaa ma
hadaanaa” atasema “Allahu akbaru alaa maa razaqanaa min bahi-
imatil ana’am wal hamdulillah alaa maa ablaanaa” akiwa katika idd
ya kuchinja ni mustahabu alete takbira baada ya sala kumi na tano ya
kwanza ni swala ya adhuhuri katika siku ya Idd na ya mwisho ni
swala ya asubuhi ya siku ya kumi na tatu katika mwezi wa dhul –
hijja.
977. Akihudhuria maamuma na imamu yuko kwenye rukuu inajuzu kunuia
201
Al-Masailul Islamiyah
Page 216
kisha ataleta takbiratul -ihram na anaenda kwenye rukuu na inah-
esabika kuwa ni rakaa.
978. Akisahahu tashahudi au moja ya sijida mbilli katika swala ya Idd kwa
tahadhari ya sunna alete kadha ya alichokisahau baada ya swala, na
akifanya kinacholazimu sijida ya kusahau ni lazima alete sijida ya
kusahau na akishuku katika Idadi ya rukuu na kunuti na akawa ame-
jishughulisha na kinachofuatia basi asizingatie shaka yake.
HUKUMU ZA SAUMU
979. Saumu ni kujizuia na vitu vyote ambavyo vinafuturisha ( ambavyo
vinamtoa mtu katika funga) kuanzia Adhana ya Alfajiri hadi Adhana
ya magharibi kwa kutekeleza amri ya Mwenyezi Mungu, tutataja
vinavyotengua saumu baadae
NIA
980. Si wajibu mfungaji kutamka kwa ulimi au kwa moyo mfano mtu
kusema “ nafunga kesho” bali inatosha kujizuia na vinavyobatilisha
saumu kuanzia adhana ya Alfajiri mpaka adhana ya magharibi kwa
kutekeleza amri ya Mwenyezi Mungu lakini ili awe na yakini kwam-
ba amefunga kwa muda wote inamlazimu kujizuia na vinavyobatil-
isha saumu kabla adhana ya Alfajiri kwa muda mchache na kufuturu
baada ya adhana ya magharibi kwa muda mchache vile vile.
981. Inajuzu mfungaji kunuia kwa kila siku katika siku za mwezi wa
Ramadhani kwa saumu ya siku inayofuata na ni bora kunuia katika
usiku wa kwanza wa mwezi wa Ramadhani kwa nia ya kufunga
mwezi mzima.
982. Muda wa nia ya funga ya mwezi wa Ramadhani ni mwanzo wa usiku
mpaka adhana ya asubuhi.
202
Al-Masailul Islamiyah
Page 217
983. Muda wa nia ya saumu ya sunna ni mwanzo wa usiku mpaka kuza-
ma jua kwa kadri ya nia, ikiwa hajajishughulisha na kitu cha kuten-
gua saumu mpaka wakati wote huo na akanuia saumu ya sunna basi
saumu inasihi.
984. Mwenye kulala kabla ya adhana ya asubuhi bila ya kunuia saumu
akiamka kabla ya adhana na akanuia funga inasihi funga yake, iwe
funga yake ni ya wajibu au ya sunna na lau akiamka baada ya
adhuhuri haitatosha kunuia funga ya wajibu.
985. Akitaka kuleta saumu ambayo siyo ya mwezi wa Ramadhani ni
wajibu kwake kuiainisha saumu mfano anuie “ nafunga kadha au
nadhiri” lakini katika mwezi wa Ramadhani sio lazima anuie
“nafunga mwezi wa Ramadhani” bali akifunga kwa kutojua au
kusahau kwamba yuko katika mwezi wa Ramadhani na akanuia
vinginevyo anahesabiwa kuwa kafunga mwezi wa Ramadhani. Ikiwa
anajua ni mwezi wa Ramadhani na akanuia saumu isiyokuwa ya
mwezi wa Ramadhani kwa makusudi hata hesabiwa si katika mwezi
wa Ramadhani wala saumu nyingine ambayo amenuia.
986. Akifunga mfano kwa nia ya mwanzo wa mwezi wa Ramadhani,
kisha akatambua baadae kwamba ilikuwa siku ya pili au ya tatu ya
mwezi wa Ramadhani inasihi funga yake.
987. Akinuia kufunga kabla adhana ya Asubuhi kisha akazimia na kuzin-
duka katikati ya mchana, kwa tahadhari ya wajibu atimize saumu
ya siku hiyo na kuilipa kadha siku nyingine.
988. Akinuia kufunga kabla ya adhana ya asubuhi kisha akalala na asi-
amke ila baada ya magharibi, itasihi saumu yake.
989. Hakuna mushikeli mwenye kujiajiri kulipa kadha ya saumu ya maiti
kufunga saumu yake ya sunna, lakini kwa yule ambaye alikuwa na
203
Al-Masailul Islamiyah
Page 218
kadha ya saumu iliyopita haijuzu kwake kuleta saumu ya sunna na
lau akifunga saumu ya sunna kwa kusahau akikumbuka kabla ya
adhuhuri inabatilika saumu yake ya sunna na inajuzu kubadili nia
yake ya sunna kwa nia ya saumu ya kadha ambayo ni wajibu wake
na lau akikumbuka baada ya adhuhuri itakuwa imebatilika saumu
yake ya sunna na lau akikumbuka baada ya magharibi itakuwa ime-
sihi saumu yake ya sunna
990. Kafiri akisilimu katika mwezi wa Ramadhani kabla ya Adhuhuri,
haitosihi saumu yake hata kama hajala kitu chochote kwa muda wote
huo na hata kama atakuwa amenuia kabla ya Adhuhuri.
991. Akifunga siku ya shaka kwamba ni mwisho wa Shaban au mwanzo
wa mwezi.wa Ramadhani kwa nia ya saumu ya kadha au saumu ya
sunna au vinginevyo kisha akajua wakati huo ni siku ya mwezi wa
Ramdahani inamuwajibikia abadili nia yake ya mwanzo aliyokuwa
nayo kwenda kwenye nia ya mwezi wa Ramadhani
VINAVYOTENGUA SAUMU
992. Vitenguzi vya saumu ni kumi:-
1. Kula
2. Kunywa
3. Jimai
4. Punyeto
5. Kumzulia Mwenyezi Mungu uongo au Mtume Muhammad (
saww) au Maimamu ( as) au Fatma Zahara (as)
6. Kufika vumbi zito kwenye koo
7. Kuzamisha kichwa chote kwenye maji
8. Kubaki na janaba au hedhi au nifasi mpaka adhana ya asubuhi
9. Kupiga bomba
10. Kujitapisha makusudi
204
Al-Masailul Islamiyah
Page 219
1 na 2 Kula na kunywa
993. Akila mfungaji au akinywa kitu kwa makusudi basi saumu yake
inabatilika ni sawa kile kilicholiwa au kilichonywewa ni kili-
chozoeleka kama vile mkate, maji na mfano wake au visivyozoeleka
kama vile kula udongo na kunywa maji maji ya miti ni sawa kili-
choliwa au kilichonywewa ni kidogo sana au ni kingi inabatilika
saumu hata kwa kurudisha maji maji ya mswaki mdomoni baada ya
kuutoa kwake na kumeza maji maji yake kwa haraka isipokuwa yaki-
malizika maji maji ya mswaki katika maji ya mdomoni kiasi kwam-
ba haihesabiki kuwa amemeza maji maji ya kutoka nje.
994. Mfungaji akijua kuingia kwa Alfajiri na akawa anakula ni wajibu
ateme kile alichokitia mdomoni kwa haraka na lau akikimeza kwa
kusudi itabatilika saumu yake na inamuwajibikia kulipa kadha na
kutoa kafara. Akila mfungaji au akinywa kitu kwa kusahau, haito-
batilika saumu yake.
995. Ni vizuri zaidi mfungaji kujiepusha kutumia bomba kwa ajili ya tiba,
sindano zenye kuongeza lishe mwilini au kuongeza nguvu, hakuna
tatizo kutumia sindano zingine kwani hazibatilishi saumu kama sin-
dano za ganzi na sindano za dawa.
996. Mfungaji akimeza mabaki ya chakula yaliyobaki kwenye meno yake
kwa makusudi inabatilika saumu yake.
997. Mwenye kutaka kufunga si wajibu kwake kuondosha mabaki ya
chakula yaliyobaki kwenye meno yake kabla ya adhana ya Alfajiri
lakini akijua au akapata yakini kwamba mabaki yataingia kwenye koo
lake wakati wa mchana ikiwa hakutoa mabaki hayo kwenye meno
yake na kikaingia kitu katika mabaki ya chakula kwenye koo lake
inabatilika saumu yake kwa tahadhari.
205
Page 220
998. Kumeza mate hakubatilishi saumu hata yakijikusanya mdomoni
kutokana na kuhisi athari ya uchachu na vinavyofanana na hivyo.
999. Mfungaji akipatwa na kiu kali kiasi kwamba anapatwa na matatizo au
akiogopa kupata madhara kwa sababu ya kiu, inajuzu kwake kunywa
maji kiasi cha kumwondoshea madhara lakini inabatilika saumu yake
na ni wajibu kujiepusha na vitu vingine vinavyobatilisha saumu
mchana wote ikiwa ni katika mwezi wa Ramadhani.
1000. Kumtafunia mtoto chakula au ndege na kuonja na mfano wake
ambapo kwa kawaida hakifiki mpaka kwenye koo haibatilishi
saumu hata kama ikifika kwenye koo ghafla lakini ikiwa alikuwa
anajua mwanzo kwamba chakula kitafika mpaka kwenye koo ita-
batilika saumu yake na inamlazimu ailipe na ni wajibu atoe kafara
pia.
JIMAI
1001. Jimai inabatilisha saumu hata kama hakuingiza ila kiasi cha kichwa
cha dhakari na ikawa manii hayajatoka . Akiingiza kiasi kidogo cha
kichwa cha dhakari na ikawa hayajatoka manii haibatiliki saumu
yake.
1002. Akitia shaka je ameingiza kiasi cha kichwa cha dhakari au laa inasi-
hi saumu yake.
1003. Akifanya jimai kwa kusahau kwamba amefunga au kulazimishwa (
kwa nguvu bila ya hiyari yake) saumu yake haibatiliki, lakini
akikumbuka aliye sahau au akaacha kulazimishwa ni wajibu
kuacha jimai na kama hataacha basi inabatilika saumu yake.
206
Al-Masailul Islamiyah
Page 221
PUNYETO “ KUCHEZEA UTUPU”
1004. Mfungaji akifanya punyeto kwa kutumia njia ya kuchezea utupu
wake kujitoa manii na akajitoa manii saumu yake inabatilika.
1005. Yakimtoka mtu manii bila ya hiyari yake haibatiliki saumu yake,
lakini akifanya yale ambayo yanamfanya kutoka manii bila ya hiyari
inabatilika saumu yake.
1006. Akijua mfungaji kwamba akilala mchana ataota, haitomlazimu
kuacha kulala na akilala na akaota haitabatilika saumu yake.
1007. Akiamka mfungaji katika hali ya kutoka manii haimlazimu
kujizuia kutoka manii.
1008. Mfungaji aliyejiotea akijua kubakia manii katika njia ya mkojo na
kwamba asipokojoa kabla ya kuoga yatamtoka manii baada ya
kuoga, inalazimu kwa tahadhari ya sunna akojoe kabla ya kuoga
1009. Mfungaji akimchezea mtu kwa kusudi la kutoa manii inabatilika
saumu yake kwa tahadhari hata kama hayatamtoka manii.
1010. Mfungaji akimchezea mtu sio kwa kusudio la kutoka manii, ikiwa
anamatumaini kwamba manii hayatamtoka inasihi saumu yake,
hata kama yatatoka bila kutarajia, lakini ikiwa hakuwa na matu-
maini ya kutotoka manii saumu yake itabatilika kama yatamtoka
207
Al-Masailul Islamiyah
Page 222
KUMZULIA MWENYEZI MUNGU UONGO,
MTUME (SAWW) NA MAIMAMU (AS).
1011. Akinasibisha mfungaji kwa makusudi uongo kwa Mwenyezi
Mungu au Manabii au Maimamu watukufu (as) kwa kutamka au
kuandika au kuashiria na mfano wake inabatilika saumu yake hata
kama atatubu haraka au akisema nimesema uongo, na kwa tahad-
hari ya wajibu kama atamsingizia Fatma Zahara ( as) vilevile
inabatilisha saumu.
1012. Akinukuu kitu kutoka kwa Mwenyezi Mungu au Nabii au Imamu
maasum (as) kwa itikadi kwamba alichokinukuu ni sahihi kisha
baadae akabaini kuwa sio sahihi, saumu yake haibatiliki.
1013. Ikiwa anajua kwamba kunasibisha uongo kwa Mwenyezi Mungu
au Mtume wake ( saww) inabatilisha saumu na akakusudia kunasi-
bisha kwa yale anayojua uongo wake, kisha akajua baadae kwamba
yale aliyoyasema yalikuwa ya kweli, atalipa kadha ya siku hiyo kwa
tahadhari ya wajibu.
1014. Akiulizwa mfungaji je, amesema Mtume ( saww) maudhui haya au
hapana? Na ilikuwa inampasa aseme hapana lakini yeye akajibu
kwa kusudi ndio badala ya hapana basi inabatilika saumu yake
1015. Akitoa habari kuhusu Mwenyezi Mungu au Mtume wake ( saww)
za kweli, kisha akasema nimesema uongo au akanasibisha juu yao
uongo usiku kisha akatilia mkazo katika mchana wa funga inabati-
lika saumu yake.
208
Al-Masailul Islamiyah
Page 223
KUFIKA VUMBI ZITO KWENYE KOO
1016. Kufika vumbi zito kwenye koo kunabatilisha saumu, ni sawa likiwa
ni vumbi la kilicho halali kuliwa, kama vile vumbi la unga wa
ngano, au vumbi la kilichoharamu kuliwa, kama vile vumbi la udon-
go, na kwa tahadhari lisifike kabisa vumbi lisilokuwa zito kooni pia.
1017. Vumbi zito likitimka kwa sababu ya upepo na akawa hajazuia mfun-
gaji vumbi kufika kooni kwa kutokuwa mwangalifu bila ya kughafi-
lika na vumbi likafika kooni inabatilika saumu yake.
1018. Kwa tahadhari ya wajibu usimfikie mfungaji moshi mzito wa sigara
na tumbaku na mfano wake kwenye koo pia, hakuna mushikeli kati-
ka moshi mdogo wa kawaida uliopo katika bafu.
1019. Ikiwa mfungaji hakujihifadhi likaingia vumbi zito au moshi mzito
na mfano wake vikaingia kwenye koo ikiwa alikuwa na matumaini
au yakini ya kutofika mpaka kwenye koo inasihi saumu yake, na
ikiwa aliacha kujihifadhi kwa dhana ya kutoingia mpaka kwenye
koo basi inamlazimu kwa tahadhari kuleta kadha ya saumu hiyo.
1020. Akisahau kwamba amefunga na akaacha kujihifadhi kutofika vumbi
mpaka kwenye koo lake au kuingia vumbi na mfano wake vikain-
gia mpaka kwenye koo lake bila ya hiyari yake, haibatiliki saumu
yake.
209
Al-Masailul Islamiyah
Page 224
KUZAMISHA KICHWA KWENYE MAJI
1021. Mfungaji akizamisha kichwa chake kwenye maji (Yaani akaingiza
kichwa chake chote kwenye maji ) kwa kusudi inabatilika saumu
yake na hakuna kafara juu yake, hata kama mwili wake umebaki nje
ya maji, lakini haitabatilika saumu yake lau akizamisha mwili wake
wote kwenye maji na kikabaki kichwa chake nje ya maji.
1022. Akiingiza nusu ya kichwa chake kwenye maji mara moja na akain-
giza nusu nyingine kwa mara nyingine haibatiliki saumu yake.
1023. Akishuku kwamba je ameingiza na amezamisha kichwa chake
chote katika maji au laa inasihi saumu yake.
1024. Akizamisha kichwa chake katika maji lakini zikabakia nywele za
kichwa chake nje ya maji inabatilika saumu yake.
1025. Kwa tahadhari ya wajibu asizamishe kichwa chake kwenye maji
mudhafu.
1026. Akianguka mfungaji kwenye maji bila ya hiyari yake na akaingiza
kichwa chake chote kwenye maji au akazamisha kichwa chake chote
kwenye maji kwa kusahau kwamba amefunga haibatiliki saumu
yake.
1027. Mfungaji akijiingiza mwenyewe kwenye maji na alikuwa na uhaki-
ka kwamba maji hayatofunika kichwa chake, yakifunika kichwa
chake haitobatilika saumu yake, ama ikiwa hakuwa na uhakika na
akajiingiza kwenye maji, na maji yakafunika kichwa chake inam-
lazimu alete kadha ya saumu hiyo kwa tahadhari ya wajibu.
1028. Akizamisha kichwa chake chote kwenye maji kwa nia ya kuoga na
akawa amesahau kwamba amefunga inasihi kuoga kwake na funga
210
Al-Masailul Islamiyah
Page 225
yake.
1029 Akikusudia kuzamisha kichwa chake chote katika maji kwa ajili ya
kuoga na anajua kwamba amefunga, ikiwa saumu yake ni saumu ya
mwezi wa Ramadhani au ya wajibu maalumu inabatilika kuoga
kwake na saumu yake, na ikiwa saumu yake ni ya sunna au ya waji-
bu usio kuwa maalumu kwa wakati, mfano saumu ya kafara inasihi
kuoga kwake na inabatilika funga yake.
1030. Akizamisha kichwa chake chote katika maji kwa ajili ya kuokoa
(mtu) aliye zama kwenye maji inamlazimu kuleta kadha ingawa
kumuokoa yule mtu ni wajibu
KUBAKI NA JANABA AU HEDHI AU NIFASI
MPAKA ALFAJIRI
1031. Mwenye janaba asipooga mpaka adhana ya alfajiri kwa kusudi au
wadhifa wake ulikuwa ni kutayamamu na akawa hajatayamamu kwa
kusudi mpaka ikafika alfajiri inabatilika saumu yake katika mwezi
wa Ramadhani au kadha yake, ama zisizokuwa hizo katika funga za
wajibu na sunna haibatiliki, na kwa tahadhari ya sunna kutoacha
kuoga au kutayamamu kabla ya alfajiri, hasa katika wajibu maalum
kama vile saumu ya nadhiri ya siku maalum.
1032. Asipooga au asipotayamamu mpaka adhana ya Alfajiri katika
saumu ya wajibu ya wakati maalum kama vile saumu ya Ramadhani,
lakini sio kwa kusudi, au kama akizuiwa na mtu kuoga au kutaya-
mamu inasihi saumu yake.
1033. Mwenye janaba ambaye anataka kuleta saumu ya wajibu kama vile
211
Al-Masailul Islamiyah
Page 226
saumu ya mwezi wa Ramadhani, ikiwa hajaoga kwa kusudi mpaka
wakati ukawa mfinyu ni wajibu atayamamu na afunge na saumu
yake itasihi, ingawa ni bora kwake alipe kadha ya saumu hiyo pia.
1034. Mwenye janaba akisahau kuoga katika mwezi wa Ramadhani na
akakumbuka baada ya kupita siku ni wajibu arudie saumu ya siku
hiyo, na akikumbuka baada ya siku nyigine inamlazimu kulipa
kadha ya siku ambazo anayakini kuwa alikuwa na janaba, mfano
kama hakujua amebaki na janaba siku tatu au nne ni wajibu alipe
saumu ya siku tatu kwa babu ndio kiasi alicho na yakini.
1035. Mwenye kukusudia kupata janaba katika siku za Ramadhani kati-
ka wakati usiotosheleza kuoga na kutayamamu inabatilika saumu
yake, na ni wajibu kwake kulipa kadha na kafara ,lakini akisababi-
sha kupata janaba katika wakati unaotosha kwa kutayamamu ni
wajibu kwake atayamamu na afunge ,na ni bora alipe kadha ya siku
hiyo.
1036. Mwenye kuwa na janaba katika usiku wa mwezi wa Ramadhani au
akajua kwamba lau akilala hataamka mpaka alfajiri, ni wajibu
kwake asilale, na akilala na asiamke mpaka alfajiri inabatilika
saumu yake na ni wajibu kwake kadha na fakara.
1037. Akilala mwenye janaba usiku katika mwezi wa Ramadhani inaju-
zu kwake kulala mara ya pili kabla ya kuoga ikiwa ni kawaida
yake kuamka kabla ya alfajiri, na ikiwa sio kawaida yake kuamka
inajuzu kwake kulala kabla ya kuoga lau akitarajia kuamka mara
ya pili kabla ya adhana ya Alfajiri, na kwa tahadhari asilale mpaka
aoge.
1038. Mwenye kuwa na janaba usiku katika mwezi wa Ramadhani aki-
tambua au ni kawaida yake kuamka kutoka usingizini kabla ya
adhana ya Alfajiri ikiwa amenuia kuoga baada ya kuamka kwake na
akalala na nia hiyo mpaka Alfajiri inasihi saumu yake.
212
Al-Masailul Islamiyah
Page 227
1039. Mwenye janaba katika usiku wa mwenzi wa Ramadhani na ambaye
anajua au anatarajia kwamba ataamka kabla ya adhana ya Alfajiri
ikiwa hakutaka kuoga baada ya kuamka au akasitasita kwamba aoge
au laa lau akilala na asiamke inabatilika saumu yake na ni juu yake
kulipa kadha pamoja na kafara.
1040. Akijiotea mfungaji mchana sio wajibu kwake kufanya haraka kuoga
japo ni bora kufanya hivyo.
1041. Akiamka mfungaji katika mwezi wa Ramadhani baada ya adhana
ya Alfajiri akakuta amejiotea inasihi saumu yake hata kama aki-
tambua kuwa amejiotea kabla ya adhana
1042. Mwenye kutaka kulipa kadha ya saumu ya mwezi wa Ramadhani
akibakia na janaba mpaka adhana ya Alfajiri inabatilika saumu yake
hata kama hakufanya hivyo kwa makusudi.
1043. Mwenye kutaka kulipa kadha ya saumu ya mwezi wa Ramadhani
akiamka baada ya adhana ya Alfajiri na akakuta amejiotea na aka-
tambua kwamba amejiotea kabla ya adhana ikiwa wakati wa kadha
ni mfinyu, mfano ikiwa ni juu yake kulipa kadha ya siku tano na
haikubakia hadi mwezi wa Ramadhani ila siku tano tu, inamlazimu
afunge siku hiyo kwa tahadhari na afunge badala yake baada ya
mwezi wa Ramadhani vilevile, na ikiwa wakati wa kadha sio mfu-
nyu inabatilika saumu yake.
1044. Akibakia na janaba mpaka adhana ya Alfajiri katika saumu ya waji-
bu isiyokuwa saumu ya mwezi wa Ramadhani au kadha yake laki-
ni sio kwa makusudi ikiwa saumu hiyo ni ya wajibu maalumu kwa
wakati, mfano ikiwa aliweka nadhiri kufunga siku hiyo inasihi
saumu yake na ikiwa siyo ya wajibu maalumu mfano saumu ya
kafara basi kwa tahadhari ya sunna afunge badala ya siku hiyo siku
nyingine
213
Al-Masailul Islamiyah
Page 228
1045. Akitoharika mwanamke kutokana na hedhi au nifasi kabla ya adha-
na ya Alfajiri na akawa hajaoga kwa makusudi au ilikuwa wadhifa
wake ni kutayamamu na akawa hajatayamam kwa makusudi inaba-
tilika saumu yake katika mwezi wa Ramadhani bali na katika kadha
na katika kila wajibu maalumu vile vile kwa tahadhari.
1046. Mwanamke ambaye anatoharika kutokana na hedhi au nifasi kabla
ya adhana ya Alfajiri pia mwenye janaba ikiwa wakati hautoshi
kwa kuoga, akitaka kufunga ni wajibu kwake kutayamamu na
inasihi saumu yake kwa ilivyo na nguvu zaidi, ni sawa sawa iliku-
wa ni saumu ya mwezi wa Ramadhani au ya wajibu maalumu au ya
sunna.
1047. Akitoharika mwanamke kutokana na damu ya hedhi au nifasi kabla
ya adhana ya Alfajiri na muda ukawa hautoshi sio kwa kuoga wala
kutayamamu, au akajua baada ya adhana kwamba alishatoharika
kabla ya adhana akitaka kufunga saumu ya wajibu maalumu kama
vile saumu ya mwezi wa Ramadhani inasihi saumu yake, vivyo
hivyo ikiwa saumu yake ni ya sunna au wajibu isiyo kuwa maalu-
mu kama vile saumu ya kafara, inasihi saumu yake kwa kauli yenye
nguvu zaidi.
1048. Akitoharika mwanamke kutokana na damu ya hedhi au nifasi baada
ya adhana ya Alfajiri au akaona damu ya hedhi au nifasi katikati ya
mchana inabatilika saumu yake hata kama imekaribia magharibi.
1049. Akisahau mwanamke kuoga josho la hedhi au nifasi na akakumbu-
ka baada ya siku au zaidi inasihi saumu ya siku alizofunga
1050. Mwanamke mwenye istahadha akileta josho zilizotajwa katika
hukumu za istihadha inasihi saumu yake.
1051. Mwenye kugusa maiti inajuzu kwake kufunga bila ya kuoga muogo
wa kugusa maiti na akigusa maiti katika hali ya kufunga haibatiliki
214
Al-Masailul Islamiyah
Page 229
saumu yake.
KUPIGA BOMBA
1052. Kupiga bomba katika utupu wa nyuma kwa vitu vya maji maji
inabatilisha saumu na hakuna kafara juu yake hata kama ni dharu-
ra au ilikuwa ni kwa ajili ya tiba, hakuna tatizo katika bomba isiyo
ya maji maji japo ni bora kujiepusha nayo.
KUTAPIKA
1053. Akikusudia mfungaji kutapika hata kama akilazimika kwa ajili ya
maradhi na mfano wake inabatilika saumu yake na hakuna kafara
juu yake lakini akitapika kwa kusahau au bila hiyari yake inasihi
saumu yake.
1054. Akiweza mfungaji kuzuia kutapika inalazimu ajizuie, ikiwa haita-
sababisha madhara au matatizo juu yake.
1055. Akiingia mbu au mfano wake katika koo lake lazima amtoe ikiwe-
zekana na wala haibatiliki saumu yake, lakini akijua kumtoa kwake
itamsababisha kutapika haimlazimu kumtoa na inasihi saumu yake.
1056. Akicheua na kikapanda kitu mpaka kwenye koo lake au mpaka
kwenye kinywa chake ni wajibu akiteme nje na lau akimeza bila
hiyari yake inasihi saumu yake lakini ikiwa hakijafika kwenye koo
lake basi hakuna tatizo
HUKUMU YA VITENGUZI
215
Al-Masailul Islamiyah
Page 230
1057. Akileta mfungaji moja ya vitenguzi kwa kusudi inabatilika saumu
yake na hakuna tatizo kwayo ikiwa sio kwa makusudi, lakini aki-
lala na janaba na ikawa hajaoga mpaka adhana ya Alfajiri inabatili-
ka saumu yake.
1058. Mtu yeyote akiingiza kitu katika koo la mfungaji kwa lazima au
akaingiza kichwa chake kwenye maji kwa kumteza nguvu haitaba-
tilika saumu yake, lakini akilazimishwa kubatilisha saumu yake
kama lau akiambiwa ikiwa huli chakula tutakudhuru kimali au kim-
wili akala kuepuka madhara inabatilika saumu yake.
1059. Inamlazimu mfungaji asiende sehemu ambayo anajua kwamba ana-
weza kulazimishwa kufungua na akifanya wakati huo kinachoten-
gua saumu kwa kulazimishwa inabatilika saumu yake.
YALIYO MAKURUHU KWA MFUNGAJI
1060. Ni makuruhu kwa mfungaji kufanya mambo yafuatayo:-
1. Kuweka dawa kwenye macho
2. Kupaka wanja, kama ladha yake au harufu yake itafika hadi kwe-
nye koo
3. Kufanya kila chenye kusababisha udhaifu kama vile kuumika au
kujisaidia kwa wingi
4. Kuvuta ugoro “puani” ikiwa hajui kufika kwake hadi kooni, na
kwa tahadhari ya wajibu ni kuacha hayo pamoja na kujua kuwa
utafika hadi kooni
5 .Kunusa mimea yenye harufu (manukato)
6. Mwanamke kukaa ndani ya maji
7. Kuingiza vitu (vikavu) katika njia ya haja kubwa
8. Kuloanisha nguo ambayo iko mwilini
9. Kun’goa jino na kila ambacho kinasababisha kutoka damu mdomoni
10. Kupiga mswaki kwa mti mbichi
216
Al-Masailul Islamiyah
Page 231
11 .Kutia maji mdomoni au kisichokuwa maji mdomoni bila ya sababu
12 .Kumbusu mke bila kusudi la kutoka manii
13 .Kitendo ambacho kinachosababisha kuamsha matamanio na ikiwa ni
kwa kusudi la kutoka manii inabatilika saumu yake.
MAMBO AMBAYO NI WAJIBU KULIPA
KADHA NA KUTOA KAFARA
1061. Mfungaji akikusudia kutapika au kuzama katika maji au kujipiga
bomba kwa kitu cha maji maji mchana au akiwa na janaba usiku na
akaamka kama tulivyoeleza katika Mas’ala yaliyotangulia, kisha
akalala mara ya pili na akawa hajaamka mpaka adhana ya Alfajiri
ni wajibu kwake kadha tu, na lau akileta kitenguzi kingine kwa
makusudi ikiwa anajua kuwa jambo hili linabatilisha saumu yake ni
wajibu kwake kadha na kafara, lakini kafara katika kukusudia kuse-
ma uongo juu ya Mwenyezi Mungu au Mtume na Ahlul- bait wake
(as) ni katika upande wa tahadhari ya wajibu, na katika kukusudia
kutapika au kuzama kwenye maji au kupiga bomba kwa kitu cha
maji maji ni katika upande wa tahadhari ya sunna.
KAFARA ZA SAUMU
1062. Ambaye ni wajibu kutoa kafara ya saumu ya mwezi wa Ramadhani
inamlazimu kumuacha mtumwa huru au afunge miezi miwili mfu-
lulizo au alishe maskini sitini au ampe kila mmoja miongoni mwao
kibaba ( robo tatu ya kilo ) ya ngano au shairi au mfano wake, na
ikiwa hataweza hivi vitu anakuwa na hiyari baina ya kufunga siku
kumi na nane mfululizo au alishe mafukara kadri atakavyoweza, na
ikiwa hakuweza kufunga wala kulisha ni wajibu kwake alete isti-
ghifari kwa Mwenyezi Mungu kwa kusema mara moja (
Astaghafiru llaahi) na kwa tahadhari ya wajibu atoe kafara atakapo-
weza na kupata uwezo wa kimali.
217
Al-Masailul Islamiyah
Page 232
1063. Mfungaji akifanya jimai mara nyingi wakati wa mchana wa mwezi
wa Ramadhani atatoa kwa kila mara kafara ikiwa amemwingilia
kwa halali, ama ikiwa kumwingilia kwake ni haramu ni wajibu
kwake kila mara atoe kafara zote tatu kwa pamoja.
1064. Akileta mfungaji kitenguzi kisichokuwa jimai kisha akamwingilia
mke wake kwa tahadhari ya wajibu atoe kafara ya kila moja katika
hayo.
1065. Akileta mfungaji kitendo cha halali ambacho kinabatilisha saumu
kisichokuwa jimai, kama vile kunywa maji, kisha akaleta kitendo
cha haramu kinachobatilisha saumu kisicho kuwa jimai pia, kama
lau akila chakula cha haramu inamtosha kafara moja kwa yote.
1066. Akicheua mfungaji na kikapanda kitu mpaka mdomoni kwake, aki-
kimeza makusudi inabatilika saumu yake na ni wajibu kwake kadha
na kafara pamoja, na ikiwa kile kitu kinaharamishwa kuliwa kwake
kama lau akicheua ikatoka damu mpaka mdomoni mwake kisha
akameza damu kwa kusudi inabatilika saumu yake na ni wajibu juu
yake kulipa kadha, na kwa tahadhari ya wajibu pia kutoa kafara ya
kukusanya zote.
1067. Akiweka nadhiri ya kufunga siku maalumu akibatilisha saumu
yake katika siku hiyo kwa makusudi ni wajibu wake amuache
mtumwa huru au afunge miezi miwili mfululizo au alishe masikini
sitini.
1068. Mfungaji akikusudia kubatilisha saumu yake kisha ukamtokea
udhuru usiokuwa wa hiyari kama hedhi au nifasi au maradhi sio
wajibu kwake kutoa kafara
1069. Akipata yakini kwamba ni mwanzo wa Ramadhani na akabatilisha
saumu yake kwa kusudi kisha akabaini kwamba ilikuwa mwisho wa
218
Al-Masailul Islamiyah
Page 233
Shabani sio wajibu kwake kafara.
1070. Mfungaji akifanya jimai katika mwezi wa Ramadhani mke wake
ambaye amefunga, ikiwa amemlazimisha katika kumwingilia (
yaani hakuwa radhi) ni wajibu kutoa kafara yake na kafara ya (
mke wake) pia, ama ikiwa alikuwa ameridhia kuingiliwa ni waji-
bu kwa kila mmoja atoe kafara yake.
1071. Mfungaji akikimwingilia mke wake ambaye amefunga katika
mwezi wa Ramadhani hali akiwa amelala bila ya kuelewa ni
wajibu kwake kafara moja na inasihi saumu ya mke na siyo waji-
bu kwake kulipa kadhaa wala kafara.
1072. Ambaye hafungi kwa ajili ya safari au maradhi haijuzu kwake
kumlazimisha mke wake ambaye amefunga kufanya jimai, lakini
akimlazimisha kumwigilia sio wajibu kutoa kafara.
1073. Ni wajibu kutozembea kutoa kafara lakini sio wajibu kufanya hara-
ka.
1074. Ambaye analipa kadha ya saumu ya mwezi wa Ramadhani
akikusudia kufanya kinachobatilisha saumu baada ya adhuhuri ni
wajibu juu yake kulisha maskini kumi, kila maskini kibaba na
akishindwa hivyo afunge siku tatu.
MAMBO AMBAYO NI WAJIBU KULIPA
219
Al-Masailul Islamiyah
Page 234
KADHA YA SAUMU BILA KAFARA
1075. Ni wajibu kulipa kadha ya saumu bila kafara katika mambo yafu-
atayo:-
1. Akikusudia mfungaji kujitapisha au kuzama katika maji au kupiga
bomba za sindano za maji maji mchana wa mwezi wa Ramadhani haku-
na kafara ila katika upande wa tahadhari ya sunna.
2. Akiwa na janaba usiku wa mwezi wa Ramadhani na ikawa hakuzin-
duka katika usingizi wake mara ya pili mpaka adhana ya Alfajiri kwa
namna ya mifano ambayo imepita katika mas’ala yaliyotangulia.
3. Ambaye hajafanya kinachotengua saumu lakini hakunuia saumu au
amekusudia kutokufunga au anakusudia kufanya kinachobatilisha
saumu - kwa tahadhari.
4. Kusahau kuoga janaba katika mwezi wa Ramadhani na akafunga
pamoja na janaba siku moja au siku nyingi.
5. Mwenye kuleta kinachobatilisha saumu bila ya kuhakikisha kuwa ni
asubuhi katika mwezi wa Ramadhani kisha akabaini kuingia kwa asu-
buhi ni wajibu kwake kulipa kadha ya siku hiyo, na vile vile mwenye
kuleta kinacho batilisha saumu baada ya kuhakikisha kuwa ni asubu-
hi kwa kudhania kuingia asubuhi, bali hata mwenye kushuku kuingia
kwa asubuhi baada ya kuhakiki na akaleta kinachobatilisha kisha aka-
baini kuingia kwa asubuhi ni wajibu kwake kulipa kadha
6. Mtu kupewa taarifa kutoingia asubuhi akaleta vinavyobatilisha kwa
kauli ya mtoa habari kisha ikabainika kwake baada ya muda kwamba
ilikuwa asubuhi.
7. Akipewa taarifa na mtu kuingia kwa asubuhi akawa hajaamini haba-
ri aliyopewa na mtoa habari au akachukulia kuwa mtoa habari ana mfa-
220
Al-Masailul Islamiyah
Page 235
nyia mzaha akaleta vinavyobatilisha kisha ikabainika kwake baada ya
muda kwamba ilikuwa asubuhi.
8. Akifungua kipofu kwa kutegemea habari ya mtoa habari kisha aka-
baini kutoingia kwa magharibi.
9. Akiwa na yakini kuingia kwa magharibi katika anga safi kwa sababu
ya giza akafungua kisha akabaini kwamba haikuwa imeingia maghari-
bi, lakini akiwa na matumaini ya kuingia magharibi katika anga lilofu-
nikwa kwa mawingu haimlazimu kulipa kadha pindi atakapofuturu
kisha ikabainika kutoingia kwa magharibi.
10. Akiingiza maji katika mdomo wake kwa kuleta ubaridi au bila ya
sababu yakaingia katika koo lake bila ya hiyari yake, na ama lau aki-
sahu kwamba amefunga akameza maji au akasukutua kwa ajili ya udhu
yakaingia maji katika koo lake bila hiyari yake hatolipa kadha.
1076. Akiingiza katika mdomo wake kitu kisichokuwa maji na kikaingia
katika koo lake bila hiyari yake au akisukutua kwa maji yakaingia
mpaka kwenye koo lake bila hiyari sio wajibu kwake kulipa kadha.
1077. Ni makuruhu kwa mfungaji kukithirisha kusukutua na akitaka
kumeza mate yake baada ya kusukutua ni bora ateme mara tatu kisha
ameze mate yake.
1078. Akipata shaka mfungaji je imeingia magharibi au laa , haijuzu
kwake kufuturu, lakini akishuku je imekuwa alfajiri au laa, inajuzu
kwake kufuturu baada ya kupata uhakika na kuchunguza
221
Al-Masailul Islamiyah
Page 236
HUKUMU ZA SAUMU YA KADHA
1079. Kichaa akipona kichaa chake sio wajibu kwake kulipa kadha kwa
yaliyompita katika saumu siku za kichaa chake.
1080. Akisilimu kafiri siyo wajibu kwake kulipa kadha ya saumu iliyom-
pita katika siku za ukafiri wake, lakini lau akiritadi mwislam kisha
akasilim baada ya kuritadi ni wajibu kwake kulipa kadha kwa
yaliyompita katika saumu siku za kuritadi kwake.
1081. Ni wajibu kulipa kadha kwa yale yaliyompita katika saumu kwa
sababu ya kulewa au kwa kutumia kwake kitu cha kulevya kwa ajili
ya matibabu ya wajibu.
1082. Akifungua kwa siku nyingi kwa udhuru kisha akashuku wakati wa
kuondoka udhuru ikiwa ni kutokana na uzembe ni wajibu kwake
kwa tahadhari afunge siku nyingi zaidi kiasi cha kupata matumaini,
mfano lau akisafiri kabla ya mwezi wa Ramadhani na wala hajui
kwa uzembe, amerudi katika siku ya tano au ya sita katika mwezi wa
Ramadhani, ni wajibu wake afunge siku sita kwa tahadhari, ama
ikiwa hajui wakati wa kuondoka udhuru bila ya uzembe, inajuzu
kwake alete kadha kwa uchache yaani siku tano, ingawa kwa tahad-
hari ya sunna alipe kadha ya nyingi zaidi yaani siku sita.
1083. Ikiwa ni wajibu alipe kadha ya Ramadhani nyingi na akawa hajaai-
nisha katika nia kwamba anayoileta ni kadha ipi katika zile
Ramadhani, inahesabika kuwa ni kadha ya Ramadhani ya kwanza.
1084. Inajuzu kwa mwenye kufunga kadha ya mwezi wa Ramadhani
kufungua kabla ya adhuhuri ikiwa muda wa kadha sio mfinyu.
222
Al-Masailul Islamiyah
Page 237
1085. Mtu akipitwa na saumu ya mwezi wa Ramadhani kwa ajili ya hedhi
au nifasi au maradhi na akafa kabla ya kumalizika mwezi wa
Ramadhani sio wajibu kulipiwa kadha kwa yaliyompita katika
saumu ya mwezi huo.
1086 Akipitwa na saumu ya mwezi wa Ramadhani kwa ajili ya marad-
hi na yakaendelea maradhi yake mpaka Ramadhani nyingine hai-
tomuwajibikia kulipa kadha kwa yale yaliyompita katika saumu ya
mwezi huo, ni wajibu kwake ampe fakiri kwa kila siku kibaba cha
chakula, yaani ngano au mkate wake au kibaba cha shairi au mkate
wake, ama ikimpita saumu kwa ajili ya udhuru kama safari na
ukaendelea udhuru wake mpaka Ramadhani nyingine inalazimu
kwa tahadhari ya wajibu alipe saumu kwa siku ambazo zimempita
na ampe fakiri kibaba kwa kila siku.
1087. Ugonjwa ukichukua miaka mingi ni wajibu kwake kulipa kadha ya
Ramadhani ya mwisho tu baada ya kupona na atoe kibaba cha cha-
kula kwa kila siku iliyopita katika miaka iliyopita, yaani ngano,
shairi au mikate yake, tende au zabibu.
1088. Akichelewesha kadha ya saumu ya mwezi wa Ramadhani kwa
miaka mingi ni wajibu kwake kulipa kadha na kutoa fidia moja kwa
kila siku iliyompita.
1089. Akifungua katika mwezi wa Ramadhani kwa kusudi ni wajibu aili-
pe na afunge badala ya kila siku moja ( afunge) siku sitini au alishe
mafakiri sitini au amuache mtumwa huru, na ikiwa hatolipa
yaliyompita mpaka Ramadhani nyingine inamlazimu kutoa kibaba
kingine badala ya kila siku ambayo hakufunga ukiongezea na kafa-
ra, na inamlazimu vile vile kulipa saumu zilizompita.
1090. Ni wajibu kwa mtoto mkubwa kulipa yale yaliyompita baba yake
aliyefariki katika hali ya uhai wake katika saumu na swala kwa
223
Al-Masailul Islamiyah
Page 238
mujibu wa maelezo ambayo yamepita katika mas’ala yaliyotangu-
lia, na vivyo hivyo amlipie mama yake baada ya kufariki kwake
yale yaliyompita katika uhai wake katika saumu na swala , kwa
tahadhari wajibu.
1091. Ikiwajibika kwa baba kulipa kadha ya saumu ambayo sio saumu ya
mwezi wa Ramadhani, mfano saumu ya nadhiri, inamlazimu mtoto
mkubwa kumlipia kwa tahadhari.
HUKUMU ZA SAUMU YA MSAFIRI
1092. Msafiri ambaye ni wajibu kwake kupunguza swala ni wajibu asi-
funge pia, na msafiri ambaye anakamilisha swala, mfano ambaye
safari ni kazi yake au safari yake ni safari ya maasia, ni wajibu afun-
ge.
1093. Hakuna mushikeli kusafiri katika mwezi wa Ramadhani lakini ni
makuruhu kusafiri ikiwa ni kwa ajili ya kukimbia saumu.
1094. Ikiwajibika kwa mtu funga maalum isiyokuwa saumu ya mwezi
wa Ramadhani kama vile saumu ya nadhiri maalum kwa wakati,
basi ni lazima asisafiri katika siku hiyo maadamu halazimiki kusa-
firi -tahadhari ya wajibu - na akisafari ni lazima akusudie kukaa
siku kumi na afunge kama inawezekana
1095. Akiweka nadhiri kufunga na akawa hajaainisha siku ambayo atafun-
ga kwayo haijuzu kuileta akiwa safarini, lakini lau akiweka nadhi-
ri kufunga siku maalumu katika safari basi lazima ailete katika safa-
ri, na vivyo hivyo akiweka nadhiri kufunga siku hiyo maalumu, ni
sawa akiwa katika safari au hayuko safarini ni wajibu kufunga siku
hiyo hata kama akiwa safirini.
224
Al-Masailul Islamiyah
Page 239
1096. Inajuzu kwa msafiri kufunga sunna kwa siku tatu katika Mji wa
Madinatul- munawara kwa kuomba haja.
1097. Kwa yule ambaye hajui kwamba safari inabatilisha saumu akifunga
katika safari na katikati ya mchana akatambua hukumu, inabatilika
saumu yake, na asipotambua mpaka magharibi inasihi saumu yake.
1098. Akisahau kwamba yeye ni msafiri au akasahau kwamba saumu ya
msafiri ni batili na akafunga katika safari inabatilika saumu yake.
1099. Akisafiri mfungaji baada ya Adhuhuri ni wajibu akamilishe saumu
yake, na akisafiri kabla ya Adhuhuri na akakusudia kukata masafa
ya kisheria ( kama ilivyopita katika swala ya msafiri ) inalazimu
kutengua saumu yake pindi anapofika katika mpaka wa kupungu-
zia ( yaani kutokuonekana kuta za mji na kutosikika adhana yake),
na akibatilisha saumu yake kabla ya hapo ni wajibu kwake kafara
kwa tahadhari ya wajibu.
1100. Akifika mfungaji kabla ya adhuhuri katika mji wake au sehemu
ambayo anataka kukaa siku kumi hapo ikiwa hajaleta vinavyobati-
lisha saumu mpaka wakati huo ni wajibu afunge siku hiyo, na ikiwa
ameleta vinavyobatilisha saumu sio wajibu kwake kufunga siku
hiyo.
AMBAYE SIO WAJIBU KWAKE SAUMU
1101. Ikiwa hawezi kufunga saumu au saumu ina mletea matatizo kwa
ajili ya uzee sio wajibu kwake kufunga, lakini inamlazimu kutoa
kibaba cha chakula kwa maskini kwa kila siku kama yalivyotangu-
lia maelezo yake.
1102. Yule ambaye hawawezi kufunga kwa ajili ya uzee akiweza na aka-
pata upya uwezo wa kufunga baada ya mwezi wa Ramadhani inam-
lazimu alipe yale yaliyompita kwa tahadhari.
225
Al-Masailul Islamiyah
Page 240
1103. Mwenye kiu ( ambaye anakuwa na kiu sana na hawezi kuvumilia
kiu au inamletea matatizo sana) sio wajibu kwake saumu na inam-
lazimu kutoa badala ya kila siku kibaba cha chakula kwa fakiri, kwa
mifano iliyopita maelezo yake na kwa tahadhari ya sunna asinywe
maji kwa wingi ila kwa kiwango cha dharura na inamlazimu kuli-
pa kadha kwa yaliyompita akiweza kufunga katika mwaka huo.
1104. Mwanamke anayenyonyesha mwenye maziwa machache, ni sawa
awe ni mama wa mtoto au ameajiriwa au ananyonyesha bila mali-
po, ikiwa saumu inamdhuru au inamdhuru anaye nyonya sio waji-
bu kwake kufunga, na ni wajibu atoe kwa fakiri badala ya kila siku
aliyofungua kibaba cha ngano au shairi au mikate yake, na ni waji-
bu alipe yaliyompita katika saumu akiweza kufunga katika mwaka
huo, na akijitolea mwenye kunyonyesha mtoto bila ya malipo au
akachukua ujira kwa baba wa mtoto au mama wa mtoto au mtu
mwingine akitoa ujira wake sio wajibu kwa mama kumpa mnyo-
nyeshaji mtoto, na kufunga.
1105. Mwanamke ambaye hawezi kufunga katika mwaka kwa sababu ya
kubeba mimba au kunyonyesha wala hakuweza kulipa katika
mwaka huo kwa sababu hiyo hiyo sio wajibu kwake kufunga wala
kulipa kadha, ni wajibu kutoa kwa maskini kwa kila siku vibaba
viwili vya chakula, kibaba baada ya mwezi wa Ramadhani na kiba-
ba kingine mwisho wa mwaka, yaani kabla Ramadhani ya pili.
NJIA ZA KUTHIBITI MWANZO
WA MWEZI
1106. Unathibiti mwanzo wa mwezi kwa mambo matano:-
1. Mtu mwenyewe kuuona mwezi mwandamo.
2. Kutoa habari ya kuonekana kwake watu ambao inapatikana yaki-
ni kutokana na maneno yao na vivyo hivyo kwa kila ambacho mtu
226
Al-Masailul Islamiyah
Page 241
anapata yakini kwa sababu yake.
3. Kupata habari kwa ( watu wawili) waadilifu kwamba wameona
mwezi usiku, lakini wakihitalifiana katika wasifu wa mwezi hau-
tothibiti mwanzo wa mwezi.
4. Kumalizika kwa mwezi uliotangulia wa shabani siku thelethini,
hivyo unathibiti mwanzo wa mwezi wa Ramadhani na vivyo
hivyo kwa miezi mingine.
5. Kiongozi wa kidini akitangaza kuonekana kwa mwezi.
1107. Akihukumu kiongozi wa sharia “Marja’a” kuthibiti mwanzo wa
mwezi inalazimu kutekeleza hukumu yake hata kwa yule asiyemfu-
ata, ikiwa hakuhukumu kiongozi mwingine kupinga. Lakini
mwenye kujua kwamba kiongozi wa kisheria amekosea katika
hukumu yake basi hawezi kufanya kwa mujibu wa hukumu ya kion-
gozi huyo.
1108. Hauthibiti mwanzo wa mwezi kwa utabiri wa wanasayansi na wana-
jimu, lakini mtu akipata yakini kwa sababu ya habari yao ni
wajibu kufanya kwa mujibu wa habari yao.
1109. Ukithibiti mwezi mwandamo katika mji, haimaanishi kuthibiti kwa
watu wa mji mwingie ila ikiwa miji miwili imekaribiana au ikiju-
likana kwamba anga lao ni moja.
SAUMU AMBAZO NI HARAMU NA
MAKURUHU
1110. Inaharamishwa kufunga katika Iddil-fitiri na Idi Al- adhuha na vile
vile inaharamishwa kufunga katika siku ya shaka kwamba ni mwi-
sho wa shabani au ni mwanzo wa mwezi wa Ramadhani kama ata-
funga kwa nia ya mwanzo wa Ramadhani, na inaharamishwa kufun-
227
Al-Masailul Islamiyah
Page 242
ga katika siku za tashiriqi (mibano) kwa mwenye kuwa Minaa.
1111. Inaharamishwa kwa mwanamke kufunga sunna ikiwa hiyo ni katika
kupoteza haki za mume wake na kwa tahadhari ya sunna asifunge
sunna bila ya idhini yake hata kama hadhuru haki yake.
1112. Inaharamishwa kwa mtoto kufunga sunna ikiwa inaleta maudhi kwa
wazazi wake au babu yake.
1113. Mwenye kujua kuwa saumu haimdhuru ni wajibu wake afunge hata
kama akiambiwa na daktari kuwa saumu inamdhuru, na mwenye
kuwa na yakini kwamba saumu inamdhuru au akadhani hivyo ni
wajibu asifunge hata kama akiambiwa na daktari kwamba saumu
haimdhuru na lau akifunga na hali ni hiyo saumu yake haitasihi
SAUMU YA SUNNA
1114. Ni sunna kufunga siku zote za mwaka ukiacha siku zilizotajwa
ambazo ni haramu au makuruhu kufunga na imetiliwa mkazo kufun-
ga baadhi ya siku ambazo ni: Siku ya Al hamisi katika mwanzo wa
kila mwezi, Al hamisi ya mwisho na Jumatano ya kumi la kwanza la
kila mwezi, na ikiwa hajafunga katika siku hizi ni mstahabu kwake
alipe, ikiwa hatalipa kadha pia ni mstahabu atoe kwa fakiri badala ya
kila siku - kibaba yaani gramu750 takribani - ya ngano au shairi au
unga wake au mikate yake au 6/12 ya uzito wa fedha halisi – gramu
moja na robo - na saumu ya siku ya kumi na tatu, kumi na nne na
kumi na tano katika kila mwezi. Na saumu ya mwezi wa Rajab,
Shabani na saumu ya siku ya Nairuzi na siku ya nne mpaka ya tisa
katika mwezi wa shawwali na siku ya ishirini na tano na ishirini na
tisa katika mwezi wa Dhil- qaad na siku ya kwanza mpaka ya tisa
katika mwezi wa Dhil-hija ( siku ya Arafa) lakini ikiwa udhaifu
unaosababishwa na saumu unamzuia kuleta dua siku ya Arafa ni
228
Al-Masailul Islamiyah
Page 243
makuruhu kufunga siku hiyo, na saumu ya Iddil-ghadiri ( 18 Dhil-
hija) na siku ya Mubahala ( 24 Dhil –hija) na siku ya kwanza, ya
tatu na ya saba katika Muharam na siku ya kuzaliwa Mtume (saww)
( 17 Rabiul-Awwal) na saumu ya siku ya kumi na tano katika mwezi
wa Jamaadul-ulaa na siku ya kupewa utume Mtume (saww ) 27
Rajab.
1115. Lau akijishughulisha kwa saumu ya mustahabu sio wajibu kwake
kuitimiza mpaka magharibi, bali kama akialikwa na ndugu yake
muumini kwenye chakula ni mustahabu kuitika wito wake na kufun-
gua katikati ya mchana
SAUMU YA MAKURUHU
1116. Ni makuruhu kufunga siku ya Ashuraa na siku inayohisiwa kuwa niArafa au Iddul - Adhuha
WATU AMBAO NI SUNNA KUJIZUIA KULA
1117. Ni sunna kwa watu sita kujizuia kula katika mwezi wa Ramadhani
hata kama hawafungi:-
1. Msafiri ambaye amekula safarini kisha akarudi kwenye nchi
yake kabla ya Adhuhuri au akafika sehemu ambayo anataka
kukaa hapo siku kumi.
2. Msafiri ambaye anafika katika nchi yake baada ya adhuhuri au
sehemu ambayo anataka kukaa hapo kwa siku kumi.
3. Mgonjwa ambaye anapona kabla ya adhuhuri na akawa amek-
wisha kula kabla ya hapo.
4. Mgonjwa ambaye anapona baada ya adhuhuri, Mwanamke
229
Al-Masailul Islamiyah
Page 244
ambaye ametoharika katika damu ya hedhi au nifasi katikati ya
mchana.
5. Kafiri ambaye anasilimu baada ya Adhuhuri.
1118. Ni sunna kwa mfungaji aswali magharibi na isha kabla ya kufuturu,
lakini kama kuna mtu ambaye anamsubiri mezani au anashauku sana
na chakula kiasi kwamba mawazo yake yote hayatakuwa kwenye
swala ni bora afuturu kwanza, lakini afanye haraka kuswali kwa
wakati wa fadhila kadri inavyowezekana.
HUKUMU ZA KHUMSI
1119. Khumsi ni wajibu katika vitu saba:-
1. Faida inayotokana na biashara
2. Madini
3. Kanzi
4. Mali ya halali iliyochanganyikana na mali ya haramu
5. Vito vya thamani vinavyotolewa baharini
6. Ngawira za vita
7. Ardhi anayoinunua kafiri dhimmiyi (aliye katika himaya ya
dola ya kiislam) kwa mwislamu
Faida inayopatikana kutokana na biashara
1120. Ni wajibu kutoa khumsi katika ziada, baada ya kutoa matumizi ya
mwaka mzima.
1121. Ni wajibu kutoa khumsi inapofikia kiwango maalum, itolewa moja
ya tano 20%.
1122. Kiwango maalumu cha madini ya dhahabu ni gramu 68, fedha ni
gramu 472 –kiwango hiki ni baada ya kutoa gharama zote.
230
Al-Masailul Islamiyah
Page 245
1123. Ni wajibu khumsi igawanywe mafungu mawili:-
1. Fungu la maseyidi: Ni wajibu wapewe maseyidi maskini au
maseyidi mayatima ambao ni mafukara au msafiri ambaye ni
seyid.
2. Fungu la pili: ni la Imamu na katika zama hizi anapewa
Mujitahidi ambaye ametimiza masharti au linatumika katika
upande atakaotoa ruhusa litumike.
HUKUMU ZA ZAKA
1124. Zaka ni wajibu katika mambo tisa:-
1- Ngano 2 – Shairi 3 - Tende
4 - Zabibu 5- Dhahabu 6 - Fedha
7- Ngamia 8 -Ng’ombe 9 -Mbuzi na Kondoo
Masharti ya Zaka:-
1125. Zaka ni wajibu inapotimia kiwango maalum. Kiwango cha Ngano,
Shairi, Tende na Zabibu ni kilo gram 847 na gram 207 baada ya
kutoa gharama zote, na kiwango cha zaka yake ni 1/10 ikiwa ime-
nyeshewa na mvua na kama imemwagiliwa zaka yake ni 1/20
Kiwango cha Dhahabu
1126. Dhahabu ina viwango viwili:-
1- Kiwango cha kwanza ni gram 72 na zaka yake ni 1/40.
2- Kiwango cha pili ni gramu 4/14 yaani zikiongezwa gram 4/14 katika
gramu 72 ni wajibu kutoa 1/40 kutoka katika jumla ya gramu 4/86.
Kiwango cha Fedha
231
Al-Masailul Islamiyah
Page 246
1127.Fedha ina viwango viwili:-
1. Mithiqal 105 ambayo ni sawa na gram 104 takribani na zaka yake ni
1/40.
2. Mithqal 21 ambayo ni sawa na gram 6/12 yaani inapoongezeka katika
kiwango cha awali na zaka yake ni 1/40.
Zaka ya Ng’ombe, Ngamia, mbuzi na Kondoo
1128.Katika wanyama kuna masharti mawili:-
1- Wasifanye kazi kwa muda wa mwaka mzima.
2- Wawe wanakula majani mbugani wenyewe wasikatiwe majani na kul-
ishwa.
Kiwango cha ngamia
1129. Kiwango cha kwanza ni ngamia watano zaka yake ni mbuzi mmoja.
Kiwango cha pili ni ngamia kumi zaka yake ni mbuzi wawili.
Kiwango cha tatu ni ngamia kumi na tano, zaka yake ni mbuzi
watatu. Kiwango cha nne ni ngamia ishirini zaka yake ni mbuzi
wanne. Kiwango cha tano ni ngamia ishirini na tano zaka yake ni
mbuzi watano. Kiwango cha sita ni ngamia ishirini na sita na zaka
yake ni ngamia ambaye ameingia mwaka wa pili. Kiwango cha
saba ni ngamia thelathini na sita na zaka yake ni ngamia aliyeingia
mwaka wa tatu. Kiwango cha tisa ni ngamia sitini na moja na zaka
yake ni ngamia aliyeingia mwaka wa tano. Kiwango cha kumi ni
ngamia sabini na sita na zaka yake ni ngamia wawili waloingia
mwaka tatu. Kiwango cha kumi na moja ni ngamia tisini na moja
zaka yake ni ngamia wawili walioingia mwaka wa nne. Kiwango cha
kumi na mbili ni mia na ishirini na moja na kuendelea, hapo atah-
esabu arobaini arobaini na atatoa kwa kila ngamia arobani ngamia
mmoja mwenye miaka mitatu au atahesabu hamsini hamsini na ata-
toa kwa kila ngamia hamsini ngamia mmoja mwenye miaka minne.
232
Al-Masailul Islamiyah
Page 247
Kiwango cha Ng’ombe
1130. Kiwango cha kwanza ni ng’ombe thelathini na zaka yake ni
ndama aliyeingia mwaka wa pili. Kiwango cha pili ni ng’ombe
arobaini na zaka yake ni ndama aliyeingia mwaka wa tatu, idadi
ikiwa zaidi ya viwango hivyo zitahesabiwa thelathini thelathini au
arobaini arobaini na zaka yake ina tolewa kama tulivyotaja hapo juu.
Kiwango cha Mbuzi na Kondoo
1131.Kiwango cha kwanza ni mbuzi arobaini na zaka yake ni mbuzi
mmoja. Kiwango cha pili ni mbuzi mia na ishirini na moja na zaka
yake ni mbuzi wawili. Kiwango cha tatu ni mbuzi mia mbili na moja
na zaka yake ni mbuzi watatu. Kiwango cha nne ni mbuzi mia tatu na
moja na zaka yake ni mbuzi wanne.Kiwango cha tano ni mbuzi mia
nne na kuendelea, hapa atahesabu mia mia na kila mia zaka yake ni
mbuzi mmoja. Sio lazima kutoa zaka kutoka katika mbuzi wanao-
tolewa zaka bali inatosha kulipa kutoka kwenye mbuzi wake wengine
au kutoa kiasi cha thamani kinacholingana na kima chake au kutoa
kutoka katika aina nyingine.
1132. Wanaopewa zaka ni watu nane1 – Fakiri
2 - Masikini naye ni ambaye hali yake ni mbaya
zaidi kuliko fakiri
3- Anayekusanya zaka kwa amri ya Imamu au naibu wa Imamu
4-Wanaozoezwa nafsi zao nao ni:-
i) Makafiri ambao wakipewa zaka wanaelemea upande wa
Uislamu au watawasaidia waislamu katika vita
ii) Waislamu ambao nidhaifu wa imani
5- Kununulia watumwa na kuwaacha huru
233
Al-Masailul Islamiyah
Page 248
6- Wenye madeni ambao wameshindwa kulipa
7- Katika njia ya Mwenyezi Mungu, katika mambo yenye manufaa
kwa waislamu wote mfano, kujenga misikiti, shule, hospitali n.k
8- Msafiri ambaye ameishiwa na masurufu ya safari.
1133. Ni wajibu anayechukua zaka awe Shia Ithna Asharia, kama akitoa
kitu kutoka katika zaka kwa yeyote kwa kuamini kuwa ni shia ni
wajibu arudie kutoa zaka, isipokuwa kama atampa kutoka katika
fungu la wanaozoezwa nyoyo zao.
Nia ya Zaka
1134. Ni wajibu kwa anayetoa zaka akusudie kujikurubisha kwa Allah
(swt) pia ni wajibu kubainisha anachokitoa kuwa ni zaka ya mali au
ni zaka ya Fitri. Lakini kama ikiwa ni wajibu wake kutoa zaka ya
ngano au shairi hailazimu kuainisha kwamba anayotoa ni zaka ya
ngano au shairi.
1135. Zaka ya fitri inakuwa wajibu kwa kila mtu ambaye ni baleghe,
mwenye akili timamu, mwelewa na sio fakiri, kutoa yeye na (kum-
tolea) kila mmoja katika familia yake kilo tatu takriban kwa fakiri,
za ngano, shairi, mtama n.k na kama akitoa thamani ya moja ya vitu
hivi inatosha.
1136. Ambaye hamiliki chakula chake cha mwaka mzima na wala hana
kazi ambayo inamuwezesha kupata chakula chake cha mwaka yeye
na familia yake anahesabiwa kuwa ni fakiri na wala sio wajibu
kwake zaka ya fitri.
1137. Ni wajibu kumtolea zaka ya fitri kila anayezingatiwa kuwa ni kati-
ka familia yake awe mdogo au mkubwa, mwislamu au kafiri, ni
wajibu kumpa mahitaji yake au laa, awe anaishi katika mji wa mtoa-
ji au laa.
234
Al-Masailul Islamiyah
Page 249
1138. Ni wajibu kwa mwenyeji kumtolea zaka ya fitri mgeni anayekutem-
belea kabla ya magharibi kwa ridhaa yake.
Matumizi ya Zaka ya Fitiri
1139. Zaka ya fitiri inaweza kutumiwa katika moja ya mambo tuliyoyata-
ja katika zaka ya mali.
Nia ya Zaka ya Fitiri
1140. Ni wajibu wakati wa kutoa zaka ya fitri kunuia nia ya kujikurubisha
kwa Allah ( swt) na kutekeleza amri yake.
1141. Ikiwa mtu atatoa zaka ya fitri kabla ya mwezi wa Ramadhani
haitasihi na kwa tahadhari asiitoe ndani ya mwezi wa Ramadhani,
lakini kama akimkopesha fakiri mali kabla ya mwezi wa Ramadhani
kisha ikamuwajibikia zaka ya fitri baadae inajuzu kuhesabia deni
katika fitri.
HUKUMU ZA HIJA
1142. Hija ni wajibu kwa Muislamu mara moja katika maisha, ni wajibu
wa haraka kwa mwenye uwezo.
1143. Hija ya kiislamu ni wajibu kwa masharti manne:-
1. Mtu awe amebaleghe, si wajibu kwa mtoto ambaye bado haja-
baleghe lakini ni sunna kwa mtoto kuhiji akiruhusiwa na walii
wake.
235
Al-Masailul Islamiyah
Page 250
2. Awe mwenye akili, si wajibu kwa mwendawazimu.
3. Awe huru si wajibu kwa mtumwa, lakini ni sunna kwa mtumwa
aende hija akiruhusiwa na walii wake.
4. Awe na uwezo na uwezo unamaanisha mambo yafuatayo:-
i) Awe na matumizi na nauli ya kutosha awe na uwezo wa kiafya
ambao unamruhusu kuhiji.
iii). Kusiwe na kizuizi njiani, muda uwe unatosha kufanya ibada
ya hija.
1144. Ni sunna kwa asiyekuwa na uwezo wa kimali kuhiji.
1145. Ambaye hajatimiza masharti na akahiji katika hiyo hali, wajibu wa
hija hautaondoka kwake bali ni wajibu ahiji atakapotimiza mashar-
ti.
1146. Hija ya kujitolea ni mtu kumuambia asiyemiliki kitu, mimi nitaku-
pa matumizi yako na ya familia yako maadamu upo katika hija,
wakati huo hija itakuwa wajibu kwake na kama atahiji katika hali
hii itakuwa imemtosheleza kuhiji na sio wajibu tena kuhiji hata
kama masharti yatatimia
1147. Aliyekuwa na uwezo katika miaka iliyopita kisha hakuhiji ni wajibu
ahiji vyovyote itakavyowezekana hata kama amekosa uwezo.
1148. Si wajibu kwa mtu kuuza nyumba yake, kipando chake au vyombo
vyake ili aende hija.
1149.Mwenye kuwa na mali ya kuhiji lakini hawezi kwenda hija kwa
sababu ya uzee au maradhi basi ni wajibu kumpa mtu mwingine
akahiji kwa niaba yake.
236
Al-Masailul Islamiyah
Page 251
1150. Mtu akiweka nadhiri na akamuahidi Mwenyezi Mungu kwenda hija
ni wajibu aende hija hata kama alishaenda hija kabla.
1151. Inajuzu katika hija ya sunna mtu anuie kwa niaba ya Mtume (saww)
au Maimamu Maasumin (as) na wengineo waliokuwa hai au
waliotangulia mbele ya haki na ataandikiwa thawabu za hija kama
anavyoandikiwa aliyenuia hija kwa niaba yake.
1152. Mwanamke akitokwa na hedhi kabla ya ihramu, atahirimia katika
hali hiyo na akitoharika kabla ya kusimama arafa atawajibika alete
mambo ya umra, na kama hakutoharika mpaka muda wa kusimama
arafa ni wajibu abadili na anuie, “Hija ya Ifradi” na atasimama arafa
katika hiyo hali na kuleta matendo ya hija kisha analeta umra ya
mufradi, vile vile mwanamke akitokwa na hedhi au akipatwa na
nifasi baada ya Ihramu na kabla ya tawafu.
1153. Ikitokea tofauti baina ya shia na suni katika mwandamo wa mwezi
kama haitawezekana kuleta mambo ya hija kutokana na mtizamo wa
shia, basi itaruhusiwa kuleta kutokana na mtazamo wa suni na hija
itasihi.
MIGAWANYO YA HIJA
1154. Hija imegawanyika sehemu tatu:-
1. Hija ya tamatui
2. Hija ya Qiraan
3. Hija ya ifraad
1155. Hija ya tamatui ni wajibu kwa aliye mbali na mji wa Makka kwa
farsakha kumi na sita (16) au zaidi, hija ya Qiraan na hija ya Ifraadi
237
Al-Masailul Islamiyah
Page 252
ni wajibu kwa wanaoishi mji wa Makka na aliyembali na mji huo
kwa chini ya farsakha 16.
1156. Ambaye wadhifa wake ni hija ya tamatui ni lazima alete umra kabla
ya hija na ambaye wadhifa wake ni hija ya Qiraan au Ifraad ni lazi-
ma alete umra baada ya hija.
Tofauti kati ya Qiraan na Ifraad ni kuwa mwenye kuhiji hija ya Qiraan
anavaa ihram akiwa na mnyama wake, lakini mwenye kuhiji hija ya ifraad
hawi pamoja na mnyama wake.
1157. Hija ya tamatui ina amali mbili:-
1. Umra tamatui
2. Na hija tamatui
UMRA TAMATUI
1158. Amali za umra tamatui ni tano nazo ni:-
1. Ihram
2 Kuzunguka ka’aba tukufu mara saba
3. Kuswali rakaa mbili za tawafu katika maqamu Ibarahim (as) au
nyuma yake
4. Kukimbia “sa’ayi” baina ya safa na mar’wa
mara saba.
5 Kupunguza nywele au ndevu au kukata kucha.
HIJA TAMATUI
1159. Hija tamatui ina amali kumi na tatu:-
1. Ihram
2. Kusimama arafa
3. Kusimama mash’ari - muzdalifa”
4. Kurusha mawe Aqaba - Mina
238
Al-Masailul Islamiyah
Page 253
5.Kuchinja mnyama - Mina
6.Kunyoa au kupunguza nywele- Mina
7. Tawafu ya ziara
8. Rakaa mbili za swala ya tawafu ya ziara
9. Sa’ayi “kukimbia” kati ya safa na marwa
10. Tawafu nisaa
11. Rakaa mbili za tawafu nisaa
12.Kulala Mina usiku wa kumi na moja, kumi na mbili na waka-
ti mwingine ni wajibu kulala usiku wa kumi na tatu pia.
13. Kurusha mawe katika sehemu tatu Mina siku ya kumi na moja,
kumi na mbili na siku ya kumi na tatu kama akilala Mina.
AMALI ZA UMRA
Ihram
1160. Ihram ni amali ya kwanza katika amali za umra tamatui, wakati wa
ihram kwa ajili ya umra tamatui ni katika miezi ya hija (mfungo
mosi, mfungo pili na mfungo tatu).
MIQAATI (VITUO)
1161. Sehemu ya kuvalia ihramu huitwa Miqati na miqati ni moja ya sehe-
mu zifuatazo:-
1. Masjidi Shajara ni kituo cha watu wa Madina
2. Waadil aqiq ni kituo cha watu wapitao njia ya Iraki
3. Qurnul maanazil ni kituo cha watu wanaopita kutoka Twaif
4. Yalamlam ni kituo cha watu wanaopita kutoka Yemen
5. Al – Juhfa ni kituo cha watu wa Misri na Sham (Syiria na
239
Al-Masailul Islamiyah
Page 254
Jodan).
1162. Ni wajibu kwa kila mtu ahirimie katika kituo chake kama tulivyo-
taja na inasihi kwa mtu kuhirimia kabla ya kufika katika kituo kwa
kuweka nadhiri.
VITU VILIVYO WAJIBU KATIKA
IHRAM
1153.Vilivyowajibu katika ihram ni vitu vitatu:-
1. Nia: Anuie hivi (Nahirimia kwa ajili ya umra tamatui kwa kuji-
kurubisha kwa Mwenyezi Mungu) ,na maana ya kuhirimia ni
kujilazimisha kuacha vitu ambavyo tutavitaja baadae.
2. Tal- biya (wito): alete tal- bia nne kama ifuatavyo: “Labaika
Allahumma labaika, labaika laa sharika laka labaika, innal-
hamda wa niamata laka wal - mulku, laa sharika laka”.
3. Kuvaa nguo mbili: Ni wajibu kwa wanaume, na si kwa wana-
wake, japokuwa ni kwa tahadhari ya sunna kwa mwanamke
angalau mwanzo tu.
1164. Ni wajibu nguo hizo ziwe tohara na zisiwe za hariri wala ngozi ya
mnyama ambaye ni haramu na zisiwe nyepesi kiasi kwamba mwili
unaonekana.
YALIYO WAJIBU KUJIEPUSHA WAKATI
WA IHRAM
1165. Ni wajibu kwa aliyevaa Ihram kujiepusha na vitu ishirini na nne:-
1. Kuwinda mnyama wa nchi kavu au kumsaidia anayewinda, kula
windo au kuchinja ila ikiwa ni wanyama wakali wa porini
240
Al-Masailul Islamiyah
Page 255
ambao inaruhusiwa kujilinda nao kutokana na madhara.
2. Kuwakaribia wanawake kwa kuwaingilia au kubusu au kuwaan-
galia kwa matamanio.
3. Kuoa au kuozesha au kuwa shahidi.
4. Kujitoa manii kwa mkono (punyeto) au kitu chochote.
5. Kutumia manukato kama miski, zafarani au udi, kwa kula,
kunusa, kujipaka mafuta n.k, pia ni haramu kuziba pua kuto-
kana na harufu inayokarahisha.
6. Kuvaa nguo zilizoshonwa kwa wanaume, lakini inajuzu kuvaa
kimkoba cha kuhifadhia fedha hata kama kitakuwa kimeshon-
wa.
7. Kupaka wanja.
8. Kujitazama katika kioo.
9 Kuvaa soksi kwa mwanaume au chochote kinachofunika mguu.
10. Kufanya ufuska yaani kusema uongo, matusi au kujifakhari-
sha.
11. Kujadili – kuapa nayo ni kusema (laa wallaahi) – hapana wal-
lah na kwa tahadhari ya wajibu ni kujiepusha na viapo kabi-
sa.
12. Kuuwa wadudu kama viroboto, kunguni, chawa n.k.
13. kuvaa pete kwa kukusudia kuwa ni pambo.
14. Kutokuvaa mapambo kwa ujumla kama kujipaka hina au
kuvaa bangili, hereni, isipokuwa kama anavivaa muda wote .
241
Al-Masailul Islamiyah
Page 256
15. Kufunika kichwa chote au sehemu ya kichwa au sikio kwa
wanaume bali ni haramu hata kujistiri kwa hina.
16. Mwanamke kusitiri uso wake kwa kitambaa kizito.
17. Kujipaka mafuta.
18 Kung’oa nywele kichwani au sehemu nyingine ya mwili hata
kama ni unywele mmoja na hakuna tatizo kama nywele zita-
dondoka wakati wa udhu.
19. Kujitoa damu hata kama kwa kupiga mswaki.
20. Kung’oa jino hata kama damu haitatoka.
21. Kukata kucha.
22. Kujifunika mwavuli kwa wanaume wakati wa kutembea laki-
ni hakuna tatizo kujifunika nyumbani.
23. Kukata mti au kun’goa mmea katika haram tukufu.
24. kubeba silaha kama bunduki au panga n.k.
KAFARA YA VITU VILIVYO HARAMISHWA
KATIKA IHRAM.
1166. Vitu ishirini na nne vilivyoharamu katika ihram vimegawanyika
katika sehemu tatu:-
1. Vilivyo haramu na ukivifanya kunawajibisha kafara tu.
2. Vilivyo haramu na ukivifanya hakuwajibishi kafara.
3. Vitu ambavyo kuvifanya kwake kunabatilisha hija na tunataja
baadhi ya kafara kwa muhtasari
1167. Kafara ya vitu vilivyoharam katika ihram:-
242
Al-Masailul Islamiyah
Page 257
1. Kafara ya kuwinda imeelezwa kwa kirefu katika ibada ya hija.
2. Kafara ya kufanya jimai ni kutoa ngamia au ng’ombe au kondoo
kama ilivyoelezwa kwa ufafanuzi zaidi katika ibada ya hija.
3. Kafara ya kufunga ndoa kama mwanaume atamwingilia mwa-
namke ni ngamia kwa mwenye kufunga ndoa.
4. Kafara ya kufanya punyeto ni kama kafara ya kumwingilia mwa-
namke, na katika baadhi ya hali inabatilisha hija.
5. Kafara ya kutumia manukato ni kondoo.
6. Kafara ya kuvaa nguo iliyoshonwa ni kondoo.
7. Kafara ya kujipaka wanja ni kondoo.
8. Kafara ya kumtazama mwanamke ni kondoo.
9. Kafara ya kuvaa soksi ni kondoo.
10.Kafara ya ufuska ni kuomba msamaha.
11.Kafara ya kujadiliana ni ngamia au ng’ombe au kondoo.
12.Kafara ya kuua chawa ni kutoa sadaka ya kulisha maskini.
13. Kafara ya kujipamba ni kondoo kwa tahadhari.
14. Kafara ya kuvaa pete ni kondoo.
15. Kafara ya kufunika kichwa kwa wanaume ni kondoo.
16. Kafara ya mwanamke kufunika uso ni kondoo.
17. Kafara ya kujipaka mafuta ni kondoo.
18. Kafara ya kunyoa nywele ni kondoo au kufunga siku tatu au
kulisha maskini sita.
19. Kafara ya kujitoa damu ni kondoo.
20. Kafara ya kung’oa jino ni kondoo.
21. Kafara ya kukata kucha ni kondoo wawili.
22. Kafara ya kujifunika mwavuli kwa wanaume ni kondoo.
23. Kafara ya kukata mti au kung’oa mmea wa haram ni ng’ombe
au kondoo.
24. Kafara ya kuvaa silaha ni kondoo.
2. TAWAFU
243
Al-Masailul Islamiyah
Page 258
1168. Mwenye kuhiji ataingia Makka baada ya kuhirimia umra na ataleta
amali ya pili ya umra ambayo ni kuzunguka ka’aba tukufu.
1169. Namna ya kutufu: Kaaba iwe mkono wake wa kushoto na kuzungu-
ka pembeni mwake mara saba na aanzie katika jiwe jeusi na amali-
zie hapo.
1170. Katika tawafu mambo yafuatayo ni sharti:-
1. Nia, atie nia kuwa anatufu
2. Tohara kutokana na hadathi kubwa kama vile janaba, hedhi,
nifasi na hadathi ndogo yaani awe na udhu
3. Tohara ya nguo na mwili
4. Mwanaume awe ametahiriwa
5. Kustiri uchi na ni wajibu kwa mwenye kujistiri yale yote
ambavyo ni wajibu kwa mwenye kujistiri katika swala
6. Tawafu: Iwe kati ya ka’aba tukufu na maqamu
Ibrahimu
7. Jiwe la Ismaili liwe ndani ya tawafu
8. Mwili wote uwe nje ya ka’aba.
3. SWALA YA TAWAFU
1171. Amali ya tatu ni kuswali swala ya tawafu katika
maqamu Ibarahim au nyuma yake.
1172. Swala ya tawafu ni kama swala ya asubuhi na
unatia nia ya kuswali swala ya tawafu.
4. SA’I
244
Al-Masailul Islamiyah
Page 259
1173. Amali ya nne katika amali za umra ni sa’i yaani kukimbia baina ya
safa na mar’wa mara saba, na katika sehemu hii ni wajibu kwa
mwenye kuhiji akate masafa kati ya safa na mar’wa mara saba kwa
kuanzia safa na kumalizia mar’wa.
1174. Kutoka safa kwenda mar’wa inahesabika kuwa ni mzunguko mmoja,
na kurudi kutoka mar’wa kwenda safa ni mzunguko mwingine.
1175. Nia ya kukimbia sa’i.
5 - KUNYOA AU KUPUNGUZA
1176. Baada ya kukamilisha Sa’i ni wajibu kuleta amali ya tano ambayo ni
kupunguza nywele.
1177. Kupunguza: Inamaanisha kukata sehemu ya nywele za kichwa au
kukata kucha.
1178. Baada ya kunyoa, vitu vilivyokuwa haramu kwa ajili ya ihramu
vitakuwa halali ila viwili amabvyo uharamu wake ni kwa ajili ya
utukufu wa haram navyo ni :-
1. kuwinda
2. kukata mti au kung’oa mmea wa haram.
UMRA YA MUFRAD
1179. Akitaka mtu kuleta umra peke yake atafanya amali mfano wa amali
ya umra tamatui, lakini ataongeza tawafu nisai na swala ya tawafu
nisai.
AMALI ZA HIJA TAMATUI
245
Al-Masailul Islamiyah
Page 260
1180. 1. Kuhirimia Hija
Mambo ya hija ni kumi na tatu kama tulivyosema na amali ya kwanza ni
kuvaa Ihramu, ni juu ya mwenye kuhiji baada ya kukamilisha mambo ya
umra, ahirimie mara ya pili kwa ajili ya hija, na tofauti ni kuwa kuhirimia
umra inakuwa katika moja ya vituo tulivyovitaja na kuhirimia hija
inakuwa Makka na ni sunna iwe katika msikiti mtukufu.
1181. Wakati wa kuhirimia hija ni baada ya kumaliza umra tamatui mpaka
wakati wa kusimama arafa.
2. KUSIMAMA ARAFA
1182. Amali ya pili katika amali za hija ni kusimama Arafa, yaani awe
katika uwanja wa Arafa kuanzia adhuhri katika siku ya Arafa (siku
ya tisa) mpaka kuzama kwa jua.
1183. Anuie katika kisimamo hiki.
3. KUSIMAMA KATIKA MASH’ARI “MUZDALI-DA”
1184. Ni wajibu kwenda Mash’ari baada ya kutoka Arafa baada ya kuza-
ma jua na awepo katika Mash’ari tangu mapambazuko ya Al-fajiri
mpaka kuchomoza kwa jua katika siku ya Idd ambayo ni siku ya
kumi.
1185. Inapokaribia kuchomoza kwa Al fajiri katika hiyo siku ni wajibu
mwenye kuhiji anuie na kusimama katika mash’ari.
4 – 6 AMALI ZA MINA.
246
Al-Masailul Islamiyah
Page 261
KUTUPA MAWE, KUCHINJA NA KUNYOA
1186. Ni wajibu kwenda Mina baada ya kuchomoza jua katika siku ya Idd
na kufanya amali tatu:-
1. Kurusha mawe katika Aqaba (nayo ni jamaratul kubra) kwa
mawe saba madogo kwa taratibu moja baada ya jingine
2. Kuchinja ngamia au ng’ombe au kondoo
3. Kunyoa kichwa chote au kupunguza, kama hija yake ni ya
kwanza kwa tahadhari ya sunna anyoe kichwa chote.
7 – 11 – AMALI ZA MAKKA.
1187. Baada ya kukamilisha amali za Mina mwenye kuhiji anaweza kwen-
da Makka siku hiyo hiyo ya Idd na kufanya amali tano:-
1.Tawafu ya ziara mara saba
2. Rakaa mbili za tawafu ya ziara kwenye maqamu Ibrahimu au
nyuma yake
3. Sa’i “kukimbia” baina ya safa na mar’wa
4. Tawafu nisai, nayo ni kama tawafu ya hija
5. Rakaa mbili za tawafu nisai.
12. – KULALA MINA
1188. Ni wajibu kwa mwenye kuhiji kulala Mina siku ya kumi na moja,
kumi na mbili na ya kumi na tatu pia, na kiwango cha wajibu kulala
mina ni nusu ya usiku kuanzia mwanzo wake au mwisho wake, na
inajuzu kujishughulisha na ibada Makka badala ya kulala mina.
1189. Kama mwenye kuhiji hakulala ni wajibu atoe kafara kwa kila siku
kondoo na atahesabika ameasi akiacha kulala mina japokuwa hija
yake ni sahihi.
247
Al-Masailul Islamiyah
Page 262
13. KUTUPA MAWE
1190. Ni wajibu kwa mwenye kuhiji kutupa mawe sehemu tatu katika
mchana wa siku alizolala mina, yaani siku ya kumi na moja, kumi na
mbili na siku ya kumi na tatu kama akilala mina, atatupa mawe saba
katika nguzo ya kwanza, mawe saba nguzo ya katikati mawe saba
na jamratul aqaba mawe saba, na kwa kufanya hivi atakuwa ame-
kamilisha amali za hija.
HUKUMU ZA NDOA
1191. Ni wajibu katika ndoa ya daima na ndoa ya muda kusoma swigha
“tamko” la ndoa na wala haitoshi kuchukuana kwa kuelewana, ama
wanaooana wasome wenyewe au waweke wakili atakayesoma kwa
niaba yao.
1192. Na wakili sio sharti awe mwanaume bali inajuzu awe mwanamke
kwa kumuwakilisha mwanaume au mwanamke.
1193. Haijuzu kwa mwanamke na mwanaume kuangaliana kama mume na
mke mpaka wapate yakini kuwa wakala wao tayari ameshafunga
ndoa, na dhana haitoshi.
1194.Inajuzu kwa mtu mmoja kusoma swigha ya ndoa kwa pande zote
mbili au kusoma swigha kwa niaba ya mwanamke kwa kujiozesha
mwenyewe, iwe katika ndoa ya daima au ya muda, lakini ni bora
kufanya tahadhari kwa kuwakilishwa na watu wawili.
Namna ya kufunga ndoa ya daima
1195. Ikiwa wenye kuoana watasoma swigha wenyewe basi mwanamke
atasema baada ya kubainishwa kiwango cha mahari “zawajtuka naf-
siy alaa swadaqil maalum” Nimekuozesha nafsi yangu kwa mahari
248
Al-Masailul Islamiyah
Page 263
maalumu), kisha mwanaume aseme haraka “Qabitu nikaaha”
(Nimekubali kuoa). Kama waoaji watawakilishwa katika kufunga
ndoa, kama jina la mwanamke ni Fatma na jina la mwanaume ni
Ahmad basi wakili wa mwanamke atasema: Zawwajtuka muwaki-
latiy Fatwimah muwakilaka Ahmad alaswadaaqil maalum
“Nimemuozesha wakala wangu Fatma wakala wako Ahmad kwa
mahari maalum”, kisha wakili wa mwanaume atasema haraka
Qabiltu nikaha limuwakiliy Ahmad “Nimekubali nihaha kwa niaba
ya wakala wangu Ahmadi kwa mahari maalumu”.
Namna ya kufunga ndoa ya muda.
1196.Kama wanaooana watafunga ndoa wenyewe, basi mwanamke atase-
ma baada ya makubaliano ya mahari na muda: Zawajtuka nafsiy fiyl
mudatil maalumati wa alaa swadaqil maalum “Nimekuozesha nafsi
yangu kwa muda maalum na kwa mahari maalumu”, kisha
mwanaume atasema haraka: Qabiltu “nimekubali”, na ndoa inasihi,
na kama wataweka wakala basi wakala wa mwanamke atasema:
Zawajtu muwakilatiy muwakilaka fiy mudatil maalumati wa alaa
swadaqil maalum“Nimemuozesha wakala wangu, wakala wako kwa
muda maalumu na kwa mahari maalum”, kisha wakala wa
mwanaume atasema haraka: Qabiltu nikaha limuwakiliy
“Nimekubali ndoa kwa niaba ya wakala wangu”, ndoa inasihi.
1197. Masharti ya ndoa:-
Ndoa ifungwe kwa lugha ya kiarabu kwa kutamkwa kwa usahihi na
kama wanaooana hawajui kiarabu, basi waweke mtu wa kufunga
ndoa kwa niaba yao anayefahamu kiarabu vizuri, na kama
haitawezekana kabisa, basi ifungwe kwa lugha yeyote, lakini ni
wajibu waseme maneno yanayo maanisha: “Nimekuozesha na
nimekubali” katika lugha yao.
Ni wajibu ndoa ifungwe kwa kusoma swigha kwa pande mbili,
kwamba mwanamke akusudie kwa kusema: “Nimekuozesha nafsi
249
Al-Masailul Islamiyah
Page 264
yangu kwamba nimekuwa mke wako, na mwanaume akusudie kwa
kusema: Nimekubali nikahi” nimeridhia hayo.
Wanaofunga au wanaofungisha ndoa wawe wamebaleghe.
Kama wakala atafungisha ndoa ni lazima ataje majina ya
wanaooana.
Wanaooana wawe wameridhia kuoana, kama mwanamke akilaz-
imishwa kukubali katika dhahiri, lakini ikajulikana kuwa ameridhia
moyoni ndoa inasihi.
1198. Kama atakosea kutamka hata herufi moja ndoa itabatilika kwa tahad-
hari kwamba itabadilisha maana yake.
1199. Kama mtu atamuozesha mwanamke kwa mawanaume bila ya rid-
haa yao, kisha wakaridhia baadae kwa kutamka, ndoa inasihi.
1200. Binti aliyebaleghe ambaye anaelewa masilahi yake kama akitaka
kuolewa, naye ni bikira ni bora achukue idhini kwa baba yake au
kwa babu yake kwa upande wa baba na wala sio lazima kuchukua
idhini kwa mama yake au kwa kaka yake.
1201. Kama baba na babu hawapo na binti sio bikira basi sio lazima kupa-
ta idhini kwa baba au kwa babu wa upande wa baba tu.
Kasoro ambazo inajuzu kuvunja ndoa
kwa ajili yake
1203. Kama mwanaume atajua baada ya ndoa kuwa mke ana moja kati ya
kasoro hizi inajuzu kuvunja ndoa:-
Wazimu
Ukoma
Mbalanga
250
Al-Masailul Islamiyah
Page 265
Upofu
Kiwete
Njia ya mkojo na ya hedhi kuwa ni moja au sehemu ya haja kubwa
na njia ya hedhi kuwa moja
Kuota mfupa au nyama ndani ya uke na unazuia jimai
Kama mwanamke atajua kuwa mume wake amekatika uume au
hana nguvu za kiume au amehasiwa basi inajuzu kuvunja ndoa.
1204. Mume akivunja ndoa kwa moja ya kasoro tulizozitaja basi ni waji-
bu watengane bila ya talaka.
1205.Mwanamke akivunja ndoa kwa sababu mume wake hana nguvu za
kiume, basi ni wajibu kwa mume kumpa nusu ya mahari, lakini
kama mwanaume au mwanamke akivunja ndoa kwa moja ya aibu
tulizozitaja, kama hawajaonana kimwili sio wajibu kwa mwanaume
kumpa mwanamke chochote, na kama atamwingilia basi ni wajibu
ampe mahari yote.
Wanawake ambao ni haramu kuwaoa
1206. Ni haramu kuoa wanawake ambao ni mahramu mfano, mama, binti,dada, mama mkwe, shangazi, mama mkubwa au mdogo, bibi, mju-kuu, binti wa dada yako mke wa baba, na mke wa mtoto wako.
1207. Ukioa mwanamke kisha ukamwingilia basi, binti wa mke wako,
binti wa binti wa mke wako na binti wa mtoto wa kiume wa mke
wako wanakuwa ni mahramu wako na ni haramu kuwaoa.
1208. Haijuzu kuoa binti ambaye ni mchumba wa mtu mwingine maadam
bado anamafungamano naye.
1209. Wafuatao ni maharimu wa mwanaume: Shangazi wa baba yake,
mama mkubwa au mama mdogo wa baba yake, shangazi wa babu
yake, shangazi wa mama yake, mama mkubwa au mama mdogo wa
mama yake, shangazi wa bibi yake, mama mkubwa au mdogo wa
251
Al-Masailul Islamiyah
Page 266
bibi yake.
1210. Wafuatao ni maharimu wa mwanamke: Mkwe, babu ambaye ni
mzazi wa wa baba mkwe, mtoto wa mume wake na mtoto wa mtoto
wa mume wake, wawe wamezaliwa au bado.
1211. Haijuzu kuoa binti wa dada wa mke na binti wa kaka yake bila ya
idhini ya mke, lakini akioa bila ya idhini ya mke wake na baadaye
akatoa idhini basi ndoa itasihi.
1212. Mtu akizini na shangazi na mama mkubwa au mdogo kabla ya
kumuoa binti wa shangazi au mama, basi haijuzu tena kumuoa huyo
binti.
1213. Mtu akimuoa binti wa shangazi au wa mama mkubwa au mdogo na
kabla ya kumwingilia akazini na shangazi au na mama mkubwa au
mdogo ni bora achukue tahadhari ajitenge nae.
1214.Mtu akizini na mwanamke ni bora achukue tahadhari asimuoe binti
wa huyo mwanamke aliyezini naye, kama mtu akioa mwanamke
kisha akamwingilia na baada ya hapo akazini na mama mkubwa,
basi mke wake hatakuwa haramu, japo ni bora atengane naye bila ya
talaka.
1215.Haijuzu mwanamke wa kiislamu kuolewa na kafiri, mkristo, myahu-
di au asiyekuwa hao. Haijuzu kwa mwislamu kuoa mwanamke
kafiri, lakini inajuzu kuoa mwanamke wa kikristo au wa kiyahudi
ndoa ya daima au ya muda.
1216.Kama atazini na mwanamke ambaye yuko kwenye eda ya talaka
rejea basi mwanamke huyo atakuwa haramu kwake, na akizini na
mwanamke ambaye yuko katika eda ya ndoa ya muda au katika eda
ya kufiwa basi inajuzu baada ya hapo kumuoa.
252
Al-Masailul Islamiyah
Page 267
1217. Mtu akizini na mwanamke ambaye hana mume wala hayupo katika
eda inajuzu kumuoa, lakini ni bora achukue tahadhari ya kusubiri
mpaka huyo mwanamke aone damu ya hedhi kisha amuoe.
1218. Ni haramu kuoa mwanamke akiwa katika eda.
1219. Mtu akijua kuwa mwanamke huyu ana mume pamoja na hivyo
yeye akamuoa, basi ni wajibu watengane na asimuoe tena.
1220. Mtu akizini na mwanamke mwenye mume basi huyo mwanamke
hatakuwa haramu kwa mume wake hata kama hatatubu, japo ni
bora kwa mume wake ampe talaka lakini ni wajibu ampe mahari
yake yote.
1221. Mtu akimlawiti kijana basi mama wa huyo kijana, dada yake na
binti yake wanakuwa ni haramu kwa mwenye kulawiti
1222.Mtu akimlawiti mtu baada ya kumuoa mama yake au dada yake au
binti yake basi mke wake hatakuwa haramu kwake.
1223. Mtu aliyehirimia hija kisha akaoa hali ya kuwa amehirimia ndoa
inabatilika, kama alikuwa anajua kuwa ndoa katika hali ya Ihramu ni
haramu pamoja na hivyo akaoa basi mwanamke huyo atakuwa hara-
mu kwake milele.
1224. Ni haramu kuoa ukiwa katika hali ya Ihramu.
1225.Mwanaume kama hatafanya tawafu nisai katika hija basi mke wake
atakuwa haramu kwake, na vile vile mwanamke kama hatafanya
tawafu nisai mume wake atakuwa haramu kwake, lakini wakifanya
hiyo tawafu uharamu utaondoka.
253
Al-Masailul Islamiyah
Page 268
1226. Mwanamke akipewa talaka tatu anakuwa haramu kwa mume wake,
lakini akiolewa na mume mwingine kisha akaachika au huyo mume
wake akifa, basi inajuzu aolewe na mume wake wa kwanza.
Hukumu za ndoa ya daima
1227. Mwanamke aliyeolewa ndoa ya daima haruhusiwi kutoka ila kwa
idhini ya mume wake, ni wajibu asimkatalie mume wake anapotaka
kustarehe naye, na asimnyime unyumba bila ya sababu ya kisheria,
na akimtii mume wake katika hilo, basi ni wajibu kwa mume wake
kumpatia chakula, mavazi na sehemu ya kukaa (nyumba), na kama
mwanaume hatamtimizia hayo itakuwa ni deni awe na uwezo au laa.
1228. Kama mwanamke akimnyima unyumba, basi hastahiki mavazi na
nyumba, lakini mahari atapewa.
1229. Haijuzu kwa mwanaume kumlazimisha mke wake kufanya kazi za
nyumbani.
1230. Mwanamke ambaye anamtii mume wake lakini hatoi matumizi, basi
inajuzu kwake katika hali hii achukue matumizi katika mali ya
mume wake bila ya idhini yake ikiwa anajiweza, lakini kama haji-
wezi basi sio wajibu kumtii mume wake wakati wa kutafuta riziki.
1231. Sio wajibu kwa mwanaume kulala kwa mke wake usiku katika kila
siku siku nne.
1232. Haijuzu kwa mwanaume kuacha kumwingilia mke wake zaidi ya
miezi minne. Ikiwa ni mmoja kwa shahiri
1233. Kama mahari haijabainishwa wakati wa kufunga ndoa, ndoa itasihi,
na mwanaume kama atamwingilia basi ni wajibu ampe mahari.
1234. Kama wakati wa kufunga ndoa hawatabainisha muda wa kulipa
254
Al-Masailul Islamiyah
Page 269
mahari ya mke, basi inajuzu kwa mke kumnyima unyumba mume
wake mpaka apewe mahari, sawa sawa mwanaume awe na uwezo au
laa, lakini mke akiridhia kumpa unyumba kabla ya kupewa mahari
basi haijuzu kwake tena kumnyima unyumba baada ya hapo bila ya
udhuru wa kisheria.
Ndoa ya mut’a “Muda”
1235. Ni kwa tahadhari ya wajibu usiache kuonana kimwili na mke wa
muda zaidi ya miezi minne.
1236. Mke wa ndoa ya muda hana haki ya kupewa matumizi hata kama
amebeba mimba ya mume wake.
1237. Mke wa muda hana haki ya kumtaka mume wake kulala kwake
kama ambavyo hamrithi mume wake na mume pia hamrithi mke.
1238. Mke wa ndoa ya muda kama hajui kuwa hastahiki kupata matumizi
na hastahiki kumtaka mume wake kulala kwake ndoa itasihi, na
haimlazimu mume wake chochote kwa sababu ya kutokujua kwake.
1239. Inajuzu kwa mke wa muda kutoka bila ya ruhusa ya mume wake,
lakini kama kutoka kwake kutasababisha haki za mume wake
kupotea itakuwa ni haramu kutoka bila ruhusa.
1240. Mke wa ndoa ya muda kama atazawadiwa na mume wake muda
uliobakia, basi ni wajibu apewe mahari yote waliyoafikiana na hii
ni kama amemwingilia, na kama hajamwingilia atampa nusu ya
mahari.
1241. Inajuzu kwa mwanaume kufunga ndoa ya daima na mke wake wa
ndoa ya muda kabla ya muda wa ndoa ya muda kwisha, pia anaweza
kumuoa kwa mara ya pili ndoa ya muda, akiwa katika eda ya ndoa
ya muda ya kwanza.
255
Al-Masailul Islamiyah
Page 270
Hukumu za kuangalia
1242. Ni haramu kwa mwanaume kuangalia mwili wa mwanamke ajin-
abiya, pia ni haramu kuangalia mwili wa binti ambaye umri wake
haujatimia miaka tisa, lakini anatambua baya na zuri, ni haramu
kuangalia hata nywele zake na kwa mwanamke pia ni haramu
kuangalia mwili wa mwanaume ajinabii.
1243. Hakuna tatizo kwa mwanaume kuangalia uso na viganja vya
mwanamke wa kikristo na wa kiyahudi.
1244. Ni wajibu kwa mwanamke kusitiri mwili wake pamoja na nywele
zake kwa mwanaume ajinabii, na kwa tahadhari asitiri mwili wake
kwa mtoto wa kiume ambaye hajabalehge lakini anaelewa kizuri na
kibaya.
1245. Ni haramu kuangalia uchi wa mwingine, hata uchi wa mtoto
anayetambua zuri na baya, lakini mume na mke inajuzu kwao kuan-
galiana mwili mzima.
1246. Ni wajibu kwa mwanaume asiangalie mwili wa mwanaume kwa
matamanio, na mwanamke asiangalie mwili wa mwanamke kwa
matamanio.
1247. Katika hali ya dharura inajuzu kwa nesi kumchoma sindano
mwanamke mwenzake au mwanaume ambaye sio mume wake, au
kusafisha uchi wa mwanamke mwenzake au uchi wa mwanume
ambaye sio mume wake, na kama akitaka kugusa uchi wa
mwanaume ni wajibu avae glovsi katika viganja vyake halafu aguse
au apige sindano au asafishe.
1248. Katika hali ya dharura inajuzu kwa mwanaume kumtibu mwanamke
ajinabiya kwa kumwangalia mwili wake au kumgusa, lakini kama
256
Al-Masailul Islamiyah
Page 271
anaweza kumtibu bila ya kumwangalia au kumgusa ni lazima
asimwangalie au asimguse.
1249.Yeyote akilazimika kumtibu mwingine kuangalia uchi wake na haku-
na njia nyingine ila kuangalia uchi basi hakuna tatizo katika hilo.
Mas’ala katika ndoa
1250. Anayeogopa kufanya haramu kwa sababu hajaoa basi ni wajibu aoe.
1251. Mume akiweka sharti katika ndoa kuwa mke awe bikra, kisha
ikabainika kuwa hana bikra basi inajuzu kwake kuvunja ndoa.
1252. Ni haramu kwa mwanamke na mwanaume kukaa faragha katika
sehemu ambayo hakuna uwezekano wa mtu mwingine kuingia, sawa
sawa wawe katika ibada, katika maongezi mengine au wamelala au
wako macho, lakini ikiwa kuna uwezekano wa kuingia mtu
mwingine hakuna tatizo.
1253. Kama mwanaume atabainisha mahari wakati wa ndoa, lakini katika
nia yake hatompa hiyo mahari, ndoa itasihi lakini ni wajibu atoe hiyo
mahari.
1254. Mwislamu ambaye anakanusha kuwepo Allah au Nabii au siku ya
mwisho au hukumu katika hukumu za wajibu kama vile swala na
saumu, na anajua kuwa ni katika wajibu wa dini basi atakuwa ni
murtadi.
1255. Mwanamke akiritadi kabla ya kuingiliwa na mume wake basi ndoa
yake itabatilika, na kama ataritadi baada ya kuingiliwa naye ameko-
ma kutokwa na damu ya hedhi pia ndoa itabatilika, lakini kama
hajakoma kutokwa damu ya hedhi ni wajibu akae eda, na kama
atasilimu kabla ya muda wa eda kwisha ndoa yake haitabatilika, na
257
Al-Masailul Islamiyah
Page 272
akibakia katika kuritadi kwake mpaka muda wa eda ukaisha basi
ndoa inabatilika.
1256. Mwanaume aliyezaliwa katika uislamu akirtadi mke wake anakuwa
haramu kwake, na ni wajibu kwa mwanamke akae eda ya kufiwa
ambayo ni miezi mnne na siku kumi.
1257. Mwanaume ambaye hajazaliwa katika uislamu kisha akasilimu,
halafu akaritadi kabla hajamwingilia mke wake basi ndoa inabatili-
ka, na kama ataritadi baada ya kumwingilia mke wake, kama mke
wake atakuwa katika umri wa kupata damu ya hedhi basi ni wajibu
wake akae eda ya kufiwa, na kama mume wake atasilimu kabla ya
muda wa eda haujaisha basi ndoa haibatiliki, la sivyo inabatilika
1258. Mwanamke akiolewa akiwa na binti wa mume mwingine, basi
mume wake wa pili anaweza kumuozesha huyo binti kwa kijana
wake wa mke wake mwingine, vile vile akimuozesha kijana wake
binti basi yeye anaweza kumuoa mama wa binti huyo.
1259. Kama mwanamke akizini kisha akapata mimba haijuzu kuitoa hiyo
mimba.
1260. Kama mwanaume atazini na mwanamke asiyeolewa wala hana eda,
kama atamuoa baada ya hapo kisha akazaliwa mtoto na hawajui
kuwa ni wa halali au ni wa haramu atakuwa ni mtoto wa halali.
1261. Kama mtu akioa mwanamke na hajui kuwa yuko katika eda au laa,
na mwanamke naye hajui, kisha akazaliwa mtoto atakuwa ni wa
halali kisheria, lakini kama mwanamke anajua kuwa yuko katika eda
basi mtoto atakuwa ni wa huyo mwanaume kisheria, lakini ndoa
itakuwa ni batili.
1262.Mwanamke akisema nimekoma kutokwa na damu ya hedhi au akise-
ma mimi sina mume, kauli yake itakubaliwa, lakini kama atakuwa
anatuhumiwa kwa uongo itabidi ufanyike uchunguzi.
258
Al-Masailul Islamiyah
Page 273
1263. Mwanaume akioa kisha akaambiwa huyo mwanamke ana mume na
akasema mimi sina mume na kama haijathibiti kisheria kuwa
alikuwa na mume basi ni wajibu kauli ya mwanamke ikubaliwe.
1264. Haijuzu kwa baba kumtenganisha binti yake na mama yake kabla
hajatimiza miaka saba, na kwa mtoto wa kiume kabla hajatimiza
miaka miwili.
1265. Binti akibaleghe tu ni sunna kufanya haraka kumuozesha kwani
Imamu Swadiq (as) amesema: “Katika maisha mazuri ya mtu
asitoke hedhi binti yake nyumbani kwake”.
1266. Kama mwanamke ataelewana na mume wake asipewe mahari ili
mume wake asioe mwanamke mwingine basi ni wajibu kwa
mwanamke asiombe mahari, na ni wajibu kwa mwanaume asioe
mwanamke mwingine.
1267.Mtoto wa zinaa akioa na akapata mtoto atakuwa ni mtoto wa halali.
128. Mwanaume akimwingilia mke wake katika mwezi wa Ramadhani au
katika hedhi atakuwa ameasi na kupata dhambi, lakini mtoto
atakayezaliwa kutokana na hicho kitendo atakuwa ni wa halali.
1269.Mwanamke akipata yakini kuwa mume wake amefariki safarini na
baada ya eda ya kufiwa akaolewa, kisha akarudi mume wake wa
kwanza kutoka safarini, ni wajibu watengane na mume wa pili na
atakuwa halali kwa mume wake wa kwanza, lakini kama mume wa
pili alisha mwingilia ni wajibu kwa mwanamke baada ya kutengana
akae eda, na mume wa pili ampe mahari yote, lakini sio wajibu kwa
mume wa pili kumpa matumizi akiwa katika eda.
259
Al-Masailul Islamiyah
Page 274
HUKUMU ZA TALAKA
1270. Ni sharti kwa mwanaume anayetoa talaka kwa mke wake, awe ame-
baleghe, awe na akili timamu, awe na hiyari, na kama atalazimish-
wa kutoa talaka, basi talaka itakuwa batili, ni sharti pia kukusudia
talaka kama atasema swigha ya talaka kwa mzaha haitasihi.
1271. Ni sharti wakati wa kutoa talaka mke awe ametoharika kutokana na
damu ya hedhi na damu ya nifasi na mume wake asiwe
amemwingilia katika hiyo tohara
1272. Talaka ya mke inasihi akiwa katika hali ya hedhi na nifasi katika
mambo matatu yafuatayo:-
Kama mume hajamwingilia baada ya ndoa.
Akijua kuwa ana mimba na kama hajajua kuwa ana mimba akam-
taliki katika hali ya kuwa na hedhi kisha baadae ikabainika kuwa
alikuwa na mimba, basi ni bora arudie talaka kwa mara nyingine
Kama mume akiwa mbali na mke akawa hajui kuwa ametoharika
kutokana na damu ya hedhi na nifasi au laa.
1273. Kama atampa mke wake talaka kwa kudhania hana hedhi, kisha
ikabainika baadaye kuwa alikuwa na hedhi wakati wa kupewa tala-
ka basi talaka itakuwa batili, na kama atatoa talaka kwa kudhania
kuwa ana hedhi lakini ikabainika baadae kuwa alikuwa tohara basi
talaka inasihi, anayejua kuwa ana hedhi au nifasi kisha akasafiri na
akataka kumpa talaka akiwa safarini ni wajibu asubiri atoharike
kutokana na hedhi au nifasi katika muda wake wa kawaida kisha
atamtaliki akitaka.
1274. Mwanaume akitaka kumpa talaka mke wake asiyepata hedhi kwa
ajili ya maradhi ni wajibu asimwingilie kwa muda wa miezi mitatu
260
Al-Masailul Islamiyah
Page 275
tangu alipomwingilia kisha ampe talaka.
1275. Talaka ni lazima iwe kwa lugha ya kiarabu na isikilizwe na wanaume
wawili waadifilifu, kama mume mwenyewe akitaka kusoma swigha
ya talaka na jina la mke ni Fatma ni wajibu aseme “Zaujatiy
Faatwimat twaaliq”, na kama ataweka wakala ni lazima wakala
aseme “Zaujatu Muwakily twaaliq”
1276. Mwanamke wa ndoa ya muda hana talaka bali kutoka kwa mume
wake ni kumalizika kwa muda wa ndoa au azawadiwe muda ulioba-
ki, kwa mume kusema “wahabtukil- mudah”, na wala sio lazima
ishuhudiwe na mashahidi wawili na wala sio sharti asiwe na hedhi.
Eda ya Talaka
1277. Binti ambaye hajatimia miaka tisa na mwanamke ambaye amekoma
kutokwa damu ya hedhi hawana eda, na mume wake kama
atamwingilia kisha akampa talaka basi inajuzu kuolewa baada ya
kupewa talaka bila ya kukaa eda. Lakini haijuzu kumwingilia binti
mdogo.
1278. Mwanamke ambaye anapata hedhi akipewa talaka ni wajibu akae
eda yaani akipata hedhi mara tatu eda inaisha, lakini akipewa talaka
kabla hajaingiliwa basi hakai eda anaweza kuolewa tu baada ya
kupewa talaka.
1279. Mwanamke ambaye haoni damu yake ya hedhi na ana umri waku-
pata hedhi akipewa talaka na mume wake ni wajibu akae eda kwa
muda wa miezi mitatu.
1280. Mwenye mimba akipewa talaka eda yake inaisha akijifungua tu au
kwa mimba kuharibika mfano kama akipewa talaka kisha akajifun-
gua baada ya saa eda inaisha.
261
Al-Masailul Islamiyah
Page 276
Eda ya ndoa ya muda
1281.Mwanamke ambaye aliolewa ndoa ya muda, muda ukiisha eda yake
ni kuona hedhi mbili na mwanamke ambaye hapati hedhi ni kwa
tahadhari ya wajibu asiolewe kwa muda wa siku arobaini na tano.
Eda ya mwanamke ambaye amefiwa na mume
1282. Eda ya mwanamke ambaye amefiwa na mume ni miezi minne na
siku kumi.
1283. Ni haramu kwa mwenye eda kuvaa nguo zenye mapambo, kupaka
wanja na kila aina ya mapambo.
Talaka ya bain na talaka rejea
1284. Talaka ya baain ikishatolewa haijuzu kwa mwanaume kumrejea
mke wake bila ya ndoa mpya.
1286. Talaka ya baain imegawanyika sehemu tano:-
Talaka ya binti ambaye hajatimia miaka tisa
Talaka ya mwanamke ambaye amekoma kutokwa damu ya hedhi
Talaka ya mke ambaye hajaingiliwa baada ya ndoa
Talaka ya kujivua na mubaraati
Talaka ya mke aliyepewa talaka tatu.
1287. Talaka rejea ni talaka ambayo inajuzu kwa mwanaume kumrejea
mke wake akiwa katika eda bila ya kufunga ndoa upya.
262
Al-Masailul Islamiyah
Page 277
Hukumu za talaka rejea
1288. Mwanaume anaweza kumrejea mke wake kwa njia mbili:-
Atamke kauli inayomaanisha kuwa amemrejea
Afanye kitendo kinachoonyesha kuwa amemrejea.
1289. Mwanaume akimpa talaka mke wake talaka tatu na alikuwa anam-
rejea katika talaka ya kwanza na ya pili au alimwacha mara mbili
kisha akamuoa upya baada ya kila talaka anakuwa haramu kwake
mpaka aolewe na mwanaume mwingine, kama akipewa talaka na
mume wa pili inakuwa halali kumuoa baada ya hapo kwa masharti
yafuatayo:-
Mume wa pili amuoe ndoa ya daima.
Mume wa pili amwingilie kimwili na ni bora atokwe na manii.
Mume wa pili amtaliki au afe.
Eda ya talaka ya mume wa pili au eda ya kufiwa ya mume wa pili
imalizike.
Talaka ya kujivua
1290. Talaka ya kujivua ni mwanamke kumpa mume wake mali ili apewe
talaka.
1291. Mume mwenyewe akitaka kusoma swigha ya talaka basi atasema
“Zaujatiy Fatwimah khaala’atuha a’laa maa badhalat”
Talaka ya mubaraati
1292. Talaka ya mubaaraati ni mume na mke kuchukiana wote, basi mke
atampa mume wake mali ili apewe talaka.
263
Al-Masailul Islamiyah
Page 278
1293. Kama mume mwenyewe atampa talaka basi atasema “Baaraatu zau-
jatiy Fatwimah a’ala mahariha fahiya twaliqu”
1294. Ni wajibu mali anayoichukua mume katika talaka ya mubaaraati isi-
zidi mahari, lakini hakuna tatizo kama itazidi katika kujivua.
Mas’ala katika eda na talaka
1295. Mwanaume akizini na mwanamke ajinabiya kwa dhana kuwa ni
mke wake ni wajibu kwa mwanamke akae eda.
1296. Mwanaume akizini na mwanamke na anajua kuwa sio mke wake
sio wajibu kwa mwanamke kukaa eda, iwe amejua kuwa
mwanaume sio mume wake au amedhania kuwa ni mume wake.
1297. Mwanaume akimhadaa mke wa mtu apewe talaka ili yeye amuoe
na mwanamke akafanya hivyo na mume wake akampa talaka, basi
talaka na ndoa zitasihi, lakini mume aliyemuoa na mwanamke wat-
apata dhambi kubwa sana.
1298. Mwanamke ambaye mume wake amepotea na anataka kuolewa na
mume mwingine ni wajibu arejee kwa mujitahidi mwadilifu au
wakala wake na kufanya kulingana na maoni yake.
Hukumu za kujivua na mubaaraati
1299.Talaka ya mubaaraati ni kama talaka ya kujivua katika hukumu zote
ila katika mambo matatu:-
Chuki katika mubaarati inakuwa katika pande zote mbili lakini kati-
ka kujivua chuki inakuwa kwa mwanamke tu.
Ni lazima mali anayoichukua mwanaume katika mubaraati isizidi
264
Al-Masailul Islamiyah
Page 279
mahari lakini katika talaka ya kujivua inaweza ikazidi mahari.
Mwanaume akitoa talaka ya mubaaraati kwa lafdhi ya mubaaraati
basi ni kwa tahadhari ya sunna baada ya “Baar’atuki” aseme hara-
ka “Faanti twaaliqu” kinyume na talaka ya kujivua.
HUKUMU ZA KUCHINJA MNYAMA NA
KUMUWINDA KWAKE
1300. Akichinjwa mnyama ambaye ni halali kuliwa katika njia ambayo
tutaitaja baadae, nyama yake itakuwa halali na mwili wake ni tohara
awe wa porini au wa nyumbani.
1302. Mnyama aliyeingiliwa na mtu au mnyama aliyezoea kula vinyesi
vya watu asipotoharishwa kisheria nyama yake haitakuwa halali
baada ya kuchinjwa.
1303. Akiwinda wanyama wa porini ambao nyama zao ni halali kama
vile swala, au mnyama ambaye nyama yake ni halali ambaye
alikuwa wa nyumbani kisha akawa wa porini kama ng’ombe,
ngamia wa nyumbani akikimbia atakuwa ni tohara na halali, lakini
wanyama wa nyumbani kama mbuzi, kuku wa nyumbani na
wanyama halali wa porini wanao fugwa nyumbani hawawi tohara
wala halali kwa kuwindwa.
1304. Wanyama wa porini ambao ni halali kuliwa wanakuwa tohara au
halali kwa kuwindwa wanapokuwa na uwezo wa kukimbia au kuru-
ka, hivyo kifaranga cha ndege hakiwi halali kama hakiwezi kuruka
au mtoto wa swala hawi halali kama hawezi kukimbia.
1305. Mnyama ambaye ni halali kuliwa na asiyekuwa na damu inayotoka
kwa kasi kama samaki, akijifia atakuwa tohara lakini haijuzu kuli-
wa .
265
Al-Masailul Islamiyah
Page 280
1306. Mnyama ambaye ni haramu kuliwa kama nyoka hawawi halali kwa
kuchinjwa lakini mzoga wake ni tohara.
1307. Mnyama akizaa mtoto amekufa au akitolewa tumboni amekufa ni
haramu kula nyama yake.
NJIA YA KISHERIA YA KUCHINJA
1308. Njia ya kisheria ya kuhalalisha mnyama ni kukata mishipa minne
chini ya shingo na haitoshi kukata kidogo bali ni wajibu kuikata
kwa ukamilifu.
1309. Akikata baadhi ya mishipa minne kisha akasubiri hadi akafa kisha
akamalizia mishipa mingine hata kama hajasubiri kwa muda mpaka
kufa kwa mnyama huyo akawa hajakata mishipa kwa mfuatano
kama ilivyozoeleka, kama atakata mishipa iliyobaki kabla ya kufa
kwa mnyama atakuwa ni halali, lakini kwa tahadhari ya sunna ni
kujiepusha na huyo mnyama.
1310. Mbwa mwitu akikata shingo ya mbuzi kiasi kwamba mishipa minne
haijabaki ambayo ni wajibu kuikata wakati wa kuchinja, huyo mnya-
ma atakuwa haramu, lakini kama akikata baadhi ya shingo au sehe-
mu nyingine na mishipa minne ikawa imebakia nyama yake
inakuwa tohara na halali kama atachinjwa kisheria.
MASHARTI YA KUCHINJA
1311. Kuchinja kisheria kuna masharti matano:-
Mchinjaji awe ni muislamu, mwanaume au mwanamke asiye dhi-
hirisha uadui kwa watu wa nyumba ya Mtume na kama atakuwa ni
mtoto wakiislamu anayejua zuri na baya inajuzu kuchinja.
266
Al-Masailul Islamiyah
Page 281
Achinjwe mnyama kwa kisu kikali, kama hakitapatikana na mnya-
ma akataka kufa bila kuchinjwa inajuzu atumie kitu chochote kikali
kama chupa, jiwe n.k.
Amuelekeze kibla wakati wa kuchinja yaani (uso wa mnyama,
mikono, miguu na tumbo vielekezwe kibla na kama hakumuelekeza
kibla kwa kukusudia nyama itakuwa haramu, lakini akisahau au
akiwa hajui au akiwa hajui upande wa kibla au hakuweza
kumwelekeza mnyama kibla hapatakuwa na tatizo akimchinja kati-
ka hali hizi.
Akitaka kuchinja au kuweka kisu shingoni ataje jina la Mwenyezi
Mungu kwa nia ya kuchinja na inatosha kusema “Bismaillah” na
akitaja jina la Mwenyezi Mungu sio kwa nia ya kuchinja, mnyama
hatatoharika na nyama yake itakuwa haramu, na vile vile kama
hakutaja jina la Mwenyezi Mungu kwa kutojua lakini hakuna tatizo
kwa aliyesahau.
Ajitikise mnyama angalau mtikisiko mdogo baada ya kuchinjwa,
mfano kupepesa jicho, kutikisa mkia au miguu yake.
NJIA YA KISHERIA YA KUCHINJA NGAMIA
1312. Akitaka kumhalalisha ngamia ili awe tohara na halali ni wajibu kwa
kuongezea kuzingatia masharti yaliyo tangulia katika kuchinja atain-
giza kisu au kinachofanana na kisu katika “luba” nayo ni sehemu ya
juu iliyoingia ndani ambayo imekutana na shingo na hii inaitwa
“nahri”, kudunga inalazimu kumuelekeza kibla yaani uso wake
uelekee kibla.
1313. Ni bora wakati wa kumdunga ngamia awe amesimama na hakuna
tatizo kama atakuwa amelala kwa ubavu ila aelekee kibla.
14. Kama atachinjwa ngamia badala ya nahri au ikatumika nahri kwa
267
Al-Masailul Islamiyah
Page 282
mbuzi au ng’ombe badala ya kuchinjwa nyama zitakuwa ni haramu na
mwili utakuwa ni najisi, lakini akikata mishipa ya ngamia kisha akatu-
mia njia ya nahri kwa njia tuliyoitaja nyama yake itakuwa halali na
mwili wake utakuwa tohara ,na pia mbuzi au ng’ombe ikitumika njia
ya nahri na kabla ya kufa ikakatwa mishipa minne nyama zitakuwa ni
halali na miili yao itakuwa ni tohara.
1315. Mnyama akiwa mkaili na ikashindikana kuchinjwa kwa njia iliy-
otajwa kisheria au akiangukia kisimani kiasi kwamba anataka kufa
huko na haikuwezekana kumchinja kisheria, inajuzu kumjeruhi kati-
ka sehemu yeyote ya mwili ili afe kwa sababu ya jeraha ,na atakuwa
halali na haimlazimu kumuelekeza kibla lakini lazima azingatie
masharti mengine tuliyoyataja katika kuchinja.
MAMBO YA SUNNA WAKATI WA KUCHINJA
1316. Ni sunna katika kuchinja mambo yafuatayo:-
1. Ni sunna katika kumchinja mbuzi amfunge mikono yake miwili na
mguu mmoja ama ng’ombe, ni sunna kumfunga mikono miwili na
miguu pia na anauacha mkia, ama ngamia ni sunna kumfunga mikono
na kwa ndege ni sunna amuache baada ya kumchinja ili afurukute.
2. Mwenye kuchinja aelekee kibla.
3. Ampe mnyama maji kabla ya kumchinja.
4. Asimtese mnyama, anoe kisu chake vizuri na afanye haraka kumch-
inja na asimuonyeshe kisu kabla ya kuanza kumchinja.
YALIYO MAKURUHU WAKATI WA KUCHINJA
1317. Ni makuruhu katika kuchinja mambo yafuatayo:-
1. Kukata mishipa kuanzia kisogoni
2. Kutenganisha kichwa cha mnyama na mwili kabla ya kutoka kwa
roho, lakini akifanya hivyo kwa kughafilika, au kwa sababu kisu ni
268
Al-Masailul Islamiyah
Page 283
kikali mno na bila yakutarajia hivyo haitakuwa makuruhu
3. Kumchuna mnyama kabla ya kutokwa na roho
4. Kukata nyama yake kabla ya kutokwa na roho
5. Kumchinja mnyama na mwingine anamwangalia
6. Kumchinja mnyama usiku au mchana kabla jua halijapetuka katika
siku ya ijumaa, hakuna tatizo wakati wa dharura na haja
7.Mfugaji kumchinja mnyama aliyemlea mwenyewe.
HUKUMU ZA KUWINDA KWA SILAHA
1318. Akiwinda mnyama wa porini aliye halali kuliwa kwa silaha,
nyama yake inakuwa halali na mwili wake unakuwa tohara kwa
masharti matano:-
Silaha ya kuwindia iwe ni yenye kukata kama vile kisu, panga au
kitu kikali kama mshale ambao makali yake yanakata mwili wa
mnyama, mtu akiwinda kwa kutumia mtego au fimbo au jiwe na
mengineyo na mnyama huyo akafa kwa ajili hiyo, hatatoharika na
nyama yake itakuwa ni haramu.
Na kuwinda kwa silaha za moto kama vile bunduki kama risasi yake
ina makali ya kuweza kuchana mwili wa mnyama basi huyo mnya-
ma atakuwa tohara na nyama yake pia ni halali, na kama silaha haina
makali kiasi kwamba inaingia kwenye mwili wa mnyama kwa
nguvu na kumuua, kwa dhahari ni halali lakini akimuunguza kwa
joto lake na akafa kwa sababu hiyo utohara wake na uhalali wake ni
mahali pa mushikeli.
Ni wajibu muwindaji awe muislamu au mtoto wa muislamu mwenye
kutofautisha kati ya zuri na baya, na pindi anapowinda kafiri au
mwenye uadui na watu wa nyumba ya Mtume (saww) mnyama huyo
269
Al-Masailul Islamiyah
Page 284
hatakuwa halali.
Atumie silaha ya kuwindia na kama atarusha risasi sehemu pasina
kukusudia kupiga mnyama kisha akapiga mnyama bila ya kutege-
mea mnyama hatakuwa halali na pia hatokuwa tohara.
Ataje jina la Mwenyezi Mungu wakati wa kutumia silaha na asipota-
ja jina la Mwenyezi Mungu kwa kukusudia mnyama huyo hatakuwa
halali, lakini akisahau hakuna tatizo.
Akute mnyama ameshakufa au amkute akiwa hai na wakati wa
kuchinja ukawa mfinyu, kama muda ulikuwa unamruhusu kuchinja
halafu akaacha kumchinja mpaka akafa nyama yake itakuwa ni hara-
mu.
1319. Wakishirikiana watu wawili katika kuwinda mmoja muislamu na
mwingine ni kafiri na mmoja akataja jina la Mwenyezi Mungu na
mwingine hakutaja kwa makusudi huyo mnyama hatakuwa halali.
1320. Akiwinda kwa silaha au mbwa wa wizi windo litakuwa ni halali
kwake, lakini atakuwa ameasi na ni wajibu wake atoe ujira kwa
mwenye silaha au mbwa.
1321 Akiwinda kwa upanga au mfano wake akawa amemkata mnyama
vipande viwili na kwa kuzingatia masharti, na mnyama akakatika
vipande viwili na kikabaki kichwa na shingo kwa kujitenga na
mwili, akikuta amekufa atakuwa halali vipande vyote na vile vile
akimkuta hai lakini hakupata wakati mpana wa kumchinja, ama
wakati wa kuchinja ukiwa mpana na ikawezekana kumchinja, basi
kipande kilichojitenga na kichwa kitakuwa haramu, na upande
wenye kichwa utakuwa halali kama atamchinja kisheria, la sivyo
huo upande pia uatakuwa haramu.
270
Al-Masailul Islamiyah
Page 285
1322. Akiwinda mnyama na akamchinja na wakakuta tumboni mwa mnya-
ma kuna mtoto mfu, kama amekamilika kimaumbile na akawa
ameota manyoya au sufi na ikawa kifo cha mtoto kimesababishwa
na kuchinjwa kwa mnyama huyo, mtoto atakuwa tohara na halali.
KUWINDA KWA KUTUMIA MBWA
1323. Mbwa akiwinda mnyama wa porini ambaye nyama yake ni halali
utohara na uhalali wa huyo mnyama utatimia kwa masharti sita:-
1. Mbwa awe amefundishwa kiasi kwamba akitumwa anaenda na aki-
ambiwa simama anasimama na ikawa ni kawaida yake kiasi kuwa
hawezi kula kabla ya kufika mwenyewe na hakuna tatizo akimla mnya-
ma bila kutarajia
2. Atumwe na mwenyewe kushika mnyama na kama mbwa akiondoka
kushika mnyama bila ya kuamrishwa na mwenyewe huyo mnyama
atakuwa haramu.
3. Na anayemtuma mbwa awe ni muislamu au mtoto wa muislamu
mwenye kutofautisha kati ya kheri na shari, na kama anayemwamrisha
ni kafiri au ana chuki na watu wa nyumba ya Mtume (saww) windo la
huyo mbwa litakuwa haramu.
5. Ataje jina la Mwenyezi Mungu pindi anapomwamuru mbwa na kama
ataacha kutaja jina la Mwenyezi Mungu kwa kukusudia hilo windo
litakuwa haramu na kama atakuwa amesahau haitakuwa na mushikeli.
6. Mnyama afe kwa sababu ya kujeruhiwa na meno ya mbwa kama atam-
nyonga mnyama au akifa kwa kukimbia au kuogopa hatakuwa halali
7. Mwenye kumtuma mbwa amkute amekufa au akimkuta hai wakati wa
271
Al-Masailul Islamiyah
Page 286
kuchinja ukawa ni mfinyu, kama wakati ukiwa unatosha kumchinja
mfano, amkute akiwa anapepesa macho yake au kutikisa mkia au miguu
kama hatomchinja mpaka akafa hata kuwa halali.
KUVUA SAMAKI
1324. Akivua samaki mwenye magamba kwenye maji na akafia nchi kavu
atakuwa ni tohara na nyama yake ni halali na akifia kwenye maji
atakuwa ni tohara lakini nyama yake ni haramu, ama samaki
ambaye hana magamba yeye ni haramu hata kama akitolewa
kwenye maji akiwa hai na akafia nchi kavu.
1325. Sio sharti mvuvi wa samaki awe muislamu na pia si wajibu kutaja
jina la Mwenyezi Mungu wala kuelekea kibla na kumchinja kwa
kisu, hivyo inajuzu kula samaki aliyevuliwa na kafiri lakini ni
wajibu muislamu azingatie kuvua kwake na ajue kuwa samaki ame-
vuliwa akiwa hai na amefia nchi kavu.
1326. Samaki aliyekufa ambaye hajulikani kuwa amevuliwa akiwa hai au
amekufa, kama samaki atakuwa kwa muislamu atakuwa halali na
kama atakuwa kwa kafiri atakuwa haramu hata kama akisema
amemvua akiwa hai, ila mtu akipata matumaini kwa maneno yake.
1327. Hailazimu kujiepusha kula samaki aliye hai.
KUWINDA SENENE/NZIGE
1328. Akimshika senene/nzige hai kwa mkono wake au kwa njia nyingine
atakuwa ni halali baada ya kufa kwake na si lazima aliyeshika
senene awe muislamu, na pia si lazima kutaja jina la Mwenyezi
272
Al-Masailul Islamiyah
Page 287
Mungu wakati wa kuwashika, na ukiwapata senene kwa kafiri na
haijulikani kuwa amewachukua wakiwa hai au wakiwa wamekufa
hawatakuwa halali kuliwa hata kama akisema amewachukua waki-
wa hai, ila kama atapata matumaini kutokana na maneno yake.
HUKUMU ZA KULA NA KUNYW A
1329. Ni halali kula nyama ya kuku, njiwa, ndege wenye mwiba nyuma ya
mguu na ni haramu kula popo, tausi na kila ndege ambaye ana
makucha kama vile kipanga, mwewe na ambaye kupiga mabawa
wakati wa kuruka ni mara chache kuliko kutulizana, na kila ndege
asiye na mwiba nyuma ya mguu wake ila ikiwa kupiga mabawa ni
kwingi kuliko kutulizana basi atakuwa halali.
1330. Kama kipande cha nyama kikijitenga na mwili wa mnyama mfano:
Mkia au kipande cha nyama ambacho kinakatwa kwa mbuzi aliye
hai, kipande hicho ni najisi na ni haramu.
1331. Ni haramu vitu vifuatavyo kwa mnyama aliyechinjwa kisheria:-
1. Kinyesi
2. Damu
3. Uume
4.Uke
5. Mfuko wa kuhifadhi mtoto tezi na kokwa mbili
8. Kitu mfano wa punje katikati ya ubongo
9. Kandama
10. Mshipa wa uti wa mgongo
11. Makamasi nyongo kibofu
12. Mboni ya jicho mishipa iliyo baina ya kwato.
1332. Ni haramu kula chochote kinachomzuru mtu kwa madhara makub-
wa.
273
Al-Masailul Islamiyah
Page 288
1333. Ni makuruhu kula nyama ya punda na farasi na kama mtu aki-
waingilia wanyama hawa nyama zao zitakuwa ni haramu, na ni
wajibu kuwatoa nje ya mji na kuwauza sehemu nyingine.
1334. Na mtu akimwingilia mnyama mwenye kuliwa kama ng’ombe na
mbuzi, basi mkojo na kinyesi chake kitakuwa najisi na maziwa
yatakuwa haramu kunywewa, na ni wajibu kumuuwa mnyama huyo
kwa haraka na mwenye kumwingilia alipe thamani yake kwa
mwenye ng’ombe.
1335. Ni haramu kukaa sehemu inayonywewa pombe au kileo chochote,
na pia ni haramu kula chochote katika meza inayonywewa pombe
juu yake.
1336. Ni wajibu kwa kila muislamu kumlisha na kumnywesha muislamu
mwenzake anayekaribia kufa kwa njaa au kwa kiu na kumuokoa
kutokana na mauti na kuhiliki, na vivyo hivyo kwa kila nafsi yenye
kuheshimika.
MAMBO YA SUNNA WAKATI WA KULA
1337. Ni sunna katika kula mambo yafuatayo:-
1. Kuosha mikono miwili kabla ya kula
2. Kuosha mikono miwili baada ya kula
3. Mwenye nyumba aanze kula kabla ya yeyote na amalize baada ya
kumaliza wote.
4. Kutaja jina la Mwenyezi Mungu unapoanza kula lakini kama kwenye
meza kuna vyakula vingi basi atataja jina la Mwenyezi Mungu katika
kila aina ya chakula.
5. Kula kwa mkono wa kulia
6. Ale kwa vidole vitatu au zaidi na asile kwa vidole viwili.
7. Ale kinachomuelekea katika chakula kama wanaokula ni wengi
274
Al-Masailul Islamiyah
Page 289
8. Ale tonge dogo
9. Ale kwa muda mrefu na wala asifanye haraka katika kula
10.Atafune chakula vizuri
11.Alambe vidole vyake baada ya kula
12.Amshukuru Mwenyezi Mungu baada ya kula
13.Achokonoe meno yake baada ya kula lakini asichokonoe kwa kijiti cha
mkomamanga, muwa wala kwa mti wa mtende.
14. Aokote mabaki ya chakula yaliyodondoka kwenye meza na kuyala na
kama atakuwa anakula porini au jangwani ni sunna kuwaachia ndege
na wanyama
15. Ale chakula mwanzo wa mchana na mwanzo wa usiku na asile katikati
ya mchana na katikati ya usiku
16. Aanze kula kwa chumvi na kumalizia kwa chumvi
17. Aoshe matunda kabla ya kuanza kula
18. Alale chali baada ya chakula na kuweka mguu wake wa kulia juu ya
mguu wa kushoto.
YALIYO MAKURUHU WAKATI WA KULA
1338. Yaliyomakuruhu wakati wa kula ni:-
1. Kula wakati umeshiba
2. Kula sana
3. Kuangalia uso wa mwenzako wakati wa kula.
4. Kula chakula cha moto
5. Kupuliza unachokula au unachokunywa
6. Kukata mkate kwa kisu
7. Kuweka mkate chini ya chombo
8. Kula nyama na kutobakisha kitu kwenye
mfupa
9. Kumenya matunda ambayo yanawezekana kuliwa bila kumenywa
10. kutupa tunda kabla ya kulila kwa ukamilifu.
275
Al-Masailul Islamiyah
Page 290
MAMBO YA SUNNA WAKATI WA KUNYWA MAJI
1339. Yafuatayo ni sunna wakati wa kunywa:-
1. Anywe maji kwa kunyonya
2. Anywe maji mchana kwa kusimama na usiku kwa kukaa
3. Amtaje Mwenyezi Mungu kabla ya kunywa na baada ya kunywa
amshukuru Mwenyezi Mungu
4. Anywe maji kwa funda tatu
5. Awe na kiu ya maji na asinywe bila ya kuwa
na kiu.
6. Amkumbuke Imamu Hussein “as” na watu wa nyumba ya Mtume
na awalaani waliomuuwa Imamu Husein.
YALIYO MAKURUHU WAKATI WA
KUNYWA MAJI
1340.Ni makuruhu wakati wa kunywa mambo yafuatayo:-
1. Kunywa maji sana
2. Kunywa maji baada ya kula chakula chenye mafuta
3. Kunywa maji usiku kwa kusimama
4. Kunywa maji kwa mkono wa kushoto
5. Kunywa maji katika sehemu iliyovunjika au iliyo na mapengo
katika kikombe.
HUKUMU ZA MIRATHI
1341. Ambao wanarithi kwa nasaba ni tabaka tatu:-
Kwanza: Wazazi wa marehemu na watoto wake, kama hakuna watoto basi
watoto wa watoto wao na kuteremka chini, na anarithi kwao kila aliyeku-
276
Al-Masailul Islamiyah
Page 291
wa karibu zaidi kwa marehemu na maadamu anapatikana mmoja katika
tabaka hili hatarithi yeyote kutoka katika tabaka la pili.
Pili: Babu, bibi na ndugu wa marehemu na kama hawapo basi watoto wao
wanarithi na kila aliye karibu zaidi na marehemu na maadamu anapatika-
na yeyote katika tabaka hili harithi yeyote kutoka katika tabaka la tatu.
Tatu: Ami, shangazi, mjomba na mama wadogo wa marehemu na watoto
wao na maadamu anapatikana yeyote kati ya ami, shangazi, mjomba na
mama wadogo hatorithi yeyote kati ya watoto wao, lakini kama marehemu
ataacha Ami wa upande wa baba tu na mtoto wa Ami wa upande wa baba
na mama, mtoto wa ami wa upande wa baba na mama atarithi bila ya Ami
wa upande wa baba tu.
1342. Kama marehemu hana ami, shangazi,mjomba na mama wadogo
wala watoto wao wala watoto wa watoto wao watarithi ami wa baba
yake na mama yake, shangazi zao na wajomba zao kama hawapo
watoto wao na kama hawapo basi wanarithi ami, shangazi, wajom-
ba na mama wadogo wa babu na bibi yao na kama hawapo basi
watarithi watoto wao.
1343.Mume na mke kila mtu anamrithi mwenzake kwa utaratibu utakao
kuja pamoja na kila tabaka katika matabaka matatu yaliyotajwa.
MIRATHI YA TABAKA LA KWANZA
1344. Marehemu akiacha mtu mmoja katika tabaka la kwanza kama vile
baba au mama au mtoto wa kiume au mtoto wa kike anarithi mali
yote na kama ataacha watoto wa kiume wengi au watoto wakike
wengi mali itagawanywa sawa baina yao, na kama ataacha mtoto
mmoja wa kiume na mtoto mmoja wa kike mali itagawanywa sehe-
mu tatu, mtoto wa kiume atapewa sehemu mbili na mtoto wa kike
atapewa sehemu mmoja, na kama ataacha watoto wa kiume wengi
na watoto wa kike wengi basi mali itagawanywa kwa namna
277
Al-Masailul Islamiyah
Page 292
ambayo mtoto wa kiume atarithi mara dufu ya mtoto wa kike.1345. Kama marehemu ataacha wazazi wawili mali itagawanywa sehemu
tatu mzazi wa kiume atapewa sehemu mbili na mzazi wa kike ata-pewa sehemu moja, na kama marehemu ataacha pamoja na nduguwawili wa kiume au dada wawili au kaka na dada wawili na wotewakawa ni wa upande wa baba tu au wa upande wa mama waohawatarithi kwa marehemu maadamu marehemu ana baba na mamaisipokuwa mama wa marehemu kwa sabau yao atarithi moja ya sita“1/6” na mali iliyobaki atapewa baba wa marehemu.
1346. Marehemu akiacha wazazi wawili na binti mmoja kama marehemuhana kaka wawili wala dada wawili au dada wanne au kaka mmojana dada wawili wa upande wa baba mali itagawanywa sehemu tano,baba na mama kila mmoja atarithi sehemu moja na binti atarithisehemu tatu na kama marehemu ana kaka wawili au dada wanne aukaka na dada wawili wa upande wa baba mali itagawanywa sehemusita baba na mama kila moja atapata sehemu moja na binti atapewasehemu tatu, sehemu iliyobaki “1/6” itagawanywa sehemu nne babaatapewa sehemu moja na binti atapewa sehemu zilizobakia kwamfano kama itagawanywa mali ya marehemu sehemu 24 binti ata-pewa sehemu 15, baba atapewa sehemu 5 na mama atapewa sehemu4.
1347. Marehemu akiacha wazazi wawili na mtoto wa kiume mali itagawa-
nywa sehemu sita wazazi wawili kila mmoja atapewa sehemu moja
na sehemu nne atapewa mtoto wa kiume, na akiacha pamoja nao
watoto wengi wa kiume au watoto wengi wa kike mali itagawanywa
sawa baina yao, ama wakiwa ni watoto wa kiume na watoto wa kike
mali itagawanywa kwa namna ambayo mtoto wa kiume atachukua
mara dufu ya mtoto wa kike.
1350. Marehemu akiacha baba na mtoto mmoja wa kiume au mama na
mtoto mmoja wa kike mali itagawanywa sehemu sita sehemu moja
anapewa baba au mama na sehemu zilizobaki anapewa mtoto wa
kiume.
278
Al-Masailul Islamiyah
Page 293
1351. Marehemu akiacha baba na mtoto wa kiume na binti au mama na
watoto wa kiume na binti mali itagawanywa sehemu sita, sehemu
moja anapewa baba au mama na sehemu zilizobakia zitagawanywa
kwa namna ambayo mtoto wa kiume atapata mara dufu ya binti.
1352. Marehemu akiacha baba na binti mmoja au mama na binti mmoja
mali itagawanywa sehemu nne sehemu moja atapewa baba au mama
na baki atapewa binti.
1353. Marehemu akiacha baba tu na watoto wa kike wengi au mama tu na
watoto wengi wa kike mali itagawanywa sehemu tano, sehemu moja
atapewa baba au mama na sehemu zilizobakia zitagawanywa kwa
watoto wa kike kwa usawa.
1354. Kama marehemu hajaacha mtoto wa kiume wala binti watarithi
watoto wa watoto wake wa kiume hisa ya watoto wa kiume hata
kama wao watakuwa ni wanawake, na watoto wa kike watarithi hisa
ya watoto wake wa kike hata kama watakuwa ni wanaume mfano,
kama marehemu ataacha mjukuu wa kiume wa binti yake na mjukuu
wa kike wa mtoto wake wa kiume mali itagawanywa sehemu tatu,
sehemu moja atapewa mtoto wa kiume wa binti yake na sehemu
mbili atapewa mtoto wa kike wa mtoto wake wa kiume.
MIRATHI YA TABAKA LA PILI
1355. Tabaka la pili linalorithi kwa nasaba ni babu, bibi, ndugu wa kiume
na wa kike wa marehemu na kama hajaacha ndugu wakiume na
wakike basi watoto wao ndio watarithi.
1356. Marehemu akiacha ndugu wa kiume tu au ndugu wa kike tu basi
mali yote ni yake, na wakiwepo ndugu wa kiume wengi na ndugu wa
kike wengi wa wazazi wawili mali itagawanywa baina yao kwa
usawa, na ikiwa ndugu wa kiume wengi na ndugu wa kike wengi
279
Al-Masailul Islamiyah
Page 294
ndugu wa kiume watarithi mara dufu ya ndugu wa kike, mfano kama
ataacha ndugu wa kiume wawili na ndugu mmoja wa kike mali ita-
gawanywa sehemu tano kila ndugu wa kiume atapewa sehemu mbili
na ndugu wa kike atapewa sehemu moja.
1357. Kama marehemu ataacha ndugu wa kiume na ndugu wa kike wa
wazazi wawili, ndugu wa kiume na ndugu wa kike wa upande wa
baba tu hawatarithi, kama ataacha ndugu wa kiume au ndugu wa
kike wa upande wa baba tu atarithi mali yote, na akiacha ndugu wa
kiume kama ndugu wakiwa wengi wa upande wa baba tu mali ita-
gawanywa baina yao kwa usawa, na kama ataacha ndugu mmoja wa
kiume na ndugu wakike wengi mwanaume atarithi mara dufu ya
mwanamke.
1358. Marehemu akiacha ndugu wa kiume mmoja au ndugu wa kike
mmoja tu wa upande wa mama, atarithi mali yote na akiacha ndugu
wa kiume wengi au ndugu wa kike wengi wa upande wa mama tu
mali itagawanywa baina yao kwa usawa. Marehemu akiacha ndugu
wa kiume na ndugu wa kike wa wazazi wawili au ndugu wa kiume
na ndugu wa kike wa upande wa baba tu na ndugu wa kiume au wa
kike wa upande wa mama tu, ndugu wa upande wa baba tu hawata-
rithi na mali itagawanywa sehemu sita, sehemu moja atapewa ndugu
wa kiume na ndugu wa kike wa upande wa mama tu, na sehemu zili-
zobaki ni za ndugu wa kiume, na ndugu wa kike wa wazazi wawili
na wanaume watarithi mara dufu ya wanawake.
1359. Marehemu akiacha ndugu wa kiume na ndugu wa kike wa wazazi
wawili, ndugu wakiume na ndugu wakike wa upande wa baba tu na
ndugu wa kiume na ndugu wakike wa upande wa mama tu ndugu wa
kiume na ndugu wa kike wa upande wa baba hawatarithi na mali ita-
gawanywa sehemu tatu, sehemu itagawanywa baina ya ndugu wa
kiume na ndugu wa kike wa mama kwa usawa na iliyobakia wata-
pewa ndugu wa wazazi wawili na mwanaume atapata mara dufu ya
mwanamke.
280
Al-Masailul Islamiyah
Page 295
1360. Marehemu akiacha kaka na dada wa upande wa baba tu na kaka au
dada wa upande wa mama tu mali itagawanywa sehemu sita, sehe-
mu moja ni ya kaka au dada wa upande wa mama, na iliyobaki ita-
gawanywa baina ya kaka na dada wa upande wa baba tu na mwa-
naume atapata mara dufu ya anayopata mwanamke.
1361. Marehemu akiacha kaka na dada na mke, mke atarithi kwa namna
ambayo utakuja ufafanuzi wake, na kaka na dada watarithi kwa
namna iliyotangulia kutajwa katika mas’ala yaliyotangulia, vivyo
hivyo akifa mke na akaacha kaka, dada na mume wake, mume ata-
rithi nusu ya mali na kaka na dada watarithi kwa namna iliyotajwa
katika mas’ala yaliyotangulia, lakini kurithi kwa mke au mume hai-
punguzi hisa ya kaka na dada wa wazazi wawili au wa upande wa
baba tu.
1362. Marehemu akiacha babu au bibi ni sawa awe wa upande wa baba au
wa upande wa mama tu, atarithi mali yote, babu akiwepo mzazi wa
babu hatarithi.
MIRATHI YA TABAKA LA TATU
1363. Tabaka la tatu ni Ami wa marehemu, wajomba, mama wadogo na
watoto wao kama hatakuwepo yeyote katika tabaka lililotangulia.
1364. Marehemu akiacha Ami, shangazi ni sawa awe ni wa upande wa
wazazi wawili au wa upande wa baba tu anarithi mali yote, na akia-
cha Ami wengi au shangazi wengi mali itagawanywa baina yao kwa
usawa.
1365. Marehemu akiacha mjomba au mama mdogo anarithi mali yote na
akiacha mjomba na mama mdogo na wote ni wa upande wa wazazi
wawili au wa upande wa baba tu mali itagawanywa baina yao kwa
usawa na kwa tahadhari waelewane katika kugawana.
281
Al-Masailul Islamiyah
Page 296
MIRATHI YA MUME NA MKE
1366. Mke akifariki na akawa hajaacha watoto mume anarithi nusu ya mali
yake na inayobaki wanapewa watu wengine wa upande wa mke na
ikiwa ana watoto kwa huyo mume au kwa mume mwingine mume
anarithi robo ya mali yake na iliyobaki wanarithi wengine.
1367. Mume akifariki na akawa hajaacha watoto, mke anarithi robo ya
mali na iliyobaki wanarithi wengine na kama ana watoto kwa huyo
mume au kwa mume mwingine mke atarithi moja ya nane (1/8).
1368. Mke harithi ardhi na wala harithi nyumba, jengo na miti, lakini ana-
rithi thamani yake.
1369. Mke akitaka kurithi ardhi au kutumia vitu ambavyo havirithi ni waji-
bu atake idhini kwa warithi wengine na vivyo hivyo warithi wengi-
ne kwa tahadhari ya wajibu wasitumie vitu ambavyo mke anarithi
thamani yake kabla hawajampa hisa yake isipokuwa kama atatoa
idhini vinginevyo muamala utakuwa batili.
1370. Kama marehemu ana mke zaidi ya mmoja na hana watoto robo ya
mali yake itagawanywa kwa wake zake kwa usawa na kama ana
watoto (1/8) moja ya nane ya mali yake itagawanywa kwa wake
kwa usawa.
1371. Kama ataoa mke katika hali ya maradhi kisha akafa kwa maradhi
hayo mke wake atamrithi hata kama hakumwingilia.
1372. Mke akiachwa talaka rejea kisha akafa katika eda mume wake atam-
rithi, vivyo hivyo kama mume atafariki ndani ya eda yake mke ata-
rithi, lakini kama mmoja akifa baada ya kumalizika eda ya talaka
282
Al-Masailul Islamiyah
Page 297
rejea au katika eda ya talaka bain hatamrithi.
1374. Mwislamu anarithi kwa kafiri lakini kafiri harithi kwa mwislamu
hata kama atakuwa ni mtoto wa marehemu au baba yake.
1375. Mtu akimuuwa yeyote kwa makusudi au kwa dhulma hatamrithi.
TALAQIN YA MAIT
283
Al-Masailul Islamiyah
Page 298
284
Al-Masailul Islamiyah
Page 299
285
Al-Masailul Islamiyah
Page 300
BACK COVER
Historia fupi ya Ayatullah al-Udhmaa Sayyid Sadiq Shirazi (dama
dhilluhu).
Amezaliwa katika mwezi wa Dhilhijjah mwaka 1360 Hijria mwafaka namwaka 1948 Miladia katika mji mtukufu wa Karbala, Iraq.
Amesoma kwa marjaa taklidi na maulamaa wakubwa katika vyuo vikuu
vya kidini (hawza) hadi akafikia daraja la juu kabisa la kutoa fatwa na ijti-
hadi na kuwa mujtahidi.
Amelelewa katika nyumba kongwe ya ukoo wenye elimu kubwa na
uliobobea katika fikihi, ijtihadi, jihadi na kujitolea.
Ayatullah Shirazi amekua na kupambika umri wake kwa moyo wa ikhlasi,
ucha Mungu, amali na fikra njema zinazokwenda sambamba na
mafundisho ya Qur’ani Tukufu na Ahlul Bait (a.s.).
Ametunga vitabu vingi katika viwango mbalimbali ya ufahamu, miongoni
mwao vikiwepo:
Sharh al-‘Urwatu ‘l-Wuthqaa, Ijtiha wa Taqlid, Bayanu ‘l-Usul, Qa’idah
La Dharar Walaa Dhiraar, n.k.
Vivyo hivyo, ameandika vitabu vya masomo kwa ajili ya wanafunzi wa
Hawza, k.v. Rawdhah Fiy Sharh al-Lum’ah, Sharh al-Sharaa’i’, Sharh at-
Tabsirah, Sharh Suyuti, Sharh Samadiyyah, Mu’jazi Fiy Mantiq, n.k.
Zaidi ya miaka ishirini sasa, Ayatullah Sayyid Sadiq Shirazi amekuwa aki-
toa darsa za khariji za Usuli Fikihi ambazo ni darsa za juu kabisa katika
Hawza. Wanafunzi na hata maulamaa waliofikia daraja la ijtihadi ni mion-
goni wa wenye kuhudhuria darsa zake na kunufaika kwazo.